Title December 2019

UPAKO NI NINI?

Upako ni nini?

Upako wa Roho Mtakatifu au  kwa kiingereza (anointing of the Holy spirit). Ni neno lenye tafsiri pana kidogo. Linaloweza kumaanisha Nguvu au uwezo wa kipekee mtu anaoupekea kutoka kwa Roho Mtakatifu.. kumsaidia  kufanya jambo Fulani kirahisi zaidi,. au kufanya jambo ambalo hapo mwanzo alikuwa hawezi kulifanya.

Kibiblia zamani, mtu kabla hajatawadhwa kuwa mfalme alikuwa anatiwa mafuta,.. kiashirio cha mafuta yaliyomwagwa ndani ya roho yake kama baraka kutoka kwa Mungu ya kumsaidia yeye kuwa mtawala..(2Wafalme 9:6)

Vilevile watumishi wa Mungu kama makuhani, na manabii, nao pia walikuwa wanatiwa mafuta,.. kabla ya kuanza kutumika katika kazi ya Mungu.(Kutoka 29:7, )

Upako katika agano jipya:

Lakini katika agano jipya, vipo pia vigezo vya kutiwa mafuta,.. na vigezo hivyo havitegemei kunyunyiziwa mafuta ya aina yoyote ndani ya mtu,.. Bali kinyume chake ni kwa kuyatenda maagizo ya Mungu..

Tunamwona mtu mmoja katika biblia ambaye Mungu alimtia mafuta(upako) mengi zaidi ya watu wote waliowahi kuishi chini ya jua.. na huyo si mwingine zaidi ya YESU KRISTO,.. yeye mafuta yale yote aliyotiwa yalikuja juu yake kwa sababu moja tu..nayo ni hii: alipenda haki, na kuchukia maasi.

Waebrania 1:8 Lakini kwa habari za Mwana asema, Kiti chako cha enzi,Mungu,ni cha milele na milele;. Na fimbo ya ufalme wako ni fimbo ya adili.

9 Umependa haki, umechukia maasi; Kwa hiyo Mungu, Mungu wako, amekutia mafuta, Mafuta ya shangwe kupita wenzio.

Unaona Kristo, alipenda haki na kuchukia maasi, na ndio maana alitiwa mafuta kushinda sisi wote.

Tuwe kama yeye:

Vilevile na sisi tukiwa watu wa namna hiyo kama yeye wa kupenda haki na kuchukia maasi.. basi tuwe na uhakika kuwa Mungu naye atatutia mafuta mengi kupita kiasi katika maisha yetu na katika kumtumikia yeye..tutakuwa na upako wa kupita kiasi.

Tofauti na inavyodhaniwa na wengi leo hii, kwamba ukitaka upako,.. ni kwenda kufunga  kuomba sana  milimani, au kwenda kuwekewa mikono na mtumishi huyu au mtumishi Yule,.. hiyo sio sahihi..Ni vizuri tukifanya hivyo lakini huku nyuma tunafanya yampendezayo Mungu..Lakini kama hatufanya hayo na huku tunatafuta mafuta ya Roho Mtakatifu basi tuwe na uhakika kazi tunayoifanya ni bure..

vigezo vya kuupokea upako:

Ni lazima kwanza tujazwe Roho, na Kujazwa Roho si kwa kunena kwa lugha,. bali ni kwa kulitii Neno la Mungu kama ilivyokuwa kwa Bwana wetu Yesu Kristo,.. yaani kuwa watakatifu kama jina lake mwenyewe Roho Mtakatifu lilivyo..Ndipo hapo na yeye ataachilia mafuta yake(upako) ndani yetu.

Hivyo kama wewe bado huna Roho wa Mungu ndani yako, fahamu kuwa huwezi kufanya jambo lolote,.. huwezi kuyaelewa maandiko, huwezi kuishinda dhambi, wala huwezi kumtumikia Mungu..Vilevile huwezi kwenda mbinguni haijalishi unajitihada kiasi gani..

Warumi 8:9 “Lakini ikiwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu, ninyi hamwufuati mwili; bali mwaifuata roho. Lakini mtu awaye yote asipokuwa na Roho wa Kristo, huyo si wake”.

Lakini ikiwa utapenda Bwana akupe kipawa hicho, basi fahamu kuwa kipawa hicho ni bure,,, na wala hakiihitaji kutumia nguvu kukipata..Jambo la kwanza unalopaswa kufanya ni kutubu kwanza kwa  kumaanisha kabisa kuacha dhambi zako zote,, kisha ukishatubu sasa na kusema kuanzia leo, mimi na ulimwengu basi, na kuanza kumtazama Kristo,. na kutaka kujifunza Neno lake kwa bidii..Mungu akishaona umegeuka na kuacha uliyokuwa unayafanya basi atakusamehe,. na AMANI YA AJABU itaingia ndani yako..Na yeye atasimama kukusaidia kwa namna ambayo hujawahi kuiona katika maisha yako.

Tafuta ubatizo:

Kisha bila kupoteza muda nenda katafute mahali utakapobatizwa katika ubatizo sahihi.. wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa Jina la YESU KRISTO,. sawasawa na (Matendo 2:38) ili uukamilishe wokovu wako, na kumruhusu Roho Mtakatifu kuingia ndani yako, na kuweka makao yake milele ndani yako..

Ukishafanya hivyo kwa moyo wa dhati bila kigugumizi, basi fahamu kuwa Roho wa Kristo ameshaingia ndani yako,. muda mfupi baadaye atakushushia vipawa vyake., kwa jinsi apendavyo yeye, aidha lugha, aidha maono, aidha ndoto, aidha uinjilisti,au unabii n.k.. Wewe tu mwenyewe utaona badiliko ndani yako siku baada ya siku..atakuwa anakufundisha na kukuongoza katika njia ya kweli yote, kwasababu yale mafuta yake tayari ameshayamwaga ndani yako.

1Yohana 2: 27 “Nanyi, mafuta yale mliyoyapata kwake yanakaa ndani yenu, wala hamna haja ya mtu kuwafundisha; lakini kama mafuta yake yanavyowafundisha habari za mambo yote., tena ni kweli wala si uongo, na kama yalivyowafundisha, kaeni ndani yake”.

Hivyo atakufundisha, na kukupa upako halisi unaotoka kwake, na sio ule feki unaouzwa na manabii wa uongo katika chupa,. na vifungashio mabarabarani, upako unaotoka kuzimu, usioweza kuyageuza maisha yako.

Fanya hivyo, Na Bwana akusaidie katika kukamilisha hatua zote hizi.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Amen.

Mada Nyinginezo:

UMUHIMU WA ROHO MTAKATIFU KATIKA KUZAA MATUNDA.

JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?

SIKU ILE NA SAA ILE.

Je! hizi roho saba za Mungu ni zipi? na je zinatofautiana na Roho Mtakatifu?

ALIKUWAKO NAYE HAYUKO, NAYE YU TAYARI KUPANDA KUTOKA KUZIMU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

KIJITO CHA UTAKASO.

Kijito cha Utakaso, Ni kijito cha  Damu ya Yesu, kidhihirishwacho kwa ubatizo wa maji mengi..Kama vile Maji ya farakano yalivyotumika katika Agano la kale kutakasa, katika Agano jipya yanatumika maji ya ubatizo.

Katika Agano la Kale, ilikuwa hata kugusa tu maiti, mtu tayari ameingia Unajisi, hivyo ilimpasa akafanye utakaso kwanza kabla ya kuingia katika kusanyiko la Bwana..

Hesabu 19:11 “Mtu agusaye maiti ye yote atakuwa najisi muda wa siku saba;

12 naye atajitakasa kwa yale maji siku ya tatu, na siku ya saba atakuwa safi; lakini kama hajitakasi siku ya tatu, ndipo na siku ya saba hatakuwa safi.

13 Mtu awaye yote agusaye maiti wa mtu aliyekufa, asijitakase, yuatia unajisi maskani ya Bwana; na mtu huyo atakatiliwa mbali na Israeli; maana, hayo maji ya farakano hayakunyunyizwa juu yake, atakuwa najisi; unajisi wake ukali juu yake bado”.

Na kulikuwa pia na sheria kali  kwa mtu ambaye atakataa kujitakasa kwa kujiosha katika mji yaliyoamriwa. Ambayo ni maji ya farakano (Au maji ya Utakaso kwa jina lingine).

Tunasoma hayo katika..

Hesabu 19:20 “Lakini mtu atakayekuwa najisi, naye hataki kujitakasa, mtu huyo atakatiliwa mbali katika mkutano, kwa sababu amepatia unajisi mahali patakatifu pa Bwana; hayo maji ya farakano hayakunyunyizwa juu yake; yeye yu najisi”. 

Katika Agano jipya, watu wote ambao hawajampa Yesu Kristo maisha yao, au kwa lugha rahisi HAWAJAOKOKA!..Hao ni watu najisi mbele za Mungu…Hivyo hawastahili hata kumwabudu Mungu katika hali walizopo, hawastahili hata kumsogelea Mungu wala kuuliza  kitu chochote kutoka kwake..Watu wengi sana hawalijui hilo…

Soma..

Ezekieli 14:3 “Mwanadamu, watu hawa wametwaa vinyago vyao na kuvitia mioyoni mwao, nao wameweka kwazo la uovu wao mbele ya nyuso zao. Je! Ni laiki yangu niulizwe na wao katika neno lo lote?

4 Basi sema nao, uwaambie, Bwana MUNGU asema hivi; Kila mtu wa nyumba ya Israeli atwaaye vinyago vyake na kuvitia moyoni mwake, na kuliweka kwazo la uovu wake mbele ya uso wake, na kumwendea nabii; mimi, Bwana, nitamjibu neno lake sawasawa na wingi wa sanamu zake”

Na wala hawawezi kumwomba Mungu wala kumtolea sadaka..kwasababu ni Najisi…

kumbu.23:18 “Usilete ujira wa kahaba, wala mshahara wa mbwa, katika nyumba ya Bwana, Mungu wako, kwa ajili ya nadhiri yo yote; kwani haya ni machukizo kwa Bwana, Mungu wako, yote mawili”

Ni kitu gani kinachowafanya wawe Najisi?

Jibu Ni dhambi zilizomo ndani yao ndizo zimewafanya wawe NAJISI, machoni pa Mungu…Biblia inasema katika..

Marko 7:21 “Kwa maana ndani ya mioyo ya watu hutoka mawazo mabaya, uasherati,

22 wivi, uuaji, uzinzi, tamaa mbaya, ukorofi, hila, ufisadi, kijicho, matukano, kiburi, upumbavu.

23 Haya yote yaliyo maovu yatoka ndani, nayo yamtia mtu unajisi”

Unaona?..Dhambi ndizo zinazomtia mtu unajisi mbele za Mungu..Na Watu najisi hawawezi kumsogelea Mungu hata kidogo..Na watu najisi ni watu wote watendao dhambi, (yaani ambao hawajaokoka)...watu wote wenye chuki, wasengenyaji, waasherati, wezi, wavaaji vimini, suruali, nguo fupi na zilizo nusu uchu, wote wajipakao wanja, lipstick, na kuvaa wigi n.k...Mungu huwa anajificha uso wao wasimwone, maombi yao yanakuwa hayajibiwi…Kwakuwa ni Najisi mbele za Mungu.

Biblia inasema…

Isaya 59:1″ Tazama, mkono wa Bwana haukupunguka, hata usiweze kuokoa wala sikio lake si zito, hata lisiweze kusikia;

2 lakini maovu yenu yamewafarikisha ninyi na Mungu wenu, na dhambi zenu zimeuficha uso wake msiuone, hata hataki kusikia.

3 Kwa maana mikono yenu imetiwa unajisi kwa damu, na vidole vyenu vimetiwa unajisi kwa uovu; midomo yenu imenena uongo, ndimi zenu zimenong’ona ubaya”

Sasa watu wa Agano la kale walitakasika kwa kuoshwa kwenye maji…Lakini sisi watu wa Agano jipya wanatakasika kwa kuoshwa kwenye kijito cha Damu ya YESU. Kijulikanacho kama KIJITO CHA UTAKASO.

Katika kijito hicho cha utakaso, Mtu atazama na kuoshwa katika hicho na unajisi wake wote unaondoka..

Sasa Mtu anaoshwaje ndani ya hicho kijito cha utakaso?

Kwanza kwa kutubu: kutubu maana yake ni kukiri kwamba ulikuwa mkosaji na hivyo umeamua kugeuka na kuacha kufanya uliyokuwa unayafanya…Hicho kinafananishwa na kitendo cha kuvua nguo zako zote kabla ya kuingia kuoga  kwenye kijito chochote kile.

Pili: Unajitosa kwenye kijito cha Utakaso..Kijito hicho ni Ubatizo wa Maji mengi ..Yaani baada tu ya kutubu, hatua inayofuata ni kwenda kubatizwa katika ubatizo sahihi… Kumbuka ubatizo sahihi sio wa kunyunyiziwa maji, au sio wa utotoni wala sio wa Baba, mwana na Roho Mtakatifu..Ubatizo sahihi ni wa kuzamishwa mwili wote katika maji mengi sawasawa na Yohana 3:23.. na katika jina la YESU KRISTO sawasawa na (Matendo 2:38).

Kwa kuzama katika kijito hicho..Kwa nje utaonekana kama umezama kwenye maji ya ubatizo lakini katika Roho utaonekana umezama katika kijito cha damu ya YESU.. Kuzamishwa mwili wote katika maji mengi ni ishara inayoonesha umezamishwa roho yako katika kijito cha damu ya Yesu kiletacho utakaso…Na hivyo dhambi zako zote zitakuwa zimeondolewa kwa tendo hilo..Na hautahesabika kuwa najisi tena mbele za Mungu.

Matendo 2:38 “Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu”

Je umeoshwa leo dhambi zako zote?..

Je unastahili kumsogelea Mungu? au je wewe ni najisi?..Kama bado hujachovya kwenye hicho kijito cha utakaso  unasubiri nini?..Tubu leo mwambie Bwana Yesu  leo nakuja mbele zako, mimi ni mkosaji, naghairi mabaya yangu yote leo,..Naomba unisamehe dhambi zangu zote…..Nakuomba unipokee sawasawa na Neno lako lisemalo kwamba “wote wajao kwako hutawatupa nje kamwe”..Nakuomba unipe neema ya kukujua wewe siku zote za maisha yangu. Amen.

Ukiwa umeomba hivyo au hata zaidi ya hivyo..Basi fahamu ya kuwa Mungu si mwongo..Ameshakusamehe haijalishi dhambi zako zilikuwa ni nyingi kiasi gani..

Sasa hatua inayofuata ni ya MUHIMU SANA. Nenda katafute Ubatizo sahihi kwa hali na mali..Umejifunza hapo juu, maana ya kijito cha Utakaso..Kitafute hicho kwa hali na mali…Kama unafahamu mahali unaweza kupata huduma hiyo ya ubatizo fanya hivyo haraka, maana shetani hapendi kuona unakwenda mbinguni…Na kama hufahamu basi unaweza kuwasiliana nasi kwa namba hizi +255789001312 tutakuelekeza mahali karibu ni ulipo..ambapo unaweza kupata huduma hiyo.

Bwana akubariki sana..

Kumbuka Biblia inasema katika..1Wathesalonike 4:7 “Maana Mungu hakutuitia uchafu, bali tuwe katika utakaso”.

Na tena Inasema…

Waebrania 10:10 “Katika mapenzi hayo mmepata utakaso, kwa kutolewa mwili wa Yesu Kristo mara moja tu”.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Maran atha!


Mada Nyinginezo:

JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?

ROHO HUTUOMBEA KWA KUUGUA KUSIKOWEZA KUTAMKWA!

Nini maana ya kusali kwa kupayuka payuka?

UWE MWAMINIFU HATA KUFA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

MWANANCHI WA UFALME WA MBINGUNI

Mwananchi ni mtu aliye na uraia wa Nchi fulani.

Kwamfano mtu aliyezaliwa Taifa la Tanzania ni mwananchi wa Tanzania, Kadhalika lipo Taifa la kimbinguni..Na hilo yeyote anayezaliwa katika Taifa hilo anaitwa Mwananchi wa Taifa la Mbinguni..Na kila mwananchi analindwa na katiba.

Biblia inasema katika..

1Petro 2:9 “Bali ninyi ni mzao mteule, ukuhani wa kifalme, Taifa takatifu, watu wa milki ya Mungu, mpate kuzitangaza fadhili zake yeye aliyewaita mtoke gizani mkaingie katika nuru yake ya ajabu;

10 ninyi mliokuwa kwanza si taifa, bali sasa ni taifa la Mungu; mliokuwa hamkupata rehema, bali sasa mmepata rehema”.

Huwezi kuzungumzia Taifa bila kuhusisha mwananchi wa hilo taifa. Palipo na Taifa ni lazima pawepo na wananchi..Na Taifa la Mbinguni lina wananchi wake.

Hebu tuzitafakari dondoo chache hizi muhimu, ili zitusaidie kuelewa ni namna gani ufalme wa Mbinguni unafanya kazi.

KATIBA

  • Mwananchi wa Taifa lolote ni lazima aongozwe na kitabu kimoja muhimu kinachoitwa KATIBA,…Ambapo ndani ya kitabu hicho ndipo zinapopatikana sheria na taratibu zote za kuishi katika nchi hiyo husika…
  • Mwananchi yoyote anayeishi kulingana na KATIBA,.Ataishi kwa amani na furaha na kufanikiwa katika nchi hiyo..Kwani hatavunja sheria za nchi hiyo na hivyo kumfanya awe mwananchi bora na mwenye kukubalika.
  • Kila Mwananchi analindwa na Katiba..Licha ya katiba kutumika kama mwongozo wa kila mwananchi..lakini pia katiba hiyo hiyo inatumika kama chombo cha kumlinda mwananchi..Kwamba Mwananchi yoyote hapaswi kunyimwa haki yake, uhuru wake, pamoja na kuhatarishiwa amani yake..Hivyo mtu au kitu chochote kitakachokwenda nje na sheria hiyo..na kuipoteza amani ya raia..Basi mtu huyo au kitu hicho kitachukuliwa hatua kali ya kisheria.
  • Kila mwananchi ni mali ya Nchi husika..Hakuna mtu yeyote ambaye ni mali yake mwenyewe. Si ruhusa kisheria mtu kujiua!..Mtu yeyote hata anayejaribu kujiua anakwenda kinyume na katiba ya nchi na hivyo akibahatika kusalimika atakabiliwa na mashitaka ya MAUAJI!.

Kwa dondoo hizo chache. Tumeweza kujua Mwananchi ni nani na Majukumu yake ni yapi na usalama wake ni upi.

Hivyo tupo tayari sasa kujifunza juu ya upande wa Pili wa uraia wa MBINGUNI. Kumbuka mbingu ni Taifa kama tulivyosoma hapo juu..Kwahiyo hebu tutafakari pia dondoo chache zifuatazo ili tuelewe zaidi.

  • Kama vile Mwananchi wa kawaida anakuwa anaongozwa na katiba..Vivyo hivyo na mwananchi wa Mbinguni ni lazima aongozwe na KATIBA ya Kimbinguni..Ambayo hiyo si nyingine zaidi ya BIBLIA (Kitabu kitakatifu).
  • Kama vile raia wa nchi endapo akiishi kwa katiba ya nchi atafanikiwa, kadhalika Raia wa kimbinguni endapo akiishi kulingana na katiba ya kimbinguni ndipo atakapofanikiwa na kuishi maisha yasiyo na mashaka.Lakini akiishi kinyume na katiba ya ufalme wa mbinguni, basi atapata matatizo ya kushitakiwa, kufungwa au hata kuuawa.
  • Tatu kama vile kila mwananchi wa kawaida anavyolindwa na katiba ya nchi, vivyo hivyo Raia wa ufalme wa mbinguni anakuwa analindwa na katiba. Katiba ya nchi inasema ni wajibu wa vyombo vya usalama kuhakikisha usalama wa wananchi na mali zao muda wote..Hivyo jukumu la kumlinda mwananchi ni la serikali kupitia vyombo vya dola…Mwananchi wa kawaida hana ruhusu ya kubeba silaha mkononi na kutembea nayo barabarani.. silaha yake ni kuishi kulingana na katiba basi…jukumu la ulinzi ni la vyombo vya dola…Kadhalika Mwananchi wa ufalme wa mbinguni haruhusiwi kubeba silaha yoyote ya kimwili, jukumu la kupambana na maadui zetu ni jukumu la Malaika watakatifu, hao ndio wanaobeba silaha na kutupigania upande wetu…silaha yetu kubwa ni NENO LA MUNGU (katiba) huo ndio upanga wetu.

Biblia inasema katika..

Waefeso 6:11 “Vaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kuzipinga hila za Shetani.

12 Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho.

13 Kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama.

14 Basi simameni, hali mmejifunga kweli viunoni, na kuvaa dirii ya haki kifuani,

15 na kufungiwa miguu utayari tupatao kwa Injili ya amani; 6.16 zaidi ya yote mkiitwaa ngao ya imani, ambayo kwa hiyo mtaweza kuizima mishale yote yenye moto ya yule mwovu.

17 Tena ipokeeni chapeo ya wokovu, na upanga wa Roho ambao ni neno la Mungu; 6.18 kwa sala zote na maombi mkisali kila wakati katika Roho, mkikesha kwa jambo hilo na kudumu katika kuwaombea watakatifu wote”

Hivyo Mwananchi yoyote wa Ufalme wa mbinguni hana budi Kuifahamu katiba kikweli kweli…Kama vile ilivyo jukumu la kila mwananchi kuifahamu katika ya nchi yake.

Sasa Madhara ya kutoifahamu Biblia ni nini?

Madhara ya kutoifahamu biblia(Neno la Mungu) kwa Mwananchi wa Taifa la Mbinguni,.hayatofautiani sana na madhara ya mwananchi wa kawaida kutoifahamu katiba.

Mwananchi asiyeifahamu katiba, ni rahisi kufanya makosa  na asijue kama anafanya makosa..Ni rahisi kwenda kulala na ndugu yake wa damu, na wakati hajui sheria ya nchi (katiba) inasema kwamba ni kosa mtu yeyote kulala na ndugu wake wa damu, hukumu yake ni kifungo cha maisha.

Kadhalika anaweza akagombana tu na ndugu yake na kwa hasira akaenda kumchomea nyumba yake, pasipo kujua katiba inasemaje kwa mtu anayepatikana kwa kosa la kuchoma nyumba..Kosa la kuchoma nyumba kulingana na sheria ya nchi yetu, hukumu yake ni kifungo cha maisha. Sasa mambo madogo tu kama hayo yanaweza kumsababishia akapoteza maisha yake yote kutumikia vifungo.

Hatari ya kutoijua Biblia kwa mwamini.

Vivyo hivyo mwananchi wa Taifa la mbinguni asipoielewa katiba ya mbinguni (yaani biblia) inasema nini, anaweza kujikuta anafanya mambo akidhani anampendeza Mungu kumbe anamchukiza Mungu pakubwa..na adhabu yake ikawa ni ziwa la moto milele..Mtu anaweza akawa ni mlevi akidhani ulevi si dhambi..anaweza akawa mwasherati akidhania uasherati sio dhambi..anaweza akawa mwabudu sanamu akidhani sio dhambi..n.k

Pia madhara mengine ya kutoijua katiba ni KUONEWA NA KUNYANYASWA. Mwananchi asiyeijua katiba ya nchi yake hata mtu akija tu anaweza kumtishia na kumnyima haki yake..lakini kama anaijua hawezi kubabaishwa kwasababu anaelewa vizuri sheria za nchi..Hivyo ni ngumu kupoteza haki yake..Vivyo hivyo Mwananchi wa Ufalme wa mbinguni asipoielewa vizuri biblia ni rahisi adui shetani kumnyang’anya haki yake. Utaona anapelekeshwa huku na huku, majaribu haya na yale..kuteswa huku na kule..Yote hayo ni kwasababu haijui biblia Neno la Mungu.

Na Dondoo ya mwisho kabisa ni kwamba kila mtu ili awe Mwananchi halali wa Taifa hilo ni lazima awe  amezaliwa katika hilo Taifa (Huo ndio utambulisho wake wa kwanza),.. Vivyo hivyo katika Uraia wa ufalme wa mbinguni..Ni lazima mtu azaliwe katika ufalme huo.

Na mtu hazaliwi kwa damu na nyama, bali anazaliwa kwa Roho na kwa Maji ndipo ahesabike kuwa ni Mwananchi wa Taifa la Mbinguni.

Sasa mtu anazaliwaje kwa Maji na kwa Roho?

Maana ya kuzaliwa kwa maji ni kubatizwa kwa maji mengi (Yohana 3:23) Na kwa Jina la Yesu (Matendo 2:38). Na maana ya kuzaliwa kwa Roho ni kupata ubatizo wa Roho Mtakatifu. Hatua hizo mbili ndio zinazokufanya uwe umezaliwa mara ya pili na kuwa Mwananchi wa ufalme wa Mbinguni.

Yohana 3:3 “Yesu akajibu, akamwambia, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa mara ya pili, hawezi kuuona ufalme wa Mungu.

4 Nikodemo akamwambia, Awezaje mtu kuzaliwa, akiwa mzee? Aweza kuingia tumboni mwa mamaye mara ya pili akazaliwa?

5 Yesu akajibu, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa kwa maji na kwa Roho, hawezi kuuingia ufalme wa Mungu.

6 Kilichozaliwa kwa mwili ni mwili; na kilichozaliwa kwa Roho ni roho.

7 Usistaajabu kwa kuwa nilikuambia, Hamna budi kuzaliwa mara ya pili”.

Je umezaliwa mara ya PILI?. Je wewe ni Mwananchi wa Taifa teule la kimbinguni..Je wewe ni mrithi?..Kumbuka FALME NA MATAIFA YA DUNIA YOTE YATAPITA…Lakini UFALME WA MBINGUNI UTADUMU MILELE..NA RAIA WAKE WATADUMU MILELE!!.

Yapo mengi ya kujifunza juu ya ufalme huu wa mbinguni tukilinganisha na ufalme wa duniani..lakini Muda usingetosha kuyaandika yote hayo, lakini kwa haya machache, yatatupa chachu ya kuzidi kuutafuta ufalme wa mbinguni kila siku kwa bidii.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAP

Bwana akubariki sana

Tafadhali share na wengine.

Maran atha!


Mada Nyinginezo:

INJILI NI NINI?

Mbona Mungu anaruhusu watu wapate shida, ilhali ana uwezo wa kutuepusha?

UFALME WA MUNGU HAUPATIKANI KIRAHISI.

JE! UNAYO NAFASI MBINGUNI?

KUWA MAKINI NA MITANDAO, NI SHIMO REFU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Yule aliyemzuia Yohana asimsujudie alikuwa ni Mwanadamu au Malaika?

Yule aliyemzuia Yohana asimsujudie katika Ufunuo 19:10 alikuwa ni nani, Je! ni Mwanadamu au Malaika?

JIBU: Tusome…

Ufunuo 19: 10 “ Nami nikaanguka mbele ya miguu yake, ili nimsujudie; akaniambia, Angalia, usifanye hivi; mimi ni mjoli wako na wa ndugu zako walio na ushuhuda wa Yesu. Msujudie Mungu. Kwa maana ushuhuda wa Yesu ndio roho ya unabii”.

Mtu anayetumika kama wewe huyo ni Mjoli wako. Mfanyakazi anayefanya kazi kama ya kwako huyo ni mjoli wako na wewe ni mjoli wake…Hivyo katika Mstari huo hapo juu Yohana alikuwa anataka kumsujudia yule aliyekuwa anazungumza naye,aliyekuwa anamwonyesha maono yale…Lakini akamzuia na kumwambia mimi ni mjoli wako (maana yake ninayafanya kazi kama ya kwako ya utumishi)..na pia wa ndugu zako (yaani wanadamu wenzake ambao ndio sisi tulio na ushuhuda wa Yesu).

Malaika ni wakina nani?

Kwasababu Biblia inasema Malaika ni roho watumikao..wanaotuhudumia sisi(Soma Waebrania 1:3-14)..Kadhalika na sisi wanadamu tunaomtumikia Mungu ni Watumishi wa Mungu vile vile…tunaotumika katika Ufalme wa Mbinguni..Hivyo sisi pamoja na malaika ni Watumishi wa Mungu wa mbinguni…Kwahiyo sisi ni wajoli wa Malaika na Malaika vile vile ni wajoli wetu.

Kwahiyo tukirudi kwenye hilo swali linalouliza.. “aliyemzuia Yohana asimsujudie alikuwa ni Mwanadamu au Malaika?”…Jibu lake ni kwamba alikuwa ni MALAIKA. Kwasababu Yohana tangu mwanzo alikuwa haonyeshwi maono yale na mwanadamu yoyote…bali Malaika ambaye naye huyo Malaika aliyapokea maono hayo kutoka kwa Yesu Kristo mwenyewe. Hakuna mwanadamu yoyote aliyehusika hapo kwa namna moja au nyingine..

Ufunuo 1:1 “Ufunuo wa Yesu Kristo, aliopewa na Mungu awaonyeshe watumwa wake mambo ambayo kwamba hayana budi kuwako upesi; naye akatuma KWA MKONO WA MALAIKA akamwonyesha mtumwa wake Yohana”

Wapo watu wanakosa shabaha katika hilo kudhani kuwa Yule alikuwa ni mtakatifu Fulani aliyekufa zamani au aliyepaa pengine Musa au Eliya, au Nabii Fulani, kwamba ndiye aliyemwambia maneno hayo asimsujudie kwa kuwa yeye ni mjoli wake na wa ndugu zake walio na ushuhuda wa Yesu. Japo ambalo si la kimaandiko..Lakini sasa tunajua kuwa yule hakuwa mwanadamu bali ni Malaika wa mbinguni.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Bwana akubariki.

Maran atha!

Mada Nyinginezo:

UFUNUO: Mlango wa 19

DANIELI: Mlango wa 1

ESTA: Mlango wa 1 & 2

Uasherati wa Kiroho maana yake nini?

ALIKUWAKO NAYE HAYUKO, NAYE YU TAYARI KUPANDA KUTOKA KUZIMU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

MSIJISUMBUE KWA NENO LOLOTE.

“Msijisumbue kwa neno lolote;….(Wafilipi 4:6)

Vita nyingine kubwa ambayo inapiganwa katika akili ya mkristo, ni vita ya hofu ya maisha,.. kwamba kesho yangu itakuwaje, nitakula nini, nitavaa nini, nitakuwa wapi miaka 5 mbeleni,.. nikiendelea katika hali hii hii uzee wangu utakuwaje, kodi ya nyumba mwezi ujao ikiisha nitapata wapi nyingine, watoto wangu wakiugua kwa ghafla fedha ya matibabu makubwa nitaitolea wapi? n.k.n.k… hayo ni mawazo ambayo yanapenya katikati ya mawazo yetu, wakati mwingine aidha tunataka au hatutaki,, na madhara yake ni kuwa jambo hii likishakita mizizi ndani yetu, sasa Neno KUSUMBUKIA ndipo linapozaliwa..

Tunaanza Kujisumbua kwa mawazo mengi usiku na mchana, kwa nguvu nyingi, kwa gharama zozote ili tu ufikie malengo hayo..Sasa sio vibaya kufikiria mambo yajayo na kuyawekea mipango..lakini kupo kufikira kuliko sahihi na kupo kufikiria kusiko sahihi… Kufikiri kusiko sahihi kunaleta HOFU!!

Bwana alilifahamu hilo, na anajua kabisa kwa jinsi tulivyo hapa duniani tumezungukwa na mambo mengi ya kidunia, hofu ya maisha ni lazima ituvamie,…. lakini yeye alitupa suluhisho sahihi la sisi kuweza kuishinda hali hiyo akasema..

Wafilipi 4:6 “Msijisumbue kwa neno lolote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu”.

Unaona, anasema, msijisumbue kwa Neno lolote, sio moja, au mawili, au matatu, bali lolote.., anajua yapo mengi hayawezi kuisha, makubwa kwa madogo,hivyo lolote lile tusijisumbue nalo, yatatufanya tutoke katika mstari wa wokovu na fikra zetu za kutazama mambo ya mbinguni,.. bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu,”…

Hizo ni nguzo muhimu sana..

Tunapokutana na changamoto za ki-maisha, au shida Fulani, tusianze kupaniki kwa haraka na kuanza kuzichosha fahamu zetu,… kuwaza sana hadi kukosa usingizi, hapana bali tunapaswa tuchukue haja zetu hizo katika maombi, tumpelekee yeye haja zetu hizo, kwasababu anasema pia..

1Petro 5:6 “Basi nyenyekeeni chini ya mkono wa Mungu ulio hodari, ili awakweze kwa wakati wake;

7 huku mkimtwika yeye fadhaa zenu zote, kwa maana yeye hujishughulisha sana kwa mambo yenu”.

Unaona Mungu anajishughulisha sana na mambo yetu, pale tunapojinyenyekeza mbele zako na kumtwika yeye kila shida yetu.. ukitaka kufahamu hilo kama Mungu anajishughulisha kweli na mambo yetu, angalia huo moyo wako unaodunda miaka na miaka hatujawahi kuununulia betri ili uendelee kudunda kila saa,.. wala hujawahi kuuhudumia au kuufanyia service yoyote ili ufanye kazi vizuri, lakini fahamu yeye ndiye Mungu anayeudundisha kila wakati..hata chakula tunachokila tumboni baada ya hapo hatushughulikii mmengenyo wake..mwili ndio unaofanya hiyo kazi wenyewe…wewe huhusiki hata kidogo…Sasa ikiwa hatujajisumbukia kwa hilo kwanini kuumiza vichwa kwa hayo yaliyosalia..?

Jaribu kutafakari tena  vizuri:

Angalia, kucha zako, zinavyokuwa, na nywele zako ambazo kila siku unazikata.., haijawahi kutokea hata sikumoja ukawa na hofu kwamba ahaa, pengine hizi nywele zinaweza zisiote tena, embu ngoja nikazitafutie mbolea nzuri za kuziwekea ili ziote vilevile kwa rangi ile ile,.. sasa ikiwa hayo hatuwezi kuyasumbukia ambayo yanayo umuhimu mkubwa zaidi kuliko kazi zetu, na nyumba zetu, na nguo zetu kwanini tuiruhusu hofu?…Huwezi kumtumikia Mungu ukiwa na hofu, huwezi kusonga mbele ukiwa na hofu, kazi ya Mungu huwezi kuifaya ukiwa na stress..Ukishaona unahofu kali kuhusu kesho fahamu kuwa Mungu hayupo hapo..kwasababu Roho wa Mungu kamwe hamletei Mtu hofu bali Amani na kabla ya kuanza kuzungumza na wewe na kukupa ufunuo fulani,..ataanza kushughulika kwanza na hofu iliyopo ndani yako..hiyo ikishaondoka ndipo azungumze na wewe..

Hivyo tukiwa waombaji, kudumu katika sala itatusaidia kuuvuta uwepo wa Mungu karibu zaidi na sisi Mungu muweza wa yote asiyeshindwa na lolote,.. Mungu aliyeumba milima, na bahari, nyangumi wa kubwa, na mabara, Mungu aliyeumba dhahabu zote na almasi zote za ulimwengu mzima,… aliyeumba matajiri na maskini, aliyeumbwa wafalme na viongozi wote, huyo ndiye anayekuambia Usijisumbue kwa Neno lolote, bali nitwike mimi fadhaa zako,niachie mimi wewe endelea kuwaza mambo ya ufalme wa mbinguni..

JE! TUKIJIFUNZA KUWA WATU WANA NAMNA HIYO, FAIDA YAKE NI IPI?

Ukiendelea sasa kusoma mstari ule ule mbele kidogo utaona unasema hivi..

Wafilipi 4:6 “Msijisumbue kwa neno lolote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu.

7 Na amani ya Mungu, ipitayo akili zote, itawahifadhi mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu”.

Umeona hapo chini? Anasema “NA AMANI YA MUNGU, ipitayo akili zote, itawahifadhi mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu”… Ukishamtwika yeye fadhaa zako zote, na shida zako zote, ukaondoa ufahamu wako wote katika matatizo yanayokuzunguka… ukijua kabisa yeye mwenyewe atayashughulikia..Basi ile AMANI yake itashuka juu yako wakati huo huo…hiyo ni amani ipitayo fahamu zote, amani ya ki-Mungu si ya kibinadamu, ambayo hiyo huwa ikishushwa juu ya mwanadamu, anakuwa mtu mwingine kabisa,

Watu wanaweza kumshangaa inakuwaje mtu huyu yupo katika hali hii au hali ile, amefiwa na ndugu zake wote, hana hiki au hana kile, kodi inakaribia kuisha.. lakini anayofuraha na amani kuliko hata sisi wenye kila kitu, yeye ndiye anayekuja kutufariji sisi? ..Hawajui kuwa hiyo ndiyo Amani ipitayo fahamu zote…Sio kwamba matatizo hayapo! Yapo lakini…Amani ya Kristo imeyafunika na hivyo huna hofu.

Zaburi 127:2b……. Yeye humpa mpenzi wake usingizi’.

Amani hiyo ikimwingia mtu vizuri, hofu yote inaondoka, anaishi kama ndege ambaye anaamka asubuhi akimwimbia Mungu nyimbo za furaha, na kabla ya kwenda kulala anamwimbia Mungu nyimbo za furaha, hajali kesho yake itakuwaje, kwamba kitakuwepo au hakitakuwepo..Lakini hata siku moja Mungu hutasikia kuwa Mungu amemnyima rizki..

Lakini amani hiyo ni ngumu kuifikia kwa namna ya kawaida kama hatutakuwa watu wa kuomba, na watu wa kushukuru, pamoja na kujijengea utaratibu wa kulitafakari Neno lake kwa wakati mwingi kwa kadri tuwezavyo mpaka. Ipo Mifano mingi ya kujifunza ndani ya Neno la Mungu..Tusiposoma Neno hatutaijua na hivyo kupungukiwa nguvu za rohoni.

Bwana akubariki.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengine:

Mada Nyinginezo:

FAIDA ZA MAOMBI.

MAJARIBU MATATU YA YESU KRISTO

KISIMA CHA MAJI YA UZIMA NI KILE KILE CHA ZAMANI.

SIKU ILE NA SAA ILE.

Rudi Nyumbani:

Print this post

SIKUJA KULETA AMANI DUNIANI, BALI MAFARAKANO.

Kwanini Bwana Yesu alisema sikuja kuleta amani duniani, bali mafarakano.

Luka 12: 51 “Je! Mwadhani ya kwamba nimekuja kuleta amani duniani? Nawaambia, La, sivyo, bali mafarakano.

52 Kwa kuwa tokea sasa katika nyumba moja watakuwamo watu watano wamefarakana, watatu kwa wawili, wawili kwa watatu.

53 Watafarakana baba na mwanawe, na mwana na babaye; mama na binti yake, na binti na mamaye; mkwe mtu na mkwewe, mkwe na mkwe mtu”.

Fananisha mstari huu na..

Yohana 14:27 “ Amani nawaachieni; amani yangu nawapa; niwapavyo mimi sivyo kama ulimwengu utoavyo. Msifadhaike mioyoni mwenu, wala msiwe na woga”.

Swali ni Je! maneno haya ya Bwana Yesu yanajichanganya yenyewe?..Maana sehemu moja anasema sikuja kuleta amani duniani..Na sehemu nyingine anasema Amani nawaachieni.

Tukiisoma Biblia pasipo msaada wa Roho Mtakatifu hatutaambulia chochote..zaidi ya kuona Biblia ina kasoro nyingi. Lakini tukiisoma kwa Msaada wa Roho Mtakatifu tutanufaika pakubwa na kuelewa mengi.

Ni vizuri kufahamu kuwa Mtu aliye katika dhambi, akiamua kukata shauri la kumpokea Yesu moyoni mwake..Kuna mambo mawili yatatokea maishani mwake… kwanza atapata amani Fulani ya moyo isiyoelezeka…Hiyo amani inaletwa na Roho Mtakatifu mwenyewe…ataanza kuhisi kuna wepesi Fulani na tumaini la ajabu limeingia ndani yake, ambalo limemsababishia amani isiyokuwa ya kawaida…Alikuwa anahofu na huzuni anaanza kuhisi faraja, alikuwa hana tumaini lakini anaanza kuona matumaini n.k

Kupoteza amani nyingine;

Lakini pia pamoja na amani hiyo ya kiMungu kuingia ndani yake..Kuna amani nyingine mtu huyo ataipoteza…Na hiyo ni AMANI YA NJE…Ndio hapo kutokana na kuokoka kwake wale marafiki zake waliokuwa wanakwenda naye kufanya mambo mabaya wanaanza kumchukia, wengine wanaanza kukwaruzana na wazazi wao, wengine wanaanza kugombana na ndugu zao wa kike na wakiume n.k..Sasa amani hiyo ya nje ambayo Inapotea ndiyo Bwana Yesu aliyokuwa anaizungumzia katika Mstari hapo juu unaosema kwamba amekuja kuleta mafarakano.

Lakini kumbuka amani ile ya ndani ya wokovu inakuwa ipo pale pale (Hiyo haiondoki)…yaani mtu pamoja na kwamba kakorofishana na ndugu, au jamaa na marafiki kutokana na imani yake kwa Kristo, lakini bado mtu huyo huyo kila siku moyoni mwake anakuwa anapata amani na faraja na furaha isiyo na kifani kwa kumjua Yesu Kristo.

Gharama ya uanafunzi:

Tunapomfuata Kristo kumbuka siku zote, Huwezi kuepuka kupoteza amani yako ya nje na watu wanaokuzunguka…ulikuwa mshirikina sasa umeacha, washirikina wenzako wataendeleaje kukupenda?..Ulikuwa msengenyaji sasa umeacha, wasengenyaji wenzako wataachaje kukuchukia na kuanza kukusengenya wewe? Na mambo mengine yote ni hivyo.

Gharama ya kuingiza amani ndani ya moyo wako ni kuiopoteza amani ya nje.

Bwana atusaidie tusikwepe gharama hizo, na zaidi ya yote tushinde na zaidi ya kushinda katika Jina la Yesu Kristo.

Ubarikiwe.

Mada Nyinginezo:

JE! NI KWELI UMEMFUATA YESU?

TUMEPEWA, SI KUMWAMINI TU KRISTO, ILA NA KUTESWA KWA AJILI YAKE;

TUUTAZAME PIA MWISHO WA UJENZI WETU.

Biblia inamaana gani kusema;aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi?

ROHO MBAYA KUTOKA KWA BWANA.

 

Rudi Nyumbani:

Print this post

KRISIMASI (CHRISTMAS) NI NINI? JE IPO KATIKA BIBLIA?

SWALI: Krisimasi ni nini, Je! ni kweli Yesu alizaliwa tarehe 25 disemba, Je ni sahihi kwa mkristo kusheherekea Krisimasi?


Krisimasi au kwa lugha ya kigeni Christmas, Ni neno lenye muunganiko wa maneno mawili: Kristo na masi/misa na hivyo  kuunda neno Kristo-masi, au misa ya Kristo, inayomaanisha  pia ibada ya Kristo.

Ni siku ambayo mabilioni ya wakristo duniani kote wanaisheherekea kama siku ya kuzaliwa kwa mwokozi wetu Yesu Kristo, ambayo inadhaniwa kuwa ilikuwa ni tarehe 25 ya mwezi Disemba. Hivyo kila mwaka siku kama hii na tarehe kama hii wakristo wengi sana wanaienzi kama siku ya kuzaliwa kwa shujaa wa wokovu wetu YESU KRISTO.

Lakini Je! kimaandiko Yesu alizaliwa tarehe 25 Disemba?

Hakuna mahali popote katika biblia inatoa tarehe au mwezi wa kuzaliwa kwa Bwana wetu Yesu Kristo. Ni kwa kutathimini tu majira na mazingira yaliyokuwa yanaendelea siku ya kuzaliwa kwake ndiyo iliyopelekea kuzaliwa siku  na miezi tofauti tofauti kama hiyo.

Sasa kutokana na kuwa na mitazamo mingi tofauti tofauti, makundi mengi yamezaliwa na kila moja linadai mwezi wake na tarehe yake. Mengine yanaamini Kristo alizaliwa mwezi Aprili, mengine yanaamini Kristo alizaliwa mwezi Agosti… na mengi septemba na mengine octoba na mengine Disemba n.k.. Lakini lililopata umaarufu mkubwa ni hilo la mwezi Disemba..Lakini Je! Kristo alizaliwa kweli mwezi huo?

Zipo Sababu kadhaa kwenye maandiko zinazothibitisha kuwa Yesu hakuzaliwa mwezi Disemba.

kama tukisoma kitabu cha Luka tunaweza kupata kiashirio kimojawapo… tunaona kuwa malaika Gabrieli alimtokea Zakaria kuhani (babaye Yohana mbatizaji) siku fulani maalumu ambayo tayari ilikuwa imeshapangwa na mbingu, nayo tunasoma ilikuwa ni siku ya zamu za ukuhani wa ABIYA.

Luka 1: 5 “Zamani za Herode, mfalme wa Uyahudi, palikuwa na kuhani mmoja, jina lake Zakaria, wa ZAMU YA ABIYA, na mkewe alikuwa mmojawapo wa uzao wa Haruni, jina lake Elisabeti.

6 Na wote wawili walikuwa wenye haki mbele za Mungu, wakiendelea katika amri zote za Bwana na maagizo yake bila lawama.

7 Nao walikuwa hawana mtoto, maana Elisabeti alikuwa tasa, na wote wawili ni wazee sana.

8 Basi ikawa, alipokuwa akifanya kazi ya ukuhani katika taratibu ya zamu yake mbele za Mungu,

9 KAMA ILIVYOKUWA DESTURI YA UKUHANI, kura ilimwangukia kuingia katika hekalu la Bwana ili kufukiza uvumba”.

Ahaa! Tusoma Kumbe katika siku za zamu za Abiya.. ambazo alikuwa anafanya kazi za kikuhani ndizo Zekaria alizotokewa na malaika Gabrieli. Sasa ili kufahamu zamu ya Abiya ilikuwa inaangukia katika miezi ipi turudi katika agano la kale tusome ndipo tutakapopata majibu ya majira ya ambayo Zekaria alitokewa na Malaika Gabrieli.

Na kama tunavyosoma katika 1Nyakati 24. Inasema:

1Nyakati 24: 7 “Kura ya kwanza ikamtokea Yehoiaribu, na ya pili Yedaya;

8 ya tatu Harimu, ya nne Seorimu;

9 ya tano Malkia, ya sita Miyamini;

10 YA SABA HAKOSI, YA NANE ABIA;

11 ya kenda Yeshua, ya kumi Shekania;

12 ya kumi na moja Eliashibu, ya kumi na mbili Yakimu;

13 ya kumi na tatu Hupa, ya kumi na nne Yeshebeabu;

14 ya kumi na tano Bilga, ya kumi na sita Imeri;

15 ya kumi na saba Heziri, ya kumi na nane Hapisesi;

16 ya kumi na kenda Pethahia, ya ishirini Ezekieli;

17 ya ishirini na moja Yakini, ya ishirini na mbili Gamuli;

18 ya ishirini na tatu Delaya, ya ishirini na nne Maazia”.

Kwahiyo hapo tunaweza kuona zamu ya Abiya ilikuwa ni ya NANE katika ufanyaji wa kazi za kikuhani. Na kazi hizo zilikuwa zinafanyika sabato mpaka sabato yaani wiki mpaka wiki,.. hivyo zama ya Abiya iliangukia wiki ya 8 katika utendaji kazi wa kikuhani. Na tunajua kuwa mwaka wa kiyahudi hauanzi kama huu wa kwetu huku, januari hapana bali huwa unaanza mwanzoni mwa mwezi april,.. na hivyo ukihesabu hapo majuma mawili utaona zamu hiyo inadondokea katikati ya mwezi wa 6.

Kwahiyo mpaka hapo tunaweza kusema sasa Zekaria kumbe alitokewa majira ya mwezi wa 6 na muda mfupi baada ya hapo pengine mwezi wa 6 mwishoni au wa 7 mwanzoni mkewe Elizabethi alipata mimba, na biblia inatuambia pia miezi 6 baada ya kupata mimba kwake Elizabethi Malaika Gabrieli alimwendea Bikiria Mariamu na kumpasha habari za yeye kupata mimba ya Bwana Yesu (Luka 1:26).

Hivyo mpaka hapo tunaona itakuwa imeshafika mwezi wa 12 katikati, au mwezi wa kwanza mwanzoni, ndipo mimba ya Bwana wetu YESU ilipotungishwa. Na tunajua kuwa baada ya miezi 9 mtoto huwa ndio anazaliwa, sasa ukipiga hesabu utaona kuwa uwezekano mkubwa wa kuzaliwa kwa Bwana wetu YESU KRISTO unaweza angukia katikati ya mwezi wa 9 au mwanzoni mwa mwezi wa 10, kwa kalenda yetu sisi. Na ndio maana utaona pia Bwana Yesu alianza kuhubiri akiwa na miaka 30 na akamaliza  kuhubiri akiwa na miaka 33 na nusu, na siku aliposulibiwa wote tunajua  ilikuwa ni Mwezi wa nne (April). Kwahiyo ukihesabu vizuri hapo utagundua alianza kuhubiri kati ya mwezi wa 9 hadi wa 10, ambao ndio mwezi aliozaliwa, ili kutumizia jumla ya miaka mitatu na nusu ya huduma yake.

Zipo pia thibitisho nyingine zinaonyesha kuwa Kristo alizaliwa majira hayo lakini hatuwezi kuziandika zote hapa. Kwahiyo Yesu hakuzaliwa tarehe 25 Disemba..

Je! Chimbuko la Kristo kuzaliwa tarehe 25 Disemba limetoka wapi?

Kwa kufuata na kuzaliwa kwa mungu ya kirumi TAMUZ ndipo tarehe hii ikageuzwa na kuwa ndio siku ya kuzaliwa kwa Bwana wetu YESU KRISTO.

Lakini je! wanaodhimisha siku hiyo tarehe 25 Disemba (Krisimasi) wanafanya makosa?.

 Jibu ni hapana biblia haijatoa amri juu ya kuadhimisha siku ya kuzaliwa kwa Yesu (krisimasi) mahali popote, kwamba ifanyike au isifanyike, na hivyo yeyote anayefanya hivyo ikiwa ni kwa lengo lake binafsi kwamba anaona umuhimu wa kuunda siku yake inayoweza kukaribiana na siku ya kuzaliwa kwa Yesu ili amtukuze na kumfurahia Mungu, Iwe ni Aprili, iwe ni Agosti, iwe ni Septemba, Iwe ni Octoba, Iwe ni Disemba iwe ni siku yoyote ile hatendi dhambi maadamu kaiweka wakfu kwa Mungu wake, ili kumwabudu na kumshukuru kwa kupewa zawadi ya wokovu duniani.

Hivyo kama unaiadhimisha siku maadamu unaidhamisha kwa Bwana wako na si kwa mungu mwingine mgeni, ni vizuri zaidi na itakuwa ni ya Baraka kwako hata kama ni tarehe 25 Disemba, siku ya Krisimasi kama utaifanya kuwa ni siku ya kumsifu Mungu na kumshukuru Mungu itakuwa ya Baraka kwako.lakini kama utaifanya hiyo kuwa ni siku yako ya kuabudu sanamu au kwenda kufanya uzinzi, au kunywa pombe, au kwenda disko, au kwenda kwenye anasa ni heri usingeihadhamisha kabisa kwasababu jambo unalolifanya ni machukizo makubwa..Unamsulibisha Kristo mara ya pili.

Fanya uamuzi sahihi;

Je! Umeokoka? Unafahamu kuwa hizi ni siku za mwisho na KRISTO yupo mlangoni sana kurudi?..  Dalili zote zinaonyesha kuwa hichi kizazi tunachoishi mimi na wewe kinaweza kushuhudia tukio la kurudi kwa pili kwa Kristo..Unaongojea nini?

Tubu dhambi zako leo, ukabatizwe kwa JINA LA YESU KRISTO upate ondoleo la dhambi zako, Kisha Bwana atakupa kipawa cha Roho wake mtakatifu kukulinda mpaka siku ile ya UNYAKUO.

Bwana akubariki.

Nikutakie Krisimasi Njema, Na heri ya mwaka mpya ujao!

Kwa mafundisho zaidi ya Neno la Mungu/maombezi/wokovu/ushauri wasiliana nasi kwa namba hizi +255693036618/ +255789001312

Au jiunge na kundi letu la mafundisho Whatsapp kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

Je! ni sahihi kwa Mkristo kusherekea siku yake ya kuzaliwa.[Birth day]?

Sabato halisi ni lini, Je! ni Jumapili au Jumamosi?, Ni siku gani itupasayo kuabudu?

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

Rudi Nyumbani:

Print this post

ALIKUWAKO NAYE HAYUKO, NAYE YU TAYARI KUPANDA KUTOKA KUZIMU.

Ni nani huyo “alikuwako naye hayuko, naye yu tayari kupanda kutoka kuzimu.?”

Shalom, Jina la Yesu Kristo Bwana wetu lizidi kubarikiwa daima Tunapaswa tukumbuke kuwa Kila tunapoiona siku mpya, basi ndivyo tunavyopiga hatua nyingine kuufikia ule mwisho..Zile dalili kuu za mwisho wa dunia zimeshatimia, hivyo wakati wowote tunaweza kulishuhudia tukio la unyakuo wa kanisa..Na kwa wale watakaobaki nao pia watazishuhudia kazi za mpinga-Kristo pamoja na mapigo yote ya Mungu aliyoyazungumzia katika Ufunuo 16

Hivyo tunapaswa tuwe macho vilevile tuwe na maarifa ya kutosha kuzijua njama za shetani,..Inasikitisha kuona kuwa watu wengi bado wanadhani mpinga-Kristo ni mtu ambaye atatoka sehemu isiyojulikana, na kwamba atakuwa ni mtu wa ajabu sana.. vilevile kazi zake zitaonekana ikishafika kipindi cha dhiki kuu, hatujui kuwa roho hii ilishaanza kutenda kazi tangu zamani, ikaleta uharibifu wake kwa sehemu, na ndiyo hiyo hiyo itakayoleta dhiki kuu wakati wa mwisho… kwa kutumia ufalme wake ule ule uliotumia mwanzoni.

Kama vile maandiko yanavyosema:

Mhubiri 1:9 “Yaliyokuwako ndiyo yatakayokuwako; na yaliyotendeka ndiyo yatakayotendeka; wala jambo jipya hakuna chini ya jua”

Ni kweli kuwa hata kazi za mpinga-Kristo hazitakuwa mpya, zilishakwisha kuanza tangu zamani, na alishawahi kuzifanya huko nyuma na ni kitu kile kile ambacho atakuja kukifanya tena huko mbeleni,.. Kama Bwana wetu Yesu Kristo tunavyomtazamia kuja kwake… Na tunafahamu kuwa atatoka mbinguni, yeye mpinga-Kristo ana kitu gani hasa cha ziada tusijue atokako?..Hivyo usitazamie mambo makubwa sana, wala usitazamie mambo mapya sana, ..wala usitazamie atotokea nje ya ufalme tofauti na ule ule aliotokea nao mwanzo kuleta uharibifu..

Sasa tukirudi katika kitabu cha Ufunuo sura ya 17, tunaona Yohana akionyeshwa yule mwanamke kahaba, aliyeketi juu ya mnyama mwekundu sana.

tusome..

Ufunuo 7:1 Akaja mmoja wa wale malaika saba, wenye vile vitasa saba, akanena nami, akisema, Njoo huku, nitakuonyesha hukumu ya yule kahaba mkuu aketiye juu ya maji mengi;

2 ambaye wafalme wa nchi wamezini naye, nao wakaao katika nchi wamelevywa kwa mvinyo ya uasherati wake.

3 Akanichukua katika Roho hata jangwani, nikaona mwanamke, ameketi juu ya mnyama mwekundu sana, mwenye kujaa majina ya makufuru, mwenye vichwa saba na pembe kumi.

4 Na mwanamke yule alikuwa amevikwa nguo ya rangi ya zambarau, na nyekundu, amepambwa kwa dhahabu, na kito cha thamani, na lulu, naye alikuwa na kikombe cha dhahabu mkononi mwake, kilichojawa na machukizo, na machafu ya uasherati wake.

5 Na katika kipaji cha uso wake alikuwa na jina limeandikwa, la siri, BABELI MKUU, MAMA WA MAKAHABA NA MACHUKIZO YA NCHI.

6 Nikamwona yule mwanamke amelewa kwa damu ya watakatifu, na kwa damu ya mashahidi wa Yesu. Nami nilipomwona nikastaajabu ajabu kuu.

7 Na yule malaika akaniambia, Kwani kustaajabu? Nitakuambia siri ya mwanamke huyu, na ya mnyama huyu amchukuaye, mwenye vile vichwa saba na zile pembe kumi.

8 Yule mnyama uliyemwona alikuwako, naye hayuko, naye yu tayari kupanda kutoka kuzimu na kwenda kwenye uharibifu. Na hao wakaao juu ya nchi, wasioandikwa majina yao katika kitabu cha uzima tangu kuwekwa misingi ya ulimwengu, watastaajabu wamwonapo yule mnyama, ya kwamba alikuwako, naye hayuko, naye atakuwako.

9 Hapo ndipo penye akili zenye hekima. Vile vichwa saba ni milima saba anayokalia mwanamke huyo.

10 Navyo ni wafalme saba. Watano wamekwisha kuanguka, na mmoja yupo, na mwingine hajaja bado. Naye atakapokuja imempasa kukaa muda mchache.

11 Na yule mnyama aliyekuwako naye hayuko, yeye ndiye wa nane, naye ni mmoja wa wale saba, naye aenenda kwenye uharibifu.

12 Na zile pembe kumi ulizoziona ni wafalme kumi, ambao hawajapokea ufalme bado, lakini wapokea mamlaka kama wafalme muda wa saa moja pamoja na yule mnyama.

13 Hawa wana shauri moja, nao wampa yule mnyama nguvu zao na mamlaka yao.

14 Hawa watafanya vita na Mwana-Kondoo, na Mwana Kondoo atawashinda, kwa maana Yeye ni Bwana wa Mabwana, na Mfalme wa Wafalme, na hao walio pamoja naye ndio walioitwa, na wateule, na waaminifu.

mwonekano wake:

Kumbuka mwanamke huyu anaonekana amelewa kwa damu za watakatifu na damu ya mashahidi wa Yesu,..Unaweza kujiuliza amelewaje lewaje, amewezaje kuwachinja hao watu wote na kunywa damu yake, angali yeye ni mwanamke tu?… Utagundua kuwa ni kwasababu hakuwa peke yake,bali ni yule mnyama anayemwendesha chini yake ndiye anayemsaidia kufanya hizo kazi…

Na mnyama huyo biblia inasema alikuwepo naye hayupo naye yupo tayari kupanda katika uharibifu..Ili kufahamu kama alikuwepo lini,.. tunapaswa turudi kwenye historia kidogo, wakati Yohana anaonyeshwa maono hayo tayari utawala wa Rumi ulikuwa umeshawaua wayahudi wengi sana,.. na watakatifu wengi sana..Kuanzana na Kristo mwenyewe Bwana wetu, Ni warumi ndio waliomsulubishwa..baadaye tena AD 70 uliuwa wayahudi wengi, na kuliteketeza hekalu,.. jambo ambalo Bwana Yesu alishalitabiri katika Mathayo 24, juu ya kuhusuriwa kwa Yerusalemu, baadaye tena katika majira ya kanisa la Pili hadi wakati wa matengenezo ya Kanisa, Rumi hii ambayo baadaye ilikuja kuwa ya kidini chini ya Kanisa Katoliki ilihusika na mauaji ya watakatifu Zaidi ya milioni 68, wasiokuwa na hatia yoyote, waliuliwa kwasababu tu waliishika Imani yao, na kukataa mafundisho mengine ambayo hayakuwa mafundisho ya mitume..Kama Yohana 16:2 inavyosema “naam, saa yaja atakapodhania kila mtu awauaye ya kuwa anamtolea Mungu ibada.”

Maangamizi yake:

Historia inaonyesha hakuna ufalme wowote, au dini yoyote, wala utawala wowote uliowahi kuuwa wakristo kwa idadi kubwa ya watu namna hiyo,..zaidi ya utawala wa KiRumi.. sio tu kuifikia idadi hiyo , bali hata kukaribia idadi hiyo haijawahi kutokea..

Dini ya kikatoliki iliyokuwepo wakati ule si sawa na iliyopo sasahivi, wakati ule ilikuwa mtu yeyote ambaye anaonekana tu kwenda kinyume na Imani ile adhabu yake ilikuwa ni kifo,.. na ilikuwa imeenea kila mahali, ilikuwa ni dini ya kitaifa, unaaishi chini ya uongozi wa kidini (Ilikuwa ni serikali ya kidini), hakukuwa na mtu wa kawaida aliyeruhusiwa kusoma biblia kama ilivyo sasahivi, isipokuwa viongozi wa juu sana wa kanisa hilo..,

Si Chuki:

Tunapozungumza hivi sio kwamba tunatangaza chuki,.. au tunahukumu..au tunashambulia imani za wengine.. au tunaonyesha kwamba upande mmoja unajua zaidi ya mwingine.. au tunawachukia wakatoliki, au tunatangaza Imani mpya au dhehebu jipya. Hilo sio lengo hata kidogo,… lakini tunazungumza ukweli wa kimaandiko, ili kwamba anayetaka kuelewa aelewe na kila mtu asikie ukweli… UTAWALA WA RUMI, NA DINI YA RUMI NDIYO MAKAO MAKUU YA SHETANI NA MPINGA-KRISTO ATAKAYEKUJA!…Kwasababu huko nyuma alikuwepo alishatenda kazi hizo, naye yupo sasa hivi, isipokuwa amepoa kwa muda na ndiye atakayepanda na kwenda katika uharibifu siku za usoni.

Pembe Kumi:

Tukilifahamu hilo tunaweza kuona ni wakati gani huu tunaishi, kwamba ule mwisho umekaribia sana, na moja ya hizi siku utawala huu utapata nguvu tena, na safari hii hautaleta dhiki peke yake bali utatumia mataifa kusababisha dhiki, hizo ndio zile pembe 10 za Yule mnyama.

Mpinga-Kristo atakayetokea huko kwa kupitia kiti cha UPAPA.. atazitumia serikali zote za dunia nzima kuhimiza chapa..Na mtu yeyote atayeonekana hana chapa hiyo basi adhabu yake itakuwa ni mateso na kifo, kama wakati ule ule wa makanisa ya mwanzo..

Unaweza kuona tunaishi katika kipindi cha hatari kiasi gani?,..kumbuka “Alikuwako, naye hayuko, naye yu tayari kupanda kutoka kuzimu.

Kama wewe hujaokoka unasubiri nini?. Kila kiumbe kinafahamu wakati tuliobakiwa nao ni mchache hadi shetani mwenyewe anajua hilo na ndio maana anafanya kazi zake kwa kasi mno,.. kama tunavyoona wimbi zito la manabii wa uongo waliopo sasahivi..Tendo lililobaki ni kuTubu dhambi zako haraka kama hujatubu…kisha ukabatizwe kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako (Matendo 2:3), na Bwana mwenyewe atakupa kipawa cha Roho wake Mtakatifu kukulinda na kukuongoza katika kuijua kweli yote. Mpaka ile siku ya Unyakuo.

Ubarikiwe.

Maran atha!

Mada Nyinginezo:

CHAPA YA MNYAMA

MPINGA-KRISTO

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

KWANINI DAUDI ALIKUWA NI MTU ALIYEUPENDEZA MOYO WA MUNGU?

 

NI KIPI MUNGU ANACHOKITAZAMA ZAIDI, MOYO AU MWILI?

Rudi Nyumbani:

Print this post

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 7 (Yeremia na Maombolezo)

Jina la Yesu Kristo libarikiwe. Karibu katika mwendelezo wa mafunzo ya vitabu vya Biblia.

Tulishapitia vitabu 15 vya kwanza, kama hujavipitia nakushauri uvipitie kwanza ili tuende pamoja katika vitabu hivi vya mbele….Kitabu cha Mwisho kilikuwa ni kitabu cha Ezra..Ambaye tuliona Biblia inamtaja kama Mwandishi mwepesi…Ezra alitokea baada ya Wana wa Israeli kuingia Babeli.. kama tulivyojifunza huko nyuma kimtitiriko basi vile vitabu vya manabii kama vile Isaya, Yeremia,Ezekieli Danieli, na vinginevyo vingepaswa vitangulie kuorodheshwa kwenye kabla ya kitabu cha Ezra, lakini ameruhusu viwe katika mtiririko huo kwa mapenzi yake mwenyewe.

Na leo kwa Neema za Bwana tutaviangalia vitabu viwili vya Nabii mmoja, ambavyo matukio yake yalitangulia kabla ya wakati wa Ezra..Navyo ni vitabu vya YEREMIA pamoja na MAOMBOLEZO. Vitabu hivi viwili viwili vimeandikwa na mtu mmoja (Yeremia)…Tumeviruka vitabu vya hapo katikati vinavyofuata baada ya kitabu cha Ezra kama vile Nehemia, Esta, Ayubu, Zaburi, Mithali, na Ayubu, tutakuja kuvipitia hapo baadaye. Hivyo nakushauri baada ya kusoma somo hili, wewe mwenyewe chukua nafasi ya kuvipitia vitabu hivyo viwili, Na Bwana atakufunulia na mengi Zaidi ya haya, kwani hapa tunaandika kama summary tu.

Kuitwa kwa Yeremia:

Kama wengi wetu tunavyojua kuwa Yeremia Mungu alimwita tangu akiwa mdogo sana..na aliambiwa atakuwa Nabii wa Mataifa. Sasa kama ni mwanafunzi wa Biblia utagundua kuwa Huduma kubwa ya Yeremia ilikuwa ni kuwatabiria mataifa juu ya hukumu Mungu atakayoileta juu ya Mataifa yote ulimwenguni kutokana na maasi ya dunia. Ikiwemo na Taifa la Mungu (Israeli) humo humo.

Mungu alitaka kuiadhibu dunia kwa kupitia Babeli. Aliupa Ufalme wa Babeli nguvu, ambao aliutumia huo kuwa kama fimbo kwa mataifa yote duniani ikiwemo Israeli ndani yake. Babeli iliyalazimisha mataifa yote yalitumikie taifa hilo. Na Mungu aliruhusu hilo ili kuyakomesha mataifa ya dunia yanayofanya maasi..Sasa kumbuka sio kwamba Babeli lilikuwa ni Taifa takatifu hapana!.Ni Mungu tu alilichagua kama chombo chake kutimiza kusudi fulani tu!..Baada ya kumaliza kutimiza kusudi hilo, nalo pia Mungu aliliadhibu kwa maasi yake.

Hivyo Mungu akamtuma Yeremia kuyaambia mataifa hayo hatari iliyopo mbele yao..Wengi walimdharau Yeremia na kumwona Nabii wa uongo,..wengine walimwona ni kibaraka wa mfalme Nebkadneza wa Babeli…wengine walimwona kama ni kimtu tu kimejizukia kutabiri tabiri ujinga..n.k Lakini Yeremia alikuwa ni Nabii kweli wa Mungu.

Kuhubiri kwa Yeremia:

Alizunguka kwenye mataifa yote mpaka Misri kwa Farao (Soma Yeremia 25:5-29)..kumwonya lakini hawakumsikia.. Na mwisho akamalizia kwa Taifa lake Teule kulionya kuwa litakwenda Utumwani miaka 70 lisipotaka kujinyenyekeza lakini nalo pia halikusikia..Ukisoma kitabu cha Yeremia na 2Wafalme wa pili utaona ni jinsi gani Yeremia alivyosumbuliwa na Sedekia Mfalme wa Israeli.

Kutokana na wana wa Israeli kutokutii, Unabii wa Yeremia ukatimia juu yao..Wakauawa na Nebukadneza mfalme wa Babeli na wengine wakachukuliwa mateka na kwenda kukaa huko kwa miaka 70.

Siku hiyo ya maangamizi ilipofika wana wa Israeli walichukuliwa mateka mpaka Babeli…Na Nabii Yeremia ndiye alikuwa ni nabii pekee aliyeyashuhudia maangamizi hayo na uteka huo.. siku hiyo ilikuwa ni siku ya uchungu sana, maana theluthi ya watu walikufa kwa Tauni na wengine kwa njaa kutokana na kukosekana chakula wakati huo, kwani mji huo ulikuwa umehusuriwa kwa muda mrefu sana, na majeshi ya Babeli hivyo, hata chakula ndani ya mji kilikuwa ni shida, kwasababu hakukuwa na kinachoingia wala kutoka, theluthi nyingine walikufa kwa kuuawa kikatili na jeshi la Nebkadneza, wanawake na Watoto walichinjwa chinjwa kama kuku na theluthi nyingine walichukuliwa Mateka huku wamefungwa mpaka Babeli Utumwani. Mapigo hayo manne ndiyo yaliyoipata Israeli yaani NJAA, TAUNI,UPANGA na KUCHUKULIWA MATEKA.

Tunasoma hayo katika;

Ezekieli 5: 11 “Kwa sababu hiyo, kama mimi niishivyo, asema Bwana MUNGU, hakika kwa kuwa umepatia unajisi patakatifu pangu, kwa matendo yako yote niyachukiayo, na kwa machukizo yako yote, kwa sababu hiyo mimi nami nitakupunguza; wala jicho langu halitaachilia, wala sitaona huruma.

12 Theluthi yenu mtakufa kwa tauni, na kwa njaa watakomeshwa ndani yako; na theluthi yenu wataanguka kwa upanga pande zako zote; na theluthi yenu nitawatawanya kwa pepo zote, kisha nitafuta upanga nyuma yao.

13 Hivyo ndivyo ghadhabu yangu itakavyotimia, nami nitatosheleza hasira yangu juu yao, nami nitafarijika; nao watajua ya kuwa mimi, Bwana, nimenena kwa wivu wangu, nitakapokuwa nimeitimiza ghadhabu yangu juu yao”.

Na maneno hayo yalitimia kama yalivyo. Theluthi walikufa kwa njaa na tauni, theluthi nyingine kwa kuuawa kwa upanga, na theluthi nyingine kwenda Babeli. Israeli pakabakia kuwa tupu!..Na nabii Yeremia alikuwa anayashuhudia hayo.. Jambo hilo likamhuzunisha sana, maana aliwaonya sana waIsraeli wamgeukie Mungu lakini wakakataa, hivyo maangamizi hayo yalimchoma moyo sana kwani aliyashuhudia kwa macho yake yaliyokuwa yanatendeka…Ndipo kwa msukumo wa Roho akaandika kitabu cha MAOMBOLEZO. (Kitabu hichi killiandikwa na Yeremia mwenyewe)..Kuombolezea kilicholikumba Taifa teule la Mungu..

KITABU CHA MAOMBOLEZO;

Taifa ambalo hapo kwanza lilikuwa linaogopwa!..lenye utisho wa ki-Mungu..Taifa ambalo Mfalme mkuu wa dunia Sulemani alitokea, taifa ambalo Mungu wake alisifika kwa kutokushindwa na lolote,..leo hii linakwenda utumwani!!…Taifa ambalo Mungu alilitoa Misri kwa mkono Hodari na kumwaibisha Farao leo hii linarudi tena utumwani kwa aibu kuu kama hiyo!!?..Hayo kweli ni maombolezo na uchungu mkali. Ndio maana ukisoma kitabu cha Maombolezo utaona jinsi Nabii Yeremia anavyoitaja Israeli kwa kulifananisha na “binti Sayuni au mwanamke mjane”

Anasema…

Maombolezo 1:1 “Jinsi mji huu ukaavyo ukiwa, Huo uliokuwa umejaa watu! Jinsi alivyokuwa kama mjane, Yeye aliyekuwa mkuu kati ya mataifa! Binti mfalme kati ya majimbo, Jinsi alivyoshikwa shokoa! (shokoa maana yake ni kibarua wa ngazi ya chini kabisa!)

2 Hulia sana wakati wa usiku, Na machozi yake yapo mashavuni; Miongoni mwa wote waliompenda Hakuna hata mmoja amfarijiye; Rafiki zake wote wamemtenda hila, Wamekuwa adui zake”…. 5 Watesi wake wamekuwa kichwa, Adui zake hufanikiwa; Kwa kuwa Bwana amemtesa Kwa sababu ya wingi wa makosa yake; Watoto wake wadogo wamechukuliwa mateka Mbele yake huyo mtesi.

6 Naye huyo binti Sayuni Enzi yake yote imemwacha; Wakuu wake wamekuwa kama ayala Wasioona malisho; Nao wamekwenda zao hawana nguvu Mbele yake anayewafuatia.”

Maombolezo 1:16 “Mimi ninayalilia mambo hayo; Jicho langu, jicho langu linachuruzika maji; Kwa kuwa mfariji yu mbali nami, Ambaye ilimpasa kunihuisha nafsi; Watoto wangu wameachwa peke yao, Kwa sababu huyo adui ameshinda.

17 Sayuni huinyosha mikono yake; Hakuna hata mmoja wa kumfariji; Bwana ametoa amri juu ya Yakobo, Kwamba wamzungukao wawe watesi wake; Yerusalemu amekuwa kati yao Kama kitu kichafu.

18 Bwana ndiye mwenye haki; Maana nimeiasi amri yake; Sikieni, nawasihi, enyi watu wote, Mkayatazame majonzi yangu; Wasichana wangu na wavulana wangu Wamechukuliwa mateka”.

Anaendelea na kusema..

Maombolezo 2: 1 “Jinsi Bwana alivyomfunika binti Sayuni Kwa wingu katika hasira yake! Ameutupa toka mbinguni hata nchi Huo uzuri wa Israeli; Wala hakukikumbuka kiti cha miguu yake Katika siku ya hasira yake.

2 Bwana ameyameza makao yote ya Yakobo, Wala hakuona huruma; Ameziangusha ngome za binti Yuda Katika ghadhabu yake; Amezibomoa hata nchi Ameunajisi ufalme na wakuu wake.

3 Ameikata pembe yote ya Israeli Katika hasira yake kali; Ameurudisha nyuma mkono wake wa kuume Mbele ya hao adui, Naye amemteketeza Yakobo kama moto uwakao, Ulao pande zote”.

Ukiendelea kusoma mlango wa tatu pia ni maombolezo tu kwa kilichotokea juu ya Taifa la Mungu..

Maombolezo 3: 42 “Sisi tumekosa na kuasi; Wewe hukusamehe.

43 Umetufunika kwa hasira na kutufuatia; Umeua, wala hukuona huruma.

44 Umejifunika nafsi yako kwa wingu, Maombi yetu yasipite.

45 Umetufanya kuwa takataka, na vifusi Katikati ya mataifa.

46 Juu yetu adui zetu wote Wametupanulia vinywa vyao.

47 Hofu imetujilia na shimo, Ukiwa na uharibifu”.

Na Baada ya maombolezo hayo, Yeremia kwakuwa ni nabii wa Mungu na Anamjua Mungu sana. Alijua kuwa mateso hayo ni ya muda tu!. Hayatadumu milele, ni ya kitambo tu!. Ni kweli wamemwasi Mungu na Mungu kawakasirikia hata kuwauza kwa maadui zao…lakini ni kwa muda tu. Kwasababu Mungu hawezi kumtupa mtu milele. Kwa kulijua hilo akaandika maneno yafuatayo..

Maombolezo 3: 31 “Kwa kuwa BWANA HATAMTUPA MTU HATA MILELE.

32 MAANA AJAPOMHUZUNISHA ATAMREHEMU, Kwa kadiri ya wingi wa huruma zake.

33 Maana moyo wake hapendi kuwatesa wanadamu. Wala kuwahuzunisha.

34 Kuwaseta chini kwa miguu Wafungwa wote wa duniani,

35 Kuipotosha hukumu ya mtu Mbele zake Aliye juu,

36 Na kumnyima mtu haki yake, Hayo Bwana hayaridhii kabisa”.

Unaona ijapokuwa wameuzwa lakini Mungu anatoa maneno ya matumaini kuwa hatawatupa milele,.. ipo siku inakuja watafunguliwa kutoka katika utumwa wao..Na watarudi tena kuwa Taifa teule la Mungu endapo wakitubu huko walipo…

Ni nini tunajifunza hapo?

Kuudharau unabii ni kubaya sana. Hususani unabii unaokutabiria mwisho wa mambo yote. Wengi wanapenda kutabiriwa mambo mazuri tu! Lakini hawapendi kuambiwa kuwa mshahara wa dhambi ni mauti. Nabii Yeremia yeye mwenyewe hakupenda kuwatabiria watu kila siku habari za hukumu ijayo..Lakini ilimbidi afanye vile ili watu angalau wasalimike kwa maana ni kweli hukumu ilikuwa ipo karibu sana..sasa itamfaidia nini awafiche halafu aje kuona ndugu zake wanachinjika mbele ya macho yake. Ni heri awaambie wakatae wenyewe kama alivyofanya kuliko asingewaambia halafu awaone wanachinjika vile, ni heri aonekane anahukumu kuliko kutowajuza watu kinachokuja mbeleni…Nafikiri haya maombolezo aliyoyaandika hapo juu yangekuwa yenye uchungu mara elfu kama wakingekufa pasipo kujua chochote.

Huyo ni Nabii wa kweli ambaye anawaambia ukweli juu ya mwisho wao huku yeye mwenyewe akiomboleza..sio kwamba alikuwa anafurahia. Kadhalika Bwana Yesu anatuonya.. “kuna hukumu inakuja”..Hatuambii hivyo huku anafurahia..bali huku anatuombolezea kwa yatakayotukuta tusipotubu. Mshahara wa nguo fupi uvaazo na make-up uwekazo usoni ni jehanamu!! huo ndio ukweli usisikilize watu wanaokudanganya huko na huko wanaojiita ni watu wa Mungu..mshahara wa uzinzi na uasherati ni jehanamu, mshahara wa ufisadi, na kutokusamehe ni jehanamu. Mshahara wa kuishi nje ya Kristo vile vile ni jehanamu.

wokovu ni sasa:

Kama hujampa Kristo Maisha yako. Haijalishi unatenda haki kiasi gani upo hatarini sana. Hivyo nakushauri ufanye uamuzi sahihi leo, kwasababu huijui Kesho.

Bwana akubariki sana.

 

Ikiwa utapenda kupitia uchambuzi wa vitabu vilivyotangulia bofya hapa >>> VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 6

Na kwa mwendelezo bofya hapa >> VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 8 (Kitabu cha Ezekieli)

Kwa maombezi/ Ushauri/ Ratiba za Ibada/Maswali/ Whatsapp/ Piga namba hizi: +255693036618/ +255789001312

Maran atha!

Mada Nyinginezo:

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1

Yeshuruni ni nani katika biblia?

KANUNI RAHISI YA KUFANIKIWA.

JINSI YA KUJIWEKA KARIBU NA MUNGU.

Rudi Nyumbani:

Print this post