Jibu: Ni kweli Kristo alizichukua dhambi zetu kama biblia inavyosema katika kitabu cha Petro..
1Petro 2:24 “Yeye mwenyewe alizichukua dhambi zetu katika mwili wake juu ya mti, tukiwa wafu kwa mambo ya dhambi, tuwe hai kwa mambo ya haki; na kwa kupigwa kwake mliponywa”.
Lakini hiyo haimaanishi kuwa tumeshakamilika asilimia mia kwamba hatutakuwa na kasoro zozote kuanzia hapo na kuendelea…Kasoro chache chache na madhaifu machache chache bado tutaendelea kuwa nayo mpaka siku tutakapopata ukombozi wa miili yetu (Waefeso 4:30).
Wakati parapanda ya mwisho itakapolia hapo ndipo tutapata ukombozi wa miili yetu, na tutakuwa wakamilifu asilimia zote kwasababu tutapewa miili mingine isiyo na kasoro wala madhaifu.. lakini sasa ulimwenguni bado tupo katika mapambano, bado tupo vitani, bado ibilisi yupo, bado tutapitia vipindi vya kukosea vidogo vidogo, lakini si vya kutuangusha kabisa!!.. Kama kile Petro alichopitia wakati anakutana na Paulo kule Antiokia (Soma Wagalatia 2:11-14).
Vile vile tutapitia vipindi vya kuudhiwa, na kupata hasira, tutapitia vipindi vya kukosea kuongea, kukosea kutenda, tutapitia vipindi pia vya kuwakosa wengine pasipo kujua au kwa kujua, tutapitia vipindi vya kumkosa Mungu kwa kujua au kwa kutokujua n.k.. sasa kwa kasoro hizo zote tunazozibeba ni lazima tuwe watu wa kuomba rehema na toba mara kwa mara ili muda wote tudumu katika usafi na pia Bwana anyooshe mapito yetu..
Hiyo ndiyo sababu pia Bwana Yesu akatufundisha kuomba toba na rehema kila mara..
Luka 11:1 “Ikawa alipokuwa mahali fulani akiomba, alipokwisha, mmoja katika wanafunzi wake alimwambia, Bwana, tufundishe sisi kusali, kama vile Yohana alivyowafundisha wanafunzi wake.
2 Akawaambia, Msalipo, semeni, Baba [yetu uliye mbinguni], Jina lako litakaswe, Ufalme wako uje, [Mapenzi yako yatimizwe, hapa duniani kama huko mbinguni.]……………….
4 UTUSAMEHE DHAMBI ZETU, kwa kuwa sisi nasi tunamsamehe kila tumwiaye. Na usitutie majaribuni [lakini tuokoe na yule mwovu]”.
Kwahiyo ni lazima kuomba rehema na toba kila siku, kwasababu bado tupo katika mwili, na pia ni ishara ya unyenyekevu kwa Mungu.
Bwana atubariki.
Maran atha!
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Mada Nyinginezo:
Ni kwa namna gani, upendo husitiri wingi wa dhambi? (1Petro 4:8).
SALA YA BWANA. (Namna ya kuiomba)
Jibu: Tusome,
Isaya 66:3 “Yeye achinjaye ng’ombe ni kama yeye amwuaye mtu; na yeye atoaye dhabihu ya mwana-kondoo ni kama yeye avunjaye shingo ya mbwa; na yeye atoaye matoleo ni kama yeye atoaye damu ya nguruwe; na yeye afukizaye uvumba ni kama yeye abarikiye sanamu; naam, wamezichagua njia zao wenyewe, na nafsi zao zafurahia machukizo yao”.
Mstari huo tukiusoma kama ulivyo ni rahisi kutafsiri kuwa “Biblia imekataza kuchinja wanyama na kula nyama”…lakini kiuhalisia hiyo sio maana yake kabisa…kwasababu kama hiyo ingekuwa ndio maana yake basi pia hapo imekataza matoleo… na tunajua matoleo ni jambo linalokubalika mbele za Mungu (Warumi 25:26).
Sasa tukisoma kuanzia ule mstari wa kwanza utaona Mungu anawakemea au kuwaonya wale watu ambao wanakusanya vingi na vikubwa na kwenda kumtolea Mungu, wakidhani kuwa Mungu anapendezwa na sadaka zao hizo kubwa na nyingi na huku mioyoni wapo mbali na Mungu.
Na utaona Bwana anazidi kusema.. “Mbingu na dunia ni mali yake, hakuna chochote tutakachoweza kumpa yeye ambacho kitakuwa cha kipekee”…ikifunua kuwa Mungu hana haja na vitu bali mioyo yetu, kwasababu kila kitu ni chake.
Isaya 66:1 “BWANA asema hivi, Mbingu ni kiti changu cha enzi, na dunia ni mahali pa kuweka miguu yangu; mtanijengea nyumba ya namna gani? Na mahali pangu pa kupumzikia ni mahali gani?
2 Maana mkono wangu ndio uliofanya hivi vyote, vitu hivi vyote vikapata kutokea, asema BWANA; lakini mtu huyu ndiye nitakayemwangalia, mtu aliye mnyonge, mwenye roho iliyopondeka, atetemekaye asikiapo neno langu”.
Umeona?..Mtu mnyonge ndiye atakayemwangalia Bwana, mtu mwenye roho iliyopondeka, atetemekaye asikiapo neno lake…Maana yake mtu wa namna hii atakapoleta sadaka yake ndio Mungu atakayoikubali, lakini mtu mwovu na mwenye kiburi Mungu haitaki sadaka yake.
Sasa endapo mtu mwovu anayemkataa Mungu analeta sadaka yake mbele za Mungu, sadaka yake hiyo inaonekana kama ni sadaka ya hatia.
Kama akileta Ng’ombe na kumpeleka kwa Kuhani kama sadaka ya kuteketezwa, Bwana ataiona sadaka hiyo kama ni kafara ya Mtu sio ya ng’ombe, hivyo atajitafutia laana badala ya baraka.
Utaona maandiko yanazidi kulisisitiza hilo katika Mithali 15:8
.
Mithali 15:8 “Sadaka ya mtu mbaya ni chukizo kwa BWANA…”
Ndio maana katika Isaya 66, Bwana anasema..
Isaya 66:3 “Yeye achinjaye ng’ombe ni kama yeye amwuaye mtu; na yeye atoaye dhabihu ya mwana-kondoo ni kama yeye avunjaye shingo ya mbwa; na yeye atoaye matoleo ni kama yeye atoaye damu ya nguruwe; na yeye afukizaye uvumba ni kama yeye abarikiye sanamu; naam, wamezichagua njia zao wenyewe, na nafsi zao zafurahia machukizo yao”.
Kwahiyo tunachoweza kujifunza ni kuwa, Bwana hapendezwi na matoleo mabaya, yeye alisema kulitii Neno lake ni bora kuliko dhabihu Soma (1Samweli 15:22).
Hivyo usipeleke madhabahuni fedha haramu, fedha iliyopatikana kwa rushwa, kwa wizi, kwa uuuzaji wa vitu haramu kama bangi, pombe, sigara au hata kwa uuzaji wa mwili.
Kumbukumbu 23:18 “Usilete ujira wa kahaba, wala mshahara wa mbwa, katika nyumba ya BWANA, Mungu wako, kwa ajili ya nadhiri yo yote; kwani haya ni machukizo kwa BWANA, Mungu wako, yote mawili”
Vile vile hatupaswi kumtolea Mungu dhabihu huku hatuna mapatano sisi kwa sisi..
Mathayo 5:23 “Basi ukileta sadaka yako madhabahuni, na huku ukikumbuka ya kuwa ndugu yako ana neno juu yako,
24 iache sadaka yako mbele ya madhabahu, uende zako, upatane kwanza na ndugu yako, kisha urudi uitoe sadaka yako”
Bwana Yesu atusaidie.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Nyama zilizosongolewa ni zipi?Je kunywa damu ni dhambi?
HAPAKUWA NA NAFASI YA KUPITA KWA YULE MNYAMA ALIYEKUWA CHINI YANGU.
Kwanini Bwana aliwalenga mbwa na nguruwe tu katika Mathayo 7:6?
UPENDO NI NINI NA JE! KUNA AINA NGAPI ZA UPENDO?
Jibu: Tusome,
Yohana 11:14 “Basi hapo Yesu akawaambia waziwazi, Lazaro amekufa.
15 Nami nafurahi kwa ajili yenu kwamba sikuwako huko, ili mpate kuamini; lakini na twendeni kwake.
16 Basi Tomaso, aitwaye Pacha, akawaambia wanafunzi wenziwe, Twendeni na sisi, ili tufe pamoja naye”
Kwa haraka ni rahisi kutafsiri kuwa Tomaso alitaka na yeye kwenda kufa pamoja na Lazaro, lakini kiuhalisia sio hivyo!.
Tomaso hakutaka kwenda kufa pamoja na Lazaro, bali hapo alimaanisha “kwenda kufa pamoja na Bwana Yesu”.
Ili tuelewe vizuri tuanze kusoma kisa hicho kuanzia juu mstari ule wa tano..(Zingatia vipengele vilivyoainishwa kwa herufi kubwa).
Yohana 11:5 “ Naye Yesu alimpenda Martha na umbu lake na Lazaro.
6 Basi aliposikia ya kwamba hawezi, alikaa bado siku mbili pale pale alipokuwapo.
7 Kisha, baada ya hayo, akawaambia wanafunzi wake, TWENDENI UYAHUDI TENA.
8 Wale wanafunzi wakamwambia, Rabi, JUZIJUZI TU WAYAHUDI WALIKUWA WAKITAFUTA KUKUPIGA KWA MAWE, NAWE UNAKWENDA HUKO TENA?
9 Yesu akajibu, Je! Saa za mchana si kumi na mbili? Mtu akienda mchana hajikwai; kwa sababu aiona nuru ya ulimwengu huu.
10 Bali akienda usiku hujikwaa; kwa sababu nuru haimo ndani yake.
11 Aliyasema hayo; kisha, baada ya hayo, akawaambia, Rafiki yetu, Lazaro, amelala; lakini ninakwenda nipate kumwamsha.
12 Basi wale wanafunzi wakamwambia, Bwana, ikiwa amelala, atapona.
13 Lakini Yesu alikuwa amenena habari ya mauti yake; nao walidhania ya kuwa ananena habari ya kulala usingizi.
14 Basi hapo Yesu akawaambia waziwazi, Lazaro amekufa.
15 Nami nafurahi kwa ajili yenu kwamba sikuwako huko, ili mpate kuamini; lakini na twendeni kwake. 16 Basi Tomaso, aitwaye Pacha, akawaambia wanafunzi wenziwe, TWENDENI NA SISI, ILI TUFE PAMOJA NAYE”
Katika kisa hiki tunaona Bwana Yesu anawapa taarifa wanafunzi wake ya kurejea tena kule Uyahudi ambapo walitaka kumpiga mawe mpaka afe!.. na taarifa hiyo ikawashitusha wanafunzi inakuwaje anataka kurudi tena huko kwenye hatari! (Maana yake si ndo anaenda kufa sasa!)…
Lakini Tomaso aliposikia wanafunzi wenzake wakimhoji hivyo, ndipo na yeye akawashauri kwamba wasimwache aende pake yake huko uyahudi, bali nao pia waende pamoja naye, ili kama ikitokea kauawa basi na wao wafe pamoja naye!.
Ni moyo mzuri aliokuwa nao Tomaso, lakini hakujua kuwa kufa kwaajili ya Kristo ni Neema na si jambo la kujiamulia tu au kujivunia kwamba linaweza kutendeka kwa uwezo wa mtu.
Mtume Petro alijaribu hilo zoezi kama la Tomaso likamshinda, kwasababu alidhani anaweza kufa ajili ya Kristo kwa nguvu zake..
Luka 22:31 “Akasema, Simoni, Simoni, tazama, Shetani amewataka ninyi apate kuwapepeta kama vile ngano;
32 lakini nimekuombea wewe ili imani yako isitindike; nawe utakapoongoka waimarishe ndugu zako.
33 Akamwambia, Bwana, niwapo pamoja nawe, mimi ni tayari kwenda gerezani AU HATA KIFONI.
34 Akasema, Nakuambia, Petro, jogoo hatawika leo, kabla wewe hujanikana mara tatu ya kuwa hunijui”.
Zaidi sana huyu Tomaso ambaye alitaka kwenda kufa pamoja na Bwana, siku Bwana anakamatwa alimkimbia, hakuonekana!..(huenda ndo alikuwa Yule kijana aliyekimbia uchi, Marko 14:52)…na zaidi sana hata baada ya kufufuka kwake bado ilikuwa ni ngumu kuamini mpaka alipotokewa na Bwana Yesu..(huyo ndio mtu aliyetaka kwenda kufa na Yesu Yerusalemu)
Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba Tomaso hakutaka kwenda kufa na Lazaro, vinginevyo ingekuwa haina maana… lakini kinyume chake alitamani kwenda kufa pamoja na Bwana kwasababu aliamini huo ni ushujaa mkuu wa Imani.
Jambo tunaloweza kujifunza ni kuwa, hatupaswi kuzitumainia nguvu zetu, hatuwezi kusema tutamtumikia Mungu kwa nguvu zetu, hatuwezi kujivuna kuwa tutafanya hiki au kile kwa nguvu zetu, bali siku zote hatuna budi kuwa katika hali ya unyenyekevu, na kujishusha mbele za Bwana, kama tunatamani kufa kwaajili ya Bwana kifo cha kishujaa, basi tumalizie kwa kusema, BWANA TUSAIDIE…
Na chochote kile tukifanyacho au tukikusudiacho ni lazima kumalizia kwa kusema “KWA MSAADA WA BWANA KITAFANIKIWA”.. Lakini tukijivuna kuwa tunaweza hiki au kile, tutaishia kumkana na hata kumsaliti.
Bwana akubariki.
Maran atha!
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Kwa kuwa ni shida mtu kufa kwa ajili ya mtu mwenye haki;
TUKIO LA MUSA NA ELIYA KUMTOKEA BWANA, LIMEBEBA UJUMBE GANI?
Je ni kweli kila nafsi itaonja mauti kulingana na (Zaburi 89:48)?
Nini maana ya “mtakayoyafunga duniani, yatakuwa yamefungwa mbinguni”?
Swali: Je mapepo yanaweza kuviingia vitu visivyo na uhai kama mawe, milima, bahari, maji au nyumba, na hata kubadilisha maumbile ya hivyo vitu?
Jibu ni LA! Mapepo hayawezi kuviingia vitu visivyo na uhai bali yanaweza kuvitumia vitu visivyo na uhai.. mapepo hayawezi kuyaingia mawe au maji au mchanga au maji kama vile yanavyoingia ndani ya mtu, na kuviendesha vitu hivyo kama yanavyowaendesha wanadamu… Sehemu pekee ambayo mapepo yanaweza kuingia ni ndani ya viumbe hai kama wanadamu na wanyama, basi!
Biblia imerekodi mara kadhaa mapepo kuingia ndani ya watu (Luka 8:27) na pia ndani ya wanyama soma Marko 5:12-13. Lakini hakuna mahali popote panapoonyesha mapepo yamewahi kuingia ndani ya mawe au katika maji au katika mchanga, au katika matofali au katika gari la farasi au katika chakula..
Mapepo yanachoweza kufanya ni kuvitumia tu vitu vya asili, kwamfano yanaweza kuvumisha upepo lakini si kuingia ndani ya upepo, vile vile yanaweza kutetemesha ardhi lakini si kuiingia ardhi, yanaweza kuitikisa bahari lakini si kuiingia bahari… uwezo ambao hata sisi wanadamu tunao, sisi tunaweza kuvumisha upepo tukiwa na kifaa kinachoitwa feni, lakini si kuuingia upepo, vile vile tunaweza kutengeneza mawimbi ya bahari kwa vyombo maalumu n.k, lakini hiyo haimaanishi kuwa tumeiingia bahari na kuiendesha bahari kama vile tunavyoiendesha mikono yetu au miguu yetu.
Na mapepo ni hivyo hivyo, hayana uwezo wa kuviingia vitu visivyo na uhai.
Kwahiyo tunachopaswa kufanya ili roho za mapepo zisiweze kutumia vitu vya asili kutuletea matatizo ni sisi kudumu katika usafi na utakatifu pamoja na kuomba… tukifanya hivyo shetani na mapepo yake hawawezi kutumia vitu vinavyotuzunguka kutuletea madhara, hawawezi kuzitumia nyumba zetu kama vituo vyao vya mikutano.
Lakini tusipojisogeza karibu na Mungu, basi shetani atatumia vitu vyote kutudhuru, atatumia ardhi, bahari, mabonde, na magari na hata nyumba kutuletea matatizo…
Isaya 13:21 “Lakini huko watalala hayawani wakali wa nyikani; na nyumba zao zitajaa bundi; mbuni watakaa huko; na majini watacheza huko”
Maran atha!
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
AINA ZA MAJINI, MAJINA YAO, KAZI ZAO, NA TIBA ZAKE.
Je! Ni sawa kuingia katika shamba la mtu mwingine na kula jinsi utakavyo?
Je ni viatu gani Musa aliambiwa avivue? Vya mwilini au vya rohoni? (Kutoka 3:5).
Jibu: Tusome,
Waefeso 2:20 “Mmejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii, naye Kristo Yesu mwenyewe ni jiwe kuu la pembeni”
Hapo maandiko yanasema tumejengwa juu ya “Msingi wa Mitume na Manabii “na si juu ya “Mitume na Manabii” .. Na pia inasema tumejengwa juu ya “Msingi” na si juu ya Misingi ya mitume na manabii. Ikiwa na maana kuwa Msingi ni mmoja tu, ambao tumejegwa juu yake, (mbele kidogo tutakuja kuuona huo msingi ni nini).
Sasa yapo maswali mawili hapo ya kujiuliza; 1) Hawa Mitume na Manabii ni akina nani na 2) Huo msingi ni nini?
1) Mitume na Manabii:
Mitume na Manabii wanaozungumziwa hapa katika Waefeso 2:20 sio hawa waliopo sasa, Bali ni wale walioandika biblia, kama Musa, Yeremia, Hosea, Ezekieli na Malaki vile vile mitume wale 12 wa Bwana pamoja na wengine kama akina Paulo, ambao waliandika biblia.
Mtu yeyote aliyepo sasa, au atakayekuja kutokea na kujiita mtume au nabii, basi afahamu kuwa andiko hilo la Waefeso 2:20 halimhusu hata kidogo. Na shetani amewapandikiza watu wengi kiburi (watu wanaojulikana kama mitume na manabii wa leo), na kuanza kujivuna kuwa wao ndio Msingi wa kanisa.. Jambo ambalo si la kweli hata kidogo.
2) Msingi
Msingi ambao sisi tumejengwa juu yake ni ule waliokuwa nao Mitume, ikiwa na maana kuwa kile Mitume walichokifanya msingi, ndicho hicho hicho sisi (kanisa la Mungu) tunajengwa juu yake. Sasa ni kitu gani Mitume na Manabii wa kwenye biblia walikifanya msingi?… Hicho si kingine zaidi ya YESU KRISTO MWENYEWE!!!. Huyu ndiye Msingi wa kanisa na ndiye aliyekuwa msingi wa mitume, na ndio msingi wetu sisi na bado ataendelea kuwa msingi siku zote.
1Wakorintho 3:11 “Maana msingi mwingine hakuna mtu awezaye kuuweka, isipokuwa ni ule uliokwisha kuwekwa, yaani, YESU KRISTO”.
YESU KRISTO ndio Mwamba ule ambao yeye mwenyewe alisema kuwa kanisa lake litajengwa juu yake.
Mathayo 16:13 “Basi Yesu akaenda pande za Kaisaria-Filipi, akawauliza wanafunzi wake akasema, Watu hunena Mwana wa Adamu kuwa ni nani?
14 Wakasema, Wengine hunena u Yohana Mbatizaji, wengine Eliya, wengine Yeremia au mmojawapo wa manabii.
15 Akawaambia, Nanyi mwaninena mimi kuwa ni nani?
16 Simoni Petro akajibu akasema, WEWE NDIWE KRISTO, MWANA WA MUNGU ALIYE HAI.
17 Yesu akajibu, akamwambia, Heri wewe Simoni Bar-yona; kwa kuwa mwili na damu havikukufunulia hili, bali Baba yangu aliye mbinguni.
18 Nami nakuambia, Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala milango ya kuzimu haitalishinda”.
Umeona? Mwamba unaonenewa hapo sio Petro bali ni yeye YESU MWENYEWE!.. yaani huo Ufunuo Petro alioupata wa YESU KUWA MWANA WA MUNGU Ndio MSINGI, na NDIO MWAMBA ambao kanisa litajengwa juu yake.
Kanisa lolote leo ambao YESU sio kiini cha Imani hiyo, hilo sio kanisa la kweli, vile vile imani yoyote ile isiyomweka YESU kama msingi badala yake inawemweka mwanadamu mwingine au mnyama au sanamu basi imani hiyo ni imani ya Uongo n.k
Mahubiri yoyote yasiyomweka YESU msingi, hayo ni mahubiri kutoka kwa Yule adui.
Mtumishi yoyote Yule, awe mchungaji, mwalimu, mtume, nabii au mwinjilisti asiyemweka YESU kama kiini na kitovu cha Mafundisho huyo si wa kweli, kwa mujibu wa maandiko.
Vile vile mtu yeyote ajiitaye Mkristo na Yesu si msingi wa maisha yake, huyo ni mkristo jina tu wa uongo.
Bwana atusaidie tumweke Yesu msingi wa maisha yetu.
Maran atha!.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Je huduma za mitume na manabii, zinaendelea kufanya kazi hadi sasa?
Nitamjuaje nabii wa Uongo?
Wana wa Manabii walikuwa ni watu gani?
Jibu: Tusome..
Wafilipi 3:2 “Jihadharini na mbwa, jihadharini na watendao mabaya, jihadharini na wajikatao”
Hapa kuna makundi matatu yaliyotajwa ambayo tunapaswa tujihadhari nayo, kundi la Kwanza ni “MBWA” kundi la Pili ni “WATU WAJIKATAO” na kundi la tatu ni “WATU WATENDAO MABAYA”.
Sasa kabla ya kwenda kuangalia Mbwa ni watu wa namna gani, kwanza tuyatazame haya makundi mawili ya mwisho, ambayo ni watu wajikatao na watenda mabaya..
Watu “watendao mabaya” wanaozungumziwa hapo, ni watu walio ndani ya imani lakini wanatenda mabaya.. watu hawa biblia imetuonya tujihadhari nao, yaani tusichangamane.. Mtume Paulo alizidi kuliweka hili vizuri katika kitabu cha 1Wakorintho 5:9-11.
1Wakorintho 5:9 “Naliwaandikia katika waraka wangu, kwamba msichangamane na wazinzi.
10 Sisemi msichangamane kabisa na wazinzi wa dunia hii, au na wenye kutamani, au na wanyang’anyi, au na wenye kuabudu sanamu; maana hapo ingewalazimu kutoka katika dunia.
11 Lakini, mambo yalivyo, naliwaandikia kwamba msichangamane na mtu aitwaye ndugu, akiwa ni mzinzi au mwenye kutamani au mwenye kuabudu sanamu au mtukanaji au mlevi au mnyang’anyi; mtu wa namna hii msikubali hata kula naye”.
Lengo la kutochangamana na makundi haya ya watu walio ndani ya kanisa lakini ni watenda mabaya, ni ili wajisikie aibu kwa wanayoyafanya na hatimaye wageuke na kutubu.
Kundi la Pili: Ni “Watu Wajikatao”.. kumbuka hapa anasema “watu wajikatao” na sio “watu wajikataao” kuna tofauti ya kujikata na kujikataa.. hapa wanazungumziwa watu wanaojikata!.. Sasa ni watu gani hao wanaojikata?.. si wengine bali walikuwa ni wayahudi ambao walikuwa wanashinikiza tohara, kuwa ndio dalili ya kukubaliwa na Mungu..
Lilikuwepo kundi la walioamini, ambao hata sasa lipo lililokuwa linasisitiza tohara kuwa ni jambo la lazima, na kwamba mtu asipotahiriwa hawezi kukubaliwa na Mungu. Watu hawa walikuwa kweli wamemwamini Yesu lakini sheria za torati bado zilikuwa zinawaendesha, ambazo kimsingi hizo haziwezi kumkamilisha mtu, bali Neema ya Yesu pekee… kushika mwezi, mwaka, siku, sabato haya yote hayafai katika kumkamilisha mtu.
1Wakorintho 7:19 “Kutahiriwa si kitu, na kutokutahiriwa si kitu bali kuzihifadhi amri za Mungu.
20 Kila mtu na akae katika hali ile ile ambayo alikuwa nayo alipoitwa”
Kwa maelezo mengine marefu kuhusiana na watu wajikatao unaweza kufungua hapa >>> WATU WAJIKATAO
Na kundi la Tatu na la Mwisho, ambalo biblia imetaja tujihadhari nalo ni kundi la “MBWA”.
Sasa utajiuliza hawa “Mbwa” ni akina nani?
Bwana Yesu aliwataja wazi kabisa hawa Mbwa ni wakina nani.. Tusome..
Mathayo 7:15 “Jihadharini na MANABII WA UONGO, watu wanaowajia wamevaa mavazi ya kondoo, walakini kwa ndani ni MBWA-MWITU WAKALI.
16 Mtawatambua kwa matunda yao. Je! Watu huchuma zabibu katika miiba, au tini katika mibaruti”
Umeona?… Kumbe Mbwa wanaozungumziwa hapo ni “Manabii wa Uongo” na tena hawajatwi kama Mbwa tu!, bali kama “Mbwa-Mwitu” tena wakali!.. maana yake wasiohurumia kundi.. Na hatutawatambua kwa mionekano yao, kwasababu kwa nje wamevaa mavazi ya kondoo, (wanafanana na watumishi wa kweli wa Mungu) lakini tutawatambua kwa matunda yao, maana yake kwa yale wanayoyafundisha na wanayoyaishi.
Na manabii wa uongo ni mjumuisho wa Mitume wa Uongo, wachungaji wa uongo, waalimu wa Uongo, pamoja na waimbaji wa Uongo. Kwaufupi watu wote wanaosimama kutangaza injili kwa wengine! Lakini maisha yao ya ndani si wakristo, ila kwa nje wanasifika kama watumishi wa Mungu.
Ikiwa mtu atasimama na kuhubiri injili nyingine tofauti na ile iliyoandikwa katika biblia, basi huyo kibiblia ni “Mbwa”, ikiwa mtu atahubiri injili isiyo ya wokovu, badala yake ya kumpoteza mtu au kumfanya afurahie dhambi..mtu huyo kibiblia ni Mbwa, na tumetahadharishwa kukaa mbali naye.
Nabii wa Kweli wa Mungu atakuwa kama Musa!, Mpole kuliko wote, na mwenye kuwaelekeza watu kwa Mungu na si kwake wala kwa shetani.
Kumbukumbu 13: 1 “Kukizuka katikati yako nabii, au mwotaji wa ndoto, akikutolea ishara au ajabu,
2 ikatukia hiyo ishara au hiyo ajabu aliyokuambia akisema, Na tuifuate miungu mingine usiyoijua, tuitumikie hiyo;
3 wewe usiyasikize maneno ya nabii yule, au yule mwotaji wa ndoto, kwa kuwa Bwana, Mungu wenu, yuawajaribu, apate kujua kwamba mwampenda Bwana, Mungu wenu, kwa mioyo yenu yote na roho zenu zote.
4 Tembeeni kwa kumfuata Bwana, Mungu wenu; mcheni na kushika maagizo yake na kuisikia sauti yake, nanyi mtumikieni na kushikamana naye”
Je! Unaongozwa na nani?.. Manabii wa Uongo, Miujiza na Ishara au NENO LA MUNGU?.
Kumbukumbu 6:4 “Sikiza, Ee Israeli; Bwana, Mungu wetu, Bwana ndiye mmoja.
5 Nawe mpende Bwana, Mungu wako, kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa nguvu zako zote”.
Maran atha!
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Watu wajikatao ni watu wa namna gani? (Wafilipi3:1).
Mstari huu una maana gani? “Tupa chakula chako usoni pa maji; Maana utakiona baada ya siku nyingi”. (Mhubiri 11:1)Kutekewa maana yake nini?(Mathayo 22:12)
Mungu anatufundisha kusamehe mara saba sabini, ila Kwanini yeye hakumsamehe Adamu alipoasi?.
HAKUONA MAHALI PA KUTUA KWA WAYO WA MGUU WAKE.
Jibu: Tusome kuanzia mstari wa 8 ili tuweze kuelewa vizuri..
Mathayo 22:8 “Kisha akawaambia watumwa wake, Arusi i tayari, lakini wale walioalikwa hawakustahili.
9 Basi enendeni hata njia panda za barabara, na wote mwaonao waiteni arusini.
10 Watumwa wale wakatoka wakaenda njia kuu, wakakusanya wote waliowaona, waovu kwa wema; arusi ikajaa wageni.
11 Lakini alipoingia yule mfalme ili kuwatazama wageni wake, akaona mle mtu mmoja asiyevaa vazi la arusi.
12 Akamwambia, Rafiki, uliingiaje humu nawe huna vazi la arusi? NAYE AKATEKEWA”.
“Kutekewa” kunakozungumziwa hapo si Kutekewa maji au kinywaji fulani, hapana!…Bali maana yake Ni “KUKOSA MANENO”…
Mtu anayekosa Neno la kujibu pale anapoulizwa, mtu huyo Ndio katekewa..
Katika habari hiyo Bwana Yesu anatoa mfano wa mtu aliyeishiwa maneno baada ya kukutwa hana vazi la harusi.
Hali itakayokuwa kwa wengi katika Ile siku ya mwisho. Maandiko yanaonyesha kuwa katika siku ya mwisho, Bwana atawakataa watu wengi, ambao hawakuwa na vazi la Harusi walipokuwa duniani.
Na vazi la harusi maandiko yameweka wazi kuwa Ni “Matendo ya haki ya watakatifu”.
Ufunuo 19:8 “Naye amepewa kuvikwa kitani nzuri, ing’arayo, safi; kwa maana kitani nzuri hiyo ni matendo ya haki ya watakatifu”
Katika siku ile wengi watadhani Ni dini zao zintakazowapa kibali Cha kuingia uzimani, wengine watadhani Ni Imani zao n.k. pasipo kujua kuwa bila utakatifu hakuna mtu atakayemwona Mungu.
Waebrania 12:14 “Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na huo utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao”
Na Utakatifu hatuupati kwa nguvu zetu, Bali kwa msaada wa Bwana.
Tunapotubu kwa kudhamiria kabisa kuacha dhambi zetu, na kubatizwa katika ubatizo sahihi Kama bado hatujabatizwa Basi Bwana anatupa Roho wake mtakatifu ambaye huyo ndiye atakayetusaidia sisi kuweza kuwa wakamilifu na watakatifu.
Hivyo tukiupata utakatifu katika maisha yetu, Basi katika Roho tutaonekana mbele zake tumevaa vazi la harusi na hivyo siku Ile hatutatekewa mbele zake, hatutaishiwa maneno.
Lakini tukiyakosa hayo, huku tukitumainia dini zetu, na madhehebu yetu, na theologia zetu… basi tujue kuwa tutakosa cha kujibu mbele zake siku Ile..
Mathayo 7:21 “Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.
22 Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi?
23 Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu”.
Maran atha!
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
BALI WANA WA UFALME WATATUPWA NJE!.
TAFUTA KWA BIDII KUWA MTAKATIFU.
Je! Ni halali kuoa/kuolewa na mtu ambaye tayari anao watoto?
Jibu: Adhabu iliyompata Adamu na Hawa, haikutokana na hasira ya Mungu!.. bali ilikuwa ni matokeo ya walichokifanya.
Hebu tafakari mfano huu…. “unamwonya mtu asile kitu Fulani kwasababu unajua madhara ya hicho kitu kwamba endapo akikila basi kitamsababishia apofuke macho na hata kufa huko baadaye, kwasababu kina sumu mbaya ndani yake”.
Lakini huyo mtu ambaye ulimtahadharisha asifanye hivyo, hakukusikiliza wewe badala yake akaenda kula hicho kitu ambacho madhara yake ni kupofuka macho na hata kufa. Na siku alipokula wewe ukajua na kwa huzuni ukaenda kumwuliza kwanini ulikula?..yeye akatoa sababu zake anazozijua yeye, kisha wewe ukamwambia kwamba.. “kwasababu umekula hicho kitu basi macho yako yatapofuka siku si nyingi na pia utakufa!.
Sasa swali ni je!, kwa wewe kumwambia hivyo kwamba “atapofuka macho na kufa” je umemhukumu, au umemwambia tu mambo yatakayompata kutokana na kitu alichokifanya?.. Au je kwa wewe kumwambia hivyo, kuna uhusiano wowote wa wewe kumsamehe au kutomsamehe?.. Jibu ni la!, wewe umemwambia tu madhara ya alichokifanya na kuanzia pale utaanza kumhurumia na kumtafutia suluhisho ili ile sumu iliyoingia ndani yake iweze kutoka….
Ndicho kilichotokea pale Edeni, adhabu aliyoipata Adamu na Hawa ni kwasababu ya matokeo ya walichokifanya na si kwasababu ya hasira ya Mungu!!. Na Mungu kwa huruma zake, kuanzia pale ndio akaanza mpango wa kumponya mwanadamu kwa madhara aliyoyaingiza katika maisha yake.
Na ndipo akapata mpango bora, ambao huo utaondoa moja kwa moja madhara yaliyoingia ndani ya Mwanadamu, na mpango huo si mwingine zaidi ya ule wa kumtoa Mwanawe wa pekee YESU KRISTO, aje kufa kwa ajili ya dhambi zetu, na kutukomboa, kuanzia hapo Mungu akamtoa Adamu pale Edeni ili amweke katika mpango mpya na ulio kamili, utakaomkamilisha.
Yesu Kristo pekee ndiye tiba ya KIFO ambacho kilikuwa kimeingia katika maisha yetu tangu siku ile wazazi wetu, Adamu na Hawa walipoasi.
Yohana 11:25 “Yesu akamwambia, Mimi ndimi huo ufufuo, na uzima. Yeye aniaminiye mimi, ajapokufa, atakuwa anaishi”
Yesu Kristo ndiye tiba ya mambo yote, ndiye suluhisho la matatizo yote ya maisha, na pasipo yeye sisi hatuwezi kufanya lolote.
Yohana 15:5 “Mimi ni mzabibu; ninyi ni matawi, akaaye ndani yangu nami ndani yake, huyo huzaa sana; maana pasipo mimi ninyi hamwezi kufanya neno lo lote”.
Na nje ya Yesu Kristo hapana wokovu..
Matendo 4:12 “Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo”
Je! Umempokea Yesu katika maisha yako?.. je umebatizwa katika ubatizo sahihi? Je umepokea Roho Mtakatifu wa kweli?. Kama bado unasubiri nini?
Maran atha!
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
JUMA LA SABINI (70) LA DANIELI
KWANINI YESU NI ADAMU WA PILI?
NAFASI YA MWANAMKE KATIKA KANISA
BASI TUENDELEE KUMJUA MUNGU,NAYE ATATUJILIA KAMA MVUA YA VULI.
Maandiko yanaonyesha kuwa YESU ni Mungu na pia ni NABII. Ni sawa na mkuu wa nchi anaweza kuwa RAISI kwa wananchi, lakini pia anaweza kuwa BABA au MAMA kwa watoto wake. Hivyo mtu mmoja anaweza kuwa na vyeo zaidi ya kimoja kufuatana na mazingira aliyopo. Raisi akiwa ofisini ataitwa Raisi, akiwa nyumbani kwake na watoto wake ataitwa Baba/mama.
Vile vile Kristo akiwa mbinguni ni Mungu, akiwa duniani ni Mwana wa Adamu na Nabii na Mwokozi, na akiwa ndani yetu ni Roho Mtakatifu.
Sasa ni wapi maandiko yanatuonyesha kuwa Yesu alikuwa ni Nabii?
Luka 24:19 “Akawauliza, Mambo gani? Wakamwambia, Mambo ya Yesu wa Nazareti, ALIYEKUWA MTU NABII, mwenye uwezo katika kutenda na kunena mbele za Mungu na watu wote”
Kumbukumbu 18:15 “Bwana, Mungu wako, atakuondokeshea nabii miongoni mwa ndugu zako kama nilivyo mimi; msikilizeni yeye”.
Vile vile ni wapi maandiko yanatuonyesha kuwa Yesu alikuwa Mwana wa Mungu?
Mathayo 16:15 “Akawaambia, Nanyi mwaninena mimi kuwa ni nani?
16 Simoni Petro akajibu akasema, Wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai.
17 Yesu akajibu, akamwambia, Heri wewe Simoni Bar-yona; kwa kuwa mwili na damu havikukufunulia hili, bali Baba yangu aliye mbinguni”
Na ni wapi maandiko yanatuonyesha kuwa YESU alikuwa Mungu?
Tito 2:13 “tukilitazamia tumaini lenye baraka na mafunuo ya utukufu wa Kristo Yesu, Mungu mkuu na Mwokozi wetu”
Soma pia 1Timotheo 3:16 na Yohana 1:1.
Kwahiyo Yesu ni yote katika vyote, na ndio Mwokozi wa Ulimwengu, na ndiye Njia ya kufika mbinguni. Hakuna mwanadamu yeyote atakayefika mbinguni isipokuwa kwa njia yake yeye.
Je umempokea Yesu?.. Kama bado unasubiri nini?
Bwana akubariki.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Bwana Yesu alikufa akiwa na umri gani?
Je shetani anaweza kushusha moto kutoka mbinguni?
Tofauti kati ya maandiko na Neno ni ipi?
KUMBE MUNGU ANAWEZA KUKULIPA KWA USICHOSTAHILI!
Mathayo 6:30 “Basi, ikiwa Mungu huyavika hivi majani ya kondeni, yaliyopo leo, na kesho hutupwa kalibuni, je! Hatazidi sana kuwavika ninyi, enyi wa imani haba?”
Neno hili “kalibu” limerudiwa pia kutajwa katika Luka 12:28, na maana ya neno hili ni “TANURU LA MOTO”. Kwa kawaida baada ya kusafisha mazingira, kwa kuondoa Nyasi au takataka huwa zinatupwa katika tanuru la moto, sasa tanuru hilo ndilo linaloitwa “Kalibu”, Na Bwana Yesu alitoa mfano huo kuonyesha maisha yetu jinsi yalivyo na thamani mara nyingi zaidi kuliko maua ya kondeni.
Kwani kama Mungu anavyoyavika utukufu maua ya kondeni, kwa rangi rangi zake za kuvutia, basi sisi ni zaidi sana mbele zake kuliko hayo MAUA ya kondeni, ambayo leo yapo lakini kesho yanatupwa motoni.. Sisi tuna thamani mbele zake kuliko maua, maana yake sisi atatuvisha zaidi kuliko Maua, atatulisha zaidi kuliko ndege, atatubariki kuliko viumbe vyote vya asili. Huo ni upendeleo wa kipekee sana.
Tunachopaswa kufanya ni kuutafuta tu ufalme wake na haki yake, halafu hayo mengine ya chakula, mavazi tumwachie yeye, kasema atatuzidishia, na yeye kamwe hawezi kusema uongo.
Luka 12:29 “Ninyi msitafute mtakavyokula wala mtakavyokunywa; wala msifanye wasiwasi,
30 kwa maana, hayo yote ndiyo watafutayo mataifa ya duniani, lakini Baba yenu anajua ya kuwa mna haja na hayo.
31 Bali utafuteni ufalme wa Mungu, na hayo mtaongezewa.
32 Msiogope, enyi kundi dogo; kwa kuwa Baba yenu ameona vema kuwapa ule ufalme”
Maran atha!
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Je suruali ni vazi la kiume tu?
Wakati wakina Shadraka wanatupwa katika tanuru la moto, Danieli alikuwa wapi?