Category Archive Home

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

Siku ya unyakuo itakukutaje?


Shalom.Jina la Bwana wetu Yesu Krito libarikiwe.

Karibu tujifunze Biblia..Je unajua kuwa kuna siku Kristo atakuja kuwachukua wateule wake? Na kwenda nao mbinguni?..Je unajua watakaokwenda mbinguni ni wachache sana?…Biblia inasema njia ile imesonga na mlango ni mwembamba?..

Mathayo 7:14 “ Bali mlango ni mwembamba, na njia imesonga iendayo uzimani, nao waionao ni wachache”.

Je unajua…baada ya unyakuo kupita…watu watakaoachwa watajuta sana?..Wengi watatamani muda urudishwe dakika 5 tu nyuma angalau watubu…lakini watakuwa wameshachelewa…Je unajua karibia kila mtu duniani tayari kashaonyeshwa aidha kwa ndoto au kwa maono siku ya unyakuo? awe mwenye dhambi au asiye mwenye dhambi…tayari kashaota ndoto angalau moja inayohusiana na kurudi kwa Kristo mara ya pili?. Na wengi wao wanaoonyeshwa hayo wanakuwa wameachwa?..Na wanapata hisia kali sana baada ya kuamka na wanashukuru Mungu imekuwa ni ndoto na wala si kitu cha kweli?.

Binafsi nilishawahi kuota ndoto kama hizo mara kadhaa zamani sana…na zote nilikuwa najiona nimeachwa ni chache sana nilijiona nimekwenda na Bwana lakini nyingi nimeachwa.…na nikiwa ndani ya ndoto nilikuwa nalia na kuomboleza na kumwomba Mungu anirudishe muda angalau dakika 5 nyuma kabla ya unyakuo nirekebishe mambo yangu!…na nikishtuka kutoka usingizini nashukuru Mungu kwamba ni ndoto na si kitu halisi..Hivyo nakwenda kutubu na kumuahidi Mungu kuzidi kujitakasa ili nisije nikaachwa kwenye unyakuo halisi utakapofika…

Lakini yote hayo ni tisa..kumi ni siku tutakayokutana na tukio lenyewe la kuachwa kwenye unyakuo!!…

Siku moja, muda mrefu kidogo umepita, tulikuwa ndani ya nyumba nyakati za jioni kama saa moja na nusu hivi usiku…Umeme ulikatika mtaa mzima..Kukawa na giza lile tororo kabisa..tukaamua kutoka ndani kukaa nje…Na Mahali tulipokuwa tunaishi sio mahali penye watu wengi wanaojichanganya na wengine ni mahali ambapo ikifika jioni tu ni kimyaa na kila mtu kajifungia kwake..Sasa wakati tumekaa nje kidogo tulikuwa wawili mimi na ndugu yangu…tukasema hebu tutazame juu kidogo tuangalie nyota utukufu wa Mungu mbinguni…

Siku hiyo haikuwa na mawingu hivyo nyota zilikuwa zinaonekana vizuri hata zile zinazotembea….….Sasa wakati tunatazama juu ulitokea mwanga fulani wa ajabu wenye rangi unaokaribiana na blue hivi unaong’aa sana, kama mita 5 hivi juu yetu..ukimulika kutokea upande wa magharibi kuelekea upande wa mashariki..na ulikuwa kama unasogea hivi…. Haukuwa na sauti hata kidogo lakini ulikuwa na mwangaza mkali na ulidumu kwa muda kama wa sekunde 3 hivi au Zaidi kidogo..halafu ukatoweka!..ulimulika pale tulipokuwepo kote kukawa kama mchana hivi…

Haukuwa mwanga wa radi kwasababu kipindi hicho kilikuwa ni kipindi cha kiangazi, na wala haikuwa ile mianga inayotokea inamulika bila sauti yoyote wakati wa vipindi vya mvua. Siku hiyo juu hakukuwa na wingu hata moja ni nyota tuu zilikuwa zimetanda anga zima..tokea kaskazini, kusini mashariki mpaka magharibi..hakukuwa na dalili ya wingu…Na mwanga huo hakuja na sauti yoyote…Nakumbuka siku chache tu nyuma tulikuwa tunazungumzia masuala ya unyakuo..Na tulikuwa tunaufahamu ule mstari unaosema…

Luka 17:24 “kwa kuwa, kama vile umeme umulikavyo toka upande huu chini ya mbingu hata upande huu chini ya mbingu, ndivyo atakavyokuwa Mwana wa Adamu katika siku yake.”

Kwahiyo baada ya tukio hilo..Mstari huo ukaja kichwani haraka sana!…tukajua kwamba kuna uwezekanano tayari unyakuo umeshapita na tumeachwa…Baada ya hapo ilikuja hisia moja ambayo siwezi kuilezea, ambayo tangu huo wakati ndio ikanifanya nisichukulie tena kiwepesi suala la kubaki kwenye unyakuo…

Nilihisi kuvunjika moyo na kujuta majuto ambayo sijawahi kuyajuta…Nilianza siku zote nilikuwa nafanya nini mpaka siku hii imenikuta kama mjinga…Nikaanza kuwaza siku chache tu mbeleni nakwenda kumshuhudia mpinga-Kristo kwa macho yangu..siku chache mbeleni nakwenda kupokea chapa…siku chache mbeleni nakwenda kukutana na dhiki kuu, kama sitakufa basi nitashuhudia mapigo yote yale yaliyoandikwa kwenye kitabu cha Ufunuo sura ya 16, maji kuwa damu, jua kutiwa giza, mvua ya mawe n.k..Nikawaza siku chache tu mbeleni hakutakuwa tena na ndugu, wala mama, wala marafiki…wala hakutakuwa tena na kitu kinachoitwa nyumbani…wala hakutakuwa tena na kufanya kazi..Mwisho wa mambo yote umeshafika!.

Nikawaza tena wakati huu sasa hivi watakatifu, waliojitakasa na kuyachukia Maisha yao kwaajili ya Kristo wanafarijiwa mbinguni..sasa hivi Paulo, anafutwa machozi na tabu zake zote zinageuzwa kuwa furaha…Nikarudi kuwaza tena..Nikifa katika dhiki kuu ninakwenda kusimama mbele ya kiti cha hukumu..kuonana uso kwa uso na Yesu Kristo… na mwishowe kuhukumiwa nakwenda kutupwa kwenye ziwa la moto.. Nikakumbuka tena hakuna kutubu katika hii hali tuliyopo sasa..Wakati tunatafakari hayo wote wawili tulijua unyakuo umepita na tumeachwa….Tukawaza tutajibu nini mbele ya kiti cha hukumu.

Usiku ulizidi kuingia nikitamani hata mvua inyeshe ili tujifariji kwamba angalau ulikuwa ni mwanga wa radi ya mvua lakini wapi hakuna chochote…Nikatazama tena ujirudie juu ili pengine tuseme ni kawaida mianga mianga kupiga wakati wa mvua lakini wapi…..hakuna kilichotokea!…palikuwa pakame na juu kulikuwa kweupe vile vile, nyota zimetanda kote na hakuna hata dalili ya wingu …Zile hisia kali za kutazamia mambo yatakayoikumba dunia zilikuwa tayari zimeshafunika hisia za wakati tuliopo…nilitamani siku hiyo iwe ndoto..nizinduke usingizini nitubu kwa kumaanisha kubadilika kabisa..lakini wapi! Ilikuwa ni hali halisi kabisa..

Ndipo asubuhi Bwana akaanza kutufundisha…kwamba haukuwa unyakuo, bali Bwana alikuwa anataka kutufundisha hali itakayotukuta endapo tukiukosa unyakuo..(Na pia kuhusu jambo lingine ambalo halihusiani na hii mada ya leo alituambia kuhusu tukio hilo). Lakini kikubwa ni kuhusu siku ile itakavyokuwa. Na hisia zitakazowapata watu siki hiyo.

Hisia hizo ndizo zitakazowakuta wengi watakaoukosa unyakuo..na siku hiyo watakaoumia sana ni wale ambao tayari kwa namna moja au nyingine walishawahi kuisikia injili huko nyuma lakini hawakutubu au walipuuzia…ambao jana tu walitoka kuhubiriwa lakini wakaikataa injili au wakaipuuzia, ambao juzi tu wametoka kusikia au kusoma habari za kuja kwa Yesu mara ya pili lakini walipuuzia…Hao ndio watakaoomboleza sana na kulia..wengine wote wataona kawaida.

Hiyo kwetu ilikuwa ni ishara kubwa sana ambayo Mungu alizungumza na sisi..Kwa kweli ilitubadilisha Maisha yetu tangu huo wakati…Mpaka leo hii siwezi kuisahau hiyo hisia…nasema nikose chochote lakini sio UNYAKUO..Na namshukuru Mungu kwa kuzungumza na mimi kwa ishara ya nje kabisa kwani angesema nami kwa ndoto tu kama siku zote pengine nisingechukulia kwa uzito kwa kiwango hicho na mpaka leo ningebaki kuchukulia kuachwa ni jambo la kawaida.

Ndugu Kuna uchungu wa ajabu na hisia mbaya sana kwa watu watakaoukosa unyakuo…Hebu jiweke kwenye mazingira leo hii ndio unyakuo umepita na umeachwa?..utajisikiaje! labda unaweza usielewe sasa mpaka siku hali hiyo itakapokukuta…Lakini usitamani uwepo..Siku hiyo utasikia unyakuo umepita masaa machache tu umepishana na mahubiri ya kukuonya utubu.

Je! Umejiweka tayari?..Biblia inasema katika Waebrani 10:37 “Kwa kuwa bado kitambo kidogo sana, Yeye ajaye atakuja, wala hatakawia”.

Leo hii unasema unyakuo bado sana..siku hiyo ikifika utatamani urudishwe dakika 5 nyuma urekebishe mambo yako lakini utakuwa umeshachelewa.

Kama hujaokoka leo mlango wa Neema upo wazi..Hivyo pale ulipo jinyenyekeze kwa Mungu..Mwombe akusamehe dhambi zako zote ulizokuwa unazifanya za makusudi na ambazo sio za makusudi..Kisha baada ya kutubu fanya kama ulivyotubu..acha kufanya dhambi ulizokuwa unazifanya…kama ulikuwa mwasherati..acha uasherati, ulikuwa mwizi vivyo hivyo unaacha, ulikuwa unavaa nusu uchi..unaacha..ulikuwa mtazamaji wa picha chafu mitandaoni unazifuta na kuanza maisha mapya..

Ukishafanya hivyo Kristo atakupa amani ya ajabu moyoni mwako.Amani hiyo utakayoipata ndio itakuwa uthibitisho wa msamaha wako..Baada ya kufanya hivyo nenda kabatizwe kama hujabatizwa, ubatizo sahihi ni ule wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo. Na Roho Mtakatifu ndani yako atakuongoza katika mambo mengine yaliyosalia ikiwemo kukupa uwezo wa kushinda dhambi na ufahamu wa kuyaelewa maandiko. Ukiishi katika hali hiyo biblia imetupa uhakika wa kunyakuliwa Kristo atakaporudi..Hakuna namna yoyote ambayo unaweza usinyakuliwe.

Bwana azidi kutupa Neema yake tushinde ulimwengu huu kama yeye alivyoshinda. Ili siku ile tuifarahie karamu aliyotuandalia mbinguni milele.

Maran atha!

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

UNYAKUO.

Ule mfano wa wanawali 10 (Mathayo 25), wale watano hawakuwa na mafuta ya ziada katika chupa zao je yale mafuta ya ziada yanawakilisha nini?

SIKU YA TAABU YA YAKOBO.

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

DHAMBI ILIYOMKOSESHA SHETANI:

Rudi Nyumbani:

Print this post

Tofuati kati ya Myahudi, Mwisraeli na Muebrania ni ipi?

Tofuati kati ya Myahudi, Mwisraeli na Muebrania ni ipi?


Haya ni maneno matatu tofauti lakini kiuhalisia yanangumzia kitu kimoja..Ni sawa na useme, mtanzania, mtanganyika, na mswahili..Ni yule yule isipokuwa inategemea unamzungumzia katika nyanja ipi.

Ndivyo ilivyo kwa taifa la Israeli. Waebrania chimbuko lake ni Ibrahimu na kwa mara ya kwanza jina hilo linaonekana katika kitabu cha (Mwanzo 14:13) likimtambulisha Ibrahimu,ambapo kwa wakati huo akiitwa Abramu. Na baadaye tena tunaona Yusufu naye akitajwa kwa jina hilo (Mwanzo 39:14, 17)…Hivyo ni jina lililokuwa linawatambulisha wazao wote wa Ibrahimu, Japo biblia haitoi tafsiri yoyote halisi ya jina hilo, wengine wanasema jina hilo lina maana ya aliyevuka kutoka ng’ambo.

Lakini Israeli, ni jina jipya la Yakobo mwana wa Isaka, mjukuu wa Ibrahimu. aliitwa vile kutokana na kwamba alishindana na malaika wa Bwana usiku kucha katika mueleka na kumshinda, hivyo jina lake likabadilishwa na kuitwa Israeli, hivyo Watoto wake wote, waliozaliwa baada yake waliitwa wana wa Israeli, hadi walipoingia utumwani Misri walijulikana kwa majina yote mawili yaani wana wa waisraeli au waebrania. Lakini jina Israeli lilipata nguvu Zaidi hadi wakiwa wanarudi na kukaa katika nchi yao ya Ahadi..walifahamika kama waisraeli.

Lakini miaka mingi ilipopita na Taifa la Israeli kugawanyika katika pande kuu mbili, kaskazini na kusini. Wale waliokuwa upande wa kaskazini walibakia na jina hilo la Israeli, lakini waliokuwa katika upande wa kusini waliitwa Wayudea..Kutoka katika Neno Yuda, kwasababu  taifa la Yuda ndilo lililokuwa linatawala upande wa kusini.

Lakini sasa mataifa yote yalipochukuliwa utumwani, yaani wale wa kaskazini  kupelekwa Ashuru, na wale wa kusini kupelekwa Babeli, kama tunavyosoma waliorudi kwa asilimia kubwa katika nchi yao ni wale wa kusini waliopelekwa Babeli mara baada ya ile miaka 70 kuisha iliyotabiriwa na Danieli.. Hivyo walivyorudi jina lao waliendelea  nao , wakijulikana kama wayudea, na ndio huko huko jina WAYAHUDI wayahudi lilipozaliwa..Maana ya wahayudi  ni watu wa ardhi ya Uyahudi,au  Yudea au Yuda. Hivyo watu wote wa taifa zima wakaitwa Wayahudi ikijumlisha hata na wale wachache waliorudi kutoka Ashuru  walijulikana wote kama  Wayahudi.

Lakini hiyo haikubadilisha asili yao kuitwa Waisraeli au Waebrania.

Kutokana na kuwa watu wa Yuda ndio Mungu aliwachagua kusimamia ujenzi wa hekalu na mji mtakatifu wa Mungu.Vilevile ndilo Kabila lililokuwa linatazamiwa kumleta Masihi wa ulimwengu duniani, Hivyo  hiyo ililifanya kabila hilo liwe lenye misingi ya kiimani Zaidi ya mengine. Hivyo mwisraeli yoyote aliyejiita myahudi kwa wakati ule alikuwa ni sharti awe anazingatia dini na desturi zote za kiyahudi.

Hata leo hii, Taifa la Israeli ni kubwa lenye watu wengi waliozaliwa kule, ambao kiuraia wanajulikana kama waisraeli wengine waislamu, wengine wakristo, wengine hawana dini, lakini pamoja na wingi wao, na utaifa wao, si wote walio wayahudi. Wayahudi ni wale ambao wanashikilia misingi ya torati na tamaduni zao za kidini.. wanashika sikukuu zote zilizoamuriwa kwenye torati, vilevile wanafanya ibada kama vile za agano la kale.

Hivyo kwa ufupi, Myahudi yeyote anaweza kuitwa mwisraeli, au mwebrania lakini Mwisraeli yeyote hawezi kuitwa myahudi. Kama vile mtu yeyote aliyezaliwa Tanzania hata kama ni mzungu anaweza kuitwa mtanzania..Lakini sio kila mtu aliyezaliwa Tanzania anaweza akawa mswahili.. Mswahili ni jambo linaloendana na chimbuko la watanzania na lugha zao na desturi zao za asili.

Hiyo ndio Tofuati kati ya Myahudi, Mwisraeli na Muebrania

Ubarikiwe. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

Je! wayahudi wote wataokolewa hata kama ni watenda dhambi, Kwasababu wote ni uzao wa Ibrahimu?

MZEITUNI HALISI UTAKAPOPACHIKWA.

NG’OMBE MWEKUNDU ALIYEZALIWA ISRAELI, ANAFUNUA NINI?

CHUKIZO LA UHARIBIFU

UNYAKUO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

JE KUCHOMA MAITI NI DHAMBI?

Je kuchoma maiti ni dhambi? mpaka iteketee kabisa na kuwa jivu?..Kwamfano maiti ya mtu aliyeokoka kuichoma kama wanavyofanya wahindu ni dhambi?..je hizo ni ibada za wafu?..mtu akifa roho yake inakwenda wapi?

JIBU: Kila kitu kinachofanywa na wanadamu kina sababu…hakuna kitu kinachofanyika bila sababu..katika Maziko, watu wanaoosha maiti kuna sababu kwanini wanafanya vile..kadhalika watu wanaoosha maiti na yale maji kupikia pia ipo sababu ya wao kufanya hivyo..Wanaokata kipande cha nyama ya maiti na kula kabla ya kumzika ipo sababu ya wao kufanya hivyo..

Kwahiyo hata wanaochoma maiti ipo sababu ya wao kufanya hivyo.. hawachomi basi tu kufanya mazingira yawe masafi..hapana! bali wanasababu kubwa kufanya hivyo..Na sababu hiyo ni ya kiroho…

Wahindu wanaamini kwamba mtu akifa roho yake inakuwa inaelea hapa hewani…lakini roho ya mtu yule bado inakuwa ina uwezo wa kuona na kuhisi mazingira iliyokuwepo..Na hiyo ni kutokana na ule mwili ulioacha hapo chini. Mwili ule unaizuia ile roho kuendelea na safari yake ya kwenda mbinguni..Kwahiyo ili kuifanya ile roho isibakie hapo juu muda mrefu..wahindu wanauchoma ule mwili kwa moto wote uteketee..ili roho isibaki kuutazama mwili na kuendelea kuishi katikati ya mazingira iliyokuwa inaishi.

Na baada ya mwili ule kuchomwa basi ile roho itakwenda mbinguni kwa haraka.

Je Mtazamo huo ni sahihi?

Jibu ni la!..Mtu akishakufa kama ni mwenye haki roho yake inakwenda moja kwa moja mahali panapojulikana kama paradiso au peponi…na anakuwa hana mawasiliano tena na mwili wake. Kadhalika aliyekufa katika dhambi anakwenda mahali pajulikanapo kama kuzimu/jehanamu. Naye pia anakuwa hana mawasiliano na mwili wake uliokufa.

Kwahiyo ni uongo wa shetani kusema kwamba mwili unazuia roho kwenda mbinguni..hivyo unapaswa uchomwe moto!..Hizo ni IBADA ZA WAFU. Kama zinavyofanywa na kanisa katoliki za kuwaombea wafu!.

Hivyo shetani amewadanganya watu wafanye hivyo (wachome maiti)..Kwasababu anajua kitendo hicho ni kama sadaka…Kumbuka sadaka zote katika agano la kale zilikuwa zinafanyika kwa kuchomwa…Sadaka ya kuteketezwa ilikuwa inafanyika kwa kumchukua aidha mwanakondoo au mbuzi na kumchinja na hatimaye kumkatakata na kuuweka mwili wake juu ya madhabahu na kuuchoma kwa moto mpaka uteketee kabisa..Na kitendo hicho kilikuwa kinaleta matokeo makubwa sana katika ulimwengu wa roho. Na madhabahu ilikuwa inatengenezwa kwa mawe kadhaa na juu ya mawe hayo zinapangwa kuna na kondoo anawekwa juu  yake…kama tu wahindu wanavyoteketeza maiti zao.

Katika agano la kale Ili dhambi ifunikwe ni lazima sadaka ya kuteketezwa ifanyanyike..Na mambo mengine yote ili yafanikiwe ni lazima sadaka ya kuteketezwa itumike.

Sasa baada ya Agano jipya kuja..sadaka hizo Mungu alizifuta!…Yesu Kristo kwa kupigwa kwake na kufa kwake pale msalabani yeye ndiye akafanyika kuwa sadaka kwa ajili yetu.(Soma Waebrania 10:1-10)..Hatuhitaji tena maiti ya kondoo kuteketezwa kwa moto juu ya madhababu ndipo tupate msamaha wa dhambi…Damu ya Yesu Kristo inatosha.

Lakini shetani kazi yake ni kucopy vitu na kuvigeuza na kuvitumia kwa faida zake..Naye pia akaiga mfano huo wa sadaka za kwanza za kuteketezwa kufanya shughuli zake…leo mtu akienda kwa waganga ataambiwa apeleke mbuzi, au kuku achinjwe na damu ipatikane..sehemu nyingine ataambiwa amchinje na kumchoma moto…majivu akatupe baharini n.k

Sasa shetani kwa kuimarisha uchawi wake akaona maiti za mbuzi na kuku hazitoshi…sasa akahamia kwa maiti za watu…Na hizo atazipataje kirahisi?..kwa kuanzisha mafundisho hayo potofu ya roho kuelea hewani… ili watu wachome maiti na kafara iwe imeshafanyika… Na matokeo ya kafara hizo ni kuingiza mapepo ndani ya watu hususani wafiwa na washiriki wa kafara hiyo.

Baada ya kumaliza kafara hiyo mtu yule aliyeshiriki..hali yake ya kiroho inakuwa mbaya zaidi kuliko alivyokuwa hapo kwanza.

Sasa sisi wakristo hatupaswi kabisa kufanya hayo mambo…kwasababu yanahusiana na ibada za wafu..Na biblia imetuonya tusifanye hivyo au mambo yanayokaribiana kufanana na hayo..

Ezekieli 20:31 “Tena mtoapo matoleo yenu, na kuwapitisha watoto wenu motoni, je! Mnajitia unajisi kwa vinyago vyenu vyote hata leo? Na mimi je! Niulizwe neno nanyi, Enyi nyumba ya Israeli? Kama mimi niishivyo, asema Bwana MUNGU, sitaulizwa neno na ninyi”.

Soma tena..

2 Wafalme 17:16 “Wakaziacha amri zote za Bwana, Mungu wao, wakajifanyizia sanamu za kusubu, yaani, ndama mbili, wakafanya na Ashera, wakaliabudu jeshi lote la mbinguni, wakamtumikia Baali.

17 Wakawapitisha watoto wao, waume na wake, motoni, wakapiga ramli, wakafanya uchawi, wakajiuza nafsi zao wapate kufanya yaliyo maovu machoni pa Bwana, hata kumkasirisha.

18 Kwa hiyo Bwana akawaghadhibikia Israeli sana, akawahamisha mbali na uso wake; wala hapana aliyesalia ila kabila ya Yuda peke yake”

Hivyo si sahihi kuchoma maiti..(kuchoma maiti ni dhambi!).. Maiti ikiungua yenyewe labda kwa ajali ya moto mpaka kufikia jivu..hapo hakuna ibada yoyote iliyohusika..majivu yake yatakwenda kuzikwa na hakuna ibada yoyote ya kiroho hapo… lakini kama ikihusisha masuala ya imani au ibada tayari ni dhambi kubwa mbele za Mungu.

Bwana akubariki.

Je umeokoka?..Au bado unaupenda ulimwengu?..kumbuka shetani yupo kasambaza kila kona upotofu wake..Na tunaishi katika siku za mwisho za kurudi Yesu Kristo. Unyakuo upo karibu sana kutokea na watakatifu watakwenda na Bwana. Je utakuwa miongoni mwao?..Hivyo tubu leo kama hujatubu na Bwana atakupokea, na kukupa Roho wake Mtakatifu.

Maran atha! jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

NINI KINATOKEA BAADA YA KIFO?

https://wingulamashahidi.org/2018/06/27/maswali-na-majibu/

Bwana alimaanisha nini kusema “waache wafu wazike wafu wao.(Mathayo 8:21)?

HERI WAFU WAFAO KATIKA BWANA

KUZIMU ni mahali pa namna gani, Je! huko wanaishi watu wakifa na kwenda kupata mateso au ni vinginevyo?

Roho za Wanyama zinakwenda wapi baada ya kifo? Je! Watafufuliwa?

Wokovu wa milele/ Ulinzi wa daima (eternal security) Je! ni neno la kimaandiko?

MKUU WA ANGA.

NGUVU ILIYOPO KATIKA MAAMUZI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

HAJANENA KAMWE MTU YE YOTE KAMA HUYU ANAVYONENA.

Yohana 7:45 ‘’Basi wale watumishi wakawaendea wakuu wa makuhani na Mafarisayo. Nao wakawaambia, Mbona hamkumleta?

46 Wale watumishi wakajibu. Hajanena kamwe mtu ye yote kama huyu anavyonena.

47 Basi Mafarisayo wakawajibu, Je! Ninyi nanyi mmedanganyika?

48 Ni nani katika wakuu amwaminiye, au katika Mafarisayo?

Amen. Leo hii tujiulize ni kwanini mtu aliye maarufu kuliko wote duniani kwa wakati wote na vizazi vyote ni YESU KRISTO?.

Ukiona hivyo ujue si bure kuna kitu alichokuwa nacho ambacho hakuna mtu mwingine duniani anacho,. Leo hii kitabu kinachosomwa kuliko vitabu vyote duniani ni biblia, kinachofuata chini yake hakikaribii hata chembe, na katika hiyo hiyo biblia ni miongoni mwa vitabu vinavyosomwa zaidi ni vitabu vya injili vinavyozungumzia maisha ya YESU, na maneno ya Yesu Kristo kwa ujumla. Ukiona hivyo ujue si bure bure tu, lipo jambo watu wameona ndani yake.

Wale watu waliotaka kwenda kumkamata Yesu na kumfunga, wakidhani yule alikuwa ni mtu wa kawaida tu labda pengine ni mwana mapinduzi ametokea anataka kuipundua nchi, au mwanasiasa Fulani kama wengine, au mwanaharakati huru, au jasusi, lakini walipokutana na maneno yaliyotoka kwenye kinywa chake..Matarajio yao yaligeuzwa, Nia zao zilibadilishwa, fahamu zao zikafunguliwa..Na wakakiri kwa vinywa vyao.

Hajanena kamwe mtu ye yote kama huyu anavyonena…, Kauli hiyo inathitisha kuwa walizunguka sehemu nyingi kushughulika na watu wa namna yake, wamekutana na wengi, wamewasikia wengi, na kufanikiwa kuwakamata, lakini walipofika kwa huyu, na kusikia maneno yale.. walikiri kwa vinywa vyao, hawajawahi kuona mtu aliyenena kama yeye..Maneno yaliyojaa neema, na uweza, na nguvu, na matumaini, na faraja, na elimu, na maarifa, na uzima, na roho.

Sasa ni miaka 2000 imepita, lakini kila kizazi, kinashuhudia hajatokea mtu yeyote mfano wa Yesu Kristo mwenye maneno ya kipekee kama yeye. Walikuwepo wengi wameondoka…Lakini kwa Kristo maneno yake yaliposikiwa yalipenya mpaka kwenye vilindi vya mioyo ya watu.

Embu fikiria mtu anayekuambia maneno haya;

Mathayo 11:28 “ Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.

29 Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu;

30 kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi..”

Anakuambia tena.

Yohana 4:13 ‘’Yesu akajibu, akamwambia, Kila anywaye maji haya ataona kiu tena;

14 walakini ye yote atakayekunywa maji yale nitakayompa mimi hataona kiu milele; bali yale maji nitakayompa yatakuwa ndani yake chemchemi ya maji, yakibubujikia uzima wa milele.

Maneno hayo ni matamu sana…”

Sikia na haya..

Yohana 11:25 “Yesu akamwambia, Mimi ndimi huo ufufuo, na uzima. Yeye aniaminiye mimi, ajapokufa, atakuwa anaishi;

26 naye kila aishiye na kuniamini hatakufa kabisa hata milele. Je! Unayasadiki hayo?”

N.k N.k. Yapo mengi..Hakuna kiongozi yeyote wa dini alishawahi kuahidi maneno kama haya na akayatelekeza, hata sasa hakuna..Na ndivyo inavyojulikana kwa watu wote, na dini zote, hakuna kama YESU KRISTO, Na kamwe hatakuwepo mtu anayenena maneno yaliyojaa neema kama yeye.

Maneno yake yamewabadilisha maelfu kwa maelfu, mamilioni kwa mamilioni, yamehakikishwa, yamethibitishwa ni kweli..Hakuwa mwanasiasa yule, kuahidi mambo ambayo hawezi kuyatimiza, Hata wewe leo hii ukiamua kumwamini na kumfuata kweli kweli, zile chemchemi za maji ya uzima alizozisema miaka 2000 iliyopita zitaanza kutiririka ndani yako leo..

Kama umelemewa na mizigo ya dhambi, na masumbufu ya maisha haya mpaka umekata tamaa ya kuishi, ukimfuata, atakupumzisha kweli kweli, kama alivyoahidi,..Utapata tumaini jipya, na mwanzo mpya wa maisha, hakuna aliyekwenda kwake akajuta..utafutaji wa mali hautakupa faraja!..Umezitafuta miaka yote je zimekufariji?..zaidi sana zinakutia presha kuliko kukufariji..

Na ndio maana maandiko yanasema..

Zaburi 34:8 “Onjeni mwone ya kuwa Bwana yu mwema; Heri mtu yule anayemtumaini”.

Onja na wewe, Yesu anayehubiriwa ulimwenguni kote, anaokoa kweli maisha ya watu, usimwache akupite.

Ikiwa bado unatanga tanga na ulimwengu..unasubiri nini? .Ikiwa bado unatazamia mtu mwingine atakayekutamkia maneno mazuri na ya faraja Zaidi ya Kristo, nataka nikuambie hautampata na hatakuwepo,. Tubu dhambi zako leo anza mwanzo mpya na Kristo. Hapo ulipo Bwana anaweza kukuokoa ikiwa utamaaanisha kweli kutubu. Unachopaswa kufanya ni kupiga magoti na kumweleza Kristo kuwa unahitaji msamaha wake na msaada wake. Na kwamba umemaanisha kuwa kuanzia leo na kuendelea utakuwa mwanafunzi wake, na utamfuata kwa gharama zote..Sasa Ukishatubu kuwa kumaanisha kabisa, ujue kuwa Kristo ameshakusamehe, kwasababu yupo hapo pembeni mwako kukusikia..

Unachopaswa kufanya, hatua inayofuata ni kuonyesha toba yako kwa vitendo, na tendo la kwanza ni kuacha yale mambo maovu uliyokuwa unayafanya nyuma, kukaa mbali nayo,..yote pamoja na vichochezi vyake.. pili unatafuta ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO, kama hujabatizwa hivyo… na tatu ni kutafuta ushirika wakristo wa kweli walio karibu nawe na kujumuika nao..ili uweze kujifunza Neno la Mungu, kumega mkate na kusali kwa pamoja.

Na Kwa kufanya hivyo utakuwa umemdhihirishia Mungu toba yako kuwa ni kweli kwa Matendo yake..Na yeye akishaona hivyo atakuhakikishia ulinzi wa daima ikiwa hutatia nia ya kugeuka nyuma..atahakikisha anakupa uwezo wa kufanyika mwana wa Mungu. Hiyo ikiwa na maana kuwa atakuvika uwezo wa kufanana na Yesu Kristo, kwa neema zake. Na kuanzia hapo utaweza kuishinda dhambi kirahisi kwasababu Roho wa Mungu atakuwa ameshaachiliwa juu yako.

Bwana akubariki.jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

MTETEZI WAKO NI NANI?

BASI MUNGU AKAMUADHIMISHA SANA..

UFUNUO: Mlango wa 1

SAUTI NI SAUTI YA YAKOBO, LAKINI MIKONO NI YA ESAU.

Sanduku la Agano lilikuwa linawakilisha nini katika Agano jipya?

Rudi Nyumbani:

Print this post

MKUU WA ANGA.

Mkuu wa anga ni nani?


Shalom karibu tuongeze maarifa ya kumjua Mungu wetu..na sio tu kumjua Mungu wetu bali hata kumjua adui yetu…Hata wanyama wa porini wasio na akili huwa wanajifunza kuwatambua marafiki zao na kadhalika maadui zao…Nyumbu atakakula nyasi pamoja na pundamilia na swala, lakini akimwona tu simba kwa mbali basi atakimbia kuyanusuru maisha yake..kwanini? ni kwasababu huko nyuma tayari alishajifunza kumjua adui yake ni nani…na rafiki yake ni nani. Na sisi wakristo tunapaswa tuwe hivyo hivyo…

Leo tutajifunza kwa ufupi juu ya wakuu wa anga…Sasa wapo wakuu wa giza na kadhalika wakuu wa anga..hizo ni roho mbili tofauti. Wakuu wa giza wapo saba…na wakuu wa anga wapo wengi.

Mkuu wa giza aliyepo sasahivi ni wa saba na wa mwisho. Huyu ndiye Pepo mwenye nguvu kuliko wale sita waliotangulia..na kazi zake rasmi zilianza kudhihirishwa mwanzoni mwa karne ya 20 na mpaka leo bado anaendelea kutenda kazi. Kazi yake kubwa huyu ni kuchochea giza Nene duniani..kwa kuwafanya watu wawe vuguvugu, ndiyo jukumu kubwa alilokabidhiwa na shetani.

Shetani anajua tunaishi katika siku za mwisho na muda wake umekaribia kuisha sana..hivyo anachokifanya ni kuwafanya watu wawe vuguvugu sana, na tageti yake sio mtu asiyeamini hapana, tageti yake ni mtu anayeiona kuwa ni mkristo…Anamfanya mtu awe nusu mshirikina nusu mwungwana..Nusu mwombaji nusu mzinzi, nusu mwimbaji wa nyimbo za kumsifu Mungu nusu mshabiki wa mambo na nyimbo za kidunia…Nusu mchungaji nusu mzinzi n.k Hataki kuwafanya watu wawe wazinzi moja kwa moja kwasababu anajua wakiwa baridi kabisa ni rahisi kushtuka usingizini na kutubu…anataka wawe vuguvugu ili iwe rahisi wao kujihesabia haki, na mwisho wa siku watakapokufa wajikute jehanamu badala ya mbinguni…

Ndio maana leo hii..utamwona mtu kavaa kikahaba, na ukijaribu kumwuliza umeokoka atakuambia ndio mimi nimeokoka na jana tu nilikuwa kanisani…huyo huyo ukiiangalia simu yake anaboyfriend ambaye anatembea naye..na ukijaribu kumwambia usipotubu utakwenda hukumuni atakwambia unamhukumu…na atakufunulia maandiko baadhi tu ilimradi ajionyeshe yeye yupo sawa…Sasa hilo ndio lengo kuu la shetani.

Lakini ukimfuata kahaba ambaye hana mpango kabisa na Mungu wala hajui habari za Mungu..ukimwambia tu kidogo habari za dhambi anazozifanya na kwamba asipogeuka atapotea..jambo la kwanza atakiri kuwa yeye ni mwenye dhambi, na hiyo inamfanya iwe rahisi kwake kutubu hata kwa kulia …Sasa shetani ndio kitu ambacho hakitaki hicho…anajua watu baridi kabisa ni rahisi kuigeukia injili…hivyo anafanya juu chini watu wawe vuguvugu. Ili iwe ngumu kumgeukia Mungu wao…

Na faida nyingine shetani anayoipata pindi watu wanapokuwa vuguvugu ni kutapikwa na Mungu…Anajua Mungu hapendezwi na watu vuguvugu..anasema ni heri mtu angekuwa baridi kabisa..yaani angekuwa mwasherati moja kwamoja au kahaba au muabudu sanamu moja kwa moja kuliko kuwa vuguvugu..amesema atamtapika.

Ufunuo 3:15 “Nayajua matendo yako, ya kuwa hu baridi wala hu moto; ingekuwa heri kama ungekuwa baridi au moto.

16 Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa changu.

17 Kwa kuwa wasema, Mimi ni tajiri, nimejitajirisha, wala sina haja ya kitu; nawe hujui ya kuwa wewe u mnyonge, na mwenye mashaka, na maskini, na kipofu, na uchi”.

Hiyo ndiyo kazi ya mkuu wa giza hili..Sasa chini yake wapo wapo wakuu wa anga…hawa kazi yao ni kukusanya taarifa za watu na kushinikiza kueneza uvuguvugu duniani kote..Ni kama Raisi alivyo na wakuu wake wa mikoa…ambao kazi yao ni kuifanya kazi ile ile ya Raisi katika mikoa waliyopo..ni kama wawakilishi wa Raisi huko katika majimbo yao.

Wakuu wa anga wanatumia anga kuleta madhara yao..Kama vile sisi wanadamu tutumiavyo anga kuharakisha maendeleo yetu..kwamba tunatumia anga kusafiri haraka kwa chombo kama ndege..tunatumia anga kurusha wawimbi yetu ya redio na tv pamoja na internet..kiasi kwamba mtu yupo Ulaya unaweza kumwangalia mtu mwingine hapa Tanzania mubashara dakika hiyo hiyo…Kadhalika tunatumia anga kuhifadhi vyombo vyetu kama satellite..ambayo hiyo inatusaidia kutabiri hali ya hewa, mabadiliko ya tabia ya nchi..kufuatilia maeneo tuliyopo..kwa kutumia tu simu yenye program ya satelaiti tunaweza kujiona mahali tulipo..mahali tunapokwenda hata tunaweza kuona mabati ya nyumba zetu…mbali na hayo hata vita vya siku hizi vikuu ni vya angani n.k

Sasa wakuu wa anga nao wanafanya mambo kama hayo kwa kutumia elimu zao za giza…wao hawatumii sayansi..lakini wanatumia elimu yao ambapo wanauwezo wa kujua kiwango cha uvuguvugu uliopo duniani..wanauwezo wa kumjua mtu mmoja mmoja..wana uwezo wa kujua wanadamu wanaomcha Mungu na wasiomcha Mungu..

Sasa mambo yote hayo wanaweza kuyajua kwa kutumia anga..ndio maana wanaitwa wakuu wa anga..Na lengo lao kubwa ni lile lile kuifanya dunia iwe vuguvugu..

Wanafanya vita na wakristo waliookoka na waliosimama kweli kweli…wanatafuta kila njia ya kumwangusha..ili awe vuguvugu!..watamtumia watu ili kumshawishi afanye uasherati…na maroho ambayo yatamwamshawishi na kumwambia mbona Daudi alifanya na akasamehewa?..Na wewe nenda kafanye uasherati utatubu tu!..Na mtu akishaingia huko kufanya dhambi za makusudi kama hizo baada ya kuujua ukweli Mungu anamtapika…Na siku zote hakuna mtu anayeweza kurudia matapishi yake..

Kadhalika mtu ni mlevi..shetani atamwambia usiwe mlevi siku zote hivyo..angalau toa toa sadaka…Na Yule mtu kwa kusikiliza ushawishi huo badala ya kutubu kabisa na kuacha ulevi ndipo akamtolee Mungu wake….yeye atakwenda kujifunza kumtolea Mungu sadaka na hali yake ya ulevi ile ile..akiamini kuwa moyoni Mungu anapendezwa na yeye…Na ukijaribu kumwambie atubu anasema yeye ni mkristo na ni mtoaji…ukiendelea zaidi anakwambia usimhukumu..Mtu wa namna hiyo tayari kashatimiza lengo la mkuu wa giza hili…(Soma Mhubiri 5:1) soma tena Mithali 15:8 “Sadaka ya mtu mbaya ni chukizo kwa Bwana; Bali maombi ya mtu mnyofu ni furaha yake”.

Mwambie mtu mizaha na matusi ni dhambi..usengenyaji ni dhambi, rushwa ni dhambi..atakwambia mimi naendaga kanisani na naijua biblia yote na natoa fungu la 10..Hicho ndicho kiburi shetani anachopambana kila siku kukiingiza ndani ya watu.

Bwana atusaidie sana shetani asitupate kwa njia hizo..Je! bado unamtii mkuu wa anga hili kwa kuendelea kuwa vuguvugu?..Au umesimama na kuwa moto?..bado unaendelea kuvaa vimini na huku unahudhuria kanisani?..bado unaendelea kupaka wanja, na kuvaa mawigi na unakwenda kanisani na unajiona upo sawa na Mungu…Yesu anakuambia..unajiona u utajiri lakini ni maskini, na mnyonge na mwenye mashaka…Lakini ametoa shauri kwamba utubu nawe utakuwa tajiri.

Waefeso 2:1 “Nanyi mlikuwa wafu kwa sababu ya makosa na dhambi zenu;

2 ambazo mliziendea zamani kwa kuifuata kawaida ya ulimwengu huu, na kwa kumfuata mfalme wa uwezo wa anga, roho yule atendaye kazi sasa katika wana wa kuasi;

3 ambao zamani, sisi sote nasi tulienenda kati yao, katika tamaa za miili yetu, tulipoyatimiza mapenzi ya mwili na ya nia, tukawa kwa tabia yetu watoto wa hasira kama na hao wengine”.

Na kumbuka Mkuu wa anga hili na mkuu wa giza hili hatuwashindi kwa kuingia kwenye maombi ya mfungo..wala kwa kurusha mishale ya moto angani…Tunamshinda tu kwa kuamua kubadilika na kumgeukia Kristo kikamilifu..kwa kuzikataa kazi za shetani zote…kama ulikuwa ni mwasherati unaamua kugeuka, ulikuwa mlevi unageuka na kuacha ulevi kwa imani…Na baada ya kugeuka, unatubu na kwenda kubatizwa..kisha Roho Mtakatifu ndani yako atakuongoza na kukutia katika kweli yote ya kimaandiko.

Na silaha nyingine ya kumshinda wakuu hao ni kulifahamu Neno, ambalo hiyo inatokana na kujifunza kusoma biblia mwenyewe na kujifunza sehemu nyingine tofauti tofauti..Ndani ya Biblia utajifunza kuhesabiwa haki kwa Imani..utajifunza kuukulia wokovu na kusimama thabiti..pamoja na kujua nguvu iliyopo katika jina la Yesu na damu ya Yesu.

Waefeso 6:12 “Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho.

13 Kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama.

14 Basi simameni, hali mmejifunga kweli viunoni, na kuvaa dirii ya haki kifuani,

15 na kufungiwa miguu utayari tupatao kwa Injili ya amani;

16 zaidi ya yote mkiitwaa ngao ya imani, ambayo kwa hiyo mtaweza kuizima mishale yote yenye moto ya yule mwovu.

17 Tena ipokeeni chapeo ya wokovu, na upanga wa Roho ambao ni neno la Mungu;”

Bwana akubariki sana. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

MKUU WA GIZA.

JE VIBWENGO NI KWELI VIPO?

NGUVU ILIYOPO KATIKA MAAMUZI.

ASKOFU MKUU NA MCHUNGAJI MKUU NI NANI?

MTINI, WENYE MAJANI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Je! Ni halali kuoa/kuolewa na mtu ambaye tayari anao watoto?

SWALI: Shalom Naomba kuuliza Je, ni halali kwa mimi kumuoa binti ambaye alishazaa na mtu mwingine bila kuishi nae Je, naweza kufunga naye ndoa ya kikristo na ikawa halali?


JIBU: Hapo yapo mambo mawili. Ikiwa binti huyo alikuwa ameshaolewa, halafu akaachika kwa sababu yoyote ile, labda pengine amekosana na mume wake, au amefumaniwa katika uzinifu na hivyo ameachwa, au sababu nyingine yoyote tofauti na kifo cha mumewe tu! Au kwasababu ya kufukuzwa kwa ukristo wake..Mtu huyu hapaswa kuolewa na mwanamume yeyote Yule.. Maana akifanya hivyo biblia inasema anazidi, na Yule pia aliyemuoa biblia inasema naye pia azini.

Marko 10:11 “Akawaambia, Kila mtu atakayemwacha mkewe na kuoa mwingine azini juu yake;

12 na mke, akimwacha mumewe na kuolewa na mtu mwingine, azini”.

Luka 16:18 Kila amwachaye mkewe na kumwoa mke mwingine azini; naye amwoaye yeye aliyeachwa na mumewe azini.

Hivyo ili uwe katika mkono salama, usiangukie hukumu, ikiwa umegundua mwanamke huyo yupo katika hali hiyo unapaswa umuache mara moja..hata kama ulishazaa naye watoto.

Lakini kama mwanamke huyo, alipata tu mimba akiwa katika dhambi, kwa uasherati,  Hivyo na baadaye akaja akatubu na kumgeukie Mungu wake. Na sasa anataka kwenda kuolewa  basi hapo ni uchaguzi wako mwenyewe wewe unayetaka kuoa, ukiridhia kuwa naye  katika hali hiyo akiwa na watoto, ni sawa hakuna shida yeyote ukimuoa, kwasababu hapo mwanzo alikuwa hajaolewa. Lakini kama hajaridhia hafanyi dhambi pia kutokumuoa, ukitafuata ambaye hana watoto.

Na hiyo inalenga pande zote mbili, hata na kwa mwanaume pia..Ikiwa ameacha ndoa yake akaenda kuoa tena, biblia inasema azini, na Yule aliyeolewa naye vilevile azini..Lakini kama alikuwa hajaoa, lakini kazaa katika uzinzi na sasa amemgeukia Mungu katubu na amekuwa mkristo, anaweza akaoa, na isiwe anafanya dhambi mbele za Mungu.

Hizi ndio sababu pekee zinazoweza kumfanya mtu iwe halali kwake kuoa/kuolewa na mtu ambaye tayari anao watoto.

Ubarikiwe.jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

NDOA NA HARUSI TAKATIFU.

Je! ni halali kutoa cheti kwa wakristo wanaooa?

NDOA NA TALAKA:

Yeshuruni ni nani katika biblia?

Nini Tofauti kati ya uzinzi na uasherati ?

Rudi Nyumbani:

Print this post

WAZAZI WA YOHANA NA YAKOBO.

Shalom, Ni siku nyingine Bwana ametupa kuiona kwa neema zake, hivyo nakukaribisha tuzidi kuyatafakari maneno ya uzima..

Leo tutajifunza juu ya wazazi wa mitume wawili wa Yesu, (Yohana na Yakobo)..Na tutaona pia ni jinsi gani wazazi wanavyoweza kuyaathiri maisha ya watoto wao ya rohoni kwa kiasi kikubwa. Kama tulivyotangulia kuona katika masomo yaliyopita, kwamba mzazi akimlea mtoto wake, na kumfundisha kumuheshimu, Basi Mungu anaamvika kilemba cha neema kichwani pake. Na neema hiyo si nyingine Zaidi ya ile ya kumjua Kristo kwa mapana yake na marefu yake(Mithali 1:8-9) na kuja kuwa msaada kwa wengine.

Na tutaona pia mwitikio wa wazazi jinsi unavyopaswa uwe kwa watoto wao pale wanapochukua uamuzi wa kumfuata Yesu. Tutajifunza kwa kuziangalia tabia za wazazi wa Yohana na Yakobo. Lakini awali ya yote,nataka utafakari jambo hili, Ulishawahi kujiuliza kwanini miongoni wa wale mitume 12 ni watatu tu ndio waliokuwa karibu sana na Yesu?.

Na miongoni mwa hao watatu, wawili walikuwa ndugu, na huyo mwingine ni Petro. Na mtume ambaye alipendwa na Yesu kuliko wote, ambaye kila wakati alikuwa akiegema kifuani mwa Yesu alikuwa ni mmojawapo wa hao wawili..Ni kwanini? Je! Mitume wengine walikuwa na mapungufu mengi? Jibu ni Hapana…Lakini kwanini Yesu aliwapenda hao wawili mpaka akawapa jina lao spesheli, akawaitwa Boanerge yaani wana wa ngurumo..(Soma Marko 3:17).

Yote hayo si kwa bidii zao tu peke yake lakini pia juhudi za wazazi zilichangia,..Embu tuwatazame kwa ufupi wazazi hawa tukianzana na Baba yao..tusome.

Mathayo 4:18 “Naye alipokuwa akitembea kando ya bahari ya Galilaya, aliona ndugu wawili, Simoni aitwaye Petro, na Andrea nduguye, wakitupa jarife baharini; kwa maana walikuwa wavuvi.

19 Akawaambia, Nifuateni, nami nitawafanya kuwa wavuvi wa watu.

20 Mara wakaziacha nyavu zao, wakamfuata.

21 Akaendelea mbele, akaona ndugu wengine wawili, Yakobo wa Zebedayo, na Yohana nduguye, ambao walikuwamo chomboni pamoja na Zebedayo baba yao, wakizitengeneza nyavu zao; akawaita.

22 Mara wakakiacha chombo na baba yao, wakamfuata”.

Mwanzoni kabisa mwa wito, Yesu alipowaona vijana hawa wawili kuwa wanamfaa kwa kazi yake ya utume..Moja kwa moja alikwenda na kuwaita wakiwa katikati ya baba yao..katikati ya biashara ya baba yao waliyokuwa wanaifanya..Lakini Utaona baba yao hakuleta ukinzani wowote katika jambo hilo,..Aliwaachilia Watoto wake waende kwa moyo wote, afadhali ingekuwa ni mmoja, bali aliwaacha wote wawili wamfuate Yesu..

Jambo ambalo, si rahisi kwa mzazi yeyote wa kawaida wa leo kufanya hivyo, kuwaachilia Watoto wake wamtumikie Kristo,..Lakini kwake ilikuwa tofuati hakuona shida aachiwe vyombo vyake vya kazi, aitende kazi ile peke yake,pamoja na watu wa mshahara na uzee wake ilimradi tu wanawe waupate wokovu..

Tukimwangalia mama tena..

Mathayo 20:20 “Ndipo mama yao wana wa Zebedayo akamwendea pamoja na wanawe, akamsujudia, na kumwomba neno.

21 Akamwambia, Wataka nini? Akamwambia, Agiza kwamba hawa wanangu wawili waketi mmoja mkono wako wa kuume, na mmoja mkono wako wa kushoto, katika ufalme wako.

22 Yesu akajibu akasema, Hamjui mnaloliomba. Je! Mwaweza kunywea kikombe nitakachonywea mimi? Wakamwambia, Twaweza.

23 Akawaambia, Hakika mtakinywea kikombe changu; lakini kuketi mkono wangu wa kuume na mkono wangu wa kushoto, sina amri kuwapa, bali watapewa waliowekewa tayari na Baba yangu.

Embu jaribu kutafari mama huyu alivyokuwa anawatakia mema Watoto wake, aliona kufuatana na Yesu tu haitoshi hapa duniani haitoshi, bali pia wawe karibu na Yesu hata katika huo ulimwengu unaokuja. Alikuwa anawatafutia tu fursa nzuri Watoto wake huko mbeleni.. Wewe unadhani Watoto hao..wataachaje kupendwa na YESU, na kuwa vinara kwa Kristo. Kwasababu hawamtumikii Kristo kwa presha, bali kwa sapoti yote kutoka hata kwa wazazi wao.

Unadhani, wazazi wa mitume wengine walikuwa hawajui kuwa Watoto wao wanatumika na Bwana?. Walikuwa wanajua sana, lakini hakuna hata mmoja mzazi wake anaorodheshwa katika huduma za Yesu isipokuwa wazazi wa hawa vijana wawili.

Pengine walikuwa hawaoni umuhimu wowote, wa wao kuongozana na Yesu..Wameacha shughuli zao, fedha zao, biashara zao, ya nini tena kuwasapoti..hawakuwa na muda..Lakini wazazi wa mitume hawa wawili walikuwa bega kwa bega na Watoto wao, hadi hatua ya mwisho kuhakikisha kuwa hawamkosi Yesu..Na mwishowe wakawa miongoni mwa wale watatu waliopendwa na Yesu.

Hata leo hii, ikiwa wewe ni mzazi, au unajiandaa kuwa mzazi..Utakapomwona mtoto wako anaonyesha uelekeo wa kumpenda Mungu, unapaswa uwe wa kwanza kumsapoti. Kama unaweza kuwa wa kwanza kumsapoti kumnunulia kitabu cha shuleni, kwanini usimsapoti kumnunulia biblia, na vitabu vyenye mafundisho ya Neno la Mungu. Kwanini usimweke chini wa wachungaji wako wamfundishe Neno la Mungu?..Unajuaje kuwa kwa bidii yako hiyo utamkuza Samweli, au Yakobo, au Yohana?.

Bwana atusaidie tunapojifunza mifano ya wazazi hawa ili na sisi tuwe na mioyo kama hiyo hiyo kwa Watoto wetu.

Ubarikiwe sana. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

VIGEZO VYA KUWA KARIBU NA YESU KRISTO KATIKA ULIMWENGU UJAO.

Roho, Nafsi, na Mwili vina utofauti gani?

KUTOKUIHUBIRI INJILI,KUNA MADHARA GANI?

Ni sahihi kumuita Mariamu mama wa Mungu?

Je! ni sahihi kwa Mkristo kusherekea siku yake ya kuzaliwa.[Birth day]?

Rudi Nyumbani:

Print this post

LAKINI HAITAKUWA HIVYO KWENU.

Lakini haitakuwa hivyo kwenu.


Shalom, Karibu tuzidi tujifunze Neno la Mungu.

Mathayo 20: 24 “Na wale kumi waliposikia, waliwakasirikia wale ndugu wawili.

25 Lakini Yesu akawaita, akasema, Mwajua ya kuwa wakuu wa Mataifa huwatawala kwa nguvu, na wakubwa wao huwatumikisha.

26 Lakini haitakuwa hivyo kwenu; bali mtu ye yote anayetaka kuwa mkubwa kwenu, na awe mtumishi wenu;

27 na mtu ye yote anayetaka kuwa wa kwanza kwenu na awe mtumwa wenu;

28 kama vile Mwana wa Adamu asivyokuja kutumikiwa, bali kutumika, na kutoa nafsi yake iwe fidia ya wengi”.

Jinsi dunia inavyoenenda ni tofauti kabisa na wakristo wanavyopaswa kuenenda…Kama Bwana Yesu alivyosema hapo juu, watu wa mataifa huwatawala kwa nguvu na mkubwa wao huwatumikisha…lakini haitakuwa hivyo kwenu..Ikifunua kuwa hekima ya dunia hii ni kinyume na hekima ya Mungu…Hekima ya dunia hii, mdogo anamtumikia Mkubwa…lakini Hekima ya kimbinguni mkubwa ndiye anayemtumikia mdogo….

Hekima ya kidunia inasema ukimbilie ukubwa ili usiwe mtumwa…lakini hekima ya kimbinguni inasema ukimbilie udogo ili uwe mkubwa…

Hekima tena ya kidunia inasema…Mpende akupendaye na umchukie anayekuchukia…lakini hekima ya kimbinguni inasema “mpende adui yako mwombee yeye anayekuudhi”..adui yako akiwa na njaa mlishe, akiwa na kiu mnyweshe…(Soma Mathayo 5:44 na Warumi 12:20).

Hekima ya dunia hii inasema ukiipatia nafsi yako kila kitu chema cha ulimwengu huu ndio maana ya maisha…lakini hekima ya Mungu inasema “aipataye nafsi yake ataipoteza na aipotezaye kwa ajili ya Kristo ataipata”…Kwahiyo karibia mambo yote ya ulimwengu yanakwenda kinyume na hekima ya Mungu…Ndio maana inakuwa ni ngumu mtu wa kidunia kumwambia kwamba kuna siku hii dunia tunayoishi itafikia mwisho na kwamba mwisho huo umekaribia sana na siku moja hili jua tunaloliona litatiwa giza…atakuona ni mtu wa ajabu kwasababu yeye anaona dunia mbona bado ni mahali salama?..itawezekanikaje jambo hilo..kwamba eti siku moja jua litiwe giza?..Atakuona kuna kau-pumbavu Fulani kapo kichwani mwako..

Ndio maana biblia ikasema…

katika 1 Wakorintho 1:18 “Kwa sababu neno la msalaba kwao wanaopotea ni upuzi, bali kwetu sisi tunaookolewa ni nguvu ya Mungu.

19 Kwa kuwa imeandikwa, Nitaiharibu hekima yao wenye hekima, Na akili zao wenye akili nitazikataa.

20 Yu wapi mwenye hekima? Yu wapi mwandishi? Yu wapi mlete hoja wa zamani hizi? Je! Mungu hakuifanya hekima ya dunia kuwa ni upumbavu?

21 Kwa maana katika hekima ya Mungu, dunia isipopata kumjua Mungu kwa hekima yake, Mungu alipenda kuwaokoa waaminio kwa upuzi wa lile neno linalohubiriwa.”

Unaona?..Hebu leo hii itafute hii hekima ya Mungu..ambayo imekataliwa na watu wengi…kama wewe ni mkristo na ulikuwa hujui kwamba unapaswa uwapende wanaokuchukia anza kufanya hivyo leo…Usiisikilize hekima ya dunia ambayo kwa nje inaonekana ni tamu, lakini mwisho wake ni upotevu…inayokuambia usimwache adui yako kuishi…na mbaya Zaidi hekima hiyo ya kidunia imeshaanza kuhubiriwa hata mpaka makanisani kana kwamba ni hekima ya ki-Mungu.

Kama ulikuwa hujui kwamba ili uwe mkubwa kuliko wote ni sharti uwe mdogo kuliko wote..anza kufanya hivyo leo…Kama wewe ni boss mahali ulipo tumika kana kwamba wewe sio boss tumika kuliko hata wale uliowaajiri…kuwa mpole kuliko yule mfanyakazi wa chini kabisa uliomwajiri…Ndivyo mbele za Mungu utakavyoonekana Mkubwa…Na ndivyo Mungu atakavyozidi kukupandisha juu. Mungu anasema Musa alikuwa ni mtu aliyekuwa mpole kuliko wote ulimwenguni, lakini kwa kupitia upole wake Mungu alimfanya kuwa kichwa cha wana wa Israeli.(Hesabu 12:3).

Bwana Yesu alikuwa ni mkubwa kuliko wote lakini aliwaosha miguu wanafunzi wake ambao wengine hata walimsaliti na kumkana..Na pamoja na kujua kuwa atasalitiwa na kukanwa lakini aliwaosha miguu hivyo hivyo na kuendelea kula nao na kunywa nao kwa upendo wote…Je wewe unaweza kufanya hivyo kwa watu waliopo chini yako?..ambao unajua kabisa wamekufanyia hiki au kile?..Kama huwezi basi tambua una hekima ya ulimwengu huu lakini hauna hekima ya ki-Mungu.

Na mambo mengine yote ni vivyo hivyo..Hekima hii inaingia ndani ya mtu kwa kujifunza Neno la Mungu…kuna tofauti kati ya kusoma na kujifunza…

Kujifunza Maana yake unajiingiza mwenyewe kwenye darasa ambalo utausoma mstari na kuutafakari kwa kina na kwa msaada wa Roho kupata ufunuo kutoka katika huo mstari..Na hauhusomi wakati kichwa chako kimevurugika na mambo mengine ya ulimwengu…hakikisha unapata utulivu wa kutosha…katika hali ya utulivu ndipo sauti ya Mungu inasikika..Roho Mtakatifu ataanza kukufundisha jambo moja baada ya lingine..na utaona mwenyewe kwa jinsi gani dunia ipo mbali na hekima ya Mungu…na hata wewe binafsi ulivyokuwa mbali na hekima ya Mungu.

Vilevile kama tutaipuuzia hii hekima ya Mungu na kujiona tunajua Zaidi ya Neno lake..Basi tufahamu kuwa Hekima hiyo mbele za Mungu ni upuuzi..

1Wakorintho 3:18 Mtu asijidanganye mwenyewe; kama mtu akijiona kuwa mwenye hekima miongoni mwenu katika dunia hii, na awe mpumbavu, ili apate kuwa mwenye hekima.

19 Maana hekima ya dunia hii ni upuzi mbele za Mungu. Kwa maana imeandikwa, Yeye ndiye awanasaye wenye hekima katika hila yao.

3.20 Na tena, Bwana anayafahamu mawazo ya wenye hekima ya kwamba ni ya ubatili.

Bwana akubariki. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

MAOMBI KWA WENYE MAMLAKA.

JE SALA YA ROZARI TAKATIFU NI YA KIMAANDIKO?

Kwanini yule mtu hakukutwa na vazi la arusi wakati alialikwa?

KUVUNJA MAAGANO YA UKOO.

Je ni wakina nani ambao hawataonja mauti mpaka siku ya kuja Bwana?

Rudi Nyumbani:

Print this post

HISTORIA YA ISRAELI.

Moja ya maswali yanayoulizwa na wengi ni kutaka kujua juu ya Historia ya Israeli/Taifa la Israeli/Wana wa Israeli..Lakini kiuhalisia historia ya Israeli ipo kwenye biblia. Ukisoma kitabu cha Mwanzo, Kutoka, Mambo ya Walawi, Kumbukumbu la Torati, hesabu, Yoshua, waamuzi pamoja na vitabu vya wafalme..vimeelezea vizuri sana kuhusu Taifa la Israeli/wana wa Israeli…

Hakuna mahali popote ambapo pameelezea vizuri historia ya Israeli kama kwenye Biblia takatifu..Hata kurasa kama Wikipedia na kamusi nyingine zote..zinatoa taarifa zao kuhusu Taifa la Israeli kwa kunukuu kutoka kwenye Biblia..Hivyo hakuna mahali pengine historia ya Taifa hilo inaweza kupatikana isipokuwa katika Biblia takatifu. Tatizo kubwa tulilonalo wengi wetu hatupendi kusoma Biblia, badala yake tunapenda kutafuta kusimuliwa au kufupishiwa habari fulani na watu ambao tayari wameshaisoma.

Hivyo hakuna tabia nzuri kama tabia ya kusoma Neno la Mungu..Matokeo ya kutolisoma Neno la Mungu (yaani Biblia) na kusubiriwa kutafsiriwa..Ni mwishowe kudondokea katika mikono ya mawakala wa shetani..ambao kazi yao ni kuipotosha kweli na kuingiza uongo katikati ya kweli. Na mtu akishadanganywa hawezi kujua kama kadanganywa au la..kwasababu hasomi biblia mwenywe.

Hivyo leo tuitazame kwa ufupi Historia ya Israeli.

Taifa la Israeli lilianza kwa ahadi…Yaani mtu mmoja aliyeitwa Ibrahimu alimpendeza Mungu, Hivyo Mungu akamwahidi kuwa atakuwa Taifa kubwa.

Mwanzo 12:1 “Bwana akamwambia Abramu, Toka wewe katika nchi yako, na jamaa zako, na nyumba ya baba yako, uende mpaka nchi nitakayokuonyesha;

2 nami nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa, na kukubariki, na kulikuza jina lako; nawe uwe baraka;

3 nami nitawabariki wakubarikio, naye akulaaniye nitamlaani; na katika wewe jamaa zote za dunia watabarikiwa”

Ahadi hiyo ilianza kutimia baada ya Ibrahimu kupata mtoto wa kwanza wa kiume..ambaye alimwita Isaka (Alikuwa na mwingine aliyemwita Ishmaeli lakini Ishmaeli hakuwa mwana wa Ahadi kwasababu alizaliwa na mwanamke mwingine)..Baadaye Isaka akamzaa Yakobo..Na Yakobo ambaye ni mjukuu wa Ibrahimu akazaa watoto 12. Hawa watoto 12 wa kiume waliozaliwa na Yakobo…waliitwa wana wa Yakobo…au watoto wa Yakobo…

Lakini ulipofika wakati fulani Yakobo jina lake lilibadilishwa na kuwa ISRAELI…Tafsiri ya jina Israeli ni “MSHINDI”. Hivyo kama jina lake limebadilika kadhalika na watoto wake hawakuitwa tena wana wa Yakobo bali wana wa ISRAELI. Na majina yao yalikuwa ni RUBENI, LAWI, ZABULONI, ISAKARI, NAFTALI, DANI, YUDA, SIMEONI, GADI, ASHERI, YUSUFU, na BENYAMINI.

Hawa wana 12, walioa wake na kuzaa watoto wengi..na watoto wao nao pia wakaoa na kuzaa watoto na wajukuu na vitukuu..Hatimaye Taifa likaanza kuwa kubwa na kufikia watu elfu 10, elfu 20, laki mpaka milioni..Kila kizazi kilichokuwa kinatokea kilirekodiwa asili ya Baba yake wa kwanza…kama ni Rubeni, au Lawi, au Gadi au mwingine yoyote alijulikana asili yake…Hivyo  majina ya Baba zao yakageuzwa na kuwa MAKABILA YAO. Hivyo kila mtu alikuwa na kabila lake miongoni mwa yale 12.

Sasa Kuna mambo waliyafanya wana wa Israeli yakawapeleka Misri, ambapo waliingia kwa amani lakini wakatoka kwa ushindani mkali. Baada ya kutolewa Misri na mkono wa Mungu mwenyewe…walianza safari ya kuelekea nchi ya Ahadi. Ijulikanayo kama KAANANI. Iliwachukua miaka 40 kukamilisha safari yao mpaka kufikia nchi ya Ahadi…Wakiwa njiani ndio huko huko Mungu akawa anazungumza nao na kuwapa AMRI za kuzishika na SHERIA ili wakafanikiwe wanapoiendea hiyo nchi ya Ahadi. Amri hizo zikiwemo kumtumikia na kumsujudia Mungu wao mmoja tu yeye peke yake aliyewatoa katika nchi Misri, nyumba ya utumwa…nyingine ni kuwaheshimu wazazi, kutokuiba, kutokuzini n.k

Walipoingia nchi ya Ahadi waligawanyiwa nchi hiyo kulingana na makabila yao.. kabila lenye watu wengi lilipewa sehemu kubwa ya ardhi, kadhalika lenye watu wachache lilipewa urithi mdogo.

Wana wa Israeli walipitia vipindi virefu vya kumsahau Mungu na kumrudia..Kizazi kilichofanya mabaya zaidi kiliadhibiwa na Mungu..na kile kilichofanya vizuri katika kuzishika amri na sheria za Mungu kilibarikiwa na kufanikiwa. Hivyo Mungu aliwafikisha katika nchi hiyo na kuwafanya kuwa wengi sana mamilioni..Na kutimiza Ahadi Mungu aliyemwahidia Ibrahimu.

Ilipofika wakati wa Ahadi ya Mungu kuuokoa ulimwengu..alimtuma mwanawe mpendwa ambaye alizaliwa katika Taifa hilo la Israeli…katika mnyororo wa kabila la YUDA. Yesu alizaliwa Maskini lakini alikuwa Mfalme..alikufa kifo cha aibu lakini alipofufuka alipata heshima…Yesu alifanyika kuwa wokovu kwa waisraeli wenyewe pamoja na watu wa mataifa.

Watu wa Mataifa ni watu wa mataifa mengine yote tofauti na taifa la Israeli. Waisraeli jina lingine wanaitwa WAYAHUDI..Wayahudi ndio hao hao waisraeli..hivyo uonapo mahali popote wanataja wayahudi basi fahamu kuwa ni hao hao waisraeli…sehemu nyingine wanatajwa kama Waebrania.

Taifa la Israeli lilijulikana kama Taifa teule la Mungu kwasababu ndio Taifa pekee duniani kote ambalo lilikuwa linamuabudu Mungu wa kweli YEHOVA. Aliyeumba mbingu na nchi…Mataifa mengine yaliyosalia yalikuwa yanaabudu sanamu, mizimu, miti na wanadamu. Ni Israeli pekee ndilo lililokuwa linamwabudu Mungu wa kweli..Ndio maana likaitwa Taifa Teule.

Mpaka leo Taifa hili bado lipo…na bado ni kipenzi cha Mungu…Ingawa wayahudi sasa hawamwamini Yesu kama Masihi.. lakini biblia imetabiri katika siku za mwisho watamwagiwa roho ya Neema na watamkubali Kristo.

Kijeografia, Taifa hili lipo katika Bara la ASIA, Eneo linalojulikana kama mashariki ya kati…Waisraeli kimwonekano wanakaribia kufanana na waarabu lakini si waarabu, wapo wayahudi pia wanaoishi mataifa mengine ya nje….Na nchi ya Israeli ni ndogo tu kama Mkoa wa Njombe wa Tanzania, lakini ina utajiri mwingi japokuwa asilimia kubwa ni jangwa…Na kwa sehemu watu wake wamejaliwa kuwa na uwezo wa ubunifu na uvumbuzi.

Idadi ya waisraeli waliopo Israeli sasahivi inakadiriwa kuwa Milioni 9. Nchi ya Israeli ndiyo nchi pekee duniani yenye idadi kubwa ya maadui kuliko nchi nyingine zote..Kwani imezungukwa na nchi za kiarabu pande zote ambazo zinalipinga vikali Taifa hilo.

Pamoja na maadui wote hao lakini bado Mungu anawashindania. Kwasababu anakusudi nao katika siku za mwisho. Kwani baada ya unyakuo wa kanisa kupita Mungu atalirudia tena Taifahilo kwa nguvu  na kuwapa watu wake moyo wa Toba…Wayahudi wote watatubu kwa machozi na maombolezo kwa uchafu wote wanaoufanya na kwasababu walimsulibisha Masihi wao…na Bwana atawaasamehe na kuanza kuwashindania tena kama nyakati za kale…na mataifa yote yatapanga vita dhidi ya Taifa hilo na Mungu atalishindia yote..

Hatuwezi kuandika mambo yote hapa kuhusu Taifa hilo…lakini kwa urefu kasome binafsi biblia hususani vile vitabu vitano vya Musa, ukihitaji kujua kama Israeli ilikuwa na mfalme au la kasome kitabu cha Wafalme..Ukitaka kujua kama Israeli ilishawahi kwenda utumwani tena kwa mara nyingine kasome kitabu cha Mambo ya nyakati..Ukitaka kujua kuhusu Hekalu la Mungu lililokuwepo Israeli kasome kitabu cha Wafalme…Ukitaka kujua Makuhani walikuwa ni wakina nani, na majukumu yao, na mavazi na kwa jinsi gani sadaka zilikuwa zinatolewa katikakati ya wana wa Israeli kasome kitabu cha mambo ya walawi…

Ukitaka kujua kwa urefu safari ya wana wa Israeli..mambo yaliyowakuta njiani wakati wanakwenda kaanani kasome kitabu cha Hesabu..Ukitaka kujua ni kwa namna gani walishindana vita na kutwaa urithi wao wakati wanaingia kaanani kasome kitabu cha Yoshua.

Ukitaka kujua sheria walizopewa, na hukumu pamoja na ahadi na aina ya vyakula walivyoamuriwa wale na vile walivyoambiwa wasile kasome kitabu cha kumbukumbu la Torati..Na ukitaka kujua ni kwa jinsi gani watarudiwa katika siku hizi za mwisho kasome kitabu cha Warumi.

Na mengine baadhi fungua masomo mengine mwisho wa somo hili..

Bwana akubariki. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Je umeokoka?..una uhakika wa kwenda mbinguni?..Kumbuka yeye ajaye anakuja upesi wala hatakawia.


Mada Nyinginezo:

WAISRAELI WENGI SANA WANARUDI KWAO SASA.

NG’OMBE MWEKUNDU ALIYEZALIWA ISRAELI, ANAFUNUA NINI?

MAMBO YATAKAYOTOKEA ISRAELI SIKU ZA HIVI KARIBUNI.

BONDE LA KUKATA MANENO.

NITAFANYA YERUSALEMU KUWA JIWE LA KUWALEMEA .

MPAKA UTIMILIFU WA MATAIFA UTAKAPOWASILI.

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!

Rudi Nyumbani:

Print this post

HALI ZETU JINSI ZINAVYOWEZA KUATHIRI UTOAJI WETU.

Mithali 11:24 “Kuna atawanyaye, lakini huongezewa zaidi; Kuna azuiaye isivyo haki, lakini huelekea uhitaji”.

Shalom, Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe. Karibu tena tuyatafakari maandiko.

Kuna kanuni Mungu kaziweka katika maisha ambazo ni vizuri tukazielewa ili tusije tukajikuta tunaangamia kwa kukosa maarifa, na kukosa maarifa ni pamoja na kuhangaika huku na huko kutafuta maombezi wakati misingi ya Neno la Mungu iliyo imara tumeiacha nyuma..

Kwamfano mtu anaweza akawa anasumbuliwa na tatizo Fulani labda tuseme, na nguvu za giza,.. lakini kwa kukosa tu maarifa ya kujua kwamba damu ya Yesu Kristo ndiyo inayoondoa mizizi yote ya nguvu za giza ndani ya mtu, pale anapoamua tu kuokoka kwa kumaanisha na kubatizwa..Sasa mtu huyo kwa kutolizingatia hilo anataka mambo hayo yaondolewe kwa njia ya maombezi na huku bado yupo katika dhambi, bado ni mzinzi, bado anaishi na mke/mume ambaye si wake, bado ni mlevi, bado anavaa mavazi yake ya kikahaba, na wakati huo huo anataka kuombewa mapepo yamtoke.

Sasa Kwa namna ya kawaida mapepo hayo hayamwacha yamesoge pembeni tu. Atajiona kama amepata tu unafuu, lakini baada ya muda tena hali yake itamrudia, na itakuwa mbaya zaidi kuliko hata ilivyokuwa hapo mwanzo.

Hiyo yote ni kutokana na kukosa maarifa sahihi ya kulitatua tatizo lake.

Jambo lingine ambalo tunapaswa tujifunze pia, Ni katika suala la utoaji. Kwa hali ya kibinadamu kutoa huwa ni kugumu kuliko kupokea..Licha ya kuwa utoaji ni nguzo muhimu kwa mtu yeyote Yule (awe mwenye dhambi asiwe mwenye dhambi )…

Lakini linapuuziwa na wengi hata na kwa watu waliookoka.

Lakini fahamu kuwa ukitaka uwe mtoaji mzuri, unapaswa uishinde hali yako ya sasa.. “Hali zetu ni adui mkubwa wa matoleo yetu”…Siku zote ukiangalia hali yako ilivyo, ukianza kupiga gharama hujafanya hiki, hujafanya kile, hata kama wewe ni bilionea utoaji wako bado utakuwa ni mgumu tu, ..kwasababu Utawaza sijawekeza kwenye hichi au kwenye kile. Vivyo vivyo hata na kwa Yule aliye na kipato cha kawaida naye akishaanza kujifikiria tu hali yake ilivyo, sijanunua, tv, sijanunua simu, sijanunua viatu, n.k. basi utoaji wake naye ndipo unapopitia ukinzani.

Kwasababu kile alichonacho hakitamtosha kukidhi matakwa yake, na huku tena afikirie kumsaidia mtu mwingine bado itakuwa ngumu, au kutoa sadaka hapo hapo kwake yeye vilevile itakuwa ngumu. Nataka nikumbie kila siku tutakuwa na uhitaji tu, hatutakoma kuwa na mahitaji hata tufanikiwe vipi, kikubwa ni kuzishinda hali zetu.

Lakini kanuni za Mungu ni tofauti, kama tukiweza kuzishinda hali zetu, au bajeti zetu, na kusema ngoja nifungue mkono wangu kwa hiki au kile, kumsaidia huyu mwenye uhitaji au Yule, au kutoa sadaka, na kuisapoti kazi ya Mungu isonge mbele, kawapa mayatima kitu kidogo, tukinyoosha mikono yetu katika mambo kama hayo ..Basi tujue kuwa huo ndio utakuwa mwanzo wa Baraka zetu, lile wingu la utukufu wa Mungu litatembea na sisi wakati wote.

Na andiko hili litatimia juu yetu;

“Kuna atawanyaye, lakini huongezewa zaidi; Kuna azuiaye isivyo haki, lakini huelekea uhitaji”.

Kwa jicho la kibinadamu utaonekana kama ni mtu usiyekuwa na malengo, au mtu usiyekuwa na bajeti ya maisha, lakini Mungu hatakuacha..Siku zitakuja siku zitakwenda, ipo milango ambayo Mungu atahakikisha anakufungulia ki-miujiza miujiza, utashangaa, umewezaje kuvuka hapa au pale, Utashangaa kile ulichokipoteza Mungu anakurudishia na zaidi, na utakuwa umepata faida mara mbili..kujiwekea hazina mbinguni, na hapa duniani.

Luka 6:38 “Wapeni watu vitu, nanyi mtapewa; kipimo cha kujaa na kushindiliwa, na kusukwa-sukwa hata kumwagika, ndicho watu watakachowapa vifuani mwenu. Kwa kuwa kipimo kile kile mpimacho ndicho mtakachopimiwa”.

Lakini kama kila kitu tunachokipata tunasema hichi ni cha kwetu tu,.tuna malengo mengi ya kufanya, mwaka huu nataka nifanye hivi au vile hivyo kwasasa sina fedha ya kwenda nje ya bajeti yangu..Siwezi kumsaidia ndugu yangu huyu mwenye shida hii, siwezi kuwasidia yatima wale, siwezi kumtolea Mungu…nataka nikuambie tutajiona kama tunakusanya, na fedha zetu hazipotei bure,zipo katika bajeti, lakini tutabakia katika hali hiyo hiyo miaka nenda miaka rudi, na mwisho wa siku tutajikuta malengo yetu kuyafikia bado yapo mbali na sisi..

Na hivyo Neno hili nalo pia linatimia juu yetu: “Kuna azuiaye isivyo haki, lakini huelekea uhitaji”.

Tutaelekea uhitaji ikiwa tutazuia matoleo yetu,..Hivyo utoaji ni jambo la muhimu sana, katika kuvuta Baraka za Mungu katika maisha yetu. Tendo moja la utoaji lina nguvu hata mara elfu kumi zaidi ya Maneno tunayomuomba Mungu kila siku atubariki katika sala. Lakini pia kumbuka katika kumtolea Mungu madhabahuni au katika kazi yake..zingatia kuwa msafi kwasababu Mungu wetu hapedezwi tunapomtolea sadaka na wakati ndani ya mioyo yetu tupo mbali naye…

Na ili tuwe watoaji wazuri, tupunguze msisitizo katika kuzitazama hali zetu za sasa. Na Bwana atatubariki, kama alivyoahidi katika Neno lake, kwasababu yeye si mwongo.

Ubarikiwe.jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

NGUVU ILIYOPO KATIKA MAAMUZI.

HERI NINYI MLIAO SASA, KWA SABABU MTACHEKA.

DHAMBI INAZAA KIFO.

UPAKO NI NINI?

JE VIBWENGO NI KWELI VIPO?

Rudi Nyumbani:

Print this post