Category Archive Home

UTAFIKA WAKATI WA WEWE KUACHWA NYIKANI.

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe. Karibu tujifunze biblia leo tena.

Vipo vipindi tofauti tofauti ambavyo kila mkristo atavipitia…maana biblia inasema katika..

Mhubiri 3:1 “Kwa kila jambo kuna majira yake, Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu.2 Wakati wa kuzaliwa, na wakati wa kufa; Wakati wa kupanda, na wakati wa kung’oa yaliyopandwa; ….

4 Wakati wa kulia, na wakati wa kucheka; Wakati wa kuomboleza, na wakati wa kucheza”.

Hata uwe unampendeza Mungu kiasi gani/ hata uwe mkamilifu mbele za Mungu kiasi gani..ni lazima utapitia vipindi vya kulia tu katika Maisha yako!..ni kweli asilimia kubwa ya Maisha yako itatawaliwa na furaha na amani..lakini ni lazima utapitia tu vipindi tofauti tofauti vya kulia na vya huzuni.

Sasa katika Imani pia vipo vipindi ambavyo utamwona Mungu sanaaa..na vipindi ambavyo hutamwona (utaona kuna ukimya Fulani maishani mwako)!…Sio kwamba atakuwa amekuacha kabisa! Au hakufuatilii wala kukusaidia…Hapana atakuwa yupo anakuona na kukujua lakini atakuwa kama amejiepusha na wewe”. Bwana Yesu kuna kipindi alisema “Mungu wangu, Mungu wangu mbona umeniacha”…hivyo huo wakati wa kuachwa upo!…Wengi hawalijui hili, ndio maana wanapopitia kipindi Fulani cha Maisha wanarudi nyuma na kuuacha wokovu…

Sasa leo tutajifunza hicho kipindi ni kipi lakini kabla ya kuendelea mbele zaidi hebu usome mfano huu taratibu sana, kisha tutaendelea…

Luka 15:3  “Akawaambia mfano huu, akisema, 

4  Ni nani kwenu, mwenye kondoo mia, akipotewa na mmojawapo, asiyewaacha wale tisini na kenda NYIKANI, aende akamtafute yule aliyepotea hata amwone? 

5  Naye akiisha kumwona, HUMWEKA MABEGANI PAKE AKIFURAHI. 

6  Na afikapo nyumbani kwake, huwaita rafiki zake na jirani zake, akawaambia, Furahini pamoja nami, kwa kuwa nimekwisha kumpata kondoo wangu aliyepotea. 

7  Nawaambia, Vivyo hivyo kutakuwa na furaha mbinguni kwa ajili ya mwenye dhambi mmoja atubuye, kuliko kwa ajili ya wenye haki tisini na kenda ambao hawana haja ya kutubu”.

Mfano huo unaonyesha ni jinsi gani..Bwana anaweza akawaacha kondoo 99 nyikani na kwenda kumtafuta kondoo mmoja aliyepotea. Umewahi kujiuliza kwanini awaache wale kondoo 99, na kwanini asiende nao?..na kwanini awaache NYIKANI na si kwenye zizi, mahali palipo salama?…

Maana yake ni kwamba anawaacha peke yao sehemu ya wazi isiyo na uzio, ambayo inaonekana ni sehemu hatari, lakini ni salama….Sehemu ambayo Wanyama wakali wanapita, sehemu ambayo inaogopesha!…na mbaya zaidi wanaachwa peke yao…Na lengo la Bwana kuwaacha ni ili akatafute kondoo wengine..

Sasa hao kondoo walioachwa nyikani pengine ni wewe unayepitia ukame sasa, humwoni Bwana kama ulivyomwona wakati umeokoka. Sasa ufanye nini katika hiyo nyika yenye utata?

Kumbuka hapo ni nyikani, mahali pasipo na uzio.. hivyo sio wakati wa kuzunguka zunguka huko na kule…kaa hapo hapo ulipo ndio mahali salama!…hapo hapo mahali Bwana alipokuacha!..(maana yake ni kwamba anaelewa kabisa mahali alipokuacha  utakuwa salama mpaka atakaporudi) tulia hapo hapo hata kama ukitazama kushoto humwoni Bwana, ukitazama kulia umwoni Bwana kama ilivyokuwa hapo kwanza…wewe tambua kuwa hapo ulipo upo sehemu salama..lishike Neno lake lile lile na Imani!…

Haupo ndani ya uzio, ikiwa na maana kuwa  vishawishi vya kukuvuta utoke kwenye mstari wa wokovu, utaviona, usianze kuzurula…wala kuhama hama…tulia hapo hapo….Hali kadhalika pembeni unaweza kuona dalili ya kudhurika na wanyama wanaopita kule, na unaweza kuona kama vile hakuna ulinzi, usiogope! Kaa hapo hapo ndio sehemu salama (aliyekuacha hapo sio mjinga)….Hivyo tumia muda wako kujifunza Neno na kuwaimarisha wengine na kuwalinda wasitoke kwenye hifadhi ya Mungu..kwa kuwafundisha wokovu na kuwafariji mpaka wakati wa Bwana kurudi.

Kumbuka tena kuna wakati Fulani Kristo alikuweka mabegani alipokupata…lakini si wakati wote utakuwa mabegani mwake…wakati ukiwa mabegani mwake ulikuwa unamwona kwenye ndoto kila siku, ulikuwa unauhisi uwepo wake kila mahali, ulipomwomba kitu ulikipata papo kwa hapo…(wakati huo ulikuwa mabegani mwake, mbingu ilifurahia kukupata) lakini hautakuwa hivyo siku zote…utafika wakati utashushwa mabegani na wewe utakwenda kuungana na wenzako nyikani na Bwana atakwenda kutafuta kondoo wengine waliopotea.

Kama ni leo umempa Kristo Maisha yako, basi uwe tayari kwa hicho kipindi kuja mbele yako. Jifunze kumwelewa sana Bwana wakati huu wa sasa, ambao unamwona sana… kwasababu wakati wa ukame utafika!..kama hutamwelewa sana wakati huu, wakati wa kuachwa nyikani utaikimbia na kuiacha nyika.

Na hapo ndipo watu wengi walipopotelea. Imani ni ya kuilinda sana.

Bwana atubariki

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

MAJARIBU MATATU YA YESU KRISTO

MASHAHIDI 40 WALIOUAWA MJINI SEBASTE, NI UJUMBE KWETU.

IKIMBIE DHAMBI KWA GHARAMA ZOZOTE ZILE!

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

UNYAKUO.

JUMA LA 70 LA DANIELI

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

MAJONZI YA MTUME PAULO KWA NDUGU ZAKE.

Ukisoma kitabu cha Warumi sura ya 9, ya 10, na ya 11..utaona mambo mazito sana mtume Paulo aliyokuwa akiyazungumza juu ya ndugu zake wayahudi. Akieleza jinsi neema ya Mungu ilivyoondolewa kwao, kiasi kwamba hata wangehubiriwa vipi injili wasingeweza kuipokea.

Chukua muda kwa wakati wako, pitia sura hizo kwa utulivu sana, ukisoma juu juu hutaona chochote, lakini ukisoma kwa utulivu huku ukimwomba Roho Mtakatifu akusaidie, nakuambia hutaichezea hata kidogo hii neema tuliyopewa sisi watu wa mataifa.

Mtume Paulo alipewa kulijua hilo mpaka akawa anasema, anayo huzuni nyingi, na maumivu yasiyokoma moyoni mwake kwa ajili ya ndugu zake (yaani wayahudi), maumivu ya kila siku, akijua kuwa wokovu umeondolewa kwao..

Kiasi kwamba alitamani hata kama ingewezekana yeye  mwenyewe aupoteze wokovu wake, atengwe na Kristo ili kusudi kwamba ndugu zake wote wapone, basi angefanya hivyo..soma..

Warumi 9:1  “Nasema kweli katika Kristo, sisemi uongo, dhamiri yangu ikinishuhudia katika Roho Mtakatifu,

2  ya kwamba nina huzuni nyingi na maumivu yasiyokoma moyoni mwangu.

 3  Kwa maana ningeweza kuomba mimi mwenyewe NIHARIMISHWE NA KUTENGWA NA KRISTO kwa ajili ya ndugu zangu, jamaa zangu kwa jinsi ya mwili”;

Kauli hiyo si rahisi kuizungumza, lakini kwa huruma ya watu wengine, na huzuni unayoisikia moyoni mwako inakulazimu uitamke, si kwamba unatamani iwe hivyo, lakini kama ingewezekana.. Ni sawa leo umuone mtoto wako mchanga, kapata ajali halafu kakatika mikono, halafu anatapata tapa pale chini kwa maumivu,akilia, ni wazi kuwa utatamani ungeyapitia wewe yale maumivu yake..Kuliko kumuona anaendelea kuteseka katika ile hali.

Ndivyo ilivyokuwa kwa mtume Paulo, alitamani kama ingekuwa inawezekana yeye kuharamishwa, (kufanywa kuwa mwana-haramu,atengwe na Kristo) kusudi kwamba ndugu zake wayahudi waiamini Injili waokolewe.. Lakini ilikuwa haiwezekani.

Ndugu kama hufahamu wakati ule wa kanisa la kwanza ni wayahudi wachache sana, waliiamini Injili, japokuwa ilikuwa ni mamilioni waliokuwa wanaisikia, na ndio maana ukisoma mbele kidogo mtume Paulo anasema.

Warumi 9.27  “..Hesabu ya wana wa Israeli,ijapokuwa ni kama mchanga wa bahari,ni mabaki yao tu watakaookolewa”

Waliokolewa wachache sana, mpaka akasema, kama Mungu asingewaachia mabaki basi wangefananishwa na Sodoma na Gomora,(yaani akiwa na maana asingeokoka myahudi hata mmoja wakati wao)..

Na hiyo yote ilikuwa ni kwasababu waliikataa neema ya wokovu iliyoletwa na Yesu Kristo, alipokuwa duniani, na kuendelea na njia zao za kumtafuta Mungu, huku wamemweka Kristo pembeni. Ikapelekea mlango wa neema kufungwa juu yao. Na ndio maana utaona haijalishi walikuwa na bidii kiasi gani kwa Mungu lakini hawakuweza kuuona mlango wa neema hata kidogo kwasababu tu walimkataa Kristo (kasome Luka 13:34-35). Mtume Paulo alisema hivyo katika ile sura ya 10

Warumi 10:1  “Ndugu zangu, nitakayo sana moyoni mwangu, na dua yangu nimwombayo Mungu, ni kwa ajili yao, ili waokolewe.

2  Kwa maana nawashuhudia kwamba wana juhudi kwa ajili ya Mungu, lakini si katika maarifa”.

Hilo jambo linaendelea mpaka sasa, takribani miaka 2000 imepita, lakini  bado mlango wa neema haujafunuliwa kwao. Na hiyo yote ni ili mimi na wewe (watu wa mataifa), tuipokee neema.

Lakini mwisho kabisa mtume Paulo alipewa siri na Mungu, na siri hiyo aliiweka wazi akataka sisi nasi tuijue (yaani mimi na wewe), kwamba utafika wakati ambao Mungu atawarehemu tena..Na kikisha fika hicho kipindi basi sisi tufahamu Habari yote ndio imeishia hapo, kama mtu yeyote wa mataifa atakuwa hajaingia ndani ya Kristo, ndio basi tena..Soma

Warumi 11:25  “Kwa maana, ndugu zangu, sipendi msiijue siri hii, ili msijione kuwa wenye akili; ya kwamba kwa sehemu ugumu umewapata Israeli, mpaka utimilifu wa Mataifa uwasili.

26  Hivyo Israeli wote wataokoka; kama ilivyoandikwa, Mwokozi atakuja kutoka Sayuni; Atamtenga Yakobo na maasia yake”.

Jiulize wayahudi kwa miaka 2000 wanautafuta uso wa Mungu lakini hawaupati, unadhani siku hiyo neema ikiondolewa kwetu, sisi tutaipatia wapi? Na dalili zote zinaonyesha wakati wao upo karibuni sana…Tayari taifa hili lilishachipuka tangu mwaka 1948, unadhani ni nini kinachosubiriwa hawa watu Mungu asiwageukie? Usiku na mchana wapo pale kwenye “ukuta wa maombolezo wa Nehemia” wanamlilia Mungu awaokoe (hayo yalikuwa ni majonzi ya mtume Paulo)..Lakini Bwana anakawia kidogo kwa ajili yangu mimi na wewe.

Moja ya hizi siku, Mungu atakisikia kilio chao,.mlango wa neema utafunguliwa kwao, na kwetu utafungwa,. Huo ndio ule wakati wa mwenye nyumba kusimama na kuufunga mlango, na watu watakuwa wakisimama nje na kugonga wafunguliwe lakini Bwana atawaambia siwajui mtokako.(Luka 13:25-28)…Duniani kutakuwa na kilio na kusaga meno.

Hivyo tunaposikia maneno haya, tujitathimini Je! Ni kweli bado tupo ndani ya Kristo? Au tupo vuguvugu. Kama wewe unaisikia injili na bado unasua sua basi uingie sasa kwa nia yote acha kusitasita kwenye mawazo mawili muda unazidi kwenda, kwasababu siku hizi ni za mwisho. Lango hili likishafungwa, halitafunguliwa kamwe.

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

MZEITUNI HALISI UTAKAPOPACHIKWA.

MADHARA YA KUTOA MIMBA.

TABIA YAKO NI YA MNYAMA GANI?

MAHALI UNAPOPASWA USIMVUMILIE SHETANI HATA KIDOGO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Ulokole ni nini? Na kwanini wakristo waliookoka wanaitwa walokole?

Ulokole/ Walokole wametoka wapi?


JIBU: Kabla ya kwenda kujua maana ya ulokole, ni muhimu kujua kwanza maana ya neno ‘kanisa’..Tafsiri ya kwanza ya kanisa sio “jengo” bali ni “mkusanyiko wa watu waliomwamini Yesu”..Kwahiyo popote palipo na mkusanyiko wa watu waliomwamini Yesu, tayari hilo ni kanisa hata kama hakuna jengo. Soma mistari ifuatayo itakusaidia Matendo 2:47,1Wakorintho 1:2,14:5,14:23,15:9,16:19 n.k

Na kanisa la Kristo ni moja tu duniani kote ambalo linajulikana kama Bibi-arusi wa Kristo…Hilo ndio linajumuisha wakristo wote waliomwamini Yesu na kuoshwa dhambi zao kwa damu yake (kumbuka hapa hatuzungumzii madhehebu), bali kanisa la Kristo moja ambalo pia sio jengo, bali watu wote duniani waliomwamini Yesu. Na watu hawa ambao ndio kanisa la Kristo, ndio watakaokuja kunyakuliwa siku ya parapanda katika tukio lijulikanalo kama UNYAKUO WA KANISA. Unaitwa unyakuo wa kanisa na si makanisa…kwasababu kanisa la Kristo ni moja tu.

Lakini sasa Kanisa la Kristo ni kweli ni moja lakini lina washirika wengi, na haliwezi lote kukusanyika pamoja na kwa wakati mmoja kufanya ibada, au kumwabudu Mungu, kama ni hivyo basi halina budi kuwepo na makusanyiko tofauti madogo madogo katika kila eneo ili kukamilisha kusudi lile lile la kukusanyika pamoja…Ndio hapo wakristo waliopo Mkoa wa kilimanjaro watakusanyika kivyao, na waliopo Morogoro watakusanyika kivyao huko waliko, n.k..

Lakini kumbuka Imani ni moja, na Kristo ni yule yule anayeabudiwa kote, utendaji kazi unaweza ukawa unatofautiana kulingana na kanisa na kanisa, lakini Imani ni sharti iwe ile ile moja, Bwana mmoja, Roho Mmoja, Ubatizo mmoja sawasawa na (Waefeso 4:3-7), tofauti na hapo hilo ni jambo lingine.

Sasa katika mkoa huo huo wa Morogoro pia sio wakristo wote wapo Morogoro mjini, kuna wengine wapo vijiji vya ndani huko…hao nao hawana budi wakusanyike huko walipo, hakuna sababu ya kusafiri mpaka mjini….na huko vijijini pia kuna uwezekano wa watu wasiwe karibu karibu…hivyo tena yatazaliwa makundi mengine madogo madogo mengi kulingana na mahali, hata inaweza kufikia kanisa likawa na watu watano..lakini yote yenye imani moja. Umbali ndio unaosababisha yajigawanye hivyo.

Sasa haya makanisa mengi madogo madogo ambayo yanakuwa katika eneo husika kwa kiingereza yanajulikana kama LOCAL CHURCHES, (Yaani kanisa la eneo husika aidha mtaa, au kijiji).

Na makanisa haya zamani, kutokana na uchache wa watu yaliyonayo na maeneo yalipo mengi yaliishia kudharaulika… na asilimia kubwa ya washirika wake ni maskini…kwasababu wengi wanaoishi vijijini au katika miji midogo midogo si matajiri kulinganishwa na wale wanaoishi mijini. Hivyo walidharaulika lakini kama biblia inavyosema kuwa..

Yakobo 2:5 “Ndugu zangu wapenzi, sikilizeni, Je! Mungu hakuwachagua maskini wa dunia wawe matajiri wa imani na warithi wa ufalme aliowaahidia wampendao”

Hivyo hao waliodharaulika na kujulikana kama “Local churches”… ndio waliokuwa wa kiroho zaidi..Ishara nyingi na miujiza mingi ilifuatana na haya makanisa madogo madogo, kuliko hayo makubwa, …ndio watu waliokuwa na bidii zaidi ya kumtafuta Mungu, na ndio waliokuwa wanamheshimu zaidi Mungu.

Sasa kutokana na makanisa hayo madogo madogo kufahamika kama local churches…na washirika wao ndio wakajulikana kama “local people”..na kwa lugha yetu hii wakatafsiriwa kama (wa-locally) au WALOKOLE.

Hivyo kama mtu utaitwa mshamba kwa sababu unamwamini Yesu na kuzishika amri zake basi hiyo ni THAWABU. Kuliko kama utaitwa mwenye Elimu na wa-kisasa na huku umemwacha Kristo.

Ufunuo 3:17 “Kwa kuwa wasema, Mimi ni tajiri, nimejitajirisha, wala sina haja ya kitu; nawe hujui ya kuwa wewe u mnyonge, na mwenye mashaka, na maskini, na kipofu, na uchi.

18 Nakupa shauri, ununue kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto, upate kuwa tajiri, na mavazi meupe upate kuvaa, aibu ya uchi wako isionekane, na dawa ya macho ya kujipaka macho yako, upate kuona”

Usijisifie ukubwa wa kanisa unaloabudu, wala wingi wa watu wa kanisani kwenu…Jisifie Yesu uliye naye maishani mwako hata kama upo kanisa la watu watano..jitathmini je! unazishika amri zake hapo ulipo?, je! unaishi kulingana na neno lake? Kiasi kwamba hata parapanda ikilia utakwenda naye!..Je hapa nilipo nanufaika roho yangu kiasi gani?..kama sinufaiki rohoni ni heri nikatafute wenzangu wenye Imani ya kweli hata kama ni wachache, ninusuru roho yangu..kuliko kuendelea kwenye umati wa watu wengi na kuipoteza nafsi yangu…

Ni heri nijulikane mlokole lakini naenda mbinguni kuliko kukubalika na kila mtu, mwisho wa siku naishia kwenda jehanamu. Na kama pia hapo ulipo penye watu wachache huoni dalili ya kuurithi uzima wa milele ni heri ukaenda kutafuta penye watu wengi ambao wanakwenda mbinguni..Lakini siku zote kumbuka mlango ni mwembamba na njia ile imesonga na ni wachache wanayoiona…na mlango ni mpana wa njia iendayo upotevuni na wengi wanauendea.

Bwana akubariki na Bwana atusaidie.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Je! Bikira Maria ni MALKIA WA MBINGUNI?

MIHURI SABA

Wafilisti ni watu gani.

YEREMIA

MWANAMKE ULIYEKOMAA KI-UMRI, ITAMBUE HUDUMA YAKO.

UNYAKUO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

MANENO ALIYOWEZA KUTAMKA YESU TU PEKE YAKE.

Yapo maneno ambayo huwezi kuzungumza, isipokuwa kwanza unaelewa vizuri ni nini unazungumza vinginevyo unaweza kujiweka kwenye kitanzi mwenyewe na kuingia matatizoni..

Kuna wakati Bwana aliwaambia wale watu wanaoshindana naye maneno haya…

“Ni nani miongoni mwenu anishuhudiaye ya kuwa nina dhambi..”? (Yohana 8:46)

Maneno haya si mepesi kabisa, Kumbuka juu kidogo tu kwenye sura hiyo hiyo swali la namna hii hii aliwauliza wale watu waliomfumania yule mwanamke katika uzinzi, lakini majibu yake ni kuwa sio tu kutomtupia yule mwanamke mawe, bali pia waliona aibu kuendelea kubaki maeneo yale, kwa mtihani huo mgumu waliopewa.

Yohana 8:7 “Nao walipozidi kumhoji, alijiinua, akawaambia, Yeye asiye na dhambi miongoni mwenu na awe wa kwanza wa kumtupia jiwe.

8 Akainama tena, akaandika kwa kidole chake katika nchi.

9 Nao waliposikia, wakashitakiwa na dhamiri zao, wakatoka mmoja mmoja, wakianzia tangu wazee hata wa mwisho wao;

akabaki Yesu peke yake, na yule mwanamke amesimama katikati”.

Unaona? Lakini hapa na yeye pia anajiweka katika hicho kitanzi na kuwauliza watu.. Ni nani miongoni mwenu anishuhudiaye ya kuwa nina dhambi?

Jaribu kujiweka wewe katika hiyo nafasi ukiwa kama kijana wa miaka 33 ambaye tayari umeshapitia mambo mengi katika maisha, halafu unasimama katikati ya umati wa watu wanaoshindana na wewe, unawauliza ni nani kati yenu anayenishuhudia kuwa nina dhambi?

Je! Wewe unaweza kusema hayo maneno?(Mimi siwezi)..Ndugu zako wote wamesimama karibu nawe , marafiki zako wote uliowahi kuishi nao na kusoma nao, wote pia wamesimama karibu hapo, majirani zako nao wapo, wafanyakazi wenzako wanasimama hapo vilevile halafu unawauliza wote “Kati yenu ninyi ni nani anayenishuhudia kuwa nina dhambi”..

Ni nani alishawahi kuniona au kusikia nimemsengenya mtu, ni nani nilishawahi kumdanganya au alishawahi kunisikia nadanganya, ni wapi nilishawahi kutamani, ni wapi nilishawahi kumvunjia mtu heshima, au kumwonea wivu, au kumwekea kinyongo, au kuonyesha unafki, kumfokea, kumtukana? ..Kama yupo hapa asimame, au ajitokeze, asimeme wewe siku fulani nilikuona ukikwepa kodi kwenye ile biashara yenu ya useremala…

Lakini wote waliosimama pale, hakuonekana hata mmoja aliyekuwa na la kumshitaki Yesu..sio jambo rahisi kama tunavyofikiri,

Na ndio maana mahali pengine biblia inasema..

1Petro 2:22 “Yeye hakutenda dhambi, wala hila haikuonekana kinywani mwake.”

Ni Yesu peke yake, katika ulimwengu mzima, katika vizazi vyote, ambaye tangu amezaliwa mpaka anakufa, hakuwahi kutenda dhambi hata moja, japokuwa alipitia majaribu mazito ya dhambi kuliko hata sisi.

Ndugu yangu Kwa YESU pekee mimi nimetia nanga! Sijui kwako?, kwasababu hakuna mwingine kama yeye, huyu pekee ndio wa kumtumainia, ni huyu pekee ndio wa kumtegemea kutusaidia kushinda huu ulimwengu kama yeye alivyoshinda, ni huyu huyu pekee ndio atakayetuokoa tukimwamini. Mimi na wewe tukimfanya kuwa rafiki wa maisha yetu, jambo la kwanza na la ajabu ni kuwa anatusamehe dhambi zetu zote, halafu anatuhesabia haki bure pasipo matendo yetu kwa neema, kiasi kwamba mbele za Mungu tunaonekana kuwa tumestahili haki yote.

Kisha baada ya hapo anamtuma Roho wake Mtakatifu ndani yetu. Ambaye kazi yake ni kutupa sisi nguvu ya kuishinda dhambi kama yeye alivyoishinda, na kutuongoza katika kuijua kweli yote.

Hivyo kama bado hujaokoka, saa ya wokovu ni sasa, fanya haraka mkaribishe Yesu maishani mwako. Kama umezichoka dhambi kweli, kama hutaki nafsi yako ipotee, basi mkimbilie Yesu haraka maadamu muda upo, Lakini tukikataa kuyasikia maneno yake basi yeye naye atatuacha, na kutuona tu kama sio watu tuliochaguliwa na Baba yake soma..

8:46 “Ni nani miongoni mwenu anishuhudiaye ya kuwa nina dhambi? Nami nikisema kweli, mbona ninyi hamnisadiki?

47 Yeye aliye wa Mungu huyasikia maneno ya Mungu; hivyo ninyi hamsikii kwa sababu ninyi si wa Mungu”.

Natumaini wewe leo utayasikia maneno yake.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

RABI, UNAKAA WAPI?

NENO HILI NI GUMU,NI NANI AWEZAYE KULISIKIA?

Yeshuruni ni nani katika biblia?

KUMBUKA, VIVUKO VYA YORDANI VINAKUNGOJA MBELENI.

NA MTU MMOJA AKAVUTA UPINDE KWA KUBAHATISHA, AKAMPIGA MFALME

UNYAKUO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

AHADI ZA MUNGU.

Ahadi za Mungu ni za kweli kabisa,.. Lakini tatizo kubwa linalotukabili  sisi wanadamu ni kutokujua njia Mungu anazozitumia kutimiza ahadi zake.

Na hiyo inawafanya watu wengi waishie kukata tamaa pale anapoona mbona ahadi za Mungu zimechelewa, pengine nimemkosea Mungu, au Hanisikii..

Fahamu kuwa wakati wa Mungu kutimiza ahadi zake, sio lazima uwe ule wakati ulioupanga wewe Tena mara nyingi huwa anauchagua ule wakati ambao haufahau, wakati ambao mambo yote yanaokana yameharibika, mipango imevurugika, umeshachelewa, hapo ndipo Mungu anasimama ili kutimiza ahadi zake kwako.

  • Utamwona Ibrahimu, alipokuwa na miaka 75 Mungu alimwambia nitakupa mwana, na nitakufanya kuwa taifa kubwa.. Jaribu kufiria katika uzee ule, ungedhani labda, baada ya mwaka mmoja tu, ndio Mungu angemtimizia ahadi yake, ili viungo vya uzazi visife kabisa..Lakini tunaona Mungu aliendelea kusubiri, hadi miaka karibia 25 mbeleni, akiwa sasa na umri karibia na miaka 100 ndio Mungu anamtembelea na kumpa mtoto.

Na hakupewa tu mtoto basi, bali na mwili wake pia ulirudishwa na kuwa kama wa kijana, yeye pamoja na mke wake Sara.

Lakini Ibrahimu katika kipindi chote hicho hapo katikati hakumkosea Mungu imani na ndio maana akaitwa baba wa Imani, tunasoma hilo katika..

Warumi 4:18 “Naye aliamini kwa kutarajia yasiyoweza kutarajiwa, ili apate kuwa baba wa mataifa mengi, kama ilivyonenwa, Ndivyo utakavyokuwa uzao wako.

19 Yeye asiyekuwa dhaifu wa imani, alifikiri hali ya mwili wake uliokuwa umekwisha kufa, (akiwa amekwisha kupata umri wa kama miaka mia), na hali ya kufa ya tumbo lake Sara.

20 Lakini akiiona ahadi ya Mungu hakusita kwa kutokuamini, bali alitiwa nguvu kwa imani, akimtukuza Mungu;

21 huku akijua hakika ya kuwa Mungu aweza kufanya yale aliyoahidi.

22 Kwa hiyo ilihesabiwa kwake kuwa ni haki”.  

  • Unaona? Vivyo hivyo Yusufu naye , tayari alishapewa neon la ahadi katika ndoto, kuwa upo wakati atakuzwa kiasi kwamba mpaka ndugu zake watakuja kumwinamia. Lakini hilo halikutimia kwa wakati ule ule alioonyeshwa, kinyume chake akiwa na umri wa miaka 17 aliuzwa na ndugu zake, akawa mtumwa kule Misri mpaka anafikia miaka 30 ndio hizo ndoto zinakuja kutimia.

Na hazikutimia akiwa nyumbani mwa Potifa hapana, bali zilitimia akiwa gerezani, mahali ambapo hapana tumaini lolote, la kuishi. Kwa kipindi karibu cha miaka 2 akiwa kule gerezani, siku moja isiyokuwa na jina Mungu alimtembelea na kumwinua, akatoka na kufanywa kuwa Waziri mkuu na makamu wa Raisi wa taifa kubwa lililokuwa lina nguvu kuliko yote ulimwenguni wakati ule (Misri).

Hivyo zipo ahadi za Mungu nyingi katika biblia ambazo tukianza kuzichambua hapa moja baada ya nyingine hatuwezi kumaliza zote..

Ahadi za Mungu kwa mkristo:

Hiyo ni kutupa tu hamasa mimi na wewe ambao pengine umesubiria ahadi za Mungu kwa muda mrefu sasa na bado hujaona matokeo yoyote. Unachopaswa kufanya ni kusubiri ndugu yangu, huku ukiendelea kumtumikia Mungu kwa moyo ule ule wa kwanza.

Unaweza ukawa ni mtumishi wa Mungu, na umejaribu kuacha kila kitu ili tu uifanye kazi yake..Nataka nikuambie endelea hivyo hivyo, upo wakati utafika ile hadi yake ya kuwa UTAPATA MARA MIA, itatimia juu yako, haijalishi ni miaka miwili tokea sasa, au 5 au 10 au 20, lakini fahamu kuwa ukiendelea kung’ang’ania njia yako bila kuiacha, utavuna ulichopanda.

Mungu atakulipa tu, mema, ukiwa hapa hapa duniani, na vyote ulivyovipoteza utarejeshewa vyote mara mia. (Marko 10:28-30) Hivyo endelea kumtumikia MUNGU.

Vilevile Bwana aliposema, usisimbukie maisha ule nini, unywe nini, avae nini, bali utafute kwanza ufalme wake na haki yake na hayo mengine utazidishiwa. Basi fahamu kuwa ukijikita kuutafuta kwanza uso wa Mungu, na kutaka kumjua yeye, ni ahadi yake kuwa  hatakuacha ufe njaa, bali atahakikisha kuwa anakuhudumia ili uendelee kuishi,..Kwasababu unautafuta ufalme wake..Hiyo ni kweli kabisa hawezi kudanganya.. Ahadi za Mungu ni thabiti.

Vivyo hivyo na ahadi nyingine yoyote aliyowahi kukuahidia , endelea tu kuingoja, wakati wake utafika tu,. Kikubwa usiuache wokovu wako na utakatifu wako kama wewe umeokoka.

Lakini kama hujaokoka, basi hakuna ahadi yoyote ya Mungu inayoweza kutimia juu yako. Hivyo unachopaswa kufanya ni kumpa Kristo maisha yako ili ayaokoe, kwani hizi ni siku za  mwisho na Unyakuo upo karibu,..Moja ya hizi siku mabadiliko makubwa sana yatatokea duniani. Na dhiki kuu itaanza, hivyo mgeukie muumba wako kabla ya hizo za hatari hazijakufikia kwa ghafla.

Bwana akubariki.

Ahadi za Mungu ni Yakini.

Mada Nyinginezo:

KWA KUVUMILIA AKAIPATA ILE AHADI.

TABIA YA KIPEKEE USIYOIJUA KUHUSU NENO LA MUNGU.

UNYAKUO.

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

FAHAMU JINSI KRISTO ANAVYOPONYA WATU ROHO.

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!

Rudi Nyumbani:

Print this post

YEREMIA

Yeremia alikuwa ni nabii aliyezaliwa Israeli (Kwa asili alikuwa ni Myahudi)..na alitokea nyakati za mwisho mwisho kabisa, karibia na wakati wa Israeli kuchukuliwa mateka Babeli. Ni nabii aliyetabiri na kushuhudia kuteketezwa kwa mji wa Yerusalemu na watu kuchinjwa na baadhi kuchukuliwa mateka. Tafsiri ya jina lake ni “Yehova atapandisha au atanyanyua” .Unaweza kutazama tafsiri za baadhi ya majina hapa >>>Maana ya majina na tafsiri zake

Kama jina lake lilivyo, Yeremia alitabiri Israeli kunyanyuliwa tena na Mungu baada ya kushushwa chini..alisema..Bwana atawarudia tena watu wake baada ya kukaa ugenini miaka 70.

Yeremia 25:11 “Na nchi hii yote pia itakuwa ukiwa, na kitu cha kushangaza; nayo mataifa haya watamtumikia mfalme wa Babeli miaka sabini.

12 Na itakuwa miaka hiyo sabini itakapotimia, nitamwadhibu mfalme wa Babeli, na taifa lile, asema Bwana, kwa sababu ya uovu wao, nayo nchi ya Wakaldayo pia; nami nitaifanya kuwa ukiwa wa milele”.

Yeremia tofauti na manabii wengine, yeye aliitwa na Mungu katika utumishi akiwa na umri mdogo na ni moja ya manabii waliopitia mateso mengi sana katika huduma zao, lakini Mungu hawaacha!..na Mungu alimtuma kwa mataifa mbali mbali…Manabii wengine wa Israeli kama Samweli, Ezekieli,Musa, Malaki na wengineo hawakutumwa kwa watu wa Mataifa, isipokuwa kwa watu wa jamii yao tu (yaani kwa wasraeli wenzao!). Yeremia na wengine wachache ndio pekee waliotumwa watoke nje ya mipaka ya Israeli kusema na watu wa Mataifa ya mbali.

Yeremia 1:4 “Neno la Bwana lilinijia, kusema,

 5 Kabla sijakuumba katika tumbo nalikujua, na kabla hujatoka tumboni, nalikutakasa; nimekuweka kuwa nabii wa mataifa.

  6 Ndipo niliposema, Aa, Bwana MUNGU! Tazama, siwezi kusema; maana mimi ni mtoto.

7 Lakini Bwana akaniambia, Usiseme, Mimi ni mtoto; maana utakwenda kwa kila mtu nitakayekutuma kwake, nawe utasema kila neno nitakalokuamuru. ”

Mungu alimtuma Yeremia kwa mataifa mengi ulimwenguni, kuyatangazia hukumu…kwamba yote yatawekwa chini ya utawala mgumu wa Nebukadneza kama yasipotubu na kuacha njia zao mbaya…na mataifa hayo yote hayakuisikiliza sauti ya Yeremia nabii na yote kuishia kuwekwa chini ya mikono ya Nebukadneza (kasome Yeremia 25:15-28) ikianza na Yuda. (Na Yeremia  aliifanya kazi hiyo ya Mungu kwa uaminifu mpaka alipokuwa mzee.)

Kwa maelezo ya urefu kuhusu Nabii huyu, vitabu alivyoandika, na huduma yake ilivyokuwa kwa mapana fungua hapa >> Vitabu vya Biblia (sehemu ya 7)

Wito wa Mungu hauna mipaka, Mungu anaweza kukuita na kukutuma katika umri mdogo kama Yeremia, na vile vile anaweza kukuita na kukutumia katika umri mkubwa, kama Elisha. Kwa wito wowote ule tutakaoitwa na Mungu, tunapaswa tuwe waaminifu.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 4

MAOMBI YA TOBA.

Kwanini Kristo hakuitwa Imanueli badala yake akaitwa Yesu?

PARAPANDA ITALIA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Yesu ni Mungu?, Na Kama ni Mungu kwanini alikufa?

SWALI: Je! Yesu ni Mungu? Na Kama ni Mungu kwanini alikufa?


JIBU: Yesu alikuwa ni Mungu katika mwili (1Timotheo 3:16)…lakini hakuja kutafuta kuabudiwa wala kusujudiwa!…Mpaka Mungu amevaa mwili na kuja ulimwenguni, maana yake hajaja kutafuta kuabudiwa, kama angekuwa amekuja kutafuta utukufu wake basi, kulikuwa hakuna haja ya kuuvaa mwili na kushuka duniani, naamini Mbingu ilikuwa inamtosha…. hivyo ni lazima atakuwa amekuja kwa kusudi lingine na si la kutafuta utukufu. Hapo ndipo wengi wa wasio wakristo wanaposhindwa kuelewa, na baadhi ya walio wakristo.

Unapoona askari wa kuongoza barabarani (Traffic man), kaondoka barabarani na kaenda nyumbani kubadilisha nguo zake hizo nyeupe…na akavaa nguo za kiraia na kuingia mtaani basi ni dhahiri kuwa huko mtaani alikokwenda hajakwenda kutafuta kuongoza magari bali kaenda kutafuta mambo yake mengine ya kawaida..labda anaenda hospitalini au sokoni au kusalimia ndugu na marafiki, au kufuatilia mambo yake mengine ambayo ni tofauti na ya kikazi….. (ni kweli bado atabaki kuwa askari, lakini yupo nje ya ofisi yake), hivyo hataweza kuyatumia yale mamlaka aliyonayo ya kuongoza magari,…na akiwa barabarani na nguo zake za kiraia, hata watu wanaweza wasimtambue kama ni askari, atakuwa kama raia wengine tu, na magari atakuwa anayakwepa tu kama raia wengine, na atazingatia sheria zote za barabarani kama raia wengine…

Na Bwana Yesu ni hivyo hivyo…alipokuwa mbinguni alikuwa ni Mungu, anayestahili kuabudiwa na kuheshimiwa…aliposhuka duniani alikivua kile cheo cha Kiungu…na kuwa kama mwanadamu (kwa lengo la kuja kumkomboa mwanadamu na si kuabudiwa kama Mungu)..na baada ya kumaliza akarudi mbinguni alikotoka katika cheo chake.

Hivyo akiwa kama mwanadamu alikuwa hana budi aishi kama wanadamu wengine, hana budi awe mtu wa ibada kama watu wengine, hana budi ale, anywe, alale, achoke, apitie yote mwanadamu wa kawaida anayopitia na hata ikiwezekana afe…ili tu kusudi lake lililomleta duniani litimie la kumkomboa mwanadamu…lakini alikuwa bado ni Mungu.

Wafilipi 2: 5 “Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu;

6 ambaye yeye mwanzo alikuwa YUNA NAMNA YA MUNGU, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho;

7 bali ALIJIFANYA kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu;

8 tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba”.

Umeona hapo mstari wa 7?..unasema “ALIJIFANYA”..kama unakielewa Kiswahili vizuri utakuwa unajua maana ya “KUJIFANYA”..Maana yake ni kama kujigeuza/kuigiza kuwa kitu Fulani na kumbe sio…kwa lengo la kutimiza kusudi Fulani tu!…Hivyo Bwana Yesu aliyejifanya kuwa hana utukufu…ili ashuke aje kutukomboa na kutuonyesha njia jinsi mwanadamu kamili anayemcha Mungu anapaswe awe.

Hivyo kufa kwa Bwana Yesu, hakumfanyi yeye asiwe Mungu..na pia muujiza mkubwa duniani na mbinguni sio kutokufa!!… Huo ni muujiza mdogo sana…..“miujiza mkubwa ni uwezo wa mtu kuutoa uhai wake na kisha kujirudishia ule uhai”..Huo ndio muujiza mkubwa kuliko yote!..na uwezo huo alikuwa nao Yesu pekee yake.

Yohana 10:17 “Ndiposa Baba anipenda, kwa sababu nautoa uhai wangu ili niutwae tena.

18 HAKUNA MTU ANIONDOLEAYE, BALI MIMI NAUTOA MWENYEWE. NAMI NINAO UWEZA WA KUUTOA, NINAO NA UWEZA WA KUUTWAA TENA. Agizo hilo nalilipokea kwa Baba yangu”.

Sasa utauliza ni wapi, Yesu aliutoa uhai wake mwenyewe?…kasome Luka 23:46-47. Bwana Yesu aliutoa uhai wake mwenyewe! Hakuna mtu aliyemsaidia kuutoa..hata Pilato alishangaa imekuwaje amewahi kufa kiasi kile (Marko 15:44). Na aliurudisha uhai wake mwenyewe baada ya siku tatu (kule kaburini hakuna mtu aliyeenda kumfufua au kumwombea afufuke).

Alijirudishia uhai wake mwenyewe!..Nadhani huo ni muujiza mkubwa sana.. Je wewe unaweza kufanya hivyo????

Hata mfano nikikuwekea watu wawili mbele yako mmoja hawezi kuukata mguu wake na mwingine anao uwezo wa kuukata na kuurudisha….nikakwambia kati ya hao wawili ni yupi hapo wa kuogopwa zaidi??..Bila shaka utaniambia “Yule mwenye uwezo wa kuukata mguu wake na kisha kujirudisha tena ndiye wa kuogopwa zaidi kuliko huyo mwingine”.

Kwahiyo kuupima uungu wa Bwana Yesu na kifo chake ni hoja dhaifu!!..miungu ya kipagani ndio isiyo na uwezo wa kufanya hayo..lakini Mungu wa mbingu na nchi (YESU KRISTO) anaweza kufanya mambo yote. Mpaka sasa katika historia hajatokea nabii yoyote wala mtume yeyote aliyofanya miujiza kama aliyofanya Bwana Yesu, sasa kwanini asiwe Mungu?. Na siku moja atarudi na kila jicho litamwona na kila goti litapigwa, na kila kinywa kitakiri…Wengi itakuwa ni jambo la kushtukiza sana kwao, kwasababu hawataamini kwamba kweli ndiye!..kwasababu walidanganyika wakiwa duniani kwamba hatarudi.

Lakini anatupenda na wala hataki mtu yoyote apotee bali wote tuifikie toba, ili tuokoke na tuje kutawala naye milele.

Bwana atubariki tuzidi kumjua yeye!

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

Mbona Mungu anaruhusu watu wapate shida, ilhali ana uwezo wa kutuepusha?

Katika biblia Neno “Mshenzi” linatajwa.Kwanini liwekwe?

Kile kinara cha Taa ndani ya Hekalu la Sulemani kilikuwa kinawakilisha nini?

Je! Ni kweli ubatizo wa maji hatuuhitaji tena?

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Yuko azuiaye sasa hata atakapoondolewa! ni nani huyo?

SWALI: Naomba unisaidie hii 2 wathesalonike 2:7 “Yuko azuiaye sasa Hadi atakapoondolewa, naomba unisaidie huu mstari unamaanisha Nani huyo anayezuia na Ni kwa nini?”


JIBU: Ukianzia kusoma tokea mistari ya juu kidogo utaona inazungumzia habari za mpinga-Kristo ambaye biblia inamtaja kama “Asi” kwamba mwisho wa dunia hautafika kwanza kabla ya yeye kufunuliwa hapa duniani..

Kwasababu wakati ule, watu wa kipindi kile walidhani kuwa pengine wapo tayari katika wakati wenyewe wa mwisho wa dunia, Lakini mtume Paulo aliwapa siri ambayo alifunuliwa na Roho Mtakatifu na kuwaambia, ule mwisho hautakuja kwa namna hiyo, bali ni sharti kwanza yule Asi (yaani Mpinga-Kristo) afunuliwe duniani, aonekane kazi zake na mienendo yake, na kwamba watu wakishamwona huyo sasa ndio wajue kuwa dunia itakuwa na kipindi kifupi sana cha kuendelea kuwepo, ambacho si zaidi ya miaka 7 kulingana na unabii wa kibiblia.

Lakini pamoja na hayo aliendelea kuwasisitiza kuwa japokuwa Asi mwenyewe (Mpinga-Kristo), hajafunuliwa kwa wakati wao lakini ile siri yake ilikuwa imeshaanza kutenda kazi, akiwa na maana kuwa mienendo ya mpinga-Kristo ilikuwa imeshaanza kuonekana tangu ule wakati isipokuwa tu ilikuwa katika siri..Bado haijapata nafasi yote.

2Wathasalonike 2:5 “Je! Hamkumbuki ya kuwa wakati nilipokuwapo pamoja nanyi naliwaambieni hayo?

6 Na sasa lizuialo mwalijua, yule apate kufunuliwa wakati wake.

7 Maana ile siri ya kuasi hivi sasa inatenda kazi; lakini yuko azuiaye sasa, hata atakapoondolewa.

Sasa swali ni kwanini siri hiyo ya kuasi isijidhihirishe yote tangu ule wakati hata sasa ambapo imepita zaidi ya miaka 2000?.

Mtume Paulo anasema ni kwasababu Yupo azuiaye, Na huyo sio mwingine zaidi ya “Roho Mtakatifu”. Ikumbukwe kuwa Roho Mtakatifu ndiye mtunza uhai wa vitu vyote na viumbe vyote tangu mwanzo, Mungu asingeiumba hii dunia iwe makao mazuri ya watu kama sio Roho wake kutua kwanza juu ya uso wa nchi. Hii ikiwa na maana akiondolewa basi dunia inarudia katika hali yake ya ukiwa kama ilivyokuwa hapo mwanzo.

Leo hii unaona ni kwanini watu wanamtafuta Mungu, ni kwasababu Roho Mtakatifu anafanya kazi ndani yao, ni kwanini wanaomba?, sababu ni hiyo hiyo ya Roho Mtakatifu, ni kwanini duniani hakuna vita vikali vya kiatomiki ambavyo vinaweza kuichakaza dunia mara moja nikwasababu Roho Mtakatifu anazuia..Ni kwanini Volcano, haviimezi dunia yote, ni kwasababu Roho Mtakatifu anazuia.

Lakini upo wakati ambapo, Mungu atamwondoa duniani kazi yake itakapoisha. Ambayo itaisha na watakatifu wa Mungu watakaonyakuliwa siku ile kwenda mbinguni. Maana yake kwamba ikitokea leo hii unyakuo umepita, basi na kazi ya roho Mtakatifu ya kuokoa (yaani ya kuwavuta watu kwa Mungu), na kuzuia amani duniani nayo inakuwa imeisha, Anaondoka..Ndio hapo yule Asi (yaani Mpinga-Kristo) naye anapata nafasi ya kufanya uharibifu wake wa kuleta dhiki kuu duniani, hapo ndipo mataifa yote duniani nayo yanapata nafasi ya kukusanyika kuleta vita kuu ya dunia ambayo haijawahi kutokea, hapo ndipo baadhi ya mapepo yaliyokuwa kifungoni yanaachiliwa duniani kwa muda ili kuwatesa watu, hapo ndipo dunia nayo itapoteza muhimili wake, matetemeko makubwa yatatokea duniani, volcano zitafumuka ardhini, jua litazima na mwezi kuwa damu na nyota kuanguka..na dunia itarudia kuwa ukiwa kama ilivyokuwa kabla ya Edeni.

Yaani hayo yote yatatimia ndani ya kipindi kifupi tu cha miaka saba.

Jiulize, unyakuo ukipita leo, mimi na wewe tutakuwa wapi?. Bwana alisema tutawezaje kupona tusipouthamini wokovu mkuu namna hii?

Hizi ni nyakati za hatari. Tubu dhambi kama bado hujafanya hivyo, na kama tayari basi zidi kudumu ndani ya neema ya Kristo mpaka siku ya mwisho wa unyakuo.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

Je! Shetani alitolea wapi uovu?

Nitaitofautishaje sauti ya Malaika na ya Roho Mtakatifu?

 Je! Ni sahihi kutumia maji ya upako,katika kufanya maombezi?

WAKATI ULIOKUBALIKA NDIO SASA.

JE NI HALALI KUOA WAKE WENGI AU KUTOA TALAKA?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Agano jipya ni nini?

Agano jipya ni nini?


Tukitamka neno “agano jipya”  tunathibitisha kuwa lilishawahi kuwepo agano la zamani (La kale) hapo kabla.

Hivyo ili kufahamu agano jipya ni nini, ni vizuri kwanza ukapata msingi wa agano la Kale, lilikuwaje.

Kama tunavyojua Biblia imeundwa na maagano makuu wawili, yaani jipya na la kale.

  1. Agano la Kale:

Sasa msingi wa agano la kale ulitoka kwa mtu mmoja aliyeitwa Ibrahimu. Mungu alipomuita hakumuita ilimradi tu, bali aliingia agano naye akamwambia atambariki na kumfanya kuwa baba wa mataifa mengi, ikiwa tu atakuwa mkamilifu na atakwenda  katika njia zake..Tusome.

Mwanzo 17:1 “Abramu alipokuwa mtu wa miaka tisini na kenda, Bwana akamtokea Abramu, akamwambia, Mimi ni Mungu Mwenyezi, uende mbele yangu, ukawe mkamilifu. 

2 Nami nitafanya agano langu kati ya mimi na wewe, nami nitakuzidisha sana sana. 

3 Abramu akaanguka kifudifudi. Mungu akamwambia, akasema, 

4 Mimi, agano langu nimefanya nawe, nawe utakuwa baba wa mataifa mengi, 

5 wala jina lako hutaitwa tena Abramu, lakini jina lako litakuwa Ibrahimu, kwani nimekuweka uwe baba wa mataifa mengi. 

6 Nitakufanya uwe na uzao mwingi sana, nami nitakufanya kuwa mataifa, na wafalme watatoka kwako. 

7 Agano langu nitalifanya imara kati ya mimi na wewe, na uzao wako baada yako, na vizazi vyao, kuwa agano la milele, kwamba nitakuwa Mungu kwako na kwa uzao wako baada yako. 

8 Nami nitakupa wewe na uzao wako baada yako nchi hii unayoikaa ugeni, nchi yote ya Kanaani, kuwa milki ya milele; nami nitakuwa Mungu wao. 

9 Mungu akamwambia Ibrahimu, Nawe ulishike agano langu, wewe na uzao wako kwa vizazi vyao baada. yako. 

10 Hili ndilo agano langu utakalolishika, kati ya mimi na wewe, na uzao wako baada yako, Kila mwanamume wa kwenu atatahiriwa. 

11 Mtatahiriwa nyama ya magovi yenu, na jambo hilo litakuwa ishara ya agano kati ya mimi na ninyi”.

Unaona, Jinsi Mungu alivyokuwa mwaminifu, baadaye Mungu akaja kumtimizia kweli agano aliliomuahidia, kwa jinsi uzao wake ulivyokuwa unaongezeka duniani kwa kasi, Lakini wakati huo wote uzao wake ulikuwa haumjui Mungu vizuri, ulikuwa bado haujajua kanuni za agano hilo ambalo Mungu aliloingia na Ibrahimu baba yao linavyopaswa liwe..

Ndio hapo wakiwa kule jangwani sasa Mungu anamtumia Musa kusema nao na kuwapa sheria na amri za kuzishika ili wafanikiwe..

Sheria hizo ndizo zilizoandikwa katika vitabu vya Torati: yaani

  • Mwanzo
  • Kutoka
  • Hesabu
  • Mambo ya Walawi
  • Kumbukumbu la Torati.

Hivyo vitabu hivyo vitano vilikamilisha Sheria yote ya Agano hilo ambalo Mungu aliingia na Ibrahimu.

Lakini hiyo peke yake haikuwa inatosha wana wa Israeli kumfahamu Mungu katika ukamilifu wote, Hivyo ilipasa  Mungu azungumze nao mara kwa mara kupitia watu mbalimbali wakamilifu na manabii wake.. Mfano tunamwona mtu kama Ayubu, Esta, Ruthu, kwa kupitia maisha ya hawa Mungu aliwafundisha wana wa Israeli jinsi ya kuishi katika njia zake. Vilevile akawa anasema nao mara kwa mara kupitia manabii wake wengi na waamuzi na mfano Samweli, Isaya, Yeremia, Danieli, Yona,Malaki N.k.

Hivyo kwa kupitia hao pia, na vitabu vyao walivyoviandika, iliwasaidia wana wa Israeli walishike na kulikumbuka agano ambalo aliingia nao zamani.

Kwahiyo tunapovisoma vitabu 39 vya Agano la Kale,.. tunafahamu kuwa ni jumuisho la sheria zote na kanuni zote za Mungu kwa wale alioingia nao agano kupitia Ibrahimu.

Sasa mpaka hapo umeshapata msingi wa Agano la kale kwa ufupi lilipoanzia..


      2.  Tukirudi kwenye agano jipya..

Hilo ni agano lingine lili bora zaidi kuliko lile la Ibrahimu.,

Hili nalo  Mungu aliingia katika agano na mtu mmoja tu, kama vile alivyoingia na Ibrahimu.. Na mtu huyo si mwingine zaidi ya YESU KRISTO.

Ibrahimu alipewa tu uzao wake wa kimwili, lakini huyu alipewa uzao wa wote wenye mwili wakimwamini tu kwa kuzaliwa mara ya pili.

Na ndio maana kuna umuhimu wa kila mmoja wetu kuzaliwa mara ya pili ili tufanyike kuwa uzao wake. yeye mwenyewe alisema..

Yohana 3:3  “Yesu akajibu, akamwambia, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa mara ya pili, hawezi kuuona ufalme wa Mungu”.

Na kubatizwa kwetu ndio ishara ya tohara yenyewe ya rohoni kama ilivyokuwa kwa Ibrahimu na watoto wake wote walipotahiriwa kwa kutolewa magovi. Vivyo hivyo na sisi tunapaswa tukabatizwe kama ishara ya kutahiriwa mioyo yetu.

Lakini tukishazaliwa mara ya pili, hilo tu peke yake haitoshi, ni sharti pia tujue kanuni, na amri Mungu anazozitaka za agano hili ili tuweze kudumu ndani yake. Kama Uzao wa Ibrahimu ulivyopewa.

Hapo ndipo vitabu vya Injili ya Yesu Kristo, na vile  vya mitume, viliandikwa kwa ajili yetu ili sisi sote tutakapovisoma na kuvishika basi tuweze kudumu na kuimarika katika hilo agano jipya la Damu ya Yesu Kristo.

Ndipo hapo tunakutana na vitabu 27 vya agano jipya.

Hivyo kwa kwa hitimisho fupi.. Agano jipya ni agano Mungu aliloingia na Yesu pamoja na uzao wake wote. Ambao mimi na wewe tunahesabiwa katika uzao huo  kwa kumwamini Yesu na kubatizwa.

Tukifanikiwa kufanya hivyo basi na baraka zote, Mungu alizomuahidia Yesu Kristo, na sisi sote pia tunazishiriki na kuzirithi, ikiwemo uzima wa milele.

Bwana akubariki.

Je! Na wewe upo ndani ya agano jipya? Kama bado basi fanya hima ukaribishe Yesu leo ndani ya maisha yako akuokoe ufanyike uzao wa kifalme. Kumbuka hii ni neema ambayo sisi watu wa mataifa hatukustahili, hivyo uiichezee hata kidogo..

1Petro 2:9  “Bali ninyi ni mzao mteule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu wa milki ya Mungu, mpate kuzitangaza fadhili zake yeye aliyewaita mtoke gizani mkaingie katika nuru yake ya ajabu; 10  ninyi mliokuwa kwanza si taifa, bali sasa ni taifa la Mungu; mliokuwa hamkupata rehema, bali sasa mmepata rehema”.

Haleluya.

Mada Nyinginezo:

TOBA IGUSAYO MOYO WA BWANA.

Je! habari ya Yusufu, inabeba ujumbe gani kwa agano jipya?

Bwana aliposema “sikuja kutangua torati bali kuitimiliza” alikuwa anamaanisha nini?

UTIMILIFU WA TORATI.

TAZAMA, MWISRAELI KWELI KWELI, HAMNA HILA NDANI YAKE!

Sanduku la Agano lilikuwa linawakilisha nini katika Agano jipya?

KUTAHIRIWA KIBIBLIA

MWAKA WA BWANA ULIOKUBALIWA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

UPENDO WA MUNGU.

Upendo wa Mungu ni upi?


Kwanza kabla ya kufahamu upendo wa Mungu upoje, ni muhimu kufahamu aina za upendo. Zipo aina kuu tatu za upendo.

  1. Aina ya kwanza ni Upendo unaotokana na hisia, ujulikanao kama EROS. Huu ndio upendo wa mke na mume, katika biblia tunaweza kuona Sulemani akiueleza kwa mapana na marefu katika kitabu cha Wimbo ulio Bora.

Wimbo ulio bora 1:13 “Mpendwa wangu ni kama mfuko wa manemane Ukilazwa usiku maziwani mwangu. 

14 Mpendwa wangu ni kama kishada cha hina, Katika mizabibu huko Engedi. 

15 Tazama, u mzuri, mpenzi wangu, U mzuri, macho yako ni kama ya hua.  16 Tazama, u mzuri, mpendwa wangu, Wapendeza, na kitanda chetu ni majani; 

17 Nguzo za nyumba yetu ni mierezi, Na viguzo vyetu ni miberoshi.”

  1. Upendo wa pili ni ule unaozuka kutokana na mahusiano mtu mmoja alio nao kwa mwingine, almaarufu kama PHILEO,. Huu unaweza ukawa upendo wa mtu na ndugu yake, mchezaji mwenzake, mfanyakazi mwenzake, mwanafunzi mwenzake, mkristo mwenzako, n.k. ni upendo ambao kama hakuna kitu cha kuwaunganisha pamoja, au faida fulani kupatikana, hauwezi kuzaliwa.

Upendo wa namna hii sio upendo mkamilifu sana (ikiwa na maana haujafikia viwango vile vyenyewe),  mkristo, kwasababu hata wenye dhambi wanaweza kuwa nao, Na ndio maana Bwana Yesu alisema..

Mathayo 5.46  “Maana mkiwapenda wanaowapenda ninyi mwapata thawabu gani? Hata watoza ushuru, je! Nao hawafanyi yayo hayo?

47  Tena mkiwaamkia ndugu zenu tu, mnatenda tendo gani la ziada? Hata watu wa mataifa, je! Nao hawafanyi kama hayo?

48  Basi ninyi mtakuwa wakamilifu, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu”.

  1. Upendo wa tatu ndio mkuu kuliko yote unajuliana kama AGAPE (UPENDO WA KI-MUNGU).

Huu ndio Upendo ambao Yesu alikuwa anaulenga kila mahali, Ni upendo usiokuwa na masharti, Unampenda mtu bila ya kuwa na sababu yoyote ya kukufanya umpende, haijalishi awe nawe anakupenda au hakupendi, anakuchikia au hakuchukii,  anakusema vibaya au hakusemi vibaya..Unapenda bila masharti, aina hii ya upendo ndio aliokuwa nao Yesu.

Biblia imeziorodhesha tabia za Upendo huo wa ki-Mungu katika kitabu cha Wakoritho wa kwanza. Tusome.

 1Wakoritho 13:4  “Upendo huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu; upendo hautakabari; haujivuni; 5  haukosi kuwa na adabu; hautafuti mambo yake; hauoni uchungu; hauhesabu mabaya;

6  haufurahii udhalimu, bali hufurahi pamoja na kweli;

7  huvumilia yote; huamini yote; hutumaini yote; hustahimili yote.

8  Upendo haupungui neno wakati wo wote; bali ukiwapo unabii utabatilika; zikiwapo lugha, zitakoma; yakiwapo maarifa, yatabatilika”.

Hivyo mpaka hapo sasa umeshauelewa huu upendo wa Mungu ni upi? Ni upendo usiojali wewe ni nani na ndio maana biblia ilisema..

Yohana 3:16 “Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele”.

Hivyo kama wewe ni mwenye dhambi ujue kuwa Mungu anakupenda na ndio maana anataka kukuokoa usiende kuzimu na dhambi zako, haijalishi ulimkosea kiasi gani, leo hii yupo tayari kukusamehe na kukupa uzima wa milele, Hivyo usikiapo ujumbe huu, usiufanye moyo wako kuwa mgumu bali, mgeukie yeye na akusemehe dhambi zako.

Hizi ni siku za mwisho ukifa na dhambi zako hakika utakwenda kuzimu.

Shalom.

Upendo wa Mungu, ni wa kipekee sana.

Mada Nyinginezo:

JINSI NEEMA YA MUNGU ILIVYOKUWA KUBWA KWA MKE WA LUTU.

JINA LA MUNGU NI LIPI?

UUMBAJI BORA WA MUNGU, UPO NDANI YA MWANADAMU.

UNYAKUO.

HUYU MELKIZEDEKI NI NANI?

Kwanini Yesu Kristo ni mwana wa Adamu?

WINGU KUBWA LA MASHAHIDI.

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita..

Rudi Nyumbani:

Print this post