Category Archive Uncategorized @sw-tz

Sala ya Toba na Rehema.

Ni jambo jema kutafuta sala ya toba na rehema, angali muda upo.

Inawezekana umemkosea Mungu sana, na leo unatamani kujua kama ipo njia ya kumrudia yeye tena, inawezekana, umeua, au umetoka nje ya ndoa, au umetoa mimba, umemtukana Mungu, umeiba, umeenda kwa waganga, umewavunjia heshima wazazi wako, umeaudhi watu wengine n.k.

Inawezekana pia wewe ni mmojawapo wa ambao wameona kuendelea kuishi Maisha bila Mungu ni kupotea tu, na umeamua sasa uutafute uso wake. Basi kama wewe ni mmojawapo, uamuzi ulioufikiria ni mzuri sana, Na yapo makusudi makubwa sana Mungu kukufikisha mahali hapa,

Bwana Yesu alisema..

Yohana 6:37  “Wote anipao Baba watakuja kwangu; wala ye yote ajaye kwangu sitamtupa nje kamwe”.

Kama leo umeamua kudhamiria kweli kutubu dhambi zako, basi ni ahadi yake kuwa hatakutupa nje kamwe! Kuanzia huu wakati na kuendelea utaona maajabu makubwa sana katika Maisha yako kama ilivyokuwa hata kwetu.

Kinachohitajika ni wewe tu, kumaanisha kabisa kutoka katika moyo wako kwamba kuanzia leo, wewe na dhambi basi! Ulimwengu nyuma Yesu mbele, hilo tu, pekee linatosha wewe kuupokea wokovu wa Bwana..Anataka kukusamehe lakini ni mpaka pale wewe utakapojutia na kusema mimi ninauaga ulimwengu kwa miguu yote miwili.

Wengi wanadhani ni sala Fulani tu, ndio inayompa mtu wokovu, hapana, nitakuonyesha sehemu kwenye biblia mwanamke mmoja mwenye dhambi nyingi (kahaba) kwa kujutia tu makosa yake, mpaka kulia machozi mengi sana mbele za Yesu..Hilo peke yake lilitosha kwa Yesu kuuona moyo wake uliomaanisha kutubu  na saa ile ile Yesu akamwambia, UMESAMEHEWA DHAMBI ZAKO. Soma (Luka 7:36-48), utathibitisha hilo.

Hivyo hata na wewe leo ukitia Nia kweli kweli, basi sala fupi nitakayokuambia uiombe  hapo mbele kidogo, italeta mabadiliko makubwa sana katika Maisha yako ya rohoni. Kwasababu moja kwa moja Kristo anakwenda kuingia ndani  yako kukubadilisha, na kuanzia huu wakati na kuendelea ataendelea kuwa na wewe kukusaidia kushinda na baadhi ya yale mambo ambayo ulikuwa huwezi.

Hivyo kama upo tayari kutubu leo dhambi zako, basi

Basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie maisha yako yote kama ilivyokuwa hata kwetu sisi. Sasa unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Yesu mwokozi yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU  MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.

AMEN.

Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako.

Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.

Pia unaweza kuihifadhi tovuti yetu hii , katika kumbukumbu zako (www.wingulamashahidi.org), ili wakati mwingine ikusaidie, kwani yapo mafundisho mengi Zaidi ya 1000  na maswali mengi ya biblia yaliyojibiwa, ambayo unaweza ukajifunza na kuimarika kiroho sana, ukiwa hata hapo hapo nyumbani kwako kwenye simu yako.

Ubarikiwe sana

Mada Nyinginezo:

TOBA IGUSAYO MOYO WA BWANA.

YESU MPONYAJI.

WAKAKAA KWAKE SIKU ILE. NAYO ILIKUWA YAPATA SAA KUMI.

UMEFUMBULIWA MACHO YAKO YA KIROHO?

NINI KINATOKEA BAADA YA KIFO?

MKATAE SHETANI NA MAWAZO YAKE YA KIBINADAMU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Je! Ni kweli kuna samaki mtu (Nguva) Baharini.

Ndio yupo samaki ajulikanaye kama nguva, kwa lugha ya kiingereza anaitwa Sea cow, kwa maelezo yake marefu juu ya mwonekano wake na jinsi anavyozaa, na kuishi baharini msome Wikipedia kwa link hii>> https://sw.wikipedia.org/wiki/Nguva

Lakini huyu samaki nguva sio kama wale watu wanaomaanisha kwamba anakiwili wili cha mwanadamu na mkia wa samaki (samaki mtu).. Katika uumbaji wa Mungu hakuna kiumbe kama hicho, wala huwezi kukikuta katika bahari yoyote duniani.

Viumbe hawa walianza kuzungumziwa tangu zamani kwenye hadithi za kimila za mataifa mbali mbali,huko Asia na Ulaya lakini katika maisha halisi hawapo, wengine wanasema samaki hao wanaweza wakaongea kama mwanadamu, lakini hilo jambo ni batili.

Katika Biblia kiumbe kama huyu hajatajwa, aliyetajwa ambaye kidogo aliweza kumkaribia mwanadamu ni NYOKA peke yake, Na hiyo ilikuwa ni kabla hajalaaniwa(Mwanzo 3:1)..Yeye ndiye aliyekuwa mwerevu kuliko wanyama wote mwituni, aliweza kuongea kama mtu, na alikuwa anatembea kwa miguu, lakini alipolaaniwa ndio akawa nyoka huyu ambaye tunayomwona sasa, anatembea kwa matumbo, hata akili yoyote.

Kwahiyo baada ya hapo hakukuwa na kiumbe mwingine yeyote aliyemkaribia mwanadamu.

Lakini pia ni vizuri kufahamu, mambo mengi sana ya ki-pepo, yanahushishwa na hivi viumbe vya kudhaniwa wasio halisi.. kwamfano Dragoni, joka lenye vichwa saba litoalo moto mdomoni, ni mungu wa jamii Fulani huko Asia, hususani China, ambaye kiuhalisia nyoka huyo hayupo duniani, fuatilia tena tembo mwenye mikono mingi huko India, samaki mtu, n.k.

Hivyo kuwa makini na elimu kama hizo, ni rahisi kushawishiwa kuwa viumbe kama hao wapo, na kupewa maelekezo jinsi ya kuwaona au kukutana nao, kumbe hujui ndivyo unavyoingizwa katika elimu za mashetani na mwisho wa siku unazama kabisa huko, unadhani umefanikiwa kuwaona kumbe ni mapepo yaliyojigeuza kwa mfano wa hivyo viumbe visivyo halisi..

Hizi ni siku za mwisho za hatari biblia inasema..

1 Timotheo 4 :1 “Basi Roho anena waziwazi ya kwamba nyakati za mwisho wengine watajitenga na imani, wakisikiliza roho zidanganyazo, na mafundisho ya mashetani;”

Unaona? Mafundisho ya mashetani yamezaa kila kona..Na kama husomi biblia yako, basi upo hatarini kuchukuliwa nayo moja kwa moja..Je! Umempa Yesu maisha yako? Kama sivyo unasubiri nini, huoni kama upo hatarini? Kumbuka hizi ni nyakati za mwisho. Ni heri ukayasalimisha maisha yako kwake, na yeye ni mwaminifu atakuokoa na kukusamehe makosa yako yote, haijalishi ulifanya dhambi kiasi gani.

Ubarikiwe.

Group la whatsapp Kwa mgawanyo bora wa masomo download App hapa>> App wingu la mashahidi

Mada Nyinginezo:

TAZAMA, NASIMAMA MLANGONI.

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

 

MAFUNDISHO YA MASHETANI

NAO WATAKAOUAWA NA BWANA WATAKUWA WENGI.

ZIKIMBIE TAMAA ZA UJANANI! NA MTU YEYOTE ASIUDHARAU UJANA WAKO.

PARAPANDA ITALIA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

PARAPANDA ITALIA.

Siku moja inapopita, ndivyo tunavyoikaribia ile siku kuu ya kwenda mbinguni, siku ile ya Parapanda kulia, ambapo watakatifu wote duniani wataisikia, hakika itasikiwa na wao tu, na sio kila mtu duniani kama wengi wetu tunavyodhani…Watu wenye dhambi wakati huo hawataisikia parapanda hiyo hata chembe..

Siku hiyo pengine itakuwa ni asubuhi kwa upande wetu, au jioni au  usiku wa manane ukiwa umelala.. Kama wewe ni mtakatifu utasikia sauti nzuri ya shangwe, ikiambatana na parapanda ya Mungu, na wale wafu waliokufa katika Kristo, wao nao pia wataisikia kutoka kule makaburini, na kufufuka na kuanza kutembea duniani, na wewe utawaona, halafu ghafla, tutaliona jeshi kubwa la malaika likitokea, likiambatana na Bwana, na wakati huo huo ghafla tutaona miili yetu ikibadilishwa kutoka katika miili hii ya unyonge ya mauti na kuwa miili ya utukufu, wakati hilo likuwa linaendelea katika kipindi kifupi sana cha kufumba na kufumbua tutajikuta mawinguni na Bwana YESU, huo ndio wakati tutaenda naye kule mbinguni kula naye ile karamu ya mwana kondoo aliyokwenda kutuandalia miaka 2000 iliyopita.

Unaweza kudhani jambo hilo ni bado sana, lakini nataka nikuambie mimi na wewe tunaishi katika yale majira ya kuja kwa Bwana mara ya pili. Dalili zote zinaonyesha, Angalia milipuko ya magonjwa mfano wa Tauni (Corona) yaliyotabiriwa na Bwana Yesu yakitokea ulimwenguni (Luka 21:11)..Hiyo ni dalili ya kwamba tupo ukingoni mwa wakati kuliko tunavyoweza kudhani, angalia tena kuchipuka kwa taifa la Israeli, yaani mtini, ndio kunathibitisha kabisa wakati wa majira ya mataifa(yaani mimi na wewe) upo ukingoni.

Jambo ambalo wakristo wengi hatufahamu, ni pale tunapodhani Mungu ana ile kauli ya “wengi wape”..Yaani, kwasababu ulimwengu huu uliojawa na uovu na waovu wengi Mungu hawezi kuuangamiza au kunyakua wale wachache walio waaminifu kwake..

Yesu alisema kama ilivyokuwa katika siku za Nuhu, na kama ilivyokuwa katika siku za Lutu, jiulize, waliookoka katika siku za Nuhu walikuwa ni wangapi kama sio 7 tu katika ya mabilioni ya watu waliokuwa ulimwenguni, vilevile waliookoka katika siku za Lutu walikuwa wangapi kama sio watatu katika ya Malaki ya watu waliokuwa katika miji ile ya Sodoma na Gomora,

Ukitazama tena kwa ukaribu utaona aliye nyakuliwa alikuwa  ni mtu mmoja tu (HENOKO) kati ya watu wote waliokuwa wanaishi kipindi chote kabla ya gharika, kwasababu ni yeye tu peke yake ndiye aliyempendeza Mungu.

Vivyo hivyo katika wakati huu watakaonyakuliwa ni wale tu watakaompendeza Mungu, hao ndio peke yao watakaosikia Parapanda ya Mungu ikilia kutoka mawinguni, hata kama watakuwa ni watu 100 katika ulimwengu mzima, hao tu ndio watakoenda, wengine wote waliosalia hawatajua chochote, watashangaa tu mbona kundi dogo la watu wachache sana halipo duniani..

Wengine watadhani, wameibiwa tu, wengine watadhani wametoroka, n.k. Lakini ulimwengu hautaelewa chochote kwasababu litakuwa ni kundi dogo sana, kumbe hawajui wenzao siku nyingi tayari wapo mbinguni wakila karamu ya mwana kondoo, lakini huku chini kitakachokuwa kinaendelea ni dhiki kuu ya mpinga Kristo. Na baada ya hapo ni maangamizo.

1Wathesalonike 4:16  “Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko, na sauti ya malaika mkuu, na parapanda ya Mungu; nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza.

17  Kisha sisi tulio hai, tuliosalia, tutanyakuliwa pamoja nao katika mawingu, ili tumlaki Bwana hewani; na hivyo tutakuwa pamoja na Bwana milele.

18  Basi, farijianeni kwa maneno hayo.”

Ndugu yangu jiulize, Yesu akirudi leo utakuwa katika upande upi? Na injili zote hizi ulizosikia utajitetea vipi siku ile kusema hujaambiwa? Ishara zote hizi za siku za mwisho utajitetea vipi siku ile mbele za Mungu? Mungu ni mwingi wa rehema lakini pia ana ghadhabu nyingi.

Ili kufahamu vizuri ni jinsi gani tunaishi katika siku za mwisho angalia MADA nyingine, mwisho kabisa wa somo hili, uone ni wakati gani huu tunaishi..

Kama hujaokoka, basi huu ndio wakati wako wa kuyatengeneza mambo yako na Kristo, ili kusudi kwamba hata ikitokea paraparanda italia leo usiku basi uwe na uhakika kuwa na wewe utakwenda kumlaki mawinguni. Unachopaswa kufanya ni kukusudia tu kumkaribisha Yesu maishani mwako, kwa kutubu dhambi zako kwa kumaanisha kabisa kuziacha, na kuwa tayari kuyaanza Maisha mapya  ya wokovu.

Kama utamaanisha kufanya hivyo ni ahadi yake kuwa atakuja ndani yako na wewe kuanzia huo wakati utaanza kuona badiliko kubwa ndani yako, hivyo kama upo tayari kufanya hivyo sasa,

Basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie maisha yako yote kama ilivyokuwa hata kwetu sisi. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU  MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.

AMEN.

Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.

Ubarikiwe sana.

Tazama mada nyingine chini zinazoeleza Habari za kurudi kwa Kristo duniani..

Mada Nyinginezo:

UNYAKUO.

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

MAONO YA NABII AMOSI.

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

RAFIKI MWEMA.

Rafiki mwema ni nani?


Uzuri ni kwamba kila mmoja wetu alishawahi kuwa na rafiki au marafiki katika maisha yake.. Kama ulishawahi kuwa na marafiki wengi utagundua kuwa wengine walikuwa marafiki zako kwasababu mliendana tu tabia hivyo tu,, na  wengine walikuwa marafiki kutokana na maslahi Fulani au mazingira Fulani au fursa Fulani, labda shuleni,  au kwenye biashara au kazini, au katika mambo ya kiimani n.k…

Kati ya hao wapo ambao ni wa kudumu yaani mnaweza kupotezana hata kwa muda mrefu lakini urafiki wenu ukadumu palepale, au mazingira Fulani yakatokea aidha ya kutofautiana kipato lakini bado urafiki wenu ukaendelea kudumu,  na wapo ambao ni wa muda tu, kukitokea kutengana kidogo, au mazingira Fulani kubadilika basi urafiki huo unakufa hapo hapo..

Lakini kwa vyovyote vile katika makundi yote hayo swali ni je utawezaje kumtambua rafiki mwema?

Jibu ni rahisi rafiki mwema, ni Yule ambaye atauweza kuutoa uhai wake ili wewe upone. Kwamfano, rafiki  yako asikie wewe umelazwa figo zako zote mbili zimekufa upo hoi kitandani mahuti huti, ili uishi ni lazima figo zote mbili zipatikane kutoka kwa watu wengine ili upachikwe wewe uendelee kuishi, Halafu wakati huo huo anatokea rafiki yako, ambaye hana hata undugu na wewe, mlikutana tu mkaendana tabia, mkashirikiana pamoja..

Na sasa anakuambia rafiki yangu, mimi leo hii nimeamua kuzitoa figo zangu zote mbili, ili wewe upone, Unaweza ukajiuliza huyu mtu anawaza nini? Akitoa figo zake sisi yeye atakufa, na itakuwa hasara tu ile ile..Ukizingatia yeye bado anayo malengo yake mengi ya maisha, mimi ninafaida gani kwake? Pengine unamkatalia Lakini yeye bado anakusisitiza kuwa anakwenda kutoa figo zake zote mbili afe ili wewe upone.. Na kweli anakwenda kufanya hivyo. Anatolewa unapewa wewe na yeye muda huo huo anakufa.. Je! Mtu kama huyo si zaidi ya rafiki mwema kwako?

Ukweli ni kwamba Katika ulimwengu mzima hakuna mtu anayeweza kufanya hivyo..

Lakini habari njema ni kwamba yupo ambaye aliweza kufanya hivyo kwa ajili yangu na wewe ili tupone..Na mtu huyo si mwingine zaidi ya YESU, alisema mwenye hivi…

Yohana 15:13 “Hakuna aliye na upendo mwingi kuliko huu, wa mtu kuutoa uhai wake kwa ajili ya rafiki zake.

14 Ninyi mmekuwa rafiki zangu, mkitenda niwaamuruyo”.

Upendo huu ni zaidi ya upendo wa ndugu, Ndugu yako hawezi kuifikia hatua hii, ya kufa ili wewe uokoke, lakini Kristo alikufa ili mimi na wewe tupate uzima wa milele..

Na ndio maana maandiko yanasema..

Mithali 18: 24 Ajifanyiaye rafiki wengi ni kwa uangamivu wake mwenyewe; Lakini yuko rafiki aambatanaye na mtu kuliko ndugu.

Sasa huyu rafiki aambatanaye kuliko ndugu, ndio YESU KRISTO mwenyewe..

Hivyo ukimkaribisha huyu maishani mwako, ni uhakika kuwa utakuwa salama, na hutakuwa na wasiwasi kwamba utapotea tena baada ya hapo, kwasababu yeye tayari alishalipa gharama za upotevu wako kabla hata hujazaliwa. Kwahiyo kama ukimfanya leo kuwa rafiki yako, basi atakuwa rafiki yako kweli kweli, na mema yote utayaona..

Lakini ule mtari wa 14 anasema..

“Ninyi mmekuwa rafiki zangu, mkitenda niwaamuruyo.”

Unaona?  Ili na wewe Yesu awe rafiki yako ni sharti utii anayokuamuru.. Kama ulikuwa ni mwenye dhambi unatubu dhambi zako zote kwa kumaanisha kuziacha, kisha unakwenda kubatizwa katika maji mengi kama alivyotupa  maagizo katika Mathayo 28:19, Na baada ya hapo atakutia muhuri kwa Roho wake Mtakatifu atayemwachilia ndani yako wakati huo huo. Na hapo ndipo utakuwa na uhakika kuwa sasa umeshafanyika kuwa rafiki yake.

Ikiwa upo tayari kufanya hivyo..

Basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie maisha yako yote kama ilivyokuwa hata kwetu sisi. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU  MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.

AMEN.

Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.

Ubarikiwe sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

WAKAKAA KWAKE SIKU ILE. NAYO ILIKUWA YAPATA SAA KUMI.

YESU MPONYAJI.

Maana ya ‘Usimjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake’

KILA MMOJA WENU AJUE KUUWEZA MWILI WAKE.

HAPO NDIPO WATU WALIPOANZA KULIITIA JINA LA BWANA.

HATA NA BARNABA PIA AKACHUKULIWA NA UNAFIKI WAO!!

Rudi Nyumbani:

Print this post

KUTOMZUIA MTOTO WAKO NI DHAMBI.

Shalom, karibu tujifunze biblia…Kuna madhara makubwa sana ya kutombana mwanao..na kumruhusu tu kufanya lolote analojiamulia, kwa kuogopa kuwa atakuchukua…

Mtoto kamwe hawezi kukuchuku! unapomwonya au kumbana.…Hebu jiulize wewe wakati ukiwa mdogo, mzazi wako alipokuzuia au alipokubana ufifanye jambo Fulani je ulimchukia?…ni wazi kuwa hukumchukia zaidi uliona tu ni kama mzazi hakipendi kile kitu na si kwamba hakupendi wewe.

Vivyo hivyo na wewe unapombana mwanao asifanye vitu Fulani Fulani ambavyo unaona vina muelekeo mbaya wa kumletea madhara mwanao huko mbeleni, hufanyi dhambi…unapoona kuna tabia inaanza kukithiri ya kupenda kutazama Tv kwa muda mrefu, usiache kuithibiti hiyo tabia..Unapoona kuna tabia ya kuanza kuzurura zurura…mbane, si kila siku ni ya kwenda kucheza cheza na kutazama Tv, ni lazima ziwepo siku za kujifunza Neno nyumbani, watoto wana vichwa vizuri sana vya kushika mambo/kukariri…Kwahiyo katika hali walizopo ni lazima uwape mistari ya kuishika kichwani, hata kama hawaielewi sasa, lakini itakaa ndani yao kama akiba, watakapokuwa watu wazima itakuwa tayari ipo kichwani, hivyo watakapoanza kuitafakari watakuwa hawana kazi ya pili ya kuikariri tena…

 Na pia ni lazima ziwepo siku za kujisomea masomo ya shuleni wawapo nyumbani, ni lazima yawepo masaa ya kumfundisha mwanao kusaidia vijishuhuli vidogo vidogo..Hata kama hakuna shughuli yoyote ya kusaidia (labda nyumbani wapo wafanya kazi wa kutosha)…usikubali mwanao abweteke, mtengenezee kazi ya kufagia, kupika, kuosha vyombo, kupasi, kufua nguo, kufanya usafi n.k..Pia mtume mahali kama dukani n.k..Na pia unapoona kuna vijitabia vya kiburi na utundu vinaanza basi tumia kiboko kidogo kuvidhibiti…

Mithali 23:13 “Usimnyime mtoto wako mapigo; Maana ukimpiga kwa fimbo hatakufa.

14 Utampiga kwa fimbo, Na kumwokoa nafsi yake na Kuzimu”.

sio dhambi na wala hatakuchukia….Usiusikilize uongo wa shetani moyoni mwako kwamba ukimrudi mwanao atakuchukia…Kamwe watoto hawana chuki, wala vinyongo…

Ukiona mtu anakinyongo na mtu Fulani kwa kitu alichofanyiwa utotoni…kiuhalisia kinyongo hicho kilimwingia baada ya yeye kuwa mkubwa na kukitafakari kile kitu kibaya alichofanyiwa…Lakini katika hali ile ya utoto aliyokuwepo hakuwa na ufahamu huo…Hivyo hata mtoto leo hii ukimwadhibu kwa kosa lolote lile hawezi kukuchukia badala yake atajifunza kutokukifanya kile kitu….na siku atakapokuwa mkubwa ndipo atakumbuka zile adhabu na atakapotafakari kwamba ulikuwa unamwadhibu au ulikuwa unambana kwa kwa faida yake mwenyewe ndipo atakapokupenda zaidi…atasema moyoni mwake kama mama/baba asingenizuia na ile tabia yangu sijui leo ningekuwa wapi..na hivyo atakupenda zaidi kuliko kukuchukia lakini tabia ya kutombana mwanao kwa kuogopwa kuchukiwa…nakuambia ukweli siku mtoto Yule atakapokuwa mtu mzima na kutafakari ni jinsi gani ulivyokuwa unamwangalia tu anapotukana, au anapofanya mambo yasiyofaa pasipo kumwambia chochote atakuchukia na kusema hukuwa unamjali.

Kumbuka Uzao wa Tumbo lako ni thawabu yako mwenyewe…Mtoto uliyepewa ukimtunza vyema ni kwa thawabu yako mwenyewe katika siku za baadaye…

Zaburi 127:3 “Tazama, wana ndio urithi wa Bwana, UZAO WA TUMBO NI THAWABU”.

Mithali 22:6 “Mlee mtoto katika njia impasayo, Naye hataiacha, hata atakapokuwa mzee”.

Pia kama bado hujapata mtoto na umeolewa/umeoa….usiwe na hofu, mwamini Mungu, usijiangalie umri uliopo, hata kama ni miaka 50..wapo waliozaa wakiwa na miaka 90 sembuse wewe mwenye miaka 60?..Kwahiyo wakati wa Mungu ni bora kuliko wa wanadamu..zidi kujitenga na ulimwengu na kuishi maisha ya utakatifu na kumcha Mungu kama kawaida…hayo mengine mwachie Baba, huwa anafanya njia mahali pasipo kuwa na njia, na mahali pasipoonekana dalili….na huwa anarudishaga miaka iliyoliwa na parare kwa watoto wake..Hivyo muamini Mungu na mngojee. Na upatapo mtoto kumbuka siku zote kwamba kutombana kufanya mambo yasiyofaa ni kwa hasara yako mwenyewe na yake pia.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

KAMA ZILIVYOKUWA SIKU ZA NUHU NA ZA LUTU.

USIPUNGUZE MAOMBI.

KWANINI TUNAPASWA TUJIZUIE?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Isaya 43, USIOGOPE!

Isaya 43:1 “Lakini sasa, Bwana aliyekuhuluku, Ee Yakobo, yeye aliyekuumba, Ee Israeli, asema hivi, Usiogope, maana nimekukomboa; nimekuita kwa jina lako, wewe u wangu.

2 Upitapo katika maji mengi nitakuwa pamoja nawe; na katika mito, haitakugharikisha; uendapo katika moto, hutateketea; wala mwali wa moto hautakuunguza.

3 Maana mimi ni Bwana, Mungu wako; Mtakatifu wa Israeli, mwokozi wako, nimetoa Misri kuwa ukombozi wako; nimetoa Kushi na Seba kwa ajili yako.

4 Kwa kuwa ulikuwa wa thamani machoni pangu, na mwenye kuheshimiwa, nami nimekupenda; kwa sababu hiyo nitatoa watu kwa ajili yako; na kabila za watu kwa ajili ya maisha yako”.

Kuhukulu maana yake ni “kutengeneza”..Kwahiyo hapo Bwana anamwambia Yakobo aliyemtengeneza na kumuumba kwamba asiogope!. Yakobo anayezungumziwa hapo sio Yule Yakobo mwana wa Isaka…Yule alishakufa kitambo lakini Yakobo anayezungumziwa hapa ni Taifa la Israeli, Taifa zima la wana wa Israeli ndio linalojulikana kama Yakobo..Na ndilo linaambiwa lisiogope!..wapitapo katika maji mengi Mungu atakuwa pamoja nao.. na katika mito, hawatagharikishwa; na waendapo katika moto, hawatateketea; wala mwali wa moto hautawaunguza..Kwasababu alikuwa wa thamani machoni pa Bwana.

Haya ni maneno machache tu lakini ya faraja kubwa sana…Kama Mungu analikumbuka agano lake na Ibrahimu kwa watu wake Israeli..kamwe hawezi kulisahau agano la mwanawe mpendwa Yesu Kristo, ambaye alikuja kufa kwa ajili yetu sisi na kutufanya kuwa Taifa teule na Takatifu, watu wa milki yake. Agano lake hilo la ukombozi, linatufanya tuonekane wa thamani sana kuliko lile la kwanza. Na hivyo maneno hayo pia yanatuhusu sisi tuliomwamini Yesu, na wewe ambaye utamwamini leo…kwamba USIOGOPE!…Usiogope vitisho vya adui!..usiogope magonjwa!..usiogope shida na majaribu!..Bwana Mungu wako ndiye aliyekuhuluku(yaani aliyekutengeneza)…

Majaribu unayoyapitia sasa ni maji mengi…lakini amesema atakuwa pamoja na wewe!…shida unazozipitia sasa baada tu ya kusimama kiimani ni mafuriko, lakini amesema hayatakugharikisha!..misiba na mateso unayoyapitia sasa ni miali ya moto, lakini amesema haitakuunguza! Hivyo jipe moyo, simama endelea mbele..kwasababu wewe ni wa thamani machoni pake.

Na mwisho amesema “kwa sababu hiyo nitatoa watu kwa ajili yako; na kabila za watu kwa ajili ya maisha yako”…Maana yake ni kwamba maisha yako kwake yanathamani kuliko ya watu wengine wasiomtumainia yeye na Taifa lingine lisilomcha yeye.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

Wenye kubatizwa kwa ajili ya wafu ni wakina nani?

Mtu astahiliye hofu ni yupi?

MWEZI NI ISHARA GANI KWETU?

Rudi Nyumbani:

Print this post

FAHAMU TAFSIRI ZA NDOTO MBALIMBALI.

Ndoto ni eneo ambalo watu wengi wanadanganywa na kupotoshwa Na hiyo yote ni kutokana na kukosa maarifa ya kutosha. Wapo watu wengi mitandaoni, wanaowaeleza watu tafsiri za ndoto mbalimbali zao na mwisho wanaambatanisha na dawa zao za kibishara wakiwadanganya watu kuwa hizo zitaleta suluhisho la matatizo yao.

Wengi wa hao watu kama si wafanyabiashara basi ni waganga wa kienyeji na hawana lolote la kukusaidia zaidi ya kukuongezea matatizo. Kumbuka Ndoto si tatizo la kimwili hivyo hakuna tiba yoyote ya kimwili kama vile dawa ya kunywa au ya kumeza itakayoweza kuleta suluhisho la ndoto zako.

Kwa ufupi Zipo ndoto za aina tatu, 

  1. Zinazotokana na Mungu:
  2. Zinazotokana na shetani
  3. Zinazotokana na mtu mwenyewe.

Ndoto zinazotokana na Mungu zinachukua sehemu ndogo sana ya ndoto zote mtu anazoota kila siku naweza kusema hata asilimia 5 tu ya ndoto zote ulizowahi kuota,..

Vivyo hivyo na za shetani nazo hazina asilimia kubwa ya ndoto unazoziota mara kwa mara.

Lakini ndoto zinazotokana na mtu mwenyewe hizi ndizo zinazochukua sehemu kubwa ya ulimwengu wa ndoto za wanadamu. Na hapa ndipo watu wengi wanapokosa shabaha, wakidhani kila ndoto tu wanayoita ni lazima iwe na tafsiri, au ni lazima iwe imebeba ujumbe maalum.

Sasa hizo aina mbili za kwanza, (yaani ndoto za Mungu, na za Shetani) huwa zinabeba maana kubwa sana rohoni, ili kufahamu jinsi ya kuweza kuzitambua aina hizi za ndoto  fungua hapa..>>> Tofauti kati ya ndoto za Mungu na Shetani

Leo hii nitajikita kuorodheshea baadhi ya ndoto ambazo watu wengi wanaota na hawajui nyingi kati ya hizo zinatokana na mwili wenyewe..

Ukiota Hizi  uzipuuzie, wala usihangaike kutafuta maana zake, kwasabu hizi huwa zinakuja aidha kutokana na shughuli nyingi..

  • Kwamfano wewe ni mkulima, hivyo kila siku kuota upo shambani unalima, au unaota pembejeo au mazao, hilo ni jambo la kawaida…

Soma..

Mhubiri 5:3 “Kwa maana ndoto huja kwa sababu ya shughuli nyingi;..”

  • Au kama akili yako muda wako wote kutwa kuchwa ilikuwa unafikiria masomo tu, basi jua kuota unafanya mitihani litakuwa  ni jambo la kawaida,
  • Vilevile ndoto za namna hii zinakuja kutokana na mabadiliko ya mwili. Kama ulilala una njaa, basi tarajia usiku kuota unakula kula hushibi, kama ulikunywa maji mengi na hivyo kibofu kimejaa, tarajia usiku kuota unakojoa kojoa mkojo hauishi, n.k.

Isaya 29: 8  “Tena itakuwa kama mtu mwenye njaa aotapo, kumbe, anakula; lakini aamkapo, nafsi yake haina kitu; na kama mtu mwenye kiu aotapo, kumbe, anakunywa; lakini aamkapo, kumbe, anazimia, na nafsi yake inatamani; hivyo ndivyo utakavyokuwa huo wingi wa mataifa waletao vita juu ya mlima Sayuni”.

Hivyo watu wengi wanaota ndoto nyingi za namna hiyo, na nyingine ubongo unazitengeneza wenyewe. Kwamfano utakuta mtu anatafuta kufahamu Tafsiri za ndoto mbalimbali kama hizi:

  1. Kunyonyesha mtoto: Wanaoota ndoto hizi asilimia kuwa ni wanawake, kwasababu wao ndio akili yao sehemu kubwa ilishajengeka katika mazingira ya kuwa na Watoto hata kama hajazaa..Hivyo kuota unaonyenyesha haliwezi kuwa ni jambo la ajabu
  2. Vivyo hivyo kuota mbwa:
  3. kuota  panya,
  4. Wengine wanatafuta kujua ndoto za magari zinamaanisha nini: Magari tunakutana nayo kila siku barabarani.
  5. ukiota unaswali, .
  6. Maana ya ndoto nyevu,
  7. kuota una nywele ndefu,
  8. ndoto ya kufua nguo,
  9. tafsiri ya ndoto ya harusi.
  10. kuota unavua samaki, na za  kuogelea,
  11. Kuota umegeuza nguo
  12. Ndoto za kuogelea
  13. Kuota ajali
  14. Kuota umeua mtu
  15. Kuota upinde wa mvua
  16. Ndoto za meli
  17. Kuota unanyeshewa na mvua
  18. Maana ya ndoto za kuolewa
  19. Unachuma matunda
  20. Unakunywa pombe
  21. Umevaa nguo nyeupe, 
  22. Ndoto za mayai
  23. Ndoto ya Nyama
  24. Ndoto za asubuhi
  25. Kuota unaoga
  26. Kuota Wanyama, kama mbuzi, sungura, kinyonga, kobe, ngamia, tembo, mamba, kiboko, nyani,paka, mbwa, ng’ombe.N.k. Zote hizi zipuuzie tu.Hazina maana yoyote kwako.
  27. Kuota wadudu kama sisimizi, siafu, konokono, mchwa, mbu, nge, mjusi, mende,tandu
  28. Kuota mapacha.
  29. Kuota jirani, ndugu yako,
  30. Kuota unakula mkaa.
  31. Kuota unatapika.
  32. Watu wanavuna.
  33. Ndoto za kutembea peku.
  34. Unafagia, Unalia,
  35. Kumuota raisi, waziri mkuu, makamu wa raisi, mbunge. Hawa kila siku unawaona kwenye Tv, au unawasikia kwenye Radio, ni lazima utawaota tu usiku siku moja.
  36. Ndoto Juu ya mpenzi wako.
  37. Kuota kabati.
  38. Unafua nguo,
  39. Unaosha vyombo, Maiti,
  40. Kuota jeneza
  41. Ukiota karanga, vitunguu, nyanya, pilau, sherehe,
  42. Kuota Unauza duka

Nakadhilika, Nakadhalika..zipo nyingi, nyingine unazijua wewe mwenyewe, hatuwezi kuziorodhesha zote hapa.. Lakini zote hizo hazina umuhimu wa kutafuta kujua maana zake. Kwasababu ukienda kwa mtindo huo utachanganyikiwa mwilini na rohoni.

Kikubwa ni kufahamu kuwa njia Kuu  ambayo Mungu aliichagua kuzungumza na wanadamu ni kupitia Neno lake (Biblia tu)

Ikiwa wewe ni mwenye dhambi nataka nikuambie hizi ni nyakati za mwisho, Mafundisho mengi ya uongo, na ya mashetani yamezaa kila mahali, Usipotaka kusimama, shetani ni lazima akuzombe kwenye aina ya mafundisho hayo ya mashetani na kukupa tafsiri ya kila ndoto unayoita….

Tubu mgeukie Mungu wako, dalili zote zinathibitisha hilo kuwa tunaishi katika siku za mwisho. Maisha yako yapo hatarini sana, kwani hujui siku yako ya kuondoka ni lini, na hata kama hutaondoka leo au kesho, lakini UNYAKUO upo karibuni sana.. Yesu yupo mlangoni kuja kuwachukua wateule wake.

Kutoa shanga za wanawake maarufu kama vile pendanti, http://www.swisswatch.is/ best replica watches chokers na. Nunua vito vya thamani katika aina mbalimbali za metali na vito ili kuendana na tukio lolote.

Angalia hali halisi ya ulimwengu ulivyo sasa halafu niambie ni dalili ipo Yesu aliyosema kuhusu siku za mwisho haijatimia, angalia magonjwa ya mlipuko, angalia tetesi za vita, angalia matetemeko, angalia kuongozeka kwa maasi duniani,..yote hayo yalitabiriwa.

Huu si wakati wa kuangalia mambo mengine Zaidi ya wokovu wako. Nani ajuaye leo hii Mungu kakupitisha kwenye ukurasa huu ni ili Akuokoe? Kwasababu anaompango mkubwa na wewe maishani mwako?

Hivyo kama wewe ni mwislamu usiogope kumkabidhi YESU Maisha yako leo, fungua tu moyo wako mruhusu atende kazi, nawe utaona badiliko la ajabu atakalolileta ndani yako.

Ikiwa upo tayari kufanya hivyo basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie maisha yako yote kama ilivyokuwa hata kwetu sisi. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU  MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, . NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.

AMEN.

Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.

Ubarikiwe sana.

Bofya chini kwa kujiunga na magroup yetu ya Whatsapp, kwa  mafundisho ya kila siku.

Mada nyinginezo:

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita..

CHUKIZO LA UHARIBIFU

UNYAKUO.

MIJI YA MAKIMBILIO.

WAKATI ULIOKUBALIKA NDIO SASA.

MAHALI UNAPOPASWA USIMVUMILIE SHETANI HATA KIDOGO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

WAKATI WA JUA KALI NDIO WAKATI WA KAZI:

Hebu tuchukue muda kidogo kuisoma habari ifuatayo naamini tutajifunza kitu,

1Samweli 11: 1 “Ikawa, kama baada ya mwezi mmoja, Nahashi, Mwamoni ,akakwea na kupanga marago juu ya Yabesh-gileadi;na watu wote wa Yabeshi wakamwambia Nahashi, Fanya mapatano nasi,na sisi tutakutumikia.

2 Huyo Nahashi, Mwamoni, akawaambia, Kwa sharti hii mimi nitapatana nanyi, kila mtu ang’olewe jicho la kuume; na kwa jambo hilo nitawashutumu Waisraeli wote pia.

3 Basi wazee wa Yabeshi wakamjibu, Tuachie siku saba, ili tutume wajumbe waende mipakani mwote mwa Israeli; kisha, ikiwa hakuna atakayetuokoa, tutakutokea.

4 Hivyo wajumbe wakafika Gibea ya Sauli, wakasema maneno hayo masikioni mwa watu; na watu wote wakainua sauti zao wakalia.

5 Na tazama, Sauli akaja akifuata ng’ombe kutoka kondeni; naye Sauli akauliza, Watu hawa wana nini, hata wakalia? Wakamwambia maneno ya watu wale wa Yabeshi.

6 Na roho ya MUNGU IKAMJILIA SAULI KWA NGUVU, hapo alipoyasikia maneno yale, na hasira yake ikawaka sana.

7 Naye akatwaa jozi ya ng’ombe, akawakata-kata vipande, kisha akavipeleka vile vipande mipakani mwote mwa Israeli kwa mikono ya wajumbe, kusema, Ye yote asiyetoka nyuma ya Sauli na Samweli, ng’ombe zake watatendwa vivi hivi. Basi utisho wa Bwana ukawaangukia wale watu, wakatoka kama mtu mmoja.

8 Naye akawahesabu huko Bezeki; Waisraeli walikuwa mia tatu elfu, na Wayuda thelathini elfu.

9 Nao wakawaambia hao wajumbe waliokuja, Waambieni watu wa Yabesh-gileadi, Kesho, WAKATI WA JUA KALI, mtapata wokovu. Basi wale wajumbe wakaenda, wakawaarifu watu wa Yabeshi; nao walifurahiwa.

10 Kwa hiyo watu wa Yabeshi walisema, Kesho tutawatokea, nanyi mtatufanyia yote myaonayo kuwa ni mema.

11 Ikawa, kesho yake, Sauli akawapanga watu katika vikosi vitatu; nao wakaingia katikati ya marago kwenye zamu ya asubuhi, wakawapiga Waamoni hata WAKATI WA JUA KALI; kisha ikawa wale waliosalia wakatawanyika, hata wasiachwe wawili wao pamoja”.

Biblia inasema taa ya mwili ni jicho, maana yake mtu akitolewa macho anakuwa kipofu, giza linaingia katika mwili wake wote, hebu fanya utafiti wa kufunga macho yako uone utakachokiona…bila shaka ni giza tupu…

Mathayo 6:22 “Taa ya mwili ni jicho; basi jicho lako likiwa safi, mwili wako wote utakuwa na nuru.

23 Lakini jicho lako likiwa bovu, mwili wako wote utakuwa na giza. Basi ile nuru iliyomo ndani yako ikiwa giza; si giza hilo!”

Kwahiyo kwa tukio hilo hapo juu, kuna wakati Mfalme wa Moabu alitaka kuingia katika ardhi ya Israeli inayoitwa Yabeshi, na alipoingia kwasababu ya wingi wa majeshi yake akawatishia Israeli vikali, nao wakaogopa, wakanyenyekea chini yake wakamwambia fanya mapatano nasi (maana yake kama unataka kitu chochote kutoka kwetu hata kama ni kodi tutakupatia)..lakini Yule mfalme kwa kiburi akasema hatataka kitu chochote bali kumng’oa kila mtu wa mji huo wa Yabeshi jicho la kuume…Na lengo la kuwaambia hivyo ni ile awaaibishe na pia aliingize giza katika mji ule, kwasababu alijua jicho la mtu ndio mwangaza wake..mtu hakuna chochote anaweza kufanya.

Jambo hilo liliwahuzunisha watu wa Yabeshi, mpaka kufikia hatua ya kwenda kuomba msaada wa ndugu zao waisraeli walio kwenye majimbo mengine, na wakati huo Israeli walikuwa wameshajitakia mfalme, na walimteua Sauli…lakini kila mtu alikuwa anamdharau Sauli kwa kuwa walimwona kama ni kijana laini asiye na uwezo wa kutawala wala wa vita. Lakini biblia inasema ROHO YA MUNGU ilimjia Sauli kwa nguvu na kumpa moyo wa ujasiri na ushujaa, na kutoka kwenda kuwapiga wamoabu na kuwaangamiza wote kabisa…Lakini jambo pekee ni kwamba hawakuwapiga wakati wa jioni, au wakati wa asubuhi, bali waliwapiga wakati wa JUA KALI linaloangaza…Kuashiria kuwa wao sio WANA WA USIKU bali wa Mchana.. Na kamwe Nuru ya macho yao haiwezi kuzimwa…wala giza haliwezi kuingia kwao.  Hivyo kwa imani waliwaua wakati wa jua kali..

Kama tujuavyo wakati wa jua kali, ndipo watu wanazimia nguvu, ndio wakati watu wanachoka haraka, ndio wakati ambao mwili unapungukiwa maji….Lakini kwa majeshi ya Bwana, hicho ni kinyume chake…wakati wa mchana ndio wakati wa kushinda na kupambana…

Wakati wa mchana(jua kali) ndio wakati wa kuingia vitani, wakati wa mchana ndio wakati wa kwenda kuyavamia majeshi ya adui, wakati wa mchana ndio wakati wa kwenda kuteka nyara, ndio wakati wa kumnyang’anya shetani mateka, wakati wa jua kali ndio wakati wa kuhubiri injili..

Bwana Yesu alisema…

Yohana 9:4 “Imetupasa kuzifanya kazi zake yeye aliyenipeleka maadamu ni mchana, usiku waja asipoweza mtu kufanya kazi

5 Muda nilipo ulimwenguni, mimi ni nuru ya ulimwengu.”.

Wakati huu wa jua kali ndio wakati adui yetu kukosa nguvu, ndio wakati anaoungua, ndio wakati ambao anakimbilia kivulini na mafichoni…hivyo ndio wakati wa kumfuata huko kwa vishindo kama Sauli alivyofanya, na kumwangusha na kumnyang’anya mateka sio wakati wa sisi kulitafuta giza au kivuli kama wao.. “Na Yesu ndio Nuru yetu, ndio jua letu..na sisi ni wana wa Nuru, jua lake halituchomi wala halituumizi wala halituchoshi, wala halitumalizi maji mwilini”..linawadhoofisha maadui zetu lakini si sisi.

Isaya 18:4 “Maanaa Bwana ameniambia hivi, Mimi nitatulia, na kuangalia katika makazi yangu, kama wakati wa mwangaza mweupe wa JUA KALI, mfano wa wingu la umande katika hari ya mavuno”.

Ifanye kazi ya Mungu wakati huu wa Neema, wakati huu wa jua kali…usiku unakuja ambao hutaweza…wakati adui atakuwa na nguvu…na wakati huo ni kipindi cha dhiki kuu…wakati ambao neema ya Yesu itafungwa…huo ndio wakati wa mamlaka ya nguvu za giza kutenda kazi..kutatokea dhiki isiyo ya kawaida!. Yule joka atakapopata nguvu…..Bwana atuepushe na hiyo dhiki, ili wakati huo utakapofika utukute tuwe tumeshanyakuliwa na watakatifu wengine kwenda mbinguni kwa baba na tumeshaimaliza kazi yake.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

Je kupiga miayo ni ishara ya mapepo?

USIHUZUNIKE.

USIISHIE KUTAZAMA JUU, ENDELEA MBELE.

Nuhu alipataje ujuzi wa kuwatambua wanyama wale wote na kuwaweka ndani ya Safina?

JE! UMEFUNDISHWA?

Rudi Nyumbani:

Print this post

WAKATI ULIOKUBALIKA NDIO SASA.

Biblia inasema kila jambo na majira yake (Mhubiri 3)…maana yake ni kwamba hata mti una majira yake ya kuzaa matunda…sio kila wakati, tutakwenda kukuta maembe katika mti wa muembe…Inahitajika uwe ni msimu wa maembe ndipo mti uzae…Haijalishi huo mti utaumwagilia maji kiasi gani, au utauwekea mbolea kiasi gani…Kama sio msimu wake wa kuzaa hautazaa….Hiyo yote ni kwasababu gani?..Ni kwasababu kila jambo lina majira yake.

Vivyo hivyo katika roho, tangu Bwana wetu Mkuu Yesu Kristo, apae juu mbinguni kwenda kutuandalia makao..majira yalibadilika…kabla ya hapo hakukuwa na mlango wowote wa sisi kumzalia Mungu matunda anayoyataka…ikiwa na maana waliokuwa na fursa ya kumjua Mungu kwa undani na kunufaika sana walikuwa ni manabii wa Mungu wachache waliochaguliwa..na si watu wote, Roho Mtakatifu alikuwa anashuka juu ya watu wa Mungu wachache aliowachagua…kasome vizuri habari ile ya Musa katika..

Hesabu 11:24 “Musa akatoka, akawaambia watu maneno ya Bwana; akawakutanisha watu sabini miongoni mwa wazee wa watu, akawaweka kuizunguka Hema.

25 Ndipo Bwana akashuka ndani ya wingu, akanena naye, akatwaa sehemu ya roho iliyokuwa juu ya Musa, akaitia juu ya wale wazee sabini; ikawa, roho hiyo ilipowashukia, wakatabiri, lakini hawakufanya hivyo tena.

26 Lakini watu wawili walisalia kambini, jina la mmoja aliitwa Eldadi, na jina la wa pili aliitwa Medadi; na roho ile ikawashukia; nao walikuwa miongoni mwao walioandikwa, lakini walikuwa hawakutoka kwenda hemani; nao wakatabiri kambini.

27 Mtu mmoja kijana akapiga mbio, akaenda akamwambia Musa, akasema, Eldadi na Medadi wanatoa unabii kambini.

28 Yoshua mwana wa Nuni, mtumishi wa Musa tangu ujana wake, akajibu akasema, Ee bwana wangu Musa, uwakataze.

29 Musa akamwambia, Je! Umekuwa na wivu kwa ajili yangu; INGEKUWA HERI KAMA WATU WOTE WA BWANA WANGEKUWA MANABII NA KAMA BWANA ANGEWATIA ROHO YAKE.

30 Kisha Musa akaenda akaingia kambini, yeye na wale wazee wa Israeli”.

Umeona hapo mstari wa 29?.. Musa anasema ingekuwa heri kama watu wote wa Bwana, Bwana angewatia roho yake…Ikiwa na maana kuwa ni wachache tu waliochaguliwa kwa Neema ndio waliokuwa wananufaika na kipawa cha Roho Mtakatifu. Wengine wote walitamani lakini hawakukipata. Kwanini?..ni kwasababu haukuwa wakati wala majira ya kitu hicho, kushuka kwa watu wote.

Lakini Bwana Mungu wetu, ambaye ni alitabiri kwamba utafika wakati Roho huyu atamwagwa kwa wote wenye mwili…huo utakuwa ni msimu wa kuzaa matunda…Kwahiyo watakaozaliwa msimu huo watakuwa na bahati sana..Na wakati huo si mwingine zaidi ya tangu ule wakati Bwana wetu alipopaa mbinguni mpaka wakati huu wa sasa tunaouishi sisi.. Bwana alisema…

Yoeli 2:27 “Nanyi mtajua ya kuwa mimi ni katikati ya Israeli, na ya kuwa mimi ndimi Bwana, Mungu wenu, wala hakuna mwingine; na watu wangu hawatatahayari kamwe.

28 Hata itakuwa, baada ya hayo, ya kwamba nitamimina roho yangu juu ya wote wenye mwili; na wana wenu, waume kwa wake, watatabiri, wazee wenu wataota ndoto, na vijana wenu wataona maono”

Hii ni neema ya ajabu sana, ambayo hatupaswi tuipuuzie…Huu ndio wakati uliokubalika wa Bwana kutumwagia kipawa chake cha Roho Mtakatifu pasipo ubaguzi…Ndio maana biblia inasema katika…

2Wakorintho 6:1 “Nasi tukitenda kazi pamoja naye twawasihi msiipokee neema ya Mungu bure.

2 (Kwa maana asema, Wakati uliokubalika nalikusikia, Siku ya wokovu nalikusaidia;tazama,wakati ULIOKUBALIKA NDIYO SASA; tazama siku ya wokovu ni sasa)”

Ndugu huu ndio wakati uliokubalika…biblia inasema watu wa zamani walikitamani hichi kipindi tunachoishi sisi…wafalme walikitamani, wakuu walitamani waonje kipawa cha Roho Mtakatifu, waliomba na kusubiri, lakini walikufa bila kuifikia hii saa tuliyopo sasa..Lakini sisi ndio tupo hiyo saa, ambayo yule Roho aliyeshuka juu ya Musa, ndiye huyo huyo ambaye tunamiminiwa sisi wengine ambao hata hatustahili…Ni neema ya namna gani?..Tukose kila kitu lakini tusimkose Roho Mtakatifu kwasababu huyo ndiye Muhuri wa Mungu (Waefeso 4:30)..

Je umempokea huyu Roho Mtakatifu?..kama bado fahamu kuwa anapatikana bure kwa yeyote ambaye atamuhitaji, lakini hatumuhitaji kwa mdomo bali kwa vitendo..maana yake ni hii: Ili ashuke juu yako ni lazima utubu kwa kumaanisha kuacha dhambi kweli kweli…kwasababu yeye ni Roho Takatifu ya Mungu, na hivyo haichangamani na uchafu wa aina yoyote,

kwahiyo unatubu kwa dhati kabisa na kwa vitendo..kama ulikuwa unaiba unaacha wizi na kuwarudishia uliowaibia mali zao kama bado unazimiliki, kama ulikuwa unajiuza, unaacha na kufuta namba za wote uliokuwa unajishughulisha nao katika kazi hiyo, kama ulikuwa unafanya uchafu wowote ule kama kujichua, unatazama picha chafu, ulikuwa mfiraji, msagaji, mlaji rushwa, muuaji n.k unaviacha vyote hivyo…kisha unakwenda kwa Yesu, na kumwomba rehema…Na Bwana wetu mwenye huruma akiona umegeuka kwa vitendo namna hiyo…tayari Yule Roho wake Mtakatifu atakuwa ameshakukaribia sana, utaanza kuona ni kama vile ulikuwa unatembea na kuchoka na ghafla nguvu mpya imekuingia…

Na kukamilisha muhuri huo wa Roho Mtakatifu ndani yako, nenda katafute ubatizo sahihi haraka sana, na ubatizo sahihi kulingana na maandiko ni ule wa maji mengi na kwa jina la BWANA YESU KRISTO…Kumbuka jina la Bwana Yesu ndio Jina la Baba, Mwana na Roho Mtakatifu…Hakuna jina lingine tulilopewa sisi wanadamu litupasalo kuokolewa kwalo isipokuwa jina la Yesu.

Matendo 2:37 “Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu?

38 Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.

39 Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu wamjie.

40 Akawashuhudia kwa maneno mengine mengi sana na kuwaonya, akisema, Jiokoeni na kizazi hiki chenye ukaidi”.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

MWAKA WA BWANA ULIOKUBALIWA.

USIMWOGOPE YEZEBELI.

NGUVU ILIYOPO KATIKA MAAMUZI.

FUKUZA TAI WOTE JUU YA SADAKA YAKO.

JIRANI YANGU NI NANI?

KILA KIUNGO LAZIMA KISHUGHULIKE.

MPINGA-KRISTO

Rudi Nyumbani:

Print this post

Tofauti kati ya kuungama na kutubu ni ipi?

Kuungama kunakwenda sambamba na kutubu.

Kuungama ni kitendo cha kukiri, au kukubali makosa yako kuwa wewe ni mwenye dhambi au ulikosa na hivyo unahitaji kusamehewa.

Mathayo 3:5 “Ndipo walipomwendea Yerusalemu, na Uyahudi wote, na nchi zote za kandokando ya Yordani;
6 naye akawabatiza katika mto wa Yordani, huku wakiziungama dhambi zao”.

Matendo 19:17 “Habari hii ikajulikana na Wayahudi wote na Wayunani waliokaa Efeso, hofu ikawaingia wote, na jina la Bwana Yesu likatukuzwa.
18 Na wengi wa wale walioamini wakaja wakaungama, wakidhihirisha matendo yao”.

1Yohana 1:8 “Tukisema kwamba hatuna dhambi, twajidanganya wenyewe, wala kweli haimo mwetu.
9 Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote”.

Lakini kutubu ni kitendo chenyewe cha kujutia  yale uliyoyaungama tayari (yaani makosa yako)..Ili usamehewe. Na hii inaambatana na kukusidia kuyaacha kivitendo yale uliyokuwa unayafanya kwa kuomba msamaha .

Mathayo 12:41 “Watu wa Ninawi watasimama siku ya hukumu pamoja na watu wa kizazi hiki, nao watawahukumu kuwa wamekosa; kwa sababu wao walitubu kwa mahubiri ya Yona; na hapa yupo aliye mkuu kuliko Yona”.

Mathayo 21:28 “Lakini mwaonaje? Mtu mmoja alikuwa na wana wawili; akamwendea yule wa kwanza, akasema, Mwanangu, leo nenda kafanye kazi katika shamba la mizabibu.

29 Akajibu akasema, Naenda, Bwana; asiende.

30 Akamwendea yule wa pili, akasema vile vile. Naye akajibu akasema, Sitaki; baadaye akatubu, akaenda.

31 Je! Katika hao wawili ni yupi aliyefanya mapenzi ya babaye? Wakamwambia, Ni yule wa pili. Basi Yesu akawaambia, Amin nawaambia, watoza ushuru na makahaba wanatangulia mbele yenu kuingia katika ufalme wa Mungu.

32 Kwa sababu Yohana alikuja kwenu kwa njia ya haki, ninyi msimwamini; lakini watoza ushuru na makahaba walimwamini, nanyi hata mlipoona, hamkutubu baadaye, ili kumwamini.”

Na ndio maana mtu hawezi kusema nimetubu kama hajaungama dhambi zake, Yaani hajakubali kuwa amekosa mbele za Mungu, kwamba yeye ni mwenye dhambi na hivyo anahitaji rehema.

Mithali 28:13 “Afichaye dhambi zake hatafanikiwa; Bali yeye aziungamaye na kuziacha atapata rehema”.

Hivyo kutubu kunaambatana na kuungama, kama ukienda mbele za Mungu halafu huoni kosa lako nini, basi hapo hakuna toba yoyote.

Ubarikiwe.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

 

Mada Nyinginezo:

Kwanini Bwana alirejea Tiro na Sidoni kwa mfano wa Sodoma?

Bwana aliposema kuwa yeye ni “Mungu wa miungu” alikuwa na maana gani?..je! yeye ni Mungu wa sanamu?

 

Kwanini Mungu hakumuua Nyoka, akamwacha Hawa ajaribiwe katika bustani ya Edeni?

TOBA IGUSAYO MOYO WA BWANA.

MATUNDA YAPATANAYO NA TOBA!

Rudi Nyumbani:

Print this post