Category Archive Home

JE NI DHAMBI KUWA NA MAHUSIANO KABLA YA NDOA?

Mahusiano ya uchumba, ni tofuati na mahusiano ya kimapenzi. Yapo mahusiano ya uchumba ambayo mtu anakuwa nayo kwa mtu aliyemchumbia, hilo halina tatizo maadamu halihusanishwi na vitendo vyovyote vya zinaa. Watu hao wawili wanaweza wakakutana wakala pamoja, wakazungumza pamoja, wakafurahi pamoja, wakatembeleana nyumbani kwao, wakaweka mpingano pamoja..lakini si kulala, pamoja, au kukaribiana kimapenzi au kuonyesha dalili zozote za kukaribiana kihisia, ..

Lakini wapo watu wanaosema, huyu tayari kashakuwa mke wangu, hivyo hakuna shida, sasa nikifanya naye tendo la ndoa si tayari kashakuwa wangu nitamuoa tu?..

Lakini kabla hujafikiria kuwaza hivyo, embu jaribu kuwaza kwanza ni kwa nini lile tendo linaitwa Tendo la Ndoa?..Ulishawahi kujiuliza hivyo?.Linaitwa hivyo kwasababu ni tendo linalofanywa na wanandoa tu peke yao..Nje ya hapo haijalishi unampenda sana huyo mwenzako au unamalengo naye makubwa kiasi gani au kwamba atakuja kuwa mke wako baadaye au mume wako, haijalishi huo  tayari ni uasherati..Na waasherati wote Mungu atawahukumu.

Kama ingekuwa ni rahisi hivyo tu, hata mtu anayekutana na kahaba barabarani na kwenda kufanya naye uasherati basi na yeye angejitetea na kusema siku moja nitakuja kumuoa wacha nifanye nae kwanza..Unaona? Hilo jambo halimfanyi yeye kutokuwa muasherati…Tendo la ndoa linalofanywa kwa watu ambao sio wanandoa ni dhambi.

Waebrania 13.:4 Ndoa na iheshimiwe na watu wote, na malazi yawe safi; kwa maana waasherati na wazinzi Mungu atawahukumia adhabu.

Hivyo ikiwa wewe umempenda binti, na umeshamchumbia, ili ndoa yako ikubaliwe na Mungu..Subiri mpaka wakati Mungu atakapokuunganisha naye rasmi mbele ya Kanisa la Kristo. Na ni kwanini iwe ni katika kanisa la Kristo na si penginepo. Ni kwasababu Mungu unayetaka awaunganishe ndipo alipo. Wapo wengine wanafungishwa ndoa za kimila, au za kiserikali n.k…Unaweza kuziita ni ndoa lakini hizo zote Sio ndoa za kikristo..Ambazo zinaweza kupokea Baraka za Kristo mwenyewe.

Kwasababu kabla ndoa haijaitwa ndoa ni lazima kuwe na makubaliano na mapatano na maagano fulani, sasa kama ukifungishwa nje ya Kristo, hapo ndipo utakutana na nyingine zinaruhusu kuolewa au kuoa mke zaidi ya mmoja, nyingine zinaruhusu kuachana wakati wowote mnapochokana, nyingine ni lazima mtambike, n.k. mambo ambayo yanakinzana kabisa na mpango wa Kristo.

Hivyo ndugu/Dada,..Ndoa yako ikipitia hatua sahihi Kristo anazozihitaji. Basi ujue zipo Baraka tele za kindoa ambazo Mungu ataziachilia kwako na kwa uzao wako baadaye ikiwemo ndoa yenu kupokea ulinzi wa kiMungu tangu huo wakati. Lakini ukiwa na haraka na kuvuruga mipango, na kukimbilia kufanya jambo ambalo wakati wake haujafika, ujue kwa hakika kabisa Mungu hayupo na wewe, na hata ndoa yako hataibarikiwa…Na jaribu kuangalia utaona wengi wa wanaofanya hivyo, mwisho wa siku hawaoani, au wanazaa, na baadaye wanaachana, na watoto wanabakia kuwa na mazazi mmoja,.Hiyo yote ni matokeo ya kuwa na mahusiano ya kimapenzi nje ya ndoa.

Hivyo ikiwa leo hii upo katika mahusiano ya kimapenzi(ngono) na mwenza wako, mpaka mmeshafikia hatua ya kuzaa, acha mara moja, mkatubu dhambi zenu wote wawili, kwa kumaanisha kabisa kisha muanze utaratibu wa kwenda kufungishwa ndoa yetu kanisani..Na hapo ndipo Bwana atakapowatazama na kuwaangazia rehema zake…Lakini vinginevyo ukiendelea kufanya hivyo ujue kuwa wewe ni mwasherati mbele za Mungu.

1Wakorintho 6:9  “Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? Msidanganyike; waasherati hawataurithi ufalme wa Mungu, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wafiraji, wala walawiti,

10  wala wevi, wala watamanio, wala walevi, wala watukanaji, wala wanyang’anyi”.

Fanya hivyo Na Bwana atakubariki.

Mada Nyinginezo:

Nini Tofauti kati ya uzinzi na uasherati ?

MOTO HUFA KWA KUKOSA KUNI.HATA UASHERATI NAO

NJIA SAHIHI YA KUMPATA MWENZA WA MAISHA KIBIBLIA.

CHAPA YA MNYAMA

 

JINSI SODOMA NA GOMORA ILIVYOKUWA INAVUTIA SANA..

JINSI NEEMA YA MUNGU ILIVYOKUWA KUBWA KWA MKE WA LUTU.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

Rudi Nyumbani:

Print this post

KIFO CHA MTAKATIFU PERPETUA NA FELISTA.

Kifo cha mtakatifu perpetua na felista kimebeba ujumbe gani kwetu?

Perpetua alizaliwa huko Tunis (Mji mkuu wa Tunisia) Afrika ya Kaskazini mwaka unaokadiriwa kuwa wa 182, alizaliwa katika familia ya kitajiri, yenye kuheshimika sana, baba yake alikuwa ni mpagani, lakini Perpetua aliupokea Ukristo na kuwa mfuasi kamili wa Kristo, japo historia haionyeshi ni kipindi gani aligeuzwa kuwa mkristo..Lakini ilifika wakati mfalme wa Kirumi aliyeitwa Septimius Severus…Alipiga marufuku ukristo katika majimbo ya Afrika kaskazini, kwamba mtu yoyote asijihusishe na imani yoyote ya kikristo au ya kiyahudi..Wakati huo Perpetua alikuwa anaishi na mume wake, pamoja na kijakazi wake aliyeitwa Felista, na katoto chake kachanga alichokuwa bado anakinyonyesha wakati huo ..

Sasa wakati agizo hilo linatolewa Perpetua alikuwa katika mafundisho ya kuelekea kubatizwa, lakini alibatizwa kabla ya kupelekwa gerezani..Ndipo baadaye yeye pamoja na wenzake wanne, wote walikamatwa na kupelekwa gerezani.

Baba yake kusikia vile, alikwenda moja kwa moja mpaka gerezani kumtazama binti yake ili kutafuta njia ya kumtoa, ndipo akamshauri Perpetua aukane ukristo, atoke gerezani aendelee na maisha yake ya kawaida..

Lakini Perpetua alimwambia Baba yake maneno haya.. “Baba unakiona hichi chungu hapa?”

Akasema ndio,

Je kinaweza kuitwa jina lingine tofauti na vile kilivyo?

Akasema, hapana!

Basi hata mimi siwezi kuitwa jina lingine tofuati na mimi nilivyo..Mkristo.

Ilipofika Siku ya pili Perpetua, alihamishwa gereza alilokuwepo na kupelekwa gereza lingine zuri zaidi ili aweze kumnyonyesha mtoto wake…Lakini baba yake hakukata tamaa alimfuata tena siku nyingine, lakini safari hii alikuja kwa kumbembeleza sana.

Akimwambia…Nihurumie mwanangu!, nihurumie mwanangu!, ikiwa ninastahili kweli kuitwa baba yako, ikiwa nimekupenda zaidi hata ya kaka zako, ikiwa nimekulea mpaka umefikia hatua hii ya heshima..basi nihurumie mimi baba yako..kubali kukataa tu wewe sio mkristo.

Akamdondokea, mpaka magotini akambusu mikono yake..akamwambia, mwanangu usiniache nikapata aibu kama hii katikati ya watu. Fikiri juu ya kaka zako, fikiri juu ya mama yako, fikiri juu ya shangazi zako, fikiri hata juu ya huyu mtoto wako mchanga ambaye hataweza kuishi pindi utakapokufa..Ghairi hayo maamuzi yako magumu!, uendelee na maisha yako ya kawaida.

Perpetua alizidi kuwa imara na msimamo yake akamtia moyo baba yake..Akaendelea kukaa kule kule gerezani.

Na Siku ya kuhojiwa ilipofika Perpetua na wenzake walipandishwa kizimbani mbele ya gavana, Na wenzake walipoulizwa kwanza juu ya msimamo wao walikiri kuwa wao ni wakristo, na wote wakakataa ibada za mfalme. Swali likageuzwa kwa Perpetua, naye akaulizwa na Gavana kuhusu msimamo wake.

Wakati huo baba yake alikuwa hapo karibu, amembeba mtoto wake yule, akamwambia, kubali ibada za mfalme, achana na hiyo imani yako, mwonee huruma mtoto wako.

Lakini Perpetua akasema mbele ya wote..Siwezi kufanya hivyo!!

Gavana akamuuliza, kwahiyo wewe ni mkristo.

Ndio! Perpetua alijibu..

Baba yake akaingilia kati akimlazimisha Pepertua aikane imani, lakini Hawakuwa na muda tena, wakamchukua yeye na wenzake wakawapeleka katika viwanja vya michezo (Arena) ili wauawe. Kufika kule kuliwa na wanyama wakali ambao tayari wameshaandaliwa, ambapo wanyama kama chui, dubu walikuwa wanaachiliwa kwa wanaume, na nyati kwa wanawake..wakamtupa Perpetua na yeye pamoja na wenzake, na kijakazi wake Felista ambaye kwa wakati huo alikuwa ni mjamzito naye..

Akaachiliwa nyati, akamchota Perpetua juu, wakati akiwa chini akaende kumsaidia kijakazi wake Felista, huku wote wamelowa damu..Wakaona haitaoshi wakawaleta kwa wauaji wa kirumi katika ma-arena hayo ili wauliwe kwa upanga..

Perpetua alikufa mwaka wa 203 akiwa bado mama mdogo mwenye umri wa miaka 22, hakuona ujana wake kuwa ni kitu kuliko Kristo, hakuona heshima yake ya kitajiri kuwa ni kitu kuliko Kristo, wala hakuhesabu kuikana imani kisa baba, au mama au mtoto wake.. Bali aliisimamia imani hadi dakika ya mwisho..

Biblia inatuambia..

Waebrania 11:35 “…..Lakini wengine waliumizwa vibaya hata kuuawa, wasikubali ukombozi, ili wapate ufufuo ulio bora;

36 wengine walijaribiwa kwa dhihaka na mapigo, naam, kwa mafungo, na kwa kutiwa gerezani;

37 walipigwa kwa mawe, walikatwa kwa misumeno, walijaribiwa, waliuawa kwa upanga;

Swali la kujiuliza kwetu sisi hususani kwako wewe mwanamke kutokana na mada hii:

Je unauthamini wokovu wako vipi?..Unasema umeokoka lakini kuacha kuvaa vimini na masuruali na manguo ya utupu, unaona ni vigumu, unajiona wewe ni kijana, Perpetua pengine alikuwa ni kijana Zaidi yako, tena aliyezaliwa katika nyumba ya kitukufu ya kitajiri pengine kuliko wewe, lakini hakuudosha utakatifu wake.

Kila tusomapo habari kama hizi tusiishie tu kuzisoma kama hadithi bali tufahamu kuwa..tunahimizwa na sisi pia tupige mbio kama hao, na kutupa kila mzigo wa dhambi unaotulemea na kutuzungika kwa upesi, kwasababu hawa ndio watakaotuhuku siku ile mbele za Bwana..kuwa walikuwa wazuri kushinda sisi lakini hawakuikana imani, walikuwa katika hatari kubwa kuliko sisi lakini hawakuupuuzia wokovu, walikuwa ni matajiri kuliko sisi lakini hawakusema utajiri wangu ni kizuizi nisikane nafsi..Walikuwa ni wajawazito, na wenye watoto wachanga, lakini hawakuthamini hicho zaidi ya wokovu wao..wewe na mimi tutajibu nini mbele za Bwana siku ile? Au tunafikiri watu hao walikuwa hawasikii maumivu, au walikuwa wana roho sana..hapana, ni walikana tu!..Biblia inasema hata Eliya hakuwa mtu wa ajabu sana, alikuwa ni mtu mwenye tabia sawa na sisi, lakini walijikana kwa gharama zote.

Waebrania 12:1 “Basi na sisi pia, kwa kuwa tunazungukwa na wingu kubwa la mashahidi namna hii, na tuweke kando kila mzigo mzito, na dhambi ile ituzingayo kwa upesi; na tupige mbio kwa saburi katika yale mashindano yaliyowekwa mbele yetu”

Ubarikiwe.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

Vichwa saba vya mnyama wa kwenye Ufunuo 13 na 17, Ni nini?

BONDE LA KUKATA MANENO.

Yeremia 33:3 (NIITE NAMI NITAKUITIKIA)

TUWATAFAKARI NZIGE WA JANGWANI.

INJILI KULINGANA NA TEKNOLOJIA

JINSI NEEMA YA MUNGU ILIVYOKUWA KUBWA KWA MKE WA LUTU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

KUPATA MAONO YA MBINGUNI SIO KUFIKA MBINGUNI.

Kupata maono ya mbinguni sio kufika mbinguni…ndio mwanzo wa safari.

Bwana anatupenda, na wakati mwingine anawachukua baadhi ya watu (sio wote) ili kuwaonyesha mambo yaliyopo kule nyumbani, juu kwa baba yetu.

Anawapeleka kuwaonyesha mambo mazuri aliyowaandalia wanawe, anawaonyesha makazi yao ya kuduma yasiyoharibika na hazina zinazowangoja kule nga’mbo ikiwa watashinda..Anawaonyesha utajiri aliowaandalia na heshima na utukufu..anawaonyesha ni kwa jinsi gani mbingu inavyowatamani na ilivyojiandaa vya kutosha kuwalaki…na mambo mengine mengi ambayo hata hayaelezeki.

Ni mfano tu wa Wana wa Israeli baada ya kutolewa nchi ya Misri na kufikishwa kule jangwani..ambapo maili chache kabla kufika nchi ya Ahadi…Mungu aliwatuma wakaipeleleze nchi ya ile waliyoahidiwa, na aliruhusu waende watu wachache sana(yaani watu 12 tu) ndio walioteuliwa kwenda kuipeleleza…Na walifika kweli Kaanani na kuipeleleza walirudi kila mtu na jibu lake…lakini wote walikubaliana na jambo moja  kuwa nchi ile ilikuwa ni njema sana na imejaa unono na maziwa na asali, na baraka tele na kweli ni nchi yenye urithi mzuri usioelezeka.

Hesabu 13:1 “Kisha Bwana akanena na Musa, akamwambia,

 2 Tuma watu, ili waende wakaipeleleze nchi ya Kanaani, niwapayo wana wa Israeli; katika kabila ya baba zao mtamtuma mtu mmoja, kila mtu na awe mkuu kati yao.

3 Basi Musa akawatuma kutoka nyika ya Parani kama alivyoagizwa na Bwana; wote walikuwa ni watu walio vichwa vya wana wa Israeli……..

17 Musa akawapeleka ili waipeleleze nchi ya Kanaani, akawaambia, Pandeni sasa katika Negebu mkapande milimani,

18 mkaitazame nchi ni ya namna gani; na watu wanaokaa ndani yake, kwamba ni hodari au dhaifu, kwamba ni wachache au wengi;

 19 na nchi wanayoikaa kwamba ni njema au mbaya; kwamba wanakaa katika matuo au katika ngome;

 20 nayo nchi ni ya namna gani, kwamba ni nchi ya unono au ya njaa, kwamba ina msitu au sivyo. Iweni na moyo mkuu, mkayalete matunda ya nchi. Basi wakati ule ulikuwa wakati wa kuiva zabibu za kwanza.

21 Basi wakapanda wakaipeleleza nchi toka jangwa la Sini hata Rehobu, mpaka kuingia Hamathi.

22 Wakapanda katika Negebu, wakafika Hebroni; na Ahimani, na Sheshai, na Talmai, wana wa Anaki, walikuwako huko. Nao Hebroni ulijengwa miaka saba kabla ya Soani wa Misri.

 23 Wakafika bonde la Eshkoli, na huko wakakata tawi lenye kishada kimoja cha zabibu, wakalichukua kwa mti kati ya watu wawili; wakaleta makomamanga pia, na tini.

24 Bonde lile liliitwa bonde la Eshkoli kwa sababu ya hicho kishada walichokata huko wana wa Israeli.

25 Wakarejea baada ya kuipeleleza nchi, mwisho wa siku arobaini.

 26 Wakaenda wakafika kwa Musa, na kwa Haruni, na kwa mkutano wote wa wana wa Israeli, katika jangwa la Parani, huko Kadeshi; wakawaletea habari, wao na mkutano wote, wakawaonyesha matunda ya nchi.

27 Wakamwambia wakasema, TULIFIKA NCHI ILE ULIYOTUTUMA, NA HAKIKA YAKE, NI NCHI YENYE WINGI WA MAZIWA NA ASALI, NA HAYA NDIYO MATUNDA YAKE”.

Watu hawa ni kweli walifika katika ile nchi…lakini sio kwamba kwasababu wamefika basi ndio hawana haja ya kurudi tena kwa wenzao…Muda wa wao kufika kule ulikuwa bado…walikwenda tu kuonyeshwa nafasi zao kule…Lakini bado walikuwa hawajaiteka ile nchi, walipaswa warudi kwanza wakapange vita wapambane wayaondoshe yale majitu yaliyoshikilia urithi wao katika nchi ya Ahadi ambayo wameahidiwa, wakishawaangusha ndipo waimiliki…

Ndio maana Bwana Yesu alisema katika..

 Mathayo 11:12 “ Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatikana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka”

Shetani sasa kashikilia nafasi zetu katika ulimwengu wa roho, tunapaswa tumwangushe chini kabla ya kufika nga’mbo, na vita tunapambana hapa hapa duniani…tutakapomwangusha chini ndipo tutazirithi baraka zetu….(na tunamwangusha chini kwa kuishi Maisha matakatifu na makamilifu ya Neno la Mungu, yanayompendeza yeye),….hatuna budi kupambana vita hapa…kusikia tu mbinguni ni kuzuri tumeandaliwa hiki na kile haimaanishi kwamba ndio tayari tumekwishafika…bado kuna vita vya kupambana kumwangusha shetani katika Maisha yetu..

Shetani hataki tuende mbinguni kabisa, hataki hata kidogo kwasababu anajua uzuri tutakaoukuta kule, … anapambana sana kuhakikisha hatufiki kule, kama alivyopambana na wana wa Israeli kuhakikisha hawafiki nchi ya Ahadi, au hata wakifika basi watafika wachache sana na kwa shida sana..Hebu tafakari katika ule umati wote waliotoka Misri Zaidi ya watu milioni 2 waliofanikiwa kuingia nchi ya Ahadi walikuwa ni watu wawili tu (2)! Na iliwachukua miaka 40 kuingia tu ile nchi ambayo ni maili chache tu, safari ya mwezi mmoja tu. Alikuwa ananyanyua kila aina ya vikwazo walipokuwa njiani..aliwatumia mpaka manabii wa uongo kuwaangusha wana wa Israeli walipokuwa njiani.

Na sisi ni hivyo hivyo…mbinguni hatuendi kwa miguu kama wana wa Israeli walivyokwenda Kaanani, kama tutaishi Maisha ya kutoujali wokovu kama baadhi ya wana wa Israeli walivyokuwa, tutaangamizwa na hatutaurithi ufalme wa mbinguni, kama tukikubali maneno ya manabii wa uongo kama baadhi ya wana wa Israeli walivyokubali kuyasikiliza maneno ya akina Kora na Balaamu basi na sisi hatutairithi nchi.

Kama hatutamheshimu Mungu kama baadhi ya wana wa Israeli walivyokosa kumheshimu Mungu wakiwa safarini basi haijaishi tumeikaribia mbinguni  kiasi gani hatutairithi.. Kama tutakata tamaa na kutoamini kwamba tunaweza kufika mbinguni basi hatutafika kweli kama wale watu ambao baada ya kwenda kanaani kuipeleleza walileta ripoti za kuwaogopesha watu, na wote walikufa..

1Wakorintho 10:5  Lakini wengi sana katika wao, Mungu hakupendezwa nao; maana waliangamizwa jangwani.

6 BASI MAMBO HAYO YALIKUWA MIFANO KWETU, KUSUDI SISI TUSIWE WATU WA KUTAMANI MABAYA, KAMA WALE NAO WALIVYOTAMANI.

7  Wala msiwe waabudu sanamu, kama wengine wao walivyokuwa; kama ilivyoandikwa, Watu waliketi kula na kunywa, kisha wakasimama wacheze.

8  Wala msifanye uasherati, kama wengine wao walivyofanya, wakaanguka siku moja watu ishirini na tatu elfu.

9  Wala tusimjaribu Bwana, kama wengine wao walivyomjaribu, wakaharibiwa na nyoka.

10  Wala msinung’unike, kama wengine wao walivyonung’unika, wakaharibiwa na mharabu.

11  Basi mambo hayo yaliwapata wao kwa jinsi ya mifano, yakaandikwa ili kutuonya sisi, tuliofikiliwa na miisho ya zamani.

12  Kwa hiyo anayejidhania kuwa amesimama na aangalie asianguke”.

Biblia inasema..

Ufunuo 21:7  “Yeye ashindaye atayarithi haya, nami nitakuwa Mungu wake, naye atakuwa mwanangu.

8  Bali waoga, na wasioamini, na wachukizao, na wauaji, na wazinzi, na wachawi, na hao waabuduo sanamu, na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili”

Ufunuo 21:27  “Na ndani yake hakitaingia kamwe cho chote kilicho kinyonge, wala yeye afanyaye machukizo na uongo, bali wale walioandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo”

Mpe leo Yesu Maisha yako kama hujampa. Na pia jikane nafsi yako, jitwike na msalaba wako mfuate Yesu kama ulikuwa hujafanya hivyo..Safari yetu karibia inafika ukingoni, na shetani ndivyo anavyozidi kuongeza jitihada kuwapunguzia watu kasi ya kuingia uzimani..

Kumbuka mtume Paulo alichokisema, aliponyakuliwa kule juu na kuonyeshwa mambo ambayo hayatamkiki, Hiyo ni kuonyesha ni kwa jinsi yalivyo ya ajabu na ya kushangaza kiasi kwamba hata lugha haziwezi kuelezea, (2Wakorintho 12:4)..sasa unasubiri nini..Kimbilia kwa YESU ayaokoe maisha yako.

Ubarikiwe.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

RABI, UNAKAA WAPI?

JINA LA MUNGU NI LIPI?

NINI MAANA YA SISI KUWA WATOTO WA MUNGU?

TUNA WAJIBU WA KUOMBEA MAHALI TULIPO.

ZIFAHAMU NAMBA KATIKA BIBLIA NA MAANA ZAKE.

HISTORIA YA ISRAELI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

LIVUNJENI HEKALU HILI, NAMI KATIKA SIKU TATU NITALISIMAMISHA.

Livunjeni hekalu hili nami katika siku tatu nitalisimamisha..

Mara nyingine Bwana Yesu alipotaka kufikisha ujumbe Fulani, alikuwa anatumia mfano wa mahali husika ili kuchanganya mada mbili kwa wakati mmoja …Kwamfano utaona wakati ule mitume wa Bwana Yesu waliposahau kuchukua ile mkate ambayo ilibaki wakaanza kugombana wao kwa wao kwa kulaumiana kwanini hawakuibeba, …lakini Bwana Yesu alipowasikia, mabishanao yao alitumia mfano mwingine kuzungumza nao kana kwamba alikuwa hamaanisha hicho walichokuwa wanakibishania kwa wakati huo..

Marko 8:13 “Akawaacha, akapanda tena chomboni, akaenda zake hata ng’ambo.

14 Wakasahau kuchukua mikate, wala chomboni hawana ila mkate mmoja tu.

15 Akawaagiza, akasema, Angalieni, jihadharini na chachu ya Mafarisayo na chachu ya Herode.

16 Wakabishana wao kwa wao, kwa kuwa hawana mikate.

17 Naye Yesu akatambua, akawaambia, Mbona mnabishana kwa sababu hamna mikate? Hamfahamu bado, wala hamjaelewa? Je! Mioyo yenu ni mizito?

18 Mna macho, hamwoni; mna masikio, hamsikii? Wala hamkumbuki?

19 Nilipoivunja ile mikate mitano na kuwapa wale elfu tano, mlichukua vikapu vingapi vimejaa vipande? Wakamwambia, Kumi na viwili.

20 Na ile saba kuwapa wale elfu nne, mlichukua makanda mangapi yamejaa vipande? Wakamwambia, Saba.

21 Akawaambia, Hamjafahamu bado?”

Unaona hapo? Bwana Yesu alitumia mfano wa chachu, na kusema, jilindeni na chachu ya mafarisayo…Lakini mitume wakadhani anazungumzia chachu ya mikate ya mafarisayo, hiyo ikiwafanya wazidi kugombana zaidi ili apate kuwanasa vizuri,..Hapo ndipo Bwana akapata nafasi ya kuwakemea kwa kukosa kwao ufahamu, akawaambia hamjafahamu bado?, mimi sizungumzii habari za mikate, mmesahau ni mikate mingapi mlikusanya kama masalia wakati ule?, hamjafahamu bado, hamjaelewa, mioyo yenu ni mizito, hamna imani kwa Mungu bado kuwa hata sasa anaweza kuwafanyia muujiza kama ule ule wa mikate mengine mkala mkashiba, pasipo kuwa na chochote?…lakini bado mnamtilia shaka Mungu?…Mimi sizungumzii habari za mikate ninaachomaanisha ni jilindeni na mafundisho ya mafarisayo..

Sasa utaona hapo mitume walipata mafundisho mawili, la kwanza ni kutokana na kile walichokuwa wanakifiria juu ya tumbo, kuwa Mungu bado anaweza kuwahudumia hata kama kunaonekana hakuna mlango wa kupata chakula, na cha pili ni kuhusu mafundisho ya mafarisayo (ambayo yanafananishwa na chachu/hamira) ambayo kazi yake ni kuumua na kupindua uhalisia wa Neno la Mungu…Lakini waliupata ule ujumbe uliokuwa unawahusu kwa wakati wao.

Ndivyo hivyo hata wakati ule Bwana Yesu alipokwenda hekaluni, akaona jinsi watu walivyoweka tumaini lao lote katika lile hekalu, jinsi lilivyokuwa limepambwa kwa namna ya ajabu, jinsi lilivyokuwa kubwa, na kukarabatiwa kwa muda mrefu wa miaka 46 na Herode..jinsi watu wengi walivyokuwa wanatoa sadaka zao kwa ajili ya hekalu lile.. Lakini jicho la Bwana Yesu lilikuwa linaona mbali zaidi yao, lilikuwa linaona muda si mrefu hekalu lile halitakuwepo, litakuwa limebomolewa, mahali pale patakuwa pamechomwa moto, watu watauawa na kuchinjwa kama kuku..lakini wale watu hawakuliona hilo, walikuwa wanajisifia tu majengo yake, hawaoni wakati umekaribia mji huo waliokuwepo ambao wanaupenda utateketezwa kwa moto…

Ndipo sasa wakati Bwana akiwa pale hekaluni anavuruga vuruga bishara zao.. wayahudi wakamfuata na kumuuliza, Ni ishara gani utuonyeshayo, kwamba unafanya haya?

Yesu akawajibu…

Yohana 2:19 “…..Livunjeni hekalu hili, nami katika siku tatu nitalisimamisha.

20 Basi Wayahudi wakasema, Hekalu hili lilijengwa katika muda wa miaka arobaini na sita, nawe utalisimamisha katika siku tatu?

21 Lakini yeye alinena habari za hekalu la mwili wake.

22 Basi alipofufuka katika wafu, wanafunzi wake wakakumbuka ya kuwa alisema hivi, wakaliamini lile andiko na lile neno alilolinena Yesu”.

Unaona, Bwana Yesu alimaanisha kweli juu ya hekalu la mwili wake kuwa atakufa na siku ya tatu atafufuka, lakini pia alitaka wafikirie vile vile juu ya habari za kubomolewa kwa hekalu, ili awafundishe jambo..lakini wengi wao hawakuwa tayari kutaka kujua zaidi, wakamwona kama karukwa na akili..anazungumza ujinga.

Lakini baadaye wanafunzi wake wanyenyekevu waliliweka hilo akilini…wakaanza tena kumwonyesha majengo ya hekalu lile ambalo yeye alisema watu walibomoe,..jinsi lilivyojengwa vizuri kwa mawe ya thamani…

Mathayo 24:1 “Yesu akaenda zake, akatoka hekaluni; wanafunzi wake wakamwendea ili kumwonyesha majengo ya hekalu

2.Hamyaoni haya yote? Amin, nawaambieni, Halitasalia hapa jiwe juu ya jiwe ambalo halitabomoshwa”.

Lakini wanafunzi walivyosikia vile, hawakuishia pale, walizidi kuendelea kutaka kujua hatma ya hayo mambo itakuwaje, wakamfuata sasa faraghani, wakiwa peke yao tu Bwana, ndipo wakamuuliza..mambo hayo yatakuwa lini? Nayo ni nini dalili ya kuja kwako? Na ya Mwisho wa dunia? Maswali matatu.

Hapo sasa ndipo Bwana Yesu akaanza kuwafunulia hatua kwa hatua, mambo yatakayotendeka kuanzia ule wakati, mpaka siku mji ule utakapozingirwa na majeshi, na hekalu kubomolewa, mpaka siku za mwisho..ambayo maneno haya hata sisi wa kizazi hiki tunayatumia kama dira ya kutambua majira ya kuja kwa Bwana Yesu..Soma Mathayo 24, Marko 13, na Luka 21. Utaona habari zote za siku za mwisho zitakavyokuwa.

Lakini mafunuo hayo yote yalitoka katika Neno moja tu la Kubomolewa kwa hekalu..Kama mtume wasingetaka kujua zaidi, basi habari za kuteketezwa kwa Yerusalemu na warumi mwaka 70W.K, ambapo watu waliuawa kikatili, wasingekaa wajue pia habari za manabii wa uongo, na kusimama kwa chukizo la uharibifu wasingekaa wajue..

Vivyo hivyo hata sasa, tukiwa tayari kutaka kujua zaidi juu ya maneno ya Bwana wetu Yesu Kristo katika Neno lake, kwa kumaanisha kujifunza Neno lake na sio kusoma tu kama gazeti, ndipo tunapojijengea nafasi nzuri ya kupokea mafunuo zaidi yamuhusuyo yeye.

Lakini kama tutasoma biblia juu juu tu, na kusema aa hii haiwezekani, au tunasema kile Bwana alimaanisha vile sio hivi..Tutabakia, kuujua upande mmoja tu wa maandiko..Na kufanana na wale watu waliomsulubisha pale msalabani na kumdhihaki…walisikia tu upande mmoja (livunjeni hekalu hili)

Zaburi 25:14 “Siri ya Bwana iko kwao wamchao, Naye atawajulisha agano lake”.

Hivyo Bwana atusaidie tuzidi kumjua Zaidi yeye, mpaka tutakapofikia ukamilifu.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

Rudi Nyumbani:

Print this post

Je! ni dhambi kuchukua riba?

Biblia inasema tusikopeshe kwa riba, je! Wanaowakopesha watu kwa riba wanafanya dhambi?


JIBU: Biblia imezuia kutozana riba ndugu kwa ndugu tu..lakini kwa wengine nje ya ndugu sio dhambi kuwatoza riba.

Kumbukumbu 23:19 “Usimkopeshe ndugu yako kwa riba; riba ya fedha, riba ya vyakula, riba ya kitu cho chote kikopeshwacho kwa riba;

20 mgeni waweza kumkopesha kwa riba, ila usimkopeshe ndugu yako kwa riba; ili Bwana, Mungu wako, apate kukubarikia katika yote utiayo mkono wako, katika nchi uingiayo kuimiliki”.

Kwa mfano ndugu yako unamwona anayoshida, anaomba umkopeshe fedha kidogo, halafu wewe unatumia ile fursa kumwambia aongeze na kiwango kingine cha fedha juu yake(riba), kama faida yako, Hiyo ni dhambi, akikopa, basi arudishe kile kile alichokopa..Usigeuze shida za ndugu yako kuwa mtaji..

Katika hali ya kawaida hata bila kuambiwa na mtu au kufundishwa, ukiwa na nyumba ya biashara, halafu ndugu yako wa karibu amekuja kukaa hapo kwa kipindi fulani tu.. Huwezi kumwambia alipie kodi kamili kama watu wengine, anaweza kulipia tu zile gharama za kawaida ndogo ndogo lakini sio kulipia kila kitu..hakuna mtu mwenye utu anaweza kumfanyia hivyo ndugu yake.

Hali kadhalika katika Ukristo, wote tuliomwamini Yesu Kristo tunafanyika kuwa ndugu..Upendo wa Kristo unatuunganisha pamoja.tunakuwa tunapendana bila masharti..Upendo huo unatufanya kusiwepo hata na hamu ya kutaka faida kutoka kwa ndugu zetu katika Imani kama vile ilivyo katika ndugu zetu wa mwili. Ndio hapo biblia inatuasa kwamba tusitozane riba sisi kwa sisi. Lakini kwa mtu mwingine nje na ndugu zetu wa kimwili na kiimani, tunaweza kuwatoza ili tupate faida katika tunavyovifanya..kwasababu riba ndio inayokifanya kile kitu au ile shughuli ile iendelee mbele zaidi.

Lakini tukiwatoza ndugu zetu kwa lengo la kupata faida hapo upendo wa Kristo haupo ndani yetu, na hivyo tunafanya dhambi na kumkosea Mungu.

Ezekieli 22:12 “Ndani yako wamepokea rushwa ili kumwaga damu; umepokea riba na faida; nawe kwa choyo umepata mapato kwa kuwadhulumu jirani zako, nawe umenisahau mimi, asema Bwana MUNGU.

 Ubarikiwe.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

USILETE UJIRA WA KAHABA, NYUMBANI KWA MUNGU.

Je! ni sahihi kwa Mkristo kusherekea siku yake ya kuzaliwa.[Birth day]?

USIWE NA HOFU, USHUKAPO CHINI.

EWE MKE! HESHIMA YAKO IPO KWA WAKWE ZAKO.

JINSI NEEMA YA MUNGU ILIVYOKUWA KUBWA KWA MKE WA LUTU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

KUOTA UMEACHWA NA GARI.

Kuota umeachwa na gari, Maana yake ni nini?


Hii ni ndoto inayowapata watu wengi sana.Hususani wale ambao walishaokoka, lakini mambo mengine ya kidunia yanawasonga sasa hivi..Au walisharudi nyuma kabisa na kuacha wokovu

Ndogo hii inakuja katika maumbile tofuati tofauti wengine wanaota wameachwa na ndege, wengine wanaota wameachwa na wenzao ambao walikuwa wanakwenda pamoja,  lakini wengi wao wanaota wameachwa na gari walilokuwa wanasafiria.

Kwa mfano mtu mmoja alinihadhithia ndoto hii, ambayo rafiki yake aliiota ikawa inamsumbua sana..

Aliota alikuwa kwenye basi anasafiri, sasa lile basi likafika mahali kwenye foleni, na yeye baada ya kuona vile limesimama pale,  akaamua kushuka kidogo, na aliposhuka tu lile gari likaanza safari, anasema akaanza kulikimbilia, kumbe wakati analikimbilia kulikuwa na watu wengi nao wanalikimbilia lile gari, mchanganyiko wamama, watoto, na watu wengine n.k. Lakini baadaye yeye akajitahidi kwa nguvu sana kuliwahi akafanikiwa kuingia lakini kwa shida sana, na alipofika ndani akakuta siti yake imeshakaliwa na mtu mwingine..Ikimbidi ajikalie tu mwenyewe pale pembeni, lakini baada ya muda mfupi mzee mmoja akatokea akamsukuma atoke hata pale alipokuwa amekaa, akiwa hana sehemu ya kukaa kwa bahati nzuri akaona siti moja ipo wazi pembeni yake akaenda kuikalia na muda huo huo akashtuka..

Nilipo hoji nikagundua kuwa mtu huyo alikuwa ameokoka lakini baadaye alirudi nyuma, amesongwa na mambo ya ulimwengu huu..Na pale Mungu alikuwa anamwonyesha mwenendo wake jinsi ulivyo alipoona anakawia kukipata kile alichokuwa anakitafuta katika njia yake ya wokovu akaamua kwenda kukitafuta katika mambo ya ulimwenguni..Na hiyo itamgharimu kwasababu upo wakati atatamani kurudi lakini itakuwa ngumu sana kwake kwasababu wokovu sio safari ya kujaribu jaribu kama yule mke wa Lutu alivyofanya, aligeuka mara moja tu, na saa hiyo hiyo akageuka kuwa jiwe la chumvi.

Ikiwa na wewe ni mfano wa mtu kama huyu umeota ndoto ya namna hii umeachwa na basi ujue huo ni ujumbe kamili kutoka kwa Mungu, kuwa unaupoteza wokovu wako, na kuwa ukiendelea katika hali hiyo inayoendelea sasahivi ya kujitenga na wokovu, au kusongwa na mambo ya ulimwengu basi hautaupata tena daima na nafasi yako atapewa mwingine..

Lakini kama wewe hujaokoka kabisa yaani Bwana YESU hajayabadilisha maisha yako, wala huna habari na Mungu.. wewe umekuwa mkristo jina tu, au Muislamu, au huna dini kabisa..Hapo ni Mungu anakuonyesha jinsi gani inavyoogopesha na inavyosikitisha mtu unapoachwa safarini..Sasa jiulize, kwa mtu ambaye haujaanza kabisa safari, yeye atakuwa katika hofu nyingi kiasi gani?..Ndivyo ilivyo hali yako wee Upo katika dhambi, upo mautini, mbingu ipo mbali na wewe.

Sikia sauti ya Kristo, inayokuambia njoo kwangu leo.. Uanze naye safari njema ya kuelekea ufalme wa mbinguni. Kukutana na ujumbe kama huu si bure, Ni Mungu anazungumza na wewe.

Yesu anasema..

Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi.(Yohana 14:6)..

Ikiwa unataka na wewe kwenda mbinguni basi YESU ndiye njia..wala hakuna mwingine.

Vile vile biblia inasema..

Isaya 35:8 “Na hapo patakuwa na njia kuu, na njia, nayo itaitwa, Njia ya utakatifu; wasio safi hawatapita juu yake; bali itakuwa kwa ajili ya watu hao; wasafirio, wajapokuwa wajinga, hawatapotea katika njia hiyo”.

Dunia hii inapita na mambo yake..Utauhangaikia huu ulimwengu mpaka lini, Ukifa leo, ni nani atakuwa mgeni wako huko uendako?. Ni nani atakayekupokea, utaulizwa safari yako ilikuwa ya kuelekea wapi, utajibu nini..Kwanini leo usichukue tiketi yako mkononi, uanze maisha mapya na Bwana Yesu..Kwasababu ni kweli atayabadilisha maisha yako na wewe mwenyewe utaona ni jinsi gani umeianza safari njema, ya uhakika na yenye matumaini..Ulevi, uzinzi, starehe, sema leo ni mwisho ninaamua kumgeukia Kristo.

 Ikiwa unataka kufanya hivyo leo.

Basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie maisha yako yote kama ilivyokuwa hata kwetu sisi. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU  MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.

AMEN.

Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.

Ubarikiwe sana

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

FUATILIA NDOTO HII, UTAJIFUZA KITU.

PENGINE MUNGU ALISHASEMA NAWE KWA NJIA HII.

KUOTA UPO UCHI.

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

USHUHUDA WA RICKY:

Rudi Nyumbani:

Print this post

MAPAMBANO DHIDI YA SHETANI.

Mapambano dhidi ya shetani.

Katika vita siku zote wanaopambana ni wanajeshi dhidi ya wanajeshi..na si raia dhidi ya wanajeshi…Na ndio maana vita huwa vinakuwa ni vigumu sana na vikali…hiyo yote ni kwasababu mwanajeshi anafundishwa kwenda kupambana na mwanajeshi mwenzake ambaye anautaalamu kama yeye, ambaye ni mjuzi wa silaha kama yeye, ambaye anavaa dirii ya kuzuia risasi kifuani kama yeye anavyovaa..ambaye anavaa chepeo kichwani ambayo ni ngumu isiyoweza kuingia risasi kama yeye anavyovaa…ambaye anasilaha na vifaa vya kijeshi kama vya kwake…

Ndio maana unaweza kuona Taifa moja linajiongezea uwezo wa silaha za kijeshi kila kukicha ni kwanini?….Ni kwasababu wanajeshi wanapokwenda vitani wanakwenda kupambana na watu wanaotumia vifaru kama wao…wanakwenda kupambana na watu wenye ujuzi kama wao…Kwa ufupi wanakwenda kupambana na watu wanaofanana na wao karibia kila kitu..na hawaendi kupambana na raia.

Na wakishafanikiwa kumaliza jeshi la maadui basi huwa hawana muda ya kuwaua raia,.. wanachokifanya ni kuchukua tu rasilimali zao, na kuwachukua raia mateka au kuwafanya watumwa wao basii…hawana muda wa kuwaua…kwasababu vile vifaru walivyokuwa wanavitumia vitani havikuwa kwaajili yao bali kwaajili ya wanajeshi wao…

Sasa na sisi wakristo tunafananishwa na wanajeshi waendao vitani…na Biblia inatuambia “Tutwae silaha zote za Mungu”

Waefeso 6:11  “Vaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kuzipinga hila za Shetani

12  Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho.

13 Kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama.

14  Basi simameni, hali mmejifunga kweli viunoni, na kuvaa dirii ya haki kifuani,

15  na kufungiwa miguu utayari tupatao kwa Injili ya amani;

16  zaidi ya yote mkiitwaa ngao ya imani, ambayo kwa hiyo mtaweza kuizima mishale yote yenye moto ya yule mwovu.

17  Tena ipokeeni chapeo ya wokovu, na upanga wa Roho ambao ni neno la Mungu;

18  kwa sala zote na maombi mkisali kila wakati katika Roho, mkikesha kwa jambo hilo na kudumu katika kuwaombea watakatifu wote;”

Kumbuka na sisi hatuendi kupigana na watu wa shetani…bali tunakwenda kupambana na Adui yetu Shetani mwenyewe na mapepo yake. Na kama sisi tulivyo ndivyo na yeye alivyo…kama na sisi tulivyo na upanga mkononi na yeye anao upanga mkononi..kama sisi tulivyo na ngao na yeye pia anayo ngao ya kuzuia mishale kutoka kwetu..kama sisi tulivyo na chepeo kichwani mwetu na yeye ni hivyo hivyo anayo ya kwake…Kwahiyo hapo vita ni lazima viwe vikali tu..kinachohitajika ni kuwa na uwezo wa kuutumia upanga kuliko yeye, kuwa na uwezo wa kuitumia ngao kuliko anavyoitumia yeye, kuwa na uwezo wa kutumia chepeo kuliko anavyoitumia yeye..hiyo ndio njia tu ya kumshinda Adui shetani. Lakini kama yeye anauwezo mkubwa wa kutumia silaha zake kuliko wewe basi atakushinda tu, haijalishi una upanga mkononi, au ngao au chepeo….

Sasa Kwanini tunashika upanga wa Roho mkononi ambao ni Neno la Mungu?..Ni kwasababu Adui yetu na yeye ameshika upanga mkononi…kutupinga sisi…Ndugu usifikiri shetani halijui Neno?…. Analifahamu vizuri sana..na kama biblia inavyosema Neno la Mungu ni upanga ukatao kuwili…maana yake adui akiupata anaweza kuutumia kukuua hata wewe…Hivyo shetani naye ameshikilia upanga wa Neno la Mungu akipambana dhidi yetu…

Kama alivyopambana na Bwana Yesu akiwa kule jangwani…alimwambia Bwana Yesu “imeandikwa hivi katika maandiko”…Na Bwana akawa anamjibu “tena imeandikwa hivi”..Katika ulimwengu wa roho hapo ni pambano kati ya Bwana Yesu na shetani…shetani anaurusha upanga dhidi ya Bwana na Bwana anauzuia na kwa ushapu anamkata na upanga wake ulio mkononi..

Lakini endapo Bwana angekuwa halijui Neno..shetani angemkata kwa Neno hilo hilo..Lakini kwasababu alikuwa analijua kulitumia Neno vizuri aliweza kumshinda shetani..

Kwahiyo ukienda kupambana na Adui shetani na mapepo yake..kama hulijui neno na namna ya kulitumia ipasavyo hakika atakumaliza, kwasababu na yeye kaushikilia upanga unaofanana na wako….(Mapambano dhidi ya shetani  yatakuwa makali sana kwako)

Katika siku hizi za mwisho biblia imetabiri kuwa upendo wa wengi utapoa…Upendo unaozungumziwa hapo ni upendo wa kumpenda Mungu…na si wa kumpenda mwanamke/mwanamume. Watu wengi watakuwa hawana habari ya Neno la Mungu. Leo utamwuliza mtu mara ya mwisho kujifunza mwenyewe binafsi biblia ni lini? Bila kusubiri kutafsiriwa na mtumishi Fulani?..atakuambia ni muda mrefu sana..na hata akisoma, anasoma sura moja mbili kamaliza…Nyakati hizi mbaya tulizopo sio nyakati za kusoma sura moja ya biblia na kutulia baada ya wiki ndio unasoma nyingine…hapo shetani hashindani na wewe anakuona tu kama raia ambaye huna madhara kwake hivyo anakuchukua mateka tu, kama wanajeshi wanavyowachukua raia mateka..

Sasa siku hizi za mwisho, shetani kashawachukua wengi mateka…inawezekana hata wewe umeshachukuliwa lakini hujijui tu, (kwasababu huna silaha yoyote mkononi mwako ya kumwogopesha)…sasa choropoka leo anza kuzifaa silaha chini chini kwa kuanza kujifunza Neno, na baadaye utoke upambane naye ili ukiisha mshinda uwafungue mateka wale wote aliokuwa amewateka kwa uongo wake na kuwafanya kuwa mateka yake kwa uongo wake… wewe wageuze wawe mateko wa Kristo wote aliowateka yeye, kwa elimu yako ya uongo na tabu zake… Kama biblia inavyotuambia..

2 Wakorintho 10:3  “Maana ingawa tunaenenda katika mwili, hatufanyi vita kwa jinsi ya mwili;

4  (maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome;)

5  tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu; NA TUKITEKA NYARA KILA FIKIRA IPATE KUMTII KRISTO;

6  tena tukiwa tayari kupatiliza maasi yote, kutii kwenu kutakapotimia”

Na silaha hiyo ni NENO LA MUNGU..Ukilifahamu Neno la Mungu, Bwana atakutumia kumnyang’anya shetani mateka…na yeye atabaki hana kitu..na jeshi la Bwana litakuwa kubwa zaidi kuliko lake.

Sasa utawezaje kuanza kujivika silaha hizo.?

Kwanza tubu, mpe Yesu Kristo maisha yako kama hujaokoka..kisha jikane nafsi na beba msalaba wako..Halafu anza kupunguza mizigo katika maisha yako ya kila siku, ondoka kwenye magroup yote ya kidunia katika mitandao, Kanunue biblia leo kama huna… “Biblia ya maandishi sio ya kwenye simu”,..kila siku tenga muda mrefu wa kusoma Neno, na unaposoma zima simu na pia kaa sehemu ya utulivu..kisha yasome maandiko na utaona mambo Bwana atakayokufunulia ambayo ulikuwa huyajui…usisome kimstari kimoja au sura moja…Soma angalau kitabu kizima…kwasababu ufunuo wa Roho unaachiliwa pale unapolielewa Neno katika msingi wake, lakini ukisoma kijimstari kimoja hutaelewa chochote na hutapata ufunuo wowote. Soma kitabu cha Injili ya Mathayo uone ni vitu vingapi ulikuwa huvijui na jinsi gani likuwa vinakupita tu na shetani alivyokuwa anakudanganya.

Wakolosai 3: 16 “Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu katika hekima yote..”

Na siku zote kumbuka, mapambano dhidi ya shetani hayajaisha.

Bwana akubariki.

Tafadhali share na wengine, na pia kama utapenda kuyapata masomo haya kwa njia ya whatsapp au email au inbox yako ya facebook basi utatutumia ujumbe mfupi, hali kadhalika unaweza kuyapata bure kwa njia ya internet, tembelea website yetu hii kwa masomo Zaidi /www wingulamashahidi org/.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

JILINDE NA UNAJISI, UNA MADHARA MAKUBWA.

Kwanini kila nikitaka kusali naingiwa na uvivu?

NAMNA YA KUITAMBUA SAUTI YA MUNGU INAPOZUNGUMZA NA WEWE

RABI, UNAKAA WAPI?

Shetani ni nani?

KWA VILE ALIVYOKUWA MTU WA HAKI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

YA KALE YAMEPITA, TAZAMA YAMEKUWA MAPYA

2Wakorintho 5.17 “Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita tazama! Yamekuwa mapya”.

Kuwa kiumbe mpya sio kuwa “mtu mpya”…Mtu ni yule yule isipokuwa tabia zinabadilishwa….Mtu wa tabia za asili anania mambo ya ulimwengu huu…Furaha yake ni kula na kunywa  na anasa kama mnyama tu. Mnyama kamwe hawezi kufikiri kwamba akifa ataenda wapi, na wala hajali chochote isipokuwa watoto wake tu…

Kikubwa katika maisha ya wanyama wanachokijua ni kula, kunywa, kuzaliana, kulea watoto wao na kujiburudisha katika mazingira tofauti tofauti. yanayopatikana katika mazingira ya ulimwengu huu basii…Hali kadhalika hali yake mtu ambaya hajazaliwa mara ya pili..vitu vya pekee vinavyoutawala ufahamu wake ni kuwa na maisha bora katika kiulimwengu huu, aoe/aolewe…awe na nyumba nzuri, awe na mali na maisha bora…na baada ya hapo afe.

Hakuna chochote kinachomhimiza afikiri kuwa kuna maisha baada ya hapa. Fungu lake lipo katika ulimwengu huu.

Lakini mtu aliyezaliwa mara ya pili..biblia inasema anakuwa amevuka kutoka mautini kuingia uzimani, na anakuwa amefanyika kiumbe kipya…akili yake inakuwa imebadilishwa na kuwa akili ya kimbinguni..mawazo yake yanaelekea mbinguni tu…

Vitu vya ulimwengu huu avipate au asivipate hiyo inakuwa haimsumbui sana kwasababu anajua anao utithi wa mbingu zilizo tajiri kuliko mamlaka zote na falme zote duniani.

Je ya kale yamepita kwako? je umefanyika kiumbe kipya?

Kama bado unasubiri nini usiingie ndani ya Yesu leo?..Mkabidhi Yesu maisha yako uokolewe. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

Uasherati wa Kiroho maana yake nini?

Ubatizo wa moto ni upi?

NITAPOKEAJE NGUVU YA KUSHINDA DHAMBI?

NJIA SAHIHI YA KUMPATA MWENZA WA MAISHA KIBIBLIA.

AMANI YA BWANA /AMANI YA MUNGU.

UMUHIMU WA KUZALIWA MARA YA PILI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

CHEMBE YA NGANO ISIPOANGUKA KATIKA NCHI, IKAFA,

Chembe ya ngano isipoanguka katika nchi, ikafa, hukaa hali iyo hiyo peke yake; bali ikifa, hutoa mazao mengi”.


Shalom, Jina kuu la mwokozi wetu Yesu Kristo libarikiwe. Karibu tujifunze maneno ya Mungu yanayobubujisha uzima wa milele ndani yetu.

Kama tunavyosoma katika biblia kuna wakati ambao huduma ya Bwana wetu Yesu Kristo ilifika katika kilele chake, yaani habari zake zilivuma karibia kila mahali, sehemu zote habari zake zilikuwa zinazungumziwa,..Mpaka watu kutoka mataifa mbali mbali wakawa wanakuja kutaka kumwona YESU. Na kuja kwao hakukuwa kwa ajili ya kufuata miujiza tu hapana, bali kwa lengo la kupata wokovu aliokuwa nao.

Mpaka ikafikia wayunani nao wakawa wanatafuta kumwona Yesu..

Yohana 12:20 “Palikuwa na Wayunani kadha wa kadha miongoni mwa watu waliokwea kwenda kuabudu kwenye sikukuu.

21 Basi hao walimwendea Filipo, mtu wa Bethsaida ya Galilaya, wakamwomba, wakisema, Bwana, sisi tunataka kumwona Yesu”.

Unaona?? Lakini Bwana alipoona mazingira yale, na mwitikio ule mkubwa wa watu wengi na wengine kutoka mataifa mbalimbali, aliwaambia wanafunzi wake maneno haya..

Yohana 12:24 “Amin, amin, nawaambia, Chembe ya ngano isipoanguka katika nchi, ikafa, hukaa hali iyo hiyo peke yake; bali ikifa, hutoa mazao mengi”.

Aliwapa mfano huo ulio hai wa chembe ya ngano, ili kuwafundisha watu ni kwanini Mungu ampokee, kwanini Mungu amtukuze kiasi kile, ambapo sisi watu wa kizazi hiki ndio tunaojua ni kwa namna gani Mungu amemtukuza Bwana wetu YESU kwa namna isiyokuwa ya kawaida, leo hii mtu aliye maarufu kuliko wote duniani kwa wakati wote ni YESU KRISTO, na mtu anayezungumziwa sana, kwa kila dakika na kila sekunde moja ni YESU, na jina linalotajawa mara nyingi Zaidi kulingana na takwimu za dunia ni YESU KRISTO, haijalishi ni watu wangapi maarufu watapita hapo katikati lakini yeye atabakia kuwa mtu asiye karibiwa hata kwa nukta moja kwa sifa, na umaarufu duniani kwa wakati wote…

Lakini siri ya yeye kuwa hivyo, ndio ilikuwa katika ule mfano wa chembe (mbegu) ya ngano..akawaambia kama ngano isipotupwa ardhini, ikachimbiwa chini sehemu chafu, ikaoza, na mwisho wa siku ikafa kabisa, basi haiwezi kuzaa na kutoa mazao, na kuletea faida yoyote ulimwenguni.. itaendelea kubakia tu palepale ghalani, katika hali ile ile kwa miezi na miezi na miaka kwa miaka.. Hiyo ni kanuni ya asili kabisa, inajulikana hata kwa mbegu nyingine zote.

Bwana Yesu alikubali kufa kwanza, na kuonekana sio kitu, kwa ulimwengu, soma

(Isaya 53:3 “Alidharauliwa na kukataliwa na watu; Mtu wa huzuni nyingi, ajuaye sikitiko; Na kama mtu ambaye watu humficha nyuso zao, Alidharauliwa wala hatukumhesabu kuwa kitu.”),

Unaona? ulimwenguni wote ulimchukia kwa maisha yake ya kuchukia dhambi, alionekana kama mtu baki duniani,na hiyo ilimfanya aonekana pia kama amerukwa na akili soma..(Marko 3:21)

Yohana mbatizaji alisema alikuja kwake, wala walio wake hawakumpokea (Yohana 1:11).. Alikiri kabisa kwa ndugu zake, kuwa ulimwengu hauwezi kuwachukia wao, bali unamchukia yeye kwasasabu anazishuhudia kazi zake kuwa ni mbovu (Yohana 7:7)..

Embu mwangalie jinsi alivyojikana nafsi,..Jinsi alivyokubali kuoza kwa habari ya ulimwenguni..Lakini hapa sasa Mungu anamtukuza, anamletea mataifa, waje wamsujudie, wanadhani ilitokea tu juu juu.. Ndipo anapowaambia wanafunzi wake..

Yohana 12:24 “Amin, amin, nawaambia, Chembe ya ngano isipoanguka katika nchi, ikafa, hukaa hali iyo hiyo peke yake; bali ikifa, hutoa mazao mengi.

25 Yeye aipendaye nafsi yake ataiangamiza; naye aichukiaye nafsi yake katika ulimwengu huu ataisalimisha hata uzima wa milele.

26 Mtu akinitumikia, na anifuate; nami nilipo, ndipo na mtumishi wangu atakapokuwapo. Tena mtu akinitumikia, Baba atamheshimu”.

Hata na sisi leo hii ni kwanini wokovu wetu unaonekana umekwama mahali Fulani..yaani tangu tuliposema tumeokoka hadi leo, hatuoni badiliko lolote katika roho zetu..ni kwasababu hatukujikana nafsi..Hatukukubali kuoza ardhini kwa habari ya ulimwengu..

Tulipookoka tulikuwa bado tunataka tuonekana ni wa kisasa, kwamba na sisi tunajua kwenda na wakati, na fashion za kiulimwengu, tuvae na sisi vimini vyetu kama zamani, tuvae suruali zetu kama zamani tusiwe tofauti na wale wanenguaji..tuendelee kuhudhuria katika kumbi za starehe..tuendelee kulewa vilabuni, tuendelee kukaa na watu wanaozungumza maneno ya mizaha muda wote,..tuendelee na biashara zetu haramu..tuzidi kuwa wakidunia..tusipende kujifunza maneno ya Mungu marefu, tupende mafundisho mepesi mepesi, tunayotutabiria mafanikio..n.k.

Kwa namna hiyo Bwana Yesu anatuambia..tutabaki katika hali hiyo hiyo katika roho..miaka nenda miaka rudi..hutaona badiliko lolote katika roho yako, hutaona Bwana akikupigisha hatua nyingine rohoni..utakuwa unakwenda kanisani unarudi, unahudhuria madarasa ya biblia kila siku..Lakini maisha yako hayana ushuhudu wowote..

Yaani kwa kifupi ukiulizwa tangu siku uliposema umeokoka hadi leo, ni jambo gani Mungu kakuongezea ndani ya maisha yako, utasema sijaona.. Hatuzungumzii masuala ya fedha, kwasababu si kila mwenye fedha amebarikiwa, japo Baraka zinaweza kuambata na fedha..lakini fedha si lazima ziambatane na Baraka..Tunachozungumzia ni mafanikio yako ya rohoni..Je! Roho yako imenufaishwa na huo wokovu kiasi gani tangu uliposema umeokoka?..

Damu ya YESU imeleta badiliko gani jipya katika maisha yako? Je! Zile chemchemi za maji ya uzima zinabubujika ndani yako? Je! Roho Mtakatifu anakushuhudia ndani yako kuwa wewe ni mwana wa Mungu?, Je! Siku kwa siku unamwona akitembea katika maisha yako,

Je! Wokovu wako ulishawahi kuwa faida kwa wengine nao pia wakaupokea?..Je! ndani yako dhambi imekuwa mbali na wewe kiasi gani?..Je utakatifu ni mrahisi kwako? N.k

Kama ni La! Basi ujue mbegu yako haijaoza..na ndio maana huna matunda yoyote..

Kama unafikiria kutubu dhambi zako..basi ujue kuwa toba inaambatana na kitendo cha kujikana nafsi, mahali ambapo unasema msalaba mbele dunia nyuma..Unakuwa tayari kuchekwa kwa ajili ya wokovu wako..Unakuwa tayari kuonekana ni mshamba kwa ajili ya wokovu wako, unakuwa tayari kuonekana umerukwa na akili kwa ajili ya kukubali kwako kuishi maisha matakatifu..

Hapo ndipo unapooza…mbinguni unaonekana umeipoteza nafsi yako,..mpaka unakufa kabisa kwa habari ya ulimwengu..Sasa baada ya hapo, Mungu ndipo anapokuhuisha na kuanza kukuchipua tena kutoka ardhini, na kidogo kidogo anakukuza, anakutoa hatua moja hadi nyingine, unaanza kumwona Mungu katika viwango vya tofauti na pale mwanzo, unauhisi ule uhalisia wa wokovu ndani yako yako..

Na ghafla utashangaa anakufikisha mahali ambapo, wewe mwenyewe hukudhania kama ungeweza kufika kwa wakati huo..na hata yale uliyoyapoteza Mungu anakurudishia kwa wakati wake ukifika..Mwisho wa siku unakuwa na matunda kote kote…

Hivyo ndugu, kama hujaubeba msalaba, basi tujikane nafsi leo mfuate Yesu..maana huko ndipo yeye anapotungojea wote. Ili na sisi tubarikiwe kama yeye, tusibaki katika hali ile ile rohoni siku zote.

Shalom. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

JIKANE NAFSI MTEULE WA MUNGU.

TABIA YA KIPEKEE USIYOIJUA KUHUSU NENO LA MUNGU.

HAKIKISHA UNALIELEWA NENO.

NI NANI ALIYEWALOGA?

JINSI SODOMA NA GOMORA ILIVYOKUWA INAVUTIA SANA..

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

TUWATAFAKARI NZIGE WA JANGWANI.

MAONO YA NABII AMOSI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

USIWE NA HOFU, USHUKAPO CHINI.

Shalom, Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe.

Mungu anapotaka kumtoa mtoto wake sehemu moja kwenda nyingine anakuwa kama anamrudisha kwanza nyuma ili ampandishe juu katika hatua nyingine…Vitu vya asili pia vinatufundisha, ili Mshale uweze kwenda mbali Zaidi ni lazima uvutwe nyuma kwa nguvu kwa kadiri iwezekanavyo kutoka katika ule uta..ukiuvuta kidogo utakwenda mbali kidogo, ukiuvuta nyuma sana, utakwenda mbali zaidi, vivyo hivyo katika mkuki, au manati. Kila kitu ili kufike mbali ni lazima kirudishwe nyuma kidogo. Kwasababu nguvu ya kwenda mbali Zaidi inaanzia nyuma zaidi.

Baada ya Mungu kuona ukamilifu wa Ayubu, jinsi anavyomcha yeye na anavyojiepusha na uovu…aliona anastahili kubarikiwa baraka mara mbili Zaidi..na ulipofika wakati wa kumbariki alimshusha kwanza chini na kumnyang’anya vile vyote alivyokuwa navyo…na baada ya kumnyang’anya ni sawa na mshale uliovutwa nyuma unaojiandaa kuachiwa uende mbali zaidi , Na,tunaona baadaye Ayubu alipoachiliwa alikuja kupata vitu mara mbili Zaidi.

Mungu alipoona uaminifu wa Danieli katika nafasi yake ya uwakili wa Uajemi aliowekwa kwamba hali-rushwa wala haibi na kwamba ni mwaminifu siku zote katika nafasi yake…ulipofika wakati wa kumpandisha cheo cha ju Zaidi alikuwa hana budi kushushwa kwenye nafasi ile ya chini kabisa mpaka kupelekwa kwenye tundu la simba kuuawa…hapo alikuwa ni sawa na upinde uliovutwa nyuma, na ulipoachiwa alipanda juu Zaidi..akawa mkuu zaidi ya maliwali wote (Danieli 6:28)

Mungu alipoona uaminifu wa Mordekai katika geti la Mfalme kwamba ni mwaminifu, hali rushwa, na katika nafasi yake hajawa mnafiki wala mtu mwenye nia mbaya na mfalme, Zaidi ya yote alimwokoa mfalme na mauti ya watu wabaya, aliokuwa anafanya nayo kazi..Mungu alipoona huo moyo wake mwema na mkamilifu na alipotaka kumpandisha juu…Mordekai alikuwa hana budi kwanza kuvutwa chini, kwani tunaona alitengenezewa visa vya kuuawa mpaka Adui yake mkubwa akaenda kuchonga mti mrefu ili amtundike Mordekai kwa ruhusa ya Mfalme..na Mordekai alikuwa yupo hatarini kufa kama alivyokuwa Danieli…

Lakini Mungu alimwokoa Mordekai na kumpandisha cheo cha juu Zaidi na kuwa mkuu wa majemedari wa Uajemi..Kutoka kuwa mlinzi mpaka kuwa mkuu wa majeshi…Lakini ilikuwa ni lazima kwanza ashushwe chini kiwango cha kukaribia na kufa.

Na ipo mifano mingi katika biblia ya namna hiyo ambapo kabla ya Bwana kumpandisha mtu kutoka ngazi moja kwenda nyingine…anakuwa anamrudisha kwanza ngazi moja chini ili apande juu Zaidi. Hakuna njia ya mkato.

Kwahiyo usiogope unapoona umepoteza kitu fulani unachoona cha muhimu katika Maisha yako, labda kazi au mali kwasababu ya haki unazozifanya…Ukiona umepoteza vyote hivyo na kufikia hatua upo hatarini hata kupoteza Maisha yako, au heshima yako basi fahamu kuwa ni Bwana amekupenda na anataka kukunyanyua juu Zaidi na pale ulipokuwepo…katika hatua kama hiyo usiache uaminifu wako kwasababu ameiona haki yako na hivyo anataka kukupandisha juu Zaidi kama alivyomfanyia Danieli. Lakini njia ya kupandishwa ndio kama hiyo aliyotumia kwa watumishi wake katika biblia..(unatikiswa kwanza kidogo)

Ukiona hata umefungwa kwa kesi ambayo ni ya kusingiziwa au kwa jinsi isivyo haki, ukiona umefilisika kwa sababu hufanyi biashara za magendo na umekataa biashara zisizo halali..hiyo isikusumbue hata kidogo upo katika kipindi cha kuvutwa chini ili upande juu Zaidi..Ni jambo la muda tu!..

Ukiona unamcha Mungu na hapo kwanza mambo yako yalikuwa yanaenda vizuri.. lakini ghafla mambo yameharibika kunatokea visa hivi na vile…kunatokea maadui wengi sana, hatua kama hiyo unapofikia usimchukie mtu bali ujue kuwa upo katika kipindi cha kushushwa ili upandishwe. Hivyo ndivyo Mungu anavyofanya ili kumpandisha mtu kutoka ngazi moja kwenda nyingine.

Lakini kama umepoteza vyote kwasababu ulikuwa mwasherati, au kwasababu umekamatwa unakula rushwa, au fisadi au kwasababu ya wizi au jambo lolote baya ukafungwa au ukafilisika…hapo ni Bwana amekurudi ili utubu…uache wizi wako, uache uasherati wako, uache rushwa zako, uache mambo yote mabaya unayoyafanya na umgeukie yeye kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote. Na baada ya kufanya hivyo ndipo atakufanyia hayo mengine. Lakini usipotubu hakuna lolote litakalotokea la kukunufaisha. Kwasababu hapo Mungu hajakushusha ili akupandishe juu, bali ili utubu kwanza!

Lakini kama unamcha Bwana, umeokoka, umejitenga kweli kweli na ulimwengu..usiogope! tena majaribu yanapokuja ya namna hiyo unapaswa ufurahi kwasababu ndio wakati wa kukumbukwa kwako.

Bwana akubariki. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

MAISHA ULIYOPITIA NYUMA NI USHUHUDA TOSHA WA WEWE KUMTUMIKIA MUNGU

DHAMBI ILIYOMKOSESHA SHETANI:

Roho, Nafsi, na Mwili vina utofauti gani?

JINSI NEEMA YA MUNGU ILIVYOKUWA KUBWA KWA MKE WA LUTU.

BWANA HUWAJUA HAO WAMKIMBILIAO.

RABI, UNAKAA WAPI?

UFUNUO: Mlango wa 1

CHAPA YA MNYAMA

Rudi Nyumbani:

Print this post