Title Devis

JE UPENDO WAKO UMEPOA?

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe. Karibu tuyatafakari Pamoja maandiko.

Kuna hili andiko ambalo ni maarufu sana kwetu, ambalo ni unabii Bwana alioutoa na kusema kuwa utatimia kipindi kifupi sana kabla ya kurudi kwake mara ya pili duniani.. Na neno hilo tunalisoma katika Mathayo 24:12 inasema;

“Na kwa sababu ya kuongezeka maasi, UPENDO WA WENGI UTAPOA”.

Sasa mpaka biblia imesema upendo wa wengi utapoa, maana yake ni kwamba hapo kwanza walikuwa na upendo thabiti kabisa uliokubaliwa na Mungu lakini sasa, hawanao tena…Na kwa haraka haraka ni rahisi kufikiri, kuwa upendo wa kwanza unaozungumziwa hapo, ni ule wa kupendana sisi kwa sisi, Ndio! Huo ni upendo lakini sio wa kwanza bali ni wa pili…, Jicho la Mungu, halikuuona upendo huo, bali liliona upendo mwingine ulio mkuu kupita huo, ambao ni upendo wa KUMPENDA MUNGU.

Marko 12.28 “………..Katika amri zote ni ipi iliyo ya kwanza?

29 Yesu akamjibu, YA KWANZA ndiyo hii, SIKIA, ISRAELI, Bwana Mungu wetu ni Bwana mmoja;

30 nawe MPENDE BWANA MUNGU WAKO KWA MOYO WAKO WOTE, NA KWA ROHO YAKO YOTE, NA KWA AKILI ZAKO ZOTE, NA KWA NGUVU ZAKO ZOTE.

31 Na ya pili ndiyo hii, Mpende jirani yako kama nafsi yako. Hakuna amri nyingine iliyo kuu kuliko hizi”

Hivyo upendo wa Kwanza unaozungumziwa kwamba utapoa kwa watu wengi, katika siku za mwisho ni UPENDO WA KUMPENDA MUNGU KWA MOYO WOTE, AKILI ZOTE na NGUVU ZOTE. Na baada ya huo ndio unafuata upendano wa sisi kwa sisi.

Na hao “wengi” waliozungumziwa hapo…sio watu wa kidunia, kwasababu watu wa kidunia kwa kuanzia tu, tayari hawampendi Mungu….Bali hao “wengi” wanaozungumziwa hapo kwamba hapo kwanza walikuwa na upendo wa kumpenda Mungu lakini sasa UMEPOA ni “wakristo (Yaani wale ambao tayari walikuwa wamemwamini Yesu)”, hao ndio wengi wanaozungumziwa kwamba siku za mwisho upendo wao wa kumpenda Mungu utapoa…

Maana yake ni hii, kipindi karibia na unyakuo (ambacho kipindi ndicho hichi tuishicho), kutakuwa na jopo kubwa la wakristo wanaorudi nyuma…Na hiyo ni kutokana na kuongezeka kwa maasi duniani. Wakristo wengi watakuwa vuguvugu..

Mtu hapo kwanza alikuwa ni mwombaji, lakini ghafla anaacha kuwa mwombaji, anakuwa bize kutafuta mambo mengine, hapo kwanza alikuwa ni mhubiri, sasa ni mhubiri wa mambo maovu, hapo kwanza alikuwa ni mnyenyekevu mbele za Mungu, lakini sasa ni mwenye kiburi, hapo kwanza alikuwa analisoma Neno kwa bidii, na kuweza hata kugundua mitego na mahubiri madanganyifu, lakini sasa hawezi tena, hapo kwanza alikuwa anajitoa kwa tabu usiku na mchana kuhakikisha injili inakwenda mbele lakini sasa hafanyi hivyo tena, hapo kwanza alikuwa mvumilivu, sasa ni mtu mwenye hasira na visasi, hapo kwanza alikuwa anapiga mbio katika Imani bila kuchoka, lakini sasa amepoa, na kuzimia… Hawa ndio ambao upendo wao umepoa.

Ufunuo 2:2 “Nayajua matendo yako, na taabu yako, na subira yako, na ya kuwa huwezi kuchukuliana na watu wabaya, tena umewajaribu wale wajiitao mitume, nao sio, ukawaona kuwa waongo;

3 tena ULIKUWA na subira na kuvumilia kwa ajili ya jina langu, wala hukuchoka.

4 LAKINI NINA NENO JUU YAKO, YA KWAMBA UMEUACHA UPENDO WAKO WA KWANZA.

5 BASI, KUMBUKA NI WAPI ULIKOANGUKA; UKATUBU, UKAYAFANYE MATENDO YA KWANZA. Lakini, usipofanya hivyo, naja kwako, nami nitakiondoa kinara chako katika mahali pake, usipotubu”,

Katika Mstari huo wa 3, Bwana Yesu anasema…tena “ulikuwa na Subira na kuvumilia …” maana yake ni kwamba kwasasa huna tena hiyo Subira na huna uvumilivu tena, umerudi nyuma.

Lakini kwasababu Yesu ni wa rehema, anatoa ushauri. Urudi, ukatubu, UKAFANYE MATENDO YAKO YA KWANZA, (rudi kuwa mwombaji kama hapo mwanzo, rudi kuwa mvumilivu kama kwanza, hubiri Habari njema za ufalme kama ulivyokuwa unafanya hapo mwanzo, rudi kuwa mpole kama kwanza, n.k). Itakuwa heri.

Lakini usipofanya hivyo anasema, atakuja kukiondoa kinara chako mahali pake, kama usipotubu.

Kinara, ni chanzo cha NURU katika Maisha yako.  Kila mwanadamu, na kila kanisa na kila nchi inayo kinara cha taa yake. Hiyo ni kwaajili ya kumpa Nuru mtu, au kanisa au nchi. Na nuru hiyo ni ya rohoni na mwilini. Kikiondolewa hicho kinara juu ya mtu, anakuwa hawezi kwenda mbele katika Maisha yake ya rohoni na mwilini…kiza kinaingia katika Maisha yake ya rohoni na mwilini.

Kadhalika kinara kikiondolewa katika kanisa, kiza kinaingia, kanisa hilo linapoteza uelekeo na kupotea na Taifa ni hivyo hivyo.. Wana wa Israeli kuna kipindi kinara chao kiliondolewa na matokeo yake ni Taifa zima kuuawa kikatili na waliosalia kupelekwa utumwani Babeli.

Hivyo usikubali kurudi nyuma ndugu yangu, unayesoma ujumbe huu..Kumbuka kinara bado kipo katika maisha yako ndio maana unaona angalau bado kuna neema katika Maisha yako, lakini usipuridi katika mstari uliouacha, upo hatarini kuingia gizani.Ukizingatia hizi ni nyakati za maasi kuzidi ulimwenguni.

Bwana akubariki

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Mada Nyinginezo:

Rudi Nyumbani:

Print this post

Kinubi ni nini katika biblia? (1Samweli 16:16, 23)

Vyombo vya muziki vilivyotumika zamani katika biblia viligawanyika katika makundi makuu matatu.

  1. Vyombo vilivyopulizwa: Mfano Baragumu, filimbi, Tarumbeta, pembe, panda,
  2. Vyombo vilivyopigwa na kutoa sauti : Mfano Tari, Zomari, ngoma, kengele.
  3. Vyombo vilivyopigwa kwa kukwanyuliwa nyuzi zake: Mfano kinanda, kinubi, zeze, Santuri.

Kinubi, ni moja ya ala ya muziki, iliyopigwa kwa kukwanyua nyuzi zake aidha kwa kidole au kwa kifaa kingine kidogo. Kinubi kwa wayahudi kilikuwa kinatengenezwa kwa nyuzi kumi za utumbo mdogo wa kondoo.

Kuona jinsi kinavyopigwa..tazama video hii youtube >> https://www.youtube.com/watch?v=cS5d2wD8OoI

Bibia inamuonyesha Daudi alikitumia kifaa hichi, kwa ajili ya kumtuliza Mfalme Sauli, pale roho mbaya kutoka kwa Bwana ilipokuwa inamjia.

1Samweli 16:16 “Basi bwana wetu na atuamuru sisi watumishi wake waliopo hapa mbele yako watafute mtu aliye stadi wa kupiga kinubi; basi itakuwa, roho ile mbaya kutoka kwa Mungu itakapokujilia, yeye atapiga kinubi kwa mkono wake, nawe utapona…..

23 Ikawa, ile roho mbaya kutoka kwa Mungu ilipomjilia Sauli, ndipo Daudi akakishika kinubi, akakipiga kwa mkono wake, naye Sauli akaburudishwa, na ile roho mbaya ikamwacha”.

Wana wa Lawi pia walivitumia kumsifia Mungu wakati hekalu la Mungu lilipokuwa linajengwa.(2Nyakati 5:12)

Biblia pia inatuonyesha wale watu watakaotoka katika dhiki kuu siku ile, watakuwa na vinubi vyao mikononi wakimwimbia Kristo.

Ufunuo 15:2 “Tena nikaona kitu kama mfano wa bahari ya kioo iliyochangamana na moto, na wale wenye kushinda, watokao kwa yule mnyama, na sanamu yake, na kwa hesabu ya jina lake, walikuwa wamesimama kando-kando ya hiyo bahari ya kioo, wenye vinubi vya Mungu.

3 Nao wauimba wimbo wa Musa, mtumwa wa Mungu, na wimbo wa Mwana-Kondoo, wakisema, Ni makuu, na ya ajabu, matendo yako, Ee Bwana Mungu Mwenyezi; Ni za haki, na za kweli, njia zako, Ee Mfalme wa mataifa”.

Je! Na sisi tunapaswa tutumie vinubi katika kumwimbia Mungu?

Jibu ni ndio, ala yoyote ile ya mziki, iwe ni ngoma, iwe ni gitaa, iwe ni njuga, iwe ni zeze, iwe ni marimba, n.k. vinafaa katika kumwimbia Mungu. Isipokuwa tu hatupaswi kuimba kwa staili za kinua. Bali tunapaswa tumwimbie Mungu katika uzuri na utakatifu.

Zaburi 150:1 “Haleluya. Msifuni Mungu katika patakatifu pake; Msifuni katika anga la uweza wake.

2 Msifuni kwa matendo yake makuu; Msifuni kwa kadiri ya wingi wa ukuu wake.

3 Msifuni kwa mvumo wa baragumu; Msifuni kwa kinanda na kinubi;

4 Msifuni kwa matari na kucheza; Msifuni kwa zeze na filimbi;

5 Msifuni kwa matoazi yaliayo; Msifuni kwa matoazi yavumayo sana.

6 Kila mwenye pumzi na amsifu Bwana. Haleluya”.

Bwana akubariki.

Tazama ala nyingine za muziki chini.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618.

Jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

Santuri ni nini? (Danieli 3:5,10)

Matoazi na Matari ni nini? (Kutoka 15:20)

Aina za dhambi

Kijicho ni nini? (Marko 7:22)

USIPIGE MATEKE MCHOKOO!

GOGU NA MAGOGU, Katika biblia ni nani?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Matoazi na Matari ni nini? (Kutoka 15:20)

SWALI: Shalom, Naomba kuuliza maana ya MATOAZI kama vyombo vya muziki ni chombo gani? Asante sana


JIBU:

Matoazi, na  Matari ni jamii moja,, Hizi ni za ala za muziki, ambazo zilitumika kwa matukio tofauti tofauti , aidha kusifu, kuimba, kusherehekea, kukaribisha, kupongeza na wakati mwingine kwenye miendo ya  vitani.. zikiimbwa huwa zinashikiliwa na mkono mmoja na mkono mwingine unatumika kupiga toazi au tari kwa utashi, na kupigwa kwake ni lazima kuambatane na kucheza. Tazama picha.

Ili kuelewa kinadharia zaidi, unaweza kutazama video hizi chache Youtube, uone jinsi upigwaji wake ulivyo.

https://www.youtube.com/watch?v=4UJT9sM_ABo

https://www.youtube.com/watch?v=xbhk5yYgUxI

Katika biblia tunaona, wakati ule Daudi alipokuwa analileta sanduku la Bwana, Yerusalemu, yeye na Israeli wote walikusanyika na kumchezea Mungu kwa nguvu zao zote, na moja ya kifaa cha muziki walichokitumia kumwimbia Mungu kwa nguvu zile z kilikuwa ni Matoazi

2Samweli 6:5 “Daudi na nyumba yote ya Israeli wakacheza mbele za Bwana kwa nguvu zao zote, kwa nyimbo, na kwa vinubi, na kwa vinanda, na kwa matari, na kwa kayamba, na kwa matoazi”.

Hata alipowaweka Walawi kwa kazi mbalimbali za kikuhani, wale aliowaweka katika zamu za uimbaji, wote walibeba matoazi yao, kwa ajili ya kumwimbia Mungu.

1Nyakati 15:15 Na wana wa Walawi wakalichukua sanduku la Mungu mabegani mwao kwa miti yake, kama vile Musa alivyoamuru, sawasawa na neno la Bwana.

16 Kisha Daudi akamwambia mkuu wa Walawi, kwamba awaagize ndugu zao waimbaji, pamoja na vyombo vyao vya kupigia ngoma, vinanda, na vinubi, na matoazi, wavipige na kupaza sauti kwa furaha.

Soma pia 1Nyakati 13:8, 16:42, 25:1. 2Nyakati 29:25

miriamu na matari

Tunamwona tena Miriamu, dada yake Musa, siku ile, Mungu alipowapigania na kuwaangamiza maadui zao wamisri katika bahari ya Shamu, biblia inatuambia Miriamu pamoja na wanawake wengine waliondoka na kumchezea Mungu sana, na ala walizotumia yalikuwa ni haya Matari.

Kutoka 15:20 “Na Miriamu, nabii mke, ndugu yake Haruni, akatwaa tari mkononi mwake; wanawake wakatoka wote wakaenda nyuma yake, wenye matari na kucheza”.

Tunamwaona Yeftha naye alipotoka vitani, kwa ushindi, binti yake akatokea ili kumlaki kwa kumchezea, na kifaa alichokitumia kilikuwa ni haya Matari.

Waamuzi 11:34 “Kisha Yeftha akafika Mispa nyumbani kwake, na tazama, binti yake akamtokea kumlaki, na matari na machezo; naye alikuwa ni mwanawe pekee; hakuwa na mwingine, mwana wala binti, ila yeye”.

Je hata sasa na sisi tunaruhusiwa kumchezea Mungu kwa matari?

Ndio Mungu anapaswa afurahiwe, kwa midundo tofauti tofauti na ala tofauti tofauti za muziki, ikiwa akina Miriamu, na Daudi, na wana wa Israeli wote walimchezea Mungu kwa nguvu zao zote, hata sisi tunapaswa tufanye hivyo na zaidi, kwa mambo makuu Mungu  anayotutendea kila siku na zaidi sana kwa kutupa zawadi ya mwanawe mpendwa YESU KRISTO ili atuokoe.

Lakini jambo la kuzingatia ni kuwa uchezaji wetu haupaswi kufanana na ule wa watu wa kidunia, wala uimbaji wetu haupaswi kufanana na ule wa watu wa kidunia, Vinginevyo sifa zetu zitabadilika na kuwa kufuru mbele za Mungu. Hilo ni la kulizingatia sana. Tuchezapo tucheze kwa jinsi Mungu atakavyotuajilia, lakini sio kumchezea Mungu kwaito, na mfano wa staili za kidunia ambazo hazimpendezi Mungu.

ZABURI 150

1 Haleluya. Msifuni Mungu katika patakatifu pake; Msifuni katika anga la uweza wake.

2 Msifuni kwa matendo yake makuu; Msifuni kwa kadiri ya wingi wa ukuu wake.

3 Msifuni kwa mvumo wa baragumu; Msifuni kwa kinanda na kinubi;

4 Msifuni kwa matari na kucheza; Msifuni kwa zeze na filimbi;

5 Msifuni kwa matoazi yaliayo; Msifuni kwa matoazi yavumayo sana.

6 Kila mwenye pumzi na amsifu Bwana. Haleluya.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618.

Jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

AGANO LAKO LINABEBWA NA NANI?.

Mkatale ni nini katika biblia? (Matendo 16:24)

USIPIGE MATEKE MCHOKOO!

NA BAADA YA LILE TONGE, SHETANI AKAMWINGIA.

KWANINI KRISTO AFE?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Bwana Yesu alimaanisha nini kusema “Saa yangu haijawadia?”

SWALI: Bwana Yesu alimaanisha nini kumwambia mama yake, “Saa yangu haijawadia”?

Yohana 2:1 “Na siku ya tatu palikuwa na arusi huko Kana, mji wa Galilaya; naye mama yake Yesu alikuwapo.

2 Yesu naye alikuwa amealikwa arusini pamoja na wanafunzi wake.

3 Hata divai ilipowatindikia, mamaye Yesu akamwambia, Hawana divai.

4 Yesu akamwambia, Mama, tuna nini mimi nawe? Saa yangu haijawadia”.

JIBU: Saa anayoizungumzia hapo ni saa ya Yesu kutukuzwa duniani, lakini sio kutukuzwa tu peke yake, bali pia na siku ya mateso yake,

Sasa katika habari hiyo, Mama yake, alitazamia Yesu awasaidie wale watu kwenye shughuli yao waliyoiandaa, na bila shaka tarajio lake halikuwa Yesu atoe fedha au nguvu kazi, hapana tarajio lake lilikuwa ni Yesu afanye muujiza, na kwa tukio hilo Yesu atatukuzwa..Lakini Yesu kwa kulijua hilo alimkatiza mama yake, ni sawa na alimwambia mama unataka nitukuzwe kwa tendo hili?, Nina nini mimi nawe?, Saa yangu ya kutukuzwa haijafika, ikifika ni lazima nitukuzwe tu, lakini haitakuwa kutukuzwa kwa njia hii tu peke yake, bali itakuwa na  mateso pia, kwasababu Hiyo nayo ni saa yangu.

Na ndio maana utaona katika matukio ya aina hizi mbili, Yesu alilisema neno hilo.

Tukio la kwanza ni pale walipotaka kumkamata ili kumuua , na alipokaribia kwenda msalabani alisema Neno hilo,

Yohana 7:30 “Basi wakatafuta kumkamata; lakini hakuna mtu aliyeunyosha mkono wake ili kumshika, kwa sababu saa yake ilikuwa haijaja bado”.

Akimaanisha saa yake ya mateso yenyewe haijaja..

Yohana 13:1 “Basi, kabla ya sikukuu ya Pasaka, Yesu, hali akijua ya kuwa saa yake imefika, atakayotoka katika ulimwengu kwenda kwa Baba, naye ali amewapenda watu wake katika ulimwengu, aliwapenda upeo”.

Kote huku akimaanisha saa ya mateso..

Yohana 12:27 “Sasa roho yangu imefadhaika; nami nisemeje? Baba, uniokoe katika saa hii? Lakini ni kwa ajili ya hayo nilivyoifikia saa hii.

28 Baba, ulitukuze jina lako. Basi ikaja sauti kutoka mbinguni, Nimelitukuza, nami nitalitukuza tena”.

Unaona? Na sehemu ya pili ni pale, watu walipomtukuza sana, aliita ni saa yake, ambayo ndio hiyo mama yake alikuwa anaitazamia wakati ule,  utaona baada ya kumfufua Lazaro, na watu wengi kutoka mataifa mbalimbali wakawa wanataka kuja kumuona, na watu wakamtandikia nguo zao, na miti ya mitende wakimwimbia Hosana kwa sauti kuu mpaka mji ukataharuki.. ndipo hapo alisema tena maneno hayo;

Yohana 12:21 “Basi hao walimwendea Filipo, mtu wa Bethsaida ya Galilaya, wakamwomba, wakisema, Bwana, sisi tunataka kumwona Yesu.

22 Filipo akaenda, akamwambia Andrea; kisha Andrea na Filipo wakamwambia Yesu.

23 Naye Yesu akawajibu, akasema, SAA IMEFIKA ATUKUZWE MWANA WA ADAMU”.

Hivyo popote unapoona Yesu anasema SAA YANGU, jua anamaanisha saa ya kutukuzwa kwake, na saa ya mateso yake.

Amen.

Nasi pia tuna saa zetu hapa duniani, Mungu akitaka kututukuza, ni lazima kicheko na huzuni viambatane nasi, Yesu alitumia mfano wa SAA ya mwanamke azaapo kufananisha na saa zetu.

Yohana 16:21 “Mwanamke azaapo, yuna huzuni kwa kuwa saa yake imefika; lakini akiisha kuzaa mwana, haikumbuki tena ile dhiki, kwa sababu ya furaha ya kuzaliwa mtu ulimwenguni.

22 Basi ninyi hivi sasa mna huzuni; lakini mimi nitawaona tena; na mioyo yenu itafurahi, na furaha yenu hakuna awaondoleaye”.

Mhubiri 3: 1 Kwa kila jambo kuna majira yake, Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu.…..4 Wakati wa kulia, na wakati wa kucheka; Wakati wa kuomboleza, na wakati wa kucheza”.

Bwana atusaidie, tuyatuambue majira yetu.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618.

Jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

Je! mabalasi Bwana Yesu aliyoyatumia kugeuzia maji kuwa divai, yalitumika tu kwa kazi hiyo?

CHEMBE YA NGANO ISIPOANGUKA KATIKA NCHI, IKAFA,

KWANINI NAYAWEZA MAMBO YOTE KATIKA YEYE ANITIAYE NGUVU?

JIFUNZE KULIGAWANYA VYEMA NENO LA MUNGU.

SIKU ZA WATUMISHI WA MUNGU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

KWANINI KRISTO AFE?

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe.

Swali la msingi: Kwanini Kristo afe, si angekuja tu kuhubiri na kufundisha njia ya wokovu na kisha apae zake kurudi juu alipotoka, kulikuwa na sababu gani ya kufa?. Leo tutajifunza sababu chache za kifo cha Bwana Yesu. Kwa kuchunguza vitu vya asili, kumbuka vitu vingi vya asili vinahubiri injili, Ndio maana sehemu kadhaa Bwana Yesu alikuwa anasema maneno haya..

Luka 13:18  “Kisha alisema, Ufalme wa Mungu umefanana na nini? NAMI NIUFANANISHE NA NINI? 

19  Umefanana na punje ya haradali aliyotwaa mtu akaitupa katika shamba lake; ikamea, ikawa mti; ndege wa angani wakakaa katika matawi yake. 

20  Akasema mara ya pili, NIUFANANISHE NA NINI UFALME WA MUNGU?”.

Maana yake ufalme wa mbinguni, umeandikwa katika vitu vya asili, umeandikwa katika Maisha ya kawaida tunayoishi, katika shughuli tunazozifanya n.k

Sasa Umuhimu wa Kifo cha Bwana Yesu, pia tunaweza kuupata kwa kupitia vitu hivi hivi vya asili, kama tukivitafakari kwa hekima.

Zifuatazo ni sababu chache za Umuhimu wa Kifo cha Bwana Yesu.

  1. Sababu ya kwanza, Ile Bwana Yesu aliyoitoa mwenyewe katika kitabu cha Yohana.

Yohana 12:24  “Amin, amin, nawaambia, Chembe ya ngano isipoanguka katika nchi, ikafa, hukaa hali iyo hiyo peke yake; bali ikifa, hutoa mazao mengi”.

Hapo Bwana alikifananisha kifo chake na jinsi chembe ya ngano, inavyopandwa…Siku zote ukichukua mbegu yeyote, ile ya mahindi, au maharage, ukiifunga ndani ya gunia mahali ambapo haitaingiliwa na wadudu, ile mbegu inaweza kukaa hata miaka 5, bila kuharibika, na bila kumea chochote… Lakini utakapoichukua na kuitupa ardhini, ikazama chini ya udongo, ikapatwa na umande wa ardhini, ikaoza, wadudu wakaitembelea kidogo, wakala gamba lake la nje, ikanuka kidogo..Ndipo hapo itaanza kumea, na mwishoni kuwa mche mkubwa au hata mti, na kuzaa matunda mengi, yenye mbegu nyingi…Lakini isipopitia hizo hatua haitazaa chochote.

Na hiyo ndio sababu ya Kristo kufa..Kristo asingekufa na kufufuka, Injili isingefika duniani kote, Mataifa tusingepata wokovu…Lakini baada ya kufa, akatuletea nguvu ya Roho Mtakatifu juu yetu, kwa uweza na nguvu..Neno lake likasambaa duniani kote mpaka leo. Hivyo ilikuwa ni muhimu sana Kristo afe.

  1. Sababu nyingine ya kufa kwa Yesu, ni ili azizike dhambi zetu.

Kumbuka kuwa Kristo alibeba dhambi zetu, laumu zetu alizibeba, kwaufupi mbele za Mungu alikuwa ni mwenye hatia kwaajili yetu. Kutokana na dhambi zetu kuwa nyingi, Baba yake (ambaye ndio Baba yetu) aliuficha uso wake kwa muda ule alipokuwa pale msalabani, ndio maana akalia..Mungu wangu..Mungu wangu mbona umeniacha?..

Wagalatia 3:13 “ Kristo alitukomboa katika laana ya torati, KWA KUWA ALIFANYWA LAANA KWA AJILI YETU; maana imeandikwa, Amelaaniwa kila mtu aangikwaye juu ya mti”.

Kwahiyo suluhisho pekee ya kuitoa hiyo laana juu yake ilikuwa ni KUFA, Asingekufa ile laana ingeendelea kukaa juu yake, Mungu angeendelea kujitenga naye vile vile siku zote.. Hivyo pale alifanyika najisi/laana kwaajili yetu.. Kwa dhambi zetu, ikasababisha Mungu kujitenga naye..

Sasa kifo kimefananishwa na usingizi, Siku zote mtu akiwa amechoka sana, hata uumpe pesa kiasi gani, hawezi kuundoa ule uchovu, hata umpe chakula cha aina gani hawezi kuundoa ule uchovu, suluhisho la kumfanya mtu arudie ukakamavu wake ni kulala..Akishalala akiamka, ule uchovu wote utakuwa umetoweka, na atarudi ukakamavu upya.

Na kifo kazi yake ni hiyo hiyo, ilikuwa haina budi Kristo, afe ili azike uchovu wa dhambi zetu, na afufuke akiwa katika upya.

Pia tunaweza kujifunza kwa vifaa vichache tunavyovitumia kama simu au computer… Simu ikileta usumbufu (imeganda, au imekuwa slow sana)..mara nyingi suluhisho ni kuizima na kuiwasha (kui-restart).

  1. Faida ya tatu ya kifo cha Bwana Yesu, ni ili azipokee baraka (Yaani apokee urithi).

Kristo alipokufa na kufufuka ndipo akaenda kuketi mkono wa kuume wa Mungu Baba, mamlaka yote na urithi wote akawa amekabidhiwa rasmi…

Waebrania 9:16  “Maana agano la urithi lilipo, lazima iwepo mauti yake aliyelifanya.

17  Kwa maana agano la urithi lina nguvu palipotukia kufa kwa mtu; kwa kuwa halina nguvu kabisa, akiwa yu hai yeye aliyelifanya”

Sasa ni kwa namna gani kifo kihusiane na urithi?

Turudi kwenye mfano ule ule wa kifaa kinachoitwa simu au computer..kama wewe ni mtumiaji wa simu, zinazojulikana kama simu-jacha (smartphone) au computer.. Utakuwa unajua kwamba ili kila unapotaka kuongeza program nyingine, ili ifanye kazi, inakuambia ukizime na kukiwasha kifaa chako..ili kile ulichokiongeza kiweze kufanya kazi.

Ukitaka simu yako iwe na uwezo kutumia internet, huna budi kutumiwa zile settings na shirika la huo mtandao, na kisha wakishakutumia watakuambia zima simu yako na kuiwasha. Sasa unaweza kujiuliza ni kwanini wakwambie uzime na kuiwasha..Kwanini wasikwambie tu, endelea kuitumia hivyo hivyo.

Na Kristo, ni hivyo hivyo, alikabidhiwa mamlaka na Baba akiwa hapa duniani sawasawa na Marko 28:18, lakini Mamlaka hayo ili yaweze kuwa na nguvu zaidi, hana budi Bwana Yesu, kufa na kufufuka.

Kwahivyo kwa hayo machache, Ilikuwa ni lazima Kristo afe, na kufufuka ili Mamlaka yake iwe na nguvu. (Kwa urefu wa habari hiyo fungua hapa >> FAHAMU KINACHOMGHARIMU MUNGU, KUTOA URITHI WAKE.

Bwana atusaidie Mauti ya Yesu iwe na nguvu kwetu pia. Biblia inasema tunapomwamini Yesu, tunatakiwa tufe pamoja naye na kufufuka pamoja naye na kuketi pamoja naye katika roho..

Na tunakufa na kufufuka pamoja na Kristo kwa njia ya Ubatizo..Utauliza hiyo inapatikana wapi kwenye biblia..?

Warumi 6:3  “Hamfahamu ya kuwa sisi sote tuliobatizwa katika Kristo Yesu tulibatizwa katika mauti yake?

4  BASI TULIZIKWA PAMOJA NAYE KWA NJIA YA UBATİZO KATIKA MAUTI YAKE, kusudi kama Kristo alivyofufuka katika wafu kwa njia ya utukufu wa Baba, vivyo hivyo na sisi tuenende katika upya wa uzima”.

Ndio maana ubatizo sahihi ni wa muhimu sana, ni kitu kidogo cha dakika moja lakini shetani hakipendi milele. Atamfanya mtu apende kuogelea katika fukwe za bahari masaa hata matano, lakini hatamruhusu aingie kwenye maji hayo hayo abatizwe kwa dakika mbili tu, kwa jina la Yesu. Hataruhusu hilo kamwe!..atahakikisha anamletea huyo mtu mapepo ya kumshawishi, na kuona kile kitu hakina maana au ni kutumiza matakwa ya mwanadamu na si Mungu.

Kwasababu anajua mtu yule akiingia kwenye yale maji kwaajili ya ubatizo, na huku moyoni ametubu kabisa kwa kudhamiria kuziacha dhambi zake, anajua atakapoingia kwenye yale maji, basi maisha yake yatabadilika na kuketi karibu na Kristo katika ulimwengu wa roho, kwasababu atakuwa kafufuka pamoja na Kristo.. Jambo ambalo hawezi kuliruhusu hata kidogo.

Ndugu kama ni wewe mmojawao ambaye ulishawishika na shetani namna hiyo, leo hii mpinge, katafuta kubatizwa, ubatizo sahihi wa maji tele na kwa jina la Yesu Kristo popote pale na kwa gharama zozote, usikubali kuendelea kubaki nyuma kiroho.

Ikiwa utahitaji kubatizwa, basi wasiliana nasi kwa namba hizo hapo chini, au tutafute inbox.

Pia kama hujampokea Yesu maishani mwako, hiyo ndio hatua ya kwanza unayotakiwa uifanye, KUMBUKA YESU NDIYE NJIA, KWELI NA UZIMA. Hakuna njia nyingine zaidi yake yeye. Hivyo mpokee leo moyoni mwako na katafute ubatizo sahihi, na utaona mabadiliko makubwa sana katika maisha yako.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618.

Jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

KWANINI NI YESU KRISTO WA NAZARETI?

YESU MPONYAJI.

RABI, UNAKAA WAPI?

WAKAKAA KWAKE SIKU ILE. NAYO ILIKUWA YAPATA SAA KUMI.

USINIE MAKUU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Aina za dhambi

Aina za dhambi ni zipi?


Dhambi zimegawanyika katika makundi makuu manne:

  1. Dhambi za makusudi,
  2. Dhambi zisizo za makusudi
  3. Dhambi za kutotimiza wajibu
  4. Dhambi za kutokujua.

1) Dhambi za Makusudi:

Hizi ni dhambi ambazo mtu anajua kabisa biblia imekataza kuzifanya lakini yeye anakwenda kuzitenda hivyo hivyo . Mfano wa dhambi hizi ni kama uzinzi, wizi, uuaji, aubuduji sanamu, ushirikina,  rushwa n.k.

Luka 12:47 “Na mtumwa yule aliyejua mapenzi ya bwana wake, asijiweke tayari, wala kuyatenda mapenzi yake, atapigwa sana”.

Hesabu 15:30 “Lakini mtu afanyaye neno lo lote kwa kusudi, kama ni mzalia, kama ni mgeni, huyo amtukana Bwana; na mtu huyo atakatiliwa mbali na watu wake.

31 Kwa sababu amelidharau neno la Bwana, na kuyavunja maagizo yake; mtu huyo atakatiliwa mbali, uovu wake utakuwa juu yake”.

2) Dhambi za kutotimiza wajibu:

Hizi ni dhambi ambazo mtu anafanya kwa kupuuzia wajibu wake au majukumu yake yeye kama mtu wa Mungu. Hizi zimegawanyika katika mafungu matatu;

  • Wajibu wa kuwaombea wengine:

1Samweli 12:23 “Walakini mimi, hasha! NISIMTENDE BWANA DHAMBI KWA KUACHA KUWAOMBEA NINYI; lakini nitawaelimisha katika njia iliyo njema, na kunyoka”

  •  Wajibu wa kuwahubiria wengine habari njema:

Ezekieli 3:18 “Nimwambiapo mtu mbaya, Hakika utakufa; wewe usimpe maonyo, wala husemi na huyo mtu mbaya ili kumwonya, kusudi aache njia yake mbaya na kujiokoa roho yake; mtu yule mbaya atakufa katika uovu wake; lakini damu yake nitaitaka mkononi mwako.

19 Lakini ukimwonya mtu mbaya, wala yeye hauachi ubaya wake, wala njia yake mbaya, atakufa katika uovu wake; bali wewe umejiokoa roho yako.

20 Tena mtu mwenye haki aiachapo haki yake, na kutenda uovu, nami nikiweka kikwazo mbele yake, atakufa; kwa sababu hukumwonya, atakufa katika uovu wake, wala matendo yake ya haki aliyoyatenda hayatakumbukwa; lakini damu yake nitaitaka mkononi mwako.

21 Bali ukimwonya mwenye haki, kwamba yule mwenye haki asitende dhambi, tena ikiwa yeye hatendi dhambi, hakika ataishi, kwa sababu alikubali kuonywa; nawe umejiokoa roho yako”.

  • Wajibu wa kuwasaidia wengine:

Siku ile ya Mwisho, Kristo atakapokuja biblia inasema atawatenganisha kondoo na mbuzi. Kondoo ni wale watu ambao walitimiza wajibu wao wa kuwasaidia watakatifu waliohudumu katika kazi ya Mungu wakiwa hapa duniani, na mbuzi ni wale ambao walipuuzia na kudharau, hawakujua wajibu wao, wa kutoa vitu Mungu alivyowabariki kuwasaidia watenda kazi wa Mungu.

Mathayo 25:31 “Hapo atakapokuja Mwana wa Adamu katika utukufu wake, na malaika watakatifu wote pamoja naye, ndipo atakapoketi katika kiti cha utukufu wake;

32 na mataifa yote watakusanyika mbele zake; naye atawabagua kama vile mchungaji abaguavyo kondoo na mbuzi;

33 atawaweka kondoo mkono wake wa kuume, na mbuzi mkono wake wa kushoto.

34 Kisha Mfalme atawaambia wale walioko mkono wake wa kuume, Njoni, mliobarikiwa na Baba yangu, urithini ufalme mliowekewa tayari tangu kuumbwa ulimwengu;

35 kwa maana nalikuwa na njaa, mkanipa chakula; nalikuwa na kiu, mkaninywesha; nalikuwa mgeni, mkanikaribisha;

36 nalikuwa uchi, mkanivika nalikuwa mgonjwa, mkaja kunitazama; nalikuwa kifungoni, mkanijia.

37 Ndipo wenye haki watakapomjibu, wakisema, Bwana, ni lini tulipokuona una njaa, tukakulisha, au una kiu tukakunywesha?

38 Tena ni lini tulipokuona u mgeni, tukakukaribisha, au u uchi, tukakuvika?

39 Ni lini tena tulipokuona u mgonjwa, au kifungoni, tukakujia?

40 Na Mfalme atajibu, akiwaambia, Amin, nawaambia, kadiri mlivyomtendea mmojawapo wa hao ndugu zangu walio wadogo, mlinitendea mimi.

41 Kisha atawaambia na wale walioko mkono wake wa kushoto, Ondokeni kwangu, mliolaaniwa, mwende katika moto wa milele, aliowekewa tayari Ibilisi na malaika zake;

42 kwa maana nalikuwa na njaa, msinipe chakula; nalikuwa na kiu, msininyweshe;

43 nalikuwa mgeni, msinikaribishe; nalikuwa uchi, msinivike; nalikuwa mgonjwa, na kifungoni, msije kunitazama.

44 Ndipo hao pia watajibu, wakisema, Bwana, ni lini tulipokuona wewe una njaa, au una kiu, au u mgeni, au u uchi, au u mgonjwa, au u kifungoni, tusikuhudumie?

45 Naye atawajibu, akisema, Amin, nawaambia, Kadiri msivyomtendea mmojawapo wa hao walio wadogo, hamkunitendea mimi.

46 Na hao watakwenda zao kuingia katika adhabu ya milele; bali wenye haki watakwenda katika uzima wa milele”.

3) Dhambi za kutokukusudia:

Mfano wa dhambi hizi ni kama; Mtu amepandwa na hasira, sasa kutokana na hasira zile   ukampiga mwenzake  na kumuua, lakini lengo lake lilikuwa sio kumuua, au kumpiga n.k. Hiyo ni aina ya dhambi ambayo mtu akifanya anapaswa akatubu, asipotubu, ni kosa litakalompeleka motoni.

Walawi 4:1 “Bwana akanena na Musa, na kumwambia,

2 Haya, nena na wana wa Israeli, uwaambie, Kama mtu ye yote akifanya dhambi pasipo kukusudia, katika neno lo lote ambalo Bwana amelizuilia lisifanywe, na kutenda neno lo lote la maneno hayo;

3 kama kuhani aliyetiwa mafuta akifanya dhambi, hata analeta hatia juu ya watu; ndipo na atoe kwa ajili ya dhambi yake aliyoifanya, na kumsongeza kwa Bwana ng’ombe mume mchanga mkamilifu, kuwa ni sadaka ya dhambi.

4 Naye atamleta huyo ng’ombe na kumweka mlangoni pa hiyo hema ya kukutania, mbele za Bwana; naye ataweka mkono wake kichwani mwake ng’ombe, na kumchinja huyo ng’ombe mbele za Bwana.

5 Kisha huyo kuhani aliyetiwa mafuta atatwaa baadhi ya damu ya huyo ng’ombe, na kuileta ndani ya hiyo hema ya kukutania;

4) Dhambi za kutokujua:

Ni dhambi ambazo mtu anafanya kwa kutokujua kama anachofanya ni kosa au la.

Luka 12:48 “Na yule asiyejua, naye amefanya yastahiliyo mapigo, atapigwa kidogo. Na kila aliyepewa vingi, kwake huyo vitatakwa vingi; naye waliyemwekea amana vitu vingi, kwake huyo watataka na zaidi”.

Utajiuliza ni kwanini, mtu wa namna hii aadhibiwe? Jibu ni kwamba kutojua sheria, haimaanishi kuwa sheria haitakuhukumu, ni kama tu ilivyo katika sheria za kidunia, mtu akivunja sheria kwa kisingizio cha kutoijua sheria haimfanyi mtu huyo asishitakiwe. Huwezi kwenda kumbaka mtoto mchanga, na ukasema sikujua kama sheria inakataza kitendo hicho, na adhabu yake ni kali hivyo, uachwe huru.. Unaona ni wajibu wako kuijua sheria. Ndivyo ilivyo katika sheria za Mungu.

Mtu mwovu siku ile hawezi kujitetea kwa chochote, ikiwa leo hii itaendelea na uovu wake, haijalishi atasema simjui Mungu kwa namna gani.

Bwana atusaidie tuzikwepe dhambi hizo zote kwa neema yake. Hakika tutashinda ikiwa tutadumu tu katika neema ya Roho Mtakatifu.

Je umeokoka? Je! Unajua kuwa hizi ni nyakati za mwisho, na hukumu ya kiti cheupe che enzi cha mwanakondoo ipo karibuni?  Kama upo nje ya wokovu unangoja nini, embu leo fanya uamuzi mwema wa kumgeukia muumba wako. Kumbuka biblia inatuambia;

Warumi 6:23 “Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti; bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu”.

Ikiwa upo tayari kutubu dhambi zako na kumpokea Bwana leo, basi fungua hapa kwa ajili ya kupata maelekezo muhimu ya kufanya. >>>  SALA YA TOBA

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618.

Jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

Nini maana ya “kila tendo lisilotoka katika imani ni dhambi?”

KWANINI NI LAZIMA TUFE KWA HABARI YA DHAMBI?.

TOBA IGUSAYO MOYO WA BWANA.

AKIJUA YA KUWA ANA WAKATI MCHACHE TU”.

Nini Maana ya Hosana?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Kitabu kifupi katika biblia ni kipi, na ujumbe wake ni upi?

Kitabu cha waraka wa pili wa Yohana ( 2 Yohana ) ndicho kitabu kifupi kuliko vyote katika biblia nzima, kina sura moja tu na mstari 13, kinapatikana katika agano jipya. Ili kujua ujumbe wake ni nini, fungua hapa >>>  WARAKA WA PILI WA YOHANA.


Lakini tukirudi katika agano la kale, kitabu kilicho kifupi kuliko vyote ni Kitabu cha Obadia, (japo sio kifupi kuliko vyote katika biblia nzima) chenyewe kina sura moja tu na mistari 21,

Kitabu hichi kinaeleza mambo mabaya yaliyofanya nchi ya Edomu kwa ndugu zao wayahudi.  Edomu ni taifa lililozaliwa na Esau yule ndugu yake Yakobo. Hivyo mataifa haya mawili yangepaswa yawe ni ndugu na kushirikiana katika shida na raha.

Lakini ilipotekea shida katika Israeli, wakati ule wanachukuliwa utumwani na Nebukdreza, na miji yao kuchomwa na kuteketezwa, hawa Waedomu huwakuja kuwasaidia ndugu zao waisraeli, badala yake walikuwa wanafurahia kwa kilichokuwa kinatendeka, Na kibaya zaidi walikuwa wanawasapoti maadui wa ndugu zao kufanya hivyo.

Obadia 1:11 “Siku ile uliposimama upande, siku ile wageni walipochukua mali zake, na watu wa kabila nyingine walipoingia katika malango yake, na kumpa kura juu ya Yerusalemu, wewe nawe ulikuwa kama mmoja wao.

12 LAKINI USIITAZAME SIKU YA NDUGU YAKO, siku ya mashaka yake, wala usisimange juu ya wana wa Yuda siku ya kuangamizwa kwao; wala usinene maneno ya kiburi katika siku ya shida yao.

Hivyo Mungu akaliona hilo ndipo akatumia kinywa cha nabii Obadia, kuitamkia hukumu Edomi, akasema nchi yao nayo itaangamizwa, na wageni wataitawala,

Obadia 1:4 “Ujapopanda juu kama tai, Ijapokuwa kioto chako kimewekwa kati ya nyota, Nitakushusha kutoka huko; asema Bwana”.

Na zaidi ya yote Mungu atawarejesha wana wa Israeli tena, na kuwamilikisha nchi hiyo. Lakini wao wataangamizwa, kwasababu hawakuona uchungu juu ya ndugu yao wa damu.

Obadia 1:17 “Bali katika mlima Sayuni watakuwako wenye kuokoka, nao utakuwa mtakatifu; na nyumba ya Yakobo watamiliki milki zao.

18 Na nyumba ya Yakobo itakuwa moto, na nyumba ya Yusufu itakuwa mwali wa moto, na nyumba ya Esau itakuwa mabua makavu, nao watawaka kati yao, na kuwateketeza; wala hatasalia mtu awaye yote katika nyumba ya Esau; kwa kuwa Bwana amesema hayo”.

Tunajifunza nini?

Tunapaswa tuoneane huruma sisi kwa sisi, na kusaidiana kinyume chake tukiwa tunafurahia mabaya yawapate wapendwa wetu, na kibaya zaidi tunashirikiana na wale wanaowaangamiza tujue kuwa Mungu anaweza kutugeuzia kibao na sisi kama alivyofanya kwa Waedomi. Atamwokoa yule ndugu yako, lakini wewe atakuangamiza.

Vilevile inatufundisha kuwasaidia wale walio wadhaifu wa imani, Ikiwa tutaona mtu fulani anashida ya kiroho, na shetani anataka kumwangamiza, na sisi, hutaki kuchukua hatua yoyote kwenda  kumfundisha au kumuhubiria, hilo nalo ni kosa kama walilolifanya waedomi.

Hivyo Bwana atusaidie tuwe na moyo wa kusaidiana  kama kitabu hichi Obadia kinavyotufundisha. Ni kitabu kifupi lakini kina ujumbe mzito sana kwetu.

Shalom.

Kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618.

Jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1

Biblia ina vitabu vingapi?

KWANINI NI YESU KRISTO WA NAZARETI?

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

USIIGEUZE NYUMBA YA MUNGU KUWA PANGO LA WANYANG’ANYI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Kwanini wajane vijana hawakupaswa kuandikwa?

SWALI: Kwanini Mtume Paulo, alimkataza Timotheo asiwaandike wajane vijana? Je wajane vijana hawapaswi kusaidiwa au?


Jibu: Kabla ya kwenda kwenye jibu la swali letu, kuna mambo muhimu ya kufahamu kwanza ya utangulizi.

Katika kanisa la kwanza kulikuwa na utaratibu wa kuwasaidia wazee, hususani wale wenye umri mkubwa sana. Ambao hawawezi kufanya kazi wala hawana mtu wa kuwasaidia, kama Watoto au wajukuu.

Sasa haikuwa kila mzee tu, anayejiunga na kanisa alikuwa anasaidiwa la! Haikuwa hivyo, Kulikuwa na vigezo au sifa za wazee waliokuwa wanastahili kusaidiwa. Na sifa hizo tunazisoma katika kitabu cha Timotheo..

1Timotheo 5:9  “Mjane asiandikwe isipokuwa umri wake amepata miaka sitini; naye amekuwa mke wa mume mmoja;

10  naye ameshuhudiwa kwa matendo mema; ikiwa amelea watoto, ikiwa amekaribisha wageni, ikiwa amewaosha watakatifu miguu, ikiwa amewasaidia wateswao, ikiwa amefuata kwa bidii kila tendo jema”.

  1. Sifa ya kwanza ni lazima awe mjane:

Maana yake ni kwamba kama sio mjane, anaye mume..basi huyo tayari anaweza kuhudumiwa na Mume wake, kwa mahitaji yake, hivyo asiandikwe kwenye orodha ya wanaostahili kusaidiwa na kanisa ili kanisa lisije likalemewa.

  1. Sifa ya pili, hata akiwa Mjane, ni lazima umri wake uwe ni miaka 60 na Zaidi:

Maana yake ni kwamba akiwa chini ya umri huo, bado anayo nguvu za kufanya kazi za kujipatia kipato, hivyo anaweza kuendelea kufanya kazi zake za mikono huku akiendelea na kazi ya kuhudumu katika kanisa..Ili kanisa lisije likalemewa.

  1. Ni ya tatu ni lazima awe Mke wa Mume mmoja:

Maana yake ni kwamba kabla ya mume wake kufa, awe na rekodi ya kuwa na huyo huyo mume  mmoja, na sio awe na rekodi ya kuwa na wanaume wengi. Mwanamke yeyote mwenye hiyo rekodi ya kuwa na wanaume wengi, hana sifa ya kuandikwa kwenye orodha ya wanaohitaji kusaidiwa.

  1. Na sifa ya nne na ya mwisho, ni lazima awe na rekodi ya matendo mema.

Maana yake ni kwamba sio tu mtu, kazeeka hivyo anaona sehemu ya kwenda kumalizia pensheni ya uzeeni ni kanisani, hivyo anakwenda kujiunga ili tu awe ana hudumiwa. Biblia imesema watu wa namna hiyo wasiandikwe..Watu wanaopaswa kuandikwa ni lazima wawe na rekodi ya kuifanya kazi ya Mungu katika kanisa Pamoja na matendo mema, na utakatifu.

  • Kama ni mwanamke ni lazima awe na rekodi ya kuwaosha watakatifu miguu, kwa miaka kadhaa ndani ya kanisa
  • Ni lazima awe na rekodi ya matendo mema, maana yake ni kwamba tangu aamini, mpaka anafikia uzee hana picha yoyote mbaya aliyoiacha..kwamfano hajarekodiwa kuwa mzinzi, hajawahi kukutwa akiwa mtukanaji, au mlevi, au mshirikina n.k
  • Amerekodiwa kuwa mkaribishaji, maana yake mwenye upendo kwa watu wote, na si mchoyo.

Sasa hapo biblia imeruhusu watu wenye sifa hizo kusaidiwa, lakini haikusema kila mwanamke anayefikia umri wa miaka 60 au Zaidi na ni mjane, ni lazima aandikwe kwenye orodha ya watakaosaidiwa. Hapana!!.. Kama mjane ana miaka Zaidi ya 60, na una uwezo mzuri wa kiuchumi, hapaswi kuandikwa, vile vile kama anao Watoto, au ndugu ambao wanaweza kumtunza vizuri, ni mume tu ndio hana, vile vile hapaswi kuandikwa. Wanaondikwa ni wale wajane kweli kweli ambao hawana mtu yeyote waliyebakiwa naye wa kuwasaidia, wamebaki wenyewe. Na tumaini lao lote lipo kwa Bwana, hao ndio wanaopaswa kuwekwa kwenye orodha ili kanisa lisilemewe.

1Timotheo 5:3  “Uwaheshimu wajane walio wajane kweli kweli.

4  Lakini mjane akiwa ana watoto au wajukuu, na wajifunze kwanza kuyatenda yaliyo wajibu wao kwa jamaa zao wenyewe, na kuwalipa wazazi wao. Kwa kuwa hili lakubalika mbele za Mungu.

5  Basi yeye aliye mjane kweli kweli, ameachwa peke yake, huyo amemwekea Mungu tumaini lake, naye hudumu katika maombi na sala mchana na usiku”

1Timotheo 5: 16  “Mwanamke aaminiye, akiwa ana wajane, na awasaidie mwenyewe, Kanisa lisilemewe; ili liwasaidie wale walio wajane kweli kweli”.

Sasa tukirudi kwenye swali, ni kwanini wajane vijana hawapaswi kuandikwa?.

Sababu ya kwanza tumeshaiona hapo juu, ni ili kanisa lisilemewe, kwasababu wanao nguvu na uwezo wa kufanya kazi, hivyo fungu hilo la posho, ni heri likawasaidie wale ambao hawana uwezo kabisa wa kufanya kazi, wenye umri mkubwa, ambao hawana tumaini kabisa.

Sababu ya pili ndiyo hiyo tunayoisoma katika 1Timotheo 5:11-15.

Tusome..

1Timotheo 5:11  “Bali wajane walio vijana ukatae kuwaandika hao, maana, wakizidiwa na tamaa kinyume cha Kristo, wataka kuolewa;

12  nao wana hukumu kwa kuwa wameiacha imani yao ya kwanza.

13  Tena, pamoja na hayo, hujifunza kuwa wavivu, wakizunguka-zunguka nyumba kwa nyumba; wala si wavivu tu, lakini ni wachongezi na wadadisi, wakinena maneno yasiyowapasa.

14  Basi napenda wajane, ambao si wazee, waolewe, wazae watoto, wawe na madaraka ya nyumbani; ili wasimpe adui nafasi ya kulaumu.

15  Kwa maana wengine wamekwisha kugeuka na kumfuata Shetani”

Ni ukweli usiopingika kuwa asilimia kubwa ya wanawake ni “watu wa kupenda udadi, au umbea, kutafuta tafuta kujua mambo ya watu wengine”.. Na wengi wa hao ni wale ambao hawana shughuli maalumu za kufanya, na wenye umri kati ya miaka 20-45 na wengine hadi 50. Mwanamke wa rika hili, akishakosa shughuli ya kufanya, na Zaidi akiwa hajaolewa, ni rahisi sana kuchukuliwa na hiyo roho ya udadisi dadisi. Na wivu wivu, tofauti na mwanamke ambaye ameolewa au mwenye shughuli maalumu ya kufanya. Kwasababu mwanamke aliyeolewa atakuwa akili yake yote ipo katika kuiendesha familia yake na kuitunza na kuangalia Watoto wake.

Sasa katika kanisa pia wapo wanawake, ambao ni wa rika hilo, Ambao baada ya waume zao kufa wamekuwa wajane, hivyo na wenyewe wanajiweka kwenye kundi hilo la wanawake wajane ambao kazi yao ni kudumu katika sala na maombi na kuhudumu kanisani siku zote (tumaini lao lote lipo kwa Bwana 1Timotheo. 5:5)… Hivyo na wao wanajiweka katika kundi la watu wanaohitaji kusaidiwa na kanisa.

Lakini tatizo lilionekana kwamba wengi wa wanawake hawa ambao ni vijana, wanakuja kugeuka tabia siku za mbeleni na kuanza kujiingiza kwenye mahusiano yasiyo rasmi, na tabia hizo za udadisi. Na hivyo hivyo wanakuwa wameiacha Imani ambayo walikuwa nayo hapo kwanza. Na hivyo kujiingia kwenye hukumu, kwasababu wameiacha Imani.

Kuacha Imani ya kwanza, maana yake kuacha njia ya haki waliyokuwa wanaiendea hapo kwanza.

Kwahiyo wanawake hawa, biblia imesema wasiandikwe, badala yake ni vizuri wakaolewa tena, ili wazae Watoto, wawe na majukumu, kwasababu watakapokuwa na majukumu na watakapokuwa na Watoto, watakuwa busy na familia zao, hivyo si rahisi kushawishika kuwaka tamaa na kuwa wadadisi, tofauti na wakitanga tanga bila kuwa na majukumu, ni rahisi kuchukuliwa na tamaa za kila namna.

Lakini pia kumbuka si wanawake wote ambao ni wajane na ni vijana, wana tabia hizo…Hapana!..Hapo biblia imemaanisha ni wengi wao, lakini si wote. Wapo ambao ni  wajane vijana, au hawajaolewa lakini wanaishikilia Imani, Ingawa wapo wachache sana. Katika biblia alikuwepo mwanamke aliyeitwa Ana, ambaye aliishikilia Imani bila kuiacha tangu mume wake alipokufa angali akiwa bado binti mdogo, na mpaka akiwa na miaka 80, hakuiacha Imani. Na Mungu akampa neema ya kumjua mtoto Yesu kuwa ndiye Masihi katika uchanga ule. Wakati wengine hata Yesu alipokuwa mtu mzima bado hawakumwamini.

Luka 2:36  “Palikuwa na nabii mke, jina lake Ana, binti Fanueli, wa kabila ya Asheri, na umri wake ulikuwa miaka mingi, alikuwa amekaa na mume miaka saba baada ya uanawali wake.

37  Naye ni mjane wa miaka themanini na minne; haondoki katika hekalu, ila huabudu usiku na mchana kwa kufunga na kuomba.

38  Huyu alitokea saa ile ile akamshukuru Mungu, na wote waliokuwa wakiutarajia ukombozi katika Yerusalemu akawatolea habari zake”.

Bwana atubariki

Maran atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618.

Jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

Wanaowachukua wanawake wajinga mateka ni akina nani?

Je! Mungu anaupendeleo kwa wanaume zaidi ya wanawake?

TUJIFUNZE JAMBO KWA WANAWAKE HAWA WAWILI:

Kwanini wanawake wengi huwa wanalipuka mapepo?

CHUKI ULIZO NAZO KWA MAADUI ZAKO, SIZO ALIZONAZO MUNGU JUU YAO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Nguo za magunia katika biblia ni zipi?

Nguo za magunia( au mavazi ya magunia) ndiyo mavazi ya namna gani ?

Magunia kama biblia inavyotafsiri ni tofauti na inavyotafsiriwa sasa, Leo hii ukizungumzia magunia unamaanisha labda mifuko aina ya Salfeti (Sulphate) ambayo yanatumika sana sana katika kuhifadhia nafaka, au utakuwa unazungumiza magunia yaliyoshonwa kwa nyuzi za katani.

Lakini mavazi ya magunia, biblia haiyatafsiri kama mavazi yaliyotengenezwa kwa mojawapo ya malighafi hizo (salfeti au nyuzi za katani). Bali mavazi ya magunia yaliyozungumziwa kwenye biblia ni mavazi yaliyotengenezwa kwa MANYOYA YA MBUZI.

Nguo hizo zilitengenezwa mahususi, kuashiria aidha vitu hivi viwili Maombolezo au Toba

   1. Maombolezo.

Watu zamani za biblia waliopitia misiba, au majanga walikuwa wanavaa nguo hizo za magunia kuonyesha hali ya maombolezo, kuonyeshwa kuguswa na tatizo hilo, na kwamba wapo katika huzuni na si furaha..

Mfano wa hao ni Rispa aliyeomboleza baada ya kufiwa na wanawe.

2Wafalme 21:10 “Naye Rispa, binti Aya, akatwaa nguo ya magunia akajitandikia mwambani, tangu mwanzo wa mavuno hata waliponyeshewa mvua toka mbinguni; wala hakuacha ndege wa angani kukaa juu yao mchana, wala wanyama wa mwitu usiku”

Tunaona mfano mwingine ni wana wa Israeli, baada ya kupata msiba wa kupelekwa utumwani..biblia inasema iliwapasa wavae mavazi ya magunia kwa maombolezo..

Yeremia 4: 8 “Kwa sababu hiyo jifungeni NGUO ZA MAGUNIA; ombolezeni na kulia kwa uchungu; kwa maana hasira kali ya Bwana haikugeuka na kutuacha”

Yeremia 6:26 “Ee binti wa watu wangu, ujivike NGUO YA MAGUNIA, na kugaagaa katika majivu; fanya maombolezo, kama maombolezo kwa ajili ya mwana wa pekee, maombolezo ya uchungu mwingi; maana mwenye kuteka nyara atakuja juu yetu ghafula”.

Mifano mingine watu waliovaa mavazi ya magunia, kuashiria maombolezo unaweza kuisoma katika mistari ifuatayo (2Wafalme 6:30, 2Wafalme 19:1)

        2. Toba

Watu pia walipotaka kujisongeza mbele za Mungu, kwa toba..walivaa nguo za magunia, kuashiria hali ya unyenyekevu, na kujishusha, kwamba wao si kitu mbele ya Mungu mkuu, na hivyo kutaka rehema kutoka kwake. Mfano wa watu hao ni nabii Danieli.

Danieli 9:3 “Nikamwelekezea Bwana Mungu uso wangu, ili kutaka kwa maombi, na dua, pamoja na kufunga, na KUVAA NGUO ZA MAGUNIA na majivu.

4 Nikamwomba Bwana, Mungu wangu, nikaungama, nikasema, Ee Bwana, Mungu mkuu, mwenye kutisha, ashikaye maagano na rehema kwao wampendao, na kuzishika amri zake”

Na mfano mwingine ni watu wa Ninawi..

Yona 3: 5 “Basi watu wa Ninawi wakamsadiki Mungu; wakatangaza kufunga, WAKAJIVIKA NGUO ZA MAGUNIA, tangu yeye aliye mkubwa hata aliye mdogo.

6 Habari ikamfikia mfalme wa Ninawi, naye akaondoka katika kiti chake cha enzi, AKAVUA VAZI LAKE, AKAJIVIKA NGUO ZA MAGUNIA, na kuketi katika majivu”

Na wengine mfano wa hao, unaweza kuwasoma katika mistari ifuatayo (2Wafalme 19:1, Nehemia 9:1).

Je wakristo sasa Nasi pia tunapaswa kuvaa mavazi ya magunia pindi tunapotubu kwa Mungu wetu au tunapomboleza pindi tunapopitia na misiba?.

Huo ni uchaguzi wa mtu avae au asivae. Lakini biblia haijatoa amri kwamba lazima mtu avae magunia anapotubu.. Ilichotia msisitizo ni hichi..

Yoeli 2:12 “Lakini hata sasa, asema Bwana, nirudieni mimi kwa mioyo yenu yote, na kwa kufunga, na kwa kulia, na kwa kuombolea;

13 RARUENI MIOYO YENU, WALA SI MAVAZI YENU, MKAMRUDIE BWANA, Mungu wenu; kwa maana yeye ndiye mwenye neema, amejaa huruma; si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa rehema, naye hughairi mabaya”

Hapo inasema turarue mioyo yetu na si mavazi yetu…Kumbuka mavazi yanayozungumziwa hapo ndio hayo ya magunia, na si vile vimini, au mavazi yasiyo ya heshima yanayovaliwa na wadada. Hayo mtu anapookoka hapaswi kabisa kuendelea kuyavaa.

Je umeurarua moyo wako kwa Bwana? Kama bado Ni vyema ukafanya hivyo mapema

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618.

Jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

MAVAZI YA NDANI NA YA NJE.

MAVAZI YAPASAYO.

JE KUVAA PETE NI DHAMBI?

MWANAMKE ULIYEKOMAA KI-UMRI, ITAMBUE HUDUMA YAKO.

JE! UNAYATUNZA MAVAZI YAKO?

Rudi Nyumbani:

Print this post

TUMEPEWA AMRI YA KUKANYAGA NGE NA NYOKA.

Jina la Bwana wetu Yesu libarikiwe. Unapomkiri Yesu kwa Kinywa, au unapojisalimisha kwa Yesu, kwa kudhamiria kabisa, dakika hiyo hiyo..Shetani anaangushwa juu yako, kama umeme…Na anawekwa chini ya miguu yako na unakabidhiwa mamlaka, juu yake.

Luka 10: 18  “Akawaambia, Nilimwona Shetani, akianguka kutoka mbinguni KAMA UMEME.

19  Tazama, NIMEWAPA AMRI YA KUKANYAGA NYOKA NA NGE, NA NGUVU ZOTE ZA YULE ADUI, wala hakuna kitu kitakachowadhuru”

Hapo kuna vitu vitatu ambavyo unapewa amri juu ya hivyo.

Amri ya kukanyaga NYOKA. 2). amri ya kukanyaga NGE na 3). amri ya kukanyaga NGUVU ZOTE ZA YULE ADUI.

  • 1. Amri ya kukanyaga Nyoka

Nyoka ni kiumbe anayeuma (au anayeng’ata kwa kutumia mdomo)..Silaha yake kubwa ni mdomo na mate yake, hana silaha nyingine kiasi kwamba ukikibana kile kichwa hakuna atakachoweza kufanya ili kukudhuru. Nyoka ni mfano wa Watu wanaotumika na shetani, kwa kujua au kwa kutokujua kukudhuru wewe kupitia maneno wanayoyazungumza…Yaani kwaufupi silaha yao ni maneno..

Zaburi 143:1 “Ee Bwana, uniokoe na mtu mbaya, Unihifadhi na mtu wa jeuri.

2 Waliowaza mabaya mioyoni mwao, Kila siku huondokesha vita.

3 Wamenoa ndimi zao kama nyoka, Sumu ya fira i chini ya midomo yao”

kobra

Fira ni nyoka aina ya KOBRA, Sasa hao Biblia imesema tumepewa amri juu yao..”kuwakanyaga”…Sasa hatuwakanyagi na sisi kwa kuwarudishia maneno.. Hapana, tukifanya hivyo na sisi tutakuwa ni nyoka kama hao. Lakini tunakanyaga vichwa kwa kuyapuuza maneno yale, na kuyazuia yasiingie moyoni mwetu..

Kwasababu ukiyaruhusu yaingie moyoni mwako, yatakuwa sumu kwako na yatakudhuru.. Hivyo unayapuuzia yale maneno na kuyapiga mateke, hiyo ni silaha kubwa sana..Ambayo kwa hiyo utaweza kuwakanyaga nyoka wote.. (Kumbuka nyoka hapo ni lugha ya rohoni, usimwite kamwe ndugu yako nyoka hata kama ni mbaya kiasi gani kwako).

  • 2. Amri ya kukanyaga NGE.

Nge ni mdudu anayeuma kwa kutumia MKIA, na si Mdomo kama nyoka. Hawa ni jamii ya watu ambao wanatumika na shetani pasipo kujua au kwa kujua. Ambao kwa mbele ni wazuri lakini kwa nyuma wanatumia mkia kukudhuru,  na kama unavyojua mkia wa nge, umepanga juu ukazunguka lengo lake ni kukuchoma wewe kwa nyuma, pasipo kujua ni nani kakudhuru.

Hivyo shetani anaweza kutumia watu wanaoonekana ni wazuri kwa nje lakini kumbe ni wenye madhara juu yako, watu wa namna hiyo tumepewa amri ya kuwakanyaga..Hatuwakanyagi kwa kuwachukia wala kufanya nao vita bila wao kujijua, tukifanya hivyo na sisi tutakuwa nge, ambao hatungati kwa mdomo lakini tunang’ata kwa mkia..Hivyo na hawa tumepewa silaha ya kushughulika nao, na hiyo si nyingine Zaidi ya MIGUU YETU, Maana yake kutotafuta tafuta wanachokiwaza juu yetu wala kukifikiri juu yako wanatuwazia nini, maana yake wewe unasonga mbele, hufuatilii wewe unaendelea mbele na mambo yako unayoyafanya.

Kama vile watu wanavyolikanyaga neno la Mungu chini, maana yake ni kwamba wanalipuuzia, wanaendelea na mambo yao,  vivyo hivyo na wewe unakanyaga maneno yao, au hila zao…kwa kuzipuuzia, na kwajinsi unavyozidi kuzipuuza ndivyo zinavyozidi kuishiwa nguvu, kwasababu utakuwa umempa Mungu nafasi kubwa ya kukupigania, na mwisho wa siku watatubu na kushawishika kumwamini Mungu wako, na utakuwa umeokoa roho zao.

  • 3. Amri ya kukanyaga nguvu zote za yule mwovu.

Kipengele hicho ndio cha mwisho na cha Muhimu sana..Ambacho shetani hataki watu wakijue wala wakielewe, kwasababu kinamhusu yeye mwenyewe na mapepo yake, na wala hakiwahusu watu anaowatumia..

Shetani anapenda kuwaaminisha watu kuwa yeye ana nguvu sana, na hivyo akishika mahali ni ngumu yeye kutolewa..Hivyo watu wengi wamefungwa na nguvu za Ibilisi kwa muda mrefu kwasababu tu ya Imani hiyo ndani yao.  Utakuta mtu anaumwa, au anapitia tatizo Fulani, na lile tatizo ndani yake kashalikuza na kuwa kubwa mno, na kuamini kuwa inahitajika nguvu nyingi sana za rohoni kuliondoa, au  upako mwingi kuliondoa..Wengine wanatokewa kabisa na mapepo wazi, wangine yanawajia katika ndoto, wengine wananyanyaswa na mashetani usiku, kiasi kwamba hata wanaogopa kulala wenyewe. Wengine wanatishiwa na kusumbuliwa na shetani kwa namna ambayo hata wanashindwa kusimulia, mwisho wa siku wanakata tamaa hata ya kuishi. Na kundi hili lipo kubwa sana.

Sasa watu kama hawa, shetani amewashika kwa kutumia Imani yao kupata nafasi ya kuwatesa.

Biblia inasema hapo, tumepewa Amri ya KUKANYAGA… Unaelewa maana ya kukanyaga???…Kukanyaga maana yake ni KULIPOTEZEA JAMBO!!..Kulishusha hadhi, kulipunguza nguvu, kuliabisha, kulidhalilisha, kulidharau. Hiyo ndio maana ya kukanyaga, wala kukanyaga sio kuingia kwenye maombi ya mifungo ya masafa, hapana hiyo sio maana yake.. Maana yake ni kuliweka chini yako jambo. Kama tu vile watu wanavyolikanyaga chini neno la Mungu, wanafanya hivyo kwa kulidharau…Kitendo cha kukidharau kitu tayari umekikanyaga chini.

Waebrania 10.28 “Mtu aliyeidharau sheria ya Musa hufa pasipo huruma, kwa neno la mashahidi wawili au watatu.

29 Mwaonaje? Haikumpasa adhabu iliyo kubwa zaidi mtu yule aliyemkanyaga Mwana wa Mungu, na kuihesabu damu ya agano aliyotakaswa kwayo kuwa ni kitu ovyo, na kumfanyia jeuri Roho wa neema?”

Umeona hapo?. Watu wote wanaoihesabia damu ya agano la Yesu kuwa ni kitu ovyo, na kumdharau (au kwa lugha ya sasa, ni kuipotezea), watu hao ndio wanahesabika kama wamemkanyaga Mwana wa Adamu.

Ni hivyo hivyo, mtu anayehesabia kazi za shetani kuwa ni kitu ovyo, hapo anakuwa amemkanyaga chini, ya miguu yake.

Hivyo kwa silaha ile ile tunayotumia kukanyaga nyoka na nge, ndiyo hiyo hiyo tunayotumia KUZIKANYAGA NGUVU ZOTE ZA YULE ADUI. Wala hakuna silaha nyingine, shetani asikuogopeshe ikiwa upo tayari ndani ya Kristo..

Maana yake ni hii.

Baada ya kumkiri Yesu, kama ulikuwa unaumwa na kuamini kwamba ni ngumu kupona ugonjwa ulio nao, HILO wazo unaanza kulidharau ndani yako, kuanzia sasa (unalikanyaga!)..

> Shetani alikuwa amekutishia kwamba dhambi yako haisameheki, unalidharau hilo wazo, na kulipoteza kwenye akili yako..

> Mapepo yalikuwa yanakuhubiria kwamba utakufa kila siku kwenye mawazo yako, unayapotezea hayo mawazo na kuyadharau, na kusema hilo halipo..kwa jinsi unavyozidi kuyashusha hadhi hayo mawazo ya shetani, na uongo wake huo…ndivyo na yenyewe yanavyozidi kukosa nguvu juu yako na hatimaye kupotea kabisa.

> Maroho yalikuwa yanakukaba usiku, Hizo sauti zinazokuambia kwamba  yatarudi tena huzitilii maanani..acha kabisa kuyapa hayo mapepo heshima kubwa kiasi hicho!, yashushe hadhi..

> Mandoto ya ajabu ajabu shetani alikuwa anakutumia, anza kuyapotezea wala usiyatafakari tafakari, wala usitafute kujua maana zake, yaache yapite…yakanyage chini!.. usiyakuze, kwenye kichwa chako kana kwamba ni kitu cha muhimu sana.

> Mawazo shetani anayokuletea kwamba mapepo yatakudhuru, hayo mawaza anza kuacha kuyawaza, yakanyage chini, badala yake huo muda tumia kutafakari mambo mengine, tumia kutafakari Maneno ya Mungu, hapo utakuwa unammaliza nguvu shetani kwa kasi sana..Maana shetani kazi yake ni kukutisha wewe ili uanze kumfikiria yeye na kumkuza kwenye akili yako, ndipo apate nguvu juu yako..sasa wewe nenda kinyume naye.

>Shetani alikuwa amekuaminisha kwamba ni lazima kila siku aje akutese, yakatae hayo mawazo, wala usiyatafakari, tena yasahau kabisa kwenye kichwa chako, na wala usipate ratiba ya kufikiri jinsi anavyokutesaga..kwa jinsi unavyozidi kumpotezea, naye anapotea..

Kwasababu Miguu yetu ni silaha kubwa na ina nguvu kuliko vichwa vya nyoka, ina nguvu kuliko mikia ya nge, na ina nguvu kuliko nguvu za adui shetani.

Likumbuke hili neno..Luka 10: 18  “Akawaambia, Nilimwona Shetani, akianguka kutoka mbinguni KAMA UMEME. 19  Tazama, NIMEWAPA AMRI YA KUKANYAGA NYOKA NA NGE, NA NGUVU ZOTE ZA YULE ADUI, wala hakuna kitu kitakachowadhuru”

Bwana akubariki.

Kama hujaokoka kumbuka hizi ni siku za mwisho na Yesu anakaribia kurudi, biblia inasema itatufaidia nini tukiupata ulimwengu mzima na kupata hasara za nafsi zetu?..Tafakari neno hilo kwa makini, hivyo kama utaamua leo kumpa Kristo Maisha yako, utakuwa umefanya jambo la busara sana, ambalo hutakaa ujutia katika maisha yako, hivyo kwa msaada Zaidi na maombezi fungua hapa >> SALA YA TOBA.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618.

Jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

MKUU WA UZIMA AKUWEKE HURU.

SALA YA UPONYAJI/MAOMBI YA UPONYAJI.

UPONYAJI WA ASILI

KWA KUPIGWA KWAKE SISI TUMEPONA.

WEWE NI BWANA UNIPONYAYE.

Rudi Nyumbani:

Print this post