Title Devis

NI NINI TUNAJIFUNZA KWA DEMA NA MARKO?

Biblia inatuonyesha Dema na Marko walikuwa ni watenda kazi wazuri sana pamoja na Mtume Paulo, Tunayasoma hayo katika kitabu cha Filemoni 1:24

“na Marko, na Aristarko, na Dema, na Luka, watendao kazi pamoja nami”.

Lakini pamoja na kwamba walikuwa ni watenda kazi pamoja na Paulo, tunaona kila mmoja alikuwa na historia yake tofauti, ambayo leo hii tunaweza kuitazama na kupata funzo ndani yake.

MARKO

Tukianzana na huyu Marko, mwanzoni kabisa mwa huduma ya mtume Paulo, ya kuipeleka injili kwa watu wa mataifa, utaona akiwa na Barnaba, walimchukua pia huyu Marko kama msaidizi wao katika safari yao ya utume Mungu aliowapa. Lakini kama tunavyosoma katika maandiko, walipopita nchi kadhaa wa kadha, ghafla Marko alibadilika tabia, hatujui sababu ni nini iliyomfanya awe vile pengine, aliona kazi ile ni ngumu, au aliona haina faida yoyote.. Na hatimaye akawaacha Paulo na Barnaba solemba katika kilele cha utumishi, akarudi zake alipotokea, (Soma Matendo 13:13)

Jambo hilo liliwaumiza kama sio kuwafadhaisha sana mitume hususani Paulo, kuona kwamba mtu ambaye angepaswa kuwafariji na kuwatia moyo ndio anakuwa wa kwanza kuwakimbia. Na ndio maana wakati wa ziara ya pili, Paulo alipotaka tena kusafiri kwenda kuyathibitisha makanisa, aligoma kwenda na huyo Marko shambani mwa Bwana, Kwasababu alijua kigeugeu chake.

Matendo 15:37 “Barnaba akaazimu kumchukua Yohana aliyeitwa Marko pamoja nao.

38 Bali Paulo hakuona vema kumchukua huyo aliyewaacha huko Pamfilia, asiende nao kazini.

39 Basi palitokea mashindano baina yao hata wakatengana. Barnaba akamchukua Marko akatweka kwenda Kipro”.

Lakini pamoja na hayo biblia inatuonyesha huyu Marko alikuja kugeuka baadaye , pengine alitubu na kutambua makosa yake, akaona hapa naelekea kulipoteza taji langu, hivyo akaendelea kufanya utumishi wa Mungu, na baadaye kabisa utaona mtume Paulo akimpokea tena, akisema ni mtenda kazi pamoja naye. Na huyu Marko ndiye aliyekiandika hicho kitabu cha Marko ambacho mpaka leo hii tunakisoma.

DEMA

Sasa tukimtazama na mtendakazi wake mwingine aliyejulikana kama Dema, yeye alikuwa katika utumishi mzuri sana na Paulo, pengine tangu mwanzoni kabisa mwa huduma alikuwa naye, lakini ilifika wakati pengine kwa kuona kuna ugumu fulani, akaamua kabisa kuachana na utume, hivyo akamwacha mtume Paulo peke yake vifungoni, ni heri angemwacha tu, kisha aende kuifanya kazi ya Mungu sehemu nyingine.. Lakini mtume Paulo anasema, aliupenda ulimwengu huu.

Yaani aliacha kabisa utumishi wa Mungu akayarudia mambo ya kale ya ulimwenguni, na wala hakurudi tena shambani mwa Bwana. Embu fikiria mtu huyu jinsi alivyouvunja moyo wa Mungu na Paulo. Pengine mwenzake Marko alikuwa anamwangalia, na kumwonya asifanye hivyo, kwasababu mwisho wake utakuwa ni mbaya, kwasababu yeye naye alijaribu kufanya hivyo lakini hakuona faida yoyote, lakini Dema hakusikia akaona ni heri arudie anasa zake, zile ziara zote za kuzunguka kuhubiri injili ndio mwisho, hakuna faida yoyote. Nitarudia miradi yangu mikubwa n.k.

2Timotheo 4:10 “MAANA DEMA ALINIACHA, AKIUPENDA ULIMWENGU HUU WA SASA, akasafiri kwenda Thesalonike; Kreske amekwenda Galatia; Tito amekwenda Dalmatia”.

Sasa mambo haya tunaweza kudhani hayatokei hata sasa.

Biblia inasema, TUISHINDANIE IMANI, ambayo tumekabidhiwa sisi watakatifu mara moja tu.

Yuda 1:3 “Wapenzi, nilipokuwa nikifanya bidii sana kuwaandikia habari ya wokovu ambao ni wetu sisi sote, naliona imenilazimu kuwaandikia, ili niwaonye kwamba mwishindanie imani waliyokabidhiwa watakatifu mara moja tu.”

Unaona Mungu hategemei sana mwanzo wetu, anautazama na mwisho wetu utakuwaje. Kama Dema alikuwa ni mtendakazi mzuri sana, mpaka Mtume Paulo anajivunia kwa kumtaja katika nyaraka zake nyingi, usidhani hakukuwa na watendakazi wengine wakati ule, walikuwepo,  lakini alijivunia Zaidi  Dema pengine kwa bidii yake..

Wakolosai 4:14 “Luka, yule tabibu mpendwa, na Dema, wanawasalimu”.

Lakini mwisho wa siku anageuka na kuisaliti Imani, unadhani na sisi tusipoishindania Imani hatutaisaliti vivyo hivyo pale tunapoona mambo hayajaenda kama tunavyotaka?. Imani ya wokovu ni ya kuishindania kweli kweli haijalishi ni mazingira gani utapitia, kwasababu Bwana Yesu  alisema tangu kipindi cha Yohana mbatizaji hadi sasa ufalme wa mbinguni unapatikana kwa nguvu, na wenye nguvu ndio wanaouteka (Mathayo 11:12).

Utajiuliza ni kwanini Bwana Yesu alisema tangu kipindi cha Yohana mbatizaji na sio tangu kipindi cha akina Musa au Eliya, au Daudi?..Alisema vile kufuatana na maisha ya Yohana mbatizaji, jinsi alivyojikana nafsi kumtafuta Mungu, mtu ambaye hakujali mazingira aliyopo, hakujali nguo alizovaa, hakujali chakula alichokula, kule jangwani maadamu yupo sawa na Mungu wake, hiyo ilitosha.. Sasa kama yeye aliushindania hivyo, hata sisi hatuna budi kuishindania vivyo hivyo kama yeye, kulingana na maneno ya Yesu.

Mpaka mtume Paulo anakaribia kwenda kufa, na kusema IMANI NIMEILINDA, usidhani ilikuwa ni jambo jepesi jepesi, alipitia tabu zote lakini hakuukana au kuusaliti wokovu wake.

Itakuwa ni ajabu sana kama utataka kwanza uoelewe au upate kazi nzuri, au upate pesa ndio usimame katika wokovu, kwa namna hiyo kamwe hutakaa uustahimili wokovu, kwasababu hata kama Mungu akikupa hayo yote, kukitokea mtikisiko kidogo tu, utarudi nyuma kuuacha wokovu kama Dema.

Hivyo mapambano ya Imani yapo. Shikilia sana wokovu wako bila kuangalia au kujali mazingira, maana hiyo ndio tiketi yako ya kwenda mbinguni. siku hizi ni za mwisho. Maisha ni mafupi sana.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

TUMEKUWA TAMASHA KWA DUNIA; KWA MALAIKA NA WANADAMU.

MWANZO WA INJILI YA YESU KRISTO.

KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 1

Nini maana ya “kila tendo lisilotoka katika imani ni dhambi?”

NJIA YA KUPATA WOKOVU.

PINDO LA VAZI LAKE SASA LIMEREFUSHWA.

Rudi nyumbani

Print this post

TUMEKUWA TAMASHA KWA DUNIA; KWA MALAIKA NA WANADAMU.

Paulo alipouna utumishi wake, na wenzake jinsi ulivyo, na kuona magumu anayoyapitia katika huduma yake, mwisho wa siku alisema maneno haya..

1Wakorintho 4:9 “Maana nadhani ya kuwa Mungu ametutoa sisi mitume mwisho, kama watu waliohukumiwa wauawe; kwa sababu TUMEKUWA TAMASHA kwa dunia; kwa malaika na wanadamu.

10 Sisi tu wapumbavu kwa ajili ya Kristo, lakini ninyi ni wenye akili katika Kristo; sisi tu dhaifu, lakini ninyi mna nguvu; ninyi mna utukufu, lakini sisi hatupati heshima.

11 Hata saa hii ya sasa, tuna njaa na kiu, tu uchi, twapigwa ngumi, tena hatuna makao;

12 kisha twataabika tukifanya kazi kwa mikono yetu wenyewe. Tukitukanwa twabariki, tukiudhiwa twastahimili;

13 tukisingiziwa twasihi; tumefanywa kama takataka za dunia, na tama ya vitu vyote hata sasa:.

Kumbuka Matamasha ya zamani sio kama haya tuliyo nayo sasa.

Matamasha ya zamani yalikuwa yanafanyika katika viwanja vikubwa sana vya michezo, na michezo yenyewe vilevile  haikuwa  kama hii tuliyonayo sasa hivi, mfano mpira, au riadha, hapana, bali ni michezo ya kupigana miereka ya kufa na kupona, , ambayo ilikuwa inapiganwa na watu waliobebea sana katika vita, watu hawa walikuwa aidha ni wafungwa walioshindikana, kwa kesi za mauaji au watumwa, walionunuliwa kutoka mbali, hivyo walichokuwa wanafanya ni kuwachukua na kuwapeleka katika mafunzo haya ya muda mrefu kujifunza kupigana

Hivyo wakati Fulani unafika, ndio wanawaleta sasa kwenye viwanja hivyo vikubwa ili wapambane, ambapo maelfu ya watu walikuwa wanakusanyika kutazama mapigano hayo. Hayakuwa mapigano ya  miereka kama tunayoyaona sasa hivi kwenye Tv, watu wanaumizana tu kidogo halafu baadaye wanaachana hapana, bali mapigano kweli kweli ya kushika mapanga na ngao.

Kule juu kila mtu akikaa akimshangilia mchezaji wake., Na mwishoni ni lazima mmojawapo auawe. Na wakati mwingine ilikuwa ni kupigana na wanyama wakali kama vile, simba, chuo au vifaru.

Sasa wakristo wa kwanza waliokuwa wanauawa, waliingizwa kwenye viwanja hivi, vya mapambano, vilivyojulikana kama Arena. na huko ndani wanakutana na hawa wapiganaji waliobebea na kama sio hao basi waliachiliwa wanyama wakali kama Simba au chui, wapambane nao. Kwa namna ya kawaida unaelewa ni nani atashinda hapo. Kwasababu sikuzote wakristo sio wapiganaji, pengine watakachofanya tu ni kutafuta njia ya kunusuru maisha yao, lakini mwisho wa siku watauliwa tu, . Kumbuka wakati huo waelfu wa watu wapo majukwaani wanawatazama kama vile tamasha, wakishabikia, na kufurahia, kama vile timu Fulani ya simba na Yanga inacheza.

Sasa Mtume Paulo aliutolea mfano huo kuonyesha ni jinsi gani watumishi wa Mungu, wanavyoonekana duniani leo hii. Wanatolewa ili watazamwe jinsi wanavyouawa, Paulo alisema tunakufa kila siku, 1Wakorintho 15:31,

Na kama vile teknolojia ilivyokuja juu sana, watamazaji wa matamasha wameongeza, kiasi kwamba sio tu wale walio kwenye viwanja wanaona mchezo wote, bali na wa mbali pia, vivyo hivyo, dhiki hizi wa watumishi wa Mungu zinaonekana mpaka kwa malaika wa Mungu mbinguni, wanatuona na kutuhurumia.

Lakini kwanini Mungu aruhusu iwe hivyo?

Hiyo inatupa chachu ya mambo mawili, la kwanza, ni kuwa wewe kama mtumishi wa Mungu, ufanyapo kazi ya Mungu, fahamu kuwa wewe ni kama tamasha la ulimwengu, matusi ni lazima yawe sehemu ya maisha yako, dhihaka zitakuwa zako, kupigwa na wakati mwingine kufukuzwa na kuuliwa vitakuwa vyako, hivyo kama vile Bwana Yesu alivyosema..

Luka 6:22 “Heri ninyi watu watakapowachukia, na kuwatenga, na kuwashutumu, na kulitupa nje jina lenu kama neno ovu, kwa ajili ya Mwana wa Adamu.

23 Furahiwani siku ile na kuruka-ruka, kwa kuwa, tazama, thawabu yenu ni kubwa mbinguni, maana, baba zao waliwatenda manabii vivyo hivyo”.

Vivyo hivyo na wewe furahi kwasababu ufalme wa mbinguni ni wako.

Lakini kwa wewe ambaye unahubiriwa injili na unaipuuzia, unatoa maneno ya dhihaka, unacheka, unatukana, unaleta fitina, ujue kuwa, Bwana Yesu alisema maneno haya vilevile..

Mathayo 10:14 “Na mtu asipowakaribisha wala kuyasikiliza maneno yenu, mtokapo katika nyumba ile, au mji ule, kung’uteni mavumbi ya miguuni mwenu.

15 Amin, nawaambia, itakuwa rahisi nchi ya Sodoma na Gomora kustahimili adhabu ya siku ya hukumu, kuliko mji ule”.

Unaona, ikiwa unaigeuza kazi ya Mungu kama tamasha tu la kusikiliza, kuambiwa, kuona wengine wanamtafuta Mungu lakini wewe unakuwa kama mshabiki tu, na hutaki kukitendea kazi kile ulichoambiwa, ujue huko ng’ambo adhabu yako itakuwa ni  kubwa sana.. Zaidi hata ya wale watu wa Sodoma na Gomora, ambao kulingana na maneno ya Bwana Yesu tunaona hadi sasa adhabu yao haijaisha, sasa jiulize wewe utakuwa wapi?

Bwana alisema pia..

Luka 12:47 “Na mtumwa yule aliyejua mapenzi ya bwana wake, asijiweke tayari, wala kuyatenda mapenzi yake, atapigwa sana.

48 Na yule asiyejua, naye amefanya yastahiliyo mapigo, atapigwa kidogo. Na kila aliyepewa vingi, kwake huyo vitatakwa vingi; naye waliyemwekea amana vitu vingi, kwake huyo watataka na Zaidi”.

Jiulize wewe unaishi kwa ajili ya nini? Kama watumishi wa Mungu wanapitia adhabu ya Mungu wakiwa hapa duniani, jiulize wewe mwenye dhambi utaonekania wapi siku ile kama mtume Petro alivyosema katika 1Petro 4:15-17 Kumbuka mbinguni hakitaingia kinyonge..Unauchukulia wokovu wako juu juu tu, ufahamu kuwa unyakuo ukipita leo, huendi popote. Hata kama utasema wewe ulibatizwa, au ulimpa Yesu maisha yako, hutakwenda popote ndugu. Usipojikana nafsi na kumfata Yesu, utabakia hapa hapa duniani. Nivyo ilivyo hukumu ipo.

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

MAUAJI YA HALAIKI NDANI YA KANISA.

MATARAJIO YA KILA MWANADAMU DUNIANI NI YAPI?

Hanithi ni nini katika biblia? (kumbukumbu 23:17)

CHUKIZO LA UHARIBIFU

MWANZO WA INJILI YA YESU KRISTO.

KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 1

Rudi nyumbani

Print this post

MAUAJI YA HALAIKI NDANI YA KANISA.

Mwaka 1994 kulizuka vita mbaya ya kikabila huko nchini Rwanda, Vita hivyo vilidumu kwa miezi mitatu tu, lakini maafa yaliyotokea, yalizidi hata vita zilizopiganwa kwa miaka mingi katika mataifa mengine. Ni heri vifo vingekuwa vya kupigwa bunduki tu basi, lakini watu walikuwa wakiuliwa kinyama wakichinjana na wengine kuchomwa moto makanisani, mpaka leo dunia haiwezi kusahau yaliyotokea Rwanda wakati ule.

Ilikuwa ni vita vya makabila mawili tu, lakini mapambano yake yalitisha sana, kwani ndani ya muda huo mfupi watu zaidi ya laki nane waliuliwa. Hiyo inatukumbusha mauaji mengine kama haya, katika biblia,. Na yenyewe yalikuwa ni kati ya pande mbili, watu wa taifa moja. Na hao si wengine zaidi ya Yuda na Israeli.

Ilifika wakati Hawakuwezi kukaa tena pamoja, na hiyo ni kwasababu  hawakujua chanzo cha tatizo lao ni nini, mpaka wakaanza kupigana, hatujui vita hiyo ilichukua siku ngapi, pengine moja, au mbili tu, lakini watu waliouawa siku hiyo walikuwa ni laki 5 (500,000). Jaribu kutengeneza picha taifa dogo kama mji wa Daresalaam, wanaanguka watu laki tano, si jambo la kawaida kabisa, hayo ni zaidi ya mauaji ya halaiki. Katika biblia nzima hakujawahi kutokea Israeli kuwaua hata maadui zao kwa idadi kubwa kama hiyo waliouana wao kwa wao. Walikuwa na maadui wakubwa kama vile wafilisti, lakini hawakuwahi kuwaua kwa idadi kubwa namna hiyo.

2Nyakati 13:15 “Ndipo wakapiga kelele watu wa Yuda; ikawa, watu na Yuda walipopiga kelele, Mungu akampiga Yeroboamu na Israeli wote mbele ya Abiya na Yuda.

16 Wana wa Israeli wakakimbia mbele ya Yuda; naye Mungu akawaua mikononi mwao.

17 Abiya na watu wake wakawapiga mapigo makuu; hata wakaanguka wameuawa wa Israeli mia tano elfu, watu wateule.

18 Ndivyo walivyotiishwa wana wa Israeli wakati ule, wakashinda wana wa Yuda, kwa kuwa walimtegemea Bwana, Mungu wa baba zao.

19 Abiya akamfuata Yeroboamu,”

Hiyo ni kuonyesha kuwa vita vya ndani huwa ni vibaya zaidi kuliko vita vingine vyote. Na haviwi rahisi kuvizima, vinapoa tu muda lakini baadaye tena vitanyanyuka, kama ilivyokuwa kwa Israeli huo ni mfano wa vita moja tu, vilipita vita nyingine nyingi na zote zilileta maafa mengi, utadhani lile sio taifa la Mungu.

Tunaweza kudhani vita hivi havipo sasa..

Kumbuka Israeli ni kivuli cha kanisa la rohoni linaloendelea sasa hivi. Leo hii duniani kuna madhehebu zaidi ya 30,000 na yote yanadai kuwa ni ya Ki-kristo.  Hivyo ni sawa na kusema wote ni Taifa la Israeli, isipokuwa makabila tofauti tofuati. Lakini hatujui kuwa hiyo ni dalili mbaya sana. Hadi sasa tulipofikia vita za kidhehebu zimerindima, mauaji ya kiroho yanayoendelea katikati ya watu wanaomwamini Kristo, siku baada ya siku tena yanaongeza kwa idadi kubwa sana. Huyu anapigana na huyu, na yule anapigana na huyu..Mwisho wake ni nini,?

Lazima tujue Israeli iligawanyika kwasababu gani..Iligawanyika kwa sababu moja tu ya Sulemani, kuacha kuenenda katika njia za Mungu na kuenda kuitolea miungu mingine sadaka, lakini wakati huo huo, ndani yake kulikuwa na ahadi za Mungu ambazo alimuahidi baba yake, hivyo ili Mungu kutimiza haki yote ya ahadi na adhabu, ndipo akaugawanya ufalme wake na kumpa mtu mwingine, na wakati huo huo akamwachia ufalme kidogo kwa ajili ya Daudi baba yake. (1Wafalme 11:9-14) Huo ndio ulikuwa mwanzo wa Israeli kugawanyika. Lakini kama waisraeli baada ya pale wangetaka kumrudia Mungu wao, ni wazi kuwa Mungu angeurejesha ufalme kwa uzao mmoja wa Daudi na Israeli yote ingekuwa kitu kimoja.

Vivyo hivyo leo hii ni kwanini Kanisa la Kristo limegawanyika? Ni kwasababu tunaye Kristo ndani yetu, na wakati huo huo tunaabudu mambo mengine, Mungu ametuadhibu kwa kutugawanya kama ilivyo leo hii. Na matokeo ya kugawanyika ni vita. Vita hizi zitaendelea kama hatutarudi kwenye misingi ya Neno, kama hatutajua kosa letu ni nini, tutauana sana,  biblia inasema hivyo..

Bwana alisema..

Yohana 16:2 “Watawatenga na masinagogi; naam, saa yaja atakapodhania kila mtu awauaye ya kuwa anamtolea Mungu ibada”.

Imefikia hatua badala mtu akuelekeze kwa Kristo anakuelekeza kwenye dini yake, ili ujenge chuki na wale wengine wasio wa dhehebu lao, ukristo umehama sasa kutoka katika kuelekeza mapambano dhidi ya adui wa nje (shetani) hadi kujikita katika mapambano ya sisi kwa sisi. Kilichojaa ndani yetu ni udhehebu na udini, tukidhani hivyo ndivyo vinavyompendeza Mungu.

Bwana anasema, tutokea huko, tumrudie yeye.

Ufunuo 18:4 “Kisha nikasikia sauti nyingine kutoka mbinguni, ikisema, Tokeni kwake, enyi watu wangu, msishiriki dhambi zake, wala msipokee mapigo yake”.

Ondoka kwenye kamba hizi kamba za kidhehebu, ndugu yangu. Shikamana na Kristo kwa wakati huu uliobakiwa nao hapa duniani, hakikisha huyo ndiye anayekaa katika moyo wako kuliko jambo lingine lolote.

Bwana akabariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Chuo cha vita vya Bwana ni kipi?(Hesabu 21:14)

NAYE AKASIMAMA JUU YA MCHANGA WA BAHARI.

Nini maana ya Dirii, Chapeo na Utayari?

NAMNA YA KUITAMBUA SAUTI YA MUNGU INAPOZUNGUMZA NA WEWE

SI MAPEPO YOTE NI YA KULIPUKA.

THAWABU YA UAMINIFU.

Rudi nyumbani

Print this post

PINDO LA VAZI LAKE SASA LIMEREFUSHWA.

Isaya, alionyeshwa maono mengine ya ajabu mbinguni, Pengine hakuelewa umuhimu na maana ya maono yale, lakini sisi wa leo ndio tunaweza kuelewa vizuri.. Alipochukuliwa katika maono mbinguni alimwona Mungu akiwa ameketi katika kiti chake cha enzi kilichonyanyuliwa juu sana, juu kweli kweli. Na moja ya vitu ambavyo vilishangaza macho yake, ni kuhusu lile vazi lake, kwani lilipofika chini, halikuishia palepale bali liliendelea kumwagika, mpaka kufunika hekalu zima juu mbinguni.

Maono hayo aliyoonyeshwa Isaya yalichukua picha ya ufalme wa kidunia, hususani kwenye zile ngome kubwa sana, kama vile Ashuru na Misri zilizokuwa zinaitikisa dunia wakati ule wa nabii Isaya. Wafalme wao walivaa mavazi ambayo yalimwagika kwa nyuma, kuashiria utukufu wa enzi zao, hivyo  yalikuwa yakisogea umbali kadhaa tu. tazama mfano wa picha juu.

Lakini vazi hili aliloonyeshwa Isaya lilikuwa ni la kipekee sana, lenyewe lililijaza Hekalu zima mbinguni, kuonyesha utukufu wake ni Zaidi sana ya ule utukufu wa mavazi  ya kidunia aliyoyazoea.

Isaya 6:1 “Katika mwaka ule aliokufa mfalme Uzia nalimwona Bwana ameketi katika kiti cha enzi, kilicho juu sana na kuinuliwa sana, NA PINDO ZA VAZI LAKE ZIKALIJAZA HEKALU.

2 Juu yake walisimama maserafi; kila mmoja alikuwa na mabawa sita; kwa mawili alifunika uso wake, na kwa mawili alifunika miguu yake, na kwa mawili aliruka.

3 Wakaitana, kila mmoja na mwenzake, wakisema, Mtakatifu, Mtakatifu, Mtakatifu, ni Bwana wa majeshi; dunia yote imejaa utukufu wake”.

Sasa, Isaya alionyeshwa tu katika lugha ya picha, lakini sisi tunaoishi agano jipya tunajua maana halisi ya Pindo la vazi la Mungu ni nini, na lina umuhimu gani kwetu. Mtu wa kwanza aliyelitambua hilo ni yule mwanamke aliyetokwa na damu kwa muda wa miaka 12 bila kupata tiba yoyote. Lakini siku alipokwenda kuligusa pindo la vazi la Yesu, alijua lilibeba ufunuo gani, japo alilipata  kwa shida sana kwasababu halikuwa refu, na umati mkubwa wa watu ulikuwa unamsonga lakini alipobahatika kugusa tu, muda ule ule ugonjwa wake sugu, uliisha.

Mathayo 9:20 “Na tazama, mwanamke aliyekuwa na ugonjwa wa kutoka damu muda wa miaka kumi na miwili, alikuja kwa nyuma, akaugusa upindo wa vazi lake.

21 Kwa maana alisema moyoni mwake, Nikigusa tu upindo wa vazi lake nitapona.

22 Yesu akageuka, akamwona, akamwambia, Jipe moyo mkuu, binti yangu; imani yako imekuponya. Yule mwanamke akapona tangu saa ile”.

Mpaka baadaye watu wengi, walipoligundua hilo, kumbe hata katika pindo tu la vazi lake kuna uponyaji, na sio lazima upate vazi lake zima..wakawakusanyana makutano mengi, wakawa wanaomba Bwana akipita angalau awaruhusu watu wale waliguse pindo la vazi lake, wapone.. Na wote waliogusa kweli waliponywa..

Marko 6:56 “Na kila alikokwenda, akiingia vijijini, au mijini, au mashambani, wakawaweka wagonjwa sokoni, wakamsihi waguse ngaa pindo la vazi lake; nao wote waliomgusa wakapona”.

Ni nini Bwana alikuwa anawaonyesha?

Sasa kwa kipindi Yesu alipokuwa duniani, vazi lake lilikuwa ni la kawaida tu, haliburuzi kwasababu alikuwa hajawa bado mfalme, lakini sasa anaketi kama MFALME MKUU huko mbinguni, na kama tunavyojua wafalme wenye nguvu sana ni lazima wavae mavazi ambayo pindo zake zinaburuza chini,walau kwa mita kadhaa.

Lakini Isaya anaonywesha maono, ya Kristo akiwa kwenye kiti chake cha Enzi, na vazi lake halipo pale tu alipo, bali limeburuza mpaka kufikia hatua ya kulijaza hekalu zima. Haleluya..

Na kama tunavyojua HEKALU la Kristo ni Kanisa lake, yaani mimi na wewe.

1Wakorintho 3:16 “Hamjui ya kuwa ninyi mmekuwa hekalu la Mungu, na ya kuwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu”?

Hiyo ni kuonyesha kuwa Kristo anaponya kweli kweli, na uponyaji wake sasa, si kama ule wa zamani,  ambapo alikuwa bado hajaketi kama Mfalme mwenye vazi refu,.. Lakini Kama tu alivyokuwa duniani aliponya kwa namna isiyokuwa ya kawaida vile, vipi wakati huu ambapo, uponyaji wake umesambaa katika kanisa lake lote, mahali popote, sehemu yoyote, wakati wowote..Mwite tu Kristo atakuponya. Kama unao ugonjwa unakusumbua, mwite Kristo atakuponya hapo ulipo. Kwasasa huhitaji nabii Fulani, au mtume Fulani, au mchungaji Fulani, au mwalimu Fulani akuombee, wewe mwenyewe ulipo vazi lake, linakufikia ukiwa hapo chumbani kwako unamwomba..Vazi hilo limefika kwako.

Vilevile, ataiponya na Roho yako, ikiwa tu utamwita kwa moyo wa kweli wa kumaanisha. Kristo amemwaga utukufu wake kweli kweli, usiruhusu neema ya wokovu ikupite hivi hivi, kwasababu upo wakati atasimama katika kiti chake che enzi, na neema itakuwa imekwisha kabisa.. bali atasimama kuhukumu.

Je!, unatambua hilo? Unatambua kuwa kanisa tunaloishi ndio kanisa la mwisho lijulikanalo kama Laodikia? Na kwamba hakutakuwa na kanisa lingine Zaidi ya hili kulingana na maandiko katika kitabu cha Ufunuo 1-3. Unasubiri nini mpaka neema ikupite, ukifa leo huko utakapokwenda utakuwa mgeni wa nani, mambo ya dunia ndio unayoyahangaikia lakini mambo ya ufalme wa mbinguni, umeyatupilia kando, hujui kuwa ndio shetani anavyotaka uendelee kuwa hivyo, ili siku ile ikujie ghafla uachwe. Yatafakari maisha yako, ufanye uamuzi sahihi, kwasababu hapa duniani hatuna muda mrefu rafiki yangu. Ulijue tu hilo. Unyakuo upo karibu sana.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Nini maana ya “mkilichukia hata vazi lililotiwa uchafu na mwili”?

kwanini yule kijana aliitupa ile nguo ya kitani chini na kukimbia uchi?

Ni nani aliyesema “Nitume mimi”? katika (Isaya 6:8)

UFUNUO: Mlango wa 11

JE! NI WAPI UTAPOKEA HISIA ZA KWELI ZA KI-MUNGU?

Rudi nyumbani

Print this post

JE! NI WAPI UTAPOKEA HISIA ZA KWELI ZA KI-MUNGU?

Yapo mambo mengi yasiyo ya kawaida aliyoyafanya Bwana Yesu..Lakini kuna mojawapo ningependa tujifunze leo.. Na jambo lenyewe linapatikana katika habari hii..

Marko 7:32 “Wakamletea kiziwi, naye ni mwenye utasi, wakamsihi amwekee mikono.

33 Akamtenga na mkutano faraghani, akatia vidole vyake masikioni mwake, akatema mate, akamgusa ulimi,

34 akatazama juu mbinguni, AKAUGUA, akamwambia, Efatha, maana yake, Funguka”.

Uponyaji wa mtu huyu, ulikuwa ni wa kitofauti sana na ponyaji nyingine zote Yesu alizozifanya.. Kwani nyingine zilihitaji Yesu kutamka tu, au kutoa maagizo Fulani machache n.k., lakini hili lilihitaji jambo lingine la kipekee sana.. Nalo ni hisia za ndani kabisa za rohoni.

Bwana alipomwita huyu mtu, na kujua tatizo lake, moja kwa moja akamwekea vidole vyake masikioni, kisha akatema mate akamgusa ulimu..Sasa hakuishia hapo tu kama alivyofanya kwa baadhi ya watu wengine aliowaponya, labda kuwapa maagizo Fulani, kama alivyofanya kwa huyu tunayemsoma katika Yohana 9:6 …

Yohana 9:6 “Alipokwisha kusema hayo, alitema mate chini, akafanya tope kwa yale mate. Akampaka kipofu tope za macho,

7 akamwambia, Nenda kanawe katika birika ya Siloamu, (maana yake, Aliyetumwa). Basi akaenda na kunawa; akarudi anaona”.

Hapana, lakini kwa huyu, ilihitaji Yesu achukue hatua nyingine Zaidi ya rohoni.. Ya kuugua, Ya kuona huruma ya kupitiliza juu ya mtu huyu ambaye alikaa katika hali hiyo ya utasi na uziwi kwa muda mrefu..Ilihitaji aihisi hali yake kwa undani Zaidi isivyokuwa kawaida.

Hivyo ili kupata hisia hizo ilimbidi sasa, ajue ni wapi atazitolea, kwasababu hivi hivi tu haziji vinginevyo atakuwa unafanya kinafki..Ndipo hapo akatazama juu mbinguni..

Alijua huruma ipo kwa Mungu tu mbinguni, alijua upendo upo juu, alijua uponyaji wa kweli unatoka kwa Baba yake juu na si kwa mwingine awaye yote..sasa kitendo cha yeye kuelekeza uso wake mbinguni, ilimsaidia kuvuta kwa haraka ile huruma ya ki-Mungu ndani yake, na hapo hapo akajikuta ANAUGUA sana moyoni..huruma ikamjaa isiyokuwa ya kawaida, na pindi aliporudisha macho yake tu chini, hakumwona yule mtu kama alivyomwona hapo mwanzo.. Bali alimwona kwa jicho la huruma nyingi sana, na ndipo saa hiyo hiyo aliposema EFATHA..yaani funguka..Na yule mtu akawa mzima kabisa.

Ni nini tunajifunza?

Hatuwezi kuwahurumia wengine, hatuwezi kuwaganga wengine mioyo, hatuwezi kuwasaidia wengine ikiwa tu hisia hizi hatuna ndani yetu, ikiwa macho yetu, wakati wote hatuyaelekezi mbinguni, tusitegemee tutaugua mioyoni mwetu kwa Kristo alivyokuwa anaugua kwa ajili yetu.

Mpaka kupelekea kuwa tayari kuuawa kwa ajili yetu sisi tulio dhambini..

Bwana Yesu alisema..

Luka 6:36 “Basi, iweni na huruma, kama Baba yenu alivyo na huruma”.

Luka 7:12 “Na alipolikaribia lango la mji, hapo palikuwa na maiti anachukuliwa nje, ni mwana pekee wa mamaye ambaye ni mjane, na watu wa mjini wengi walikuwa pamoja naye.

13 Bwana alipomwona alimwonea huruma, akamwambia, Usilie”.

Huruma za Yesu utazisome sehemu nyingi sana kwenye maandiko kwa muda wako unaweza kuvipitia hivi vifungu Marko 6:34, Mathayo 9:36, 20:34,

Kumbuka Upendo wa kweli, huruma ya kweli inatoka kwa Mungu tu peke yake. Ndicho Yesu alichokifanya.. hakuwatazama wanadamu ndipo kuugua kuje ndani yake, hakuitazama milima, hakuwatazama wanyama bali alitazama juu mbinguni Baba yake mwenye rehema alipo, ndipo huruma ikamjaa moyoni.

Nasi pia tuyaelekeze macho yetu mbinguni, ili tupokee hisia hizi za kweli za Mungu, hisia ambazo zitavuta uponyaji wa ki-Mungu kwa haraka sana. Hisia ambazo zitajenga kuombeana na kusaidiana, Na kuhudumiana.

Na kuelekeza macho yetu mbinguni, maana yake si kuangalia angani, hapana, bali ni kumsoma Mungu wetu kwa bidii, na kujua anataka nini kwetu, na hiyo inakuja kwa kulitafakari Neno lake, pia kwa kusali, na kufunga na kumfanyia ibada..

Hayo yote tukiyafuata itatupelekea kuzipokea hisia hizi za Kristo kwa wingi wote, na matokeo yake tutafukuza roho zote za chuki, na vinyongo, na hasira, fitina, wivu na mashindano ndani yetu.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

BWANA AYAGANGE NA MACHO YETU PIA.

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA WARAKA WA PILI WA YOHANA.

JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?

Je! Kuna malaika wangapi mbinguni?

JE! HAMPOTEI KWA SABABU HII?

Rudi nyumbani

Print this post

JE! HAMPOTEI KWA SABABU HII?

Jina la Bwana wetu Yesu libarikiwe daima. Karibu tuyatafakari maandiko pamoja ndugu yangu.

Wakati ule masadukayo walimfuata Bwana Yesu, na kumuuliza maswali ambayo, ndio yaliyowafanya waamue kuwa  masadukayo kama walivyo wasioamini  kuwa kuna kitu kinachoitwa ufufuo wa wafu. Na swali lenyewe lilikuwa ni kuhusu ndoa baada ya kifo..Walikuwa na sababu nzuri kabisa za kufikirika kwa akili za kibinadamu, kwamba kama kiyama ipo basi Musa asingeruhusu mtu kuoa mke wa mtu baada ya kufa, ili huko ng’ambo kusiwe na migongano ya kindoa,.Lakini kama aliruhusu kuoa mke wa marehemu, ni wazi kuwa mambo yote ni ya hapa hapa duniani, hakuna kufufuliwa wafu.

Embu Tusome kwa ufupi habari yenyewe na pale mwishoni lipo jambo ambalo Bwana atatufundisha siku ya leo..

Anasema..

Marko 12:18 “Kisha Masadukayo, watu wasemao ya kwamba hakuna kiyama, wakamwendea, wakamwuliza na kusema,

19 Mwalimu, Musa alituandikia ya kwamba ndugu ya mtu akifa, akamwacha mkewe wala hana mtoto, ndugu yake amtwae yule mkewe akampatie ndugu yake mzao.

20 Basi kulikuwa na ndugu saba, wa kwanza akatwaa mke, akafa, asiache mzao.

21 Wa pili naye akamtwaa akafa, wala yeye hakuacha mzao. Na wa tatu kadhalika;

22 hata na wote saba, wasiache mzao. Mwisho wa wote yule mwanamke akafa naye.

23 Basi, katika kiyama atakuwa mke wa yupi katika hao? Maana wote saba walikuwa naye.

24 Yesu akajibu, akawaambia, JE! HAMPOTEI KWA SABABU HII, KWA KUWA HAMYAJUI MAANDIKO WALA UWEZA WA MUNGU?

Kama tunavyosoma hapo kulingana na maneno ya Bwana Yesu, aliona watu hao wamepotea, na kupotea kwako kulichangiwa na sababu mbili kubwa, ya kwanza 1) Walikuwa hawayajui maandiko 2) Walikuwa hawaujui uweza wa Mungu.

Hizi ni sababu kuu ambazo zinaweza kumfanya mtu apotee hata leo hii, aidha katika Dini za uongo kama hawa Au arudi nyuma katika ulimwengu kabisa aseme, haya mambo hayawezekani.

  1. Tukianzana na kutokuujua uweza wa Mungu

Hawa mafarisayo, waliishi kwa fikra za kibinadamu na sio kwa fikra za Ki-Mungu, hawakukaa kujiuliza hao malaika wanaishije ishije huko mbinguni, bila kuoana au kuzaliana lakini bado wanaishi kwa furaha mbele za Mungu. Hata leo hii, Hawakujua kuwa Mungu pia anao uwezo wa kuwafanya kama Malaika. Akaondoa katika miili yao tamaa za mwili, wakawa ni miili ya utukufu isiyokuwa na mapungufu, isiyosinzia, isiyoumwa, isiyochoka kama wao..Hilo hawakuliwaza, kwasababu hawakuujua uweza wa Mungu kuwa unaweza kufanya na hilo pia.

Imani kama hizo hata leo zipo katika baadhi ya dini, wakidhani kuwa mtu akifa atakwenda kupewa wake 70 huko mbinguni. Hiyo yote ni kwasababu hatuujui uweza wa Mungu.

Kukosa kuujua uweza wa Mungu hata sasa, kunawafanya watu wengi, wapotee sana, wakidhani pia Mungu hawezi kuwaokoa wanadamu wakiwa hapa duniani..kwa kuwafanya wawe watakatifu..Na hiyo inawapelekea wajidanganye hivyo hivyo kwamba hakuna mtu anayeweza kushinda dhambi akiwa duniani, na matokeo yake wanakufa katika dhambi zao, na mwisho wa siku wanajikuta wapo kuzimu.

Kumbe hawajua uweza huo wa kufanywa wakamilifu hautoki kwa mwanadamu bali kwa Mungu pale mtu anapomwamini na kumpokea. Alisema..

Yohana 1:12 “Bali wote waliompokea ALIWAPA UWEZO wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake;”

Mtu akimwamini Kristo, na kumtii yeye, kitu kinachotokea kwake ni kupokea uwezo mpya, wa kufanyika mwana wake wa kushinda dhambi. Ukishindwa kuyajua hayo, basi ni rahisi sana kupotea..

2) Sababu ya pili ni: Ni kutojua Maandiko.

Tukirudi kwenye lile swali lao walilomuuliza tunaona mbele kidogo Bwana akiwauliza, HAMJASOMA?. Akitazamia kuwa kama wangekuwa wamesoma vema wasingekuwa na swali kama hilo..

Marko 12:26 “Na kwa habari ya wafu ya kwamba wafufuliwa, hamjasoma katika kitabu cha Musa, Sura ya Kijiti, jinsi Mungu alivyomwambia, akisema, Mimi ni Mungu wa Ibrahimu, na Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo?

27 Yeye si Mungu wa wafu, bali wa walio hai. HIVYO MWAPOTEA SANA”.

Unaona? Dini ambayo ilikuwa imeshakita mizizi yenye wafuasi wengi, kama baadhi ya dini nyingi leo hii duniani lakini kumbe ilikuwa imeshapotea kwa kutoyajua tu maandiko.

Leo hii watu wengi wamepotoshwa kwa kutoyafahamu maandiko, ukiona unaabudu sanamu, Ukiona unashikilia sabato na kusema huo ndio muhuri wa Mungu, wakati biblia inasema muhuri wa Mungu ni Roho Mtakatifu (Waefeso 4:30) ujue umepotoshwa na dini, ukiona unaabudu sanamu na kudhani kuwa zile ni viunganishi au vipatanishi na Mungu basi ujue umepotoshwa.

Hivyo sote kwa pamoja ni sharti tuufahamu uweza wa Mungu, kwamba hapa duniani wokovu upo, na watakatifu pia wapo, na kwamba pasipo utakatifu hakuna mtu atakayemwona Mungu asipokuwa nao sawasawa na (Waebrania 12:14) vilevile tuyasome maandiko, tuyatafakari sana, kila siku ili tusije tukazama katika madanganyo ya dini au madhehebu, au upotofu wa kidunia uliopo leo hii duniani.

Tukizingatia hayo mawili kama Bwana Yesu alivyosema, tusahau kupotea.

Bwana akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Tofauti kati ya ufunuo, unabii na maono ni ipi?

KUMBE MUNGU ANAWEZA KUKULIPA KWA USICHOSTAHILI!

Neema ni nini?

Je! Ni dhambi kumpiga au kumuua mnyama bila sababu yoyote?

CHANGIA SASA.

MAPEPO YANATAFUTA HIFADHI NDANI YAKO KWA BIDII SANA.

Rudi nyumbani

Print this post

Tofauti kati ya ufunuo, unabii na maono ni ipi?

  1. UFUNUO

Ufunuo ni jambo ambalo hapo kabla lilikuwa limesitirika au limefungwa lakini sasa limefunuliwa. Kwa mfano katika biblia, utaona, Watu wengi walishindwa kumtambua Yesu ni nani, wengine walidhani ni Yeremia, wengine, mmojawapo wa manabii wa kale, wengine ni Yohana mbatizaji, Lakini Yesu alipowauliza mitume wake, Petro akasema, wewe ndiye Kristo mwana wa Mungu aliye hai. Yesu kusikia vile tunaona akamwambia maneno haya;

Mathayo 16:17 “Yesu akajibu, akamwambia, Heri wewe Simoni Bar-yona; kwa kuwa mwili na damu HAVIKUKUFUNULIA HILI, bali Baba yangu aliye mbinguni.

18 Nami nakuambia, Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala milango ya kuzimu haitalishinda”.

Unaona, Petro alifunuliwa, siri ambayo ilikuwa haijulikani na watu hapo kabla.

Vivyo hivyo na sisi tunahitaji ufunuo wa Roho Mtakatifu kuyaelewa  maandiko vinginevyo tutakuwa tunakisia tu au hatuyaelewi pale tunapoyasoma.

2) MAONO.

Ni taarifa ya rohoni ambayo mtu anapokea kutoka kwa Mungu,aidha anapokuwa usingizini, au akiwa macho. Anajikuta anaona vitu ambavyo hakupanga kuviona, na taarifa hizo zinaweza kuwa kwa mafumbo, au kwa uwazi, na zinaweza kueleza matukio yaliyopita au ya hapo hapo, au yale yatakayokuja baadaye.

Katika biblia tunaona watu wengi sana wakionyeshwa Maono..

Matendo 10:1 “Palikuwa na mtu Kaisaria, jina lake Kornelio, akida wa kikosi kilichoitwa Kiitalia,

2 mtu mtauwa, mchaji wa Mungu, yeye na nyumba yake yote, naye alikuwa akiwapa watu sadaka nyingi, na kumwomba Mungu daima.

3 Akaona katika maono waziwazi, kama saa tisa ya mchana, malaika wa Mungu, akimjia na kumwambia, Kornelio!

4 Akamtazama sana, akaogopa akasema, Kuna nini, Bwana? Akamwambia, Sala zako na sadaka zako zimefika juu na kuwa ukumbusho mbele za Mungu.

5 Sasa basi, peleka watu Yafa, ukamwite Simoni, aitwaye Petro”.

3) UNABII

Ni taarifa ya wakati ujao, (utabiri wa rohoni), ambayo Mungu anautoa moja kwa moja, hiyo inaweza kuwa katika maneno ya mtu anayozungumza bila yeye kujua, mfano utasoma mstari huu kuhani mkuu alitoa unabii pasipokujua kama yeye aliutoa.

Yohana 11:51 “Na neno hilo yeye hakulisema kwa nafsi yake; bali kwa kuwa alikuwa Kuhani Mkuu mwaka ule, alitabiri ya kwamba Yesu atakufa kwa ajili ya taifa hilo”.

au kwa njia ya kuambiwa au kuhubiriwa,

Ufunuo 11:3 “Nami nitawaruhusu mashahidi wangu wawili, nao watatoa unabii siku elfu na mia mbili na sitini, hali wamevikwa magunia”.

Hii ikiwa na maana kuwa katikati ya mafundisho, au mahubiri, Mungu huwa anatoa unabii wa mambo yajayo ndani yake.

1Timotheo 1:18 “Mwanangu Timotheo, nakukabidhi agizo hilo liwe akiba, kwa ajili ya maneno ya unabii yaliyotangulia juu yako, ili katika hayo uvipige vile vita vizuri”;

Kwa njia ya kuonyeshwa au kwa maono.

Yuda 1:14 “Na Henoko, mtu wa saba baada ya Adamu, alitoa maneno ya unabii juu ya hao, akisema, Angalia, Bwana alikuja na watakatifu wake, maelfu maelfu”,

Pia  kitabu chote cha Ufunuo ni kitabu kitabu cha unabii, ambacho Yohana alionyeshwa kwa njia ya maono.

Ufunuo 22:6 “Kisha akaniambia, Maneno haya ni amini na kweli. Naye Bwana, Mungu wa roho za manabii, alimtuma malaika wake kuwaonyesha watumwa wake mambo ambayo hayana budi kuwako upesi.

7 Na tazama, naja upesi; heri yeye ayashikaye maneno ya unabii wa kitabu hiki”.

Bwana akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

CHUKIZO LA UHARIBIFU

Mafundisho

UFUNUO: Mlango wa 1

Tofauti kati ya ndoto na Maono ni ipi?

THAWABU YA UAMINIFU.

Rudi nyumbani

Print this post

THAWABU YA UAMINIFU.

Kwa kawaida Mungu huwa hatoi karama zake zote kwa mkupuo, bali huwa anakupa kwanza kidogo kisha anaupima auminifu wako au uadilifu wako katika hicho, kisha akishaona umekithaminisha ndipo baadaye anakumwagia vyote vilivyobakia kwa wingi.

Leo tutaitazama mifano miwili ya watu walioambiwa maneno hayo naamini kwa kuisoma itakuongeza nguvu katika eneo hili la uaminifu,, wa kwanza tutauona kutoka katika maandiko na wa pili katika shuhuda za watu walitutangulia kwenye Imani.

Katika biblia, tunaona mtu mmoja aliyeitwa Yoshua, kuhani mkuu, ambaye Mungu alimwambia maneno haya;

Zekaria 3:6 “Kisha malaika wa Bwana akamshuhudia Yoshua, akisema,

7 Bwana wa majeshi asema hivi, Kama ukienda katika njia zangu, na kama ukishika maagizo yangu, ndipo utakapoihukumu nyumba yangu, nawe utazilinda nyua zangu, NAMI NITAKUPA NAFASI YA KUNIKARIBIA KATI YAO WASIMAMAO KARIBU”.

Huyu Yoshua alichaguliwa na Mungu kuwa kuhani mkuu wakati ule ambapo wana wa Israeli wanaondolewa tena Babeli, kumbuka huyu si yule Yoshua aliyewavusha wana wa Israeli Yordani, kutoka jangawani hapana, bali ni mwingine kabisa.

Sasa wakati akiwa Yerusalemu, Mungu akamchagua na kumtakasa, akamtia mafuta, awe kuhani wake, kuwapatanisha wayahudi wote.. Lakini tunasoma ahadi nyingine hakuzipokea palepale, bali zilitegemea kwanza uaminifu wake, ndipo Mungu ampatie ahadi hizo baadaye..

Mungu alimwahidi kuwa ikiwa atakuwa mwaminifu, ndipo ataihukumu nyumba yake, na vilevile atampa nafasi ya kumkaribia yeye, kati ya hao wasimamao karibu yake. Ulishawahi kujiuliza ni wakina nani hao wasimamao karibu na Mungu?.. Hapa duniani sio watu wote watakuja kusimama karibu na Mungu tutakapofika kule ng’ambo hata kama watakuwa wameokoka.

Ni sawa na leo hii, si watu wote wanaweza kusimama karibu na raisi wa nchi, kama hawajaalikwa na yeye, au kama hawana nafasi yoyote au cheo chochote katika serikali. Utagundua ni mawaziri tu, na watu wakubwa wakubwa wa serikalini, au familia yake tu ndio wanaoweza kumkaribia yeye. Lakini wengine wote mtakuwa mkimtazama kwenye Tv, au majukwaani.

Na vivyo hivyo kwa Mungu, wapo watu tayari ambao wameshawekwa karibu na Mungu,kutokana na uaminifu wao wa juu walipokuwa hapa duniani, katika maandiko tunawafahamu baadhi, wa kwanza ni Ibrahimu,

Mathayo 8:11 “Nami nawaambieni, ya kwamba wengi watakuja kutoka mashariki na magharibi, nao wataketi pamoja na Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo katika ufalme wa mbinguni;”

Wengine wakiwemo, akina Musa na Eliya, Wakina Danieli, watu waliopendwa na Mungu, wengine ni Ayubu, Samweli, akina Daudi aliyeupendeza moyo wa Mungu, Henoko, Mitume 12 wa Yesu, ambao Bwana aliwaahidia wataketi katika viti 12 wakiyahukumu makabila 12 ya Israeli, Yohana mbatizaji ambaye katika uzao wa wanawake hakuna aliyewahi kuwa mkuu Zaidi yake, wengine ni kama Mtume Paulo ambaye alitenda kazi kuliko wakristo wote wa wakati ule. Na pia wale mashahidi wawili ambao tunawasoma katika  ufunuo ambao wanafananishwa na ile mizeituni miwili,N.k.

Ufunuo 11:4 “Hao ndio ile mizeituni miwili na vile vinara viwili visimamavyo mbele za Bwana wa nchi”.

Sasa hawa wote, ni watu ambapo wanasimama karibu sana na Mungu.. Hivyo Yoshua naye kama kuhani mkuu aliahidiwa ofa hiyo, kwamba kama akiwa mwaminifu, na yeye pia ataingizwa katika kundi  hilo dogo la watu watakaosimama karibu na Mungu, tengeneza picha unasimama karibu na Mungu muumba wa Mbingu na nchi na malaika..si jambo dogo hilo. Na sisi pia tutamani nafasi hizo.

Vivyo hivyo, leo tutamtazama mtu mwingine ambaye alitokea katika kizazi chetu aliyeitwa WILLIAM BRANHAM.

Ikiwa hujawahi kumfahamu mtu huyu, ushuhuda wake ulikuwa ni wa kipekee sana, hatuwezi eleza habari yake yote hapa,  lakini, kwa ufupi ni kuwa alizaliwa mwaka 1909, huko Marekani, katika familia ya kimaskini sana, elimu yake iliishia darasa la saba tu, lakini tangu akiwa mdogo Mungu alianza kumuonyesha maono mengi, ambayo mengine hakujua tafsiri yake ni nini, mengine aliyaona yakitimia muda mfupi baadaye,..Lakini alipokuwa mtu mzima, akiwa kama mchungaji wa kanisa dogo la kibaptisti baada ya kupitia shida nyingi, ikiwemo kufiwa na mke na mtoto wake, hakuacha kumtafuta Mungu kwa bidii.

Siku moja usiku wakati anasali kama saa 9 hivi, kumuuliza Mungu ni nini maana kusudi lake duniani, alitembelewa na Malaika wa Bwana, akamwambia, nimetumwa kutoka uweponi mwa Mungu, kukuambiwa kuwa maisha yako ya kutokueleweka, ni kukuonyesha kuwa Mungu amekuchagua kulibeba kusudi lake kwa watu..Akaambiwa atapewa karama ya uponyaji, na kama akiwa mwaminifu utafika wakati utakuwa na uwezo wa kujua hata siri za mioyo ya watu, na hukuna ugonjwa wowote utakaoisimama mbele yako hata saratani yenyewe..(Kwa kipindi hicho ugonjwa wa saratani ndio uliokuwa tishio duniani)

Ni kweli mtu huyu baada ya hapo alionyesha uaminifu wake kwa Mungu, na yote aliyoahidiwa yalikuja kutimia muda mfupi sana katika huduma yake .. alianza kufahamu siri za mioyo ya watu, wote waliosimama mbele yake katika mstari kuombwa, Na Zaidi ya hayo Mungu akamzidishia na ishara za ajabu, ilifikia wakati nguzo ya Moto ilitokea na kutua Juu yake, mbele ya kanisa akiwa anahubiri, na ikapigwa picha na kuwekwa katika makumbusho za kihistoria huko Marekani, baada ya kuthibitishwa na FBI, kuwa picha hiyo ni ya kimiujiza, ndio hiyo hapo unayoina katika katika ujumbe huu.

Si hilo tu wakati Fulani akiwa anawabatiza watu katika mto mmoja huko Marekani mwaka 1933, ghafla kulitokea nuru kubwa kama nyota na kutua juu yake, watu wote waliokuwepo pale waliiona, habari hizo zilishapishwa katika magazeti mengi maarufu huko Marekani..Na wakati alipokuwa akiwabatiza watu anasema alisikia sauti ikimwambia kama vile Yohana mbatizaji alivyotumwa kutangulia kuja kwa kwanza kwa Kristo, vivyo hivyo na ujumbe wako utatangulia kuja kwa pili kwa Kristo.

William Branham mpaka sasa, ni mwinjilisti ambaye wanazuoni na wanatheolojia wa dini wanamkumbuka kwa ishara na maajabu yaliyokuwa yanafuata naye katika huduma yake. Ya kuhubiri injili ulimwenguni kote.

Ikiwa utapenda kupata historia yake ndefu..tutumie ujumbe inbox ..

Lakini hiyo yote ni kutokana na uaminifu aliokuwa nao kwa Bwana.. Hakuhubiri udhehebu, kinyume chake, aliikemea roho za kidhehebu ambazo zinawafunga wakristo wasimtambue Mungu, na hiyo ikampelekea kuchukiwa sana na watu wa dini. Injili yake iliegemea katika kuwaelekeza watu kwa Yesu, na sio kwake, au kwa mtu Fulani, alikemea dhambi, hususani katika uvaaji mbaya wa wanawake.. Na matokeo yake Bwana akamtukuza na yeye. Mafundisho yake yaliegemea katika Misingi ya Neno tu.

Hivyo Ujumbe wake umekuwa kama MBIU kwa kanisa la mwisho la Laodikia ambalo ndio sisi tunaoishi, kwamba tutoke huko kwenye Kamba za udini na udhehebu tumwabudu Mungu katika Roho na Kweli.William ni mjumbe wa kanisa la letu la Laodikia.

Sasa kwa mifano hiyo miwili ,nataka  uone ni jinsi gani, Mungu anauthamini uaminifu wa mtu. Hata Musa kule jangwani aliuthamini kwanza muujiza wa kijiti kuteketea moto, ndipo Mungu akampa na mingine kikubwa Zaidi.  Kila mmoja wetu anapaswa awe mwaminifu katika kitu alichopewa na Mungu. Leo hii utaona Mungu kampa mchungaji kanisa, na kwa neema zake limeanza kukua kidogo, lakini itapita miaka miwili, mitatu, utasikia amefumaniwa katika uzinzi, mwingine amejilimbikizia mali zote za kanisa.. huko ni kukosa uaminifu kwa kile ulichopewa na Mungu.

Mungu anaweza kukupa karama Fulani katika kanisa, lakini baada ya kipindi Fulani unaanza kujiona wewe ni wewe, unaanza kuonyesha kiburi, huko ni kukosa uaminifu kwa kile kidogo ulichopewa. Unabadilika kama Yeroboamu unasahau kuwa ni Mungu ndiye aliyekupa,.. Kila mmoja wetu alieyokoka, kuna kitu Mungu amempa lakini tukishindwa kuwa waamifu navyo, tukavidharau, tukawa hatuvitendei kazi, kamwe tusitazamie kuwa Mungu atakaa atupe ahadi nyingine za juu zaidi ambazo alikuwa amekusudia kutupa.

Hivyo kuanzia leo mimi na wewe tuanze kujenga uaminifu kwa vile vichache Bwana alivyotupa.

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

HISTORIA YA WILLIAM BRANHAM

KAMA MKRISTO FAHAMU ZIPO HATUA UTAPIGISHWA NA MUNGU.

KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 1

JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?

UFUNUO: Mlango wa 19

Rudi nyumbani

Print this post

Je! ni sahihi kwa mkristo kujifukiza?

SWALI: Nina swali mtumishi. Je mkristo aweza kujifukiza katika kipindi hiki cha changamoto za kupumua. Biblia inasema nini juu ya hili. Je, neno hili kwenye Ayubu 5:3 inazuia kujifukizia?

Ayubu 5:3 “Nimewaona wapumbavu wakishusha mizizi; Lakini mara niliyalaani maskani yake”.

JIBU: Kujifukiza ni tiba mojawapo kama zilivyo tiba nyingine. Mtu mmoja anaweza kuumwa na akaenda kumeza dawa za hospitalini, na mwingine akaenda kuchemsha mwarobaini akanywa. Na wote wakawa wazima.

Jambo ambalo si sahihi, ni pale tiba hiyo inapotolewa “sadaka kwa sanamu” nikiwa na maana kuwa pale inapohusianishwa na uganga au Imani potofu ambazo mara nyingi zinaambatanisha na masharti Fulani ambayo hata hayana uhusiano wowote na hiyo dawa kwamfano labda utaambiwa unywapo sema maneno Fulani, au nenda kainywee makaburini, au usinywe mbele ya watoto wako, au unyapo hakikisha upo uchi n.k… Sasa hizo ndio Mungu amekataza kwasababu ni ibada za sanamu.

Lakini tukirudi kwenye huo Mstari wa Ayubu 5:3 haizungumzii mizizi hii tunayoifahamu kama dawa, hapana, bali habari hiyo inazungumzia jambo lingine kabisa jinsi wenye dhambi wanavyoweza kujiimarisha kiasi cha kukita mizizi chini, wakijiwekea hazina nyingi, na kujijengea maboma makubwa, lakini hata hivyo, Mungu atawalaani na kuziangamiza maskani zao. Ukianzia kusoma tokea mistari ya juu utapata picha kamili ya habari hiyo.

Hivyo, kwa mkristo kujivukiza, si makosa, lakini pia ni vizuri tukajua sababu ya magonjwa haya kulipuka ni nini. Mungu hajayaleta ili tuyatafutie tiba hapana, Bali haya ni mapigo kutoka kwa Mungu na hilo lipo wazi yanayotutambulisha kuwa sisi kama dunia tumemsahau yeye, na pia  tunaishi katika siku za mwisho sawasawa na maneno ya Yesu katika , (Luka 21:11).

Swali ni je! Umeokoka? Je Yesu yupo ndani yako? Kama jibu ni hapana, basi ujue upo katika wakati wa hatari sana. Na wewe upo ndani ya hiyo hiyo ghadhabu ya Mungu iliyoachiliwa wakati huu tunaoishi, Hivyo fanya uamuzi wa busara, mkaribishe Yesu maishani mwako katika dakika hizi za majeruhi tunazoishi, Kabla mabaya hayajakufikia.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

https://wingulamashahidi.org/2019/09/01/je-ni-vema-kwa-mkristo-kwenda-hospitali-au-kutumia-miti-shamba-anapougua/

Rudi nyumbani

Print this post

Nini maana ya “Ulipo mzoga, ndipo watakapokutanika tai?

SWALI: Shalom naomba kufahamu maana ya huu mstari..

Luka 17:37 “Wakajibu, wakamwuliza, Wapi, Bwana? Akawaambia, Ulipo mzoga, ndipo watakapokutanika tai”.


JIBU: Kabla ya wanafunzi wa Yesu kumuuliza Bwana hilo swali “WAPI?”..Kuna maneno ambayo yalitangulia juu kidogo, ambayo tukiyasoma yatatusaidia kuelewa vizuri huo mstari ulimaanisha nini, embu tusome kidogo.

Luka 17:22 “Akawaambia wanafunzi, Siku zitakuja mtakapotamani kuona siku moja katika siku zake Mwana wa Adamu, msiione.

23 Tena watawaambia, Tazama, kule! Tazama, huku! Msiondoke mahali mlipo, wala msiwafuate”;

Ukisoma kwenye Mathayo imeeleza kwa undani zaidi, inasema..

Mathayo 24:23 “Wakati huo mtu akiwaambia, Tazama, Kristo yupo hapa, au yuko kule msisadiki.

24 Kwa maana watatokea makristo wa uongo, na manabii wa uongo, nao watatoa ishara kubwa na maajabu; wapate kuwapoteza, kama yamkini, hata walio wateule.

25 Tazama, nimekwisha kuwaonya mbele.

26 Basi wakiwaambia, Yuko jangwani, msitoke; yumo nyumbani, msisadiki”.

Maneno hayo Yesu aliyatanguliza kama angalizo la nyakati za hatari zitakazotokea siku za mwisho, akiwaonya kwamba wengi watakuja wakiwavuta watu kwao wakiwaambia Kristo yupo huku au kule, kwa maneno yao ya ushawishi, wakijinadi, tuna hichi au kile, sisi tuna miujiza mikubwa, sisi tuna upako wa mafuta mabichi, sisi ni wataalumu wa tiba za kiroho, sisi tuna makanisa makubwa kuliko yote duniani n.k.

Hivyo Yesu kwa kulijua hilo kwamba litakuja kutokea akawapa tahadhari wanafunzi wake kwamba wasitoke kuwafuata, wasiwe wepesi kuwaendea, wabaki mahali walipo, wasiende popote, kwasababu watawapotosha..

Sasa katika mazingira hayo ya kutokwenda mahali popote ndipo wanafunzi wake mwishoni wakamuuliza swali, NI WAPI sasa patakuwa sahihi pa kwenda..au tutakwenda wapi?

Ndipo Yesu akawaambia palipo na mzoga ndipo watakaposanyika Tai.. Ikiwa na maana mahali palipo na chakula cha Tai ndipo watakapokuja hapo na kukusanyika..

Na kama tunavyojua ndege aina ya tai wanaouwezo wa kuona mbali sana, leo hii kama kuna mnyama kafa porini na angani hakuna ndege yoyote, ukikaa baada ya muda mfupi utawaona tai wengi wamekusanyika hapo.. utajiuliza wametokea wapi na wakati anga lilikuwa jeupe halina ndege hata mmoja? Ni kwasababu jicho la Tai huwa linaona chakula kutokea mbali sana. Tai anaona mahali ambapo wewe huwezi kumwona.

Ni kama tu vile, mahali Fulani pawe na kinyesi cha mnyama au mtu, dakika si nyingi utaona nzi wengi wamekusanyika, na utajiuliza wametoka wapi wadudu hao na mahali hapo ni porini..Jibu ni kwamba, Mungu kawaumbia uwezo mkubwa wa kunusa vitu vya asili yao, tokea mbali, na ndio maana utawaona hata kama eneo hilo limejificha namna gani, wataenda tu.

Vivyo hivyo na wana tai wa Mungu, Kristo kawawekea uwezo Fulani wa kujua chakula chao halisi kilipo haijalishi ni wapi walipo watakipata tu. Tai si kama kuku, ambaye anaona vya hapo chini tu, bali Tai anaona vya mbali sana. Vivyo hivyo na sisi kama ni wanatai, ni lazima tuwe wa kufuata kile chakula kilicho chetu tu..Si kila chakula cha kukikurupukia kisa kipo karibu na sisi, au kinavutia..

Bali tuwe na macho ya tai ya kujua chakula chetu kipo wapi..

Hizi siku za mwisho, usiwe wa kukurupukia kila aina ya mafundisho, au imani. Kristo ameshatuonya..

Tafuta chakula cha wakati wako unaoishi.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Mada Nyinginezo:

Rudi nyumbani

Print this post