Title Devis

Juya ni nini kwenye biblia? (Mathayo 13:47)

Juya maana yake ni jarife, au wavu wa kuvulia samaki.

Habari hiyo inapatikana kwenye vifungu hivi vya maandiko;

Habakuki 1:13 “Wewe uliye na macho safi hata usiweze kuangalia uovu, wewe usiyeweza kutazama ukaidi, mbona unawaangalia watendao kwa hila; na kunyamaza kimya, hapo mtu mwovu ammezapo mtu aliye mwenye haki kuliko yeye;

14 na kufanya wanadamu kuwa kama samaki wa baharini, kama vitu vitambaavyo, ambavyo havina mtawala?

15 Yeye huwatoa wote kwa ndoana yake, huwakamata katika wavu wake, na kuwakusanya katika JUYA lake; ndiyo sababu afurahi na kupendezwa.

16 Kwa sababu hiyo huutolea wavu wake sadaka, na kulifukizia uvumba JUYA lake; kwa sababu kwa vitu vile fungu lake limenona, na chakula chake kimekuwa tele.

17 Je! Atawatoa walio katika wavu wake, asiache kuwaua watu wa mataifa daima”?

Na katika agano jipya Bwana Yesu aliutumia pia mfano wa Juya la mvuvi kufananisha na jinsi mwisho wa dunia utakavyokuwa.

Mathayo 13:47 “Tena ufalme wa mbinguni umefanana na juya, lililotupwa baharini, likakusanya samaki wa kila namna;

48 hata lilipojaa, walilivuta pwani; wakaketi, wakakusanya walio wema vyomboni, bali walio wabaya wakawatupa.

49 Ndivyo itakavyokuwa katika mwisho wa dunia; malaika watatokea, watawatenga waovu mbali na wenye haki,

50 na kuwatupa katika tanuru ya moto; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno”.

Lakini ni ujumbe gani mkubwa tunaupata kwenye mfano wa  Juya?

Hapo katika mfano wa Yesu tunaona walivuliwa samaki wa aina zote na kupelekwa nje kabisa ya pwani, ikiashiria kuwa wanadamu wote watavunwa ile siku ya mwisho, wawe ni watakatifu wawe ni waovu wote watavunwa, maana yake ni kuwa kila mmoja wetu atahusika, tutatolewa kwenye huu ulimwengu wa sasa, na hapo ndipo walio wema wataenda mbinguni kwa Mungu na wale walio waovu watatupwa katika ziwa la moto.

Na kibaya zaidi siku zenyewe ndio hizi tuishizo. Wakati wowote paraparanda italia, na mwisho utafika, Je bado upo vuguvugu, bado unautumaini ulimwenguni usiodumu milele?.

Kama wewe ni mwenyewe dhambi na unataka leo Yesu ayaokoe maisha yako. Ili ikitokea hata mwisho umefika leo, uwekwe kapuni mwa Bwana, basi uamuzi huo ni mzuri sana. Kumbuka biblia inasema saa ya wokovu ni sasa, Na wakati uliokubalika ni huu.

Kama ni hivyo fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba na Mungu akubariki  >>>> SALA YA TOBA

Tazama pia maneno mengine ya biblia chini.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

LAKINI USIKU WA MANANE, PAKAWA NA KELELE.

UMEFUMBULIWA MACHO YAKO YA KIROHO?

UNYAKUO.

https://wingulamashahidi.org/ikabodi-maana-yake-ni-nini/

Biblia inamaanisha nini inaposema “Tusitweze unabii”?

Rudi Nyumbani:

Print this post

SIKU ZA WATUMISHI WA MUNGU.

Luka 17:26  “Na kama ilivyokuwa siku za Nuhu, ndivyo itakavyokuwa katika siku zake Mwana wa Adamu. 

27  Walikuwa wakila na kunywa, walikuwa wakioa na kuolewa, hata siku ile Nuhu aliyoingia katika safina, gharika ikashuka ikawaangamiza wote.

28  Na kadhalika, kama ilivyokuwa katika siku za Lutu, walikuwa wakila na kunywa, walikuwa wakinunua na kuuza, wakipanda na kujenga; 

29  lakini siku ile Lutu aliyotoka Sodoma kulinyesha moto na kibiriti kutoka mbinguni vikawaangamiza wote”.

Jina la Bwana wetu Yesu libarikiwe. 

Unabii huo ulitolewa na Bwana wetu Yesu mwenyewe kupitia kinywa chake, haukutolewa kwa kutumia kinywa cha  Mtume Paulo, au Yohana, au Petro au hata Luka mwenyewe aliyekiandika hichi kitabu, bali ni Bwana mwenyewe ndiye aliyeutoa…akilelezea jinsi ujio wake unavyofananishwa.

Katika unabii huo aliufananisha na siku za Nuhu pamoja na za Lutu. Sasa pamoja na mengi aliyoyafananisha kwamba watu watakuwa wakioa na kuolewa (ndoa za jinsia moja), watu watakuwa wakila na kunywa (karamu za ulafi pamoja na ulevi)kama nyakati za Nuhu, pia katika siku za ujio wake watu watakuwa wakiuza na kununua (biashara haramu na za magendo) kama ilivyokuwa nyakati za Lutu

Lakini pamoja na hayo yote ambayo mengi ya hayo yameshatimia..kuna vipengele viwili ningependa tuvione katika mistari hiyo, ambavyo ukiisoma kwa haraka haraka ni rahisi kuvipita tu. Na vipengele hivyo ni 1) KAMA ZILIVYOKUWA SIKU ZA NUHU na 2) KAMA ZILIVYOKUWA SIKU ZA LUTU

Katika vipengele hivyo hakusema “kama zilivyokuwa siku za gharika, au kama zilivyokuwa siku za maangamizi ya moto ya Sodoma na Gomora”..Bali utaona anatumia siku za Nuhu na siku za Lutu…

Sasa Nuhu na Lutu walikuwa ni watumishi wa Mungu.. Kwasababu walionywa na Mungu juu ya maangamizi yanayokuja mbeleni na pia wakapewa nafasi ya kwenda kuwahubiria wengine.

Lutu kabla ya kutolewa Sodoma, alihubiriwa na wale malaika wawili mambo yatakayokwenda kutokea kipindi kifupi mbele na akapewa nafasi ya kwenda kuwahubiria wakwe zake, na ndugu zake pia, ikiwemo mke wake, wanawe wawili na ndugu zake.. Waliokubali ni mke wake pamoja na wanawe wawili, wengine walimwona kama kikaragosi tu kinacholeta habari za mababu.

Mwanzo 19:12 “Basi wale watu wakamwambia Lutu, Je! Unaye mtu hapa zaidi? Mkwe, wanao, na binti zako, na wo wote ulio nao katika mji, uwatoe katika mahali hapa; 

 13 maana tutapaharibu sisi mahali hapa, kwa kuwa kilio chake kimezidi mbele za Bwana; naye Bwana ametupeleka tupaharibu. 

 14 Lutu akatoka akasema na wakweze, waliowaposa binti zake, akasema, Ondokeni mtoke katika mahali hapa kwa sababu Bwana atauharibu mji huu. Lakini akawa kama achezaye machoni pa wakweze”

Vivyo hivyo Nuhu kabla ya kuingia safinani alihubiriwa na Mungu juu ya hukumu itakayokwenda kutokea kipindi kifupi mbele, na pia akapewa nafasi ya kwenda kuwahubiria ndugu zake, lakini waliokubali kuambatana naye ni mke wake na wanawe watatu, pamoja na wake za wanawe, jumla watu 8 tu..wengine wote walimwona kama fundi mbao aliyerukwa na akili.

Hivyo utaona hapa Bwana Yesu anazitaja kama siku ni ZAO.. Na anazifananisha na siku za ujio wake.. Maana yake ni kwamba siku za ujio wake, atawanyanyua watumishi wake mfano wa Nuhu na Lutu kuonya ulimwengu juu ya hukumu ijayo.

Ndugu..hukumu ipo!.. Wakina Nuhu wapo wengi leo, katika kila Taifa na mkoa..(Watumishi wote wanaouonya ulimwengu juu ya siku za mwisho ni wakina Nuhu na Lutu), na hizi ndizo siku zao… “zinaitwa Siku za Hao watumishi” na sio “siku za kuangamizwa dunia”..Lutu alionekana anacheza mbele za wakwe zake.

Kibaya zaidi ni kwamba, watu wengi watakaokuwa wanasikia habari hizo wataoana kama wanacheza tu nao pia, wanapiga ngonjera, wamekosa kazi ya kufanya,.Lakini mwisho utakapowakuta kwa ghafla ndipo watakajuta majuto yasiyoelezeka…

Ukiona unasikia habari za mwisho wa dunia kwa nguvu, jua ndio injili ya kumalizia hiyo, baada ya hapo ni hukumu. Hizi ni siku za mwisho, siku za Watumishi wa Mungu..Na zitaisha!

Je umempokea Kristo? Kwa kutubu na kubatizwa?.. kama bado unasubiri nini?.. Yesu yu karibu kurudi, hivi karibuni hutasikia tena ukiombwa uingie ndani ya safina, hutasikia tena sauti ya Roho Mtakatifu ikikushawishi kutubu..kutakuwa na ukimya nje na ndani, mlango wa Neema utakuwa umeshafungwa, kitakachobakia ni hukumu..

Watu wa kipindi cha Nuhu walisubiri Mungu azungumze nao pengine kwa kutumia jua ndipo waamini, hivyo wakaishia kumdharau Nuhu, vivyo hivyo wa kipindi cha Lutu. Wakati huu ambao watu wanaidharau injili ya kurudi kwa Kristo, hatupaswi kufanana na  wao hata kidogo.

Hivyo ndugu mpokee Kristo leo kama hujafanya hivyo, kisha nenda katafute ubatizo sahihi wa maji mengi (Yohana 3:23) na kwa Jina la YESU, ambalo ndio jina la Baba, mwana na Roho Mtakatifu (Matendo 2:38, Mathayo 28:19), na kuanzia wakati huo Roho Mtakatifu ataingia ndani yako na kukuongoza na kukutia katika kweli yote ya maandiko.. Na utaiepuka hukumu ambayo ipo karibuni kuujilia ulimwengu wote.

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

WANA WA MUNGU, NA BINTI ZA WANADAMU.

SIKU ZA MWISHO WA DUNIA.

Naomba kujua watakaoenda mbinguni je! ni wengi au wachache?

KUTAKUWA NA MATETEMEKO YA NCHI, NJAA NA TAUNI.

JINSI DHAMBI INAVYOMGHARIMU MTU SANA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Daawa ni nini kama tunavyosoma katika biblia?

Daawa ni madai, au mashitaka, malalamiko, au hukumu.

Kwamfano pale mwenzako anapokukosea, au amekudhulumu, au amekutukana au amekufanyia jambo baya, na unataka kwenda kumshitaki , sasa hilo shitaka au madai ndio kwa jina lingine linaitwa  Daawa.

1Wakorintho 6:1 “Je! Mtu wa kwenu akiwa ana daawa juu ya mwenzake athubutu kushitaki mbele ya wasio haki, wala si mbele ya watakatifu?

2 Au hamjui ya kwamba watakatifu watauhukumu ulimwengu? Na ikiwa ulimwengu utahukumiwa na ninyi, je! Hamstahili kukata hukumu zilizo ndogo?

3 Hamjui ya kuwa mtawahukumu malaika, basi si zaidi sana mambo ya maisha haya”?

Unaona, biblia inatushauri sisi kama watakatifu tukiwa na daawa/shitaka juu ya ndugu zetu wa kikristo, hatupaswi kuyapeleka kwa watu wasioamini watusaidie kuamua, badala yake tunapaswa tuyawasilishe mbele ya kanisa, sisi kwa sisi wenyewe tuyaamue, Kwasababu Mungu mwenyewe ametupa jukumu hilo la kuhukumu mambo ya mwili kwa haki, kwasababu hata huko tutakapokwenda tutawahukumu malaika pia biblia inatuambia ..Hivyo basi, hakuna sababu ya kupelekana mahakamani, ili watu waioamini watusaidie kutoa hukumu, wakati sisi wenyewe tupo na tunayo hukumu ya haki zaidi ya wale wengine kule. Hivyo daawa zetu zote, zinapaswa ziamuliwe na kanisa.

Mistari mingine inayoeleza juu ya Neno hili, ni kama ifuatayo:

Ayubu 31:13 “Kama nimeidharau daawa ya mtumishi wangu, au ya kijakazi changu, Waliposhindana nami;

14 Basi Mungu atakapoinuka nitafanya nini? Naye atakapozuru, nitamjibuje?

15 Je! Huyo aliyenifanya mimi ndani ya tumbo, siye aliyemfanya na yeye? Si yeye mmoja aliyetufinyanga tumboni”?

 

Kumbukumbu 16:19 “Usipotoe maamuzi; wala usipendelee uso wa mtu; wala usitwae rushwa; kwa kuwa rushwa hupofusha macho ya wenye akili, na kugeuza daawa ya wenye haki”.

 

Kumbukumbuku 17:8 “Ikiwa limezuka neno lililo zito kukupita wewe, katika maamuzi kati ya damu na damu, na kati ya daawa na daawa, na kati ya pigo na pigo, nayo yashindaniwa katika malango yako; ndipo nawe uondoke, ukwee uende mahali atakapochagua Bwana, Mungu wako”;

Mengine ni hii: (2Samweli 15, Ayubu 5:8, 23:4,29:16,35:14)

Hiyo ndio tafsiri ya Neno hilo, pia angalia tafsiri ya maneno mengine chini..

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Jabari ni nini, kama linavyotumika kwenye biblia?

Areopago ni nini? Kwanini mtume Paulo walimpeleka huko?

MAMBO MENGINE HAYATOKI ISIPOKUWA KWA KUFUNGA.

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 8 (Kitabu cha Ezekieli)

 

TOFAUTI KATI YA HEKALU, SINAGOGI NA KANISA NI IPI?

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!

Rudi Nyumbani:

Print this post

Neno beramu lina maana gani katika biblia?

Beramu ni nini?


Beramu ni jina lingine la neno BENDERA. Hivyo mahali popote kwenye biblia unapolisoma neno hili basi fahamu kuwa linamaanisha bendera.

Hesabu 1:52 “Na wana wa Israeli watazipanga hema zao, kila mtu katika marago yake mwenyewe, kila mtu hapo ilipo beramu yake mwenyewe, kama majeshi yao yalivyo”.,

Vipo vifungu vingi katika biblia, vinavyolitaja neno hili hatuwezi kuvihorodhesha hapa vyote, kwahiyo kama unahitaji kuvijua baadhi yao, basi soma kitabu cha Hesabu sura ile ya pili yote utakutana na Neno hili sehemu kadha wa kadha.

Lakini beramu/bendera sikuzote inasimama badala ya nini?

Tunafahamu kuwa kila bendera tunayoiona mahali fulani imesimamishwa, aidha kwenye mji, au chama, au jamii n.k. huwa  ina maana yake.

Nyingine zimebeba historia ya jamii husika/taifa, nyingine zimebeba tunu, nyingine zinaeleza tabia ya nchi, au vitu vya asili vya nchi n.k.

Hivyo hata rohoni napo, kila mmoja wetu kwa namna moja au nyingi ni lazima atakuwa ameshikilia bendera mojawapo inayomwakilisha yeye.

Na ndio maana leo hii ukienda kwenye mabalozi yote, ni lazima uone bendera ya nchi yake inayoiwakilisha imesimamishwa pale. Hiyo ni kukutambulisha kuwa umefika katika makao ya muda ya nchi ile.

Hivyo mambo yote yahusuyo nchi hiyo huko ugegenini utasaidiwa ukifika pale, huduma zote utapewa sawasawa tu na kama ungekuwa katika nchi yako.

Vivyo hivyo na hapa duniani, kila mmoja wetu ni balozi wa mahali Fulani. Na tunatambuliwa kwa beramu/bendera zetu rohoni.

Ikiwa wewe ni mwenye dhambi, moja kwa moja unapeperusha bendera ya kuzimu, kwa matendo yako maovu, ambayo asili yake ni kuzimu na mkuu wake ni ibilisi.

Lakini kama wewe ni mtakatifu, nawe pia ni lazima upeperushe bendera ya ufalme wa mbinguni kwa matendo yako, ambayo ni lazima yawe ya kumpendeza Mungu, na pili uwe unaihubiri injili(kuwashuhudia wengine habari njema).

Kama hayo mawili huyafanyiki ndani yako na unasema umeokoka, hakuna beramu/bendera yoyote unayoipeperusha ya ufalme wa mbinguni duniani.

Hivyo jitathimini maisha yako ni beramu gani unaipeperusha, katika hichi kipindi kifupi tuliobakiwa nacho hapa duniani. Je, ni ya mbinguni au kuzimu?

Lakini ikiwa leo hii unasema mimi na dhambi basi, nataka Yesu anibadilishe maisha yangu kuanzia leo , nataka anifanye kiumbe kipya nianze na mimi kuipeperusha beramu ya Yesu maishani mwangu. Basi uamuzi huo ni wa busara sana kwako, ambao utaufurahia maisha yako yote. Bwana anasema:

Na uzuri ni kuwa yeye mwenyewe anasema “yeye ajaye kwangu sitamtupa nje kamwe” (Yohana 6:37)..

Hivyo kama upo tayari na umemaanisha  kufanya hivyo leo, basi fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba.>>>KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

https://wingulamashahidi.org/ikabodi-maana-yake-ni-nini/

Jabari ni nini, kama linavyotumika kwenye biblia?

Neno Korbani linamaanisha nini? (Marko 7:11)

Mahuru ndio nini?

UNYAKUO.

Areopago ni nini? Kwanini mtume Paulo walimpeleka huko?

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Naomba kujua nini maana ya kuteguka uvungu wa paja?

SWALI: Yakobo aliposhindana na Malaika alishikwa uvungu wa paja akateguka…Naomba kujua nini maana ya kuteguka uvungu wa paja?

Mwanzo 32:24 “Yakobo akakaa peke yake; na mtu mmoja akashindana naye mweleka hata alfajiri.

25 Naye alipoona ya kuwa hamshindi, alimgusa panapo uvungu wa paja lake; ukateguka uvungu wa paja la Yakobo alipokuwa akishindana naye.

26 Akasema, Niache, niende, maana kunapambazuka. Akasema, Sikuachi, usiponibariki.

27 Akamwuliza, Jina lako n’nani? Akasema, Yakobo.

28 Akamwambia, Jina lako hutaitwa tena Yakobo, ila Israeli, maana umeshindana na Mungu, na watu, nawe umeshinda”.


Jibu: Uvungu wa paja, ni eneo la juu ya paja ambapo mfupa wa paja umekutana na ule wa kiuno. Kama tunavyosoma hapo Yakobo baada ya kushindana na Yule malaika kwa masaa mengi sana usiku kucha bila kuwa na dalili yoyote ya kumwacha, tunaona biblia inatuambia Yule malaika, alimtengua uvungu wa paja lake.

Kumbuka kutegua/kutengua ni tofauti na kuvunja,..Kitu kikivunjwa maana yake ni kinaharibiwa, kinahitaji kuunganishwa, lakini kikitenguka maana yake ni kinahama eneo lililopo kwa muda tu.. Hivyo kwa namna ya kawaida mwanadamu maeneo yote ambayo mifupa miwili inakutana huwa ni rahisi kutenguka, husani pale anapoanguka sehemu ndefu, au kubanwa au kuvutwa kwa nguvu mahali penye maongeo,  kwa mfano goti, au viwiko vya mikono au miguu, vidole, bega au kwenye paja..  Na huwa inaambatana na maumivu makali sana, ambayo maumivu yake yanafanana tu ya yale ya kuvunjika, wakati mwingine yanamfanya mtu asindwe kabisa kutembea kama sio kuchechemea, na mpaka yaishe inaweza kuchukua wiki mbili mpaka tatu au Zaidi.

Sasa Yakobo yeye, alitenguliwa kwenye huu mfupa mkubwa wa paja, ambao ndio mkubwa na maumivu yake ndio  makali kushinda yote.

Lakini kwanini Mungu afanye vile, Ni jambo gani tunajifunza hapo?

Baraka za Mungu ni za kuzipigania, na sio hilo tu, bali pia zinaambatana na maumivu.. Ukitaka Mungu akubariki kubali kukutana na mapigano na maumivu  fulani, Jina la Israeli halikuja hivi hivi, lilikuwa ni la jasho na maumivu. Vivyo hivyo na sisi, tusikubali kuambiwa njoo, ubarikiwe, na huku, hatutaki kusikia gharama za kubarikiwa, ambazo ni kuishi maisha ya kubarikiwa.

Maisha ya kubarikiwa ni kama haya:

Bwana Yesu alisema Mathayo  6:38 “Wapeni watu vitu, nanyi mtapewa; kipimo cha kujaa na kushindiliwa, na kusukwa-sukwa hata kumwagika, ndicho watu watakachowapa vifuani mwenu. Kwa kuwa kipimo kile kile mpimacho ndicho mtakachopimiwa”.

Lakini kama ulichonacho unajilimbikizia wewe tu mwenyewe, Na hapo hapo bado unataka nawe pia ubarikiwe, hilo jambo halipo!. Ipo mifano mingi sana..Ikiwa humtolei Mungu, tena kile kinachokugharimu kabisa, mpaka unaona maumivu rohoni, ni ngumu kubarikiwa na Mungu.

Si wakati wote unahitaji kuomba ili Mungu akuone, unahitaji kufanya zaidi..Pale ulipo unaanza, Mtume Yohana alimwambia Gayo, maneno haya 1Yohana 1:2 “Mpenzi naomba ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya yako, kama vile roho yako ifanikiwavyo”.

Utajiuliza huyu Gayo ni nani, kwanini hakumwandikia kila mtu waraka ule wa mafanikio, bali Gayo tu peke yake, Hivyo ukitaka kujua ni kwanini alimwandikia yeye na si wengine, nenda kasome sura ile yote ujue ni mambo mangapi alijitoa kwa Mungu katika kuwahudumia watakatifu na kuwakaribisha wageni wale waliokuwa wanasafiri kuipeleka injili na kuwapatia mahitaji yao, mpaka sifa zake zikavuma katika kanisa lote.. Hapo ndipo Mtume Yohana kwa uongozo wa Roho Mtakatifu akaongozwa kumwandikia maneno  yale ya baraka.

Lakini hiyo ilikuwa ni mashindano na maumivu makali ya kuinyima nafsi yake.

Vivyo hivyo na sisi, tukumbuke kuwa Baraka za Mungu zitaambatana na kutenguliwa miguu yetu..Kama tupo tayari kwa hayo basi tuingie mapambano, Na tunaingia mapambanoni, sio kwa maneno bali kwa matendo.

Bwana atubariki sote, katika safari yetu ya imani.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

https://wingulamashahidi.org/ushirikina-na-madhara-yake/

NI NANI ATAKAYETUTENGA NA UPENDO WA KRISTO?

Nifanye nini ili niishi maisha ya ushindi siku zote?

Nyamafu ni nini?

“Ninyi ni chumvi ya dunia” Andiko hilo lina maana gani?

HISTORIA YA ISRAELI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Jabari ni nini, kama linavyotumika kwenye biblia?

Jabari maana yake ni mtu hodari, asiyeogopa, shujaa.

Isaya 49:24 “Je! Aliye hodari aweza kunyang’anywa mateka yake, au jeshi lao waliofungwa halali wataokoka?

25 Naam, Bwana asema hivi, Hata jeshi la wafungwa wake aliye hodari watapokonywa mikononi mwake, na mateka yake aliye JABARI wataokoka; kwa maana nitateta na yeye atetaye nawe, nami nitawaletea wana wako wokovu”.

Unaona, Jabari ni mtu shujaa lakini kibiblia kuna majabari wa aina mbili,

  1. Jabari katika kutenda maovu, na katika kutumainia mambo ya mwilini kama vile mali n.k.
  2. Na majabari katika kutenda mema na kuishindania imani, na kuvipiga vita vya kiroho.

 

  • Mfano wa Jabari katika maovu. Ni kama hawa tunaowasoma katika biblia.

Zaburi 52:1Kwa nini kujisifia uovu, EWE JABARI? Wema wa Mungu upo sikuzote.

2 Ulimi wako watunga madhara, Kama wembe mkali, Ewe mwenye hila

3 Umependa mabaya kuliko mema, Na uongo kuliko kusema kweli.

4 Umependa maneno yote ya kupoteza watu, Ewe ulimi wenye hila.

5 Lakini Mungu atakuharibu hata milele; Atakuondolea mbali; Atakunyakua hemani mwako; Atakung’oa katika nchi ya walio hai.

6 Nao wenye haki wataona; Wataingiwa na hofu na kumcheka; 7 Kumbe! Huyu ndiye mtu yule, Asiyemfanya Mungu kuwa nguvu zake. ALIUTUMAINIA WINGI WA MALI ZAKE, NA KUJIFANYA HODARI KWA MADHARA YAKE.

8 Bali mimi ni kama mzeituni Umeao katika nyumba ya Mungu. Nazitumainia fadhili za Mungu milele na milele.

9 Nitakushukuru milele kwa maana umetenda; Nitalingojea jina lako kwa kuwa ni jema; Mbele ya wacha Mungu wako.

  • Lakini majabari katika kuishindania imani ni kama hawa, tunaowasoma katika..

Waebrania 11:33 “ambao kwa imani walishinda milki za wafalme, walitenda haki, walipata ahadi, walifunga vinywa vya simba,

34 walizima nguvu za moto, waliokoka na makali ya upanga. Walitiwa nguvu baada ya kuwa dhaifu, WALIKUWA HODARI KATIKA VITA, walikimbiza majeshi ya wageni.

35 Wanawake walipokea wafu wao waliofufuliwa. Lakini wengine waliumizwa vibaya hata kuuawa, wasikubali ukombozi, ili wapate ufufuo ulio bora;

36 wengine walijaribiwa kwa dhihaka na mapigo, naam, kwa mafungo, na kwa kutiwa gerezani;

37 walipigwa kwa mawe, walikatwa kwa misumeno, walijaribiwa, waliuawa kwa upanga; walizunguka-zunguka wakivaa ngozi za kondoo na ngozi za mbuzi; walikuwa wahitaji, wakiteswa, wakitendwa mabaya;

38 (watu ambao ulimwengu haukustahili kuwa nao), walikuwa wakizunguka-zunguka katika nyika na katika milima na katika mapango na katika mashimo ya nchi.

39 Na watu hao wote wakiisha kushuhudiwa kwa sababu ya imani yao, hawakuipokea ahadi;

40 kwa kuwa Mungu alikuwa ametangulia kutuwekea sisi kitu kilicho bora, ili wao wasikamilishwe pasipo sisi”.

 

Swali ni Je! Wewe ni Jabari katika nini?

Jibu unalo, lakini ikiwa upo katika ouvu, au mambo ya kidunia, basi Yesu anaweza kukufanya kuwa Jabari lake teule ikiwa tu leo utampokea..Ukipomkea  atakusamehe dhambi zako zote, atakufanya kuwa mwana wake,atakuondolea laana zote, atakupa Roho wake Mtakatifu bure, atakupa amani, na kikubwa zaidi atakupa na uzima wa milele .

Unasubiri Nini? Tangu ulipoanza kuitumikia dunia imekupa nini? Hivyo usikawie, ikiwa umedhamiria kwa moyo wako wote, kumkaribisha Yesu katika maisha yako, basi fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Sasa Ikiwa ufuata maaelekezo hayo hapo juu, basi kuanzia sasa wewe ni JABARI la Bwana Yesu. Na utamwona atakavyoanza kutembea na wewe kukutengeneza..

Bwana akubariki.

1Wakorintho 16:13 “Kesheni, simameni imara katika Imani, fanyeni kiume, mkawe hodari”.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Biblia inamaanisha nini inaposema “Tusitweze unabii”?

Baradhuli/Mabaradhuli ni nini au ni nani kwenye biblia?

WINGU KUBWA LA MASHAHIDI.

Areopago ni nini? Kwanini mtume Paulo walimpeleka huko?

NA YEYE ALIYEKETI JUU YA WINGU AKAUTUPA MUNDU WAKE JUU YA NCHI, NCHI IKAVUNWA.

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Baradhuli/Mabaradhuli ni nini au ni nani kwenye biblia?

Baradhuli ni nani/ ni nini kama lilivyotumika kwenye biblia?


Kibiblia Baradhuli ni mtu asiyefaa, mpumbavu sana, aliyevuka mipaka

Ipo mistari kadha wa kadha inayoeleza tabia za watu wabaradhuli. Kwa mfano:

  1. Watu wanaoabudu miungu mingine kwa makusudi mbali na Mungu wa Israeli, muumba wa mbingu na nchi, hao ni mabaradhuli kibiblia.

Wanaokwenda kwa waganga wa kienyeji angali wanajua kabisa wanachokifanya ni kinyuma na mapenzi ya Mungu, wanaofanya uchawi, wanaofanya matambiko n.k. Hao ni mabaradhuli kibiblia.

Kumbukumbuku 13:12 Ukisikia yasemwa habari ya miji yako mmojawapo, akupayo Bwana, Mungu wako, ukae humo, ukiambiwa,

13 Kumetoka katikati yako MABARADHULI kadha wa kadha, wamewapotoa wenyeji wa mji wao, wakisema, Twendeni tukaabudu miungu mingine msiyoijua;

14 ndipo nawe uulize na kutafuta, ukiuliza kwa bidii; nawe angalia, ikiwa kweli, na jambo lile halina shaka, kwamba machukizo mfano wa haya yafanyika katikati yako;

15 hakika yako uwapige wenyeji wa mji ule kwa makali ya upanga, kwa kuwaangamiza kabisa, pamoja na vitu vyote vilivyomo, na wanyama walio humo, kwa makali ya upanga.

  1. Mabaradhuli pia ni watu wanaomwaga damu isiyo na hatia.

Ukisoma kitabu cha Waamuzi utaona Gideoni alikuwa na watoto sabini na wawili, lakini baada ya Gideoni kufa, mtoto wake mmoja aliingiwa na tamaa kutawala sehemu ya Gideoni hivyo akaamua kuwaua ndugu zake wote waliosalia ili yeye afanywe muamuzi badala yake, Ndipo biblia inatuambia alikwenda kuwaajiri watu Mabaradhuli ili kutekeleza adhma yake hiyo ya uuaji,..Hao watu wakashirikiana naye kuwaua ndugu zake wote siku moja juu ya jiwe. (Waamuzi 9:1-5).

  1. Mabaradhuli ni watu wanaofanya vitendo vya ubakaji na ulawiti.

Ukisoma tena kitabu cha Waamuzi 19  utamwona Yule mlawi ambaye alikuwa na suria wake, aliyekwenda kufanya ukahaba, kitendo ambacho kilimpelekea amrudishe nyumbani kwa baba yake, hivyo akakaa kule kwa muda wa miezi 4, ndipo baadaye akaghahiri akaamua amfuate surua wake amrudishe kwake, sasa alipokuwa njiani mji mmoja wa ugenini, alikaribishwa na mzee mmoja wa mji ule. Lakini usiku mambo yalibadilika kwani wale watu wa mji ule wa Benyamini, waliizingira nyumba wakataka wapewe hao wageni walale nao..Kama tunavyoijua habari Yule mlawi akaona ni heri amtoe suria wake wamfanye waliyotaka kumfanya..Wakafanya hivyo mpaka asubuhi baadaye Yule Suria akafa..

Waamuzi 19:22 “Hapo walipokuwa wakifurahisha mioyo yao, tazama, watu wa mji huo, watu MABARADHULI wakaizingira hiyo nyumba pande zote, wakagonga mlango; wakasema na huyo mwenye nyumba, huyo mzee, na kumwambia, Mlete nje mtu yule aliyefika nyumbani kwako, ili tupate kumjua”.

Soma sura yote ya 19,20 na 21, upate picha kamili, na nini kiliendelea baada ya pale..

  1. Mabaradhuli pia ni watu waasi.

Watu wanaoshikamana na viongozi waasi, au waliokosa heshima katika jamii.

2Nyakati 13:7, Waamuzi 11:3.

Je mpaka sasa mabaradhuli wapo?

Unapaswa ujiulize je! tabia mojawapo ya hizo unazo?

Kumbuka kuwa waovu wote, sehemu yao ni katika lile ziwa la moto. Ikiwa wewe ni muuaji, wewe ni baradhuli, ikiwa wewe ni mchawi(unakwenda kwa waganga) wewe ni baradhuli, n.k.

Ufunuo 21:8 “Bali waoga, na wasioamini, na wachukizao, na wauaji, na wazinzi, na wachawi, na hao waabuduo sanamu, na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili”.

Lakini tumaini lipo kwa Yesu tu peke yake. Yeye peke yake ndiye anayeweza kuyageuza maisha yako na kukusaheme kabisa kabisa. Na kukufanya kuwa mwana wake.

Je! unahitaji kuokoka leo?

Unahitaji Yesu ayabadilishe maisha yako leo?

Unahitaji kupokea Roho Mtakatifu?

Biblia inasema..

Isaya 1:18 “Haya, njoni, tusemezane, asema Bwana. Dhambi zenu zijapokuwa nyekundu sana, zitakuwa nyeupe kama theluji; zijapokuwa nyekundu kama bendera, zitakuwa kama sufu.

19 Kama mkikubali na kutii mtakula mema ya nchi”;

Kama ndivyo basi fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Bwana akubariki.

Mada Nyinginezo:

MWEZI WA ABIBU/NISANI NI MWEZI GANI?

Arabuni maana yake ni nini?

LAKINI USIKU WA MANANE, PAKAWA NA KELELE.

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Areopago ni nini? Kwanini mtume Paulo walimpeleka huko?

Areopago ni nini?


Areopago ni baraza kuu la Waathene au mahali walipokutanika wakuu wa Athene. Kwa ajili ya kuzungumza mambo mbalimbali ya muhimu,kama vile kusikiliza   kesi zinazohusiana na mauaji au dini,  au kutoa hukumu, au kuchambua mambo mengine yenye uzito katika jamii.

Eneo hili lilikuwa upande wa kaskazini magharibi mwa mji wa Athene,Ukigiriki, na lilijengwa ya juu ya mwamba mkubwa.

Baraza hili, lilifanana na lile baraza la wayahudi ambalo, wazee pamoja na kuhani mkuu walikuwa wanakutanika kutoa mashahuri juu ya kesi za kidini, kama vile ilivyokuwa wakati wa Bwana Yesu (Mathayo 26:57-68)

Sasa Mtume Paulo alipofika katika mji huu na kuanza kuhubiri, tunaona baada ya habari zake kusikika sana katikati ya jamii ya waethene, walimkamata na kumpeka mbele ya baraza hili kuu (Areopago) ili kumsikiliza vizuri juu ya imani yake.

Tusome:

Matendo 17:16 “Paulo alipokuwa akiwangojea huko Athene na kuona jinsi mji ule ulivyojaa sanamu, roho yake ilichukizwa sana ndani yake.

17 Basi katika sinagogi akahojiana na Wayahudi na waliomcha Mungu, na wale waliokutana naye sokoni kila siku.

18 Na baadhi ya Waepikureo na Wastoiko, wenye ujuzi, wakakutana naye. Wengine wakasema, Mpuzi huyu anataka kusema nini? Wengine walisema, Anaonekana kuwa mtangaza habari za miungu migeni, kwa maana alikuwa akihubiri habari za Yesu na ufufuo.

19 Wakamshika, wakamchukua AREOPAGO, wakisema, Je! Twaweza kujua maana ya elimu hii mpya unayoinena?

20 Kwa maana unaleta mambo mageni masikioni mwetu, tutapenda kujua, basi, maana ya mambo haya.

21 Kwa maana Waathene na wageni waliokaa huko walikuwa hawana nafasi kwa neno lo lote ila kutoa habari na kusikiliza habari za jambo jipya.

22 Paulo akasimama katikati ya AREOPAGO, akasema, Enyi watu wa Athene, katika mambo yote naona ya kuwa ninyi ni watu wa kutafakari sana mambo ya dini.

23 Kwa sababu nilipokuwa nikipita huko na huko na kuyaona mambo ya ibada yenu, naliona madhabahu iliyoandikwa maneno haya, KWA MUNGU ASIYEJULIKANA. Basi mimi nawahubirini habari zake yeye ambaye ninyi mnamwabudu bila kumjua……

32 Basi waliposikia habari za ufufuo wa wafu wengine walifanya dhihaka; wengine wakasema, Tutakusikiliza tena katika habari hiyo.

33 Basi hivi Paulo akaondoka akawaacha.

34 Baadhi ya watu wakashikamana naye, wakaamini; katika hao alikuwamo Dionisio, MWAREOPAGO, na mwanamke mmoja jina lake Damari, na watu wengine pamoja na hao”.

Kama tunavyoona wapo miongoni mwa hao wakuu wa baraza wapo waliodhihaki, na wapo walioamini kama vile huyo Dionisio mwareopago.

Je Ma-areopago yanaendelea mpaka sasa?

Ndio, Hata sasa katika agano jipya ma-areopago yapo mengi, Bwana Yesu alishayazungumzia na kuonya kuwa watakatifu watakutana nayo katika safari zao za Imani, na katika kuhubiri injili.. Lakini Bwana Yesu alitupa kanuni ya kusimamia, akasema hivi;

Mathayo 10:17 “Jihadharini na wanadamu; kwa maana watawapeleka mabarazani, na katika masinagogi yao watawapiga;

18 nanyi mtachukuliwa mbele ya maliwali na wafalme kwa ajili yangu, kuwa ushuhuda kwao na kwa mataifa.

19 Lakini hapo watakapowapeleka, msifikiri-fikiri jinsi mtakavyosema; maana mtapewa saa ile mtakayosema.

20 Kwa kuwa si ninyi msemao, bali ni Roho wa Baba yenu asemaye ndani yenu”.

Hivyo, kama umeokoka,au unahubiri injili na ukajikuta umewekwa katikati ya viongozi wa dini, hupaswi kuogopa Areopago lolote..Kwasababu Bwana ameahidi kuwa na wewe.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

KWA MUNGU ASIYEJULIKANA.

SIRI YA KUFANIKIWA KWA MTUME PAULO.

JIFUNZE KULIGAWANYA VYEMA NENO LA MUNGU.

Israeli ipo bara gani?

Mto Frati upo nchi gani, Umuhimu wake katika biblia ni upi?

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

Rudi Nyumbani:

Print this post

MAASI KUONGEZEKA NI ISHARA YA NINI?.

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe..Ni neema Bwana katujalia kuliona jua tena siku ya leo, karibu tuyatafakari maandiko Pamoja..

Kama tunavyojua tunaishi katika siku za mwisho, na kila dakika inayosogea mbele ndivyo tunavyozidi kuusogelea ule mwisho…Hivyo leo tu tayari tumeshapunguza siku nyingine moja, kati ya zile chache zilizobakia mbele yetu, kuufikia ule mwisho.

Lakini Pamoja na hayo biblia inatuonya kuwa mojawapo ya dalili za kurudi kwa pili kwa Kristo ni kuongezeka kwa MAASI NA MAARIFA. Leo hatutazungumzia sana juu ya kuongezeka kwa maarifa, kama utapenda kufahamu juu ya hilo basi utatutumia ujumbe inbox tukutumie somo lake. Lakini leo tutaangalia juu ya kuongezeka kwa MAASI,(Mathayo 24:12) ambapo tutajifunza kitu cha muhimu sana. Na pia nakushauri kabla ya kusoma somo hili, tenga muda pitia somo fupi lililotangulia kabla ya hili lenye kichwa kinachosema “Usiseme, Kwani siku za kale kupita siku hizi? Maana si kwa hekima uulizavyo neno hilo?” kwasababu linamahusiano mkubwa sana na hichi tutakachokwenda kujifunza leo.

Ukiyatafakari Maisha ya leo unaweza kusema, ni afadhali na jana na juzi kuliko leo kwa jinsi maasi yanavyozidi kuongezeka…Upendo wa wengi unapoa, mauaji yanaongezeka, chuki zinaongezeka, visasi, ubinafsi, wizi, uasherati na kila aina ya uchafu, unazidi kuongezeka…

Hiyo yote ni ishara ya kurudi kwa pili kwa Kristo, Lakini swali la kujiuliza ni je!.. kwanini ishara ya mabaya ndio iwe dalili ya kurudi kwa Yesu, na si Ishara ya mazuri, yaani kwanini Bwana Yesu asingesema kabla ya kurudi kwake Mema yataongezeka sana?.

Jibu ni kwamba…wakati wa Kristo kurudi, (yaani kipindi kifupi kabla ya kutokea mawinguni) Kiwango cha utakatifu cha watakatifu kitakuwa kipo juu sana.. Na ishara mojawapo ya kuwa kiwango cha utakatifu kimekuwa kikubwa ni kiwango cha maovu kuwa kikubwa.

Ndugu unapoona dhambi zimezidi mipaka, jua kuwa sehemu Fulani mema yamezidi sana… Inaweza isiwe ni watu wengi wanatenda hayo mema, lakini hata kama ni mmoja tu! Basi atakuwa anatenda mema kwa kiwango kikubwa..

Wengi hawalioni hili wakifikiri kwamba kwasababu dhambi ni nyingi katika kipindi hichi basi hakuna kabisa watu wanaompendeza Mungu. Usilisahau hilo siku zote (Maovu kuwa juu ni ishara ya utakatifu pia kuwa juu). Ukiona kuna maasi makubwa sana katika mji fulani jua upande mwingine katika mji huo huo kuna wakamilifu au mkamilifu wa kiwango kikubwa sana.

Wakati Mungu amechukizwa na maasi ya Sodoma na Gomora, wakati huo huo Mungu alikuwa amependezwa sana na mtu mmoja aliyeitwa Ibrahimu, ambaye tunamwita sasa Baba wa Imani, Hivyo Ishara ya maasi kuongezeka Gomora ni ishara ya wema kuongezeka kwa mtu Fulani wa Mungu mahali fulani. Ukiona dunia inazidi kuoza sasa, jua ni ishara kuwa kuna watakatifu mahali Fulani wanazidi kujitakasa sana.

Ukiona sasa hivi kuna wanawake wengi wanaotembea nusu uchi barabarani, na hata wanaingia makanisani wakiwa hivyo… usifikiri ni wote wapo hivyo…Hiyo ni ishara ya kuiogopa sana, kwasababu ni ishara kuwa kuna mwanamke/wanawake mahali Fulani wanaojiheshimu na kujisitiri sana, na kumheshimu Mungu kwa viwango vya kimbinguni..

Unapoona kuna wimbi la manabii wa uongo..ni jambo la kuogopa wala sio la kucheka na kudharau, kwasababu hiyo ni ishara kwamba kuna kuna watumishi wa Mungu wa kweli. Biblia inasema katika siku za mwisho magugu na ngano vyote vitakomaa.. hivyo ukiona shambani magugu yamekomaa jua na ngano pia zimekomaa…Ndio maana mavuno yanakuja.

Hata Maisha ya kawaida yanatufundisha..Ijapokuwa miaka hii watu wanaonekana duniani kuwa dhaifu, na magonjwa kuongezeka na uwezo kupungua…lakini ukifuatilia rekodi, utagundua kuwa bado zinavunjwa kila mwaka.

Mtu mwenye mbio kuliko wote anaishi miaka yetu hii hii ambayo watu wanakula vibaya, watu wana magonjwa sana n.k. kumbe katikati ya kizazi ambacho watu ni wadhaifu watakuwepo watu ambao ni Hodari kuliko wote katika historia?.

Na katika Imani ni hivyo hivyo…Katikati ya maovu ya dunia yaliyokithiri, Bwana anao watu wake walio waaminifu, wakati wa mfalme Ahabu ambapo Yezebeli mke wake aliifanya Israeli kuwa nchi ya kichawi kiasi kwamba manabii wote waliouliwa, lakini mahali Fulani alikuwepo Eliya Mtishbi, na kama hiyo haitoshi walikuwepo pia manabii wengine 7000 ambao hakupigia goti baali katika mji, Bwana aliojisazia.. Hivyo ndugu huu sio wakati wa kusema aaah! dunia imeharibika yote, hivyo na mimi lazima niwe mwovu…au aaah siku hizi hakuna watakatifu hivyo hakuna haja ya mimi pia kujitakasa..n.k Usikubali kuusikiliza huo ni uongo wa shetani ambao upo kama KILEVI, shetani anawalevya watu wote wa ulimwengu, wafikiri kwamba hali inafanana kila mahali na kwa kila mtu.

Likumbuke hili neno.. Mhubiri 7:10 “Usiseme, Kwani siku za kale kupita siku hizi? Maana si kwa hekima uulizavyo neno hilo”.?

Bwana atusaidie tufumbuke macho..na tuzidi kujitakasa. Maadamu wakati siku ile inakaribia.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312


 

Mada Nyinginezo:

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

MAONO YA NABII AMOSI.

Wanaowachukua wanawake wajinga mateka ni akina nani?

YONA: Mlango wa 4

UFUNUO: Mlango wa 3 part 3

Rudi Nyumbani:

Print this post

Ibada ni nini,Na je ili ikamilike inapaswa iwe na nini na nini?

SWALI: Ibada ni nini, Na je ili ibada ikamilike inapaswa iwe na nini na nini? Na je ni siku gani maalumu ya kufanya ibada?


Ibada ni kitendo chochote kifanywacho kuonyesha unyenyekevu wa hali ya juu, utiifu, heshima, shukrani,  na utukufu, aidha  kwa Mungu au kitu kingine, na hiyo inaambata na mambo kadha wa kadha, ikiwemo kusifu, kuabudu, kusujudu, kuimba, kufunga, kutoa sadaka, na kushiriki maagano ya imani, Na vilevile kujitoa mwili wako kuvitumikia, hiyo nayo ni ibada kamili.

Kibiblia kuna ibada za aina tatu

  1. Ibada kwa Mungu.
  2. Ibada kwa shetani.
  3. Na ibada za wanadamu walizojitungia wenyewe kwa Mungu.
  1. Tukianzana na ibada kwa Mungu:

Hizi, ni zote tuzifanyazo aidha kanisani au manyumbani kwetu wenyewe, tunapokutana kumwimbia na kumwabudu Mungu, au kumshukuru, au kushiriki meza ya Bwana, hiyo tayari ni ibada kwa Mungu.

Matendo 13:2 “Basi hawa walipokuwa wakimfanyia Bwana ibada na kufunga, Roho Mtakatifu akasema, Nitengeeni Barnaba na Sauli kwa kazi ile niliyowaitia”.

Na kama tulivyosema awali hata kujitoa mwili wako kwa ajili ya kutenda matendo yote yampendezayo Mungu ni ibada kamili tayari..

Warumi 12:1 “Basi, ndugu zangu, nawasihi, kwa huruma zake Mungu, itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, ya kumpendeza Mungu, ndiyo ibada yenu yenye maana”.

  1. Ibada kwa Shetani.

Hizi kwa jina lingine ndio ibada za sanamu. Ambazo biblia imezikemea sehemu nyingi sana katika biblia. Unapokwenda kuisujudia sanamu yoyote ile, iwe na mfano wa mtakatifu Fulani mbinguni, tayari hiyo ni ibada kamili  ya sanamu.. Inayomtia Mungu wivu wa kukuangamiza haraka sana.

Kutoka 20:4 “Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu cho chote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini duniani, wala kilicho majini chini ya dunia.

5 Usivisujudie wala kuvitumikia; kwa kuwa mimi, Bwana, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu; nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao,

6 nami nawarehemu maelfu elfu wanipendao, na kuzishika amri zangu”.

1Wakorintho 10:14 “Kwa ajili ya hayo, wapenzi wangu, ikimbieni ibada ya sanamu”.

 Lakini kama hilo halitoshi, unaweza pengine ukawa husujudii masanamu, lakini mwili wako unafanya maasi, hiyo nayo ni ibada kamili ya sanamu sawasawa na kusujudia vinyago.

Wakolosai 3:5 “Basi, vifisheni viungo vyenu vilivyo katika nchi, uasherati, uchafu, tamaa mbaya, mawazo mabaya, na kutamani, ndiyo ibada ya sanamu”;

  1. Ibada watu walizojitungia wenyewe kwa Mungu:

Hizi ni ibada ambazo, hazitokani na Mungu wala shetani, bali zinatokana na watu wenyewe, wamejitungia wakidhani kuwa wanamfanyia Mungu, kumbe wanafanya kimakosa..

Wakolosai 2:20 Basi ikiwa mlikufa pamoja na Kristo mkayaacha yale mafundisho ya awali ya ulimwengu, kwa nini kujitia chini ya amri, kama wenye kuishi duniani,

21 Msishike, msionje, msiguse;

22 (mambo hayo yote huharibika wakati wa kutumiwa); hali mkifuata maagizo na mafundisho ya wanadamu?

23 Mambo hayo yanaonekana kana kwamba yana hekima, KATIKA NAMNA YA IBADA MLIYOJITUNGIA WENYEWE, na katika kunyenyekea, na katika kuutawala mwili kwa ukali; lakini hayafai kitu kwa kuzizuia tamaa za mwili.

Na zina madhara yake makubwa, kwasababu wakati mwingine zinasababisha hata watu waue watu wengine wakidhani kuwa ndio wanampendeza Mungu, kama tu walivyokuwa wanafanya Warumi na Wayahudi kwenye kanisa la kwanza, na jinsi zinavyofanywa na baadhi dini leo hii duniani kuchinja watu. Zote hizo ni ibada ambazo watu wamejitungua lakini hazitokani na Mungu.

Yohana 16:2 “Watawatenga na masinagogi; naam, saa yaja atakapodhania kila mtu awauaye ya kuwa ANAMTOLEA MUNGU IBADA.

Hivyo kwa kuhitimisha ni kuwa, ibada halisi ni moja tu, nayo ni kwa Mungu muumba wa mbingu na nchi (YEHOVA), na Kristo wake aliyesulibiwa kwa ajili ya dhambi zetu sisi wanadamu. Na maagizo pekee ya ibada hiyo halisi yanapatikana katika biblia tu.. Ibada nyingine yoyote tofauti na hiyo, ni machukizo makubwa kwake.

Na pia tunaikamilisha kwa miili yetu kama biblia inavyotufundisha, kwa kuishi maisha yampendezayo Bwana, ndio ibada yenye maana, ikiwa tutakuwa tunahudhuria kanisani kila siku, tunamwabudu Mungu usiku na mchana, tunamtolea matoleo mengi, tunashiriki meza ya Bwana kila wiki halafu matendo yetu, au miili yetu tumeiuza kwa shetani, ibada zetu bado ni batili..Zinakuwa ni ibada za sanamu, au ibada tulizojitungia tu sisi wenyewe.

Lakini kama utayakamilisha yote ya rohoni na mwilini, basi ibada hiyo  inafaa sana mbele za Mungu, na inathawabu nyingi sana. Wanaomfanyia Mungu ibada kamili wanakuwa marafiki wa karibu sana Mungu.

Na pia hakuna siku maalumu ya kumfanyia Mungu ibada, kwani ibada yetu halisi ipo rohoni, hivyo wakati wowote na muda wowote uwapo na nafasi inaingia uweponi mwa Mungu, kumsifu, kumshukuru, kumwabudu, kumtolea dhabihu za shukrani n.k.. Lakini pia ipo ibada ya watakatifu wote, ambayo inafanyika kila juma, hivyo ikiwa ni jumapili au Jumamosi, inapaswa ifuatwe. Kama tulivyoambiwa tusiache kukutanika pamoja..

Bwana wetu atusaidie sote, tuweze kuyakamilisha hayo.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

USILETE UJIRA WA KAHABA, NYUMBANI KWA MUNGU.

Nyama zilizosongolewa ni zipi?Je kunywa damu ni dhambi?

JE KUVAA PETE NI DHAMBI?

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!

CHAPA YA MNYAMA

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

LAKINI USIKU WA MANANE, PAKAWA NA KELELE.

Rudi Nyumbani:

Print this post