Waebrania 4:14 “Basi, iwapo tunaye kuhani mkuu aliyeingia katika mbingu, Yesu, Mwana wa Mungu, na tuyashike sana maungamo yetu”
Kuungama maana yake ni kukiri kwa wazi jambo fulani mbele ya wote… Katika ukristo tunaungama kwa “kukiri kwa vinywa vyetu kuwa Yesu ni Bwana na mwokozi wa maisha yetu, na kukiri kwa vinywa vyetu kuwa sisi ni wenye dhambi, na kutubu!”.. sawasawa na Warumi 10:10.
Warumi 10:9 “Kwa sababu, ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, utaokoka.
10 Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu”.
Biblia inazidi kutufundisha kuwa ni lazima TUYASHIKE MAUNGAMO YETU, maana yake tusikiri tu kwa vinywa na kusahau, bali yale tuliyoyakiri mbele za Mbingu na Nchi, hayo TUYAISHI siku zote za maisha yetu.
Sasa swali tunayashikaje/tunayaishije Maungamo yetu?.
Tusome 1Timotheo 6:12.
1Timotheo 6:12 “PIGA VITA VILE VIZURI VYA IMANI; SHIKA UZIMA ULE WA MILELE ULIOITIWA, ukaungama maungamo mazuri mbele ya mashahidi wengi
13 Nakuagiza mbele za Mungu anayevihifadhi hai vitu vyote, na mbele za Kristo Yesu, aliyeyaungama maungamo mazuri yale mbele ya Pontio Pilato”.
Kumbe tunayashika Maungamo yetu kwa kuvipiga vita vya Imani, na kushika ule uzima wa milele tulioitiwa!. Hebu tutazame moja baada ya lingine.
1.PIGA VITA VYA IMANI.
Vita vipo vingi, lakini kama wakristo tumeagizwa kupigana vita vya aina moja tu!, NAVYO NI VILE VYA IMANI!. Na vita hivyo hatupambani na wanadamu wenzetu, bali na roho za mapepo na falme zao katika ulimwengu wa roho…
Waefeso 6:11 “Vaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kuzipinga hila za Shetani.
12 Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho”.
Kwa maelezo marefu kidogo kuhusiana na vita hivi vya Imani na jinsi ya kupambana fungua hapa >>> TUZIDI KUWA HODARI KATIKA BWANA.
2) SHIKA UZIMA WA MILELE.
Yohana 17:2 “kama vile ulivyompa mamlaka juu ya wote wenye mwili, ili kwamba wote uliompa awape uzima wa milele.
3 Na uzima wa milele ndio huu, WAKUJUE WEWE, MUNGU WA PEKEE WA KWELI, NA YESU KRISTO ULIYEMTUMA”.
Uzima wa milele maana yake ni “kumjua sana Mungu na Yesu Kristo aliyemtuma”… Hivyo tunavyodumu katika kutafuta kumjua Mungu na siri iliyopo ndani ya mwanae Yesu Kristo ndivyo uzima wa milele unavyozidi kudumu ndani yetu. Lakini tutakapopunguza kumtafuta Mungu, ndivyo ule uzima wa milele unavyozidi kufifia ndani yetu.
Je unayashika Maungamo yako?.
Bwana atusaidie.
Maran atha!
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mafundisho mengine:
JINSI YA KUPIGANA MAOMBI YA VITA.
Jina Kuu la ukombozi wa roho zetu, (Jina la YESU KRISTO) lihimidiwe daima!
Karibu katika mwendelezo wa uchambuzi wa vitabu vya biblia, tumekwisha kuvitazama vitabu kadhaa vya nyuma na leo tutavitazama vitabu vitatu vya mbele, ambavyo ni kitabu cha Yoeli, Amosi na Obadia. Hivyo ni vizuri kwanza kusoma vitabu hivi mwenyewe katika biblia, ndipo ukapitia uchambuzi huu, na kumbuka uchambuzi huu ni ufupisho tu!, na si wa kutegemea kama darasa kamili au ufunuo kamili wa vitabu hivi, hivyo ni muhimu sana kusoma biblia na kumruhusu Roho Mtakatifu afunue, ndipo masomo mengine yafuate juu yake.
Ikiwa bado hujavipitia vitabu vya awali, ni vizuri ukavipitia kwanza kabla ya vitabu hivi ili tuweze kwenda pamoja.
KITABU CHA YOELI:
Kitabu cha Yoeli, ni kitabu cha 29 katika orodha ya vitabu vya agano la kale, na kimeandikwa na Nabii Yoeli mwenyewe, mapema katika karne ya 8 kabla ya Kristo, kipindi cha Mfalme Uzia wa Yuda, na maana ya jina “Yoeli” ni “Yahwe ni Mungu”.
Kitabu cha Yoeli kina Milango (Sura) tatu tu!, na kila sura/mlango una ujumbe tofauti.
Yoeli: Mlango wa kwanza.
Katika mlango wa kwanza Nabii Yoeli, anaelezea madhara yaliyoletwa na Nzige, na parare, na madumadu waliotokea Israeli. Historia inaonyesha kipindi cha miaka kadhaa kabla ya Yoeli kuandika kitabu hiki, kulitokea Janga ambalo lililetwa na Mungu kutokana na maasi.
Na janga hilo lilikuwa la Kuzuka kwa Nzige, parare na madumadu ambao walikula mazao yote, na kutokusaza chochote, Uharibifu wa Nzige hao uliwashangaza wote, kwani walikula mazao yote.
Na baada ya pigo hilo, ndipo Mungu anampa Nabii Yoeli ujumbe wa kuwaambia watu wake, kwamba watafakari hayo yaliyotokea, na wapate akili, na kutubu,.. watafakari jinsi wadudu hao walivyoharibu mazao kiasi kwamba makundi yote ya watu waliathirika, mpaka makuhani pia waliadhirika kwani hakikupatikana hata cha kutoa katika nyumba ya Mungu, maana yake zile sadaka za unga zilizokuwa zinatolewa ndani ya hekalu hazikutolewa tena..(Yoeli1:9).
Yoeli 1:1 “Neno la Bwana lililomjia Yoeli, mwana wa Pethueli.
2 Sikieni haya, enyi wazee; Sikilizeni, enyi wenyeji wote wa nchi. Je! Mambo haya yamekuwako katika siku zenu, Au katika siku za baba zenu?
3 Waarifuni watoto wenu habari yake, Watoto wenu wakawaambie watoto wao, Na watoto wao wakakiambie kizazi kingine.
4 Yaliyosazwa na tunutu yameliwa na nzige; na yaliyosazwa na nzige yameliwa na parare; na yaliyosazwa na parare yameliwa na madumadu.
5 Levukeni, enyi walevi, mkalie; Pigeni yowe, ninyi nyote mnywao divai; Kwa sababu ya divai mpya; Maana umekatiliwa mbali na vinywa vyenu.
6 Maana taifa limepanda juu ya nchi yangu, Lenye nguvu, tena halina hesabu; Meno yake ni kama meno ya simba, Naye ana magego ya simba mkubwa.
7 Ameuharibu mzabibu wangu; ameuvunja mtini wangu; ameyaambua magamba yake kabisa; ameuangusha chini; matawi yake yamefanywa kuwa meupe”.
Kutokana na pigo hilo la Nzige, Mungu anawaita watu wake wote watubu!, ikiwemo makuhani, wafunge kwa kulia na kuomboleza, na tena wafunge katika saumu ya kweli (Yoeli 1:13-14).
Yoeli: Mlango wa 2.
Katika mlango wa Pili, Mungu analifananisha jeshi hilo la Nzige na jeshi atakalolinyanyua la watu ambao watavamia Israeli na kuharibu watu na vitu, kwa jinsi hiyo hiyo ya Nzige walivyoharibu mazao! Kwasababu ya maasi ya Israeli. Hivyo anazidi kuwaasa watubu!, kwa kupiga mbiu kwa watu wote, kwani jeshi hilo la watu ambao Bwana analifananisha na nzige litakapopita litapageuza Israeli jangwa (Yoeli 2:3), na Mungu atalipa uwezo wa kuharibu kwa uharibifu mkuu (Soma Yoeli 2:4-10).
Lakini katika Mstari wa 12, Bwana anarudia kutoa shauri la kutubu! Ili aiponye nchi kutokana na pigo la nzige, waliokula mazao, vile vile kwa pigo ambalo atakwenda kulipiga Taifa hilo kwa jeshi la watu wabaya atakaowatuma kuwadhuru.
Yoeli 2:12 “Lakini hata sasa, asema Bwana, nirudieni mimi kwa mioyo yenu yote, na kwa kufunga, na kwa kulia, na kwa kuombolea;
13 rarueni mioyo yenu, wala si mavazi yenu, mkamrudie Bwana, Mungu wenu; kwa maana yeye ndiye mwenye neema, amejaa huruma; si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa rehema, naye hughairi mabaya.
14 N’nani ajuaye kwamba hatarudi na kugeuka, na kutuachia baraka nyuma yake, naam, sadaka ya unga, na sadaka ya kinywaji, kwa Bwana, Mungu wenu?
15 Pigeni tarumbeta katika Sayuni, Takaseni saumu, kusanyeni kusanyiko kuu;
16 Kusanyeni watu, litakaseni kusanyiko, Kusanyeni wazee, kusanyeni watoto, Na hao wanyonyao maziwa; Bwana arusi na atoke chumbani mwake, Na bibi arusi katika hema yake.
17 Hao makuhani, wahudumu wa Bwana, na walie Kati ya patakatifu na madhabahu, Na waseme, Uwaachilie watu wako, Ee Bwana, Wala usiutoe urithi wako upate aibu, Hata mataifa watawale juu yao; Kwani waseme kati ya watu, Yuko wapi Mungu wao?
Mstari wa 17-32: (Ahadi ya kuponywa miaka ya njaa)
Bwana anatoa ahadi ya marejesho ya chakula katika miaka iliyoliwa na parare na nzige (katika pigo la Nzige). endapo watatubu!
Yoeli 2:25 “Nami nitawarudishia hiyo miaka iliyoliwa na nzige, na parare, na madumadu, na tunutu, jeshi langu kubwa nililotuma kati yenu.
26 Nanyi mtakula chakula tele na kushiba, na kulihimidi jina la Bwana, Mungu wenu, aliyewatendea mambo ya ajabu; na watu wangu hawatatahayari kamwe.
27 Nanyi mtajua ya kuwa mimi ni katikati ya Israeli, na ya kuwa mimi ndimi Bwana, Mungu wenu, wala hakuna mwingine; na watu wangu hawatatahayari kamwe”.
Lakini haiishii tu kutoa ahadi ya kuponya miaka iliyoliwa na Nzige, bali pia Bwana anatoa ahadi nyingine ya kipekee ya kuwabariki watu katika roho, (yaani kuwamwagia Roho wake Mtakatifu).
Yoeli 2:28 “Hata itakuwa, baada ya hayo, ya kwamba nitamimina roho yangu juu ya wote wenye mwili; na wana wenu, waume kwa wake, watatabiri, wazee wenu wataota ndoto, na vijana wenu wataona maono;
29 tena juu ya watumishi wenu, wanaume kwa wanawake, katika siku zile, nitamimina roho yangu”.
Mlango wa 3 wote unahusu ahadi ya Bwana ya kuwapigania Israeli dhidi ya majeshi yaliyowaonea, baada ya wao kutubu, na kumrudia yeye.
Sasa tukirudi katika biblia, tunasoma baada ya Nabii Yoeli kuondoka, Israeli hawakutubu kikamilifu, ijapokuwa walipigwa na janga hilo la Nzige, na parare na madumadu na tunutu..lakini waliendelea kuwa vile vile, mpaka Bwana alipotimiza neno lake hilo la kuleta jeshi la watu ambao wataharibu nchi mfano wa hao nzige waliotangulia, na jeshi halikuwa lingine Zaidi ya lile la Wakaldayo, ambalo Bwana Mungu aliliruhusu lifike Yuda na kuharibu hekalu na kuwaua wayahudi wengi na baadhi yao kuwachukua utumwani Babeli.
Na kule utumwani walikaa miaka 70, na baada ya ile miaka 70, Danieli alisimama kutubu kwa niaba yao baada ya kuujua unabii wa Yeremia kuhusu muda wao wa kukaa utumwani, na waliporejea Bwana aliwapa majuma 69 (ambayo ni miaka 483) ya kuujenga Yerusalemu kabla ya kutimiza ahadi yake ya kumwanga Roho Mtakatifu.
Na miaka hiyo ilipotimia Bwana aliachilia Roho wake mtakatifu sawasawa na ahadi yake aliyoiahidi, katika Yoeli 2:28, ambapo ilitimia ile siku ya Pentekoste (Matendo 2:17).
Matendo 2:14 “Lakini Petro akasimama pamoja na wale kumi na mmoja, akapaza sauti yake, akawaambia, Enyi watu wa Uyahudi, na ninyi nyote mkaao Yerusalemu, lijueni jambo hili, mkasikilize maneno yangu.
15 Sivyo mnavyodhani; watu hawa hawakulewa, kwa maana ni saa tatu ya mchana;
16 lakini jambo hili ni lile lililonenwa kwa kinywa cha nabii Yoeli,
17 Itakuwa siku za mwisho, asema Mungu, nitawamwagia watu wote Roho yangu, na wana wenu na binti zenu watatabiri; na vijana wenu wataona maono; na wazee wenu wataota ndoto.
18 Naam, na siku zile nitawamwagia watumishi wangu wanaume na wanawake Roho yangu, nao watatabiri”.
Na mpaka leo hii Roho Mtatifu yupo, na ndiye Muhuri wa Mungu juu ya mtu (Warumi 8:9, Waefeso 4:30, 2Wakorintho 1:22).
Kwa undani Zaidi kuhusiana na wadudu hawa (parare, nzige, madumadu na tunutu) na ujumbe gani wa ziada wamebeba kiroho, fungua hapa >>>Nzige, Parare, madumadu na tunutu ni wadudu gani? (Yoeli 2:25)?
KITABU CHA OBADIA:
Kitabu cha Obadia ni kitabu kilichoandikwa na Nabii Obadia mwenyewe, na kina Mlango mmoja tu!, hivyo kukifanya kuwa kitabu kifupi kuliko vitabu vyote vya agano la kale. Maana ya jina ‘Obadia’ ni “Mtumishi wa Bwana”.
Kitabu cha Obadia kinahusu Hukumu Mungu alioitangaza juu ya Taifa la Edomu (Nchi ya Edomu sasahivi ni maeneo ya kusini-magharibi mwa nchi ya Yordani).
Kwaasili Edomu ulikuwa ni urithi wa Esau aliyekuwa ndugu yake Yakobo! (Mwanzo 25:30 na Mwanzo 36:8)... Na tangu Esau na Yakobo wakiwa tumboni mwa mama yao, walikuwa wakipambana!.
Mwanzo 25:22 “Watoto wakashindana tumboni mwake. Naye akasema, Ikiwa ni hivi, kuishi kwanifaa nini? Akaenda kumwuliza Bwana.
23 Bwana akamwambia,Mataifa mawili yamo tumboni mwako,Na kabila mbili za watu watafarakana tangu tumboni mwako.Kabila moja litakuwa hodari kuliko la pili,Na mkubwa atamtumikia mdogo.
24 Siku zake za kuzaa zilipotimia, tazama! Mapacha walikuwamo tumboni mwake”
Kutokana na unabii huo wa Esau kupambana na Israeli, ulifika wakati kiburi cha wana wa Esau (Edomu) kilinyanyuka kwa kiwango kikubwa..kwani walijinyanyua mbele za Mungu na kufanya dhambi na vile vile kuwafanyia mabaya makubwa wana wa ndugu yao Yakobo (yani wana wa Israeli). Na hivyo Mungu kutamka hukumu juu yao kwa kinywa cha Nabii wake Obadia.
Obadia 1:1 “Maono yake Obadia. Ndivyo asemavyo Bwana MUNGU juu ya Edomu; Tumepata habari kwa Bwana, Na mjumbe ametumwa kati ya mataifa, Akisema,Haya,inukeni ninyi;Na tuinuke tupigane naye.
2 Tazama, nimekufanya mdogo kati ya mataifa; Umedharauliwa sana.
3 Kiburi cha moyo wako kimekudanganya, Wewe ukaaye katika pango za majabali, Mwenye makao yako juu sana; Asemaye moyoni, Ni nani atakayenishusha mimi?
4 Ujapopanda juu kama tai, Ijapokuwa kioto chako kimewekwa kati ya nyota, Nitakushusha kutoka huko; asema Bwana”.
Lakini mbali na hilo, historia inaonyesha kuwa kipindi Wakaldayo wameuhusuru Yerusalemu na baadaye kuivamia na kuharibu mali, wana wa Edomu walishirikiana na wakaldayo kushirikiana nao, na hata kuchukua mali nyingi za wana wa Israeli, sawasawa na unabii huo alioutoa Obadia miaka mingi kabla ya wana wa Israeli kuchukuliwa utumwani..
Obadia 1:11 “Siku ile uliposimama upande, siku ile wageni walipochukua mali zake, na watu wa kabila nyingine walipoingia katika malango yake, na kumpa kura juu ya Yerusalemu, wewe nawe ulikuwa kama mmoja wao”.
Hivyo kwa kosa hilo na mengine ambayo hayajatajwa katika biblia, Bwana Mungu alitangulia kuwaonya lakini hawakutubu, hivyo ulipofika wakati Edomu iliadhibiwa sawasawa na hukumu hiyo, lakini pia iliyopo sasa itakuja kuadhibiwa katika vita vya mwisho vya Ezekieli 38.
Maelezo kwa kina kuhusu Edomu fungua hapa >>>Edomu ni nchi gani kwasasa?
Na baada ya Bwana kuiadhibu Edomu, kutokana na mabaya waliyoifanyia Israeli, Bwana anatoa ahadi ya kuijenga Yerusalemu, baada ya ubaya wao kupita.
Obadia 1:18 “Na nyumba ya Yakobo itakuwa moto, na nyumba ya Yusufu itakuwa mwali wa moto, na nyumba ya Esau itakuwa mabua makavu, nao watawaka kati yao, na kuwateketeza; wala hatasalia mtu awaye yote katika nyumba ya Esau; kwa kuwa Bwana amesema hayo”.
Ni nini tunajifunza katika kitabu hiki cha Obadia?..
Tunachoweza kujifunza kikubwa ni kwamba Mungu anatoa unabii unaokuja kama onyo!, ili yamkini mtu au Taifa lisije kuangukia katika hukumu ya Mungu, Watu wa Edomu walipewa unabii huu kama ushauri kwamba wakati wa msiba wa Israeli wasishirikiane na watu wakaldayo, na onyo hilo walipewa miaka mingi kabla ya Israeli kuja kuvamiwa na wakaldayo, lakini hawakutii unabii huo, na wakafanya waliyoyafanya na leo hii hawapo!.. Wanaoishi Edomu sasa si wana wa Esau bali wana wa Ishmaeli, ambao kulingana na unabii wa kibiblia watafutwa katika vile vita vya Ezekieli 38, na 39, kama walivyofutwa hawa wana wa Edomu.
Na sisi vile vile hatupaswi kutweza unabii (yaani kudharau unabii wa kibiblia). Unabii wa biblia unasema kuwa siku za mwisho watatokea watu wa dhihaka, watu wasiotii wazazi wao, wakaidi, wasiotaka kufanya suluhu, watukanani n.k (soma 2Timotheo 3:4), na kwamba watu wa namna hii hawataurithi ufalme wa Mungu.
Sasa unabii huu ni kweli utatimia, hivyo si wa kuutweza/kuupuzia..kwasababu ni kweli siku za mwisho, ambazo ndizo hizi hawa watu wametokea, hivyo hatupaswi kuwa miongoni mwa watakaotimiza unabii huo wa watakaodhihaki na kupotea, badala yake tutimize unabii wa watakaokolewa kwa kumfuata Mungu na kuitii Injili.
1Wathesalonike 5:20 “ msitweze unabii;”
Bwana atusaidie.
Usikose mwendelezo..
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mafundisho mengine:
VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 13 (Kitabu cha Hosea).
VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 12 (Kitabu cha Isaya)
VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 11 (Mithali, Wimbo ulio bora, Mhubiri)
Vitabu vya Deuterokanoni ni vya kiMungu?
Kwanini Mungu anasema tusiwe na ‘tabia’ ya kupenda fedha? Tuwe radhi na vitu tulivyo navyo?. Ujasiri gani unaotaka kutuaminisha kwa kauli hiyo katika zama hizi ambazo tunajua bila fedha huwezi kutatua changamoto nyingi za kimaisha?
Waebrania 13:5 Msiwe na tabia ya kupenda fedha; mwe radhi na vitu mlivyo navyo; kwa kuwa yeye mwenyewe amesema, Sitakupungukia kabisa, wala sitakuacha kabisa. 6 Hata twathubutu kusema, Bwana ndiye anisaidiaye, sitaogopa; Mwanadamu atanitenda nini?
JIBU: Ametuagiza hivyo kwasababu ya hakikisho alilotuahidia katika kauli yake aliyosema “sitakupungukia kabisa, wala sitakuacha kabisa”. Ukiitafakari kauli hiyo haimaanishi kuwa hatutakaa kamwe kupitia vipindi vya kupungukiwa, hapana, lakini anasema sitakupungukia ‘kabisa’, yaani ikafikia hatua ya kukosa kabisa hitaji Fulani, mpaka kufa na kuwa omba-omba barabarani, hapo hatutapafikia.
Daudi anasema..
Zaburi 37:25 Nalikuwa kijana nami sasa ni mzee, Lakini sijamwona mwenye haki ameachwa Wala mzao wake akiomba chakula
Umeona ameahidi kuwa nasi nyakati zote,
Ni kweli upo wakati ambapo ukiitazama baadaye yako au kesho yako unaona giza, lakini bado Bwana anasema usiwe na hofu, kwasababu hiyo kesho yenyewe itajisumbukia, yeye mwenyewe atatengeneza njia ya namna ya kukusaidia katika siku hiyo uliyopo.
Lakini ubaya ni pale ambapo tutataka Mungu atupe sawasawa na wingi tunaoutarajia. Kibiblia hilo sio hakikisho la Bwana, anaweza kukupa cha wakati huo tu, au akakupa zaidi ya hivyo ulivyomwomba. Ni jinsi yeye apendavyo, na anafanya hivyo kwa sababu zake mwenyewe ambazo ni njema kwako, lakini mwisho wa siku yote yatakuwa sawa tu, usiwe na hofu.
Pia ni vema kufahamu kuwa kauli hiyo haitufanyi sisi kuwa wavivu tusubirie tu kitu kutoka kwake. Hapana, anataka tujishughulishe katika sehemu mbili.
Sehemu ya kwanza ni kuutafuta ufalme wake, na haki yake.
Mathayo 6:33 Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa. 34 Basi msisumbukie ya kesho; kwa kuwa kesho itajisumbukia yenyewe. Yatosha kwa siku maovu yake.
Yaani uwe katika utumishi wa Bwana, unamtafuta na unaifanya kazi yake, kama vile mwajiriwa, alivyo katika utumishi wake. Ukifanya hivyo kwa uaminifu Bwana hawezi kukupungukia kabisa atakupa tu rizki yako, kwa njia zake mwenyewe.
Na sehemu ya pili ni aidha tuwe katika kufanya kazi za mikono. Tunapojishughulisha, na kitu Fulani cha kutupatia kipato, Bwana atatusaidia huko huko, tutajazwa mema yake.
Na kwasababu Bwana hataki mioyo yetu izame kule moja kwa moja, anataka tupate na nafasi ya kumfanyia ibada, na ndio maana ameahidi hatatuacha kabisa, Hivyo usione shida kufunga biashara yako, na kwenda kwenye maombi muda wa maombi ufikapo, jumapili kuahirisha kazi zako zote na kwenda nyumbani kwa Bwana, ondoa hofu kuwa utapoteza wateja. Kumbuka tu ile kauli ya sitakuacha kabisa, wala kukupungukia kabisa.
Hata kama utapoteza hiyo, Bwana atakufungulia rehema zake na kukupatia iliyo bora zaidi ya ile.
Hivyo kwa hitimisho ni kuwa wewe kama mwana wa Mungu, hupaswi kuweka moyo wako kwenye mali au fedha, yaani kufikiria kwamba bila kuwekeza sana maisha yako huko utapata shida mbeleni. Hapana, bali upatapo kingi au kidogo, basi ridhika maadamu Kristo yupo ndani yako, ameahidi kukusaidia nyakati zote.
Bwana akubariki.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mafundisho mengine:
Nijapokuwa sipo kwa mwili, lakini nipo pamoja nanyi kwa roho,
Kupiga ramli ni nini katika biblia?
Je kauli ya Bwana Yesu inajichanganya? Katika Yohana 8:14 na Yohana 5:31?
Kwanini Mungu aliwaagiza wana wa Israeli wasikisaze chakula?
Jiepushe na tamaa ya Mali/kupenda fedha.
Wafilipi 4:8 Hatimaye, ndugu zangu, mambo yo yote yaliyo ya kweli, yo yote yaliyo ya staha, yo yote yaliyo ya haki, yo yote yaliyo safi, yo yote yenye kupendeza, yo yote yenye sifa njema; ukiwapo wema wo wote, ikiwapo sifa nzuri yo yote, yatafakarini hayo.
Katika vifungu hivyo utaona neno “yoyote” limetumika sana. Ikiwa na maana yapo mengi, ya aina mbalimbali, ambayo hayajaandikwa hapo. Na hapo biblia inaegemea katika “yale yaliyo mema”.
Tukumbuke kuwa biblia haijaandika matendo yote mema mwanadamu anayopaswa kuyafanya. Kama ingekuwa hivyo basi kingekuwa ni kitabu kikubwa sana, ambacho hakuna mwanadamu yoyote angeweza kukimaliza kwa kukisoma. Lakini imetoa kama muhtasari tu, au mwongozo wa kufuata.
Kwamfano huwezi, kuona katika maandiko tunaagizwa ‘tuimbe kwaya kanisani’, lakini hayo ni moja na yenye kupendeza, au kuona tunaambiwa tuhubiri injili kwa njia ya maigizo. Lakini, tumebuni wenyewe na mwenye dhambi anapotizama filamu hizo, huwa inachangia katika kuwasogeza karibu kwa Kristo. Maadamu havitoki nje ya maudhui mema.
Au tunapotumia vipaza sauti, au tunaposambaza vipeperushi vya injili barabarani, huwezi ona agizo hilo, popote kwenye maandiko. Lakini ni moja ya yale yaliyo ya kweli.
Hivyo kwa hitimisho ni kuwa yapo mambo mengi ambayo tunaweza kuyafanya, na Bwana hatuzuii kuyatafakari, ndio maana akamalizia kwa kusema ‘yatafakari hayo’. Maana yake tutafiti na tutumie njia zote, ambazo tunaona hatma yake itakuwa ni kuujenga ufalme wa Mungu, au kuufanya upendeze zaidi.
Angalia katika ujuzi wako, angalia katika elimu yako, ni kwa namna gani utafanya jambo la ki-Mungu lenye kukuletea sifa njema kwake. Utumishi wa Mungu sio pale madhabahuni tu kuhubiri, utumishi wa Mungu ni mpana. Hivyo Hapo hapo ulipo tafakari ni kwa namna gani utaujenga ufalme wa Mungu wako, na Bwana atakupa akili njema.
Bwana akubariki.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618 Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group
Mafundisho mengine:
MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA KITABU CHA TITO.
Nini maana ya kikombe cha maji ya baridi(Mathayo 10:42)?
Mambo yale yaliyo mbali, na yale yaendayo chini sana,
NAFASI YAKO NI IPI KATIKA MWILI WA KRISTO?
Matulizo ya mapenzi ni nini? (Wafilipi 2:1).
Birika ni nini?, na yale Matao matano katika birika la Bethzatha ni nini?
Karibu tujifunze biblia.
(Masomo maalumu kwa wanandoa).
Waebrania 13:4 “Ndoa na iheshimiwe na watu wote, na malazi yawe safi; kwa maana waasherati na wazinzi Mungu atawahukumia adhabu”.
Hapa biblia inataja vitu viwili; 1) NDOA NA IHESHIMIWE NA WATU WOTE, na 2) MALAZI YAWE SAFI.
Tutazame moja baada ya lingine.
1.NDOA NA IHESHIMIWE NA WATU WOTE.
Hapa anasema “Na iheshimiwe na watu wote”..maana yake si mtu mmoja tu au wawili au watatu, bali wote. Sasa swali ni makundi gani ya watu wanaopaswa kuiheshimu ndoa, na ndoa inaheshimiwaje.
Kundi la kwanza la watu wanaopaswa kuiheshimu ndoa, ni wanandoa wenyewe!..(Na kumbuka ndoa ni ile ya mume mmoja na mke mmoja). Na kundi la pili ni watu wa nje, wasiohusiana na hiyo ndoa.
Kwa wanandoa wanapaswa kuiheshimu ndoa yao kwa kuzuia kitu chochote ambacho kinaweza kuifanya ndoa hiyo iwe ndaifu au ivunjike. Na vitu vinavyoweza kufanya ndoa iwe ndaifu au kuvunjika kabisa ni pamoja na kukosa maelewano, Ugomvi, mafarakano, kukosa utii na upendo,uvumilivu, na uaminifu..haya ni baadhi ya mambo yanayodhoofisha ndoa na hata kuivunja kabisa.
Hivyo wanandoa ni lazima wafanye wawezavyo kutunza upendo wao wa kwanza walipokutana, Amani yao kwanza, furaha yao kwanza, maelewano yao kwanza, na mengineyo mazuri waliyokuwa nayo kipindi wanakutana. Kwa kufanya hivyo watakuwa wameiheshimu ndoa yao na itadumu daima.
Na kwa namna gani wanandoa wanaweza kurudisha upendo wao wa kwanza?…si kwanjia nyingine bali ile ya kutubu na kunyenyekea, na kujazwa Roho Mtakatifu, kwamaana yeye pekee (Roho wa Mungu) ndiye mwenye kutoa matunda yanayohitajika katika ndoa..
Wagalatia 5:22 “Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu, upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria”.
Kundi la pili la watu linalopasa kuheshimu Ndoa, ni watu wa nje wasio wanandoa. Ikiwa na maana kuwa mtu yeyote wa nje iwe ndugu, au rafiki, au jamaa, au jirani, au mpita njia, hapaswi kuwa sababu ya ndoa ya mwingine kudhoofika au kuvunjika.
Maana yake kama huhusiki na ndoa hiyo, basi hupaswi kupanda mbegu za fitina katika hiyo ndoa, hupaswi kufanya wanandoa wachukiane, watengane, waumizane, au wafanye lolote litakalowatolea heshima wanandoa hao. Unachopaswa kufanya ni kuwaombea na kuwashauri ikiwa wamefungua mlango huo!, na ushauri unaopaswa kuwapa ni ule wa kibiblia na si wa kidunia.
Vile vile wewe kama mtu usiyehusika na ile ndoa, hupaswi kumtamani mke/mume wa jirani yako, wala kujaribu kumshawishi uwe naye!..ni lazima uiheshimu ndoa yake, vile vile hupaswi kuanzisha mahusiano yoyote yenye viashiria vya kukushuku, au kuleta tashwishi kuhusu uhusiano wako na yeyote katika ndoa, ni lazima ukae mbali kwa kadiri uwezavyo, isipokuwa kwa sababu maalumu ambazo zitaweza kueleweka katika pande zote mbili. (Kwa kufanya hivyo utakuwa umeiheshimu ndoa ya mwingine).
2.MALAZI YAWE SAFI.
Hili ni jambo la Pili: Malazi yawe masafi.
Malazi yanayozungumziwa hapa ni mahali wanandoa wanapokutana kimwili, maana yake mahali hapo panapaswa pawe pasafi daima, pasiwe pachafu!. Na uchafu unaozungumziwa hapo si usafi ule wa vumbi katika kitanda, au jasho la mwili, (huo unafaa lakini sio unaozungumziwa hapo).
Uchafu unaozungumziwa hapo ambao ni najisi ni uchafu wa Zinaa, pamoja na kukutana kimwili kinyume na maumbile kwa wanandoa.
Unapokuwa mwanandoa ni amri kutokutana kimwili na mwanamke/mwingine tofauti na uliyefunga naye ndoa!, unapolala na mtu mwingine hapo umefanya malazi kuwa machafu, na ni dhambi kubwa!. Vile vile katika kukutana ni lazima iwe kwa namna ya asili. Na si kinyume na maumbile!. Biblia inasema wafiraji hawataurithi uzima wa milele.
1Wakorintho 6:9 “Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? Msidanganyike; waasherati hawataurithi ufalme wa Mungu, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, WALA WAFIRAJI, WALA WALAWITI”
Soma pia 1Timotheo 1:10.
Iheshimu ndoa yako, vile vile heshimu ndoa za wengine.
Je umeokoka?..Fahamu kuwa Kristo anarudi!, na tupo nyakati za hatari.
Maran atha.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618 Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group
Mafundisho mengine:
MISTARI YA BIBLIA KUHUSU NDOA.
Pale mwanandoa mmoja anaposhindwa kutimiza wajibu wake ufanyaje?
FAMILIA TAKATIFU: Marimu na Yusufu.
KWANINI NDOA NYINGI ZINAVUNJIKA? (Sehemu ya 2: Upande wa wanawake)
SWALI: Kikombe cha maji ya baridi ni kipi Bwana alichokitaja katika;
Mathayo 10:42 Na mtu awaye yote atakayemnywesha mmojawapo wa wadogo hawa ngaa kikombe cha maji ya baridi, kwa kuwa ni mwanafunzi, amin, nawaambia, haitampotea kamwe thawabu yake
JIBU: Ni kawaida mtu anayetoka kufanya kazi ngumu, labda ya shamba, au wanaoshiriki katika michezo labda riadha au mipira, utaona huduma ya kwanza wanayoihitaji, sio chakula, bali ni maji, kwasababu mwili huwa unapoteza maji mengi sana pale jasho linapotoka. Na gharama ya maji sikuzote ni ndogo kuliko chakula. Hivyo mtu yeyote huwa ni rahisi kupata huduma hiyo, kwani mtu anaweza kumtolea ndani mwake kwenye pipa lake la kutunzia maji masafi, au kuchota kisimani, na kumpa n.k. Na pale anapompa ya baridi kabisa basi humfanya mtu yule ayanywe yale maji sio tu kwa kukata kiu lakini pia kwa burudiko.
Vivyo hivyo na Bwana naye anawafananisha watu wake, na watenda kazi waliotoka kufanya kazi ya kuchosha, hivyo na wenyewe huwa wanakuwa na kiu chao, wanahitaji maji yao. Lakini zaidi sana maji baridi. Na mtu anayefanya hivyo Mungu amemuahidia kumpa thawabu yake.
Yanaweza kuwa ni vyakula: Kwamfano umuonapo, mtumishi wa Mungu labda anahudumu au anahubiri pengine kwenye masoko, au mahali fulani kwa muda mrefu, na wewe ukathamini kumpatia chakula au hata chupa ya maji. Akanywa au akala akashiba akamshukuru Mungu. Hiyo ni thawabu kwako kwa Mungu.
Yaweza pia kuwa sadaka yako: Kile kidogo, kinachoweza kumtunza hata kwa siku hiyo, kwa ajili ya usafiri, au sabuni, au vocha kwa ajili ya mahitaji yake madogo madogo. Bwana amekuahidia pia thawabu yako hata kama utakiona ni kidogo, si zaidi ukampa vya ziada? Kinabadilika kuwa kikombe cha maji ya baridi.
Yaweza kuwa pia ni “vitu”: Mfano mwingine hana fedha au chakula, lakini ana kitu Fulani cha kumpa, labda nguo, au kiatu, au simu, au huduma n.k. Hicho nacho Bwana anakihesabu kama kikombe cha maji ya baridi.
Hivyo kwa hitimisho ni kuwa zipo thawabu mbalimbali ambazo Bwana anatoa, kwa kutenda mema, zipo thawabu za kuwasaidia maskini, zipo thawabu za kuwasaidia ndugu, lakini zaidi pia Bwana ameahidi thawabu kwa wale wote wanaowajali watumishi wake.
Bwana akubariki.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618 Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group
Mafundisho mengine:
JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA.
JE NI KIKOMBE KIPI UTAKINYWEA SIKU ILE?
Jibu: Tusome,
Waebrania 8:13 “Kwa kule kusema, Agano jipya, amelifanya lile la kwanza kuwa kuukuu. Lakini kitu kianzacho kuwa kikuukuu na kuchakaa ki karibu na kutoweka”.
Neno “kuukuu” maana yake ni “kitu kilichochakaa/ kilichoisha muda wake”.. Hivyo hapo biblia inaposema kuwa Agano la kwanza amelifanya kuwa kuukuu tafsiri yake rahisi ni kwamba “Agano la kwanza yaani lile la kale amelifanya kuwa chakavu (lililoisha muda wake)/ lisilofaa tena”.
Lakini swali ni je!.. kupitia mstari huo inamaanisha kuwa Agano la kale litapotea kabisa na halitatumika?…kiasi kwamba halifai tena wala halitatumika?
Jibu ni la! Bwana Yesu alisema mwenyewe kuwa “hakuna yodi moja wala nukta moja ya torati itakayoondoka (soma Mathayo 5:18)”… Na Zaidi sana alisema hakuja kuitangua torati bali kuitimiliza.
Mathayo 5:17 “Msidhani ya kuwa nalikuja kuitangua torati au manabii; la, sikuja kutangua, bali kutimiliza.
18 Kwa maana, amin, nawaambia ,Mpaka mbingu na nchi zitakapoondoka,yodi moja wala nukta moja ya torati haitaoondoka ,hata yote yatimie”.
Sasa swali linarudi pale pale kama hivyo ndivyo kwamba Bwana YESU hakuja kuitangua torati bali kuitimiliza, na kwamba agano la kale bado litaendelea kuwepo, ni kwanini hapo katika Waebrania 8:13 biblia iseme kuwa litatoweka kabisa?. Je! Biblia inajichanganya??
Jibu ni La! biblia haijichanganyi bali tafakari zetu ndizo zinazojichanganya!.
Ili tuelewe vizuri tutafakari mfano ufuatao.
Kampuni moja limetoa aina Fulani la gari, na aina hiyo ya gari ikatumika kwa miaka kadhaa, lakini baada ya miaka 10 ikatoa toleo lingine jipya la aina ile ile ya gari, na hivyo kampuni hilo likaacha kuzalisha lile toleo la kwanza lililo dhaifu na kujikita katika uzalishaji wa toleo jipya.
Sasa ni wazi kuwa kwa jinsi miaka inavyozidi kwenda lile toleo la kwanza litaenda kupotea kabisa na kubaki hili la pili… kwa lugha nyepesi tunaweza kusema kuwa… “Kampuni lile limelifanya toleo la kwanza kuwa kuu, na hivyo lipo karibuni kutoweka kabisa”.
Lakini kwa kutoa toleo jipya haimaanishi kuwa limelipinga lile la kwanza, kwamba badala ya kuzalisha magari sasa linazalisha treni. Hapana! Bali kinyume chake limeliimarisha lile la kwanza, ikiwa na maana kuwa kama tairi za toleo la kwanza zilikuwa dhaifu, basi toleo la pili limeziongezea uimara, lakini gari ni lile lile, vile vile kama mwonekano wa toleo la kwanza ulikuwa si mzuri basi toleo la pili limeongeza uzuri wa kimwonekano lakini gari ni lile lile.
Na ndivyo katika habari ya agano jipya na lile la kale, Hakuna kilichoondolewa, na kuletwa kingine kipya, bali ni kile kile kilichokuwepo kimeimarishwa Zaidi, kuwa bora Zaidi, kuwa imara Zaidi, kuwa chenye uwezo Zaidi n.k
Kwamfano biblia inasema katika mojawapo ya amri katika agano la kale kuwa “usizini” ikaishia hapo… Sasa hii amri ilikuwa ni dhaifu, kwasababu inasema usizini tu!, mtu anaweza asizini kweli lakini moyoni mwake akalipuka tamaa..
Lakini sasa Bwana YESU aliye mjumbe wa agano jipya anakuja kuitimiliza amri hiyo kuwa “mtu amtazamaye mwanamke kwa kumtamani amekwisha kuzini naye nafsini mwake”. Hata kabla ya kwenda kufanya kile kitendo.
Mathayo 5:27 “Mmesikia kwamba imenenwa, Usizini;
28 lakini mimi nawaambia, Kila mtu atazamaye mwanamke kwa kumtamani, amekwisha kuzini naye moyoni mwake”
Na vile vile katika amri ya “kuua” ni hivyo hivyo…(soma Mathayo 5:21-22).
Kwahiyo kwa lugha nyepesi ni kwamba Agano la pili ni toleo jipya la Agano la kwanza. Lakini mambo ni yale yale.
Sasa swali lingine.. Ni wakati gani ambapo agano la kale lilianza kuwa kuu kuu?
Jibu: Ni wakati wa kuja kwa Bwana Yesu kwa mara ya kwanza.
Kipindi Bwana Yesu alipokuja, yeye ndiye mwanzilishi wa agano jipya, na kuanzia huo wakati ndio agano la kale katika maarifa yake machanga lilipoanza kuisha muda wake, na mpaka leo hatulitumii tena, limetoweka! Na nguvu katika damu ya Yesu ndani ya agano jipya inatawala.
Ndio maana maarifa machanga ya agano la kale, mfano matumizi ya damu za wanyama kama sadaka za kafara zimebaki kutumiwa na watumishi wa shetani, na katika ukristo Damu ya Yesu ndio utimilifu wa Torati za kafara. Na yeyote anayetumia kafara za wanyama leo hii, awe anajiita mtumishi wa Mungu au mtu yeyote yule anafanya ibada za miungu.
Kwahiyo leo hii katika ukristo hatuna matambiko, wala kafara za wanyama, wala utakaso kupitia damu za wanyama, wala hatuishi kwa kujizuia kuua lakini mioyoni tuna hasira, au tamaa.. bali tunaishi kwa Roho mtakatifu na tunamuabudu Mungu katika roho na kweli.
Bwana atubariki.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mafundisho mengine:
Je! waliokufa kabla ya Bwana Yesu wataokolewaje?
LISHIKILIE SANA LILE AGIZO LA KWANZA.
Tofauti kati ya ufalme wa mbinguni na ufalme wa Mungu ni ipi?
SWALI: Nini maana ya Mhubiri 10:9 Mwenye kuchonga mawe ataumizwa kwayo; Naye apasuaye miti huona hatari katika hiyo.
JIBU: Mstari huu unatuonyesha hatari ya kazi yoyote inayotendwa na mtu. Hapo ametumia mfano wa wanaochonga mawe. Wajenzi wa zamani walikwenda kuchonga mawe miambani kwa ajili ya ujenzi wa majengo yao, lakini wakiwa kule walikutana na hatari nyingi, aidha kuangukiwa na mawe hayo, na kuwaponda viungo vyao, vifaa vyao vya uchongaji kuwajeruhi.
Vilevile anatumia tena mfano wa wanaopasua miti, kwa ajili ya mbao za ujenzi, bado na wao pia wanakutana na hatari, aidha kuangukiwa na miti yenyewe, au shoka kuteleza na kumjeruhi mtu au yeye.
Kumbukumbu 19:5 kama aingiapo mtu na mwenziwe mwituni kwenda kukata kuni, akapeleka mkono wake na shoka ili kukata mti, likatoka shoka katika mpini, likampiga yule mwenziwe hata akafa; basi na akimbilie katika miji hii mmojawapo awe hai.
Ni sawa na mjenzi ambaye amezoea kupiga sana nyundo au kuwepo maeneo ya ujenzi muda wake mwingi, utaona upo wakati nyundo itateleza na kumponda kidole chake, au atakanyaga msumari n.k. Tofauti na kama angekuwa hajishughulishi na kazi hiyo yupo nyumbani tu.
Hii ni kufunua nini rohoni?
Kama wana wa Mungu tufahamu kuwa kazi yake ya kwenda kung’oa mapando ya mwovu, katika shamba la Bwana tutarajie kukutana na madhara yake, si wakati wote utakuwa ni mwepesi tu (yaani kuvuna), zipo nyakati tutakutana na kupigwa, au kudhalilishwa, au kufungwa na wakati mwingine hata kuuawa. (Mathayo 10:17-19)
Mtume Paulo alipokuwa katika ziara zake za kupanda ukristo Asia na Ulaya, alikutana na hatari nyingi, ikiwemo kupigwa mawe na watu wabaya, kufungwa, na kurushiwa vitisho mbalimbali. Wamishionari kama dr David Livingstone walioleta injili Afrika zamani walikutana na hatari za magonjwa kama malaria, na wanyama wakali.
Lakini katika yote, Bwana ameahidi, mafanikio makubwa, kuliko hatari zake. Hivyo hatupaswi kuogopa na kudhani kuwa kazi ya Mungu ni kazi ya kwenda kujichinja wakati wote. Hapana, zipo nyakati nyingi za raha, na mafanikio makubwa ya rohoni yasiyokuwa na ghasia yoyote, lakini Bwana hajatuficha pia hatari zake wakati mwingine. Ili tutakapokutana nazo tusihuzunike moyo na kukata tamaa, bali tuendelee na kazi.
Bwana akubariki.
Je! Umeokoka? Je! Umesamehewa dhambi zako? Kama ni la, ni nini kinachokusubirisha? Ukifa leo utakwenda wapi, kumbuka lipo ziwa la moto, kumbuka ipo hukumu kwa waovu. Tubu leo mgeukie Kristo akusafishe dhambi zako, Ukabatizwe katika jina la Yersu Kristo upokee ondoleo la dhambi. Hizi ni siku za mwisho, Kristo anakaribia kurudi.
Ikiwa upo tayari leo kufanya hivyo basi fungua hapa kwa mwongozo huo>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Bwana akubariki.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618. Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group
Mafundisho mengine:
Yeye abomoaye boma, nyoka atamwuma.
Je! fedha ni jawabu la mambo yote? (Mhubiri 10:19).
Fahamu maana ya Mithali 28:20 Mtu mwaminifu atakuwa na baraka tele;
NI KWA NAMNA GANI SHETANI ANAIZUIA INJILI?
Jibu: Tusome,
Mhubiri 10:19 “Karamu hufanywa kwa ajili ya kicheko, Na divai huyafurahisha maisha; NA FEDHA HULETA JAWABU LA MAMBO YOTE”.
Kulingana na huu mstari je ni kweli fedha ni jawabu la kila kitu?.
Jibu ni La! Fedha haitoi jawabu la mambo yote, kama ndio basi fedha ingeweza kununua uzima wa milele, hivyo kusingekuwa na haja ya Bwana Yesu kutoa uhai wake kwaajili ya uzima wa roho zetu.
Lakini biblia inatufundisha kuwa tumekombolewa kwa damu ya Yesu na si kwa fedha.
1 Petro 1:18 “Nanyi mfahamu kwamba mlikombolewa si kwa vitu viharibikavyo, kwa fedha au dhahabu; mpate kutoka katika mwenendo wenu usiofaa mlioupokea kwa baba zenu
19 bali kwa damu ya thamani, kama ya mwana-kondoo asiye na ila, asiye na waa, yaani, ya Kristo”.
Vile vile fedha haiwezi kutibu kifo, wala kununua amani, kwasababu wapo watu wenye pesa nyingi lakini hawana amani n.k.
Lakini kama hivyo ndivyo kwamba fedha si jawabu la mambo yote, kwanini biblia iseme ni jawabu la mambo yote?.
Ili kupata jibu la swali hili ni vizuri tukausoma mstari huo kwa kutafakari kwa kina sehemu za kwanza za mstari huo na zile za mwisho.
Mstari huo unaanza kwa kusema.. “Karamu hufanywa kwa ajili ya kicheko” na unaendelea kwa kusema… “Na divai huyafurahisha maisha”…na unamalizika kwa kusema “NA FEDHA HULETA JAWABU LA MAMBO YOTE”.
Sasa swali ni mambo gani hayo ambayo fedha inaleta majibu yake?.
Jibu: Ni mambo hayo yanayotajwa hapo juu, maana yake yahusuyo karamu hizo ziletazo kicheko zenye ulevi…. na si mambo mengine tofauti na hayo.
Na kweli mambo ya kidunia karibia yote jawabu lake ni fedha, maana yake ukiwa na fedha utaweza kuyafanya au kuyapata, na ukizikosa fedha pia unaweza kuyakosa.
Anasa zote za kidunia zinahitaji pesa, na wanaotaka anasa wanazitafuta pesa kwasababu hilo ndio jibu lake.
Lakini wana wa Mungu, hawaishi kwa fedha wala fedha si jawabu la mambo yao yote…bali Damu ya Yesu ndio jawabu la mambo yao yote.
Wana wa Mungu hata pasipo pesa wanaweza kuishi vizuri kabisa, na pia hawana tabia ya kupenda fedha, bali fedha yao ni Damu ya Yesu katika Roho Mtakatifu.
Je upo ndani ya agano la damu ya Yesu au Mungu wako ni fedha?.
Waebrania 13:5 “Msiwe na tabia ya kupenda fedha; mwe radhi na vitu mlivyo navyo; kwa kuwa yeye mwenyewe amesema, Sitakupungukia kabisa, wala sitakuacha kabisa”
Maran atha!
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mafundisho mengine:
Aibusu midomo atoaye jawabu la haki (Mithali 24:26)
KUOTA UNAPEWA PESA, KUNA MAANISHA NINI?
Pesa za bindoni ni nini?(Marko 6:8)
Zipo tabia au mienendo ambayo inaweza kurithishwa kutoka kwa wazazi au mababu/mabibi kwenda kwa watoto au wajukuu. Kama vile jinsi sura, maumbile, rangi, kimo, na mwonekano vinavyoweza kurithishwa kutoka kwa mzazi kwenda kwa mtoto, kiasi cha kwamba mtoto anazaliwa na anakuwa amefanana na baba yake vile vile au bibi yake au mama yake….halikadhalika mambo ya ndani kama vile tabia au mienendo, mtu anaweza kurithi kutoka kwa wazazi wake au mababu zake/mabibi zake.
Ikiwa na maana kuwa kama Mzazi alikuwa na tabia ya ulevi kuna uwezekano na mwana wake naye akaja kuichukua hiyo tabia kama hatashughulika nayo, vile vile kama Mama alikuwa ni kahaba kuna uwezekano na binti naye akaja kuwa kahaba vile vile.
Ezekieli 16:44 “….KAMA MAMA YA MTU ALIVYO, NDIVYO ALIVYO BINTI YAKE”.
Kama mzazi alikuwa ni mtu wa hasira, au mwuaji ni rahisi na mwanae kuja kuwa mtu wa namna hiyo hiyo, kama mzazi au babu alikuwa mwizi, au mkorofi ni rahisi na mtoto wake au mjukuu wake kuja kuchukua hiyo tabia.
Hivyo ni muhimu sana kushughulika na Mienendo ya kurithi!… Ukiona una tabia fulani ambayo pia ipo au ilikuwepo kwa wazazi wako basi shughulika na hiyo tabia mapema.
Zifuatazo ni njia za kushughulika na tabia za Kurithi.
1. ZAMA KATIKA AGANO LA DAMU YA YESU.
Damu ya Yesu pekee ndio inayovunja na kufuta maagano yote ya ukoo na tabia zote za kurithi. Utauliza kivipi?..tusome maandiko yafuatayo..
1Petro 1:18 “Nanyi mfahamu kwamba mlikombolewa si kwa vitu viharibikavyo, kwa fedha au dhahabu; MPATE KUTOKA KATIKA MWENENDO WENU USIOFAA MLIOUPOKEA KWA BABA ZENU;
19 bali kwa DAMU YA THAMANI, kama ya mwana-kondoo asiye na ila, asiye na waa, yaani, ya Kristo”.
Hapo anasema “MPATE KUTOKA KATIKA MWENENDO USIOFAA MLIOPOKEA KWA BABA ZENU”..Kumbe kuna mienendo inatoka kwa mababa na si yetu!, bali tumepokea!.. na sasa ni kitu gani kinaweza kuifuta hiyo mienendo?..si kingine bali ni Damu ya Yesu pekee sawasawa na huo mstari wa 19.
Na tunaoshwaje kwa Damu ya Yesu?..
Si kwa njia nyingine bali ile ya KUTUBU, kwa kumaanisha kuacha hiyo mienendo tuliyoirithi na hatua ya pili ni KUBATIZWA katika ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Bwana Yesu na hatua ya tatu na ya mwisho ni KUPOKEA ROHO MTAKATIFU. (sawasawa na Matendo 2:38).
Baada ya hapo ile damu ya Yesu ambayo mpaka leo inatiririka pale Kalvari katika ulimwengu wa Roho, itakutakasa kwa namna isiyoweza kuonekana kwa macho na utakuwa safi, na mizizi ya tabia zote za kurithi itakuwa imekufa hapo..tabia za hasira, vinyongo, chuki, ukahaba, uhuni, vita, wizi, ulevi, uchoyo, ubinafsi n.k zitakuwa zimeondoka.
2.DUMU KATIKA UTAKASO
Baada ya kupokea utakaso wa Damu ya Yesu kwa njia ya kutubu na kubatizwa na kupokea Roho Mtakatifu sawasawa na Matendo 2:38, hatua inayofuata si kulala tu!, na kusubiria matokeo!!…bali ni kudumu katika agano hilo la Damu ya Yesu, kwanjia ya kuomba mara kwa mara na kuondokana na vichocheo vyote vya dhambi, pamoja na kumtumikia Mungu.
Usitubu na kubatizwa halafu ukaendelea kwenda kwa waganga, au kufanya matambiko ya ukoo, au kutenda dhambi..(hapo zile tabia hazitakuondoka bali ndio zitakita mizizi zaidi)
Lakini ukizingatia hayo maandiko yanayotufundisha kwa moyo wote, basi fahamu kuwa hakuna tabia yoyote ya kurithi itakayosalia ndani yako, bali utakuwa safi daima na hivyo hata kufanyika baraka kwa vizazi vyako vilivyopo na vitakavyokuja. Na Zaidi sana badala ya watoto wako kurithi tabia za kishetani kutoka kwako watarithi tabia za kiungu, kwasababu tabia za kurithi zinakuwa pia zinabeba laana na baraka nyuma yake..
Maran atha.
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255789001312 au +255693036618
Mafundisho mengine:
Tofauti ya kazi ya Damu ya Yesu na Jina la Yesu ni ipi?
UMUHIMU WA KUZALIWA MARA YA PILI.
TABIA KUU TATU ZA WAHUBIRI WALIORUDI NYUMA NA KUMWACHA MUNGU.
NDIPO HUENDA AKACHUKUA PEPO WENGINE SABA.