Maombi(uombaji) ni nyenzo namba moja ya kumfikisha mtu uweponi mwa Mungu kwa haraka sana. Na kama tunavyofahamu sikuzote mtu yeyote aliyepo mbele za uso wa Yehova mwenyewe, uwezekano wa yeye kujibiwa mahitaji yake yote upo. Hivyo shetani kwa kulijua hilo hataki, mtu wakati wowote mtu afike huko hivyo anachofanya ni kumletea tu saikolojia za kipepo ili zimfanye asidhubutu kutaka kwenda kusali wakati wowote.
Na baadhi ya saikolojia hizo ni hizi:
Siku zote Kabla ya mtu hajafikiria tu kwenda kuomba, mawazo ya kwanza yanayomjia kichwani pake ni “nimechoka”..Ataanza kufikiria Nimekuwa kazini siku nzima, sijapata muda wa kupumzika, hata kidogo, hapa nilipo usingizi wenyewe umenikamata, najisikia homa homa, hivyo wacha leo nipumzike nitaomba siku nyingine..
Mwingine atasema nimefanya kazi ya Mungu siku nzima, tangu asubuhi hadi jioni hata sasa bado wapo watu wananitegemea nikawafundishe, nina mialiko mingi ya mikutano hivyo wiki hii nimechoka wacha nisiende kusali..
Lakini Bwana wetu Yesu Kristo yeye alikuwa anachoka kuliko hata sisi kwa utumishi mgumu kwa kuzunguka huko na kule, Utaona upo wakati baada ya kuwahubiriwa makutanao siku nzima mpaka imeshafika jioni badala awaage aende akapumzike kidogo, kinyume chake aliwalazimisha mitume wake watangulie mashuani, yeye akabaki nyuma kwenda kusali mlimani, alikaa kule masaa mengi, akisali, sio kwamba hakuwa amechoka hapana. Lakini alijua umuhimu wa maombi.
Mathayo 14:22 “Mara akawalazimisha wanafunzi wake wapande chomboni na kutangulia mbele yake kwenda ng’ambo, wakati yeye alipokuwa akiwaaga mkutano.
23 Naye alipokwisha kuwaaga makutano, alipanda mlimani faraghani, kwenda kuomba. Na kulipokuwa jioni, alikuwako huko peke yake.
24 Na kile chombo kimekwisha kufika katikati ya bahari, kinataabika sana na mawimbi; maana upepo ulikuwa wa mbisho.
25 Hata wakati wa zamu ya nne ya usiku Yesu akawaendea, akienda kwa miguu juu ya bahari.”
Sisi pia, kwanini Neno “Nimechoka” linataka kuchukua nafasi ya maombi yetu?.Kwamwe tusikiendekeze hicho kigezo cha nimechoka kuchukua nafasi yetu ya maombi.
2. Sina Muda wa kuomba:
Neno lingine shetani analoliwekwa kwenye vichwa vya watu ni hili “sina muda wa kuomba”..kwani nimetingwa na mambo mengi, na shughuli nyingi nipo bize sana…Nimekutana na Watu wengi wakiniambia maneno haya, wanasema wanashindwa kwenda ibadani au kuomba kwasababu ya kukosa muda….Wapo pia watumishi wa Mungu wanaosema mimi nipo bize sana na huduma hivyo sina muda wa kuomba binafsi muda mrefu, ninamialiko mingi ya semina, sehemu mbali mbali..
Lakini nataka nikuambie pia tunaye Bwana wetu Yesu Kristo ambaye ndiye kielelezo cha utumishi wetu, yeye alikuwa bize kuliko hata sisi, muda mwingine makutano walikuwa wanamsonga, muda wote wanataka awafundishe lakini biblia inatuambia..alijieupua, akaenda kutafuta mahali pa utulivu akaomba huko..
Luka 5:15 “Lakini habari zake zikazidi kuenea, wakakutanika makutano mengi wamsikilize na kuponywa magonjwa yao.
16 Lakini yeye alikuwa akijiepua, akaenda mahali pasipokuwa na watu, akaomba”.
Alifanya vile kwasababu alijua hata ile huduma aliyokuwa anaifanya ilihitaji maombi ili iweze kusimama, ni jambo la kushangaza kama tutasema sisi ni watumishi wa Mungu halafu tunakosa muda wa kuomba…Nasi pia tujiepue tupate muda wa kuomba binafsi.
Jambo lingine ni hili shetani analileta kichwani,.. mbona ninaweza kuyamudu tu Maisha yangu bila maombi?..Ni kweli utayamuda Maisha yako ya kidunia, lakini sio Maisha yako ya wokovu.
Utamudu kwenda disko, utamudu kuendelea kuwa mlevi, utamudu kuiba, utamudu kuwa mwasherati na utamudu kuwa bize na kazi zako kuliko hata hata kumtafuta Mungu na mambo mengine yanayofanana na hayo utayamudu kwasababu hayo yote hayahitaji maombi.
Lakini ukisema umeokoka halafu sio mwombaji, basi ujue hutaweza kuyashinda majaribu ya aina yoyote ile, Bwana Yesu mwenyewe alisema..Kesheni mwombe msije mkaingia majaribuni..Unadhani alikuwa anatania, unadhani shetani ataufurahia wokovu wako, ustarehe tu, halafu mwisho wa siku uende mbinguni?. Atakutafuta tu na kama wewe sio mwombaji basi huwezi kuchomoka,..na ndio maana taamaa za mwili unashindwa kuzitawala, kwasababu huombi, unashindwa kuwa na kiasi kwasababu muda wa maombi huna, hauuhisi uwepo wa Mungu maishani mwako, kwasababu wewe sio mwombaji..
Yakobo 4:1 “Vita vyatoka wapi, na mapigano yaliyoko kati yenu yatoka wapi? Si humu, katika tamaa zenu zifanyazo vita katika viungo vyenu?
2 Mwatamani, wala hamna kitu, mwaua na kuona wivu, wala hamwezi kupata. Mwafanya vita na kupigana, wala hamna kitu kwa kuwa HAMWOMBI!”
Maombi ni Mafuta ya wokovu, kama vile gari lisivyoweza kwenda bila Petrol vivyo hivyo, wokovu wako hauwezi kupiga hatua yoyote bila kuwa maombi..
Saikolojia nyingine ya ki-shetani ni hii ya kudhani kuwa maombi yako hayawezi kujibiwa. Unaona kama ukiomba utapoteza muda bure,.Nataka nikuambie, Maombi yote yanasikiwa ikiwa utaomba sawasawa na mapenzi yake, lakini sio jambo la kufanya siku moja halafu basi Kesho unaendelea na mambo yako mengine, maombi ni sehemu ya Maisha ya mkristo ni mwendelezo, majibu ya maombi mengine yanakuja kwa kuomba tena na tena, leo, Kesho, Kesho kutwa n.k…lakini katika kuomba huko Bwana Yesu ametupa uhakika kuwa Ombi lolote la namna hiyo mwisho wa siku ni lazima lijibiwe tu..haliwezi kuachwa..
Luka 18:1 “Akawaambia mfano, ya kwamba imewapasa kumwomba Mungu sikuzote, wala wasikate tamaa”.
Mathayo 7:7 “Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtaona; bisheni, nanyi mtafunguliwa; 8 kwa maana kila aombaye hupokea; naye atafutaye huona; naye abishaye atafunguliwa”.
Mwisho, nataka nikuambie Wapo watu wanadhani wanaweza kuvumbua njia nyingine ya kuwasiliana na Mungu kirahisi au watapata suluhisho la matatizo yao Zaidi ya maombi..Fahamu kuwa Bwana wetu Yesu ameshatusaidia kufanya utafiti, sasa usitafute utafiti mwingine wa kwako wewe au wa kwangu mimi mbali na ule aliouthibitisha Yesu wa maombi..Yeye alikuwa hana dhambi hata moja, alikuwa ni mtakatifu sana, lakini katika utakatifu wake wote huo hakutupilia mbali suala la maombi alilifanya kama nyenzo ya yeye kufikia malengo yake, alifanya maombi kuwa sehemu ya Maisha yake..
Na wakati mwingine alikuwa anaomba kwa jasho na machozi mengi, na hata damu ilimtoka, akisihi mpaka akawa anasikilizwa…
Vinginevyo asingepokea kitu, Je mimi na wewe ambao si wakamilifu kama Bwana Yesu tunapaswaje?..tunaona raha gani kuishi Maisha ya kutokuomba halafu tunajiita bado ni wakristo..?
Waebrania 5:7 “Yeye, siku hizo za mwili wake, alimtolea yule, awezaye kumwokoa na kumtoa katika mauti, maombi na dua pamoja na kulia sana na machozi, akasikilizwa kwa jinsi alivyokuwa mcha Mungu”;
Hivyo tusitafute njia ya mkato..Kama tunataka tumwone Mungu akitembea katika Maisha yetu kwa ukaribu Zaidi na sisi, huu ndio wakati wa kuanza upya tena kwa nguvu za Maombi. Bwana alituambia walau saa moja kwa siku..Hivyo tujitahidi, tupambane, tushindane, tusiruhusu uongo wa shetani utuvurugie uombaji wetu, tusiruhusu, kukosa muda kutuvurugia ratiba yetu, tusiruhusu kutegemea nguvu zetu na akili zetu kutuharibia uombaji wetu..
Tuombe, tuombe, tuombe..
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
https://wingulamashahidi.org/mafundisho-ya-ndoa/
Unajua ni kitu gani kilikuwa kinaendelea siku chache kabla ya Nuhu kuingia Safinani?…Mungu alimwambia Nuhu ingia wewe na mke wako na watoto wako na wanyama wote ndani ya safina..
Sasa kitendo tu cha Nuhu kuingia mule , muda huo huo Mungu aliufunga mlango. Lakini cha kushangaza zaidi ni kuwa tendo la kufunga mlango halikumaanisha kuwa mvua itaanza kunyesha siku hiyo hiyo, hapana tunasoma mvua haikunyesha siku ile ile, bali ilisubiri muda wa siku saba, ndipo baadaye gharika ikashuka.. Mwanzo 7:13-17
Jambo tunaweza kuona hapo ni kuwa mlango wa wokovu ulikuwa umeshafungwa siku kadhaa nyuma kabla ya siku yenyewe ya maangamizi kufika..Pengine baadhi ya watu kuona jinsi mlango ule ulivyofungwa kwa namna isiyokuwa ya kawaida, walighahiri mawazo yao, wakamfuata Nuhu, wakamgongea mlango, wakimwambia Nuhu tufungulie tumegundua ni kweli hii dunia inakwenda kuangamizwa yote hivi karibuni hivyo na sisi tunataka kuzisalimisha roho zetu, tunakusihi utufungulie na sisi tuingie ndani…
Jibu la Nuhu, lilikuwa ni nini?, Mimi sikuufunga mlango, ni Mungu ndiye aliyeufunga na sijui katumia njia gani kuufunga kwasababu sioni hata komeo, wala kufuli pembeni, ni kama vile tumesakafiwa humu ndani, nitawasalidieje ndugu zangu..Ombeni, kwa Mungu labda atawasikia na kuwafungulia huu mlango kwasababu siku yenyewe ya maangamizi naona bado haijafika..
Pengine wale watu wachache waliokuwa pale nje, wakaanza kumlilia Mungu kwa machozi sana ili wafunguliwe mlango lakini hakukuwa na aliyejibu.. wengine walidhihaki na kuona Nuhu ndo kaamua kabisa kujisakafia ndani afie kule,..lakini wale wachache pengine wakaendelea kumsihi Nuhu kutafuta njia ya kuingia safinani.. Siku tano kabla ya gharika, wakaongezeka na wengine tena, nao pia wakawa wanamwambia Nuhu tufungulie ndugu zako, kwa maana kutokana na hali hii tunaoiona inavyoendelea sasa hivi, hii dunia siku chache sana inakwendwa kuangamizwa tufungulie Nuhu, tumetubu na ndio maana tumekuja kabla ya maangamizi yenyewe kufika tunakuomba utufungulie….Lakini Nuhu jibu lake lilikuwa ni lile lile sikuufunga mlango mimi..
Siku tatu kabla gharika, watu bado wanabisha hodi tu, wanatafuta upenyo mdogo lakini hawaoni, siku mbili kabla ya gharika, wanazidi kumsumbua Nuhu labda atafute kiupenyo cha mlango kwa huko ndani uvunje tuingie, lakini biblia inatuambia safina ile ilipigwa lami nje na ndani, hivyo hakukuwa na uwezekano wa kuivunja kiurahisi…
Mpaka ilipotimia siku ile ya gharika yenyewe kushuka,walikuwepo wengi sana pale nje ya safina wakimlilia Mungu, na kubisha hodi kwa bidii sana..lakini walikuwa tayari wameshachelewa..
Ndugu Biblia inatuambia wazi kama ilivyokuwa wote wakaangamia…hakuna aliyesalimika….Sasa biblia inatuambia kama ilivyokuwa katika siku za Nuhu ndivyo itakavyokuja kuwa katika siku za kuja kwake mwana wa Adamu..Bwana Yesu alisema wazi kabisa..
Luka 13:24 “Jitahidini kuingia katika mlango ulio mwembamba, kwa maana nawaambia ya kwamba wengi watataka kuingia, wasiweze.
25 Wakati mwenye nyumba atakaposimama na kuufunga mlango, nanyi mkaanza kusimama nje na kuubisha mlango, mkisema, Ee Bwana, tufungulie; yeye atajibu na kuwaambia, Siwajui mtokako;
26 ndipo mtakapoanza kusema, Tulikula na kunywa mbele yako, nawe ulifundisha katika njia zetu.
27 Naye atasema, Nawaambia, Siwajui mtokako; ondokeni kwangu ninyi nyote mlio wafanyaji wa udhalimu.
28 Ndipo kutakapokuwa na kilio na kusaga meno, mtakapomwona Ibrahimu na Isaka na Yakobo na manabii wote katika ufalme wa Mungu, nanyi wenyewe mmetupwa nje”.
Wengi tunadhani mambo hayo yatayokea baada ya kufa, jibu la ni La!, Hayo mambo yatakuwa ni hapa hapa duniani kipindi kifupi kabla ya unyakuo kupita…kuna watu watatamani sana waingizwe katika orodha ya watakaonyakuliwa lakini itakuwa ni ngumu tena..
Fahamu kuwa kitendo cha unyakuo sio kitendo cha kuotea tu, kwamba tunaishi ilimradi tu,halafu siku ile ikifika tutatoweka tu kwa bahati, hapana, Unyakuo unao HATUA zake..Na wale watakaonyakuliwa watajijua kabisa…jambo ambalo hawatajua ni siku yenyewe ya kuondoka, lakini watapewa uhakika huo wa kuondoka wakiwa bado wapo hapa hapa duniani kama vile ilivyokuwa kwa Eliya..
Sasa uhakika huo watautolea wapi?
Ukisoma kitabu cha ufunuo sura ya 10 yote utaona yapo mambo ambayo Yohana alionyeshwa akiwa katika kile kisiwa cha Patmo yahusuyo sauti za zile ngurumo saba, ambapo alipotaka kuziandika aliambiwa asubiri kwanza asiandike….Sasa hizo ni siri ambazo Mungu amezitunza kwa ajili ya bibi-arusi wake anayejiwekwa tayari leo hii kwa unyakuo.. Siri hizo hazijaandikwa mahali popote kwenye biblia..Lakini wakati huo utakapofika, Mungu atazihubiri duniani…Na hizo ndizo zitakazomvuta bibi-arusi ndani ya safina tayari kwa unyakuo siku yoyote..
Sasa wale ambao sio bibi-arusi wa Kristo,watakaposikia hizo jumbe zinahubiriwa, ndipo na wao watakaposhtuka ahaa!! Kwa mambo haya, ndio tunajua sasa unyakuo kweli ni siku yoyote..Hapo ndipo na wao watakapoanza shamra shamra za kumtafuta Mungu kwa kumaanisha, ndipo watakapoanza kubisha na kugonga kwa nguvu, wakitamani nao wahesabiwe..Siku hizo wataitafuta hiyo neema kwa bidii zote lakini hawataipata…
kwasababu mwana wa Adamu ameshasimama na kuufunga mlango…
Hao ndio wale wanawali wapumbavu, waliokwenda kutafuta mafuta na waliporudi wakakuta mlango umeshafunga..Ndivyo itavyokuja kuwa siku za hivi karibuni..(Soma Mathayo 25:1-12)
Nataka nikuambie ukishasikia tu ujumbe mwingine wa tofauti unapita duniani kote kwa nguvu nyingi za Mungu na udhihirisho mwingi, na kusikia mambo mageni masikioni mwako, yahusuyo safari ya kwenda nyumbani kwa Baba, kama bado wewe ni mkristo vuguvugu, basi ujue habari yako imeshakwisha mlango wa neema umekwisha fungwa..Ni heri kama utakuwa umesimama katika utakatifu na imani kwasababu hapo ndipo utakapopata uhakika wa kuondoka kwako hivi karibuni..Lakini kama wewe ni vuguvugu kwasababu hapa hatuzungumzii wale ambao ni baridi kwasababu wao hawataelewa chochote kitakachokuwa kinaendelea, tunamzungumzia wewe ambaye ni vuguvugu, habari yako siku hiyo itakuwa imekwisha..
Wewe ndio itakaoshuhudia wenzako wakienda mbinguni,..Utakuwa umelala na mume wako ambaye kila siku unamwona anajibidiisha kumtafuta Mungu na wewe utajikuta umeachwa, utakuwa unazungumza na mke wako na ghafla ataondoka, mwanao atakuwa amekwenda shule siku hiyo utashangaa harudi…Na ndio maana biblia inatuasa, TUJIWEKE TAYARI, kwa maana hatujui ni siku gani ajapo Bwana ..Hii dunia haina muda mrefu, Unyakuo si jambo la kulichukulia juu juu tu, ukiukosa ule, hali itakayokuwa inaendelea hapa duniani haielezeki, Bwana Yesu anavyosema utalia na kusaga meno alimaanisha kweli hivyo kwamba kusema hivyo kuwa kutakuwa na maombolezo ya ajabu kwa wale ambao watakuokosa unyakuo.
Bwana atutie nguvu katika safari yetu.
Maran Atha.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
USIPOWATAMBUA YANE NA YAMBRE, KATIKA KANISA LA KRISTO, UJUE UMEPOTEA.
Shalom. Jina kuu la Mwokozi wetu Yesu Kristo, libarikiwe.
Karibu tujifunze biblia.
Mathayo 3:5 “Ndipo walipomwendea Yerusalemu, na Uyahudi wote, na nchi zote za kandokando ya Yordani;
6 naye akawabatiza katika mto wa Yordani, huku wakiziungama dhambi zao.
7 Hata alipoona wengi miongoni mwa Mafarisayo na Masadukayo wakiujia ubatizo wake, aliwaambia, Enyi wazao wa nyoka, ni nani aliyewaonya ninyi kuikimbia hasira itakayokuja?
8 Basi zaeni matunda yapasayo toba;
9 wala msiwaze mioyoni mwenu kwamba, Tunaye baba, ndiye Ibrahimu; kwa maana nawaambia ya kwamba Mungu aweza katika mawe haya kumwinulia Ibrahimu watoto.
10 Na shoka limekwisha kuwekwa penye mashina ya miti; basi kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa motoni”
Soma tena mstari wa 7 “Hata alipoona wengi miongoni mwa Mafarisayo na Masadukayo wakiujia ubatizo wake, aliwaambia, Enyi wazao wa nyoka, ni nani aliyewaonya ninyi kuikimbia hasira itakayokuja? ”
Tunaweza kuiweka vizuri hiyo sentensi kwa namna hii “Enyi wazao wa nyoka ni nani aliyewadanganya(maana yake ni nani aliyewaonya) kwamba mtaiepuka hukumu inayokuja kwa njia hiyo mnayoitaka nyie?”..Njia gani?…Njia hiyo ya kuja kutaka kubatizwa na huku bado hamtaki kuacha dhambi zenu…Ni nani aliyewahubiria kuwa mtaikwepa hukumu kwa namna hiyo?…Maana yake mnafikiri kuwa kwa kuja kubatizwa tu hiyo inatosha kuikwepa hukumu itakayokuja….Mnajidanganya!…ZAENI MATUNDA YAPATANAYO NA TOBA!…Maana yake ni kwamba baada ya kutubu ishini kulingana na kutubu kwenu..Kama ulikuwa ni mwasherati, tubu na UACHE UASHERATI! Usiufanye tena, kama ulikuwa na kiburi tu na uache kuwa mwenye kiburi tena, kama ulikuwa mlevi unatubu na kuachana na ulevi wako, n.k..Huu ubatizo hautakuwa na msaada wowote kwenu kama mtakuja tu kubatizwa na huku bado hamjaacha matendo yenu mabaya. Huo ndio ujumbe Yohana Mbatizaji alikuwa anataka kuwapa wale Mafarisayo na Masadukayo.
Mafarisayo walisikia injili ya Yohana, wakaogopa, lakini wakasema aah ngoja tukabatizwe na sisi ili pengine tutaokoka huko mbeleni, lakini mioyoni mwao walikuwa hawana mpango wa kubadilika haka kidogo,..Walitaka kuugeuza ubatizo wa Yohana kama dini tu!..kama ni Liturujia mpya tu ya kufuata, kama katekisimo tu!..lakini walikuwa hawajui lengo kuu la ule ubatizo ni nini.. Lengo lake kuu lilikuwa ni kutubu na KUACHA DHAMBI!..sio kwenda kulowekwa kwenye maji na kurudi kuendelea na Maisha yako ya dhambi kama kawaida, na jina lako liwe limeshaandikwa mbinguni. Sio hivyo kabisa.
Vivyo hivyo na leo, ubatizo sio dini, na wala sio lebo ya kwamba Mungu anataka watu waliobatizwa ndio wawe wamepata tiketi ya kuingia mbinguni haijalishi wanaishije, yeye anataka tu watu wabatizwe.. hapana! Mungu anataka watu waliotubu na KUACHA DHAMBI. Hao ndio mbele za Mungu ubatizo wao una maana lakini kama mtu hujatubu kwa KUACHA DHAMBI, mtu huyo anamdhihaki Mungu.
Ukimuuliza mtu je umeokoka anakujibu, mimi nimebatizwa!..ukimuuliza tena je una uhakika wa kwenda mbinguni anakujibu ndio nilishabatizwa. Ubatizo hauna uhusiano wowote na kwenda mbinguni kama hujatubu kwa kuacha dhambi..Ndicho mafarisayo walichokuwa wanaenda kufanya kwa Yohana.
Umesema tu umetubu lakini bado unaendelea kuvuta sigara, bado unaendelea na uasherati, unaendelea na ulevi na ulawiti na usagaji, na pornography, halafu unasema umebatizwa au unakwenda KUTAFUTA UBATIZO, Ukidhani ndio unampendeza Mungu, na kwamba ndio utakwenda mbinguni..nataka nikuambie hapo unakwenda kujitafutia tu Laana badala ya Baraka.
Kutubu maana yake ni kugeuka na kuacha kile ulichokuwa unakifanya, na sio kusema tu mdomoni nimeacha na ilihali Maisha yako bado yapo vile vile. Ikiwa haupo tayari kuokoka, basi ni heri usiugize wokovu, wala usijiite hivyo, kwasababu ndivyo unavyomtia Mungu wivu kwa mienendo yako.
Watu wa Ninawi Mungu aliwasamehe kwasababu Aliona matendo yao kwamba wamegueka, wameacha mambo maovu waliyokuwa wanayafanya, hiyo ndiyo ikawafanya Waepukane na hukumu ile ambayo ilikuwa inawajia, na Mungu hakuona midomo yao kwamba wametubu kwa midomo ndipo awasamehe, hapana! bali matendo yao ndiyo yaliyosababisha wao kusamehewa.
Yona 3:10 “Mungu akaona MATENDO YAO, ya kuwa wameiacha njia yao mbaya. Basi Mungu akalighairi neno lile baya, ambalo alisema atawatenda; asilitende”
Hali kadhalika, usifanyike kuwa mzao wa nyoka, kwa kutafuta kutimiza maagizo ya Mungu na huku moyoni huna mpango wa kutenda mapenzi yake. Hizo ni tabia za Nyoka kibiblia. Mafarisayo wanamwendea Yohana kubatizwa na huku mioyoni mwao ni wale wale watu wenye viburi, wanaopenda utukufu, wenye wivu, wenye chuki, …maana japokuwa walikuwa wanamwendea Yohana kubatizwa lakini mioyoni mwao walikuwa wanamchukia n.k
Kama umeamua kumfuata Yesu leo, basi kubali pia kubeba na msalaba wako, kabla ya kwenda kubatizwa piga gharama kabisa kwamba unakwenda kuacha dhambi moja kwa moja, kwamba dunia ndio umeipa mgongo hivyo, msalaba mbele, ulimwengu umeuacha nyuma..Na kwa kufanya hivyo ndipo utaona nguvu za Mungu katika Maisha yako zikikusaidia na kukuongoza na ndivyo Mungu atakavyokukaribia Zaidi na kukupenda. Na kukubariki.
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
AINA YA MAADUI UTAKAOKUTANA NAO KATIKA SAFARI YAKO YA WOKOVU.
Nyimbo za Injili ni zipi?, waimbaji wanapaswa waitendeje huduma hiyo?..
Shalom. Karibu tuongeze maarifa kuhusu Neno la Mungu..Tukilijua Neno la Mungu vyema, tutayajua mapenzi ya Mungu na hivyo tutaishi kulingana na yeye anavyopenda na tutabarikiwa.
Moja ya karama ya muhimu sana katika Mwili wa Kristo ni karama ya uimbaji. Sasa ni wazi kuwa mtu yoyote anaweza kuimba, awe mwanamume au mwanamke..Lakini yupo ambaye akiimba nyimbo au akiimbisha basi kunaambatana na nguvu fulani za kipekee za Roho Mtakatifu. Sasa nguvu hizo sio za kuwafanya watu waanguke au walie..Hapana bali nguvu hizo ni zile zinazomfanya mtu apate badiliko fulani la rohoni, ageuke kutoka kuwa mwenye dhambi mpaka kuwa mtakatifu.
Mwimbaji huyu anapoimba au anapoimbisha, basi Roho yule yule anayeshuka juu ya watu wakati Mchungaji anahubiri ndio huyo huyo anayeshuka juu ya watu wakati anaimbisha.
Sasa huduma ya uimbaji sio huduma ya kutafuta fedha, kama vile huduma nyingine yoyote katika mwili wa Kristo isivyo ya lengo la kutafuta fedha wala umaarufu. Mchungaji au Mwalimu anapohubiri katika kanisa lake, na anapoalikwa mahali pengine au Taifa lingine kwenda kuihubiri Injili, hapaswi kwenda kule kwa lengo la kutafuta fedha. Biblia inasema tumepewa bure tutoe bure..Hivyo atakwenda kule alikoalikwa na atahubiri bure..Ndio wale waliomwalika watamgharimia nauli, pamoja na malazi na makazi kwa huo wakati, lakini hapaswi kwenda kwa lengo la kutafuta malipo/mshahara. Kama waliomwalika watakuwa na moyo mwingine na kusema hatutapenda mtumishi huyu aondoke mikono mitupu, hivyo kwa kuguswa kwao wakampatia chochote kile iwe fedha, au mali..hapo sio dhambi kupokea..lakini Mchungaji, au mwalimu au mtu yoyote yule hapaswi kuomba chochote, wala kuonyesha dalili ya kuwa mhitaji.
Mungu anajua kuwahudumia watu wake, haihitaji yeye kusaidiwa, hivyo aliposema…”Tumepewa bure tutoe bure alimaanisha kabisa”..kwamba kwa namna yoyote ile atawafungulia watumishi wake mlango wa kula na kunywa hata njia hiyo.
Vivyo hivyo na uimbaji wa nyimbo za injili. Mtu yeyote aliyepewa karama hiyo hapaswi kuwa kama wasanii wa nyimbo za ulimwengu ambao wapo kwa lengo la kutafuta fedha kwa sanaa zao hizo. Mtu mwenye karama ya uimbaji atafanya kazi ya Mungu bure pasipo malipo..akifika mahali kaalikwa kwenda kuongoza nyimbo za kumsifu Mungu na kumwabudu, hapaswi kutazamia malipo kwa namna yoyote ile. Anapaswa afanye kazi yake ya uimbaji kwa uaminifu kama ya mchungaji aliyealikwa…aimbe nyimbo za injili na kuhakikisha neema ya Mungu imeshuka juu ya watu, hiyo ndio inapaswa iwe furaha yake ya kwanza, na lengo lake kuu la kwenda pale.
Hali kadhalika hapaswi kubadilika kimavazi na kufanana na wasanii wa kidunia..Kazi ya Mungu sio ya kuonyesha uanamitindo…kwamba leo umevaa hiki, kesho unavaa kile, ili watu wakuone jinsi unavyojua kuvaa…Vaa nguo za heshima, kama ni mwanamke vaa gauni refu haijalishi ni la gharama au sio la gharama, lakini lazima liwe la kujisitiri, hupaswi kwenda kufanya huduma huku umevaa suruali, huku mgongo upo wazi, huku umejichubua uso, huku umeweka make up mfano wa Mwanamke Yezebeli wa kwenye biblia..hali kadhalika mwanaume hupaswi kwenda kufanya huduma huku umenyoa kidunia, huku umevaa nguo za kubana, huku umejipamba mpaka unakaribia kufanana na wanawake.
Ukifanya hivyo na kwenda kufanya huduma na mambo hayo machafu utakuwa bado hujaelewa nini maana ya kumtumikia Mungu, utakuwa unamdharau Mungu na madhabahu yake, na utakapoambiwa ukweli utaona kama unaonewa WIVU, hakuna wivu hapo unaoonewa, ni kwa faida yako binafsi..Unakwenda kuzitafutia laana badala ya baraka ndugu…..Unapoacha kusimama katika Neno la Mungu na kujilinganisha na wasanii wa kidunia, ni sawa na mchungaji aliyeacha majukumu yake madhabahuni na kujilinganisha na wanasiasa waliopo bungeni.
Ndugu yangu, uliyejaliwa karama ya uimbaji..Utumie kwa utukufu wa Mungu, kama wachungaji ambao wamealikwa kutembea dunia yote kuhubiri hawabweteki na kwanini wewe unabweteka na kujiharibia huduma yako kwa kuwaiga hao wasanii wa kidunia au hata baadhi ya wanaojiita wasanii wa injili ambao hawajaelewa maana ya kumtumikia Mungu?
Sasa utauliza je! Sitakiwi kabisa kwenda kurekodi nyimbo zangu studio?
Hapana unapaswa ukazirekodi kabisa tena kwa bidii nyingi, kwa uongozo thabiti wa Roho Mtakatifu, ili injili ienee kwa wengi, na kuwa msaada na baraka kwa wengi..Lakini katika hiyo usiigeuze kuwa ndio sehemu ya kupatia fedha na utajiri. Weka bei ya bidhaa hiyo ambayo inalingana na gharama ulizoingia, na faida kidogo kwaajili ya msingi wa kazi zitakazofuata kama hizo na si kwaajili ya kupata fedha, wala kwaajili ya kujiandaa kuwa msanii maarufu. Na hupaswi kukasirika unaposikia watu wanabarikiwa kwa nyimbo ulizoimba, au wanaziimba nyimbo zilizotungwa na wewe pasipo kukutaja wewe wala kukupa malipo…Hupaswi kukasirika, zaidi ya yote unapaswa ufurahi kwasababu injili ya Kristo inakwenda mbele.
Kwasababu hata wachungaji ndio hivyo hivyo, wanapotengeneza kitabu..na mafunuo waliyoyapata na kuyaandika ndani ya kile kitabu yatakwenda kufundishwa huko na huko, kila mahali na hata kumrudia yeye mwenyewe…na wala hawasemi wala kuchukia kwamba ule ufunuo ni wa kwao na kwamba wana hati miliki nao, mtu mwingine hapaswi kuhubiri bila idhini yao. Kama yupo Mtumishi wa namna hiyo, basi huyo naye bado hajaelewa nini maana ya kuwa mtumishi, kwasababu injili ya Kristo haihubiriwi kwa hati miliki. Lakini kama hujawahi kuona kwanini wewe muimbaji uchukie na kukwazika kuona mtu anaimba nyimbo uliyoiimba wewe bila hata kukutaja au kukutambua?.
Ukiona unasikia huo wivu basi fahamu kuwa bado kuna kasoro ndani yako, upo kutafuta umaarufu na faida kupitia kazi ya Mungu, na haupo kwa lengo la kuisambaza injili. Huna tofauti na Yuda Iskariote.
Hivyo zingatia hayo machache mtu wa Mungu, na Bwana atakusaidia, kama una huduma yoyote ndani yako ya kuhudumu kwa nyimbo za injili, tenga muda uilinganishe na huduma nyingine katika mwili wa Kristo jinsi zinavyofanya kazi, ili upate hekima na ufahamu jinsi ya kuitenda kazi ya Mungu katika shamba lake.
Bwaan akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Ukisoma ule waraka wa pili ambao Paulo alimwandikia Timotheo kuanzia ile sura ya tatu mstari wa 1-9, utaona jinsi Paulo alivyoanza kumweleza Timotheo juu ya mambo yatakayotokea siku za mwisho..Lakini alianza kwa kumwambia neno hili “siku za mwisho kutakuwako nyakati za hatari”.. Jiulize ni kwa nini alimwambia hivyo?. Alimwambia hivyo kwasababu aliona jinsi wimbi kubwa la watu wenye mfano wa utauwa (wanaonekana kama ni watu wa Mungu), lakini wakizikana nguvu zake, watakavyonyanyuka na kuwapoteza wengi.
Hao watu hawakuwepo wakati mwingine wowote isipokuwa tu watatokea katika siku za mwisho, yaani watu wanaoonekana ni watumishi wa Mungu, wanaoonekana wanawaongoza watu katika njia za kweli, lakini kumbe nyuma ya mgongo wanazikana nguvu za Mungu..
Sasa hizi nguvu za Mungu ni zipi?..
Biblia inatueleza “Neno la msalaba” ndio nguvu ya Mungu..
1Wakorintho 1:18 “Kwa sababu neno la msalaba kwao wanaopotea ni upuzi, bali kwetu sisi tunaookolewa ni nguvu ya Mungu”.
Sehemu nyingine inaiita injili kama “uweza wa Mungu (POWER)” Warumi 1:16.
Unaona Injili inayolenga ukombozi wa msalaba, inayowafanya watu wautazame msalabani, watubu dhambi , wakapate msamaha na ondoleo la dhambi zao, hapo ndipo nguvu za Mungu zilipo..
Hakuna mahali popote biblia inasema nguvu za Mungu zipo katika mali, au biashara na majumba..Hayo hayawezi kumfanya mtu apate uzima wa milele…Sasa watu wa namna hii ndio watanyanyuka sana katikati ya kanisa la Mungu, ambao watakuwa wanajifanya ni wanatangaza habari za wokovu, kumbe wanahubiri mambo yao mengine, hawana habari na injili ya toba, wala hata haiwavutii, wala hawajali kwamba mtu wanayemchunga na kuchukua sadaka zake anaweza kufa leo na kwenda kuzimu kutokana na dhambi zake, hilo hawalijali wao wapo radhi kuwasisitizia tu mafanikio ya miili yao, lakini si roho zao.
Wengine wapo radhi, kuwakaririsha mapokeo ya dini zao, ili watu wawe tu wa kidini, wajue litrujia, wasome rozari, na sala zote za marehemu, lakini hao hao watu ukiwauliza je umeokoka, watakauambia mimi si mlokole, ukiwauliza, Je! Unajua kuwa kuna kitu kinachoitwa Unyakuo, watakauambia..sijui unazungumzia kitu gani!!..Sasa embu fikiria mtu wa namna hiyo mbinguni atakwendaje?..Lakini hayo yote ni kiongozi wake hajawahi kumwambia hayo mambo, ni kiongozi ambaye anao mfano wa utauwa lakini anazikana nguvu za Mungu..
Sasa Paulo aliwafananisha watu hawa na Yane na Yambre ambao walinyanyuka wakati wa Musa..Jinsi walivyokuwa wanapingana naye..
2Timotheo 3:8 “Na kama vile Yane na Yambre walivyopingana na Musa, vivyo hivyo na hawa wanapingana na ile kweli; ni watu walioharibika akili zao, wamekataliwa kwa mambo ya imani.
9 Lakini hawataendelea sana; maana upumbavu wao utakuwa dhahiri kwa watu wote, kama vile na upumbavu wa hao ulivyokuwa Dhahiri”.
Sasa kama uwafahamu Yane na Yambre ni wakina nani…
Walikuwa ni wale wachawi wa Farao ambao Musa alipokuwa anafanya miujiza na wao walikuwa wanafanya ili tu kumpinga Musa.
Unaona? Jambo pekee ambalo lilikuwa linawatofautisha hawa wachawi wawili (Yane na Yambre) na Musa, halikuwa miujiza..hapana, hata wao kwa sehemu fulani walipewa kufanya miujiza, jambo pekee lililowatofautisha na Musa, ni UJUMBE waliobeba.. Musa alikuja na ishara lakini alikuwa na Ujumbe nyuma ya ishara zile..Nao ndio huu “Bwana asema hivi! Waache watu wangu huru,waende kunitumikia”..Lakini Yane na Yambre hawakuwa na ujumbe wowote isipokuwa kupinga tu, na kuwaburudisha na kuwatumainisha wamisri kwa miujiza yao,..Ni wana-mazingaombwe tu!..Mtu anayefanya mazingaumbwe siku zote hana ujumbe wowote kwa mazingaombwe yake, anafanya tu kuburudisha watu, na wala wakati mwingine anaweza asiongee kuanzia anaanza mazingaombwe yake mpaka anamaliza. Na wakina Yane walikuwa hivyo hivyo.
Musa alikuwa na ujumbe wa ukombozi, wa kuwatangazia watu uhuru watoke katika utumwa mgumu wa Farao, Ambao kwa sasa sisi tuliookolewa tunafananishwa na wana wa Israeli pale tunapomwamini Kristo, tunaokolewa kutoka katika utumwa wa dhambi wa Ibilisi.
Sasa ukiona, mtu anakujia na miujiza na ishara hizi au zile, lakini hana ujumbe wowote wa kukutoa Misri (kukutoa kwenye utumwa wa dhambi), Basi ujue kuwa unaongozwa na Yane na Yambre(wana mazingaombwe), watumishi wa shetani.. Haijalishi watashika biblia, haijilishi watakuombea upone kiasi gani, Yane na Yambre waliweza kuyafanya hayo yote, haijalishi watafanya miujiza mingi vipi, kama hawana ujumbe wa kukurudisha msalabani upate ukombozi wa roho yako, Ujue hao ni Yane na Yambre tu wanakuongoza…
Ndio hao sasa mtume Paulo anaowazungumzia kuwa “wenye mfano wa utauwa, lakini wakikana nguvu zake”…..Hizi ndio nyakati zenyewe za hatari zinazozungumziwa hapo. Mahali popote unapoongozwa embu jipime nafsi yako, je tangu umekuwa hapo ni kitu gani kimeongezeka katika Maisha yako ya rohoni kwa ujumla, Je! Mahusiano yako na Mungu yameongezeka au yapo pale pale?, Kama sivyo basi ujue upo chini ya Yane na Yambre wa siku za mwisho.
Na kibaya Zaidi kama hujui, watu waliochangia kuufanya moyo wa Farao kuwa mgumu ni hawa wachawi wawili..Kama sio wao basi pengine Farao angeshatubu zamani..(Ingawa ni Mungu mwenyewe ndiye aliyeruhsu). Vivyo hivyo leo hutaki kumgeukia Kristo na kutaka kutubu dhambi zako na kutafuta utakatifu kwasababu tayari wapo akina Yane na Yambre wanaokupumbaza na miujiza, ukikumbushwa habari ya utakatifu na kwenda mbinguni, unasema nabii wetu/kiongozi wetu wa kidini mbona hajawahi kutufundisha hayo, na miujiza mbona inafanyika mingi tu..
Ndugu siku ukifa na kujikuta upo kuzimu, hutakuwa na la kujitetea, kwasababu biblia inatuambia..mtu akifa matendo yake yanafuatana naye (Ufunuo 14:13)..Haisema majumba yake, au magari yake, au bishara yake, au dhehebu lake, inasema matendo yake..Sasa kama nabii wako au mchungaji wako, anakutumaisha na mambo ya ulimwengu huu na wewe unaona raha, nataka nikuambie siku ile vyote pamoja na mali zako, pamoja na huyo kiongozi wako wa imani, aliyekuwa anakufundisha kujiwekea hazina duniani badala ya mbinguni, wote watakuaga pale makaburini, utakuwa umebakia wewe mwenyewe, utashangaa ni matendo yako tu yapo na wewe..hayo ndiyo yatakayoeleza hatma yako ni nini..
kwasababu biblia imeshatuonya jinsi ya kuendana na watu wa namna hii, hivyo ni wajibu wako wewe binafsi kutumia akili, kwa kuutafuta uhusiano wako binafsi na Mungu wako…Kuupima wokovu wako kama upo sawasawa au la, na kama haupo! Basi ndio ufanye bidii kumtafuta Kristo kwa moyo wako wote na kwa nguvu zako zote, katika hichi kipindi kifupi tulichobakiwa nacho, maadamu muda unao..
2Wakorintho 13:5 “Jijaribuni wenyewe kwamba mmekuwa katika imani; jithibitisheni wenyewe. Au hamjijui wenyewe, kwamba Yesu Kristo yu ndani yenu? Isipokuwa mmekataliwa”
Usisubiri ufe ndipo ujue kuwa ulikuwa kwenye njia isiyo sahihi, amka usingizi, anza kuyatengeneza Maisha yako.
Waefeso 5:14 “Hivyo husema, Amka, wewe usinziaye, Ufufuke katika wafu, Na Kristo atakuangaza”.
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group
Mada Nyinginezo:
Jiepusha na dhambi ya wivu/husuda ambayo mwisho wake ni mauaji.
Silaha moja kubwa shetani anayoitumia kuwadhuru watu ni wivu…mtu mwenye wivu ni rahisi kutumiwa na shetani kwa viwango vikubwa sana… Mauaji mengi yanasababishwa na wivu, uchawi mwingi unatokana na wivu, hila nyingi zinatokana na wivu..na mambo yote mabaya yanatokana na wivu.
Hivyo ni muhimu kujifunza kutokuwa na wivu ili tusiwe kifaa cha kutumiwa na shetani kuwadhuru wengine.
Roho ya wivu ndiyo iliyowafanya Mafarisayo na Masadukayo wamchukie Bwana, pale walipoona Bwana anatenda miujiza ambayo wao hawawezi kuitenda, pale walipoona Bwana anawarejeza watu wengi kwa Mungu kuliko wao…Na mioyoni Roho Mtakatifu alikuwa akiwashuhudia kabisa kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu…na walikuwa wanajua kabisa katumwa na Mungu lakini kwasababu ya wivu..wakawa wanajitoa ufahamu na kumkufuru.. Soma..
Mathayo 22:15 “Ndipo Mafarisayo wakaenda zao, wakafanya shauri, jinsi ya kumtega kwa maneno.
16 Wakatuma kwake wanafunzi wao pamoja na Maherodi, wakasema, Mwalimu, twajua ya kuwa wewe u mtu wa kweli, na njia ya Mungu waifundisha katika kweli, wala hujali cheo cha mtu awaye yote, kwa maana hutazami sura za watu”.
Unaona, walijua kabisa Kristo alikuwa mtu wa kweli aliyetumwa na Mungu..
Soma tena.. Yohana 3:1-3 utalithibitisha hilo…
Yohana 3:1 “Basi palikuwa na mtu mmoja wa Mafarisayo, jina lake Nikodemo, mkuu wa Wayahudi.
2 Huyo alimjia usiku, akamwambia, Rabi, twajua ya kuwa u mwalimu, umetoka kwa Mungu; kwa maana hakuna mtu awezaye kuzifanya ishara hizi uzifanyazo wewe, isipokuwa Mungu yu pamoja naye”.
Lakini pamoja na hayo yote nguvu ya wivu ilikuwa kubwa ndani yao ikazidi nguvu ya kumpenda..na hatimaye wakafanya hila mpaka za kutaka kwenda kumsulubisha mfalme wao..Walimsulubisha moyoni wakijua kabisa huyu ni mwana wa Mungu aliyetumwa kutoka mbinguni…Hilo halikuwa na shaka mioyoni mwao. Walijua kabisa ndiye mfalme aliyetabiriwa kuja ulimwenguni.
Na hata walipompeleka kwa Pilato..Haraka sana Pilato ambaye hakuwa Myahudi akajua kuwa hakukuwa na kosa lolote alilolifanya Bwana Yesu ambalo linastahili yeye kusulubiwa lakini ni kwasababu tu ya wivu…Hawa wayahudi wamesikia tu wivu alivyojiita yeye ni mwana wa Mungu..Hilo tu! Wala hakuna lingine…walimwonea wivu kwa miujiza aliyokuwa anaitenda ambayo wao walishindwa kuitenda na wala hakuna lingine, na jinsi anavyowajalia watu wengi kupata wokovu…Kwahiyo hata Pilato aliliona hilo kama biblia inavyosema katika..
Marko 15:9 “Pilato akawajibu, akisema, Je! Mnataka niwafungulie mfalme wa Wayahudi?
10 Kwa maana alitambua ya kuwa wakuu wa makuhani wamemtoa kwa HUSUDA.
11 Lakini wakuu wa makuhani wakawataharakisha makutano, kwamba afadhali awafungulie Baraba”.
Sasa neno ‘HUSUDA’ maana yake ni ‘WIVU’ soma tena (Mathayo 27:17-18)..Kwahiyo unaona Pilato alishawajua kabisa hawa watu ni wivu ndio uliowafanya watake kumwua Yesu na wala hakuna lingine..alijua kabisa mioyoni mwako wanamwamini Yesu na kwamba “Yesu katoka kwa Mungu, na ni mfalme wao” lakini kwa kuwa wamemwonea wivu ndio maana wanataka afe…Ndio maana Pilato alikuwa akiwauliza kwa kurudia rudia.. “kama kweli wamemaanisha kumuua mfalme wao”
Yohana 19:13 “Basi Pilato, aliposikia maneno hayo, akamleta Yesu nje, akaketi juu ya kiti cha hukumu, mahali paitwapo Sakafu ya Mawe, au kwa Kiebrania, Gabatha.
14 Nayo ilikuwa Maandalio ya pasaka, yapata saa sita. Akawaambia Wayahudi, TAZAMA, MFALME WENU!
15 Basi wale wakapiga kelele, Mwondoshe! Mwondoshe! Msulibishe! Pilato akawaambia, JE! NIMSULIBISHE MFALME WENU! Wakuu wa makuhani wakamjibu, Sisi hatuna mfalme ila Kaisari”.
Wivu ni mbaya sana unakufanya umkane Mtu, hata kama unamwamini na kumpenda…
Na ndio maana mwishoni kabisa baada ya kusulubishwa Bwana Yesu, Pilato aliandika anwani juu ya msalaba wa Bwana Yesu kwa lazima.. “Yesu Mnazareti, Mfalme wa Wayahudi”
Yohana 19:19 “Naye Pilato akaandika anwani, akaiweka juu ya msalaba, imeandikwa, YESU MNAZARETI, MFALME WA WAYAHUDI.
20 Basi anwani hiyo waliisoma wengi katika Wayahudi; maana mahali pale aliposulibiwa Yesu palikuwa karibu na mji; nayo iliandikwa kwa Kiebrania, na Kirumi, na Kiyunani.
21 Basi wakuu wa makuhani na Wayahudi wakamwambia Pilato, Usiandike, Mfalme wa Wayahudi; bali ya kwamba yule alisema, Mimi ni mfalme wa Wayahudi.
22 PILATO AKAJIBU, NILIYOANDIKA NIMEYAANDIKA”.
Unaona hapo?..Pilato aling’ang’ania kuandika anwani ile kwa lazima?…kwanini?..ni kwasababu anaujua unafiki wa mafarisayo..mioyoni mwao walimwamini lakini mdomoni walimkana na kumtukana na kumsulubisha na hiyo yote ni kwasababu ya wivu tu!. Na ndio maana Pilato akaandika anwani ile.
Yohana 12:42 “Walakini hata katika wakuu walikuwamo wengi waliomwamini; lakini kwa sababu ya Mafarisayo hawakumkiri, wasije wakatengwa na sinagogi”.
Sasa sio wote kabisa waliomwamini, Bwana Yesu…wapo ambao ni kweli hawakumwamini kabisa pamoja na ishara zote zile alizozifanya…lakini asilimia kubwa ya mafarisayo na wakuu wa makuhani walimwamini Bwana mioyoni mwao lakini WIVU ukawasababisha kumsulubisha Bwana, na sio Bwana tu bali hata mitume wake walisumbuliwa na mafarisayo hao hao..na yote hiyo ni kutokana na wivu tu.
Matendo 5:16 “Nayo makutano ya watu wa miji iliyoko kandokando ya Yerusalemu wakakutanika, wakileta wagonjwa, nao walioudhiwa na pepo wachafu; nao wote wakaponywa.
17 Akaondoka Kuhani Mkuu na wote waliokuwa pamoja naye, (hao ndio walio wa madhehebu ya Masadukayo), WAMEJAA WIVU,
18 wakawakamata mitume wakawaweka ndani ya gereza;”
Hiyo ndiyo silaha shetani aliyotumia kumpeleka Bwana msalabani…Na silaha hiyo hiyo anaitumia leo kuangamiza watu..Je! na wewe una wivu?…kama unaingiwa na wivu ndugu yako akipata jambo Fulani ambalo wewe huna ujue unakaribia kufanyika chombo cha shetani kumwangamiza, kama unasikia wivu jambo Fulani zuri ndugu yako, au jamii yako, au rafiki yako analolifanya, kama unasikia wivu, mwingine anapooa, au anapoolewa au anapofanya hiki au kile..au anapotoka hatua moja mpaka nyingine…kuna hatari kubwa ya kufanyika chombo cha shetani. Na wivu ukizidi sana unakuwa huna tena huruma..unakuwa unatamani kifo kwa huyo ndugu yako kama vile Kaini, alivyomwonea wivu ndugu yake mpaka akaenda kumwua.
Hivyo ni kwa namna gani utashinda Wivu?
Kwanza ni kwa kumpa Yesu Kristo maisha yako?..Unapookoka Bwana anakufanya kuwa kiumbe kipya, na ya kale yote yanakuwa yamepita, unakuwa umefanyika kiumbe kipya…Ule utu wa zamani, Bwana anauzika, Nia yako Bwana anaigueza kutoka kutazama vitu vya ulimwengu huu vinavyopita na kutazama mambo ya ulimwengu ujao ya milele yasiyoharibika..Hivyo kunakuwa hakuna shughuli yoyote ya kidunia ambayo itaweza kukupa wivu ndani ya moyo wako kwasababu nia yako imeshageuzwa na kuutazama ulimwengu ujao ambao utajiri wake na hazina yako hauna mwisho.
Pili baada ya kuokoka unapaswa uanze kujiwekea hazina yako mbinguni, Biblia inasema hazina yako ilipo ndipo na moyo wako utakapokuwepo…Hazina yako ikiwa kubwa katika mambo ya ulimwengu huu na moyo wako lazima utakuwa huko huko, hilo haliepukiki, kama ndoto zako kubwa kuliko zote ni wewe kupata mali nyingi sana ili hatimaye watu wote waje kukuona na kukuangukia na kukuheshimu, hapo roho ya wivu hauwezi kuiepuka, kwasababu atakapotokea mtu kakuzidi kidogo tu au unamwona ananyanyuka utamwonea wivu. Ndicho kilichowakuta mafarisayo na masadukayo, walikuwa na ndoto kubwa za wao waonekane wapo juu ya watu wote, na alipotokea mwingine mwenye nguvu kuliko wao wakaishia kumwonea wivu.
Lakini kama hazina yako ipo mbinguni, kwamba ndoto yako kubwa ni siku ile uirithi mbingu kwa daraja la kwanza, na kuwa na thawabu kubwa kule, kamwe hutakaa umwonee mtu wivu kwa vitu vya kidunia vinavyopita…Hazina yako inapoongezeka mbinguni, mawazo yako, akili yako, na moyo wako wote unakuwa kule, unakuwa kila siku unatafakari utukufu na thawabu zinazokungoja kule, na hivyo habari ya kuanza kuona wivu kwa vitu vya kidunia unakuwa huna..
Na hazina ya mbinguni unaitengeneza kwa kumpendeza Mungu na kwa kuifanya kazi yake…Na kazi yake sio kuhubiri tu, bali hata ile ya kuosha choo cha nyumba ya Mungu ni kazi yake yenye thawabu kubwa kule, hata ile ya kuwaombea watakatifu ni kazi yake yenye thawabu kubwa sana…n.k Unapofanya hayo bila ulegevu Roho Mtakatifu kila siku atakuwa anakushuhudia ndani yako kwamba thawabu yako ni kubwa mbinguni, na inazidi kuongezeka siku baada ya siku, hivyo kamwe huwezi kumwonea wivu mtu aliyeoa/ kuolewa na wewe hujaolewa, au jirani yako ambaye ni bilionea..
Ufunuo 2:17 “Yeye ashindaye nitampa baadhi ya ile mana iliyofichwa, nami nitampa jiwe jeupe, na juu ya jiwe hilo limeandikwa jina jipya asilolijua mtu ila yeye anayelipokea………
26 Na yeye ashindaye, na kuyatunza matendo yangu hata mwisho, nitampa mamlaka juu ya mataifa,
27 naye atawachunga kwa fimbo ya chuma, kama vyombo vya mfinyanzi vipondwavyo, kama mimi nami nilivyopokea kwa Baba yangu”……
Ufunuo 3:5 “Yeye ashindaye atavikwa hivyo mavazi meupe, wala sitalifuta kamwe jina lake katika kitabu cha uzima, nami nitalikiri jina lake mbele za Baba yangu, na mbele ya malaika zake”………..
12 Yeye ashindaye, nitamfanya kuwa nguzo katika hekalu la Mungu wangu, wala hatatoka humo tena kabisa, nami nitaandika juu yake jina la Mungu wangu, na jina la mji wa Mungu wangu, huo Yerusalemu mpya, ushukao kutoka mbinguni kwa Mungu wangu, na jina langu mwenyewe, lile jipya…….
21 Yeye ashindaye, nitampa kuketi pamoja nami katika kiti changu cha enzi, kama mimi nilivyoshinda nikaketi pamoja na Baba yangu katika kiti chake cha enzi”.N.k
Bwana akubariki sana.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Je ni kweli kuna samaki nguva?..Je kwenye biblia nguva katajwa?
Jibu: Ukweli ni kwamba hakuna mahali popote katika biblia palipotajwa uwepo wa samaki aina ya nguva. Maana yake ni kwamba hakuna kiumbe cha namna hiyo kilichoumbwa na Mwenyezi Mungu.
Lakini utauliza je! hicho wanachokiona watu ni nini? ambacho kimaumbile kinaonekana nusu mtu nusu samaki?
Jibu ni kwamba vinavyoonekana na watu vyenye umbo kama hilo ni roho za mapepo. Kumbuka biblia inasema shetani anao uwezo wa kujigeuza na kuwa hata Malaika wa Nuru (Kasome 2Wakorintho 11:14), sasa si zaidi kujigeuza na kuwa kiumbe kiumbe kingine chochote chenye umbo la ajabu?. Anao huo uwezo, anaweza kujiguza na kuwa kama nusu mtu nusu mbuzi, anaweza kujigeuza na kuwa nusu mtu nusu nyoka, vivyo hivyo anao uwezo wa kujigeuza na kuwa nusu mtu nusu samaki (ambao ndio hao wanaojulikana kama nguva).
Sasa shetani na mapepo yake wote wanao huo uwezo wa kujigueza na kuwa hivyo viumbe vya ajabu..Na lengo lao ni lile lile moja..Kuwapoteza wanadamu na kuwaweka mbali na kweli ya Mungu, na hatimaye wafe katika dhambi zao na kuingia Jehanamu ya moto, wala hana lingine. Hivyo shetani kila siku anabuni njia mpya za kuwafanya watu wawe wabaya zaidi na kuzidi kuuamini uongo wake.
Sasa haya mapepo ambayo yanajigeuza maumbile..huwa hayawatokei wala hayawaingii watu waliookoka (Yaani waliomwamini Yesu Kristo na kuoshwa dhambi zao kwa damu yake). Huwa yanawatokea na kuwaingia watu ambao katika roho wapo dhaifu sana, na hao ni wale wote ambao wapo nje ya Neema ya Yesu Kristo. Huwa yanawajia katika ndoto, kuwahimiza kufanya jambo fulani lililo kinyume na neno la Mungu au kuwapa hisia ambayo ni kinyume na Neno la Mungu..
Na hisi kubwa na ya kwanza yanayopeleka kwa mtu ni hisia ya ZINAA na UASHERATI. Kwasababu hiyo ndio dhambi ya kwanza ambayo shetani anatumia kumwangusha nayo mwanadamu na ndio Dhambi ya asili.
Hisia ya pili ni.. kutenda mabaya, aidha kuabudu sanamu, au miungu, kuwa mshirikina, au wakati mwingine yanamletea mtu hisia za kuwa na chuki na jamii ya watu fulani, au mtu fulani na kumpeleka hata kutamani kuua, au kuiba au kudhuru. Hiyo ndio kazi ya mapepo hayo yanapomwingia mtu ndani yake…na haya yana majina mengi (wengine wanayaita majini, wengine vibwengo n.k)..lakini ndio hayo hayo mapepo…
Mapepo haya yakiwemo hayo yanayojigeza na kuwa huo mfano wa nguvu, huwa hayamtokea mtu kwa macho, yanakuwa ni roho ambazo zinamwingia mtu au zinatembea na mtu, na mtu anaweza kuziona tu katika ndoto..lakini si katika macho ya asili..Lakini pia kama mtu huyo hali yake ya roho ipo chini sana yanaweza kumtokea kabisa na akayaona dhahiri, wengi wa wanaoyaona hayo ni wale ambao ni wachawi au waganga, au washirikina…ambao wameshajiuza kwa shetani kikabisa.
Kwahiyo nguva si kiumbe kilichoumbwa ambacho kinaishi baharini, bali ni roho za mapepo, kama umewahi kuota upo na nguva au umewahi kumwona..Basi tambua kuwa hali yako katika roho ipo chini sana na ni hatari.
Hivyo suluhisho ni kumpa Yesu maisha yako, unapoamua kugeuka na kutubu kwa kumaanisha kuacha dhambi na maisha ya machafu uliyokuwa unaishi huko nyuma, na kwenda kubatizwa katika ubatizo sahihi, roho hizo zitakuacha hata pasipo kwenda kuwekewa mikono na mtu yoyote na utakuwa huru mbali na utumwa wa roho za mapepo.
Bwana akubariki sana.
Kwa mgawanyo bora wa masomo download App hapa>> App wingu la mashahidi
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
SWALI: Mimi Nina MUNGU Wangu ambae Ni ALLAH subhanallah…sasa kwanini nimkabidhi maisha Yesu wakati naye alizaliwa Kama mimi?
JIBU: Mama yako alizaliwa kama wewe…lakini ilifika wakati Mwenyezi Mungu aliyakabidhisha maisha yako kwake. Ili uwe salama, ulindwe, uhifadhiwe, ulishwe na upendwe..na pamoja na hayo ufundishwe kanuni za maisha ambazo peke yako bila wazazi au mlezi usingeweza kujifunza.
Vivyo hivyo ulipaswa ukae chini ya sheria za wazazi wako ndipo uweze kufanikiwa, endapo ungekuika sheria hizo basi maishani usingefanikiwa….Na kama sio Mwenyezi Mungu kuyakabidhisha maisha yako kwa wazazi wako ambao wamezaliwa kama wewe, maisha yako yangukuwa magumu sana hapa duniani au hata pengine usingezaliwa kabisa au kama ungezaliwa ungekufa.
Vivyo hivyo Yesu alizaliwa kama sisi tulivyozaliwa, (Ingawa hakuzaliwa na dhambi ya asili kama sisi, kwasababu mimba yake ilitungishwa kwa uwezo wa Roho Mtakatifu), na katika nyakati hizi za uovu na mateso na dhiki za ulimwengu.
Mungu kwa huruma zake na kwa jinsi anavyotupenda akamtuma huyu Yesu Kristo, ili awe kama mzazi kwetu kwasababu sisi wenyewe hatutaweza kwa nguvu zetu na kwa akili zetu kujiongoza..Ndio maana hatuna budi wote tuyakabidhi maisha yetu kwake ili tuwe salama sasa na ahera.
Yohana 3:16 “Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.
17 Maana Mungu hakumtuma Mwana ulimwenguni ili auhukumu ulimwengu, bali ulimwengu uokolewe katika yeye.
18 Amwaminiye yeye hahukumiwi; asiyeamini amekwisha kuhukumiwa; kwa sababu hakuliamini jina la Mwana pekee wa Mungu”
Yesu anapoingia maishani mwetu, anatupa furaha, faraja, amani, upendo na tunapata ulinzi dhidi ya Adui shetani na mapepo yake yote, siku zote za maisha yetu na tumaini la uzima wa milele.
Bwana Yesu akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Ni mistari ipi shetani anapenda kuitumia kuwaangusha watu waliosimama?
Shetani akitaka kumwangamiza mtu aliye mwamini Mungu, anachofanya ni anamchukua na kumpeleka juu sana,.. hamwachi pale alipo, kwasababu anajua mtu aliye chini hata akinguka, ataumia kidogo tu, lakini bado akawa na uwezo wa kusimama na kuendelea mbele tena..Badala yake anachokifanya yeye ni anamchukua na kumpelekea juu sana kwenye kilele cha mnara, mahali ambapo anajua akifanya kosa kidogo tu, na kuteleza basi habari yake ndio inakuwa imeishia pale pale…
Ndivyo alivyofanya kwa Bwana wetu Yesu, alimnyanyua na kumpeleka juu sana kwenye kilele cha hekalu,..Na wakati anampandisha, akaanza kumuhubiria Zaburi ya 91 moyoni mwake (Hii ndio zaburi shetani anayoitumia sana kama silaha yake)…
Inayozungumzia jinsi Mtu yule aliyekubaliwa na Mungu anavyopokea ulinzi wa kipekee kutoka kwa Mungu, haijalishi itakuwa ni wakati wa mchana au wa usiku, haijalisha atakuwa anazungukwa na magonjwa ya hatari kiasi gani ambayo ni tuishio katika dunia yaliyowaangamiza watu makumi elfu, lakini kwake yeye hayatamgusa hata moja..Jinsi mtu huyo anavyofunikwa chini ya mbawa zake ili mabaya yasimpate.. jinsi atakavyowekwa mahali pa juu..jinsi atakavyowakanyaga simba na majoka, na jinsi Mungu atakavyomtumia malaika zake wamlindie njia zake zote, asiteleze….
Kwa muda wako pitia zaburi yote ya 91, uone jinsi inavyouzungumzia ulinzi wa kipekee anaoupokea Mtu yule aliyekubalika na Mungu..lakini hapa tutatazama tu vifungu vichache..
Zaburi 91:10 “Mabaya hayatakupata wewe, Wala tauni haitaikaribia hema yako.
11 KWA KUWA ATAKUAGIZIA MALAIKA ZAKE WAKULINDE KATIKA NJIA ZAKO ZOTE.
12 MIKONONI MWAO WATAKUCHUKUA, USIJE UKAJIKWAA MGUU WAKO KATIKA JIWE.
13 Utawakanyaga simba na nyoka, Mwana-simba na joka utawaseta kwa miguu.
14 Kwa kuwa amekaza kunipenda Nitamwokoa; na kumweka palipo juu, Kwa kuwa amenijua Jina langu.
15 Ataniita nami nitamwitikia; Nitakuwa pamoja naye taabuni, Nitamwokoa na kumtukuza;
16 Kwa siku nyingi nitamshibisha, Nami nitamwonyesha wokovu wangu”.
Unaona? sasa Wakati anampandisha juu sana, alikuwa anamthibitishia mistari hiyo kichwani pake..Na kweli shetani alichokuwa anamwambia Bwana ni sahihi kabisa, lakini sio katika mazingira yale..Na alipomfikisha pale juu sasa, ndipo akamwambia huu ni wakati wa wewe kujitupa chini kwasababu Bwana Mungu wako amekupenda na kukuthibitisha, hakuna baya lolote litakaloweza kukupata …. Hivyo usiogope kujitupa chini kwasababu malaika zake wapo kila mahali ili Wakulinde katika njia zako zote. Na Mikononi mwao watakuchukua, Usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe
Unaweza kudhani alimaanisha jitupe tu chini kikawaida peke yake, La, sio hivyo tu.. shetani alimaanisha pia dondoka, kutoka katika msimamo wako wa Imani kidogo tu. Ukifanya hivyo Mungu wa mbinguni hatakuacha uangamie kabisa kwani atakutumia malaika zake ili kukurudisha pale ulipokuwa.
Lakini shetani alijua kitakachofuata baada ya pale ni nini..kwasababu alishawahi kuwaangusha watu wengi kwa njia hiyo hiyo akadhani itakuwa hivyo pia na kwa Bwana wetu Yesu Kristo.
Lakini Bwana alimwambia Neno fupi tu..Imeandikwa “Usimjaribu Bwana Mungu wako”.
Kama wewe ni umesimama katika wokovu, nataka nikuambie, katika mahali ambapo unapaswa uwe napo makini basi ni hapa..
Kwenye mahubiri yanayokuaminisha kwamba wewe umekubaliwa na Mungu wakati wote.., na hivyo unaoulinzi wa kipekee kutoka kwake.. kama hujui hiyo ndio mistari shetani anayoipenda kuitumia kuliko mistari mingine yeyote ili kukuangusha wewe uliyesimama..
Ni kweli Mungu ameahidi kufanya hivyo lakini ni kwanini aje kukuhubiria hivyo hivyo kila siku , hakuhubirii habari nyingine za kumcha Mungu? …Jiulize kwanini shetani hakumwambia Bwana, kwa maana imeandikwa mpende Bwana Mungu wako, kwa moyo wako wote, kwa akili zako zote, na kwa nguvu zako zote…Badala yake anamwambia kwa kuwa imeandikwa atakuagiza malaika zake wakulinde, usiteleze….Utaona Ni mistari ya kusifiwa tu, na kufarijiwa tu na ya kutoa sifa tu ili ujione wewe ni kitu Fulani mbele za Mungu…hata kama utakuwa katika mahusiano mabaya na Mungu, atakuletea tu hiyo mistari..
Na kibaya Zaidi siku hizi za mwisho mafundisho ya namna hii ndio yanapewa kipaumbele, pale tunapohubiriwa kwamba Mungu ametukubali, Mungu ametuweka juu, hatutakwenda chini, maadui zetu watashindana wala hawatashinda, watakuja kwa njia moja lakini watatoweka kwa njia saba….mahubiri kama haya tunayapenda, ni kweli ni maneno ya Mungu lakini kumbuka hayo ndiyo yanayokupeleka katika kilele cha hekalu ili kukuangamiza kama hutakuwa makini..
Sasa ukiwa katika kilele cha mahubiri kama hayo, hutaki kusikia kingine chochote, hapo ndipo ibilisi anakuletea mambo maovu, kwasababu shetani alishakujaza ujasiri wote kuwa wewe ni mteule wa Mungu, huwezi kupotea?, Inakuwa ni rahisi kwako wewe kwenda kufanya uzinzi, kwasababu shetani ndani anakuhubiria na kukwambia Mungu anaelewa, bado anakupenda, ulishaokoka,atakulinda..Mungu haangalii mavazi yako, haangalii vimini vyako, anaangalia moyo wako, wewe ni mshindi tayari usikubali kushindwa…hata ukiendelea tu kuvaa uchi uchi na kutembea barabarani, haina shida wewe ni mtoto wa Mungu.
Kumbe hujui ndio ndio unaukaribia mwisho wako..Ukiingia huko ndio moja kwa moja, utakuwa umeshateleza na kuanguka kama yeye alivyoanguka alivyoasi zamani, Na mpaka utakapofika chini tayari umeshakuwa mfu rohoni..hufai tena.
Hizi ni siku za mwisho. Utakatifu hauhubiriwi, bali maneno ya kututia faraja tu, ya kutufanya tujione kuwa sisi tumekubaliwa na Mungu, ili kwamba tuendelee kustarehe katika dhambi zetu..
Waebrania 12:14 “Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, NA HUO UTAKATIFU, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao”
Bwana atusaidie.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
JINSI WATU WANAVYOZAMA KATIKA USHIRIKINA NA UCHAWI.
JE! UMEFANYIKA KUWA MWANAFUNZI WA BWANA?
VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 6
MJUMBE WA AGANO.
NIFANYE NINI ILI NILITIMIZE KUSUDI LA MUNGU.
Kwanini Shetani ni joka wa zamani?
Shalom, ni kwa neema za Mungu wetu tumeliona tena jua leo..wapo ambao hawakupata nafasi hiyo, hivyo hatuna budi kumshukuru sana Mungu wetu. Karibu tujifunze Neno la Mungu chakula cha kweli cha roho zetu.
Biblia inasema katika..
Ufunuo 20:1 “Kisha nikaona malaika akishuka kutoka mbinguni, mwenye ufunguo wa kuzimu, na mnyororo mkubwa mkononi mwake.
2 Akamshika yule joka, yule nyoka wa zamani, ambaye ni Ibilisi na Shetani, akamfunga miaka elfu;”
Shetani anajulikana kama joka wa zamani..ikiwa na maana kuwa ameishi muda mrefu, na ameishi katika hali hiyo hiyo ya ujoka tangu zamani…Na kama unavyojua kitu chochote ambacho kimeishi muda mrefu, kwa mfano mtu aliyeishi muda mrefu ni lazima atakuwa anajua mambo mengi…wazee wenye umri mkubwa wanakuwa wanajua mambo mengi zaidi kuliko vijana..
Kwasababu wamekumbana na mambo mengi katika maisha yao na wamejifunza mambo mengi, wamejifunza kutokana na makosa yao na kutokana na makosa ya watu wengine…hivyo hawawezi kufananishwa hata kidogo na watoto waliozaliwa hivi karibuni.
Vivyo hivyo shetani naye anajulikana kama joka wa zamani…
maana yake ni kwamba anajua mambo mengi sana yamhusuyo mwanadamu…alikuwepo tangu Edeni, anamjua Adamu kwa sura na tabia hajamsahau,..anamjua Hawa…anamjua Nuhu, na alikuwa anashuhudia jinsi dunia ilivyokuwa inaangamizwa kwa gharika…alikuwepo anatazama…Bado anaikumbuka sura ya Ibrahimu na ya Sara…anakumbuka ni wapi walipomsumbua katika maisha yao..Anamkumbuka Musa..na bado anazijua tabia zake zote na anaujua udhaifu wake..Anayo sura ya Danieli na ya Nebukadneza, na ya Eliya kichwani mwake na anazikumbuka tabia zao…Na zaidi ya yote anamfahamu sana Mkuu wa Uzima Yesu Kristo, anakumbuka matukio yote tangu anazaliwa mpaka alipokuwepo kule jangwani akimjaribu, na alipokufa na kufufuka, anajua nguvu zake na mamlaka yake aliyonayo sasa…
Vivyo hivyo anawajua watu, anawajua watu na tabia zao, anajua wanapenda nini, na hawapendi nini…Ameviona vizazi vyote tangu Adamu mpaka sasa…Hebu jiulize wewe tu mpaka umri ulioufikia sasa ambao pengine haujazidi hata miaka 60 lakini tayari umeshajua tabia za baadhi ya watu na baadhi ya makabila kiasi kwamba pengine hata ukimwona tu mtu Fulani tayari umeshajua kundi la kumweka hata kabla ya kuendelea mbele sana…Sasa kama wewe na miaka yako hiyo 50 tu tayari unajua jamii za watu na tabia zao…Unafikiri shetani atakuwa anawajua wanadamu kwa kiwango gani?..maana yeye tangu Edeni mpaka leo yupo.
Nataka nikuambia anawajua wanadamu vizuri..anajua ni wapi pa kuwashikia watoto, watu wazima na wazee…kwasababu mwanadamu ni Yule Yule…na biblia inasema hakuna jipya chini ya jua…anajua namna ya kummaliza mtu mchanga kiroho pindi tu anapotaka kujaribu kumtafuta Mungu…kwasababu alishajaribu kwa watu kadhaa huko nyuma wa vizazi vilivyopita na akafanikiwa…Anajua ni jinsi gani anaweza kuwaangusha watumishi wa Mungu..kwasababu alishajaribu huko nyuma na akafanikiwa kwa baadhi hivyo anatumia huo huo uzoefu kwa watu wa vizazi vyote. Anajua jinsi ya kuwazuia watu wasisali, wasimtafute Mungu n.k kwasababu alishaijaribu hiyo njia huko nyuma na ikafanya kazi.
Ndugu mpendwa usipoingia ndani ya Yesu kisawasawa hutamweza shetani kwa vyovyote vile anazo akili nyingi za kukuzidi wewe na mimi, ukisema humtaki Bwana Yesu na kwamba unaweza kujizuia usizini bila hata ya kuwa ndani ya Kristo, unapoteza muda wako! Siku moja utazini tu..alishawajaribu watu kama nyie huko nyuma na akawanasa hivyo wewe sio wa kwanza kuwaza hivyo au kujaribu hivyo..Ukisema naweza kufanya hichi chema au kile bila kuwa ndani ya Yesu..nataka nikuambie ni muda tu unaupoteza..watu kama nyie shetani alishawatafutia suluhisho lake pengine hata zaidi ya miaka 2000 iliyopita huko nyuma…wewe unaweza kukiri ni wa kwanza lakini kumbe hata ni wa milioni 10 kwenye kalenda zake na orodha zake za watu waliojaribu kufanya kama wewe huku wakiwa nje ya Kristo na akawashinda..
Hivyo wewe uliyezaliwa juzi huwezi kumzidi hekima Yule aliyekuwepo miaka mingi iliyopita huko nyuma…(Hujui ni kwanini shetani anaitwa mungu wa ulimwengu huu? Ni kwasababu anajua mambo ya wanadamu sana kuliko mwanadamu yoyote yule).
Ndio maana Bwana Yesu alimwambia kwamba siku zote anayawaza yaliyo ya wanadamu na si ya Mungu.. Kwanini? kwasababu anakesha kumsoma mwanadamu na namna ya kumtawala. Kasome (Mathayo 16:23)..
Hivyo utauliza kama shetani anayajua mambo ya wanadamu kiasi hicho, kiasi kwamba hakuna upenyo wa kuweza kumzidi ni nani basi atasalimika?
Jibu ni kwamba pamoja na ukongwe wake wote wa kuwafahamu wanadamu, yupo mmoja ambaye ni mkongwe zaidi yake..Na huyo si mwingine zaidi ya Mungu mwenyezi aliye Baba yetu ambaye tunamwabudu sisi kupitia Yesu Kristo(Danieli 7:9). Huyo anajulikana kama MZEE WA SIKU.
Danieli 7:13 “Nikaona katika njozi za usiku, na tazama, mmoja aliye mfano wa mwanadamu akaja pamoja na mawingu ya mbingu akamkaribia HUYO MZEE WA SIKU, wakamleta karibu naye.
14 Naye akapewa mamlaka, na utukufu, na ufalme, ili watu wa kabila zote, na taifa zote, na lugha zote, wamtumikie; mamlaka yake ni mamlaka ya milele, ambayo hayatapita kamwe, na ufalme wake ni ufalme usioweza kuangamizwa”.
Baba yetu anatujua kuliko shetani anavyotujua..shetani anauzoefu wa kutuangusha lakini Hekima iliyo kwa Mungu inauwezo hata wa kuyajua mawazo yake na nia yake na mipango yake, na kuyaangusha chini mawazo yake..chochote anachotaka kukifikiria kwa uzoefu wake, sisi tulio ndani ya Kristo tayari tunauwezo wa kuitegua mitego yake..hekima ile ya Kiungu inaingia ndani yetu ambayo inatupa uwezo wa kuzitambua na kuziangusha fikra zote za shetani. Lakini hekima hiyo wanapewa wale tu wanaomwamini mwanae mpendwa Yesu Kristo.
Wengine wote walio nje ya Kristo kamwe hawataweza kumshinda Yule joka wa zamani ambaye ni Ibilisi..watapelekwa kule shetani anakotaka waende..hata kama hawataki, ndio maana mtu ambaye hajaokoka kisawasawa kamwe hawezi kuwa na Amani, na hawezi kuishinda dhambi, na mapenzi ya ulimwengu huu ndio anayoyatenda…wakati mwingine anapanga hiki lakini mwishoni kinaishia kuwa kingine…kwanini? Ni kwasababu anataka kujiongoza mwenyewe na kudhani anaweza kufanikiwa kwa nguvu zake na akili zake.
Hivyo kama hujaokoka, bado tumaini la kumshinda Yule joka lipo, Hekima ya kiMungu inataka kuingia leo ndani yako…usimsikilize shetani anayekuwambia akilini mwako sasahivi kwamba huwezi kuokoka kwamba unadhambi nyingi na Mungu hawezi kukusamehe…ndivyo alivyowaambia watu wengi wa vizazi vya nyuma na kuwaangusha..anatumia ukongwe wake tu…lakini wewe leo mkatae na mkane kwa vitendo…Amua leo kuacha dhambi, na kutubu, amua kuacha kwenda disko, amua kuacha kusengenya, amua kuacha ulevi na uasherati na Bwana atakupenda sana…Na hekima ya ajabu itokayo kwa yule MZEE WA SIKU, (YEHOVA) Mungu wetu,itaingia ndani yako itakayoweza kutambua mitego yake na hila zake…
Mithali 2:6 “Kwa kuwa Bwana huwapa watu hekima; Kinywani mwake hutoka maarifa na ufahamu;
7 Huwawekea wanyofu akiba ya hekima kamili; Yeye ni ngao kwao waendao kwa ukamilifu;
8 Apate kuyalinda mapito ya hukumu, Na kuhifadhi njia ya watakatifu wake.
9 Ndipo utakapofahamu haki na hukumu, Na adili, na kila njia njema.
10 Maana hekima itaingia moyoni mwako, Na maarifa yatakupendeza nafsi yako;”
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 78900131
Mada Nyinginezo:
ANGUKO LA UFALME WA SHETANI:
ZIFAHAMU HUDUMA KUU (10) ZA SHETANI DUNIANI.
NI NANI ALIYEWALOGA?
JINSI NEEMA YA MUNGU ILIVYOKUWA KUBWA KWA MKE WA LUTU.
DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.
MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.
CHUKIZO LA UHARIBIFU