Title Devis

NA BAADA YA LILE TONGE, SHETANI AKAMWINGIA.

Shalom, leo tutajifunza madhara ambayo tunaweza kuyapata pale tunapoukataa  ule upendo wa mwisho kabisa wa Yesu Kristo.

Yuda alikuwa ni mtume wa Yesu, lakini kama tunavyojua habari yake, alikuwa mwizi, na pia hakuwa na upendo  wa dhati kwa Bwana.. Tunaona katika biblia hali hiyo ya uasi aliendelea nayo kwa muda mrefu sana, lakini katika kipindi hicho chote haikuleta madhara yoyote katika maisha yake, aliendelea kutembea na Yesu, aliendelea kushiriki baraka zote za Yesu kama mmojawapo wa mitume wengine..

Mpaka anafikia hatua ya kwenda kupatana na wakuu wa makuhani ili kumsaliti Yesu bado,  nafasi alikuwa nayo ya kuahirisha mawazo yake, uwezo huo alikuwa nao, isitoshe alikuwa anaona Yesu akimpa viashiria vingi kuwa anavyovifanya anaweza kuviahirisha, lakini hilo halikumwingia moyoni mwake. Mpaka siku ile walipokuwa wameketi chakulani jioni na Yesu akaanza kuwatawadha miguu, kuonyesha upendo wake kwao, akamtawadha na Yuda miguu yake, huku Yuda akiyatazama macho ya Emanueli yenye upole, yasiyo na kosa lolote, akisikia kabisa rohoni anashuhudiwa kuwa anachojaribu kukifanya sicho sawa..aghahiri mawazo yake, haoni mpaka Bwana wake amekuja kumuosha miguu yake, kumthibitishia kuwa miguu yake haitakiwi kuwa myepesi kukimbilia maovu.. Lakini hilo halikuwa kitu kwa Yuda.

Mpaka dakika ya mwisho kabisa tuona Kristo anaonyesha Upendo wake wa mwisho, wa kuchukua chakula chake cha heshima na kumgawia Yuda peke yake, kama heshima ya kipekee, tusome;

Yohana 13:21 “Naye alipokwisha kusema hayo, Yesu alifadhaika rohoni, akashuhudia akisema, Amin, amin, nawaambieni, Mmoja wenu atanisaliti.

22 Wanafunzi wakatazamana, huku wakiona shaka ni nani amtajaye.

23 Na palikuwapo mmoja wa wanafunzi wake, ameegama kifuani pa Yesu, ambaye Yesu alimpenda.

24 Basi Simoni Petro akampungia mkono, akamwambia, Uliza, ni nani amtajaye?

25 Basi yeye, hali akimwelekea Yesu kifua chake, akamwambia, Bwana, ni nani?

26 Basi Yesu akajibu, Ndiye mtu yule nitakayemtowelea tonge na kumpa. Akatowelea tonge, akalitwaa akampa Yuda, mwana wa Simoni Iskariote.

27 NA BAADA YA HILO TONGE SHETANI ALIMWINGIA. Basi Yesu akamwambia, Uyatendayo yatende upesi.

28 Wala hakuna mtu katika wale walioketi chakulani aliyeijua sababu ya kumwambia hivyo.

29 Kwa maana wengine walidhania, kwa kuwa Yuda huchukua mfuko, ya kwamba Yesu alimwambia kama, Nunua mnavyovihitaji kwa sikukuu; au kwamba awape maskini kitu.

30 Basi huyo, akiisha kulipokea lile tonge, akatoka mara hiyo. Nako kulikuwa ni usiku”.

Sasa Tonge sio ule mkate wa Pasaka, au sio ule mkate aliowapa wanafunzi wake kama mwili wake waule siku ile, hapana, Tonge ni chakula cha heshima kilichokuwa kinaandaliwa na wayahudi zamani, ambacho   kinaweza kikawa na mkate au kitu kingine, lakini sana sana kilitumika mkate, ambacho hicho mtu alikuwa anampa Yule mtu anayemuheshimu sana, au wa muhimu kwake, ili kuinyesha thamani yake.  Hivyo aliyeuandaa aliuchua mkate huo na kuuchovya katika mboga iliyoandaliwa pamoja na huyo mtu aliyemwandalia.

Utaliona Hilo katika kipindi cha Ruthu, alivyoitwa na Boazi kwake..

Ruthu 2:14 “Tena wakati wa chakula huyo Boazi akamwambia, Karibu kwetu, ule katika mkate wetu, na ulichovye tonge lako katika siki yetu. Basi akaketi pamoja na wavunaji, nao wakampitishia bisi, naye akala akashiba, hata akasaza”.

Soma pia Ayubu 31:16, na Mithali 23:6, utaliona neno hilo.

Sasa alichokifanya Bwana ndicho hichi, kumpa Yuda heshima ya kipekee, wa kuchovya donge lake pamoja naye,. Kuonyesha upendo wake wa kipekee kwake.

Lakini mara baada ya kula tu, angali moyo wake bado hujaiacha nia ya kumsaliti   biblia inatuambia shetani akamwingia saa hiyo hiyo …Akawa amefikia “point of no return”. Hii Ikiwa na maana kuwa sasa shetani anayo nafasi ya kumchukua huyu mtu asilimia 100, anaweza kumwendesha kwa jinsi anavyotaka, (amepata hati miliki maalumu) na ndio hapo utaona akawaendea wale makuhani na kuwapa mikakati yote ya kumkamata Yesu. Na Mwisho wa siku yeye mwenyewe akajiua, kwasababu tayari alikuwa ameshavaliwa na pepo mkuu mwenyewe ibilisi.

Na sisi vivyo hivyo, Kristo anapotuonyesha upendo wake kwetu, na hatuoni jambo lolote baya likitokea kwenye maisha yetu pale tunapofanya dhambi kwa makusudi, pengine unazini na upo kanisani, na huoni jambo lolote baya likikutokea, na saa nyingine unamwomba Yesu akutendee jambo Fulani na anakutendea, na wewe unadhani itaendelea hivyo hivyo kila siku..

Upo wakati atakuonyesha upendo mkubwa zaidi ya huo, (atakumegea Tonge lake) na kama usipojua nini maana ya Upendo huo kwamba  anakutaka wewe utubu, wewe ukadhani anafurahishwa na unachokifanya, na ndio maana kukubariki, ujue tayari mwisho wako umefika. Ibilisi anakuingia na hapo ndipo unapokuwa mwisho wako.

Hivyo tusipumbazwe na rehema za Kristo. Tukiona hatuadhibiwi kwa makosa yetu, tuogope kwasababu utafika wakati tutakabidhiwa shetani moja kwa moja.

Bwana akubariki.

Hizi ni nyakati za mwisho Je! Umeokoka? Je! Umepokea Roho Mtakatifu. Kumbuka Yesu ndio mwokozi wa ulimwengu. NA HUO NDIO UKWELI PEKEE ULIODUMU DUNIANI KWA WAKATI WOTE.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618.

Jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

BIRIKA LA SILOAMU.

Sikukuu ya kutabaruku ni ipi?

KWANINI NI YESU KRISTO WA NAZARETI?

CHAPA YA MNYAMA

MTUMWA SI MKUU KULIKO BWANA WAKE.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Pesa za bindoni ni nini?(Marko 6:8)

Bwana Yesu aliposema pesa za bindoni alimaanisha pesa za mfukoni.. mfuko unaozungumziwa ni ule wa kuvaa kiunononi ambayo ndio ilitumika zamani. tazama picha.

Marko 6:7 “Akawaita wale Thenashara, akaanza kuwatuma wawili wawili, akawapa amri juu ya pepo wachafu;

8 akawakataza wasichukue kitu cha njiani isipokuwa fimbo tu; wala mkate, wala mkoba, wala pesa za bindoni”;

Ni kwanini Bwana Yesu alisema hivyo?

Ieleweke kuwa Bwana Yesu hakumaanisha kuwa injili haihitaji fedha, wala mahitaji hapana, injili inahitaji fedha, tena sana ili isonge mbele.…Lakini hapo alikuwa halengi kazi ya injili   bali  aliwalenga wale wapeleka injili. Kwamba hao ndio wanapaswa wasifikiri kuwa inahitajika maandalizi mengi au makubwa ili wao wamtumikie Mungu.

Bwana aliwatuma wao kama wao, na mambo mengine yote aliwapa huko mbele ya safari. Na ndio maana sehemu nyingine aliwauliza hapo nilipowatuma hamna kitu  Je!  Mlipungukiwa na chochote? Wakasema hapana.

Luka 22:35 “Akawauliza, Je! Hapo nilipowatuma hamna mfuko, wala mkoba, wala viatu, mlipungukiwa na kitu? Wakasema, La!

Hiyo ni kuonyesha kuwa mahitaji ya muhimu aliwapatia. Huko walipoenda.  Hata na sisi, tunapaswa tujue kuwa tunapotaka kumtumikia Mungu tusifikirie sana hali zetu, labda tutaanzia wapi,au  tuna nini, au hatuna nini, hilo wazi tuliondoe, Ni kweli wazo hilo ni gumu kulipokea lakini ndio maagizo ya Bwana.. tunapaswa tuyaamini, na kwamba yeye mwenyewe atatupatia.

Shalom.

Jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

Fitina maana yake nini kwenye biblia?

Kijicho ni nini? (Marko 7:22)

MZAZI, JALI MAISHA YA KIROHO YA MTOTO WAKO.

Kwanini wale dubu waliowauwa vijana wa Elisha walikuwa wa kike?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Fitina maana yake nini kwenye biblia?

Fitina ni nini?

Katika biblia Fitina maana yake ni “kufanya mageuzi au mapinduzi”. Mtu ambaye anataka kufanya mapinduzi labda ya kimamlaka, kutokana na kwamba labda hakubaliani na serikali yake, au mamlaka yake, na hivyo akakusanya watu kadhaa na kutafuta kuiangusha serikali, kwa lugha ya kibiblia mtu huyo anafanya fitina.

Katika biblia (Agano la kale) tunaona mifano ya watu kadhaa waliofanya fitina katika biblia..

  • SHALUMU:

Huyu Shalumu, alimng’oa  Mfalme Zekaria kwenye kiti chake kwa hila, na yeye akatawala mahali pake

2Wafalme 15: 10 “Na Shalumu mwana wa Yabeshi akafanya fitina juu yake, akampiga mbele ya watu, akamwua, akatawala mahali pake……

15 Basi mambo yote ya Shalumu yaliyosalia, na fitina aliyoifanya, tazama, yameandikwa katika kitabu-chatarehe cha wafalme wa Israeli.”.

  • HOSHEA:

Huyu naye alimng’oa madarakani mfalme Peka wa Israeli kwa kumuua na kutawala mahali pake.

2Wafalme 15:30 “Na Hoshea mwana wa Ela akafanya fitina juu ya Peka mwana wa Remalia, akampiga, akamwua, akatawala mahali pake, katika mwaka wa ishirini wa Yothamu mwana wa Uzia.”

Na wengine wengi ambao unaweza kuwasoma katika mistari hii..(2Wafalme 17:4, 2Wafalme 21:23, 2Nyakati 13:6)

Katika agano jipya pia tunaona mifano ya baadhi ya watu waliofanya fitina.

  • BARABA:

Huyu Baraba, alipanga kunyanyuka kinyume na mamlaka iliyokuwa inatawala, akataka kufanya mapinduzi…Na pia aliua watu kadhaa katika harakati zake hizo za mapinduzi..

Luka 23: 18  “Wakapiga kelele wote pamoja, wakisema, Mwondoe huyu, utufungulie Baraba.

19  Naye ni mtu aliyetupwa gerezani kwa ajili ya FITINA iliyotokea mjini, na kwa uuaji”

Na katika kanisa la Kristo pia kuna fitina za shetani.

Fitina ndani ya kanisa la Kristo ipoje?..Ni pale mtu anapotaka KULIPINDUA NENO LA MUNGU, na kulisimamisha lake.

Warumi 16:17  “Ndugu zangu, nawasihi, waangalieni wale WAFANYAO FITINA na mambo ya kukwaza kinyume cha mafundisho mliyojifunza; mkajiepushe nao.

18  Kwa sababu walio hivyo hawamtumikii Bwana wetu Kristo, bali matumbo yao wenyewe; na kwa maneno laini na ya kujipendekeza waidanganya mioyo ya watu wanyofu”.

Asilimia kubwa ya watu WANAOLIPINDUA NENO LA MUNGU, na kulisimamisha lao, ni ili tu wapate faida Fulani, labda fedha, ndio biblia inasema hapo, watu wa namna hiyo hawamtumikii Kristo bali matumbo yao. Hawa wanaweza kuupindua Uponyaji wa Yesu uliopo katika JINA LAKE, na kulazimisha uwe katika Maji, au mafuta..lengo lao wala si kwasababu wana huruma sana, lengo lao ni ili wauze hayo maji na mafuta mengi wapate pesa, ndio maana yanawekwa kwa kiwango kidogo lakini bei kubwa.

Tumeonywa tujihadhari nao.. tusichukuliwe na fitina zao.

Hali kadhalika wapo wahubiri wanaomfitini Kristo, na kutafuta kuchukua nafasi yake, ili waabudiwe au waonekane ni miungu-watu, hawa nao pia tumeonywa tujiepushe nao.

Je umeokoka?. Kama bado unasubiri nini tubu leo na kumpokea Kristo, unyakuo upo karibu

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

Nini tofauti kati ya Husuda, faraka na uchafu?

Hazama ni nini katika biblia?(Ezekieli 16:12, Kutoka 24:47)

MATUNDA 9 YA ROHO MTAKATIFU

RUDI KUMPA MUNGU UTUKUFU.

KITABU CHA UZIMA

KITABU CHA UCHAWI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 9 (Kitabu cha Ayubu).

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe, karibu katika uchambuzi wa vitabu vya biblia, tumekwisha jifunza vitabu kadhaa vya mwanzo, kama utakuwa hujavipitia na ungependa kufanya hivyo, basi unaweza kufungua hapa>> VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1

Na leo tutazidi kusonga mbele, kwa kutazama kitabu kimoja Zaidi ambacho ni kitabu cha Ayubu.

KITABU CHA AYUBU.

Kitabu cha Ayubu ndio kitabu kikongwe kuliko vitabu vyote vya biblia, Kitabu hichi kiliandikwa kabla ya kuandikwa kitabu cha Mwanzo. Kitabu cha Mwanzo kiliandikwa na Nabii Musa, kadhalika na kitabu hichi cha Ayubu, ni nabii Musa huyo huyo ndiye aliyekiandika.

Nabii Musa alikiandika kwanza kitabu hichi kisha ndio vikafuata vitabu vingine vingine vya torati kama kitabu cha Mwanzo, kutoka n.k.. Sasa sio kwamba Musa alikuwepo wakati Ayubu anaishi duniani na akawa ananakili Maisha aliyokuwa anayapitia hapana!.. Ayubu aliishi miaka mingi sana kabla ya Nabii Musa kutokea, na mambo yote Ayubu aliyoyapitia yalinakiliwa na Ayubu mwenyewe Pamoja na watu waliomzunguka Ayubu (maana yake marafiki zake na ndugu zake). Hivyo hata baada ya kufa Ayubu, historia ya Maisha yake iliendelea kuwepo, lakini haikuwepo katika mpangilio bora,  Sasa Musa alipokuja kutokea miaka mingi baadaye, kwa uongozo wa kiMungu alikusanya Pamoja taarifa zote za Ayubu kwa usahihi na kuziweka kwenye mfumo wa kitabu, ndio kikatokea hicho kitabu cha Ayubu tunachokisoma leo katika biblia.

Kitabu cha Ayubu kinaanza na Historia ya Ayubu mwenyewe mahali alipozaliwa na uelekevu wake kwa Mungu. Ayubu alizaliwa katika nchi ya “Usi”. Nchi ya Usi kwasasa ni maeneo ya kusini mwa nchi ya YORDANI. (kufahamu nchi ya Yordani ilipo, unaweza kutazama ramani).

Ayubu aliishi kabla ya Ibrahimu, hivyo hakuwa Mwisraeli. Lakini alimjua Mungu wa kweli wa mbingu na nchi na alimcha yeye, kutoka kwa mababu zake (akina Nuhu)

Kitabu cha Ayubu kimegawanyika katika Sehemu kuu 4.

  • Sehemu ya kwanza (1) ni kuanzia Mlango wa kwanza hadi ule Mlango wa pili (Sehemu hii inaelezea wasifu wa Ayubu  na  majaribu aliyoyapitia)
  • Sehemu ya Pili(2) ni kuanzia mlango wa 3 hadi mlango wa 38, ni (Sehemu hii inaelezea majibizano ya Ayubu na Rafiki zake watatu)..
  • Sehemu ya tatu (3) ambayo ni ule mlango wa 39 hadi 41, Bwana anaingilia kati majibizano yao na kuyakatisha..
  • Na sehemu ya nne(4) na ya mwisho ambayo ni ule mlango wa 42 Mungu anapitisha hukumu kwa Ayubu na wale marafiki zake watatu kwa mazungumzo yao.

Tukianza na sehemu ya kwanza:

Sehemu hii ni ile milango miwili ya mwanzo, na ndio milango iliyo mirahisi kuieleweka kuliko milango mingine yote inayofuata. Hapa inaelezea Ayubu jinsi alivyokuwa Mkamilifu na mwelekevu mbele za Mungu, kwamba alikuwa ni mcha Mungu na ni mtu aliyejiepusha sana na uovu.

Lakini pia katika Sura hizi mbili za Mwanzo ndizo Sura pekee katika biblia nzima zilizotupa, taswira kamili ya kinachoendelea katika katika mamlaka yaliyopo juu yetu sisi wanadamu. Sura hizi ndizo zimetufumbua macho na kuelewa kuwa kumbe wakati sisi tunaendelea na Maisha yetu, kuna mmoja anatushitaki mbele za Mungu, na ndiye sababu ya majaribu yetu yote tunayoyapitia. Ni ukurasa mmoja tu katika biblia lakini umekuwa muhimu sana kwetu. Inaeleza jinsi sababu ya mwenye haki wakati mwingine kupitia majaribu. Sasa ili kujua kwa urefu ni kwa namna gani mashitaka hayo yanaendelea juu mbinguni dhidi yetu, unaweza kufungua hapa na kusoma upatapo nafasi >>> JINSI SHETANI ANAVYOZUIA MAJIBU YA MAOMBI YETU.  Kwasasa hatutaingia sana huko.

Sehemu ya Pili: 

Sehemu hii ni kuanzia ule mlango wa 3 hadi wa 38, Sehemu hii ni imeelezea majibizano kati ya Ayubu na Rafiki zake watatu, walioitwa ELIFAZI, BILDADI, na SOFARI.

Marafiki hawa walikuwa ni marafiki wa Ayubu wa kitambo kirefu, na walikuwa wamejaa hekima ya ki-Mungu ndani yao. Na waliposikia Rafiki yao kapatwa na majanga yale, na misiba ile walitoka huko walipokuwepo kuja kumliwaza na kumshauri.

Rafiki zake hawa walikuja na Mashauri yao, lakini hawakujua kuwa Mashauri yao hayakuwa yaliyonyooka mbele za Mungu. Wenyewe katika akili zao waliamini asilimia mia moja kwamba Ayubu kuna mahali atakuwa alimkosea Mungu ndio maana akapatwa na majanga yale, walitumia mitazamo yao tu, hawakujua kuhusu vita vilivyokuwa vinaendelea mbinguni. Hivyo walikuja kwa nia moja tu, KUMWAMBIA AYUBU ATUBU!!, Atubie dhambi zake zote alizozifanya kwa siri, zilizompelekea apate majanga yote yale. Kwasababu walimwambia hakuna mtu anayeweza kukutwa na majanga yale, kama hajamkosea Mungu.

 Na Ayubu alipowaambia kwamba hajafanya chochote kilicho kibaya cha siri, bado hawakumwamini Ayubu..waliendelea kumwambia kwamba amemkosea Mungu. Hivyo ikawa mlolongo mrefu wa mashauriano, kila mmoja akitumia hekima yake kutoa Mashauri yake dhidi ya Ayubu. Ayubu naye akitumia hekima zake kuwajibu kuwa hajafanya kosa lolote..mazungumzo yakawa marefu mno, mwishoni wakachoka kumshauri Ayubu, kwasababu alionekana anajihesabia haki machoni pake mwenyewe. Akatokea kijana mmoja aliyeitwa Elihu, naye pia akajaribu kutoa Mashauri yake kwa Ayubu na Rafiki zake watatu.

Na katika mazungumzo yao wote wanne (yaani Ayubu na Rafiki zake watatu, yalikuwa yamfikia Mungu juu pasipo wao kujua, na Mungu alikuwa anawasikiliza. Sasa kwa urefu pia kuhusu huduma za hawa Rafiki zake Ayubu, Na kufahamu jinsi, shetani anavyoweza kuwatumia watu wanaoitwa watumishi wa Mungu kuwamaliza watumishi wengine wakamilifu,  fungua hapa kwa ajili ya somo hilo kwa urefu >> HUDUMA YA ELIFAZI, BILDADI NA SOFARI, 

Sehemu ya Tatu:

Baada ya mazungumzo yao yote, Mungu anamjibu Ayubu kwa upepo wa kisulisuli, maana yake kwa Tufani, jambo ambalo Ayubu hakuwahi kuliona hapo kabla, na anaanza kwa kumuuliza.

Ayubu 38:1 “Ndipo Bwana akamjibu Ayubu katika upepo wa kisulisuli, na kusema,

2 Ni nani huyu atiaye mashauri giza Kwa maneno yasiyo na maarifa?”

Maana yake ni “Ni nani huyo anayehoji kazi zangu kwa maneno ya upumbavu”…Swali hilo Mungu alimwuliza Ayubu, akimlenga Ayubu na marafiki zake watatu.. Kutokana na maneno waliyokuwa wanazungumza, juu ya Mungu alichomfanyia Ayubu.

Na ukiendelea kusoma mpaka huo Mlango wa 41, utaona Bwana anaendelea kumuuliza maswali Ayubu, kuhusu utukufu wake, ambayo maswali hayo hayana majibu mpaka sasa..(Ili Ayubu ajue kuwa hakuna mtu yeyote anayeweza kuzihoji kazi zake wala kuzipatia majibu)…Mfano wa swali moja Mungu alilomuuliza Ayubu ni ili..

Ayubu 38:4 “Ulikuwa wapi nilipoiweka misingi ya nchi? Haya! Sema, kama ukiwa na ufahamu.

5 Ni nani aliyeamrisha vipimo vyake, kama ukijua? Au ni nani aliyenyosha kamba juu yake?”

Hili swali hakuna mtu anaweza kutoa jibu lake. Na maswali mengine mengi aliyoulizwa unaweza kuyasoma mpaka mlango ule wa 41.

Sehemu ya Nne:

Na baada ya Mungu kumuuliza Ayubu hayo maswali.  Ayubu alikosa majibu, na akajinyenyekeza akatubu, naye akajiona alikosea sana katika kunyanyua mdomo wake kuzihoji hoji kazi za Mungu, Pamoja na marafiki zake, ijapokuwa hakuzihoji kwa ubaya, lakini kitendo cha kushindana tu, tayari alitambua lilikuwa ni kosa. Hivyo akatubu mbele za Mungu kwa kuvaa nguo za magunia, na kufunga mdomo wake. Utasoma habari hiyo katika ule mlango wa 42.

Ayubu 42:1 “Ndipo Ayubu akamjibu Bwana, na kusema.

 2 Najua ya kuwa waweza kufanya mambo yote, Na ya kuwa makusudi yako hayawezi kuzuilika.

 3 Ni nani huyu afichaye mashauri bila maarifa? KWA MAANA, NIMESEMA MANENO NISIYOYAFAHAMU, MAMBO YA AJABU YA KUNISHINDA MIMI, NISIYOYAJUA.

4 Sikiliza, nakusihi, nami nitanena; Nitakuuliza neno, nawe niambie.

 5 Nilikuwa nimesikia habari zako, kwa kusikia kwa masikio; Bali sasa jicho langu linakuona.

 6 Kwa sababu hiyo NAJICHUKIA NAFSI YANGU, NA KUTUBU KATIKA MAVUMBI NA MAJIVU”.

Na baada ya Ayubu kujinyenyekeza na kujua kosa lake, Bwana aliwageukia wale Rafiki zake watatu, Elifazi, Bildadi na Sofari, ambao ndio waliomfanya Ayubu, azungumze maneno mengi, na zaidi ya yote, maneno yao ndio yaliyozihoji vibaya kazi za Mungu kuliko hata Ayubu. Hivyo Mungu akawakasirikia na kutaka kuwaadhibu.

Ayubu 42:7 “Basi ikawa, baada ya Bwana kumwambia Ayubu maneno hayo, Bwana akamwambia huyo Elifazi Mtemani, Hasira zangu zinawaka juu yako, na juu ya hao rafiki zako wawili; kwa kuwa ninyi hamkunena yaliyo sawa katika habari zangu, kama alivyonena mtumishi wangu Ayubu.

 8 Basi sasa, jitwalieni ng’ombe waume saba, na kondoo waume saba, mkamwendee mtumishi wangu Ayubu, mjisongezee sadaka ya kuteketezwa; na huyo mtumishi wangu Ayubu atawaombea ninyi; kwa kuwa nitamridhia yeye, nisiwatende sawasawa na upumbavu wenu; kwani ninyi hamkunena maneno yaliyonyoka katika habari zangu, kama alivyonena mtumishi wangu Ayubu.

 9 Basi Elifazi, Mtemani, na Bildadi, Mshuhi, na Sofari, Mnaamathi, wakaenda, wakafanya kama vile Bwana alivyowaamuru; naye Bwana akamridhia Ayubu”.

Na mwisho, katika kitabu hichi tunaona, tunaona Mungu akimuhurumia Ayubu na kumbariki tena na kumpa mara dufu ya vile alivyokuwa navyo.

Kuonyesha jinsi mwisho wa Mungu ulivyo mwema.

Kwa hitimisho katika kitabu hichi tunajifunza mambo yafuatayo:

1 .  Kumcha Bwana na kuepukana na uovu kama Ayubu:

2. Uvumilivu wakati wa majaribu: (Yakobo 5: 11 Angalieni, twawaita heri wao waliosubiri. Mmesikia habari ya subira yake Ayubu, mmeuona mwisho wa Bwana ya kwamba Bwana ni mwingi wa rehema, mwenye huruma.)

3. Kuishi Maisha ya usafi: kwasababu mshitaki wetu ibilisi, anapeleka mashitaka kuhusu sisi kila siku. Kama alimshitaki Ayubu kwa uzuri wake, unadhani tukiwa wabaya atakuwa anapeleka nini mbele za Mungu kama si kutuchongea tuangamizwe.

4. Kutokuwa na mashindano ya dini (hata kama unajua kitu, sio busara kulumbana na mtu asiyetaka kuamini unachokiamini) Ayubu alijua yupo sahihi, na marafiki zake hawapo sahihi, lakini kitendo cha kujibizana vile, ikawa tayari ni jambo lisilompendeza Mungu. Hivyo na sisi hatupaswi kuwa hivyo (Tito 3:9, 2Timotheo 2:14).

5. Mwenye haki kupitia mateso, haimaanishi Mungu hayupo naye; Tofauti na mitazamo ya watu wengi leo hii, wakishaonekana tu mtu aliyeokoka, anapitia hali Fulani mbaya labda ni hali ngumu ya kifedha, au ni magonjwa, basi moja kwa moja wanahitimisha kuwa Mungu amemwacha, au Mungu hayupo pamoja naye.

6. Kuwaombea Rafiki zetu na maadui zetu. (Hapo tunaona japokuwa Ayubu aliudhiwa na kukoseshwa na marafiki zake hao, lakini mwishoni aliwaombea rehema kwa Mungu, na wala hakuwalaani, na kwa kufanya vile {yaani baada ya kuwaombea tu}ndio ikafungua mlango wa baraka zake za mwisho).

Ayubu 42:10 “Kisha Bwana akaugeuza uteka wa Ayubu, hapo alipowaombea rafiki zake; Bwana naye akampa Ayubu mara mbili kuliko hayo aliyokuwa nayo kwanza”.

Hivyo na sisi tukitaka kufungua milango ya baraka hatuna budi kuwapenda adui zetu, na kuwaombea wale wanaotuudhi sawasawa na maneno ya Bwana wetu Yesu aliyotuasa katika..

Luka 6:27  “Lakini nawaambia ninyi mnaosikia, Wapendeni adui zenu, watendeeni mema wale ambao wawachukia ninyi,

28  wabarikieni wale ambao wawalaani ninyi, waombeeni wale ambao wawaonea ninyi”

Je umeokoka? Kama bado unasubiri nini ndugu?..Kristo anarudi, je akirudi leo kulichukua kanisa utakuwa wapi?..hayo Maisha ya uasherati, ulevi na anasa yanakusaidia nini sasa? Zaidi ya kukuharibu tu?.

Kama leo utaamua kuokoka utakuwa umefanya uamuzi bora ambao hautaujutia, ni vizuri ukafanya hivyo sasa, na wala usingoje kesho…kwamaana hujui yatakayozaliwa ndani ya siku moja.. Hivyo kama upo tayari kutubu leo na kumpokea Kristo fungua hapa kwa msaada Zaidi >>> SALA YA TOBA.

Usikose mwendelezo wa vitabu vinavyofuata.

Bwana akubariki.

Kwa maombezi/ Ushauri/ Ratiba za Ibada/Maswali/ Whatsapp/ Piga namba hizi: +255693036618/ +255789001312

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

KUJIPAMBA NI DHAMBI?

DANIELI: Mlango wa 1

UTAWALA WA MIAKA 1000.

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

KWANINI NI YESU KRISTO WA NAZARETI?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Kijicho ni nini? (Marko 7:22)

Kijicho ni nini kibiblia?


Kijicho ni kitendo kilichoaminika na jamii nyingi za zamani, kwamba mtu anaweza kukusababishia madhara au kukuletea laana, kwa kukutazama tu kwa macho yake, na hiyo inaweza ikawa amekusudia au hajakusudia kufanya hivyo. Na hiyo  huwa inasababishwa na wivu.

Imani hii hata sasa ipo kwa watu wengi, wanaamini kuwa jicho la mtu linaweza kukuloga, au kukuletea mikosi, gundu, magonjwa. N.k. Hivyo wanatumia vitu kama hirizi, na matambiko kujilinda na madhara ya watu hao.

Lakini Je katika Marko 7:22 Yesu alimaanisha hicho?

Tusome;

Marko 7:21 “Kwa maana ndani ya mioyo ya watu hutoka mawazo mabaya, uasherati,

22 wivi, uuaji, uzinzi, tamaa mbaya, ukorofi, hila, ufisadi, KIJICHO, matukano, kiburi, upumbavu.

23 Haya yote yaliyo maovu yatoka ndani, nayo yamtia mtu unajisi”.

Ni wazi kuwa Yesu hakumaanisha kijicho hicho kinachoaminiwa na wengi, hapana, bali hapa alimaanisha, JICHO OVU, jicho la uchoyo, jicho la wivu, na husuda.

Kuna mahali alisema..

Mathayo 20:15 “Si halali yangu kutumia vilivyo vyangu kama nipendavyo? Au jicho lako limekuwa ovu kwa sababu ya mimi kuwa mwema”?

Maneno hayo aliyasema alipokuwa anatoa ule mfano wa Yule mtu aliyewaajiri wafanyakazi wake shambani, na mwisho wa siku akawalipa wote sawa, bila kujali huyu alifanya sana, na huyu kidogo,.Vivyo hivyo na sisi macho yetu  yanaweza yakawa maovu kwasababu ya mtu mwingine kuwepwa upendeleo kama wetu, pengine mfanyakazi mpya amekuja na analipwa mshahara sawa au zaidi ya sisi tuliokuwepo kwa muda wa miaka 20 hapo kazini. Sasa kule kuona wivu, kutaka apewe kidogo kuliko wewe, hicho ndicho kijicho chenyewe ambacho Kristo anachokizungumzia kwamba  kinamtia mtu unajisi.

Sehemu nyingine kwenye biblia inasema;

Kumbukumbu 15:9 “Jitunze, msiwe na neno lisilofaa moyoni mwako, kusema, Umekaribia mwaka wa saba, mwaka wa maachilio; JICHO LAKO LIKAWA OVU juu ya nduguyo usimpe kitu; naye akamlilia Bwana juu yako, ikawa ni dhambi kwako”.

Unaona, aina nyingine ya kijicho ndio hiyo, kumdhulumu mtu haki yake kwa lengo la kumfanya aendelee kukutumikia, au pengine kwa wivu tu ili asifaidike akaweza kujitegemea. Hivyo wewe unadhamiria kumdhulumu haki yake ya utumishi kwako. Inaweza ikawa ni housegirl wako au houseboy wako au mlinzi wako, unapomnyima maslahi yake, hicho ni kijicho ambacho kitakutia unajisi na kukufanya usikubaliwe na Mungu.

Na ndio maana Bwana Yesu alisema;

Mathayo 6:22 “Taa ya mwili ni jicho; basi jicho lako likiwa safi, mwili wako wote utakuwa na nuru”.

Tunapaswa tuliondoe “jicho ovu” ndani yetu, Na hiyo inatokana na jambo moja tu, nalo ni kuushinda wivu. Wivu ukiondoka ndani ya mtu hataona uchungu kwa mwenzake kufanikiwa, hataona sababu ya kumdhulumu mfanyakazi wake, hataona sababu ya kumuundia visa jirani yake. Na matokeo yake Kijicho hufa ndani yake. Bwana atusaidie tuyatendee kazi na hayo. Ili nafsi zetu zisinajisike.

Shalom.

Tazama tafsiri za maneno mengine ya biblia chini.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Nini tofauti kati ya Husuda, faraka na uchafu?

MZAZI, JALI MAISHA YA KIROHO YA MTOTO WAKO.

GOGU NA MAGOGU, Katika biblia ni nani?

Nini maana ya K.K, na B.K?  (B.C na A.D).

NI KWA NAMNA GANI ROHO HUTUTAMANI KIASI CHA KUONA WIVU?

SAMEHE KUTOKA NDANI YA MOYO WAKO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

MZAZI, JALI MAISHA YA KIROHO YA MTOTO WAKO.

Kuna pepo moja lililowasumbua sana mitume wa Yesu, hilo halikuwa sawa na pepo mengine waliyokutana nayo, walihangaika nalo mchana kutwa lakini hawakufua dafu mpaka alipokuja Bwana Yesu mwenyewe kulikemea na kulitoa.

Lakini leo hatutazungumzia juu ya pepo hilo kwasababu habari yenyewe tunaijua, ila katika habari hiyo lipo jambo ambalo ni vizuri sisi tukajifunza, husasani kwa wazazi au walezi, wanaoishi na watoto wadogo. embu tusome tena alichokifanya Yesu kisha, tuende kwenye ujumbe wenyewe..

Marko 9:20 “Wakamleta kwake; hata alipomwona, mara yule pepo alimtia kifafa; naye akaanguka chini, akagaa-gaa, akitokwa na povu.

21 Akamwuliza babaye, AMEPATWA NA HAYA TANGU LINI? Akasema, TANGU UTOTO.

22 Na mara nyingi amemtupa katika moto, na katika maji, amwangamize; lakini ukiweza neno lo lote, utuhurumie, na kutusaidia”.

Sasa katika habari hiyo, usidhani Yesu alikuwa hajui matatizo ya huyo mtoto ndio maana akamwuliza vile, Kumbuka Yesu alikuwa anajua kila kitu wala alikuwa hana haja ya mtu kumuadhithia chochote, biblia inatuambia hivyo katika  Yohana 16:30, Lakini  aliuliza vile kwa lengo la kutaka watu wote wajue matatizo ya Yule mtoto yalianzia wapi, na ndio maana akamuuliza vile yule mzazi “Amepatwa na haya tangu lini?”.

Ndipo yule mzee akamjibu na kusema,  “amepatwa na haya tangu utotoni”. Ulishawahi  kuutafakari vizuri huu mstari, tangu utotoni? ..Hiyo ni kutuonyesha kuwa kuna mapepo ambayo, agenda yao kuu, ni watoto. Kwasababu yanajua yakianzia katika msingi, baadaye yatakuwa ni magumu kutoka.

Inashangaza leo hii kuona wazazi hawajali maisha ya kiroho ya watoto wao, wanaona kama wao ni watoto tu, shetani hawezi kuwashambulia, hawajui kuwa wanapaswa kulindwa kwasababu shetani huwa hatambui cha mtoto au cha mzee, lengo lake ni kuharibu. Kama alimuingia Nyoka ambaye ni mnyama tu, ataachaje kumwingine mtoto ambaye ni mwanadamu? ndio target yake kubwa?

Mzazi, anamruhusu mtoto wako mdogo atezame tv masaa 24 wakati wote hata zile programu ambazo haziendani na umri wake anamwacha azitazame, anamwacha asikilize miziki ya kidunia, tena Zaidi ya yote unafurahi anapocheza,  lakini nyimbo za tenzi hata moja haujui, Mzazi mwingine hata hampeleki mtoto wake Sunday school ili afundishwe njia ya kikristo angali akiwa mdogo, yeye anachojua ni kumnunulia mtoto wake nguo nzuri tu, kumtafutia nursery nzuri ya kusoma, anajali vya mwilini vya mwanawe anapuuzia na vile vya rohoni. Hata kumwombea mtoto wake anashindwa.

Nachotaka nikuambie ni kuwa tusipowawekea msingi mzuri watoto wetu, shetani atatusaidia kuwawekea wake, kama alivyofanya kwa mtoto wa huyu mzee tunayesoma habari zake.  Lile pepo lina haki ya kuwa gumu kutoka kwasababu tayari lilikuwa na msingi tangu utotoni. Na ukiangalia lengo la hilo pepo si lingine zaidi ya kumwangamiza tu, mara litake kumtupa kwenye maji, kwa bahati nzuri pengine watu wanamuona wanamuokoa, mara litake kumtupa kwenye moto, lakini Mungu anafungua rehema zake anaepukika.

Leo hii utaona kumenyanyuka kundi kubwa la watoto ambao wanaonyesha tabia ambazo hazieleweki chanzo chake ni nini, na wewe unaweza ukadhani ni yeye anafanya kumbe ni pepo ambalo tayari lilishamvaa tangu utotoni ndio linaonyesha tabia hizo ndani yake.

Wazazi ndio wanapaswa waanze kubadilika, ndio watoto wabadilike.  Wewe kama mzazi, kama hutaonyesha kujali maisha ya kiroho ya mtoto wako, usidhani mtoto atabadilika mwenyewe au atakuwa na tabia njema huko mbeleni.

Mithali 22:6 “Mlee mtoto katika njia impasayo, Naye hataiacha, hata atakapokuwa mzee”

SASA UTAYAZUIAJE MAPEPO YA UHARIBIFU KAMA HAYO YASIMWINGIE MWANAO?

Kwanza ni kwa kutumia kiboko: Biblia inasema hivyo, …Pale unapoona kuna tabia Fulani ambayo sio nzuri, mfano kiburi, anatukana, hana nidhamu, hapo hapo hupaswi kuiacha hiyo tabia imee, mpaka hilo pepo liumbike ndani yake.. Utalitoa hilo kwa kiboko.

Mithali 23:13 “Usimnyime mtoto wako mapigo; Maana ukimpiga kwa fimbo hatakufa.

14 Utampiga kwa fimbo, Na kumwokoa nafsi yake na Kuzimu”.

Pili Ni  kwa kumfundisha kanuni za imani: Unamfundisha biblia, unamfundisha nyimbo za kikristo, unamfundisha kusali, unamfundisha hata kukariri  vifungu vya biblia, hata kama hataelewa sasahivi lakini vitabaki moyoni mwake kama hazina itakayokuja kumsaidia baadaye. Na  hakikisha pia unampelekea kwenye mafundisho ya watoto kanisani.

Tatu  Unamwombea; Mara kwa mara unahakikisha unamfunika mwanao, kwa damu ya Yesu Kristo, unatenga muda mrefu wa kumuombea.

Na Nne unamzuia kufanya/kutazama mambo ambayo hayapasi: Si lazima kila unachokitazama wewe, mtoto naye akitazame, magemu anayoyacheza mtoto si yote yanamaudhui mazuri, vilevile nguo unazomvisha mtoto si zote ni njema. Hivyo jifunze kumchagulia mtoto vinavyomfaa.

Ukizingatia hayo, basi mapepo kama hayo ambayo ni hatari na sugu, hayatamkuta mwanao. Kumbuka biblia inasema shetani ni kama simba angurumaye, akitafuta mtu ammeze, hivyo usipuuzie haya maagizo, mjenge mwanao, mjenge mdogo wako, mjenge mtoto yoyote auishiye naye.

Na Bwana atakubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618.

Jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

TUMEFANYIKA KUWA WANA WA MUNGU!

AGENDA KUBWA YA SHETANI KWA KANISA HILI LA LAODIKIA.

KILEMBA CHA NEEMA, JE! UMEMVIKA MWANAO?

RUDI KUMPA MUNGU UTUKUFU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

JE NI LAZIMA KUBADILISHA JINA BAADA YA KUOKOKA?

Jina la Bwana wetu Yesu, libarikiwe. Karibu tujifunze biblia.

Katika biblia Mungu hakuwabadilisha watu majina kutokana na tafsiri za hayo majina. Ni muhimu kufahamu sana hili, vinginevyo shetani anaweza kukutesa na tafsiri ya jina lako. Kwasababu usipomwelewa Mungu jinsi anavyotenda kazi, utachukuliwa na kila aina ya upepo wa elimu, na mafundisho ya mashetani, ambayo kazi ya hizo elimu ni kuwafunga watu wala sio kuwafungua, Kuwatwisha watu mizigo mizito na wala si kuwatua.

Yohana 8:36 “Basi Mwana akiwaweka huru, mtakuwa huru kweli kweli”

Sasa hebu tuangalie watu wachache waliobadilishwa majina katika biblia, na tafsiri za majina yao kabla na baada ya kubadilishwa, ndipo tutajua tabia ya Mungu.

  1. Ibrahimu

Huyu mara ya kwanza alikuwa anaitwa “Abramu”. Tafsiri ya jina Abramu ni “Baba aliyeinuliwa” na Ibrahimu tafsiri yake ni “Baba wa mataifa mengi”.

Sasa kulingana na tafsiri hizo, sio kwamba Mungu aliona tafsiri ya jina lake la kwanza ilikuwa ni mbaya, na hivyo akataka kumpa jina jipya lenye tafsiri zuri, hapana!..ilikuwa ni nzuri tu… kuitwa “Baba aliyeinuliwa” sio jina baya, lakini ilipofika wakati wa Mungu kumpa agano kwamba atakuwa Baba wa mataifa mengi, ndipo jina lake likabadilishwa na kuwa Ibrahimu. (Hivyo lilibadilishwa kwasababu ya huduma iliyopo mbele yake).

  1. Sara

Huyu alikuwa ni mke wa Ibrahimu, ambaye hapo kwanza alikuwa anaitwa “Sarai” maana yake ni “binti wa mfalme” lakini jina lake lilibadilishwa na kuwa “Sara” ambalo maana yake ni “mama wa wana wa wafalme”. Hivyo halikubadilishwa kwasababu lilikuwa na maana mbaya, bali kwasababu ya Ahadi ya Mungu, ya mumewe Ibrahimu kuwa Baba wa mataifa mengi, hivyo hana budi na yeye kuwa mama wa mataifa na wafalme wengi,  Ni sawa wewe ubadilike sasa kutoka kuitwa mtoto, na kuitwa Baba wa watoto wengi…au kutoka kuitwa binti mpaka kuitwa mama wa mabinti wengi..(Ni kutokana na kubadilika majukumu, umetoka kwenye utoto sasa umeingia kuwa mama/baba)

  1. Yakobo

Mtu wa tatu ni Yakobo, mwana wa Isaka, jina lake lilibadilishwa kutoka kuitwa Yakobo hadi kuitwa Israeli.. Tafisiri ya jina “Yakobo” ni “mshika kisigino”..Jina hilo aliitwa kutokana na jinsi alivyozaliwa, kwani alipozaliwa alizaliwa huku kamshika ndugu yake kisigino.(Mwanzo 25:26)..na Tafsiri ya jina Israeli ni “Kushindana na Mungu”. Sasa Yakobo jina hilo halikubadilishwa kutokana na tafsiri yake ni mbaya..Hapana bali ni kutoka na ahadi mpya Mungu aliyokwenda kumpa baada ya kushindana na yule malaika na kumshinda..Kwasababu kama tafisiri ya Jina Yakobo lingekuwa ndio sababu ya Mungu kumbadilisha jina, basi Mtume wa Yesu aliyeitwa Yakobo, angepaswa naye pia abadilishwe jina. Na aliyeandika kitabu cha Yakobo, naye pia angepaswa abadilishwe.. Lakini tunaona hawajabadilishwa, lakini bado waliendelea kuwa Mitume wa Yesu, waaminifu mpaka mwisho.

  1. Petro

Petro hapo kwanza alikuwa anaitwa Simoni.. Yohana 1:42  “Akampeleka kwa Yesu. Naye Yesu akamtazama, akasema, Wewe u Simoni, mwana wa Yohana; nawe utaitwa Kefa (tafsiri yake Petro, au Jiwe)”.  Sasa tafsiri ya jina Simoni ni “Amesikia”.. Na tafisiri ya Kefa/Pertro ni “jiwe dogo la kurusha” na sio “mwamba”. Hivyo kwa hali ya kawaida, Simoni ndio lenye tafsiri bora kuliko Petro..

Sasa utaona Bwana Yesu hakumbadilisha jina Simoni kwasababu lina maana mbaya, hapana bali ni kwasababu ya huduma yake inayokwenda kuanza, kwamba Bwana atamtumia kama jiwe lake, kwa kazi yake. Sasa jina “Simoni” lingekuwa na tafsiri mbaya inayomchukiza Mungu au yenye madhara kiroho kwa Petro, basi angembadilisha pia mtume wake mwingine miongoni mwa wale 12, ambaye naye pia alikuwa anaitwa Simoni mkananayo (Mathayo 10:4). Kwasababu Bwana asingeweza kumbadilisha mtume mmoja na kumwacha mwingine mwenye jina kama hilo hilo. (Kwahiyo Petro naye alibadilishwa kutokana na huduma iliyopo mbele yake)

  1. Sauli

Na wa mwisho tunayeweza kumwona ni Mtume Paulo ambaye hapo kwanza alikuwa anaitwa “Sauli” ambapo tafsiri ya jina hilo ni “Ombea” (mf. Kuombea kitu fulani kwa Mungu), hiyo ndiyo tafisiri ya jina Sauli, lakini jina hilo lilikuja kubadilishwa na kuwa “Paulo” ambalo maana yake ni “Mdogo”.

Hivyo unaona hapo, jina lake halikubadilishwa kwasababu lilikuwa na tafsiri mbaya, hata wewe katika hali ya kawaida ungeambiwa uchague uitwe jina lenye tafsiri ya “mdogo” au uitwe jina lenye tafsiri ya “Ombea”..Bila shaka ungechagua lenye tafsiri ya “ombea”. Lakini Mungu alimbadilisha Sauli na kumpa hilo lenye tafisiri ya mdogo.

Na kwanini Mungu alimpa jina hilo Paulo?. Ni kwasababu ya huduma yake, ambayo anakwenda kuifanya hapo mbeleni (ambayo itampasa awe mdogo sana na mnyenyekevu).

Waefeso 3:7  “Injili hiyo ambayo nalifanywa mhudumu wake, kwa kadiri ya kipawa cha neema ya Mungu niliyopewa kwa kadiri ya utendaji wa uweza wake.

8  MIMI, NILIYE MDOGO KULIKO YEYE ALIYE MDOGO WA WATAKATİFU WOTE, nalipewa neema hii ya kuwahubiri Mataifa utajiri wake Kristo usiopimika;

9  na kuwaangaza watu wote wajue habari za madaraka ya siri hiyo, ambayo tangu zamani zote ilisitirika katika Mungu aliyeviumba vitu vyote”.

 Kwahiyo jambo kubwa la kujifunza ni kwamba… tafsiri za majina yetu, hazina maana sana mbele za Mungu wetu. Ndio ni vizuri kuwa na jina lenye tafsiri nzuri, lakini hilo halikusogezi mbele za Mungu. Kwasababu majina yaliyoandikwa kwenye kitabu cha uzima, hayajaandikwa kulingana na maana za majina hayo, bali kulingana na matendo ya mtu.

Watakuwepo wengi mbinguni ambao majina yao hayana tafsiri nzuri, na vile vile watakuwepo wengi kuzimu wenye majina mazuri, watakuwepo wakina Ibrahimu wengi kuzimu, watakuwepo wakina Paulo wengi kuzimu, watakuwepo wakina Petro wengi kuzimu, na watakuwepo wakina Yohana wengi kuzimu. Vile vile watakuwepo wakina Sauli wengi mbinguni, watakuwepo wakina Yakobo wengi mbinguni, watakuwepo wakina matatizo wengi mbinguni, watakuwepo wakina Majuto wengi mbinguni, watakuwepo wakina masumbuko wengi n.k

Kwahiyo baada ya kuokoka, Tafsiri ya jina lako isikusumbue sana. Kama umependa kulibadilisha kwa mapenzi yako mwenyewe (kwamba hupendwi kuitwa hilo jina katikati ya jamii yako)ni sawa hutendi dhambi, na Kama Bwana amekuongoza kubadilisha jina lako pia ni sawa fanya hivyo!!, lakini kama Bwana hajakuongoza wala usiwe na hofu,  wala usitishwe na elimu zilizozagaa kwamba utapata mikosi kwa jina hilo, au jina hilo ni kikwazo kwako na mafanikio yako.

Kuwa tu kama Simoni Mkananayo mwanafunzi wa Yesu, ambaye jina lake lilibakia kuwa lile lile, lakini bado aliendelea kuwa mwanafunzi wa Yesu..ijapokuwa mwenzake alibadilishwa na kuwa Petro, yeye aliendelea kuwa vile vile Simoni. Kwasababu Mungu hatembei na wewe kwasababu ya tafsiri bora ya jina lako, bali kwasababu ya uaminifu wako kwake katika kuyafanya mapenzi yake. Kama vile asivyobagua rangi, vivyo hivyo habagui watu kutokana na tafsiri za majina yao.

Katika Biblia kuna mtu anaitwa Tabitha au Dorkasi, tafisiri ya jina hilo ni “Paa” kasome Matendo 9:36, sasa “paa” kwa lugha inayoeleweka ni “mnyama Swala”..Lakini pamoja na jina lake hilo lenye tafisiri isiyo na maana, tunasoma Tabitha alimpendeza Mungu sana..

Matendo 9:36 “ Na mwanafunzi mmoja alikuwako Yafa, jina lake Tabitha, tafsiri yake ni Dorkasi (yaani paa); mwanamke huyu alikuwa amejaa matendo mema na sadaka alizozitoa”.

Kadhalika katika biblia kuna mtu aliyeitwa Yabesi (1Nyakati 4:9-10), huyu alipewa jina lenye tafsiri mbaya ya HUZUNI, lakini alimpendeza Mungu sana.(Kwa habari zake ndefu unaweza kututumia ujumbe inbox). Na ipo mifano mingine mingi kwenye biblia ambayo hatuwezi kuitaja hapa yote. Lakini kwa hiyo michache itoshe tu kusema kwamba, Kama ulikuwa na hofu na tafsiri ya jina lako, badilisha mtazamo sasa..Anza kuwa na hofu na mwenendo wa maisha yako katika hatima ya maisha yako, zaidi ya tafisir ya jina lako.

Ufunuo 20:12  “Nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wamesimama mbele ya hicho kiti cha enzi; na vitabu vikafunguliwa; na kitabu kingine kikafunguliwa, ambacho ni cha uzima; na hao wafu wakahukumiwa katika mambo hayo yaliyoandikwa katika vile vitabu, SAWASAWA NA MATENDO YAO”.

Hivyo utazame mwenendo wako, je umesimama katika Imani sawasawa?..Je matendo yako yanampendeza Mungu?..kama bado basi rekebisha leo kabla hujafikia mwisho wa siku zako za kuishi hapa duniani.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

JINA LAKE KWA KIEBRANIA NI ABADONI, NA KWA KIYUNANI NI APOLIONI.

HAPO NDIPO WATU WALIPOANZA KULIITIA JINA LA BWANA.

CHAKULA CHA ROHONI.

CHAKULA CHA ROHONI.

TUMEPEWA MAMLAKA YA KUKANYAGA NG’E NA NYOKA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Kwanini wale dubu waliowauwa vijana wa Elisha walikuwa wa kike?

SWALI: Bwana Yesu apewe sifa Ukisomo kitabu cha 2 WAFALME 2:24 napenda kuelewa mbona pale wanatokea dubu wawili wa kike mwituni na sio wa kiume?

2Wafalme 2:24 “Akatazama nyuma akawaona, akawalaani kwa jina la Bwana. Wakatoka dubu wawili wa kike mwituni, wakawararua vijana arobaini na wawili miongoni mwao”.


JIBU: Tofauti na sisi wanadamu, kwa upande wa wanyama, asilimia kubwa ya wanyama wenye asili ya kike (majike) huwa  wanakuwa ndio wakali zaidi, na washapu kuliko wa jinsia ya kiume. Utaona kwa simba, Dubu na kadhalika. Majike ndio wawindaji n.k.

Ukisoma Mithali 17:12 inasema;

“Afadhali mtu akutwe na dubu aliyenyang’anywa watoto wake, Kuliko na mpumbavu katika upumbavu wake”.

Hapo imetumia mfano wa dubu mke, na sio dume, hii ni kuonyesha kuwa hao ndio wakali zaidi hususani pale wanapokuwa na watoto.

Utasoma tena sehemu nyingine Mungu alijifananisha na dubu mke, kwa hasira yake atayaoichia juu ya Israeli kwasababu ya makosa yaliyofanya kinyume chake. Akaifananisha hasira yake na hasira ya dubu jike.

Hosea 13:7 “Basi nimekuwa kama simba kwao; kama chui nitavizia njiani;

8 nitakutana nao kama dubu aliyenyang’anywa watoto wake; nami nitararua nyama ya mioyo yao; na huko nitawala kama simba; huyo mnyama mkali atawararua.

9 Haya ndiyo maangamizo yako, Ee Israeli, ya kuwa wewe u kinyume changu mimi, kinyume cha msaada wako”.

Ni nini tunajifunza? Kwanini walitumiwa dubu wa kike na sio wa kiume?

Hiyo ni kuonyesha uwezo wa jamii ya kike , kuwa wanawake, wanaweza kuwa vyombo viteule vya kumponda ibilisi kwa Bwana, ikiwa tu watasimama katika nafasi zao katika wokovu. Wanawake waliosimama ibilisi anawaogopa sana, kwasababu anajua  madhara yatakayoyasababisha katika ufalme wake.

Hivyo ikiwa wewe ni mwanamke unapaswa usimama sasa, uwe na ushujaa kama wa dubu jike, rarua, angamiza, teketeza  kazi zote za shetani bila kuona huruma yoyote, kwasababu uwezo huo unao ndani yako.

Zaburi 68:11 “Bwana analitoa neno lake; Wanawake watangazao habari ni jeshi kubwa;”

Bwana akubariki

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

KIFO CHA MTAKATIFU PERPETUA NA FELISTA.

KIAMA KINATISHA.

HIZI NI NYAKATI ZA KUJIINGIZA KWA NGUVU.

TUMEPEWA MAMLAKA YA KUKANYAGA NG’E NA NYOKA.

SALA YA UPONYAJI/MAOMBI YA UPONYAJI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

GOGU NA MAGOGU, Katika biblia ni nani?

Neno Gogu na Magogu limeonekana sehemu mbili katika biblia, Sehemu ya kwanza ni katika kitabu cha Ezekieli 38:2, na katika Ufunuo 20:8.

Sasa ni vizuri kujua kwanza Magogu ni nini, ndipo tuje kwa Gogu.

Magogu sio wingi wa Gogu.. hapana!.. bali ni jina la mtu mmoja, ambalo tunalipata katika kitabu cha Mwanzo 10:2.

Mwanzo 10: 1 “Hivi ndivyo vizazi vya wana wa Nuhu, Shemu, na Hamu, na Yafethi. Na kwao walizaliwa wana wa kiume baada ya gharika.

2 Wana wa Yafethi ni Gomeri, na MAGOGU, na Madai, na Yavani, na Tubali, na Mesheki, na Tirasi.

Hivyo “Magogu” alikuwa ni Mjukuu wa Nuhu, alikuwa ni Mtu. Sasa mtu huyu biblia haijaeleza alikuwa ni mtu mwenye sifa gani, lakini kutokana na uwepo wake katika sehemu nyingine za biblia, inaonekana wazao wake walikuja kuwa watu Hodari kipindi hicho, na mwenye uwezo mkubwa sana wa kijeshi, na kiuchumi, mfano wa Nimrodi aliyeujenga Babeli.

Na Magogu naye ni hivyo hivyo, uzao wake ulikuja kuwa Hodari..na kuwa Taifa lenye nguvu kijeshi, na watu hao wote kwa ujumla wakaitwa Magogu kufuatia jina la baba yao huyo.

Kama vile mji wa Moabu ulivyoitwa kufuatia jina la baba yao aliyeitwa Moabu. (Mwanzo 19:37 “Yule mkubwa akazaa mwana, akamwita jina lake Moabu; huyo ndiye baba wa Wamoabi, hata leo”)

Na Magogu ni hivyo hivyo, Uzao wake ulikuja kuitwa kwa jina hilo la Magogu, na nchi yao ikaitwa nchi ya Magogu, kufuatia jina la baba yao huyo aliyeitwa Magogu.

Tunalisoma hilo vizuri katika Ezekieli..

Ezekieli 38:1 “Neno la Bwana likanijia, kusema,

2 Mwanadamu, kaza uso wako, umwelekee GOGU, wa NCHI YA MAGOGU, mkuu wa Roshi, Mesheki, na Tubali, ukatabiri juu yake”,

Na nchi hiyo lilikuwa upande wa kaskazini mwa Asia na Ulaya, ambayo sasahivi ni Maeneo ya nchi ya Urusi.  Hatima ya hilo Taifa la Magogu, biblia haijaieleza, lakini ni wazi kuwa lilikuja kupotea kama yalivyopotea mataifa mengine yaliyokuwa hodari kama Babeli.

Sasa baada  ya kujua hilo, twende kipengele cha pili, cha GOGU. Kama tulivyotangulia kusema Magogu sio wingi wa Gogu. Bali Gogu ni kiongozi wa Taifa la Magogu. Yaani mfalme wa taifa la Magogu. Kwahiyo tunaposoma, neno Gogu na Magogu, Ni sawa na kusema Farao na Misri, au Sulemani na Israeli.

Ndio maana tunasoma hapo katika Ezekieli 38:3… “useme, Bwana MUNGU asema hivi; Tazama, mimi ni juu yako, Ewe GOGU, mkuu wa Roshi, na Mesheki, na Tubali;”

Umeona hapo mstari wa 2, unasema Gogu mkuu wa…. Neno “mkuu wa” linaashiria ni kiongozi, hivyo Gogu ni jina la kiuongozi kama vile Farao, au Sultani. Na Magogu ni Taifa hilo lenye nguvu ambalo linatawala mataifa mengine madogo madogo (Tubali, Mesheki na Roshi)

Sasa kama tulivyotangulia kusema huo mji wa Magogu haupo tena wala mkuu wake Gogu hayupo…Lilikuwepo enzi hizo, lakini sasa halipo tena, lakini huo unabii wa Ezekieli 38 bado haujatimia.. Ambapo ukisoma hiyo Ezekieli 38 yote, utaona inazungumzia Habari za vita vitakavyopiganwa Israeli, ambapo Mataifa mengi katika nchi ya mashariki ya kati (kwasasa ni mataifa ya kiarabu), yataungana pamoja na Gogu na Magogu, atakayekuwepo kipindi hicho kuja kuivamia Israeli, lakini biblia inasema Gogu atashindwa vibaya sana Pamoja na mataifa hayo aliyoshirikiana naye.

Sasa huyo Gogu na Magogu, atakuwa ni nani, kama mji huo ulishapotea kitambo?..

Gogu atakayeasisi vita hivyo vya Ezekieli 38, Uthibitisho wote unaonyesha kuwa atakuwa si mwingine Zaidi ya Mkuu wa Taifa la URUSI .

Kwanini ni Taifa la Urusi, ndio linalofananishwa na Magogu na si Taifa lingine?.

Kwasababu ndio taifa lililopo kaskazini mwa Asia na ulaya, eneo lile lile Magogu walipokuwepo, pili ndio taifa lenye nguvu kijeshi kaskazini mwa Ulaya, mfano wa magogu wa mwanzo.

Hivyo Urusi ndiyo itakayotimiza unabii huo wa Gogu na Magogu, wakati wa vita hivyo.

Mbali na hilo tunakuja kuona tena Gogu na Magogu, wakitokea mwishoni mwa Utawala wa miaka elfu moja. Sasa ni muhimu kufahamu kuwa sio wale wale, wamezaliwa tena upya..hapana…bali ni roho ile ile iliyokuwa inaiendesha Gogu na Magogi kipindi cha zamani, sasa imerudi tena kutenda kazi katika zama hizo, ni kama tu vile Babeli ilivyokuwepo wakati wa zamani na kupata nguvu na kujulikana duniani kote, na kutiisha mataifa yote chini,  lakini ikaja kuanguka, ikapotea kabisa…Lakini bado tena tunakuja kuiona ipo, imerudi tena katika kitabu cha Ufunuo. Sasa haimaanishi kwamba ni Babeli ile ile imerudi,  bali ni ile roho iliyokuwa inaiendesha Taifa hilo nyakati za zamani, imerudi na kuivaa na kuliendesha Taifa Fulani lingine siku za mwisho..

Hivyo Gogu na Magogu, wa kwenye Mwanzo wa kwenye Ezekieli 38 (yaani Taifa la Urusi), sio wa kwenye Ufunuo 20:8 (mwishoni mwa utawala wa miaka elfu), ingawa roho ni ile ile moja, inayofanya kazi ya kukusanya mataifa na kupambana na Taifa la Mungu.

Je umempokea Kristo? Kama bado, kumbuka tunaishi ukingoni mwa nyakati kabisa na Kristo yupo karibuni kurudi, na mpinga kristo kuanza kufanya kazi yake, ya kuwatia watu chapa. Kama unafikiri ni utani kwamba Kristo hatarudi, siku moja utayahikiki haya maneno unayoyasikia. Wakati huo waliokudanganya na wao watagundua kuwa walidanganywa, itakuwa ni huzuni sana.. Je utakuwa wapi siku hiyo?. Kama hujampokea Kristo na leo hii unasema upo tayari kumpokea Kristo na kudhamiria kutubu basi fungua hapa kwa msaada >> SALA YA TOBA

Mungu akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 8 (Kitabu cha Ezekieli)

JE WEWE NI LAZARO YUPI, WA KWANZA AU WA PILI?

WAFALME WATOKAO MAWIO YA JUA.

Watakaodanganywa baada ya miaka 1000,watatoka wapi?

ULIMWENGU WA ROHO UPO NA UNA MADHARA KATIKA MAISHA YETU! 

Rudi Nyumbani:

Print this post

Wevi na wanyanga’anyi waliomtangulia Yesu walikuwa ni wapi?

SWALI: Bwana Yesu asifiwe mtumishi habari ya uzima, samahani nini swali;  Yohana 10:7-8 inasema;

“7 Basi Yesu aliwaambia tena, Amin, amin, nawaambieni, Mimi ndimi mlango wa kondoo.

8 Wote walionitangulia ni wevi na wanyang’anyi; lakini kondoo hawakuwasikia”.

Hapo sijaelewa Bwana alichokimaanisha aliposema wote waliomtangulia walikuwa ni wevi na wanyang’anyi?


JIBU: Mstari huo hauzungumzii, wale waliomtangulia Bwana yaani Manabii na makuhani  wa agano la kale hapana, kwani wao ndio waliokuwa wanamwandalia njia yeye, aliye mlango wa kondoo wenyewe.

Bali mstari huo ulikuwa unawazungumzia watu waliokuwa wanajifanya kuwa wao ndio masihi ( yaani Mwokozi) kama yeye. Hao ndio alikuwa anawasemea hapo, kwamba ni wevi na wanyang’anyi na kwamba kondoo wa kweli wa Mungu hawakuwafuata.

Kumbuka wana wa Israeli kwa muda mrefu walikuwa wanangojea masihi ambaye atawaokoa katika shida zao, na dhambi zao kama ilivyotabiriwa katika torati. Hivyo ilikuwa ni jambo la kawaida kutangulia ma-kristo wa uongo wengi kabla yake wakijifanya wao ndio. Utalithibitisha hilo katika maneno ya Yule Gamalieli, mwalimu wa torati, pale alipokuwa anahojiana na wakuu wa makuhani juu ya mitume walichokuwa wanakifanya kwa habari ya Yesu..Alisema;

Matendo 5:35 “akawaambia, Enyi waume wa Israeli, jihadharini jinsi mtakavyowatenda watu hawa.

36 Kwa sababu kabla ya siku hizi aliondoka Theuda, akijidai ya kuwa yeye ni mtu mkuu, watu wapata mia nne wakashikamana naye; naye aliuawa na wote waliomsadiki wakatawanyika wakawa si kitu.

37 Baada ya mtu huyo aliondoka Yuda Mgalilaya, siku zile za kuandikiwa orodha, akawavuta watu kadha wa kadha nyuma yake, naye pia akapotea na wote waliomsadiki wakatawanyika.

38 Basi sasa nawaambia, Jiepusheni na watu hawa, waacheni; kwa kuwa shauri hili au kazi hii ikiwa imetoka kwa binadamu, itavunjwa,

39 lakini ikiwa imetoka kwa Mungu hamwezi kuivunja; msije mkaonekana kuwa mnapigana na Mungu”.

Unaona, hapo anasema alitangulia, Theuda, na Yuda Mgalilaya, na walikuwepo na wengine wengi  pia biblia haijawazungumzia tu. Kwahiyo  wezi na wanyang’anyi Yesu aliokuwa anawazungumzia hapo ndio hawa.

Hata sasa wevi  na wanyang’anyi Bwana Yesu aliwatabiri watakuwepo katika siku za mwisho. Ndio wale aliowaita Makristo wa uongo na manabii wa uongo.

Mathayo 24:24 “Kwa maana watatokea makristo wa uongo, na manabii wa uongo, nao watatoa ishara kubwa na maajabu; wapate kuwapoteza, kama yamkini, hata walio wateule”.

Hivyo Kristo ameshatuonya, ni wajibu wetu kuwa macho, na hiyo inakuja kwa kuwa wakristo kweli kweli na kumruhusu Roho Mtakatifu kutenda kazi ndani yetu.

Swali ni Je! Umeokoka? Na Kama umeokoka Je! Umesimama? Kumbuka, makristo hawa watajaribu kuwadanganya yamkini hata wateule, hiyo ni kuonyesha kuwa ni jinsi gani ilivyo ngumu kuwatambua kama wewe utakuwa ni mkristo jina tu, au mkristo vuguvugu. Hizi si nyakati tena za kukaa gizani.

Ni heri ukaanza maisha yako upya na Kristo leo. Ikiwa bado hujaokoka, na unataka leo kumpa Yesu maisha yako, basi uamuzi huo utakuwa ni wa busara sana kwako. Kama jibu ni ndio .Fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya toba na kupokea maagizo mengine ya rohoni>>>>  SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

USIIGEUZE NYUMBA YA MUNGU KUWA PANGO LA WANYANG’ANYI.

UNAWAFAHAMU MANABII WA UONGO?

WALIOITWA NI WENGI, ILA WATEULE NI WACHACHE.

FUATILIA NDOTO HII, UTAJIFUZA KITU.

MTETEZI WAKO NI NANI?

Rudi Nyumbani:

Print this post