SWALI: Huu mstari una maana gani? Amos 9:2 “Wajapochimba waingie katika kuzimu, mkono wangu utawatoa huko; nao wajapopanda hata mbinguni, nitawatelemsha toka huko”
JIBU: Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe, Ni muhimu kufahamu sio kila mahali panapozungumzia Neno mbinguni katika biblia panamaanisha “mbinguni kule Malaika watakatifu walipo” Hususani katika agano la kale. Neno mbinguni pia linaweza kutumika na wapagani kumaanisha mbingu yao, kadhalika mbinguni kunaweza kumaanisha “sehemu iliyo inuka sana”.
Mtu aliyejiinua sana moyo wake katika roho anaonekana amepanda mpaka mbinguni.
Hali kadhalika sio kila mahali panalipoandikwa neno “kuzimu” katika biblia hususani agano la kale, kuna maanisha kule kuzimu, roho za viumbe walioasi zilipo!..hapana! sehemu nyingine panapotajwa neno kuzimu panamaanisha mahali pa chini sana. Kwamfano mtu aliye katika vifungo vingi vilivyomfanya awe chini sana, katika roho ni kama yupo kuzimu. (Yona na Mariamu na Hana).
Kwamfano tunaweza kusoma mistari ifuatayo ili tupate kuelewa vizuri.
Yona 2:1 “Ndipo Yona akamwomba Bwana, Mungu wake, katika tumbo la yule samaki,
2 Akasema, Nalimlilia Bwana kwa sababu ya shida yangu, Naye akaniitikia; KATİKA TUMBO LA KUZİMU NALİOMBA, Nawe ukasikia sauti yangu.
3 Maana ulinitupa vilindini, Ndani ya moyo wa bahari; Gharika ya maji ikanizunguka pande zote; Mawimbi yako yote na gharika zako zote zimepita juu yangu”
Sasa hapo Yona sio kwamba alishuka kuzimu, mahali pa wafu, hapana, bali katika mazingira ya lile tumbo la samaki alilokuwemo ndio akakufananisha na KUZIMU. Mahali pabaja mfano wa kuzimu. Na mtu anapokuwa katika mazingira hayo yanayofananishwa na kuzimu, anaweza kupandishwa juu na kutoka huko, kama Yona na Hana mama yake Samweli.
1Samweli 2:6 “Bwana huua, naye hufanya kuwa hai; Hushusha hata kuzimu, tena huleta juu.
7 Bwana hufukarisha mtu, naye hutajirisha; Hushusha chini, tena huinua juu”
Na andiko lingine ndio hilo la kwenye Amosi 9:2 “Wajapochimba waingie katika kuzimu, mkono wangu utawatoa huko; nao wajapopanda hata mbinguni, nitawatelemsha toka huko”
Lakini mtu anayeshuka katika ile kuzimu halisi ya sehemu ya wafu walioasi, biblia inasema hawezi kurudi tena wala hawezi kutoka huko.
Ayubu 7:9 “Kama vile wingu likomavyo na kutoweka, Ni vivyo huyo ashukaye kuzimuni hatazuka tena kabisa. Hatarudi tena nyumbani kwake, Wala mahali pake hapatamjua tena”.
Kwahiyo unaweza ukawa unapitia hali fulani katika hii dunia, ambapo mahali ulipo ni kama kuzimu, kila kona unaona giza limekuzunguka na mashaka, huoni unafuu popote, nataka nikuambie lipo tumaini kwa Kristo, maadamu bado unaishi, Bwana anaweza kukunyanyua tena na kukutoa huko Kuzimu, ulipo na kukupandisha juu, Hivyo Mwamini, omba kwa bidii na mshukuru, siku isiyokuwa na jina utaona miujiza.
Vivyo hivyo unaweza kuwa katika mahali fulani, au ukawa katika nafasi fulani na moyo wako ukainuka sana, pengine ukajiona ni mungu-mtu, kila mtu anakuogopa, kila mtu anakuhofu au wewe ukajiona ni bora sana kuliko wengine wote wanaokuzunguka, nataka nikuambia mbele za Mungu, umejiinua na kufika mbinguni, na biblia inasema wote wajikwezao watashushwa (Luka 14:11).
Kwa maelezo marefu kuhusu mbungini fungua hapa >> mbinguni ni wapi?
Hivyo mstari huo katika Amosi hauzungumzii Mbingu halisi, Malaika watakatifu waliopo, bali wala hauzungumzii Kuzimu halisi, wafu waliokufa katika dhambi walipo… Bali inazungumzia hali fulani ya maisha ambayo mtu yupo chini sana mfano wa kuzimu, na hali fulani ya maisha ambayo mtu kajiinua sana juu mfano wa mbingu.
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
ALIKUWAKO NAYE HAYUKO, NAYE YU TAYARI KUPANDA KUTOKA KUZIMU.
Kuota unajifungua kuna maanisha nini?
Ndoto hii inaweza ikawa na maana mbili, maana ya kwanza ambayo ninaweza kusema inawapata wengi, ni ile inayotokana na shughuli nyingi au mambo tuliyowahi kuyapitia, au kuyawaza, au kuyatenda mara kwa mara huko nyuma.
Biblia inasema.
Mhubiri 5:3 “Kwa maana ndoto huja kwa sababu ya shughuli nyingi;…….”.
Hivyo sishangai kama ndoto hii atakuwa anaotwa na mwanamke, kwasababu yeye kwa sehemu kubwa katika maisha yake, amekuwa akiwaza pengine siku moja atajifungua, au hivi karibuni anakwenda kujifungua au mwengine tayari huko nyuma alishawahi kujifungua,..
Hivyo matukio kama hayo kujirudia rudia katika ndoto zake litakuwa ni jambo la kawaida sana. Kwahiyo kama wewe ni mmojawapo wa wanaoyapitia hayo, basi ipuuzie tu ndoto ya namna hiyo, kwasababu haina maana yoyote rohoni.
Lakini maana ya pili, ambayo ni ya rohoni, ni kwamba ikiwa ndoto hii umekujia kwa namna ambayo sio ya kawaida, yaani kwa uzito mkubwa sana, na unahisi kuna uzito Fulani ndani ya moyo wako, basi ujue ndoto hiyo imebeba ujumbe. Na tafsiri yake ni kuwa lipo jambo zuri au baya linakwenda kukujia, kulingana na ulichokuwa unakifanya katika maisha yako.
Tunajua sikuzote mpaka mtu anafikia hatua ya kuzaa ni wazi kuwa tayari huko nyuma alishabeba mimba kwa muda mrefu, hivyo angalia katika maisha yako ni nini umekuwa ukikibeba, na ukikisubiria, basi ujue hivi karibuni utakwenda kukiona kikijidhihirisha (kukuletea matokeo fulani). Kama umekuwa ukifanya jambo jema basi tazamia kuona matunda ya wema wako hivi karibuni.
Luka 1:30 “Malaika akamwambia, Usiogope, Mariamu, kwa maana umepata neema kwa Mungu.
31 Tazama, utachukua mimba na kuzaa mtoto mwanamume; na jina lake utamwita Yesu.
Lakini kama wewe ni mwenye dhambi (yaani haupo ndani ya Kristo) basi jiandae hivi karibuni kukutana na matunda ya mambo maovu uliyokuwa unayafanya katika maisha yako,
biblia inasema..
Ayubu 15:35 “Wao hutunga mimba ya madhara, na kuzaa uovu, Nalo tumbo lao hutengeza udanganyifu”.
Zaburi 8:14 “Tazama, huyu ana utungu wa uovu, Amechukua mimba ya madhara, amezaa uongo”
Yakobo 114 “Lakini kila mmoja hujaribiwa na tamaa yake mwenyewe huku akivutwa na kudanganywa.
15 Halafu ile tamaa ikiisha kuchukua mimba huzaa dhambi, na ile dhambi ikiisha kukomaa huzaa mauti”.
Unaona wanachozaa sikuzote watu waovu ? Na ndio maana sehemu nyingine inasema..
Mathayo 3:10 “Na shoka limekwisha kuwekwa penye mashina ya miti; basi kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa motoni”.
Hivyo jiangalie wewe katika maisha yako yote, na mambo yako yote unayoyatenda Je, ni jambo gani unakwenda kulizaa hivi karibuni? Je! ni uzima, au mauti?
Lakini habari njema ni kuwa Yesu leo anaweza kukuokoa, na kukufanya umzalie matunda mazuri, na akabatilisha mabaya yote ambayo yamepangwa mbele yako, ikiwa tu utakubali kumruhusu ayageuze maisha yako, Yeye yupo tayari kukusamehe ikiwa utakuwa tayari kutubu kwa moyo wako wote, Hivyo ikiwa upo tayari kufanya hivyo leo, basi uamuzi huo ni wa busara sana. Unachotakiwa kufanya ni kufungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba.>>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Na Mungu peke yake atakigeuza unachokizaa kiwe chema.
Bwana akubariki sana.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Au jiunge kwa kubofya link hii>>
Kwa mgawanyo bora wa masomo download App hapa>> App wingu la mashahidi
Mada Nyinginezo:
HERODE NA PILATO, MAADUI WAWILI WAPATANA.
Mwaloni ni nini? Na je unafunua nini rohoni?
Arabuni maana yake ni nini?
MOTO HUFA KWA KUKOSA KUNI.HATA UASHERATI NAO
UNYAKUO.
Mtu akikufanyia fadhila ya hali ya juu, ni wazi kuwa nafsi yako haitatulia mpaka na wewe utakapohakikisha umemrudishia naye pia fadhila..hiyo ni hali ya kawaida ya kibinadamu kabisa, hata kama hakitafikia kile alichokufanyia walau utaonyesha shukrani kwa kumwombea dua kwa Mungu.
Hata sisi tunapookoka, tunapogundua kuwa kumbe kuna mtu alitupenda upeo, kumbe kuna mtu alikufa kwa ajili ya dhambi zetu na kama asingekufa leo hii sisi tungekuwa ni wa kuzimu.
Ni dhahiri kuwa kama tumeithamini fadhila hiyo ya kipekee basi na sisi ni lazima tutaonyesha kurudisha kitu Fulani kwake, ni kweli hatuwezi kumrudishia fadhila za matendo yetu mema kama yeye aliyotufanyia, kwasababu mpaka hapa tulipo tulishamkosea Mungu mara nyingi sana. Lakini fadhili tunayoweza kumrudishia ni kuupeleka Upendo wake, uwafikie na wengine, ambao bado haujawafikia, ili nao pia waokolewe kama sisi. Na hiyo ndio inayotufanya tuwahubirie injili na wengine, na kuwaombea.
Mtume Paulo alisema maneno haya;
2Wakorintho 5:14 “MAANA, UPENDO WA KRISTO WATUBIDISHA; maana tumehukumu hivi, ya kwamba mmoja alikufa kwa ajili ya wote, basi walikufa wote”;
Unaona? Vivyo hivyo na sisi, huu upendo wa ajabu wa Yesu kutoa maisha yake kwa ajili yetu sisi bure, ugeuke na kuwa deni kwetu,..Huu ndio utupe sababu ya kuwapelekea watu wengine habari njema, tusiuchukulie bure tu..
2Wakorintho 6:1 “Nasi tukitenda kazi pamoja naye twawasihi msiipokee neema ya Mungu bure.
2 (Kwa maana asema, Wakati uliokubalika nalikusikia, Siku ya wokovu nalikusaidia;tazama,wakati uliokubalika ndiyo sasa; tazama siku ya wokovu ni sasa)”.
Kama wewe umeokolewa mshukuru Mungu sana kwa neema hiyo , lakini kumbuka wapo watu wengi wanaohitaji kuokolewa kama wewe, swali tujiulize tangu tumeokoka Je viungo vyetu vimeleta faida yoyote kwa Kristo? Je kilishamleta mmoja katika neema ya wokovu au la? Kama karama yako haijawahi kufanya hivyo, badala yake imetumika kuwaburudisha tu watu, basi ujue karama hiyo ni feki, haijatoka kwa Mungu.
Hivyo kwa pamoja sote, tuufanye upendo wa Kristo kama deni kwetu. Huo utubidiishe kumtumikia Mungu, kwa karama zetu na kwa tulivyonavyo, ili neema ya Mungu iwafikie na wengine kama sisi nao pia waufurahie wokovu wa Bwana wetu Yesu Kristo.
Kilichoawafanya mitume waupindue ulimwengu kwa wakati wao, ni kwasababu kwa pamoja waliutambua Upendo wa Kristo, hivyo ukageuka kuwa deni kwao, wakamtumikia Mungu kwa vyote walivyokuwanavyo, na ndio maana na hapo wanasema Upendo wa Kristo watubidiisha, vivyo hivyo na sisi, tuugeuze Upendo huu kuwa deni.
Na Bwana atatuonekania katika maisha yetu.
Shalom.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
UWEZA WA MUNGU UNAONEKANA WAPI?
Mungu aliposema Yesu ni mwanawe pekee, alimaanisha hakuwa na wengine?
LAKINI USIKU WA MANANE, PAKAWA NA KELELE.
MISTARI YA BIBLIA KUHUSU UPENDO.
Ndoto ya Kuota unapigana na mtu kuna inamaanisha nini?
Ndoto hii inaweza ikawa na maana mbili, maana ya kwanza, ni kuwa upo katika mashindano, Na maana ya pili ni kuwa upo katika vita.
Tukianzana na maana ya kwanza ambayo ni mashindano.
Kwa namna ya kawaida, ikiwa kipo kitu Fulani ambacho kinathamani fulani, na wote mnakitamani au kukigombania ili mkipate, au mmoja anakizuia ili kisipatikane, ni rahisi kutokea kutokuelewa na mwisho wa siku mapigano, kwamfano wengine wanaishia kupigana kisa, fedha, wengine madini, wengine fursa, wengine wapenzi, na wengine thawabu n.k,
Na ndio maana utamwona mtu kama Yakobo katika biblia, alipiigania thawabu yake sana usiku kucha kwa kushindana mweleka na Yule malaika aliyemtembelea usiku..
Mwanzo 32:24 “Yakobo akakaa peke yake; na mtu mmoja akashindana naye mweleka hata alfajiri.
25 Naye alipoona ya kuwa hamshindi, alimgusa panapo uvungu wa paja lake; ukateguka uvungu wa paja la Yakobo alipokuwa akishindana naye.
26 Akasema, Niache, niende, maana kunapambazuka. Akasema, Sikuachi, usiponibariki.
27 Akamwuliza, Jina lako n’nani? Akasema, Yakobo.
28 Akamwambia, Jina lako hutaitwa tena Yakobo, ila Israeli, maana umeshindana na Mungu, na watu, nawe umeshinda”.
Hivyo kama wewe umeokoka halafu ukaota, unapigana na mtu muda mrefu mpaka unachoka, ni mapambano tu, Hapo ni Mungu anakukumbusha habari ya Yakobo, kwamba unapaswa utafute thawabu zake kwa nguvu mpaka uzipate, kuliko kitu kingine chochote unachoweza kukitafuta katika hii dunia. Hiyo ndio tafsiri ya kwanza.
Tafsiri ya pili: Kuota unapigana ni ishara ya vita.
Wakati mwingine, watu wanaweza kupigana, si kwa ajili wanagombania kitu Fulani, hapana, bali ni kwa ajili ya chuki, wivu, fitna, kiburi, n.k..Lengo kuu ni kutaka kukuangamiza tu basi,
Hivyo kuota unapigana na mtu, pia inaweza ikawa ni ishara una vita vya kiroho, na vita hivyo vinatoka upande wa ibilisi, haijalishi ni kwa kupitia wachawi,au mapepo, au watu wa kawaida, au vyovyote vile, lakini upo katika vita, Hivyo kama wewe upo ndani ya Kristo, zidisha ukaribu wako na Mungu katika maombi, na kujifunza Neno,..Kwasababu Bwana anasema..
Waamuzi 8:33 “kisha itakuwa, asubuhi, mara litakapokucha jua, wewe utaamka asubuhi na mapema, na kuushambulia mji huo; tena, angalia, hapo yeye na wale watu walio pamoja naye WATAKAPOKUTOKEA NJE KUPIGANA NAWE, ndipo utapata kuwatenda kama utakavyopata nafasi”.
Lakini kama wewe hujaokoka, ni wazi kuwa upo hatarini, hivyo tahadhari hizi zichukue,
Mpe leo Yesu maisha yako ayaokoke, haijalishi wewe ni wa dini gani,au dhehebu gani, Yesu Kristo anawaokoa watu wote. Ikiwa leo utakubali kutubu dhambi zako zote kwa kumaanisha kabisa kuziacha, atakusamehe na kukukubadilisha na kukupa Roho wake, ambaye atakaa ndani yako milele..Na ndiye atakayekulinda na mipenyo yote ya ibilisi katika maisha yako, kwasababu tayari utakuwa ndani ya ulinzi wa ki-Mungu.
Hivyo kama leo upo tayari kufanya hivyo, basi fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba, na maombezi>>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Kumbuka hizi ni siku za mwisho, na shetani anawinda roho za watu, kwa bidii sana ili awaangamize, kwasababu anajua wakati aliobakiwa nao ni mchache, na ndio maana unaona mapambano tu, hivyo usipuuzie wokovu ndugu yangu.
Ukiwa umefungua hapo juu na kufuata maelekezo yote, Basi Bwana akubariki sana, na Hongera kwa kuokoka.
Kwa mgawanyo bora wa masomo download App hapa>> App wingu la mashahidi
Pia tazama masomo mengine chini ya kukusaidia kukua kiroho.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
JIEPUSHE NA UNAJISI.
NA ROHO NA BIBI-ARUSI WASEMA, NJOO!
Ibada ni nini,Na je ili ikamilike inapaswa iwe na nini na nini?
MKUMBUKE MKE WA LUTU.
CHUKIZO LA UHARIBIFU
HASIRA YA MUNGU KUKUWAKIA, KWA KUTOMZUNGUZIA TU MUNGU IPASAVYO.
Jina la Bwana wetu Yesu libarikiwe.
Karibu tujifunze Biblia,
Umewahi kujiuliza kwanini siku zote vita vya wanajeshi vinakuwaga ni vigumu? Haijalishi watakuwa wamevaa mavazi gani ya kujikinga na silaha na risasi, lakini bado vita huwa vinakuwa vigumu? Umewahi kujiuliza ni kwanini?
Ni kwasababu wale wanaokwenda kupambana nao wapo kama wao…Adui naye kashikilia silaha kama ya kwao, wamepitia mafunzo kama ya kwao, nao pia wamevaa mavazi ya kujikinga na risasi kama wao. Kwaufupi karibia kila kitu alilichonacho mwanajeshi adui yake naye anacho..Hapo ndipo unapokuja ugumu wa vita. Na sio tu katika vita, bali hata katika michezo wanaocheza watu wa kidunia..Michezo yao inakuwa ni migumu kwasababu wapinzani wao nao pia wamejiandaa kama wao, wana mbinu kama zao, na pia wana akili kama zao..
Na katika ulimwengu wa roho tunapaswa tulitambue hilo. Kwamba tupo vitani, na tunayepambana naye hayupo mikono mitupu, bali naye pia ni askari kama sisi.
Pale tunaposoma andiko la kwenye Waefeso 6:11 kwamba “Vaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kuzipinga hila za Shetani.” Maana yake ni kwamba shetani naye upande wa pili kashika silaha kama sisi. Angekuwa si askari kama sisi biblia isingetuambia tushike ngao, ngao ya nini kama unayepambana naye hana silaha kali? Unaona.
Kwaufupi katika ulimwengu wa roho, wote tunafanana kimwonekano…shetani na mapepo yake pamoja na sisi. Wote tumevaa silaha.
Ukizidi kusoma hiyo habari ya kwenye Waefeso utaona biblia inasema tukamate upanga wa roho ambao ni Neno la Mungu…sasa jambo la muhimu kufahamu ni kuwa upanga huo huo (yaani Neno la Mungu) shetani pia anao. Na upanga huo huo tunaotumia kumkata, ndio huo huo anaotumia na yeye kutukata sisi tusipokuwa watashi.
Utauliza ni wapi shetani amewahi kuwa na Neno la Mungu (na kulitumia hilo kumkata mtu wa Mungu)?
Kasome Luka 4:9-13, uone jinsi alivyolitumia kumshambulia Bwana kule jangwani.
Hivyo mwanajeshi wa kweli aliye vitani hafurahii tu kubeba bunduki au mkuki na kuvaa kijeshi, kwasababu anajua hata adui yake naye kashika bunduki kama yake, na anajua asipokuwa makini anaweza kufa na silaha zake mkononi, hivyo anachojiaminisha nacho ni UTASHI wa kutumia silaha yake, uwezo wa kukwepa, uwezo wa kukinga, na ushapu na ushupavu. Kwahivyo ndivyo atakavyomshinda adui yake, lakini akilala tu na kusema tayari ana bunduki mkononi, tayari amevaa nguo ya kuzuia risasi basi ni dhahiri huyo mwanajeshi anakwenda kufa huko.
Ndugu kama askari tusifurahie tu kulikariri Neno, bali tufurahie uwezo wa kulichambua vyema, kama aliokuwa nao Bwana Yesu…Kwasababu biblia inasema Neno la Mungu ni upanga ukatao kuwili, lina makali pande zote kama sime, maana yake pia adui yako akilishika anaweza kukudhuru nalo na ukakatikakatika kabisa.
Na kama tulivyotangulia kusema kuwa shetani na mapepo yake ni wanajeshi kama sisi, yamevaa makombati, na yanaouwezo mzuri wa kutumia silaha, hivyo ni ushapu wetu, na utashi wetu ndio utakaowashinda…Sasa utauliza ni wapi biblia inasema kwamba mapepo ni majeshi?
Waefeso 6:11 “Vaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kuzipinga hila za Shetani.
12 Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya MAJESHİ YA PEPO WABAYA katika ulimwengu wa roho”.
Hebu jiulize kwanini biblia haijatumia neno hapo “umati wa pepo wabaya” badala yake imetumia neno “jeshi”?.. maana yake ni kwamba haya maroho nayo yamevaa silaha na makombati, yapo vitani kupambana…hayapo hayapo tu!
Pia tunaweza kusoma andiko lingine linalozungumzia majeshi ya mapepo wabaya..katika Luka 8:30 “Yesu akamwuliza, Jina lako nani? Akasema, JİNA LANGU Nİ JESHİ; kwa sababu pepo wengi wamemwingia”
Kwanini yalipoulizwa majina yao, hayakusema “jina letu umati” badala yake yakasema “jeshi”?. Hiyo ni kuonyesha kuwa yapo vitani, yameshika silaha. Na sisi wakristo hatupaswi kulala, tunapaswa tusimame tushike silaha!. Na tuongeze utashi wa hali ya juu katika kutumia silaha (yaani Neno la Mungu).
Hivyo hatuna budi kuingia ndani sana katika kujifunza Neno la Mungu, na kuweza kulitumia. Bwana wetu Yesu alikuwa mfano mzuri…Shetani alikuja na Neno, lakini Bwana alikuwa na Neno zaidi ya lile..hivyo shetani alipomtupia ule upanga, Bwana aliukinga na kumkata kwa utashi aliokuwa nao wa kuweza kulitumia Neno.
Vivyo hivyo katika maisha na katika wokovu tuna vitu vingi sana, ambavyo shetani anatutesa navyo kwasababu tu hatujui jinsi ya kulitumia Neno vizuri(hatuna utashi, wala ushapu, wala uzoefu wa Neno). Neno tunalo, lakini jinsi ya kulitumia ndipo tunaposhindwa na hivyo adui shetani analitumia hilo hilo kutumaliza.
Sasa Ni kwa namna gani tutaweza kulitumia Neno vizuri ili kuzishinda hila za shetani? Ni kwa kujifunza kwa bidii Neno, na si kusoma tu!. Ipo tofauti kubwa sana ya kusoma na kujifunza Neno. Mtoto wa darasa la kwanza aliyejifunza kusoma leo…ukimpa kitabu cha biolojia cha kidato cha sita, anaweza kukisoma chote, na hata kukariri baadhi ya picha na vimaneno. Lakini hapo bado hajajifunza chochote…haijalishi kakariri mistari mingapi ya kitabu hicho.
Hivyo na sisi hatupaswi kuisoma biblia tu peke yake, bali tunapaswa tujifunze..Maana yake tunakaa chini tunasoma kitabu kimoja, na kukitafakari, na kwenda kutafuta zaidi huku na huko, maarifa juu ya hicho kitu, ili kukijazia nyama kile tulichokisoma. Na si kusoma mstari mmoja tu! Pasipo kuelewa kiini cha huo mstari toka juu, na kujisifu kwamba tunazo silaha.
Bwana atusaidie na kuzidi kutujaza Roho wake mtakatifu, ili tuweze kulitumia vyema neno lake.o
2Timotheo 2:15 “Jitahidi kujionyesha kuwa umekubaliwa na Mungu, mtenda kazi asiye na sababu ya kutahayari, UKİTUMİA KWA HALALİ NENO LA KWELİ”
Bwana atubariki.
Kama hujaokoka! Bwana Yesu yupo mlangoni kurudi.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
ZIKIMBIE TAMAA ZA UJANANI! NA MTU YEYOTE ASIUDHARAU UJANA WAKO.
Jina la Bwana wetu na mwokozi wetu Yesu Kristo lihimidiwe daima.
Natumai u mzima, hivyo nakukaribisha tuyatafakari kwa pamoja maneno ya uzima ya Mungu wetu,.
Leo tutatazama tukio moja kati ya mengi yaliyokuwa yanaendelea kipindi kifupi kabla ya Kristo kuingia katika mateso makali ya kusulibiwa. Na tukio lenyewe ni lile na maadui wawili kukutana tena na kupatana…,Ambao ni Herode na Pilato.
Luka 23:11 “Basi Herode akamfanya duni, pamoja na askari zake, akamdhihaki, na kumvika mavazi mazuri; kisha akamrudisha kwa Pilato.
12 Basi siku ile ile Herode na Pilato walipatana kwa urafiki kwa maana hapo kwanza walikuwa na uadui wao kwa wao”.
Ulishawahi kujiuliza ni kwanini hawa watu wasipatanishwe na mambo mengine ya msingi mfano ya kidiplomasia, au ya kiuchumi, mpaka wapatanishwe na kukamatwa kwa mtu Fulani mwenye haki?. Utajiuliza Yesu alikuwa ana umuhimu gani kwao? Kwani ni yeye ndiye aliyewagombanisha? Kwanza wao walikuwa ni warumi Yesu ni myahudi, wao wapo Israeli kwa lengo la kutimiza mambo yao ya kiutawala na kuhakikisha nchi inastawi na kupeleka kodi nzuri kwa mkuu wao Kaisari aliyeko huko Rumi kwao, maelfu ya maili kutoka hapo walipo, Hivyo Yesu hakuwa na umuhimu wowote kwao, kwasababu yeye hakuwa mwanasiasa wala mfanyabiashara, au jasusi fulani..
Hivyo ukitazama kwa ukaribu utagundua kuwa muungano ule haukuwa wa kawaida, Bali ni muungano uliobuniwa na mamlaka tofauti na wanaoujua wao, na hiyo si nyingi zaidi ya ile ya mamlaka ya giza.
Na ndio maana kipindi kifupi kabla Bwana Yesu hajakamatwa kule Gethsemane, aliwaambia wale waliokuja kumkamata kuwa huu ndio WAKATI WA MAMLAKA YA GIZA kutenda kazi (soma Luka 22:52-53).
Mamlaka ya giza siku zote, ikitaka kuleta dhiki, huwa inafanya kazi ya kuwakutanisha na kuwapatanisha kwanza pamoja wakuu, hata wale maadui walioshindikana wa muda mrefu, inawapatanisha..Na inafanya hivyo ili kuongeza nguvu ya kutimiza azma yake ya maangamizi, na si kingine..
Na ndio maana, kipindi kile Kama Herode na Pilato wasingeungana, Bwana Yesu asingesulibiwa kwa namna yoyote ile, kwasababu amri ilipaswa iidhinishwe na pande zote mbili,. Na sio tu hao wafalme wawili waliungana, bali biblia inatuambia pia pamoja na mataifa, na watu wa Israeli ikiwemo waandishi na makuhani, waliungana pamoja ili kufanya shauri la kumwangamiza Kristo. Mpaka mafarisayo na Masadukayo ambao kutwa kuchwa walikuwa wakikinzana lakini waliungana kipindi hicho (Kasome Mathayo 22:34).
Matendo 4:25 “ nawe ulinena kwa Roho Mtakatifu kwa kinywa cha babaetu Daudi, mtumishi wako, Mbona mataifa wamefanya ghasia, Na makabila wametafakari ubatili?
26 WAFALME WA DUNIA WAMEJIPANGA, NA WAKUU WAMEFANYA SHAURI PAMOJA Juu ya Bwana na juu ya Kristo wake.
27 MAANA NI KWELI, HERODE NA PONTIO PILATO PAMOJA NA MATAIFA NA WATU WA ISRAELI, walikusanyika katika mji huu juu ya Mtumishi wako mtakatifu Yesu, uliyemtia mafuta”
Umeona hapo, timu ya kumwangamiza Yesu ilikuwa ni kubwa sana kuliko unavyoweza kudhani na sehemu kubwa ya hiyo ilikuja kwa kupatana kwa maadui.
Ndivyo itakavyokuwa katika dhiki kuu ndugu yangu. Roho ya mpinga-Kristo, itayakutanisha mataifa takribani yote ulimwenguni, na kitakachowakutanisha sio mikataba ya amani unayoiona leo hii inayosainiwa kila siku, sio makubaliano ya kiuchumi, wala sio mazungumzo ya kidiplomasia, hayo hayawezi kuipatanisha dunia hata kidogo, yameshafanyika mara nyingi huko nyuma, mpaka leo hii hakuna hata moja lililowezekana..
Kitakachokuja kuipatanisha dunia na kuwa na serikali moja ya makubaliano ambayo bila hiyo mtu hataweza, kuuza wala kununua, wala kuajiriwa itakuwa ni ya mamlaka ya giza, juu ya UKRISTO halisi ulimwenguni. Utajiuliza ukristo una nguvu gani mpaka uyasababishe mataifa yaungane?,
jibu ndio kama lile la Bwana Yesu, kwani yeye alikuwa na ushawishi gani mpaka Herode na Pilato maadui wa muda mrefu waungane,. Utagundua kuwa shetani ni lazima afanye hivyo ili atimize agenda yake vizuri.
Hapo ndipo wale ambao watakaokuwa wameukosa unyakuo, watayashuhudia haya, ghafla tu kutatokea visa visivyokuwa na mashiko ambavyo vitawalenga wakristo wale walioachwa kwenye unyakuo, na hivyo vitasababisha dunia nzima uinganishwe chini ya mfumo mmoja wa mpinga-kristo, Hapo ndipo kutakuwa na dhiki ambayo haijawahi kutokea tangu dunia iumbwe, na hiyo itawalenga wale wanawali vuguvugu waliokukosa unyakuo, ambao hawatakuwepo kwenye huo mfumo wao.
Mambo hayo ndugu yangu, yapo mlangoni kutokea, na yatakuja kwa ghafla sana, dalili karibia zote za mwisho wa dunia zimeshatimia, siku yoyote unyakuo utapita, na ndio maana Bwana Yesu anataka kutuepusha na huo wakati mbaya sana, wa kuharibiwa kwa ulimwengu.
Anasema,
Ufunuo 3:10 “Kwa kuwa umelishika neno la subira yangu, mimi nami nitakulinda, utoke katika saa ya kuharibiwa iliyo tayari kuujilia ulimwengu wote, kuwajaribu wakaao juu ya nchi.
11 Naja upesi. Shika sana ulicho nacho, asije mtu akaitwaa taji yako.
Je! tumejiwekaje tayari? Je na sisi tumelishika Neno la subira yake? Bwana Yesu akirudi usiku wa leo tunao uhakika wa kwenda naye mbinguni?. Kama hatuna uhakika huo, ni dhahiri kuwa tutababaki, hivyo ni heri tuyasalimishe maisha yetu kwa Bwana ayaokoe ndani ya hichi kipindi kifupi tulichobakiwa nacho. Na yeye mwenyewe atahakikisha anatufikisha ng’ambo salama.
Maran Atha.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
SWALI: Katika 2Wakorintho 6:7, Hizo Silaha za Mkono wa kuume na za mkono wa kushoto ni zipi?
JIBU: Tusome,
2Wakorintho 6:7 “katika neno la kweli, katika nguvu ya Mungu; kwa silaha za haki za mkono wa kuume na za mkono wa kushoto”
Mkono wa kuume ni mkono wa kulia, Hivyo kulingana na hilo andiko zipo silaha za mkono wa kulia na za mkono wa kushoto. Lakini kiuhalisia zipo silaha za miguuni pia, na za kifuani na za kichwani..Lakini hapa tutakwenda kuzizungumzia hizi za mikononi tu, maana ndizo zilizotajwa hapa.
Sasa swali hizo silaha ni zipi?
Jibu tunalipata katika kitabu cha Waefeso.
Waefeso 6:13 “Kwa sababu hiyo twaeni SİLAHA zote za Mungu, mpate kuweza kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama.
14 Basi simameni, hali mmejifunga kweli viunoni, na kuvaa dirii ya haki kifuani,
15 na kufungiwa miguu utayari tupatao kwa Injili ya amani;
16 zaidi ya yote MKİİTWAA NGAO YA İMANİ, ambayo kwa hiyo mtaweza kuizima mishale yote yenye moto ya yule mwovu.
17 Tena ipokeeni chapeo ya wokovu, na UPANGA WA ROHO ambao ni neno la Mungu”
Ukimsoma vizuri huyu Askari utaona Kashika UPANGA mkono mmoja na Mkono wa pili kashikilia NGAO. Sasa hizo mbili “Ngao pamoja na Upanga” ndio silaha za mkono wa kuume na kushoto.
Biblia imeelezea hapo Ngano ni nini? Kwamba ni Imani,..Maana yake ni kwamba Imani ni silaha, na inafungiwa mkononi, maana yake haipaswi kuangushwa hata kidogo, tukiwa nayo hiyo, tuna uwezo wa kuizima mishale yote ya adui shetani, Vile vile kwa Imani tunaweza kufanya mambo yasiyowezekana Kulingana na Waebrania 11.
Na pia biblia imeelezea Upanga ni nini? Kwamba ni Neno la Mungu..Tukiwa na Neno la Mungu la kutosha ndani yetu, shetani na majeshi yake hawatatuweza kamwe. Tutamkata na majeshi yake vipande vipande, kwasababu tunalijua Neno.
Waebrania 4:12 “Maana Neno la Mungu li hai, tena lina nguvu, tena lina ukali kuliko upanga uwao wote ukatao kuwili, tena lachoma hata kuzigawanya nafsi na roho, na viungo na mafuta yaliyomo ndani yake; tena li jepesi kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo.
13 Wala hakuna kiumbe kisichokuwa wazi mbele zake, lakini vitu vyote vi utupu na kufunuliwa machoni pake yeye aliye na mambo yetu”
Hivyo IMANI na NENO LA MUNGU, ni pacha, wanakwenda pamoja…na vyote vinashikiliwa mkononi na si miguuni, na vinategemeana…kama biblia inavyosema katika Warumi…
Warumi 10:17 “Basi İMANİ, chanzo chake ni kusikia; na kusikia huja kwa NENO LA KRİSTO”.
Umeona hapo? Hizo ndio silaha mbili za Mkono wa kuume na kushoto.
Je! Na wewe unazo?..Kumbuka hizo huwezi kusema unazo kama hujawa askari, na lazima kuwe na vita mbele yako?. Kama hakuna vita vyovyote vya kiimani unavyopambana basi wewe bado sio askari, hauhitaji ngao wala upanga mikononi mwako. Kama unakwenda disko, au bar au kujiuza…Ngao ya nini hapo? Unakinga nini kutoka kwa yule adui? Katika roho mikono yako inaonekana imebeba matatizo tu.
Lakini unapokuwa mkristo kweli kweli na kuacha mambo yote ya dunia, hapo wewe ni askari tena unayeogopeka katika ulimwengu wa adui shetani, Na pia ndio unayewindwa zaidi, hivyo inakugharimu kukisha kila wakati ili usipatikane na madhara.
Bwana atujalie tuwe maaskari wa bora wa Kristo, huku tumevaa silaha zote za haki.
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Shalom, Karibu tuyatafakari maneno ya uzima ya Bwana wetu.
Ndugu, ukilikosa tumaini ambalo linapatikana kwa YESU tu peke yake, ni ngumu kuimaliza hii safari yako hapa duniani salama, haijalishi utajifanya una furaha kiasi gani, furaha hiyo ni feki ndugu yangu, huwezi kuushinda huu ulimwengu uliojaa vishawishi na shida na taabu, na mitego mingi ya adui, huwezi..Haijalishi utasema nina pesa nyingi kiasi gani, bado utafika mahali utachukuliwa na maji tu, hata ukimtegemea mwanadamu Fulani, bado uzima wa milele hutaweza kuupata.
Na ndio maana kuna wakati Bwana Yesu alisema ili nyumba iwe salama, ni lazima ijengwe kwanza juu ya msingi, vinginevyo ikijengwa bila msingi upo wakati hata upepo wa kasi ukivuma tu, nyumba hiyo itakuwa gofu.. Na msingi huo ni Yesu Kristo. Soma..
Mathayo 7:24 “Basi kila asikiaye hayo maneno yangu, na kuyafanya, atafananishwa na mtu mwenye akili, aliyejenga nyumba yake juu ya mwamba;
25 mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, isianguke; kwa maana misingi yake imewekwa juu ya mwamba”.
Lakini pia upo wakati utapitia mahali ambapo huwezi kuchimba msingi chini yako, kwasababu chini yapo maji mengi, ipo bahari, lipo ziwa, n.k. kwamfano wanaosafiri kwa meli, wanajua ili kujilinda na hatari ya upepo mkali au dhoruba, inawapasa watembee na kifaa kingine cha kipekee , kinachoitwa NANGA.
Nanga kazi yake ni kwenda chini sana, kuhakikisha inashuka mahali ambapo bahari au ziwa linaishia, na kukutana na mwamba chini, kisha inajikita pale,, sasa ikishanasa hapo hata dhoruba ya upepo mkali ikipita kule juu ni ngumu kikipindua chombo..
Sifa ya Nanga ni kuwa inakwenda mbali sana, kutafuta msingi.. Jambo ambalo kitu kingine chochote hakiwezi kufanya..msingi wa nyumba unashuka mita mbili tatu, lakini nanga inashuka hata mita 300 au 500, kutafuta mwamba.
Ndivyo ilivyo kwa mtu aliyempokea Yesu kwa moyo wake wote leo,..Mungu anachofanya kuanzia huo wakati ni kuwa anamshushia nanga ya roho , inayoitwa TUMAINI, ambayo hiyo inakwenda moja kwa moja mpaka kwenye moyo wa Kristo (Mwamba halisi), kukuanganisha wewe na yeye, kiasi kwamba hata mawimbi makali vipi yaje mbele yako, hayawezi kukugharikisha..japokuwa chini yako hakuonekani msingi wowote.
Utapitia misukosuko ya kila namna, utapitia dhiki, utapitia kuumizwa, utapitia kila aina ya taabu kwa ajili ya imani yako, lakini kung’olewa katika mstari wa wokovu ni jambo ambalo halitawezekana daima.. Watu wataangalia msingi wako mbona hatuooni, wataoni ni kikamba tu kidogo kimeshuka majini, lakini huko chini kuna chuma kizito kinene, kimejikita kwenye mwamba mgumu sana (Yesu Kristo) Kiasi kwamba huwezi kutikiswa, na wimbi lolote la ibilisi.
Waebrania 6:18 “….sisi tuliokimbilia kuyashika matumaini yale yawekwayo mbele yetu;
19 TULIYO NAYO KAMA NANGA YA ROHO, YENYE SALAMA, YENYE NGUVU, yaingiayo hata mle mlimo ndani ya pazia,
20 alimoingia Yesu kwa ajili yetu, mtangulizi wetu, amekuwa kuhani mkuu hata milele kwa mfano wa Melkizedeki”.
Lakini kama hujampa Kristo maisha yako, au upo vuguvugu tu, yaani mguu mmoja nje, mwingine ndani, haueleweki, basi Tumaini hili Mungu hawezi kuliweka ndani yako..Na ndio hapo utashangaa, mtu dhoruba kidogo tu imemjia kashaurudia ulimwengu, ni kwasababu hakuchagua kumfuata Yesu kwa moyo wake wote..Nanga ile haikushushwa kukutana na mwamba usiotikisa ulionana chini ya bahari.
Ndugu wokovu ni jambo halisi sana, na ni nguvu ya Mungu kwelikweli, mtu yeyote anayedhamiria kumfuata Yesu, nanga hii ni lazima atashushiwa asilimia mia. Usijitumainishe na dini, au dhehebu, au mtu yeyote anayejiita mtume au nabii, au chochote kile, vyote haviwezi kukuokoa hapa duniani ni Kristo tu peke yake.
Na wokovu unakuja kwa kuamini, na kubatizwa, unapooamini moja kwa moja unakuwa tayari na kwenda kubatizwa pia katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO. Na baada ya hapo unaanza kuishi maisha ya mtu kama aliyeokolewa..
Hapo ndipo Mungu analeta tumaini hili ndani yako, ambalo wimbi lolote la adui halitaweza kukuondosha..
Hivyo kama wewe upo nje ya Kristo au ulikuwa vuguvugu na ndio maana ulimwengu ukakushinda, ni wakati wako sasa huu kufanya uamuzi sahihi, dhamiria wewe mwenyewe kwanza kutoka katika moyo wako, kisha piga magoti tubu kuonyesha kwamba unahitaji msaada kutoka kwa Mungu, na kukiri makosa yako, kisha anza hatua za kutafuta ubatizo sahihi wa kuzamishwa kwenye maji mengi (kama utahitaji wasiliana nasi),.Na baada ya hapo anza kuishi maisha yanayoendeana na toba yako..
Na kuanzia huo wakati na kuendelea utaona mabadiliko makubwa maishani mwako kwa Yule Roho Mtakatifu atakapokuwa ameletwa ndani yako.. Kwasababu wokovu una nguvu zaidi ya jambo lingine lolote hapa duniani.
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Daawa ni nini kama tunavyosoma katika biblia?
Naomba kujua nini maana ya kuteguka uvungu wa paja?
JE! KUNA UCHAWI KATIKA KUTENDA WEMA?
JIEPUSHE NA UNAJISI.
WEWE NI BWANA UNIPONYAYE.
Naomba kujua nini maana ya kuteguka uvungu wa paja?
Marijani ni nini?
Ni madini ya thamani, yenye rangi iliyo katikati ya wa waridi/pinki na nyekundu iliyokolea (rangi ya damu). Yamezoeleka kuitwa kwa jina la kiingereza “Ruby”. Tazama picha juu.
Kwenye biblia madini haya yametajwa sehemu nyingi kufunua vitu mbalimbali;
Kwamfano, katika Ayubu, inasema thamani ya hekima, haiwezi kufananishwa na thamani ya kito chochote, sio dhahabu wala marijani wala chochote, thamani ya hekima ipo mbali sana.
Ayubu 28:17 “Dhahabu na vioo haviwezi kulinganishwa nayo; Wala kubadili kwake hakutakuwa kwa vyombo vya dhahabu safi.
18 Havitatajwa fedhaluka wala bilauri; Naam, kima cha hekima chapita marijani”.
Maombolezo 4:7 “Wakuu wake walikuwa safi kuliko theluji, Walikuwa weupe kuliko maziwa; Miili yao, walikuwa wekundu kuliko marijani, Na umbo lao kama yakuti samawi”.
Ezekieli 27:16 “Shamu alikuwa mfanya biashara kwako, kwa sababu ya wingi wa kazi za mkono wako walifanya biashara kwa zumaridi, na urujuani, na kazi ya taraza, na kitani safi, na marijani, na akiki, wapate vitu vyako vilivyouzwa”.
Mithali 3:13 “ Heri mtu yule aonaye hekima, Na mtu yule apataye ufahamu.
14 Maana biashara yake ni bora kuliko biashara ya fedha, Na faida yake ni nyingi kuliko dhahabu safi.
15 Yeye ana thamani kuliko marijani, Wala vyote uvitamanivyo havilingani naye”.
Mithali 8:11 “Maana hekima ni bora kuliko marijani; Wala vyote vinavyotamanika havilingani nayo”.
Mithali 20:15 “Dhahabu iko, na marijani tele; Lakini midomo ya maarifa ni kito cha thamani”.
Vilevile biblia inataja ukubwa wa thamani wa mwanamke aliye mwema, na kusema thamani yake ni zaidi ya dini la marijani.
Mithali 31:10 “Mke mwema, ni nani awezaye kumwona? Maana kima chake chapita kima cha marijani”.
Hivyo na sisi, tukijikita kuitafuta Hekima, basi ni zaidi ya tunavyoitafuta almasi, au dhahabu, au ruby, au dini lingine lolote, kwasababu thamani na utajiri wa hekima na maarifa, ni wa kudumu, lakini mali na vito ni vya kupita tu.
Na hekima ya Mungu ni YESU KRISTO biblia inatuambia hiyo katika 1Wakorintho 1:23-24
Hivyo ukimpata Yesu kweli kweli katika moyo wako, umepata vyote, vya mwilini na rohoni..
Faidi yako ni kuwa hata ukifa unaouhakika wa uzima wa milele.
Swali ni je! Mimi na wewe tumeshamkaribisha Yesu maishani mwetu? Kama sivyo basi huu ndio wakati. Hivyo ikiwa utapenda kufanya leo uamuzi huo, basi fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba >> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Bwana akubariki.
Tazama maana ya mawe mengine katika biblia, pamoja na masomo chini.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Bilauri ni nini kibiblia?(Ufunuo 21:11,22:1)
Zabarajadi ni nini katika biblia (Ufunuo 21:20)?
NI NANI ATAKAYETUTENGA NA UPENDO WA KRISTO?
NGUVU YA HEKIMA NA AKILI
UNYAKUO.
Bilauri ni glasi, Na kama tunavyojua glasi huwa zina mwonekano mzuri wa kung’ara na wakuvutia, usiositiri uchafu, zimetengenezwa kwa madini yanayoitwa Crystal, tazama picha juu,
Katika biblia sehemu nyingi Neno hili limetumikia, na hiyo ni kufunua uzuri wa kitu, au mtu au Mungu au mahali fulani..Kwa mfano utaona, mstari huu,
Wimbo 7:2 “Kitovu chako ni kama bilauri iliyoviringana, Na isikose divai iliyochanganyika; Tumbo lako ni mfano wa chungu ya ngano, Iliyozungukwa na ugo wa nyinyoro”;
Kuonyesha uzuri, aliokuwa nao mpenzi wake anayemzungumzia hapo.
Ukisoma tena;
Mithali 23:31 “Usiitazame mvinyo iwapo ni nyekundu; Iitiapo bilauri rangi yake, ishukapo taratibu”
Pia,
Ezekieli 1:22 “Tena juu ya vichwa vya viumbe hai palikuwa na kitu mfano wa anga, kama rangi ya bilauri, lenye kutisha, limetandwa juu ya vichwa vyao”.
Vilevile..
Ufunuo 4:6 “Na mbele ya kile kiti cha enzi kulikuwa na mfano wa bahari ya kioo, kama bilauri; na katikati ya kile kiti cha enzi, na pande zote za kile kiti, walikuwako wenye uhai wanne, wamejaa macho mbele na nyuma”.
Soma pia; Ufunuo 22:1 na,
Ufunuo 21:10 “Akanichukua katika Roho mpaka mlima mkubwa, mrefu, akanionyesha ule mji mtakatifu, Yerusalemu, ukishuka kutoka mbinguni kwa Mwenyezi Mungu;
11 wenye utukufu wa Mungu, na mwangaza wake ulikuwa mfano wa kito chenye thamani nyingi kama kito cha yaspi, safi kama bilauri”;
Unaona?
Hivyo, kwa ufupi ni kuwa makao tuliyoandaliwa kule mbinguni, hayaelezeki kwa namna ya kibinadamu, na ndio maana utaona hapo biblia inatumia neno “KAMA”, kama Bilauri/glasi, lakini bado bilauri lenyewe halielezea ipasavyo uzuri uliopo kule, hivyo, cha kufanya ni mimi na wewe, tufanye bidii ili tuwe na uhakika kuwa yaliyopo kule hatuyakosi.
Na hiyo inakuja kwanza kwa kutubu dhambi zetu kwa kumaanisha kabisa kuziacha, kisha, tukishatubu tunakubali kwenda kubatizwa katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi, na kwa jina la Yesu Kristo, kwa ajili ya ondoleo la dhambi zetu, sawasawa na Matendo 2:38, na baada ya hapo Roho Mtakatifu ataletwa ndani yetu, ili kutufundisha na kututia katika kweli yote. Mpaka siku ile ya unyakuo itakapofikia.
Je! na wewe upo tayari kufanya hivyo leo? Kama upo tayari basi fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba na mambo mengine. >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA
Na Bwana akubariki sana.
Pia angalia maana nyingine za maneno ya biblia chini.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Zabarajadi ni nini katika biblia (Ufunuo 21:20)?
Neno beramu lina maana gani katika biblia?
JE KANISA LITAPITIA DHIKI KUU?
MAJONZI YA MTUME PAULO KWA NDUGU ZAKE.
Kwanini Bwana aliongea na Abramu baada ya kutengeana na Lutu?
MPINGA-KRISTO