Ukiangalia ujenzi wa kwanza wa hekalu na ule wa pili utaona kuna utofauti fulani, Kwanza ule wa kwanza uliojengwa na mfalme Sulemani, ulikuwa ni wa utajiri mwingi, ambao ulikuwa tayari umeshakusanywa na Daudi baba yake Sulemani huko nyuma, pili ulikuwa ni wa amani, na utulivu, kiasi kwamba hata siku ile unapokamilika hakukusikika kelele wala sauti ya nyundo (1Wafalme 6:7).. Lakini ujenzi wa hekalu la pili ambalo lilibomolewa na mfalme Nebukadneza, ulikuwa ni wa shida sana, ulikuwa ni wenye vikwanzo vingi sana, vilevile uliozungukwa na maadui wengi, ili kukwamishwa tu Hekalu lile lisijengwe.
Ni kawaida ya shetani huwa akishajua jambo fulani au ujenzi fulani unafanyika, ambao utaleta madhara makubwa katika ufalme wake huko mbeleni, au utakuwa na utukufu mkubwa Zaidi wa Mungu ni lazima alete vipingamizi vingi..Na ndivyo ilivyokuwa katika ujenzi huu, Mungu aliwaambia wayahudi kuwa utukufu wa nyumba hiyo ya pili utakuwa ni mkuu kuliko ule wa nyumba ya kwanza (Hagai 2:9). Hivyo shetani kulijua hilo akanyanyua vipingamizi vingi sana.
Na miaka kadhaa tu kabla ujenzi huo haujaanza Mungu alishamwonyesha Danieli jinsi utakavyokuwa wa shida na mgumu.
Danieli 9:25 ‘Basi ujue na kufahamu, ya kuwa tangu kuwekwa amri ya kutengeneza na kuujenga upya Yerusalemu hata zamani zake masihi aliye mkuu; kutakuwa na majuma saba; na katika majuma sitini na mawili utajengwa tena pamoja na njia kuu zake na handaki, naam, KATIKA NYAKATI ZA TAABU’.
Hivyo Zeruababeli na Yoshua walipooanza kuijenga nyumba, mwanzoni tu wakakumbana na mikono ya maadui zao, wakawatisha wasiijenge, mpaka wakaenda kuomba kibali kutoka kwa mfalme, kazi hiyo isiendelee, mpaka baada ya miaka mingi kupita Mungu anawanyanyua tena mioyo yao na kuwaambia waanze kazi wasiogope.,Ndipo Mungu akawa pamoja nao na kuimaliza.
Lakini baada tena muda mrefu kupita hapo tayari hekalu limeshakamilika, shetani hakupumzika alilivamia tena hekalu, na kuharibu kuta zake, hapo ndipo tunaona Mungu akimnyanyua mtu mwingine aliyeitwa Nehemia, ili kuzisimamisha tena kuta za mji na kulikarabati hekalu, lakini mambo hayakuwa maraisi kama ilivyokuwa.
Maadui waliwalemea wakina Nehemia, ukipata nafasi pitia mwenyewe kitabu cha Nehemia usome jinsi walivyopata tabu..Mpaka ikafikia wakati sasa, kila mjenzi anabidi ajifunze na ujuzi mwingine wa ziada..Kwamba sio tu kujenga, bali pia kulinda..Kila mjenzi alilazimika kubeba silaha zake mgongoni, na wakati huo huo alikuwa anajenga..ili kwamba ikitokea tu maadui zao wamewavamia wakati wowote, basi wawezi kupambana nao. Na wengine walikuwa wakipokezana..wakati wanajenga wengine wanalinda.
Nehemia 4:16 “Ikawa tokea wakati huo, nusu ya watumishi wangu walitumika katika kazi hiyo, na nusu yao wakaishika mikuki, na ngao, na pinde, na darii; na maakida walikuwa nyuma ya nyumba yote ya Yuda.
17 Watu wale walioujenga ukuta, na wale waliochukua mizigo, walijitweka wenyewe, kila mtu alifanya kazi kwa mkono mmoja, na kwa mkono wake wa pili alishika silaha yake;
18 nao wajenzi, kila mtu alikuwa na upanga wake, umefungwa ubavuni mwake, ndivyo alivyojenga. Na yeye aliyepiga baragumu alikuwa karibu na mimi.
19 Nikawaambia wakuu, na mashehe na watu wengine; Kazi hii ni nyingi, tena kubwa, nasi tumetawanyika juu ya ukuta, kila mtu mbali na mwenzake;
20 basi mahali po pote mtakaposikia sauti ya baragumu, enendeni huko, mkatujie; Mungu wetu atatupigania.
21 Hivyo tukajitia kAtika kazi hiyo; na nusu yao waliishika mikuki, tangu alfajiri hata nyota zikatokea.
22 Kadhalika, wakati ule ule, nikawaambia watu, Kila mtu na akae ndani ya Yerusalemu pamoja na mtumishi wake, wapate kuwa walinzi wetu wakati wa usiku, na kufanya kazi wakati wa mchana.
23 Basi mimi, na ndugu zangu, na watumishi wangu, na watu wa ulinzi walionifuata, hatukuvua nguo zetu hata mmoja; kila mtu alikwenda kuteka maji akichukua silaha yake.
Sasa hilo lilikuwa ni hekalu la kimwili linapitia changamoto hizo, vipi kuhusu hekalu la Mungu la rohoni..ambalo ni kanisa lake? (2Wakorintho 6:16)..Tukisema kanisa hatumaanishi jengo hapana bali tunamaanisha waliomwamini Kristo..maana hiyo ndiyo tafsiri yake.. Shetani ataleta mapambano na Zaidi ya mapambano.. Kanisa la Mungu halisimami kirahisi rahisi kama wengi wanavyodhani, shetani hawezi kutulia kuangalia tu watu wanaokoka wanamfuata Kristo, wanapata uzima wa milele na asilete vipingamizi vingi..
Na hapo ndipo tunapolazimika kuvaa silaha zote za Injili kama tunavyozisoma katika Waefeso 6 ili tuweze kumpinga adui..Na silaha mojawapo ni MAOMBI.
Waefeso 6:18 ‘kwa sala zote na maombi mkisali kila wakati katika Roho, mkikesha kwa jambo hilo na kudumu katika kuwaombea watakatifu wote;
19 pia na kwa ajili yangu mimi, nipewe usemi kwa kufumbua kinywa changu, ili niihubiri kwa ujasiri ile siri ya Injili;
20 ambayo kwa ajili yake mimi ni mjumbe katika minyororo; hata nipate ujasiri katika huyo kunena jinsi inipasavyo kunena’.
Unaona, mstari wa 19 na 20 Mtume Paulo hakuona aibu kuomba aombewe..Vivyo hivyo na watumishi wote wa Mungu hata sasa tunahitaji maombi yako ili kazi ya Mungu isikwamishwe na hila zote za shetani. Hata sisi tunaoandika masomo haya mitandaoni tunaomba maombi yenu sana..kwasababu ni vipingamizi vingi sana tunakumbana navyo..wakati mwingine shetani anaharibu vifaa tunavyotumia kuandika masomo haya, inatugharimu tutumie hivyo hivyo tu kwa shida…Wakati mwingine unapomaliza tu kuandaa na kutaka ku-post ibilisi anaharibu network nzima lakini kwa upande wa masomo tu, inaweza kukuchua hata masaa 2 au zaidi ku-post somo moja tu, lakini cha ajabu wakati huo huo network iko vizuri unapofungua kurasa nyingine, wakati mwingine unapanga ufanye hichi au kile cha kiMungu lakini kinanyanyuka hiki au kile kukukwamisha..Na changamoto nyingine nyingi tu ambazo huwezi kutaja moja moja hapa..Hivyo kwa nje mambo yanaweza kuonekana yapo vizuri lakini nyuma kuna vita vingi sana vinaendelea..
Hivyo maombi yako, yana mchango mkubwa sana kwetu na kwa wengine, na kwa ajili ya injili ya Mungu isonge mbele..Sisi wenyewe hatuwezi, hivyo tuombeane sote..Adui yetu shetani anapoona watu wengi wanamgeukia Mungu hawezi kutulia.
Hakuna silaha nyingine tutakayoweza kumshinda shetani Zaidi ya maombi.
1Wathesalonike 5:25 “Ndugu, tuombeeni”
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii 0789001312Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group
Mada Nyinginezo:
KAMA MHUBIRI NI WOKOVU UPI UNAUPELEKA KWA WATU?
UFUNUO: Mlango wa 11
DANIELI: Mlango wa 9
WALE WAZEE ISHIRINI NA WANNE (24), WANA KAZI GANI?
Nifanye nini ili niondokane na Hofu maishani mwangu?
HATA NA BARNABA PIA AKACHUKULIWA NA UNAFIKI WAO!!
JE KUJIUA NI DHAMBI?
Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe…
Tunasoma Bwana wetu Yesu Kristo alipoanza huduma yake alianza peke yake…lakini akiwa katikati ya huduma hiyo, kama wengi wetu tunavyojua aliwatafuta wanafunzi ambao hao baada ya yeye kuondoka wataiendeleza kazi aliyokuwa anaifanya yeye. Aliona kuwa mavuno ni mengi na yeye peke yake hatoshi inahitajika jeshi kubwa. Hivyo aliwatafuta wanafunzi wengi sana…idadi yao haijulikani lakini ni wengi…Miongoni mwa hao wanafunzi wengi aliokuwa nao akawatenga mitume 12..Kwaajili ya madarasa maalumu…Kuna mambo ambayo mitume 12 walikuwa wanaambiwa na Bwana ambayo wanafunzi wengine walikuwa hawaambiwi..
Lakini ilifika kipindi Mitume wakapelekwa mazoezini kama vile wanafunzi wa vyuoni wanavyopelekwa field leo..Bwana aliwatuma wazunguke kila mahali, watoe pepo wafufue wafu n.k…lakini na hiyo Bwana aliona haitoshi pia akawaagiza tena wanafunzi wengine 70 waende wakafanye kazi zile zile za Mitume 12..
Luka 10:1 “Basi, baada ya hayo Bwana aliweka na wengine, sabini, akawatuma wawili wawili wamtangulie kwenda kila mji na KILA MAHALI ALIPOKUSUDIA KWENDA MWENYEWE.
2 Akawaambia, Mavuno ni mengi, lakini watenda kazi ni wachache; basi mwombeni Bwana wa mavuno apeleke watenda kazi katika mavuno yake”.
Sasa nataka tuone huo mstari unaosema “wamtangulie kwenda kila mji na kila mahali alipokusudia kwenda mwenyewe”.
Kuna mahali ambapo Kristo anakusudia kwenda mwenyewe lakini anatutuma sisi tuende kwa niaba yake….Kumbuka hatuendi mahali sisi tunapotaka kwenda bali yeye alipokuwa anataka kwenda mwenyewe…Ikiwa na maana kuwa tunakwenda kutimiza kusudi, na malengo ya mtu mwingine…Na sio malengo yetu. Sisi ni mawakili tu..Ni sawa Raisi amtume mtu fulani amwakilishe kwenye sherehe fulani aliyoalikwa kwenye Taifa lingine…Yule aliyetumwa ni mwakilishi tu…anapeleka pongezi, au shukrani au maombi kwa niaba ya yule aliyemtuma…hana la kuongeza wala la kupunguza kutoka kwenye nafsi yake mwenyewe.
Kadhalika tunapokuwa wakristo sisi ni wa wakilishi wa Yesu Kristo mahali tunapotumwa…Hatuna hati miliki ya injili, hivyo tunapaswa tuseme kile anachotaka sisi tukiseme..tunapaswa tufikie malengo yale anayotaka yeye afikie…Kwa ufupi tufanye kazi ile ile ambayo angekuwa yeye yupo hapo angeifanya.
Lakini tunapokuwa wakristo halafu hatuifanyi kama anavyotaka yeye…maana yake sisi ni waasi. Mtu asiyekuwakilisha vyema kama ulivyomwambia akuwakilishe maana yake huyo mtu tayari kashakuwa adui yako. Unakwenda na kuwahubiria watu injili ambayo Yesu Kristo hakuihubiri ni kujitafutia laana badala ya baraka..Biblia inasema hivyo katika..
Wagalatia 1:6 “Nastaajabu kwa kuwa mnamwacha upesi hivi yeye aliyewaita katika neema ya Kristo, na kugeukia injili ya namna nyingine.
7 Wala si nyingine; lakini wapo watu wawataabishao na kutaka kuigeuza injili ya Kristo.
8 Lakini ijapokuwa sisi au malaika wa mbinguni atawahubiri ninyi injili yo yote isipokuwa hiyo tuliyowahubiri, na alaaniwe.
9 Kama tulivyotangulia kusema, na sasa, nasema tena, mtu awaye yote akiwahubiri ninyi injili yo yote isipokuwa hiyo mliyoipokea, na alaaniwe”.
Bwana Yesu alihubiri toba na ubatizo lakini wewe unasema hayo sio ya msingi..hapo unajitafutia laana…Bwana Yesu alihubiri kwamba tusishindane na mtu mwovu, tuwaombee wale wanaotuudhi, na tuwapende adui zetu..wewe unahubiri mlaani adui yako na mchukie anayekuchukia..Bwana Yesu alifundisha kwamba tusilale usingizi bali tukeshe katika roho nasi tuwe kama watu wanaomngojea yeye..Wewe unahubiria watu na kuwawekea mazingira ya kuzidi kuzama katika ulimwengu,..Bwana Yesu alihubiri mtu amwachaye mkewe na kwenda kuoa mwingine azini..wewe unafungisha ndoa za watu waliowaacha waume wao au wake zao, Bwana Yesu alifundisha kutawadhana miguu ni jukumu la Kila mwamini, lakini wewe unafundisha ule ulikuwa ni mfano tu wa rohoni n.k.
Je hayo unayoyahubiri Kristo angekuwa yupo hapo angewahubiria watu hayo unayoyahubiri wewe?..angewavumilia watu wanaowaacha wake zao na kwenda kuoa wengine?…angekuwa anafanya fanya mizaha unayofanya fanya leo madhabahuni au unapotumika? comedy..je angewahubiria watu waje kupokea magari na majumba na huku wanaangamia kwa uasherati wao na anasa zao?…
Je wewe ni mwakilishi mwema?..Bwana atusaidie tuwe wawakilishi wema kila siku katika kazi yake.
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255789001312
Mada Nyinginezo:
HATARI YA KUHUBIRI INJILI TOFAUTI NA ILIYOANDIKWA KWENYE BIBLIA.
KWA VILE ALIVYOKUWA MTU WA HAKI.
Utii ni nini? na ni nani tunayepaswa kumtii au kutokumtii?
LOLOTE ATAKALOWAAMBIA FANYENI.
Mitume wote waliopita walikuwa ni watu weupe hata manabii wote waliopita hadi Ma-papa ni ngozi nyeupe. ni kweli ngozi nyeusi ililaaniwa ?
CHUKIZO LA UHARIBIFU
CHAPA YA MNYAMA
Shalom, Jina la Mfalme mkuu Yesu Kristo libarikiwe.
Nakukaribisha katika kuyatafakari maandiko, Kama vile Paulo alivyomwambia Timotheo “Hata nitakapokuja, ufanye bidii katika kusoma..”(1Timotheo 4:13)..Nasi pia tunapaswa tuonyeshe bidii hiyo hiyo katika kusoma Neno la Mungu kwasababu kila siku yapo mambo mapya Mungu anahitaji tuyaone.
Hivyo, leo tutajifunza juu ya mtume mmoja wa kipekee kidogo anayeitwa Mathiya. Mtume huyu hatumsomi mahali pengine popote katika vitabu vya injili isipokuwa katika kitabu cha Matendo ya mitume. Mtume Huyu hakuwa miongoni mwa wale 12, lakini baadaye tunakuja kusoma alihesabiwa kuwa ni mmojawapo wa wale 12 kama wengi wetu tunavyojua, Na siri ya yeye kuhesabiwa kuwa mmojawapo wale mitume 12 wa Bwana, imeandikwa pale katika biblia, embu tusome:
Matendo 1:15 “Siku zile akasimama Petro kati ya hao ndugu (jumla ya majina ilipata mia na ishirini), akasema,
16 Ndugu, ilipasa andiko litimizwe, alilolinena Roho Mtakatifu zamani kwa kinywa cha Daudi, katika habari za Yuda aliyewaongoza wao waliomkamata Yesu;
17 kwa sababu alikuwa amehesabiwa pamoja na sisi, akapata sehemu ya huduma hii.
18 (Basi mtu huyu alinunua konde kwa ijara ya udhalimu; akaanguka kwa kasi akapasuka matumbo yake yote yakatoka.
19 Ikajulikana na watu wote wakaao Yerusalemu; hata konde lile likaitwa kwa lugha yao Akeldama, maana yake, konde la damu.)
20 Kwa maana imeandikwa katika chuo cha Zaburi, Kikao chake na kiwe ukiwa, Wala asiwepo mtu mwenye kukaa humo;
21 Basi katika watu waliofuatana nasi wakati wote Bwana Yesu alipokuwa akiingia na kutoka kwetu,
22 kuanza tangu ubatizo wa Yohana, hata siku ile alipochukuliwa kwetu kwenda juu, inapasa mmoja wao awe shahidi wa kufufuka kwake pamoja nasi.
23 Wakaweka wawili, Yusufu, aitwaye Barsaba, aliyekuwa na jina la pili Yusto, na Mathiya.
24 Kisha wakaomba, wakasema, Wewe, Bwana, ujuaye mioyo ya watu wote, tuonyeshe ni nani uliyemchagua katika hawa wawili,
25 ashike mahali katika huduma hii na utume huu, alioukosa Yuda, aende zake mahali pake mwenyewe.
26 Wakawapigia kura; kura ikamwangukia Mathiya; naye akahesabiwa kuwa pamoja na mitume kumi na mmoja”.
Unaona huo mstari wa 21 na 22, unatuambia Mathiya ni mtu aliyefuatana na mitume wa Bwana tangu siku za mwanzoni kabisa mwa huduma ya Yesu, mpaka siku ile ambayo Ananyakuliwa mbinguni. Japo kulikuwa na mabonde mengi na hatari nyingi za kuuliwa na wayahudi, lakini huyu Mathiya hakuacha kuongozana na Bwana pamoja na mitume wake, japo kuna wakati wanafunzi wengi walijitenga na Kristo na kurudi nyuma kutokana na mafundisho yake ambayo hawakuyaelewa, lakini huyu Mathiya hakurudi nyuma…Mahali ambapo wanafunzi wake waliacha kila kitu na kumfuata Yesu, Mathiya naye alifanya hivyo japo Kristo hakumuhesabia kama mmoja wa mitume wake 12.
Embu tengeneza picha siku ile Bwana YESU ametoka kusali ndio anakwenda kuwateua mitume wake 12 wa kufuatana naye, katikati ya wanafunzi wengi aliokuwa nao,..Kumbuka Huyu Mathiya naye alikuwa pale, na akamwona Bwana anampita hana habari naye anawafuata wanafunzi wengine..Ingekuwa ni wewe upo hapo ingekuwa ni rahisi kuvunjika moyo. Lakini yeye kutokuchaguliwa hakukumfanya ajione hastahili kuwa mwanafunzi wake, au asifuatane na Bwana..
Lakini hakujua kuwa kwa kujitoa kule, na kumpenda Bwana kule, kumbe tayari siku nyingi ameshaandikiwa kuwa atakuwa miongoni mwa wale mitume 12.. Lakini mpaka Bwana anaondoka hajawahi kumwambia jambo hilo.. Hilo linakuja kuthibitika kwa vinywa vya mitume wake, wakisapotiwa na maandiko haya..
Zaburi 109:8 “Siku zake na ziwe chache, Usimamizi wake na atwae mtu mwingine”.
Usimamizi wa Yuda ambaye alitiwa mafuta na Yesu mwenyewe, ambaye aliheshimiwa na Yesu, ambaye alikula meza moja na Yesu, hapa inachukuliwa na Mathiya.
Hata leo hii, huhiitaji Bwana akutokee kama ilivyokuwa kwa mitume, ili kukuthibitisha wewe unaweza kuwa ni mteule wake, huhitaji Bwana akupe maono Fulani ndio umtumikie, huhitaji upitie shule Fulani ya biblia ndio upate uthibitisho kuwa Mungu yupo na wewe..Bwana anachohitaji kwako ni uaminifu wako kwake, tangu siku ile ulipoitikia wito wa kuokoka, ili wakati wake ukifika akunyanyue kama Mathiya..
Bwana alikuwa na wanafunzi wengi sana, lakini si wote walidumu naye wakati wote, walikuwa wanakuja na kuondoka, wanakuja na kuondoka, lakini waliodumu kuanzia mwanzo hadi mwisho ni wawili tu yaani Mathiya na Yule mwingine aliyeitwa Yusufu kati ya mamia ya wanafunzi waliokuwa wanamfuata.. Kama tu vile Yoshua na Kalebu walivyoingia nchi ya ahadi wao tu kati ya mamilioni ya watu waliotoka Misri.
Na Mathiya kumbukumbu lake halitafutika milele.. Tunaposoma kitabu cha Ufunuo juu ya ule mji Mtakatifu Yerusalemu mpya ushukao kutoka mbinguni wenye misingi 12 na malango 12..Na katika misingi ile pameandikwa majina 12 ya wale mitume 12 wa Yesu, (Ufunuo 21:14) ..Sasa jina mojawapo ni la huyu Mathiya.
Lakini safari yake haikuibukia juu juu tu yaani siku ile ya kura, bali ilianzia mbali, tangu wakati wa Yohana mbatizaji..Vivyo hivyo na sisi, tumtii Kristo sasa, tuyatii maagizo yake yote anayotuelekeza hata kama hatutaona tofauti yoyote nje leo hii, lakini mwisho wa siku ataonyesha tofauti yetu tusipozimia mioyo.. Tukiokoka tusiishi kama watu ambao Mungu hawatambui, tujue kuwa siku moja ya wokovu wetu inathamani kubwa sana mbele za Mungu.
Ubarikiwe sana.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii 0789001312
Mada Nyinginezo:
VIFO VYA MITUME WA YESU/ JINSI MITUME WALIVYOKUFA.
JIFANYIE RAFIKI KWA MALI YA UDHALIMU.
JINSI BWANA ALIVYOWACHAGUA MITUME WAKE.
TIMAZI NI NINI
INGIENI KWA KUPITIA MLANGO ULIO MWEMBAMBA.
MIILI YA UTUKUFU ITAKUWAJE?
YONA: Mlango wa 4
TAZAMA, MWISRAELI KWELI KWELI, HAMNA HILA NDANI YAKE!
Shalom. Karibu tujifunze Biblia, ambalo ndio Neno la Mungu, Mwanga wa njia yetu na Taa iongozayo miguu yetu.
Biblia inasema…Mungu anawaangazia jua lake waovu na wema…(Mathayo 5:45), na anawanyeshea mvua yake wenye haki na wasio haki..Maana yake ni kwamba…Riziki Mungu anawapa watu wote…Hata mchawi akienda kupanda mbegu zake shambani kwake…Mungu atazinyeshea mvua na zitaota.
Sasa msingi wa Neno hili la “Yeye anawaangazia jua lake waovu na wema na kuwanyeshea mvua wenye haki na wasio haki” ndio utakaotupa picha kamili kuelewa kwamba baraka yoyote, au upendeleo wowote tunaopokea kutoka kwa Mungu sio uthibitisho namba moja wa kuonyesha kwamba tupo sawa na Mungu au hatupo sawa na Mungu…Kwasababu kumbe baraka hizo hizo zinaweza kuwapata wote waovu na wema kwa pamoja…Ndio maana unaona leo hii hata waovu wanafanikiwa sana.
Sasa sio kwamba tuwe waovu ndio tuwe tumepata tiketi ya kubarikiwa…Hapana!..Biblia inasema..katika Zaburi 92:7 “Wasio haki wakichipuka kama majani Na wote watendao maovu wakistawi. Ni kwa kusudi waangamizwe milele”. Kwahiyo tusitafute kuwa waovu ili tufanikiwe.
Kadhalika Miaka ya watenda mabaya itafupishwa. Mtu mwovu atalifurahia jua kwa kitambo, ataifurahia neema kwa kitambo, ataufurahia wema wa Mungu kwa kitambo…lakini kifo kitamjia kwa ghafla.
Hivyo usifurahie kupata mafanikio fulani au baraka fulani, au kupata fursa fulani mbele yako baada ya kumwomba Mungu, na huku ndani ya moyo wako umemwacha Mungu ukayatafsiri mafanikio yale kama ni uthibitisho wa Mungu kupendezwa na wewe….kamwe usifanye hivyo!..kumbuka neno hili kuwa “Mungu anawanyeshea mvua waovu na wema”. Kwahiyo hata ukiwa mwovu hiyo haimzuii Mungu kukupa chakula.
Kadhalika usitafsiri majibu Mungu aliyokupa ya uponyaji..kwamba ulikuwa na ugonjwa fulani au tatizo fulani na ukamwomba Mungu naye akakuponya na wakati huo huo bado ni mlevi, mwasherati, kwamba uponyaji ulioupokea ni kwasababu Mungu amependezwa na wewe
Katika biblia kuna Mfalme mmoja ambaye alirasimisha ibada za sanamu katika Taifa la Israeli, mfalme huyo alikuwa anaitwa Yeroboamu…alitengeneza sanamu mbili za ndama akaziweka moja kaskazini mwa Israeli nyingine kusini, akawaambia Israeli wote kwamba sanamu hizo ndiyo miungu iliyowatoa wao Misri, hivyo wasiende Yerusalemu kuabudu bali wapande kwenda kuzisujudia sanamu hizo. Hivyo akawageuza mamilioni ya Wana wa Israeli mioyo na kuwafanya kuwa nusu-wachawi kwa muda mrefu kwa jinsi walivyokwenda kuziabudu sanamu hizo za ndama huko alikoziweka…
Na siku ya kuzivumbua sanamu hizo..alitengeneza madhababu juu yake na kutoa kafara…wakati anatoa kafara…akatokea nabii mmoja aliyetumwa na Mungu akatabiri mbele ya ile madhabahu kwamba siku inakuja ambayo itabomolewa na makuhani watakaohudumu katika hiyo madhabahu watachinjwa juu yake..Na huyu Mfalme alipomwona yule Nabii akanyosha mkono wake kutoa amri ya kukamatwa..Wakati anamnyooshea tu mkono wake…Ule mkono biblia unasema ukakatika …
Sasa maana yakukatika sio kwamba ulinyofoka na kuanguka chini hapana…bali maana yake ulikufa ule mkono…na ukakauka ukawa kama mkono wa maiti iliyokauka…ulikauka ukawa kama kijiti kikavu…ukawa hauna hisia hata kidogo..kama mkono uliopata kiharusi…Mfalme kuona vile akamwomba yule Nabii amwombee rehema kwa Mungu wake ili mkono wake urudi…na alipoombewa akapokea uponyaji wake siku hiyo hiyo na akaendelea na shughuli zake za kichawi…wala hakugeuka kubadilika..Na ndio Mfalme aliyefanya maovu kuliko wafalme wote waliowahi kutokea Israeli…yeye pamoja na mfalme Ahabu mumewe Yezebeli. Kasome 1Wafalme 12 na 13.
Sasa unaweza kuona huyu Mfalme alikuwa ni nusu-mchawi lakini katika uovu wake alimwomba Mungu amponye na Mungu akasikia na kumponya…na baada ya kuponywa aliendelea na Maisha yake ya ouvu…kwasababu alitaka tu apate uponyaji ili aweze kuendelea na maisha yake ya dhambi kama kawaida…… Sasa uponyaji alioupokea haukuwa uthibitisho wa kuwa Mungu amependezwa na yeye…Ni rehema za Mungu tu kwasababu yeye anawanyeshea mvua wenye haki na wasio haki…Lakini haimaanishi kuwa anapendezwa na wasio haki…Ndio maana huyu Mfalme Bwana alikuja kumwambia atakufa.
1Wafalme 14:10 “tazama, kwa hiyo mimi nitaleta mabaya juu ya nyumba yake Yeroboamu, nami nitamkatia Yeroboamu kila mwanamume, aliyefungwa na aliyeachwa katika Israeli, nami kuondoa nitawaondoa waliobaki wa nyumba yake Yeroboamu, kama mtu aondoavyo mavi, hata itakapokwisha pia”
Hiyo ndiyo imekuwa kawaida ya Mungu wetu…yeye huwanyeshea mvua waovu na wema…huwapa uponyaji makahaba na wasio makahaba endapo watamlilia, huwapa mali waovu na wasio waovu, huwanyanyua wenye haki na wasio haki..Hivyo kamwe usitumie kipimo cha wema wa Mungu juu yako kutafsiri uwepo wa Mungu katika Maisha yako…Hivyo ni vitu viwili tofauti.
Watakuwepo watu waliobarikiwa na mali kuzimu, watakuwepo watu walioponywa magonjwa yao na kuwa wazima kuzimu, watakuwepo watu kuzimu ambao waliofanyiwa mambo mengi mazuri na Mungu wakiwa duniani tena wakiwa ni waovu. Na wenye shuhuda nyingi tu, jinsi Mungu alivyowapigania katika mambo yao. N.k.
Uwepo wa Mungu juu ya Maisha yako unapimwa kwa maisha ya utakatifu unayoishi…Usifurahi umeponywa na huku bado unaendelea kuvaa vimini, Usifurahie unapata riziki kimiujiza na huku unakula rushwa, ukafikiri Bwana anapendezwa na wewe, usifurahie umetoka tu kuzini na mtu ambaye si mume wako, halafu kesho ukapata promosheni ya kupandishwa cheo kazini..ukadhani baraka hizo ni uthibitisho wa Mungu kupendezwa na wewe.
usifurahie uliombewa ukapona kansa na huku bado umemwacha mke wako au mume wako na unadhani Mungu yupo na wewe!..Usifurahie ulifunga siku kadhaa ukamwomba Mungu akupe nyumba na kweli akakupa na huku bado Maisha yako hutaki kujitakasa ukahitimisha kwa muujiza ule Mungu anapendezwa sana na wewe ndio maana akakuponya, au akakupa hiki au kile…kumbuka yeye anawanyeshea mvua waovu na wema…hivyo sio jambo kubwa sana yeye kukupa uponyaji wake angali ukiwa bado na ukahaba wako…Lakini usipotubu…Neno lake lipo pale pale..waasherati na wafiraji, na wezi, na waabudu sanamu, na wachawi, sehemu yao ni katika lile ziwa la Moto.
1Wakorintho 6:9 “Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? MSIDANGANYIKE; waasherati hawataurithi ufalme wa Mungu, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wafiraji, wala walawiti,
10 wala wevi, wala watamanio, wala walevi, wala watukanaji, wala wanyang’anyi”.
Bwana akubariki sana…ikiwa hujamkabidhi Yesu Kristo Maisha yako..fanya hivyo leo angali tunao bado huu muda mchache…
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii 0789001312
Mada Nyinginezo:
UNAWAFAHAMU MANABII WA UONGO?
Ni sahihi kumuita Mariamu mama wa Mungu?
JISHUSHE ILI MUNGU AKUHUDUMIE.
USIPOKUWA MWAMINIFU, NAFASI YAKO ITACHUKULIWA.
Biblia ni nini?
SAYUNI ni nini?
JIBU: Kuna mambo mawili ya kufahamu jambo la kwanza ni kuwa mara baada ya huu ulimwengu wa sasa kuisha, kutakuwa na utawala mwingine mpya ujulikanao kama utawala wa amani wa Yesu Kristo wa miaka 1000 (Ukisoma Ufunuo 20:6 utaona jambo hilo). Na mara baada ya huo utawala wa miaka 1000 kuisha kutakuwa na umilele ambapo wakati huo ndio ile mbingu mpya na nchi mpya vitafunuliwa..Na maskani ya Mungu itakuwa ni pamoja na wanadamu. Ambapo Mungu atafanya makao yake na wanadamu milele na milele isiyokuwa na mwisho (Ufunuo 21:3)
Sasa katika ule utawala wa miaka 1000, ambapo Kristo atarudi na watakatifu wake aliowanyakua zamani, (Yuda 1:14) utakuwa ni utawala wa amani lakini bado biblia inarekodi waovu watakuwepo pia (Isaya 65:20)…Lakini katika mbingu mpya na nchi mpya ambayo itaanza mara baada tu ya utawala huu wa miaka elfu moja kuisha, waovu hawatakuwepo kabisa.
Sasa hawa waovu watakaokuwepo ndani ya utawala huo (waliozaliwa humo) ndio watakaotawaliwa na watakatifu wakati ule utakapofika.. Na ndio maana Bwana Yesu anatuhimiza sasa na kutuambia..
Ufunuo 2:26 “Na yeye ashindaye, na kuyatunza matendo yangu hata mwisho, nitampa mamlaka juu ya mataifa,
27 naye atawachunga kwa fimbo ya chuma, kama vyombo vya mfinyanzi vipondwavyo, kama mimi nami nilivyopokea kwa Baba yangu.
28 Nami nitampa ile nyota ya asubuhi.
29 Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa”.
Vilevile katika huo utawala wa miaka elfu moja, na pia baada ya utawala huo kupita kutakuwa na shughuli maalumu (au tuseme sekta maalumu) ambazo Mungu ameziandaa zifanywe na zisimamiwe na watakatifu wake tu. Lakini sasa hizo hazifanywi na kila mtakatifu tu, hapana, bali zitafanywa kulingana na auminifu wa mtakatifu husika alipokuwa hapa duniani..Tunasoma hilo katika.
Mathayo 24:45 “Ni nani basi yule mtumwa mwaminifu mwenye akili, ambaye bwana wake alimweka juu ya nyumba yake, awape watu chakula kwa wakati wake?
46 Heri mtumwa yule, ambaye bwana wake ajapo atamkuta akifanya hivyo.
47 Amin, nawaambieni, atamweka juu ya vitu vyake vyote.
48 Lakini mtumwa yule mbaya akisema moyoni mwake, Bwana wangu anakawia;
49 akaanza kuwapiga wajoli wake, na kula na kunywa pamoja na walevi;
50 bwana wake mtumwa huyo atakuja siku asiyodhani, na saa asiyojua,
51 atamkata vipande viwili, na kumwekea fungu lake pamoja na wanafiki; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.
Unaona? Sasa hapa ndipo yatakapotokea matabaka hata katikati ya watakatifu. Wale ambao walikuwa waaminifu katika kazi ya Mungu na katika utakatifu wakiwa hapa duniani watapewa vyeo vya juu zaidi katika enzi ya Mungu, na wale waliokuwa waaminifu kidogo watapewa kidogo..kama Bwana Yesu alivyosema katika kitabu cha Luka…
Luka 19:16 “Akaja wa kwanza, akasema, Bwana, fungu lako limeleta faida ya mafungu kumi zaidi.
17 Akamwambia, Vema, mtumwa mwema; kwa vile ulivyokuwa mwaminifu katika neno lililo dogo, uwe na mamlaka juu ya miji kumi.
18 Akaja wa pili, akasema, Bwana, fungu lako limeleta mafungu matano faida.
19 Akamwambia huyu naye, Wewe uwe juu ya miji mitano.
20 Akaja mwingine akasema, Bwana, hili ndilo fungu lako, ambalo nililiweka akiba katika leso.
21 Kwa maana nilikuogopa kwa kuwa u mtu mgumu; waondoa usichoweka, wavuna usichopanda.
22 Akamwambia, Nitakuhukumu kwa kinywa chako, mtumwa mwovu wewe. Ulinijua kuwa ni mtu mgumu, niondoaye nisichoweka, na kuvuna nisichopanda;
23 basi, mbona hukuiweka fedha yangu kwa watoao riba, ili nijapo niipate pamoja na faida yake?
24 Akawaambia waliosimama karibu, Mnyang’anyeni hilo fungu, mkampe yule mwenye mafungu kumi”
Hivyo kwa kuhitimisha ni kwamba, vyeo vitakuwepo na kutawala pia kutakuwepo..Isipokuwa kutawala kutaishia katika ule utawala wa miaka 1000, lakini vyeo na ngazi zitaendelea mpaka umilele kwenye mbingu mpya na nchi mpya.. kwasababu huko hakutakuwa na waovu tena, Isipokuwa sote tutamilika na yeye. Lakini sote hatutakuwa ngazi moja…
2Timotheo 2:12 “Kama tukistahimili, tutamiliki pamoja naye; Kama tukimkana yeye, yeye naye atatukana sisi”;
Hivyo tufanye bidii ili tuwepo na Bwana katika utawala wake na mpaka mwisho hadi tutakapoifikia ile nchi mpya na mbingu mpya..
2Petro 3:13 “Lakini, kama ilivyo ahadi yake, mnatazamia mbingu mpya na nchi mpya, ambayo haki yakaa ndani yake.
14 Kwa hiyo, wapenzi, kwa kuwa mnatazamia mambo hayo, fanyeni bidii ili mwonekane katika amani kuwa hamna mawaa wala aibu mbele yake”.
Ubarikiwe.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255693036618/ +255789001312
Au Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp
Mada nyinginezo
KWANINI KUWE NA UTAWALA WA MIAKA 1000
MBINGU MPYA NA NCHI MPYA. (Sehemu ya 2)
Kati ya Unyakuo,dhiki kuu, utawala wa miaka 1000 kipi kinaanza
USITOKE NJE YA HIFADHI YA MUNGU.
Easter ni nini?..Na je tunaruhusiwa kuisheherekea?
Shalom, Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe.
Bwana Yesu alisema maneno yafuatayo…
Mathayo 24:23 “Wakati huo mtu akiwaambia, Tazama, Kristo yupo hapa, au yuko kule msisadiki.
24 Kwa maana watatokea makristo wa uongo, na manabii wa uongo, nao watatoa ishara kubwa na maajabu; wapate kuwapoteza, kama yamkini, hata walio wateule”.
Bwana Yesu anapomwita mtu, au anapomvuta mtu kwake kitu cha kwanza kumwonesha sio kanisa la kujiunga…bali Neno lake. Ni muhimu kulijua hilo ili tusidanganyike na roho zituambiazo..”tazama Kristo yupo hapa ama kule”
Zamani kidogo kuna mtu alitutumia ujumbe akatuambia… “Ameota ndoto, alikuwa ndani ya kanisa lake ambalo ndilo analokwenda siku zote…katika hiyo ndogo alijiona alikuwa anaimba na kuabudu kwa furaha pamoja na washirika wenzake…wakati anaabudu kwa nje ya kanisa akamwona mdada mwingine ambaye anamfahamu anamwangalia kama kwa kumhuzunikia hivi…Na alipoona anamwangalia sana na tena kwa huzuni…yeye kitu Fulani kikamjia kwenye kichwa chake, kwamba pengine hayupo sehemu salama…hivyo akaamua kutoka kule ndani alipokuwa anaimba na wenzake na akamfuata Yule dada aliyekuwepo kule nje!..Na huyo dada alipomfuata aligundua kuwa anasali kanisa Fulani analolijua kisha akashtuka usingizini” .
Baada ya ndoto hiyo akatutumia meseji kwamba anahisi Mungu anamwambia aondoke hilo kanisa alilopo sasa aende kwenye kanisa lingine…ambalo ni la Yule dada aliyemwona kwenye ndoto. Akatuhadithia na hiyo ndoto aliyoiota. Ikabidi tuanze kumhoji kanisa alilopo sasa hivi ni kanisa gani! Akatutajia..na hilo analotaka kwenda pia akatutajia.. Tulichokuja kugundua kuwa mahali anaposali sasa pana uafadhali mkubwa sana kuliko kule alikokuwa anataka kwenda…
Kwanza mahali anaposali panahubiriwa maonyo ya siku za mwisho kwa nguvu, na pia wanafundishwa utakatifu, pamoja na wanawake kujiheshimu kwa kujisitiri, ni mahali ambapo wanawake hawavai suruali, hawavai mawigi, hawaruhusiwi kuvaa vimini, hawapaki wanja na mambo yote ya kidunia hayaruhusiwi kanisani…Na huko anakotaka kwenda ni mahali ambapo mambo hayo yote ni ruksa…kuvaa suruali na kuingia nazo kanisani ni ruksa, kujipodoa na kuingia kanisani ni ruksa, na wala hakuna msisitizo wowote wa ujio wa pili wa Kristo.
Tukamwuliza huyu dada ni kitu gani ambacho unahisi hakiendi sawa katika kanisa ulilopo sasa?..akasema hakuna..kila kitu kipo sawa, kanisani hakuna tatizo lolote kuna amani na kuna upendo tu. Lakini naogopa hiyo ndoto niliyoiota isije kuwa Mungu ananionya niondoke halafu simtii?.
Tukamwambia hiyo ndoto sio ya Ki-Mungu…Mungu kamwe hawezi kumtoa mtu kwenye kanisa na kumwonyesha kanisa…kamwe hafanyi hivyo!..Atamtoa mtu kwenye kanisa na kumwonyesha Neno lake kwanza…hicho ndicho kitu cha kwanza kumwonyesha…Kwamfano mtu anaweza kuwa katika kanisa ambalo kunafanyika ibada za sanamu….Sasa Roho Mtakatifu akitaka kumwondoa mtu hapo..hatamwonyesha kanisa Fulani lingine labda la kiroho akajiunge…kamwe hatafanya hicho kitu…atakachofanya ni kumwonyesha kwanza yule mtu maandiko yanavyosema…Atamwonyesha kwanza Neno linasema “usijifanyie sanamu ya kuchonga wala mfano wa kitu chochote kilicho juu mbinguni, wala duniani, wala chini kuzimu usivisujudie wala kuvitumikia (Kutoka 20:4)”.
Hilo ndilo Neno la kwanza atakalomwonyesha…na kwa kupitia hilo neno sasa ndipo mtu atapata ufahamu kuwa hayupo sehemu salama…na kuondoka pale alipo kwenda kutafuta mahali pengine ambapo hataabudu sanamu kulingana na Neno lile….Lakini Mungu hawezi kuliruka Neno lake na moja kwa moja kukupeleka kwenye kanisa Fulani…kama ilivyokuwa kwa huyu dada..Lazima akuonyeshe kwanza kuna kitu hakipo sawa kulingana na Neno mahali ulipo ndipo uondoke…lakini kama huoni chochote halafu unasikia kitu kinakuambia uondoke hizo ni roho zidanganyazo zisemazo “Kristo yupo huku au kule..”
Sasa hiyo roho inamtoa huyu dada mahali ambapo wanawake wanajisitiri na kumpeleka mahali ambapo ataruhusiwa kuvaa vimini na kuingia navyo kanisani, ataruhusiwa kujipodoa, mahali ambapo hatakemewa dhambi wala kukumbushwa habari za ujio wa pili wa Bwana Yesu.
Ndugu usikimbilie kutafuta kanisa..tafuta kulijua Neno la Mungu…ukilifahamu hilo ndipo utakapoweza kujua mahali ulipo kama ni salama au sio salama..kadhalika sio kila ndoto unayoota inatoka kwa Mungu…Nyingine zinatoka kwa Ibilisi, hivyo hupaswi kuamini kila roho, bali unapaswa uijaribu…na huwezi kuijua kama hiyo ndoto inatoka kwa Ibilisi au kwa Mungu kama hulijui Neno (Hivyo Neno la Mungu litabaki kuwa msingi wa kila kitu)….Usipolijua Neno Siku zote utatii kila ndoto na kumbe zinakupeleka upotevuni..Na jambo la mwisho la kufahamu ni kwamba…Sio kila ndoto ina maana!..nyingine zinatokana na shughuli zetu za kibinadamu tu(Mhubiri 5:3)… Usitafute kujua tafsiri ya kila ndoto unayoota nyingine ziache zipite.
Kama ni Mungu anazungumza na wewe katika ndoto usiwe na papara!… yeye mwenyewe atakutengenezea njia rahisi tu ya kuielewa tafsiri ya hiyo ndoto kama imetoka kwake..inaweza isiwe siku hiyo hiyo au wiki hiyo hiyo, lakini itafika saa na siku itaijua tafsiri yake…Unachopaswa kufanya ni kudumu katika utakatifu na maombi na kusoma Neno lake.
Hivyo kwa kuhitimisha…Lijue sana Neno hiyo ndiyo silaha yetu..Na pia usihangaike huku na huko kutafuta ni kanisa gani lipo sahihi…hangaika usiku na mchana kujifunza Neno la Mungu, hangaika usiku na mchana kutafuta kuijua biblia inasema nini?…hangaika kumjua Yesu Kristo ni nani katika Maisha yako?,..kujua biblia inasema nini kuhusu uumbaji, kuhusu siku tunazoishi, kuhusu ubatizo kwanini uwepo?, kwanini tumeumbwa, kwanini tuanguke dhambini, na kwanini tuokolewe…isome sana kwasababu majibu yote yamo kwenye biblia…soma kitabu cha Matendo angalia kanisa la kwanza lilianzaje!..soma kitabu cha wakoritho angalia upendo unapaswa uweje, Soma kitabu cha Waebrania angalia tunaokolewaje kwa agano la damu.. tenga muda mrefu kusoma vitabu vyote taratibu na kwa umakini…na ufahamu utakaoupata huko kwa msaada wa Roho Mtakatifu ndipo utakaoamua ni wapi utulie,…Bwana atautumia huo kukuweka sehemu sahihi ya kumwabudu yeye.
Ubarikiwe sana.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii 0789001312
Mada Nyinginezo:
MPINGA-KRISTO
MUUNGANIKO WA MADHEHEBU NI MPANGO WA MPINGA-KRISTO.
Nifanye nini ili niondokane na Hofu maishani mwangu?
Utii ni nini? na ni nani tunayepaswa kumtii au kutokumtii?
Nifanye nini ili niwe na uhakika nikifa naenda mbinguni?
MADHABAHU NI NINI?
MAANA YA RANGI KIBIBLIA.
USILALE USINGIZI WAKATI WA KUMNGOJEA BWANA.
Shalom, Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe.
Leo tutaona kimaandiko ni jinsi gani Roho wa Mungu anavyowasaidia watu kuyaelewa maandiko. Watu wengi, wanaposoma biblia na kuona kama ni ngumu haieleweki hususani vile vitabu vya manabii, kama vile Danieli, Isaya, Ezekieli, Yeremia, Zekaria, Ufunuo na vinginevyo, basi wanakata tamaa kabisa ya kuvimaliza, wanaona ni afadhali tu waache, au wanaona pengine hawastahili kufahamu habari zile kwasasa ni za watumishi Fulani tu, au viongozi Fulani wa dini waliokomaa ndio wanaouwezo wa kuelewa.
Lakini nataka nikuambie kutolielewa Neno la Mungu, sio ujinga, bali Mungu mwenyewe ndio karuhusu sehemu nyingine kulifunga kwa makusudi maalumu ili awafunulie wale waliotayari kujifunza (Danieli 12:4, Mathayo 13:11-14). Hivyo leo tutaangazia mfano mmoja wa kwenye biblia ili na wewe kwa kupitia habari hii, upate motisha ya kupenda kujifunza Neno la Mungu peke yako ukiongozwa na Roho Mtakatifu mwenyewe.
Sasa tukisoma kile kitabu cha Matendo ya Mitume tunaona habari ya mtu mmoja aliyetoka Kushi kwenda kuhiji Yerusalemu, Mtu huyu hakuwa myahudi, wala hakuwa chini ya viongozi wa kidini wa kiyahudi kama Gamalieli na wenzake, bali alikuwa ni kiongozi tu mkuu wa nchi hiyo ya Kushi (ambayo kwasasa ni nchi ya Ethiopia), lakini mtu huyu alimpenda Mungu wa Israeli, na hiyo ikawa inamfanya kila wakati wa sikukuu za kiyahudi na yeye awe anapanda Yerusalemu kuungana na wayahudi wengine kumwabudu Yehova.
Lakini pia alikuwa ni mtu aliyependa kujifunza maandiko. Tunasoma alipokuwa anarudi kutoka Yerusalemu akiwa kwenye gari lake, safarini kurejea nyumbani, biblia inatuambia mule ndani ya gari lake alikuwa akisoma vitabu vya manabii vya agano la kale..Kitabu cha Isaya sura ile ya 53, Mtu huyu alikuwa hayaelewi haya maandiko hata kidogo, pengine alikuwa anayasoma kwa kuyarudia tena na tena,labda pengine atapata tafsiri yake, au ufunuo..akifikiria habari ile ilikuwa inamzungumzia nani, anawaza moyoni mwake, mistari ile inamaanisha nini,..
Sasa kwa kitendo tu kama kile cha kutia nia kutaka kujua maana ya maneno yale..Hapo hapo Roho Mtakatifu akaanza kufanya kazi, akaanza kumwandalia mwalimu wa kumfundisha tokea mbali sana na yeye alipokuwepo.. Roho Mtakatifu akamtafutia mtu, akampata Filipo.. Filipo akiwa huko Samaria akihubiri na kubatiza watu, Roho Mtakatifu akamkatisha kazi yake, na kumwambia anza safari kuelekea mahali pasipo kuwa na watu, Kusini Njia ya jangwa la Gaza, Wakati anaondoka pengine Filipo anawaza kichwani kwake mbona Mungu anafanya niache maelfu ya watu huku Samaria na kuniambia niende huku mahali pasipokuwa na watu..Lakini yeye alitii kwasababu alijua Mungu anamakusudio yake, pengine alidhani huko anapokwenda atakutana na watu wengi zaidi ya wale aliowaacha Samaria,..Akasafiri kupita jangwa lile mpaka akafika mahali akaliona gari Fulani kwa mbali njiani, Roho Mtakatifu akamwambia lisogelee karibu kabisa..Na yeye akalisogelea, alipolisogelea akamwona mtu ndani yake yupo bize akisoma kwa sauti kitabu cha Isaya sura ile ya 53…
Ndipo kuanzia hapo Filipo akaanza kuzungumza naye tusome..
Matendo 8:26 “Malaika wa Bwana akasema na Filipo, akamwambia, Ondoka ukaende upande wa kusini hata njia ile itelemkayo kutoka Yerusalemu kwenda Gaza; nayo ni jangwa.
27 Naye akaondoka, akaenda; mara akamwona mtu wa Kushi, towashi, mwenye mamlaka chini ya Kandake malkia wa Kushi, aliyewekwa juu ya hazina yake yote; naye alikuwa amekwenda Yerusalemu kuabudu,
28 akawa akirejea, ameketi garini mwake akisoma chuo cha nabii Isaya.
29 Roho akamwambia Filipo, Sogea karibu na gari hili, ukashikamane nalo.
30 Basi Filipo akaenda mbio, akamsikia anasoma chuo cha nabii Isaya; akanena, Je! Yamekuelea haya unayosoma?
31 Akasema, Nitawezaje kuelewa, mtu asiponiongoza? Akamsihi Filipo apande na kuketi pamoja naye.
32 Na fungu la Maandiko alilokuwa akilisoma ni hili, Aliongozwa kwenda machinjoni kama kondoo, Na kama vile mwana-kondoo alivyo kimya mbele yake amkataye manyoya, Vivyo hivyo yeye naye hafunui kinywa chake.
33 Katika kujidhili kwake hukumu yake iliondolewa. Ni nani atakayeeleza kizazi chake? Kwa maana uzima wake umeondolewa katika nchi.
34 Yule towashi akamjibu Filipo, akasema, Nakuomba, nabii huyu; asema maneno haya kwa habari ya nani; ni habari zake mwenyewe au za mtu mwingine?
35 Filipo akafunua kinywa chake, naye, akianza kwa andiko lilo hilo, akamhubiri habari njema za Yesu.
36 Wakawa wakiendelea njiani, wakafika mahali penye maji; yule towashi akasema, Tazama, maji haya; ni nini kinachonizuia nisibatizwe?
37 Filipo akasema, Ukiamini kwa moyo wako wote, inawezekana. Akajibu, akanena, Naamini ya kwamba Yesu Kristo ndiye Mwana wa Mungu.]
38 Akaamuru lile gari lisimame; wakatelemka wote wawili majini, Filipo na yule towashi; naye akambatiza.
39 Kisha, walipopanda kutoka majini, Roho wa Bwana akamnyakua Filipo, yule towashi asimwone tena; basi alikwenda zake akifurahi.
Unaweza kuona hapo, Mkushi Yule sio tu aliishia kuyaelewa maandiko yale bali maandiko yale bali pia yalimpelekea kupata mpaka na ubatizo. Lakini hiyo yote ni kwasababu alitia nia moyoni mwake ya kutaka kuyatafakari maandiko kufahamu maana ya yale yaliyoandikwa. Na ndipo akafunuliwa mambo ambayo, hata kuhani mkuu kule Yerusalemu alikuwa hayajui, viongozi wote wa dini na waandishi wanayasoma kila siku lakini hawayaelewi..anakuja kufunuliwa mkushi ambaye hana ujuzi wowote na torati.
Vivyo hivyo na wewe na mimi, Kama umeokoka na unaye Roho Mtakatifu ndani yako, sio wakati wa wewe kukaa kungojea fundisho Fulani uletewe na mhubiri Fulani, au mchungaji Fulani tu peke yake,..Anza kwa kujijengea utaratibu wa wewe mwenyewe kuyatafakari maandiko binafsi kwa bidii na kumwomba Mungu akufunulie, ndipo hapo Mungu atakapotumia njia zake yeye mwenyewe alizozipanga kukufunulia, aidha kwa ufunuo au kwa muhubiri, hapo ndipo utakapopata uhakika kuwa Roho Mtakatifu amesema na wewe.. Wapo wengine wanasema nilikuwa ninautafakari sana mstari Fulani jana usiku, lakini sikuelewa, ghafla kesho yake nikasikia mhubiri Fulani anauhubiri mstari ule ule au nikakutana na mafundisho yale yale,.Hiyo ni ishara kuwa Mungu amemfunulia maana ya mstari ule. Sasa zipo njia nyingine nyingi ambazo Mungu anaweza kumfunulia mtu ikiwa tu atataka yeye mwenyewe kufahamu.
Lakini usikae tu bila kujishughulisha, kusubiria tu kufundishwa wakati wote, ujue kuwa yapo mambo ambayo Roho Mtakatifu anataka kukufundisha wewe kama wewe, vile vile anataka kukujengea uwezo wa wewe kuisikia sauti yake. Hivyo kama wewe umeshaokoka anza kuchukua hatua ya kuyatafakari maandiko bila kuogopa hichi ni kitabu cha manabii kisichoeleweka, au sio, suala la kutafsiri sio lako bali ni la Mungu, yeye mwenyewe ndiye atakayekufungulia njia zake za kuliewa.
Ubarikiwe sana.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii 0789001312
Mada Nyinginezo:
SEHEMU YA MAANDIKO ILIYOFICHWA.
KITABU CHA UZIMA
WAKAMTUKANA MUNGU, WALA HAWAKUTUBU.
Nifanye nini ili niondokane na Hofu maishani mwangu?
Utii ni nini? na ni nani tunayepaswa kumtii au kutokumtii?
KUOTA UNAKULA CHAKULA.
Pamoja na mengi tunayoweza kujifunza kwa Mariamu mama yake Yesu..lakini pia yapo mengi ya kujifunza kwa Yusufu Babaye Yesu. Leo kwa Neema za Bwana tutajifunza tabia moja ya Yusufu ambayo katika hiyo itatusaidia nasi kujifunza kumpendeza Mungu.
Mathayo 1:19 “Naye Yusufu, mumewe, kwa vile alivyokuwa mtu wa haki, asitake kumwaibisha, aliazimu kumwacha kwa siri.
20 Basi alipokuwa akifikiri hayo, tazama, malaika wa Bwana alimtokea katika ndoto, akisema, Yusufu, mwana wa Daudi, usihofu kumchukua Mariamu mkeo, maana mimba yake ni kwa uweza wa Roho Mtakatifu.
21 Naye atazaa mwana, nawe utamwita jina lake Yesu, maana, yeye ndiye atakayewaokoa watu wake na dhambi zao”.
Kwanza ni muhimu kufahamu kuwa Yusufu hakuwa baba wa damu wa Bwana wetu Yesu Kristo. Kama tunavyofahamu Mimba ya Bwana Yesu ilitungwa kimiujiza (kwa uweza wa Roho Mtakatifu)..hakukuhusisha Baba wa kimwili. Hivyo Bwana wetu Yesu Kristo hakuwa na baba wa kimwili.
Lakini pamoja na hayo tunajifunza tabia moja ya Yusufu ambaye alimkubali kama mwanawe wa kimwili. Na tabia hiyo sio nyingine Zaidi ya kuwa na HAKI..Mtu mwenye haki anakuwa anaonekana kuwa na haki mbele za Mungu, kadhalika anakuwa na haki mbele za Watu na pia anakuwa mwenye kutenda haki.
Hivyo kipindi fulani alimposa huyu mwanamke Mariamu..na akiwa katika hatua za kumwoa ghafla akamwona anaujauzito…Ni wazi kuwa Mariamu hakumwambia siku ile ya kwanza Malaika Gabrieli alipomtokea…aliificha siri ile, akiwaza pengine itakuwaje siku Yusufu akifahamu jambo hilo…Na mimba ikaendelea kukua mpaka ikafika kipindi ikaanza kuonekana kwa macho..na Yusufu akaiona.
Ilikuwa ni kipindi kigumu sana kwa Mariamu…akiwaza endapo Yusufu akimkataa itakuwaje!..jamii itamwelewaje?..Ni nani atakayeamini eti kwamba kapata mimba bila kukutana na mwanamume?..Ni wazi kuwa hakuna ambaye angemwelewa…Hivyo ni mawazo juu ya mawazo. (Ndugu kubeba kusudi la Mungu si jambo ambalo ni la kueleweka, wala si jambo la kupata heshima..lina gharama zake kubwa). Mariamu akiwa katika hali hiyo pengine alisema litakalo kuwa na liwe…Mimi nitamtegemea Bwana. (Hivyo ilihitaji Imani kubwa sana, kuitunza ile mimba isiyokuwa na Baba..haikuwa jambo jepesi). Leo tu hebu mwanamke apate mimba katika mazingira yasiyoeleweka eleweka ya uzinzi uone kama hatakwenda kuitoa…lakini haikuwa hivyo kwa Mariamu.
Baada ya Yusufu kugundua ile mimba…hata hakumuuliza Mariamu akaazimu kumwacha kwa siri…kwasababu alijua tayari kashakutana na mwanamume…Lakini katika ndoto Malaika akamwambia asimwache mkewe kwasababu mimba ile haikupatikana kwa uasherati bali kwa uwezo wa Roho Mtakatifu. Malaika yule katika ndoto akamtajia na jina la mtoto…Na alipokwenda kumuuliza pengine Mariamu na yeye akamuhadithia vile vile na jina la mtoto ni lile lile, hivyo hiyo ikawa ni uthibitisho wa kwamba mtoto yule ni wa kipekee katoka kwa Mungu..
Sasa hawa wawili Mariamu na Yusufu, mumewe wameshalitatua tatizo (wote wamekubali kuwa mimba ile ni ya kimiujiza)…Sasa Vipi kuhusu watu wa nje watawaelewaje?…Je! Yusufu atoke tu na kwenda kutangaza nje huko kuwa mke wangu kapata mimba kimiujiza?..si ataonekana mwendawazimu kwa watu wa kizazi alichopo?..nani atamuamini?….zaidi sana atamsababishia mke wake matatizo hata ya kupigwa kwa mawe kwa kosa la uzinzi…kwasababu watamhoji katolea wapi ile mimba?..Hivyo hapo inahitajika hekima nyingine ya ziada.
Na hekima hiyo si nyingine Zaidi ya kukubali tu kuchukua mashutumu…Yusufu ikambidi akubali kwamba yule ni mtoto wake kabisa….kwa namna nyingine tunaweza kusema “akakubali aonekane na watu kuwa alikutana na Mariamu kipindi kabla hawajaoana, na kwamba ile mimba ni ya kwake”..Alifanya hivyo kuzuia kumwaga lulu zake mbele za nguruwe…kama Bwana Yesu alivyokuja kusema huko mbeleni.
Mathayo 7: 6 “Msiwape mbwa kilicho kitakatifu, wala msitupe lulu zenu mbele ya nguruwe, wasije wakazikanyaga chini ya miguu yao, wakageuka na kuwararua”.
Hivyo pengine kama Yusufu kutukanwa basi alitukanwa…kama kudharauliwa alidharauliwa, kama kuonekana ni mtu mwenye tamaa alionekana hivyo…Watu wote wakaona ni mtu tu mwenye tamaa kwanini asingesubiri wafunge ndoa ndipo amkaribie mkewe?..walionekana yeye na mkewe Mariamu wote ni waasherati, na huyo mtoto atakayezaliwa atakuwa kazaliwa katika zinaa… Na mambo mengine mengi…
Leo hii wengi wanapenda Bwana Yesu aje katika Maisha yao…lakini wanazikimbia gharama za kumpokea Yesu…(Yusufu na Mariamu hawakuzikimbia) badala yake walizikabili walisema liwalo na liwe…itakuja kujulikana baadaye ukweli ni upi…Acha leo tuonekane ni watu waovu na tusiofaa lakini siku moja tutang’aa na kutukuzwa.
Luka 6:22 “Heri ninyi watu watakapowachukia, na kuwatenga, na kuwashutumu, na kulitupa nje jina lenu kama neno ovu, kwa ajili ya Mwana wa Adamu.
23 Furahiwani siku ile na kuruka-ruka, kwa kuwa, tazama, thawabu yenu ni kubwa mbinguni, maana, baba zao waliwatenda manabii vivyo hivyo”
Ndugu kumpokea Yesu maana yake ni kukubali mashutumu, kukubali kuonekana mjinga..kukubali kudharauliwa, kukubali kuchukiwa, kukubali dhiki na wakati mwingine kudhihakiwa. Ukiona umempokea Yesu Kristo na unapendwa na watu wote katika hatua za awali basi bado hujampata.
Unapoona aibu leo kuacha kuvaa vimini, na suruali kwasababu unaogopa kuonekana mshamba..Usitegemee kamwe Mungu kutembea na wewe..Bado kusudi la Mungu halipo ndani yako..Unapokataa leo kuacha kuvaa mawigi na hereni na kupaka lipstick, wanja na kujipamba na mavipodozi…ukweli ni kwamba bado Kristo hajaingia ndani yako..upo katika njia ielekeayo upotevuni…pengine kanisani huambiwi haya, kwasababu wanahisi hivi au vile, labda utawakimbia lakini leo umeyasikia na umeyasoma…Utakwenda jehanamu ya moto usipoyaacha!!.
Usipotaka kuacha ulevi kisa tu unaogopa utaonekanaje na jamii ya walevi wenzako..fahamu kuwa Mungu hayupo na wewe kabisa, unapokataa kuacha wizi, uasherati, ufanyaji masturbation, utoaji mimba, ulaji rushwa, ulawiti, ufiraji, utukanaji, uuaji, n.k Mungu yupo mbali na wewe sana..kama ulisikia mahali wanakuambia kuwa ukiambiwa mambo hayo unahukumiwa…Leo hii isikie tena hukumu hiyo!..huko uendako unapotea!.
Mariamu na Yusufu walibaki wenyewe…wanarudi mjini kwao Bethlehemu pengine hata ndugu zao kule hawakuwa na habari nao, hata kuwatengea chumba na kuishia kwenda kupanga, na huko walikopanga hata pia hawakupata nafasi..Mfalme mkuu Yesu Kristo akazaliwa katika zizi la ng’ombe..na Huyo aliyezaliwa katika zizi la ng’ombe leo hii ndio sababu ya wokovu wetu sisi…Leo hii hata kuzaliwa kwake kwenye zizi la ng’ombe ni fahari kwetu. Haleluya!.
Je ungependa kumgeukia leo Kristo kwa moyo wako wote? Na kuacha dhambi na kukubali kubeba msalaba wako na kumfuata yeye na kuwa mwenye haki kama Yusufu?..Kumbuka tunaishi katika siku za mwisho na Kristo yupo mlangoni sana kurudi..Dakika hii tunapozungumza hayupo tena zizini..yupo mbingu za Mbingu, katika Nuru isiyoweza kukaribiwa biblia inasema hivyo katika..1Timotheo 6:14-16.
Kama upo tayari kufanya hivyo sasahivi.. basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie maisha yako yote kama ilivyokuwa hata kwetu sisi. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.
EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, .
NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.
ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.
AMEN.
Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.
Fanya hayo na Bwana azidi kukubariki.
Tafadhali share na wengine, kadhalika kama utapenda kupata masomo haya kwa njia ya whatsapp,au inbox inaweza kututumia ujumbe mfupi inbox, pamoja na namba yako ya whatasapp..Vile vile tunakukaribisha kutembelea website yetu hii kwa mpangilio mzuri wa masomo haya na yaliyotangulia..
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii 0789001312
Mada Nyinginezo:
MARIAMU AKUTANA NA ELISABETI.
MARIAMU
URIMU NA THUMIMU NI NINI KATIKA BIBLIA?
JIHADHARI NA KUOSHWA MIGUU ISIVYOPASWA.
MIILI YA UTUKUFU ITAKUWAJE?
WAKAMCHA BWANA, NA KUITUMIKIA MIUNGU YAO WENYEWE.
WALE WAZEE ISHIRINI NA WANNE (24), WANA KAZI GANI?
MTU ASIYE PAMOJA NAMI YU KINYUME CHANGU.
Tabia pekee inayoufautisha uzao wa Mungu na ule wa ibilisi, ni kwamba ule wa Mungu unapohubiriwa kuhusu habari ya dhambi na madhara ya dhambi baada ya kufa huwa unatabia ya kuitikia mara moja na kwenda kutubu kwa kuugua na kumaanisha kweli kuacha dhambi zake, kama vile watu wa Ninawi. Au pale unapoadhibiwa kutokana na makosa yake, basi ni rahisi kutambua makosa yao na kugeuka, kama vile ilivyokuwa kwa Daudi..
Lakini uzao wa ibilisi ni tofauti sana. Unapoelezwa habari za hukumu, badala utubu, wenyewe huwa unakwenda kinyume unaokuwa wa kwanza kupinga, kwa nguvu zote..badala ushukuru kwa kuelezwa habari za uzima wa milele, utaona unaanza kutoa maneno ya kejeli..Na pale inapotokea Mungu anaudhibu kwa makosa yake, hapo ndipo maneno ya kufuru yataanza kutoka katika vinywa vyao. Labda mtu ni mzinzi halafu Mungu kampiga kwa magonjwa ya zinaa yasiyoponyeka, badala atubu kwa makosa yake aliyoyafanya, utamwona anamtukana Mungu na kusema Mungu gani huyu anaruhusu watu wake wateseke, n.k anasahau kuwa ni kwa makosa yake ndio yamemkuta hayo yote..
Halikadhalika siku ile Mungu atakapoiadhibu hii dunia kwa mapigo yake 7 ya mwisho, kwa wale waovu wote ambao watakuwa wamebakia duniani, biblia inatuambia badala watubu, waombe rehema Mungu awasamehe kwa maovu yao, Lakini kwao itakuwa ni kinyume chake..Watamtukana Mungu na kulikufuru jina lake.
Ufunuo 16:8 “Na huyo wa nne akakimimina kitasa chake juu ya jua, nalo likapewa kuwaunguza wanadamu kwa moto.
9 Wanadamu wakaunguzwa maunguzo makubwa, nao wakalitukana jina la Mungu aliye na mamlaka juu ya mapigo hayo; wala hawakutubu wala kumpa utukufu.
10 Na huyo wa tano akakimimina kitasa chake juu ya kiti cha enzi cha yule mnyama; ufalme wake ukatiwa giza; wakatafuna ndimi zao kwa sababu ya maumivu,
11 wakamtukana Mungu wa mbingu kwa sababu ya maumivu yao, na kwa sababu ya majipu yao; wala hawakuyatubia matendo yao”.
Unaona? Uzao wa Nyoka unavyojidhirisha wazi wazi. Hao ndio wale tangu kuwekwa misingi ya ulimwengu walikuwa wameshaandikiwa hukumu (Ufunuo 13:8 na 17:8). kama tu vile shetani na mapepo yake walivyo leo hii, japo wanajua kuwa wamekosa, wanajua kuwa ziwa la moto linawangoja huko mbeleni lakini mioyo wa toba hata chembe haupo ndani yao, wala hauwezi kuwepo ndani yao kinyume chake ndivyo anavyozidi kuiharibu kazi ya Mungu,Na kumkufuru Mungu.
Leo hii ukishajiona, habari za hukumu hazikuogopeshi tena hata kidogo, Nataka nikuambie hali yako ya rohoni ni mbaya, sana, una dalili ya kuangukia katika hili kundi la watoto wa ibilisi kamili.. Kama leo hii habari za toba ni kama hadithi tu, ukihubiriwa YESU yupo mlangoni kurudi unasema hilo jambo halipo, unaishia kudhihaki tu na kukejeli na kutukana..moyoni mwako.. Nataka nikuambie upo hatarini sana.
Yuda 1:17 “Bali ninyi, wapenzi, yakumbukeni maneno yaliyonenwa zamani na mitume wa Bwana wetu Yesu Kristo,
18 ya kwamba waliwaambia ya kuwa, Wakati wa mwisho watakuwako watu wenye kudhihaki, wakizifuata tamaa zao wenyewe za upotevu.
19 Watu hao ndio waletao matengano, watu wa dunia hii tu, wasio na Roho.
Tukizidi kuwaona Watu wa namna hii basi ni dalili madhubuti inayothibitisha kuwa tunaishi nyakati za mwisho. Na hivi karibuni Bwana atatokea mawinguni na watakatifu wake, kukomesha kauli kama hizo na kufuru zake zote wanadamu wanazozitoa.
Yuda 1:14 “Na Henoko, mtu wa saba baada ya Adamu, alitoa maneno ya unabii juu ya hao, akisema, Angalia, Bwana alikuja na watakatifu wake, maelfu maelfu,
15 ili afanye hukumu juu ya watu wote, na kuwaadhibisha wote wasiomcha Mungu, kwa ajili ya kazi zao zote za upotevu walizozitenda bila kumcha Mungu, na kwa ajili ya maneno magumu yote ambayo hao wenye dhambi wasiomcha Mungu wameyanena juu yake”.
Siku ya hukumu inakuja ndugu, Dunia hii imeshaharibika sana, haina muda mrefu, haya mambo yote unayoyaona yanaelekea kufikia mwisho, usidanganyike na amani unayoiona kama ni amani iliyopo duniani biblia inasema pale wasemapo kuna amani ndipo uharibifu unapokuja kwa ghafla, na hawataokoka (1Wathesalonike 5:1-3)…Kama vile unavyopenda kujionyesha mbele za watu wewe ni mtanashati, unavaa vizuri utokapo kwenda mjini, lakini pengine unamatatizo mengi ya siri..kadhalika watu wote unaopishana nao huko barabarani wamependeza wengine wanamatatizo kuliko yako..kadhalika vyote unavyoviona huko nje na duniani kote vinavyovitua nyuma yake vina matatizo makubwa sana…Uzuri wa dunia usikupumbaze na kudhani dunia haina matatizo…Mwisho wa mambo yote umekaribia..na dakika zinavyozidi kwenda ndivyo tunavyozidi kuukaribia ule mwisho..
Na hata kama dunia itakuwa bado miaka 200 mbele je wewe binafsi utakuwa na muda huo wa kuishi?..Muda wako ni mfupi sana hapa duniani..Kama bado unazunguka zunguka kutafuta njia ya uzima mbali na Kristo, acha kupoteza muda, kama bado unaishi maisha ya dhambi na uovu, hutaki kutega sikio lako kusikia habari za hukumu inayokuja, na umilele unaokuja…wakati utafika utakapoungana na kundi hili kufungua kinywa chako kumtukana Mungu wako aliyekuumba wewe..Lakini itasaidia nini, kwasababu biblia inasema Mungu hadhiakiwi..Utakufa na kuelekea katika lile ziwa la Moto, na nafsi yako itakuwa imesahaulika milele.
Lakini kwanini hayo yote yakukute angali unao uwezo wa kuyakwepa sasa?. Katika Muda huu mfupi uliobakiwa nao Mungu anataka kuyabadilisha maisha yako, akuburudishe akupe na uzima wa milele, akulinde wakati wote ukiwa hapa duniani, akupe na tumaini la uzima wa milele baada ya kufa..Kama upo tayari kufanya hivyo leo, basi ujue atakusamehe makosa yako yote na dhambi zako zote ulizowahi kuzifanya huko nyuma, na kufuru zako zote ulizowahi kumtolea huko nyuma..Pengine ulizitoa kwa ujinga tu, na pasipo kujua madhara yake.. leo hii Yupo tayari kukusamehe..Ni wewe tu kuufungua moyo wako.
Hivyo kama umeamua kufanya hivyo Basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie maisha yako yote kama ilivyokuwa hata kwetu sisi. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.
EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, . NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.
ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.
AMEN.
Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.
Ubarikiwe sana
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii 0789001312
Mada Nyinginezo:
UFUNUO: Mlango wa 16.
CHUKIZO LA UHARIBIFU
MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.
Nifanye nini ili niwe na uhakika nikifa naenda mbinguni?
KUWA MAKINI NA MITANDAO, NI SHIMO REFU.
WALE WAZEE ISHIRINI NA WANNE (24), WANA KAZI GANI?
Nifanye nini ili niondokane na Hofu maishani mwangu?
Neno Hofu linatokana na kuogopa. mfano ukishaogopa kitu Fulani tu basi hapo hapo hofu inaingia na mashaka pia.. tuchukulie mfano umekutana na nyoka njiani, usipomuogopa ni wazi kuwa hofu haiwezi kukuingia bali utaweza aidha kumpisha apite, au kukabiliana naye. Lakini ukishaogopa tu, basi hapo hapo hofu nayo inapata nafasi, na vilevile wasiwasi au mashaka yatakujia ambayo yatakufanya udumu katika hofu ya muda mrefu kiasi kwamba hata siku ukipita karibu na majani na ukahisi kitu kidogo tu kinakugusa mguuni bado utadhani ni nyoka anakutembelea kwasababu mashaka tayari yalishakuingia..
Hivyo chanzo cha Hofu ni kuogopa. Lakini tukirudi katika biblia zipo hofu za aina mbili, ya kwanza ni hofu ya Mungu..Ambayo hii Mungu amekusudia tuwe nayo lakini si kwa lengo la kututisha sisi , hapana bali kwa kutufanya tumche yeye na kuzithamini amri zake.
1Petro 1:17 Na ikiwa mnamwita Baba, yeye ahukumuye kila mtu pasipo upendeleo, kwa kadiri ya kazi yake, enendeni kwa hofu katika wakati wenu wa kukaa hapa kama wageni.
Luka 12:4 “Nami nawaambia ninyi rafiki zangu, msiwaogope hao wauuao mwili, kisha baada ya hayo hawana wawezalo kutenda zaidi.
5 Lakini nitawaonya mtakayemwogopa; mwogopeni yule ambaye akiisha kumwua mtu ana uweza wa kumtupa katika Jehanum; naam, nawaambia, Mwogopeni huyo”.
Unaona? Mtu mwenye hofu ya Mungu, ni wazi kuwa atamuheshimu Mungu, na vilevile ataziogopa hukumu zake, Hivyo itamfanya aishi katika maisha ya uangalifu zaidi na ya kumpendeza yeye.
Lakini zipo hofu nyingine zinazoasisiwa na shetani mwenyewe, mfano wa hizi ni kama.
Hofu ya magonjwa, hofu ya kuhisi hutosamehewa na Mungu (umemkufuru Roho Mtakatifu), hofu ya maadui, hofu za kukataliwa, hofu ya uzee, hofu ya kutokufanikiwa, hofu ya kushindwa, hofu ya kesho itakuwaje, hofu iliyopitiliza ya kifo, hofu ya wachawi na mapepo kama ile waliyokuwa nayo mitume walipokuwa baharini usiku na kuona kivuli tu cha Bwana kinakuja na kuhisi kama ni mzimu umewafuata kuwaua..Hizi zote ni hofu ambazo zina asisiwa na shetani mwenyewe. N.k
Na lengo la shetani kumletea mtu hofu hizi zote ni kwa lengo la kumfanya akate tamaa, au arudi nyuma au akufuru au hata ikiwezekana afikie hatua ya kuutoa uhai wake au asione thamani kabisa ya maisha yake hapa duniani..
Hakuna njia au suluhisho lolote la kuimaliza hofu ndani ya maisha yako, mbali na Mungu, hata uwe umefanikiwa kiasi gani, hata uwe na fedha nyingi kiasi gani, hata uwe na afya njema na elimu nzuri kiasi gani, kama Mungu hayupo ndani yako basi kipengele kimojawapo cha hofu hizi kitakuvaa tu.. Na bado utakuwa unaishi katika mateso na nafsi..
1Yohana 4:16 Nasi tumelifahamu pendo alilo nalo Mungu kwetu sisi, na kuliamini. Mungu ni upendo, naye akaaye katika pendo, hukaa ndani ya Mungu, na Mungu hukaa ndani yake.
17 Katika hili pendo limekamilishwa kwetu, ili tuwe na ujasiri katika siku ya hukumu; kwa kuwa, kama yeye alivyo, ndivyo tulivyo na sisi ulimwenguni humu.
18 KATIKA PENDO HAMNA HOFU; LAKINI PENDO LILILO KAMILI HUITUPA NJE HOFU, KWA MAANA HOFU INA ADHABU; NA MWENYE HOFU HAKUKAMILISHWA KATIKA PENDO.
Unaona hapo? Ukilipata hili pendo la Mungu..Basi uhakika wa kuishinda hofu ya namna yoyote ile upo ndani yako, kwasababu hilo Pendo ndilo litakaloitupa nje hofu ya namna yoyote ile. Kwasababu pale unapoamua tu kumpa Kristo maisha yako, wakati huo huo Amani yake anaanza kuachilia juu yako ili kuiua hofu yote iliyokuwa imeufunika moyo wako kwa muda mrefu.
Yohana 14:27 “Amani nawaachieni; amani yangu nawapa; niwapavyo mimi sivyo kama ulimwengu utoavyo. Msifadhaike mioyoni mwenu, wala msiwe na woga”.
Yesu anatoa amani ambayo huwezi kuipata kwa mtu yeyote, wala kutoka katika dini yeyote wala katika chuo chochote kile, yeye hakufariji katika hofu yako kwa wanadamu wafanyavyo bali anakupa Amani inayoondoa hofu yote.
Mathayo 11:28 “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.
29 Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu;
30 kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi”.
Mimi kabla sijaokoka nilikuwa ni mtu mwenyewe hofu ya hukumu, na ya maisha isiyokuwa ya kawaida, mpaka ilifikia wakati ikanifanya nijione kama maisha yangu hayana thamani yoyote na kujisemea moyoni kwanini Mungu aliniumba mimi si ni heri angeniumba mjusi au ndege ningekuwa sina hatia yoyote ile..lakini ashukuruwe Mungu ulipofika wakati wa YESU kunifungua kutoka katika minyororo hiyo ya shetani..Na kunipa wokovu..Tangu huo wakati hadi sasa nimekuwa nikiisha maisha ya amani nyingi sana..Sina hofu yoyote haijalishi nipo katika hali gani ile amani yake ya tumaini la uzima wa milele linabubujika ndani yangu kila siku.
Sina hofu ya wachawi, wala hukumu, wala ya kushindwa, wala ya chochote kwasababu, Pendo lake kalimwaga ndani yangu..
Vivyo hivyo na wewe leo hii, ukiwa tayari kumruhusu Bwana Yesu ayabadilishe maisha yako, atakupa AMANI hii ambayo anaitoa bure..Unachopaswa kufanya ni kufungua tu moyo wako leo..
Kama upo tayari kufanya hivyo leo basi nataka nikuambie uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao utaufurahia maisha yako yote kama ilivyokuwa hata kwangu mimi. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.
EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.
ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.
AMEN.
Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako.
Na ile amani ya Mungu utaanza kuiona inaumbwa upya ndani yako.
Vile vile baada ya kutubu kwako bila kukawia kawia, unahitaji kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.
Luka 12:32 “Msiogope, enyi kundi dogo; kwa kuwa Baba yenu ameona vema kuwapa ule ufalme”
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii 0789001312Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group
Mada Nyinginezo:
IFANYE KAZI YA MUNGU PASIPO HOFU!
TOA SADAKA ISIYO NA KASORO KWA BWANA.
Nifanye nini ili niwe na uhakika nikifa naenda mbinguni?
WINGU KUBWA LA MASHAHIDI.
KWANINI NAYAWEZA MAMBO YOTE KATIKA YEYE ANITIAYE NGUVU?
NJIA SAHIHI YA KUMPATA MWENZA WA MAISHA KIBIBLIA.
MUUNGANIKO WA MADHEHEBU NI MPANGO WA MPINGA-KRISTO.
UNAMALIZAJE MWAKA WAKO, JE NA MUNGU AU SHETANI?