Maji ya uzima, tunayoyasoma katika biblia sio maji ya chemchemi, wala ya bombani, wala kisimani, wala ya mto Yordani ulioko kule Israeli na wala sio maji ya upako, yanayouzwa leo huku na huko.
Maji ya uzima ni jambo lingine la kiroho ambalo leo ningependa tuliangalie kidogo.
Katika kitabu cha Yohana, Bwana Yesu alijaribu kugusia kidogo kuwa maji ya uzima yaliyo hai…sio maji ya kisimani..
Yohana 4:5“ Basi akafika kunako mji wa Samaria, uitwao Sikari, karibu na lile shamba ambalo Yakobo alimpa Yusufu mwanawe.
6 Na hapo palikuwa na kisima cha Yakobo. Basi Yesu, kwa sababu amechoka kwa safari yake, akaketi vivi hivi kisimani. Nayo ilikuwa yapata saa sita.
7 Akaja mwanamke Msamaria kuteka maji. Yesu akamwambia, Nipe maji ninywe.
8 Kwa maana wanafunzi wake wamekwenda mjini kununua chakula.
9 Basi yule mwanamke Msamaria akamwambia, Imekuwaje wewe Myahudi kutaka maji kwangu, nami ni mwanamke Msamaria? (Maana Wayahudi hawachangamani na Wasamaria.)
10 Yesu akajibu, akamwambia, Kama ungaliijua karama ya Mungu, naye ni nani akuambiaye, Nipe maji ninywe, UNGALIMWOMBA YEYE, NAYE ANGALIKUPA MAJI YALIYO HAI.
11 Yule mwanamke akamwambia, Bwana, huna kitu cha kutekea, na kisima ni kirefu; basi umeyapata wapi hayo MAJI YALIYO HAI?
12 Je! Wewe u mkubwa kuliko baba yetu, Yakobo, aliyetupa kisima hiki, naye mwenyewe akanywa maji yake, na wanawe pia, na wanyama wake?
13 Yesu akajibu, akamwambia, Kila anywaye maji haya ataona kiu tena;
14 walakini ye yote atakayekunywa maji yale nitakayompa mimi hataona kiu milele; BALI YALE MAJI NITAKAYOMPA YATAKUWA NDANI YAKE CHEMCHEMI YA MAJI, YAKIBUBUJIKIA UZIMA WA MILELE.
15 Yule mwanamke akamwambia, Bwana, unipe maji hayo, nisione kiu, wala nisije hapa kuteka”.
Umeona hapo? jinsi Bwana alivyomfafanulia huyo mwanamke kuwa Yale maji anayoyadhania ya kisimani, sio maji ya uzima..Bali maji ya uzima ni kitu kingine kabisa lakini chenye tabia zinazofanana na hayo maji ya asili.
Sasa swali hayo maji ni nini?
Bwana Yesu, yeye mwenyewe alitupa majibu ya swali hili katika kile kitabu cha Yohana.
Yohana 7:37 “ Hata siku ya mwisho, siku ile kubwa ya sikukuu, Yesu akasimama, akapaza sauti yake akisema, Mtu akiona kiu, na aje kwangu anywe.
38 Aniaminiye mimi, kama vile maandiko yalivyonena, MITO YA MAJI YALIYO HAI ITATOKA NDANI YAKE.
39 Na NENO HILO ALILISEMA KATIKA HABARI YA ROHO, ambaye wale wamwaminio watampokea baadaye; KWA MAANA ROHO ALIKUWA HAJAJA, kwa sababu Yesu alikuwa hajatukuzwa”.
Umeona hapo?..Maji ya uzima ni ROHO MTAKATIFU.
Maana yake mtu anayepokea Roho Mtakatifu, anakuwa amekata kiu yote ya dhambi.
Kiu ya kunywa pombe na kuvuta sigara inakufa..kiu ya kufanya zinaa na uasherati inakufa, kiu ya kufanya mabaya inakufa, na mambo mengine yote mabaya..
Kwasababu yeye anatoa raha ambayo inazidi raha zote zinazopatikana katika mambo hayo ya ulimwengu yasiyompendeza yeye..
Ndio maana kuna umuhimu mkubwa sana wa kumpokea Roho Mtakatifu.
Lakini pia jambo la muhimu kufahamu ni kuwa MAJI HAYA YA UZIMA maandiko yanasema TUNAYANUNUA. Lakini si kwa fedha, wala kwa mali..BALI KWA MAISHA YETU!. Yaani tunapompa Yesu maisha yetu, hiyo ni gharama tosha ya kununua maji hayo.
Fedha haiwezi kununua hayo maji..kwasababu si maji ya kimwilini bali ya kiroho.
Isaya 55:1 “Haya, kila aonaye kiu, njoni majini, Naye asiye na fedha; njoni, nunueni mle; Naam, njoni, nunueni divai na maziwa, Bila fedha na bila thamani.
2 Kwani kutoa fedha kwa ajili ya kitu ambacho si chakula? Na mapato yenu kwa kitu kisichoshibisha? Nisikilizeni kwa bidii, mle kilicho chema, Na kujifurahisha nafsi zenu kwa unono”.
Umeona tena hapo??..anasema Njooni MNUNUE bila fedha na si NJOONI MCHUKUE BILA FEDHA. Maana yake hayo maji yananunuliwa lakini si kwa fedha bali kwa kitu kingine..Na hicho si kingine zaidi ya MAISHA YETU. Yaani kumpa yeye na kubatizwa.
Swali ni je??. Umempokea huyu Yesu? Na kubatizwa ubatizo sahihi wa maji tele na kwa Jina la Yesu?..Kumbuka hiyo ndiyo tiketi pekee ya kuyapata hayo maji, hakuna njia nyingine.
Bwana Yesu anasema..
Ufunuo wa Yohana 22:17 “Na Roho na Bibi-arusi wasema, Njoo! Naye asikiaye na aseme, Njoo! Naye mwenye kiu na aje; na yeye atakaye, na ayatwae maji ya uzima bure”.
Je unayataka maji ya uzima leo?
Mwamini Yesu na tubu dhambi zako leo kwa kumaanisha kuziacha, na ukabatizwe kama bado hujafanya hivyo.
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312 Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp
Mada Nyinginezo:
Tusome,
Warumi 3:22 “ni haki ya Mungu iliyo kwa njia ya imani katika Yesu Kristo kwa wote waaminio. Maana hakuna tofauti;
23 kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu;”
Hapo maandiko yanasema “Wote wamefanya dhambi” na sio “Wote wanafanya dhambi”. Ikiwa na maana kuwa kuna dhambi ambayo imeshafanyika huko nyuma ambayo imewafanya wote wawe katika dhambi.
Na dhambi hiyo si nyingine Zaidi ya ile ya Adamu na Hawa. Maandiko yanasema kwa kukosa kwake mtu mmoja Adamu, sisi wote tumeingia katika hali ya kukosa.
Warumi 5:19 “Kwa sababu kama kwa kuasi kwake mtu mmoja watu wengi waliingizwa katika hali ya wenye dhambi, kadhalika kwa kutii kwake mmoja watu wengi wameingizwa katika hali ya wenye haki”.
Umeona?..Kwa dhambi ya Adamu na sisi tunaonekana tumefanya dhambi, kwasababu tulikuwa katika viuno vya Adamu, wakati Adamu anafanya makosa hayo..Hivyo kwa dhambi yake ikafanya vizazi vyake vyote kuwa katika dhambi. Ndio maana wanadamu wote tunazaliwa na dhambi ya asili bila hata ya sisi kutaka, tunazaliwa tayari tukiwa tumepungukiwa na utukufu wa Mungu.
Ndio maana utaona mtoto anazaliwa na hasira, uchoyo, kiburi n.k.. Hiyo ni kutoka na dhambi ya asili aliyoirithi kutoka kwa Adamu. Na ndio maana maandiko yanasema “wote tumetenda dhambi” na sio tunatenda dhambi.
1 Yohana 1:8 “Tukisema kwamba hatuna dhambi, twajidanganya wenyewe, wala kweli haimo mwetu.
9 tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote.
10 Tukisema kwamba hatukutenda dhambi, twamfanya Yeye kuwa mwongo wala neno lake halimo mwetu”.
Na hiyo ndio sababu pia tunamhitaji Bwana Yesu, atuondolee hiyo dhambi ya asili.
Kwasababu Kristo anafananishwa na Adamu wa pili. Maana yake kama Adamu wa Kwanza alivyotuingiza matatizoni sisi wanawe katika vizazi vyote, kadhalika Adamu wa pili (yaani Yesu Kristo), atatuingiza katika hali ya kuwa watakatifu, endapo tukimwamini na kumpokea..
Warumi 5:18 “Basi tena, kama kwa kosa moja watu wote walihukumiwa adhabu, kadhalika kwa tendo moja la haki watu wote walihesabiwa haki yenye uzima.
19 Kwa sababu kama kwa kuasi kwake mtu mmoja watu wengi waliingizwa katika hali ya wenye dhambi, kadhalika kwa kutii kwake mmoja watu wengi wameingizwa katika hali ya wenye haki”.
Pale tunapompokea na tunapotubu dhambi zetu na kupokea kipawa cha Roho Mtakatifu, tunakuwa tumezaliwa mara ya pili, na hivyo ile dhambi ya asili tuliyozaliwa nayo inaondoka. Tunakuwa watakatifu, kwasababu Kristo anashusha nguvu ya kipekee juu yetu ya kutusaidia kushinda dhambi…Hivyo tunajikuta tunaishi maisha ya utakatifu na usafi bila sheria.
1Yohana 3:9 “Kila mtu aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi, kwa sababu uzao wake wakaa ndani yake; wala hawezi kutenda dhambi kwa sababu amezaliwa kutokana na Mungu”
Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba, wote walio ndani ya Kristo, dhambi haiwatawali, kwasababu wameuvua utu wa kale na kuvaa utu upya.
2Wakorintho 5:17 “Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita tazama! Yamekuwa mapya”.
Na ndio maana maandiko pia yanatuonyesha kuwa watakatifu waliopo duniani ndio wanaompendeza Mungu..ikimaanisha kuwa duniani kuna watakatifu.
Zaburi 16:3 “Watakatifu waliopo duniani ndio Walio bora, Hao ndio niliopendezwa nao”.
Je! Na wewe ni Mtakatifu?.. Umempokea Yesu na kutubu na kubatizwa ubatizo sahihi?. Kama bado kumbuka Kristo yupo mlangoni, na atakaporudi atawachukua tu wale wateule wake na kwenda nao mbinguni, yaani wale wote waliozaliwa mara ya pili, na kuishi maisha ya utakatifu. Lakini wengine waliosalia ambao hawamtaki yeye watatupwa katika lile ziwa la moto.
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
https://wingulamashahidi.org/2018/07/04/5-swali-je-kuna-dhambi-kubwa-na-ndogo-na-kama-hakuna-je-mtu-aliyeua-na-aliyetukana-je-watapata-adhabu-sawa/
Jina la Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo libarikiwe. Karibu tujifunze biblia Neno la Mungu wetu.
Maandiko yanasema kuwa wapo watatu washuhudiao mbinguni, na vile vile wapo watatu washuhudiao duniani.
1Yohana 5:7 “Naye Roho ndiye ashuhudiaye, kwa sababu Roho ndiye kweli.
8 Kwa maana wako watatu washuhudiao [mbinguni, BABA, NA NENO, NA ROHO MTAKATIFU, na watatu hawa ni umoja.
9 Kisha wako watatu washuhudiao duniani], ROHO, NA MAJI, NA DAMU; na watatu hawa hupatana kwa habari moja. Tukiupokea ushuhuda wa wanadamu, ushuhuda wa Mungu ni mkuu zaidi; kwa maana ushuhuda wa Mungu ndio huu, kwamba amemshuhudia Mwanawe”.
Lakini swali la kujiuliza ni je!, hao watatu NI WAKINA NANI na WANASHUHUDIA NINI na WANASHUHUDIAJE?
Kama ukianzia juu kidogo katika habari hiyo utaona Mtume Yohana alikuwa anajaribu kuelezea habari za ushuhuda wa Yesu kuwa ndiye “Mwana wa Mungu”. Alikuwa anajaribu kuelezea kuwa habari ya kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu, sio jambo la kutunga tu!, bali mbingu na nchi zimelishuhudia hilo. Na akawa anajaribu kueleze vitu vikuu vilivyoshuhudia au kulithibitisha hilo, vilivyopo duniani na vilivyopo mbinguni..
Na vitu hivyo ndio Mtume Yohana kwa ufunuo wa Roho anaviorodhesha. Kwamba kwa duniani ni ROHO, MAJI na DAMU.. Na kwa mbinguni ni BABA, NENO na ROHO. Sasa ni kwa namna gani vitu hivi vinashuhudia
1Yohana 5:5 “Mwenye kuushinda ulimwengu ni nani, isipokuwa ni yeye aaminiye ya kwamba YESU NI MWANA WA MUNGU?
6 Huyu ndiye aliyekuja kwa maji na damu, Yesu Kristo; si katika maji tu, bali katika maji na katika damu.
7 Naye Roho ndiye ashuhudiaye, kwa sababu Roho ndiye kweli”.
Hebu tuanze kuutazama Ushuhuda kutoka mbinguni.
Tusome.
Mathayo 3:16 “Naye Yesu alipokwisha kubatizwa mara akapanda kutoka majini; na tazama, mbingu zikamfunukia, akamwona ROHO WA MUNGU akishuka kama hua, akija juu yake;
17 na tazama, SAUTI KUTOKA MBINGUNI IKISEMA, HUYU NI MWANANGU, MPENDWA WANGU, ninayependezwa naye”.
Hapo tunaona vitu vitatu vimeshirikiana kumshuhudia Kristo kama ni Mwana wa Mungu. Cha kwanza ni SAUTI ambayo ndio NENO. (Huyu ni Mwanangu mpendwa wangu). Cha pili ni BABA ambaye ndiye kazungumza maneno hayo, na cha tatu ni ROHO ambaye ndiye kashuka juu yake kama Hua (yaani njiwa)..kuyathibitisha maneno ya Baba.
Kwahiyo unaweza kuona hapo BABA, kazungumza NENO kutoka mbinguni, kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu kweli, na Kamshusha ROHO wake kulithibitisha neno lake hilo.
Hivyo kutimiza hilo Neno linalosema wapo watatu washuhudiao mbinguni BABA, NENO na ROHO.
Lakini Sehemu ya pili inasemaje?.. Wapo watatu pia washuhudiao duniani, nao ni ROHO, DAMU NA MAJI..Sasa ni kwa namna gani hawa wanashuhudia kuwa ni kweli Yesu ni Mwana wa Mungu, kama vile Baba alivyoshuhudia kwa Neno na Roho?.
Tusome,
Yohana 19:33 “Lakini walipomjia Yesu na kuona ya kuwa amekwisha kufa, hawakumvunja miguu;
34 lakini askari mmojawapo alimchoma ubavu kwa mkuki; na mara IKATOKA DAMU NA MAJI.
35 NAYE ALIYEONA AMESHUHUDIA, NA USHUHUDA WAKE NI KWELI; naye anajua ya kuwa anasema kweli ili ninyi nanyi mpate kusadiki”.
Umeona hapo?. Huyu Askari alipofika kwa Bwana Yesu na kumchoma ubavuni kwa mkuki, akashangaa kuona MAJI mengi yanatoka, jambo ambalo sio la kawaida, na baadaye inatoka DAMU. Kwa ishara ile Askari yule akakiri ya kwamba YESU NI MWANA WA MUNGU, na hapo Mtume Yohana anatia msisitizo kuwa “huyo Askari aliyeona ameshuhudia na ushuhuda wake ni kweli”.
Sasa utauliza mbona hapo maandiko hayajaonyesha kama Askari huyo kashuhudia kwamba YESU NI MWANA WA MUNGU kwa tukio hilo?.
Jibu ni kwamba alishuhudia hilo, na kukiri kwamba YESU NI MWANA WA MUNGU Baada ya kulishuhudia tukio hilo la kifo cha Yesu.Tunaweza kusoma habari hiyo vizuri tena katika kitabu cha Marko..
Marko 15:39 “Basi yule akida, aliyesimama hapo akimwelekea, alipoona ya kuwa alikata roho jinsi hii, akasema, Hakika mtu huyu alikuwa Mwana wa Mungu”.
Kwahiyo MAJI na DAMU vilivyotoka katika mwili wa Bwana Yesu, Na SAUTI (yaani NENO) la BABA, lililoshuka juu yake wakati anabatizwa. VINASHUHUDIA KUWA YESU NI MWANA WA MUNGU. Kadhalika Maji yaliyotoka ubavuni mwa Yesu, na Damu yake iliyomwagika Kalvari, vinatushuhudia kuwa Yesu ni Mwana wa Mungu.
Ndio maana na sisi ili Baba atushuhudie kuwa ni WANA WA MUNGU, kama alivyomshuhudia mwanaye ni lazima na sisi tuwe na ushuhuda wa MAJI, na ROHO na DAMU tukiwa hapa duniani.
Maana yake ni kwamba lazima tubatizwe kwa MAJI na kwa ROHO MTAKATIFU na kutakaswa kwa DAMU. Tusipofanya hivyo sisi sio wana wa Mungu mbele za Baba mbinguni na wala hatatushuhudia. Bwana Yesu aliposhuka pale Yordani kubatizwa kwa MAJI na ROHO aliposhuka juu yake ndipo sauti ikasikika kuwa yeye ni mwana wa Mungu. Na sisi ni hivyo hivyo, ni lazima tuwe na ushuhuda huo wa kubatizwa kwa maji na kwa Roho Mtakatifu, ili Damu ya Yesu iweze kutusafisha.. kutushuhudia kuwa sisi ni wana wa Mungu.
Yohana 3:5 “Yesu akajibu, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa kwa maji na kwa Roho, hawezi kuuingia ufalme wa Mungu”.
Leo hii ubatizo unapuuziwa sana na wengi ni kwasababu bado hawajaelewa ufunuo uliopo katika ubatizo.
Ukielewa ufunuo uliopo katika ubatizo, ndipo utajua hicho kitu ni cha umuhimu kiasi gani.. Ilimpasa Kristo abatizwe ili sauti ije juu yake kuwa yeye ni Mwana wa Mungu, inatupasaje sisi?.. Ubatizo ni tendo dogo lakini lina madhara makubwa sana katika Roho.
Na kumbuka ubatizo halisi na wa kweli, si ule wa vichanga bali ni lazima mtu ajitambue na kuamua kukiri kwa kinywa chake, Bwana hakushindwa kubatizwa wakati akiwa na siku nane, kipindi anakwenda kutahiriwa.. vyote hivyo viwili vingeweza kwenda pamoja.. Lakini ilimpasa awe mtu mzima kwanza.
Vile vile ubatizo sahihi ni kwa jina la BWANA YESU KRISTO, kulingana na Matendo 2:38, Matendo 8:16, Matendo 10:48, na Matendo 19:5.
Bwana atufumbue macho tuzidi kumwelewa.
Maran atha.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
Jibu: Tusome,
Kumbukumbu 23:18 “Usilete ujira wa kahaba, wala mshahara wa mbwa, katika nyumba ya Bwana, Mungu wako, kwa ajili ya nadhiri yo yote; kwani haya ni machukizo kwa Bwana, Mungu wako, yote mawili”.
Neno “Mbwa” kama linavyotumika hapo, linamaanisha “Mwanaume anayejiuza mwili wake”, kwa lengo la kupata fedha, kama vile mwanamke anayejiuza anavyojulikana kama Kahaba, vivyo hivyo mwanaume anayejiuza alijulikana kama “mbwa”.
Na kujiuza huko kuko kwa namna mbili. Namna ya kwanza ni mwanaume anayejiuza kwa wanawake, na namna ya pili, ni mwanaume anayejiuza kwa wanaume wenzake (yaani Hanithi). Makundi haya yote mawili yanajulikana kama “mbwa” kibiblia.
Hivyo Mungu alikataza kwa mtu yeyote awe mwanamke au mwanaume anayejiuza mwili wake na kupata fedha, asizilete hizo fedha katika nyumba ya Mungu kama sadaka, kwaajili ya nadhiri, na si tu nadhiri bali pia kama sadaka!..kwani ni machukizo mbele zake.
Mithali 15: 8 “Sadaka ya mtu mbaya ni chukizo kwa Bwana; Bali maombi ya mtu mnyofu ni furaha yake”.
Kwahivyo biblia inatufundisha kuwa Utakatifu ndio sadaka ya kwanza kwa Mungu wetu..Maana yake tusipokuwa watakatifu wa mwili na roho, na tukaenda kumtolea sadaka, huku hatutaki wala hatuna mpango wa kubadilika, bado ni wazinzi, bado ni waasherati, bado ni makahaba, bado ni wachawi, bado ni watu tuliojaa vinyongo na chuki..basi tujue kuwa sadaka ile tunayokwenda kuitoa ni machukizo makubwa sana kwa Bwana. Kwasababu kitu cha kwanza Bwana anachotafuta kwetu si PESA, wala SADAKA, bali anataka tuwe wakamilifu, anataka tupate Rehema..
Mathayo 9:13 “Lakini nendeni, mkajifunze maana yake maneno haya, NATAKA REHEMA, WALA SI SADAKA; kwa maana sikuja kuwaita wenye haki, bali wenye dhambi”.
Bwana Yesu mwenyewe alitupa ushauri mzuri, wa namna ya kumtolea Mungu..kwamba tujitakase kwanza kabla ya kwenda kumtolea yeye, ili sadaka yetu ikubalike na iwe na matokeo. Na kujitakasa huko sio kujitakasa leo, na kesho kurudia yale yale..bali ni kule kwa badiliko la kudumu ndani yetu..
Mathayo 5:23 “Basi ukileta sadaka yako madhabahuni, na huku ukikumbuka ya kuwa ndugu yako ana neno juu yako,
24 iache sadaka yako mbele ya madhabahu, uende zako, upatane kwanza na ndugu yako, kisha urudi uitoe sadaka yako”.
Kinyume chake tukimtolea sadaka na huku hatuna mpango wa kuacha maisha yetu mabaya ya dhambi, tufahamu kuwa sadaka zetu hazitakubaliwa na zaidi ya yote hatutaurithi uzima wa milele..Na maandiko yanasema wazi kuwa waasherati na MBWA hawataurithi uzima wa milele.
Ufunuo 22:14 “Heri wazifuao nguo zao, wawe na amri kuuendea huo mti wa uzima, na kuingia mjini kwa milango yake.
15 Huko nje wako mbwa, na wachawi, na wazinzi, na wauaji, na hao waabuduo sanamu, na kila mtu apendaye uongo na kuufanya”
Bwana atubariki na kutujalia neema zake.
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
Kwanini Bwana aliwalenga mbwa na nguruwe tu katika Mathayo 7:6?
Ulishawahi kujiuliza hoja ya msingi shetani aliyotumia kumshitakia Yesu mpaka kufanikiwa kumpeleka msalabani ilikuwa ni ipi?
Tukilifahamu hilo tutaelewa ni wapi ibilisi anapandaa ili kuwaletea dhiki wakristo katika siku za mwisho.
Ukisoma biblia utaona Wakati ule wayahudi wanatafuta sababu nyingi sana za kumshitaki Bwana Yesu lakini hawakuziona, mpaka dakika za mwisho mwisho wakatokea na hoja nyingine moja, ambayo ilikuwa na mashiko sana kwao..
Na hoja yenyewe ilikuwa ni katika lile HEKALU.
Mathayo 26:59 “Basi wakuu wa makuhani na baraza yote wakatafuta ushuhuda wa uongo juu ya Yesu, wapate kumwua;
60 wasiuone wangawa walitokea mashahidi wa uongo wengi.
61 Hata baadaye wawili wakatokea, wakasema, Huyu alisema, Naweza kulivunja hekalu la Mungu, na kulijenga kwa siku tatu.
Nataka ujifunze jambo moja, kulikuwa na kauli nyingi sana zenye makwazo ambazo wayahudi wangeweza kuzisimamia kumuulia Yesu, kwamfano alipowaita wao ni wa baba yao Ibilisi na sio Ibrahimu(Yohana 8:44). Kwa kauli kama hiyo kwamfano ingetosha tu kumfanya wamuue. Lakini sio hiyo ya kusema “Bomoeni hili Hekalu nami nitalijenga ndani ya siku tatu…”
Ulishawahi kujiuliza, kwanini kauli hiyo ilipata nguvu?
Hilo ni jambo ambalo shetani alijaribu kulijenga tangu zamani za akina Zerubabeli katika ujenzi wa Hekalu, kama wewe ni msomaji wa biblia, utakumbuka kuwa kipindi wanalijenga Hekalu la pili, maadui zao (ambao hawakuwa wayahudi) waliomba waungane nao ili kulijenga hekalu la Mungu, lakini Zerubabeli na wenzake kwa ufunuo wa Roho, wakawakatalia, kwasababu walijua madhara yake yatakayokuja huko baadaye (Ezra 4:3)..
Lakini muda mrefu ulipopita mamia ya miaka, hekalu hilo lilichakaa, likawa kama limepitwa na wakati, kwa ujenzi wake. Hapo ndipo akatokea mtawala mmoja wa ki-Rumi aliyeitwa HERODE, Akaomba alikarabati hekalu lile,. Sasa wayahudi bila ya Kutaka kumuuliza Mungu, wakakurupuka wakamruhusu, hivyo Herode akaanza kulikarabati tena, akalijenga kwa fedha nyingi sana na kwa muundo wa kisasa.
Muda alioutumia kukarabati ulizidi hata muda uliotumika kujenga Hekalu lile, kwani Herode alitumia miaka 46 kulikarabati, (Soma Yohana 2:20 utaona), wakati wakina Zerubabeli walitumia miaka isiyozidi 7. Na alifanikiwa kulipamba kweli kweli, mpaka wakati Fulani mitume wakaenda kumuonyesh Bwana uzuri wa jengo hilo jinsi lilivyopambwa vizuri.
Sasa kitendo kile kilikuwa na agenda ya ibilisi nyuma yake. Kwasababu alijua upo wakati Masihi atakuja, na ataingia katika hekalu lile na kuwafundisha watu sheria za Mungu, Hivyo akatumia nguvu zake nyingi sana kutafuta namna ya kupalimiliki. Ndipo hapo akamwingia Herode, ambaye roho ya mpinga-Kristo ilikuwa nyuma yake, mtu ambaye alikuwa hana hata upendo na Mungu, na ndio maana wakati tu Kristo anazaliwa badala afurahie mwokozi kaja ulimwenguni, kinyume chake akatuma watu kwenda kumuangamiza, lakini cha ajabu ndio mtu huyo huyo aliyelikarabati Hekalu la Mungu.
Sasa kwasababu yeye ndiye aliyelitengeneza upya. Mamlaka yote ikahamia mikononi mwake kutoka kwa wayahudi, wayahudi wakawa hawana la kusema, hapo ndipo akaanzisha biashara kubwa kubwa sana , ndani ya hekalu, akalifanya pia kuwa kama eneo la kitalii, la watu kuja kushangaa uzuri wake.
Vilevile kukawekwa sheria kali, mtu yeyote akitaka kufanya jambo, au kuleta mfumo mpya ni lazima kwanza apokee kibali kutoka kwa HERODE, vinginevyo utaonekana kama ni muhalifu, na msaliti, ambaye anastahili adhabu ya kifo.
Kwahiyo, hakukuwa na mtu aliyeweza kufumbua kinywa chake, kukemea jambo lolote baya lililofanyika katika hekalu la Mungu takatifu, kwa hofu ya Herode na wayahudi. Hivyo hiyo ikaifanya hali ikaendelea kuwa mbaya kupindukia hadi wakati Kristo anatokea dunia,
Ibilisi alijua kabisa, mwisho wa Siku Bwana Yesu, ni lazima aje aingie katika hekalu lake takatifu. Na kweli wakati ulifika akaingia, ndipo akasambaratisha biashara zote, na shughuli zote zilizokuwa zinaendelea ndani ya Hekalu.
Wayahudi kuona vile, wakadhani maagizo hayo kapewa na Herode ndipo walipomuuliza…..
Luka 20:2 “wakamwambia, wakisema, Tuambie, unatenda mambo hayo kwa mamlaka gani? Tena, ni nani aliyekupa mamlaka hii?”
Na baada ya kugundua kuwa hakuyapokea Kwa Herode, hapo ndipo wakajua mtu huyu ni msaliti, na gaidi, anataka kutuletea harufu mbaya duniani, ili sisi tuonekane kama waasi, ni lazima tumuue.
Ndipo wakamshitakia kwa kitendo chake kile, na kauli ile.
Nachotaka tuone ni kwamba. Shetani anafahamu kuwa Kristo yupo mlangoni kurudi tena mara pili kulinyakua kanisa lake takatifu. Hivyo alichokifanya tangu kile kipindi cha mitume hadi sasa ni kujiingiza kwa siri , ili kujifanya kama analisaidia kanisa la Mungu..
Lakini lengo lake sio Kristo, na ndio maana utaona sasa, madhehebu mengi ya uongo, yamefanikiwa sana, lakini ukijaribu kuchunguza mifumo yao utaona ipo mbali sana na biblia.
Ukiuliza ibada za sanamu za kumwomba bikira Maria zipo wapi kwenye biblia, au kwenda toharani tunakupata wapi, utaishia kuonekana ni msaliti, na gaidi, msambaza, chuki. Shetani sikuzote hataki mfumo wake mbovu kuhojiwa.. Hataki kwasababu anajua pale sio mahali pake.
Leo hii, bado hajapokea nguvu kamili,za kuleta uharibifu kwa watu, wakati unafika atapokea nguvu ya kuleta mauaji kwa wale wakristo ambao UNYAKUO utakuwa umewapita. Atataka kuwaondosha wote asibakie mtu.
Je! Umeokoka ndugu yangu? Au bado unajisifia dini na madhehebu? Hautanyakuliwa kwa dhehebu lako zuri, utanyakuliwa kwa kukamilishwa katika wokovu, yaani kutubu na kubatizwa na kupokea Roho Mtakatifu, na kuishi katika utakatifu. Tubu leo kama hujatubu, Kumbuka wakati wowote Kristo anarudi.
Maran Atha.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
Je! Wokovu umekufikia?
Wengi wanasema wamepata wokovu lakini kiuhalisia wokovu bado haujawafikia.
Leo napenda tujifunze juu ya viashiria vinavyorhibitisha kuwa wokovu umetufikia, au umefika nyumbani kwetu.
Tusome habari za mtu mmoja aliyeitwa Zakayo, ambaye kupitia yeye tutajua kama wokovu na sisi umefika nyumbani kwetu au la!
Luka 19:1-10
“1 Naye alipoingia Yeriko alipita katikati yake.2 Na tazama, palikuwa na mtu, jina lake Zakayo, mkubwa mmoja katika watoza ushuru, naye ni tajiri.
3 Huyu alikuwa akitafuta kumwona Yesu ni mtu wa namna gani, asiweze kwa sababu ya umati wa watu, maana ni mfupi wa kimo.
4 Akatangulia mbio, akapanda juu ya mkuyu apate kumwona, kwa kuwa atakuja kuipitia njia ile.
5 Na Yesu, alipofika mahali pale, alitazama juu, akamwambia, Zakayo, shuka upesi, kwa kuwa leo imenipasa kushinda nyumbani mwako.
6 Akafanya haraka, akashuka, akamkaribisha kwa furaha.
7 Hata watu walipoona, walinung’unika wote, wakisema, Ameingia kukaa kwa mtu mwenye dhambi.
8 Zakayo akasimama, akamwambia Bwana, Tazama, Bwana, nusu ya mali yangu nawapa maskini, na ikiwa nimenyang’anya mtu kitu kwa hila namrudishia mara nne.
9 Yesu akamwambia, Leo wokovu umefika nyumbani humu, kwa sababu huyu naye ni mwana wa Ibrahimu.
10 Kwa kuwa Mwana wa Adamu alikuja kutafuta na kuokoa kile kilichopotea”.
Nataka tuuone huo mstari wa 8, ni kitu gani Zakayo alichokifanya kikamsababisha mpaka Mwokozi Yesu aseme.. “Leo Wokovu umefika nyumbani humu”
Na kitu chenyewe ndicho hicho tunachokisoma..huo mstari wa 8.
“8 Zakayo akasimama, akamwambia Bwana, Tazama, Bwana, nusu ya mali yangu nawapa maskini, na ikiwa nimenyang’anya mtu kitu kwa hila namrudishia mara nne.”
Umeona?..Zakayo alijiona yeye ni mwenye dhambi, na kutubu…lakini aliona toba ya midomo peke yake haitoshi, na ilihali mali nyingi alizonazo ni kutokana na kuwadhulumu watu..akaona aib mbele za Bwana na vile vile moyo wake ukamchoma.
Alichofanya alitoa nusu ya mali yake yote iliyo ya halali na kuwapa masikini, na zaidi ya yote, wale wote aliowadhulumu aliwarudishia mara 4,.
Maana yake ni kwamba kama kuna kiwanja alimdhulumu mtu, alimrudishia mara 4, maana yake viwanja 4..
Kama kuna fedha alimdhulumu mtu, alimrudishia mara 4..
Na huo moyo wa toba yenye matendo ndio Bwana aliokuwa anauhitaji.. Na Bwana ndio akamwambia maneno yale “Leo wokovu umefika nyumbani humu”
Hebu jiulize leo ndugu, tangu umempokea Yesu, vile vitu vya wizi ulivyoiba, umemrudishia mwenyewe?..au umetubu tu kwa mdomo na kuishia hapo, na kuendelea kuwa navyo?
Zile mali za dhuluma ulizozipata bado unafurahia kukaa nazo baada ya kuokoka?..Zakayo hakuona vyema kukaa nazo, aliona aibu mbele za Bwana na alipoziondoa na ndipo Wokovu ulipoingia nyumbani mwake.
Sisi tunaonaje raha kubakiwa na simu za wizi?, Kubakiwa na fedha za dhuluma, kubakiwa na heshima wa hila n.k
Bwana wetu hafurahiwi na toba za midomo tu!..bali na za matendo,
Tunapotubu ni lazima na maisha yetu yabadilike, hata watu wa nje waone kweli pale pana mtu aliyebadilika, watu wa nje hawashawishiki kwa maneno ya midomo tu, ndipo waamini kuwa tumebadilika..wanashawishika wanapoona umewarudishia vile ulivyowadhulumu.
Kadhalika hawatashawishika kusikia kuwa umetubu kwa mdomo huku mavazi yako na mwonekano wako ni bado ule ule wa kikahaba au kihuni.
Wakikuona bado unavaa nguo za kubana, bado unavaa vimini, bado unajipamba uso kama Yezebeli, haijalishi unahudhuria kanisani kila siku kiasi gani..bado watakuona wewe ni kahaba na muhuni tu.
Wakisikia umetubu lakini bado huyo mke uliye naye si wako ni wa mtu mwingine, huyo mume uliye naye si wako ni wa mtu mwingine, hawashawishiki hata kidogo..na zaidi ya yote Kristo hakujui.
Tunapotubu hatuna budi kuzaa matunda yanayotokana na toba zetu hizo..
Mathayo 3:8-10
“ 8 Basi zaeni matunda yapasayo toba;9 wala msiwaze mioyoni mwenu kwamba, Tunaye baba, ndiye Ibrahimu; kwa maana nawaambia ya kwamba Mungu aweza katika mawe haya kumwinulia Ibrahimu watoto.
10 Na shoka limekwisha kuwekwa penye mashina ya miti; basi kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa motoni”.
Je! Toba yako ina matunda?
Kama bado basi ni wakati wa kuanza upya, kama ni mwanamke baada ya kutubu weka mbali vipodozi vyote, kaa mbali na dhuluma na biashara haramu..na kama ni mwanamume ni hivyo hivyo, kuviondoa vyote ulivyovipata kwa dhuluma na kujitenga na udunia.
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
SWALI: Mtume Paulo alikuwa anamaanisha nini aliposema..”Wengine wanahubiri habari za Kristo kwa sababu ya husuda na fitina; na wengine kwa nia njema.”(Wafilipi 1:15)? Huko kuhubiri injili kwa husuda ndio kukoje?
JIBU: Ili kuelewa Paulo alimaanisha nini ni vema tukaisoma habari yote tokea juu..
Wafilipi 1:12-18
[12]Lakini, ndugu zangu, nataka mjue ya kuwa mambo yote yametokea zaidi kwa kuieneza Injili;
[13]hata vifungo vyangu vimekuwa dhahiri katika Kristo, miongoni mwa askari, na kwa wengine wote pia.
[14]Na wengi wa hao ndugu walio katika Bwana, hali wakapata kuthibitika kwa ajili ya kufungwa kwangu, wamezidi sana kuthubutu kunena neno la Mungu pasipo hofu.
[15]Wengine wanahubiri habari za Kristo kwa sababu ya husuda na fitina; na wengine kwa nia njema.
[16]Hawa wanamhubiri kwa pendo, wakijua ya kuwa nimewekwa ili niitetee Injili;
[17]bali wengine wanamhubiri Kristo kwa fitina, wala si kwa moyo mweupe, wakidhani kuongeza dhiki za kufungwa kwangu.
[18]Yadhuru nini? Lakini kwa njia zote, ikiwa ni kwa hila, au ikiwa ni kwa kweli, Kristo anahubiriwa; na kwa hiyo nafurahi, naam, nami nitafurahi.
Waraka huu Paulo aliuandika akiwa gerezani..Sasa akiwa huko kifungoni kulizuka makundi mawili ya watu ambao walianza kuihubiri injili kama ile ile aliyoihubiri..
Kundi la kwanza lilikuwa na Nia njema kwa Bwana kama ile aliyokuwa nayo Paulo. Kuzihurumia roho za watu na kuifanya kazi ya injili kwa kujitoa kwa upendo bila kujali kama wanapata faida yoyote au la..
Lakini kundi la pili lilikuwa la tofauti..lilianza kuhubiri kwalengo la kumkomoa Paulo na kutaka kujionyesha kuwa na wao wana mamlaka kama yake..N hiyo yote ni kwasababu ya kukua na kujulikana sana kwa huduma ya Paulo ulimwenguni..Hivyo wivu ulipowajaa wakatumia fursa ya kufungwa kwake kuhubiri injili kwa lengo la kumuonyesha Paulo hana chochote cha ziada kushinda wao.
Na wengine wakawa wanahubiri huku wakimnenea habari mbaya ili tu kumzidishia vifungo vyake kwa maaskari.
Lakini cha ajabu ni kuwa taarifa hizo zilipokewa tofauti na Paulo..badala ya kuchukia ndio kwanza akafurahia..kwasababu hata kwa njia hiyo injili inahubiriwa na watu wanaokoka..
Ni jambo gani tunaweza kujifunza kwa Paulo na hao wahubiri injili kwa fitina..
Hiyo ni kuonyesha kuwa injili inaweza kuhubiriwa na mtu yeyote na ikaleta matokeo yale yale ya wokovu..hata sasa wapo wahubiri wengi wa uongo wanawavuta watu wa Kristo..lakini hilo haliwafanyi wao kupokelewa na Kristo siku ile ya hukumu..
Bwana Yesu aliliweka wazi hilo katika;
Mathayo 7:21-23
[21]Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.
[22]Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi?
[23]Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu.
Hivyo tuwe makini na kuhubiri kwetu..Je Nia yetu ni kwa Bwana? au kwa lengo la kushindana na mtumishi fulani au mtume fulani au mchungaji fulani au nabii fulani…
Vivyo hivyo…Sisi kama wahubiri hatuna haja ya kurudisha mashambulizi pale tunapoona watumishi wa uongo wanashindana nasi..ikiwa injili wanayoihubiri ni ya kweli basi sisi tufurahie matunda kama alivyofanya Paulo..hayo mengine tumuchie Mungu atayahukumu mwenyewe siku ile..
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
Ni kwa namna gani malaika wa mbinguni wanaweza kutuhubiria sisi injili?
Je! Watu ambao hawajawahi kusikia injili kabisa siku ya mwisho watahukumiwa?
Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe, karibu tujifunze biblia neno la Mungu wetu, ambalo ni taa iongozayo miguu yetu na Mwanga wa njia yetu.
Leo tutajifunza juu ya mtu mmoja aliyeitwa Theofilo, ambaye biblia haijaeleza habari zake kwa urefu lakini amehusika pakubwa sana katika kuieneza injili.
Lakini kabla ya kwenda kumtazama huyu Theofilo hebu tuweke msingi kidogo kwa kuelewa juu ya baadhi ya nyaraka za kwenye biblia.
Katika maandiko hususani agano jipya tunaona nyaraka kadhaa, zikiandikwa kwa watu fulani, ambazo hizo zimekuwa msaada hata kwetu sisi wa nyakati hizi.
Kwamfano tunaona waraka ambao Paulo alimuandikia Timotheo, au Tito au Filemoni…Nyaraka hizo zilikuwa zinawasaidia hao watu kuwajenga na kuwaimarisha katika utumishi wao, lakini tunaona Mungu aliziruhusu zienee na kusomwa na watu wengi hata mpaka wakati wetu huu.
Hawa wakina Tito, Filemoni, na Timotheo hawakujua kuwa barua hizo walizotumiwa na Paulo zitakuja kusomwa na maelfu ya vizazi mbeleni..wao pamoja na Paulo hawakulijua hilo.
Ni sawa na wewe leo umwandikie Barua ndugu yako aliyeko mbali, lakini ipite miaka mingi sana huko mbele uje usikie hiyo barua uliyomuandikia inasomwa duniani kote..bila shaka utashangaa…Ndivyo ilivyokuwa kwa Paulo na hawa wakina Timotheo, Tito na Filemoni..waliandikiana barua wao kwa wao kwa lengo la kuimarisha utumishi wao.. lakini kumbe Mungu alikuwa ana malengo makubwa sana na hizo barua..
Hapa tumechukua mifano ya hawa watatu Timotheo, Tito na Filemoni kwasababu ndio wanaojulikana sana..
Lakini pia katika maandiko pia kulikuwa na mtu mwingine wa kipekee sana, ambaye hajulikani sana lakini alichangia pakubwa sana katika uandishi wa vitabu vya biblia.. mtu huyu si maarufu sana ukilinganisha na hawa wakina Timotheo..
Na mtu huyo si mwingine zaidi ya THEOFILO MTUKUFU.
Kama vile kulivyokuwa na waraka wa kwanza na wa pili Paulo aliomwandikia Timotheo, kulikuwepo pia na waraka wa kwanza na wa pili kwa Luka aliomwandikia huyu mtu anayeitwa Theofilo.
Wengi wetu hatujui kuwa kitabu cha Luka na cha Matendo ya Mitume, ni nyaraka maalumu kwa mtu Fulani, hazikulengwa kwa watu wote, au kwa kanisa kwa ujumla…bali zilikuwa ni barua maalumu kwa mtu Fulani ambaye ndiye huyu Theofilo, yaani maana yake ni kwamba kitabu cha Luka na Matendo ya Mitume.. kwa lugha nyingine kingeweza kuitwa Waraka wa Kwanza kwa Theofilo, na waraka wa pili kwa Theofilo..Kwasababu vitabu hivyo viwili vilikuwa ni waraka kwa Theofilo kama kitabu cha Timotheo wa kwanza na wa pili.
Sasa huyu Theofilo alikuwa ni nani?
Kwa ufupi ni kwamba huyu Theofilo, alikuwa ni mkuu fulani, ambaye inasemekana alikuwa Mrumi, na wala hakuwa myahudi. Alikuwa ni mtu mwenye cheo, lakini alikuwa ni mtu wa kipekee sana.
Kwani ulifika wakati akasikia habari zinazomhusu Yesu, na Mitume wake pamoja na Paulo. Lakini hakuwa na uhakika nazo, huku anasikia hichi kule anasiki kile n.k Kipindi anasikia hizo habari, tayari Bwana Yesu ameshaondoka na Mtume Paulo alikuwa ameshakuwa mzee sana, na Mitume walikuwa wameshatawanyika duniani kote..
Hivyo alichikifanya kwasababu alikuwa ni mtu mkubwa, na mwenye cheo, kwa hekima alikwenda kumtafuta mtu mmoja anayeitwa Luka ambaye alikuwa anatembea sana na Mtume Paulo katika safari zake.
Na lengo la kumtafuta huyu Luka ni ili apate taarifa za kutosha na uhakika wa mambo aliyokuwa anayasikia na kuambiwa na watu yamhusuyo Yesu na Mitume wake. Hivyo akamsihi na kumwomba amuandikie kwa waraka mambo yote, tukio moja baada ya lingine tangu kuzaliwa kwa Yesu, kupaa kwake na Matendo yake yote, pamoja na matendo yote ya Mitume.
Hatujui alimsapoti Luka kwa kiwango gani, kwaajili ya kuifanikisha hiyo kazi, lakini aliifanya kwa moyo.
Na Luka kwasababu alikuwa ni mmoja wa watu waliokuwa wanapenda Mungu na mwenye elimu kubwa ya ufalme wa Mungu, na hata ya kidunia,(kwani alikuwa ni Tabibu) alimuandikia huyu Mtukufu Theofilo, tukio moja baada ya lingine, tangu kuzaliwa kwa Yesu, mpaka kupaa kwake mbinguni, na hakuishia hapo tu..bali akaendelea kumwandikia habari za mitume wake aliowaacha baada ya kupaa kwake..
Akamwandikia matendo yao, jinsi walivyohubiri injili kwa nguvu za Roho na kufanikiwa kuanzia Yerusalemu mpaka mwisho wa dunia.. Na huko huko akamwelezea pia habari za Paulo jinsi alivyoipeleka injili kwa mataifa yote, safari zake na mafanikio yake yote.
Na Luka baada ya kukusanya taarifa hizo na kuziandika, ndipo akamtumia huyu Theofilo nyaraka hizo…Na nyaraka hizo ndizo tunazozisoma leo ambazo ni kitabu cha LUKA NA MATENDO YA MITUME.
Na bila shaka Theofilo baada ya kuzipokea nyaraka hizo mbili, aliridhika pakubwa sana, utata ukaondoka kichwani mwake na akamtukuza Mungu..na kuelewa na kupata uhakika wa mambo yote..
Hebu kwa ufupi tusome muhtasari wa nyaraka hizo Luka alizomwandikia Theofilo, na kisha tuende kutazama ni nini tunachoweza kujifunza kutoka kwa huyu mtu.
Luka 1:1 “Kwa kuwa watu wengi wametia mikono kutunga kwa taratibu habari za mambo yale yaliyotimizwa katikati yetu,
2 kama walivyotuhadithia wale waliokuwa mashahidi wenye kuyaona, na watumishi wa lile neno tokea mwanzo,
3 NIMEONA VEMA MIMI NAMI, KWA KUWA NIMEJITAFUTIA USAHIHI WA MAMBO HAYO YOTE TANGU MWANZO, KUKUANDIKIA KWA TARATIBU, THEOFILO MTUKUFU,
4 UPATE KUJUA HAKIKA YA MAMBO YALE ULIYOFUNDISHWA”.
Huo ni waraka wa kwanza wa Luka aliomwandikia Theofilo Mtukufu..waraka mwingine wa pili ni kama ufuatao..
Matendo 1:1 “ Kitabu kile cha kwanza nalikiandika, THEOFILO, katika habari ya mambo yote aliyoanza Yesu kufanya na kufundisha,
2 hata siku ile alipochukuliwa juu, alipokuwa amekwisha kuwaagiza kwa Roho Mtakatifu wale mitume aliowachagua;
3 wale aliowadhihirishia nafsi yake, kwa dalili nyingi, baada ya kuteswa kwake, ya kwamba yu hai, akiwatokea muda wa siku arobaini, na kuyanena mambo yaliyouhusu ufalme wa Mungu”.
Huo ni waraka wa pili wa Luka aliomwandikia huyu Theofilo.
SASA NI NINI TUNAJIFUNZA KWA THEOFILO?.
Kabla ya kujua ni nini tunajifunza hebu tafakari ni mambo mangapi mazuri na ya kujenga tunayoyapata ndani ya hivyo vitabu viwili vya LUKA na MATENDO YA MITUME?.
Kama wewe ni msomaji wa biblia utajua ni jinsi gani, vitabu hivyo viwili vilivyokuwa vya muhimu na vyenye mafunzo mengi ya kiimani.
Theofilo aliona si vyema kusikia habari za Yesu juu juu tu, alitaka kujua alizaliwaje, katika mazingira gani, ndugu zake ni wakina nani, alihubiri nini, kwa muda gani, na alikufaje, alifufukaje na yupo wapi sasa hivi..Pengine alitaka hivyo kwa ajili ya faida yake na ya watoto wake na ndugu zake..
Lengo ni ili asipelekwe pelekwe na kila upepo wa elimu uliozagaa huko na huko, ili asichukuliwe na upotoshaji unaomhusu Yesu na wanafunzi wake..Hivyo akamtafuta Luka ambaye alikuwa ni mwenye elimu nyingi, na mwanafunzi wa Imani ya kikristo, amwandikie kwasababu aliamini ndiye chanzo salama na sahihi cha taarifa kwa wakati huo.
Na Luka akatimiza kiu yake kwa kumtafutia habari hizo kwa urefu na kumwandikia zote.
Ndio maana hapo Luka unaona anamwambia “NIMEONA VEMA MIMI NAMI, KWA KUWA NIMEJITAFUTIA USAHIHI WA MAMBO HAYO YOTE TANGU MWANZO, KUKUANDIKIA KWA TARATIBU, THEOFILO MTUKUFU”
Na kama tulivyojifunza, huyu Theofilo hakuridhika kusikia habari za Yesu tu! Na matendo yake..bali alizidi kutamani kujua Matendo ya Mitume wa Yesu kwa urefu.. kwani alikuwa anasikia tu habari za Mitume wake juu juu, alikuwa anamsikia tu Paulo, lakini yeye akataka kujua huyu Paulo ni nani, ni jinsi gani alimpokea Yesu, safari zake zilikuwaje, ni nini aliyopitia akiwa safarini, hatua kwa hatua..na Luka akamwandikia habari zote hakuacha kitu!
Hebu jiulize kwa kupitia safari na maisha ya Paulo tunayoyasoma katika kitabu cha Matendo ya Mitume tumejifunza mangapi leo?, Bila shaka ni mengi sana.. tumejifunza kumbe katika safari ya imani kuna kupanda na kushuka, wakati mwingine kuna kupitia dhiki na vifungo n.k.
Hivyo Theofilo kwa kutamani kuyajua hayo, na kutafuta kwa bidii taarifa hizo za Bwana Yesu, imekuwa msaada na kwetu sisi pia.
Kadhalika na sisi tunajunza hayo hayo…
Kwamba hatuna budi kuwa kama Theofilo..kuhusiana na masuala ya ufalme wa Mbinguni..
tunapotia bidii kutafuta kulijua Neno la kweli la Mungu, taarifa zile haziji kutusaidia sisi peke yetu, bali pia wengine, na hata vizazi vijavyo.. kwasababu kwa kutafuta huko..kutakuja kuwafaa wengine na kuwabariki wengine huko mbeleni, na kuwa kumbukumbu bora kwetu.
Unapoona Neno katika maandiko hulielewi kwanini usitafute kwa bidii kulijua na kisha kuliandika au kuwafundisha wengine au watoto wako kwa msaada wa wao?..Leo utaona halina maana lakini hujui Mungu kalikusudia nini mbeleni.
Pengine Theofilo aliutaka ule waraka kwa faida yake tu na watoto wake, kumbe Mungu alikuwa na mpango na huo waraka kwa mamilioni ya watu huko mbeleni. Hata sisi kuna mambo ambayo tunaweza kuyafanya sasa, tukidhani yanaishia hapa tu kumbe Mungu ana malengo nayo kuwa msaada kwa maelfu ya watu mbeleni..
Hebu jiulize ni taji kubwa kiasi gani alilonalo huyu Theofilo?.. ambaye hata hakuwa Myahudi?..
Siku ile atasimama na kumwambia Bwana kwa utafiti wake na bidii yake ya kutaka kujua habari za Kwake na Mitume wake, imekuwa Baraka watoto wake na ndugu zake, lakini Bwana atamwonyesha mabilioni ya watu katika vizazi vya mbeleni waliobarikiwa kwa jitihada yake hiyo..
Kwasasa huyu Theofilo hajui chochote kwasababu kalala, lakini siku ya ufufuo, ndipo atakapojua jinsi thawabu yake ilivyo kubwa..Na naamini kama angejua angetafuta pia habari nyingine nyingi ili apate taji bora zaidi.
Kwa bidii yake kitabu cha Luka na Matendo ya Mitume kimeweza kuwepo!.
Mathayo 8:11 “Nami nawaambieni, ya kwamba wengi watakuja kutoka mashariki na magharibi, nao wataketi pamoja na Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo katika ufalme wa mbinguni”
Na sisi Bwana atujalie tufanye jambo ambalo litatusaidia sisi na vizazi vijavyo..
Marana atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
WEKA KUMBUKUMBU YA MAMBO BWANA ANAYOKUFANYIA KWASABABU YATAKUFAA MBELENI.
Ulishawahi kuyatafakari kwa makini haya maneno ya Bwana Yesu?
Yohana 8:38 “Niliyoyaona kwa Baba ndiyo niyanenayo; nanyi vivyo hivyo mliyoyasikia kwa baba yenu ndiyo myatendayo”.
Maneno hayo aliwaambia wayahudi (Mafarisayo na waandishi) kipindi kile walipotaka kumuua?. Lakini unaweza kujiuliza ni lini walishakaa chini na kumsikiliza shetani, akizungumza nao kisha akawapa maagizo ya kumwangamiza Bwana Yesu? Ni lini?
Hatuwezi kudhani kuwa shetani alishawahi kukaa chini, na kuanza kunong’ona kwenye masikio yao, na kuwaambia “sasa wanangu wakati wa kumuua Yesu umefika haya nendeni”, Hilo halipo, lakini Bwana Yesu hawezi kusema uongo, ni lazima aliwaona wakimsikiliza shetani, kisha wakaitii sauti yake, na wakafanikiwa kuyafanya yale yote waliyoagizwa na shetani kutenda.. Na ndio maana ukiendelea kusoma pale, utaona anasema..
Yohana 8:44 “Ninyi ni wa baba yenu, Ibilisi, na TAMAA ZA BABA YENU NDIZO MPENDAZO KUZITENDA. Yeye alikuwa mwuaji tangu mwanzo; wala hakusimama katika kweli, kwa kuwa hamna hiyo kweli ndani yake. Asemapo uongo, husema yaliyo yake mwenyewe; kwa sababu yeye ni mwongo, na baba wa huo”.
Ndugu, sauti ya shetani, kamwe usitazamie utaisikia katika maono au ndoto, au kwa mapepo, hali kadhalika sauti ya Mungu vivyo hivyo, Utaisikia sauti ya Mungu kwa kutazama tu yale Mungu anatenda.. Vilevile utaisikia na kuielewa sauti ya shetani pale unapotazama ni nini anatenda..
Kwamfano, tukianzana na hawa wayahudi, ilifikia wakati walimwonea Yesu wivu kisa Mungu anamtumia kwa ukamilifu wote kuwavuta watu wote kwenye nuru, hapo ndipo wakaingiwa na wazo la kutaka kumuua, wazo ambalo walishawahi kuona watu fulani huko nyuma wakilifanya likawaletea matunda, na wao pia wakalichukua. Kumbe hawajui hilo wazo ndio sauti ya shetani yenyewe ikiwapa maelekezo.
Hata leo, wazo la wewe kutaka kurudi nyuma kuzini, tayari hiyo ni sauti ya shetani, na ndio hapo unaitii kwa kuanza kutazama picha za ngono mitandaoni, unafanya punyeto, unakwenda disco, unatazama muvi zenye maudhui ya mapenzi mapenzi wakati wote, hujui kuwa ni tamaa za ibilisi unazozifanya.. yaani katika ulimwengu wa roho, Yesu anakuona umeketi na shetani kwenye meza moja, ukimsikiliza sauti yake kwa makini sana.
Lakini vivyo hivyo kwa watoto wa Mungu pia kanuni ni ile ile, nao wanamsikiliza Mungu kwa kumtazama vile atendavyo, Kama vile Bwana Yesu alivyosema “Niliyoyaona kwa Baba ndiyo niyanenayo”. Sio maono, hapana, Bwana aliona kazi nyingi za Mungu ulimwenguni hivyo akaziiga akazitenda..
Kwamfano moja ya kazi ambazo Yesu aliziona Baba yake anazifanya akaiga ni pamoja na kuwa na HURUMA, KUSAMEHE, KUWAPENDA MAADUI na KUFADHILI hata kwa wasio na shukrani.
Luka 6:35 “Bali wapendeni adui zenu, tendeni mema, na kukopesha msitumaini kupata malipo, na thawabu yenu itakuwa nyingi; nanyi mtakuwa wana wa Aliye juu, kwa kuwa yeye ni mwema kwa wasiomshukuru, na waovu.
36 Basi, iweni na huruma, kama Baba yenu alivyo na huruma.
Unaona, hivyo na wewe ukionyesha tabia hizo, kuonyesha fadhili kwa watu wasio na malipo kwako, basi rohoni unaonekana umeketi na Mungu kwenye meza moja ukimsikiliza kwa makini akikupa maagizo ya kufanya, hiyo ni zaidi ya sauti, au ndoto, au maono elfu kumi, unayoweza kuyasikia.
Mathayo 5:46 “Maana mkiwapenda wanaowapenda ninyi mwapata thawabu gani? Hata watoza ushuru, je! Nao hawafanyi yayo hayo?
47 Tena mkiwaamkia ndugu zenu tu, mnatenda tendo gani la ziada? Hata watu wa mataifa, je! Nao hawafanyi kama hayo?
48 Basi ninyi mtakuwa wakamilifu, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu”.
Kwahiyo, tujifunze kuitambua sauti ya Mungu wetu kwa kuzitazama kazi zake, vilevile tujifunze kuielewa sauti ya adui yetu ibilisi, ili tuweze kumkwepa na yeye, kwasababu kamwe tusitazamie, sikumoja atakuja kutunong’oneza kwenye masikio yetu “nenda ukazini”, hilo halipo.
Je! Umeokoka? Je! Unafahamu kuwa tupo katika muda wa nyongeza tu, siku yoyote Kristo anarudi. Unasubiri nini huko nje? Utajisikiaje usikie unyakuo umepita halafu wewe umebaki, utamweleza nini Bwana Yesu. Tubu dhambi zako leo kwa kumaanisha kabisa kumrudia Mungu wako, injili tuliyobakiwa nayo sio ya kubembelezewa wokovu tena, ni wewe mwenyewe kuona na kuchukua hatua. Muda umeisha.
Bwana akubariki sana.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
Je ni kweli imani ya mtu ndiyo itakayomuokoa, na si kitu kingine?
UNYAKUO.
TUMEFANYIKA KUWA WANA WA MUNGU!
Makerubi wenye sura nne, ni kweli wapo? na je! wanyama wataenda mbinguni?
SWALI:Bwana Yesu asifiwe naomba kuelewa “Kisima cha joka” na “lango la jaa” vina maana gani kama tunavyosoma katika Nehemia 2:13
JIBU: Nehemia alipopata taarifa juu ya uharibifu wa mji wa Yerusalemu, alifunga na kumwomba Mungu kwa muda mrefu, ili aende kuujenga tena mji huo, ndipo Mungu akasikia maombi yake na kumfungulia mlango wa kwenda Israeli kwa ajili ya kazi hiyo ya ukarabati.
Sasa kama tunavyosoma alipofika,hakusubiri sana, bali aliondoka usiku wa tatu yeye ni baadhi ya watu wachache, ili kuuchunguza kwanza mji, jinsi kuta zake zilivyoharibiwa. Na kati ya sehemu tano (5) alizopita mojawapo ilikuwa ni hapo penye kisima cha joka, na lango la jaa.
Kisima cha joka: Ni kisima kilichokuwa kando ya kuta za mji, kinaaminika, kiliitwa hivyo kutokana na umbile la mdomo wake jinsi ulivyofanana na nyoka., japo wengine wanaamini kuwa hapo kale kilitumiwa na wapagani kwa ajili ya miungu yao ya majini, waliyoitambua kwa jina la joka. Hivyo jina la kisima hicho liliendelea kuwa hilo hadi wakati wa baadaye, Japo hilo halijathibitishwa ni kulingana tu na mapokeo kwasababu biblia haijaeleza sababu ya kuitwa vile.
Lango la Jaa: Jaa kwa jina lingine ni jalala, hivyo, lango hili lilitumika kutolea uchafu wote wa mji (kinyesi). Huko nako Nehemia alifika.
Nehemia 2:11 Basi nikafika Yerusalemu, nikakaa huko muda wa siku tatu.
12 Kisha nikaondoka usiku, mimi na watu wachache pamoja nami; wala sikumwambia mtu neno hili alilolitia Mungu wangu moyoni mwangu, nilitende kwa ajili ya Yerusalemu; wala hapakuwa na mnyama pamoja nami, ila mnyama yule niliyempanda mwenyewe.
13 Nikatoka nje usiku, kwa njia ya LANGO LA BONDENI, nikashika njia IENDAYO KISIMA CHA JOKA, na LANGO LA JAA; nikazitazama kuta za Yerusalemu, zilizokuwa zimebomoka; na malango yake yameteketezwa kwa moto.
14 Kisha nikaendelea mpaka lango la chemchemi, na ziwa la mfalme; lakini hapakuwa na nafasi ya kupita kwa yule mnyama aliyekuwa chini yangu.
15 Kisha nikapanda usiku kando ya kijito, nikautazama ukuta; kisha nikarudi nyuma, nikaingia kwa lango la bondeni, nikarejea hivyo.
Lakini baada ya hayo yote tunaona, Nehemia haraka na mapema alianza ujenzi wa kuta za mji. Na kazi ikaja kukamilika kwa ufasaha wote,licha ya kupitia vipingamizi na vikwazo vingi kutoka kwa maadui zao.
Ni ujumbe gani tunaupata kutoka katika mawazo hayo ya Nehemia?
Ni kwamba hatuwezi kukarabati kitu bila kujua uharibifu wake upo wapi. Ni jinsi gani wakristo, tunapaswa tufumbue macho yetu tuone, uharibifu shetani aliousababisha kwenye kazi ya Mungu, jinsi watoto wanavyoharibiwa, jinsi vijana walivyopotoka kila kukicha, jinsi maasi yanavyoendelea kanisani.., Tukiyaona hayo hapo ndipo wote kwa pamoja tutaona sababu ya kumtumikia Mungu, kwa ushirikiano.
Vinginevyo tutaona kila siku mambo yote ni sawa tu, kama wale watu wa Mji Nehemia alivyowakuta wame RELAX.
Shalom.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo: