Category Archive Home

“Kinga kilichotolewa motoni “Kinafunua nini kibiblia?

SWALI: Kwanini Yoshua aliambiwa yeye ni kinga kilichotolewa motoni? Hichi kinga kilichotolewa motoni kina maana gani kibiblia?


JIBU: Kinga ni kama kijiti, hivyo inaposema kinga cha moto inamaanisha kijiti cha moto. Neno hilo utaliona sehemu kadha wa kadha katika biblia, na hususani wakati ule, Yoshua kuhani mkuu alipokuwa amesimama mbele za Mungu, na shetani naye amesimama pembeni yake kumshitaki, Lakini yule malaika aliyekuwa amesimama pembeni yake, aliyazungumza maneno haya;

Zekaria 3:1 “Kisha akanionyesha Yoshua, kuhani mkuu, amesimama mbele ya malaika wa Bwana, na Shetani amesimama mkono wake wa kuume ili kushindana naye.
2 Bwana akamwambia Shetani, Bwana na akukemee Ewe Shetani; naam, Bwana, aliyechagua Yerusalemu, na akukemee; JE! HIKI SI KINGA KILICHOTOLEWA MOTONI?
3 Basi, Yoshua alikuwa amevaa nguo chafu sana, naye alikuwa akisimama mbele ya malaika.
4 Naye huyo akajibu, akawaambia wale waliosimama mbele yake, akisema, Mvueni nguo hizi zenye uchafu. Kisha akamwambia yeye, Tazama, nimekuondolea uovu wako, nami nitakuvika mavazi ya thamani nyingi”.

Sasa ukisoma kwa ukaribu maneno hayo, utaona sio Yoshua anaambiwa yeye ni kinga kilichotolewa motoni, bali ni Yerusalemu ndio inayofananishwa na kinga kilichotolewa motoni.

Kama tunavyojua kipande chochote cha mbao kikiingia kwenye moto, huwa hakina namna ni lazima kiteketee tu, tofauti na vitu vingine kama chuma. Sasa kama kimetolewa motoni, inamaanisha kimenyakuliwa kutoka katika uharibifu uliokuwa unakila.

Hivyo Malaika wa Mungu alikuwa anamwambia shetani, kuwa Yerusalemu, ambayo Mungu alikuwa ameiteketeza ili ipotee kabisa milele, sasa ameihurumia na kuiokoa tena imsimamishie nyumba, na Yoshua huyu aliyesimama hapa ndiye atakuwa kuhani mkuu katika nyumba itakayojengwa Yerusalemu.

Israeli tangu ilipoasi Mungu  aliiweka katika  moto wa mfalme wa Babeli Nebukadreza, ili aingamize kabisa, Na ndio maana ukisoma Yeremia 29: 22 Utaona Mungu anatoa unabii kwa wale manabii wa uongo waliokuwa wanaitabiria Israeli habari za amani wakati hakuna amani, na kuwaambia kwamba huyu mfalme wa Babeli ndio atakuwa wa kwanza kuwaoka, hawa manabii katika moto.

Yeremia 29:22 “Tena katika habari zao laana itatumiwa na wafungwa wote wa Yuda, walioko Babeli, kusema, Bwana akufanye uwe kama Sedekia, na kama Ahabu, ambao mfalme wa Babeli aliwaoka motoni”

Neno hilo utaliona tena, sehemu nyingine  kwenye biblia ambapo Mungu aliiadhibu Israeli kwa mapigo ya kila namna, mfano wa Sodoma na Gomora, aliitia katika moto wa uharibifu, lakini baadhi yao aliowapa neema ya kuokoka hawakutambua kuwa wamenyakuliwa katika moto, kama vinga vilivyokuwa vinateketea, bali waliendelea kutenda maovu..

Amosi 4:7 “Tena nimeizuia mvua msiipate, ilipobaki miezi mitatu kabla ya mavuno; nami nimenyesha mvua juu ya mji mmoja, nikaizuia mvua isinyeshe juu ya mji mwingine; sehemu moja ilipata mvua, na sehemu isiyopata mvua ilikatika.
8 Basi kutoka miji miwili mitatu walitanga-tanga kuendea mji mwingine wapate kunywa maji, wasipate ya kuwatosha; lakini hamkunirudia mimi, asema Bwana.
9 Nami nimewapiga kwa ukavu na koga; wingi wa bustani zenu na mashamba yenu ya mizabibu, na mitini yenu na mizeituni yenu imeliwa na tunutu; Lakini hamkunirudia mimi, asema Bwana.
10 Nimewapelekea tauni, kama tauni ya Misri; vijana wenu nimewaua kwa upanga, na farasi wenu nimewachukulia mbali; nami nimeupandisha uvundo wa matuo yenu na kuuingiza katika mianzi ya pua zenu; lakini hamkunirudia mimi, asema Bwana.

11 Baadhi yenu nimewaangamiza, kama hapo MUNGU ALIPOIANGAMIZA SODOMA NA GOMORA, NANYI MKAWA KAMA KINGA KILICHONYAKULIWA MOTONI; LAKINI HAMKUNIRUDIA MIMI, ASEMA BWANA.

Soma pia Isaya 7:4

Hata sasa, dunia inapopitia katika majanga mengi ya maafa, lakini tukijiangalia sisi bado tupo hai, tujue kuwa ni Mungu anatutaka sisi tutubu, kama sio kwenda kumtumikia kama iliyokuwa kwa Yoshua.

Tunapoepushwa na matetemeko ya ardhi, vimbunga, magonjwa makali ya kuua kama hili la CORONA, tujue kuwa ni vinga vilivyo nyakuliwa motoni, tunapaswa tujue huu ni wakati wa kutubu na kumrudia Mungu wetu kwasababu ulimwengu upo motoni.

Lakini tukipuuzia tukajiona kama sisi ni wa kipekee sana, tujue kuwa tutakutana na adhabu kali Zaidi ya hizi tulizonazo sasa hivi. Mungu ni moto ulao.

Tuyatambue makosa yetu tumrudie Mungu.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

 

 

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengine

Mada Nyinginezo:

JINSI SHETANI ANAVYOZUIA MAJIBU YA MAOMBI YETU.

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 2

Nini maana ya uvuvio?.

Kuwatema farasi, maana yake ni nini?

UFUNUO: Mlango wa 15

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya “Tumejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii”?

Jibu: Tusome..

Waefeso 2: 20 “Mmejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii, naye Kristo Yesu mwenyewe ni jiwe kuu la pembeni”.

Katika mstari huo yapo mambo makuu mawili ya kuzingatia kwa makini.

1) Msingi na 2) Mitume na manabii

Tukianza na Msingi.

Hapo anasema mmejengwa juu ya “Msingi” na si “misingi”. Maana yake ni msingi mmoja tu, na si mingi.. Na anaendelea kwa kusema..”mmejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii”..na sio “mmejengwa juu ya mitume na manabii”.. Maana yake ni kwamba msingi waliokuwa nao mitume na manabii ndio sisi pia tunajengwa juu ya huo.. Mtu akisema “natembea juu ya misingi na kanuni za Baba yangu au babu yangu, hajamaanisha anatembea juu ya baba yake”..Bali juu ya kanuni na taratibu alizorithishwa na Baba yake, ambazo hata baba yake alikuwa anazifuata na kuziishi….Kadhalika na hapo, Neno la Mungu linasema, mmejengwa juu ya msingi wa Mitume na manabii, maana ya kuna msingi ambao Mitume na manabii walikuwa wanaiishi na kuifuata, na hatimaye wakairithisha kwa kizazi kinachofuata. Kwa misingi hiyo ndio sisi tunajengwa.

Sasa kabla ya kujua vizuri huo msingi ni nini, hebu tujue kwanza hawa Mitume na Manabii wanaozungumziwa hapo ni wakina nani?..

Tofauti na inavyodhaniwa kwamba Mitume na Manabii wanaozungumziwa hapo, ni kundi la manabii na Mitume wanaozuka leo… unakuta inatokea mtu fulani mahali fulani anayejiita Mtume au Nabii, anaanza kujigamba kwamba karama yake ndio karama kuu yakulijenga kanisa. Na kwamba yeye ndio msingi na kanisa, limejengwa juu yake. Jambo ambalo ni uongo, tena kwa asilimia zote.

Mitume na Manabii wanaozungumziwa hapo ni Manabii wote wa agano la kale, na Mitume wa kanisa la kwanza wa agano jipya.  Hao Msingi waliouweka na kuufuata ndio msingi sisi tunaojengwa juu ya huo na huo si mwingine zaidi ya  biblia takatifu, ambapo ndio tunanukuu maneno kutoka huko.  Ndio maana leo hii, msingi ni biblia takatifu, Maneno yaliyoandikwa na Mitume kama Paulo, Petro, Yohana, Yakobo n.k hayo ndio msingi wetu leo hii, ndio maana leo hatunukuu Neno la Nabii yeyote aliyepo leo, wala Mtume  yeyote aliyepo leo na kulihubiri hilo, kana kama ni Neno la Mungu, badala yake tunanukuu maneno yaliyoandikwa na Mtume Paulo, au Nabii Isaya, au Nabii Yoeli n.k..Hao ndio mitume na manabii ambao tumejengwa juu ya msingi wao.

Kwahiyo mtu yeyote anayejiita mtume au nabii au mwalimu au muinjilisti, na anasema na kujivuna kwamba kanisa limejengwa juu yake, na kujivuna kwamba yeye ndio nguzo kuu, au karama yake ndio karama kuu…kwa kufuatia huo mstari, mtu huyo anadanganya aidha kwa kujua au kwa kutokujua.

Msingi wetu sisi ni biblia takatifu, ambayo imeandikwa na mitume wa Yesu na manabii wa agano la kale, hao ndio Mababa. Na kiini cha biblia takatifu ni YESU KRISTO. Vitabu vyote katika biblia vimebeba habari au unabii wa Yesu Kristo, hakuna kitabu hata kimoja kisichobeba ufunuo wa Yesu Kristo ndani ya biblia. Kwasababu yeye ndio Mungu mwenyewe katika Mwili. (1Timotheo 3:16).

1Wakoritho 3:11 “Maana msingi mwingine hakuna mtu awezaye kuuweka, isipokuwa ni ule uliokwisha kuwekwa, yaani, Yesu Kristo”.

Je umemwamini Yesu?, umepokea Roho Mtakatifu?..Kama bado mwamini leo na kumkabidhi maisha yako, naye atakupa kipawa cha Roho wake Mtakatifu (Matendo 2:38)

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengine


Mada Nyinginezo:

Je! Imani ya mitume ipo katika maandiko?

Mtume Paulo alikuwa na maana gani kusema katika 1Wakorintho 15:31″…NIKAKUFA KILA SIKU?

TUSIWE WATU WA KUPUNGUKIWA AKILI.

JINSI PAULO ALIVYOPAMBANA NA UJINGA WA ROHONI.

POPOBAWA NI KWELI YUPO?

Rudi nyumbani

Print this post

MZUNGUKO WAKO NI UPI?

Ukichunguza utaona Mungu kaweka vitu vingi vya asili katika mzunguko wake. Na kulikuwa na sababu maalumu wa yeye kufanya hivyo..

Mhubiri 1:6 “Upepo huvuma kusi, hugeuka kuwa kaskazi; hugeuka daima katika mwendo wake, na upepo huyarudia mazunguko yake.

7 Mito yote huingia baharini, walakini bahari haijai; HUKO IENDAKO MITO, NDIKO IRUDIKO TENA”.

Hakushindwa kuufanya upepo upotelee tu huko hewani, au maji yapotelee tu ardhini, lakini ameamua kuyaweka katika mzunguko, kiasi kwamba hayo maji unayoyamwaga sasa hivi kwenye sinki, kuna wakati Fulani yatakurudia wewe  na utayatumia tena.

Hiyo ni kufunua kuwa kuna mambo mengi ya rohoni yapo kwenye mzunguko wake, na tusipoitambua mizunguko hiyo, yatatupita mengi kama sio kupata hasara nyingi sana.

Lolote unalolifanya sasa hivi, liwe ni jema au baya, moja kwa moja linaingizwa katika mzunguko huu wa rohoni usioonekana. Kama ni baya litaondoka lakini siku moja litakurudia tu.. haijalishi litachukua umbile gani.

Kama ni jema vilevile litakurudia tu, haijalishi litachukua umbile gani baadaye.. Hivyo ni vizuri ukajua wewe upo katika mzunguko upi, Na ndio maana Bwana Yesu alisisitiza sana maneno haya.

Mathayo 7:12 “Basi yo yote myatakayo mtendewe na watu, nanyi watendeeni vivyo hivyo; …”.

Luka 6:38 “Wapeni watu vitu, nanyi mtapewa; kipimo cha kujaa na kushindiliwa, na kusukwa-sukwa hata kumwagika, ndicho watu watakachowapa vifuani mwenu. Kwa kuwa kipimo kile kile mpimacho ndicho mtakachopimiwa”.

Ufunuo 13: 10 “Mtu akichukua mateka, atachukuliwa mateka. Mtu akiua kwa upanga, atauawa kwa upanga…”

Hizi ndio kanuni za asili ambazo mtu yeyote akizitumia hata kama sio mkristo, zitamletea majibu tu. Na ndio maana watu wengi wanashangaa kwanini mataifa yaliyoendelea yanazidi kutajirika, japokuwa hayamchi Mungu.

Ukiangalia utagundua kuwa  yanatoa misaada mingi  kila mwaka kwa mataifa maskini, na ndio maana yanazidishiwa.

Vilevile ukimpa Mungu, Ni kama vile umeingizwa kwenye mfumo wa mzunguko wa Baraka zake rohoni, pengine utaona kama umepoteza, lakini siku isiyokuwa na jina kitakurudia tu, kikiwa kimeshindiliwa na kusukwa sukwa, na kumwagika, kinaweza kisirudi kwa namna ile ile, lakini kitarudi kwa thamani ile ile tena mara dufu.

Mithali 11:25 “Nafsi ya mtu mkarimu itawandishwa; Anyweshaye atanyweshwa mwenyewe”.

Lakini ukiwa mwovu, unaiba, unawarusha watu, unadhulumu haki za wengine,  mchoyo, mbinafsi, unawachonganisha wengine, unaua, moja kwa moja unaingia katika mzunguko huo wa laana za waovu, na mwisho wa siku malipo yake yatakurudia kichwani pako ukiwa hapa hapa duniani, tena kwa kusukwa-sukwa na kuzidishiwa na kumwagika.

Mithali 11:31 “Tazama, mwenye haki atalipwa duniani; Basi mwovu na mkosaji si mara nyingi Zaidi”?

Kwa maneno hayo machache Mungu atufumbue macho yetu tuelewe tupo katika mzunguko upi. Ili tuishi maisha ya mafanikio hapa duniani.

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengine

Mada Nyinginezo:

HALI ZETU JINSI ZINAVYOWEZA KUATHIRI UTOAJI WETU.

KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 1

Neno Bildi linamaanisha nini kwenye biblia(Matendo 27:28) ?

Je tunapaswa tushiriki Meza ya Bwana mara ngapi?

BIBLIA INAITAJA NJIA KUU YA MFALME, NJIA HII NI IPI?

JE UPENDO WAKO UMEPOA?

Rudi nyumbani

Print this post

NI NINI KITAKACHOTUFANYA TUPIGE MBIO BILA KUPUNGUZA MWENDO?

Paulo akijua kuwa anakaribia ukingoni kabisa mwa safari yake, hakujali taarifa yoyote mbaya iliyoletwa mbele yake, utaona yeye mwenyewe anasema, mji kwa mji Roho Mtakatifu alimshuhudia kuwa vifungo na dhiki nyingi vinamngojea kule Yerusalemu alipokusudia kwenda, lakini bado alisema, siachi kupiga mbio nimalize mwendo wangu.

Matendo20:23 “isipokuwa Roho Mtakatifu mji kwa mji hunishuhudia akisema, ya kwamba vifungo na dhiki vyaningoja.

24 Lakini siyahesabu maisha yangu kuwa kitu cha thamani kwangu kama kuumaliza mwendo wangu na huduma ile niliyopokea kwa Bwana Yesu, kuishuhudia Habari Njema ya neema ya Mungu”.

Kama hilo halitoshi alipofika Kaisaria, karibu kidogo na Yerusalemu, Nabii mmoja aliyeitwa Agabo, alitokea na kumtolea unabii kwa uweza wa Roho Mtakatifu akisema, Paulo atakwenda kufungwa, na kupata dhiki, hivyo asiende, Yerusalemu.

Lakini hilo nalo halikumfanya Paulo, aache kwenda Yerusalemu, badala yake aliwaambia;

Matendo 21:13 “Ndipo Paulo alipojibu, Mnafanya nini, kulia na kunivunja moyo? Kwa maana mimi, licha ya kufungwa, ni tayari hata kuuawa katika Yerusalemu kwa ajili ya jina lake Bwana Yesu”.

Unaona, alifikia hatua, mawazo yake yote yalikuwa  ni kuimalizia kazi yake kwa kishindo, kiasi cha kutojali dhiki zozote atakazokumbana nazo mbele yake

Sasa usifikirie ni jambo rahisi kuchukua maamuzi hayo kama asingekuwa ni mtu anayefahamu ni nini anakitafuta.. Paulo alikuwa ni mtu mwenye malengo, ni mtu aliyekuwa anatazama vya mbali sana, alijua kupiga mbio huko kuna tuzo Fulani kubwa mbeleni, hivyo ni sharti aishindanie kwa nguvu ili asiikose.

1Wakorintho 9:24 “Je! Hamjui, ya kuwa wale washindanao kwa kupiga mbio, hupiga mbio wote, lakini apokeaye tuzo ni mmoja? Pigeni mbio namna hiyo, ili mpate.
25 Na kila ashindanaye katika michezo hujizuia katika yote; basi hao hufanya hivyo kusudi wapokee taji iharibikayo; bali sisi tupokee taji isiyoharibika.
26 Hata mimi napiga mbio vivyo hivyo, si kama asitaye; napigana ngumi vivyo hivyo, si kama apigaye hewa;
27 bali nautesa mwili wangu na kuutumikisha; isiwe, nikiisha kuwahubiri wengine, mwenyewe niwe mtu wa kukataliwa”

Unaona alijua sikuzote mkimbiaji ambaye anajua lengo la kukimbia kwake ni nini huwa hakimbii kwa kuubembeleza mwili, bali anakimbia huku mawazo yake yakuwa kweney tuzo iliyowekwa mbele yake, hilo ndilo linalomfanya asitembee tembee njiani, asikubali kuusikiliza mwili, kwamba umechoka, hivyo apunguze mwendo.

Hali kadhalika mkimbiaji mzuri kwa namna ya kawaida, anapokaribia mzunguko wake wa mwisho ndio huwa anaongeza mwendo Zaidi, na ndicho alichokifanya Paulo.

Embu tumtazame mtu mwingine wa mwisho ambaye safari yake sikuzote ilikuwa ni ya mwendo tu, mtu ambaye yeye hakujali kikwazo chochote alipokuwa anamalizia mwendo wake hapa duniani. Na huyo si mwingine Zaidi ya Bwana wetu Yesu Kristo.

Biblia inatuambia wakati wa kupaa kwake ulipokaribia, “ALIUKAZA” uso wake kwenda Yerusalemu.

Luka 9:51 “Ikawa, siku za kupaa kwake zilipokuwa karibu kutimia, yeye aliukaza uso wake kwenda Yerusalemu;
52 akatuma wajumbe kutangulia mbele ya uso wake; wakaenda wakaingia katika kijiji cha Wasamaria, ili kumtengenezea mahali.
53 Lakini wenyeji hawakumkaribisha kwa vile alivyouelekeza uso wake kwenda Yerusalemu”.

Kuukaza uso maana yake, ni kutokuwa tayari kuambiwa chochote, au kushauriwa chochote au kukwamishwa na chochote mpaka utimize malengo yako uliyoyakusudia mbele yako. Ndivyo ilivyokuwa kwa Bwana Yesu, wakati ambapo anajua amebakiwa na kipindi kifupi sana, amalize mwendo wake pale Yerusalemu, huku akijua moyoni mwake kuwa Mateso makali anakwenda kukumbana nayo, kusulibiwa, yeye hakujali chochote, Zaidi ndio alilazimisha kwenda huko huko.

Yohana 10:7 Kisha, baada ya hayo, akawaambia wanafunzi wake, Twendeni Uyahudi tena.
8 Wale wanafunzi wakamwambia, Rabi, juzijuzi tu Wayahudi walikuwa wakitafuta kukupiga kwa mawe, nawe unakwenda huko tena?

Je na sisi kipindi hichi cha kufunga majira, bado tunapiga mbio au tumepunguza mwendo wetu wa Imani ? Pengine tumeacha kukimbia kwasababu hatujajua malengo yetu ni nini? tunakumbana na milima mrefu, tunakata tamaa, lakini pia tunapaswa tujue jambo moja ili uitwe mlima ni lazima utakuwa na upande wa pili wa mteremko pia.

Ni heri maisha mafupi ya hapo duniani, tuyaishie kupanda mlima, lakini tutakapofika kule ng’ambo kwenye umilele tuyaishie kwenye mteremko,..

Hizi ndizo nyakati za kuzidisha mwendo, kutojali vitisho vyovyote vya kiimani, vitisho  vya ndugu, au rafiki, au majirani, kwasababu kama unyakuo hautatukuta, basi pia siku zetu za kuishi duniani zinapungua siku baada ya siku.

Hivyo tupige mbio tukijua kuwa zipo tuzo mbele yetu zinatungojea, lakini tukiwa walegevu hatutazipata.

2Timotheo 2:5 “Hata mtu akishindana katika machezo hapewi taji, asiposhindana kwa halali”.

Shalom

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengine

Mada Nyinginezo:

DAMU YA ZAKARI BIN BARAKIA.

HEKIMA YA KIMUNGU, INAINGIAJE MIOYONI MWETU?

NITAFANYA YERUSALEMU KUWA JIWE LA KUWALEMEA .

JINSI PAULO ALIVYOPAMBANA NA UJINGA WA ROHONI.

Nini maana ya neno ‘Kuabiri’ kama linavyotumika katika  biblia?

Rudi nyumbani

Print this post

ELIMA MCHAWI, ANAFANYA KAZI HADI SASA.

Sikuzote roho haiji hivi hivi tu, bila kuwa na chanzo Fulani, na chanzo hicho kinaweza kuwa mtu, au kitu au sehemu, Sasa pale yule mtu anapoondoka, huwa anaacha tabia yake Fulani inayoendelea na tabia hiyo ikishakita mizizi vizuri ndio inaitwa roho,..

Kwamfano kwenye biblia utamwona mwanamke anaitwa Yezebeli, huyu mwanamke alikuwa ni mchawi, na mzinzi, na tabia zake tunazijua vizuri kwenye biblia, jinsi alivyoiharibu Israeli na kuigeuzwa kuwa nchi ya kichawi. Lakini tunasoma mara baada ya kufa kwake, roho yake iliendelea kutembea duniani, na ndio maana miaka mingi baadaye utaona Bwana Yesu anamzungumzia tena habari zake kana kwamba bado yupo duniani, katika kitabu cha Ufunuo,

Ufunuo 2:19 “Nayajua matendo yako na upendo na imani na huduma na subira yako; tena kwamba matendo yako ya mwisho yamezidi yale ya kwanza.
20 Lakini nina neno juu yako, ya kwamba wamridhia yule mwanamke Yezebeli, yeye ajiitaye nabii na kuwafundisha watumishi wangu na kuwapoteza, ili wazini na kula vitu vilivyotolewa sadaka kwa sanamu”

Utamwona pia Eliya, pindi alipoondoka roho yake ilianza kutembea tena wakati baada ya wakati, Kumbuka hawi Eliya mwenyewe kama Eliya, Au Yezebeli kama Yezebeli, bali ile tabia  ya rohoni iliyokuwa juu ya Eliya, ndiyo inayotembea juu ya watu kadha wa kadha, Roho hiyo ilikuja juu ya Elisha, baadaye Yohana Mbatizaji n.k. na itaendelea kutembea hadi wakati wa nyakati za mwisho kabisa.(Malaki 4:5)

Halikadhali Na Bwana wetu Yesu Kristo, yeye alitembea hapa duniani, kwa miaka 33 na nusu, lakini alipoondoka, hakuondoka hivi hii ilikuwa ni sharti aichalie Roho yake katikati yetu, na ndio Roho Mtakatifu tuliye naye sasa. Kiasi kwamba mtu akiyaamini maneno yote ya Bwana Yesu moja kwa moja anampokea Roho wake ambaye atamsaidia aishi maisha kama ya Yesu.

Sasa tukishaweka msingi kama huo, tuende moja kwa moja katika somo letu la leo ambalo linamzungumzia yule Elima mchawi aliyekutana na Paulo na Barnaba  pindi walipokuwa wanahubiri injili huko Pafo, tusome.

Matendo 13:6 “Walipokwisha kupita katikati ya kisiwa chote mpaka Pafo, wakaona mtu mmoja, mchawi, nabii wa uongo, Myahudi jina lake Bar-Yesu;
7 mtu huyu alikuwa pamoja na liwali Sergio Paulo, mtu mwenye akili. Yeye liwali akawaita Barnaba na Sauli waje kwake, akataka kulisikia neno la Mungu.
8 Lakini Elima, yule mchawi (maana ndiyo tafsiri ya jina lake), akashindana nao, akitaka kumtia yule liwali moyo wa kuiacha ile imani.
9 Lakini Sauli, ambaye ndiye Paulo, akijaa Roho Mtakatifu, akamkazia macho,
10 akasema, Ewe mwenye kujaa hila na uovu wote, mwana wa Ibilisi, adui wa haki yote, huachi kuzipotoa njia za Bwana zilizonyoka?
11 Basi, angalia, mkono wa Bwana u juu yako, nawe utakuwa kipofu, usilione jua kwa muda. Mara kiwi kikamwangukia na giza, akazunguka-zunguka na kumtafuta mtu wa kumshika mkono na kumwongoza.
12 Ndipo yule liwali, alipoyaona yaliyotendeka, akaamini, akiyastaajabia mafundisho ya Bwana”`.

Huyu mtu alikuwa ni mchawi, na wakati huo huo ni nabii wa Uongo. Kazi yake na lengo lake, lilikuwa ni kuwafanya watu wasiiamini njia ya wokovu, pale tu wanapokutana na injili ya kweli ya msalaba. Ni mchawi aliyebobea kwenye kitendo cha kupinga tu, na kushawishi watu kuiacha imani, na ndio maana mtume Paulo alimwambia “Ewe mwenye kujaa hila na uovu wote, mwana wa Ibilisi, huachi kuzipotoa njia za Bwana zilizonyoka?”

Kwa kazi yake hii, mpaka akawa ameshawafikia kabisa na watu wakubwa na wenye akili kama huyu Sergio Paulo, ikiwa na maana kuwa  huku chini tayari alishaburuza.

Kama tunavyoona hapo, Paulo alipoanza kumuhubiria huyu liwali, yeye bila kupoteza muda alianza kuwabishia wakina Paulo, na kutoa hoja zake za uongo, na pengine kumwambia yule liwali hawa watu ni waongo, wapiga dili, hakuna kitu kuokoka hapa duniani, huyo Yesu aliibiwa hajafufuka, hawa ni wapotoshaji n.k.

Lakini Paulo kulijua hilo, akamkemea saa ile ile akawa kipofu kwa muda.

Sasa huyu mtu alishakufa lakini aliiacha roho yake hapa duniani, na roho hiyo inatembea kwa kasi sana, sasa hivi duniani imewavaa watu wengi, na wenyewe hawajijui kuwa wanafanyika kuwa wachawi, pasipo wao kujijua.

Kuna watu kazi yao ni kupinga tu kila habari ya Kristo, wakiona kila mtumishi wa Mungu anahubiri, au kushuhudia, wanasema ni nabii wa uongo, wanasema ni wazinzi, wakisikia injili ya kweli inahubiriwa wanasema anapotosha,

Sasa kibiblia watu kama hao ni wachawi, hawajijui tu kama wameshafikia hiyo hatua

Katika nyakati hizi za kumalizia ni kujiangalia sana, si kila wazo la kila mtu la kulisikiliza, au kulipokea haijalishi atakuwa ni ndugu yako, au rafiki yako, au mfanyakazi mwenzako. 

Bwana Yesu alisema, angalieni jinsi msikiavyo (Luka 8:18)

Kaa mbali nao, ikiwa unaona kila wakati tu wanakosoa habari za Mungu au watumishi wa Mungu, hakuna kipengele hata kimoja watakisifia, kaa mbali nao, wanakuwekea tu moyo mgumu wa kutokuamini.

Ukikutana na watu kama hao ujue unaongea na wachawi, jiupushe nao. Leo hii duniani utakutana nao wengi sana akina Elimu, Bar Yesu. Wewe jikite katika kumtafuta Muumba wako kwa bidii, mpende Mungu wako, sikiliza na soma Neno la Mungu, achana na hao wanaoipuuzia, au kukejeli kila kitu cha ki Mungu kinachokatiza mbele yao.

Jiepushe nao.

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengine

Mada Nyinginezo:

JINSI PAULO ALIVYOPAMBANA NA UJINGA WA ROHONI.

JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?

Nini maana ya neno ‘Kuabiri’ kama linavyotumika katika  biblia?

ILI NIWE KIELELEZO KWA WALE WATAKAOMWAMINI BAADAYE.

KUMTUMIKIA MUNGU, KUNAWEZA KUWE KINYUME NA MATARIJIO YAKO.

Rudi nyumbani

Print this post

Ni nani aliyesema “Nitume mimi”? katika (Isaya 6:8)


SWALI: Mtumishi wa Mungu! Bwana asifiwe, naomba ufafanuzi kidogo juu ya andiko hili katika Isaya 6:1-10 Ni Nani aliyesema “Nitume Mimi”?je Ni isaya au!? Na kwanini Isaya pia alitakaswa kwa kaa la moto?


JIBU:  Tusome baadhi ya vifungu hivyo;

Isaya 6: 5 “Ndipo niliposema, Ole wangu! Kwa maana nimepotea; kwa sababu mimi ni mtu mwenye midomo michafu, nami ninakaa kati ya watu wenye midomo michafu; na macho yangu yamemwona Mfalme, Bwana wa majeshi.
6 Kisha mmoja wa maserafi wale akaruka akanikaribia; naye alikuwa na kaa la moto mkononi mwake, ambalo alikuwa amelitwaa kwa makoleo toka juu ya madhabahu;
7 akanigusa kinywa changu kwa kaa hilo, akaniambia, Tazama, hili limekugusa midomo yako, na uovu wako umeondolewa, na dhambi yako imefunikwa.
8 Kisha nikaisikia SAUTI YA BWANA, AKISEMA, NIMTUME NANI, naye ni nani atakayekwenda kwa ajili yetu? Ndipo niliposema, MIMI HAPA, NITUME MIMI.
9 Naye akaniambia, Enenda, ukawaambie watu hawa, Fulizeni kusikia, lakini msifahamu; fulizeni kutazama, lakini msione.
10 Uunoneshe moyo wa watu hawa, ukayatie uzito masikio yao, ukayafumbe macho yao; wasije wakaona kwa macho yao, na kusikia kwa masikio yao, na kufahamu kwa mioyo yao, na kurejea na kuponywa”.

Shalom, Unabii huo ulikuwa unamuhusu Nabii Isaya mwenyewe aliyekiandika kitabu hicho, tofauti na watu wengi wanavyodhani kuwa huyo ni Yesu ndiye aliyesema maneno hayo, nitume mimi.?

Hiyo yote ni baada ya Isaya kuijiona amesimama mbele ya kiti cha enzi cha Mungu mbinguni, na kwamba muda mfupi baadaye atahitajika kufanya mahojiano na Mungu. Hivyo kwa kulijua hilo kabla hata hajasema chochote, alijitambua hali yake ilivyo kuwa yeye ni mtu mwenye midomo michafu, akiwa na maana mwongo, msengenyaji, mtukanaji n.k. Jambo ambalo halikuwa kuwa midomoni mwa Yesu, tangu anazaliwa.

Hivyoo akaomba kwanza tiba, asafishwe kinywa chake, kabla ya kuzungumza na Mungu,  ndipo hapo utaona huyo kerubi akichukua kaa la moto kutoka katika madhabahu ya Mungu kwa koleo.. Sasa zingatia hilo neno madhabahu, kaa lile halikutolewa sehemu nyingine yoyote Zaidi ya madhabahuni pa Mungu. Na pia hakupewa kipelekewa kitu kizuri mdomoni labda tuseme embe au ndizi, au tango kimponye badala yake alipelekewa kaa la moto.

Na kama tunavyofahamu moto kazi yake ni kuunguza, tena, mbaya Zaidi pale unapokutana na mdomo, jaribu kutengeza picha kaa jekundu linakuja kugusana na midomo yako, mshituko na maumivu utakayosikia hapo yatakuwa ya namna gani, ni heri ungelikanyaga kwasababu mguu kidogo ni mgumu, kuliko kukutana na ulimi.

Lakini ndiyo njia ambayo Mungu aliichagua kumponya Isaya na midomo yake michafu.

Hata leo hii, ili Mungu aweze kutuponya na midomo ya usengenyaji, uongo, fitina, kiburi, ya faraka, n.k. Ni lazima tukubali kaa la Mungu lipitishwe vinywani mwetu.

Na kaa hilo halitoki sehemu nyingine isipokuwa madhabahuni pa pake, ikiwa hatutaki kukemewa dhambi zetu, hatutaki kukaripiwa, hatutaki kuonywa kwa mafundisho sahihi ya Neno la Mungu, hatutaki kuhubiriwa maneno magumu yanayochomo mioyo yetu, ili tubadilike, kamwe, tusitegemee kama usengenyaji utaondoka vinywani mwetu.

Kama tutapenda wakati wote injili ya kupiga adui zetu, na injili za mafanikio, hatutaki kukemewa dhambi zetu, na kuelezwa uhalisia wa ziwa la moto  kamwe vinywa vyetu haziwezi kuponywa.

Hivyo tukubali kukaripiwa na Mungu, tukubali kukemewa na yeye, kwasababu kwa njia hiyo ndio kaichagua ili kutuponya sisi, hakuna short-cut, Mungu anatujua vizuri sisi wanadamu, wakati mwingine tutahitaji moto ili tuponywe.

Ufunuo 3:19 “Wote niwapendao mimi nawakemea, na kuwarudi; basi uwe na bidii, ukatubu”

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengine

Mada Nyinginezo:

Je! Wana wenu huwatoa kwa nani? maana yake ni nini?

KWANINI MIMI?

Nini maana ya uvuvio?.

UFUNUO: Mlango wa 15

Rudi nyumbani

Print this post

KUJIFUNUA KWA YESU KWA PILI.

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe daima. Ni wasaa mwingine tena ambao Mungu ametujalia kuufikia hivyo  nakukaribisha tuyatafakari  kwa pamoja maneno ya uzima ndugu yangu.

Biblia inatuambia kuwa Bwana Yesu alipofufuka kutoka kwa wafu, aliwatokea baadhi ya watu, ambao idadi yao ilikuwa kama  watu 500,(1Wakorintho 15:6) , Lakini ulishawahi kujiuliza ni kwanini iwe hivyo? Je hao watu 500 walikuwa na kitu gani cha ziada kuwashinda wengine wote mpaka watokewe wao tu?

Ni vizuri tukafahamu kuwa hii ni kawaida ya Kristo, kwamba kuna wakati  ataonekana na watu wote, lakini pia upo wakati hataonekana  na watu wote bali wachache tu aliowachagua, Na ndicho kilichotokea hapa, miaka yote 33 aliyoishi duniani, kila mtu angeweza kumtembelea kama angetaka, kila mtu angeweza kwenda kumtazama kama angetaka, lakini mara baada ya kufufuka kwake, hakuna mtu yeyote angeweza kumwona, isipokuwa Yule tu aliyejidhihirisha kwake.

Na ndio maana aliwaambia wayahudi maneno haya Yohana 7:34 “Mtanitafuta wala hamtaniona; nami nilipo ninyi hamwezi kuja”.

Sasa hawa watu 500 ambao walipata neema ya kumwona Yesu baada ya kufufuka kwake, hawakuwa ni watu tu ambao bahati imewaangukia, hawana habari na Yesu, au hawajawahi kumfuatilia au kumsikia,.. Hapana, biblia inatuambia walikuwa ni watu ambao waliambatana naye, tangu akiwa Galiliya mpaka Yerusalemu, yaani tangu ncha moja ya taifa la Israeli mpaka ncha nyingine ya Israeli.

Matendo 13:29 “Hata walipokwisha kumaliza yote aliyoandikiwa, wakamtelemsha katika ule mti, wakamweka kaburini.

30 Lakini Mungu akamfufua katika wafu;

31 akaonekana siku nyingi na wale WALIOPANDA NAYE KUTOKA GALILAYA HATA YERUSALEMU, ambao sasa ndio walio mashahidi wake mbele ya watu”.

Hawa ndio waliotokewa na Yesu mara ya pili, Ni watu ambao walitembea na Yesu, tangu zamani sana, ni watu ambao waliokuwa wanazungumzia habari zake, Mfano wake utaona ni wale watu wawili waliokuwa wanaelekea kile kijiji cha Emau baada ya kufufuka kwake(Luka 24:13)..

Hao ndio watu ambao Yesu aliona kuna umuhimu wote wa kuwatokea  katika utukufu mwingine baadaye. Siku zote wale wanaomuheshimu Mungu, Mungu nao anawaheshimu, wanaomkaribia Mungu, Mungu naye anawakaribia wao.(Yakobo 4:8). Na mmojawapo kati ya hawa ndiye aliyefanywa mtume kuchukua nafasi ya Yuda.

Sasa kutokea kwake mara ya pili kwao, haikuwa maonyesho tu. Bali Kristo aliwapa karama nyingine ambayo iliwafanya kuwa tofauti kabisa na watu wengine. Na karama yenyewe ni kuwa MASHAHIDI WA YESU.  Hao ndio waliochaguliwa na Mungu kuisambaza injili ya Kristo ulimwenguni kote, kwa nguvu za Roho wa Mungu zilizoachiliwa juu yao,

Matendo 10:40 “Huyo Mungu alimfufua siku ya tatu, akamjalia kudhihirika,

41 SI KWA WATU WOTE, BALI KWA MASHAHIDI WALIOKUWA WAMEKWISHA KUCHAGULIWA NA MUNGU, NDIO SISI, TULIOKULA NA KUNYWA PAMOJA NAYE BAADA YA KUFUFUKA KWAKE KUTOKA KWA WAFU.

42 Akatuagiza tuwahubiri watu na kushuhudia ya kuwa huyu ndiye aliyeamriwa na Mungu awe Mhukumu wa walio hai na wafu”.

Soma pia Matendo 2:31-32

Unaona Ikiwa leo hii, hatutaki kujibidiisha kumtafuta Yesu, hatutaki kujifunza Neno lake, hatutaki kusikia habari zake,tunaona kama zinatuchosha, na bado tunasema tumeokoka, tufahamu kuwa, zipo hatua ambazo kamwe hatutakaa tumfikie Yesu.

Tunakosa shabaha pale tunapodhani kumjua Yesu ni kuokoka tu, na kutoa pepo halafu basi. Hatujui kuwa YESU NDIO SIRI YA MUNGU mwenyewe.. ambao utimilifu wote wa Mungu unakaa kwa namna ya kimwili (Wakolosai 2:9). Kiasi kwamba tukifikia utimilifu wote wa kumjua yeye, basi hakuna kitu chochote hapa duniani tutakachoshindwa kufanya, au kukijua.  Na shetani hapa ndipo anapopapiga vita, kwasababu anajua siku mtu akimfahamu Yesu ipasavyo basi habari yake ndio imeishia hapo.

Waefeso 4:13 “hata na sisi sote tutakapoufikia umoja wa imani na kumfahamu sana Mwana wa Mungu, hata kuwa mtu mkamilifu, hata kufika kwenye cheo cha kimo cha utimilifu wa Kristo;

14 ili tusiwe tena watoto wachanga, tukitupwa huku na huku, na kuchukuliwa na kila upepo wa elimu, kwa hila ya watu, kwa ujanja, tukizifuata njia za udanganyifu”.

Kwahiyo na sisi tuonyeshe bidii ya kutafuta kumjua yeye, nasi tufikie hatua ya kutufanywa na mashahidi wake kweli kweli , kama alivyofanya kwa mitume wake na wale wengine mwanzoni.

Lakini tukiridhika na Yesu wa kuokokea tu, vivyo hivyo na yeye atajifunua kwetu kama huyo, lakini tukionyesha bidii ya kumtafuta, na kutaka kujua njia zake, na yeye atajifunua kwetu katika nguvu za kufufuka kwake, tutamjua kwa mapana na marefu yake, kama alivyofanya kwa wale watu wachache sana (500). Tutakuwa watu wengine kabisa.

Tuanze kulipigia hatua na hili.

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengine:

Mada Nyinginezo:

KUNA MAJIRA MUNGU ATAIVURUGA MIPANGO YETU.

Nini maana ya “mkilichukia hata vazi lililotiwa uchafu na mwili”?

JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?

Mafundisho

Mataifa ni nini katika Biblia?

Rudi nyumbani

Print this post

KWASABABU MUDA TULIOBAKIWA NAO SI MWINGI.

Mtume alituasa wakati huu wa mwisho ni wakati wa kutojishikamanisha sana na mambo ya mwilini, au ya ulimwenguni. Embu tutafakari kwa pamoja hivi vifungu hapa chini. Anasema.

1Wakorintho 7:29 “Lakini, ndugu, nasema hivi, muda ubakio si mwingi; basi tokea sasa wale walio na wake na wawe kama hawana;
30 na wale waliao kama hawalii; na wale wafurahio kama hawafurahi; na wale wanunuao, kama hawana kitu.
31 Na wale wautumiao ulimwengu huu, kama hawautumii sana; kwa maana mambo ya ulimwengu huu yanapita.
32 Lakini nataka msiwe na masumbufu. Yeye asiyeoa hujishughulisha na mambo ya Bwana, ampendezeje Bwana;
33 bali yeye aliyeoa hujishughulisha na mambo ya dunia hii, jinsi atakavyompendeza mkewe.
34 Tena iko tofauti hii kati ya mke na mwanamwali. Yeye asiyeolewa hujishughulisha na mambo ya Bwana, apate kuwa mtakatifu mwili na roho. Lakini yeye aliyeolewa hujishughulisha na mambo ya dunia hii, jinsi atakavyompendeza mumewe.
35 Nasema hayo niwafaidie, si kwamba niwategee tanzi, bali kwa ajili ya vile vipendezavyo, tena mpate kumhudumia Bwana pasipo kuvutwa na mambo mengine”.

Unaweza kupata picha alikuwa analenga nini hapo? Ni kwamba hatutakiwi tuvutwe kwenye mambo ya ulimwengu sana, mpaka tukasahau kuwa tunahitaji kumtumikia pia Mungu, angali tukiwa hapa dunia ndani ya hichi kipindi kifupi tulichobakiwa nacho.

Hii inatokea pengine mkristo mmoja ameingia katika ndoa, anasahau kabisa mambo ya Mungu, anaanza kujitaabisha na masuala ya mumewe au mkewe ampendezeje, maombi ameacha, kujifunza neno hafanyi tena.. Sasa katika mazingira kama haya Paulo alisema ukiingia kwenye ndoa, na uwe kama hujaoa, au uwe kama hujaolewa, usilikuze sana jambo hilo, mpaka likakufanya ukawa mlegevu kwa Mungu, kwasababu muda tuliobakiwa nao ni mchache.

Kwani  mambo ya kuoa au kuolewa ni ya hapa tu duniani, tukifika huko ng’ambo hayatakuwepo, hivyo si mambo ya kuyatilia mkazo sana, na kusahau mambo ya uzima wa milele  mbinguni.

Mwingine amezama katika masomo, kiasi kwamba hata muda wa kuongea na Mungu wake anakosa kabisa..

Mwingine utakuta ameingia katika biashara, na kwa bahati nzuri Mungu amemfanikisha sana, matokeo yake ni kuwa anasahau kabisa mambo ya rohoni anajikita muda wote katika biashara zake, hatengi tena muda wa kusali, au kwenda ibadani, au wa kumfanyia Mungu kitu.

Biblia inatuambia,

31 “Na wale wautumiao ulimwengu huu, kama hawautumii sana; kwa maana mambo ya ulimwengu huu yanapita”.

Ni kweli tupo katika huu ulimwengu, hatuna budi kuutumia kwa sehemu, lakini tumeaswa, tuwe kama vile hatuutumii, tuwe kama tumejiegesha tu, tusizame huko moja kwa moja, kiasi cha kutufanya tusahau kama sisi ni wapitaji, wenyeje wetu upo mbinguni.

Bali sisi tuishi kama wale mashujaa 300 wa Gideoni, ambao wenyewe, walipopelekwa mtoni kunywa maji, hawakunywa kama Ng’ombe kwa kupeleka midomo yao moja kwa moja kwenye maji, bali walikunywa kwa kuchota kwa mikono yao na kuyalamba kama mbwa midomoni,. Ikiwa na maana kuwa hata maadui zao wangeweza kuja wakati wanakunywa maji yao wasingeweza kuwaua kwa haraka kwasababu wangewaona tokea mbali , tofauti na wale wengine ambao midomo yao ilielekea kwenye maji moja kwa moja, hawaelewi kitu kingine.(Waamuzi 7:4-7)

Vivyo hivyo na sisi, tunaishi hapa duniani, lakini tunapaswa tuishi kwa kuchukulia kawaida kila kitu, ili tusimpe shetani nafasi ya kutuvuta katika mambo mengine, tusizame moja kwa moja kwenye ulimwengu, tunapaswa  tupate na nafasi kwa Mungu, kama ni shule, kama ni biashara, kama ni kazi, kama ni ndoa, kama ni sherehe, kama ni jambo lolote lile, sio la kuliumizia kichwa chako sana, au kulisumbukia, au kuliwazia kupitiliza, au kulifurahia sana.

Tukifanya Hivyo biblia inatuambia tutapata muda pia kwa Bwana. Na matokeo yake, hata siku ile ikifika haitatujilia kwa ghafla kama vile mwizi usiku. Maana biblia inasema ndivyo itakavyoujilia ulimwengu mzima. Na hiyo yote ni kwasababu watakuwa buzy katika mambo ya mwilini wakati huo.

Luka 31: 34 “Basi, jiangalieni, mioyo yenu isije ikalemewa na ulafi, na ulevi, na masumbufu ya maisha haya; siku ile ikawajia ghafula, kama mtego unasavyo;
35 kwa kuwa ndivyo itakavyowajilia watu wote wakaao juu ya uso wa dunia nzima”.

Kwahiyo kila siku  tulifahamu hili, kuwa sikumoja inapopita, ndivyo tunavyoikaribia ile siku Kuu ya Unyakuo. Hivyo ni wajibu wetu na sisi kuhakikisha ni kwa namna gani tunampendeza Mungu wetu katika hichi kipindi kifupi tulichobakiwa nacho.

Wafilipi 4: 6 “Msijisumbue kwa neno lo lote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu”.

Bwana akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengine

Mada Nyinginezo:

JIFUNZE KUELEWA MAANA YA KUOA/KUOLEWA KABLA YA KUINGIA HUKO.

UFUNUO: Mlango wa 14

Nini maana ya “yasiyokuwapo hayahesabiki”(Mh 1:15)

Kutabana ni nini? (Mika 5:12)

FAHAMU UWIANO MUNGU ANAOHITAJI KUUONA KWETU.

Rudi nyumbani

Print this post

KWANINI MIMI?

Kuna wakati unaweza kupitia mahali ukajikuta upo katika hali ambayo hujui sababu ni nini, haujui kosa lako ni lipi mpaka upokee mapigo mazito kama hayo.  Unabakia kujiuliza maswali kwanini mimi?

Ayubu alipitia mazingira kama hayo, katika maisha yake yote alijitahidi sana kuwa mkamilifu na mwelekevu mbele za Mungu, hakuruhusu dhambi imtawale katika maisha yake yote, alikuwa ni mwombaji, na mkaribishaji mzuri wa wageni, hivyo Mungu akambariki sana.

Lakini ukafika wakati, akashangaa ghafla mambo yamebadilika, mifugo yake yote imeibiwa, mali zake zote zimepotea, kama hilo halitoshi akasikia watoto wake wote 10 wamekufa kwa ajali mbaya sana ndani ya siku moja.. Wakati yupo katikati ya msiba, ghafla tena anaanza kuugua kwa magonjwa ya ajabu, kiasi kwamba inambidi akae kwenye majivu muda wote, alikondoa kiasi cha kuona mifupa tu.

Embu jiweke wewe katika hiyo nafasi, unadhani haitakuwa rahisi kumkufuru Mungu? Ni rahisi sana, na ndicho alichokifanya mke wa Ayubu. Lakini Ayubu hakumkufuru Mungu, yeye hakufikia hatua hiyo mbaya bali aliishia kusema KWANINI MIMI?

Kwanini mimi na si mtu mwingine,…Na hiyo kwanini mimi ilimpelekea mpaka kuanza kulaani, kila kitu kwenye maisha yake, akailaani mpaka siku ya kuzaliwa kwake, akaona kama vile yeye si mtu mwenye bahati, ni heri tu asingezaliwa duniani.

Ayubu 3:2 “Ayubu akajibu, na kusema;

3 Na ipotelee mbali ile siku niliyozaliwa mimi, Na ule usiku uliosema, Mtoto mume ametungishwa mimba.

4 Siku hiyo na iwe giza; Mungu asiiangalie toka juu, Wala mwanga usiiangazie.

5 Ishikwe na giza, giza tupu, kuwa yake; Wingu na likae juu yake; Chote kiifanyacho siku kuwa giza na kiitishe………

11 Mbona si kufa mimi tokea mimbani? Mbona nisitoe roho hapo nilipotoka tumboni?

12 Mbona hayo magoti kunipokea? Au hayo maziwa, hata nikanyonya?

13 Maana hapo ningelala na kutulia; Ningelala usingizi; na kupata kupumzika;”

Ayubu, kila kukicha alitamani afe.(Ayu 7:4)

Hiyo hali inawakumba watu wengi sasa hivi hususani pale wanapopitia matatizo fulani madogo au makubwa, aidha wanapofiwa na wazazi wao, au watoto wao, au wanapopoteza mali zao, au vitu vyao ya thamani, au wanapokumbana na magonjwa mazito yasiyotibika, kama vile kansa, kisukari, au ukimwi, wanajiuliza ni tatizo gani walilolifanya mpaka wayapate magonjwa hayo, mbona wanakula vizuri tu, mbona hawatendi dhambi, inakuwaje wakumbane na hizo shida kwenye miili yao.

Wengine, wanauliza kwanini mimi nizaliwe kipofu, nilimkosea nini Mungu, kwanini nizaliwe mfupi, kwanini niwe mlemavu, kwanini nina mapungufu haya n.k..

Sasa katika haya maswali , kwanini! kwanini! kwanini!.. Mungu naye alianza kumuuliza Ayubu maswali mengine ya ziada, ambayo alitaka na yeye ampe majibu yake. Ukisoma Ayubu 38 na kuendelea utaona maswali aliyoulizwa Ayubu ni yapi, ambayo tunajua yote alishindwa kuyatolea majibu yake..Kwamfano maswali haya aliulizwa;

Ayubu 38:28 “Je! Mvua ina baba? Au ni nani aliyeyazaa matone ya umande?

29 Barafu ilitoka katika tumbo la nani? Na sakitu ya mbinguni ni nani aliyeizaa?

30 Maji hugandamana kama jiwe, Na uso wa vilindi huganda kwa baridi.

31 Je! Waweza kuufunga mnyororo wa Kilimia, Au kuvilegeza vifungo vya Orioni?

32 Je! Waweza kuziongoza Sayari kwa wakati wake? Au waweza kuongoza Dubu na watoto wake?

33 Je! Unazijua amri zilizoamuriwa mbingu? Waweza kuyathibitisha mamlaka yake juu ya dunia?

34 Waweza kuiinua sauti yako mpaka mawinguni, ili wingi wa maji ukufunikize?

35 Waweza kuutuma umeme, nao ukaenda, Ukakuambia, Sisi tupo hapa?

36 Je! Ni nani aliyetia hekima moyoni? Au ni nani aliyetia ufahamu rohoni?”

Akagundua kuwa kumbe ni mambo mengi sana huku duniani, Mungu hajatupa majibu yake, , lakini tunaendelea tu kuishi nayo, wala hatuumizi vichwa vyetu kutaka kuyajua, na maisha yanaendelea kama kawaida. Sasa kwanini tutake kutolea majibu kila hali tunayopitia.

Ayubu baada ya kulijua hilo, alikaa kimya. Akamwambia Mungu hakika nilikosea kuzungumza kuzungumza maneno yasiyofaa. Na baada ya Mungu kugundua kuwa Ayubu kalijua hilo, akaugeuza uteka wake akampa mara dufu zaidi ya vile alivyovipoteza. Na sisi pia, tuliookoka, mambo yanapogeuka na kuwa ndivyo sivyo, sio wakati wa kuanza kulaumu, kwanini iwe mimi na sio Yule,..Kumbuka kila mtu anayo mapito yake, sio kila tatizo utalipatia jawabu lake sasa hivi,  pengine utakuja kujua mbeleni au usijue kabisa, kikubwa mshukuru Mungu, na usonge mbele.Wakati utafika jaribu hilo litaisha, usianza kuuliza maswali ambayo hujui majibu yake, utaishi kulaumu, Mtumaini Mungu.

Songa mbele kama mkristo uliyeokoka..Timiza wajibu wako wa kumwomba Mungu na kumshukuru, na kuishi maisha ya utakatifu, Upo wakati Mungu atakuondolea huo ugonjwa, au hilo tatizo, au hiyo shida.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengine:

Mada Nyinginezo:

HUDUMA YA (ELIFAZI, SOFARI, NA BILDADI).

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 9 (Kitabu cha Ayubu).

Maswali na Majibu

JINSI SHETANI ANAVYOZUIA MAJIBU YA MAOMBI YETU.

KWANINI KRISTO AFE?

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya “Andiko huua, bali Roho huhuisha (2Wakorintho 3:6)

Jibu: Tusome..

2Wakorintho 3:6  “Naye ndiye aliyetutosheleza kuwa wahudumu wa agano jipya; si wa andiko, bali wa roho; kwa maana andiko huua, bali roho huhuisha”.

Kuhuisha maana yake ni “kutoa uzima/uhai”, Mungu pekee ndiye anayetoa uzima na kutupa sisi. Hivyo hapo iliposema andiko huua, bali Roho huhuisha Maana yake ni kwamba, maandiko bila ufunuo wa Roho yanaweza kuipoteza roho ya mtu na kuiua kabisa (aidha mtu huyo akafa kiroho au hata kimwili kabisa). Lakini yakitumiwa kwa uongozo wa Roho, yanampa mtu uzima, na hata kama alikuwa amekufa anaweza kufufuka tena.

Sasa tutazame ni kwa namna gani andiko linaweza kumuua mtu kimwili, na baadaye kiroho.

  • Jinsi linavyoweza kumuua mtu kimwili:

Walawi 24:19 “Na mtu akimtia mwenziwe kilema; vile vile kama alivyofanya, naye atafanyiwa vivyo;

20 jeraha kwa jeraha, jicho kwa jicho, jino kwa jino; vile vile kama alivyomtia mtu kilema, naye atalipwa vivyo”.

Kumbukumbu 19:21 “Wala jicho lako lisiwe na huruma; uzima kwa uzima, jicho kwa jicho, jino kwa jino, mkono kwa mkono, mguu kwa mguu”.

Hapo anasema UZIMA kwa UZIMA, maana yake ni kwamba, mtu aliyetoa uhai wa mwenzake kwa makusudi sharti na yeye uhai wake uondolewe, au kama kamvunja jino, na la kwake pia litaondolewa, kama kampiga na kumtoboa jicho, na la kwake pia litatobolewa.

Kwahiyo hili andiko na mengine mengi yakichukuliwa kama yalivyo yanaua. Na watu wengi walikuwa wanakufa kwa maandiko hayo, ilikuwa mwanamke akifumaniwa katika uzinzi, hukumu yake ilikuwa ni kifo cha kupigwa mawe mpaka afe.

Lakini Roho Mtakatifu alipokuja, aliliweka hilo sawa kwa kinywa cha Bwana wetu Yesu Kristo na kusema..

Mathayo 5: 38  “Mmesikia kwamba imenenwa, Jicho kwa jicho, na jino kwa jino

39 Lakini mimi nawaambia, Msishindane na mtu mwovu; lakini mtu akupigaye shavu la kuume, mgeuzie na la pili.

40  Na mtu atakaye kukushitaki na kuitwaa kanzu yako, mwachie na joho pia.

41  Na mtu atakayekulazimisha mwendo wa maili moja, nenda naye mbili.

42  Akuombaye, mpe; naye atakaye kukopa kwako, usimpe kisogo

43  Mmesikia kwamba imenenwa, Umpende jirani yako, na, Umchukie adui yako;

44  lakini mimi nawaambia, Wapendeni adui zenu, waombeeni wanaowaudhi,

45  ili mpate kuwa wana wa Baba yenu aliye mbinguni; maana yeye huwaangazia jua lake waovu na wema, huwanyeshea mvua wenye haki na wasio haki”.

  • Ni kwa namna gani andiko pia linaweza kumuua mtu kiroho.

Mfano wa andiko linaloweza kumuua mtu kiroho ni hili…

1Timotheo 5:23 “Tokea sasa usinywe maji tu lakini tumia mvinyo kidogo, kwa ajili ya tumbo lako, na magonjwa yakupatayo mara kwa mara”.

Andiko hili limewapofusha watu macho na kuwafanya wawe walevi, na wasiojali  na shetani, amelipigilia msumari hili, lengo lake ni watu wafe bila kutubu ili waende jehanamu ya moto. Roho za wengi, zimekufa katika andiko hili.

Na andiko lingine ni hili.. Mhubiri 9:5 “kwa sababu walio hai wanajua ya kwamba watakufa; lakini wafu hawajui neno lo lote, wala hawana ijara tena; maana kumbukumbu lao limesahauliwa”.

Andiko hili limeua watu wengi sana kiroho, na kuishia kuamini kwamba hakuna maisha baada ya kifo, na kwamba hakuna jehanamu wala kinachoendelea..Hivyo wengi kwa andiko hili, wameona ni bora kuishi maisha ya kujipenda hapa duniani, na ya kutokujali, kwasababu baada ya kifo hakuna kitakachoendelea, hata akifanya uasherati, hakuna kwenda kuhukumiwa..Hivyo wengi wamekufa na dhambi zao kwa andiko hili. www wingulamashahidi org

Bwana Yesu, Mkuu wa Uzima alisema…

Luka 16:19  “Akasema, Palikuwa na mtu mmoja, tajiri, aliyevaa nguo za rangi ya zambarau na kitani safi, na kula sikuzote kwa anasa.

20  Na maskini mmoja, jina lake Lazaro, huwekwa mlangoni pake, ana vidonda vingi,

21  naye alikuwa akitamani kushibishwa kwa makombo yaliyoanguka katika meza ya yule tajiri; hata mbwa wakaja wakamramba vidonda vyake.

22  Ikawa yule maskini alikufa, akachukuliwa na malaika mpaka kifuani kwa Ibrahimu. Yule tajiri naye akafa, akazikwa.

23  Basi, kule kuzimu aliyainua macho yake, alipokuwa katika mateso, akamwona Ibrahimu kwa mbali, na Lazaro kifuani mwake.

24  Akalia, akasema, Ee baba Ibrahimu, nihurumie, umtume Lazaro achovye ncha ya kidole chake majini, auburudishe ulimi wangu; kwa sababu ninateswa katika moto huu.

25  Ibrahimu akasema, Mwanangu, kumbuka ya kwamba wewe uliyapokea mambo mema yako katika maisha yako, na Lazaro vivyo alipata mabaya; na sasa yeye yupo hapa anafarijiwa, na wewe unaumizwa.

26  Na zaidi ya hayo, kati yetu sisi na ninyi kumewekwa shimo kubwa, ili wale watakao kutoka huku kwenda kwenu wasiweze; wala watu wa kwenu wasivuke kuja kwetu.

27  Akasema, Basi, baba, nakuomba, umtume nyumbani kwa baba yangu,

28  kwa kuwa ninao ndugu watano, ili awashuhudie, wasije wao pia wakafika mahali hapa pa mateso.

29  Ibrahimu akasema, Wanao Musa na manabii; na wawasikilize wao.

30  Akasema, La, baba Ibrahimu, lakini kama akiwaendea mtu atokaye kwa wafu, watatubu.

31  Akamwambia, Wasipowasikia Musa na manabii, hawatashawishwa hata mtu akifufuka katika wafu”.

Hapo Roho anasema kuna hukumu baada ya kifo.

Hivyo ni muhimu sana kumpata Roho Mtakatifu, wakati wa kulisoma Neno la Mungu, kwasababu bila yeye ni vigumu kulielewa Neno la Mungu na kila utakapolisoma ni rahisi kutoa tafsiri zako, na si za Roho Mtakatifu.

Kama bado hujampokea Yesu, huwezi kamwe kuyaelewa maandiko, yatakuwa ni magumu, na kila utakapoyasoma utakuwa unapata maana ambazo sio sahihi, lakini pale tu utakapoamua kufanya uamuzi wa kumpokea Yesu moyoni mwako, na ukadhamiria kutubu na kuziacha dhambi zote unazozifanya kwa wazi na kwa siri, na ukawa tayari kwenda kubatizwa katika ubatizo sahihi wa maji tele (Yohana 3:23) na kwa Jina la Yesu Kristo, siku hiyo hiyo Roho Mtakatifu ataanza kufanya kazi ndani yako na kuumba jambo jipya.

Bwana akubariki

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312 . jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?

Kuwatema farasi, maana yake ni nini?

Wapendwa nini maana ya hili andiko “Ushuhuda wa YESU ndio ROHO YA UNABII” (ufunuo 19:10)?

IFAHAMU HUZUNI NA FURAHA YA MALAIKA.

INJILI YA MANENO LAINI ITAKUGHARIMU.

Rudi nyumbani

Print this post