Mauti ya pili ni nini?.. Ni mauti inayofuata baada ya hii mauti ya kwanza…Mauti ya kwanza ni pale roho ya Uhai inapoutoka mwili..Yaani pale tu Roho inapotengana na mwili hiyo ndiyo mauti ya kwanza. Lakini mauti ya pili ni roho kujitenga na nafsi.
Mauti ya kwanza inaweza kusababishwa na mambo mbali mbali..Inaweza kusababishwa na aidha ugonjwa fulani, au ajali fulani ambayo mtu anaweza kuipata…Lakini pia inaweza isisababishwe na ajali wala ugonjwa ikasababishwa na jambo lingine…
Hivyo mtu anapokufa katika hii mauti ya kwanza..(Yaani roho inapotengana na mwili)..Mtu huyo mwili wake unakwenda kuzikwa kaburini, unaoza na kuliwa na funza na kuwa mavumbi…lakini nafsi yake na roho yake zinakuwa hazijafa hivyo zinakwenda mahali pa wafu…
Mahali pa wafu nako kumegawanyika katika sehemu mbili..Sehemu ya kwanza ni mahali ambapo wafu waliokufa katika Kristo wanahifadhiwa..ambapo kwa lugha nyingine panaitwa peponi au paradiso..ni mahali pa raha sana na hapana mateso…
Na sehemu ya pili ni mahali panapojulikana kama KUZIMU au Jehanamu..ni mahali ambapo roho za wanadamu wote waliokufa katika dhambi zinahifadhiwa kwa muda..ni sehemu ya mateso mabaya sana.
Siku ya unyakuo itakapofika roho zilizohifadhiwa paradiso zitafufuliwa na kupewa miili ya utukufu na kwenda mawinguni na Bwana Yesu…lakini zilizosalia ambazo zipo kuzimu..siku ya hukumu zitafufuliwa nazo na kuhukumiwa kila mmoja sawasawa na matendo yake.
Yohana 5:28 “Msistaajabie maneno hayo; kwa maana saa yaja, ambayo watu wote waliomo makaburini wataisikia sauti yake.
29 Nao watatoka; wale waliofanya mema kwa ufufuo wa uzima, na wale waliotenda mabaya kwa ufufuo wa hukumu”.
Sasa roho hizi ambazo zilikuwa zipo jehanamu/kuzimu baada ya kuhukumiwa….zitakusanywa zote na kutupwa katika ziwa la moto..Ziwa la moto ni tofauti na jehanamu…Na zitaungua huko kwa muda mrefu sana…Zilizofanya maovu sana kuliko nyingine zitaungua kwa muda mrefu…na zilizofanya machache zitaungua kwa muda pungufu kidogo wa hizo nyingine…
Baada ya kipindi kirefu sana kisichoelezeka cha mateso ndani ya ziwa la moto hatimaye roho zote zilizotupwa katika ziwa la moto zitakufa..Atakayekufa wa mwisho katika jehanamu ya moto atakuwa ni shetani huyo ndiye mwenye adhabu kubwa kuliko wote..wakifuatiwa na mapepo wake, wakifuatiwa na wachungaji na waaalimu wa uongo na manabii wa uongo..na mwisho watu wengine waovu waliosalia kila mmoja kulingana na uovu alioufanya..Hiyo ndio itakuwa MAUTI YA PILI, yaani kifo katika ziwa la moto..Roho kutenganishwa na nafsi.
Ufunuo 20:12 “Nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wamesimama mbele ya hicho kiti cha enzi; na vitabu vikafunguliwa; na kitabu kingine kikafunguliwa, ambacho ni cha uzima; na hao wafu wakahukumiwa katika mambo hayo yaliyoandikwa katika vile vitabu, sawasawa na matendo yao.
13 Bahari ikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake; na Mauti na Kuzimu zikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake. Wakahukumiwa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake.
14 Mauti na Kuzimu zikatupwa katika lile ziwa la moto. Hii ndiyo mauti ya pili, yaani, hilo ziwa la moto.
15 Na iwapo mtu ye yote hakuonekana ameandikwa katika kitabu cha uzima, alitupwa katika lile ziwa la moto”.
Inajulikana na wengi kwamba ziwa la moto ni la milele lakini kiuhalisia sio la milele…Milele ilivyotumika katika kitabu cha ufunuo ni Everlasting…Yaani maana yake “kudumu muda mrefu” na si “eternal” ambayo maana yake ni milele…
Sasa kama mtu atakuwepo kuzimu milele tayari maana yake anao uzima wa milele…kitu ambacho sio kweli…Mwenye uzima wa milele ni Mungu tu..Na wana wa Mungu waliookolewa hao ndio watakaopata uzima wa milele..(yaani wataishi milele) Lakini roho zote zilizoasi zitakufa!. Biblia inasema hivyo..hata shetani naye pia atakufa…hana uzima wa milele.
Hivyo tofauti na wengi wanadhani kwamba adhabu kuu atakayoipata mwanadamu aliyeasi ni kuchomwa moto kuzimu…La! Hiyo sio adhabu…Adhabu kubwa au pigo kubwa hasa ni kuupoteza uzima wa milele..Yaani kufa na kutoweka kana kwamba hujawahi kuwepo kabisa…Na kifo hicho ni katika ziwa la moto. Hebu tafakari unakuwa haupo!
Hivyo Uzima sio kitu cha kufanyia mchezo kabisa…Tukose kila kitu lakini si uzima wa milele. Na uzima huu unapatikana kwa Yesu Kristo mwenyewe…Hivyo kama hujaokoka..mlango upo wazi sasa ila hautakuwa hivi siku zote..Tubu kwa kudhamiria kuacha kabisa dhambi, na kisha kabatizwe katika ubatizo sahihi ambao ni wa maji mengi na kwa jina la Yesu kama hujabatizwa. Na Roho Mtakatifu atakuongoza katika kweli yote na kukusaidia katika kuishi maisha masafi yanayompendeza Mungu.
Lakini kama usipotubu na kuipenda dunia..na kuendelea kuwa mlevi, mzinzi, mwasherati, mwizi, msengenyaji, mwongo, muuaji, mchawi, mla rushwa na mtoaji mimba…Biblia imeweka wazi sehemu ya watu wa namna hiyo ni ziwa la moto (Hivyo mauti ya pili ni nini?)
unapozungumzia ziwa la moto maana yake ni mauti ya pili.
Ufunuo 21:8 “Bali waoga, na wasioamini, na wachukizao, na wauaji, na wazinzi, na wachawi, na hao waabuduo sanamu, na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili”.
Bwana atusaidie. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Tafadhali share na wengine na Bwana azidi kukubairiki.
Mada Nyinginezo:
HATARI YA KUHUBIRI INJILI TOFAUTI NA ILIYOANDIKWA KWENYE BIBLIA.
Nguvu iliyopo katika maamuzi.
Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe. Karibu tujikumbushe Biblia…
Leo kwa Neema za Bwana tutajikumbusha mambo ambayo tulishawahi kujifunza huko nyuma..Kwasababu biblia inatufundisha hivyo katika 2Petro 1:12-13, 2Petro 3:1-2, na 1Wakorintho 4:17.
Na leo tutajikumbusha jambo muhimu sana ambalo linatutatiza wengi…Na hilo si lingine Zaidi ya nguvu iliyopo katika maamuzi.
Nguvu za Mungu haziwezi kuzidi maamuzi yetu sisi…Tunapomtumikia Mungu hatumtumikii kama maroboti kwamba maroboti yanakuwa hayajitambui lakini yanapelekwa tu mahali ambapo yule anayetaka kuyapeleka yawepo…Maroboti hayana maamuzi
Lakini sisi Mungu wetu hakutuumba hivyo wala hatutumikishi hivyo…Ametuumbia jambo linaloitwa maamuzi, na hivyo yeye au kiumbe chochote hakiwezi kuingilia maamuzi yetu…hata shetani hawezi!!…Sio kwamba hawezi kutufanya kuwa kama maroboti hapana uwezo huo anao…lakini hajapenda kutufanya hivyo..
Kwahiyo Mungu anapomvuta mtu kwake, ambaye amemkusudia uzima wa milele..anachofanya ni kumshawishi kwa kumpa kila sababu ya yeye kutubu…Anamfumbua macho na kuona hali aliyopo kwamba anakwenda kupotea kama asipochukua hatua hii au ile..Ni kama mtu mwingine wa pili yupo pembeni yake..anamshawishi afanye maamuzi Fulani…na endapo akikubali anakuwa anajiungamanisha na yule mtu…Lakini Roho Mtakatifu hafikii hatua ya kumteka mtu na kumfanya mateka..
Wengi wanaomba Mungu awazuie wasifanye uasherati kwa lazima…Hicho kitu hakipo!..Roho Mtakatifu ni msaidizi sio mfanyaji…Wafanyaji ni sisi, yeye ni msaidizi tu…Unapomfuata Kristo unatakiwa kwanza wewe binafsi kuutii ushauri wa Roho Mtakatifu wa kuacha uasherati…Ukishaamua wewe kutii kwa kuacha yeye anakuja hapo kukusaidia…Kwahiyo ukichukua maamuzi yako ukajumlisha na msaada wake..Hapo kamwe uasherati hautakushinda….
Kadhalika huwezi kumwomba Mungu akuachishe pombe au sigara kwa lazima…Kwamba utokee tu umeacha sigara au umeacha pombe…Nataka nikuambie Roho Mtakatifu hatendi kazi namna hiyo…Kama unataka kuacha pombe ambazo zimekufanya mtumwa kwa muda mrefu…Hatua ya kwanza ni wewe kumtii Roho Mtakatifu ambaye yupo pembeni yako anayekuambia uache pombe….hivyo mtii kwa kwenda kuvunja hizo chupa za bia zilizopo nyumbani kwako…kwa kuacha kwenda Bar, kwa kuacha kutembea na kampani za wanywaji pombe na kwa kuacha kabisa kunywa pombe…Ukishaamua kwa vitendo kama hivyo…
Basi yule msaidizi aliyeko pembeni yako, anakusaidia kushinda tamaa ya kunywa tena pombe anakuongezea nguvu …Lakini usipoamua…Miaka na miaka itapita utabakia hivyo hivyo,..utahudhuria kanisani, utawekewa mikono na kila aina ya mtumishi, lakini hakuna kitakachotokea.
Ni kwanini?..Ni kwasababu Nguvu za Roho Mtakatifu haziwezi zikazidi nguvu za maamuzi yako.
Na ndio maana Bwana Yesu anajulikana pia kama Mshauri wa Ajabu..
Isaya 9:6 “Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume; Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani”.
Mshauri ni mtu ambaye haingilii maamuzi yako lakini yupo karibu sana na mawazo yako kuyaboresha.
Kadhalika na uongo mwingine uliozagaa kila mahali ni wa watu kutenda dhambi na kusema ni shetani kawapitia…Ndugu usidanganyike hata kidogo kwa uongo huo!
Mtu anayekwenda kuzini..shetani hajampitia….kilichofanyika katika ulimwengu wa roho ni roho za mashetani zilitumwa kwa huyo mtu kumshawishi na kumpa kila sababu ya yeye kwenda kufanya uasherati…Ni kama mtu mwingine wa pembeni tena anamshawishi akafanye uasherati..atamkumbusha picha za ngono alizowahi kuziangalia, atamkumbusha uasherati wa mwisho aliowahi kuufanya na yule mtu atajaa tamaa na hivyo kwa maamuzi yake mwenyewe atanyanyuka na kwenda kutafuta kufanya kile kitendo…
Sasa huyo mtu hajashikwa na kufungwa na kupelekwa kwa lazima kufanya uasherati..la! bali kutokana na nguvu ya ushawishi iliyomshawishi na kuitii kwa hiari yake mwenyewe kaenda kufanya alichokifanya…Sasa huyu anaweza kujifariji ni shetani lakini hajui kwamba ni yeye ndiye kaamua kwenda kufanya..laiti angekataa kile kitu katika mawazo yake kamwe shetani asingeweza kumlazimisha…Kwasababu hakuna kiumbe chochote kilichoumbwa kinachoweza kuzidi maamuzi ya mtu!.nguvu iliyopo katika maamuzi ni kubwa sana.
Hivyo ndugu kama ulikuwa umekaa kwa muda mrefu huwezi kuacha kufanya masturbation..na ulikuwa unaamini kwamba ipo siku moja tu itatokea miujiza Mungu atakushukia na utaacha…nataka nikuambie ukweli…utasubiri hiyo siku miaka na miaka na haitafika!!!…Unachotakiwa kufanya ni leo leo kuamua kusema ninatubu dhambi zangu na kusema NIMEACHA!..na unaambatanisha vitendo juu yake kama dalili ya Imani yako…unafuta picha zote za ngono kwenye simu yako..unayazuia mawazo ya uasherati yajapo kichwani unayakataa..unakaa mbali na kitu chochote ambacho unajua ukikaa nacho dakika chache kitakupeleka katika mawazo ya uasherati…
Makala za kizinzi unaacha kuzisoma…magroup ya kizinzi unajiondoa, na ukikutana hata na post yoyote yenye maudhui ya kiuasherati unairuka huisomi…Vitabu na magazeti ya kiasherati unaacha kuyasoma…kuna magazeti ambayo kwa nje yanaonekana ni magazeti ya kimaadili ya kupunguza zinaa lakini ndani yake ndiyo yanayochochea zinaa kwa kasi kubwa…yana roho za usherati! Hivyo sio ya kusoma kabisa..mada mada na vikao vya mizaha unajitenga navyo…hata ukizungumza na mtu ukiona anaanza kwenda kwenye mada hizo unazikatisha…Lakini ukijiachia na kuendelea kusoma hayo magazeti, na Makala, na posti za mapenzi na magroup ya kiuasherati…pamoja na movie na matamthilia ya kidunia yenye maudhui ya mapenzi…na huku unaamini kwamba siku moja nguvu za Roho Mtakatifu zitakushukia na kukuteka na utajikuta tu umeacha kwa lazima…nataka nikuambie usiangamie kwa kukosa maarifa!!..hiyo siku haitafika.
Walioacha hawakuacha kwa njia hiyo…walimtii Mungu kwanza ambaye anaugua ndani yao kuhusu dhambi zao..na baada ya kumtii wakaamua kuacha kwa vitendo..ikiwemo kujitenga na vishawishi vyote vya kiuasherati…Huko ndiko kujikana nafsi…Na mambo mengine yote ni hivyo hivyo..ukitaka kuacha usengenyaji ni hivyo hivyo, ukitaka kuacha wizi ni hivyo hivyo…ukitaka kuacha uchawi ni hivyo hivyo…unaamua kwanza binafsi kuacha na unakwenda kuchoma vibuyu vyote ulivyonavyo..na kufuta namba za waganga wa kienyeji..na kampani za marafiki wanaohudhuria huko.
Na baada ya kufanya hayo yote…Hakikisha unakwenda kukamilisha hatua za wokovu ikiwemo kubatizwa, kufanya ushirika na waaminio wenzako, na kudumu katika kujifunza Neno la Mungu kila siku.
Bwana akubariki sana.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789 001 312 jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?
SIKUJA KULETA AMANI DUNIANI, BALI MAFARAKANO.
ROHO HUTUOMBEA KWA KUUGUA KUSIKOWEZA KUTAMKWA!
BONDE LA KUKATA MANENO.
Ubatizo wa moto ni upi?
Roho, Nafsi, na Mwili, Je! vina tofauti gani?
JIBU: Mwanadamu ameumbwa katika pande kuu mbili, Upande wa kwanza unajulikana kama utu wa ndani, na upande wa pili unajulikana kama utu wa nje.
Utu wa nje ndio huu mwili wetu, ambao unaona, unahisi, unasikia, unatembea, unalala, unakula, unatamani n.k. Yaani kwa ufupi utu huu wa nje (yaani miili yetu) imeumbwa kwa lengo la kutimiza matakwa yote ya hapa duniani.
Lakini utu wa ndani, kidogo ni mpana kuulewa tofauti na huu wa nje, kwani wenyewe haujaumbwa na kitu kimoja, bali umeumbwa na mambo makuu mawili, la kwanza ni nafsi na la pili ni roho.. Hapa ndipo watu wengi wanapochanganyikiwa namna ya kuvitofautisha vitu hivi viwili.
Ukweli ni kwamba vitu hivi viwili vimeshikana sana, kiasi kwamba hata katika biblia sehemu nyingi, inataja nafsi na sehemu nyingine roho, unashindwa kuelewa ni kipi kinacholengwa hasaa hapo?.
Tunapaswa tujue kuwa Mungu amevishikamanisha hivi vitu viwili kwa pamoja kwa makusudi kabisa kiasi kwamba vionekane kama ni kitu kimoja, lakini kiuhalisi nafsi na roho ni vitu viwili tofauti..Ni sawa na mtu achukie rangi ya blue, kisha aichanganye na rangi ya njano..Matokeo yake hapo kama wewe ulishawahi kufanya stadi za kazi unaelewa ni nini kinatokea, hapo kinachozaliwa ni rangi ya Kijani..
Sasa mtu akikuambia uchukue rangi ya kijani halafu utoe rangu ya blue ndani yake, au rangi ya njano ndani yake, ni jambo ambalo haliwezekani, au kama linawekezana basi ni gumu sana kulifanya.
Ndivyo ilivyo kwa nafsi na roho, vimeshikamanishwa pamoja, kiasi kwamba hakuna mtu awezaye kuvitenganisha isipokuwa Neno la Mungu peke yake, mwanadamu hawezi, shetani hawezi, wala kiumbe kingine chochote..
Webrania 4:12 “Maana Neno la Mungu li hai, tena lina nguvu, tena lina ukali kuliko upanga uwao wote ukatao kuwili, tena lachoma hata kuzigawanya nafsi na roho, na viungo na mafuta yaliyomo ndani yake; tena li jepesi kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo.
13 Wala hakuna kiumbe kisichokuwa wazi mbele zake, lakini vitu vyote vi utupu na kufunuliwa machoni pake yeye aliye na mambo yetu”.
Unaona hapo? Biblia inasema Neno la Mungu pekee, ndio linaloweza kuchoma hata kuzigawa nafsi na roho..Upo ufunuo mkubwa sana hapo? .Usitamani siku ile nafsi yako nafsi yako itengwe na roho yako,..ni maumivu makali sana ndani utakayoyasikia, ukitambua kuwa ndio mwisho wako umefika, kwamba hutakaa uwepo milele..
Mwanadamu au shetani au kiumbe chochote kinaouwezo wa kuutenganisha “utu” wa mtu wa nje, na ule wa ndani, kwa kufanya jambo jepesi la kumuua tu!, .lakini kuutenganisha ule utu wa ndani yaani nafsi yake na roho yake.. hakuna mtu yeyote anayeweza kufanya hivyo isipokuwa ni Mungu peke yake..
Mathayo 10:28 “Msiwaogope wauuao mwili, wasiweze kuiua na roho; afadhali mwogopeni yule awezaye kuangamiza mwili na roho pia katika jehanum”.
Tukisoma, Mwanzo pale anasema:
Mwanzo 2:7 “Bwana Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai”
Jiulize ni kwanini haijasema,.. “mtu akawa mwili hai” badala yake ikasema mtu akawa nafsi hai?. Hiyo ni kuonyesha kuwa pumzi ya uhai iliyotoka kwa Mungu iliingia ndani ya nafsi ambayo ilikuwa tayari imeshaumbwa ukisoma Mwanzo 1:27 utaona hilo …Ilipopokea pumzi hiyo ndipo ikawa nafsi hai.
Sasa pumzi ya uhai inayozungumziwa hapo ndio roho yenyewe..Ambayo inatoka kwa Mungu. Hivyo Roho ya uhai inayotoka kwa Mungu ikikutana na nafsi ambayo Mungu aliumba inamtengeneza mtu wa ndani aliye hai.
Ni sawa na unavyochanganya zile rangi mbili, ya blue na njano, kama tulivyoona hapo juu kutengeneza kijani..Sasa hichi kijani chenyewe ndio mtu wa Ndani.
Hivyo unaposoma biblia sehemu nyingine utaona inazungumzia roho, sehemu nyingine inasema, nafsi, sehemu nyingine inasema moyo, usichanganyikiwe..Fahamu kuwa inazungumzia kitu kile kile kimoja kinachomlenga huyu mtu wa Ndani. Japo ni vitu viwili tofuati.
Kwahiyo hii nafsi ndio mtu mwenyewe na ndio imebeba taarifa zote Mungu alizomuumbia mwanadamu ndani yake, kwa mfano wa Mungu, yaani upendo, furaha, sifa, wivu, ibada, utu wema n.k.. vyote hivyo vinatoka ndani ya nafsi ya mtu.
Kwahiyo ili vyote viweze kufanya kazi vilihitaji uhai ndani yake..na uhai huo ndio roho ya mtu..Ni sawa na balbu..ili iweze kuwaka na kutoa mwanga, inahitaji umeme ndani yake..Hivyo nafsi pia ili iwe hai na kuonyesha tabia zote za ki-Mungu ndani yake ilihitaji roho yenye pumzi ya Mungu ndani yake.
Hiyo ndio tofauti kati ya Roho Nafsi na Mwili..
Hivyo uulinde sana moyo wako kuliko kitu kingine chochote kama biblia inavyosema kwasababu huko ndipo zinapotoka chemchemi za maji ya uzima (Mithali 4:23).
Mhubiri 12:1 ‘Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako, Kabla hazijaja siku zilizo mbaya, Wala haijakaribia miaka utakaposema, Mimi sina furaha katika hiyo…’
6 Kabla haijakatika kamba ya fedha; Au kuvunjwa bakuli la dhahabu; Au mtungi kuvunjika kisimani; Au gurudumu kuvunjika birikani;
7 Nayo mavumbi kuirudia nchi kama yalivyokuwa, NAYO ROHO KUMRUDIA MUNGU ALIYEITOA’.
Tubu dhambi zako kama hujatubu umgukie muumba wako aliyekupa roho ya uhai bure angali muda upo..Utafika wakati kwa maumivu makali pumzi ya uhai itaondolewa kwenye nafsi yako katika ziwa la moto na kupata mauti ya pili kama inavyozungumziwa katika kitabu cha Ufunuo 2:11 na Ufunuo 22:6 na 20:14.
Ubarikiwe. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Muhtasari wa maelezo haya kwa njia ya video unaweza kuyapata hapa chini.
[embedyt] https://www.youtube.com/watch?v=hiXs2a7Im2A[/embedyt]
Roho Nafsi na Mwili, humkamilisha mwanadamu.
Mada Nyinginezo:
KUTOKUIHUBIRI INJILI,KUNA MADHARA GANI?
JE! MTUMISHI KUTOKUWA NA FEDHA NI ISHARA KUWA KUNA TATIZO KATIKA IMANI YAKE?
KILEMBA CHA NEEMA, JE! UMEMVIKA MWANAO?
NAMNA YA KUITAMBUA SAUTI YA MUNGU INAPOZUNGUMZA NA WEWE
USIPOLITENDEA KAZI NENO LA MUNGU.
Je Kwa mwanaume ni sahihi kuoa mtu uliyemzidi umri?..Na kwa upande wa mwanamke ni sahihi kuolewa na mwanaume uliyemzidi umri? (kuolewa na wanaume vijana)..Je ndoa za jinsia moja ni ishara ya nini? je watu watakuwa wakioa na kuolewa katika siku za mwisho inamaanisha nini?
JIBU: Biblia haijaweka katazo lolote kwa mwanaume kuoa mwanamke aliyemzidi umri au kwa mwanamke kuolewa na mwanaume uliyemzidi umri. Lakini kilichokataza ni tamaa.
Katika hizi siku za mwisho..Biblia imetabiri kuongezeka kwa maasi..na moja ya maasi hayo ni kuongezeka kwa Tamaa..Na Tamaa kubwa inayoikabili ulimwenguni ni tama ya uasherati…nyingine ni tamaa ya mali na umaarufu. Lakini namba moja ni tamaa ya uasherati na ya mali inashika nafasi ya pili.
Nyakati hizi za mwisho biblia imetabiri kuwa watu watakuwa wakioa na kuolewa.
Luka 17:26 ”Na kama ilivyokuwa siku za Nuhu, ndivyo itakavyokuwa katika siku zake Mwana wa Adamu.
27 Walikuwa wakila na kunywa, walikuwa wakioa na kuolewa, hata siku ile Nuhu aliyoingia katika safina, gharika ikashuka ikawaangamiza wote”
Sasa kuoa au kuolewa sio kubaya…Lakini kuoa na kuolewa kunakozungumziwa hapo ambako ni kubaya na kwamba kutakuja kutokea katika siku za mwisho ni NDOA ZA JINSIA MOJA pamoja na NDOA ZA TAMAA ZA WATU KUOANA WALIOZIDIANA UMRI.
Siku hizi za mwisho ndoa za jinsia moja zinaongezeka kwa kasi hususani katika mataifa ya Magharibi hakuna tena hofu…
Kadhalika ndoa baina ya vijana wa kiume na wanawake wazee zinaongezeka kwa kasi kutokana na tamaa…wazee wanawatamani vijana na vijana wanawatamani wazee..Na hiyo ni kutokana na wanaume wazee kuwachoka wake zao walio wazee kama wao na kutamani mabinti vijana na hivyo kuwaacha wake zao na kwenda kutafuta mabinti vijana wa kuwaoa..ili watimize haja zao za tamaa za uasherati.
Vivyo hivyo wanawake wazee wanawachoka waume zao ambao ni wazee kama wao..na hivyo kuwaacha na kwenda kutafuta kuolewa na wanaume vijana kutimiza matakwa yao ya uasherati.
Kadhalika wanawake vijana wanatafuta kuolewa na wanaume wazee kwaajili ya kupata mali…Na vivyo hivyo vijana wa kiume wanatafuta kuoa wanawake wazee kwasababu ya kupata mali vile vile…Sasa machafuko kama haya ndiyo yasiyompendeza Mungu na ndiyo yaliyosababisha hata dunia ya kwanza ya akina Nuhu kugharikishwa na maji.
Hivyo kwa mtu yoyote anayetafuta kuoa au kuolewa na mtu aliyemzidi au aliye chini ya umri wake…kwa namna hiyo hapo juu..mtu huyo anafanya dhambi…Na hivyo anaangukia katika kundi la watu waovu waliotabiriwa kutokea katika siku za mwisho kwamba ‘watakuwa wakioa na kuolewa’.
Lakini kama si kwasababu hizo hapo juu bali ni kwasababu ya upendo basi sio dhambi kuoa au kuolewa na mtu aliyekuzidi umri au aliyepungufu ya umri wako..
La Muhimu na la kuzingatia ni kwamba huyo unayekwenda kumwoa au kuolewa naye..angalau asiwe rika la mwanao au la mzazi wako…Kwasababu ni ngumu sana kutokea mwanamume akampenda mtu wa rika la mama yake au bibi kizee..Wengi ni tamaa tu!..inakuwa ni roho nyingine inawasukuma kufanya hivyo..
Pia awe hana mume kabisa (yaani hajaolewa) au hajaoa..Kama alishaoa na ameachana na mwenziwe huyo hapaswi kuoa wala kuolewa..anapaswa arudiane na mkewe au mumewe. Pia awe ni mkristo, kwasababu ndoa yoyote inayohusisha watu wa imani mbili tofauti hiyo sio ndoa ya kimaandiko kabisa.
Bwana akubariki. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Tafadhali ‘share’ na wengine.
Mada Nyinginezo:
Kutokuihubiri injili, madhara yake ni yapi?
Shalom, Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe..Karibu tujifunze Biblia mtu wa Mungu…Leo tutajifunza mambo machache muhimu yahusuyo majukumu yetu ya kuihubiri Injili.
Injili maana yake ni “Habari njema”..Habari yoyote au ujumbe wowote unaoupeleka kwa mtu au watu ulio mwema huo tayari ni injili…Zipo Injili za aina nyingi duniani lakini ipo injili moja tu ya wokovu..Au kwa lugha nyingine inaitwa “Injili ya Msalaba”…Injili ya Msalaba inamhusu Yesu Kristo mwana wa Mungu aliyetumwa kuichukua dhambi ya ulimwengu..Hiyo inahusu wokovu wa mwanadamu ambaye alipotea dhambi. Na Kumbuka wanadamu wote walipotea dhambini hivyo injili hii inamuhusu kila mmoja wetu.
Sasa Baada ya Bwana Yesu kuondoka ilikuwa ni sharti injili ihubiriwe ulimwenguni kote kwa kila kiumbe, na kwamba kila mwanadamu lazima aisikie injili hiyo ya wokovu…Na kwa hiari yake mwenyewe achague UZIMA au MAUTI. Kwasababu hiyo basi akawaagiza mitume wake akawaambia..
Marko 13.9 “Nanyi jihadharini nafsi zenu; maana watawapeleka ninyi mabarazani; na katika masinagogi mtapigwa; nanyi mtachukuliwa mbele ya maliwali na wafalme kwa ajili yangu, kuwa ushuhuda kwao.
10 NA SHARTI INJILI IHUBIRIWE KWANZA KATIKA MATAIFA YOTE”.
Hapo anasema ni SHARTI!..Maana yake ni lazima injili ifike kila mahali..Kwa uzima na kifo, hata ikigharimu uhai ni lazima injili iwafikie watu..Hivyo hilo ni jukumu tulilopewa watu wote tuliompokea Kristo..Ni lazima tuihubiri Injili…Na siku zote Mungu anatumia watu kuhubiri Injili, kawachagua watu kusimama madhabahuni kumwakilisha…kamwe hatumii wanyama, wala malaika, wala kiumbe kingine chochote kamchagua mwanadamu tu!!..
Sasa kuna hatari kubwa sana ya kutokuihubiri injili…Kuna hatari kubwa sana ya kutokuitumia karama Mungu aliyokupa katika kuwahubiria wengine..Bwana amekuokoa wewe, ili na wewe ukawe msaada kwa wengine…hajatuokoa ili tu tufurahi sisi wenyewe..Kama tunavyojua wengi wetu hatujampokea Yesu kwa kutokewa na yeye…wengi wetu tumesikia injili ikihubiriwa mahali fulani na mtu Fulani wa Mungu ndipo kwa kupitia hayo mahubiri tukaokoka… Kutokuihubiri injili ni kosa kwa mtu anayeitwa mkristo.
Kadhalika huo ndio utaratibu wa Mungu, Ni lazima tuisikie kutoka kwa mtu fulani wa Mungu…na hivyo na sisi pia lazima tuwahubirie wengine ambao nao watasikia kutoka kwetu, ni kama mnyororo huyu anamzaa huyu katika imani, huyo anamzaa Yule na kuendelea..
Sasa kama umeokolewa na hutaki kuzaa wengine…kuna hatari kubwa sana…Tukirudi kwenye biblia tunamsoma Nabii mmoja aliyeitwa EZEKIELI..Huyu alikuwa ni nabii wa Mungu wa kweli kabisa., ambaye alikuwa miongoni mwa watu wachache waliochukuliwa kwenda Babeli…wakati yupo huko Mungu mwenyewe alimtokea akamwonyesha maono akiwa ameketi katika kiti chake cha Enzi huku maserafi na makerubi wakiwa wamemzunguka pande zote..akasikia sauti ya Mungu mwenyewe..Na Mungu akamtuma aende kuwaambia wana wa Israeli maovu yao na maasi yao na mambo yatakayokuja kuwatokea huko mbeleni wasipotubu.
Lakini yeye alipotoka pale baada ya kuona maono hayo…akaenda kukaa kimya, hakuwaambia watu chochote… sio kwamba alikuwa na dharau hapana! Hakumdharau Mungu…lakini alikuwa anaogopa kuwaambia(Alikuwa na hofu)….alikuwa na uchungu kweli na hasira moyoni, kwa maovu yaliyokuwa yanafanyika katikati ya watu wake lakini alikuwa anajifikiria fikiria namna ya kuwaambia..…akakaa siku saba hawaambii hao watu maono aliyoonyeshwa na Mungu…Baada ya siku saba maono yakamjia tena na kumwonya kwa anachokifanya cha kutowaambia watu maneno ya Mungu..Mungu akamwonya vikali kwa tabia hiyo..
Ezekieli 3:15 “Ndipo nikawafikia watu waliohamishwa, huko Tel-abibu, waliokuwa wakikaa karibu na mto Kebari, nikafika huko walikokuwa wakikaa; nikaketi huko miongoni mwao muda wa siku saba, katika hali ya ushangao mwingi.
16 Hata ikawa, mwisho wa siku saba, neno la Bwana likanijia, kusema,
17 Mwanadamu, nimekuweka kuwa mlinzi wa nyumba ya Israeli; basi, sikia neno hili litokalo katika kinywa changu, ukawape maonyo haya yatokayo kwangu.
18 Nimwambiapo mtu mbaya, Hakika utakufa; wewe usimpe maonyo, wala husemi na huyo mtu mbaya ili kumwonya, kusudi aache njia yake mbaya na kujiokoa roho yake; mtu yule mbaya atakufa katika uovu wake; lakini damu yake nitaitaka mkononi mwako.
19 Lakini ukimwonya mtu mbaya, wala yeye hauachi ubaya wake, wala njia yake mbaya, atakufa katika uovu wake; bali wewe umejiokoa roho yako”.
Umeona?..Ezekieli baada ya kusikia maneno hayo kutoka kwa Bwana kwamba “damu ya mtu itakuwa juu yake endapo hatamwambia maneno aliyoambiwa amwambie”..Ndipo akaelewa hakuna suala la mizaha tena kwenye kupeleka ujumbe wa Mungu kwa watu…Tangu wakati huo chochote alichoonyeshwa aliwafikishia wahusika kama kilivyo…Kwasababu alijua atadaiwa damu!. Hakuishi maisha ya kutokuihubiri injili tena.
Ndugu..Kama Bwana anakuonyesha maono ya kuwaonya watu juu ya dhambi zao na wewe huwaambii jifunze kwa Ezekieli hapo juu, kama unafahamu Neno na uwaambii wengine kuna hatari…Ni afadhali uwaambie wakatae kwa mapenzi yao wenyewe wewe utakuwa umenawa mikono..kuliko kutowaambia kabisa…mtu huyo akitoka na kwa bahati mbaya akagongwa na gari na kufa, unadhani wewe utakuwa katika hali gani?.
Kama umefahamu kuwa wazinzi na waasherati watakwenda kuzimu wasipotubu, na wewe mwenyewe sio mwasherati kwanini usiwaambie?…Mwambie ili aokoke, suala la kumbadilisha sio juu yako…wewe kazi yako ni kuhubiri tu injili…Lakini pia kama na wewe binafsi unafanya mambo hayo hayo wanayowafanya hao basi hapo usiwahubirie kwasababu wewe mwenyewe unahitaji wokovu..Na kipofu hawezi kumwongoza kipofu mwenzake..biblia inasema hivyo.
Hivyo kama ulikuwa uhubiri..anza leo!..Kama ulikuwa unaogopa kuwaambia watu juu ya habari ya siku za mwisho anza kuwaambia..Ezekieli aliogopa kuliko wewe lakini aliposikia suala la damu ya hao watu itatakwa juu yake, aligueka mara moja na wewe hivyo hivyo geuka leo..Na Bwana atakusaidia. Ipo hatari kubwa sana ya kutokuihubiri injili
Na kama hujaokoka kabisa..Tubu leo, mlango wa Neema bado upo wazi.. ila hautakuwa hivi siku zote..Umesoma hapo juu kitu gani kitamtokea mtu Yule atakayekufa katika dhambi zake huku ameonywa na amekataa…
Eze.3:19 “Lakini ukimwonya mtu mbaya, wala yeye , wala njia yake mbaya, atakufa katika uovu wake; bali wewe umejiokoa roho yako”.
Na wewe leo umesikia injili usipotaka kutubu utakufa katika dhambi zako na madhara ya kufa na dhambi ni ziwa la moto.
kwahiyo pale ulipo mwombe Bwana msamaha, tubia uasherati wako kama ni mwasherati, ulevi wako,uongo wako, rushwa zako, usengenyaji wako,wizi wako, matusi yako… kisha katafute Ubatizo sahihi kama hujabatizwa na Roho Mtakatifu atakutakasa na kukufanya kuwa mkamilifu kama yeye alivyo mkamilifu…
Marko 1:15 “akisema, Wakati umetimia, na ufalme wa Mungu umekaribia; tubuni, na kuiamini Injili”.
Bwana akubariki.jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Shalom.
Mada Nyinginezo:
KILEMBA CHA NEEMA, JE! UMEMVIKA MWANAO?
JE VIBWENGO NI KWELI VIPO?
KISIMA CHA MAJI YA UZIMA NI KILE KILE CHA ZAMANI.
UPAKO NI NINI?
Ulinzi wa daima (eternal security) Je! ni neno la kimaandiko?
Kuota unakula chakula maana yake ni nini?
Ninakusalimu katika jina la YESU KRISTO.
Awali ya yote nitoe tahadhari, kuwa kuna wimbi kubwa la mafundisho mengi ya uongo kuhusu ndoto. Hivyo ukikosa uelewa wa tafsiri sahihi kulingana na Mungu anavyozungumzia katika Neno lake..Utajikuta unapoteza kabisa dira ya Maisha yako ya rohoni kiujumla..na kujikuta unaacha kumtazama Mungu na Neno lake na unatazama ndoto unazoziota kila siku.
Kwa ufupi ndoto zimegawanyika katika makundi makuu matatu:
Hizi zikija huwa zinakuja na ujumbe Fulani, au onyo Fulani, au tahadhari Fulani, wala hazikufanya utamani kufanya mabaya, bali zinakufanya ujirekebishe pale ulipokuwa unakosea, , au ukaze mwendo katika safari yako ya kumtafuta Mungu, au kukuhimiza ukatende tendo la haki n.k.
Mfano wa ndoto za namna hii tunaweza kuiona kwa mke wa Pilato. Alipotaka kumzuia mumewe asimlibishe Bwana Yesu,..
Mathayo 27:19 “Na alipokuwa ameketi juu ya kiti cha hukumu, mkewe alimpelekea mjumbe, kumwambia, Usiwe na neno na yule mwenye haki; kwa sababu nimeteswa mengi leo katika ndoto kwa ajili yake.
Na hizi huwa haziji mara kwa mara kama zile ndoto zinazotana na mtu mwenyewe”.
Hizi huwa zinaambatana na vitisho, au tamaa za kutenda dhambi, au mambo maovu, au hofu..Kwamfano utakuta mtu anaota akifanya uzinzi na watu asiowajua au anaowajua, au anaota anafanya matambiko, au anacheza ngoma za kimila n.k. Zote hizo ni ndoto za kutoka kwa yule adui, Na hivyo mtu anaswa azikemee. Au arekebishe mwenendo wake, ni hiyo inakuja kwa kumpa Kristo Maisha yake.
Hapa ndipo asilimia kubwa za ndoto za watu zinapoegemea..
Ndoto za namna hii, kimsingi hazipaswi kuchukuliwa kiuzito kama hizo ndoto za aina mbili tulizozizungumzia hapo juu, kwani hizi zinatengenezwa na ubongo wa mtu tu pale anapokuwa amelala.. hivyo ubongo unatengeneza ndoto kutoka katika kumbukumbuku za matukio yote aliyoyafanya siku za nyuma, au siku za hivi karibuni..
Ndio hapo utakuta mtu labda jana ameona ajali mbaya imetokea, leo usiku akaota ajali nyingi zinatokea tokea..Au jana alikuwa msibani usiku wa leo anaota ndoto ya mtu Fulani kafa na yeye yupo kwenye mazishi..Au jana alikuwa anacheza mpira, leo hii anajiona yupo uwanjani anafunga magoli mengi..Au Maisha yake yote ni ya udereva, usiku anajiona anaendasha magari mengi tofauti tofauti..n.k.
Sasa ndoto za dizaini hii, huwa hazitokani na Mungu au shetani, kwahiyo zinapokujia unachopaswa ni kuzielewa kwanza, kisha kuachana nazo usihangaike hata kutafuta maana zake, kwasababu hazina maana yoyote rohoni..
Mhubiri 5:3 “Kwa maana ndoto huja kwa sababu ya shughuli nyingi.”
Vilevile aina nyingine ya ndoto zinatokana na ubongo wa mtu, ni ndoto za kula..biblia inasema.
Isaya 29:8 “Tena itakuwa kama mtu mwenye njaa aotapo, kumbe, anakula; lakini aamkapo, nafsi yake haina kitu; na kama mtu mwenye kiu aotapo, kumbe, anakunywa; lakini aamkapo, kumbe, anazimia, na nafsi yake inatamani…”
Unaona, kama ulilala jana na njaa ni jambo la kawaida kuota unakula usiku. Mfano kuota unakula nyama, au kuota unakula wali, au kuota unakula samaki..au kuota unakula matunda,.. au kuota unakula karanga,.. au kuota unakula keki,.. au kuota unakula mayai..au kuota unakula hushibi n.k. zote hizo Ukiangalia kwa makini utagundua kuwa pengine jana usiku ulilala na njaa..Au siku za hizi karibuni ulikuwa unakula aina hiyo ya chakula.
Hivyo ndoto kama hizo zikikujia zipuuzie tu, Endelea na Maisha yako ya kawaida, Jikite Zaidi katika kulitafakari Neno la Mungu kwasababu hilo ndilo linaloweza kukutabiria Maisha yako ya mbeleni ipasavyo.
Ndoto na Maono hazinusi hata chembe kwenye Neno la Mungu, Mungu anazifananisha na kama makapi katika Neno lake..soma
Yeremia 23:28 “Nabii aliye na ndoto, na aseme ndoto yake; na yeye aliye na neno langu, na aseme neno langu kwa uaminifu. Makapi ni kitu gani kuliko ngano? Asema Bwana.
29 Je! Neno langu si kama moto? Asema Bwana; na kama nyundo ivunjayo mawe vipande vipande?”
Ikiwa hujaokoka, Mlango wa neema bado upo wazi kwako, japo hautakuwa hivyo daima. Tubu dhambi zako angali muda unao, ukumbuke kuwa tunaishi katika dakika za nyiongeza tu, Kristo yupo mlangoni kurudi kulichukua kanisa lake. Dalili zote zinaonyesha, pengine kizazi chetu hichi kitashuhudia tukio zima la unyakuo wa kanisa.
Hivyo unasubiri nini. Mgeukie Kristo.Naye atakupokea.
Ubarikiwe.
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
FAHAMU TAFSIRI ZA NDOTO MBALIMBALI.
NENO LA MUNGU NI UFUNUO MKAMILIFU.
Ijumaa kuu ni nini? Na kwanini iitwe kuu?
Nitafanya Yerusalemu kuwa jiwe la kuwalemea watu wa kabila zote;
Kitakachochochea vita kuu mbili kuu ambazo tunazitazamia kuja huko mbeleni..ambayo ya kwanza ni ile vita ya Gogu na Magogu inayozungumziwa katika kitabu cha Ezekieli 38 & 39. Na ya pili ni ile ya Harmagedoni inayozungumziwa katika Ufunuo 16:15 na Ufunuo 19:11-21 ambayo hiyo itakuwa ni Mungu mwenyewe. Ipo nyingine ya Tatu ambayo itakuja kutokea baada ya ile miaka 1000 ya utawala wa Kristo kuisha, ambayo nayo itahusisha Magogu, lakini hiyo hatutaizungumzia leo hapa.
Hiyo ya kwanza inasema mfalme wa kaskazini atashuka akiyangoza baadhi ya mataifa ya kando kando, yatakusanyika lengo lao likiwa ni kuindoa Israeli katika ramani ya dunia..Na kwasasa tunajua mfalme huyo wa Kaskazini atakuwa si mwingine Zaidi ya Taifa la URUSI, (ndio Gogu na Magogu), kwasababu hilo ndilo lipo upande wa kaskazini mwa Israeli, na ndio lenye nguvu kwa ukanda ule wote..Hivyo Siku za usoni, tendo hilo litafanyika, lakini hawatashinda, kwani watauawa kwa mauaji ya halaiki, biblia inasema kutakuwa na mizoga ya miili ya watu itafagiliwa kwa muda wa miezi saba pale Israeli.. na silaha zao watazitumia kama nishati kwa muda wa miaka 7 kwa jinsi zitakavyokuwa nyingi..
Ezekieli 39:12 “Na kwa muda wa miezi saba nyumba ya Israeli watakuwa wakiwazika, wapate kuisafisha nchi.
13 Naam, watu wote wa nchi hiyo watawazika; itakuwa ni sifa kwao katika siku ile nitakapotukuzwa, asema Bwana MUNGU.
14 Nao watawachagua watu wa kufanya kazi ya daima, watakaopita kati ya nchi, ili kuwazika waliosalia juu ya uso wa nchi, ili kuisafisha; miezi saba itakapokwisha kupita watatafuta”
Na wakati huo ndio utakaokuwa mwisho wa Taifa la Urusi halitakuwepo tena.
Na vita nyingine ni ile ya Harmagedoni, hii itaongozwa na mataifa yatokayo katika mawio ya jua, mataifa ya Mashariki ya mbali, nayo yatakuwa si mengine Zaidi ya korea, Japani, China, Tawani..haya ndio yatakayoingoza vita hiyo, na safari hii haitakuwa mataifa machache tu, hapana bali itakuwa ni mataifa yote duniani yaliyosalia yataungana na hawa viongozi wao kwa ajili ya kuipoteza tena Israeli.
Unaweza ukajiuliza ni kwanini jambo hili litokee tu kwa Israeli?.. Kwani Wana ugomvi gani hasaa mkubwa mpaka ifikie hatua mataifa yote ulimwenguni yanaungana kwenda kukishambulia ki-nchi kidogo kama kile chenye ukubwa usiozidi hata mji wa Daresalaam.
Kama ukifuatilia utagundua Israeli kwasasa hawaingilii siasa zozote…au mambo ya mataifa mengine, kama yanavyofanya sasahivi mataifa makubwa kama vile Marekani, au mataifa ya Ulaya, ambayo hayo kimsingi ndio yangepaswa yawe na sababu za kutosha za kuwa na maadui.
Lakini Israeli, haifanyi chochote lakini inachukiwa,..Watu hawajui kuwa jambo hilo linatoka kwa BWANA. Ikiwa leo hii hata bado neema haijawarudia wayahudi, tayari ni maadui wa mataifa mengi, Fikiria siku ambapo watarudiwa ni nini kitatokea?
Hili shinikizo lilipo sasa litazidi hata Zaidi ya mara mia kwa jinsi siku zinavyozidi kusogea, Mungu atanyanyua visa, mbalimbali ambavyo vitayafanya mataifa yote sasa yawe na kusudi moja la kuingamiza Israeli.. Ni Mungu mwenyewe atayachochea haya mataifa kwa namna isiyo ya kawaida, atayachochoe, kweli kweli mpaka hilo Neno litatimia linalosema…
Zekaria 12:2 “Angalia, mimi nitafanya Yerusalemu kuwa kikombe cha kuyumba-yumba kwa watu wa kabila zote, wazungukao pande zote; tena kitakuwa juu ya Yuda pia wakati wa kuhusuriwa Yerusalemu”.
3 Tena itakuwa siku hiyo, nitafanya Yerusalemu kuwa jiwe la kuwalemea watu wa kabila zote; wote watakaojitwika jiwe hilo watapata jeraha nyingi; na mataifa yote ya dunia watakusanyika pamoja juu yake.
Unaona, hiyo ndio itakayopelekea sasa mataifa yote duniani kufikia Kiama chao..
Watakusanyika pale Harmagedoni..Sasa kumbuka wakati huo Taifa la Israeli litakuwa litakuwa limeshamwamini Masihi wao Yesu Kristo, hivyo watapaza sauti zao na kumlilia, aje kuwapigania kama alivyowapigania enzi za kale. Wakati huo ambapo mataifa yote sasa yameshaizunguka nchi hiyo ndogo,.. ndipo watakapomwona mwa Adamu akishuka na mawingu kutoka mbinguni kwa nguvu na utukufu mwingi akiwa na majeshi wa watakatifu wake ambao alishawanyakua.
Na hapo ndipo mataifa yote yatakapoomboleza, lakini utakuwa ndio mwisho wao, Bwana atawauwa wote kwa upanga utokao katika kinywa chake..
Ufunuo 19:11 “Kisha nikaziona mbingu zimefunuka, na tazama, farasi mweupe, na yeye aliyempanda, aitwaye Mwaminifu na Wa-kweli, naye kwa haki ahukumu na kufanya vita.
12 Na macho yake yalikuwa kama mwali wa moto, na juu ya kichwa chake vilemba vingi; naye ana jina lililoandikwa, asilolijua mtu ila yeye mwenyewe.
13 Naye amevikwa vazi lililochovywa katika damu, na jina lake aitwa, Neno la Mungu.
14 Na majeshi yaliyo mbinguni wakamfuata, wamepanda farasi weupe na kuvikwa kitani nzuri, nyeupe, safi.
15 Na upanga mkali hutoka kinywani mwake ili awapige mataifa kwa huo. Naye atawachunga kwa fimbo ya chuma, naye anakanyaga shinikizo la mvinyo ya ghadhabu ya hasira ya Mungu Mwenyezi.
16 Naye ana jina limeandikwa katika vazi lake na paja lake, MFALME WA WAFALME, NA Bwana WA MABwana.
17 Kisha nikaona malaika mmoja amesimama katika jua; akalia kwa sauti kuu, akiwaambia ndege wote warukao katikati ya mbingu, Njoni mkutane kwa karamu ya Mungu iliyo kuu;
18 mpate kula nyama ya wafalme, na nyama ya majemadari, na nyama ya watu hodari, na nyama ya farasi na ya watu wawapandao, na nyama ya watu wote, waungwana kwa watumwa, wadogo kwa wakubwa.
19 Kisha nikamwona huyo mnyama, na wafalme wa nchi, na majeshi yao, wamekutana kufanya vita na yeye aketiye juu ya farasi yule, tena na majeshi yake”.
Wakati huo upo karibu sana, leo hii kila mmoja wetu anashuhudia kinachoendelea mashariki ya kati, kama wewe si mfuatiliaje wa taarifa za habari..anza kufuatilia habari hususani za mashariki ya kati… jifunze, au ulizia ufahamu mambo yanayoendelea ulimwenguni.. Idadi ya mataifa yanayoipinga nchi ya Israeli inazidi kuongozeka, dini zinazolichukia taifa la Israeli nazo zinaongezeka.
Hilo lote ni shinikizo kutoka kwa Bwana mwenyewe..Kutuonyesha kuwa mwisho upo karibuni sana..
Nitafanya Yerusalemu kuwa jiwe la kuwalemea watu wa kabila zote;
Na kabla hayo yote hayajatokea Utatangulia unyakuo wa kanisa kwanza..Ambao dalili zote zinaonyesha wakati wowote kuanzia sasa parapanda italia..na wafu wote waliokufa katika Kristo watafufuka na kwenda katika karamu ya mwanakondoo mbinguni..
Ila wale waliobakia mlango wa neema hautakuwa kwao tena, bali kwa wateule wa Mungu wayahudi..Leo hii unasubiri nini usimruhusu Kristo aingie maishani mwako akubalishe, usidanganywe na uvumi kama uvumi wa amani unaouna sasa hivi, huo ni kuwapumbaza watu waone kama tuna mamilioni ya miaka hapa duniani.. biblia inasema…
1Wathesalonike 5:1 “Lakini, ndugu, kwa habari ya nyakati na majira, hamna haja niwaandikie.
2 Maana ninyi wenyewe mnajua yakini ya kuwa siku ya Bwana yaja kama vile mwivi ajavyo usiku.
3 Wakati wasemapo, Kuna amani na salama, ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafula, kama vile utungu umjiavyo mwenye mimba, wala hakika hawataokolewa”.
Unaona? Tubu dhambi zote, umgeukie Kristo ndani ya wakati huu mfupi tuliobakiwa nao kabla ya parapanda kulia, tengeneza mambo yako kwasababu injili tuliyonayo sasa si ile tena ya zamani ya kuvutwa kwa maneno laini, tuliyonayo sasa ni ile ya mtakatifu na aendelee kujitakasa na mwenye dhambi aendelee kufanya dhambi..Kwani wakati wa mavuno upo karibu sana…Hivyo maombi yangu ni mimi na wewe tuangukie katika kundi la wanaojitakasa..
Bwana akubariki. jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
MPAKA UTIMILIFU WA MATAIFA UTAKAPOWASILI.
UTAWALA WA MIAKA 1000.
CHUKIZO LA UHARIBIFU
MTINI, WENYE MAJANI.
Vichwa saba vya mnyama wa kwenye Ufunuo 13 na 17, Ni nini?
Je kuzalishwa na mkunga wa kiume ni dhambi?..Je Mungu anaweza kutumia chochote kupitisha uponyaji wake?..Je jina la Yesu Kristo lina nguvu ya kuponya kabisa bila kutegemea daktari?
Kwanza ni muhimu kufahamu kuwa tatizo lolote au ugonjwa wowote ambao mtu anaweza kuupata..Mungu anauwezo wa kuuondoa pasipo mkono wa mwanadamu yoyote kuhusika…Na hiyo inatokana na Imani mtu aliyonayo kwa Mungu..Ukiamini kwa moyo wako wote, basi yote yanawezekana.
Lakini pamoja na hayo..pia Mungu anaweza kutumia chochote kupitisha uponyaji wake…Anaweza kumtumia mwanadamu, anaweza kutumia chakula au chochote kile.
Mtu anaweza akaugua akala aina fulani ya chakula akapona..sasa kiuhalisia sio chakula kilichomponya bali ni ule uponyaji Mungu aliouweka ndani ya kile chakula ndio uliomfungua…
Kadhalika anaweza kumtumia mwanadamu kumponya mtu…anawapa maarifa fulani wanadamu ambayo kwa hayo mtu anaweza kupata uponyaji kwamfano..Mtu anaweza kuugua ugonjwa fulani..labda uvimbe umeota tumboni…na madaktari wakahusika katika kuuondoa uvimbe ule kwa njia ya OPERATION na mtu akawa mzima kabisa.,Sasa hiyo ni nguvu ya uponyaji Mungu aliyoiweka kwenye maarifa ya wanadamu n.k
Ni wazi kuwa nyakati za zamani sana hakukuwepo kabisa kwa wakunga wa kiume…au kama walikuwepo walikuwa wachache sana..Lakini kwa jinsi siku zinavyozidi kwenda wanaongezeka sana..Hiyo ni kutokana na matatizo ya wanawake kuongezeka…Magonjwa ya wanawake yanapozidi kuongezeka madaktari nao wanalazimika kuongezeka na idadi kubwa madaktari wanaoongezeka ni wanaume…Hivyo wanaume wengi wanajikita kuingia kusomea mfumo wa kibaolojia wa mwanamke zaidi ya wanawake wenyewe..huku wanawake wakiwa wachache kutokana na sababu mbalimbali.
Kwasababu hiyo basi sio dhambi kuwepo kwa madaktari wa kiume katika kushughulikia matatizo ya wanawake pale wanawake wanapokosekana kwasababu..lengo la wao kuwepo sio kuongeza matatizo bali kupunguza. Hakuna mtu yeyote anayekwenda hospitalini asiyekuwa na tatizo lolote, wote wanaokwenda wanakwenda kutafuta msaada.
Hivyo kuzalishwa na mkunga wa kiume sio dhambi wala kufanyiwa operation na mwanamume sio dhambi..Zipo operation za uzazi, ambazo kizazi kinalazimika kuchanwa kuondolewa ugonjwa usiopaswa kuwemo humo..Na operation kama hizo huwa zinamlazimisha mgonjwa kuvuliwa nguo zote na kuwa kama alivyozaliwa ili matibabu hayo yaweze kufanyika..na madaktari bingwa wanaofanya hizo operation wengi ni wanaume wakiwa pamoja na manesi wa kike…Hivyo kwa mgonjwa wa kike kutibiwa kwa viwango hivyo na daktari wa kiume sio dhambi..wala wa kiume pia kutibiwa kwa viwango hivyo na daktari wa kike ambavyo vitamlazimisha kuwa tupu kabisa mbele ya matatibu sio dhambi…Kwasababu lengo ni kupata matibabu na si kitu kingine.
Na matibabu kama hayo yanafanyika kwa madaktari wa hospitalini tu kwasababu wengi wakiwa katika vyumba vya uchunguzi au operation wanakuwa zaidi ya daktari mmoja tena wa jinsia tofauti, ili kuzuia uzalilishaji na vitu kama hivyo…. na sio kwa waganga wa kienyeji…wala kwa madaktari binafsi wa mitaani ambao wanakuita tu binafsi na kukwambia uvue hichi au kile wakuchunguze..Hao kwa namna yoyote hawapaswi kuruhusiwa kufanya uchunguzi au matibabu ya namna hiyo.
Lakini yote katika yote..Bwana Yesu ndiye mponyaji mkuu..operesheni wakati mwingine zinafeli pamoja na gharama zake zote hizo kubwa…lakini Yesu Kristo hajawahi kushindwa…
Vyakula wakati mwingine vinashindwa kutuponya lakini Yesu Kristo hajawahi kushindwa..Yapo magonjwa ambayo madaktari hawayaelewi chanzo chake lakini Yesu Kristo anayajua.
Madaktari wanatibu kwa gharama kubwa za fedha, na wakati mwingine gharama za kutolewa nguo zote, au nywele zote au kiungo fulani kukatwa ndipo matibabu yaweze kufanyika..lakini Yesu Kristo anafanya bila hayo yote.
Ikiwa unaumwa ugonjwa wowote ule..Nataka na unakaribia kwenda kwenye operesheni…nataka nikuambie Yesu Kristo anaweza kukuponya kabla hujamkaribia huyo daktari..
Weka mkono mahali unapoumwa..kama ni kifuani, kichwani, tumboni..kama ni ugonjwa ambao huelewi chanzo chake weka kichwani…Yesu anajua chanzo chake..
Sasa baada ya kuweka kichwani..unaposoma sala hii ugonjwa wako unakwenda kuhama sasahivi na kutoweka kabisa..Amini tu.
“Bwana Yesu namwombe mtu ambaye simjui ni nani, wala jina lake, wala ugonjwa wake wala mahali alipo, lakini wewe unamjua jina lake, mahali alipo na tatizo alilonalo..namwombea kwa Imani katika jina lako lenye nguvu (Jina la Yesu). Kwamba kila ugonjwa na kila pandikizo lililopandikizwa ndani yake na yule adui likapate kutoweka sasahivi katika JINA LA YESU KRISTO! Amen”.
Ikiwa umeisoma hii sala niliyokuombea…Huo ugonjwa umeshaondoka na kama ugonjwa huo ulivyoondoka ndani yako…Ugonjwa wa rohoni pia unapaswa uondoke pia..Na ugonjwa wa rohoni ni dhambi.
Hizo zinaondoka ndani yako kwa kumkiri sasa Yesu Kristo ambaye amekuponya ugonjwa wako..Na baada ya kumkiri kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yako..mwambie akusamehe dhambi zote ulizowahi kuzitenda huko nyuma…na wewe mwenyewe dhamiria kuziacha…kama ulikuwa ni mwasherati..umeona utukufu wa Mungu..hivyo usifanye uasherati tena…vivyo hivyo na dhambi nyingine zote. Usizifanye tena, yasije yakakupata mabaya kuliko hayo uliyokuwa nayo.
Na baada ya kutubu haraka sana nenda katafute ubatizo. Kumbuka ubatizo sahihi ni wa muhimu sana. Na ubatizo sahihi ni ule wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa Jina la Yesu Kristo.(kulingana na Matendo 2:38). Na Roho Mtakatifu atakayeingia ndani yako atakuongoza na kukutia katika kweli yote.
Bwana akubariki sana.jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Tafadhali share na wengine.
Mada Nyinginezo:
kilemba cha neema, Je! Umemvika mwanao ?
Jina la Bwana Yesu Kristo libarikiwe..Karibu tujikumbushe mambo muhimu katika maisha yetu..Na hayo si mengine zaidi ya maonyo ya Neno la Mungu…Leo kwa Neema za Bwana tutajikumbusha majukumu machache ya wazazi juu ya watoto wetu..
Kutoka 20: 12 “Waheshimu baba yako na mama yako; siku zako zipate kuwa nyingi katika nchi upewayo na Bwana, Mungu wako”.
Neno hili ni Neno la Mungu kwa watoto wote ambao wanao wazazi…Na hata kama hawana wazazi labda wamefariki au hawaishi nao kwa namna moja au nyingine…Basi nafasi hiyo ya Baba na Mama itachukuliwa na walezi wao…Hao wanasimama kama Baba zao na Mama zao kihalali kabisa mbele za Mungu..hata kama wapo katika vituo vya malezi vya mayatima…hao walezi wao wanachukua nafasi hiyo ya Baba na Mama…wana amri kutoka kwa Mungu kuheshimiwa kama wazazi halisi…Kwasababu kuna Baraka kubwa sana katika kuwaheshimu wazazi na kuwasikiliza..
Kadhalika haijalishi mzazi ni mwovu kiasi gani lakini ni lazima kumheshimu, na kumtii haijalishi yeye hajiheshimu kiasi gani ni wajibu wa kila mtoto kumheshimu mzazi wake..Kwasababu ndio amri ya kwanza yenye ahadi…
Waefeso 6:1 “Enyi watoto, watiini wazazi wenu katika Bwana, maana hii ndiyo haki.
2 Waheshimu baba yako na mama yako; amri hii ndiyo amri ya kwanza yenye ahadi,
3 Upate heri, ukae siku nyingi katika dunia”
Kupata heri na kuishi siku nyingi ni vitu viwili tofauti…Unaweza kuishi siku nyingi lakini maisha yasiwe ya heri..Hivyo, vyote viwili vinapaswa viende pamoja…
Sasa Kitu cha Muhimu cha kufahamu kwa mzazi ni kwamba…Hatima ya mtoto, mzazi anaweza kuchangia kwa asilimia kubwa kuitengeneza au kuiharibu…Mzazi anaweza kukazana kweli kumpenda mwanawe, kumlipia karo, kumtafutia shule bora..kumpatia lishe bora, kumlinda..kumhakikishia bima ya afya n.k Lakini kama hatamtengenezea mwanawe mazingira ya kumheshimu au kumtii.. huyo mtoto hawezi kupata heri yoyote huko anakokwenda, wala hawezi kuishi maisha marefu…haijalishi atapatiwa elimu nzuri kiasi gani sasa…au atakuwa na afya nzuri kiasi gani sasa au maarufu kiasi gani…Maisha yake yatakatika katikati na yatakuwa ya tabu.
Hayo ndio mambo ya kwanza ya kuzingatia kabla hata ya kwenda kuangalia ufaulu wake wa darasani…usifurahie anapofaulu sana na huku adabu yake inazidi kwenda chini..furahia pale heshima yake na utii wake unapozidi kupanda kwasababu unajua..hata kama atapepesuka kiafya sasa..hatakufa!..ataishi muda mrefu kwasababu Neno la Mungu linasema hivyo..hata kama hana heri sasa, lakini atakuja kuwa na heri baadaye katika kipindi cha maisha yake yote..
Hivyo kazana kumfundisha awe na tabia ya kukusikiliza…chochote utakachomwambia akutii na afanye kwa kupenda na si kwa kulazimishwa lazimishwa..mfunze tabia nzuri na heshima na utiii kwako na kwa watu wengine, mvishe mavazi ya adabu na mfundishe kuwa mtii….Mjaribu mara kwa mara kuangalia utii wake umefikia wapi ukiona umepungua tafuta namna ya kuurudisha…..mtume dukani mrudishe hata mara mbili au tatu, mpime..ujue kiwango cha utii alichonacho na heshima.
Mpime anapokuwa na wageni na watu wengine anakuwa na tabia gani zisizofaa na zile zinazofaa mpongeze…ukiona kasoro tumia fimbo kidogo, maana biblia inasema ukimpiga hatakufa…Wengi hawatumii fimbo wakidhani wanamharibia ujasiri mtoto, fimbo isiyokuwa na mafunzo sahihi ndiyo inayomharibia ujasiri..lakini fimbo yenye ujumbe wa kujenga ndiyo inayomjenga zaidi mtoto…
Na Mungu alivyowaumba watoto hawana kinyongo ili kwamba waweze kutengenezeka..ukimwadhibu sasahivi baada ya nusu saa mnacheka na kufurahi, ule upumbavu utakuwa umendoka lakini upendo wake kwako bado upo…..ukimwacha sasa bila kumfunza atakapokuwa mtu mzima hali za kuwa na vinyongo na uchungu zitakapomjia itakuwa ni ngumu kumtengeneza….kila utakalomwambia atakuwa anakwambia unamnyanyasa,..mara unaingilia uhuru wake..mara hujali hisia zake, mara wewe ni mkoloni, mara unamwaibisha n.k
Pia katika utoto aliopo, mfundishe biblia..mpe mistari kadhaa ya kuikariri na kuishika kwasababu watoto wengi bado hawajaweza kuipambanua mistari..wape tu waikariri itawasaidia ukubwani..kuliko kukariri nyimbo za kidunia..pia wafundishe nyimbo za kuabudu, na kumsifu Mungu na wafundishe sala za kuomba muda wote na habari za Yesu ambazo ndizo za muhimu kuliko zote..Na wapime je hivyo unavyowafundisha au wanavyofundishwa na wengine wanavizingatia.??
Ukimpima mtoto vizuri na kujua kuwa anakutii na kukuheshimu na anaheshima kubwa ambayo mpaka watu wa nje wanaishuhudia na kusema Yule mtoto anaheshima na adabu…Basi, kuna Baraka ambazo Mungu anaziachia ambazo ulimwengu hauwezi ukaziona..hapo ndipo nyota njema ya mtoto inapoanzia..
Mithali 22: 6 “Mlee mtoto katika njia impasayo, Naye hataiacha, hata atakapokuwa mzee”…
Wengi wanaogopa kuwafundisha wanao adabu na heshima kwasababu wanahisi wakishafikisha umri Fulani labda wa kuvunja ungo au kubalehe watakengeuka..Huo ni uongo wa shetani!!…Watoto wengi wanakengeuka ukubwani kwasababu wazazi wao ambao hapo kwanza walikuwa wanawalea vizuri leo wamekengeuka!..sasa kama mzazi kakengeuka mtoto atasalimikaje?..Mzazi alikuwa anakwenda kanisani na mwombaji sasa hafanyi hivyo tena..mtoto ataendeleaje kwenda kanisani?…Mtoto alikuwa amezoea nyumbani ni mahali pa ibada sasa nyumbani kunapigwa kila siku kwenye TV, nyimbo za kidunia, mtoto ataendeleaje kuwa mtakatifu?….Lakini kama mzazi akibaki vile vile Yule mtoto kamwe hawezi kukengeuka hata atakapokuwa mzee..biblia sio kitabu cha Uongo!… Haiwezi kusema mtoto hataiacha ile njia halafu aje kuiacha!..sasa Mungu atakuwa ni mwongo.
Sasa faida nyingine ya mwisho na kuu ambayo mtoto anaweza kuipata kutoka kwako mzazi kwa kumfanya akutii na hata akusikilize na kukuheshimu katika viwango vya juu ni KUVIKWA KILEMBA CHA NEEMA KICHWANI PAKE?.
Mithali 1: 8 “Mwanangu, yasikilize mafundisho ya baba yako, Wala usiiache sheria ya mama yako,
9 Kwa maana hayo yatakuwa KILEMBA CHA NEEMA KICHWANI PAKO, Na mikufu shingoni mwako”.
Hii ni Baraka kubwa sana ambayo wazazi wengi hawaijui…Hapa duniani tunaishi kwa Neema,…Hivyo Neema ya Kristo inapokuwa nyingi juu yetu..ndipo tunapokuwa na nafasi zaidi ya kumkaribia Mungu, ndipo tunapokuwa na nafasi kubwa zaidi ya kuwa watumishi wa Mungu…Na utumishi wa Mungu sio tu ule wa kuhubiri madhabahuni hapana! bali hata ule wa Danieli ni utumishi wa Mungu..Pale Mungu anapokuweka katika ngazi Fulani ya juu na huko anakutumia kuwatunza watu wake..Hivyo Neema kama hiyo ni njema kwa mtu yeyote…Mtu anayemtumikia Mungu,.. Mungu atamheshimu biblia inasema hivyo (katika Yohana 12:26).
Sasa ni nani asiyetaka kuheshimiwa na Mungu?..Je! unataka mwanao aheshimiwe na Mungu?…Kwa kuvikwa neema ya kuwa mtumishi wake?…Ni kwa kumfanya akutii na kukuheshimu..huku na wewe ukionyesha kielelezo cha kumcha Mungu maisha yako yote ili usimwangushe..
Kuwa na mtoto ni Baraka!..Hususani kama umemvisha kilemba hicho cha neema….Neno la Mungu linasema wapeni watu vitu nanyi mtapewa kipimo cha kujaa na kushindiliwa na kusukwasukwa hata kumwagika ndivyo watu watakavyowapa kifuani mwenu…..Na wewe umempa mwanao hicho kipimo cha Neema ya Mungu juu ya kichwa chake kubwa namna hiyo…Bwana atamtumia huyo huyo kukulipa..kukurudishia kipimo cha kujaa na kushindiliwa nakusukwasukwa hata kumwagika katika siku za mbeleni..Na kwasababu mwanao au wanao watakuwa wanatembea na hiyo NEEMA kubwa sana kichwani mwao basi kila watakalomwomba Mungu, Mungu na kila watakalolifanya litafanikiwa katika maisha yao.
Kama wewe mzazi hujaokoka!..Tambua kuwa huwezi kuwavika wanao KILEMBA HICHO CHA NEEMA vichwani mwao..Wataharibikiwa na kuwa na maisha mabaya..kwasababu maisha yako wewe ni mabaya!..Hivyo ni vizuri leo hii ukamgeukia Kristo akuoshe dhambi zako kweli kweli kwa damu yake..Ili uwe mzazi/mlezi bora…Unachopaswa kufanya ni kutubu kuanzia leo na kumwambia Bwana akusamehe..akusamehe, uasherati wako kama ulikuwa unaufanya..akusamehe kwa kutowajali wanao,..akusamehe kwa kila uchafu uliokuwa unaufanya..na hivyo unamwahidi kwamba utafanya tena..
Baada ya kutubu kabatizwe katika ubatizo sahihi kwaajili ya ondoleo la dhambi (Matendo 2:38)..Kumbuka ubatizo sahihi ni ule wa kuzamishwa mwili wote kwenye maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo. Baada ya kufanya hivyo Roho Ambaye atakuwa ndani yako atakuongoza kufanya mengine yote yaliyosalia na kukupa uelewa wa ajabu wa kuyaelewa maandiko na kukusaidia kushinda dhambi ambazo kwa nguvu zako ulikuwa huwezi.
Kumbuka pia Yesu Kristo atarudi..Biblia inasema “Itatufaidia nini tuupate ulimwengu mzima na kisha tupate hasara za nafsi zetu’’..Hivyo uwe unalitafakari hilo kila siku.
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Maran atha!..Shalom.
Mada Nyinginezo:
LENGO LA SHETANI KWA WATOTO WA KIZAZI HIKI.
MOTO HUFA KWA KUKOSA KUNI.HATA UASHERATI NAO
KIMBIA! KIMBIA! KIMBIA!
UNATAKA KUBARIKIWA? BASI USIKWEPE GHARAMA ZAKE.
BONDE LA KUKATA MANENO.
Ulinzi wa daima (eternal security) ni neno la kimaandiko?
JIBU: Ulinzi wa daima, kama inavyojulikana kwa lugha ya kiingereza“eternal security”, linamaana kwamba mtu akishamwamini Kristo akaokoka, basi mtu huyo anakuwa tayari anao ulinzi wa milele wa wokovu wake, na kwamba hawezi kuanguka tena kwenda kuzimu hata iweje, kwani wewe tayari ni milki ya Mungu milele. “Once saved, forever saved”.
Wanaoamini hivyo wanasema, suala la wokovu ni la Mungu mwenyewe, anamwokoa mtu kwa neema na si kwa matendo yake mwenyewe. Na hivyo hata mtu anapochukua uamuzi wa kuupokea wokovu, hata hayo yaliyobakia pia ya kumlinda mtu huyo hadi siku wa mwisho yanakuwa ni ya Mungu..
Ni kweli ulinzi wa daima/milele ni neno la kimaandiko, kwamba ni kweli mtu akishaokolewa, Saa hiyo hiyo Mungu anampa uhakika wa uzima wa milele, anakuwa ametiwa muhuri hadi siku ya ukombozi wake, (Soma Waefeso 4:30, Warumi 8:33-34, Warumi 8:38-39)..Lakini ahadi hiyo ni kama mtu akidumu katika hiyo neema tu!. Ikiwa atafanya hivyo Mungu hawezi kumwacha akaangamia, atamshikilia mkono kila anapokwenda kuhakikisha haanguki.. Lakini kama hatataka yeye mwenyewe kudumu katika neema (Imani) hiyo, wazo hilo ni la uongo.
Ni sawa umemshika mtoto mkono na kumwambia atembee huku umemshika mkono na ukamwakikishia kwamba akiwa katika mikono yako kamwe hataanguka atakuwa salama daima..Lakini Yule mtoto akasikiliza ushauri wa mtu mwingine kwamba anaweza kutembea peke yake hivyo kwa hiyari yake mwenyewe akakataa na kusema sitaki kushikwa na wewe na akatoka mikononi mwako kwa nguvu je! Akianguka atakulaumu..na kumwambia ulimwahidia hataanguka daima atakuwa salama?..Kitu kisichofahamika na wengi ni kwamba Mungu hawezi kuvuka maamuzi yetu..Huwa hatulazimishi kufanya kitu kama sisi wanadamu tunavyolazimishana..
Hivyo tunapookolewa, hatukai tu tukijitumainisha kuwa tumeshashinda vita moja kwa moja, na kwamba tupo mikononi mwa Mungu salama…Tunapaswa tufahamu kuwa ndio kwanza tumeanza vita kwasababu Adui yetu shetani atataka kutufanya tuamue kuiacha imani..
Na ndio maana kuanzia huo wakati (baada ya kuokoka) mambo huwa hayawahi marahisi wakati mwingine tunakumbana na vita na majaribu mengi kutoka kwa adui, na misukosuko mingi ili tu tuiache imani,..Hivyo kama shetani angekuwa anajua kuwa kama mtu ameupata wokovu ndio kaupata milele, basi asingekuwa na haja ya sisi kutufuatilia tuiache Imani baada ya hapo, maana kwake yeye ingekuwa ni kazi bure.,Lakini kinyume chake kila siku anatupiga vita kwasababu anajua kuwa uwezakano wa kukipoteza kile tulichonacho upo!…Anajua pia bado kuna uwezekano wa kuupoteza ulinzi huo wa milele.
Hivyo ikiwa kama tutadumu katika mapenzi ya Mungu basi uhakika wa wokovu huo ni lazima.. Lakini ikiwa hatutailinda neema tuliyopewa kwa bidii, tukawa wazembe, yaani tunaishi tu kama tunavyotaka, uwezekano mkubwa wa kuupoteza wokovu wetu upo.
Mtume Paulo alikuwa ni mtu aliyetokewa na Kristo, aliyejitoa kweli kwa Mungu, aliyehubiri injili kwa mataifa mengi, maelfu au pengine mamilioni ya watu waliokolewa kwa kupitia huduma yake..Lakini kuna wakati alisema..
1Wakorintho 9:26 “Hata mimi napiga mbio vivyo hivyo, si kama asitaye; napigana ngumi vivyo hivyo, si kama apigaye hewa;
27 bali nautesa mwili wangu na kuutumikisha; isiwe, nikiisha kuwahubiri wengine, mwenyewe niwe mtu wa kukataliwa”.
Unaona, alishaona kumbe anaweza akawa sio tu mkristo peke yake, bali akawa hata mtumishi wa Mungu aliyeitwa, lakini mwisho wa siku akawa ni mtu wa kukataliwa (akaenda Jehanamu ya moto).
Paulo alisema vile kwa kumaanisha, sio kama kujionyesha kuwa ni yeye ni mnyenyekevu..Aliona uwezekano huo wa kupotea bado upo kwa asilimia kubwa!.
Wapo watumishi leo hii, ni wazinzi, wanadhani bado wanao ulinzi wa daima ndani yao..Wapo wachungaji ni wanywaji pombe na wavutaji sigara, wanadhani bado wanao ulinzi wa daima ndani yao..Kwamba hata wakifa watakwenda mbinguni kwasababu maandiko yanatuambia tunaokolewa kwa neema.
Nataka nikuambie, Hata Yuda, aliyechaguliwa na Kristo, mwenyewe,..Na alianza vizuri lakini hakuilinda neema aliyopewa na mwisho wa siku akaangukia katika mikono ya shetani. Sasa kama Yuda aliyetembea na Yesu miaka 3 na nusu alikengeuka…Mimi na wewe ni nani ambao hata hatujawahi kumwona Yesu tujidanganye kuwa tukishaokolewa tumeokolewa?.
Hivyo usipoithamini neema uliyopewa bure kwa damu ya Yesu Kristo, hujibidiishi kuilinda Imani yako, huko nyuma ulimaanisha kuokoka kweli, lakini leo hii, unakwenda Disko,.. unavaa nguo za uchi uchi, unatazama picha chafu mitandaoni, unasikiliza miziki ya kidunia, unakula rushwa, unakwenda kwa waganga..Nataka nikuambie kwako ulinzi huo wa daima (eternal security) ulishaondoka!!..Na hata ukifa leo hii utakwenda kuzimu na adhabu yako itakuwa kubwa Zaidi ya wale ambao hawakumjua Kristo, Haijalishi wewe ni kiongozi mzuri wa kanisani kiasi gani,..haijalishi umeshahubiri kiasi gani, haijalishi umewaleta wengi kwa Kristo kiasi gani…Usipoyafanya mapenzi ya Mungu, utapotea tu.
Ezekieli 3:20 “Tena mtu mwenye haki aiachapo haki yake, na kutenda uovu, nami nikiweka kikwazo mbele yake, atakufa; kwa sababu hukumwonya, atakufa katika uovu wake, wala matendo yake ya haki aliyoyatenda hayatakumbukwa;”
2Petro 1:10 “Kwa hiyo ndugu, jitahidini zaidi kufanya imara kuitwa kwenu na uteule wenu; maana mkitenda hayo hamtajikwaa kamwe”.
Uthamini wokovu wako, ili Mungu apate nafasi ya kukulinda..
Ubarikiwe.
Mada Nyinginezo:
CHUJIO HILI NI LA AJABU SANA!
INJILI YA KRISTO HAITANGAZWI KWA HATI MILIKI.
NI KIPI MUNGU ANACHOKITAZAMA ZAIDI, MOYO AU MWILI?
KWANINI AWE PUNDA NA SI MNYAMA MWINGINE?