Wana kumi na mbili wa Yakobo ndio waliozaa makabila 12 ya Israeli. Majina yao ni kama yafuatavyo;
Zipo kazi au majukumu ambayo makabila yote yaliwajibika kuyatekeleza mfano wa hayo ni kama kumwabudu Mungu, kuihudumia hema, ambayo baadaye ikawa hekalu, ulinzi kwa taifa (msaada wa kijeshi), kuendeleza Sheria ya Mungu kwa vizazi vyote.
Lakini pamoja na hayo, yapo majukumu ambayo yalitekelezwa Zaidi na kabila husuka kuliko mengine. ambapo mengine yaliagizwa na Mungu Moja kwa moja na mengine yalikuja Kama kipawa, walichokirimiwa . Na hatimaye yakawa ni majukumu yao.
Reubeni alipaswa kuwa na jukumu la kiuongozi, kama mzaliwa wa kwanza, lile kusudi lote la ukuhani lingepaswa liwe la lake lakini kwasababu alizini na mke wa Baba yake, akapoteza haki ya mzaliwa wa kwanza akaondolewa nafasi hiyo (mwanzo 35:22, 49:3-4).
Ijapokuwa alishushwa daraja lake. Bado alibakia kutimiza kusudi la kiulinzi upande wa mashariki mwa Israeli kwani jeshi lake, lilikiwa na watu hodari, lakini hawakuwa viongozi wa kijeshi.
Kabila la Simeoni nalo lingepaswa lichukue nafasi kuu katika Israeli, lakini lilishushwa chini kwasababu ya ukatili wao pamoja na Lawi, walipokwenda kuwaua wale washekemu ambao hawakustahili Kufanyiwa mauaji yale, kwa kosa la kumnajisi dada yao.(Mwanzo 34)
Hivyo kabila hili halikuwa na uongozi wowote wa kiroho katika Israeli, zaidi lilimezwa katika kabila la Yuda, kutimiza unabii wa Baba yao (Mwanzo 49:5-7), likabakia kuwa mchango kwenye eneo la kijeshi Israeli.
Lawi lilichukua nafasi ya kikuhani, lilihudumu katika hema na Hekalu, kufanya Upatanisho kwa wana wa Israeli, kwa sadaka mbalimbali pamoja Kufundisha Torati. (Kutoka 32:26-29).
Lawi hawakuwa urithi Israeli, bali walisambazwa katika makabila yote ya Israeli, kama Simeoni, kutimiza unabii wa Baba yao juu ya hasira walioionyesha Isiyo na huruma.(Mwanzo 49:5-7)
Kabila la Yuda lilisimama Kama kabila la Kifalme, na la kikuhani halisi wa milele (2Samuel 7:16)
Ndilo lililoandaa njia ya masihi kuja Duniani,(Mwanzo 49:10).Yuda lilichukua nafasi zote za juu, kutokana na kuwa Reubeni, Lawi na Simeoni kupoteza uwezo wa kuzishika, kwa matendo yao yasiyofaa.
Kabila Hili lilikuwa pia na askari hodari wa vita, na likasimama Kama kitovu cha kiutalawa, kivita na kiibada katika Israeli. Halikadhalika Yuda ilisimama kutunza urithi wa Israeli kwa vizazi vingi baada ya kutawanywa Kwenye mataifa yote, ndio lenyewe tu lililoweza kurudi Israeli.(Mwanzo 49:9-12)
Kabila la Dani lilikuwa na jukumu la kimahakama katika Israeli, (Mwanzo 49:16-18). Lilikuwa ninasimama katika nafasi ya maamuzi. Kuhakikisha Sheria na taratibu zake zinafuatwa ipasavyo.
Lakini pia lilisimama kusaidia Israeli, mahali popote walipoweka marago na kuondoka lilihusika kukusanya vitu vyote muhimu, na kuhakikisha watu wasiojiweza wanatembea Na kundi. (Hesabu 10:25).
Pamoja na hilo lilisimama kama mashujaa wa nyuma wa jeshi la Israeli, pale linapokwenda vitani lilisimama kulinda dhidi ya wavamizi wa nyuma.
lakini baadaye lilikuja kupoteza sifa yake ya kiuamuzi, kwasababu ya kwenda kusimamisha miungu ya kigeni na kuiabudu (Waamuzi 18).
Kabila la hekima na nguvu.
Ni kabila Ambalo lilikuwa na mchango mkubwa Katika eneo la kivita. Tunaweza kuona katika kipindi cha waamuzi kabila hili kwa uongozi wa Debora na Baraka (Waamuzi 4:6), lilimshinda Sisera.
Lakini lilisimama Kama washauri wa kiroho kwa Israeli.
Mwanzo 49:21
[21]Naftali ni ayala aliyefunguliwa; Anatoa maneno mazuri.
Katika wakati wa Kristo, eneo La wanaftali ambalo lilikuwa sehemu ya Galilaya lilidharauliwa sana, na kuonekana nyonge,(Yohana 1:46,7:52) si tu kimaendeleo lakini pia kuwa na wapagani wengi, lakini ndio mahali Ambapo palikuwa mji wa makazi ya Masihi Yesu Kristo, sawasawa na unabii alioutoa Isaya.(Mathayo 4:13-16).
Gadi lilikuwa hodari katika vita, lisilojisalimisha kirahisi kwa maadui, lilisimama Kama Walinzi wa lango la mashariki la taifa la Israeli, pembezoni mwa Reubeni.
Mwanzo 49:19
[19]Gadi, jeshi litamsonga, Lakini atawasonga wao mpaka visigino.
Ni kabila ambalo halikujikita Sana katika mchango Wa kijeshi. Bali Lilikuwa ni kabila la kibiashara Tajiri, lenye kulinda uchumi wa nchi.
Mwanzo 49:20
[20]Asheri, chakula chake kitakuwa kinono, Naye atatoa tunu za kifalme.
Ni kabila Lilipewa neema katika kutambua Nyakati na kutoa mashauri sahihi ya kufanya. lilisimama kama washauri Wa taifa.
1 Mambo ya Nyakati 12:32
[32]Na wa wana wa Isakari, watu wenye akili za kujua nyakati, kuyajua yawapasayo Israeli wayatende; vichwa vyao walikuwa watu mia mbili na ndugu zao wote walikuwa chini ya amri yao.
Walichangia maaskari wa vita, kwasababu walikaa katika fukwe, iliwafanya wawe hodari katika biashara na uchuuzi.
Mwanzo 49:13 Zabuloni atakaa pwani ya bahari, Naye atakuwa kama pwani za kuegesha merikebu, Na mpaka wake utakuwa kando ya Sidoni.
Ni kabila lililopewa nguvu, kiutawala na kijeshi , lilitimiza kusudi la kulisimamisha taifa la Israeli, hata wakati Israeli ilipogawanyika, makao makuu ya kabila zile 10, yalikuwa Ni samaria mji wa Efraimu. (Mwanzo 49: 22-26)
Ni kabila Lililokirimiwa watu hodari wa vita watumiao mashoto (Waamuzi 20:16), ambao walisimama vema katika vita, ijapokuwa lilikuwa dogo, lililojichanganya katika kabila la Yuda ndio kabila la kwanza kutoa mfano Israeli (Sauli), na baadaye mtume Paulo.
La kujifunza: Kuwa mdogo haimaanishi kuwa utakuwa wa mwisho. Bwana anasema walio wa mwisho Watakuwa wa kwanza na wa kwanza watakuwa wamwisho.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Yakobo alimaanisha nini kusema ‘ndipo BWANA atakuwa Mungu wangu’ Mwanzo 28:21
SWALI: Je mtu anaweza akawa hajaokoka akaombea mtu na Pepo likamtoka, na pia mtu anaweza akawa ameokoka akaombea mtu na pepo lisitoke ?
JIBU: Kuhusu swali la kwanza linalosema je mtu anaweza akawa hajaokoka kisha akaenda kuombea mtu mwenye pepo na hatimaye likamtoka?
Jibu ni la!, haiwezekani mtu ambaye hajaokoka, akawa na uwezo wa kutoa pepo, kwasababu pale alipo yupo chini ya vifungo vya ibilisi, haiwezekani akaenda kumfungua mtu ambaye ni mfungwa mwenzake, inahitaji mtu aliye huru ndio aweze kufanya hivyo.
Bwana Yesu alisema…
Marko 3:23-27
[23]Akawaita, akawaambia kwa mifano, Awezaje Shetani kumtoa Shetani?
[24]Na ufalme ukifitinika juu ya nafsi yake, ufalme huo hauwezi kusimama;
[25]na nyumba ikifitinika juu ya nafsi yake, nyumba hiyo haiwezi kusimama.
[26]Na kama Shetani ameondoka juu ya nafsi yake, akafitinika, hawezi kusimama, bali huwa na kikomo.
[27]Hawezi mtu kuingia ndani ya nyumba ya mtu mwenye nguvu, na kuviteka vitu vyake, asipomfunga kwanza yule mwenye nguvu; ndipo atakapoiteka nyumba yake.
Ni hatari huyo mtu akijaribu kufanya hivyo, kwasababu anaweza kukutana na madhara kama yaliyowakuta wale wana wa Skewa.(Matendo 19:13-16).
Kuhusu swali la pili linalouliza Je mtu ambaye ameokoka anaweza akaombea na pepo lisitoke?
Jibu ni ndio Ikiwa mtu huyo anakiwango kidogo cha imani, si mapepo yote yanaweza yakatoka, kwasababu mashetani yanatofautiana kimadaraja (Mathayo 12:43-45), yapo yenye nguvu kubwa ya ukinzani, mengine huitwa wakuu wa giza, mengine wafalme na wenye mamlaka. (Waefeso 6:12)
Hivyo inahitaji nguvu zaidi za kiimani ambazo zinakuja kwa njia ya mifungo na maombi.
Ndio maana mitume kuna mahali walitoa kweli pepo wengi lakini kuna mahali hawakuweza kwasababu ya uhaba wa maombi. (Mathayo 17:14-21)
Lakini uhalisia ni kuwa mtu yeyote aliyeokoka, haijalishi amedumu sana katika wokovu au ni mchanga. Anayo mamlaka ndani yake ya kutoa pepo lolote lile, isipokuwa anahitaji pia na maombi ile mengine yasishindikane kwake.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Musa alikuwa na sababu kadha wa kadha za yeye kufanye vile, ikiwemo
Kutoka 3:11
[11]Musa akamwambia Mungu, Mimi ni nani, hata niende kwa Farao, nikawatoe wana wa Israeli watoke Misri?
Musa aliogopa, kwenda kuwahubiria watu juu ya Mungu Ambaye hakulijua jina lake, kwani zamani zile, miungu yote ilifahamika kwa majina, hivyo alijiona kama kwenda kuwaambia watu habari za Mungu asiyejulikana jina lake, ni kama anawafedhehi.
Kutoka 3:13 Musa akamwambia Mungu, Tazama, nitakapofika kwa wana wa Israeli, na kuwaambia, Mungu wa baba zenu amenituma kwenu; nao wakaniuliza, Jina lake n’nani? Niwaambie nini?
Kutoka 4:1
[1]Musa akajibu akasema, Lakini, tazama, hawataniamini, wala hawataisikia sauti yangu; maana watasema, BWANA hakukutokea.
Kwasababu alikuwa hana ishara yoyote ya ki-Mungu ndani yake.
Kutoka 4:10
[10]Musa akamwambia BWANA Ee Bwana, mimi si msemaji, tokea zamani, wala tokea hapo uliposema na mtumishi wako; maana mimi si mwepesi wa kusema, na ulimi wangu ni mzito.
Pamoja na Mungu kumwakikishia kuwa atakuwa naye na kumsaidia lakini Musa bado akakataa, ndipo Mungu akaghadhibika na kumletea nduguye Haruni, kama msaidizi wake.
Jambo ambalo halikuwa mpango wa awali wa Mungu, kwani uongozi wa Haruni hakuwa kusudi kamilifu la Bwana. Sababu kadha wa kadha zilizowapelekea wana wa Israeli kupata adhabu, zilikuwa ni pamoja na uongozi dhaifu wa Haruni. Utakumbuka wakati Musa amepanda juu mlimani kuchukua zile mbao mbili za amri 10, Haruni aliachiwa uongozi kwa muda, watu walipomfuata Kwa ajili ya hatma zao, akasikiliza mapendekezo yao akawaundia sanamu ya ndama ili waiabudu, ikapelekea Mungu kuwaangamiza wana wa Israeli wengi sana, (Kutoka 32:1-6) mzizi huo ni kutokana na kutokutii kwa Musa, halikadhalika sababu ya Musa kutoiona nchi ya ahadi ilichangiwa pia na uongozi hafifu wa Haruni, kwani kule Meriba kosa alilofinya Musa la kuchukua utukufu wa Mungu, alihusika na Haruni pia. (Hesabu 20:10-12)
Hivyo ni wazi kama angekuwa na imani na Mungu, mengi yasingetokea mbeleni. Hata wakati huu wa sasa, wengi wetu tumejikuta katika machaguzi ya pili ya Mungu kwasababu tu, ya kumpotezea imani, kuwa anaweza kutenda kusudi lake lote hata katika Madhaifu yetu.
Mwamini Mungu mtegemee yeye tu.
Shikilia vifungu hivi vikusaidie.
Mithali 3:5
[5]Mtumaini BWANA kwa moyo wako wote, Wala usizitegemee akili zako mwenyewe;
Isaya 6:8
[8]Kisha nikaisikia sauti ya Bwana, akisema, Nimtume nani, naye ni nani atakayekwenda kwa ajili yetu? Ndipo niliposema, Mimi hapa, nitume mimi.
2 Timotheo 1:7
[7]Maana Mungu hakutupa roho ya woga, bali ya nguvu na ya upendo na ya moyo wa kiasi.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Kwanini Mungu alimchagua Musa, na si mtu mwingine?
Je ni sala gani inahitajika kabla ya kumchinja mnyama katika ukristo?
Je maombi ya mlimani yana ulazima wowote kwa mkristo?
Jibu: Turejee..
Mwanzo 15:16 “Na kizazi cha nne kitarudi hapa, maana haujatimia uovu wa Waamori bado”.
Ili tuelewe vizuri tuanzie ule mstari wa 13..
Mwanzo 15:13 “Bwana akamwambia Abramu, Ujue hakika ya kwamba uzao wako utakuwa mgeni katika nchi isiyo yake, watawatumikia watu wale, nao watateswa muda wa miaka mia nne.
14 Hata na taifa lile, watakaowatumikia, nitawahukumu; baadaye watatoka na mali mengi.
15 Lakini wewe utakwenda kwa baba zako kwa amani, utazikwa katika uzee mwema.
16 NA KIZAZI CHA NNE KITARUDI HAPA, MAANA haujatimia uovu wa Waamori bado”
Katika mistari hiyo Bwana MUNGU anamwambia Abramu kuhusiana na uzao wake kwamba utaenda utumwani katika nchi isiyo yake (ambayo ni nchi ya Misri) na utamtumikia Farao kwa muda wa miaka 400, na baada ya miaka hiyo watatoka Misri.
Sasa wakati Bwana anamwambia Abramu hayo maneno, Abramu alikuwa tayari yupo katika nchi hiyo ya ahadi, isipokuwa bado alikuwa hajaimiliki kwani uzao wake ulikuwa bado mdogo na ilikuwa ni sharti uende kwanza Misri, ukaongezeke huko na kukua, ndio maana Mungu anamwambia kuwa utapelekwa utumwani na kisha utarudi tena katika hiyo nchi Abramu aliyopo muda huo, na itawaondoa wenyeji wa nchi hiyo.
Sasa swali nini maana ya “Kizazi cha Nne kitarudi”..
Jibu: Zamani kizazi kimoja kilihesabika kwa miaka 100, hiko ni kizazi kimoja, kwahiyo vizazi vinne maana yake ni miaka 400.. na mwisho wa hiyo miaka 400 ndio wana wa Israeli walitoka Misri.
Lakini swali lingine ni hili: Ni kwasababu gani uzao wa Abramu ukae Misri miaka muda mwingi hivyo? (400).. Jibu tunalipata katika ule mstari wa 16 unasema..“Na kizazi cha nne kitarudi hapa, maana haujatimia uovu wa Waamori bado”
Kumbe ilihitajika UOVU WA WAAMORI UTIMIE!!..Na hiyo yote ni kuonyesha huruma za MUNGU, kwamba si mwepezi wa hasira, mpaka aachilie ghadhabu yake maana yake ni kwamba kiwango cha maasi kimezidi sana..kile kikombe cha ghadhabu kinakuwa kimejaa..
Kwahiyo hapo aliposema haujatimia uovu wa Waamori, maana yake kiwango cha maasi cha Waamori bado hakikuwa kingi kiasi cha kupigwa na MUNGU.. Lakini baada ya miaka 400 kile kiwango cha maovu na maasi ya Waamori, na ya watu wengine waliokuwa wanaishi Kanaani kilifika kilele, na ndipo MUNGU akaachilia hukumu yake kwa kuwaondoa.
Utazidi kuona MUNGU anawakumbusha wana wa Israeli kuwa sababu ya wenyeji wa Kanaani kuondolewa katika ile nchi, si kwasababu ya utakatifu wa wana wa Israeli, bali ni kwasababu ya maasi ya waliokuwa wanaikalia ile nchi.
Kumbukumbu 9:3 “Basi jua siku hii ya leo kuwa Bwana, Mungu wako, ndiye atanguliaye kuvuka mbele yako kama moto uteketezao; atawaangamiza, tena atawaangusha mbele yako; ndivyo utakavyowafukuza na kuwapoteza upesi, kama alivyokuambia Bwana.
4 USISEME MOYONI MWAKO, BWANA, MUNGU WAKO, ATAKAPOKWISHA KUWASUKUMIA NJE MBELE YAKO, UKASEMA, NI KWA HAKI YANGU ALIVYONITIA BWANA NIIMILIKI NCHI HII; KWANI NI KWA AJILI YA UOVU WA MATAIFA HAYA BWANA AWAFUKUZA NJE MBELE YAKO.
5 Si kwa haki yako, wala kwa unyofu wa moyo wako, hivi uingiavyo kuimiliki nchi yao; lakini ni kwa uovu wa mataifa haya Bwana, Mungu wako, awafukuza nje mbele yako; tena apate kuliweka imara hilo neno Bwana alilowaapia baba zako Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo.
6 Basi jua ya kuwa Bwana, Mungu wako, hakupi nchi hii nzuri uimiliki kwa ajili ya haki yako, kwa maana u taifa lenye shingo ngumu”.
Umeona?… Na MUNGU ni yule yule hajabadilika, kama alivyowavumilia Waamori, na waanaki na Wahiti waliokuwa wanaikalia ile nchi ya ahadi kwa miaka 400, anatuvumilia hata sasa, lakini uvumilivu wake ni ili sisi tutubu, kwasababu hapendi hata mmoja apotee..
Warumi 2:4 “Au waudharau wingi wa wema wake na ustahimili wake na uvumilivu wake, usijue ya kuwa wema wa Mungu wakuvuta upate kutubu?
5 Bali kwa kadiri ya ugumu wako, na kwa moyo wako usio na toba, wajiwekea akiba ya hasira kwa siku ile ya hasira na ufunuo wa hukumu ya haki ya Mungu”.
Je umeitikia wito wa YESU?, Kama bado hujageuka na kumfuata YESU basi usipoteze muda Zaidi, huu ndio wakati, duniani imefikia kilele kabisa cha maovu na maasi, muda wowote parapanda italia na kile kikombe cha ghadhabu ya MUNGU kitamiminwa duniani.
Bwana atusaidie tusiwe miongoni mwa watakaokabiliana na mkono wa BWANA.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Kichwa cha kitabu hichi kinasema “Waraka wa kwanza wa Petro kwa watu wote” Kutuonyesha kuwa Petro Ndiye mwandishi.
Waraka huu mfupi aliuelekeza kwa watakatifu wote waliotawanyika, na kuishi kama wageni maeneo ya Asia ndogo ambayo kwasasa ni nchi ya Uturuki.
Maudhui makuu ya waraka huu tunaweza kuyagawanya katika sehemu kuu nne(4):
1) Ni kuwafariji watakatifu kwa kuwaeleza juu ya utukufu walioandaliwa mbinguni utakaofunuliwa siku ya mwisho. Na kwamba kwa kulitambua hilo basi wafurahi Katika majaribu mbalimbali ya imani, yaliyo ya kitambo tu.
2) Lakini pia unalenga kuwahimiza kuishi maisha ya utakatifu ya kumpendeza Mungu katika wakati wao wa kuishi hapa duniani.
3) Vilevile wajibu wakuishi maisha ya nidhamu katika Jamii ya wasioamini inayowazunguka.
4) Halikadhalika wajibu wa viongozi kulichunga kundi la Kristo kwa uaminifu wotena wajibu wa kanisa lote kumpinga shetani.
Haya ni maelezo mafupi juu ya kila kipengele:
Petro anawahimiza watakatifu kwamba wafurahi katika majaribu mbalimbali (kuliko kuhuzunika) kwa sababu ya uthamani mkuu wa imani yao itakayolipwa siku ile ya mwisho ambayo Yesu atafunuliwa kwetu.
1 Petro 1:6-7
[6]Mnafurahi sana wakati huo, ijapokuwa sasa kwa kitambo kidogo, ikiwa ni lazima, mmehuzunishwa kwa majaribu ya namna mbalimbali;
[7]ili kwamba kujaribiwa kwa imani yenu, ambayo ina thamani kuu kuliko dhahabu ipoteayo, ijapokuwa hiyo hujaribiwa kwa moto, kuonekane kuwa kwenye sifa na utukufu na heshima, katika kufunuliwa kwake Yesu Kristo.
> Petro Anahimiza kuiga kielelezo cha Kristo ambaye yeye alikubali kuteswa ijapokuwa hakutenda Dhambi, hata alipotukanwa hakurudisha majibu. Vivyo hivyo na sisi tukubali teso lolote kwa ajili yake katika upole wote, uvumilivu na ustahimilivu.
1 Petro 2:19-21
[19]Maana huu ndio wema hasa, mtu akivumilia huzuni kwa kumkumbuka Mungu, pale ateswapo isivyo haki.
[20]Kwa maana ni sifa gani kustahimili, mtendapo dhambi na kupigwa makofi? Lakini kustahimili, mtendapo mema na kupata mateso, huu ndio wema hasa mbele za Mungu.
[21]Kwa sababu ndio mlioitiwa; maana Kristo naye aliteswa kwa ajili yenu, akawaachia kielelezo, mfuate nyayo zake.
1 Petro 4:12-16
[12]Wapenzi, msione kuwa ni ajabu ule msiba ulio kati yenu, unaowapata kama moto ili kuwajaribu, kana kwamba ni kitu kigeni kiwapatacho.
[13]Lakini kama mnavyoyashiriki mateso ya Kristo, furahini; ili na katika ufunuo wa utukufu wake mfurahi kwa shangwe.
[14]Mkilaumiwa kwa ajili ya jina la Kristo ni heri yenu; kwa kuwa Roho wa utukufu na wa Mungu anawakalia.
[15]Maana mtu wa kwenu asiteswe kama mwuaji, au mwivi, au mtenda mabaya, au kama mtu ajishughulishaye na mambo ya watu wengine.
[16]Lakini ikiwa kwa sababu ni Mkristo asione haya, bali amtukuze Mungu katika jina hilo.
Sehemu hii ya pili Mtume Petro anawahimiza watakatifu, kuwa kwasababu wanatazamia neema itakayofunuliwa siku ya mwisho ya kuja kwake Yesu Kristo (1:13), hivyo hawana budi kuishi maisha ya kiasi na utakatifu hapa duniani.
1 Petro 1:13-16
[13]Kwa hiyo vifungeni viuno vya nia zenu, na kuwa na kiasi; mkiitumainia kwa utimilifu ile neema mtakayoletewa katika ufunuo wake Yesu Kristo.
[14]Kama watoto wa kutii msijifananishe na tamaa zenu za kwanza za ujinga wenu;
[15]bali kama yeye aliyewaita alivyo mtakatifu, ninyi nanyi iweni watakatifu katika mwenendo wenu wote;
[16]kwa maana imeandikwa, Mtakuwa watakatifu kwa kuwa mimi ni mtakatifu.
1 Petro 2:1-2
[1]Basi, wekeni mbali uovu wote na hila yote, na unafiki na husuda na masingizio yote.
[2]Kama watoto wachanga waliozaliwa sasa yatamanini maziwa ya akili yasiyoghoshiwa, ili kwa hayo mpate kuukulia wokovu;
> Petro anaendelea kuwasihi watakatifu waishi kama wapitaji duniani, kwa kuziepuka tamaa za mwili.
1 Petro 2:11
[11]Wapenzi, nawasihi kama wapitaji na wasafiri, ziepukeni tamaa za mwili zipiganazo na roho.
1 Petro 4:2-3
[2]Tangu sasa msiendelee kuishi katika tamaa za wanadamu, bali katika mapenzi ya Mungu, wakati wenu uliobaki wa kukaa hapa duniani.
[3]Maana wakati wa maisha yetu uliopita watosha kwa kutenda mapenzi ya Mataifa; kuenenda katika ufisadi, na tamaa, na ulevi, na karamu za ulafi, na vileo, na ibada ya sanamu isiyo halali;
> Anaeleza pia Wajibu wa kupendana kuhurumiana, kunyenyekeana, tuwe watu wasiolipa baya kwa baya, bali wenye kubariki(3:8-12, 4:7)
> Kadhalika pia anaeleza wajibu wa wanandoa. Kwamba wake wawatii Waume zao, na kujipamba kwao kunapaswa kuwe kwa mapambo ya rohoni, Lakini pia waume kuishi na wake zao kwa akili. (3:1-7)
Katika sehemu hii ya tatu anahimiza watakatifu kuwa na mwenendo unaopasa kwa watu wasioamini, ili wakose nafasi ya kutushitaki au kutulaumu kwa lolote.
> Anagusia katika eneo la watumwa Kwamba wawatii bwana zao, si wale tu wapole bali pia wale wakali.(2:18)
> Lakini pia Watakatifu waitii kila kilichoamriwa na mamlaka.
1 Petro 2:13-15
[13]Tiini kila kiamriwacho na watu, kwa ajili ya Bwana; ikiwa ni mfalme, kama mwenye cheo kikubwa;
[14]ikiwa ni wakubwa, kama wanaotumwa naye ili kuwalipiza kisasi watenda mabaya na kuwasifu watenda mema.
[15]Kwa sababu ndiyo mapenzi ya Mungu, kwamba kwa kutenda mema mzibe vinywa vya ujinga vya watu wapumbavu;
> Lakini pia anahimiza watakatifu wawaheshimu watu wote(2:17)
Mwishoni Petro anatoa wito wa waangalizi wa kanisa la Mungu (wazee), kwamba walichunge kundi kwa hiari, sio kwa kulazimishwa au kutazamia malipo ya kifedha, bali kwa moyo.
1 Petro 5:1-3
[1]Nawasihi wazee walio kwenu, mimi niliye mzee, mwenzi wao, na shahidi wa mateso ya Kristo, na mshirika wa utukufu utakaofunuliwa baadaye;
[2]lichungeni kundi la Mungu lililo kwenu, na kulisimamia, si kwa kulazimishwa, bali kwa hiari kama Mungu atakavyo; si kwa kutaka fedha ya aibu, bali kwa moyo.
[3]Wala si kama wajifanyao mabwana juu ya mitaa yao, bali kwa kujifanya vielelezo kwa lile kundi.
> Pamoja na hayo anasisitiza watakatifu wote wawe na kiasi na kukesha, kwasababu adui yetu ibilisi ni mfano wa simba angurumaye akitafuta mtu ammeze, hivyo wana wajibu wa kumpinga sikuzote.(5:8-9)
Hitimisho:
Hivyo kwa maelezo machache ni kwamba Petro analihimiza kanisa kutembea katika uvumilivu wote na uthabiti Wa imani, pamoja na utakatifu, na kutimiza wajibu wao katika utakatifu na adabu kwa wanadamu wote, katika wakati ambao kanisa linasubiria neema kuu itakayofunuliwa siku ya mwisho Yesu atakaporudi.
Na ndivyo ambavyo sote tunapaswa tuishi hivyo sasa.
Kama mkristo je unaendelea kufurahi katika majaribu? Unaishi maisha matakatifu? Unaishi vema na jamii yako? unaifanya kazi ya Mungu? Unampinga shetani kwa kudumu katika sala?
Ikiwa hayo, unayazingatia basi, wewe ni mshirika wa neema hiyo kuu ya Mungu itakayofunuliwa siku ya mwisho.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>
https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Mwandishi na uchambuzi wa kitabu cha Wakorintho wa kwanza (1Wakorintho)
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
USIRUDI NYUMA KWA KUITUMAINIA HAKI YAKO.
JINSI SODOMA NA GOMORA ILIVYOKUWA INAVUTIA SANA..
NI LAZIMA KUISHIKILIA IMANI MPAKA MWISHO.
Mwandishi na Uchambuzi wa kitabu cha wafilipi
Kama pale mwanzo kinavyojitambulisha “Waraka wa Paulo mtume kwa wafilipi”.
Paulo ndiye mwandishi wa kitabu hiki. Ni moja ya nyaraka ambazo Paulo aliziandika akiwa kama mfungwa, aidha kule Rumi.
Maudhui makuu ya waraka huu mfupi wenye sura nne(4) yalikuwa ni kuwatia moyo watakatifu na kuwahimiza waiendeleze furaha ya Mungu ndani yao,bila kukwamishwa na dhiki za aina yoyote, lakini pia sehemu ya pili ni kuwataka wapige hatua katika mwenendo wao ndani ya injili waliyoipokea.
Tukianza na hiyo sehemu ya kwanza:
Paulo anahimiza watakatifu kufurahi katika dhiki zote, ikizingatiwa kuwa Kanisa hili lilishuhudia vifungo na mapigo mengi ya Paulo. Kama tunavyosoma kwenye Matendo 16:16-40, Kule ambapo Paulo na Sila walipigwa sana na kutupwa gerezani, biblia inatuambia kulikuwa ni huku Filipi. Lakini hata katika waraka huu bado anashuhudia kuwa dhiki zake, zimekuwa wazi kwa maaskari, na watu wote wa huko (1:12-13).
Hivyo Paulo alijua watu wa Filipi huwenda wakawa na huzuni nyingi juu yake, au juu ya injili, kutokana na dhiki nyingi walizoziona kupitia yeye.
Lakini hapa anawaeleza kuwa yeye anafuraha sikuzote katika Kristo.
> Anaendelea kueleza furaha yake haiathiriwi na watu wanaomzushia fitna ili apitie mateso, maadamu anayeathirika ni yeye si Kristo. Basi bado anafurahi..(1:17-18)
> Anasema hata akihukumiwa kifo kwa ajili ya watakatifu, bado furaha yake itazidi zaidi wala haiwezi kuathiriwa..
Wafilipi 2:17-18
[17]Naam, hata nikimiminwa juu ya dhabihu na ibada ya imani yenu, nafurahi; tena nafurahi pamoja nanyi nyote.
[18]Nanyi vivyo hivyo furahini, tena furahini pamoja nami.
Hivyo anawahimiza pia na wafilipi wafurahi kama yeye, wala wasione huzuni kwasababu ya dhiki hizi, kwasababu tumewekewa kuwa sehemu yetu katika ushuhuda wa injili.
Wafilipi 1:29
[29]Maana mmepewa kwa ajili ya Kristo, si kumwamini tu, ila na kuteswa kwa ajili yake;
Hizi ni sehemu nyingine kadha wa kadha Paulo akihimiza jambo hilo hilo,
Wafilipi 3:1
[1]Hatimaye, ndugu zangu, furahini katika Bwana.
Wafilipi 4:4
[4]Furahini katika Bwana sikuzote; tena nasema, Furahini.
Sehemu ya Pili:
Katika sehemu ya pili Paulo anahimiza watakatifu kuwa na mwenendo unaipasa injili waliyopokea. Na hiyo ni ili wasiwe na ila na lawama,na udanganyifu. Kuonyesha kuwa injili, inayo na taratibu zake..Sio kuamini tu na kusema nimeokoka…bali pia kutii agizo lake.
Wafilipi 1:27
[27]Lakini mwenendo wenu na uwe kama inavyoipasa Injili ya Kristo, ili, nikija na kuwaona ninyi, au nisipokuwapo, niyasikie mambo yenu, kama mnasimama imara katika roho moja, kwa moyo mmoja mkiishindania imani ya Injili;
Anaendelea kusema watakatifu wana wajibu wa kunia mamoja, kutenda mambo yote bila majivuno,wala manung’uniko, wala mashindano, wanapaswa kutenda yote bila ubinafsi bali na ya wengine..
Anasisitiza watakatifu wanapaswa wawe wanyenyekevu, wenye nia ya Kristo..ambaye yeye hapo mwanzo alikuwa kama Mungu lakini alijishusha kwa kukubali kuachia nafasi yake, akawa kama mtumwa, akajinyenyekeza mpaka mauti ya msalaba,lakini Mungu akamkweza zaidi ya vitu vyote..Na sisi tulioipokea injili tunapaswa tuwe na nia hiyo hiyo ya unyenyekevu.(2:1-16)
Anasisitiza zaidi Wakristo wanapaswa wawe wapole, pia wawe waombaji na wenye shukrani.(4:5)
Halikadhalika ni wajibu wetu sote kuutumiza wokovu tulioupokea kwa kuogopa na kutetemeka, kwasababu ndiye Mungu atendaye kazi ndani yetu.(2:12-13)
Pamoja na hayo Watakatifu wana wajibu pia wa kuyahakiki mambo yote yaliyo mazuri na kuyaiga, (2:1-2)
Wafilipi 4:8
[8]Hatimaye, ndugu zangu, mambo yo yote yaliyo ya kweli, yo yote yaliyo ya staha, yo yote yaliyo ya haki, yo yote yaliyo safi, yo yote yenye kupendeza, yo yote yenye sifa njema; ukiwapo wema wo wote, ikiwapo sifa nzuri yo yote, yatafakarini hayo.
Lakini pia anawatahadharisha kujiepusha na wahubiri wa uongo akianzana na wayahudi (watu wa tohara), ambao wanahubiri wokovu kwa njia ya torati zaidi ya ile tuipatayo ndani ya Kristo Yesu kwa njia ya imani. (3:1–16,)
Pamoja watumishi ambao fundisho lao ni la mambo ya duniani tu, na sio yale ya kumwelekeza mtu mbinguni (3:17-21).
Mwisho, Paulo anatoa salamu zake, na shukrani kwa huduma ya utoaji kanisa hilo lililomfanyia, na linaloendelea kumfanyia.
Hivyo kwa hitimisho, waraka huu maudhui kuu ni kuwafariji watakatifu wafurahi katika mambo yote, tukizingatia tunda la Roho ni furaha. Yesu alisema tufurahi na kushangalia pale tunapoudhiwa, kwa ajili ya jina lake. Hivyo, hakuna eneo lolote furaha ya Mungu ndani yetu ,inastahili kukatishwa. Tupitiapo magonjwa kama Epafrodito(2:25-30), shida, njaa, tumefundishwa kuyaweza yote ndani ya Kristo(4:12-3). Hivyo furaha yetu haiwezi kuathiriwa..Ilinde furaha yako.
Lakini anahimiza mwenendo upasao injili. Kwamba huo utaweza kufanikiwa pale tunapokubali kuwa na nia kama ile ya Kristo, ya unyenyekevu.
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >>
https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Rudi Nyumbani
Kama kinavyoanza kwa utambulisho wake, ‘Waraka wa Paulo mtume kwa Wakolosai’.
Paulo ndiye mwandishi wa waraka huu.
Madhumuni makuu ya waraka huu ulikuwa ni kuwasisitiza Wakolosai jinsi Yesu alivyo UTOSHELEVU WOTE, ambaye kwa kupitia yeye Uumbaji wote umekamilishwa ndani yake, lakini si hilo tu bali na utimilifu wote wa ki-Mungu unapatikana ndani yake, pamoja na hazina zote za hekima na maarifa.
Akiwa na maana kuwa mtu akimpata Kristo, hahitaji kitu kingine cha pembeni kumkamilisha yeye, Utoshelevu wote upo kwake.
Hivi ni vifungu mama,
1:15-17
“15 naye ni mfano wa Mungu asiyeonekana, mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote. 16 Kwa kuwa katika yeye vitu vyote viliumbwa, vilivyo mbinguni na vilivyo juu ya nchi, vinavyoonekana na visivyoonekana; ikiwa ni vitu vya enzi, au usultani, au enzi, au mamlaka; vitu vyote viliumbwa kwa njia yake, na kwa ajili yake. 17 Naye amekuwako kabla ya vitu vyote, na vitu vyote hushikana katika yeye”.
2:3
ambaye ndani yake yeye hazina zote za hekima na maarifa zimesitirika.
2:9
“Maana katika yeye unakaa utimilifu wote wa Mungu, kwa jinsi ya kimwili”.
Anaeleza kwa undani katika sura ile ya pili, kwamba ni kutokana na uwepo wa watu waliolivamia kanisa na kuwadanganya kwa maneno ya ushawishi, nia zao ni kuwafanya mateka kwa elimu isiyo na matunda, ya mapokeo ya kibinadamu, yasiyo ya Kristo (2:8). Kwamba mtu akishika hayo, ndio utimilifu wote unapatikana.
Vilevile kuonekana kwa baadhi ya desturi za kiyahudi ndani ya kanisa, kama vile kushika sikukuu, tohara, sabato, na mwandamo wa mwezi. Vikidhaniwa kuwa vitu hivyo vinaweza kuleta ukamilifu wote pamoja na Kristo (2:11-23)
Na pia kuzuka kwa ibada bandia za kuabudu viumbe vya rohoni (malaika), kwa mawazo kuwa mtu ataupokea ukamilifu.(2:18)
Paulo anaeleza yote hayo hayana wokovu, isipokuwa kwa njia ya haki tuliyoipokea kwa msalaba wake uliofuta hati ya mashtaka yetu, kwa mateso yake pale msalabani ambayo kwa kupitia njia hiyo tumepokea msamaha wa dhambi, pale tu tunapoamini na kubatizwa (2:12-17)
Sehemu ya tatu Paulo anaeleza kwamba kuamini ni pamoja na kuuvaa utu upya wa Kristo. Hivyo huyu mtu hatarajiwi kuendelea kuishi hivi hivi tu, kisa Kristo amemkamilisha kwa kila kitu, bali anapaswa aenende kwa Kristo mwenyewe, ayafikiri yaliyo juu, (3:1-17),
Kwa namna gani?
Kwa kuzifisha tabia za mwilini, kama uasherati, uchafu, kutamani, mawazo mabaya, ghadhabu, matusi. Lakini pia kujivika utu wema, moyo wa rehema, unyenyekevu, upole, uvumilivu, kusameheana, upendo, ibada. Vilevile si tu katika mambo ya rohoni , bali mpaka kwenye ngazi za kifamilia, kwamba wake kuwatii waume zao, na waume kuwapenda wake zao, na watoto kuwatii wazazi. Hizo ndio tabia za utu mpya.
Katika sura ya 4.
Bado Paulo aendelea kueleza huo mwenendo ndani ya Kristo, unapaswa uonekane mpaka kwa mabwana, kwa watumwa wao. Kwamba mabwana wawape watumwa haki zao, Lakini pia watakatifu wote, wanapaswa kudumu katika maombi, na kuenenda kwa hekima kwa watu wasioamini, katika usemi bora, na kujifunza kuukomboa wakati.
Na mwisho.
Paulo anawasilisha salamu za washirika wenzake wa injili, kwa Wakolosai ikiwemo, Epafra, Luka, Dema, marko, Aristarko, Yusto.
Hitimisho.
Kwa ufupi waraka huu, hueleza kwamba utoshelevu wote upo ndani ya Kristo tu na sio zaidi ya hapo, hatuhitaji kitu kingine cha pembeni kutukamilisha sisi, Lakini ni wajibu wa huyu mkristo kutembea katika maisha mapya ndani yake. Kwasababu mambo yote mawili yanakwenda sambamba hayatengani. Kristo huokoa na kutakasa wakati huo huo. Unapookolewa, saa hiyo hiyo umevikwa utu upya. Huwezi kuendelea katika dhambi.
Ni kipi cha ziada tunachoweza kujifunza katika waraka huu?.
Maombi ya Paulo na Eprafa yasiyokoma kwa kanisa hili(1:3, 9, 4:12):
Hatuna budi kujijengea desturi ya sikuzote kuliombea kanisa la Bwana, hususani mahali tulipo, pamoja na watakatifu wengine tuwajuao. Kwasababu kusimama kwa kanisa hutegemea sana maombi yasiyokoma.
Bwana akubariki. ||kiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii. Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
Nijapokuwa sipo kwa mwili, lakini nipo pamoja nanyi kwa roho,
Rudi Nyumbani
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
LIPO LA KUJIFUNZA KWA WALE MASHUJAA 37 WA DAUDI.
Nini maana ya Dirii, Chapeo na Utayari?
Amka, Ee upanga, juu ya mchungaji wangu (Zekaria 13:7-9)