Title yezebeli ni nani

YEZEBELI ALIKUWA NANI

Yezebeli, alikuwa ni Binti wa Mfalme wa Wasidoni aliyeitwa Ethbaali (1 Wafalme 16:31). Sidoni ilikuwa ni nchi iliyokuwepo Kaskazini mwa Taifa la Israeli, kwasasa nchi hiyo ni nchi ya LEBANONI.

Desturi za Wasidoni zilikuwa ni kuabudu miungu, waliabudu mungu wao maarufu aliyeitwa BAALI.

Mfalme wa Israeli aliyeitwa Ahabu alimwoa Binti huyo wa kifalme na kumleta katika Taifa la Israeli na kuwa Malkia. Na hivyo kuingiza ibada za miungu migeni ndani ya Taifa la Mungu.

Yezebeli licha tu ya kulichafua Taifa la Israeli kwa kumshawishi sana Mumewe Ahabu, alikuwa pia ni mchawi (2 Wafalme 2:9). Aliwaua manabii wengi wa kweli wa Mungu, na aliikosesha Israeli kwa sehemu kubwa sana. Mahali pengine Inamtaja Yezebeli kuwa ni Nabii wa Uongo. (Ufunuo 2:20)

Yezebeli pia ndio mwanamke pekee kwenye Biblia nzima aliyekuwa anapaka WANJA usoni na kupamba uso. Desturi za wanawake makahaba.(2 Wafalme 9:30). Mwanamke huyu ndiye Mwanamke pekee aliyeshindana na maagizo ya Mungu kuliko wanawake wote kwenye Biblia, ndiye aliyemsumbua sana Eliya na hata kufikia hatua Nabii Eliya kumkimbia, kuogopa madhara atakayoyapata kutoka kwake.

Yezebeli alikuwa na mtoto wa kike, aliyeitwa ATHALIA ambaye naye alirithi tabia zote za mama yake ambaye naye pia alikuwa anaabudu Baali, Athalia alikuwa muuaji na aliutwaa umalkia kwa nguvu ndani ya kabila la YUDA.

Yezebeli hakudumu muda mrefu kwani alikufa sawasawa na unabii uliotolewa juu yake, kwamba atakufa na mbwa watalamba damu yake. Siku ya kufa Yezebeli aliangushwa kutoka juu ya ghorofa refu na kuchuruza damu ukutani mwote, na alipofika chini farasi alimkanyaga kanyaga..na Mbwa walikumla na kubakisha viganja tu vya mikono na kifuvu (2 Wafalme 9:35)

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

NABII ELIYA NI NANI?

Rudi Nyumbani

Print this post

Wana wa Asafu ni akina nani katika biblia?

Wingu la Mashahidi
Wingu la Mashahidi
Wana wa Asafu ni akina nani katika biblia?







/

Kabla ya kuwafahamu wana wa Asafu, ni vizuri kumfahamu Asafu mwenyewe alikuwa ni nani.

Asafu alikuwa ni mmoja wa walawi ambao, mfalme Daudi alimuweka  kama kiongozi wa mbele wa sifa, atakayesimama mbele ya sanduku la Mungu daima kumsifu Mungu. (Soma 1Nyakati 6:31-32, 39).

1 NYAKATI: MLANGO 16

1 Wakaliingiza sanduku la Mungu, na kuliweka katikati ya hema aliyoipiga Daudi kwa ajili yake; wakatoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani mbele za Mungu.

2 Na Daudi alipokwisha kuitoa sadaka ya kuteketezwa na sadaka za amani, akawabariki watu kwa jina la Bwana.

3 Kisha akawagawia kila mtu wa Israeli, waume kwa wake, kila mtu mkate wa ngano, na kipande cha nyama, na mkate wa zabibu.

4 Akawaagiza baadhi ya Walawi kwamba watumike mbele ya sanduku la Bwana, wamfanyie ukumbusho, na shukrani, na sifa, Bwana, Mungu wa Israeli;

5 Asafu mkuu wao, na wa pili wake Zekaria, na Yeieli, na Shemiramothi, na Yehieli, na Matithiya, na Eliabu, na Benaya, na Obed-edomu, na Yeieli, wenye vinanda na vinubi; naye Asafu mwenye kupiga matoazi;

Kulingana na maandiko, biblia inasema huyu Asafu hakuwa tu mwimbaji, bali Mwonaji pia,

2Nyakati 29:30 “Tena Hezekia mfalme na wakuu wakawaamuru Walawi, wamwimbie Bwana sifa kwa maneno ya Daudi, na ya Asafu mwonaji. Wakaimba sifa kwa furaha, wakainama vichwa, wakaabudu”.

Baadaye, uzao wake uliendeleza  nyayo zake, na wote wakawa waimbaji katika hekalu la Mungu lililokuja kujengwa baadaye, na hata baada ya ule uhamisho wa Babeli, waliporudi bado waliweza kuwekwa katika kazi hiyo hiyo ya Sifa..

Soma, Ezra 2:41 “Waimbaji; wana wa Asafu, mia moja ishirini na wanane”.,

Pia Nehemia 7:44

Halikadhalika kuna baadhi ya Zaburi zilijulikana kama Zaburi za Asafu,Ambazo ni Zaburi 50 na ya 73-83. (Baadhi ya tafsiri zinaonyesha hivyo). Hiyo ni kuonyesha kuwa Mungu alimtumia yeye na uzao wake kwa njia ya uimbaji, kutoa nabii ambazo zinatusaidia hadi sasa.

Lakini kwasasa wana wa Asafu ni akina nani? Na tunapata funzo gani?

Wana wa Asafu ni watu wote wanaotumikia madhabahuni pa Bwana katika huduma ya kumsifu na kumwimbia Mungu. Watu hawa wanatenda kazi kubwa inayompendeza Mungu na kwa kupitia wao, Mungu huwa anapitisha, jumbe zake nyingi, na nabii nyingi zinazookoa na kuponya watu kama ilivyokuwa kwa wana  wa Asafu, hii ikiwa na maana, kwamba wakitumika vema katika kazi yao, basi ni utumishi mkubwa sana, hata Zaidi ya huduma nyingine zote.

Lakini, watu hawa walijua kanuni ya kumwimbia Mungu, walimwimbia Mungu katika “uzuri wa utakatifu”, sawasawa 1Nyakati 16:29. Tofauti na sasa, waimbaji wengi, wamekuwa wasanii, wanageuza uimbaji wa injili kuwa Sanaa na sio wito na huduma ya Kristo Yesu.

Wanasahau kuwa huduma yao ndio ya kwanza kabisa inayomkaribia Mungu Zaidi ya nyingine zote,..Huduma ya Maserafi na Makerubi malaika watakatifu wasimamao mbele ya Mungu daima

Lakini kinyuma chake, Mwimbaji wa injili, utamkuta anakata mauno, anavaa vimini, anapamba uso kama Yezebeli, anaimba kwa staili za wasanii wa kidunia.. Twategemea vipi Mungu atasema au atawaponya, au atawafungua na watu wake kupitia uimbaji huo?, Haiwezekani..Inasikitisha kuona, kanisa la sasa, kundi kubwa la watu walioharibikiwa linatoka kwa wanakwaya na waimbaji.

Kumbuka Sababu  iliyowafanya wana wa Israeli,wapelekwe utumwani haikuwa tu kuabudu maashera hapana, ilikuwa pia ni hiyo ya unafki katika kumwimbia.

Amosi 6:5 “ninyi mnaoimba nyimbo za upuzi pamoja na sauti ya vinanda, na kujifanyizia vinanda vya namna nyingi, kama vile Daudi;”

Bwana anatuonya vikali, na sisi pia atatuadhibu vikali kama tutakuwa na tabia kama za wao,  anataka anapoimbiwa aimbiwe katika “uzuri wa utakatifu” (1Nyakati 16:29)..Maana yake ni kwamba wewe mwongoza sifa, wewe mwimbaji, wewe mpiga kinanda,wewe mpiga gitaa, uwe kielelezo kuanzia mavazi yako, usemi, hadi tabia, mbele za watu. Utakatifu ndio uwe leseni yako, ya kumwimbia Mungu.

Kama utashindwa utakatifu, ni heri uache tu, ukafanye kazi nyingine, kwasababu utakuwa unajizombea laana badala ya baraka.

Mahali Mungu anasifiwa na kuabudiwa ni kuwa makini sana.. wengine walipoteza Maisha walipojaribu kuvuruga utaratibu pindi Mungu anapokuwa anasifiwa (Soma 2Samweli 6:1-11 ), Vivyo hivyo na wewe mwimbishaji kanisani, usipokuwa siriazi na huduma yako, uwezekano wa kukutwa na hayo upo mkubwa sana.

Bwana anataka sote tuwe wana wa Asafu, ili atutumie kumtukuza yeye, Pamoja na kuzungumza na watu wake, ili aziponye roho za watu..

Bwana akubariki.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

MAOMBI YA YABESI.

NI KITU GANI TUNAJIFUNZA KWA RISPA, BINTI AYA?

SOMO no.02 (BINTI WA YEFTHA).

Gongo na Fimbo ni nini? Na vinawezaje kumfariji mtu? (Zaburi 23:4).

Nini maana ya “Heri kuchagua jina jema kuliko mali nyingi”?

NI SALAMA ROHONI MWANGU Lyrics

WINGU KUBWA LA MASHAHIDI.

Mimi ni mweusi-mweusi, lakini ninao uzuri.

Rudi nyumbani

Print this post

MUME / MKE BORA KUTOKA KWA BWANA UTAMWONA UKIWA KATIKA MAZINGIRA GANI?

Nakusalimu katika jina kuu sana la Bwana wetu Yesu Kristo. Karibu tujifunze Neno la Mungu ili tupate maarifa sahihi ya kuishi hapa duniani.

Na leo tutaona mazingira ambayo ukikaa katika hayo basi Mungu atakujalia umwone mke/mume sahihi aliyekuchagulia toka mbali.

Tofauti na mazingira ya kiulimwengu ambayo yenyewe ili yakupe mke/mume wa kidunia ni sharti uwe katika mazingira ya kidunia..yaani uvae vimini, ujitembeze na suruali barabarani, unyoe viduku, uishi kama wasanii wa kidunia, uwepo disco na kwenye party party kila wakati n.k. ili uonekane.

Ukikaa katika mazingira kama hayo hakika dunia itakupatia unachokitafuta..

Lakini leo tutajifunza mazingira ya ki-Mungu… Ili Mungu akuonyeshe mke/mume sahihi tokea mbali je! Ukae katika mazingira gani.?

Tutamtazama Isaka mtoto wa Ibrahimu. Kama wewe ni msomaji wa biblia utakumbuka mpaka wakati mama yake anakufa hakuwa na mke bado.

Lakini siku moja Baba yake alipoona ni wakati sasa wa Isaka kuwa na mke alimtuma Kijakazi wake mmoja kwenda kumtafutia mke kutoka katika nchi ya mbali nchi sana ya baba zake. ..kwani hakutaka kumpatia mke kutoka katika miji ile waliyokuwepo.

Kuonyesha kuwa haijalishi utazungukwa na vijana wengi wazuri mahali ulipo, hiyo bado haikufanyi udhani mke/mume Mungu aliyekuchagulia ni lazima atoke hapo.

Sasa utaona mara baada ya yule kijakazi kutumwa kwenda kumtafutia Isaka mke na kumpata alipokuwa anarudi..Huku nyuma kuna tabia na desturi ambayo Isaka alikuwa nayo ambayo nataka leo tuione kwasababu hapa ndipo kiini cha somo letu kilipo.. Tusome..

Mwanzo 24:62-66

[62]Basi Isaka alikuwa amekuja kwa njia ya Beer-lahai-roi, maana alikaa katika nchi ya kusini.
[63]Isaka akatoka ili kutafakari kondeni wakati wa jioni; akainua macho yake, akaona, kuna ngamia wanakuja.
[64]Rebeka akainua macho, naye alipomwona Isaka, alishuka juu ya ngamia.
[65]Akamwambia mtumishi, Ni nani mtu huyu ajaye kondeni kutulaki? Mtumishi akasema, Huyu ndiye bwana wangu. Basi akatwaa shela yake akajifunika.
[66]Yule mtumishi akamwambia Isaka mambo yote aliyoyatenda.

Rudia tena Mstari wa 62 unasema…

‘Isaka akatoka ili kutafakari kondeni wakati wa jioni’.

Unaona, Pindi tu alipotoa mguu wake na kwenda kondeni kutafakari..alipojijengea desturi ya kwenda maporini mbali na makazi ya watu ili tu kupata utulivu na Mungu wake, kuutafakari ukuu wake na uweza wake na maajabu yake na ahadi zake..huko huko Mke wake alitokea..na akamwona tokea mbali..

Pengine yeye alidhani mjini alikoondoka ndipo wake wanapotokea lakini..alishangaa kule kule kondeni kwa mbali sana ngamia wanakuja wamembeba bibi arusi wake..

Hiyo ni kuonyesha Isaka haukuwa na hulka kama za vijana wengine walizokuwa nazo..alipendelea zaidi kumtafakari Mungu kuliko kuzurura zurura huko na huko.

Matokeo yake akampata Rebeka, mwanamke ambaye tunamsoma mpaka leo, licha ya kuwa alikuwa ni mwanamke anayemcha Mungu lakini bado alikuwa ni mzuri sana wa uso..Mwanzo 26:6-7

Ndugu, ikiwa unamuhitaji mke mzuri na anaye mcha Mungu basi kuwa kama Isaka..lakini ikiwa unamuhitaji Yezebeli basi ishi mfano wa hao vijana wa kidunia wanavyoishi leo hii..

Na hili pia lipo kwa upande wa pili wa mabinti..ikiwa unataka uolewe na mwanamume ilimradi tu mwanamume basi jiweke kama hao mabinti wa kidunia wanavyojiweka wanaotembea nusu uchi barabarani na kujipambapamba kama vile Yezebeli ili waonekane wanavutia..
Utampata unayemtafuta.

Lakini kinyume chake ni kuwa ukitulia katika kusudi la Mungu..unatumia muda mrefu kwa Mungu wako kuliko kutanga tanga..unamtakafakari tu yeye..nakwambia Mungu utakuongoza kwa Isaka wako tokea mbali..kama vile Rebeka alivyomwona Isaka akimfuta kutokea mbali..

Uhitaji kujionyesha onyesha ovyo..kwasababu anayekuletea mke/mume ni Mungu, si mwanadamu..wewe kaa katika kumtakafakari yeye maisha yako yote.

Kuoa utaoa, kuolewa utaolewa tu!..ukiishi maisha yanayopendeza Mungu si uongo utakutendea tu.

Daudi alisema..

Zaburi 37:25
[25]Nalikuwa kijana nami sasa ni mzee,
Lakini sijamwona mwenye haki ameachwa
Wala mzao wake akiomba chakula.

Mungu hawezi kuacha kumpa mteule wake kitu kilicho chema, na kizuri.. Hawezi kuruhusu mke/mume pasua kichwa atokee mbele ya njia yake, mtu anayemcha yeye. Hilo haliwezekani..

Hivyo kama bado hujaokoka. Tubu leo anza maisha yako upya na Bwana Yesu kwa kumaanisha kabisa..Toba ya kweli inaambatana na kuucha ulimwenguni, mkatae shetani na kazi zake zote na vimini vyake vyote, na suruali zote na viduku vyote..kamtafakari Mungu huko makondeni, hata kama utaonekana mshamba..

Ishi maisha ya kumlingana Bwana..Na bila shaka wakati utafika atamtuma malaika wake kwenda kukuletea mwenzi sahihi..Kama Ibrahimu alivyomtuma kijakazi wake, kumletea Isaka Rebeka.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

KWANINI NDOA NYINGI ZINAVUNJIKA? (Sehemu ya 1: Upande wa wanaume)

Sadaka ya unga na sadaka ya kinywaji zilikuwaje?

Je! “Mke wa ujana wako” ni yupi kibiblia?

Rudi nyumbani

Print this post

FUMBO ZA SHETANI.

Kati ya yale makanisa 7 tunayoyasoma katika kitabu cha Ufunuo, Kanisa la Thiatira, lilikuwa ni la tofauti sana, kwani lenyewe lilisifiwa sana na Bwana kwa jinsi lilivyokuwa linapanda viwango, siku baada ya siku, kiimani, kihuduma, pamoja na kiupendo, tofauti na makanisa mengine sita, hadi Bwana Yesu alilipongeza kwa  kuliambia, matendo yake ya mwisho yamezidi yale ya kwanza..(Ufunuo 2:18-29)

Lakini pamoja na kuwa lilienda katika uaminifu huo, Shetani naye hakukaa nyuma. Bali alibuni njia ya kitofauti sana ya kuliangamiza, na njia yenyewe ndio hiyo ya kutumia MAFUMBO.  Alibadili mbinu zake za kawaida, akawa anakuja tofauti na walivyotarajia. Na kwa njia hiyo alifanikiwa kulishusha kwa spidi kubwa kanisa lile, kwasababu  baadhi yao walidhani kwamba wanaendelea vizuri na Mungu, kumbe wanamwabudu shetani moja kwa moja.

Leo kwa neema za Bwana tutajifunza baadhi ya FUMBO za shetani, wengi wetu hatuzijui ambazo anazitumia hata leo, na hizo zimewafanya watu wengi warudi nyuma, kama sio kuanguka kabisa kiroho.

Hizi ndio fumbo zake;

  1. Shetani anataka tudhani kuwa hawezi kusema ukweli:

Wakati ule mtume Paulo anafika kwa mara ya kwanza, Mji huo wa THIATIRA, alikutana na kijakazi mmoja aliyekuwa  na pepo la utambuzi, na lilipomwona Paulo, lilimshuhudia Paulo ukweli, kwamba yeye ni mtumishi wa Mungu aliyejuu, na liliendelea kufanya  hivyo kwa muda mrefu tu, lengo lake likiwa ni kumpumbaza Paulo adhani ile ni roho ya Mungu ikimshuhudia, ili tu lisisumbuliwe kutenda kazi zake, Lakini mtume Paulo kwa kufunuliwa na Roho akatambua kuwa Yule sio Roho wa Mungu bali ni shetani, ndipo akalikemea likamtoka.

Mtendo 16:16 “Ikawa tulipokuwa tukienda mahali pale pa kusali, kijakazi mmoja aliyekuwa na pepo wa uaguzi akatukuta, aliyewapatia bwana zake faida nyingi kwa kuagua.

17 Akamfuata Paulo na sisi akipiga kelele, akisema, Watu hawa ni watumishi wa Mungu aliye juu, wenye kuwahubiria njia ya wokovu.

18 Akafanya hayo siku nyingi. Lakini Paulo akasikitika, akageuka akamwambia yule pepo, Nakuamuru kwa jina la Yesu Kristo, mtoke huyu. Akamtoka saa ile ile.

19 Basi bwana zake walipoona ya kuwa tumaini la faida yao limewapotea, wakawakamata Paulo na Sila, wakawakokota mpaka sokoni mbele ya wakuu wa mji;

Hata leo, Shetani anawajia watu kwa namna hii, na wao bila kujua kumbe tayari wameshanaswa katika mitego yake. Ndugu si kila habari ya kweli inatoka kwa Mungu, Nabii kukueleza habari sahihi za maisha yako, hata ibilisi anaweza kufanya hivyo. Mpime kwa Neno la Mungu, na matunda anayoyatoa ndani yake.  Hicho ndio kigezo. Usiridhishwe na maneno tu, ridhishwa na maisha nyuma ya hayo maneno.

     2)  Anataka tudhani kuwa hawezi kuwepo kanisani:

Hili hili kanisa la Thiatira, lilidhani hivyo, Mpaka Bwana Yesu alipolifumbua macho na kuliambia kuna mwanamke Yezebeli katikati yao, (Ambaye anawakilisha watumishi wa uongo waletao mafundisho mageni ndani ya kanisa),  Anawafundisha njia potofu.

Ufunuo 2:18 “Na kwa malaika wa kanisa lililoko Thiatira andika; Haya ndiyo anenayo Mwana wa Mungu, yeye aliye na macho yake kama mwali wa moto, na miguu yake mfano wa shaba iliyosuguliwa sana.

19 Nayajua matendo yako na upendo na imani na huduma na subira yako; tena kwamba matendo yako ya mwisho yamezidi yale ya kwanza.

20 Lakini nina neno juu yako, ya kwamba wamridhia yule mwanamke Yezebeli, yeye ajiitaye nabii na kuwafundisha watumishi wangu na kuwapoteza, ili wazini na kula vitu vilivyotolewa sadaka kwa sanamu.

21 Nami nimempa muda ili atubu, wala hataki kuutubia uzinzi wake.

22 Tazama, nitamtupa juu ya kitanda, na hao wazinio pamoja naye, wapate dhiki kubwa wasipotubia matendo yake;

23 nami nitawaua watoto wake kwa mauti. Na makanisa yote watajua ya kuwa mimi ndiye achunguzaye viuno na mioyo. Nami nitampa kila mmoja wenu kwa kadiri ya matendo yake.

24 Lakini nawaambia ninyi wengine mlioko Thiatira, wowote wasio na mafundisho hayo, WASIOZIJUA FUMBO ZA SHETANI, kama vile wasemavyo, Sitaweka juu yenu mzigo mwingine”.

Hata leo, wapo watu wa Mungu wazuri, wanabidii kweli katika kumtafuta Mungu, lakini hawajui kuwa viongozi wao wanawakosesha kwa Mungu pasipo wao kujua, kwamfano, wambiwapo bikira Maria anaweza kuwa mpatanishi wako na Mungu, hayo ni machukizo, ufundishwapo mafundisho ya kutumia mafuta ya upako, chumvi, sabuni n.k. kana kwamba hivyo vitu vinatosha kumponya mtu, hizo ni ibada za sanamu. Lakini kwasababu unamwamini kiongozi wako kwamba hawezi kukosea, unamtii, ukidhani Mungu atakuridhia na wewe. Kuwa makini na kila fundisho geni unaloletewa na kiongozi wako.

         3) Tudhani kuwa sikuzote anatisha na mwenye mapembe:

Wengi ukiwaambia shetani  yupoje moja kwa moja, wanachowaza katika akili yao ni kitu cha kutisha chenye mapembe, na kichwa cha nyoka. Ni kweli hivyo vitu vinamwakilisha yeye. Lakini yeye hayupo hivyo, kumbuka, alikuwa ni malaika kama malaika wengine, na alipofukuzwa hakuondolewa chochote alichokuwa nacho, hata nguvu zake, bali alifukuzwa tu kwenye makao yake mbinguni.

Kwahiyo sasa alipo bado anatumia njia yake ya uzuri kuwadanganya watu wengi. Hii imewafanya watu wadhani shetani yupo katika vitu vichafu chafu, au vibaya baya, na shida na umaskini, vichaa, na wagonjwa.. Lakini  Siku ile alimpofuata Bwana Yesu ili kumjaribu alikuja kama tajiri, mwenye milki zote za ulimwengu. Biblia inasema anaweza kujibadilisha kuwa malaika wa Nuru,

Kwahiyo usitazamie kuwa wakati wote atakufuata tu katika ndoto mbaya usiku au katika uchawi, au katika magonjwa. Wakati mwingine atakuja na amani feki, na utulivu, na utajiri. Ukadhani ni Mungu huyo kumbe ni shetani, anakutega ili kukuangamiza. Usikurupukie kila mafanikio mazuri, au fursa iliyopo mbele yako.

          4) Tudhani kuwa hawezi kuzitetea njia za Mungu.

Tunaweza kudhani shetani hawezi, kujifanya anaisapoti kazi ya Mungu, au kuitetea, unafki huo anao. Wakati ule Bwana Yesu alipowaambia wanafunzi wake kuhusiana na mateso yake, utaona wakati huo huo shetani akamwingia Petro kujifanya, yeye ni mtetezi wa Bwana..

Mathayo 16:22 “Petro akamchukua, akaanza kumkemea, akisema, Hasha, Bwana, hayo hayatakupata.

23 Akageuka, akamwambia Petro, Nenda nyuma yangu, Shetani; u kikwazo kwangu; maana huyawazi yaliyo ya Mungu, bali ya wanadamu”.

Ni kawaida yake, hata wakati akina Zerubabeli wanajenga hekalu la Bwana, maadui zao walijitokeza kwa kivuli cha kuwa wanataka kuwasaidia ujenzi, lakini walipofukuzwa ndio hapo wakaonyesha makucha yao, wao ni akina nani.(Ezra 4)

Shetani akishaona una kitu ndani yako cha ki-Mungu atakuja kwa njia ya msaada au utetezi, kuwa makini sana, na misaada unayoipokea katika utumishi wako au unachokifanya. Hakikisha unaifahamu na unaelewa kwa undani nyuma yake kuna roho gani. Vinginevyo utaingia katika matatizo makubwa sana.

         5) Tudhani kuwa hawezi kukubali kushindwa.

Si kila wakati ibilisi atakuja kama mpingamizi, au mharibifu, hapana, lengo lake litakuwa ni hilo ndio, lakini atakuja kwa ujanja wa kujionyesha ameshindwa wewe una nguvu nyingi, atajiweka chini yako, ajifanye kuwa yeye siku zote ni mnyonge tu.. lakini kumbe ameshakuweza. Ndicho kilichomtokea Yoshua alipovuka Jordani, sababu mojawapo ya yeye kushindwa kuwaondoa wenyeji  wote wa Kaanani ilikuwa ni hiyo, ya kumsikiliza shetani unyonge wake .  Pale walipojifanya, wametokea nchi ya mbali, wanaomba sharti ya amani wasidhuriwe, kwasababu wamesikia ushujaa wao,  kumbe ni watu wa karibu tu (Yoshua 9)

Leo hii mapepo yanaweza kukusifia sana, kujishusha, kusema wewe ni mkuu, unatisha,una upako, una nguvu,  yakajifanya yanatetemeka mbele zako, ili tu uchukulie mambo rahisi rahisi, lakini kumbe tayari yanatenda kazi kwa nguvu ndani yenu bila kujua.. Usikisikilize kilio cha shetani. Ni mwongo.

       6) Tudhani kuwa hajui mambo mengi.

Shetani anayotabia ya kujifanya mjinga, hajui  kila kitu. Pale Edeni alimfuata mwanamke na kuanza kumwambia Ati, hivi ndivyo Mungu alivyosema, msile “matunda ya miti yote”?. Anajifanya kama hajui, ni matunda gani yaliyokatazwa, na ndio maana anasema “miti yote”. Anakusubiria utiririke, ndipo akunasie mahali fulani.

Hila hii anayo hata sasa, huyo kijana anakuja anajifanya hajui uzinzi ni nini..anataka taarifa kwako, umwambie kwa muhtasari, ndipo hapo akupeleke mpaka kwenye vilindi vya dhambi. Kila jambo baya, kabla ya kukuingiza, atataka wewe ndio umfundishe kwanza.

Kwahiyo hiki ni kipindi cha kuishi kwa umakini, tuzijue FUMBO ZA IBILISI. Ili asifanikiwe kutunasa popote pale. Tuzitambue fikra zake, tumpinge.

Swali ni je! Umeokoka? Je! Unaouhakika kuwa Kristo akirudi leo hii, utakwenda naye mbinguni? Kumbuka hizi ni siku za mwisho kweli kweli, siku yoyote unyakuo utapita, na ibilisi analijua hilo, na ndio maana anafanya kazi kwa nguvu nyingi sana kutafuta watu wa kuwameza.

Hivyo tubu dhambi zako kwa kumaanisha kabisa kumfuata Yesu. Ili akuweke huru.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Rudi nyumbani

Print this post

Baali alikuwa nani?

Baali alikuwa ni aina ya mungu aliyekuwa anaabudiwa na watu wa kaanani na nchi za Tiro na Sidoni, ambaye kulingana na historia za wakaanani, anatajwa kuwa mwana wa mungu aliyeulikana kwa jina la El na mkewe aliyejulikana kwa jina la Ashera..hawa ndio waliomzaa huyu Baali ambaye baadaye alikuja kuabudiwa kama mungu.

Tafsiri ya jina “Baali” ni “bwana” na aliaminika kama mungu wa rutuba na wa uzao.

Aliaminika kusaidia kuongeza rutuba ya nchi, pale ambapo chakula hakikupatikana kutokana na ardhi kutozaa..basi walimwomba huyu mungu baali, ili nchi iweze kuzaa mazao.

Kadhalika pale ambapo mtu au watu walipatwa na matatizo ya kutokupata watoto, walimwomba na kumtegemea mungu huyu kwaajili ya kupata uzao.

Mungu huyu aliabudiwa sana na watu wa kimataifa, lakini ulifika wakati hata wana wa Israeli wakaanza kumwabudu.
Wana wa Israeli walianza kumwabudu baali kwa mara ya kwanza katika kile kipindi cha Waamuzi.

Waamuzi 2:11 “Wana wa Israeli walifanya yaliyokuwa ni maovu mbele za macho ya BWANA, nao wakawatumikia Mabaali.

12 Wakamwacha BWANA, Mungu wa baba zao, aliyewaleta kutoka katika nchi ya Misri, wakafuata miungu mingine, baadhi ya miungu ya watu wale waliokaa karibu nao pande zote, wakajiinamisha mbele yao; wakamkasirisha BWANA, akaghadhibika.

13 Wakamwacha BWANA, wakamtumikia Baali na Maashtorethi”.

Waliendelea hivyo na ibada hizo za mabaali, lakini si kwa kiwango kikubwa..

Hali ilikuja kuwa mbaya zaidi ulipofika wakati wa Mfalme mmoja wa Israeli aliyeitwa Ahabu, ndipo kipindi hicho ibada hizo zilishika hatamu mpaka Bwana Mungu akamtuma Eliya Nabii.

Mfalme Ahabu aliabudu baali kwa kiwango ambacho hakuna mfalme yeyote alikifikia.

1 Wafalme 16:30“ Ahabu mwana wa Omri akafanya yaliyo mabaya machoni pa BWANA kuliko wote waliomtangulia.

31 Ikawa, kama ingalikuwa neno dogo tu kuyaendea makosa ya Yeroboamu mwana wa Nebati, akamwoa Yezebeli binti Ethbaali, mfalme wa Wasidoni, akaenda akamtumikia Baali, akamsujudia.

32 Akamjengea Baali madhabahu katika nyumba ya Baali, aliyoijenga huko Samaria.

33 Ahabu akaifanya Ashera; Ahabu akazidi kumghadhibisha BWANA, Mungu wa Israeli, kuliko wafalme wote wa Israeli waliomtangulia”.

Lakini je! Baali alikuwa ni mungu kweli?

Jibu ni la!.

Mungu ni mmoja tu, aliyeziumba mbingu na nchi, jina lake YEHOVA. Hao wengine sio miungu bali ni roho za mapepo..BAALI ni pepo!..

Ndio maana haikuweza kujibu chochote mbele za uwepo wa Bwana wa majeshi, wakati ule wa Eliya.

1 Wafalme 18:26
“ Wakamtwaa yule ng’ombe waliyepewa, wakamtengeza, wakaliitia jina la Baali tangu asubuhi hata adhuhuri, wakisema, Ee Baali, utusikie. Lakini hapakuwa na sauti, wala aliyejibu. Nao wakaruka-ruka juu ya madhabahu waliyoifanya”.

Hiyo inatufundisha kuwa ibada zote za miungu na za sanamu ni chukizo kwa Bwana.

Na wote wanaoabudu sanamu, na miungu hawataurithi uzima wa milele, maandiko yanasema hivyo.

Bwana atubariki.

Group la whatsapp Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Je Mungu anaweza kumdanganya mtu?

Bwana aliposema kuwa yeye ni “Mungu wa miungu” alikuwa na maana gani?..je! yeye ni Mungu wa sanamu?

Maashera na Maashtorethi ni nini?

Mlima Gerizimu na Ebali ni ipi, na umuhimu wao rohoni ni upi?

Je Mungu anaweza kumdanganya mtu?

Rudi nyumbani

Print this post

MAASI KUONGEZEKA NI ISHARA YA NINI?.

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe..Ni neema Bwana katujalia kuliona jua tena siku ya leo, karibu tuyatafakari maandiko Pamoja..

Kama tunavyojua tunaishi katika siku za mwisho, na kila dakika inayosogea mbele ndivyo tunavyozidi kuusogelea ule mwisho…Hivyo leo tu tayari tumeshapunguza siku nyingine moja, kati ya zile chache zilizobakia mbele yetu, kuufikia ule mwisho.

Lakini Pamoja na hayo biblia inatuonya kuwa mojawapo ya dalili za kurudi kwa pili kwa Kristo ni kuongezeka kwa MAASI NA MAARIFA. Leo hatutazungumzia sana juu ya kuongezeka kwa maarifa, kama utapenda kufahamu juu ya hilo basi utatutumia ujumbe inbox tukutumie somo lake. Lakini leo tutaangalia juu ya kuongezeka kwa MAASI,(Mathayo 24:12) ambapo tutajifunza kitu cha muhimu sana. Na pia nakushauri kabla ya kusoma somo hili, tenga muda pitia somo fupi lililotangulia kabla ya hili lenye kichwa kinachosema “Usiseme, Kwani siku za kale kupita siku hizi? Maana si kwa hekima uulizavyo neno hilo?” kwasababu linamahusiano mkubwa sana na hichi tutakachokwenda kujifunza leo.

Ukiyatafakari Maisha ya leo unaweza kusema, ni afadhali na jana na juzi kuliko leo kwa jinsi maasi yanavyozidi kuongezeka…Upendo wa wengi unapoa, mauaji yanaongezeka, chuki zinaongezeka, visasi, ubinafsi, wizi, uasherati na kila aina ya uchafu, unazidi kuongezeka…

Hiyo yote ni ishara ya kurudi kwa pili kwa Kristo, Lakini swali la kujiuliza ni je!.. kwanini ishara ya mabaya ndio iwe dalili ya kurudi kwa Yesu, na si Ishara ya mazuri, yaani kwanini Bwana Yesu asingesema kabla ya kurudi kwake Mema yataongezeka sana?.

Jibu ni kwamba…wakati wa Kristo kurudi, (yaani kipindi kifupi kabla ya kutokea mawinguni) Kiwango cha utakatifu cha watakatifu kitakuwa kipo juu sana.. Na ishara mojawapo ya kuwa kiwango cha utakatifu kimekuwa kikubwa ni kiwango cha maovu kuwa kikubwa.

Ndugu unapoona dhambi zimezidi mipaka, jua kuwa sehemu Fulani mema yamezidi sana… Inaweza isiwe ni watu wengi wanatenda hayo mema, lakini hata kama ni mmoja tu! Basi atakuwa anatenda mema kwa kiwango kikubwa..

Wengi hawalioni hili wakifikiri kwamba kwasababu dhambi ni nyingi katika kipindi hichi basi hakuna kabisa watu wanaompendeza Mungu. Usilisahau hilo siku zote (Maovu kuwa juu ni ishara ya utakatifu pia kuwa juu). Ukiona kuna maasi makubwa sana katika mji fulani jua upande mwingine katika mji huo huo kuna wakamilifu au mkamilifu wa kiwango kikubwa sana.

Wakati Mungu amechukizwa na maasi ya Sodoma na Gomora, wakati huo huo Mungu alikuwa amependezwa sana na mtu mmoja aliyeitwa Ibrahimu, ambaye tunamwita sasa Baba wa Imani, Hivyo Ishara ya maasi kuongezeka Gomora ni ishara ya wema kuongezeka kwa mtu Fulani wa Mungu mahali fulani. Ukiona dunia inazidi kuoza sasa, jua ni ishara kuwa kuna watakatifu mahali Fulani wanazidi kujitakasa sana.

Ukiona sasa hivi kuna wanawake wengi wanaotembea nusu uchi barabarani, na hata wanaingia makanisani wakiwa hivyo… usifikiri ni wote wapo hivyo…Hiyo ni ishara ya kuiogopa sana, kwasababu ni ishara kuwa kuna mwanamke/wanawake mahali Fulani wanaojiheshimu na kujisitiri sana, na kumheshimu Mungu kwa viwango vya kimbinguni..

Unapoona kuna wimbi la manabii wa uongo..ni jambo la kuogopa wala sio la kucheka na kudharau, kwasababu hiyo ni ishara kwamba kuna kuna watumishi wa Mungu wa kweli. Biblia inasema katika siku za mwisho magugu na ngano vyote vitakomaa.. hivyo ukiona shambani magugu yamekomaa jua na ngano pia zimekomaa…Ndio maana mavuno yanakuja.

Hata Maisha ya kawaida yanatufundisha..Ijapokuwa miaka hii watu wanaonekana duniani kuwa dhaifu, na magonjwa kuongezeka na uwezo kupungua…lakini ukifuatilia rekodi, utagundua kuwa bado zinavunjwa kila mwaka.

Mtu mwenye mbio kuliko wote anaishi miaka yetu hii hii ambayo watu wanakula vibaya, watu wana magonjwa sana n.k. kumbe katikati ya kizazi ambacho watu ni wadhaifu watakuwepo watu ambao ni Hodari kuliko wote katika historia?.

Na katika Imani ni hivyo hivyo…Katikati ya maovu ya dunia yaliyokithiri, Bwana anao watu wake walio waaminifu, wakati wa mfalme Ahabu ambapo Yezebeli mke wake aliifanya Israeli kuwa nchi ya kichawi kiasi kwamba manabii wote waliouliwa, lakini mahali Fulani alikuwepo Eliya Mtishbi, na kama hiyo haitoshi walikuwepo pia manabii wengine 7000 ambao hakupigia goti baali katika mji, Bwana aliojisazia.. Hivyo ndugu huu sio wakati wa kusema aaah! dunia imeharibika yote, hivyo na mimi lazima niwe mwovu…au aaah siku hizi hakuna watakatifu hivyo hakuna haja ya mimi pia kujitakasa..n.k Usikubali kuusikiliza huo ni uongo wa shetani ambao upo kama KILEVI, shetani anawalevya watu wote wa ulimwengu, wafikiri kwamba hali inafanana kila mahali na kwa kila mtu.

Likumbuke hili neno.. Mhubiri 7:10 “Usiseme, Kwani siku za kale kupita siku hizi? Maana si kwa hekima uulizavyo neno hilo”.?

Bwana atusaidie tufumbuke macho..na tuzidi kujitakasa. Maadamu wakati siku ile inakaribia.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312


 

Mada Nyinginezo:

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

MAONO YA NABII AMOSI.

Wanaowachukua wanawake wajinga mateka ni akina nani?

YONA: Mlango wa 4

UFUNUO: Mlango wa 3 part 3

Rudi Nyumbani:

Print this post

Kwanini Bwana alirejea Tiro na Sidoni kwa mfano wa Sodoma?

SWALI: Kwanini Bwana Yesu aliitaja Tiro na Sidoni, kwamba kama ingeliona miujiza ile aliyoifanya kule Bethsaida ingalitubu kwa kuvaa magunia na majivu. Kwani miji hii ilikuwa ni ya namna gani, na ilifanya kosa gani?


JIBU: Tusome..

Mathayo 11:21 “Ole wako, Korazini! Ole wako, Bethsaida! Kwa kuwa kama miujiza iliyofanyika kwenu ingalifanyika katika Tiro na Sidoni, wangalitubu zamani kwa kuvaa magunia na majivu.

22 Walakini nawaambieni, itakuwa rahisi Tiro na Sidoni kustahimili adhabu zao siku ya hukumu kuliko ninyi.

23 Nawe Kapernaumu, je! Utakuzwa mpaka mbinguni? Utashushwa mpaka kuzimu; kwa kuwa kama miujiza iliyofanyika kwako ingalifanyika katika Sodoma, ungalikuwapo mji huo hata leo”.

Ukitazama kwa karibu utaona Bwana Yesu aliiona miji hiyo miwili (yaani Tiro na Sidoni), ilifanana na Sodoma na Gomora kwa tabia zake.

Kumbuka Sodoma na Gomora iliangamizwa kwa maovu yaliyopindukia, Vivyo hivyo Tiro na Sidoni ziliangamizwa, lakini wengi wetu hatufahamu iliangamizwaje? Na Kwa kosa gani..Na hiyo ni kutokana na kwamba habari zao hazipo wazi sana katika biblia kama vile zilivyokuwa za Sodoma na Gomora.

Jaribu kufikiria mpaka biblia inamfananisha mfalme wa Tiro na Shetani mwenyewe..Ujue kuwa ilikuwa inamwangaza shetani mwenyewe duniani kwa tabia zake..Tutakuja kuona huko mbele..

Sasa ukisoma agano la kale, utagundua kuwa mji huu ulikuwa ni mkubwa sana kibiashara hususani ule wa TIRO, Ujenzi wa Hekalu la Mfalme Sulemani kwa sehemu kubwa ulitegemea njenzo na vifaa kutoka katika nchi hizi mbili (Soma 1Nyakati 22:4)..

Hivyo enzi zile za wafalme, mataifa haya mawili yalitajirika kwa haraka sana, japokuwa mataifa kama Babeli na Ashuru yalikuwa bado yapo juu yao, lakini mataifa haya mawili yalikuwa na nguvu kubwa sana kiuchumi, ni sawa leo tuyaite CHINA, huku Babeli na Ashuru yabakie kuwa , Marekani na Urusi. Jinsi leo hii China ilivyochangamka kibiashara ndivyo ilivyokuwa miji hiyo miwili.

Sasa ukipata muda unaweza kusoma kitabu cha Ezekieli kuanzia sura ya 26 mpaka ya 28, Ujione jinsi mataifa haya yalivyosifiwa na Mungu kuwa imara kibiashara na kiuchumi, Na jinsi Mungu alivyoyatamkia maangamizo yao, siku moja, ambayo yatatelekezwa na mfalme wa Babeli Nebukadreza..

Ukisoma pale utaona inasema..

nchi hiyo kwa jinsi ilivyokuwa nzuri mpaka ikajiita “Ukamilifu wa Uzuri” hakuna wa kufananishwa nayo. Jinsi Ilivyokuwa kiini cha biashara cha mataifa yote, mpaka Nchi ya Tarshishi ile Yona aliyoikimbilia, ilitegemea kufanya biashara na Tiro, watu wasomi na wenye akili walikuwa wanaishi humo (TIRO).. kila aina ya biashara ya madini na mawe, biashara ya wanyama, na vifaa vya kivita zilifanyika humo. Biashara za nguo na urembo wa kila namna, biashara ya vyakula na matunda. walikuwa na jeshi kubwa la kutosha, mpaka wakawa wanawauzia silaha mataifa mengine.

Hiyo ndio ikampa kiburi mkuu wao mpaka afikie hatua ya kujilinganisha na Mungu, kutokana na Hekima na utajiri aliokuwa nao na fedha nyingi..Na Yezebeli Yule tunayemsoma kwenye biblia alitokea huko(Ndiye aliyemwingiza mungu baali Israeli)..Hivyo Mungu akapanga siku ya maangamizo yao..(Ezekieli 28:1-10)

Biblia inasema Wafalme wa kila mahali watatetemeza kwa jinsi anguko lake litakavyokuwa(Tiro), wakisema wewe uliyekuwa mwenye nguvu imekuaje umeanguka ghafla hivi, kirahisi,

Ezekieli 27:32 “Na katika kulia kwao watakufanyia maombolezo, na kukuombolezea, wakisema, Ni nani aliye kama Tiro, kama yeye aliyenyamazishwa kati ya bahari?

33 Bidhaa zako zilipotoka katika bahari, uliwajaza watu wa kabila nyingi; uliwatajirisha wafalme wa dunia, kwa wingi wa mali zako, na kwa utajiri wako”.

 

Ezekieli 26: 1 “Ikawa katika mwaka wa kumi na mmoja, siku ya kwanza ya mwezi, neno la Bwana likanijia, kusema,

2 Mwanadamu, Kwa sababu Tiro amesema juu ya Yerusalemu, Aha! Yeye amevunjika aliyekuwa lango la kabila za watu; amenigeukia; nitajazwa kwa kuwa sasa ameharibika;

3 basi Bwana MUNGU asema hivi; Tazama, mimi ni juu yako, Ee Tiro, nami nitaleta mataifa mengi kupigana nawe, kama bahari iinuavyo mawimbi yake.

4 Nao wataziharibu kuta za Tiro, na kuibomoa minara yake; tena nitakwangua hata mavumbi yake yamtoke, na kumfanya kuwa jabali tupu”.

Ukiendelea sasa kusema Ezekieli 28:11-19 utaona Mungu akitoa unabii wa shetani, na jinsi anguko lake lilivyokuwa kule mbinguni kwa kivuli hichi hichi cha mfalme wa Tiro.

Vivyo hivyo na Sidoni naye alikuwa pacha wake, soma habari iliyosalia utaona hilo. Kama vile tu Gomora alivyokuwa pacha wa Sodoma.

Sasa watu wa miji hiyo walitiwa kiburi kwa mali na fedha, wakamsahau Mungu muumba wa mbingu na nchi, wakawa wanaishi maisha ya dhambi, wanawaza tu mambo ya kidunia hadi siku moja Mungu alipoleta uharibifu wao kwa mkono wa Nebukadneza.

Lakini tunaona pale Bwana Yesu anasema.. Laiti ingeliona miujiza iliyokuwa inafanywa na yeye, basi miji hiyo miwili ambayo imefananishwa na utawala wa shetani kwa kujiinua..Watu hao wangalitubu tena kwa kuvaa nguo za magunia na majivu. Mpaka na mfalme wao angetubu.

Tengeneza picha, ni sawa na leo hii, kila mahali tunasikia shuhuda nyingi, tunaona miujiza mingi Kristo akiifanya, mpaka wafu wanafufuliwa mbele ya macho yetu lakini bado tunaupuuzia wokovu, tunaona kama ni habari za kale.

Tujiulize Je siku ile tutastahimili vipi adhabu ya hukumu?.

Ni wazi kuwa kama ziwa la moto litakuwa kali sana, basi kwa vizazi vyetu litakuwa limechochewa mara 7 zaidi,.Bwana atusaidie tusiupuuzie wokovu, Kristo alilipa gharama kubwa sana kwa ajili yetu..kwahiyo tusiudharau wokovu hata kidogo.

Bwana akubariki.

Mada Nyinginezo:

JINSI SODOMA NA GOMORA ILIVYOKUWA INAVUTIA SANA..

MAHALI UNAPOPASWA USIMVUMILIE SHETANI HATA KIDOGO.

MTANGO WA YONA.

FAHAMU JINSI KRISTO ANAVYOPONYA WATU ROHO.

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!

CHUKIZO LA UHARIBIFU

Rudi Nyumbani:

Print this post

Maneno haya yana maana gani?..” Avaaye asijisifu kama avuaye “

1.Naomba kuelezewa maana ya huu mstari tafadhali,  unaosema; Mfalme wa Israel akajibu, akasema, Mwambieni ” Avaaye asijisifu kama avuaye ”  huyu mfalme alikuwa anamaanisha nimi kusema hivyo? (1Wafalme 20:11)


JIBU: Hiyo ni mithali iliyokuwa inatumika wakati huo,  kama leo watu wanavyosema “usitukane mamba kabla hujavuka mto”..Na hapo ni hivyo hivyo…hapo huyu Benhadadi alikuwa ameshajitangazia ushindi dhidi ya Israeli kabla hata ya vita…(Ni kama vile anameshawadharau anaokwenda kupigana nao kabla hata hajapigana nao), Ndio Mfalme Ahabu akamwambia avaaye asijisifu kama avuaye…maana yake avaaye mavazi ya vita ambaye ndio kwanza anakwenda vitani asijisifu kama yule mtu ambaye tayari ameshavimaliza vita na kashinda! na hivyo sasa anavua mavazi yake na kusherehekea ushindi..Hiyo ndio maana yake huo mstari.

Na ukifuatilia Habari hiyo utaona jinsi Mungu alivyowapigania Israeli kutokana na kiburi hicho cha mfalme wa Shamu, kuwadharau Israeli Pamoja na Mungu wao.

1Wafalme 20: 10 “Ndipo Ben-hadadi akatuma kwake, akasema, Miungu wanifanyie hivi na kuzidi, yakiwa mavumbi ya Samaria yatatosha makonzi ya watu wote walio miguuni pangu.

11 Mfalme wa Israeli akajibu, akasema, Mwambieni, Avaaye asijisifu kama avuaye.

12 Ikawa, Ben-hadadi alipolisikia neno hilo, naye alikuwa akinywa, yeye na wafalme, mabandani, aliwaambia watumwa wake, Jipangeni. Wakajipanga juu ya mji.

13 Na tazama, nabii akamjia Ahabu mfalme wa Israeli, akasema, Bwana asema hivi, Je! Umeona makutano haya yote walio wengi? Angalia, nitawatia leo mkononi mwako; nawe utajua ya kuwa ndimi Bwana”.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

YEZEBELI ALIKUWA NANI

DANIELI: Mlango wa 11

NA MTU MMOJA AKAVUTA UPINDE KWA KUBAHATISHA, AKAMPIGA MFALME

Neno I.N.R.I kwenye msalaba wa Yesu maana yake ni nini?

Kwanini yule mtu afe kwa kuliwa na simba?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Kwanini yule mtu afe kwa kuliwa na simba?

Katika 1Wafalme 20:35-37, Kwanini yule mtu afe kwa kuliwa na simba baada ya kukataa kumpiga yule nabii?..je Mungu anaruhusu watu kupigana?

JIBU:Tusome

1Wafalme 20:35-37 “Basi, mtu mmoja wa wana wa manabii akamwambia mwenzake kwa neno la Bwana, Nipige, nakusihi. Akakataa yule kumpiga.

36 Akamwambia, Kwa sababu hukuisikiliza sauti ya Bwana, angalia, mara ukitoka kwangu simba atakuua. Na mara alipotoka kwake, simba alimwona, akamwua.

37 Ndipo akaona mtu mwingine, akasema, Nipige, nakusihi. Yule mtu akampiga, hata kumpiga na kumtia jeraha”

 Kuna wakati Mungu anatumia ishara za mwilini kuzungumza na watu wake au kufikisha ujumbe mahali..Kwamfano utaona Nabii Hosea aliambiwa aoe mwanamke wa kizinzi,

Hosea 1:2 “Hapo kwanza Bwana aliponena kwa kinywa cha Hosea, Bwana alimwambia Hosea, Enenda ukatwae mke wa uzinzi, na watoto wa uzinzi; kwa maana nchi hii inafanya uzinzi mwingi, kwa kumwacha Bwana”.

Lengo la Mungu kumwambia Hosea akaoe mwanamke wa kizinzi sio kuhalalisha uzinzi kwa watu wake, hapana bali ni kuwaonyesha watu wake jinsi na wao wanavyofanya uzinzi mbele zake kinyume chake katika roho…Hosea hakuwa mzinzi lakini aliambiwa akamwoe mwanamke mzinifu, ambaye ni kahaba mwenye wanaume wengi, ambaye hatulii. Sasa nafasi ya Hosea ambaye hakuwa mzinifu ilimwakilisha Mungu na huyo mwanamke wa kizinzi ililiwakilisha taifa la Israeli, kwa jinsi yule mwanamke alivyokuwa ni kahaba baada hata ya kuolewa na Hosea ndivyo Taifa la Israeli lilivyofanya uzinzi katika roho na kumwacha Mungu wao ambaye ndiye mume wao kama Isaya 55:5 inavyosema “Kwa sababu Muumba wako ni MUME WAKO; Bwana wa majeshi ndilo jina lake; na Mtakatifu wa Israeli ndiye Mkombozi wako; Yeye ataitwa Mungu wa dunia yote”

Sasa endapo Nabii Hosea angekataa maagizo yale Mungu aliyompa ya kwenda kumwoa mwanamke kahaba…na kusema hapana Bwana mimi sitaki kumuoa mwanamke yule ambaye ni mzinzi na kahaba hata nikimuoa bado ataendelea kuwapenda hao mabwana wake…Ni Dhahiri kuwa Hosea angetenda dhambi kwasababu amekataa shauri la Bwana la yeye kufanyika ishara kwa Israeli. Na hivyo angewafanya Israeli wasitubu, lakini ishara ile iliwafanya Israeli wengi watubu..Kwasababu walipokwenda kumuuliza wewe Nabii wa Mungu mbona unaoa mwanamke ambaye anamabwana wengi na zaidi ya yote tunamwona mkeo huyo yupo na mabwana wengine, unajisikiaje kwa hilo?..Ndipo Hosea atawajibu ni mfano wa nyinyi mlivyomwacha Mungu wenu ambaye ni mume wenu na kuigeukia miungu mingine kuiabudu..Hivyo mrudieni Mungu wenu ambaye ni Mume wenu kwasababu amewakasirikia sana.

Halikadhalika kuna wakati Mungu alimwambia nabii mwingine amwambie mwenzake kwamba ampige mpaka apate majeraha…ili kwa kupitia yale majeraha aonekane kama alikuwa katika vita vikali na aende kwa mfalme wa Israeli akiwa na yale majeraha…Ili mfalme adanganyike na kuamini kuwa ni kweli alikuwa kwenye mapambano kwasababu ana majeraha..na ndipo ampe fumbo ambalo litamtega…Na kweli mfalme alipomwona mtu anakuja mwenye majeraha akasema bila shaka mtu huyu atakuwa ametoka vitani kwa majeraha yale..na alipopewa lile fumbo na yule nabii kumbe lilikuwa linamhusu mfalme mwenyewe..kwasababu alimwacha huru Benhadadi ambaye alipaswa kumuua kabisa..

Hivyo akaambiwa sehemu yake ataichukua yeye. Unaweza kuisoma vizuri habari hiyo katika 1Wafalme 20:35-43.

Lakini yule mtu alikataa maagizo yale ya Mungu..ingawa aliambiwa ni maagizo kutoka kwa Mungu lakini akakataa kumpiga..hakujua kuwa kwa kukataa kule kungemfanya mfalme wa Israeli asiyaamini maneno yale ya Mungu…Na ikasababisha dhambi kwake, na ndio mbeleni akaenda kuliwa na simba..lakini yule mwingine hakulichukulia lile jambo la kumpiga nabii wa Mungu kwamba ni jambo la kumuumiza..bali aliona mbele kwamba kwa ishara ile ya majeraha ya yule nabii, mfalme ataamini ujumbe kutoka kwa yule nabii sawasawa na Neno la Mungu na hivyo atakuwa ameyatenda mapenzi ya Mungu Zaidi.

Hivyo ni jambo la kawaida kabisa Mungu kuzungumza kwa ishara za mwili, alifanya hivyo kwa Hosea, Kwa Ezekieli, na kwa manabii wengine wengi.

Bwana atubariki

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

YEZEBELI ALIKUWA NANI

Kuna haja gani ya kumwamini Yesu aliyezaliwa kama sisi?

MAMBO MANNE,YANAYODHOOFISHA UOMBAJI WAKO.

KWANINI YESU KRISTO NI WA MUHIMU KWETU SASA?

MKARIBIE BWANA ZAIDI ILI UFANYIKE NGUZO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

JE! MUNGU NI NANI?

Je Mungu ni nani?

Neno “Mungu” linatokana na neno “Muumbaji” au “mtengenezaji”…Kwahiyo hata mtu akiumba gari yeye ni mungu wa hilo gari..

Hivyo kama gari limeumbwa na mtu, kadhalika kuna kitu kilichomuumba huyo mtu ambaye ni mungu kwa gari…na kitu hicho kilichomuumba mwanadamu ndio kinachoitwa “Mungu wa miungu”…Hakiwezi kuelezewa kwa undani kwasababu hata gari haliwezi kumwelewa mtu kazaliwa wapi, mwaka gani, na anaishije… hata lingefanyaje.

Kwahiyo huyo aliyemuumba mwanadamu ndiye anayeitwa Mungu, (zingatia ‘M’ inaanza kwa herufi kubwa na si ndogo). Huyo anakaa mahali pa kiroho mbali sana panapoitwa mbinguni. Anafanana na mwanadamu lakini si mwanadamu, anatabia kama za mwanadamu lakini si mwanadamu.

Kwasababu sisi wanadamu tunaishi kwa pumzi, kwa chakula, tunahitaji mwanga ili tuone, tunahitaji maji ili tuishi, lakini huyo Mungu yeye ana pua lakini hategemei pumzi, yeye ana macho lakini hategemei mwanga kuona, yeye anaishi lakini hategemei kula, kwasababu kila kitu kimeumbwa na yeye.

Kwahiyo hatuwezi kumwelezea Mungu kwa undani kwasababu ni kitu kilichotutengeneza sisi. Kama vile ilivyo ngumu roboti nililolitengeneza mimi kwa mfano wangu na sura yangu liwe na uwezo wa kujua asili yangu au mwanzo wangu au kunichambua kwa undani mimi ni nani? hata tu huo ufahamu haliwezi kuwa nao…Vivyo hivyo Mungu tukitafuta kumchambua tutakuwa tunapoteza muda, na ndio tutakuwa tunakwenda mbali naye na kuishia aidha kupotea au kukosa majibu kwasababu upeo wake ni wa mbali sana

Lakini pamoja na hayo hajatuumba sisi kama maroboti, sisi katuumba kama wanawe, ambao anatupenda na kutujali kwa namna isiyoelezeka. Na anataka tuishi katika haya maisha kwa kufuata sheria zake ili tupate faida na kufanikiwa, kwa kulitekeleza hilo alimtuma mwanawe wa pekee duniani ili kila amwaminiye asipotee bali apate uzima wa milele. Na huyo mwanawe ndiye Yesu Kristo tunayemfahamu…

Huyu Yesu Kristo pekee ndiye aliyekabidhiwa mamlaka yote ya mbinguni na duniani, hakuna mtu yeyote atakayeweza kumfikia Mungu Baba mbinguni pasipo kupitia kwa yeye (Yesu Kristo)

Yohana 6:44 “14.6 Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi.”

Je unataka kwenda kumwona Baba mbinguni?. Kama ndio je umemwamini mwanawe mpendwa Yesu Kristo, na kutubu dhambi zako na kuoshwa kwa damu yake? kama ndio basi unalo tumaini la kumwona Mungu siku moja lakini kama hutamwamini na kuwa mtakatifu hutamwona kamwe.

Waebrania 12:14 “Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na huo utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao”;

Bwana akubariki sana.

Pia kwa Maombezi, Ushauri, Maswali au Ratiba za Ibada Wasiliana nasi kwa namba 

+225693036618/ +225789001312

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

YEZEBELI ALIKUWA NANI

Mbona Mungu anaruhusu watu wapate shida, ilhali ana uwezo wa kutuepusha?

JISHUSHE ILI MUNGU AKUHUDUMIE.

Rudi Nyumbani:

Print this post