SWALI: Kitabu cha Mathayo 27:44 na Marko 15:32b inazungumzia wale wanyang’anyi walioteswa pamoja na Yesu kuwa wote wawili walimtukana Yesu pia, ila tukisoma Luka 23:39 inasema ni mmoja ndiye alimtukana sasa kwanini inakuwa hivyo naomba unisaidie nielewe?.
JIBU: Tuvipitie vifungu vyenyewe;
Mathayo 27:44 “Pia wale wanyang’anyi waliosulibiwa pamoja naye walimshutumu vile vile.
Marko 15:32 Kristo, mfalme wa Israeli, na ashuke sasa msalabani tupate kuona na kuamini. Hata wale waliosulibiwa pamoja naye wakamfyolea.
Luka 23:39 “Na mmoja wa wale wahalifu waliotungikwa alimtukana, akisema, Je! Wewe si Kristo? Jiokoe nafsi yako na sisi.
40 Lakini yule wa pili akamjibu akamkemea, akisema, Wewe humwogopi hata Mungu, nawe u katika hukumu iyo hiyo?
41 Nayo ni haki kwetu sisi, kwa kuwa tunapokea malipo tuliyostahili kwa matendo yetu; bali huyu hakutenda lo lote lisilofaa.
42 Kisha akasema, Ee Yesu, nikumbuke utakapoingia katika ufalme wako.
43 Yesu akamwambia, Amin, nakuambia, leo hivi utakuwa pamoja nami peponi”.
JIBU: Ukisoma juu juu ni rahisi kusema maandiko yanajichanganya, lakini hakuna kinachojichanganya isipokuwa ni sisi wenyewe tunakosa shabaha ya kuyaelewa maandiko.
Habari hii inafanana na ile, ya wale watu wawili ambao Yesu alikutana nao kule makaburini wenye pepo, ukisoma pale utaona injili moja inaonyesha Bwana alikutana na vichaa wawili, wakati injili nyingine inaonyesha alikutana ni kichaa mmoja, Sasa habari hizo sio kwamba zinajichanganya, hivyo Ili kupata ufafanuzi wake basi fungua hapa >>> Wenye pepo
Sasa tukirudi kwenye habari hiyo tunaona Injili ya Mathayo na Marko inaonyesha kuwa wale wahalifu wawili walimdhihaki Bwana Yesu akiwa pale msalabani, bila upingamizi wowote . Lakini Injili ya Luka inaonyesha mmoja ndiye aliyemtukana lakini yule mwingine alimwomba rehema.
Kabla hatujalijibu swali, Tukumbuke kuwa Bwana Yesu alikuwa pale msalabani kwa muda mrefu sana usiopungua masaa 6, na wakati huo wote, wale wahalifu waliosulibiwa naye walikuwa wanautazama mwitikio wake, alipokuwa katika hali kama ya kwao, ni wazi kuwa mwanzoni wote walidhani Yesu ni kama mmojawapo wa wahalifu wenzao, na hiyo haikuwa shida wote kutoa kauli za kudhihaki na kukebehi na ndio maana injili ya Mathayo na Marko zinaonyesha kuwa wote walimkebehi..
Lakini ni wazi kuwa baadaye kidogo yule mmoja alitubu, akageuka, na hiyo ni pengine baada ya kuona utofauti wa Yesu na matendo aliyokuwa anayaonyesha pale msalabani, alipoona aliposhutumiwa hakurudisha majibu, alipoona anawaombea msamaha, akisema Baba wasamehe kwa kuwa hawajui watendalo, pengine hilo lilimgusa sana, alipoona upendo wake wa kipekee, japokuwa alikuwa matesoni..Hilo ndilo lililomfanya yule muhalifu mmoja ageuze mtazamo wake na kujua kabisa Kristo hakuwa na kosa lolote..
Na zaidi ya yote alipoona mpaka giza limeingia mchana kweupe, jambo ambalo si la kawaida.. Alitubu saa ile ile na mpaka kumwambia yule wenzake sisi ni kweli tumekosea, lakini huyu hakufanya kosa lolote linalomstahili yeye kuuawa. Ee Yesu unikumbuke katika ufalme wako.
Ni kitu gani tunajifunza?
Hiyo inatuonyesha uvumilivu wa Mungu jinsi ulivyo kwa wenye dhambi. Hata wewe mwenye dhambi Inawezekana umekuwa ukimdhihaki Mungu mara nyingi, ukizipuuzia njia zake na kuziona ni za watu waliorukwa na akili mara nyingi, hata umefikia hatua ya kuutukana wokovu waziwazi na Mungu mwenyewe., lakini bado Mungu anakupa nafasi ya kutubu leo. Lakini nafasi hiyo haitadumu milele. Kumbuka wahalifu wale wote walikufa baada ya muda mfupi, lakini mpaka sasa tunaongea mmoja yupo peponi mwingine yupo motoni.
Yule aliye motoni alipuuzia wokovu mpaka dakika ya mwisho hakujua kuwa hana muda mrefu wa kuishi. Swali ni Je! Wewe pia unatambua muda uliobakiwa nao hapa duniani? Kama hufahamu ni kwanini basi bado upo kwenye dhambi? Hivyo tubu leo Yesu akuokoe akuoshe dhambi zako, ufanyike mtoto wake kweli kweli. Hizi ni nyakati za mwisho. Majira haya ni ya kumalizia. Hivyo usiruhusu, dhambi iendelee kuwa sehemu ya maisha yako.
Maran Atha.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618.
Jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
Shekina au Shekhinah / schechinah, Ni neno la kiyahudi linalomaanisha, “kutua” au “kuweka makao” au “makazi” ya uwepo wa Mungu duniani. Hivyo utukufu wa Shekina maana yake ni kujifunua kwa uwepo wa Mungu kwa dhahiri duniani, ambapo kuonekana kwake kunaweza kuchukua mfumo wa vitu mbalimbali vya asili , kama vile moto, wingu,moshi,mwanga, kijiti kinachoteketea n.k.,..
Neno hili huwezi kulikuta kwenye biblia, lakini maudhui yake ipo ndani ya biblia. Ni neno lililoanzishwa, na waalimu wa kiyahudi , (Marabi) , na yalionekana kwenye fasihi zao na maandishi yao ya kale, kipindi cha pale katikati kutoka agano la kale kuelekea agano jipya..
Kutoka 13:20 “Nao wakasafiri kutoka Sukothi, wakapiga kambi Ethamu, kwenye mpaka wa ile jangwa.
21 Bwana naye akawatangulia mchana ndani ya wingu mfano wa nguzo, ili awaongoze njia; na usiku, ndani ya moto mfano wa nguzo, ili kuwapa nuru; wapate kusafiri mchana na usiku;
22 ile nguzo ya wingu haikuondoka mchana, wala ile nguzo ya moto haikuondoka usiku, mbele ya hao watu”.
Nakadhalika, na Kadhalika..
JE! NA SISI TUNAWEZA KUKUTANA NA UTUKUFU WA SHEKINA?
Pamoja na kwamba Mungu alijifunua dhahiri katika vitu vingi vya asili, kwa watu wachache, lakini kuna wakati ambao aliuweka mahususi kwa ajili ya kujifunua kwa watu wote, katika viwango vya juu kabisa vya utukufu wake ambao havijawahi kutokea hapa duniani.. Utukufu ambao ni zaidi ya wingu, au nguzo ya moto, au moshi, au tufani..na huo sio mwingine zaidi ya mwili wa Mwanadamu, ulioitwa YESU KRISTO. Biblia inatuambia kabisa kuwa Yesu alikuwa ni Mungu mwenyewe aliyechukua umbo la kibinadamu na kuishi na sisi (1Timotheo 3:16)
Na yeye ndiye utukufu pekee wa Mungu ambao alishawahi kufunua hapa duniani tangu dunia iumbwe..
Yohana 1:14 “Naye Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu; nasi tukauona utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee atokaye kwa Baba; amejaa neema na kweli”.
Soma tena..
Wakolosai 2:9 “Maana katika yeye unakaa utimilifu wote wa Mungu, kwa jinsi ya kimwili”.
Hivyo kwa kifupi tunaweza kusema utukufu wa shekina tulionao sasa ni YESU KRISTO. Na kila mmoja wetu ameweza kumwona Mungu zaidi hata ya wale waliotokewa katika nguzo ya moto, ikiwa tu atakubali kuingia katika neema yake..
Swali ni Je! Utukufu huo umefunuliwa ndani yako? Je Umempokea Yesu katika maisha yako?. Kumbuka hakuna njia yoyote utakayoweza kumfikia Mungu, au hata kumjua Mungu isipokuwa kwa njia ya Yesu Kristo. Jiulize, ulimwengu umekuahidia nini tangu umeanza kuutumikia? Ukweli ni kwamba haujakupa ahadi yoyote, ya kuendelea kuishi, Lakini Kristo anakuahidia uzima wa milele baada ya kufa, kwanini usichague uzima, na mengine mengi?
Kama upo tayari leo hii kuyakabidhi maisha yako kwa Yesu, ili utukufu huu halisi wa Shekina ukujue juu yako, basi huo ni uamuzi wa busara sana kwako. Ikiwa jibu ni ndio, basi fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba na kupokea maagizo mengine.>>> SALA YA TOBA
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312/ +255 693036618.
Jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
VIGEZO VYA KUWA KARIBU NA YESU KRISTO KATIKA ULIMWENGU UJAO.
Kama vile Daudi alivyokuwa shujaa, vivyo hivyo yeye naye alikuwa na mashujaa wake wengine 37 waliokuwa chini yake wakimzunguka wakati wote,walipokuwa vitani kushindana na maadui zao .
Kwa ufupi mashujaa hao waligawanyika katika makundi makuu matatu (3), Kundi la kwanza lilikuwa na mashujaa watatu wa juu, kundi la pili lilikuwa na mashujaa wawili, na kundi la tatu lilikuwa na mashujaa wengine thelathini na mbili.
Hilo kundi la kwanza la juu lenye mashujaa watatu,.mtu wa kwanza aliitwa Yashobeamu Mhakmoni, mwingine ni Eleazari na wa mwisho ni Shama.. Hawa walikuwa mashujaa kweli kweli, na kundi la chini yake kidogo alikuwepo mtu mmoja aliyeitwa Abishai na mwingine ni Benaya, hawa nao walikuwa ni mashujaa sana, halafu lile kundi la mwisho, ndio alikuwepo Uria Mhiti, na wengine, yule ambaye Daudi alimtamani mke wake, hivyo akamweka kwenye vita vikali ili auwe kisha amchukue mke wake.. Huyu alikuwa mmojawapo wa wale wengine..
Sasa embu tuwatazame baadhi ya matendo ya mashujaa hawa kwa ufupi mambo waliyoyafanya, kisha mwishoni tutapata somo la kujifunza..
1) Yashobeamu Mhakmoni:
Huyu ndio Yule shujaa wa juu zaidi ya wote, katika vita alifanikiwa kuwaua wanajeshi 800 kwa mkuki wake mmoja, Jaribu kutengeneza picha mtu mmoja anaua watu 800, huyo ni shujaa kweli kweli mfano wa Samsoni,(2Samweli 23:8)
2) Eleazari, mwana wa Dodai.
Huyu naye alifanya mambo ya kustaajabisha, walipokuwa wamekusanyika ili kupigana na wafilisti kule kondeni, Israeli wote wakakimbia akabaki yeye peke yake na Daudi tu, lakini alinyanyuka na kuwapiga wafilisti, wengi kiasi kwamba hadi mkono wake ukachoka kuua, hata alipojaribu kuuachia upanga mkono wake bado umeshikamana na upanga, tu, (1Nyakati 11:12)
2Samweli 23:9 Na baada yake kulikuwa na Eleazari, mwana wa Dodai, Mwahohi, mmojawapo wa wale mashujaa watatu waliokuwa pamoja na Daudi; walipowatukana Wafilisti waliokuwa wamekusanyika huko ili kupigana, na watu wa Israeli walikuwa wamekwenda zao;
10 huyo aliinuka, akawapiga Wafilisti hata mkono wake ukachoka, na mkono wake ukaambatana na upanga; naye Bwana akafanya wokovu mkuu siku ile; nao watu wakarudi nyuma yake ili kuteka nyara tu.
3) Shama, mwana wa Agee.
Huyu naye alikuwa kwenye mashamba ya midengu pamoja na waisraeli wengine, lakini wafilisti walipotokea wakakimbia, akabaki yeye tu peke yake kondeni, akapigana na wafilisti wengi sana akawaua yeye peke yake, hivyo akafanikiwa kulilinda lile shamba la midengu lisichukuliwe na wafilisti.(2Samweli 23:11-12)
Aliwaua kwa wakati mmoja watu 300 kwa mkuki wake,(2Samweli 23:18)
II. Benaya, mwana wa Yehoyada:
Aliwaua majitu mawili wa Kimoabu, pia alimuua simba katikati ya pango, vilevile alimuua Mmisri ambaye alikuwa mrefu sana mfano wa Goliathi, kwa kutumia silaha ya adui yake.
2Samweli 23:20…..”aliwaua simba wakali wawili wa Moabu, pia akashuka akamwua simba katikati ya shimo wakati wa theruji.
21 huyo naye akamwua Mmisri, mtu mrefu; naye huyo Mmisri alikuwa na mkuki mkononi; lakini yeye alimshukia na gongo, akamnyakulia Mmisri mkuki mkononi mwake, akamwua kwa mkuki wake mwenyewe”.
III. Mwingine ni Elhanani ambaye alimwangusha Goliathi, mfano wa yule aliyeangushwa na Daudi.
2Samweli 21:19 “Kulikuwa na vita tena na Wafilisti huko Gobu; na Elhanani, mwana wa Yairi, Mbethlehemi, alimwua Goliathi, Mgiti, ambaye mti wa mkuki wake ulikuwa kama mti wa mfumaji.
20 Kulikuwa na vita tena huko Gathi; ambako kulikuwa na mtu mrefu sana, mwenye vidole sita katika kila mkono, na vidole sita katika kila mguu, jumla yake ishirini na vinne; yeye naye alizaliwa kwa Mrefai.
21 Naye huyo alipowatukana Israeli, ndipo Yonathani, mwana wa Shama, nduguye Daudi, akamwua.
22 Hao wanne walizaliwa kwake huyo Mrefai wa Gathi; wakaanguka kwa mkono wa Daudi, na kwa mikono ya watumishi wake.
IV. Na mashujaa wengine ambao walifanya matendo ya kishujaa unaweza kuwasoma katika..2Samweli 23:14-17..
Lakini tunavyousoma ushujaa wao watu hawa, tunaweza kujiuliza Daudi aliwatolea wapi? Je aliwaiba katikati ya jeshi la Sauli?, au alienda kuwatafuta miongoni mwa watu waliokuwa na nguvu sana Israeli? Jibu ni la!
Mashujaa hawa 37, Daudi aliokuwa nao, hakuwatoa katikati ya kambi za kivita, bali walikuwa ni watu wa kawaida sana wasiokuwa na uelekeo wowote wa ki maisha, watu hohe-hahe tu, watu waliokuwa katika umaskini, wenye dhiki nyingi, wenye madeni, watu dhaifu, watu wasio na raha moyoni, ndio waliokusanyika wakawa pamoja na Daudi, na kati ya hao ndio likanyanyuka wimbi kubwa la mashujaa namna ile ambao waliogopeka na majeshi makubwa yaliyokuwepo wakati ule.
1Samweli 22:1 “Basi Daudi akaondoka huko, akakimbilia pango la Adulamu; na ndugu zake na watu wote wa mbari ya baba yake waliposikia habari hiyo, wakamwendea huko.
2 Na kila mtu aliyekuwa katika hali ya dhiki, na kila mtu aliyekuwa na deni, na watu wote wenye uchungu mioyoni mwao, wakakusanyika kwake; naye akawa jemadari wao; nao waliokuwa pamoja naye walipata kama watu mia nne”.
Sasa Daudi ni mfano wa Kristo, hata sasa Bwana anao mashujaa wake wa Injili, na bado anaendelea kuwatafuta, lakini maandiko yanatuambia mashujaa hao hawatafuti katikati ya watu wenye vyeo, watu matajiri, watu wenye ujuzi mwingi, badala yake anawatafuta katikati ya watu wasiokuwa na uelekeo wowote, watu wa kawaida sana…
1Wakoritho 1:26 “Maana, ndugu zangu, angalieni mwito wenu, ya kwamba si wengi wenye hekima ya mwilini, si wengi wenye nguvu, si wengi wenye cheo walioitwa;
27 bali Mungu aliyachagua mambo mapumbavu ya dunia awaaibishe wenye hekima; tena Mungu alivichagua vitu dhaifu vya dunia ili aviaibishe vyenye nguvu;
28 tena Mungu alivichagua vitu vinyonge vya dunia na vilivyodharauliwa, naam, vitu ambavyo haviko, ili avibatilishe vile vilivyoko;
29 mwenye mwili awaye yote asije akajisifu mbele za Mungu”.
Unaona, hivyo ndugu.. Mimi na wewe tunayo nafasi sana kubwa ya kuwa mashujaa wa Kristo ikiwa tu tutakubali kuambatana naye, hilo tu, umaskini wako sio kigezo, madeni yako sio sababu, dhiki zako sio sababu za wewe kutokuwa shujaa wa Bwana. Usije ukasema ooh! Mimi nilikuwa sina pesa ndio maana nikashindwa kukutumikia..Siku ile mashujaa kama hao watatuhukumu.
Maran Atha.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618.
Jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
Jina la Bwana wetu na Mwokozi wetu, Yesu Kristo libarikiwe…Karibu katika kuyatafakari maandiko, tumekwisha kuvipitia vitabu kadhaa vya Mwanzo, naomba kama hujavipitia na ungependa kuvipitia, basi fungua hapa >> VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1
Leo kwa neema za Bwana tutasonga mbele kitabu kingine kimoja, ambacho ni kitabu cha Zaburi.
Kitabu cha Zaburi ndio kitabu kirefu kuliko vitabu vyote katika biblia, na ndio kitabu ambacho kipo katikati ya Biblia. Sehemu kubwa ya kitabu hichi imeandikwa na Mfalme Daudi, mwana wa Yese. Lakini sio Milango yote imeandikwa na Daudi, la!..milango mingine imeandikwa na Sulemani, Mfalme Hezekia, Asafu,Musa, Ethani na Hemani.
Kitabu hichi kimeandikwa katika mfumo wa beti za nyimbo. Kwasababu maana tu ya neno lenyewe Zaburi ni “Nyimbo takatifu zilizoimbwa kwa vyombo vya muziki vya nyuzi nyuzi, kama vile santuri, kinubi na zeze”. Kama utapenda kuvijua vyombo hivyo vya nyuzi nyuzi vya muziki kwa urefu utatutumie ujumbe inbox.
Hivyo nyimbo hizi za Zaburi, ziliandikwa si kwa lengo la kuburudisha bali kwa lengo la kumshukuru Mungu, kumtukuza Mungu, kumwomba Mungu, kumsifu Mungu, kuomba ulinzi na haki .
Mfalme Daudi alizitunga nyimbo hizi katika kipindi chote cha maisha yake aliyoishi (yaani miaka 70). Hivyo hakikuandikwa kwa siku moja, au wiki moja. Kila hatua ya maisha Daudi aliyoipitia Roho ya Mungu ilishuka juu yake na kumsukuma kuandika beti za nyimbo hizo, ambazo leo tunazisoma katika biblia.
Sasa swali ni kwanini zimeandikwa katika mfumo wa Nyimbo?
Ikumbukwe kuwa Daudi tangu akiwa mdogo alikuwa na kipaji cha kupiga filimbi na kinubi..Hivyo alijifunza kumwimbia Mungu tangu akiwa mdogo, na kipaji chake hicho Mungu alichompa, kuna kipindi kilivuma mpaka hadi kikamfikia Mfalme Sauli..
1Samweli 16:14 “Basi, roho ya Bwana ilikuwa imemwacha Sauli, na roho mbaya kutoka kwa Bwana ikamsumbua.
15 Nao watumishi wa Sauli wakamwambia, Angalia, sasa roho mbaya kutoka kwa Mungu inakusumbua.
16 Basi bwana wetu na atuamuru sisi watumishi wake waliopo hapa mbele yako watafute mtu aliye stadi wa kupiga kinubi; basi itakuwa, roho ile mbaya kutoka kwa Mungu itakapokujilia, yeye atapiga kinubi kwa mkono wake, nawe utapona.
17 Basi Sauli akawaambia, VEMA, NITAFUTIENI MTU ALIYE STADI WA KUPIGA KINUBI, MKANILETEE.
18 Ndipo akajibu mmoja wa watumishi wake akasema, Tazama, nimemwona mwana mmoja wa Yese, Mbethlehemi, ALIYE STADI WA KUPIGA KINUBI, tena ni mtu shujaa, hodari wa vita, anenaye kwa busara, mtu mzuri, ambaye Bwana yu pamoja naye.
19 Basi Sauli akampelekea Yese wajumbe, akasema, Nipelekee Daudi mwanao, aliye pamoja na kondoo……….
23 Ikawa, ile roho mbaya kutoka kwa Mungu ilipomjilia Sauli, NDIPO DAUDI AKAKISHIKA KINUBI, AKAKIPIGA KWA MKONO WAKE, naye Sauli akaburudishwa, na ile roho mbaya ikamwacha”.
Hivyo kipaji hicho cha kupiga vinubi na kuimba, alichokuwa nacho Daudi, aliendelea kukitumia mpaka anaondoka Duniani.
Sasa ni Mazingira gani aliyokuwa mfalme Daudi wakati anaandika hizo Zaburi.
Daudi hakuwa anakaa tu ndani, na ghafla anaanza kujikuta anaandika nyimbo hizo. Hapana, mfano wa mazingira aliyokuwa anaandika beti hizo, ni wakati labda ametoka vitani na Mungu kampa ushindi dhidi ya maadui zake ambao pengine walikuwa ni hodari kupita wao, hivyo ile furaha anayoipata na huku anaona kama sio Mungu wasingeshinda, ile furaha inamsukuma kuandika nyimbo za kumshukuru Mungu.
Kwamfano hebu tuziangalie beti chache za Daudi katika Zaburi kasha tuzitafute ziliandikwa kipindi gani.
Tuanze na Zaburi ya 105, inasema hivi..
Zaburi 105:1 “Haleluya. Mshukuruni Bwana,liitieni jina ,Wajulisheni watu matendo yake.
2 Mwimbieni, mwimbieni kwa zaburi, Zitafakarini ajabu zake zote.
3 Jisifuni kwa jina lake takatifu, Na ufurahi moyo wao wamtafutao Bwana.
4 Mtakeni Bwana na nguvu zake, Utafuteni uso wake sikuzote ”
Je ni kwamba Daudi alikaa tu ndani?..na akachukua tu kalamu na karatasi kuandika ubeti huo?..Jibu ni la!..Ubeti huo uliandikwa kipindi Mfalme Daudi Analitoa sanduku la Agano kwa Obed-odemu kwenda mjini kwake yaani (Yerusalemu).. Hivyo kwa furaha kubwa wakati sanduku la agano linaingia tu mjini mwake, alicheza mpaka nguo zikamtoka, na alilisindikiza Sanduku hilo la agano, kwa nyimbo nyingi za santuri na vinubi…
Tusome…
1Nyakati 15:25 “ Basi Daudi, na wazee wa Israeli, na maakida wa maelfu, wakaenda, ili kulipandisha sanduku la agano la Bwana kutoka nyumbani mwa Obed-edomu kwa furaha kuu;
26 hata ikawa, Mungu alipowajalia Walawi waliolichukua sanduku la agano la Bwana, wakachinja ng’ombe saba, na kondoo waume saba.
27 Naye Daudi alikuwa amevaa joho ya kitani safi, na Walawi wote waliolichukua sanduku, na waimbaji, na Kenania msimamizi wa uchukuzi, na waimbaji; naye Daudi alikuwa amevaa naivera ya kitani.
28 Ndivyo Israeli wote walivyolipandisha sanduku la agano la Bwana kwa shangwe na kwa sauti ya tarumbeta, na kwa baragumu, na kwa matoazi, wakipiga sauti kuu kwa vinanda na vinubi.
29 Hata ikawa, sanduku la agano la Bwana lilipofika mjini kwa Daudi, Mikali binti Sauli akachungulia dirishani, akamwona mfalme Daudi, akicheza na kushangilia; akamdharau moyoni mwake”.
Sasa tukiendelea mlango wa 16 kuanzia mstari wa 9 ndiyo tunaiona Zaburi hiyo ya 105 ilipotokea.
Tusome..
1Nyakati 16:1 “Wakaliingiza sanduku la Mungu, na kuliweka katikati ya hema aliyoipiga Daudi kwa ajili yake; wakatoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani mbele za Mungu.
2 Na Daudi alipokwisha kuitoa sadaka ya kuteketezwa na sadaka za amani, akawabariki watu kwa jina la Bwana.
3 Kisha akawagawia kila mtu wa Israeli, waume kwa wake, kila mtu mkate wa ngano, na kipande cha nyama, na mkate wa zabibu.
4 Akawaagiza baadhi ya Walawi kwamba watumike mbele ya sanduku la Bwana, wamfanyie ukumbusho, na shukrani, na sifa, Bwana, Mungu wa Israeli;
5 Asafu mkuu wao, na wa pili wake Zekaria, na Yeieli, na Shemiramothi, na Yehieli, na Matithiya, na Eliabu, na Benaya, na Obed-edomu, na Yeieli, wenye vinanda na vinubi; naye Asafu mwenye kupiga matoazi;
6 nao makuhani Benaya na Yahazieli wenye baragumu daima, mbele ya sanduku la agano la Mungu. 7 Ndipo siku hiyo Daudi alipoagiza kwanza kumshukuru Bwana, kwa mkono wa Asafu na nduguze.
8 Mshukuruni Bwana, liitieni jina lake; Wajulisheni watu matendo yake.
9 Mwimbieni, mwimbieni kwa zaburi; Zitafakarini ajabu zake zote.
10 Jisifuni kwa jina lake takatifu; Na ufurahi moyo wao wamtafutao Bwana.
11 Mtakeni Bwana na nguvu zake; Utafuteni uso wake siku zote.
12 Zikumbukeni ajabu zake alizozifanya; Miujiza yake na hukumu za kinywa chake;
13 Enyi wazao wa Israeli, mtumishi wake, Enyi wana wa Yakobo, wateule wake.
14 Yeye, Bwana, ndiye Mungu wetu; Duniani mwote mna hukumu zake.
15 Likumbukeni agano lake milele, Neno lile aliloviamuru vizazi elfu. 16 Agano alilofanya na Ibrahimu, Na uapo wake kwa Isaka;
17 Alilomthibitishia Yakobo kuwa amri, Na Israeli liwe agano la milele”
Umeona?..Kwahiyo Zaburi hazikutungwa tu pasipo sababu yoyote, bali zilitungwa kila baada ya tukio fulani la ki-Mungu lililotokea katika maisha ya Daudi. Zaburi zote 150, zilindikwa kwa msukumo wa Roho baada ya tukio fulani la ki-Mungu.
Zaburi nyingine Daudi aliziandika, baada ya kuokoka kimiujiza kwenye mikono ya Sauli aliyekuwa anatafuta kumuua, hivyo akaandika nyimbo hizo kumshukuru Mungu. Na sehemu kubwa ya Zaburi ya Daudi aliandika baada ya kupata ushindi dhidi ya Maadui zake (Yaani mataifa yaliyokuwa yanafanya vita dhidi ya Israeli)
Lakini pamoja na hayo nyimbo hizo za Zaburi, licha tu ni nyimbo katika mfumo wa maombi, shukrani, sifa n.k. kwa Mungu lakini pia zina unabii ndani yake.
Na unabii wa kwanza na Mkuu ziliobeba ni unabii wa kuja kwa Masihi, yaani Yesu Kristo, na unabii wa Wana wa Israeli kuchukuliwa mateka Babeli.
Zaburi 41:9 “Msiri wangu tena niliyemtumaini, Aliyekula chakula changu, Ameniinulia kisigino chake”. Linganisha na maneno ya Bwana Yesu katika Yohana 13:18
Yohana 13:18 “Sisemi habari za ninyi nyote; nawajua wale niliowachagua; lakini andiko lipate kutimizwa, Aliyekula chakula changu Ameniinulia kisigino chake”.
Zaburi 22:18 “Wanagawanya nguo zangu, Na vazi langu wanalipigia kura”…Linganisha na Mathayo 27:35
Hivyo kitabu hiki kwa sehemu kubwa kimebeba Ufunuo juu ya Yesu..Ndio maana Baada ya Yesu kufufuka alitaja kuwa yote aliyoandikiwa katika Zaburi na torati lazima yatimie..
Luka 24:44 “Kisha akawaambia, Hayo ndiyo maneno yangu niliyowaambia nilipokuwa nikali pamoja nanyi, ya kwamba ni lazima yatimizwe yote niliyoandikiwa katika Torati ya Musa, na katika Manabii na Zaburi”
Mbali na hayo, Kitabu cha Zaburi kinatufundisha Mambo yafuatayo.
Bwana akubariki.
Usikose mwendelezo wa vitabu vinavyofuata…
Maran atha!
Kwa maombezi/ Ushauri/ Ratiba za Ibada/Maswali/ Whatsapp/ Piga namba hizi: +255693036618/ +255789001312
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618.
Jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
Biblia inaziorodhesha bahari kuu nne, tuzisome;
1 ) Bahari ya shamu: Kwa sasa inajulikana kama bahari nyekundu, (Kwa kiingereza red sea). Hii ni ile bahari ambayo wana wa Israeli waliivuka baada ya Mungu kuipasua pale walipokuwa wanafuatiliwa na maadui zao, ambapo tunaona baadaye walikuja kumezwa na bahari ile.
Kutoka 15:22 “Musa akawaongoza Israeli waende mbele kutoka Bahari ya Shamu, nao wakatokea kwa jangwa la Shuri; wakaenda safari ya siku tatu jangwani wasione maji”.
2) Bahari kubwa , au bahari ya Wafilisti, (Kutoka 23:31): Kwasasa inajulikana kama habari ya Mediteranea. Ipo upande wa Magharibi wa taifa la Israeli. Hii ndio bahari kubwa kuliko zote zinazoorodheshwa kwenye biblia.
Hesabu 34:6 “Kisha mpaka wenu wa upande wa magharibi mtakuwa na bahari kubwa na mpaka wake; hii ndiyo mpaka wenu upande wa magharibi”.
Soma pia Yoshua 9:1, 15:47, 23:4, Ezekieli 47:19
3) Bahari ya Galilaya; Au kwa jina lingine Bahari ya Tiberia, au ziwa la Genesareti au Bahari ya Kinerethi Yoshua 12:3, 13:27, 34:11. Hii ndio ile bahari ambayo Bwana Yesu alitembea juu ya maji.
Luka 5:1 “Ikawa makutano walipomsonga wakilisikiliza neno la Mungu, yeye alikuwa amesimama kando ya ziwa la Genesareti,”
Mathayo 4:18 “Naye alipokuwa akitembea kando ya bahari ya Galilaya, aliona ndugu wawili, Simoni aitwaye Petro, na Andrea nduguye, wakitupa jarife baharini; kwa maana walikuwa wavuvi”.
4) Bahari ya chumvi: Hii ni habari ndogo sana, ambapo ipo chini ya mto Yordani, maji yake ni ya chumvi nyingi sana, jambo ambalo linaifanya bahari hiyo isiwe na kiumbe wa kuishi ndani yake kama samaki, sehemu nyingine wanaiita ‘bahari mfu’(Dead Sea)
Hesabu 34:3 “ndipo upande wenu wa kusini utakuwa tangu bara ya Sini kupita kando ya Edomu, na mpaka wenu wa kusini utakuwa tangu mwisho wa Bahari ya Chumvi kuelekea mashariki”;
Kumbukumbu 3:17, Yoshua 15:2.
Shalom, tazama maeneo mengine mbalimbali ya biblia chini.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618.
Jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
Maana ya Neno Sharoni ni “uwanda” au “nchi tambarare”. Katika biblia, tunaona lipo eneo (wilaya) lililojulikana sana na waisraeli kama Sharoni, japokuwa biblia haijatolea maelezo yake mengi, Lakini ni eneo lililokuwa na rubuta nyingi, na lilikuwa lipo karibu na fukwe za ile bahari kubwa(yaani bahari ya Mediterenia), tazama ramani.
Utalisoma Neno hilo kwenye vifungu hivi vya biblia;
1Nyakati 5:16 “Nao wakakaa huko Gileadi, katika Bashani, na katika miji yake, na katika viunga vyote vya Sharoni, hata kufika mipakani mwake”.
1Nyakati 27:29 “na juu ya makundi ya ng’ombe waliolishwa katika Sharoni alikuwa Shitrai, Msharoni; na juu ya makundi waliokuwamo mabondeni alikuwa Shafati mwana wa Adlai”;
Isaya 33:9 “Nchi inaomboleza, na kulegea; Lebanoni imetahayarika na kunyauka; Sharoni imekuwa kama jangwa; Bashani na Karmeli zimepukutika majani”.
Isaya 65:10 “Na Sharoni itakuwa zizi la makundi ya kondoo, na bonde la Akori mahali pa kulala makundi ya ng’ombe, kwa ajili ya watu wangu walionitafuta”.
Na katika agano jipya utalisoma katika kifungu hichi;
Matendo 9:35 “Na watu wote waliokaa Lida na Sharoni wakamwona, wakamgeukia Bwana”.
Lakini tukisoma kitabu cha wimbo ulio bora, tunaona, lipo Ua moja linatajwa kama Ua la Uwandani, au kwa jina lingine Ua la Sharoni (Rose of Sharon). Mwandishi wa kitabu hichi, anajifananisha yeye na Ua hilo ambalo limechipuka katika nchi hiyo ya Sharoni.
Wimbo 2:1 “Mimi ni ua la uwandani, Ni nyinyoro ya mabondeni.
2 Kama nyinyoro kati ya miiba, Kadhalika mpenzi wangu kati ya binti”.
Na bila shaka Ua hili ni Kristo, yeye ndiye aliyechipuka katika bonde la ulimwengu, na uzuri wake, na mwonekano wake ulikuwa ni tofauti na mwanadamu yoyote ulimwenguni. Yeye ndiye aliye Nuru ya ulimwengu, yeye ndiye aliyeiondoa harufu mbaya ya huu ulimwengu wa dhambi, hata tukapata kibali cha kumkaribia Mungu, yeye ndiye mwokozi wa ulimwengu.
Je! Na wewe umeliona Ua hilo?, Je umempata mwokozi moyoni mwako? Kumbuka hakuna njia nyingine yoyote utakayoweza kumfikia Mungu isipokuwa kwa njia yake yeye. Hakuna mwanadamu yoyote anayeweza kumpendeza Mungu kwa nguvu zake mwenyewe isipokuwa Yesu Kristo peke yake. Ukimkosa Kristo maishani mwako, haijalishi umepata ulimwengu mzima, hesabu kuwa umepoteza kila kitu. Lakini ukimpokea yeye, hata ukikosa vyote hesabu kuwa umevipata vyote.
Uamuzi ni wako, kumbuka hizi ni siku za mwisho, Lakini ikiwa leo utapenda kuyakabidhi maisha yako kwake, Huo utakuwa ni uamuzi wa busara sana, Basi fungua hapa kwa ajili ya maelekezo ya Toba>>> SALA YA TOBA
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618.
Jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
Rudi Nyumbani:
Ezekieli 44:1 “Kisha akanirudisha kwa njia ya lango lile la nje, la mahali patakatifu lililoelekea upande wa mashariki; nalo lilikuwa limefungwa.
2 Bwana akaniambia, Lango hili litafungwa, halitafunguliwa, wala mtu awaye yote hataingia kwa lango hili, kwa maana Bwana, Mungu wa Israeli, ameingia kwa hilo; basi kwa sababu hiyo litafungwa”.
Shalom,
Kwa jinsi tunavyozidi kuishi hapa duniani ndivyo dunia inavyozidi badilika kwa kasi sana mbele ya macho yetu, na haibadiliki kuelekea pazuri, bali inabadilika kuelekea pabaya..Inabadilika kuelekea kwenye maovu mengi zaidi…Maovu ya jana ni heri kuliko ya leo…Na hiyo ndiyo inayopelekea wokovu kuwa mgumu kupatikana mioyoni mwa watu siku baada ya siku.
Ukitazama mistari hiyo, ambayo iliandikwa katika agano lake, na nabii Ezekieli inazungumzia juu ya unabii wa Masihi siku atakapokuja na kuingia hekaluni kupitia lango la mashariki, unabii huo upo mwilini na rohoni, lakini lengo leo sio kuzungumzia habari hizo .. Nachotaka uone ni huyo ujumbe uliopo hapo, kwamba, hilo lango lipo wazi lakini siku moja litafungwa, na likishafungwa kamwe halitakaa lifunguliwe tena daima.. Huo ndio ujumbe, Na wote tunajua kuwa lango hilo ni Neema ya wokovu.
Sasa tukirudi kipindi cha agano jipya, tunaona tena Yesu akilitaja lango hilo, lakini safari hii yeye halitaji tena kama “Lango”Kana kwamba ni kubwa sana.. bali analitaja kama mlango, na tena sio mlango tu, bali ni mlango mwembamba sana..tusome..
Luka 13:24 “Jitahidini kuingia katika mlango ulio mwembamba, kwa maana nawaambia ya kwamba wengi watataka kuingia, wasiweze
25 Wakati mwenye nyumba atakaposimama na kuufunga mlango,…..”.
Unaona? Sasa utajiuliza ni nini kimetokea mpaka sio lango tena bali ni mlango?
Ni kwasababu majira yanabadilika, Mlango wa mbinguni tangu zamani, Mungu aliukusudia uwe mpana ili watu wote waingie na ndivyo ulivyo, alikusudia uwe mwepesi kwa watu wote na mataifa yote kuuingia, ni LANGO pana sana. Hilo ndio lengo la Mungu hata sasa, Mungu hawezi kumminya mtu kwa makusudi kwamba akipate kile kitu kwa shida, sasa atufanyie hivyo ili iweje?.
Lakini kutokana na maovu na mambo mengi yaliyopo ulimwenguni sasa imepelekea mlango huu kuwa mwembamba sana, na hyo ni kutokana na kuzuka kwa milango mingine mingi sana ya upotevuni, na watu wamekuwa wakiiangalia kwa hiyo, na kusahau lile lango moja tu la Mungu.
Ndugu yangu, hizi ni nyakati mbaya sana tunazoishi, leo utaudharau wokovu wa Yesu Kristo, lakini alishatabiri kuwa kuna siku ataufunga mlango huu, na siku hiyo utakapofungwa ndipo watu watakapogundua kuwa walikuwa wanapuuzia kitu cha msingi sana, cha uzima wa roho zao.. Ndipo watakapoanza kubisha wafunguliwe, kumbe hawakujua kuwa lango hilo likishafungwa mara moja, halitafunguliwa tena daima. Kitakachofuata baada ya hapo ni matujo makubwa sana ambayo hayajawahi kutokea duniani kote.
Luka 13:24 “Jitahidini kuingia katika mlango ulio mwembamba, kwa maana nawaambia ya kwamba wengi watataka kuingia, wasiweze.
25 Wakati mwenye nyumba atakaposimama na kuufunga mlango, nanyi mkaanza kusimama nje na kuubisha mlango, mkisema, Ee Bwana, tufungulie; yeye atajibu na kuwaambia, Siwajui mtokako;
26 ndipo mtakapoanza kusema, Tulikula na kunywa mbele yako, nawe ulifundisha katika njia zetu.
27 Naye atasema, Nawaambia, Siwajui mtokako; ondokeni kwangu ninyi nyote mlio wafanyaji wa udhalimu.
28 Ndipo kutakapokuwa na kilio na kusaga meno, mtakapomwona Ibrahimu na Isaka na Yakobo na manabii wote katika ufalme wa Mungu, nanyi wenyewe mmetupwa nje.
29 Nao watakuja watu toka mashariki na magharibi, na toka kaskazini na kusini, nao wataketi chakulani katika ufalme wa Mungu.”
Hivyo wokovu sio wa kukwepwa, injili si ya kudharauliwa wala kupuuziwa kabisa, huu si wakati wa kumwangalia jirani, au ndugu, au mzazi, katika suala lako la wokovu, Ni wakati wa kumkimbilia Kristo na kumwangalia yeye tu, kwasababu muda uliobakia ni mchache, nani ajuaye lango hilo litafungwa leo usiku, au kesho asubuhi. Jiulize Unyakuo ukipita leo halafu ukabaki, na injili zote hizo ulizosikia, na mafundisho yote hayo uliyofundishwa na kujifunza, utaenda kujibu nini mbele ya kiti cha hukumu.
Usikubali kusongwa na jambo lolote, huu mlango umeshakuwa finyu sana. Kuiingia sio mrahisi tena kama tunavyodhani, hivyo ni wakati wa kufanya maamuzi magumu, wa kukubali kujitwika msalaba na kumfuata Yesu, na uwe tayari kwenda kubatizwa na kupokea Mtakatifu.
Bwana akubariki sana.
Ikiwa bado hujabatizwa, na utapenda kupata huduma hiyo ya ubatizo, au kumpa Kristo maisha yako, basi wasiliana nasi inbox au kwa namba hizi +255789001312 / 0693036618.
Jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
Biblia inamaana gani kusema;aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi?
Mlango uitwao “Mzuri” Unaozungumziwa katika Matendo 3:2 ndio upi?
Bisi ni nini?
Kama wengi tunavyofahamu bisi kwa mazingira yetu ni yale mahindi yanayokaangwa na kufutuka na pale yanapobadilika na kuwa na mwonekano mwingine (mweupe mweupe ) huliwa. Kwa wengine wamezoea kuyaita Popcorn lugha ya kigheni. Tazama picha kushoto.
Lakini kwa wayahudi, na jamii nyingi za watu wa mashariki ya kati, bisi zao haziwi kama hizi zetu za mahindi bali zao zinakuwa za ngano, na zinakaangwa vile vile kama zinavyokaangwa za mahindi isipokuwa tu mwonekano wake haubadilika sana, kama ulivyo wa mahindi.
Kuona jinsi inavyoandaliwa na mwonekano wake, tazama video hii >>>
https://www.youtube.com/watch?v=5fSY4YCVSoM
Hivyo mahali popote unapokutana na neno hili Bisi kwenye biblia basi ujue ni hii inayotengenezwa kwa ngano, na sio mahindi.
Kwamfano ukisoma biblia, utaona, Mungu anawapa wana wa Israeli maagizo kuwa pindi watakapovuna mavuno yao ya kwanza, wasile kwanza chochote katika walichokivuna, ikiwemo bisi, au masuke, mpaka watakapoleta kwanza kile kinachomstahili Mungu.
Walawi 23:14 “Nanyi msile mkate, wala bisi, wala masuke machanga, hata siku iyo hiyo, hata mtakapokuwa mmekwisha kuleta sadaka ya Mungu wenu; hii ni amri ya milele katika vizazi vyenu katika makao yenu yote”.
Utalisoma Neno hilo tena katika vifungu hivi;
Ruthu 2:14 “Tena wakati wa chakula huyo Boazi akamwambia, Karibu kwetu, ule katika mkate wetu, na ulichovye tonge lako katika siki yetu. Basi akaketi pamoja na wavunaji, nao wakampitishia bisi, naye akala akashiba, hata akasaza”.
1Samweli 17:17 “Ndipo Yese akamwambia Daudi mwanawe, Haya! Sasa uwachukulie ndugu zako efa ya bisi, na mikate hii kumi, ipeleke upesi kambini kwa ndugu zako;
18 ukampelekee akida wa elfu yao jibini hizi kumi, ukawaangalie, wa hali gani, kisha uniletee jawabu yao.
1Samweli 25:18 “Ndipo Abigaili akafanya haraka, akatwaa mikate mia mbili, na viriba viwili vya divai, na kondoo watano waliofanyizwa tayari, na vipimo vitano vya bisi, na vishada mia vya zabibu, na mikate ya tini mia mbili; akavipakia vitu hivi juu ya punda.
19 Akawaambia vijana wake, Haya! Tangulieni mbele yangu; angalieni, mimi nawafuata. Ila hakumwambia mumewe, Nabali.
Yoshua 5:10 “Basi wana wa Israeli wakapanga hema zao huko Gilgali; nao wakala sikukuu ya pasaka siku ya kumi na nne ya mwezi, jioni, katika nchi tambarare za Yeriko.
11 Nao wakala katika mazao ya nchi siku ya pili ya kuiandama hiyo sikukuu ya pasaka, mikate isiyotiwa chachu, na bisi, siku iyo hiyo”.
Soma pia, 2Samweli 17:28,
Je! Tunapaswa tukumbuke nini, kila tunapolisoma hili Neno?
Ni kwamba hata sisi, kwa kila Mungu anachotubariki, tusifikirie kula kwanza, mpaka tutakapohakikisha fungu la Mungu tumelitenga na kulitoa. Biblia imetumia neno bisi, kwasababu ni chakula chepesi sana kukipika, ni kitendo cha kuweka kwenye sufuria na kukikaanga na kula, jambo ambalo halihitaji maandalizi mengi kuandaa, tofauti na vyakula vingine vya ngano, hii ikiwa na maana kuwa mtu anaweza kuvuna shamba lake, na hapo hapo akaenda kuchukua ngano hiyo na kukaanga mara moja na kula. Lakini hata hivyo Mungu kakataza. .. Hivyo na sisi, hatupaswi kufikiria kutumia hata kwa vocha au kwa chipsi kile Mungu anachotubariki, kabla hatujalitenga fungu lake pembeni.
Hivyo ndio Mungu atakavyotubariki.
Shalom.
Tazama maana ya maneno mengine ya biblia chini.
Pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618.
Jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
“Jaa” ni nini katika biblia?
Jaa ni mahali ambapo uchafu unalundikwa, na uchafu huo unaweza kuwa ni kinyesi cha wanyama (yaani mbolea), au uchafu unaotokana na shughuli za kibinadamu (matakataka). Hivyo Jaa ni kama kifupi cha jalala tu.
Katika biblia tunaona neno hili likitumika..
Zaburi 133: 7 “Humwinua mnyonge kutoka mavumbini, Na kumpandisha maskini kutoka jaani”.
Maana yake Bwana anaweza kumpandisha mtu kutoka majalalani na kumpandisha juu.
Ezra 6: 11 “Pia nimetoa amri kwamba, mtu awaye yote atakayelibadili neno hili, boriti na itolewe katika nyumba yake, akainuliwe na kutungikwa juu yake; tena nyumba yake ikafanywe jaa kwa ajili ya neno hili”.
Isaya 25: 10 “Kwa maana mkono wa Bwana utatulia katika mlima huu, na Moabu atakanyagwa chini huko aliko, kama vile majani makavu yakanyagwavyo katika MAJI YA JAA”
Pia unaweza kusoma Danieli 2:5, Danieli 3:39, Maombolezo 4:5 na 1Samweli 2:8.
Katika Agano jipya neno hili limetumika mara moja tu, na Bwana Yesu Kristo katika kitabu cha Luka..
Tusome..
Luka 14:34 “Chumvi ni kitu chema; lakini chumvi ikiwa imeharibika, itiwe nini ikolee?
35 Haiifai nchi WALA JAA; watu huitupa nje. Mwenye masikio ya kusikilia, na asikie”
Kinyesi cha wanyama kikizidi kuharibika kinafaa katika mbolea, watu wanakikusanya na kukifunya mbolea baadaye, hali kadhalika takatata nyingine zote zinavyozidi kuharibika huwa hazikosi matumizi, zinaweza hata kutumika katika kuzalishe gasi ya asili, ambayo itatumika kama nishati..
Lakini chumvi ni kitu cha ajabu, ikishaharibika huwezi kuitumia kwa matumizi yoyote yale, huwezi kuitumia kwenye chakula, wala huwezi kuitumia kama mbolea, wala huwezi kuilundika pamoja na kutengeneza jalala na kuzalisha gesi, …Kwaufupi inakuwa kama mchanga tu..
Sasa Bwana Yesu alitufananisha sisi, tuliompokea yeye na chumvi..
Mathayo 5:13 “Ninyi ni chumvi ya dunia; lakini chumvi ikiwa imeharibika itatiwa nini hata ikolee? Haifai tena kabisa, ila kutupwa nje na kukanyagwa na watu.
14 Ninyi ni nuru ya ulimwengu. Mji hauwezi kusitirika ukiwa juu ya mlima”.
Umeona? Bwana anatuonya, tujihadhari tunavyoenenda katika hii dunia, matendo yetu yasije yakatuharibia sifa zetu moja kwa moja, hata tusifae tena mbele za Mungu na wanadamu.
Kwa urefu juu ya somo hili la chumvi fungua hapa >> NYINYI NI CHUMVI
Je umempokea Yesu?..Kama bado, Kristo yupo mlangoni kurudi kulinyakua kanisa lake, biblia inasema atakuja kama mwivi usiku wa manane, maana yake ni hii, wakati watu na ulimwengu unahisi bado sana, kumbe huo ndio wakati wa kurudi Kristo kulichukua kanisa lake,
Swali ni je!..Bwana Yesu akija leo, una uhakika wa kwenda naye mawinguni?. Kama huna uhakika basi huo ni uthibitisho kwamba hutaenda naye atakapokuja. Hivyo tubu leo kwa dhati na amua kuanza maisha mapya na Kristo, naye atakupokea na kukupa kipawa cha Roho wake Mtakatifu.
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618.
Jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
Shalom, Jina la Bwana Yesu libarikiwe, karibu tuyatafakari maandiko pamoja..
Ukifika mahali umepotea, na huoni mtu hata mmoja mbele yako wa kukupa msaada, lakini unapotazama chini, unaona nyayo za miguu zinaelekea upande fulani..bila shaka hatua inayofuata ni kuzifuata hizo nyayo, kwasababu unajua mwisho wa hizo nyayo ni kumfikia huyo mtu alipo.
Na Kristo sasa hayupo hapa duniani kwa namna ya mwili, yupo juu mbinguni..lakini katuachia nyayo…ambazo katika hizo tukizifuata tutamfikia yeye na kumwona macho kwa macho.
Sasa nyanyo hizo ni zipi?
Neno la Mungu linasema..
1Petro 2:20 “Kwa maana ni sifa gani kustahimili, mtendapo dhambi na kupigwa makofi? Lakini kustahimili, mtendapo mema na kupata mateso, huu ndio wema hasa mbele za Mungu.
21 Kwa sababu ndio mlioitiwa; maana Kristo naye aliteswa kwa ajili yenu, AKAWAACHIA KIELELEZO, MFUATE NYAYO ZAKE.
22 Yeye hakutenda dhambi, wala hila haikuonekana kinywani mwake.
23 YEYE ALIPOTUKANWA, HAKURUDISHA MATUKANO; alipoteswa, hakuogofya; bali alijikabidhi kwake yeye ahukumuye kwa haki”.
Tunapokuwa wapole kama Yesu alivyokuwa hapo tunaziendea nyayo zake, katika hii dunia iliyojaa upotofu, tunapostahimili mabaya, tunapotukanwa haturudishi majibu kama yeye, tunapoudhiwa ni lazima tusamehe..hapo tunazifuata nyanyo zake..na tutakapomaliza mwendo tukiwa tumezifuata nyayo hizo ni lazima tutamfikia hatutapotea.
Lakini sasa kuna nyayo nyingi duniani, kila mtu anatengeneza nyayo zake…mfano wa nyayo potofu ni hizi zinazosema… “mpende akupendaye, asiyekupenda mchukie”.. Hizi ni nyayo ambazo zinaonekana ni za faraja na za kujilinda, lakini ni nyayo potofu, mwisho wake ni upotevuni…Mwisho wake ni ziwa la moto.
Hivyo tusijifanye tunajua kumsahihisha Bwana Yesu Kristo na kufikiri, hakupaswa kuwa mpole vile… Siku zote fahamu kuwa Yesu alikuwa na uwezo wa kuwapoteza maadui zake pale kwa dakika moja tu, wala hakuna mtu ambaye angeweza kumgusa. Lakini hakuutumia huo uwezo kwasababu lengo lake ni hao watu watubu kwa wema wake..
Ndicho kitu Yesu anachotaka kwetu pia, kwamba kwa wema wetu, wengi wavutwe kwake…Lakini kama tukijiona kwamba sisi tuna ufunuo kuliko yeye, kwamba hatupaswi kuwa wapole, na wanyenyekevu, hatupaswi kuwa watu wa kusamehe wanaotuudhi, hizo njia tunazoziendea tutajikuta kwenye ziwa la moto.
Mathayo 26:51 “Na tazama, mmoja wao waliokuwa pamoja na Yesu akanyosha mkono wake, akaufuta upanga wake, akampiga mtumwa wa Kuhani Mkuu, akamkata sikio.
52 Ndipo Yesu akamwambia, Rudisha upanga wako mahali pake, maana wote waushikao upanga, wataangamia kwa upanga.
53 Ama wadhani ya kuwa mimi siwezi kumsihi Baba yangu, naye ataniletea sasa hivi zaidi ya majeshi kumi na mawili ya malaika?”
Soma tena..
Luka 9:52 “akatuma wajumbe kutangulia mbele ya uso wake; wakaenda wakaingia katika kijiji cha Wasamaria, ili kumtengenezea mahali.
53 Lakini wenyeji hawakumkaribisha kwa vile alivyouelekeza uso wake kwenda Yerusalemu.
54 Wanafunzi wake Yakobo na Yohana walipoona hayo, walisema, Bwana, wataka tuagize moto ushuke kutoka mbinguni, uwaangamize; [kama Eliya naye alivyofanya]?
55 Akawageukia, akawakanya. [Akasema, Hamjui ni roho ya namna gani mliyo nayo.]
56 Kwa maana Mwana wa Adamu hakuja kuziangamiza roho za watu, bali kuziokoa. Wakaondoka wakaenda mpaka kijiji kingine”.
Bwana atupe macho ya kuona nyayo zake, na kuzifuatia katika Jina la Yesu.
Maran atha.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618.
Jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
kwanini yule kijana aliitupa ile nguo ya kitani chini na kukimbia uchi?