JIBU: Uzao wa Mwanamke ni Uzao wa Yesu Kristo. Wote waliozaliwa mara ya pili, kwa lugha nyingine ya rohoni wanajulikana kama “uzao wa mwanamke”. Sasa ni kwasababu gani wanaitwa hivyo?.
Tukirudi Pale Edeni tunafahamu kuwa mwanadamu wa Kwanza kuumbwa alikuwa ni Adamu. Watu wote tuliopo sasa wakike na wakiume asili yetu ni kutoka kwa huyu mtu mmoja Adamu!. Ambaye anajulikana kama Adamu wa Kwanza. Alikuwa hana Baba wala Mama. Aliumbwa kwa viganja vya Mungu mwenyewe.
Lakini Adamu wa pili hakuumbwa kutoka katika mavumbi ya ardhi kama Adamu wa kwanza. Bali alizaliwa kutoka katika tumbo la Mwanamke. Na huyo si mwingine zaidi ya Yesu Kristo mwokozi wetu. (1Wakorintho 15:45) ambaye alizaliwa kutoka katika Tumbo la mwanamke anayeitwa Mariamu. Hana Baba wa kimwili ndio maana hajaitwa ni uzao wa mwanamume bali wa mwanamke. Ndivyo ilivyompendeza Mungu iwe hivyo! Hakumhusisha mwanamume katika Kumleta Kristo bali alimhusisha mwanamke peke yake!. Kwasasa ile damu safi itakayowaokoa wanadamu isiyo na mawaa, ilipaswa itoke juu, kwa Mungu mwenyewe..
Sasa Bwana Yesu kuzaliwa na Mwanamke Mariamu hakumfanyi, Mariamu au mwanamke mwingine yeyote kuwa wa kipekee sana kuliko watu wengine, na hata kufikia kiwango cha kuhusishwa na mambo ya ibada kama Kanisa Katoliki linavyofanya. Hapana! Mariamu ametumika kama njia tu..Lakini hakuna la ziada hapo, baada ya kumzaa Yesu alihitaji wokovu tu kama wanawake wengine, alihitaji kumwamini, kutubu na ubatizwa na kuishi maisha matakatifu na ya uangalifu kama watu wengine tu.
Ni sawa na Daudi alivyotumika kama njia ya cheo cha ufalme wa Kristo. Lakini hakukumfanya Daudi kuwa mtu wa kipekee sana kuliko wengine. Kwasababu Yesu mahali pengine anajulikana kama MWANA WA DAUDI! Maandiko yanasema hivyo sehemu nyingi na yeye mwenyewe Yesu alisema yeye ni mzao wa Daudi katika Ufunuo .
Ufunuo 22:16 “Mimi Yesu nimemtuma malaika wangu kuwashuhudia ninyi mambo hayo katika makanisa. Mimi ndimi niliye Shina na Mzao wa Daudi, ile nyota yenye kung’aa ya asubuhi”.
Lakini sehemu nyingine pia anasema Daudi alimuita yeye Bwana, sasa iweje yeye awe tena Mwana wake tena.
Mathayo 22:41 Na Mafarisayo walipokusanyika, Yesu aliwauliza, akisema, Mwaonaje katika habari za Kristo?
42 Ni mwana wa nani? Wakamwambia, Ni wa Daudi.
43 Akawauliza, Imekuwaje basi Daudi katika Roho kumwita Bwana, akisema,
44 Bwana alimwambia Bwana wangu, Uketi mkono wangu wa kuume, Hata niwawekapo adui zako Kuwa chini ya miguu yako?
45 Basi, Daudi akimwita Bwana, amekuwaje ni mwanawe?
Au Sasa Tuanze kuweka sanamu za Daudi na kumwomba atuombee na kumwambia salamu Daudi Baba wa Yesu tuombee huko uliko??..Unaona haiingii akilini hata kwa mtoto mchanga wa kiroho anayejifunza biblia kwa mara ya kwanza leo? kama hatuwezi kufanya hivyo kwa Daudi hatupaswi pia kufanya hivyo kwa Mariamu wala mtu mwingine yeyote. Hao wote wametumika kama njia tu ya kupitishia kusudi la Mungu.
Bwana akubariki sana.jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
Shalom.
Biblia inatuambia kipindi kifupi sana kabla ya kurudi kwa Kristo, na kile kipindi chenyewe cha kurudi kwake, kutakuwa na makundi mawili ya watu ambao watakuwa wakimwombolezea, Kundi la kwanza ni Waisraeli, biblia inatuambia hivyo katika Zekaria 12.
Zekaria 12:10 “Nami nitawamwagia watu wa nyumba ya Daudi, na wenyeji wa Yerusalemu, roho ya neema na kuomba; nao watamtazama yeye ambaye walimchoma; nao watamwombolezea, kama vile mtu amwombolezeavyo mwanawe wa pekee; nao wataona uchungu kwa ajili yake, kama vile mtu aonavyo uchungu kwa ajili ya mzaliwa wake wa kwanza.
11 Siku hiyo kutakuwa na maombolezo makuu huko Yerusalemu, kama maombolezo ya Hadadrimoni katika bonde la Megido.
12 Nayo nchi itaomboleza, kila jamaa peke yake; jamaa ya nyumba ya Daudi peke yao, na wake zao peke yao; jamaa ya nyumba ya Nathani peke yao, na wake zao peke yao;
13 jamaa ya nyumba ya Lawi peke yao, na wake zao peke yao; jamaa ya nyumba ya Shimei peke yao, na wake zao peke yao.
14 Jamaa zote zilizosalia, kila jamaa peke yake, na wake zao peke yao.”
Ufunuo 1:7 “Tazama, yuaja na mawingu; na kila jicho litamwona, na hao waliomchoma; na kabila zote za dunia wataomboleza kwa ajili yake. Naam. Amina”.
Lakini tunapaswa tujiulize, ni kwanini biblia inasisitiza sana juu ya hao walimchoma ndio watakaoomboleza, na sio labda hao waliomsulubisha au waliotemea mate, au waliopinga mijeledi au waliomvika taji la miiba, au waliomtukana au waliomuudhi…
Lakini badala yake ni wale waliomchoma?. Lipo jambo la kujifunza hapo, ili na sisi tuwe makini sana tusiwe miongoni mwa kundi hilo ambalo hukumu yake ilishatabiriwa miaka mingi hata kabla ya tukio lenyewe kutokea. Na kurudiwa kuzungumzwa tena miaka mingi baada ya tukio hilo kutokea.
Kama tukirudi kutazama matukio ya pale msalabani, utaona muda mfupi kabla ya Bwana Yesu kuchomwa mkuki ubavuni, mateso yote yalikuwa yameshamalizika. Na Kristo tayari alikuwa ameshakata roho, hivyo hata Roho yake haikuwepo tena pale. Lakini tunaona, wale askari wa kirumi, walipopewa maagizo ya kwenda kuivunja miguu yao wote waliosulibiwa msalabani. Walifanya hivyo kwa wale wafungwa wawili llakini walipofika kwa Bwana wetu YESU Kristo walimwona kama tayari ameshakufa. Hivyo hawakumvunja yeye miguu. Lakini waliamua kufanya jambo lingine ambalo pengine hawakuagizwa. Wakachukua mkuki mrefu, ili wamchome, mpaka kwenye moyo, wakithibitishe kifo chake.
Hivyo wakafanya kama walivyokusudia wakauzamisha ule mkuki kwa nguvu na kupasua mfuko wa maji unaozunguka moyo. Na kupenya mpaka kwenye moyo wa Kristo na kuupasua..Na uthibitisho kuwa ulifika mpaka kwenye moyo ni yale maji na damu vilivyotoka. Ndipo wakawa na uhakika sasa asilimia 100 huyu hata kama alikuwa katika Comma sasa atakuwa amekufa kweli kweli..
Lakini wao waliona ni kawaida, lakini kwa Mungu halikuwa ni jambo la kawaida hata kidogo. Majeraha yote ya nje Kristo aliyotiwa na wale watu Mungu hakuyaangalia, lakini lile jeraha lililoingia ndani tena isitoshe limepenyeza mpaka kwenye moyo wa Kristo. Moyo wa Mungu, hilo hakulisahau mpaka wakati wa mwisho..
Yohana 19:34 “lakini askari mmojawapo alimchoma ubavu kwa mkuki; na mara ikatoka damu na maji”.
Ndugu, maovu unayoyofanya sasahivi ni sawa na unamtia Kristo majeraha ya nje. Upo wakati hayo majeraha yatafika ndani ya moyo wake, na ukishafikia hiyo hatua Mungu hatakusemehe tena, kitakachokuwa kimebakia kwako mbeleni ni maombolezo..Leo hii ukishajiona tu umeachwa katika unyakuo basi ufahamu kuwa umemtia tayari Kristo jeraha hilo. Kinachofuata kwako ni maombolezo na kilio katika ile siku ya kisasi cha Bwana.
Kama ulikuwa hufahamu kalenda ya Mungu, ni kwamba kwasasa hivi tunachokingojea mbele yetu ni Unyakuo tu, dalili zote zimeshatimia, Na Unyakuo huo hautakuwa kwa watu wote, hapana bali utakuwa ni kwetu sisi watu wa mataifa tuliomwamini Kristo na wale wayahudi wachache sana ambao wamezaliwa katika Imani ya kikristo…(hao ndio bibi-arusi wa Kristo)
Lakini kundi la wayahudi wengi waliobakia, Unyakuo hautawahusu. Ukumbuke kuwa kwasasahivi Wayahudi wengi hawamwamini YESU KRISTO kama ni Masihi atayekuja, na hiyo yote Mungu amewapofusha macho kwa makusudi ili sisi watu wa mataifa tumwamini yeye,.Na hiyo itaendelea hadi wakati wetu utakapotia, ambapo utatimia na kitendo cha Unyakuo.
Mungu atawafumbua macho yao, nao watagundua kuwa yule waliyemsulibisha miaka 2000 iliyopita kumbe ndio aliyekuwa masihi wao..Hapo ndipo na wao watakapooanza kuomboleza kama tunavyosoma hapo juu kwenye ule mstari wa Zekaria 12, Israeli nzima kutakuwa kuna maombolezo siku hiyo..Lakini wao Mungu atawapa rehema hivyo katika ile siku ya BWANA watafichwa, kwasababu walipigwa upofu na Mungu makusudi kwa ajili yetu..Hivyo Mungu atawasamehe, na baadaye watakaokolewa na kuingia katika ule utawala wa miaka 1000,…
Lakini sasa kwa haya mataifa mengine yaliyosalia, ambayo yalikosa unyakuo watakachokuwa wanakisubiria mara baada ya ile dhiki kuu ya mpinga-Kristo kuisha itakuwa ni kilio na kusaga meno, wataomboleza kwa vile walivyomchoma Kristo kwa Maisha yao ya kutokutubu walipokuwa wanaishi duniani, hapo ndipo kutakuwa na kilio na kusaga meno, na mara baada ya mapigo hayo tunayoyasoma katika Ufunuo 16, kitakachofuata ni ziwa la moto.
Je! Na wewe leo hii Unazidi kumtia Kristo majeraha?..Hizi ni nyakati za kumalizia ndugu Tubu kwa kumaanisha kabisa kumfuata Kristo, kwasababu siku ya karamu ya mwanakondoo aliyoiandaa kwa ajili yako na mimi mbinguni imekaribia kufika sana, na muda wowote parapanda italia, tutaalikwa kule.Roho anawashuhudia watu wengi, kuwa ile siku ya karamu imeshafika mlangoni. Hivyo Bwana atusaidie tufike ng’ambo yetu salama.
Ubarikiwe. Tafadhali “Share” Ujumbe huu na kwa wengine. Na Bwana atakubariki.jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
Shetani anatolea wapi fedha, angali tunajua Fedha na dhahabu ni mali ya Bwana?.
Jina la Bwana Yesu litukuzwe. Karibu tujifunze Biblia tena.
Tunasoma katika kitabu cha Mwanzo. Baada ya Adamu na Hawa kula matunda ya mti wa ujuzi wa Mema na Mabaya ambayo waliagizwa wasiyale. Macho yao wote wawili yalifumbuliwa na kujijua kuwa wapo uchi.
Mwanzo 3:6 “Mwanamke alipoona ya kuwa ule mti wafaa kwa chakula, wapendeza macho, nao ni mti wa kutamanika kwa maarifa, basi alitwaa katika matunda yake akala, akampa na mumewe, naye akala.
7 Wakafumbuliwa macho wote wawili wakajijua kuwa wa uchi, wakashona majani ya mtini, wakajifanyia nguo”.
Matokeo ya kufumbuliwa macho ni kujisitiri. Na yaliyofumbuliwa ni macho yao ya rohoni, na si ya mwilini.
Baada ya kula tunda walichomwa mioyo na kujigundua kuwa wamefanya makosa makubwa sana. Ulishawahi kufanya kitu ambacho baada ya kumaliza kukifanya Moyo wako ukakuchoma sana! Kwa ulichokifanya?.
Au Ulishawahi kumkosea Mtu Fulani Labda ni boss wako au mkubwa wako mahali Fulani?ambaye sikuzote alikuwa ni mwaminifu kwako, na anakuamini na anakujali na kukupenda sana kwa dhati, wala hajawahi kukufanyia jambo lolote baya?. Halafu baadaye akajua ubaya uliomfanyia na hata baada ya kujua hajakuongelesha chochote.
Unajua huwa Kuna hali Fulani inakuja ambayo unaona aibu hata kukutana naye kumwangalia usoni! Unakuwa unamkwepa kwepa tu muda wote. Unaanza kujihukumu kabla hata ya yeye kukuhukumu.Hata ukikutana naye uso kwa uso unatamani uongee naye kwa dakika chache sana tena ikiwezekana huku umevaa miwani, au huku unaangalia chini. Maana utasikia aibu sio aibu. Usaliti sio usaliti, yaani hali Fulani isiyoelezeka.
Ndicho kilichowatokea wazazi wetu wa Kwanza Adamu na Hawa.
Kwa walichokifanya mbele ya macho ya Mungu iliwafanya wajione wao sio kitu tena, hawana maana tena. Wafiche wapi nyuso zao?. Wafiche wapi viungo vyao mbele za Mungu?. Watawezaje tena kumwangalia Mungu usoni, ambaye hapo kwanza alikuwa anatembea nao kama rafiki? Na anawaamini?..Ni uchungu uliochanganyikana na Aibu.
Suluhisho lililobaki ni kujificha tu mbele ya uso wa Mungu, na kutafuta njia ya kumkwepa kwepa. Ndio unaona sasa wakaamua kutengeneza nguo kwa majani ya mtini. Kumbuka hawakushona nguo kwasababu wanaoneana aibu wao kwa wao. Hapana wao walikuwa hawaoneani aibu. Waliyekuwa wanamwonea aibu ni Mungu.
Na pia nguo hizo za nyasi walizojitengenezea hazikufunika tu sehemu zao za siri, bali zilifunika mwili mzima mpaka kichwa. Kwasababu ni Aibu!. Utawezaje kuonyesha kifua chako tena mbele za Mungu? Uso tu shida, si zaidi mgongo au kifua au mapaja?. Ndio maana waliendelea mpaka kujificha katikati ya vichaka!. Kujishonea nguo za nyasi peke yake waliona haitoshi.
Ndugu sasahivi katika nyakati hizi tupo katika Bustani ya Mungu inayoitwa Neema. Bustani hii ni Bustani ya Yesu Kristo, ambayo anatembea na sisi kama Rafiki. Kama Mungu alivyotembea na Adamu pale Edeni.
Yohana 15:14 “Ninyi mmekuwa rafiki zangu, mkitenda niwaamuruyo.
15 Siwaiti tena watumwa; kwa maana mtumwa hajui atendalo bwana wake; lakini ninyi nimewaita rafiki; kwa kuwa yote niliyoyasikia kwa Baba yangu nimewaarifu”.
Neema ni kitu cha ajabu sana, Maana unaweza kupata chochote utakacho, kwa jina la Yesu, Msamaha wa dhambi unapatikana ndani ya Neema, uponyaji, Baraka n.k. Ni kama Edeni tu! Kila kitu kilikuwa kinapatikana pale bila nguvu nyingi.
Lakini Neema hii tulionayo sisi haitadumu milele maandiko yanasema hivyo. Wakati huu ambapo Yesu kwetu ni Rafiki. Kuna wakati utafika huyu huyu Yesu tunayempenda sasa na kumwona ni rafiki, Na kuufurahia wema wake atageuka na kuwa Mhukumu.
Wakati huo wewe unayeidharau injili sasa macho yako yatafumbuliwa na utasema!.. Nifiche wapi uso wangu huu na aibu hii kwa kuidharau Neema niliyokuwa nimepewa?..Hutatamani hata kusimama mbele za Bwana Yesu, ambaye leo hii anatembea kwako kama rafiki. Ambaye unaweza ukajiamulia chochote tu na asikueleze.
Adamu na Hawa hawakutamani hata kuuona uso wa Mungu kadhalika Yuda baada ya kumsaliti Bwana Yesu, yeye naye yalifumbuliwa macho yake na kujiona yupo uchi katika roho, aliona ni heri akajinyonge kuliko hata kwenda kumtazama pale msalabani. Akasema
Mathayo 27:3 “Kisha Yuda, yule mwenye kumsaliti, alipoona ya kuwa amekwisha kuhukumiwa, alijuta, akawarudishia wakuu wa makuhani na wazee vile vipande thelathini vya fedha, akasema, Nalikosa nilipoisaliti damu isiyo na hatia.
4 Wakasema, Basi, haya yatupasani sisi? Yaangalie haya wewe mwenyewe.
5 Akavitupa vile vipande vya fedha katika hekalu, akaondoka; akaenda, akajinyonga”.
Adamu na Hawa walijuta na hivyo kuishia Hukumu kubwa kama ile mpaka sisi vitukuu vya vitukuu tunashiriki laana yao.
Je! Itakuwaje siku ile macho yako yatakapofumbuliwa mbele ya kiti cha Hukumu? Ni majuto ya milele katika ziwa la moto, wala usifikiri siku ile utaona kama umeonewa! Utakiri kwamba ni kweli ulikosa na unastahili adhabu! Kama Yuda alivyokiri.
Wakati huu ambapo utukufu wa Neema ya Mungu upo. Wakati Kristo ni rafiki. Ushikilie wokovu, usisikilize uongo wa shetani, leo hii unaokuambia kunywa pombe sio shida, unaokuambia kuvaa vimini sio shida, kuvaa suruali kwa mwanamke sio shida! Kuishi na mtu ambaye hamjafunga naye ndoa sio shida!..Ukisikiliza huo uongo na kuutii ni kweli sasa hutaona kwamba ni shida sasa. Lakini siku ile utajuta sana macho yako yatakapofumbuliwa.
Waebrania 10:29 “Mwaonaje? Haikumpasa adhabu iliyo kubwa zaidi mtu yule aliyemkanyaga Mwana wa Mungu, na kuihesabu damu ya agano aliyotakaswa kwayo kuwa ni kitu ovyo, na kumfanyia jeuri Roho wa neema?
30 Maana twamjua yeye aliyesema, Kupatiliza kisasi ni juu yangu, mimi nitalipa. Na tena, Bwana atawahukumu watu wake.
31 Ni jambo la kutisha kuanguka katika mikono ya Mungu aliye hai”.
Ikiwa hujaokoka. Unapaswa uokoke sasa hivi. Na si kesho, kwasababu saa ya wokovu ni sasa. Hapo ulipo jitenge dakika chake peke yako, Omba toba ya dhati mbele ya Mungu Baba, mwambie akusamehe makosa yako yote uliyoyafanya huko nyuma na unayoyafanya sasa. Na kwamba hutaki kuyafanya tena. Na kisha baada ya toba hiyo, Amani Fulani ya kiMungu itakuja ndani yako. Ambayo utahisi kama kuna mzigo Fulani umeondoka. Amani hiyo ni uthibitisho kwamba umesamehewa.
Hivyo kuihifadhi hiyo amani shetani asiiibe, nenda katafute mahali wanapobatiza ubatizo sahihi wa maji tele na kwa jina la Yesu Kristo. Ubatizwe hapo kama hujabatizwa. Na kama ulishabatizwa hivyo kwa usahihi huna haja ya kubatizwa tena.
Utaanza kuona Roho Mtakatifu aliyeingia ndani yako akiyatengeneza maisha yako upya kwa namna ambayo hatuwezi tukaelezea hapa. Wewe mwenyewe utaona. Kikubwa hapo ni kumkubali tu Kristo tu katika Maisha yako na kufuta yote anayokulekeza, yaliyosalia yeye mwenyewe atayashughulikia.
Bwana akubariki.jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo;
Nifanyaje ili nijue kuwa uamuzi ninaokwenda kuchagua kufanya ni mapenzi ya Mungu?
DHAMBI ILIYOMKOSESHA SHETANI:
KWANINI DAUDI ALIKUWA NI MTU ALIYEUPENDEZA MOYO WA MUNGU?
JISHUSHE ILI MUNGU AKUHUDUMIE.
Ni kitu cha kushangaza jinsi injili ya Kristo, Bwana wetu inavyogeuzwa leo hii kutoka katika kitu cha kutolewa bure hadi kuwa kitu cha kutolewa kwa masharti,.Tunaweza tukadhania ni ustaarabu mzuri kufanya hivyo lakini kibiblia huo haukuwa mpango wa Kristo tangu zamani alipowaita mitume wake..kwasababu ni jambo linalozuia injili ya Kristo kusonga mbele. Na leo tutaona ni kwa namna gani.
Embu tafakari kwa utulivu jambo hili walilolifanya mitume, na majibu Bwana YESU aliyowapa,
Marko 9:38 “Yohana akamjibu, akamwambia, Mwalimu, tulimwona mtu akitoa pepo kwa jina lako, ambaye hafuatani nasi; tukamkataza, kwa sababu hafuatani nasi.
39 Yesu akasema, Msimkataze, kwa kuwa hakuna mtu atakayefanya mwujiza kwa jina langu akaweza mara kuninenea mabaya;
40 kwa sababu asiye kinyume chetu, yu upande wetu”.
Mitume walipomwona mtu huyu anatenda kazi zile zile wanazozifanya wao, wanatumia jina lile lile wanalolitumia wao, tunaweza kusema pia anawabatiza watu vilevile kama wanavyowabatiza wao, anafufua wafu vilevile kama wanavyofufua wao, badala ya wao kumfurahia na kumchukua wafanye naye kazi pamoja, kinyume chake wanamkemea na kumkataza kwamwe asikae kufanya kitu kama hicho tena, pengine walimtisha na kuahidi kumshitaki endapo atarudia kutumia jina hilo bila idhini yao…Na hiyo yote ni kwasababu moja tu, kwamba HAFUATANI NAO basi! Hakuna kingine, wala hakuna ubaya wowote waliuona ndani yake…ni kwasababu tu HAFUATANI NAO! Embu jaribu kufikiria mtu yule alipotoka pale alivunjika moyo kiasi gani..ule moto uliokuwa ndani yake ulizimishwa ghafla kwa kiasi gani, alikuwa anahubiri injili kwa kujifichaficha akiogopa labda pengine wale watu watamwona tena na kumkamata na kumpeleka kwa kadhi.
Na Zaidi ya yote alitegemea pengine hao Mitume ndio wangekuwa wakwanza kumsapoti lakini kinyume chake wakawa wakwanza kumpinga.
Hata leo hii, Hicho ndio kikwazo cha watumishi wengi wa Mungu, wapo watu wengi wanaotamani kumhubiri Kristo kwa mafundisho yao, au vitabu vyao, au nyimbo zao, lakini wanatishwa na vikwazo vya namna hiyo, wanaogopa wakifanya tu, watakamatwa na kuambiwa ni nani kakupa ruhusu ya kusambaza hiki au kile.
Wameiwekea injili hati miliki kwamba mtu huwezi kufundisha wanachokifundisha wao, mpaka upewe kibali fulani kutoka kwao, huwezi kuziimba nyimbo zao mahali fulani mpaka upewe kibali fulani kutoka kwao, ili ulipie kwanza kiwango fulani cha fedha..Injili ya Kristo nayo imegeuzwa na kuwa kama staili ya kibiashara hivi, kwamba mtu fulani amegundua aina yake ya mafundisho basi hataki mwingine aibe aifundishe sehemu nyingine, ameimba nyimbo fulani, hataki mwingine aiimbe mahali pengine kwa utukufu wa Mungu..lengo tu ni ili nyimbo yake isichuje haraka au aitwe yeye aimbe ili apate faida kidogo..Ndivyo ilivyo sasa hivi.
Kipindi fulani nyuma, kuna ndugu nilimuhubiria akakata shauri la kuokoka, hivyo akawa anahitaji abatizwe pia, kwa kuwa mkoa aliokuwepo ni mbali kidogo na mimi nilipo ikanibidi nimtafutie kanisa la kiroho liliokaribu naye abatizwe na adumu katika fundisho la pale, lakini nilipopiga simu na mhudumu mmojawapo wa kanisa alipokea, ili nimkabidhishe huyo mtu kwake, kuzungumza naye tu maneno machache na kugundua mimi sio mshirika wa makanisa yao, akasema mimi ni ndugu wa uongo, ni nani aliyenipa ruhusu hiyo, hawakutaka kusikia habari yangu, hata na huyo kondoo ambaye alikuwa anatafuta malisho..Nilihuzunika na kushangaa sana,..kwani hawakuangalia faida ya Kristo bali waliangalia je kama hichi kitu kinatoka katika jumuiya yao ya kidini kama mitume walichokuwa wanajaribu kukifanya.
Vitabu au Makala za Kikristo tunazozichapishwa, tunachopaswa kuzuia tu kwa wale wanaofanya na kuuza kwa biashara, lakini kama ni mtu ameona upo ujumbe mzuri ndani yake ambao unaweza kuwabadilisha wengine, hivyo akaamua kwenda kuchapisha Makala hizo nyingi na kwenda kuzitoa bure kwa watu wengine bila hata ya kukueleza, au kupata idhini yako, wewe unakwazika nini katika hilo? wewe hofu yako ni nini? Kwani kazi hiyo ni yako au ya Kristo?. Kwanini kila kitu unawaza kukiwekea mipaka na vizuizi, hujui kuwa kazi ya Kristo inasimama kwa ajili yako. Mwingine akisikia kuna mtu kahubiri mahali pengine kitu alichokihubiri yeye na hajatajwa jina anapata wivu?.
Kwanini upate wivu? Kuna umuhimu gani wa kukutaja wewe kama kweli una Nia ya Kristo ndani yako? Unapaswa ufurahi kwasababu ulichokizaa wewe kimekwenda kuzaa vingine vingi, sasa hiyo si ni faida? Wengine mpaka wanawapa masharti wanaowahubiria kwamba watakapohubiri mafundisho yao mahali pengine wawataje!.
Yule mtu aliyekuwa anatenda miujiza kwa jina la YESU alitambua kabisa kuwa Kristo mwenyewe yupo duniani, na kwamba angetaka kwenda kumwomba ruhusa angekwenda, lakini yeye hakuona hata ulazima wa kumwomba Ruhusa mwenye jina lenyewe badala yake aliliondoka kimya kimya na kwenda kuuendeleza ufalme,..Na Kristo hakumkemea kwa hilo wala kumwita kutaka kumjua, aliona ni sawa tu..aendelee..
Iweje sisi ambao hata hatumwoni Kristo tuwazuie wengine wasimtangaze Kristo kwa kazi zetu?. Jitafakari vizuri wewe unayejiita kiongozi wa dini, wewe unayejiita mchungaji, wewe unayejiita mwalimu, wewe unayejiita mwandishi, wewe unayejiita MWIMBAJI WA NYIMBO ZA INJILI wewe unayejiita mwinjilisti, wewe unayejiita mshirika…
Usiwe kikwazo cha injili ya Kristo kuhubiriwa.
Shalom.jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
HATARI YA KUHUBIRI INJILI TOFAUTI NA ILIYOANDIKWA KWENYE BIBLIA.
KIWANGO CHA TATU CHA IMANI.
SADAKA YA MALIMBUKO.
Yeshuruni ni nani katika biblia?
NINI MAANA YA KUSAGA MENO?
Kusaga meno ni kitendo cha kung’ata meno kwa nguvu kutokana na maumivu fulani au uchungu fulani. Kwamfano mtu aliyejikata na kisu au kujikwaa kwenye kidole utaona atang’ata meno kwa nguvu kutokana na maumuvi anayoyasikia au uchungu au hasira fulani (Soma Matendo 7:54).
Na hata wakati mwingine mpaka kung’ata huku yanasuguana. Sasa kitendo hicho ndicho kinachoitwa kusaga meno.
Katika biblia kuna sehemu kadha wa kadha zimezungumzia tendo hilo. Kwamfano utaona Bwana Yesu alipozungumzia juu ya mateso yaliyopo Jehanum hakuacha kuhusisha tendo la usagaji wa meno. Ikifunua kuwa Jehanamu sio mahali pa raha. Bali pa mateso makali sana.
Mathayo 13:41 “Mwana wa Adamu atawatuma malaika zake, nao watakusanya kutoka katika ufalme wake machukizo yote, na hao watendao maasi,
42 na kuwatupa katika tanuru ya moto, ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno”.
Mathayo 25:30 “Na mtumwa yule asiyefaa, mtupeni mbali katika giza la nje; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno”.
Mistari mingine inayofanana na hiyo, inayozungumzia kitendo cha kusaga meno ni pamoja na Zaburi 37:12, Mathayo 8:12, Mathayo 13:50. Mathayo 22:13, 25:30, Marko 9:18 na Luka 13:28.
Hiyo yote inalenga kutuonyesha ukali wa mateso yaliyopo Jehanum. Kwamba si sehemu nzuri, kutakuwa na maumivu makali na mateso kwa wale wote ambao hawajampokea Kristo na waliorudi nyuma.
Kama hujampa Yesu Kristo maisha yako, ni vyema ukafanya hivyo kabla muda wako wa kuishi duniani haujaisha. Unachopaswa kufanya ni kutubu tu mahali ulipo. Unatubu dhambi zako zote kwa kumaanisha kuziacha, na kisha unatafuta ubatizo sahihi wa maji tele na kwa jina la YESU KRISTO kulingana na Matendo 2:38. Kwa ajili ya kukamilisha wokovu wako.
Na kama ulishabatizwa katika vigezo hivyo hapo juu basi hauhitaji kubatizwa tena. Na mwisho kabisa Bwana mwenyewe atakupa kipawa cha Roho wake Mtakatifu atakayekusaidia kushinda dhambi.
Bwana akubariki.jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
usizitegemee nguvu zako kukusaidia katika jambo lolote!
Jina la Bwana Yesu Kristo libarikiwe. Karibu tujifunze Biblia, Neno la Mungu ambalo ni Taa iongozayo miguu yetu na mwanga wa njia zetu (Zab.119:105).
Leo tutajifunza kwa ufupi, ni jinsi gani Bwana hapendezwi na sisi kuzitegemea nguvu zetu wenyewe, au kuwategemea wanadamu katika matatizo yanayotukabili. Au kutegemea vitu tulivyojiwekezea.
Tutajifunza kwa kumtazama Mtu anayeitwa Daudi. Ambaye wakati Fulani alikengeuka kidogo na kutaka kuzitegemea nguvu zake mwenyewe badala ya kumtegemea Mungu. Jambo ambalo lilimchukiza sana Mungu..Ingawa aliwahi kwenda kutubu lakini tayari lilikuwa limeshaleta madhara makubwa sana katika Taifa la Israeli.
Kama ni msomaji mzuri wa Biblia utakumbuka kuna wakati Mfalme Daudi wazo lilimwingia la kwenda kuwahesabu watu. Na kama utakumbuka jambo hilo lilimchukiza sana Mungu na kusababisha watu wengi kufa Israeli. Ingawa jambo hilo Mungu aliliruhusu makusudi ili kuwalipiza kisasi wana wa Israeli kwa makosa yao. Lakini bado halikuwa mpango kamili wa Mungu.
Tunasoma Daudi alikwenda kuwahesabu watu wote na kupata jumla ya mashujaa laki 8 wenye kufuta upanga katika Israeli na mashujaa laki 5 katika Yuda..Hivyo jumla ya mashujaa waliokuwa ni milioni moja na laki tatu.(1,300,000) Hiyo ni idadi kubwa sana ya watu.
2Samweli 24:1 “Tena hasira ya Bwana ikawaka juu ya Israeli, akamtia Daudi nia juu yao, akisema, Nenda, ukawahesabu Israeli na Yuda.
2 Basi mfalme akamwambia Yoabu, jemadari wa jeshi la askari, waliokuwa pamoja naye, Zunguka sasa katikati ya kabila zote za Israeli, tangu Dani mpaka Beer-sheba, mkawahesabu watu, nipate kujua jumla ya hao watu………..”
8 Nao walipokwisha kuzunguka nchi yote, wakaja Yerusalemu mwisho wa miezi kenda na siku ishirini.
9 Naye Yoabu akamtolea mfalme jumla ya hesabu ya watu; nao walikuwa wa Israeli mashujaa wenye kufuta panga mia nane elfu; nao wa Yuda walikuwa watu mia tano elfu.
10 Ndipo moyo wake Daudi ukamchoma baada ya kuwahesabu hao watu. Naye Daudi akamwambia Bwana, Nimekosa sana kwa haya niliyoyafanya; lakini sasa, Ee Bwana, nakusihi uuondolee mbali uovu wa mtumishi wako; kwani nimefanya upumbavu kabisa.
11 Na Daudi alipoondoka asubuhi, neno la Bwana likamjia nabii Gadi, mwonaji wake Daudi, kusema,
12 Nenda, ukanene na Daudi, Bwana asema hivi, Nakuwekea mambo matatu; katika haya uchague moja, nikutendee hilo.
13 Basi Gadi akamwendea Daudi, akamweleza, akamwambia, Basi, miaka saba ya njaa ikujie katika nchi yako? Au miezi mitatu ukimbie mbele ya adui zako, huku wakikufuatia? Au siku tatu iwe tauni katika nchi yako? Fanya shauri sasa, ufikiri, ni jawabu gani nimrudishie yeye aliyenituma.
14 Naye Daudi akamwambia Gadi, Nimeingia katika mashaka sana; basi sasa na tuanguke katika mkono wa Bwana; kwa kuwa rehema zake ni nyingi; wala nisianguke katika mkono wa wanadamu”.
Sasa ukichunguza Nia ya Daudi hasa haikuwa kujua idadi ya watu wote waliokuwemo Israeli, bali utagundua kuwa Nia yake kuu ilikuwa ni kujua idadi ya wanajeshi au mashujaa alionao wa vita waliokuwepo kwenye ufalme wake wote. Kumbuka Daudi alikuwa ni mtu wa Vita. Muda wote alikuwa amezungukwa na maadui hivyo alitaka kwenda kuwahesabu wanajeshi wake ili ajiwekee matumaini katika jeshi hilo.
Hapo kabla Daudi alikuwa hajui anao idadi ya wanajeshi wangapi, alikuwa anamtegemea tu Mungu asilimia 100, ikitokea vita anaita idadi ya wanajeshi waliopo, bila kujali watakuwa ni wachache kiasi gani ukilinganisha na maadui zao kwasababu Bwana ndiye aliyekuwa jemedari wake.
Zaburi 20: 7 “Hawa wanataja magari na hawa farasi, Bali sisi tutalitaja jina la Bwana, Mungu wetu.
8 Wao wameinama na kuanguka, Bali sisi tumeinuka na kusimama.
9 Bwana, umwokoe mfalme, Utuitikie siku tuitayo”.
1Samweli 17: 45 “Ndipo Daudi akamwambia yule Mfilisti, Wewe unanijia mimi na upanga, na fumo, na mkuki, bali mimi ninakujia wewe kwa jina la Bwana wa majeshi, Mungu wa majeshi ya Israeli uliowatukana.
46 Siku hii ya leo Bwana atakuua mkononi mwangu, nami nitakupiga, na kukuondolea kichwa chako, nami leo nitawapa ndege wa angani na wanyama wa nchi mizoga ya majeshi ya Wafilisti, ili kwamba dunia nzima wajue ya kuwa yuko Mungu katika Israeli.
47 Nao jamii ya watu wote pia wajue ya kwamba Bwana haokoi kwa upanga wala kwa mkuki; maana vita ni vya Bwana, naye atawatia ninyi mikononi”
Lakini Daudi Mtu ambaye alikuwa hategemei majeshi kumwokoa. Sasa hapa anaanza kujitumainisha katika hayo. Alikuwa hategemei mikuki, panga wala fumo sasa anaanza kuvitegemea kwa kutaka kujua idadi ya wanajeshi walioshika upanga. Amesahau kuwa miaka yote Mungu hakuwahi kumwokoa kwa wingi wa jeshi au silaha alizonazo.
Hiyo ikawa ni dhambi kubwa sana ikasababishia Mungu kuyapunguza hayo majeshi yake aliyoyahesabu, kwa kuleta Tauni, wakafa watu elfu 70. Na tena hapo ni kwasababu tu ya Rehema za Mungu kuwa nyingi, endapo Bwana asingeachilia Rehema zake. Watu milioni kadhaa wangekufa. Na hayo majeshi aliyojitumainia nayo yatakuwa wapi?…Usizitegemee nguvu zako.
Ndio maana Bwana Yesu alisema mfano huu katika kitabu cha Luka.
Luka 12:19 “Kisha, nitajiambia, Ee nafsi yangu, una vitu vyema vingi ulivyojiwekea akiba kwa miaka mingi; pumzika basi, ule, unywe, ufurahi.
20 Lakini Mungu akamwambia, Mpumbavu wewe, usiku huu wa leo wanataka roho yako! Na vitu ulivyojiwekea tayari vitakuwa vya nani?
21 Ndivyo alivyo mtu ajiwekeaye nafsi yake akiba, asijitajirishe kwa Mungu”.
Je! Tumaini lako liko wapi? Kwenye mali ulizo nazo?. Au hazina ulizo nazo, au vitega uchumi vyako?. Au watoto wako?, au idadi ya wafanyakazi ulio nao? Au Bwana?. Usianze kusema sasa nina mali nyingi au fedha nyingi au salio kubwa kwenye akaunti yangu basi kesho yangu itakuwa safi, kesho yangu itakuwa ya ushindi, bali useme Ninaye Bwana moyoni mwangu kesho yangu itakuwa safi, kesho yangu itakuwa ya Baraka na ya mafanikio haijalishi niacho hiki au sina, kwasababu Bwana ndiye ngome yangu na jabali langu.
Kama ni Bwana ndiye tegemeo lako, basi umechagua fungu jema ambalo hutakuja kujutia kamwe! usizitegemee nguvu zako..Wakati wengine wanataja hazina zao wewe utalitaja jina la Bwana wa Majeshi, wakati wengine wanatumaini vitu vya ulimwengu huu, wewe unamtumainia Bwana.
Lakini kama humtumainii Bwana na unajitumainisha katika vitu ulivyowekeza hapa duniani. Kumbuka Yaliyompata Daudi yanaweza kukupata na wewe. Watu aliojitumainia Daudi kwa kwenda kuwahesabu walipunguzwa kwa Tauni ya siku tatu tu. Kadhalika Bwana atasambaratisha kila kitu unachojitumainisha kwacho leo hii. Atapunguza mali ulizonazo, atapunguza hata kile kidogo ambacho ulikuwa umeshakianza. Kwasababu yeye anasema ni Mungu mwenye wivu. Hawezi kuruhusu Vitu vya Ulimwengu huu vichukue nafasi yake yeye. Usizitegemee nguvu zako.
Bwana akubariki sana. Kama hujampa Yesu Kristo maisha yako, ni vyema ukafanya hivyo leo. Kwasababu saa ya wokovu ni sasa na si Kesho. Tubu kwa kumaanisha kuacha dhambi na Bwana atakusamehe na kukuokoa.
Maran atha! jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
UNYAKUO.
Ni sahihi kumuita Mariamu mama wa Mungu?
JISHUSHE ILI MUNGU AKUHUDUMIE.
TIMAZI NI NINI
Je! Kuna umuhimu wowote wa kujifunza Neno kila siku?
Unajua ni kwasababu gani leo hii tunaomwona Mtume Paulo ni mtu aliyekuwa amejaa mafunuo ya ndani kabisa yamuhusuyo Mungu na YESU KRISTO kiasi cha Mungu kufikia hatua ya kuyafanya mafundisho yake kuwa muhamala mkuu wa kanisa hadi sasa, ni kwasababu mtume Paulo hakuwa mtu wa kuchoka kusoma na kujifunza neno kila iitwapo leo,..Hakuwa mtu wa kulizoelea Neno la Mungu…
Tunaweza kuona mpaka wakati wa kukaribia kufa kwake, wakati anampa Timotheo maagizo ya kuliongoza na kulichunga kanisa, ameshakuwa mzee kabisa amebakisha kipindi kifupi sana cha kuishi, lakini bado anamwagiza Timetheo ampelekee vitabu vya nyaraka za maandiko avisome, kwasababu alijua bado anayo mengi ya kujifunza..
2Timotheo 4:6 “Kwa maana, mimi sasa namiminwa, na wakati wa kufariki kwangu umefika.
7 Nimevipiga vita vilivyo vizuri, mwendo nimeumaliza, Imani nimeilinda;
8 baada ya hayo nimewekewa taji ya haki, ambayo Bwana, mhukumu mwenye haki, atanipa siku ile; wala si mimi tu, bali na watu wote pia waliopenda kufunuliwa kwake.
……… 13 Lile joho nililoliacha kwa Karpo huko Troa, ujapo ulilete, na vile vitabu, hasa vile vya Ngozi’
Paulo mtu aliyehubiri Injili tangu ujana wake, Aliyekutana na Yesu uso kwa uso, alifunuliwa siri za ndani kabisa ambazo hata Mitume wengine hawakufunuliwa wakati wakiwa na Bwana Yesu hapa duniani.,..Aliyenyakuliwa mpaka mbingu ya tatu, na kuonyeshwa mambo ambayo hayaelezeki kwa namna ya kibinadamu, lakini bado mtu kama huyo hakuchoka kujifunza neno mpaka siku ya kufa kwake…Bado aliendelea kusoma kwa bidii, akitazamia Mungu kumfunulia mambo mpya ambayo hakuwahi kuyafahamu..Anamwambia Timotheo, Ujapo uvilete vile vitabu vya ngozi..
Hii inatufundisha kuwa kupokea mafunuo ni kitendo endelevu, hatupaswi kuridhika tu na kile tunachokifahamu au tulichopewa kukijua sasa na Mungu bali kila siku tunapaswa tumwombe Mungu azidi kutufumbua macho Zaidi na zaidi katika Neno lake, na kutia bidi katika kusoma Neno lake.
Ndicho alichokifanya Danieli, yeye mwanzoni kabisa ukisoma ile sura ya pili ya kitabu cha Danieli, utaona Mfalme Nebukadneza aliota ndoto ya ile sanamu kubwa yenye kichwa cha dhahabu, kifua cha fedha, kiuno cha shaba na miguu ya chuma..Ambayo Danieli alipewa tafsiri yake inayohusiana na falme 4 zitakazotawala ulimwenguni mpaka mwisho wa dunia..
Lakini utaona Danieli hakuridhika na ufunuo ule peke yake, utaona kwenye sura ya 7 anaonyeshwa mambo ya ndani Zaidi kuhusiana na zile falme 4, ambayo hakufunuliwa katika ile njozi ya kwanza ya Mfalme Nebkadneza, alionyeshwa tabia ya zile falme jinsi zitakavyosimama na kuanguka…Ukiendelea kusoma sura ya 8 utaona tena anaelezwa mambo ya ndani Zaidi jinsi falme zile zitakavyokuwa..Ukizidi kusoma kuanzia ile sura ya 11 hadi ya 12 sasa Ndivyo utakavyooona jinsi Danieli anafunuliwa mambo yote kwa uwazi anaelezwa tukio baada ya tukio kikitoka hichi kinafuata hichi, kuanzia ule ufalme aliokuwepo mpaka ule unaomfuata baada yake…
Ndipo Danieli akaelewa sasa, na ukisoma pale utaona alitamani kuendelea kufahamu Zaidi juu ya matukio ya siku za mwisho, lakini malaika yule alimwambia aache hayo si ya wakati wake bali ayatie muhuri yatafunuliwa siku za mwisho..Ni wazi kuwa kama asingeambiwa vile basi Danieli angetusaidia kujua kila tendo litakalotokea katika siku zetu hizi za mwisho.
Lakini kama angesema Ah! Huu ufunuo Mungu atakaonipa wa ziada kuhusu ndoto ya Mfalme Nebukadneza. Ule alionipa unatosha hakuna haja ya kujifunza neno na kumwomba Mungu anifunulie Zaidi basi Danieli angebakia kujua tu zipo falme 4 zitakazotawala mpaka mwisho wa dunia basi, lakini habari za chukizo la uharibifu asingezijua, habari za hukumu ya mwisho asingezijua, habari za kuja kwa masihi asingezijua, habari za Kristo kusulibiwa asingezijua, habari za majuma sabini asingejua, habari za dhiki kuu asingezijua…Endapo tu angeridhika na hali ile ile ya ufunuo aliyopewa. Na hata ukizidi kusoma utagundua Danieli alikuwa mtu msomaji sana wa vitabu, mpaka akafikia kugundua miaka Israeli waliyotabiriwa kukaa Babeli.
Danieli 9:2 “katika mwaka wa kwanza wa kumiliki kwake, mimi Danielii, kwa kuvisoma vitabu, nalifahamu hesabu ya miaka, ambayo neno la Bwana lilimjia Yeremia nabii, ya kuutimiza ukiwa wa Yerusalemu, yaani, miaka sabini”
Vivyo hivyo na sisi Mungu atusaidie tujifunze, juu ya mambo haya, tusiridhike katika hali tuliyopo, tukaona kwamba kwasababu tumeisoma biblia nzima basi hakuna jambo jipya tunaweza kujifunza tena, kwasababu tumeshausoma mstari huu au ule, basi huyu muhubiri hawezi kutuambia tena jambo jipya hapo..Neno la Mungu halina ubobeaji..
Mungu anataka sisi tukue kifikra, tukue kiimani, vilevile tukue kiroho, kutoka katika hali ya uchanga hadi hali ya utu uzima kuelewa mambo ya ndani kabisa ya rohoni.. Mafumbo magumu na hiyo yote ni kama tutakuwa tayari kujifunza neno kila siku maneno ya Mungu pasipo kuyazoelewa.
Mungu akubariki sana. Ikiwa bado hujaokoka, nadhani utakuwa unafahamu kuwa hizi ni siku za mwisho, na kwamba moja ya hizi siku parapanda italia, na wafu watafufuliwa, na kuungana na watakatifu waliopo duniani na kwa pamoja kwenda kumlaki Bwana YESU mawingu. Kuelekea katika karamu ile ya mwanakondoo, ambayo Mungu aliindaa tangu enzi na enzi kwa wale waliookolewa..Sasa utajisikiaje ikiwa wewe utakosekana katika karamu hiyo? Mimi sitaki kukosa wewe je?..Utajisikiaje umebaki huku duniani kwenye dhiki ya mpinga kristo halafu baada ya hapo uishie kwenye ziwa la moto?..Angalia jinsi Mungu alivyotupenda, kutupa YESU KRISTO ili atuokoe sisi bure kwa damu yake.
Hivyo anakuita na wewe ayaokoe Maisha yako. Tubu popote pale ulipo, ukabatizwe kisha atakupa amani ambayo utadumu nayo hadi siku ya kuja kwake.
Ubarikiwe sana.jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
RUDIA, TENA NA TENA KUMWOMBA MUNGU USIKATE TAMAA.
TABIA YA KIPEKEE USIYOIJUA KUHUSU NENO LA MUNGU.
JISHUSHE ILI MUNGU AKUHUDUMIE.
UNATAKA KUBARIKIWA? BASI USIKWEPE GHARAMA ZAKE.
Ni sahihi kumuita Mariamu mama wa Mungu?
Watu wengi wanajiuliza Roho Mtakatifu ni nani? Jibu rahisi ni kuwa Roho Mtakatifu ni Roho ya Mungu, Mungu anayo Roho kama vile mwanadamu alivyo na roho, hakuna mwanadamu yeyote asiye na roho.
Na Biblia inasema katika Mwanzo 1:26 kwamba Mwanadamu aliumbwa kwa mfano na sura ya Mungu. Ikiwa na maana kuwa kama mwanadamu ana nafsi halikadhalika Mungu naye anayo nafsi, na kama mwanadamu anayo roho vilevile na Mungu naye anayo Roho. Kwasababu tumeumbwa kwa sura yake na kwa mfano wake. Na kama vile mwanadamu anao mwili halikadhalika Mungu naye anao mwili.
Na Mwili wa Mungu si mwingine zaidi ya ule uliodhihirishwa pale Kalvari miaka 2000 iliyopita. Nao ni mwili wa Bwana Yesu Kristo, hivyo Yesu Kristo ndiye Mungu mwenyewe aliyedhihirishwa katika Mwili. Hivyo aliyemwona Yesu amemwona Mungu (Yohana 14:8-10)
1Timotheo 3:16 “Na bila shaka siri ya utauwa ni kuu. Mungu alidhihirishwa katika mwili, Akajulika kuwa na haki katika roho, Akaonekana na malaika, Akahubiriwa katika mataifa, Akaaminiwa katika ulimwengu, Akachukuliwa juu katika utukufu”.
Huyo ni Yesu anayezungumziwa hapo.
Na kadhalika roho iliyokuwepo ndani ya Mwili wa Bwana Yesu Kristo ndio Roho ya Mungu na ndiye ROHO MTAKATIFU MWENYEWE. Tunalithibitisha hilo katika kitabu cha.
Matendo 16:6 “Wakapita katika nchi ya Frigia na Galatia, wakikatazwa na Roho Mtakatifu, wasilihubiri lile neno katika Asia.
7 Walipofika kukabili Misia wakajaribu kuenda Bithinia, lakini Roho wa Yesu hakuwapa ruhusa,
8 wakapita Misia wakatelemkia Troa”.
Sasa utauliza kama Roho wa Yesu ndiye Roho Mtakatifu iweje mahali pengine Bwana Yesu anaonekana amejaa Roho Mtakatifu?. Na mahali pengine anaonekana Roho Mtakatifu akishuka juu yake?
Jibu ni kwamba, Roho wa Mungu hana mipaka kama roho zetu sisi wanadamu zilivyo na mipaka, sisi wanadamu Mungu alivyotuumba roho zetu mipaka yake ni katika miili yetu.
Haziwezi kutenda kazi nje ya fahamu zetu au miili yetu.Haiwezekani niongee na wewe hapa na wakati huo huo roho yangu ipo China. Hilo haliwezekani kwetu sisi wanadamu, isipokuwa kwa Mungu linawezekana. Roho wake anauwezo wa kuwa kila mahali, ndio maana wewe uliopo Tanzania utasali muda huu na mwingine aliyepo China atasali na mwingine aliyeko Amerika atakuwa anamwabudu Mungu muda huo huo na wote Roho Mtakatifu akawasikia na kuwahudumia kila mtu kivyake. Huyo huyo anao uwezo wa kuwepo mbinguni, na duniani ndani ya Mwili wa Bwana Yesu na wakati huo huo kuzimu, hakuna mahali asipofika.
Ndio maana utaona alikuwa ndani ya Kristo, na bado akashuka juu ya Kristo, na akaachiliwa juu yetu siku ile ya Pentekoste.
Hiyo ndiyo tofauti ya Roho wa Mungu na roho ya mwanadamu. Roho zetu zina mipaka lakini Roho wa Yesu hana mipaka.
Na ni kwanini Roho wa Yesu anajulikana kama Roho Mtakatifu?
Ni kwasababu yeye ni Roho Takatifu, hiyo ndio sifa kubwa na ya kipekee Roho wa Yesu aliyoibeba..Yeye ni mtakatifu na hachangamani na uchafu.
Na ndio maana uthibitisho wa Kwanza kabisa wa Mtu aliyempokea Roho Mtakatifu ni kuwa Mtakatifu. Umepokea uwezo wa kufanyika mwana wa Mungu, unakuwa kama YESU. Naamini mpaka hapo utakuwa umeshafahamu Roho Mtakatifu ni nani?
Je! Umepokea moyoni mwako? kama bado ni kwanini? Biblia imesema ahadi hiyo ni ya bure na tunapewa bila malipo, kwa yeyote atakayemwamini.
Matendo 2:39 “Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu wamjie”.
Gharama za kumpata huyo Roho si fedha bali ni Uamuzi tu! Ukimtafuta Mungu kwa bidii utampata Neno lake linasema hivyo..
Hivyo kanuni rahisi sana ya kumpata ni KUTUBU kwanza: Yaani unamaanisha kuacha dhambi kwa vitendo, kisha kwenda kubatizwa katika ubatizo sahihi wa maji tele (Yohana 3:23) na kwa jina la Yesu kwaajili ya ondoleo la dhambi kulingana na Matendo 2:38 ili kuukamilisha wokovu wako. Na Roho Mtakatifu ataingia ndani yako, atakayekupa uwezo wa kuwa kama yeye alivyo yaani Mtakatifu. Vilevile atakushushia na karama zake za Roho kwa jinsi apendavyo yeye juu yako. Hapo ndipo utakapopokea uwezo wa kuwa shahidi wake
Kumbuka biblia inasema wote wasio na Roho Mtakatifu hao sio wake (Soma Warumi 8:9), Hivyo ni wajibu wetu sote kumtafuta Roho Mtakatifu kwa bidii sana. Kwasababu hutaweza kumjua Mungu, wala kupokea uwezo wa kuishinda dhambi kama huna Roho Mtakatifu ndani yako.
Bwana akubariki.
Maran Atha !jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
KWANINI YESU KRISTO ALIKUJA DUNIANI?
JE UNATAMANI KUMJUA MUNGU, NA HUJUI PA KUANZIA?
KWANINI YESU KRISTO NI MWANA WA DAUDI?
ROHO HUTUOMBEA KWA KUUGUA KUSIKOWEZA KUTAMKWA!
KAMA MUNGU ANABORESHA KAZI ZAKE, KWANINI WEWE USIBORESHE ZA KWAKO?.
Kwanini nguvu za mbinguni zitikisike?.
Bwana Yesu alitabiri na kusema kipindi kifupi karibu na mwisho wa dunia kutaanza kuonekana baadhi ya ishara za kutisha kutoka mbinguni, na mambo ya ajabu sana, Na hiyo itawafanya watu wengi waingie katika hofu sana, wakijiuliza nini maana ya mambo haya na nini kitatokea baada ya hayo..
Luka 21:25 “ Tena, kutakuwa na ishara katika jua, na mwezi, na nyota; na katika nchi dhiki ya mataifa wakishangaa kwa uvumi wa bahari na msukosuko wake;
26 watu wakivunjika mioyo kwa hofu, na kwa kutazamia mambo yatakayoupata ulimwengu. Kwa kuwa nguvu za mbinguni zitatikisika”.
Kama tunakumbuka Octoba 1 mwaka 2016, kulitokea Ishara ya ajabu pale Yerusalemu Israeli, sauti kama za baragumu nyingi zilisikika zikipigwa angani (tarumbeta zikilia Israeli angani)kwa umbali mrefu sana.. Na pale ambapo sauti zilipokuwa zinatokea kulionekana mduara mkubwa sana wa wingu lililozunguka kama pete..Jambo ambalo liliwashtua wakazi wengi wa mji wa Yerusalemu sio tu Israeli peke yake, bali hata dunia nzima. Kama hujalifahamu hilo bofya link hii utazame baadhi ya video zilizo rekodi tukio hilo(youtube).
https://www.youtube.com/watch?v=AwCc45T38SU
Haikuishia hapo lakini Inaripotiwa miaka ya hivi karibuni mambo kama hayo ya ajabu yamekuwa yakitokea angani, karibu dunia nzima, mambo ambayo hayajawahi kusikika wala kuonekana siku za huko nyuma,..hata wanayansi wanakosa majibu ya maswali hayo, wengine wanadai dunia inatembelewa na viumbe kutoka sayari nyingine (Aliens), wengine wanasema hivi, wengine vile, lakini biblia imeweka wazi kabisa katika siku za mwisho nguvu za mbinguni zitatikisika, na ishara kama hizo zitaendelea kuwa nyingi, na hiyo yote tunapaswa tujiulize ni kwanini hayo yote yanatokea?..Ni kwasababu Mungu anatukumbusha kuwa ule mwisho upo karibu na hivyo tujiweke tayari kwasababu saa ya ukombozi wetu imekaribia..
Amosi 3: 6 ”Je! Tarumbeta itapigwa mjini, watu wasiogope?…”
Kusikika kwa matarumbeta kama hayo, ni kutuonyesha kuwa Upo wakati parapanda halisi ya mwisho italia na wafu waliokufa katika Kristo watafufuliwa na kupewa ile miili ya utukufu pamoja na watakatifu waliokuwa hai kisha wote kwa pamoja watanyakuliwa na kwenda kumlaki Bwana Yesu mawinguni, kisha wataenda katika karamu ya mwana kondoo waliyoandaliwa mbinguni,
Lakini kumbuka kwa wakati huo ambao tutakuwa mbinguni, huku chini dhiki kuu itakuwa inaendelea,. Kumbuka hizi ni saa za majeruhi, Injili ya Kristo iliyotabiriwa ya siku hizi za mwisho sio ile ya kuwavuta tena waje kwa Kristo hapana bali ni injili ya kuhimiza, kumtia moyo yule ambaye tayari ni mtakatifu ili azidi kuwa mtakatifu na kumuhimiza yule ambaye ni mwovu na azidi kuwa mwovu (Soma Ufunuo 22:11), …
Kwasababu wakati wa mavuno umekaribia na magugu na ngano tayari yameshajitenga..Hivyo hakuna tena muda wa kuanza kutafuta magugu ni yapi na ngano ni zipi katika shamba la Mungu…
Hivyo ndugu kama bado unasuasua ni heri ukayajenga Maisha yako sasa upya, mkaribishe Kristo katika Maisha yako, ulimwengu huu usioisha masumbufu na mahangaiko, ukiendelea nao, utajikuta unaendelea hivyo hivyo mpaka unakufa au unyakuo unakukuta kwa ghafla..Hivyo kama upo tayari leo, hapo ulipo tafuta nafasi yako mwenyewe, upige magoti, umweleze Mungu dhambi zako zote, kisha mwombe akusamehe, unafanya hivyo huku ukiwa umemaanisha na umekusudia kuacha dhambi zako kabisa kwamba kuanzia leo unataka kuishi Maisha yale Kristo anayotaka..
Na kama utakuwa umefanya hivyo kwa Imani basi fahamu kuwa Umeshasamehewa,..Amani ya Bwana itaingia ndani ya moyo wako, (Huo ndio uthibitisho wa Msamaha wako), sasa unachopaswa kufanya baada ya hapo ni kwenda kubatizwa kama hujabatizwa, Hivyo tafuta kanisa linaloamini katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na uwe kwa jina la YESU KRISTO ubatizwe sawasawa na Matendo 2:38,..Ili kuukamilisha wokovu wako, Na Bwana mwenyewe atakupa kipawa cha Roho wake Mtakatifu. Kwasababu hiyo ni ahadi aliyoiahidi kwa wale wote wanatakao mpokea. Roho Mtakatifu atakusaidia kushinda dhambi na kukupa uelewa wa maandiko kwa namna isiyokuwa ya kawaida.
Bwana akubariki sana.jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Maran Atha.
Mada Nyinginezo:
Uasherati wa Kiroho maana yake nini?
JIBU: Mtu yeyote aliyejiingiza katika mahusiano na Yesu Kristo, mtu huyo katika roho anajulikana kama ni Mpenzi wa Yesu Kristo, Na mtu anajiingiza katika mahusiano hayo kwanza kwa kumwamini YESU KRISTO, kwamba alikuja kufa kwaajili ya dhambi zake, na kwamba yeye ndiye mwokozi wa ulimwengu, Na kumwamini huko kunatokana na kuisikia Injili ya Kweli inayohubiriwa na watumishi wake (Soma 2Wakorintho 11:2)..na baada ya kumwamini anatubu kwa kumaanisha kuziacha dhambi zake na kwenda kubatizwa kwa maji na kwa Roho Mtakatifu, sasa mtu aliyepitia hatua hizo zote katika ulimwengu wa roho anajulikana kama mpenzi wa YESU KRISTO au kwa jina lingine anaitwa Bibi arusi wa Kristo.
Yeremia 3:14 “Rudini, enyi watoto wenye kuasi, asema Bwana; MAANA MIMI NI MUME WENU; nami nitatwaa mtu mmoja wa mji mmoja, na wawili wa jamaa moja, nami nitawaleta hata Sayuni;”
Sasa ikitokea Mtu wa namna hii akiacha mahusiano yake haya na Kristo na kurudia tena kuishi maisha ya dhambi, na kumdharau Roho Mtakatifu, akaenda kuzini, au kuabudu sanamu, akaenda kwa waganga wa kienyeji…kibiblia mtu kama huyo ni anafanya uasherati wa kiroho, ambao ndio unaomtia Mungu wivu, ambao unaweza kupelekea hata kifo cha ghafla kwa huyo Mtu.
Waebrania 10:28 “Mtu aliyeidharau sheria ya Musa hufa pasipo huruma, kwa neno la mashahidi wawili au watatu.
29 Mwaonaje? Haikumpasa adhabu iliyo kubwa zaidi mtu yule aliyemkanyaga Mwana wa Mungu, na kuihesabu damu ya agano aliyotakaswa kwayo kuwa ni kitu ovyo, na kumfanyia jeuri Roho wa neema?
30 Maana twamjua yeye aliyesema, Kupatiliza kisasi ni juu yangu, mimi nitalipa. Na tena, Bwana atawahukumu watu wake.
31 Ni jambo la kutisha kuanguka katika mikono ya Mungu aliye hai.”
Unaweza kupitia binafsi mistari hii inaeleza zaidi juu ya uasherati huu wa kiroho (Soma 1Nyakati 5:25-26, Zaburi 106:39, Yeremia 13:27, Ezekieli 6:9, Walawi 17:7, Ezekieli 16:27,)
Waamuzi 2:16 “Kisha Bwana akawainua waamuzi, waliowaokoa na mikono ya watu hao waliowateka nyara.
17 Lakini hawakuwasikiliza hao waamuzi wao, maana walifanya uasherati kwa kuifuata miungu mingine, wakajiinamisha mbele yao; wakageuka upesi, na kuiacha njia ile waliyoiendea baba zao, waliozitii amri za Bwana bali wao hawakufanya hivyo”.
Hivyo uasherati wa kiroho sio ndoto za kufanya mapenzi usiku na mtu au viumbe visivyojulikana, kama zinavyotafsiriwa na wengi leo, bali ni kufanya kitendo chochote kilicho kinyume na Imani yako ya kikristo, ambacho ni machukizo mbele za Mungu, na Mungu alisema yeye ni Mungu mwenye wivu,(Soma Nahumu 1:2 na Kutoka 20:4).
Wivu huo ni wivu anauona pale mtu anapokwenda kufanya vitu kinyume na ile Imani aliyokuwa nayo.
Bwana atusaidie sana.
Ubarikiwe.
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
UFUNUO: Mlango wa 13
UFUNUO: Mlango wa 17
UFUNUO: Mlango wa 18
TIMAZI NI NINI