Category Archive Home

MWAMBA WENYE IMARA

Mwamba wenye Imara, kwako nitajifichaa…” Ni wimbo wa kenye kitabu cha Tenzi, ambao unafahamika sana…lakini historia ya wimbo huu ni haujulikani na wengi.

Wimbo huu uliandikwa na Mhubiri mmoja wa kanisa la kiprotestant aliyejulikana kwa jina la “Augustus Montague Toplady” , mwenye asili ya nchi ya Uingereza. Mhubiri huyu siku moja alipokuwa anasafiri katika ziara zake za kuhubiri katika kijiji kimoja huko kaskazini mwa Uingereza mwaka huo wa 1763 kilichoitwa “Blagdom”..alipokuwa safarini alikumbana na “Dhoruba kubwa sana ya kuogopesha”.. na hakuwa na mahali pa kujificha…lakini karibu na eneo alilokuwepo palikuwa na MWAMBA MKUBWA, ambao ulikuwa na mwanya mdogo wa kujificha. Na ndipo alipokimbilia chini ya mwamba ule kwenye ule upenyo mdogo na kujificha, mpaka dhoruba ile kali ilipopita..

Sasa akiwa katikati ya upenyo wa mwamba ule, huku anatetemeka kwa baridi, ndipo kichwani ukamjia mistari ya huu wimbo…”mwamba wenye imara…kwako nitajificha..”  Akilinganisha tukio hilo la dhoruba ya mvua kubwa na dhoruba ya kimaisha, ikamsukuma kuimba Yesu ni mwamba wake wa kujifichia..mpaka leo wimbo huo umekuwa Baraka kwa zaidi ya miaka 200.

Huo ni ujumbe wa Mungu kutuonyesha kuwa palipo na dhoruba basi kuna Mwamba…Hivyo hatupaswi kuogopa tunapopitia dhoruba, tunapoona juu kumefunga, maisha yamekwama, vita ni vingi, matatizo ni mengi…tunapofikia mahali tunaona kesho hatapafika, tunapoona mwaka huu hautaisha…Huo ndio wakati wa kumtazama Bwana aliye mwamba wetu..kwake huyo tutajificha…

Mwamba huu hautoi tu hifadhi wakati wa  dhoruba, bali pia unatoa maji baridi  na uvuli wakati wa jua kali..na huo sio mwingine zaidi ya YESU KRISTO, kama mhubiri huyu Augustus alivyoimba..

1Wakorintho 10: 4 “wote wakanywa kinywaji kile kile cha roho; kwa maana waliunywea mwamba wa roho uliowafuata; na mwamba ule ulikuwa ni Kristo”.

Je upo chini ya mwamba leo?..kama haupo..je wakati wa dhoruba utajificha wapi?…wakati wa tufani utakimbilia wapi?..je wakati wa jua kali utapata wapi uvuli? Na maji ya kunywa?…hivyo mkabidhi Kristo leo maisha yako naye atakuwa mwamba kwako.

Lakini kama umeshamkabidhi tayari muda mrefu..basi usitishwe na dhoruba zinazokuja mbele yako, wala usitishwe na vipindi vya hari ya jua kali na ukame…upitiapo hali kama hizo..mwamba upo karibu nawe..Ukumbuke msalaba, na mkumbuke mwokozi, mshukuru, na jinyenyekeze chini yake…na utaona maajabu baada ya kipindi kifupi… Hivyo imba wimbo huu uliovuviwa nguvu za Roho Mtakatifu kukufariji na kukutia moyo..

Mwamba wenye imara, kwako nitajificha
Maji hayo na damu, yaliyotoka humo
Hunisafi na dhambi, hunifanya Mshindi.

Kwa kazi zote pia, sitimizi sheria
Nijapofanya bidii, nikilia na kudhii
Hayaishi makosa, ni we wa kuokoa

Sina cha mkononi, naja msalabani
Nili tupu nivike, ni mnyonge nishike
Nili mchafu naja, Nioshe mi sijafa.

Nikungojapo chini, nakwenda kaburini
Nipaapo mbinguni, nakukuona enzini
Roho yangu na iwe, rahani mwako wewe

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

TENZI ZA ROHONI

WAKATI WA JUA KALI NDIO WAKATI WA KAZI:

USIHUZUNIKE.

WAKATI WA BWANA KUKUVUSHA, NI LAZIMA ARUHUSU JESHI LA ADUI KUNYANYUKA.

USIFIKIRI FIKIRI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

HUYU SI YULE SEREMALA, MWANA WA MARIAMU?

Shalom.

Kulikuwa na sababu kwanini Yusufu awe seremala, vilevile kulikuwa na sababu pia kwanini Bwana wetu Yesu Kristo naye pia awe seremala, na sio kazi nyingine, kabla ya yeye kuanza huduma.

Tunayasoma hayo katika..

Marko 6:3 “HUYU SI YULE SEREMALA, mwana wa Mariamu, na ndugu yao Yakobo, na Yose, na Yuda, na Simoni? Na maumbu yake hawapo hapa petu? Wakajikwaa kwake”.

Soma tena..

Mathayo 13:55 “HUYU SI MWANA WA SEREMALA? Mamaye si yeye aitwaye Mariamu? Na nduguze si Yakobo, na Yusufu, na Simoni, na Yuda?”

Unaona Yesu na baba yake wote walijulikana sana mpaka kupata umaarufu kutokana na hiyo kazi yao ya Useremala, bila shaka walikuwa ni wabunifu wazuri sana, uundaji wao ulikuwa wa kipekee. Kama tunavyofahamu kazi hii, inakuwa ni pale mteja anakuja na mchoro wake na kutaka atengenezewa kitu Fulani, labda meza ya muundo fulani, au kiti au kabati zuri lenye shelfu 6 la nguo na vyombo..Sasa yeye akishamaliza kutoa maelezo yake, au mchoro wake, kwa upande wa pili anapigiwa gharama zote za material kisha anaacha pesa ya awali(advance), Halafu anaambiwa arudi labda baada ya wiki 2..

Huo muda ukishapita anarudi na kukuta kabati lake lipo tayari,safi kabisa limekamilika, anamalizia kiwango cha pesa alichobakisha, kisha analichukua kabati lake, anaondoka analipeleka nyumbani au ofisini.. Lakini ni rahisi kuliangalia ukaona kama ni kazi nyepesi, hajui taabu walisumbuka nayo wale maseremala.

Sasa Mungu kumpitisha Bwana Yesu katika ujenzi tena wa kazi ambayo ilikuwa tayari ni ya baba yake, Ni kumuonyesha kuwa upo ujenzi atakaopaswa aufanye wa kanisa ambalo kwanza lilikuwa ni la baba yake mbinguni..

Yesu kama seramala alijua ili kabati liundike, sio kusimamisha tu gogo,.. bali ilihitajika misumeno ipite, lilihitaji kufanyike vipimo vya hali ya juu, kama pa kuongezwa paongezwe na kama pa kupungwa papunguzwe,..Vilevile ilihitajika Nyundo, na misumari ya kutosha ihusike,…Na hiyo yote ni kufatana na kile alichokiona kikifanywa na baba yake au maagizo ya baba yake, na sio yake mwenyewe.

Na ndio maana alisema..

Yohana 5:19 “Mwana hawezi kutenda neno mwenyewe ila lile ambalo amwona Baba analitenda; kwa maana yote ayatendayo yeye, ndiyo ayatendayo Mwana vile vile.

20 Kwa kuwa Baba ampenda Mwana, naye humwonyesha yote ayatendayo mwenyewe; hata na kazi kubwa zaidi kuliko hizo atamwonyesha, ili ninyi mpate kustaajabu”.

Hivyo hata Kristo alipoanza kuijenga nyumba ya Mungu(Kanisa), alilijenga kwa maagizo ya baba yake, aliposema mtu yeyote akitaka kunifuata ajikane nafsi yake, ajitwike msalaba wake anifuate, alimaanisha, maagizo hayo hakujitungia mwenyewe bali aliyapokea hayo kutoka kwa Baba yake.

Aliposema aaminiye na kubatizwa ataokoka, hakujitungia mwenyewe, bali vipimo hivyo alivitoa kwa Baba yake. Kwamba ili mtu astahili uzima ni sharti amwaminiye yeye, na vilevile akabatizwe kihalili kama ipasavyo.

Aliposema duniani mna dhiki, lakini jipeni moyo,mimi nimeushinda ulimwengu, mambo hayo alionyeshwa na Baba yake kwamba kuna wakati watu wake watapaswa wapitie nyundo, na misumari mikali, na misimeno, kama yeye alivyopitia, ili wakamilishwe.

Wafilipi 1:29 “Maana mmepewa kwa ajili ya Kristo, si kumwamini tu, ila na kuteswa kwa ajili yake”

Hivyo ndugu yangu, hata mimi na wewe leo, hatuna budi kumruhusu Kristo ambaye ndiye seremala mkuu na mwaminifu wa maisha yetu atuunde tuwe kama Mungu apendavyo, tunapopitishwa na yeye katika moto, tustahimili, tunapopitishwa na yeye wakati mwingine katika dhiki, vilevile tustahimili, kwasababu tutakapokamilishwa, tutakuwa vyombo vyenye thamani nyingi sana..

Mambo hayo tutayajua vizuri tutakapofika ng’ambo kwa yale mema mazuri Mungu aliyotuandalia. Kwasababu huo ujenzi wake hauishii tu kwenye maisha yetu, bali pia kwenye Makazi yetu ya milele, aliyokwenda kutuandalia..

Yohana 14:1 “Msifadhaike mioyoni mwenu; mnamwamini Mungu, niaminini na mimi.

2 Nyumbani mwa Baba yangu mna makao mengi; kama sivyo, ningaliwaambia; maana naenda kuwaandalia mahali.

3 Basi mimi nikienda na kuwaandalia mahali, nitakuja tena niwakaribishe kwangu; ili nilipo mimi, nanyi mwepo.

4 Nami niendako mwaijua njia”.

Bwana akubariki.

Je! Umeyakabidhi maisha yako kwake?. Kama bado basi wakati wako ndio huu. Usisibiri wakati mwingine, kwasababu huo hautafika. Fanya uamuzi sasa wa kumgeukia yeye aliye mkuu wa uzima, ambaye aliyatoa maisha yake kwa ajili yako, ili upokee maisha ya milele. Natumai leo haitapita bila kumkaribisha Kristo ndani yako.

Waebrania 12:3 “Maana mtafakarini sana yeye aliyeyastahimili mapingamizi makuu namna hii ya watendao dhambi juu ya nafsi zao, msije mkachoka, mkizimia mioyoni mwenu”

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

HUYU MELKIZEDEKI NI NANI?

WAKATI WA BWANA KUKUVUSHA, NI LAZIMA ARUHUSU JESHI LA ADUI KUNYANYUKA.

HERI NINYI MLIAO SASA, KWA SABABU MTACHEKA.

WANA JUHUDI KWA AJILI YA MUNGU, LAKINI SI KATIKA MAARIFA.

TUNAMHITAJI SANA ROHO MTAKATIFU KATIKA KUYAELEWA MAANDIKO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

USIRUHUSU MUNGU AWEKE UADUI KATI YAKO NA WATU WAKO.

Bwana Yesu Kristo asifiwe.

Karibu tujifunze biblia, Neno la Mungu wetu, ambalo ndio mwanga wa njia yetu na taa iongozayo miguu yetu.

Ili tufanikiwe na tuwe na maisha mazuri siku zote ni lazima tujifunze kulitii na kulishika Neno la Mungu. Kinyume na hapo tutasumbuka sana bila sababu.

Watu wengi wanatafuta kutengeneza urafiki na undugu na watu wengi…wakitegemea marafiki hao wakati wa tabu watawafariji, au wakati wa shida watawasaidia, lakini wengi wanaishia kuumizwa na hao hao marafiki au ndugu, na kupata vile wasivyovitegemea. Unakuta urafiki utaanza vyema lakini utaishia kuwa uadui. Wengine wanatafuta wanawake/wanaume wakitazamia hao ndio watakaokuja kuwa waume zao au wake zao..lakini mwisho wanaishia kuumizana na kuharibiana maisha.

Ipo sababu ya mambo hayo kuwa hivyo…Na sababu hiyo ilianzia tangu Edeni. Hivyo kama tutalielewa somo vizuri kilichotokea Edeni basi, hatutarudia makosa ambayo tayari yalishafanywa na tukaona madhara yake.

Sasa hebu tuwatafakari hawa marafiki wawili ambao hapo kwanza walikuwa na mahusiano mazuri lakini yakaishia kuwa mabaya tena ya uadui. Na marafiki hao si wengine zaidi ya HAWA NA NYOKA. Wote hawa walikuwa wapo katika uwepo wa Mungu, na walikuwa wanakaribiana sana…lakini baada ya kuyaasi maagizo ya Mungu, Mungu akaweka uadui mkubwa katikati yao…Kiasi kwamba mpaka leo Nyoka na mwanadamu ni maadui wakubwa sana…Ukiuliza ni kiumbe gani wa kwanza anayeogopwa na wanawake wengi nadhari asilimi zaidi ya 90 watamtaja nyoka..Hiyo ni kutokana na uadui ambao Mungu aliuweka mwenyewe katikati yake yeye na nyoka.

Mwanzo 3: 14 “Bwana Mungu akamwambia nyoka, Kwa sababu umeyafanya hayo, umelaaniwa wewe kuliko wanyama wote, na kuliko hayawani wote walioko mwituni; kwa tumbo utakwenda, na mavumbi utakula siku zote za maisha yako;

15 NAMI NITAWEKA UADUI KATI YAKO NA HUYO MWANAMKE, na kati ya uzao wako na uzao wake; huo utakuponda kichwa, na wewe utamponda kisigino”.

Umesoma hapo mstari wa 15?…Watu wengi hawajui kuwa UADUI ambao unatokea ghafla kati yao na ndugu zao, au marafiki zao mwingi unawekwa na MUNGU mwenyewe na wala si shetani, na huo ni kutokana na kuacha kulitii na kulishika Neno lake.

Kwamfano utakuta mwanamke… anakutana na mtu ambaye anahisi atakuwa mume wake, na moyoni anajua kabisa hapaswi kukutana kimwili na yoyote Yule mpaka atakapoolewa(kanisani ameshafundishwa sana na yeye mwenyewe anayajua maandiko)…lakini kwa kulikaidi Neno la Mungu anaamua amridhishe Yule mwanaume na kwenda kufanya naye uasherati, akidhani baada ya kitendo hicho ndio atapendwa zaidi…kumbe kinyume chake ni kuchukiwa, baada ya hapo anashangaa Yule aliyemtegemea ampende ndio hana muda na yeye tena..na mwisho wa siku anajiona kama sio mwenye bahati.

Hivyo mwanamke hupaswi kumsogelea kabisa mwanaume, katika kipindi cha uchumba…kipindi cha uchumba sio kipindi cha kutembeleana nyumbani na huku mko wawili tu, si kipindi cha kupikiana pikiana, sio kipindi cha kukutana kutana nyumbani na huku mpo wawili tu!…kwasababu hicho ndio kipindi maalumu cha shetani kupanga kuvuruga mambo…Kama umeandaa chakula mwite mtu zaidi ya mmoja kwako pamoja na huyo mnayekaribiana kuoana lakini si nyinyi wawili tu peke yenu..na pia kumbuka huruhusiwi kabisa pia kumbusu mtu ambaye bado hamjafunga ndoa.

Mambo madogo kama hayo yanadharauliwa na wengi lakini ndio yanayovuruga mipango yote…Na kamwe usifikiri ukimheshimu Mungu, utachukiwa na Yule anayetaka kukuoa au unayetaka kumuoa…Kama ndiye Bwana aliyekusudia awe wako, hawezi kukuchukia zaidi ya yote ndio atakupenda.. Lakini mkivuka mipaka na kwenda kufanya uasherati kabla ya ndoa..hapo ndio basi tena!…kuna nafasi ndogo sana, au isiwepo kabisa ya nyinyi kuoana..mtaishia kuchukiana kwa chuki ya ajabu baada ya kipindi kifupi…mpaka mtashangaa wenyewe ni nini kimetokea…Mungu atawaweka uadui katikati yenu. Kwasababu Mungu hawezi kuunganisha wazinzi pamoja, maana lengo la Mungu kuwakutanisha kwenye ndoa ni ili awabariki…sasa hawezi kuunganisha wazinzi wawili na tena kuwabariki…atakachokifanya ni kuwaweka mbali mbali, au kuwaacha muendelee na uzinzi wenu na yeye asiwe na nyinyi (warumi 1:28).

Kama wewe ni msomi wa biblia utakuwa umewahi kusoma kisa cha Yule mototo wa Daudi aliyemtamani dada yake, na kumlazimisha alale naye…na baada tu ya kulala naye biblia inasema alimchukia kwa chuki isiyokuwa ya kawaida.

2 Samweli 13:13 “Nami nichukue wapi aibu yangu? Wewe nawe utakuwa kama mmoja wa wapumbavu wa Israeli. Basi, sasa, nakusihi, useme na mfalme; kwa maana hatakukataza kunioa.

14 Walakini yeye hakukubali kusikiliza sauti yake; naye akiwa na nguvu kuliko yeye, akamtenza nguvu, akalala naye.

15 Kisha Amnoni AKAMCHUKIA MACHUKIO MAKUU SANA; KWA KUWA MACHUKIO ALIYOMCHUKIA YAKAWA MAKUU KULIKO YALE MAPENZI ALIYOKUWA AMEMPENDA KWANZA. Amnoni akamwambia, Ondoka, nenda zako.

16 Naye akamwambia, Sivyo, kwa kuwa mabaya haya ya kunitoa ni makuu kuliko yale uliyonitendea. Lakini alikataa kumsikiliza.

17 Ndipo akamwita mtumishi wake aliyemtumikia, akasema, Mtoe sasa mwanamke huyu kwangu, ukafunge mlango nyuma yake”.

Ukianzia kusoma kuanzia mstariwa kwanza utaona, Kisa hicho ingawa mwanamke ndiye aliyelazimishwa kwa nguvu…lakini matokeo yake yalikuwa ni yale yale “CHUKI BAADA YA TUKIO”.

Kuna nguvu Fulani ya uadui inashuka kwa watu wanaovunja amri za Mungu..

Mnakubaliana kwenda kuiba au kula rushwa, mwisho wa siku ni lazima tu muishie kugombana…Mnakubaliana kufanya kazi haramu mwisho wa siku ni lazima muishie tu kuwa maadui, mnakubaliana kwenda kufanya utapeli/uuaji lazima mtaishia tu kugombana na kuchukiana na kuwa maadui, mtaanza vizuri lakini itafika kipindi mtatofautiana tu!!… fanya utafiti watu wawili wanaokaa kitako kumsengenya mwingine…huwa wanaishia na wao kugombana au kuchukiana, badala ya kuzidi kuwa pamoja..

Unakumbuka Mnara wa Babeli walianza pamoja lakini nia yao ilipokuwa katika kuujenga mji na mnara wa kisheatani, ili waabudu miungu, Mungu aliwasambaratisha, wakawa hawaelewani, huyu akisema hivi mwingine anasema hivi, wakagombana na mwisho wa siku hata lugha zikazalika nyingine…kazi ngumu waliyokuwa wameianza ikaishia pale pale.

Lakini kinyume chake kama ukiyashika maagizo ya Mungu na amri zake, na kumheshimu…Bwana anasema atakupa amani hata na maadui zako…

Mithali 16: 7 “Njia za mtu zikimpendeza Bwana, Hata adui zake huwapatanisha naye”.

Hivyo zishike amri za Mungu, na mambo yatakunyookea…ukitaka uwe na amani na ndugu zako, fomula ni hiyo hiyo.. “lishike Neno la Mungu”..usiwe kama Hawa mama yetu..aliyedhani kuuimarisha urafiki na nyoka ni kula lile tunda…kinyume chake ndio aliimarisha uadui kati yake na huyo nyoka, na hiyo roho imeendelea mpaka kwa vizazi vyake hadi leo.

Bwana atusaidie

Kama hujampa Yesu maisha yako, hapo jitenge binafsi, piga magoti tubu kwa dhati kabisa na kisha acha yote uliyokuwa unayafanya yasiyompendeza Mungu, na baada ya hapo tafuta kanisa lililopo karibu nawe la kweli, dumu hapo ujifunze Neno na pia upate kubatizwa..Na Roho mtakatifu atakuwa na wewe kukuongoza katika kweli yote.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

NAO WAKADHANI YA KUWA YUMO KATIKA MSAFARA;

VITA VYA IMANI NI VITA ENDELEVU.

VITA VYA IMANI NI VITA ENDELEVU.

KILA MMOJA WENU AJUE KUUWEZA MWILI WAKE.

KILA MMOJA WENU AJUE KUUWEZA MWILI WAKE.

DAMU YA YESU INANENAJE MEMA KULIKO YA HABILI?

Rudi Nyumbani:

Print this post

THAWABU ZA SIRI, ZA WATAKATIFU MBINGUNI.

Tutakapofikia kule ng’ambo zipo thawabu za aina mbili Mungu alizotuandalia, zipo thawabu ambazo zitajulikana na kila mmoja wetu, na zipo thawabu ambazo hatutazijua kila mtu isipokuwa hao watakaozipokea.

Kwa mfano hata ukienda leo kwenye harusi, utagundua wale wanandoa huwa wanapokea aina mbili za zawadi, zipo zile ambazo zinatangazwa hadharani au zinaonekana pale, kwamfano mtu ataleta kabati, mwingine vyombo, au mwingine ataahidi shamba n.k. vitajulikana pale na waalikwa wote. Lakini pia zipo ambazo zinakuja katika maboksi au bahasha, au mifuko maalum, ambazo huwa hazijulikani na kila mtu aliyepo pale, isipokuwa tu kwa bibi-arusi na Bwana arusi siku watakapokuja kuzifungua.

Ndio hapo pengine utakuta ameandikiwa labda hundi ya fedha nyingine kwenye bahasha, mwingine ndani kaweka simu, mwingine saa, mwingine hata ufunguo wa gari n.k…

Sasa zawadi za namna hiyo huwa hazijulikani na wale waalikwa hata kidogo, sasa yule mtu mfano akienda kuchukua lile gari alilopewa kwa siri, akawa analitumia, itakuwa ni rahisi sana wale watu kudhani kuwa lile gari ni la kwake, alilihangaikia na kulinunua kwa gharama zake, kumbe anayejua siri hiyo ni yeye mwenyewe, na yule aliyemletea zawadi.

Na itakuwa hivyo hivyo kwetu sisi tukifika mbinguni siku ile, Mungu atatupa thawabu nyingi zitakazojulikana na kila mtu, kulingana na uaminifu wako hapa duniani, lakini pia ameahidi kutoa thawabu ambazo hizo zitamuhusu muhusika mwenyewe atakayezipokea na si mtu mwingine.

Na thawabu yenyewe kasema itakuwa ni JINA JIPYA .. Embu tusome kidogo.

Ufunuo 2:15 “Vivyo hivyo wewe nawe unao watu wayashikao mafundisho ya Wanikolai vile vile.

16 Basi tubu; na usipotubu, naja kwako upesi, nami nitafanya vita juu yao kwa huo upanga wa kinywa changu.

17 Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa. Yeye ashindaye nitampa baadhi ya ile mana iliyofichwa, nami nitampa jiwe jeupe, na JUU YA JIWE HILO LIMEANDIKWA JINA JIPYA ASILOLIJUA MTU ILA YEYE ANAYELIPOKEA”.

Soma tena mtari wa 17, unasema.. .nami nitampa jiwe jeupe, na juu ya jiwe hilo limeandikwa jina jipya asilolijua mtu ila yeye anayelipokea”.

Sasa jina hilo jipya hapewi kila mtu, bali ni yule tu atayeshinda vitav ya dunia hii..Na ndio maana utaona hata, Bwana wetu naye aliposhinda, naye pia alipewa na Mungu jina hilo jipya ambalo halijui mtu isipokuwa yeye mwenyewe,.soma hapa.

Ufunuo 19:11 “Kisha nikaziona mbingu zimefunuka, na tazama, farasi mweupe, na yeye aliyempanda, aitwaye Mwaminifu na Wa-kweli, naye kwa haki ahukumu na kufanya vita.

12 Na macho yake yalikuwa kama mwali wa moto, na juu ya kichwa chake vilemba vingi; naye ana jina lililoandikwa, asilolijua mtu ila yeye mwenyewe.”

Sasa, jiulize ni kwanini atoe jina na si kitu kingine chochote.?

Ndugu jina ndio kila kitu, kwasababu jina linabeba hatma yote ya Maisha ya mtu, linaelezea heshima yake, linaeleza utajiri wa mtu,na linabeba uweza na nguvu na mafanikio yote ya mtu.

Kwamfano utaona Ibrahimu alipobadilishwa jina kutoka Abramu, na kuitwa Ibrahimu, ndipo hapo Mungu alimfungulia uzao, tena uzao mwingi kama nyota za mbinguni, kiasi kwamba hata mimi na wewe tuliookoka tumefanyika kuwa Watoto wa Ibrahimu kupitia Yesu Kristo, na Sara naye vivyo hivyo.

Mwangalie tena ni Yakobo utaona jinsi alivyobadilishwa jina na kuwa Israeli, ndipo jambo lingine rohoni likatokea, siri ambayo wengi wetu hatuijui ni kuwa, lile jina la Israeli lilikuwa na nguvu ya kuushikilia uzao wa Yakobo, kuanzia ule wakati na kuendelea bila kugawanyika, tofauti na ilivyokuwa kwa uzao wa Isaka, Utaona Isaka alizaa mapacha, ndugu kabisa wa damu, yaani Esau na Yakobo, lakini Mungu ilimpasa achague mmoja tu, Lakini Yakobo alizaa Watoto wengi, tena kwa wamama tofauti tofauti ambao undugu wao upo mbali mbali kidogo, kuliko ilivyokuwa hata kwa ndugu yake Esau, lakini kwasababu aliitwa Israeli, Watoto wake wote hadi leo, nao pia wanaitwa Israeli.

Halikadhalika, kwa Petro, na Paulo, majina yao yalipobadilishwa ndipo walifanya maajabu makubwa na kuwa Mahodari wa Imani.

Vivyo hivyo na wale watakaoshinda vita vya dunia hii kikamilifu, Mungu amewaahidia kuwapa majina mapya, ambayo hayo hayatajulikana na watu wengine, au mtakatifu yeyote isipokuwa mashujaa hao tu wa Imani peke yako… Hao wengine watakachokuja kushuhudia ni matokeo tu ya majina hayo jinsi yatakavyokuwa na uwezo wa kipekee na mamlaka katika huo ufalme unaokuja wa Yesu Kristo Bwana wetu. Hupendi kupewa jina jipya dada?, hupendi kupewa jina jipya kaka?

Hivyo mimi na wewe, tunapaswa tufanyaje ili tushinde?

Ni kwa kutubu dhambi zetu kikamilifu kama tulivyoambiwa pale juu katika mstari wa 16, na kisha kumkabidhisha njia zetu na Maisha yetu yeye peke yake ayatawale, tukiishi tu kama wapitaji hapa duniani, na pia kuifanya kazi yake kwa uaminifu kwa jinsi kila mmoja wetu alivyokirimiwa neema na Bwana wetu.

Swali ni Je umempa Kristo Maisha yako?, . Kama bado fahamu kuwa leo tumepiga tena hatua nyingine ya kuukaribia ule mwisho, na kesho kama itakuwepo tutaipiga nyingine, na kesho kutwa kama itakuwepo ndio tutakuwa tumezidi kabisa kuukaribia ule mwisho, lakini ghafla moja ya hizi siku Unyakuo utapita, na mlango wa neema utakuwa umeshafungwa. Waliopo nje hawataweza kuingia tena, na waliopo ndani hawataweza kutoka tena…Kama maandiko yanavyosema katika Mhubiri 11: 3 “Na mti ukianguka kuelekea kusini, au kaskazini, Paangukapo ule mti, papo hapo utalala”.

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA WARAKA WA TATU WA YOHANA.

UFUNUO: Mlango wa 2 part 3

KUOTA UNAKULA CHAKULA.

BIBLIA TAKATIFU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

MAOMBI YA TOBA.

Kuna tofuati kati ya sala ya toba na Maombi ya toba.

Sala ya toba, ni pale mtu anapokuja kwa mara ya kwanza kwa Kristo, pale anapoamua kuacha Maisha yake ya dhambi. Na kwamba kuanzia huo wakati na kuendelea Kristo anakuwa kiongozi wa Maisha yake, sasa, ikiwa yupo tayari kufanya hivyo basi pale anapopiga magoti, na kuonyoosha mikono yake juu, na kuomba msamaha, aidha yeye mwenyewe au kuongozwa na mtu mwingine, hiyo ndio inayoitwa sala ya toba, Na hii pia inafanywa hata kwa yule mtu ambaye alishaokoka akarudi nyuma, na sasa yupo tayari kumtumikia Mungu tena, kwa moyo wake wote.

Maombi ya toba:

Lakini Maombi ya toba, Nitofati kidogo: Haya ni lazima kwanza uwe katika wokovu.

Maombi haya ni maombi ya upatanisho. Na huwa si ya muda mfupi, au kipindi kifupi. Na mara nyingi huwa yanaambatana na kufunga kulingana na toba yenyewe inayoombwa. Mfano wa maombi haya:

  1. Toba kwa ajili ya familia/ukoo
  2. Toba kwa ajili ya Taifa/Nchi
  3. Toba kwa ajili ya Kanisa

Na nyingine yeyote inategemea na hitaji la mtu.

Kwamfano katika biblia tunaweza kuona mtu kama Danieli aliingia katika maombi ya toba kwa ajili ya taifa lake Israeli na watu wake, akiwa kule Babilioni,..Hiyo hakuiomba juu juu tu bali ilimgharimu afunge,

Danieli 9:1 “Katika mwaka wa kwanza wa Dario, mwana wa Ahasuero, wa uzao wa Wamedi, aliyetawazwa kuwa mfalme juu ya milki ya Wakaldayo; 

2 katika mwaka wa kwanza wa kumiliki kwake, mimi Danielii, kwa kuvisoma vitabu, nalifahamu hesabu ya miaka, ambayo neno la Bwana lilimjia Yeremia nabii, ya kuutimiza ukiwa wa Yerusalemu, yaani, miaka sabini. 

3 Nikamwelekezea Bwana Mungu uso wangu, ili kutaka kwa maombi, na dua, pamoja na kufunga, na kuvaa nguo za magunia na majivu. 

4 Nikamwomba Bwana, Mungu wangu, nikaungama, nikasema, Ee Bwana, Mungu mkuu, mwenye kutisha, ashikaye maagano na rehema kwao wampendao, na kuzishika amri zake;..”

Matokeo ya maombi ya toba na rehema ilimfanya Danieli sio tu kupewa hitaji lake, bali na ziada ya pale, alipomba, mambo ambayo mpaka sisi wa siku za mwisho yanayafaidi..Soma sura yote hiyo utaona jambo hilo.

Hivyo maombi ya Toba yana umuhimu sana kama ukijua inachomwomba Mungu.

Ikiwa kuna makosa fulani umeona yamefanyika katika familia yako, na Hivyo unahitaji Mungu awarehemu, unachopaswa kufanya usisali tu juu juu..Bali hakikisha unajitakasa kwanza, kisha unachukua muda wa kufunga kipindi kadhaa, Na katikati ya mfungo huo unamwomba Mungu rehema juu ya hiyo familia yako, au ukoo wako, na makosa yenu, ikijijumuisha na wewe humo humo.

Na akiwezekana kabisa mwisho wa dua zako ambatanisha na sadaka yako kwa Mungu,..Hiyo usiipeleke kwa yatima au watu wasiojiweza hapana, bali ipeleke madhabahuni pa Mungu, kanisani kwako. Kama alivyokuwa anafanya Ayubu, kwa Watoto wake(Ayubu 1:5).

Vivyo hivyo katika kuliombea taifa, au kanisa, maombi ya toba yanakwenda kwa namna hiyo hiyo.

Maombi haya yana nguvu nyingi sana. Na yanafungua vifungo vya aina mbalimbali. Hata na wale wenye dhambi Mungu anaweza kuwarehemu kwa ajili yako tu, kama alivyofanya kwa Danieli na Israeli taifa lake.

Hivyo katika maombi yako ya toba zingatia hivyo vipengele vitatu:

  • Utakaso
  • Mfungo
  • Sadaka ya upatanisho

Bwana akubariki.


Lakini pengine ninayezungumza naye bado hajaokoka, Na yupo tayari kufanya hivyo.

Kama ni wewe basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie maisha yako yote kama ilivyokuwa hata kwetu sisi. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU  MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, . NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.

AMEN

Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.

Ubarikiwe sana

Mada Nyinginezo:

FAIDA ZA MAOMBI.

Nifanye nini ili niwe na uhakika nikifa naenda mbinguni?

NINI NI KILICHOMFANYA IBRAHIMU AKUBALI KUMTOA MWANAWE SADAKA?

 

UMUHIMU WA YESU KWETU.

HUYU MELKIZEDEKI NI NANI?

IMANI NI KUWA NA UHAKIKA WA MAMBO YATARAJIWAYO.

USIPUNGUZE MAOMBI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

WAKATI WA BWANA KUKUVUSHA, NI LAZIMA ARUHUSU JESHI LA ADUI KUNYANYUKA.

Bwana Yesu asifiwe..karibu tujifunze Biblia. Leo tutajifunza kwa kifupi mojawapo ya njia Mungu anazotumia kutuharakisha kwenda kwenye mafanikio yetu.

Kitu kimoja kinachotuzuia wengi wetu kusonga mbele ni HOFU…Chochote kile mtu afanyacho katika Maisha, endapo akiondoa hofu asilimia 100, basi ni rahisi sana kufanikiwa na kupiga hatua kubwa kwa haraka sana. Hata wafanyabiashara wengi waliofanikiwa kwa namna moja au nyingine ukiwafuatilia utaona ni watu waliojaribu kuondoa hofu na kujiingiza katika kazi Fulani yenye hatari kubwa ya kupata hasara (risk takers)…Na siku zote kazi yenye hatari kubwa ya kupata hasara ikifanikiwa huwa ndio ina matokeo makubwa kuliko ile yenye hatari kidogo. Kwahiyo hofu ndio kikwazo cha watu wengi…

Hali kadhalika kwa upande wa kiroho…Tatizo ni hilo hilo…Hofu!, Leo hii Bwana akikuambia kafanye kitu fulani ambacho kinaonekana hakijawahi kufanywa na kinaonekana kina hatari nyingi, kwa hofu ni rahisi kutokwenda kukifanya…

Hebu kwa ufupi tujifunze jambo kwa wana wa Israeli wakati wa safari yao ya kutoka Misri kwenda Kaanani.

Kama wewe ni msomaji mzuri wa biblia utafahamu kuwa wakati wana wa Israeli wanatoka Misri, njiani walikutana na kipingamizi cha Bahari…Na Mungu alipanga kuipasua ile bahari mbele yao ili waivuke…Lakini kama tunavyojua moyo wa binadamu ni mgumu kuamini…Hebu jiulize endapo bahari ingepasuka mbele yao…halafu waambiwe wapite katikati ya ile bahari, bila msukumo wowote nyuma yao unadhani wangevuka????

Hebu jiweke wewe katika hiyo nafasi, umekuta bahari imefunguka kutoka ferry Dar es salaam na kuna njia imejitengeneza inakwenda mpaka Zanzibar halafu unaambiwa upite katikati ya hiyo bahari, huku pembeni unaona maji yamesimama kama ukuta..je utapita??? Jibu ni la! Hata kwa dawa hutapita..kwasababu utahisi pengine utakapofika katikati maji yatarudi yote na utaangamia….au utaanza kujihisi hisi una dhambi nyingi na hivyo endapo ukipita ukifika katikati Mungu atakuua…Sasa hiyo hali ya hofu na kuwazawaza ingeweza kukufanya usivuke kwenda Zanzibar hata kwa dawa!…Lakini hebu jiulize umeona simba anakuja nyuma yako kukufuata na njia ya kuokoka ni kupita katikati ya hiyo bahari je utaacha kupita?…

Na Bwana alilijua hilo…kwamba wana wa Israeli katika hali ya kawaida hawatavuka katikati ya ile bahari…Hivyo ili kuwalazimisha wavuke…alilileta jeshi la Farao makusudi nyuma yao….Na wana wa Israeli walipoona kuna jeshi la Farao linakuja nyuma yao, lenye mapanga na mikuki na hasira nyingi…Wakaona ile bahari si kitu mbele yao… ni heri kuingia kwenye haya maji kuliko kuchinjwa kama kuku huku tunajiona…Waliwajua wa-Misri jinsi wanavyoua kikatili…Hivyo wote kwa hofu ya kuwaogopa waMisri walijikuta wanaingia baharini bila wao kupenda tena huku wanakimbia,…na ghafla wakajikuta wameshatokezea upande wa pili bila madhara yoyote…

Ni hivyo hivyo hata leo, wakati mwingine Bwana akitaka kukuvusha na kukupeleka katika hatua nyingine…anafungua njia mbele yako ambayo kwa macho ya kawaida unaona huwezi kuvuka….Na pengine wakati unajishauri shauri kwamba utapitaje pitaje hapo, na kwamba ukijaribu utakufa! Au utapata hasara kubwa….ghafla Bwana mwenyewe anakuleta jeshi la ADUI nyuma yako, sasa lengo la lile jeshi sio kukumeza wewe…bali kukulazimisha uvuke hicho kiunzi kilichopo mbele yako, ili akakupe mafanikio mbeleni.

Ndicho kilichotokea hata wakati wa Esta?…Mungu alipotaka kuwabariki Israeli…kulikuwa hakuna namna nyingine zaidi ya kumnyanyua Hamani bin Hamedatha adui wa wayahudi….Lengo la yeye kumnyanyua vile ni ili kuharakisha baraka za wana wa Israeli..

Hivyo kama wewe ni mkristo usiogope uonapo jeshi la Adui limejipanga nyuma yako…na mbele ukitazama unaona Bahari…..Hapo usipaniki…ila tazama kwa makini hiyo bahari utaona kanjia chembamba cha nchi kavu….hako hako ndio kafuatie, usiogope mafuriko, hayatakumeza..hayo yamewekwa mahususi kwa Adui shetani na majeshi yake, na si kwaajili yako. Lakini hiyo ni endapo tu, moyoni mwako unaouhakika kuwa upo ndani ya Kristo.

Unapoona shida zimekuzingira na hakuna kupona, wakati mwingine madeni,n.k.…basi fahamu kuwa hapo ndipo wokovu upo mkubwa…Jeshi la Adui nyuma yako lenye kila silaha lisikufadhaishe…ni Bwana kalileta ili kukulazimisha wewe kupita katika ile njia iliyo nyembamba na hatari mbele yako ili utokezee upande wa pili kwenye baraka zako, usianze kufikiri kupambana na jeshi la shetani wala usianze kunung’unika, utapoteza muda wako na kumuudhi Mungu…wewe endelea mbele na tumaini lako lote liweke kwa Bwana na utauona wokovu wa Bwana na utanyamaza kimya kama Musa alivyowaambia wana wa Israeli.

Kutoka 14:10 “Hata Farao alipokaribia, wana wa Israeli wakainua macho yao, na tazama, Wamisri wanakuja nyuma yao; wakaogopa sana; wana wa Israeli wakamlilia Bwana.

11 Wakamwambia Musa, Je! Kwa sababu hapakuwa na makaburi katika Misri umetutoa huko ili tufe jangwani? Mbona umetutendea haya, kututoa katika nchi ya Misri?

12 Neno hili silo tulilokuambia huko Misri, tukisema, Tuache tuwatumikie Wamisri? Maana ni afadhali kuwatumikia Wamisri kuliko kufa jangwani.

13 Musa akawaambia watu, Msiogope, simameni tu, mkauone wokovu wa Bwana atakaowafanyia leo; kwa maana hao Wamisri mliowaona leo hamtawaona tena milele.

14 Bwana atawapigania ninyi, nanyi mtanyamaza kimya”.

Lakini kinyume chake ni kwamba mkono wa Bwana hutaweza kuuona kama utakuwa sio miongoni wa walioitwa…kumbuka si watu wote waliokuwa duniani kipindi hicho ndio waliokuwa wanaona matendo ya Mungu kama hayo bali ni wana wa Israeli peke yao..na hiyo ni kwasababu hao ndio wan a wa Ahadi walioitwa!…Hivyo na sisi kama hatutakuwa katikati ya kundi la waliomwamini Yesu..kamwe tusitazamie kuuona mkono wa Bwana ukituokoa katika majaribu…Jeshi la Adui shetani litatushambulia na kutushinda siku zote. Lakini ni matumaini yangu kuwa wewe na mimi tupo ndani ya neema ya Kristo, hivyo Bwana ni mwokozi wetu na mtetezi wetu.

Maran atha

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

MAISHA ULIYOPITIA NYUMA NI USHUHUDA TOSHA WA WEWE KUMTUMIKIA MUNGU:

TAFUTA KUWA NA AMANI NA WATU WOTE.

WANA WA MUNGU, NA BINTI ZA WANADAMU.

USISUBIRI MPAKA MUNGU AKUAMBIE, NDIO UFANYE!

NEEMA YA MZALIWA WA PILI.

UCHAWI WA BALAAMU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

WAKATI WA KRISTO KUSIMAMA,UMEKARIBIA SANA.

Tunapaswa tujue, hichi kipindi tulichopo sasa ni kipindi gani, na hicho kinachokuja mbele yetu pia kitakuwa ni kipindi gani. Kwa ufupi ni kwamba Kristo sasa yupo mbinguni ameketi katika kiti chake cha neema, ikiwa na maana kuwa mlango wa neema upo wazi wakati wowote wa mtu yeyote kuingia muda wowote.

Lakini cha kuogopesha ni kuwa biblia ilishatabiri tangu zamani hata kabla Bwana Yesu mwenyewe hajazaliwa kuwa upo wakati wa yeye kusimama kutoka katika hicho kiti chake, na kama tunavyofahamu akisimama ni tendo gani linafuata..Jibu ni kuwa anakwenda kuufunga huo mlango ambao ulikuwa wazi kwa muda mrefu..

Zekaria 2:13 “Nyamazeni, ninyi nyote wenye mwili, mbele za Bwana; kwa maana ameamka, na kutoka katika maskani yake takatifu”.

Biblia inasema hapo, Nyamazeni, maana yake wakati huo wakati utakapofika, Mungu atafumba vinywa hata vya watumishi wake, yaani kwa ufupi yatakuwa ni majira mengine, wakati huo kama mtu atakuwa bado yupo nje ya wokovu, basi hataweza kuupata tena wokovu, kwa jinsi mambo yatakavyokuwa yamebadilika wengi watatamani walau wautafute uso wa Mungu, lakini hawataupata kwasababu yule Roho Mtakatifu ambaye alikuwa ameachiliwa kushawishi mioyo ya watu wamwamini Yesu, ameshaondolewa.

2Wathesalonike 2:7 “ Maana ile siri ya kuasi hivi sasa inatenda kazi; lakini yuko azuiaye sasa, hata atakapoondolewa”.

Na ndio maana Bwana Yesu mwenyewe alisema..

Luka 13:24 “Jitahidini kuingia katika mlango ulio mwembamba, kwa maana nawaambia ya kwamba wengi watataka kuingia, wasiweze.

25 WAKATİ MWENYE NYUMBA ATAKAPOSİMAMA NA KUUFUNGA MLANGO, nanyi mkaanza kusimama nje na kuubisha mlango, mkisema, Ee Bwana, tufungulie; yeye atajibu na kuwaambia, Siwajui mtokako; 26 ndipo mtakapoanza kusema, Tulikula na kunywa mbele yako, nawe ulifundisha katika njia zetu.

27 Naye atasema, Nawaambia, Siwajui mtokako; ondokeni kwangu ninyi nyote mlio wafanyaji wa udhalimu.

28 Ndipo kutakapokuwa na kilio na kusaga meno, mtakapomwona Ibrahimu na Isaka na Yakobo na manabii wote katika ufalme wa Mungu, nanyi wenyewe mmetupwa nje”.

Ndugu yangu ambaye upo nje ya mlango, wakati huo usidhani upo mbali sana, kumbuka siku moja inapopita ndivyo tunavyoikaribia siku yenyewe. Yaani jana ilikuwa ni mbali kuliko leo, Na cha kuogopesha zaidi Bwana Yesu alisema itakuja kwa ghafla sana kwa wasio amini.. Sasa kwanini mimi na wewe yatukute hayo yote, wakati sasa njia ipo wazi?..na inapatikana bure!, hutozwi chochote wala hulipishwi chochote??… Kumbuka Lengo la Kristo sikuzote ni kutuokoa sisi tuliopotea dhambini, hana lengo la kutuhukumu sisi, kinyume chake anataka atutengeneze maisha mema angali tukiwa bado hai muda huu, ili tuweze kuyarithi vizuri yale aliyotuandalia baada ya maisha haya. Anajua kuwa maisha ya hapa duniani ni mafupi, na yamejaa ubatili, na upotofu na ndio maana katuandalia maisha ya umilele baada ya kifo.

Hivyo ndugu yangu..kama hujaupokea wokovu basi huu ni wakati wako wa kufanya maamuzi, unachopaswa kufanya ni kwanza kudhamiria kwa moyo wako wote kumfuata Yesu, pasipo kusita-sita. Na hiyo inaambatana na kuacha dhambi. Hapa ndipo wengi wetu tunapokosea, kwasababu tunamtaka Yesu lakini hatutaki kuacha dhambi..Lakini tukiwa tayari kusema Ulimwengu nyuma yangu, na Kristo mbele yangu, kuanzia leo mimi na dhambi basii!.

Mungu akishaona tu moyo wako huo, moja kwa moja Kristo anaingia maishani mwako,..Hivyo dhamiria kwanza kufanya hivyo, kisha wewe mwenyewe piga magoti, mweleze Yesu makosa yako yote, na baada ya hapo mwombe msamaha kwa moyo wa kuugua kabisa.. Na kama utakuwa umefanya hivyo kwa kumaanisha, basi ipo amani ataileta katika maisha yako ambayo ndio itakuwa uthibitisho wa toba yako, sasa hiyo ni hatua ya kwanza,,

Hatua ya pili ni ubatizo, tafuta kanisa la kiroho karibu na wewe linaloamini ubatizo sahihi wa kimaandiko (yaani ule wa kuzamishwa kwenye maji tele na kwa jina la YESU Matendo 2:38)..Kisha nenda kabatizwe haraka iwezekanavyo, (Ubatizo ni bure hauhitaji gharama zozote, wala hauna tozo la fedha zozote, gharama zako ni toba yako na kujitoa kwako kwenda kuutafuta kwa bidii), Sasa ukishakamilisha vigezo hivyo, basi Kristo atamtuma Roho wake moyoni mwako kukuongoza katika safari yako ya wokovu tangu huo wakati hata milele.(Utaona ufahamu wako anaubadilisha kwa kiwango cha ajabu kwasababu umekubali kumtii).

Na mwisho ni jukumu lako kutafuta ndugu wa kikristo, na kuhudhuria ibadani, ili ukulie wokovu na kujifunza siri za Mungu, huku ukiingojea ile siku ya shangwe ya furaha ya kumlaki Bwana wetu Yesu mawinguni kama itakukuta ukiwa bado hai..Lakini kama utakuwa umelala basi, siku hiyo ikifika utafufuliwa wewe kwanza kisha utaungana na walio hai na kwa pamoja tutaanza safari ya kwenda kula karamu ya mwana kondoo aliyotuandalia mbinguni.

Lakini maadamu bado neema tunayo, tukumbuke tu Neno hili kuwa “siku ya mwenye nyumba kusimama imekaribia”.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

MPINGA-KRISTO

VUKA UJE MAKEDONIA UTUSAIDIE.

TUWATAFAKARI NZIGE WA JANGWANI.

FANYIKA SIPORA WA KRISTO, UNYAKUO UPO KARIBU.

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

UNYAKUO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Wafilisti ni watu gani.

Wafilisti ni watu gani?


Wafilisti ni watu walioishi kaanani ambao waliokuwa maadui wakubwa sana wa Israeli enzi za agano la Kale. Hawa walikuwa ni kundi mojawapo la wenyewe wa nchi ile  kabla ya Israeli kuifikia kutoka Misri.

Lakini wana wa Israeli walipokiuka maagizo ya Mungu ya kuwaua wenyeji wote wa miji ile yaliyoikuta,ili wamiliki, wao wakazembea hawakuwaua wote, kinyume chake wakawabakisha baadhi yao ikiwemo hawa wafilisti na ndio hao baadaye wakaja kuwa mwiba mkubwa sana kwao kama vile Mungu alivyowaambia.

Kipindi baada ya kipindi walikuwa wakiwashambulia waisraeli, na walipomlilia Mungu, (Waamuzi 10:7-8 ), basi Mungu aliwanyanyulia waamuzi wa kuwaokoa kutoka katika mateso yao, mfano Samsoni.

Wafilisti kwasasa ndio Wapalestina, unaowasikia pale mashariki ya kati, jina hilo lilizaliwa kutoka katika lugha ya wagiriki, ambao waliwaita wafilisti wapalestina. Na ndio mpaka sasa limezoeleka hivyo.

Wafilisti ni nchi gani?

Kama tulivyoona wafilisti ni watu waliokutwa kaanani kabla ya wana wa Israeli, lakini sio taifa au nchi. Japokuwa enzi zile walikuwa na miji yao mikuu mitano nayo ni.

  1. Gaza,
  2. Ashdodi,
  3. gathi,
  4. Ashkeloni, na
  5. Ekroni 

(1Samweli 6:17, Yoshua 13:3).

Walikuwa na wakuu/Wafalme wao watano pia kila mmoja na mji wake soma (Waamuzi 3:3). Sasa Miji hii yote ilikuwa kusini magharibi mwa taifa la Israeli.

Lakini Habari za wafilisti zinatufundisha nini?

Yapo mambo ambayo Mungu anaweza kutuagiza kufanya yakayazembea na madhara yake yakawa  mpaka vizazi vya baadaye, kama vile tunavyoona hawa wafilisti/Wapalestina, hawakuwa mwiba tu kwa Israeli wakati ule..Bali hata sasa ni mwiba mkali sana..Kama wewe ni mfuatiliaji wa diplomasia za kimataifa utaweza kufahamu ni kitu gani kinaendelea pale Israeli saa hii , kila kukicha ni machafuko.

Hivyo tuwe makini sana na maagizo ya Mungu, anayotuagiza tusiyapuze hata kidogo,..

Na agizo mojawapo ni wokovu. Jiulize je umelizingatia?.Kumbuka biblia inasema, Yesu ndiye njia, kweli na uzima, mtu hafiki kwa Baba isipokuwa kwa njia yake yeye.. (Yohana 14:6)..Hivyo kama bado hujaokoka, basi ndugu fanya hivyo mapema, ili njia ya mbinguni uione angali nafasi unayo.

Kumbuka hizi ni siku za mwisho, Na wakati wowote Yesu anarudi kulinyakua kanisa lake, dalili zote zinaonyesha kuwa mimi na wewe tupo katika majira hayo ya kurudi kwa Kristo mara ya pili, kutokana na hali halisi inayoendelea sasa hivi duniani. Hakuna asiyejua kuwa tunaishi katika majira hayo

Hivyo tatufa wokovu kwa bidii, kama haukuwa nao.

Bwana akubariki.

Tafadhali angalia pia na mada nyingine chini..usipitwe.

Mada Nyinginezo:

MALAKI, NABII WA MWISHO KATIKA ISRAELI.

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

MAONO YA NABII AMOSI.

HUYU MELKIZEDEKI NI NANI?

MATENDO YETU YANAPIMWA KATIKA MIZANI.

MPINGA-KRISTO

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!

Rudi Nyumbani:

Print this post

Maana ya Nimempenda Yakobo, bali Esau nimemchukia”.(Warumi 9:13)

SWALI: Je Mungu anawapenda watu wote?..Kama ndivyo kwanini alisema mahali Fulani kwamba anamchukia Esau. (Warumi 9:13)


JIBU: Tusome,

Warumi 9:13 “Kama ilivyoandikwa, Nimempenda Yakobo, bali Esau nimemchukia”.

Chuki inayozungumziwa hapo sio chuki ya kinyongo, kama sisi wanadamu tulizonazo…Sisi wanadamu tukimchukia mtu “tunatamani hata Yule mtu afe au apate madhara Fulani mabaya”…Chuki ya namna hii ni mbaya sana na inatoka kwa Yule mwovu.

Lakini chuki inayozungumziwa hapo katika Warumi 9:23 ni chuki ya “kutopendezwa na mtu”…Mungu wetu anawapenda watu wote lakini hapendezwi na watu wote. Hivyo andiko hilo sio la kulitafsiri kibinadamu au kimitazamo yetu ya kibinadamu…Tukilitafsiri kwa njia hiyo basi tutashindwa kumwelewa Mungu vizuri.. “kila mahali utaona kama biblia inajichanganya”

Mstari mwingine tena ambao unazungumzia chuki ambayo usipotafsirika vizuri ni rahisi kupoteza maana kabisa ni huu..

Luka 14:25 “Makutano mengi walipokuwa wakifuatana naye, aligeuka, akawaambia,

26 Kama mtu akija kwangu naye HAMCHUKII baba yake, na mama yake, na mke wake, na wanawe, na ndugu zake waume na wake; naam, na hata nafsi yake mwenyewe, hawezi kuwa mwanafunzi wangu.

27 Mtu ye yote asiyeuchukua msalaba wake na kuja nyuma yangu, hawezi kuwa mwanafunzi wangu”.

Umeona hapo?…haimaanishi kwamba tuwachukie wazazi wetu na ndugu zetu, tusiwapende kabisa, kiasi kwamba hata tuwafanya kuwa maadui zetu ndio iwe tiketi ya sisi kumfuata Yesu na kukubaliwa na yeye…Hiyo sio tafsiri yake…bali tafsiri ya chuki inayozungumziwa hapo ni kitendo cha kuyakataa mapenzi ya ndugu zetu yanayokinzana na mapenzi ya Mungu, na kuchagua kufuata mapenzi ya Mungu zaidi ya mapenzi yao.

Kwamfano Baba/mama/ndugu anakwambia twende kwa mganga…ilihali wewe ni mkristo na unajua hayo sio mapenzi ya Mungu, hapo huna budi kuyakataa maamuzi yao na kufuata mapenzi ya Mungu…sasa kile kitendo cha wewe kuyakataa matakwa yao na kufuata matakwa ya Mungu…Mbingu inatafsiri kama “umemchukia Baba yako/Ndugu yako na umempenda Mungu”. Ingawa wewe upendo wa ndugu zako upo pale pale, unawaombea, unawahurumia, unawaheshimu na kuwajali na kuwatunza.

Ndivyo hivyo hivyo kwa Esau, Mungu hakumchukia kwa chuki za kibinadamu, kwamba hataki kumwona mbele zake, kwamba ni adui yake, na hata hataki kumweka akilini mwake…hapana! bali alimaanisha “hakupendezwa naye kwa matendo yake kama alivyopendezwa na Yakobo”.

Hivyo na sisi hatuna budi kumpendeza Mungu kila siku katika maisha yetu…ili yasitupate kama yaliyompata Esau.

Maran atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

Je! Hamna nyumba za kulia na KUNYWEA?.Mstari huu unahalalisha unywaji wa pombe?

WAKATI ULIOKUBALIKA NDIO SASA.

JE! PAKA KULIA USIKU NI ISHARA YA UCHAWI?

MWISHO WA DUNIA UTAKUJAJE?

Rudi Nyumbani:

Print this post

KWA KUWA TUMEKABIDHIWA MAUSIA NA MUNGU.

Kuna mambo ambayo Mungu anaweza kukuagiza ufanye, ukayaona kama hayana maana yoyote rohoni,ukayapuuzia tu na ukaendelea na shughuli zako kama kawaida, hata ukawa unaendelea kumtumikia Mungu, lakini hujui kuwa machoni pa Mungu ukaoekana kuwa si kitu.

Kwa mfano tukirudi kwenye maandiko, utaona kuna wakati mtume Paulo, alipokea kweli ufunuo wa Roho Mtakatifu kuwa tohara ya mwilini hamfikishi myahudi popote, awe ametahiriwa awe hajatahiriwa kama mtu huyo haishiki torati basi ni sawa na kazi bure tu.(Warumi 2:25-29)

Lakini utaona anasema tena, tohara ni muhimu kwao kwa kila njia, ikimaanisha kuwa sio jambo la wao kulipuuzia hata kidogo, Soma..

Warumi 3:1 “Basi Myahudi ana ziada gani? Na kutahiriwa kwafaa nini?

2 Kwafaa sana kwa kila njia. Kwanza kwa kuwa wamekabidhiwa mausia ya Mungu”.

Unaona, japokuwa aliwahubiria wayahudi kuwa tohara ya mwilini haiwezi kuondoa dhambi zao, lakini aliwahimiza watahiriwe wote, kwasababu lilikuwa tayari ni agizo la Mungu.

Sasa hilo lilikuwa ni agizo kwa wayahudi..

Vipi kuhusu sisi wakristo, ambao sheria yetu ililetwa na Bwana wetu YESU KRISTO?.

Yeye alisema..

Marko 16:16 “Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini, atahukumiwa”.

Kama tunavyosoma hapo sio kuamini tu, bali na kubatizwa pia..Lakini cha kushangaza wapo wakristo wanaosema, ubatizo haumpeleki mtu mbinguni, unaweza ukawa umebatizwa na maji hata ya mto Yordani na mbinguni bado usiende, kwasababu maji hayaondoi dhambi za mtu isipokuwa damu ya Yesu …mtu huyo anaendelea kusema kinachojalisha ni kumwamini Yesu tu basi,ukishatubu ndio tayari umeupata wokovu wenyewe..hayo masuala ya kubatizwa, tena kwa kuzamishwa, sio lazima kwa mkristo.. Wewe amini tu inatosha, imani yako ndio itakayokupeleka mbinguni..

Lakini Kristo anataka ufahamu jambo hili, kwamba ubatizo wafaa sana kwa kila njia, na kwanza ni kwasababu yeye ametupa maagizo hayo..hata kama kwetu hayana maana lakini kwake yanayo maana kubwa..

Tukijiona sisi ni wa rohoni sana kuliko yeye mwenyewe aliyetupa maagizo hayo, na kwamba tunajua kumtumikia kuliko kuyafuata maagizo yake.. Basi siku zote tuyakumbuke maneno yake haya aliyoyasema:

Luka 6:46 “Na kwa nini mnaniita, Bwana, Bwana, walakini hamyatendi nisemayo?

47 Kila mtu ajaye kwangu, na kuyasikia maneno yangu na kuyatenda, nitawaonyesha mfano wake.

48 Mfano wake ni mtu ajengaye nyumba, na kuchimba chini sana, na kuweka msingi juu ya mwamba; na kulipokuja gharika, mto uliishukia nyumba ile kwa nguvu, usiweze kuitikisa; kwa kuwa imejengwa vizuri.

49 Lakini yule aliyesikia ila hakutenda, mfano wake ni mtu aliyejenga nyumba juu ya ardhi pasipokuwa na msingi, mto ukaishukia kwa nguvu, ikaanguka mara; na maangamizi yake nyumba ile yakawa makubwa”.

Sisi tulio na masikio na tusikie maneno ya Bwana na tuyatii.Kumbuka Neno ubatizo tafsiri yake ni kuzamwishwa/kuzikwa, hivyo unapofikiria kwenda kubatizwa maana yake ni kuwa unakwenda kuzamishwa katika maji, mwili wote unapotelea majini, na sio kunyunyiziwa,.Na ndio hapo suala la maji mengi/ maji tele linakuja sawasawa na (Yohana 3:23). Na hiyo inaweza ikafanyika popote pale aidha mtoni, au bwawani, au baharini, au kwenye kisima kilichochimbwa, au popote pale maadamu tendo hilo liwe ni la kuzamwishwa mwili wote majini.

Vilevile ubatizwe uwe ni kwa jina lake yeye aliyekuagiza yaani YESU KRISTO anayeweza kuzifuta dhambi zetu sawasawa na (Matendo 3:38,8:16,10:48, 19:5)..Ukikamilisha hayo maagizo ipasavyo basi ujue kuwa wokovu wako ni thabiti, Na kama ingekuwa ni kupewa cheti cha kimwili basi mbingu ingekupa. Hivyo kama hujawahi kubatizwa kabisa au ulibatizwa isivyopaswa, basi wakati ndio huu kwako kwenda kufanya hivyo.

Na Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

MITHALI AU METHALI ZA BIBLIA

UTASIMAMA PEKE YAKO SIKU ILE.

RAFIKI MWEMA.

Je! Ni halali kuoa/kuolewa na mtu ambaye tayari anao watoto?

Rudi Nyumbani:

Print this post