Hazama ni nini?
Hazama ni pete ya puani.
Neno hilo utalisoma katika vifungu hivi;
Mwanzo 24:47, Kutoka 35:22,
Na pia ukisoma Ezekieli sura ya 16 yote utaona jinsi Mungu anavyolilinganisha taifa la Israeli na msichana ambaye alipozaliwa tu alitelekezwa porini na wazazi wake akiwa hata hajakatwa kitovu chake. Na Bwana alipokuwa anapita (hapa akijifananisha na mwanaume fulani), alimwona na kumuhurumia, akamchukua na kwenda kumtunza, akamkuza, akafanya naye maagano kuwa atakuwa wake, akamkuza vizuri sana, akawa mrembo sana, akamvisha mavazi mazuri, na kumpamba kwa kila aina ya mapambo ikiwemo hazama na vikuku, lakini baadaye alipokuja kuwa mtu mzima alikengeuka na kuanza kuzini na wanaume wengi, na kuwa kahaba wa kipindukia, ..
Ezekieli 16:11 “Nikakupamba kwa mapambo pia, nikatia vikuku mikononi mwako, na mkufu shingoni mwako.
12 NIKATIA HAZAMA PUANI MWAKO, na pete masikioni mwako, na taji nzuri juu ya kichwa chako.
13 Hivyo ulipambwa kwa dhahabu na fedha; na mavazi yako yalikuwa ya kitani safi, na hariri, na kazi ya taraza; ulikula unga mzuri, na asali, na mafuta; nawe ulikuwa mzuri mno, ukafanikiwa hata kufikilia hali ya kifalme.
14 Sifa zako zikaenea kati ya mataifa kwa sababu ya uzuri wako; kwa maana ulikuwa mkamilifu, kwa sababu ya utukufu wangu niliokutia, asema Bwana MUNGU”.
Lakini sasa mfano huo haumaanishi kuwa wanawake wa ki-kristo wanaruhusiwa kujipamba hapana, kumbuka huo ni mfano tu ambao Mungu aliutoa kuonyesha ni jinsi gani Israeli taifa lake alilolipamba rohoni kwa utukufu wake, tangu zamani, baadaye likaja kukengeuka kuabudu miungu mingine tofauti nay eye.
Biblia inasema..
1Petro 3:1 “Kadhalika ninyi wake, watiini waume zenu; kusudi, ikiwa wako wasioliamini Neno, wavutwe kwa mwenendo wa wake zao, pasipo lile Neno;
2 wakiutazama mwenendo wenu safi, na wa hofu.
3 Kujipamba kwenu, kusiwe kujipamba kwa nje, yaani, kusuka nywele; na kujitia dhahabu, na kuvalia mavazi;
4 bali kuwe utu wa moyoni usioonekana, katika mapambo yasiyoharibika; yaani, roho ya upole na utulivu, iliyo ya thamani kuu mbele za Mungu”.
Umeona, mwanamke wa kikristo hapaswi kuweka hazama, au vikuku, au lipstick, au wanja, au mikufu, au hereni mwilini mwake, badala yake mapambo haya anapaswa ayahamishie rohoni, kwa matendo mema. Ndivyo biblia inavyoagiza.
Kwahiyo kama wewe ulikuwa unaweza hazama au vipini puani mwako, ni vyema ukaacha. Ishi sasa maisha ya kama wanawake wacha Mungu walivyoyaishi. Mapambo yasikusababishe uikose mbingu.
Shalom.
Tazama tafsiri ya maneno mengine chini.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
MASERAFI NI NANI?
Jabari ni nini, kama linavyotumika kwenye biblia?
Pomboo ni nini katika biblia?(Kutoka 25:5, Ezekieli 16:10)
Naomba kujua nini maana ya kuteguka uvungu wa paja?
WINGU KUBWA LA MASHAHIDI.
NJONI, NUNUENI MLE NA MNYWE.
Katika biblia shetani amepewa majina tofauti tofauti na hiyo ni kutokana na aina ya kazi anazozifanya hapa duniani, kwamfano biblia inapomwita shetani/ibilisi ni kwasababu ni mpinzani na mshitaki wa roho zetu kwa Mungu ndio tafsiri ya jina hilo,.
Vilevile sehemu nyingine inapomwita Joka (Ufunuo 12), ni kwasababu ni mwongo kama alivyokuwa nyoka, na anameza roho za watu kama majoka yafanyavyo kumeza wanyama,..
Bado sehemu nyingine inamwita, mkuu wa ulimwengu huu, (Yohana 12:31,2Wakorintho 4:4), kwasababu mambo yote yaliyotukuka ulimwenguni sasa yanashikiliwa na yeye, yeye ndiye kiongozi wa hayo ..
Pia inamwita mfalme wa uweza wa anga (Waefeso 2:2) kwasababu nguvu zote za giza katika ulimwengu wa roho anazishikilia yeye, baba wa mapepo na wachawi duniani.
Vilevile sehemu nyingine inamwita mjaribu (Mathayo 4:3,1Wathesalonike 3:5), kwasababu, yeye ndio chanzo cha majaribu yote kwa mkristo..Na ndio maana Bwana Yesu alituambia kesheni mwombe msije ingia majaribuni..Kwasababu tusipoomba huyu atapata nafasi kubwa ya kutuletea majaribu ili kutuangusha.
Lakini zaidi ya yote biblia inatuonyesha kuwa atakuja kuwa na jina lingine, lijulikanalo kama Abadoni au Apolioni,.. Tafsiri ya jina hili ni MHARIBIFU…Ikiwa na maana atakuja kuwa na kazi ya kufanya uharibifu tu.
Kama leo hii unamwona shetani ni mharibifu, basi bado haujajua vizuri uharibifu wake upoje.
Tukisoma kitabu cha ufunuo, kama tunavyojua mara baada ya unyakuo wa kanisa kupita, kutafuata matukio ambayo hayaelezeki kwa namna ya kawaida. Tukiachana na yale mapigo ya vile vitasa 7 na ile siku ya Bwana mwenyewe ambayo jua hili litaondolewa, kutatangulia kwanza mapigo ya baragumu 7,..Sasa hatuwezi kuyachambua yote hapa, ikiwa utahitaji somo lake utuambia inbox tukutumie..
Lakini leo tutatazama, baragumu la tano, ambalo ndio kiini cha somo letu la Leo. Baragumu hilo litakapopigwa, biblia inatuambia, Shimo la kuzimu litafunguliwa na humo watatoka nzige wabaya sana..tusome;
Ufunuo 9:1 “Malaika wa tano akapiga baragumu, nikaona nyota iliyotoka mbinguni, imeanguka juu ya nchi; naye akapewa ufunguo wa shimo la kuzimu.
2 Akalifungua shimo la kuzimu; moshi ukapanda kutoka mle shimoni kama moshi wa tanuru kubwa; jua na anga vikatiwa giza kwa sababu ya ule moshi wa shimoni.
3 Nzige wakatoka katika ule moshi, wakaenda juu ya nchi, wakapewa nguvu kama nguvu waliyo nayo nge wa nchi.
4 Wakaambiwa wasiyadhuru majani ya nchi, wala kitu cho chote kilicho kibichi, wala mti wo wote, ila wale watu wasio na muhuri ya Mungu katika vipaji vya nyuso zao.
5 Wakapewa amri kwamba wasiwaue, bali wateswe miezi mitano. Na maumivu yao yalikuwa kama kuumwa na nge, aumapo mwanadamu.
6 Na siku zile wanadamu watatafuta mauti, wala hawataiona kamwe. Nao watatamani kufa, nayo mauti itawakimbia.
7 Na maumbo ya hao nzige yalikuwa kama farasi waliowekwa tayari kwa vita, na juu ya vichwa vyao kama taji, mfano wa dhahabu, na nyuso zao zilikuwa kama nyuso za wanadamu.
8 Nao walikuwa na nywele kama nywele za wanawake. Na meno yao yalikuwa kama meno ya simba.
9 Nao walikuwa na dirii kifuani kama dirii za chuma. Na sauti ya mabawa yao ilikuwa kama sauti ya magari, ya farasi wengi waendao kasi vitani.
10 Nao wana mikia kama ya nge, na miiba; na nguvu yao ya kuwadhuru wanadamu miezi mitano ilikuwa katika mikia yao.
11 Na juu yao wanaye mfalme, naye ni malaika wa kuzimu, jina lake kwa Kiebrania ni ABADONI, na kwa Kiyunani analo jina lake APOLIONI.
Sasa hapa biblia imetumia tu lugha ya mfano ili upate halisi ya jinsi mambo yatakavyokuwa.. Hapo anasema wakatoka nzige..Sasa hao sio nzige halisi bali hayo ni Mapepo (maroho) ambayo kwasasa yapo kifunguni..Kumbuka si idadi yote ya mapepo yafayanyayo kazi sasa, yapo mengine mengine yapo kifungoni, biblia inasema hivyo katika kitabu cha Yuda.
Sasa mapepo hayo Yamefananishwa na wale Nzige waharibifu wa mazao, na ulimwengu umefananishwa na shamba lenye mazao (Mathayo 13:38) Na kama unavyojua nzige wakipita mahali kwenye mazao ya kijani, kitendo cha masaa machache tu, hilo shamba linageuka na kuwa vijiti tu.. Ni tishio kubwa sana duniani hata sasa, fuatilia tu habari ya nzige wa jangwani walipopita Afrika Mashariki kipindi cha hivi karibu uone uharibifu wao ulivyokuwa tishio.
Sasa tunajuaje kama haya ni mapepo na si nzige halisi, ni kwasababu hayajapewa kudhuru nchi, bali wanadamu ambao hawana muhuri wa Mungu duniani. Kazi hiyo huwa inafanywa na shetani mwenyewe na malaika zake, Soma Ufunuo 7 utaona hao ambao watakuwa wameitiwa muhuri ni wakina nani. Lakini kama ikitokea unyakuo leo hii umekupita, ujue kuwa mambo hayo yatakukuta tu..
Mapepo haya yatakayoachiliwa kutoka kuzimu na moja kwa moja yatapokea oda kutoka kwa kiongozi wao mkuu shetani/Apolioni/Abadoni, kwa lengo la KUWAHARIBU wanadamu tu. Kama jinsi atakavyojulikana kwa jina hilo.
Mapepo haya yatawaingia watu, bila kizuizi chochote, mengine yatawafanya watu kuwa vichaa, na kuwatesa tu kama yalivyomtesa Yule bwana aliyekutana na Yesu kule makaburini, mengine yatawafanya watu wawe wakatili kupita kiasi, kuchukiana kitaongezeka mara nyingi zaidi, kugombana, kuumizana, na kuuana n.k. mengine yatawafanya watu wapate ajali lakini si za kuwaua, bali za kuwaumiza tu vibaya..
Mengine yatawaletea watu magonjwa yasiyo ya kawaida lakini hakuna kifo, kama vile wakati wa Ayubu, siku hiyo kama hukwenda kwenye unyakuo utakaa kwenye majivu ya kila namna kujipoza lakini wapi, utatamani kufa lakini kifo kitakukimbia, yaani kwa ufupi duniani kutakuwa na watu ambao si watu, maroho hayo yatafanya uharibifu usio kuwa wakawaida.
Mioyo ya wanadamu itaharibiwa kwa kiwango cha juu sana, na kama vile yanavyofananishwa na nzige maana yake ni kuwa mpaka hicho kipindi chao kiishe, watu watakuwa kama makapi tu, wamechoka sana..
Huo wakati ndugu yangu, si wa kuwepo, ukisikia hizi ni siku za mwisho, usidhani unyakuo ukishapita mambo yatakuwa kama unavyoyaona leo.. Ni Roho Mtakatifu ndani ya kanisa lake ndiye anayezuia hayo mambo kwasasa. Lakini kuna wakati utafika, ataondolewa, na akiondolewa anaondoka na kanisa lake takatifu (Ndio unyakuo wenyewe).Kitakachosalia duniani ni vilio tu na kusaga meno (Mathayo 25:30).
2Wathesalonike 2:5 “Je! Hamkumbuki ya kuwa wakati nilipokuwapo pamoja nanyi naliwaambieni hayo?
6 Na sasa lizuialo mwalijua, yule apate kufunuliwa wakati wake.
7 Maana ile siri ya kuasi hivi sasa inatenda kazi; LAKINI YUKO AZUIAYE SASA, HATA ATAKAPOONDOLEWA”.
Swali la kujiuliza, Je! Bado tunaudharau wokovu wa Yesu?.
Je! Bado tunaishi maisha ya kutokujali, mpaka haya mambo yote yatukute? Kama ndivyo ni heri tuyakabidhi maisha yetu kwa Bwana leo, ayaokoe. Vilevile tukabatizwe katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na Kwa jina la YESU KRISTO tupate ondoleo la dhambi zetu. Bwana wetu ni mwingi wa huruma, anatuonya mbele kabla ya mambo hayajatokea kwa ghafla. Hivyo mpokee Kristo leo na atakufanya kiumbe kipya, ulimwengu unapita na mambo yake yote, lakini Kristo na Neno lake wanadumu milele. Na yeye anatuambia itatufaidia nini kuupata ulimwengu mzima na kupata hasara za nafsi zetu?
Bwana atusaidie, Bwana atubariki sote.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Mavu ni nini?
Mavu ni wadudu jamii ya nyuki, kwa jina maarufu ni NYIGU. Maumbile yao ni makubwa zaidi ya nyuki wa kawaida, Na mauvimu yao ni kama tu yale ya nyuki..
Wametajwa mara kadha wa kadha katika biblia, na hivi ni baadhi ya vifungu vinavyowaelezea;
Kutoka 23:27 “Nitatuma utisho wangu utangulie mbele yako, nami nitawafadhaisha watu wote utakaowafikilia, nami nitawafanya hao adui zako wote wakuonyeshe maungo yao.
28 NAMI NITAPELEKA MAVU MBELE YAKO, watakaomfukuza Mhivi, na Mkanaani, na Mhiti, watoke mbele yako.
29 Sitawafukuza mbele yako katika mwaka mmoja; nchi isiwe ukiwa, na wanyama wa bara wakaongezeka kukusumbua”.
Kumbukumbu 7:19 “uyakumbuke hayo majaribu makuu yaliyoyaona macho yako, na hizo ishara, na maajabu, na mkono wa nguvu, na mkono ulionyoka, aliokutolea nje Bwana, Mungu wako; ndivyo atakavyowafanya Bwana, Mungu wako, mataifa yote unaowaogopa.
20 Tena Bwana, Mungu wako, ATAMPELEKA MAVU KATI YAO, hata hao watakaosalia, hao wajifichao, waangamie mbele zako.
21 Usiingiwe na kicho kwa sababu yao; kwa kuwa Bwana, Mungu wako, yu katikati yako, Mungu mkuu, mwenye utisho”.
Yoshua 24:11 “Nanyi mliuvuka Yordani, mkafika Yeriko; nao watu wa Yeriko wakapigana nanyi, Mwamori, na Mperizi, na Mkanaani, na Mhiti, na Mgirgashi, na Mhivi, na Myebusi; nami nikawatia mikononi mwenu.
12 NIKATUMA MAVU MBELE YENU, waliowafukuza mbele yenu hao wafalme wawili wa Waamori, si kwa upanga wako, wala kwa upinde wako”.
Katika mistari hiyo tunaona Mungu alivyowatumia wadudu hawa mavu kama silaha ya kuwafukuza maadui wa Israeli. Kufunua kuwa wapo mavu wa rohoni, ambao Mungu huwa anawatuma kuwafukuza maadui wa watakatifu duniani sasa.
Na mavu wenyewe ni malaika wa Bwana, na maadui wa watakatifu ni majeshi ya mapepo.. Mtakatifu yeyote rohoni huwa analindwa na kundi la malaika wa Bwana, hivyo shetani na mapepoo yake hawezi kumgusa kwa namna yoyote.
Lakini ikiwa mtu yupo nje ya Kristo, ibilisi ni lazima awe na mamlaka juu ya mwili wako. Na mapepo pia ni lazima yatajiamulia kufanya chochote yapendacho ndani yako, kwasababu hawapo mavu wa kukulinda wewe.
Kama hujaokoka na unahitaji kuokoka leo, basi fungua hapa kwa ajili ya sala ya Toba, >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Kumbuka Ni kwa Yesu tu unaweza kuwa salama pengine pote unapotea.
Bwana akubariki.
Tazama na tafsiri ya maneno mengine ya biblia chini.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Neno beramu lina maana gani katika biblia?
Mkatale ni nini katika biblia? (Matendo 16:24)
MUNGU HANA MBARAKA MMOJA TU!..MWAMINI.
DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.
CHUKIZO LA UHARIBIFU
Pomboo ni nini?
Pomboo ni aina ya samaki jamii ya nyangumi anayeishi baharini, Anajulikana kwa jina maarufu la DOLPHIN, Ni samaki anayezaa, pia ananyonyesha, lakini zaidi ya yote anasifa ya kuwa mnyama mwenye akili nyingi kuliko wote ulimwenguni baada ya mwanadamu. Na kuwa na tabia ya uokozi. Tazama picha juu.
Samaki huyu ni rahisi kufundishika, na ni rahisi kuishi na wanadamu.
Katika biblia pomboo(Dolphin) ametajwa sehemu nyingi, hususani katika matumizi ya ngozi yake, ambayo ilitumika katika kutekengeza hema ya kukutania, pamoja na vitu vingine vitengenezwayo kwa ngozi, kama vile viatu vya thamani.
Hivi ni baadhi ya vifungu katika biblia vinavyomtaja Pomboo.
Kutoka 25:3 “Sadaka utakayopokea mikononi mwao ni hii; dhahabu, na fedha, na shaba,
4 na nyuzi za rangi ya samawi, na za rangi ya zambarau, na za rangi nyekundu, na nguo za kitani safi, na singa za mbuzi;
5 na ngozi za kondoo waume zilizotiwa rangi nyekundu, na NGOZI ZA POMBOO, na miti ya mshita,
6 na mafuta ya ile taa, na viungo vya manukato kwa yale mafuta ya kupaka, na kwa ule uvumba wenye harufu nzuri”;
Kutoka 26:14 “Nawe fanya kifuniko cha ile hema, cha ngozi za kondoo waume zilizotiwa rangi nyekundu, na juu yake KIFUNIKO CHA NGOZI ZA POMBOO.
15 Nawe fanya hizo mbao za maskani za mti wa mshita, zenye kusimama”.
Kutoka 35:5 “Katwaeni kati yenu matoleo kwa Bwana; mtu awaye yote aliye na moyo wa kupenda, ayalete matoleo; dhahabu na fedha na shaba;
6 na nyuzi za rangi ya samawi, na za rangi ya zambarau, na za rangi nyekundu, na kitani nzuri, na singa za mbuzi;
7 na ngozi za kondoo waume zilizotiwa rangi nyekundu, na NGOZI ZA POMBOO, na mbao za mshita”;
Ezekieli 16:9 “Kisha nikakuosha kwa maji; naam, nalikuosha kabisa damu yako, nikakupaka mafuta;
10 nikakuvika nguo ya taraza, nikakupa VIATU VYA NGOZI YA POMBOO, nikakufunga nguo ya kitani safi kiunoni mwako, nikakufunika kwa Hariri”.
Mistari mingine ni kama hii;
(Kutoka 35:23, 36:19, 39:34, Hesabu 4:6,8,10,11,12,)
Ni kwanini Mungu aliruhusu hema ya kukutania ifunikwe na ngozi ya samaki hodari (pomboo)?
Kumbuka, wana wa Israeli, waliwashinda maadui zao kabisa kabisa, kwa njia ya habari tu,.pale walipojaribu kuvuka kama wao waligharikishwa,.Hivyo ni kama samaki hodari Mungu aliwavusha baharini pasipo wao kuzama..
Hiyo ni kuwakumbuksha kuwa kila watakapokusanyika mbele ya Hema, na kuitazama hiyo hema iliyofunikwa kwa ngozi ya pomboo, wakumbuke wema wa Mungu aliowafanyia wakati wanaivuka bahari ambayo kwa namna ya kawaida haiwezekani mwanadamu yeyote kuivuka isipokuwa samaki tu peke yake..
Hivyo wamtukuze yeye, na kumpa shukrani zote peke yake.
Bwana akubariki.
Tazama maana maneno mengine ya biblia chini;
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Yeshuruni ni nani katika biblia?
Kitabu cha YASHARI kinachozungumziwa katika 2Samweli 1:17-18, ni kitabu gani?
Areopago ni nini? Kwanini mtume Paulo walimpeleka huko?
Kamsa ni nini kwenye biblia? (Sefania 1:16, Wimbo 3:8)
DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.
MPINGA-KRISTO
Kupokea chanjo ni dhambi kibiblia?
Chanjo ni “ugonjwa dhaifu” unaoingizwa ndani ya mwili wa mtu, ambao mwili una uwezo wa kuudhibiti, na hivyo kuuachia mwili kumbukumbu ya ugonjwa huo pindi utakapokuja tena katika ukamilifu wote siku za mbeleni.
Ili kuelewa zaidi tafakari mfano huu “Mfanya biashara mmoja aliyefanikiwa katika biashara zake, alikuwa akihifadhi fedha zake nyumbani, na nyumba yake hiyo haukuwa na uzio zaidi ya mlango wake mmoja tu wa kuingilia ndani. Siku moja wahalifu walimvamia usiku na kujaribu kuvunja mlango wake, lakini kutokana na kwamba mlango wake ule ulikuwa imara sana na wahalifu wale hawakuwa na zana za kutosha walishindwa kuuvunja mlango ule, wakaondoka…hivyo tukio lile lilimtafakarisha sana yule mfanya biashara, na hivyo akatafuta suluhisho ili tukio kama lile lisijirudie tena, kwamba wasije wahalifu wengine wenye nguvu kuliko wale wa kwanza na kufanikiwa kuvunja mlango na kumwibia na kumdhuru, hivyo kulizuia hilo, kulipopambazuka aliita mafundi wakatengeneza uzio mkubwa kuizunguka nyumba yake yote, na pamoja na hayo akaweka na mlinzi getini pamoja na mbwa”.
Sasa ukilitafakari tukio hilo utagundua kwamba…kwa lile tukio la kwanza lililomtokea la wezi wasio na nguvu za kutosha kujaribu kuvunja mlango wake ni kama limemfungua akili mfanya biashara yule na kugundua kuwa kumbe yupo katika hatari na hivyo anapaswa kujilinda zaidi.
Sasa katika ulimwengu wa sayansi ya tiba, hao wezi dhaifu ndio wanafananishwa na “chanjo” wanapowekwa ndani ya mwili, lengo ni kuupa mwili taarifa za hatari iliyopo na hivyo kujitengenezea kinga madhubuti kwa hatari itakayokuja kutokea mbeleni iliyo mfano wa hiyo.
Kwahiyo matabibu (madaktari) wakati mtoto anapozaliwa, ili kumnusuru wanamweka mtoto chanjo hizo mbalimbali za magonjwa tofauti tofauti..lengo ni ili ule mwili wa mtoto upate taarifa na ujitengenezee kinga mapema kabla huo ugonjwa haujaja kwa nguvu siku za mbeleni. Sasa hilo ndio lengo la kwanza la Chanjo. Na kwa lengo hilo basi sio dhambi kumpa mtoto chanjo, au mtu kupokea chanjo.
Lakini pia sio lazima, kwasababu viwango vya Imani vinatofuatiana. Wapo wengine waliopewa neema ya kumwamini Mungu, na hivyo huweza kuishi bila hivyo vitu, na wasipatikane na madhara yoyote. Hao ni wachache, na wanafanya vizuri zaidi. Lakini pia sio wote wenye imani hiyo, kwahiyo nao pia sio dhambi wakipokea chanjo.
Warumi 14: 1 “Yeye aliye dhaifu wa imani, mkaribisheni, walakini msimhukumu mawazo yake.
2 Mtu mmoja anayo imani, anakula vyote; lakini yeye aliye dhaifu hula mboga.
3 Yeye alaye asimdharau huyo asiyekula, wala yeye asiyekula asimhukumu huyo alaye; kwa maana Mungu amemkubali”.
Hivyo sio dhambi kupokea chanjo!.Na hata kama unayo Imani ya kutokupokea hiyo, hupaswi kuwafanyia hivyo watoto wako, wala kuwahukumu wale wanaopokea…Ni vizuri ukawapeleka watoto wako kwenye chanjo, wewe baki na imani yako..watakapokuwa watu wazima watachagua..
Pia kuna jambo la kuzingatia. Sio kila chanjo ni lazima kupokea au kumpa mwanao, Zipo chanjo za msingi kabisa, ambazo zinajulikana katika mahospitalini, ambazo ni chache sana. Chanjo chache ni vizuri zaidi kwasababu anayetupa afya ni Mungu, na si wanadamu, KİLA KİTU TUNAPASWA TUKİFANYE KWA KİASİ. Na si kuweka tegemeo letu huko asilimia 100, kwamba ndio uhai wetu na ulinzi wetu upo huko. Tukiweka mategemeo yetu huko asilimia 100, hiyo ni dalili tosha kwamba hatuna Imani kwa Mungu hata kidogo. Jambo ambalo ni dhambi na linamtia Mungu wetu wivu na huzuni kwasababu hizo ni sawa na ibada za sanamu.
Hivyo kwa hitimisho: Kupokea Chanjo sio dhambi, wala kumpa mwanao chanjo sio dhambi…Wala kuipa mifugo yako chanjo sio dhambi. Isipokuwa inapaswa itumike kwa kiasi, kwa mimi nionavyo chanjo 3 zinatosha zikizidi sana 4. Mengine tumwamini Mungu atupaye afya na uzima, na atuponyaye. (Zaburi 107:20).
Na chanjo tunayoizungumzia hapa ni ile ya HOSPITALINI na si ya kwa waganga wa kienyeji. Chanjo za waganga wa kienyeji ambazo zinahusisha “kuchanjwa chale” ni za kishirikina, ambazo ni machukizo makubwa kwa Mungu wetu, hizo zinahusiana na ibada za sanamu na Mungu kazikataza..(Soma Walawi 19:28)
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Shalom, karibu tujifunze Biblia.
Katika kitabu cha Mwanzo tunasoma kuhusu uumbaji..Tunasoma Mungu alimwumba Mtu kutoka katika mavumbi ya nchi, lakini Zaidi ya hayo tunaona aliumba na vitu vingine vinavyoonekana kama miti, Wanyama, samaki n.k.
Sasa kama umekisoma vizuri kitabu hicho utagundua kuwa vimetajwa tu vitu na viumbe vinavyoonekana kwa macho, lakini vile visivyoonekana kwa macho havijatajwa. Kwamfano hutaona viumbe kama bakteria wametajwa hapo katika uumbaji..ingawa ni wengi kuliko idadi ya viumbe vyote vinavyoonekana kwa macho, na tena kuna aina nyingi za bakteria na virusi, hutaona pia Mungu kazitaja chembe chembe hai za damu zilizopo ndani ya mwili wa Adamu zinazoishi ndani yake na kumlinda dhidi ya maadui wa mwili wake..hali kadhalika utaona Mungu kataja mavumbi katika kitabu cha mwanzo…lakini hajataja elementi nyingine zilizo ndogo sana na nyingi kuliko mavumbi yote ya dunia na mchanga zinazoitwa protoni na elektoni, zilizopo ndani ya huo mchanga na ndani ya kila kitu.
Kwahiyo hiyo ina maana kuwa Uumbaji wa Mungu sio tu huu wa vitu tunavyoviona kwa macho, bali pia kuna vitu na viumbe vingine vingi visivyoonekana kwa macho ambavyo Mungu kaviumba pia vinavyoishi katikati yetu..Hii tunayoiona ni kama tu “summary” ya vitu vilivyoumbwa.
Na kama umegundua matatizo mengi na mafanikio mengi yanatokana na hivi vitu tusivyoviona…Kwamfano matatizo ya magonjwa yote ni kutokana na hawa bakteria au virusi. Hawaonekani lakini wanaweza kusababisha madhara makubwa, hata kifo, virusi vya korona havionekani kwa macho lakini leo hii vinausumbua ulimwengu.
Vivyo hivyo mafanikio mengi yanatokana na vitu visivyoonekana..kwamfano unaweza kushangaa inawezekanikaje kioo chenye waya waya tu kinaweza kuonyesha sura ya mtu na matukio yake..(kumbe ukifuatilia nyuma yake ni hivyo vitu vidogo sana visivyoonekana protoni na elecroni vinatumika), na umeme ni hivyo hivyo, unajiuliza ule waya mwembamba vile unawezaje kupitisha nguvu kubwa vile ya kuwezesha mashine kusukuma vyuma Na hata kusaga nafaka na kuzifanya unga, au unawezaje kupitisha moto mwingi kiasi kile cha kuchemsha maji kwa dakika tano na yakatokota kabisa. Kumbe nguvu ile inatokana na sayansi ya vitu visivyoonekana (protoni na electroni).
Kwa mantiki hiyo basi, hakuna sababu za kusema kwamba shetani hayupo kwasababu tu hatumwoni, au hakuna sababu ya kusema kwamba mapepo hayapo kwasababu hatuyaoni kwa macho, wala hatuna sababu za kusema kwamba Malaika hawapo..kwasababu tu hatuwaoni.
Matukio mengi yanayoendelea sasa duniani, yanaanzia rohoni. Hata hii dunia tu yenyewe imeumbwa kutoka katika vitu visivyoonekana..kasome Waebrania 11:3.
Kwahiyo vitu vile visivyoonekana ndio vya kuvizingatia Zaidi kuliko vile vinavyoonekana.
2Wakorintho 4:18 “tusiviangalie vinavyoonekana, bali visivyoonekana. Kwa maana vinavyoonekana ni vya muda tu; bali visivyoonekana ni vya milele”.
Na pia vipo vitu vingine ambavyo hata kwa kutumia hizo hadubini havionekani lakini vipo..na tunaamini kuwa vipo..Kwamfano Ile “nguvu ya uvutano ya sumaki” haionekani kwa njia yoyote ile. Mpaka leo hakuna mtu wala mwanasayansi aliyegundua kifaa cha kuiona..Imebakia fumbo mpaka leo.
Vivyo hivyo ndugu, ulimwengu wa roho upo, huo hauonekani kwa macho, vipo viumbe vya rohoni pia navyo havionekani kwa macho, lakini madhara yake ni makubwa katika Maisha yetu.
Kama unakiogopa kirusi cha ukimwi usichokiona kisiingie mwilini mwako kwa kujitenga na uasherati.. Basi kuna viumbe vingine vibaya kuliko hivyo virusi ambavyo vinaweza kuingia mwilini mwako kwa njia hiyo hiyo ya uasherati,(mapepo) vitakavyokuletea madhara kwenye Maisha yako moja kwa moja. Pepo mmoja tu anayeweza kuingia katika Maisha yako kwa njia ya tendo moja tu la uasherati na ana uwezo wa kukuharibia Maisha yako moja kwa moja.
Kama unaogopa kupigwa shoti usiyoiona kwa kushika nyaya za umeme bila uangalifu, basi iogope dhambi kwasababu vipo vitu katika ulimwengu wa roho vibaya kuliko kuliko umeme.. ambavyo havionekani, vyenye uwezo wa kukusababishia hata kupoteza Maisha yako ghafla utakapovisogelea tu.
Biblia ndio “hadubini yetu”. Unaposoma Neno ni rahisi kuzigundua roho hizi na jinsi zinavyotenda kazi..na namna ya kujihadhari nazo. Kwamfano biblia inasema katika Mithali…
Mithali 6:32 “Mtu aziniye na mwanamke hana akili kabisa; Afanya jambo litakalomwangamiza nafsi yake”
Hivyo mtu akilijua hili Neno na akaenda kinyume nalo, anakuwa amefungua mlango wa mapepo kuingia katika Maisha yake.. hataona kwa macho, lakini baada ya kipindi Fulani kupita ndipo atakapoona madhara yake. Madhara ya uasherati wengi wanafikiri ni yale ya kupata HIV tu basi!.. lakini hawajui kuwa mtu anaweza kutoka kufanya usherati leo na akaanguka ghafla tu na kupoteza Maisha, au akafa tu ghafla kifo kisichoeleweka, au akapata ajali au akapoteza tu ghafla kitu cha muhimu katika Maisha yake kama kazi, au heshima.
Bwana atusaidie kuyajua Zaidi mambo ya rohoni kuliko ya mwilini, na kutupa Imani Zaidi.. Nasema hivyo kwasababu siku chache tu nyuma nimekutana na pepo, kwa macho haya ya mwilini barabarani, ndipo Mungu akanipa somo kuwa hizi roho zinazurura huku duniani kutafuta watu kwa nguvu kuwaangamiza, na yanaongeza bidii siku hizi za mwisho kwasababu yanajua muda wao ni mchache, hivyo wanawinda watu kwa nguvu, ili kuwaangamiza.
Hivyo kuwa makini sana. Mambo rohoni sio kama unavyoyasikia. Ingia ndani ya Kristo uwe salama.
Maran Atha.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
KITABU CHA UZIMA
MAFUNDISHO YA MASHETANI
MIHURI SABA
MTUMAINIE YESU ASIYEISHA MATUKIO.
UFUNUO: Mlango wa 6
Mavyaa ni nani?
Neno hilo tunalipata katika mstari huu kwenye biblia;.
Mika 7:6 “Kwa maana mwana humwaibisha babaye, na binti huondoka ashindane na mamaye; na mwanamke aliyeolewa hushindana na MAVYAAYE; adui za mtu ni watu wa nyumbani mwake mwenyewe.
7 Lakini mimi, nitamtazamia Bwana; nitamngojea Mungu wa wokovu wangu; Mungu wangu atanisikia”.
Mavyaa ni Neno la kiswahili linalomaanisha mama-mkwe, – Yaani mama wa mke/mume wako.
Na kwa upande wa Baba-mkwe ni hivyo hivyo linabadilika na kuwa Bavyaa– Yaani baba wa mke/mume wako.
Hivyo kwenye mstari huo, tunapewa picha ya jinsi audui unavyoanza…Kwamba hauanzii mbali, labda kwa watu wasiotujua hapana, bali uadui wa kwanza sikuzote huanzia kwa watu nyumbani mwetu wenyewe, Lakini uadui hauji hivi hivi bali ni lazima uwe na sababu yake. Na ndio maana mstari ambao Bwana Yesu aliurejea alipokuwa anazungumzia habari za mtu kujikana nafsi yake pale anapotaka kumfuata yeye, ulikuwa ni huu, na alisema maneno haya:
Mathayo 10:34 “Msidhani ya kuwa nimekuja kuleta amani duniani; la! Sikuja kuleta amani, bali upanga.
35 Kwa maana nalikuja kumfitini mtu na babaye, na binti na mamaye, na mkwe na mkwe mtu;
36 na adui za mtu ni wale wa nyumbani mwake.
37 Apendaye baba au mama kuliko mimi, hanistahili; wala apendaye mwana au binti kuliko mimi, hanistahili.
38 Wala mtu asiyechukua msalaba wake akanifuata, hanistahili.
39 Mwenye kuiona nafsi yake ataipoteza; naye mwenye kuipoteza nafsi yake kwa ajili yangu ataiona”.
Hivyo, katika wewe safari yako ya imani, (yaani umeokoka), ni lazima uweke akilini kuwa adui za kwanza kukupinga watakuwa ni watu wa nyumbani mwako, aidha watoto wako, au binti zako, au mavyaako, au bavyaako, au kaka zako, au wajomba zako au binamu zako n.k. Usitazamie vita vikubwa kutokea mbali.
Kwasababu adui za mtu ni watu wa nyumbani mwake mwenyewe. Hivyo ukikutana nayo ushingae, songa mbele, ishinde vita, Na Bwana atakuwa pamoja na wewe.
Tazama tafsiri ya maneno mengine ya biblia chini.
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Mkatale ni nini katika biblia? (Matendo 16:24)
Daawa ni nini kama tunavyosoma katika biblia?
Jabari ni nini, kama linavyotumika kwenye biblia?
Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!
SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?
MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.
UTAWALA WA MIAKA 1000.
Mkatale ni nini?
Mkatale ni pingu ya kufungia mtu, inaweza ikawa ya chuma, au mbao nene. Na huwa inafungwa sana sana miguuni, lakini pia shingoni au mikononi,.. Tazama picha juu.
Vifungu vinavyolitaja Neno hilo katika biblia ni kama vifuatavyo;
Matendo 16:24 “Naye akiisha kupata amri hii akawatupa katika chumba cha ndani, akawafunga MIGUU KWA MKATALE.
25 Lakini panapo usiku wa manane Paulo na Sila walikuwa wakimwomba Mungu na kumwimbia nyimbo za kumsifu, na wafungwa wengine walikuwa wakiwasikiliza.
26 Ghafula pakawa tetemeko kuu la nchi, hata misingi ya gereza ikatikisika, na mara hiyo milango ikafunguka, vifungo vya wote vikalegezwa”.
Ayubu 13:25 “Je! Utalitaabisha jani lipeperushwalo? Au, je! Utayafuatia hayo mabua makavu?
26 Kwani umeandika maneno ya uchungu juu yangu, Na kunirithisha maovu ya ujana wangu;
27 Waitia MIGUU YANGU KATIKA MKATALE, na kuyaaua mapito yangu yote; Wajiandikia alama kuzizunguka nyayo za miguu yangu”;
Yeremia 20:2 “Ndipo Pashuri akampiga Yeremia, nabii, AKAMTIA KATIKA MKATALE, uliokuwa pale penye lango la juu la Benyamini, lililokuwa katika nyumba ya Bwana. 3 Hata ikawa, asubuhi, Pashuri huyo akamtoa Yeremia katika MKATALE. Ndipo Yeremia akamwambia, Bwana hakukuita jina lako Pashuri, bali Magor-misabibu”.
Soma pia Ayubu 33:11, 2Nyakati 16:10, Yeremia 29:26.
Hata sasa shetani anawatia watu katika mikatale yake ya mauti. Lakini Yesu Kristo peke yake ndiye anayeweza kuwatoa humo. Swali ni Je! Mimi na wewe Yesu ameshatuweka huru?. Kumbuka hakuna uhuru wowote nje ya Kristo, haijalishi unajiona upo salama kiasi gani, wewe bado upo kwenye mikatale mibaya ya shetani. Na lengo lake ni ufe katika hali hiyo uishie kuzimu.
Hivyo kama hujaokoka, mgeukie Kristo mapema ayaokoe maisha yako, ndani ya hichi kipindi kifupi tulichobakiwa nacho hapa duniani.
Zaburi 107:13 “Wakamlilia Bwana katika dhiki zao, Akawaponya na shida zao.
14 Aliwatoa katika giza na uvuli wa mauti, Akayavunja mafungo yao.
15 Na wamshukuru Bwana kwa fadhili zake, Na maajabu yake kwa wanadamu.
16 Maana AMEIVUNJA MILANGO YA SHABA, AMEYAKATA MAPINGO YA CHUMA”.
Bwana akubariki.
Tazama ufananuzi wa maneno mengine chini.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Jabari ni nini, kama linavyotumika kwenye biblia?
KAMA MMOJA TU NDIO HIVI! SI ZAIDI 153?
KILA MMOJA WENU AJUE KUUWEZA MWILI WAKE.
Nyamafu ni nini?
MKUU WA UZIMA AKUWEKE HURU.
Shalom. Karibu tujifunze Neno la Mungu, maadamu ule mwisho unakaribia..
Kila siku tunapaswa tukumbuke kuwa wokovu ni tunu ya thamani ambayo tunapaswa tuishikilie kwa gharama zozote, wokovu kuupata ni rahisi sana, lakini kuushikilia mpaka mwisho si kitu kirahisi, kwasababu kuna ufalme mwingine (wa giza) hapa duniani ambao upo mahususi kwa kazi hiyo moja tu ya kuhakikisha watu wanaupoteza wokovu hata kama walikuwa wameshaupata.
Na ndio hapa wahubiri tunapaswa tusisitize kwa watu, Kwasababu ndivyo walivyofanya hata na mitume (baba zetu wa imani), ukiangalia utaona mafundisho yao yote yalikuwa ni ya kutilia msisitizo suala la kuishindiania imani, wakatuambia TUISHINDANIE imani ambayo tumekabidhiwa sisi watakatifu mara moja tu.
Yuda 1:3 “Wapenzi, nilipokuwa nikifanya bidii sana kuwaandikia habari ya wokovu ambao ni wetu sisi sote, naliona imenilazimu kuwaandikia, ili niwaonye kwamba mwishindanie imani waliyokabidhiwa watakatifu mara moja tu”.
Sio kwamba walikuwa hawaoni fursa za kibiashara zilizokuwa zimewazunguka mitaani mwao, walikuwa wanaziona, pengine hata zaidi ya sisi, lakini hawakuona sababu ya kutuandikia kwenye hichi kitabu kinachoitwa biblia, kwasababu walijua vita hasaa vipo wapi, mapambano hasa ya mwanadamu duniani yapo wapi..
Tukumbuke kuwa tukibadilishwa maisha yetu, na kufanywa kuwa viumbe vipya, mambo hayatabakia kuwa vilevile kama yalivyokuwa mwanzoni.. Shetani ni lazima aamke na kuanza kuuwinda wokovu wako kwa gharama zozote zile.. atakuchukia kwa ukomo wa chuzi pale tu atakapokuona unaanza kupiga hatua katika wokovu wako, na sio katika mafanikio ya biashara yako, shida yake kubwa ni Imani yako.
Na katika kipindi ambacho unapaswa ujiandae kukutana naye uso kwa uso basi ni wakati ambapo umeanza maisha mapya ya wokovu.
Lakini kama usipoliweka hilo akilini, ukaambiwa ukiokoka basi, wewe ni wa mbinguni moja kwa moja, njoo sasa tukufundishe mambo mengine ya kidunia..Nataka nikuambie maisha yako ya rohoni yapo hatarini sana kugeuka.(Ndio maana kuna kundi kubwa la wakristo waliorudi nyuma leo hii).
Kwasababu shetani ni lazima atahakikisha analeta mambo mawili kwako, la kwanza ni DHIKI, na la pili ni UDHIA.
Mathayo 13:20 “Naye aliyepandwa penye miamba, huyo ndiye alisikiaye lile neno, akalipokea mara kwa furaha;
21 lakini hana mizizi ndani yake, bali hudumu kwa muda; ikitukia dhiki au udhia kwa ajili ya lile neno, mara huchukizwa”.
Dhiki, ni mateso unayoyapata kutokana na kile ulichokiamini; Na udhia ni maudhi utakayoyapata kutoka kwa watu, kwa kile unachokiamini, huu ndio wakati ambapo pengine hata ndugu/familia hawatakuelewa au watakutenga, ni wakati ambapo pengine utajikuta unapingwa na viongozi wako wa dini, au wanakupiga na kukufunga kisa tu umemfuata Yesu, au umekuwa na msimamo Fulani wa Neno la Mungu, ni wakati ambapo mambo yako yanaweza yasiende sawa, utapitia kuvunjwa moyo mara kadhaa, lakini Mungu atakuwa pamoja na wewe, kumbuka yote hayo yanasababishwa na shetani, ili tu kukutikisha urudi ulipotoka. Yanatokea kwa ruhusa maalumu kutoka kwa Mungu.
Lakini ni ya muda tu, hayawezi kudumu milele, Mungu hawezi kuruhusu yadumu milele. Kuna kipindi kitafika yataisha. Lakini ni wachache sana wanaoweza kuvumilia hata hicho kipindi kiishe..
Na hapa ndipo watu wengi wanaporudi nyuma. Na kuuacha wokovu. Kwasababu hawakujiandaa kwa huo wakati.
Kumbuka kuwa tutaufikia mwisho mzuri wa imani, kwa kuishindania kwa gharama zozote na kwa kuvumilia..hilo tu.
Luka 8:15 “Na zile penye udongo mzuri, ndio wale ambao kwa unyofu na wema wa mioyo yao hulisikia neno, na kulishika; kisha huzaa matunda kwa kuvumilia”.
Bwana atusaidie tuweze kuyashinda hayo yote.
Shalom.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Kamsa ni nini?
Kamsa ni Ukelele wa habari ya moto au vita (kwa lugha ya kiingereza-Battle cries)
Vifungu hivyo vinaeleza Neno hilo;
Wimbo 3:8 “Wote wameshika upanga, Wamehitimu kupigana; Kila mtu anao upanga wake pajani Kwa hofu ya KAMSA ZA USIKU”.
Sefania 1:15 “Siku ile ni siku ya ghadhabu, Siku ya fadhaa na dhiki, Siku ya uharibifu na ukiwa, Siku ya giza na utusitusi, Siku ya mawingu na giza kuu,
16 Siku ya tarumbeta NA YA KAMSA, Juu ya miji yenye maboma, Juu ya buruji zilizo ndefu sana.
17 Nami nitawaletea wanadamu dhiki, hata watakwenda kama vipofu, kwa sababu wamemtenda Bwana dhambi; na damu yao itamwagwa kama mavumbi, na nyama yao kama mavi.
18 Fedha yao wala dhahabu yao havitaweza kuwaokoa katika siku ile ya ghadhabu ya Bwana; bali nchi yote pia itateketezwa kwa moto wa wivu wake; maana atawakomesha watu wote wakaao katika nchi hii, naam, ukomo wa kutisha”.
Unaona? Ile siku kuu ya Bwana imefananishwa na ya kama kelele za vita..ambazo huwa zinatokea ghafla..Mfano tu wa Wana wa Israeli walivyozizunguka zile kuta za Yeriko kwa muda wa siku 7 na siku hiyo hiyo ya saba, wakapiga kelele kubwa sana (Kamsa) kuashiria kuwa vita vimeanza..
Na baada ya kilele kutoka, zile kuta za Yeriko zilizama chini saa ile ile, na biblia inatuambia mioyo ya watu wa Yeriko ikayeyuka (Yoshua 5:1) wakaishiwa nguvu kabisa.
Yoshua 6:20 “Basi watu wakapiga kelele, na makuhani wakazipiga tarumbeta; hata ikawa, hapo watu waliposikia sauti ya tarumbeta hao watu wakapiga kelele kwa sauti kuu sana, na ule ukuta wa mji ukaanguka nchi kabisa, hata watu wakapanda juu, wakaingia katika mji, kila mtu akiendelea kukabili mbele; wakautwaa huo mji.
21 Basi wakaangamiza kabisa vitu vyote vilivyokuwa ndani ya mji, wanaume na wanawake, watoto na wazee, na ng’ombe, na kondoo, na punda, kwa makali ya upanga”.
Ndivyo itakavyokuwa katika siku ule ya Mwisho Kristo atakapotokea mawinguni na malaika zake watakatifu.. Tarumbeta na Kamsa italia kutoka mbinguni, kuashiria kuwa mwisho wa kila mwenyewe dhambi umefika..
Siku hiyo kila jicho litamwona, na mataifa yote wataomboleza kwa kilio kisichoweza kuelezeka, lakini hiyo haitasaidia, waovu wote watakuwa kama mizoga juu ya dunia nzima. Ndugu tusitamani tuwepo katika hicho kipindi kibaya sana.
Soma Ufunuo sura ya 19 na 20 yote uone jinsi waovu watakavyoangamizwa na Bwana mwenyewe siku hiyo ikifika.
Swali ni Je! Na wewe unataka uwepo huo wakati? Mimi sitaki, Kumbuka mpaka hayo yote yatokee unyakuo utakuwa umeshapita. Watakaoshuhudia hayo ni wale wote ambao hawakwenda katika unyakuo, watakaopokea chapa ya mnyama.
Ili kufahamu kwa marefu juu ya kalenda ya matukio yote ya siku za mwisho, angalia vichwa vya masomo mengine chini.
Hivyo tubu dhambi zako kama bado wewe ni mwenye dhambi, hizi ni siku za mwisho kweli kweli , siku za Kamsa za Mungu mwenyezi.
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
SIKU YA HASIRA YA BWANA.
MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.
DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.
Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!
CHUKIZO LA UHARIBIFU