Title December 2019

JE TATIZO LA KULA KUCHA NI ISHARA YA KUWA NA MAPEPO?

Utaachaje kula kucha?..dawa ya kuacha kula kucha ni ipi?..Je ni kweli tatizo la kula kucha haisababishwi na mapepo?..Je mtu atahukumiwa kwa kosa la kula kucha?..Karibu tujifunze pamoja kwa kuongeza maarifa juu  ya mambo haya ili yaweze kutusaidia kuishi kwa amani na furaha..

Tatizo la kula kucha limekuwa limewakabili watu wengi..Na endapo ikitokea mtu anakula kucha mpaka ukubwani na anapojaribu kuacha inashindikana..basi ni rahisi kujihisi kuwa na kasoro fulani,.. Na wakati mwingine kujihisi kwamba kuna roho fulani inayomsukuma kufanya hivyo..na hivyo kumpotezea ujasiri.

Kula kucha ni kitendo ambacho mtu anakuwa katika hali fulani ya kiakili labda mawazo, au katika hali ya kutafakari kwa kina, au katika hali ya kuona aibu, au katika hali ya upweke sana, au furaha sana, au huzuni sana n.k inatofautiana kati ya mtu na mtu….ambapo mtu akiwa katika hali hiyo anajikuta vidole vimefika mdomoni pasipo hata kujijua..Na ufahamu unaporudi anajikuta tayari kashapunguza kiwango fulani cha kucha au nyama pembezoni mwa kucha. Atajaribu kuacha lakini kesho itajirudia hiyo hali…

Sasa swali ni je! ni kweli ni roho za mapepo ndio zinahusika na hiyo hali au ni Tabia tu ya mtu!.

Kwanza ni muhimu kufahamu utendaji kazi wa roho za mapepo…ndipo turudi kuamua kama ulaji kucha ni mapepo ndani ya mtu au la!..

Mapepo yanapomwingia mtu kazi ya kwanza yanayofanya ni kumfanya yule mtu awe mwovu…Mapepo yakiwa ndani ya mtu yanamfanya asipende kusoma Neno,..yanamfanya atamani kutenda dhambi, yanafanya kuwa mwasherati,..mtazamaji pornography, mtukanaji, mlawiti..yanamfanya avae vibaya (Nusu uchi)..Yanamfanya mtu anaposikia habari za injili anachukia..

Na mapepo yanampeleka mtu siku zote mbali na kweli ya Biblia…yanampeleka mtu mahali pasipo kuwa na MAJI YA UZIMA (Jangwani) Soma Luka 11:24..Na mahali ambapo watu wamekufa kiroho kama disko, bar, kwenye kamari, kwenye vikao vya usengenyaji, penye mikusanyiko ya watu wenye mizaa n.k sehemu hizo katika roho ni makaburini…Bar ni makaburi ya kiroho, disko ni makaburini,  kadhalika na madanguro na sehemu nyingine zote za kiulimwengu..

Marko 5:1 “Wakafika ng’ambo ya bahari mpaka nchi ya Wagerasi.

2 Na alipokwisha kushuka chomboni, mara alikutana na mtu, ambaye ametoka makaburini, mwenye pepo mchafu;”

Kadhalika mapepo yakiwa ndani ya mtu yanaweza kumsababishia ugonjwa fulani au udhaifu fulani,..Udhaifu huo unaweza ukawa ulemavu wa viungo au ulemavu wa kiakili, au kiufahamu… kama wa kushindwa kujizuia kufanya kitu fulani.

Ulemavu wa kiufahamu inahusisha mtu kula vitu visivyoliwa, ufahamu wa huyo mtu unampeleka kula vitu ambavyo sio kawaida mwanadamu kuvila…kwamfano mtu utakuta anatamani kula chuma, mwingine anakula sindano, mwingine anakula glasi, mwingine makaratasi, mwingine nyama mbichi unakuta hajisikii kabisa hamu ya kula nyama iliyoiva…mwingine mchanga, n.k mara nyingi watu wa namna hii wanakuwa na roho fulani inayowasukuma wao kufanya hivyo hata kama hawajijui..na ndio roho hizo hizo zinazowasukuma watu kupata hamu ya kuvuta sigara, bangi na hata kunywa pombe…Hivyo suluhisho ni kufunguliwa…ambapo tutaona namna ya kufunguliwa na hizo roho mwishoni  mwa somo hili..

Sasa kuna matatizo mengine ambayo hayasababishwi na mapepo yoyote bali tabia au hali fulani ya kimaumbile..

Kwamfano wanawake wajawazito  kutamani kula udongo (ingawa sio wote) lakini wengi wao,..sisemi udongo gunia zima..hapana bali ile hamu ya kula kiwango kidogo cha udongo..hiyo haisababishwi na mapepo bali maumbile..Mwanamke akishajifungua hiyo hali inakwisha…

Kadhalika hali ya kuvutiwa kula udongo wakati mvua kunyesha…Harufu ile ya udongo  inawavutia maelfu ya watu na hata wakati mwingine watu wanafikia hatua ya kulamba kidogo udongo..Hiyo pia haisababishwi na mapepo bali maumbile ya miili yetu jinsi yalivyoumbwa.

Pia hali ya kupenda harufu ya petrol au mafuta ya taa na kutamani kuyala..Hiyo pia haisababishwi na mapepo bali maumbile..

Lakini mambo yote haya..ni kwa kiasi, yakizidi sana kufikia kumfanya mtu anywe lita za petroli au kula magunia kadhaa ya udongo hilo ni tatizo lingine ambalo linaweza kusababishwa na roho za mapepo..hivyo tendo la kiroho linahitajika haraka kuliondoa tatizo hilo.

Sasa tukirudi katika suala la kula kucha..

Asilimia kubwa ya watu wanaokula kucha ni tatizo la kiufahamu, ambalo chanzo chake sio mapepo…Wengi wanachukua tabia hiyo kutoka aidha kwa wazazi au ndugu zao au  marafiki pindi wanapokuwa wadogo na kuendelea nayo hivyo hivyo mpaka kufikia hatua ya kuwa sehemu ya maisha yao.

Tabia ya kula kucha haina tofauti sana na tabia ya kula kifuniko cha kalamu au kulamba lamba lips, au kung’ata ng’ata meno…Ni tabia ambazo mtu alipokuwa aidha mtoto au mtu mzima, alimwona mtu fulani akifanya na hivyo yeye naye akajikuta anaiga pasipo kujitambua na hivyo kuwa ni tabia yake..

Hivyo tatizo la kula kucha sio mapepo..Hautasimamishwa kwenye kiti cha hukumu kwa kosa la kula kucha…

Kumbuka; Tunapozungumzia kula kucha hatumaanishi kula vidole mpaka vitoke damu zitoke kama bomba, au kula nyama ya vidole mpaka vidole vichuruzike damu kabisa..hapana. Hali kama hiyo ikitokea basi kuna roho nyingine ya adui inahusika hapo…Lakini kama ni kwa kiwango cha kawaida kama cha watu wengine unaowafahamu hilo halisababishwi na mapepo..

Ifuatayo ni dawa ya kuacha kula kucha.

Utaachaje kula kucha? (Zingatia mambo makuu mawili yafuatayo).

KWANZA: Ni kumkabidhi Yesu maisha. Ukitaka kuondoa tabia yoyote katika maisha yako…Kwa nguvu zako huwezi, ni lazima uhitaji nguvu za ziada…Wewe mwenyewe umeona!..Umepambana sana lakini bado…Hiyo ni kuonesha kwamba sisi wanadamu kwa nguvu zetu hatuwezi kufanya lolote…Hivyo mkabidhi Yesu Kristo maisha yako ili kwamba akusafishe na kukufanya mtu kamili…Tubu dhambi zako zote kwa kumaanisha kuziacha, tubia uasherati kama ulikuwa mwasherati, rushwa, wizi, ulevi, uvutaji sigara, rushwa, ukahaba, anasa n.k..Na ukishaacha..Hakikisha unakwenda kutafuta ubatizo sahihi kama hujabatizwa..Ubatizo sahihi ni wa kuzama mwili wote kwenye maji mengi (Yohana 3:23) na kwa jina la Yesu Kristo (kulingana na Matendo 2:38)…Na baada ya hapo Roho Mtakatifu ataingia ndani yako na kukusaidia kufanya yale ambayo ulikuwa huwezi kufanya.

Usiokoke tu kwasababu unataka kuacha kula kucha..Hapana bali okoka kwasababu unahitaji kubadilishwa maisha yako na Bwana Yesu na unataka kuwa mkamilifu kama Mungu.

PILI: Baada ya kuokoka…

Mwambie Bwana Yesu katika sala..wala usifunge wala usiingie kwenye maombi ya mkesha…Mwambie tu..“Bwana kuanzia leo sitaki kula kucha nisaidie”..Basi hivyo tu!..Ukishafanya hivyo..Hatua inayofuata ni ya muhimu sana….NENDA KANUNUE NAIL-cutter au Nail-clipper..kama hufahamu nail cutter ni nini  Tazama picha chini..

Unapoacha kula kucha, kucha zako zitaanza kukua na hivyo usipozipunguza kwa kifaa maalumu ni rahisi kushawishika kurudia kuzipugnuza kwa meno..Hivyo ili kuonyesha imani yako ipo katika matendo kanunue kifaa hicho, au kingine chochote kile kitakachotumika kupunguza kucha zako zinapokua..Usiwe na hofu wakati mwingine unaweza ukajisahau na kufikisha vidole mdomoni…Lakini kabla hujaanza kuzitafuna Roho atakusaidia kukukumbusha..hivyo unapokumbushwa kubali kutii… na hiyo hali hatimaye itaisha kabisa…haijalishi umekaa nayo kwa miaka mingapi…Itaisha!..Zipo shuhuda za waliomaliza tatizo kwa msaada wa Mungu, na kwako pia litaisha kama utapenda liishe…Na hata kama tatizo lako linasababishwa na roho za fulani za mapepo basi hatua hizi mbili ni dawa tosha ya kuziondoa hizo roho ndani yako..Hauhitaji kuombewa..Wewe fuata hizo hatua hapo juu na tatizo lako litaisha.

Bwana akuabariki.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali share na wengine nao wanufaike.


Mada Nyinginezo:

Ubatizo wa moto ni upi?

JE! MTUMISHI KUTOKUWA NA FEDHA NI ISHARA KUWA KUNA TATIZO KATIKA IMANI YAKE?

LITANIA YA BIKIRA MARIA JE! NI SALA YA KIMAANDIKO?

NI KIPI MUNGU ANACHOKITAZAMA ZAIDI, MOYO AU MWILI?

Rudi Nyumbani:

Print this post

USILETE UJIRA WA KAHABA, NYUMBANI KWA MUNGU.

Usilete ujira wa kahaba, nyumbani kwa Mungu.


Shalom, Jina la Bwana Yesu Kristo libarikiwe. Karibu tujifunze Maandiko..

Kuna mambo ambayo unaweza kuyasema ukadhani hayapo kabisa kwenye biblia..Lakini yapo!…Na kuna mambo machache yanayopuuziwa na wengi..lakini ni ya kuzingatia sana tunapomkaribia Mungu..Kitu kimoja ambacho wengi hawajui ni kwamba Mungu wetu tunayemwabudu hachangamani na uchafu…Mtu yeyote Yule aliye mchafu awe mchungaji, au mwalimu, au mwinjisti, au nabii, au muumini wa kawaida..

Mungu hawezi kutembea naye akiwa katika hali ya uchafu, hastahili hata kushiriki meza ya Bwana wala kumtolea Mungu sadaka!!…wala maombi yake hayasikilizwi wala dua zake hazimfikii…Kwa ufupi mtu huyo tayari ameshafarakana na Mungu na ni Adui wa Mungu (Soma Isaya 59:1-5)..Na endapo akilazimisha kumfanyia Mungu ibada katika hali hiyo huku anajijua kuwa yeye ni mchafu na hataki kubadilika…Mtu huyo anajitafutia laana badala ya Baraka…

Asilimia kubwa ya wahubiri wanalijua hilo, isipokuwa hawapendi kuwaambia watu ukweli..kutokana na kwamba mapato yao kanisani yatashuka…watawezaje kumwambia kahaba asitoe kwanza sadaka zake mpaka atakapomgeukia Mungu kwa moyo wake wote kwanza, kwa kuacha uasherati wake??..Hawawezi kufanya hivyo kwasababu ndio ulaji wao upo hapo! akimwambia hivyo anaogopa atakasirika na hivyo kuondoka…Lakini matokeo ya kutokufanya hivyo ni kumtafutia laana Yule anayetoa sadaka hizo haramu mbele za Mungu…

Leo tutajifunza mistari kadhaa ihusuyo habari hizo..Ambapo tukishajifunza itatusaidia kudhamiria kuokoka kwanza kwa kumaanisha kuziacha dhambi ndipo tumkaribie Mungu.

Kwanza kabisa kama hujaokoka, na unajua kabisa unastahili kuokoka lakini hutaki na unaendelea kuwa vuguvugu..Bado unaendelea kufanya kazi yako ya kujiuza kisirisiri, bado unaendelea kula rushwa kisirisiri, unaendelea kutapeli kisirisiri..Na Jumapili unakwenda kanisani kuabudu na kutoa sadaka yako kwa Mungu..NATAKA NIKUAMBIE UNAFANYA DHAMBI!!..Inawezekana hujawahi kabisa kuhubiriwa hivi kanisani kwako..lakini leo hii sikia Neno la Mungu…Acha kabisa usimtolee Mungu, sadaka hizo kwasababu ni unamdharau..unajitafutia laana badala ya Baraka…

Biblia inasema…

Kumbukumbu 23: 18 “Usilete ujira wa kahaba, wala mshahara wa mbwa, katika nyumba ya Bwana, Mungu wako, kwa ajili ya nadhiri yo yote; kwani haya ni machukizo kwa Bwana, Mungu wako, yote mawili”.

Lengo la Mungu kutuagiza kumtolea, sio kwamba anashida ya Hela,.au anatafuta kuwatajirisha watumishi wake…hapana hilo sio lengo lake..Yeye ana njia zaidi ya milioni moja ya kuwalisha watumishi wake wa kweli, tofauti na hata hiyo ya madhabahuni…Lengo lake kuu ni kutuumbia sisi moyo wa utoaji ndani yetu kama yeye alivyo mtoaji..kwamba hata ikitokea yupo mtu mwenye uhitaji katokea mbele yetu tuwe na moyo wa kutoa sehemu ya vitu vyetu na muda wetu kumsaidia…jambo ambalo linampendeza na lituletealo Baraka kutoka kwake…

Anataka tuwe wakamilifu na watakatifu kama yeye alivyo…Lakini unapokwenda kanisani na lengo la kwamba Mungu anahitaji fedha kutoka kwako au unakwenda kumpa mchungaji fedha,..Na hivyo fedha yoyote tu itakayokuja mkononi mwako hata ya rushwa ni ruksa kuipeleka nyumbani kwa Mungu…Kanisa sio benki ya madanguro wala mafisadi kwamba mafedha yote haramu ndiyo yanakwenda kuhifadhiwa huko…..Ni kujitafutia laana badala ya Baraka.

Soma tena mstari huu..

Mhubiri 5: 1 “Jitunze mguu wako uendapo nyumbani kwa Mungu; Maana ni heri kukaribia ili usikie, Kuliko kutoa kafara ya wapumbavu; Ambao hawajui kuwa wafanya mabaya”.

Unaona!..Biblia inasema ni heri ungeenda tu kusikiliza kuliko kwenda na kutoka kafara za wapumbavu ambao hawajui kuwa wanafanya dhambi…Usitie mkono wako kushiriki shughuli zozote za kanisa kama unajijua huna mpango na Mungu…Unafanya dhambi na utajitafutia laana badala ya Baraka.. Kadhalika usishiriki meza ya Bwana kama hujaokoka kikweli kweli na kupokea Roho Mtakatifu,.Kama ni mzinzi na mwasherati..pengine hukuhubiriwa kanisani, kwasababu Mhubiri wako pengine aliogopa angekwambia ukweli kwamba unatenda dhambi ungekwazika na kuhama kanisa na yeye akakosa mapato..lakini leo lisikie Neno la Mungu usiisogelee madhabahu kama hujaamua kumgeukia Yesu Kristo kikweli kweli…Usiule mwili wa Kristo, wala damu yake isivyopaswa kwasababu utajitafutia laana badala ya Baraka…

Usilete ujira wa kahaba, nyumbani kwa Mungu.

Soma…

1Wakorintho 11:27 “Basi kila aulaye mkate huo, au kukinywea kikombe hicho cha Bwana isivyostahili, atakuwa amejipatia hatia ya mwili na damu ya Bwana.

28 Lakini mtu ajihoji mwenyewe, na hivyo aule mkate, na kukinywea kikombe.

29 Maana alaye na kunywa, hula na kunywa hukumu ya nafsi yake, kwa kutokuupambanua ule mwili.

30 Kwa sababu hiyo wako wengi kwenu walio hawawezi na dhaifu, na watu kadha wa kadha wamelala. Lakini kama tungejipambanua nafsi zetu tusingehukumiwa”

Yuda hakujipambanua vizuri..akaenda kushiriki meza ya Bwana huku moyoni mwake kulikuwa na mawazo ya kumsaliti Bwana Yesu..kilichotokea ni shetani kumwingia saa hiyohiyo baada ya kupokea tonge na matokeo yake yaliishia ni kifo kasome Yohana 13:26-27 (Tonge linalozungumziwa hapo sio tonge la ugali bali mkate wa Bwana). Wakati wengine wamepokea Baraka kwa kushiriki ile meza ya Bwana, Yuda yeye kapokea laana kwa kushiriki kitendo hicho hicho…

Kadhalika Kabla ya kwenda kupokea ule mkate wala kupokea kile kikombe jiulize mara mbili mbili je!..umeokoka kweli kweli?..Kama hujaokoka na unakwenda kushiriki basi umeenda kujizolea laana badala ya Baraka.

Kadhalika kama Hujaamua kuacha dhambi na kugeuka na kukusudia kumfuata Yesu Kristo kwa moyo wako wote,..halafu unakwenda kubatizwa na huku moyoni mwako unajua kabisa hujaamua kuacha uasherati, ulevi au sigara au uchafu uliokuwa unaufanya..na hivyo ukaenda kuingia kwenye yale maji na kubatizwa nataka nikuambie utakuwa umekwenda kujitafutia laana badala ya Baraka..Kama hujaamua kumguekia Yesu kwa dhati..usiende kubatizwa kabisa..subiri mpaka wakati utakapoamua kama hiyo nafasi itakuwepo..

Usishiriki jambo lolote la kiimani kama hujaamua kweli kuwa upande wa Mungu.

Na mambo mengine yote hahusuyo madhabahu usiyafanye kama huna uhusiano wowote na Mungu…hata usimfuate Mtumishi wa Mungu kumwomba akutabirie wala kukuombea kama mwenyewe unajua moyoni huna mpango na msalaba..ni hatari kubwa sana kufanya hivyo nenda kasome kitabu cha (Ezekieli 14:3-4) na kilichomtokea mke wa mfalme Yeroboamu, uone ni nini kitamtokea mtu Yule ambaye kwa makusudi hana mpango na Mungu na bado anataka kwenda kuuliza kwa Mungu..

Usilete ujira wa kahaba, nyumbani kwa Mungu.

hata ya kuhubiri madhabahuni ni hatari,..kama hujatakaswa kwa Damu ya Yesu, usiisogelee kabisa madhabahu…

Kama ulikuwa unafanya hivyo na hujui kwamba ulikuwa unakosea..Ulikuwa hujui kwamba sadaka yako ya ukahaba ni machukizo mbele za Mungu..na sasa unataka kutubu na kujitakasa ili sadaka zako zikubaliwe mbele za Mungu..Mlango upo wazi leo..unachopaswa kufanya ni kudhamiria kwanza kuacha dhambi na kukiri kwamba ulikuwa mkosaji..kisha unatubu na kumwambia Bwana akusamehe na kukuosha tena kuwa mpya…

Ukifanya hivyo kwa kumaanisha kabisa kutoka moyoni, basi Bwana YESU atakuwa ameshakusamehe..Hivyo Baada ya hapo nenda kabatizwa kama hujabatizwa katika ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa Jina la Yesu, na kisha Roho Mtakatifu ataingia ndani yako na kukutia muhuri kuwa wake milele..

Na mwisho ni kusudia kuishi maisha ya usafi na utakatifu kuanzia huo wakati na kuendelea kulingana na maagizo ya Mungu..Hapo sadaka zako zitampendeza Mungu, na sala zako kwake zitakuwa kama manukato mazuri mbele zake, Maombi yako yatasikiwa, dua zako zitasikilizwa, sifa zako zitampendeza Mungu, kwasababu upo chini ya damu ya Emanueli, YESU KRISTO..

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

 

Bwana akubariki.

Mada Nyinginezo:

Je! ni vema kwa mkristo kwenda hospitali au kutumia miti shamba anapougua?

JISHUSHE ILI MUNGU AKUHUDUMIE.

KAMA MUNGU ANABORESHA KAZI ZAKE, KWANINI WEWE USIBORESHE ZA KWAKO?.

NI KIPI MUNGU ANACHOKITAZAMA ZAIDI, MOYO AU MWILI?

Rudi Nyumbani:

Print this post

VIFO VYA MITUME WA YESU/ JINSI MITUME WALIVYOKUFA.

Vifo vya mitume wa Yesu/ jinsi mitume walivyokufa.


Mtume pekee ambaye biblia inarekodi mauaji yake jinsi yalivyokuwa ni mtume Yakobo ndugu yake  mtume Yohana. Huyu biblia inasema katika Matendo 12:1-2, kuwa Mfalme Herode alimuua kwa Upanga, alikatwa kichwa. Lakini kwa habari ya mitume wengine waliosalia biblia haijarekodi jambo lolote kuhusu vifo vyao.

Hivyo ili kupata taarifa zihusuzo huduma zao na vifo vyao ilipasa watu warejee katika hadithi ambazo zinaamika ziliandikwa na watu ambao walikuwa karibu sana na mitume, au walioshuhudia vifo vyao. Japo habari hizo hatuwezi kuzithibitisha kuwa zina usahihi wa asilimia mia, lakini kwa sehemu kubwa zimethitishwa kuwa kweli, kulingana na kupatana kwa maneno ya mashuhuda.

Mathayo:

Mathayo alijeruhiwa vibaya na upanga alipokuwa anahubiri katika nchi ya Ethiopia kaskazini mwa Afrika. Na baadaye kukumbwa na mauti kutokana na pigo la jeraha hilo..

Mtume Yohana:

Wakati wa wimbi kubwa la dhiki za wakristo likishamiri huko  Rumi , walimkamata Mtume Yohana na kumzamisha katika karai la mafuta yaliyotokota ili afe, lakini aliokoka kimiujiza. Wakamchukua na kumpeleka  katika kisiwa cha Patmo, na huko ndipo alipoandika kitabu cha Ufunuo. Lakini baadaye aliachiwa huru na kurudi Asia ndogo ili kupeleka barua zile kwa yale makanisa saba huko Asia ndogo. Ambayo kwa leo inajulikana kama nchi ya Uturuki. Huyu ndiye mtume pekee aliyekufa kifo cha Amani katika uzee.

Mtume Petro:

Mtume Petro aliuawa huko Rumi, inasemekana, walimkamata na kusulibisha kichwa chini miguu juu, kutimiza unabii Bwana Yesu aliompa katika:

Yohana 21;17  Akamwambia mara ya tatu, Simoni wa Yohana, wanipenda? Petro alihuzunika kwa vile alivyomwambia mara ya tatu, Wanipenda? Akamwambia, Bwana, wewe wajua yote; wewe umetambua ya kuwa nakupenda. Yesu akamwambia, Lisha kondoo zangu.

18  Akasema, Amin, amin, nakuambia, Wakati ulipokuwa kijana, ulikuwa ukijifunga mwenyewe na kwenda utakako; lakini utakapokuwa mzee, utainyosha mikono yako, na mwingine atakufunga na kukuchukua usikotaka.

19  Akasema neno hilo kwa kuonyesha ni kwa mauti gani atakayomtukuza Mungu. Naye akiisha kusema hayo akamwambia, Nifuate.

Hivyo ndivyo vifo vya mitume wa Yesu vilivyokuwa.

Batholomayo au Nathanaeli:

Alikuwa ni mmishionari huko Asia, aliuliwa kwa kuchapwa na mijeli mikali mpaka kufa. Unaweza ukaona jinsi mitume walivyokufa kikatili.

Andrea:

Walimkamata na kumfunga katika msalaba uliolazwa kama alama ya “X”. Kisha wakamwacha akiwa amefungwa kwa muda mrefu ili kumwongezea mateso ya kufa kwake,  huko ukigiriki. Na Wale waliokuwa wakimfuata mfutua walisema walimsikia akisema maneno haya;

Nukuu: ”Kwa muda mrefu, nimekuwa nikiingojea kwa hamu saa hii, msalaba umekuwa wakfu sikuzote kwa mwili wa Kristo kutundikwa juu yake”.

Aliendelea kuhubiri injili mbele ya wale watesi wake akiwa pale msalabani kwa siku mbili, mpaka mauti ilipomkuta.

Thomaso:

Alipigwa mkuki  katika moja ya ziara zake za kuhubiri injili na kupanda makanisa kule India.

Filipo:

Aliuawa kwa kusulibiwa alipokuwa akiitaabikia Injili huko kaskazini mwa Asia ndogo,.Alikamatwa kwanza na kutupwa gerezani, kisha baadaye wakaja kumsulubisha. Mwaka 54 W.W

Thadeo/Yuda:

Aliuawa kwa kusulibiwa mwaka 72 W.W huko Eddessa.

Simoni, Zelote:

Alihubiri injili Mauritania, na baadaye Uingereza ambapo huko ndipo naye alipokuja kusulibiwa.

Mathia:

Huyu ndiyo yule mtume aliyechukua nafasi ya Yuda aliyemsaliti Yesu. Historia inarekodi alipigwa naye kwa mawe na mwishowe kukatwa kichwa.

Yuda Iskariote:

Huyu alijinyonga baada ya kupata maumivu makali ya kumsaliti Yesu kwa vile vipande 30 vya fedha.

Mtume Paulo:

Paulo ambaye hakuwa miongoni mwa wale mitume 12, Aliteswa na jemedari wa Kirumi Nero, na baadaye akaja kukatwa kichwa.

Mitume wengine kama vile, Luka alitundikwa juu ya mti wa mizeituni kutokana na msimamo wake na Imani yake thabiti kwa Kristo..N.k. wapo mitume wengine pia waliouwa kwa njia mbalimbali wameandikwa katika vitabu vya historia za wakristo ukipenda unaweza kusoma mwenyewe kitabu kinachoitwa FOXES BOOK OF MARTYRS.. Hivyo ndivyo vifo vya mitume wa yesu/ jinsi mitume walivyokufa.

Lakini tunajifunza Nini?

Biblia inasema;

Waebrania 12:1 “Basi na sisi pia, kwa kuwa tunazungukwa na wingu kubwa la mashahidi namna hii, na tuweke kando kila mzigo mzito, na dhambi ile ituzingayo kwa upesi; na tupige mbio kwa saburi katika yale mashindano yaliyowekwa mbele yetu”

Wingu kubwa la mashahidi linatuzunguka mimi na wewe. Watu waliokuwa tayari kufa lakini wasiiache Imani. Kwasababu walikuwa wanajua thawabu iliyowekwa mbele yao ni kubwa kiasi gani. Vilevile walikuwa anajua hukumu itakayowapata kama wakiikana Imani ni kubwa kiasi gani. 

Je! Sisi (mimi na wewe) tutawezaje kupona tusipouthamini wokovu mkuu namna hii?.

Ukiwa bado upo nje ya Kristo, kumbuka kuwa mlango wa neema hautakuwa wazi siku zote.  Tubu leo umgeukie muumba wako. Unachotakiwa kufanya Hapo ulipo chukua muda mchache piga magoti. Kisha anza  wewe mwenyewe mweleze Mungu makosa yako yote. Na kwamba unahitaji msamaha.  unahitaji msaada kutoka kwake kukusaidia kuushinda ulimwengu.

Hivyo Ikiwa utatubu kwa kumaanisha kutoka moyoni mwako. Basi ujue kuwa Mungu yupo hapo kukusikia. Na  atakusamehe dhambi zako zote. Na kukuosha kwa damu ya mwanawe YESU KRISTO. Na Amani ya ajabu itaufunika moyo wako kuanzia huo wakati.

Bila kupoteza muda. Nenda katafute kanisa la Kiroho.Ukabatizwe katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi. Na kwa jina la Yesu Kristo sawasawa na Matendo 2:38. Na Mungu mwenyewe atakumwagia kipawa chake cha Roho Mtakatifu kukusaidia siku zote. Fanya hivyo sasa na Mungu atakusaidia.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Ubarikiwe.

Mada Nyinginezo:

TUSIPOUTHAMINI WOKOVU TUTAPATAJE KUPONA?

https://wingulamashahidi.org/2019/09/01/bwana-alimaanisha-nini-aliposema-mtu-akija-kwangu-naye-hamchukii-baba-yake-hawezi-kuwa-mwanafunzi-wangu/

UNYAKUO.

UWE MWAMINIFU HATA KUFA.

UWE MWAMINIFU HATA KUFA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

MTINI, WENYE MAJANI.

Mtini, wenye majani ni upi?

Jina kuu la mwokozi wetu Yesu Kristo libarikiwe. Karibu tujifunze Neno la Mungu, Na leo tutajifunza somo lenye kichwa kinachosema “MTINI, WENYE MAJANI”..Unaweza usielewe kichwa hichi kina maana gani lakini twende pamoja mpaka mwisho naamini lipo jambo kubwa utajifunza.

Tunaona siku moja kabla Bwana Yesu kwenda kukaa na wanafunzi wake katika mlima wa mizetuni ili kuwaeleza habari za siku za mwisho, kuna jambo la kustaajabisha kidogo alilifanya mbele ya macho yako kwa makusudi kabisa..Na alifanya hivyo ili kuja kuwafundisha somo Fulani kesho yake..Na jambo lenyewe ni lile la “kuulaani mtini”

Akiwa anatoka Bethani asubuhi ili aende Yerusalemu hekaluni kufundisha alikutana na mtini njiani,(Mtini ni mti unaotoa matunda ya Tini) Embu tusome alichokifanya:..

Marko 11:12 “Hata asubuhi yake walipotoka Bethania aliona njaa.

13 Akaona kwa mbali mtini wenye majani, akaenda ili labda aone kitu juu yake; na alipoufikilia hakuona kitu ila majani; maana si wakati wa tini.

14 Akajibu, akauambia, Tangu leo hata milele mtu asile matunda kwako. Wanafunzi wake wakasikia”.

Mtini ni nini.

Mtini ni mti unaozaa matunda yanayoitwa TINI. Mti huu unastawi sana maeneo ya mashariki ya kati.

Sasa ukisoma juu juu unaweza kuona kama vile Bwana Yesu alikuwa hajui kuwa ule sio wakati wa TINI,.. na ndio maana akaulaani ule mtini kimakosa alipokosa matunda juu yake..Lakini alilifahamu hilo vizuri tutakuja kuona ni kwa namna gani hapo mbeleni kwa jinsi tunavyozidi kusoma. Lakini Kinyume chake alifanya vile kwa makusudi ili kuja kuwafundisha wanafunzi wake somo.. ambalo sisi watu kizazi hichi cha siku za mwisho ndio tunalolielewa vizuri..

Tukirudi kwenye ile Mathayo 24 yote, Bwana Yesu sasa akiwa na mitume wake pale katika Mlima wa mizeituni alianza kwa kuwaeleza dalili kuu za siku za mwisho,.. kwamba kutatokea manabii wa uongo na makristo wa uongo, kutakuwa na vita na habari za matetesi ya vita,kutaongezeka maasi, upendo wa wengi utapoa, kutasimama chukizo la uharibifu, upendo wa wengi utapoa, habari njema ya ufalme itahubiriwa katika mataifa yote n.k.

Na karibu na pale mwisho kabisa akawaambia maneno haya kwa kuwakumbusha kilichotokea nyuma:

Mathayo 24:32 “Basi kwa mtini jifunzeni mfano; tawi lake likiisha kuchipuka na kuchanua majani, mwatambua ya kuwa wakati wa mavuno u karibu;

33 nanyi kadhalika, myaonapo hayo yote, tambueni ya kuwa yu karibu, milangoni.

34 Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia.

35 Mbingu na nchi zitapita; lakini maneno yangu hayatapita kamwe”.

Sasa embu tafakari vizuri tena kwa ukaribu pale anaposema, “tawi lake likiisha kuchipuka na kuchanua majani, mwatambua ya kuwa wakati wa mavuno u karibu;”…Kumbe alijua mtini unapofikia hatua ya kuchipua, na matawi yake kuonekana basi wakati wake wa mavuno unakuwa upo karibu sana…Kumbe alilitambua hilo hata kwa ule mtini wa kwanza alioulaani, kwasababu ule ulikuwa katika hatua hiyo hiyo ya majani, lakini aliulaani usifikie hatua ya kufikia mavuno kwa haraka,, bali wa muda mrefu sana mbeleni alioufananisha na milele..

Inafunua nini?

Hii dunia ungekuta imeshakwisha tangu zamani za mitume, lakini Bwana YESU aliuvuta muda wa mavuno mbele ili zile dalili za mwisho wa dunia zisionekane kwa kipindi kile walichokuwa wanaishi…aliyakawiisha mavuno kwa mfano wa ule mtini alivyoukawiisha.

Kwasababu kumbuka MTINI huwa unapitia hatua kuu tatu,.. ya kwanza kupukutisha majani yake yote, ya pili ni kuchipua majani, na ya tatu ni kuzaa matunda…Sasa ile hatua ya kupukitisha, huwa unapukutisha majani yake kweli kweli na kuwa kama kijiti kikavu kilichonyauka… soma..

Ufunuo 6:12 “Nami nikaona, alipoifungua muhuri ya sita, palikuwa na tetemeko kuu la nchi; jua likawa jeusi kama gunia la singa, mwezi wote ukawa kama damu,

13 na nyota zikaanguka juu ya nchi kama vile mtini upukutishavyo mapooza yake, utikiswapo na upepo mwingi”.

Unaona hapo? Biblia inatoa picha jinsi nyota za mbinguni zitakavyoanguka katika siku za mwisho mfano wa mtini unavyopukutisha mapooza (majani makavu) yake.

Sasa kwasababu Bwana Yesu aliukawiisha wakati wa mavuno ndio tunaweza kuona tangu kipindi kile cha mitume hadi zaidi ya miaka elfu mbeleni,..hakukuwa na dalili za wazi zinazothibitisha kuwa mwisho upo karibu, kwa yale aliyoyazungumza katika Mathayo 24 kwamba manabii wa uongo watatokea, taifa kuondoka kwenda kupigana na taifa hayo hayakuwepo,… lakini tunaona kuanzia karne ya 20 yaani kuanzia mwaka 1900, mambo hayo yalianza kuonekana kwa kasi, vita kuu mbili za dunia zimepiganwa kwa mpigo ndani yah ii karne.., magonjwa ya kutisha ambayo hayakuwepo enzi za nyuma, yameonekana kwa kasi kuanzia karne ya 20, magonjwa ya ajabu yamezuka na bado yanaendelea kuzuka, kansa, ukimwi, ebola, zika, n.k…

Dalili zote zimetia:

Na dalili zile alizozingumzia pale zimeendelea kutimia kwa kasi, hadi sasa, mambo yote yameshatimia hususani katika hii karne ya 21 tuliyopo sasahivi.. karibu yote yameshatimia..

Hapo ndipo tunapojua sasa, wakati wa mavuno umeshafika..Ule mtini wa mwisho wa dunia umeshafikia hatua ya mavuno yake, matawi yake tunayaona…Wimbi kubwa la manabii wa uongo tunaloliona leo hii ungemweleza mtu wa mwaka wa 1980, angekushangaa na kusema hicho kitu hakiwezekani,.. lakini tazama hali ilivyo sasa, sodoma iliyopo sasa hivi duniani, ni zaidi ya ile ya Gomora..pornography mitandaoni, watu wanafanya uasherati na wanyama, simu za mikononi zimekuwa shimo refu la kuelekezea watu kuzimu n.k..Hii yote ni kutuonyesha kuwa Mtini umeshachipua..

Sasa Bwana Yesu aliwaambia wanafunzi wake..mnyaonapo hayo CHANGAMKENI, mkaviinue vichwa vyenu, kwa kuwa ukombozi wenu umekaribia.”..(Luka 21:28)

Unyakuo wakati wowote utapita. Wale waliookolewa wanapaswa wafurahie kwasababu siku yoyote tutakuwa utukufuni, Lakini wewe ambaye upo dhambini Je! Wewe ambaye unautazama ulimwengu utakuwa wapi?… Mkimbilie Kristo ndani ya hichi kipindi kifupi tulichobakiwa nacho, acha kupoteza muda, ulimwengu haukujali kama unavyofikiria wewe…Tubu dhambi zako mgeukie Mungu, naye atakupokea, na kukupa Roho wake Makatifu bure,..Unasubiri nini?.

Fanya hivyo sasa hapo uliopo piga magoti utubu, na yeye anakusikia na yupo tayari kukusamehe bure bila gharama yoyote.., kisha baada ya hapo anza kutafuta ushirika na wakristo wenzako, tupa kila nguo mbaya yoyote uliyokuwa unavaa, vimini, suruali, ma-lipstik, acha matendo yote mabaya uliyokuwa unafanya..ili kumthibitishia Mungu kweli umeamua kutubu na kumgeukia yeye..Na yeye akishaona Imani yako na Nia yako kweli umeamua kugeuka…Hiyo tayari ni sababu tosha ya yeye kukupa Roho wake Mtakatifu… atakuvika uwezo wa ajabu ambao utakusaidia kuviondoa vile vilivyosalia..

Fanya hivyo na Bwana atakubariki..Kumbuka tena.. Tunaishi katika majira ya kuchipuka kwa mtini, hivyo mavuno yapo karibu ..

Bwana akubariki.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

 

Shalom.

Mada Nyinginezo:

USISIKILIZE DHIHAKA ZA SHETANI, ZITAKUKWAMISHA.

NAMNA YA KUMTAMBUA BIBI ARUSI WA KWELI WA KRISTO.

HATUTAACHA KUJIFUNZA NENO KILA INAPOITWA LEO.

YUDA ISKARIOTE! MTUME ALIYECHAGULIWA NA BWANA YESU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Kiungo chako kimoja kikikukosesha kikate.

Bwana Yesu alikuwa na maana gani aliposema “kiungo chako kimoja kikikukosesha kikate”?


JIBU: Sentensi hiyo ina tafsiri mbili..Tafsiri ya kwanza ni ya rohoni, na pili ni ya mwilini…Tukianza na tafsiri ya rohoni ambayo inamaanisha viungo vyote vya rohoni. ..Kwamba kitu chochote kile ambacho ni kikwazo cha sisi kuingia mbinguni hicho ni sawa na kiungo, Umaarufu unaweza kuwa ni kiungo,.. marafiki wakati mwingine wanaweza kuwa ni kiungo (kwasababu wapo marafiki ambao ukikaa nao unaweza kuikosa mbingu, hivyo ni wakukata ili kuinusuru roho yako)..Shughuli ni kiungo (Zipo shughuli au kazi ambazo ukizifanya zitakukosesha mbingu haijalishi zimehalalishwa na nchi kiasi gani)..n.k

Tafsiri ya pili na ya muhimu inahusu viungo vya mwili. Mkono unaweza kukukosesha kuiona mbingu., kama mkono wako umezoea wizi., kila ukipita unatamani kudokoa, kama mkono wako umezoea kufanya masturbation, ..Kama imeshindikana kuamua kuacha kufanya hayo mambo kwa njia ya kawaida basi ni bora uukate huo mkono…ili usije ukakupeleka jehanamu ya moto… Kadhalika na ulimi wako kama unakusababisha kila dakika uzungumze mambo ya watu wengine vibaya, au uchonganishe au utukane ni heri ukaukata ili ujiokoe na ziwa la moto…

Biblia inasema…

Yakobo 3:5 “Vivyo hivyo ulimi nao ni kiungo kidogo, nao hujivuna majivuno makuu. Angalieni jinsi moto mdogo uwashavyo msitu mkubwa sana.

6 Nao ulimi ni moto; ule ulimwengu wa uovu, ule ulimi, umewekwa katika viungo vyetu, nao ndio uutiao mwili wote unajisi, huuwasha moto mfulizo wa maumbile, nao huwashwa moto na jehanum.

7 Maana kila aina ya wanyama, na ya ndege, na ya vitambaavyo, na ya vitu vilivyomo baharini, vinafugika, navyo vimekwisha kufugwa na wanadamu.

8 Bali ulimi hakuna awezaye kuufuga; ni uovu usiotulia, umejaa sumu iletayo mauti.

9 Kwa huo twamhimidi Mungu Baba yetu, na kwa huo twawalaani wanadamu waliofanywa kwa mfano wa Mungu.

10 Katika kinywa kile kile hutoka baraka na laana. Ndugu zangu, haifai mambo hayo kuwa hivyo”.

Sasa hata mambo mawili yakiwekwa mbele yangu, nikaambiwa nichague moja,..kwamba ulimi wangu ukatwe niingie mbinguni au nibaki na ulimi wangu niingie Jehanamu…Ukweli ni kwamba nitachagua kukatwa ulimi ili niingie tu mbinguni Na kila mtu ni wazi atachagua hivyo hivyo.

Na viungo vingine vyote ni hivyo hivyo..kama vinatukosesha tumepewa ruhusa ya kuviondoa..sio dhambi! ..Kama tu tunaweza kuondoa figo iliyo na kansa mwilini, ili tu mwili wote usije ukafa…kwanini tushindwe kukata kiungo kimoja ambacho tusipokitoa kitatugharimu ziwa la moto?..Kama unaweza kufanyiwa operation ya kukatwa miguu ili ugonjwa usisambae mwili mzima au kukatwa ziwa ili tu kansa isikumalize mwili wote..kwanini tushindwe kuondoa hivyo hivyo kama vinakuwa sababu ya kutupeleka jehanamu…?

kiungo chako kimoja kikikukosesha kikate.

Wengi wanapenda kulipooza hili Neno la Bwana Yesu na kusema kwamba “hakumaanisha viungo vya mwilini”..Alimaanisha viungo vya mwilini na vya rohoni..vyote viwili!!..Ni kweli tunavipenda viungo vyetu lakini kama vinakuwa ni vikwazo vya kwenda mbinguni hakuna namna..

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Bwana akubariki.

Mada Nyinginezo:

Yule aliyemzuia Yohana asimsujudie alikuwa ni Mwanadamu au Malaika?

Wenye kubatizwa kwa ajili ya wafu ni wakina nani?

Je! ni halali kutoa cheti kwa wakristo wanaooa?

NILIMWONA SHETANI, AKIANGUKA KUTOKA MBINGUNI.

Je unaweza usisamehewe hapa duniani na kule ukasamehewa?

Rudi Nyumbani:

Print this post

HERI NINYI MLIAO SASA, KWA SABABU MTACHEKA.

heri ninyi mliao sasa, kwa sababu mtacheka.

Shalom, Jina la Bwana YESU libarikiwe. Ni siku nyingine tena, Bwana ametupa pumzi yake ya uhai, hivyo hatuna budi kumshukuru kwa hili, haijalishi tu wagonjwa kiasi gani, au tunapitia katika magumu kiasi gani, maadamu tu! pumzi ipo basi tumsifu Mungu.

Leo tutaangazia ni Kwanini biblia mara kwa mara inatumia semi kama hizi: “heri leo”… “maana baadaye”…..

Hiyo inatuonyesha kuwa kile tunachopita leo hii, basi kinyume chake ndicho tutakachokipitia baadaye..Kuna kanuni fulani Mungu ameziweka katika vitu vya asili ambavyo tukivichunguza vizuri tutapata picha ya mambo yanayoendelea rohoni..Kwa mfano kuna wakati utaona muda mfupi kabla mvua kunyesha joto huwa linaongezeka kwa ghafla na kuwa kali sana pengine dakika tano au 10 hivi.. na baada ya hapo mvua kubwa inashuka yenye upepo na baridi…

Au wakati mwingine wa jioni jua linapokaribia kuzama, utagundua kuna nuru inaongezeka kiasi fulani kwa jinsi isivyo ya kawaida kisha baada ya dakika chache tu giza linakuja kuu.

Hiyo inatuonyesha kuwa kabla ya jambo fulani zuri au baya kutokea huwa kinatangulia kilicho kinyume chake..

Na ndivyo hata katika mambo ya Mungu, sikuzote Mungu kabla hajambariki mtoto wake yeyote ni lazima kwanza apitie hali fulani ya uhitaji au dhiki ili aweze kukimudu kile alichomwandalia kule mbeleni.Ndivyo alivyofanya kwa Yusufu ndivyo alivyofanya kwa wana wa Israeli kule jangwani, na ndivyo alivyofanya kwa Ayubu,..ndivyo alivyofanya kwa Nebukadneza, na ndivyo atakavyofanya kwa mtoto wake yeyote yule atakayemwita..

Na ndio maana Bwana Yesu alisema ikiwa unapitia huzuni sasa, kwa ajili ya Imani yako, hajalishi ni katika afya yako,au katika uchumi wako maadamu wewe ni mkristo, basi fahamu kuwa ipo faraja kubwa Mungu kaiweka hapo mbele kwa ajili yako ..Hivyo usiogope..afya tele ipo mbele yako, vicheko tele vipo mbele yako, chakula tele kipo mbele yako.

Mathayo 5:4 “Heri wenye huzuni; Maana hao watafarijika”

 

Luka 6:21 “Heri ninyi mlio na njaa sasa, kwa sababu mtashiba.

Heri ninyi mliao sasa, kwa sababu mtacheka”

Ukiona leo, unayo kiu ya kuyasikia maneno ya Mungu, na unatamani kumfahamu sana Mungu kwa viwango vya juu…Basi usiogope kuonekana umerukwa na akili sasa, au mtu wa itikadi kali…fahamu tu kuwa hapo mbeleni hiyo kiu haitakuwepo tena, na utamfahamu Mungu kwa viwango ambavyo si vya kawaida vya yeye anavyotaka umjue yeye, utazamishwa katika vilindi vya moyo wa Mungu, na kuonyeshwa mambo ambayo ni makubwa na magumu wanadamu wasiyoyajua..

Ukiona leo unachekwa na kudharauliwa na kuonekana kuwa wewe ni takataka kwasababu umeamua tu kumfuata Kristo basi ujue kuwa hapo mbeleni kuna kuheshimiwa na kuogopwa, na kutukuzwa kwa ajili ya Jina la YESU KRISTO.. Hiyo ndiyo kanuni..

Ukiona leo umeacha kila kitu, umekuwa tayari kupoteza hata kazi yako, au biashara yako, au mali zako, au elimu yako au hadhi yako kwa ajili ya Yesu au kwa ajili ya Injili ya Kristo isonge mbele,.. basi fahamu kuwa kupata mara 100 ya hivyo ulivyovipoteza ipo mbele yako..haijalishi itachukua miaka 5,10 au 20 au 50 lakini kabla haujafa Mungu atahakikisha amelitimiza hilo neno lake juu yako.

Mathayo 19:27 “Ndipo Petro akajibu, akamwambia, Tazama, sisi tumeacha vyote tukakufuata; tutapata nini basi?

28 Yesu akawaambia, Amin, nawaambia ya kwamba ninyi mlionifuata mimi, katika ulimwengu mpya, atakapoketi Mwana wa Adamu katika kiti cha utukufu wake, ninyi nanyi mtaketi katika viti kumi na viwili, mkiwahukumu kabila kumi na mbili za Israeli.

29 Na kila mtu aliyeacha nyumba, au ndugu wa kiume au wa kike, au baba, au mama, au watoto, au mashamba, kwa ajili ya jina langu, atapokea mara mia, na kuurithi uzima wa milele”.

Vivyo hivyo tukiona sisi wakristo tumeupoteza ulimwengu wote.,kwa ajili kumtazama Kristo na ufalme wake wa milele, mpaka tunaonekana kama vile watu tusiostahili kuwepo katika ulimwengu huu, basi tujue kuwa,.. Huu huu ulimwengu tutaupata, maana biblia inasema dunia hii itarithiwa na wenye upole( watakatifu)..Na hiyo itatimia katika utawala wa miaka 1,000 unaokuja huko mbeleni.

Mathayo 5:5 “Heri wenye upole; Maana hao watairithi nchi”.

heri ninyi mliao sasa, kwa sababu mtacheka

Lakini kinyume chake pia ni kweli, ukiona sasa umeupata ulimwengu wote, basi ujue tayari umeshaupoteza,..Ukiona kila aina ya ouvu duniani unaokuja wewe ni wako, disko ni zako, uzinzi ni wako, ulevi ni wako, starehe zote ni zako, rushwa ni yako,… wizi ni wako, dhuluma ni zako, tamaa za ujanani ni zako, vimini na suruali ni zako, viduku, na milegezo ni yako..uzinzi ni wako, fashion ni zako…Basi ujue kuwa safari yako ni fupi hapo mbeleni, nyakati za shida zinakuongojea..

Mathayo 16:25 “Kwa kuwa mtu atakaye kuiokoa nafsi yake, ataipoteza; na mtu atakayepoteza nafsi yake kwa ajili yangu, ataiona.

26 Kwani atafaidiwa nini mtu akiupata ulimwengu wote, na kupata hasara ya nafsi yake? Au mtu atatoa nini badala ya nafsi yake?

27 Kwa sababu Mwana wa Adamu atakuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika zake; ndipo atakapomlipa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake”..

Unaona? Uamuzi ni wako,.. usifurahie kuwa unayo afya nzuri sasa na huku upo mbali na Kristo,.. usifurahie unayo elimu kubwa na huku yupo mbali.., unacho hichi aunacho kile, ni mrembo ni mzuri,..fahamu kuwa Mungu ameruhusu faraja yako ikujie sasa ili wakati wa wenzako kufarijiwa wewe uwe unalia na kusaga meno..

Zaburi 62:7 “Wasio haki wakichipuka kama majani Na wote watendao maovu wakistawi. Ni kwa kusudi waangamizwe milele”

Kama wewe upo nje ya Kristo utajisikiaje usikie unyakuo umepita leo na wewe umebaki?., wakati wenzako wanafarijiwa milele mbinguni katika ile karamu ya mwana kondoo wewe upo hapa chini ukisubiri ziwa la moto wa milele. Ni majuto kiasi gani, ukikumbuka kuwa ulishahubiriwa injili mara nyingi na ukapashupaza shingo yako.

Embu leo sema Bwana Yesu usinipite, ninakukaribisha maishani mwangu tangu sasa. Sema hivyo ukimaanisha kabisa kutoka katika moyo wako kuwa kweli kuanzia leo umeamua kumfuata yeye..Ukiwa umepiga magoti yako mwombe akusafishe dhambi zako zote kwasababu hapo ulipo yupo ili kukusikia,.. tubu kabisa hata kwa machozi, na yeye hapo ulipo atakusamehe na kukupa amani ya ajabu ndani ya moyo wako..

Ukishaona hivyo, na amani imekuja ndani yako ujue amekusamehe,..unachopaswa kufanya usihangaike hangaike na huu ulimwengu bali haraka tafuta kanisa zuri la kiroho linalomuhubiri Kristo,.. uende pale, vilevile ukiwa hukubatizwa ipasavyo unapaswa ufanya haraka sana kutimiza agizo hilo muhimu Bwana Yesu alilotupa kwa kila mtu atakayeokoka, Kwamba wote tubatizwe katika ubatizo mmoja kwa jina lake..

Zipo batizo nyingi duniani ambazo si za kimaandiko lakini ubatizo sahihi ni ule wa kuzamishwa katika maji mengi (Yohana 3:23), na uwe ni KWA JINA LA YESU KRISTO sawasawa na Matendo 2:38..

Baada ya hapo Roho Mtakatifu atakutia muhuri na atakuwa kiongozi wako milele kukuongoza na kukulinda mpaka ile siku ya Unyakuo itakapofika ikiwa bado utakuwa hai.

heri ninyi mliao sasa, kwa sababu mtacheka

Bwana akulinde, Bwana akubariki.

Mada Nyinginezo:

Biblia inamaana gani kusema;aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi?

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA KITABU CHA RUTHU:

INJILI KULINGANA NA TEKNOLOJIA

https://wingulamashahidi.org/2018/06/27/maswali-na-majibu/

Rudi Nyumbani:

Print this post

KWANINI AWE PUNDA NA SI MNYAMA MWINGINE?

Kwanini awe Punda na si mnyama mwingine?

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe.

Karibu tujifunze Maandiko.

Tunaona kipindi kifupi kabla Bwana Yesu kuingia Yerusalemu aliwatuma wanafunzi wake wakamletee Mwana-punda ili alingie naye mjini..Ipo sababu kwanini alimtumia yule mtoto wa punda na si mama yake (Mathayo 21:4-5)..lakini leo hatutakwenda kuiangalia hiyo sababu..kama utapenda kufahamu ni kwanini hakumtumia Mama-punda bali mwanae…unaweza akatuambia inbox tukakutumia ujumbe wake…

Pamoja na hayo pia ipo sababu kubwa sana ni kwanini hakutumia mnyama mwingine yoyote kama vile Farasi au Ngamia kuingia naye Yerusalemu badala yake akatumia PUNDA, kwanini awe punda.. Na hali tunajua kuwa punda si mnyama wa heshima…Walau ingekuwa ni Farasi ingeleta heshima kidogo…lakini si punda?..Tofauti na wahubiri wengi waa leo hii ambao ukiota tu punda au ukifuga tu punda licha ya kumpanda ni rahisi kuambiwa una nyota ya punda!..(utaambiwa utakuwa mtumwa milele)…

Lakini haikuwa hivyo kwa Bwana wetu Yesu,..Yeye alimpanda huku akijua kuwa yeye ni mfalme anayesubiriwa mjini, na muda mfupi tu baadaye aliimbiwa na umati mkubwa kwa shangwe na vigelegele kwamba yeye ni Mfalme!!, Hosana juu mbinguni..watu walitandika mavazi yao chini na kukata matawi ya miti na kuyatandaza chini, Mfalme mkuu juu ya punda apite, na kumwimbia…Mbarikiwa, yeye ajaye kwa jina la Bwana!..Hivyo punda sio mnyama wa laana kama upotovu uliozagaa leo….

Tabia ya Punda;

Hivyo kuna ufunuo hapo kwanini awe ni punda Bwana Yesu alimtumia na si mnyama mwingine..Na leo tutajifunza kwa ufupi siri hiyo, ambapo tukishaijua tutafahamu ni jinsi gani KRISTO alikuwa ni chombo ya muhimu sana kwetu.

Pamoja na tabia nyingine nyingi Punda alizonazo…lakini anayo tabia moja kuu ambayo imewazidi Wanyama karibia wote..Na tabia hiyo ni tabia ya KUHISI HATARI ILIYOPO MBELE, AU KUHISI KITU KINACHOKUJA MBELE…Chochote cha heri au cha shari kinachokuja mbeleni Punda ni mwepesi sana kukihisi…Jambo ambalo litamfanya aidha Agome kuendelea mbele au Aende huko anakokwenda kwa Furaha…. Jamii zote za Punda wanayo hiyo tabia, hata farasi anayo lakini si kwa kiwango alichonacho Punda…(kwasababu farasi naye ni jamii ya Punda).

Biblia inasema katika

Ayubu 39:19 “Je! Wewe ulimpa farasi uwezo wake? Au, ni wewe uliyemvika shingo yake manyoya yatetemayo?

20 Ndiwe uliyemfanya aruke kama nzige? Fahari ya mlio wake hutisha.

21 Hupara-para bondeni, na kuzifurahia nguvu zake; Hutoka kwenda kukutana na wenye silaha.

22 Yeye hufanyia kicho dhihaka, wala hashangai; Wala hageuki kurudi nyuma mbele ya upanga. ……

25 Kila ipigwapo baragumu yeye husema, AHA! NAYE HUSIKIA HARUFU YA VITA TOKA MBALI, Mshindo wa maakida, na makelele”.

Unaona! Farasi anauwezo wa kusikia harufu ya vita toka mbali..Kesho kutapiganwa vita farasi leo kashajua!! (Ni kipawa ambacho Mungu kawapa)..Sasa hisia za Punda ni kubwa kuliko za Farasi. Wafugaji wazoefu wa punda wanajua!..huwa punda akigoma kufanya kitu au kwenda mahali huwa hawamlazimishi..kwasababu wanaelewa hisia alizonazo punda..

Tunasoma mfano mmoja katika Biblia wa mtu anayeitwa Balaamu, huyu alitaka kwenda kuwalaani Israeli, jambo ambalo Mungu alimkataza kulifanya..lakini yeye akashupaza shingo,..wakati akiwa njiani anaelekea kwenda kuonana na mfalme Balaki kwa lengo la kuwalaani Israeli, akiwa amempanda punda wake…Njiani alikutana na Malaika ambaye alitaka kumwua lakini cha ajabu ni kwamba Balaamu hakumwona yule malaika lakini punda alimwona!..Japokuwa Balaamu alikuwa ni mtu wa kiroho sana aliyezoea kuona malaika lakini siku hiyo hakumwona…Punda alimsaidia kumwepushia ile ajali ya kuuawa. Mpaka alipofunguliwa macho na kuiona hatari iliyopo mbele yake..hivyo asingekuwa punda Balaamu angekufa..(Kasome Hesabu 22 yote). .

Nakumbuka ilikuwa mwaka 2015, mwezi wa 10 tarehe 14..Tulikuwa tupo wawili tunapita mahali fulani huku tunazungumza habari za Mungu..Sehemu hiyo ilikuwa ni mbali kidogo na mji ni kama nusu Kijiji hivi…Ni sehemu ambayo ina wafugaji na wachungaji…Siku hiyo jua lilikuwa linawaka sana wakati tunatembea huku tunaongea..mbele yetu walitokea watu ambao walionekana wametoka porini kukusanya nyasi za ng’ombe hivyo wameziweka kwenye kigari ambacho mbele kilikuwa kinavutwa na punda watatu waliofungiwa nira. Binafsi sikuwahi kuona punda watatu wakiwa wamefungwa nira pamoja..Nimezoea kuona wawili tu…Na hata mwenzangu na yeye hakuwahi kuona hicho kitu…Basi wote kwa pamoja tukasema ngoja tusogee mbele kidogo tuona jinsi walivyozifunga hizo nira katikati ya hao punda watatu..

Wakati tunaendelea kusogea..

wale mabwana walikuwa wanawachapa waendelee kusogea mbele..maana ule mzigo ulikuwa ni mzito kidogo..Sasa wakati tunakazana kutazama zile nira katikati ya wale punda watatu, yule punda wa katikati akatoweka!. Wakabaki wawili tukaduwaa kidogo ni nini kinaendelea…Lakini wale mabwana wao ni hawakuona lolote…

Wakati tunaendelea kuangalia

tuligundua kuwa wale punda walikuwa na uwezo fulani ambao haukuwa wa kawaida..kwasababu mzigo ulikuwa mzito na viboko vingi lakini walitembea vizuri kama kawaida…Sasa kwa haraka haraka kama si mtu wa rohoni unaweza kuhisi umeona uchawi!!..lakini haukuwa uchawi, Roho Mtakatifu muda mfupi baada ya hilo tukio alizungumza na sisi kutufundisha jambo…

Tulichokiona kilikuwa ni ono!..Kwamba Bwana hata katikati ya Wanyama yupo kuwasaidia,..Na pia akatufundisha kuwa “walipo wawili au watatu yeye yupo katikati yao”..Ulikuwa ni uthibitisho tu kuwa Mungu yupo katikati yetu wakati tunazungumza habari zake… na wengine wakusanyikao katika Bwana yeye anakuwa katikati yao, mfano wa wale punda..Na wakati wale mabwana wanadhani wale punda wapo wawili tu…kumbe wale punda walikuwa wanamwona mwingine watatu akiwa katikati yao, akiwachukulia mizigo yao na maumivu yao… Haleluya!!, Hicho ndicho Roho Mtakatifu alichotufundisha siku hiyo.

Sasa tukirudi kwa kile kilichotokea wakati Bwana anaingia Yerusalemu…Unaweza kufikiri ni nini wale Punda walikiona mbele??..Farasi wangenusa vita lakini si WOKOVU uliokuwa unakwenda Yerusalemu..Ngamia wangenusa jangwa lakini Punda waliona wokovu…Waliona Amani, walimwona huyu tuliyembeba Anakwenda kuleta Ukombozi kwa viumbe vyote.

Punda alitii;

Hivyo wasingeweza kugoma..kama walivyogoma kwa Balaamu..Mbele ya Balaamu waliona kifo lakini mbele ya MASIHI YESU KRISTO WALIUONA WOKOVU!!! Haleluya. Waliona wokovu unaingia Yerusalemu, kipindi kifupi tu kijacho Roho Mtakatifu atashuka ndani ya watu kuanzia hapo Yerusalemu..waliona mabadiliko makubwa ya nyakati yanakwenda kuanza..Punda Waliona huyu atupandaye ataleta amani si tu kwa wanadamu bali hata kwa viumbe vyote..kwamba wakati utafika viumbe vyote vitawekwa huru kupitia huyu..Hivyo punda yule alitembea mbele kwenda Yerusalemu kwa furaha yote wala hakusimama njiani..

Kwasababu Biblia inasema katika..

Warumi 8:19 “Kwa maana viumbe vyote pia vinatazamia kwa shauku nyingi kufunuliwa kwa wana wa Mungu.

20 Kwa maana viumbe vyote pia vilitiishwa chini ya ubatili; si kwa hiari yake, ila kwa sababu yake yeye atiyevitiisha katika tumaini;

21 kwa kuwa viumbe vyenyewe navyo vitawekwa huru na kutolewa katika utumwa wa uharibifu, hata viingie katika uhuru wa utukufu wa watoto wa Mungu.

22 Kwa maana twajua ya kuwa viumbe vyote pia vinaugua pamoja, navyo vina utungu pamoja hata sasa”.

Ndugu kama Punda wameouona wokovu wewe kwanini usioune wokovu!..Punda walikubali kutumika wewe kwanini usikubali leo!..Punda waliupata ufunuo wa Yesu wewe kwanini hauuoni leo…Bado unaitumikia dunia ambayo mshahara wake ni mauti!!..bado mwasherati, mlevi, mzinzi, mla rushwa, msengenyaji, mwizi, mlawiti, mtoaji mimba, mvumishaji habari za uongo na mshirikina?..Utaficha wapi uso wako siku ile!..

Sasa lengo kuu sio kuwasifia punda, au kuwafanya kuwa viumbe wa kiungu!.. Kwamba wanastahili kuheshimiwa..au kutumika katika masuala ya utambuzi…Hapana! hakuna mnyama yoyote anayestahili kupewa heshima hiyo wala kuhusishwa na masuala ya Ibada…Lengo kuu ni kujifunza ni UTUKUFU ALIOUBEBA YESU KRISTO, Na kwamba kila kitu, ikiwemo viumbe vyote vimebeba ushuhuda wake…Kila mahali kwenye miti, miamba, bahari, mbingu, milima, sayari n.k kumeandikwa ushuhuda wa Yesu Kristo. Hivyo Yesu Kristo ni muhimu sana katika Maisha yetu.

Bwana anasema..

Mathayo 11:28 ‘’Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.

29 Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu;

30 kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi’’

Hivyo Kama hujamkabidhi Maisha yako…Mlango upo wazi sasa, ila hautakuwa hivyo siku zote…itafika wakati utafungwa na ukishafungwa itakuwa haiwezekani tena kuupata wokovu…Hivyo unachopaswa kufanya kama hujakoka ni hapo ulipo utubu dhambi zako zote bila kuacha hata moja…mwambie Bwana Yesu akusamehe na kwamba hutafanya tena hizo dhambi..na ukishatubu kwa kumaanisha kabisa, kuna msukumo wa ajabu utakuja ndani yako wa kukufanya utamani kumjua Mungu Zaidi…

Mkumbuke mtu yeyote ambaye hapo kwanza uliwahi kumwona ni mkristo wa kiroho, na matendo yake ni mazuri…kajiungamanishe naye huyo, na kuanzia hapo Roho Mtakatifu ataanza kutembea na wewe kukuongoza katika kuijua kweli yote ya maandiko…Pia katika hatua hizo zingatia kutafuta ubatizo haraka sana kama hukubatizwa..Ubatizo sahihi ni ule wa maji tele (Yohana 3:23),..na kwa jina la Yesu Kristo kulingana na Matendo 2:38, Na Roho Mtakatifu atafanya yaliyosalia ndani yako.

Kumbuka Yesu Kristo, ndiye NJIA, KWELI na UZIMA…Hakuna njia nyingine ya kuokolewa isipokuwa kwake yeye.jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Maran atha!

Mada Nyinginezo:

KWANINI AWE NI PUNDA NA MWANA-PUNDA?

JE! MTUMISHI KUTOKUWA NA FEDHA NI ISHARA KUWA KUNA TATIZO KATIKA IMANI YAKE?

USISIKILIZE DHIHAKA ZA SHETANI, ZITAKUKWAMISHA.

TUMAINI NI NINI?

Rudi Nyumbani:

Print this post

BONDE LA KUKATA MANENO.

Bonde la kukata maneno ni nini?

Yoeli 3:14 “Makutano makubwa, makutano makubwa, wamo katika bonde la kukata maneno! Kwa maana siku ya Bwana i karibu, katika bonde la kukata maneno.

15 Jua na mwezi vimetiwa giza, na nyota zimeacha kuangaza.

16 Naye Bwana atanguruma toka Sayuni, atatoa sauti yake toka Yerusalemu; na mbingu na nchi zitatetemeka; lakini Bwana atakuwa kimbilio la watu wake, na ngome ya wana wa Israeli”.

Biblia inatuambia kuna wakati unafika hapa mbele yetu ambao Mungu atayaleta mataifa yote katika bonde lijulikanalo kama bonde la kukata maneno, biblia imeliita pia kama Bonde la Yehoshafau ukisoma kuanzia mstari wa 12. Yehoshafua maana yake ni YEHOVA-ANAHUKUMU..Hivyo bonde hilo litakuwa ni bonde la Yehova kuya hukumu mataifa yote..

Unaweza ukajiuliza ni kwanini pia limeitwa bonde la kukata maneno.. Kwa lugha rahisi kukata maneno ni sawa na kusema kumaliza hoja, au malumbano,.. kwamfano mahali ambapo, pana malalamiko mengi labda tuseme katika Taifa fulani wananchi wake wanalamika kila siku miundo mbinu ni mibovu,..

wanashindwa kufanya shughuli zao za kimaendeleo, wanashindwa kusafiri, wanashindwa kwenda mashambani n.k.

sasa kama serikali italiona hilo na kuacha kuchukua hatua watu wake wataendelea kulalamika hivyo hivyo hata kwa karne na karne,.. sasa ili kukata maneno hayo, viongozi huwa wanachukua uamuzi wa lazima na wa haraka, aidha watalazimika kwenda kukopa pesa ili watimizie wananchi matakwa yao,.. au watatoa katika bajeti yao wahakikishe tu kuwa jambo hilo linafanyika haraka sana ili kukata maneno ya wananchi yasiendelee kuwasumbua..hivyo Kukata maneno ni kutoa suluhisho. (kwa kiingereza linaitwa Valley of decision).

Vivyo hivyo na kwa Mungu pia, leo hii yapo makundi makuu mawili ya watu yanayomlilia na kumpelekea tuhuma zao kila kila siku kundi la Kwanza ni lile linalomlilia Mungu na kumwambia ni lini Bwana utakomesha uovu juu ya nchi ili maasi yasiendelee?.

Ni lini utatulipizia kisasi juu ya maadui zetu na maadui zako? Ni lini ufalme wako utakuja duniani?…Ni lini Bwana…?

Ufunuo 6:9 “Na alipoifungua muhuri ya tano, nikaona chini ya madhabahu roho zao waliochinjwa kwa ajili ya neno la Mungu, na kwa ajili ya ushuhuda waliokuwa nao.

10 Wakalia kwa sauti kuu, wakisema, Ee Mola, Mtakatifu, Mwenye kweli, hata lini kutokuhukumu, wala kuipatia haki damu yetu kwa hao wakaao juu ya nchi?

11 Nao wakapewa kila mmoja nguo ndefu, nyeupe, wakaambiwa wastarehe bado muda mchache, hata itakapotimia hesabu ya wajoli wao na ndugu zao, watakaouawa vile vile kama wao”.

Na kundi la pili ni lile linalodhihaki, na kusema, huyo Yesu mnayemngojea mbona harudi amekufa?., kundi linalolikufuru jina la Mungu bila hofu yoyote, kundi linalojiamulia kufanya maovu tu bila kujali kuwa yupo Mungu juu, kundi linalosema hakuna Mungu,.. kama yupo basi ajitokeze tumwone, akisimama hapo na kushusha moto mbinguni, ndipo tutamsujudia..mbona anajificha, anajifichia nini ikiwa yeye ni Mungu n.k..

Umeona? Makundi yote haya yanapeleka malalamiko yao..Sasa Bwana ameiandaa siku ambayo ATAKATA MANENO HAYA YOTE..Siku hiyo ndugu usitamani uwepo..Kwasababu kabla hajatenda tendo lolote atahakikisha kwanza mataifa yote yamekusanyika pamoja, kisha atayafanya yaelekeze uso wao pale Israeli.. na uwanja wa mapambano utakuwa katika lile bonde la Yehoshefau au bonde la kukata maneno..

Sasa wakati wameshajiweka tayari kwa vita biblia inatuambia ghafla, jua na mwezi vitatiwa giza, yaani kwa wale ambao watakuwa upande wa mchana kipindi hicho watalishuhudia jua likizama saa 7 mchana, na kuwa giza tororo duniani kote,. wala hata mwezi nao hautaonekana, wala hizi nyota, wala tochi, wala taa za barabarani haziwaka..duniani kote hakutakuwa na chanzo chochote cha mwanga kwa ufupi.

Amosi 8:9 “Tena itakuwa siku hiyo, asema Bwana MUNGU, nitalifanya jua litue wakati wa adhuhuri, nami nitaitia nchi giza wakati wa nuru ya mchana”.

Kipindi hicho dunia itakuwa imeshaingiwa na hofu, wakiomboleza ni nini hiki kimetokea hapo ndipo wakatakapomwona Kristo akishuka na wingu kutoka juu pamoja na majeshi ya mbinguni..(watakatifu waliokuwa wamenyakuliwa), hapo ndipo Bwana atawaua kwa upanga utokao katika kinywa chake,.

Ufunuo 19:11 “Kisha nikaziona mbingu zimefunuka, na tazama, farasi mweupe, na yeye aliyempanda, aitwaye Mwaminifu na Wa-kweli, naye kwa haki ahukumu na kufanya vita.

12 Na macho yake yalikuwa kama mwali wa moto, na juu ya kichwa chake vilemba vingi; naye ana jina lililoandikwa, asilolijua mtu ila yeye mwenyewe.

13 Naye amevikwa vazi lililochovywa katika damu, na jina lake aitwa, Neno la Mungu.

14 Na majeshi yaliyo mbinguni wakamfuata, wamepanda farasi weupe na kuvikwa kitani nzuri, nyeupe, safi.

15 Na upanga mkali hutoka kinywani mwake ili awapige mataifa kwa huo. Naye atawachunga kwa fimbo ya chuma, naye anakanyaga shinikizo la mvinyo ya ghadhabu ya hasira ya Mungu Mwenyezi.

16 Naye ana jina limeandikwa katika vazi lake na paja lake, MFALME WA WAFALME, NA Bwana WA MABwana.

17 Kisha nikaona malaika mmoja amesimama katika jua; akalia kwa sauti kuu, akiwaambia ndege wote warukao katikati ya mbingu, Njoni mkutane kwa karamu ya Mungu iliyo kuu;

18 mpate kula nyama ya wafalme, na nyama ya majemadari, na nyama ya watu hodari, na nyama ya farasi na ya watu wawapandao, na nyama ya watu wote, waungwana kwa watumwa, wadogo kwa wakubwa.

19 Kisha nikamwona huyo mnyama, na wafalme wa nchi, na majeshi yao, wamekutana kufanya vita na yeye aketiye juu ya farasi yule, tena na majeshi yake”.

Katika kipindi hichi baada ya Kristo kuwaangamiza wale wote waliokuja kufanya vita kinyume chake ambao watakuwa ni mamilioni kwa mamilioni, hatua inayofuata ataketi na kuwahukumu wale waliosalia,.. huo ndio ule wakati wa kutenganishwa kondoo na mbuzi, mbuzi watatupwa katika lile ziwa la moto..Na hao wengine watapata neema ya kuingia katika ule utawala wa miaka 1000. Na kipindi hicho sio kwamba watu watakuwa ni wengi duniani hapana, biblia inasema watu wataadimika kuliko Dhahabu, (Soma Isaya 13:12), hivyo pengine ni watu 100 kati ya bilioni 7 waliopo duniani leo watakaosalimika, kama vile ilivyokuwa katika siku za Nuhu ilikuwa ni watu 7 kati ya mabilioni..Mungu hana wengi wape,..haangalii wingi wa watu wasiomwamini kama kigezo cha kuturehemu.

Na wakati huo sasa ndio Kristo atakapoitengeza tena hii dunia ndipo atakapotawala kama mfalme wa wafalme duniani, pamoja na wale watakatifu waliokwenda naye kwenye unyakuo na kurudi naye na wayahudi waliokuwa wamefichwa..Hao pekee ndio watakaofanana na malaika, watakaokuwa na miili ya umilele, lakini wengine watazaliana na kuongezeka mpaka mwisho wa ule utawala wa miaka 1000 utakapofika..

Hivyo unaweza ukaona ni jinsi gani hii dunia inavyoelekea pabaya, mambo hayo usidhani yatakuja kutokea miaka 800 mbeleni, tunaweza kuyashuhudia katika kizazi chetu hichi,.. kwani mataifa mengi tayari yameshaelekeza silaha zao Israeli kwa lengo la kuliondoa katika uso wa dunia unadhani ni kitu gani kimesalia..

Bonde la kukata maneno!! Lisiwe sehemu ya maisha yako.Mkaribishe Kristo maishani mwako leo ili akufanye kuwa kiumbe kipya, na kukuepusha na hukumu inayokuja..jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Bwana akubariki.

Mada Nyinginezo:

CHUKIZO LA UHARIBIFU

SIKU YA HASIRA YA BWANA.

JUMA LA 70 LA DANIELI

ZIKUMBUKE SIKU ZIJAZO ZA GIZA, KWA MAANA ZITAKUWA NYINGI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

DHAMBI INAZAA KIFO.

Dhambi inazaa kifo.

Jina la Yesu Kristo Mkuu wa Uzima.. libarikiwe!.

Bwana Yesu alisema..

Yohana 8:33 “Wakamjibu, Sisi tu uzao wake Ibrahimu, wala hatujawa watumwa wa mtu wakati wo wote; nawe wasemaje, Mtawekwa huru?

34 Yesu akawajibu, Amin, amin, nawaambia, Kila atendaye dhambi ni mtumwa wa dhambi.

35 Wala mtumwa hakai nyumbani sikuzote; mwana hukaa sikuzote”

Mtu anayetenda kazi anafananishwa na Mfanyakazi…Na mfanyakazi anaweza akawa na cheo cha juu, au cha chini…Mara nyingi wale wenye vyeo vya chini sana wanaitwa watumwa…Watumwa wengi huwa wanapitia mateso..Mshahara wanaoupata haulingani na kazi wanazozifanya…Wanalazimika kumtumikia tu Bwana wao kwasababu hawana namna nyingine ya kujikwamua kimaisha.

Kadhalika Mtu atendaye dhambi!..Biblia inasema ni mtumwa wa dhambi..Na utumwa huo unafananishwa na utumwa wa wanyama…Kwamfano mnyama kama ng’ombe anaweza kutumikishwa kulima hekari hata 1,000 katika maisha yake yote, na kuzalisha maziwa lita elfu 5,000 katika maisha yake yote..lakini mshahara wake mwisho wa siku ni KISU SHINGONI MWAKE!. Na wala hakuna mtu anayejali kufa kwake…Na nyama yake itatumika kama kitoweo, na ngozi yake kwa kutengenezea viatu, na pembe zake kutengenezea mbiu na vifungo.

Kadhalika na utumwa wa dhambi ni hivyo hivyo…Dhambi inaweza kukutumikisha miaka yote na mwisho wa siku ikakuzawadia au kukulipa KIFO. Tena wakati mwingine kifo cha kikatili.

Biblia inasema..

Warumi 6: 23 “Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti; bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu”.

Ndugu mshahara wa dhambi ni mauti biblia haidanganyi!, …Usidanganywe na Tamaa za ulimwengu huu, “wanazoziita ustaarabu mpya”… zinazokuambia kuwa na boyfriend/girlfriend ni kwenda na wakati..zinazokuambia kujipamba uso na kujichubua na kuvaa wigi na hereni ni kujipenda!..zinazokuambia mpende akupendaye asiyekupenda mwache, na hivyo hata ukiwa na mke/mume msiyeelewana kidogo tu ni ruksa kumwacha na kutafuta mwingine!…

usidanganyike na Tamaa za anasa za ujanani zinazokuambia kwenda disko sio vibaya, zinazokuambia kunywa pombe yenye kidogo sio vibaya, zinazokuambia kuvaa vimini sio vibaya ni ujana tu!..utakapofikisha umri fulani ndipo utaanza kuvaa vizuri.

Biblia inasema katika

2Timotheo 2:22 “Lakini zikimbie tamaa za ujanani; ukafuate haki, na imani, na upendo, na amani, pamoja na wale wamwitao Bwana kwa moyo safi”…

Yakobo 1:14 “ kila mmoja hujaribiwa na tamaa yake mwenyewe huku akivutwa na kudanganywa.

15 Halafu ile tamaa ikiisha kuchukua mimba huzaa dhambi, na ile dhambi ikiisha kukomaa huzaa mauti”.

Ukitenda dhambi unajitengenezea mazingira ya kukutwa na kifo cha ghafla!….Sasa sio kwamba wote wanaokufa kwa ghafla wana dhambi!.. Hapana sio wote…Lakini idadi kubwa, Zaidi ya robo tatu ya vifo vinavyotoke leo hii duniani kote.. ni matokeo ya dhambi juu ya maisha ya watu Biblia inasema hivyo..(Soma Ezekieli 18:31, Ezekieli 33:11, Ezekieli. 18:20)

Uzinzi ni kifo!. Na kifo cha uzinzi na uasherati hakitokani tu na HIV au ugonjwa Fulani wa zinaa..kama wengi wanavyodhani….Wakati mwingine vifo vya ghafla visivyokuwa na chanzo au visivyoeleweka.. vinaweza kuwa ni matokeo ya dhambi ya uasherati juu ya maisha ya mtu..Mtu aliye mwasherati anaweza akafa tu hata kwa ajali sio lazima tu HIV..

Mshahara wa kushi na mwanamke/mwanamume ambaye hamjaoana ni kujitengenezea kifo,..kumwacha mkeo/mumeo na kwenda kuoa/kuolewa na mwingine ni umejitengenezea kifo mwenyewe..(Kwasababu biblia inasema kifo ndicho kitakachowatenganisha sasa wewe umefanyika kifo katikati ya hiyo ndoa ndio maana umeitenganisha)… kutowaheshimu wazazi ni mauti!..mshahara wa rushwa, na wizi wa namna yoyote ile ni kifo,(na kifo sio tu cha kuchomwa moto! Kinaweza kuwa kingine hata ugonjwa Fulani tu! Ukakupata ghafla na kukuondoa)..mshahara wa kutoa mimba, kuua, kulawiti, kucheza kamari, kufanya uchawi, kuuabudu sanamu, usengenyaji,utukanaji n.k ni KIFO!..chaa kimwili na cha Kiroho..

Dhambi ni mauti:

Haijalishi hiyo dhambi ilikuwa inakunufaisha kiasi gani…Hata baadhi ya wanyama kama kuku wanaweza kunufaika kwa kulishwa vizuri na kupewa kila aina ya chakula ilikusudi kwamba wawe na nyama nyingi au watage sana…lakini pamoja na kunenepeshwa kwao kote..mshahara wao wa mwisho ni mauti!..Siku wasiyoitazamia na wasioitegemea msiba wao unawafika kwa ghafla..Ni idadi ndogo sana ya kuku wanaokufa kifo cha kawaida..

Unaweza ukawa unakula rushwa leo na ukafanikiwa, unaweza ukawa unaiba na unafanikiwa lakini fahamu kuwa kifo kinakuja mbele… Nataka nikuambie kifo ni kama usingizi ni kitu ambacho huwezi kukipangia wakati wa kukuvaa…kama vile unavyozama usingizini hujui dakika halisi uliyolala…utakapozinduka ndipo utakapojua kumbe muda ule ulipotelea usingizini..,Unaweza kujilaza kitandani na ukasema kabla ya kulala nitafanya hichi au kile..wakati unawaza hayo ghafla unajikuta umezinduka na hujafanya uliyokuwa unayasema..Na kifo ndio hivyo hivyo kinakuja kama usingizi, wakati unasema bado sitakufa nitatubu tu sasa kumbe tayari umeshaondoka na kujikuta tu umetokezea mahali pengine pa mateso yasiyoelezeka…

Mhubiri 8:8 “ Hakuna mwenye uwezo juu ya roho aizuie roho; WALA HANA MAMLAKA JUU YA SIKU YA KUFA; Wala hakuna kuruhusiwa katika vita vile; Wala uovu hautamwokoa yule aliyeuzoea”.

Bwana akubariki.

Ikiwa hujampa Yesu Kristo maisha yako..na dhambi zinakutesa Kristo yupo sasa kukusaidia…

Kumbuka pia kuzimu ipo!..Mahali ambapo wenye dhambi wote watatupwa kama takataka na kupata mateso yasiyoelezeka… Mlango wa Neema sasa upo wazi..Na mpatanishi wetu sisi na Mungu yupo hai leo,.. Yesu Kristo anakuita utubu dhambi zako zote na akuoshe kwa damu yake na kukupa uzima wa Milele..na kukuokoa na ghadhabu ya Mungu itakayoikumba dunia kipindi sio kirefu tokea sasa..Na yeye Mungu hapendi sisi tuangamie, ndio maana akamtuma mwanawe mpendwa Yesu Kristo..Aje atuokoe sisi bure. Usipuuzie Neema hiyo, ipokee ikufanye kiumbe kipya maadamu unaishi.

Kumbuka tena, mshahara wa dhambi ni mauti. Na matokeo ya mauti itokanayo na dhambi ni kutupwa katika lile ziwa la moto..na chanzo cha dhambi ni Tamaa..

Maran atha. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

SAUTI NI SAUTI YA YAKOBO, LAKINI MIKONO NI YA ESAU.

UPAKO NI NINI?

KWA KUWA NGUVU ZA MBINGUNI ZITATIKISIKA.

UWE MWAMINIFU HATA KUFA.

Uasherati wa Kiroho maana yake nini?

Rudi Nyumbani:

Print this post

KWANINI BWANA YESU ALISULUBIWA NA WEZI WAWILI?

Naomba kuuliza mtumishi ni Kwanini Yesu alisulubiwa na wezi wawili pale msalabani?


JIBU: Ni kweli Ilikuwa inajitosheleza kabisa Bwana wetu YESU kufa mwenyewe pale msalabani, lakini kulikuwa na sababu nyingine ya ziada Mungu kuruhusu Bwana wetu asulibiwe na wezi wengine wawili pamoja naye…

Awali ya yote tunapaswa tufahamu kuwa Bwana Yesu alikuja duniani kwa lengo la kutafuta kilichopotea, hiyo ndiyo iliyokuwa kazi yake kubwa.

Mathayo 18:11 [Kwa maana Mwana wa Adamu alikuja kukiokoa kilichopotea.]

Hivyo kama Yesu alikuja kukiokoa kilichopotea, basi tufahamu kuwa alimaanisha kweli kweli kusema vile…, kiasi kwamba hata katika dakika ya mwisho ya uhai wa watu waovu Mungu alimweka katikati yao, atimize kusudi lake hilo la kuokoa.. Na ndio maana utaona aliwekwa katikati ya wale wezi wawili kabla ya kufa kwao..Kwasababu Mungu alitamani na wao pia waokolewe hata kama hawakupata neema ya kumsikia akifundisha katika masinagogi, au hekaluni au mijini au vijijini, bali hata hapo pia ipo fursa ya kuokolewa ikiwa watamwamini..

Hiyo inafunua nini?..

Hata sasa, Kristo hatimizi lengo la kuokoa kwa wale watu ambao pengine wanayo Maisha marefu ya kuishi,… hapana bali pia analitimiza lengo hilo kwa wale ambao anajua wapo katika dhambi nyingi na siku zao za kuishi hapa duniani zinakaribia kuisha, anachofanya huwa anajisogeza karibu sana na wao, kiasi kwamba wakati mwingine anajidhihirisha hata katika mateso wanayopitia ili tu wamwamini yeye waokolewe wasipotee..Kama vile alivyofanya kwa wale wezi wawili, alipitia katika mateso yao yale yale ya kusulibiwa ili tu wamsikilize..

Lakini sasa, cha ajabu ni kuwa katikati ya makundi haya mawili wapo wanaokubali na kugeuka haraka sana..lakini pia wapo ambao badala ya kukubali ndio wanakwenda mbali Zaidi na Mungu, badala ya kutubu ndio wanakufuru Zaidi..

Ndio hapo utasikia mtu anasema, sijui yule kahaba alijuaje juaje siku zake, wiki iliyopita tu, alikwenda kanisani akatubu leo hii tumesikia amepata ajali amekufa,… ukiona hivyo ujue alimtii Kristo katika saa zake za mwisho kama vile yule mwizi wa kwanza..

Mwingine utasikia anasema, alimfukuza mhubiri fulani nyumbani kwake juzi alipokuja kumletea vipeperushi vya injili, na leo hii kwa ghafla tu tumesikia kafa kwa stroke..Mwingine utasikia lisaa limoja lililopita alipokuwa hospitalini anaendelea tu vizuri, mwinjilisti mmoja alikuja akamuhubiria akakubali kutubu, na sasa hivi tunasikia amekufa…n.k. n.k shuhuda kama hizo utazisikia zipo nyingi…utagundua wapo wanaokufuru, wapo wanaotii..

Fursa ya injili;

Na ni mara nyingi wanaobahatika kupata hiyo fursa kusikia injili muda mfupi kabla ya kuondoka kwao ni wale ambao hawajawahi kusikia kabisa injili hapo kabla! Au waliisikia kwa juu juu tu, na hawakupata kujua zaidi ingawa walitamani….Hivyo Mungu anawaletea wokovu mpaka ile siku ya kufa kwao. Ili wasife kabla hawajampokea Yesu.

Lakini kwa wale ambao walishasikia na kupuuzia, inakuwa ni ngumu sana kupata hiyo nafasi,….Wakati Bwana Yesu anasulubiwa pale msalabani kulikuwepo na watu wengine mahali pengine wanakata roho..kulikuwepo na watu wengine mahali pengine labda wanachomwa moto kutokana na wizi wao..lakini hawakupata hiyo fursa ya kusogelewa na Bwana wakati wa kifo chao kama ya hawa wezi wawili waliosulubiwa pamoja na Bwana..

Hata sasa Bwana anafanya hivyo;

Hata mimi na wewe hatujui ni mangapi yapo mbele yetu, pengine tumebakisha wiki, au mwezi, au mwaka, lakini tunaona Kristo anatuhubiria injili kwa nguvu katika hali ya uzima tuliyonayo sasa, katika hali ya kufanikiwa tuliyopo sasa.. pengine kuliko hata alivyowahi kutuhubiria hapo nyuma, Tukiona hivyo tusianze kupuuzia, au kukejeli au kudharau Neno la Mungu, badala yake tukubali kutii na kugeuka haraka sana kama ilivyokuwa kwa yule mwizi wa kwanza,…tukichelewa chelewa, tujue kuwa tunajiweka wenyewe hatarini..Kwasababu katika dunia ya sasa hakuna mtu akifika kule atasema sikusikia injili..Karibi kila mtu kashasikia habari za Yesu…

Kama unaisikia injili sasa ukiwa mzima na unaidharau, mlango wa kutubu wakati wa kufa kwako unakuwa ni mwembamba sana. Ndio maana Biblia inasema saa ya wokovu ni SASA!..Sio kesho wala baadaye..SASA!!

Na Bwana Yesu hafanyi hivyo ili apate sababu ya kutuhukumu hapana badala yake ni ili atupe uzima wa milele na atuepushe na jehanamu..Hivyo kama wewe hujatubu bado na upo nje ya Kristo , muda ndio huu fanya hivyo sasa mpe Kristo Maisha yako, na yeye atakutengeneza na kukufanya kuwa kiumbe kipya..jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Ubarikiwe.

Mada Nyinginezo:

KWANINI YESU KRISTO ALIKUJA DUNIANI?

KWANINI YESU KRISTO NI MWANA WA DAUDI?

NI KIPI MUNGU ANACHOKITAZAMA ZAIDI, MOYO AU MWILI?

MTUMAINIE YESU ASIYEISHA MATUKIO.

BUSTANI YA NEEMA.

Rudi Nyumbani:

Print this post