Category Archive Home

Kama Bwana anawajua walio wake tangu asili kwanini tunahubiri injili? (Warumi 8:29).

Jibu: Tusome,

Warumi 8:29 “Maana wale aliowajua tangu asili, aliwachagua tangu asili wafananishwe na mfano wa Mwana wake, ili yeye awe mzaliwa wa kwanza miongoni mwa ndugu wengi.

30 Na wale aliowachagua tangu asili, hao akawaita; na wale aliowaita, hao akawahesabia haki; na wale aliowahesabia haki, hao akawatukuza”.

Ni kweli maandiko hapo yanasema Bwana anawajua walio wake tangu asili.

Ili Mungu awe Mungu ni lazima ajue mambo yote, ni lazima aujue mwisho katika mwanzo. Vinginevyo asipojua hivyo, huyo sio Mungu.

Lakini pamoja na kujua hatima zetu wote, bado hajatuambia ni nani ataokolewa na nani hataokolewa. Nafasi ya kuokolewa ipo kwa wote, kadhalika nafasi ya kupotea ipo kwa wote, ni jukumu letu sisi kupambana ili tusijikute tumeingia katika hilo kundi la ambao hawataokoka na kuingia katika ziwa la moto.

Bwana Yesu alijua tangu mwanzo ni Nani atakayemsaliti, na akawaambia mapema wanafunzi wake kwamba mmoja wenu atanisaliti, Lakini hakutaja jina kwamba ni Yuda!. Aliachia hapo katikati, kila mtu ajihisi kama ni yeye, ili lengo kila mtu ajitathmini mienendo yake na ajihadhari na roho ya usaliti.

Lakini Bwana kwa kusema hivyo, hakuacha kuendelea kuwahubiria wanafunzi wake, au hata Yuda na wanafunzi pia waliendelea kuhubiri, kwasababu siri ya atakayemsaliti alikuwa nayo Bwana na sio wao..Hivyo kazi waliyokuwa nayo ni kuendelea na kuhubiri injili, na kujitahidi wasitimize huo unabii…

Marko 14:18 “Nao walipokuwa wameketi chakulani, wakila, Yesu alisema, Amin, nawaambia, Mmoja wenu, naye anakula pamoja nami, atanisaliti.

19 Wakaanza kuhuzunika, wakamwambia mmoja mmoja, Je! Ni mimi?

20 Akawaambia, Ni mmoja wa hao Thenashara, ambaye achovya pamoja nami katika kombe”.

Na hata sasa Mungu anatuambia lipo kundi litakalomsaliti, lipo litakaloingia katika ziwa la moto, lakini hajataja majina, hivyo ni wajibu wetu sisi kupambana tusiwe mojawapo ya hao.

Sasa swali tunalopaswa tujiulize kila mmoja wetu ni hili:

Utajuaje kama wewe utaangukia katika kundi la watu ambao wataingia jehanamu ya moto?..

Hautajua kwa tafsiri ya jina lako, wala kwa rangi ya uso wako, wala kwa kimo chako, wala kwa jinsia yako wala kwa kabila ulilotokea au familia uliyotokea.

Bali utajijua kwa tabia zako!. Kama maisha yako bado ni ya dhambi, ya anasa, ya kiulimwengu na uzinzi na uasherati, ya kuabudu sanamu, ya kutokujali mambo ya Ki-Mungu kama Yuda, ingawa unaonywa mara nyingi..basi fahamu kuwa upo miongoni mwa lile kundi lililotabiriwa kutourithi uzima wa milele.

Kadhalika kama upo ndani ya Kristo, na umepokea Roho Mtakatifu, na unayafanya mapenzi yake basi fahamu kuwa upo katika kundi la watu waliotabiriwa uzima wa milele.

Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba injili tunapaswa tuendelee kuihubiri kama mitume walivyoendelea na kazi hata baada ya kujua kuwa miongoni mwao yupo atakayemsaliti Bwana..zaidi sana tujihadhari na dhambi ili tusiwe miongoni mwa watakaotupwa katika ziwa la moto.

2 Timotheo 2:19 “Lakini msingi wa Mungu ulio imara umesimama, wenye muhuri hii,
Bwana awajua walio wake.
Na tena, Kila alitajaye jina la Bwana na auache uovu

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Rudi nyumbani

Print this post

Kutia mkono chini ya paja kama ishara ya kiapo, kulimaanisha nini?

Tofauti na desturi za mataifa mengi ya sasa zilivyo, kwamba mtu akitaka kuapa, huwa anashika kitabu Fulani cha dini kama vile biblia, au anaweka mkono wako kifuani ndipo anatamka kiapo chake..Zamani kulingana na desturi wa wayahudi ilikuwa ni mtu anaweka mkono wake, chini ya paja la anayemwapisha.

Pajani kibiblia ni sehemu ambayo ipo karibu sana na viungo vya uzazi.. Sehemu nyeti, ambapo hapawezi kufikiwa kama jambo lililopangwa halihitaji umakini sana. Ni sawa na leo watu wanavyotumia biblia mahakamani kuapa, ni kitabu nyeti sana, kiasi kwamba mpaka kimetumiwa hiko ni kuonyesha umakini wa kile unachotakiwa kukifanya.

Na ndivyo ilivyokuwa kwa Ibrahimu, na Yakobo. Kwamfano Ibrahimu alipotaka mwanawe Isaka apatiwe mke kutoka katika nyumba ya Ndugu yake, aliyekuwa mbali sana, alimwita mtumwa wake, akamwapisha kwamba akamletee binti sawasawa na alivyomwagiza, Hivyo ili kuthibitisha kuwa mtumwa wake atayatekeleza yale aliyoagizwa, akachukua mkono wake, na kuulia katika paja lake, kuonyesha pia kwamba yupo tayari kutii kila agizo lililoamriwa juu yake.

Mwanzo 24:2 “Ibrahimu akamwambia mtumishi wake, mzee wa nyumba yake, aliyetawala vitu vyake vyote, Tafadhali uutie mkono wako chini ya paja langu, 3 nami nitakuapisha kwa Bwana, Mungu wa mbingu, na Mungu wa nchi, kwamba hutamtwalia mwanangu mke katika binti za Wakanaani ambao nakaa kati yao;”…

9 Yule mtumishi akaweka mkono wake chini ya paja la Ibrahimu bwana wake, akamwapia katika neno hilo. 10 Kisha huyo mtumishi akatwaa ngamia kumi katika ngamia za bwana wake akaenda zake, maana mali zote za bwana wake zilikuwa mkononi mwake, akaondoka, akaja mpaka Mesopotamia, mpaka mji wa Nahori.

Jambo kama hilo tunaliona pia kwa Yakobo, siku ile alipokaribia kufa, alimwita Yusufu na kumwambia, aweke mkono wake chini ya paja lake, ali amwapie, kwamba hatamzika kule Misri bali, katika nchi ya Baba yake.

Mwanzo 47:29 “Siku za kufa kwake Israeli zikakaribia; akamwita mwanawe Yusufu, akamwambia, Kama nimeona kibali machoni pako, weka mkono wako chini ya paja langu, ukanifanyie rehema na kweli; nakusihi usinizike katika Misri.

30 Lakini nitakapolala pamoja na baba zangu, unichukue toka Misri, unizike katika kaburi lao. Akasema, Nitafanya kama ulivyosema.

31 Akanena, Niapie. Naye akamwapia. Israeli akajiinamisha kwenye mchago wa kitanda”.

Lakini sisi katika agano jipya, hatujapewa ruhusa ya kuapa bali Bwana Yesu alisema, maneno yetu yawe Ndio, ndio.. Au Sio,..sio..Na si zaidi. (Mathayo 5:33-37). Hakuna sababu ya kuapa, kwasababu hatuna mamlaka ya kutangua au kuthibitisha chochote katika maisha yetu kana kwamba vipo chini ya uwezo wetu.
Sisi si Mungu.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Naomba kujua nini maana ya kuteguka uvungu wa paja?

Je Bwana Yesu alikuwa na mchoro (tattoo) katika paja lake? (Ufunuo 19:16).

JE! NI KWELI UMEMFUATA YESU?

Kwanini Yesu aliwakataza mitume wake kumdhihirisha?

Rudi nyumbani

Print this post

MFANYE BWANA YESU MWENYEJI MAISHANI MWAKO.

Ipo tabia moja  ya kipekee ya wageni waliostaarabika. Kikawaida wageni walio wastaarabu huwa wanaonyesha tabia fulani baadhi ambazo wenyeji wanapaswa wazijue ili waweze kuchukuliana nao na kuendana nao.

Kikawaida mgeni sio mtu wa kuonyesha moja kwa moja kwamba anajitaji jambo fulani kutoka kwa mwenyeji, mgeni akija kukutembelea bila shaka hawezi kukuomba chakula hata kama ana njaa sana, utaona atakaa na wewe kimya, na  tena utakapofika wakati wa kuondoka, utaona anaondoka bila hata kukukumbusha suala la chakula, tena utaona anaondoka kwa furaha sana, na wakati mwingine hata kwa kukupa asante nyingi. Lakini moyoni, hajafurahishwa sana!.

Hivyo ni wajibu wako wewe kupambanua ni nini mgeni anahitaji kwa wakati huo. Kama ni chakula, au makazi au malazi.. Ili ajisikie yupo nyumbani kadhalika awe huru kuzungumza nawe zaidi..

Ukiona mgeni kakutembelea asubuhi jua kuna kitu anakihitaji kwako kwa asubuhi hiyo usimfanye akae mpaka jioni, wala usijifanye huelewi, ukiona mgeni kafika kwako mchana wakati wa kupata riziki, ujue ana nafasi pia katika hicho chakula, ukiona anashinda kwako mpaka jioni, ujue pengine anahitaji kulala kwako, mwekee mazingira ya kulala kwasababu pengine kuna jambo na atakapoona umemwelewa hali yake na umemruhusu ale chakula chako, au alale kwako, basi ni rahisi zaidi kusikia mengi kutoka kwake, au kukufunulia mengi.

Lakini ukimnyima riziki, au makazi, au malazi.. utafikiri kweli umemkomoa lakini hutasikia mengi, ambayo angetaka kukuambia..

Kadhalika Kristo naye kuna wakati anakuja kwetu kama Mgeni, au anatukaribia kama mgeni, na anakuwa anaonyesha tabia zote kama za mgeni. Atakuwa ana njaa, lakini atajifanya kama hana njaa, atakuwa anatamani kuja kulala na sisi lakini atajifanya kama anapita tu!. Ndicho kilichowatokea wale watu wawili waliokuwa wanakwenda Emau.

Hebu tuisome habari hiyo vizuri katika kitabu cha Luka.

Luka 24:13 “Na tazama, siku ile ile watu wawili miongoni mwao walikuwa wakienda kijiji kimoja, jina lake Emau, kilichokuwa mbali na Yerusalemu kama mwendo wa saa mbili.

14 Nao walikuwa wakizungumza wao kwa wao habari za mambo hayo yote yaliyotukia.

15 Ikawa katika kuzungumza na kuulizana kwao, Yesu mwenyewe alikaribia, akaandamana nao.

16 Macho yao yakafumbwa wasimtambue.

17 Akawaambia, Ni maneno gani haya mnayosemezana hivi mnapotembea? Wakasimama wamekunja nyuso zao.

18 Akajibu mmoja wao, jina lake Kleopa, akamwambia, Je! Wewe peke yako u mgeni katika Yerusalemu, hata huyajui yaliyotukia humo siku hizi?

19 Akawauliza, Mambo gani? Wakamwambia, Mambo ya Yesu wa Nazareti, aliyekuwa mtu nabii, mwenye uwezo katika kutenda na kunena mbele za Mungu na watu wote;

20 tena jinsi wakuu wa makuhani na wakubwa wetu walivyomtia katika hukumu ya kufa, wakamsulibisha.

21 Nasi tulikuwa tukitumaini ya kuwa yeye ndiye atakayewakomboa Israeli. Zaidi ya hayo yote, leo ni siku ya tatu tangu yalipotendeka mambo hayo;……………..

25 Akawaambia, Enyi msiofahamu, wenye mioyo mizito ya kuamini yote waliyoyasema manabii!

26 Je! Haikumpasa Kristo kupata mateso haya na kuingia katika utukufu wake?

27 Akaanza kutoka Musa na manabii wote, akawaeleza katika maandiko yote mambo yaliyomhusu yeye mwenyewe.

28 Wakakikaribia kile kijiji walichokuwa wakienda, NAYE ALIFANYA KAMA ANATAKA KUENDELEA MBELE.

29 Wakamshawishi wakisema, Kaa pamoja nasi, kwa kuwa kumekuchwa, na mchana unakwisha. Akaingia ndani kukaa nao”.

Hapo katika mstari wa 29 maandiko yanasema.. “NAYE ALIFANYA KAMA ANATAKA KUENDELEA MBELE.” Yaani baada ya kuzungumza nao muda wote huo, umefika wakati wa kuingia ndani, yeye anajifanya kama anataka kuendelea na safari!.. Hebu jiulize endapo wale watu wangekuwa wachoyo, na kusema kile chakula chetu kule ndani kinatutosha tu sisi wawili, huyu mtu mwache aendelee zake, je wangekosa mangapi?..au wangesema kile kitanda chetu kule ndani kinatutosha tu sisi wawili na si mwingine watatu, wangekosa mangapi?..Lakini tunaona walielewa hali ya mgeni kwamba kamwe hawezi kusema naomba jambo fulani kama anaona wenyeji hawana huo moyo.. Sasa hebu tuone wangekosa nini endapo wangemruhusu Bwana aende zake.. Tuendelee mbele kidogo katika mistari hiyo…

Luka 24:29 “Wakamshawishi wakisema, Kaa pamoja nasi, kwa kuwa kumekuchwa, na mchana unakwisha. Akaingia ndani kukaa nao.

30 Ikawa alipokuwa ameketi nao chakulani, alitwaa mkate, akaubariki, akaumega, akawapa.

31 Yakafumbuliwa macho yao, wakamtambua; KISHA AKATOWEKA MBELE YAO.

32 Wakaambiana, Je! Mioyo yetu haikuwaka ndani yetu hapo alipokuwa akisema nasi njiani, na kutufunulia maandiko?

33 Wakaondoka saa ile ile, wakarejea Yerusalemu, wakawakuta wale kumi na mmoja wamekutanika, wao na wale waliokuwa pamoja nao”,

Umeona, kumbe sio kila mgeni ni mgeni wa kawaida tu!, si kila anayekuomba ni kwasababu anashida, si kila anayetaka kuja kukaa na wewe ni kwasababu yake yeye, wengine wanataka kuja kwako kwa faida yako wewe, wengine wanataka kula chakula chako kwa faida yako wewe… Unyonge wa Kristo kwako ni kwasababu anataka wewe upate faida.

Hivyo hata leo hii, Kristo anakuja mioyoni mwetu kama mgeni, hivyo hatuna budi tumpe nafasi.

Jambo moja wengi wasilolijua ni kwamba Kristo sio dikteta, kwamba tunapompokea basi ataanza kututumikisha kama maroboti, siku zote anakuwa kama mgeni..maana yake unapompa nafasi zaidi ndivyo anavyojifunua kwako zaidi, unapomkataa anakuacha na kukupita..wala hakulazimishi, ingawa atakuonyesha kila dalili za kutamani kuendelea kukaa na wewe…

Na sio tu katika hatua ya kumpokea yeye, bali hata baada  ya kumpokea Yeye, endapo tukijitenga naye..na kujikuta tumezama kwenye mateso au majaribu hatakuja kutulazimisha atusaidie, atasogea karibu na sisi, kuonyesha ishara ya kutaka kutusaidia, lakini kama hatutampa basi hatatupa msaada..

Utasema hilo tunalithibitisha vipi kimaandiko…Hebu tusome kile kisa cha Bwana kutembea juu ya maji ni nini kiliwatokea mitume, na kwa jinsi gani Bwana aliwasaidia.

Marko 6:48 “Akawaona WAKITAABIKA kwa kuvuta makasia, kwa maana upepo ulikuwa wa mbisho; hata ilipopata kama zamu ya nne ya usiku akawaendea, akitembea juu ya bahari; AKATAKA KUWAPITA.

49 Nao walipomwona anatembea juu ya bahari, walidhani ya kuwa ni kivuli, wakapiga yowe,

50 kwa kuwa wote walimwona, wakafadhaika. Mara akasema nao, akawaambia, Changamkeni; ni mimi, msiogope”.

Ukisoma habari hiyo sehemu nyingine utaona, Baada ya Bwana kuingia chomboni, ule upepo ulikoma!.

Lakini nataka tuone hapo kwenye mstari wa 48, maandiko yanasema “AKATAKA KUWAPITA”.. Umewahi kujiuliza kwanini alikuwa anataka kuwapita?.. Ni kwasababu bado alikuwa hajaona kibali cha yeye kutoa msaada…ndio maana akataka kuendelea mbele

Sasa kama Kristo aliweza kufanya hivyo kwa wanafunzi wake!, ambaye aliwachagua yeye mwenyewe, atashindwaje kufanya kwangu na kwako?.

Huu ni wakati wa kumpa Kristo nafasi na kumfanya mwenyeji ndani yetu…

Unajua kabisa huelewi maandiko unapoyasoma, lakini bado humpi Yesu nafasi katika maisha yako, bado kwako ni mgeni mnyonge!.. Kwenda kanisani kwako ni jambo la kusukumwa na kulazimishwa!, kujikana nafsi kwako ni jambo zito.. ukiambiwa uache kuvaa suruali tu! Ni shida, uache vimini na mavazi yasiyo na heshima ni shida.. Kristo atajifunuaje kwako!.. Hawezi kwasababu akiangalia huku na huko anaona milango kila mahali imefungwa!… Unapitia tabu lakini hata kumtolea Mungu huwezi, zaidi sana unapinga matoleo, pasipo kujua kuwa wakati mwingine ni kwa faida yako si ya Kristo.

Je! Kristo ni mgeni au mwenyeji kwako?

Bwana Yesu anasema..

Mathayo 25:41“Kisha atawaambia na wale walioko mkono wake wa kushoto, Ondokeni kwangu, mliolaaniwa, mwende katika moto wa milele, aliowekewa tayari Ibilisi na malaika zake;

42 kwa maana nalikuwa na njaa, msinipe chakula; nalikuwa na kiu, msininyweshe;

43 nalikuwa mgeni, msinikaribishe; nalikuwa uchi, msinivike; nalikuwa mgonjwa, na kifungoni, msije kunitazama”.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya ya kila siku kwa njia ya Whatsapp  basi waweza kujiunga kwa kubofya hapa >>> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

YESU NI MFALME WA AINA GANI KWAKO? 

Je! mwanadamu wa kwanza kuumbwa ni yupi?

Kama tunaokolewa kwa neema kwanini wokovu tuupate kwa nguvu?

“Si watu wa kutumia mvinyo sana”, je tunaruhusiwa kutumia mvingo kidogo?(1Timotheo 3:8).

Hapana hata mmoja aliyethubutu kuambatana nao;

Tarshishi ni mji gani kwasasa?

Rudi nyumbani

Print this post

NI KIZAZI KIPI WEWE UPO?

Kibiblia  Kizazi ni kundi la watu linalozuka ghafla lenye tabia zinazofanana, linaweza kuzuka aidha kutokana na mabadiliko ya nyakati, au mabadiliko ya mazingira. Kwamfano, Wana wa Israeli walipokuwa Misri, chini ya Yusufu, waliishi kwa raha sana, Lakini Yusufu alipokufa pamoja na Yule Farao, kilinyanyuka kizazi kingine kisichokumbuka wema wa Yusufu, na hapo ndipo utumwa mgumu ulipoanza.

Vilevile, Wana wa Israeli walipofika katika nchi yao ya  Ahadi, mwanzoni waliishi maisha ya kumcha Mungu sana, lakini wakati ulipopita mrefu kilinyanyuka kizazi kingine kisichomjali Yehova, hapo ndipo Israeli ilipoanza kuingia katika matatizo mengi sana.(Waamuzi 2:10)

Na katika hichi kipindi cha Siku za mwisho, tunapaswa tuwe makini sana, Zipo tabia ambazo utaziona kwa watu wengi sana, lakini kiuhalisia hazikuwepo huko nyuma. Hivyo ni vizuri ukafahamu aina ya vizazi vilivyopo duniani sasa hivi  kulingana na biblia ili ujue wewe upo wapi na jinsi gani unapaswa ujiupeshe navyo.

  1. Kizazi cha uzinzi na zinaa:

 Bwana Yesu alisema..

Mathayo 12:39 “Akajibu, akawaambia, Kizazi kibaya na cha zinaa chatafuta ishara, wala hakitapewa ishara, ila ishara ya nabii Yona”.

Ni kizazi cha watu kinachozuka kinapenda tu usherati na uzinzi kuliko kitu kingine chochote ulimwenguni. Leo hii tazama  mawazo ya vijana wengi yalivyo, sikiliza mazungumzo yao,  mambo wanayoyafanya kwa siri,vitu wanavyotazama mitandaoni, video za ngono, ni jambo la kawaida kwao, na kibaya zaidi sio tu vijana, hadi wazee na watoto wamo katika kundi hili. Jambo ambalo hapo zamani halikuwepo. Hiyo ni kuthibitisha kuwa ni hiki ni kizazi kingine kimezuka, ambacho ni hatari sana.

Bwana Yesu alisema..

Marko 8:38 “Maana kila mtu atakayenionea haya mimi, na maneno yangu, katika KIZAZI HIKI CHA UZINZI na dhambi, Mwana wa Adamu atamwonea haya mtu huyo, atakapokuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika watakatifu”.

Ndugu, jiupeshe, na mkondo huu, si lazima uishe kama ulimwengu unavyotaka, kizazi hiki kimeshahukumiwa na Mungu.

     2) Kizazi cha nyoka:

Kipo kizazi cha Nyoka.

Mathayo 3:7 “Hata alipoona wengi miongoni mwa Mafarisayo na Masadukayo wakiujia ubatizo wake, aliwaambia, Enyi wazao wa nyoka, ni nani aliyewaonya ninyi kuikimbia hasira itakayokuja?

8 Basi zaeni matunda yapasayo toba;

9 wala msiwaze mioyoni mwenu kwamba, Tunaye baba, ndiye Ibrahimu; kwa maana nawaambia ya kwamba Mungu aweza katika mawe haya kumwinulia Ibrahimu watoto”.

10 Na shoka limekwisha kuwekwa penye mashina ya miti; basi kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa motoni.

Soma pia..Mathayo 12:34

Nyoka, alikuwa mwerevu sana kuliko wanyama wote mwituni, lakini alikubali kuwa chombo teule cha shetani. Uzao wake, ndio uliendelea mpaka kwa Kaini, na ndio maana watu wale walikuwa hodari sana , wagunduzi na wavumbuzi wakubwa, lakini waovu waliopindukia (Mwanzo 6:4). Ni watu ambao walikuwa hawana muda na Mungu, lakini kwa upande wa pili uzao wa Mungu, ulikuwa ni mnyenyekevu unaomtafuta Mungu usiku na mchana, vilevile na usio na masumbufu mengi ambao ulipitia kwa Sethi. (Mwanzo 4:26).

Inafunua hadi sasa, kwamba kizazi hiki kipo, Angalia dunia ya sasa, imestaarabika kuliko ile ya zamani, watu wanaelimu kubwa sana, wanagundua mambo makubwa  sana, wamekwenda mpaka mwezini, lakini ukiwagusia habari za Mungu, wanakuambia  hayo ni mawazo yako tu, hakuna Mungu,dini imetengenezwa na watu, wamejikita katika mambo ya mwilini, tu, elimu, utajiri, uvumbuzi basi, Mungu hayupo.

Ndugu, ikiwa na wewe upo katika jopo hili la watu, jiangue haraka sana, hichi ni kizazi, ambacho kipo ulimwenguni sasa.

   3) Kizazi cha watu wasiowatii wazazi wao.

Mithali 30:11 “Kuna kizazi cha watu wamlaanio baba yao; Wala hawambariki mama yao”.

Kuporomoka kwa maadili na nidhamu unakokuona leo, hakukuwepo huko nyuma. Leo utasikia mtoto anajibizana na mzazi wake, mwingine anampiga, mwingine anamzungumzia vibaya, wengine wametengeneza mpaka uadui na wazazi wao.. Kesi hizi ni nyingi sana sikuhizi..Wewe kama mtoto, wewe kama kijana, kuwa makini sana, kizazi hiki kimezuka ulimwenguni sasa. Unapoona, wenzako hawawaheshimu wazazi wao, na wewe usiwe mmojawapo.

Katika agano la kale mtu aliyejaribu kuonyesha utomvu wa nidhani kwa mzazi wake, sheria yake ilikuwa ni kifo. Jitathmini unawatii wazazi wako, Unawapenda?, unawabariki? Unawanenea mema? Unawaombea?.. Hata kama mzazi anakuudhi, huna ruhusu ya kurudisha baya kwa baya kwake. Vinginevyo upo chini ya laana ya kizazi hiki.

4) Kizazi cha watu wanaojiona siku zote wapo sawa:

Mithali 30:12 “Kuna kizazi cha watu walio safi machoni pao wenyewe; Ambao hawakuoshwa uchafu wao”.

Hili kundi ni kubwa sana, Mtamuhubiria mtu na kumwambia pasipo kumwamini Kristo, huwezi kuokolewa, yeye atakuambia, mimi naamini matendo yangu ni safi, ninaamini Mungu hiyo inatosha, siwezi kuhukumiwa. Atakuwa radhi, kujihesabia haki, hata kama ni mzinzi, au mlevi..Haoni hatia yoyote kwa anayoyafanya. Yeye anachoamini ni kuwa Mungu hawezi kumchoma motoni milele,.Nimeshakutana na watu wa namna hii wengi sana. Wanaodhani kuwa kwa kile wanachokiamini, ndio tiketi ya Mungu kuwaokoa siku ile.

Ndugu kama upo katika hili kundi jiepushe nalo, Ikiwa bado hujaokoka, mkimbilie Yesu, yeye pekee ndiye mwenye uwezo wa kukusafisha dhambi zako, na sio kile unachokiamini.

 5) Kizazi cha watu wenye kiburi:

Mithali 30:13 “Kuna kizazi cha watu ambao macho yao yameinuka kama nini! Na kope zao zimeinuka sana”.

Wapo watu ambao, kujishusha hakupo ndani yao. Wanajiona kuwa hakuna chochote kinachoweza kuwa msaada kwao, Mungu si kitu kwao, kwanini wakaombe, kwanini waende ibadani. Wapo radhi hata kuutukana wokovu, au kazi ya Mungu. Wanatumaini, mali zao, au ujuzi wao.

Kama tabia hizo zimeanza kuonekana ndani yako, geuka upesi.

  6) Kizazi wa watu wasio na huruma.

Mithali 30:14 “Kuna kizazi cha watu ambao meno yao ni panga; Na vigego vyao ni kama visu. Ili kuwala maskini waondolewe katika nchi, Na wahitaji katika wanadamu”.

Utu umeondoka duniani, Yupo radhi kufanya biashara haramu, bila kujali kinaleta madhara mangapi kwa jamii, anauza madawa ya kulevya, anauza bidhaa zilizoisha ubora, wanadhulumu haki za wajane na mayatima kwa faida zao wenyewe. Anaua, ili apate mali, n.k.

Tunayoyaona, hayakuwepo zamani, tusiwe watu wenye tamaa ya mali.

  7) Kizazi cha wenye adili:

Lakini pamoja na kuwepo kwa vizazi hivi vyote, vya watu waovu.. Biblia inasema pia, kitakuwepo kizazi cha watu wenye adili, wanaomcha Mungu, wanaotenda mapenzi yake.

Zaburi 112:1 “Haleluya. Heri mtu yule amchaye Bwana, Apendezwaye sana na maagizo yake.

2 Wazao wake watakuwa hodari duniani; Kizazi cha wenye adili kitabarikiwa”.

Na ndio maana unaona pia wapo watakatifu wa Mungu leo duniani. Hawa ndio Bwana anaowatazama, na siku moja itafika Kristo atawahamisha kutoka katika huu ulimwengu kwa tukio la UNYAKUO na kuwapeleka mbinguni. Swali ni je wewe upo katika kizazi kipi?

Matendo 2:40 “Akawashuhudia kwa maneno mengine mengi sana na kuwaonya, akisema, Jiokoeni na kizazi hiki chenye ukaidi”.

Jibu unalo moyoni mwako.

Kumbuka Unyakuo upo karibu sana, dalili zote zimeshatimia, huna haja ya kuendelea kutangatanga na huu ulimwengu tena. Mgeukie Kristo akuokoe, ili uwe mmojawapo wa kizazi cha watu waadilifu.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp yanayotumwa kila siku basi bofya hapa >>>  WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita..

BADO UPO YERUSALEMU TU..GALILAYA HUTAKI KWENDA?

Nini maana ya msiwe waalimu wengi (Yakobo 1:3)?

FANYIKA SIPORA WA KRISTO, UNYAKUO UPO KARIBU.

Marago ni nini? ( Waamuzi 10:18)

Rushwa inapofushaje macho?

Rudi nyumbani

Print this post

WITO WA MUNGU HAUVUKI NENO LAKE.

Bwana Yesu atukuzwe ndugu yangu. Karibu tuyatafakari maneno ya uzima pamoja..

Tunaposoma biblia..tujue kuwa tunausoma ufahamu wa Mungu. Mtu asiyeitafakari biblia halafu anakimbilia kwenda kumtumikia Mungu.. Ajue kuwa anajiweka katika hatari kubwa sana ya kuangamizwa na Mungu.

Ni sawa na mtu anayekimbilia kufanya biashara ambayo hajaifanyia utafiti kujua changamoto zake.faida zake na hasara zake..

Leo tutatazama ni kwa namna gani.

Ndugu usipumbazwe hata kidogo kuona Mungu anasema nawe..anakuonyesha maono makubwa..anakusifia..anakutokea..anakutuma ukawahubirie watu injili.. Usipumbazwe kabisa na jambo hilo. Kama maagizo yaliyopo katika Neno lake huyatii..Kufa unaweza tu kufa.

Jambo kama hilo tutaliona kwa Musa. Kila mtu anafahamu kuwa alitokewa na Mungu mwenyewe katika mwali wa moto. Mungu akampa ishara kubwa..akamtuma aende Misri kwenda kuwaokoa mamilioni ya watu..Lakini cha ajabu tunashangaa Mungu alitaka kumuua njiani..

Yaani kama sio mke wake Sipora,kumsaidia habari ya Musa ingekuwa imeishia pale na maono yake na wito wake.

Kutoka 4:21-25

[21]BWANA akamwambia Musa, Hapo utakaporudi Misri, angalia ukazifanye mbele ya Farao zile ajabu zote nilizozitia mkononi mwako; lakini nitaufanya mgumu moyo wake, naye hatawapa ruhusa hao watu waende zao.

[22]Nawe umwambie Farao, BWANA asema hivi, Israeli ni mwanangu mimi, mzaliwa wa kwanza wangu;

[23]nami nimekuambia, Mpe mwanangu ruhusa aende, ili apate kunitumikia, nawe umekataa kumpa ruhusa aende; angalia basi, mimi nitamwua mwanao, mzaliwa wa kwanza wako.

[24]Ilikuwa walipokuwa njiani mahali pa kulala, BWANA akakutana naye akataka kumwua.

[25]Ndipo Sipora akashika jiwe gumu na kuikata govi ya zunga la mwanawe, na kuibwaga miguuni pake akasema. Hakika wewe u bwana arusi wa damu kwangu mimi.

Sasa ni kwanini Mungu alitaka kumuua ni kwasababu alipuuzia maagizo ya msingi ya kuwatahiri watoto wake..Mambo ambayo Mungu alikuwa ameshawaagiza  wana wa Israeli wote wafanye hivyo kulithibitisha agano lake..Lakini yeye hakuona umuhimu huo..kisa tu Mungu amemtokea..amemtuma kama nabii mkuu Misri..hivyo hakuna sababu ya kuhangaika na yale mengine..

Ni wangapi leo hii wamepatwa na kiburi cha kukataa maagizo ya Mungu kama vile ubatizo sahihi wa maji..kwa kisingizio kuwa Mungu anazungumza na wao..Mungu kawatokea..Mungu kawaagiza waende kutumika..ubatizo hauna maana yoyote ukishamkiri tu Kristo inatosha..Wewe si zaidi sana ya nabii  Musa..Mungu hashindwi kukuua.

Unaweza kusema ni Musa tu peke yake yalimkuta haya..Yupo nabii mwingine huko mbeleni anaitwa Balaamu.. Yeye naye alitokewa na Mungu katika safari yake ya kwenda kuwalaani Israeli.

Mara ya kwanza Mungu akamuonya lakini hakusikia.. Akataka zaidi kufanya hivyo..baadaye Mungu akamruhusu na akamuhakikishia kuwa atakuwa pamoja naye..Lakini njiani Mungu alikuwa ameshamweka malaika wake tayari amuue. Kama si yule Punda kumsaidia habari yake ingekuwa naye imeisha pale…

Ni kwanini sasa iwe vile ni kwasababu alipuuzia maagizo ya awali ya Mungu “..amlaaniye Israeli na yeye atalaaniwa”(Mwanzo 12:3)..hivyo yeye akataka kulipindua hilo Neno kwa maono yake..au mitazamo yake mwenyewe. Akawa katika hatihati ya kufa..

Hesabu 22:12-13

[12]Mungu akamwambia Balaamu, Usiende pamoja nao; wala usiwalaani watu hawa, maana wamebarikiwa.

[13]Balaamu akaondoka asubuhi akawaambia wakuu wa Balaki, Enendeni zenu hata nchi yenu; kwa maana BWANA amekataa kunipa ruhusa niende pamoja nanyi….

Lakini baada ya kushurutishwa sana na wale wakuu wa Balaki..utaona alijifanya tena kwenda kumuuliza Mungu..hichi ndio kitu alichoambiwa mara ya pili

Hesabu 22:20-22

[20]Mungu akamjia Balaamu usiku, akamwambia, Kwa kuwa watu hawa wamekuja kukuita, enenda pamoja nao; lakini neno lile nitakalokuambia ndilo utakalolitenda, basi.

[21]Balaamu akaondoka asubuhi, akatandika punda wake, akaenda pamoja na wakuu wa Moabu.

[22]Hasira ya Mungu ikawaka kwa sababu alikwenda; malaika wa BWANA akajiweka njiani, ili kumpinga. Basi alikuwa amepanda punda wake, na watumishi wake wawili walikuwa pamoja naye.

Ndugu..tuzifahamu tabia za Mungu..wapo watu wengi wameonyeshwa mambo makubwa sana katika wito wao. Lakini unashangaa hakuna hata moja limetimia..hadi siku anakufa..Ni kwanini?

Nikwasababu alikwenda pasipo kujua kanuni za Mungu. Tuishi kwa Neno la Mungu na sio kwa ndoto au sauti au maono. Haijalishi wito huo utakuwa mkubwa kiasi gani..hauwezi kuzidi Neno lake.. Neno linasema mwanamke hana nafasi ya kufundisha kanisani (palipo na mchanganyiko wa wanaume na wanawake) 1Timotheo 2:12..Lakini mwingine atasema Mungu kaniita kuwa Mchungaji..kanitokea kabisa na kunitia mafuta..

Mama kuwa makini..kasome biblia yako kwanza umwelewe Mungu ndipo ukatumike..

Hivyo ili tuwe salama.. kabla ya kuitii sauti yoyote ya nje..Tuitii kwanza Sauti ya Mungu iliyo katika Neno lake.  Ndio hayo mengine yafuate.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp ya kila siku basi jiunge kwa kubofya hapa >>> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

USIPOTEZWE NA MANENO YA MANABII WA UONGO.

JE UNAIFANYA KAZI YA MUNGU?

MAJARIBU MATATU YA YESU KRISTO

TAFUTA MSAMAHA HALISI, NA SI MSAMAHA TU!

UTAWALA WA MIAKA 1000.

Nini maana ya “wazimu” katika biblia?

JINSI PAULO ALIVYOPAMBANA NA UJINGA WA ROHONI.

PINDO LA VAZI LAKE SASA LIMEREFUSHWA.

Rudi nyumbani

Print this post

Je Bwana Yesu alikuwa na mchoro (tattoo) katika paja lake?

Tusome..

Ufunuo 19:16 “Naye ana jina limeandikwa katika vazi lake na paja lake, MFALME WA WAFALME, NA BWANA WA MABWANA”

Mstari huu unatumika na wengi wanaohalalisha uchoraji wa tattoo katika miili yao, kuwa hata Bwana Yesu mwenyewe alijichora tattoo katika paja lake.

Je ni kweli hiyo ndio maana ya huo mstari?
Jibu ni la! Katika Maono hayo Yohana aliyoyaona, hakuona nyama ya paja la Bwana Yesu ikiwa limeandikwa hayo maneno, bali alichokiona ni vazi lililofunika paja limeandikwa maneno hayo, BWANA WA MABWANA na MFALME WA WAFALME.

Kwamfano kuna andiko linasema jifunge upanga pajani mwako..

Zaburi 45:3 “Jifungie upanga wako pajani, wewe uliye hodari, Utukufu ni wako na fahari ni yako”.

Je kwa mstari kwa huo biblia imemaanisha, kuchua upanga na kuubandika kwenye nyama ya paja?..

Bila shaka haikumaanisha hivyo bali ilimaanisha funga upanga katika ghala iliyopo viununo mwetu.

Au labda mtu akupe maagizo ya kubeba kiroba cha mzigo Begani, je atakuwa anamaanisha uvue nguo ubaki bega wazi ndio ubebe mzigo huo?.

Au mtu akwambie vaa mkanda kiunoni, atakuwa amemaanisha uvue nguo zote halafu ujifunge mkanda kwenye nyama ya kiuno chako? Jibu ni la!..bali amemaanisha katika vazi lililopo kiunoni kama ni suruali au nguo nyingine yoyote, ifungwe kwa mkanda.

Vile vile katika mwonekano mwingine wa Bwana kuna mahali, maandiko yanasema alionekana kafungwa mshipi wa dhahabu “matitini”.

Ufunuo wa Yohana 1:13 “na katikati ya vile vinara nikaona mtu mfano wa Mwanadamu, amevaa vazi lililofika miguuni, na kufungwa mshipi wa dhahabu matitini”.

Bila shaka mstari huo haukumaanisha ndani ya kifua cha Bwana kuna mshipi umedungwa wa dhahabu, bali biblia imemaanisha kwenye vazi lake la nje, sehemu ya kifua palikuwa na mshipi (yaani mkanda).

Kadhalika katika mstari huo,wa Ufunuo 19:16, biblia haijamaanisha kuwa kuna maneno yaliyoandikwa kwenye nyama ya paja, bali imemaanisha maneno yaliyoandikwa katika vazi lililofunika paja.

Hakuna mahali popote maandiko yanaagiza wala kutufundisha kujichora tattoo.

Kujichora kwa aina yoyote ile, ikiwemo kupaka hina ni dhambi kibiblia, Na wote wanaojichora hawataurithi uzima wa milele (Kwa maelezo marefu kuhusu kujichora na kujichanja kibiblia unaweza kufungua hapa Kujichota ni dhambi

Je umempokea Yesu?..je umebatizwa katika ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jinala Yesu?, Mambo haya mawili ndio msingi wa wokovu, na kila mtu lazima ayafanye ili awe mkristo.

Bwana atubariki.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp ya kila siku basi jiunge kwa kubofya hapa >>> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

JE! WEWE NI MFUNGWA WA BWANA?

NAMI NINAZO FUNGUO ZA MAUTI, NA ZA KUZIMU.

WAKAMCHA BWANA, NA KUITUMIKIA MIUNGU YAO WENYEWE.

HAPANA MFUPA WAKE UTAKAOVUNJWA.

Ni lini na wapi Ibrahimu aliioona siku ya Bwana akashangilia?

USO WAKE ULIKUWA UMEHARIBIWA SANA ZAIDI YA MTU YE YOTE.

Rudi nyumbani

Print this post

NA ABARIKIWE KILA AKUBARIKIYE, NA ALAANIWE KILA AKULAANIYE.

SWALI: Nini maana “nitawabariki wakubarikio, naye akulaaniye nitamlaani;”..Je! Ni kwa namna gani tunapaswa tulibariki taifa la Israeli.  Je! Ili tubarikiwe tunapaswa, tufunge na kuliombea Taifa la Israeli usiku na mchana, au tuwe na bendera za taifa lile makanisani kwetu au majumbani mwetu?.

Ni kwa namna gani tutapokea Baraka kwa kulibariki tu taifa hilo?


JIBU: Maneno hayo, kwa mara ya kwanza tunaona Mungu akiyatamka kwa Ibrahimu katika;

Mwanzo 12:1 “Bwana akamwambia Abramu, Toka wewe katika nchi yako, na jamaa zako, na nyumba ya baba yako, uende mpaka nchi nitakayokuonyesha;

2 nami nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa, na kukubariki, na kulikuza jina lako; nawe uwe baraka;

3 nami nitawabariki wakubarikio, naye akulaaniye nitamlaani; na katika wewe jamaa zote za dunia watabarikiwa”.

Maandiko hayo hayatupi tafsiri ya kwamba tukeshe kuliombea taifa la Israeli usiku na mchana ili tubarikiwe, hapana utaona maneno hayo, Mungu alisema akilenga wakati ambapo watu wanapanga kuliangusha, au kuliporomosha au kuliletea vitisho taifa hilo, aidha kwa kulivamia, au kuliloga, n.k. kwa namna yoyote ile, hapo ndipo anayejaribu kufanya hivyo anakumbushwa,kuwa aibarikiye Israeli, atabarikiwa, na ailaaniye Israeli atalaaniwa.

Jambo kama hilo tunalithibitisha kwa Yule Balaamu mchawi, ambaye aliajiriwa na Balaki, ili aende kuwalaani Israeli, (yaani kuwaloga) kwa ushirikina ili wasifanikiwe kuvuka katika nchi ya Balaki. Lakini Ilikuwa nusura Mungu amuue Yule Balaamu, kwa kitendo tu hicho cha kujaribu kuliloga taifa teule. Kinyume chake ikabidi alibariki ili tu awe salama..Mpaka yeye mwenyewe akakiri,na kusema hapana uchawi katika Israeli wala uganga..

Hesabu 23:21 “Hakutazama uovu katika Yakobo, Wala hakuona ukaidi katika Israeli. Bwana, Mungu wake, yu pamoja naye, Na sauti kuu ya mfalme i katikati yao.

22 Mungu amewaleta kutoka Misri, Naye ana nguvu kama nguvu za nyati”.

Hiyo ni kuonyesha kuwa, hata sasa yapo mataifa mengi ambayo yameshatangaza uadui na Israeli, mojawapo ni Somalia, na Libya, embu yaangalie mataifa hayo leo hii yapoje., na hiyo yote ni kwasababu yamejaribu kuleta vita na vitisho kwa taifa teule la Mungu, na matokeo yake ni kuwa yamepigwa, kila kukicha ni vita. Na mengine yanalitamkia maneno ya laana kama vile Palestina,, na mengine kuliwekea vikwazo.  Embu Yatazame ustawi wao hayo mataifa au hao watu leo hii walivyo.

Halikadhalika, taifa ambalo halitaki shari na Israeli, bali linalitakia mema amani na mafanikio daima, basi taifa hilo au Mtu huyo Mungu  atambariki. Hivyo  umeona hapo, inalenga katika habari ya amani na shari, yaani pale ambapo unalazimishwa utamke mabaya, uwalaani, uwatukane,  au upigane vita kinyume chao, hapo unapaswa uende kinyume chake, uwabariki, na kuwatakia amani. Ndipo utakapobarikiwa.

Lakini sio kuacha kufuata kanuni za Mungu za kimaandiko na kukesha kuliombea taifa la Israeli ili tubarikiwe. Mpaka tunasafiri kwenda kule Yerusalemu, kupokea Baraka hizo, Mungu havutiwi sana na sisi tunapofanya hivyo, anavutiwa na sisi pale tunapoishi kulingana na Neno lake, hivyo tu. Kwahiyo, usipeleke fikra zako sana Israeli, bali zipeleke kwenye maisha yako, vilevile maombi yako, yaelekeze kwa watu wenye dhambi leo hii ulimwenguni. Kesha kuwaombea hao, na kuiombea Injili.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp  yanayotumwa kila siku basi fungua bofya hapa ujiunge >>> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

ALAMA ZA BENDERA YA ISRAELI ZINAWAKILISHA NINI?

Israeli ipo bara gani?

Mataifa ni nini katika Biblia?

Bwana Yesu alimaanisha nini kusema “yamfaa afungiwe shingoni jiwe kubwa la kusagia, na kutoswa katika kilindi cha bahari?”

REKEBISHA YAFUATAYO ILI UCHUMI WAKO UKAE SAWA.

Je Mkristo kutembea na walinzi (Bodyguards),ni sawa?

Rudi nyumbani

Print this post

ALAMA ZA BENDERA YA ISRAELI ZINAWAKILISHA NINI?

Wakati Mungu anawatoa Israeli kutoka Misri, Mungu hakuwapa bendera kuwa kama Ishara ya Taifa hilo, Hivyo bendera kwa Israeli ni kitu kilichokuja kuzalika miaka mingi baada ya Kristo kuja duniani katika harakati za kutafuta uhuru.

Sasa swali, ni je zile rangi katika bendera hiyo zinawakilisha nini?, Na ile nyota iliyopo katikati ya bendera inawakilisha nini?.

Bendera ya Israeli ina rangi mbili tu! Nyeupe na Blue (kwa kiswahili Samawi).
Rangi nyeupe inawakilisha utakatifu wa Mungu. Na Blue inawakilisha utukufu wa Mungu.

Tukitazama juu mbinguni, anga linaonekana la rangi ya Blue(Samawi).

Kufunua utukufu wa Mungu.Hata vitu vingine vya asili kama milima, bahari utaona vina mwonekano wambwa wa rangi hii ya blue kufunua utukufu wa Mungu.

Lakini kitu cha mwisho katika bendera ya Israeli, ni ile alama kama ya Nyota, yenye pembe sita, iliyopo katikati ya bendera hiyo.
Alama hiyo inajulikana kama Nyota ya Daudi au Ngao ya Daudi.

Imejulikana hivyo, kwasababu inaaminika Ngao ya Daudi ilikuwa na umbile hilo mfano wa hiyo nyota, na inaaminika ngao hiyo ilikuwa ina nguvu fulani ya kiungu.
Vile vile zile pembe sita katika hiyo ngao zinawakilisha zile tabia sita za Roho wa Mungu katika Isaya 11.

Isaya 11:2 “Na roho ya BWANA atakaa juu yake, roho ya hekima na ufahamu, roho ya shauri na uweza, roho ya maarifa na ya kumcha BWANA”.

Na vile vile kama ilivyokuwa na pembe tatu mbili, moja inaangalia juu na nyingine chini, inawakilisha uhusiano wetu sisi na Mungu.

Ingawa hakuna mahali popote katika torati wala biblia nzima, nyota hiyo ilitajwa kwa sifa hizo, lakini wayahudi wa karne ya 17, walishawishika kuamini hivyo na kuitumia hiyo kama ishara ya Nembo ya Taifa lao, na hata kuitumia katika bendera yao.

Lakini katika jicho lingine, nyota hiyo inaaminika kama ishara ya Masihi, yaani Yesu Kristo, yeye ndiye Uzao wa Daudi, na ndiye ile nyota ing’aayo, ambaye Mataifa yote watamtumainia.

Ufunuo 22:16 “Mimi Yesu nimemtuma malaika wangu kuwashuhudia ninyi mambo hayo katika makanisa. Mimi ndimi niliye Shina na Mzao wa Daudi, ile nyota yenye kung’aa ya asubuhi”.

Lakini swali ni je! Bendera hiyo kwetu sisi wakristo, ina manufaa yoyote kiroho?, Kwamba tunapokuwa na bendera ya Israeli katika makanisa yetu, au katika vyombo vyetu vya usafiri, au katika nyumba zetu, tunakuwa tunajiongezea baraka??.

Jibu ni la!. Bendera ya Taifa la Israeli haituongezei chochote, zaidi sana mtu anapoiweka ndani kwake, na kuifanya kama mungu wake atakuwa anajizombea laana badala ya baraka. Kwasababu kwake yeye ni kama mungu.

Baraka pekee tunayoweza kuipata sisi ni kuishi kulingana na Neno lake na kanuni zake, utakatifu sawasawa na Waebrania 12:14, ndiyo bendera yetu, na alama ya kukubaliwa na Mungu..na sio bendera ya Israeli ndani kwetu.

Hivyo hakuna ulazima wowote wa Mkristo au mhubiri kutembea na bendera kana kwamba ndio kitovu chake cha baraka, labda atembee nayo kwa lengo lingine lakini sio hilo la kutafuta baraka kupitia hiyo.

Maandiko yaliposema “ambarikiye Israeli amebarikiwa” hiyo sio maana yake..Maana yake ni nyingine kabisa.

Bwana akubariki.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kama utapenda uwe unafikiwa na masomo ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP basi bofya hapa ujiunge moja kwa moja  >>>> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

MAISHA ULIYOPITIA NYUMA NI USHUHUDA TOSHA WA WEWE KUMTUMIKIA MUNGU

WEKA KUMBUKUMBU YA MAMBO BWANA ANAYOKUFANYIA KWASABABU YATAKUFAA MBELENI.

Neno Kupatiliza maana yake nini katika biblia?

Babewatoto ni nani katika biblia?(Isaya 34:14).

Ni kosa gani Daudi alilolifanya katika kuwahesabu watu, mpaka kupelekea vifo vya waisraeli wengi?

Maana Ya Maneno Katika Biblia.

Rudi nyumbani

Print this post

Atamaniye faida huifadhaisha nyumba yake mwenyewe;

SWALI: Nini maana ya huu mstari..

Mithali 15:27

[27]Atamaniye faida huifadhaisha nyumba yake mwenyewe;

Bali achukiaye zawadi ataishi.


JIBU: Mstari huo ni mgumu kueleweka kidogo kwasababu kiswahili kilichotumika hapo ni kile cha zamani..

Ukiangalia tafsiri nyingine..mstari huo unamaana hii.. Atamaniye kupata vingi kwa njia isiyohalali huifadhaisha nyumba yake mwenyewe bali achukiaye rushwa ataishi.

Jambo ambalo ni kweli..kwamfano Mtu anayejiingiza katika biashara ya madawa ya kulevya kwa tamaa tu ya kupata fedha nyingi..hajui kuwa mwisho wake ni kujibomoa yeye mwenyewe na pamoja nyumba yake yote.

Habakuki 2:9

[9]Ole wake yeye aipatiaye nyumba yake mapato mabaya, ili apate kukiweka kioto chake juu, apate kujiepusha na mkono wa uovu!

Mwingine utakuta anatoa rushwa ili bidhaa zake zisilipishwe kodi..lakini hajui mwisho wake utakuwa mbaya siku moja.

Lakini kinyume chake biblia inasema atakayeyakwepa hayo yote ataishi..

Sikuzote tamaa ya  za haraka haraka mwisho wake huwa ni mitegoni..

Mhubiri 4:6

[6]Heri konzi moja pamoja na utulivu,

Kuliko konzi mbili pamoja na taabu;

na kujilisha upepo.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kama utapenda uwe unafikiwa na masomo ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP basi bofya hapa ujiunge moja kwa moja  >>>> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

SABATO ILIFANYIKA KWAAJILI YA MWANADAMU NA SI MWANADAMU KWAAJILI YA SABATO!

Maana ya huu mstari ni ipi? Mithali 14:4 ‘Zizi ni safi ambapo hapana ngombe;bali nguvu za ngombe zaleta faida nyingi’.

UMEDI NA UAJEMI ZILITAWALAJE?

KUNA AINA NGAPI  ZA MAOMBI?

HUANGUA MAYAI YA FIRA, NA KUSUKA WAVU WA BUIBUI;

Print this post

Karama ya pili inayozungumziwa katika 2Wakorintho 1:15 ndio ipi?

Tusome,

2Wakorintho 1:15 “Nami nikiwa na tumaini hilo nalitaka kufika kwenu hapo kwanza, ili mpate karama ya pili

Sio wakati wote neno “karama” linapotumika kwenye biblia linamaanisha “karama ya roho kama vile unabii, uchungaji, ualimu n.k”. Bali karama pia ni neno linalomaanisha “Zawadi au Baraka”.

Kwamfano kuna andiko linasema “karama ya Mungu ni uzima wa milele”.

Warumi 6:23 “Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti; bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu”.

 Sasa hapo haimaanishi kwamba Mungu karama yake ni “Uzima wa milele” kama sisi karama zetu zilivyo kutoa unabii, au Kunena kwa lugha, au kutabiri nk.

Mungu yeye hana kipawa fulani maalumu, kwasababu vyote vinatoka kwake.

Bali hapo biblia imemaanisha kuwa “Zawadi ya Mungu ni uzima wa milele”..au “Baraka ya Mungu kwetu ni uzima wa milele”

Kadhalika Mtume Paulo aliposema  kuwa “nalitaka kufika kwenu hapo kwanza, ili mpate karama ya pili” hakumaanisha kuwa kuna karama nyingine ya pili tofauti na hiyo ya kitume aliyokuwa nayo,  au nyingine mpya  hivyo anataka kwenda kuwapa, au kuwanufaisha katika hiyo, hapana!, bali alimaanisha “Baraka ya Pili”.

Ni sawa mhubiri aliyeko Dar es Salaam, aende kuhubiri Morogoro, kwa wiki moja na kisha arudi Dar, na ghafla apate tena safari ya kwenda Dodoma kuhubiri baada ya wiki moja wakati kasharudi Dar, bila shaka hawezi kufika Dodoma bila kupita Morogoro, hivyo Mhubiri huyu akawasiliana na wale aliokwenda kuwahubiria hapo kwanza  (Watu wa Morogoro) kwamba atapita tena kuhubiri kwa siku moja na siku inayofuata atakwenda Dodoma.. Hivyo watu wa Morogoro wakawa wamepata Baraka mara mbili. Ndicho Mtume Paulo alichomaanisha hapo!.

Kwamba alishapita kwao (watu wa Korintho) na kuwabariki kwa Mafundisho akaondoka, lakini alitaka tena kupita kwao kwa mara nyingine ya pili wakati anaelekea Makedonia ili wapate Baraka mara mbili.

Maisha ya Paulo yanatufundisha kuwa na bidii na jitihada katika kuifanya kazi ya Mungu, ijapokuwa Paulo alikuwa anapitia vita vikali katika kuhubiri, lakini mara zote alitafuta kurudia kuhubiri mahali ambapo ameshapita kuhubiri.

Matendo 15:36 “Baada ya siku kadha wa kadha Paulo akamwambia Barnaba, Haya! Mrejee sasa tukawaangalie hao ndugu katika kila mji tulipolihubiri neno la Bwana, wa hali gani”.

Bwana atusaidie na sisi tuwe kama watakatifu hawa wa kanisa la kwanza.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Pia kama utapenda uwe unafikiwa na masomo ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP basi bofya hapa ujiunge moja kwa moja  >>>> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

KWANINI YESU NI ADAMU WA PILI?

Kuhubiri injili kwa husuda na fitina ndio kupi?

NA VIUNGO VYETU VISIVYO NA UZURI VINA UZURI ZAIDI SANA.

USIRUDI NYUMA KWA KUITUMAINIA HAKI YAKO.

Talanta ni nini katika biblia (Mathayo 25:14-30)

Rudi nyumbani

Print this post