Category Archive Home

JE! TUNAPASWA KUUAMINI UNABII WA SYLVIA BROWNE?

Hivi karibu mwanamke huyu amepata umaarufu mkubwa duniani japo alishafariki mwaka 2013, lakini kitabu chake kilichoitwa “End of days”, ambacho ndani yake kimeandika baadhi ya nabii zitakazotokea siku za mwisho, ndicho kilichomfanya ajulikane kwa haraka, na moja ya nabii hizo ni kuhusiana na mlipuko wa gonjwa ambalo kwasasa linajulikana kama Covid-19, kama wengi wanavyojua alitabiri kwa ufasaha kuwa kipindi cha mwaka wa 2020 kutazuka gonjwa linaloshambulia mapafu, ambalo litaathiri karibu dunia nzima, na akaongezea kusema kuwa hata hivyo gonjwa hilo litatoweka lenyewe kama lilivyokuja, na litarejea tena baada ya miaka 10 ndipo litakapotoweka moja kwa moja.

Lakini unabii mwingine alioutoa ambao ndio kiina cha ujumbe wa leo, ni ule aliosema, mwaka alioutaja kama “3020” Kutazuka viumbe wa ajabu duniani, ambao wataitwa “VAMPIRES” ni watu ambao watafufuka, na watakuwa wanaishi kwa kutegemea kunywa damu za watu, watakuwa hawapatani na mwanga, lakini baadaye watauliwa na hali itarejea kama kawaida. Hivyo watu wengi waliposikia hivyo mitazamo yao ikabadilika kuhusu mambo yajayo..

Lakini ulishawahi kujiuliza juu ya nabii nyingine alizowahi kuzitoa huyu mama? Siko kumkosoa lakini lipo japo nataka ujifunze mwisho wa makala hii ..baadhi ya hizo alisema..

Mwaka 2010 kutatokea Aliens (Viumbe kutoka sayari nyingine) duniani..Jambo ambalo halikutokea, mpaka sasa halipo.

Mwaka 2004, alitabiri Osama ameshakufa,.Lakini Osama alikuja kupatikana mwaka 2011 na kuuawa.

Ndani ya kitabu chake kimoja aliandika, chanjo ya ugonjwa wa HIV, itapatikana mwaka 2005. Lakini chanjo hiyo mpaka leo hii haijapatikana.

Na nyingine nyingi, ambazo hatuwezi kuzichambua moja moja kwasababu sio lengo la ujumbe huu kuwakosoa watu, lakini tufumbuke macho, tusipelekwe na kila aina ya mafunuo yanayokuja duniani siku hizi…

Sasa tukirudi kwenye lile la mwaka 3020 alilolisema kuwa kutatokea viumbe wajulikanao kama Vampires..Na hili limewafanya watu wengi waamini kwa asilimia kubwa kwamba watatokea, kwasababu tu lile la ugonjwa ufananao na nimonia (Corona) lilitokea kisahihi.. na wengine wamekuwa na mtazamo mwingine wa kuishi wakidhani kuwa hii dunia itaendelea kuwepo mpaka huo mwaka wa 3000 yeye alioutaja…

Ni vizuri ukafahamu biblia inatukumbusha kwamba hata kama unabii utatolewa na mtu fulani na ukawa sahihi kabisa, bila kuwa na kasoro kasoro lakini kama unakinzana na maagizo ya Mungu, hatupaswi kupokelewa hata kidogo kwani ni wa uongo, (Soma kumbukumbu 13)

Hivyo usikimbilie kuupokea kila unabii ukasema unatoka kwa Mungu, kisa tu umetokea! bila wewe kukaa chini na kuutathimini katika maandiko..

Hizi ni nyakati za mwisho, kuhusu janga hili la Corona wapo wengine wengi sana wametabiri kiufasaha kuhusu juu ya gonjwa hili kama ulikuwa hujui lakini hawakuwa wakristo fuatilia hata habari ya Novel ya the eyes of the darkness, utaona, wapo wengine wengi sana, watafute internet utawaona,.. Lakini Pia Mungu anaweza kumtuma mtu wake kabisa , atoe unabii na ukaja kutimia, na akatoa maagizo yanayokinzana na Neno lake, Kumbe Ni Mungu ndiye aliyemtuma ili akupime moyo wako kama kweli unalishika Neno lake au la!!.. Na kama ukifuata tu, ndio umekwenda na maji.. Hebu tusome kidogo andiko linalozungumzia mambo hayo…

Kumbukumbu 13: 1 “Kukizuka katikati yako nabii, au mwotaji wa ndoto, akikutolea ishara au ajabu,

2 IKATUKIA HIYO ISHARA AU HIYO AJABU ALIYOKUAMBIA akisema, Na tuifuate miungu mingine usiyoijua, tuitumikie hiyo;

3 wewe usiyasikize maneno ya nabii yule, au yule mwotaji wa ndoto, kwa kuwa Bwana, Mungu wenu, yuawajaribu, apate kujua kwamba mwampenda Bwana, Mungu wenu, kwa mioyo yenu yote na roho zenu zote”.

Sasa tukirudi kwenye maandiko hakuna mahali popote panapotabiri kuhusu ujio wa “Vampires”..Au kutokea kwa viumbe vingine kutoka sayari za mbali (Aliens).. unabii huo ni batili..Hizo ni ndoto za wanasayansi ambazo zinakinzana na Neno la Mungu..

kama hayo yatakuja kutokea basi ungeshayaona kwenye maandiko tangu zamani, kwasababu hakuna jipya chini ya jua..Kwamfano tabiri za kutokea magonjwa ya mlipuko mfano wa tauni, yalitabiriwa hivyo mtu akitabiri kuhusu hilo sio jambo la kushangaza kwasababu biblia ilishaeleza, vile vile matetemeko, au njaa, au vita,manabii wa uongo, wapinga Kristo n.k. yote hayo yapo kwenye maandiko na yalishatabiriwa.. Lakini sio watu wanaofufuka na kunyonya damu za watu, watakaofufuka ni watakatifu tu, na sio kitu kingine chochote..Yesu pekee ndio UFUFUO NA UZIMA(Yohana 11:25), Na yeye peke yake ndiye mwenye funguo za kuzimu na mauti, shetani hana tena hizo funguo, hawezi kumfufua mtu wala kumleta mtu juu kama alishanyang’anywa hayo mamlaka kitambo sana…sasa jiulize atakayewafufua hao mavempire(mazombie) Wanyonye watu damu ni Bwana Yesu?..tafakari..unaona kabisa haingii akilini, ni kinyume na maandiko?…Ufufuo uliotabiriwa ni ufufuo wa wenye haki kwa ajili ya uzima na ufufuo wa waovu kwa ajili ya kuhukumiwa kwa maovu waliyoyafanya, na si kwaajili ya kunywa damu za watu!.

Yohana 5:28 “ Msistaajabie maneno hayo; kwa maana saa yaja, ambayo watu wote waliomo makaburini wataisikia sauti yake.

29 Nao watatoka; wale waliofanya mema kwa ufufuo wa uzima, na wale waliotenda mabaya kwa ufufuo wa hukumu”.

Hivyo jihadhari na udanganyifu wa ndoto za wanasayansi..

Kwa hiyo ndugu kwa maneno mafupi..Ni kwamba tunaishi katika siku za mwisho, na siku yoyote Kristo anarudi kulinyakua kanisa lake.. anayekupa matumaini kuwa kutakuwa na miaka mingine elfu moja ya kuishi mbeleni (1000), anakupoteza, ni agenda za shetani kuwaminisha watu kuwa muda bado sana, Kwamba Kristo bado sana arudi. Ilihali Dalili zote tulizoelezwa na Kristo zimeshatimia..Hivyo ni wakati wa kujiandaa sasa, acha kufuata mafunuo yasiyo dhahiri ya siku hizi za mwisho..Yapo mengi na yataendelea kuwa mengi, kwajinsi siku zinavyozidi kusogea..Ukiyafuata utayumbishwa sana, na kupotezewa mwelekeo wa imani yako kama huna msingi mzuri wa kimaandiko..Hizi ni nyakati za mwisho kweli kweli mpinga-Kristo ameshajiweka tayari kuanza kazi na sio VAMPIRE au ALIENS.

Hivyo Tubu dhambi zako leo, mpokee Kristo, kama hujamwamini, jiweke tayari kwa kurudi kwa pili kwa Kristo duniani.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

KUTAKUWA NA MATETEMEKO YA NCHI, NJAA NA TAUNI.

Kuna ufufuo wa aina ngapi?

BASI TUENDELEE KUMJUA MUNGU,NAYE ATATUJILIA KAMA MVUA YA VULI.

Je! Ni sahihi kuoa/kuolewa na mtu uliyemzidi umri?

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

KUZIMU ni mahali pa namna gani, Je! huko wanaishi watu wakifa na kwenda kupata mateso au ni vinginevyo?

Rudi Nyumbani:

Print this post

UWEZO WA KIPEKEE.

Kuna kipindi tuliishi bila kutegemea pua zetu kupumua, kuna kipindi tuliishi bila kutegemea midomo yetu kulia chakula…Na kipindi hicho si kingine zaidi ya kile kipindi ambacho tuliishi tumboni mwa mama zetu, kwa miezi 9 tuliishi maisha ya kimiujiza ujiza.. Hakuna mwanadamu yoyote anayeishi sasa ambaye hajapitia kuishi maisha hayo ya kimiujiza.

Hivyo si ajabu Bwana alisema… “….Imeandikwa, Mtu hataishi kwa mkate tu, ila kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu (Mathayo 4:4).

Kama kuna wakati maisha hayo yaliwezekana…hata sasa kuna mambo yanaonekana kama hayawezekani lakini yanawezekana.

Inaweza kuonekana haiwezekani kabisa leo kuishi maisha makamilifu yanayompendeza Mungu…lakini nataka nikuambie hilo linawezekana kabisa..kwasababu Bwana mwenyewe alisema tutakuwa wakamilifu kama Baba yetu alivyo mkamilifu…(Mathayo 5:48). Hivyo Mungu asiyeweza kusema uongo, hawezi kuumba kiumbe ambacho anajua atakipa jukumu kubwa zaidi ya uwezo wake…Kwasababu hiyo basi jinsi alivyotuumba sisi, anajua kabisa kuna namna au mazingira ambayo tukijiweka tutakuwa wakamilifu kama yeye anavyotaka sisi tuwe.

Na ukamilifu na utakatifu tunaouzungumzia sio ule wa kujisifu na kujibeza kwamba ni mkamilifu au mtakatifu mbele za Mungu, wala sio ule wa kujihesabia haki kwamba sifanyi hichi wala kile kama mtu Fulani au watu Fulani wanavyofanya…bali ukamilifu na utakatifu unaozungumziwa ni ule wa roho ya unyenyekevu, na ya kumwogopa Mungu, ambao huo unaleta moyo wa toba siku zote mbele za Mungu na hofu ya Mungu…ambapo hofu hiyo itakuzuia wewe kutokufanya mambo yote yasiyompendeza Mungu, hofu hiyo itakufanya usidhubutu kwenda kuzini, mawazo ya uzinzi yanapokujia unayashinda ndani ya sekunde chache sana, pia hofu hiyo inakuzuia kwenda kuiba, kwenda kutoa mimba, kwenda kula rushwa, n.k..Na haikufanyi wewe kujilinganisha na wengine au kufurahia wengine wanapofanya mambo ambayo wewe huyafanyi na kujifanya bora kupita hao…Yaani unapomwona mwingine anajiuza, unapata hisia kama ni dada yako au ndugu yako wa damu ndio yupo vile, lakini sio kufurahia kana kwamba umemzidi utakatifu, na hivyo wewe ni heri kuliko yeye…Huo sio utakatifu bali ni kujibeza, ambako hakumpendezi Mungu.

Hivyo..huo uwezo wa kuwa mkamilifu kwa namna hiyo ya kumpendeza Baba…Tumeahidiwa kwenye Neno la Mungu kwamba “Unaweza ukashuka juu yetu na ni ahadi”..Tunauita ni uwezo kwasababu katika hali ya kawaida, ni ngumu kumpenda Yule mtu anayekuchukia, ni ngumu kumsamehe Yule mtu ambaye amekutendea ubaya mkubwa sana, ni ngumu kurudisha mali ya Yule mtu aliyekuibia, ni ngumu kuacha uasherati au ukahaba unaokuingizia kipato kizuri n.k…Hivyo inahitajika uwezo mwingine kushuka juu yetu. Na huo uwezo ukishuka ndio unatufanya tuishi kimiujiza kama tulivyokuwa tunaishi kipindi Fulani huko nyuma tulivyokuwa tumboni mwa mama zetu…

Tulikuwa na pua lakini tulikuwa huituitumii tumboni, tulikuwa na midomo lakini tulikuwa huutumii kula..lakini bado tulikuwa tunaishi na kukua…Hali kadhalika ukiupokea huu uwezo leo, watu watashangaa unawezaje kuishi bila kufanya uzinzi na hali una uwezo wa kufanya hayo yote, na mazingira yanakuruhusu…wewe mwenyewe utajishangaa umewezaje kuishi bila kulewa tena pombe na ilihali una fedha za kukutosha kufanya hayo yote n.k.

Sasa uwezo huo utashuka juu yako endapo tu, utakubali tu kuviacha hivyo vitu…Kitu kimoja ambacho unahitaji kufahamu wewe ambaye bado hujampokea Yesu, ni kwamba Nguvu ya Roho Mtakatifu haiwezi kuzidi nguvu ya maamuzi yetu…maana yake ni kwamba Mungu hatulazimishi kama ma-robot kufanya mapenzi yake ingawa anao uwezo wa kufanya hivyo, ila hajachagua kufanya hivyo…anachokifanya ni kutuwekea chaguzi mbili mbele yetu…tuchague UZIMA au MAUTI. Tunapochagua uzima basi ndipo anatupa Baraka zote za Uzima ikiwemo UWEZO wa kuwa kama yeye.. Lakini tukichagua mauti hatatulazimisha kutupa uzima…Hivyo uchaguzi ni wetu.

Sasa hatuchagui kwa midomo…bali kwa vitendo..Maana yake ni kwamba kama ulikuwa unafanya kazi ya Bar, unaiacha mara moja, kama ulikuwa ni msikilizaji wa miziki ya kidunia kupitia simu yako unaifuta hiyo miziki na hizo video za kidunia zote pasipo kubakiza hata moja..kama ulikuwa ni mwizi na umeiba, unamrudishia Yule mtu mali yake uliyomuibia kama bado unayo na unakusudia kuacha wizi..kama ulikuwa unajiuza unaiacha hiyo biashara, kama ulikuwa ni mlevi hivyo hivyo unaacha kwenda ile Bar, na vitu vingine vyote visivyompendeza Mungu unajilazimisha kuviacha katika maisha yako Sasa Baba wa mbinguni akiona kwamba kwa vitendo umeacha mambo hayo…Ule uwezo unaushusha juu yako wakati huo huo ulipoamua kuyaweka chini maisha ya kale…

Kwasababu umeingia gharama ya kuyavua maisha yako ya kale, na yeye Baba wa mbinguni anaingia gharama ya kukutuza wewe usirudi tena nyuma..na anakutunza kwa njia gani?..kwa njia hiyo ya kukupa UWEZO wa kushinda Dhambi, na kuwa mkamilifu.

Sasa ndani ya kipindi kifupi baada ya wewe kuamua kuacha maisha ya dhambi kwa vitendo, utaona ile kiu ya pombe inakata ghafla, ile kiu ya kufanya ukahaba inakata ghafla, hupambani vita vikali kuukataa uasherati tofauti na hapo kwanza…mpaka wewe mwenyewe utajishangaa umekuwaje?..zamani ulikuwa ukipitisha siku mbili bila kunywa pombe unasikia kuumwa, lakini utashangaa inapita wiki, mara mwezi, mara mwaka hata ile hamu haipo..ulikuwa haipiti siku bila kujichua lakini utajikuta imepita wiki, mwezi na mwaka bila hata kukikumbuka hicho kitendo…sasa ukishafikia hatua kama hiyo basi ule uwezo umeshamiminwa ndani yako…na uwezo huo utaambatana na mambo mengine ya muhimu kama tuliyoyataja hapo juu..utajikuta unakuwa na hofu ya Mungu, na mtu wa kumpenda Mungu na kuzidi kujitenga na ulimwengu, pamoja na kuwa msaada kwa wengine ambao hawajaingia ndani ya Neema hiyo.

Kwahiyo kama wewe bado hujamwamini Yesu Kristo na bado hujapokea huo uwezo, tambua kwamba bado nafasi unayo…nguvu hiyo ni kutubadilisha ni zawadi kwetu sote kutoka kwa Baba, endapo tu tukimwamini Yesu..Hivyo basi popote pale ulipo tenga muda kadhaa peke yako binafsi, mwombe Mungu rehema..kisha kusudia kuacha yale yote uliomwomba akurehemu…Kumbuka kutubu maana yake ni kugeuka!..Hivyo matendo yako yana maana sana mbele za Mungu Baba zaidi ya maneno yako..

Pia inawezekana umeshamwamini Yesu, lakini umeomba muda mrefu uwezo huu ushuke juu yako, lakini bado huoni chochote, bado unajikuta unafanya punyeto, bado unajikuta unarudi kwenye ulevi, uasherati na ushirikina…kama unapitia hali kama hiyo basi fahamu kuwa hukutubu vizuri…Uliomba tu rehema..kwamba Bwana akusamehe tu hiki na kile..lakini hukukusudia kuviacha vile vitu kwa vitendo..bado ulikuwa ni miziki kwenye simu yako, bado ulikuwa unatembelea zile site za pornograph bado ulikuwa umejiungamanisha na makundi yale ya ulevi na walevi, na ndani kwako kulikuwa na chupa za bia, bado ulikuwa unarudi kwenye kazi yako ya Bar n.k..Hiyo ndio maana ule uwezo haukushuka ndani yako..lakini leo bado unayo nafasi..Tubu tu kwa kuacha hayo mambo na Bwana atakushushia uwezo huo wa kuishi kimiujiza kama aliokupa wakati ule ulipokuwa tumboni mwa mama yako.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

MUUNGANIKO WA MADHEHEBU NI MPANGO WA MPINGA-KRISTO.

NAMI NINAZO FUNGUO ZA MAUTI, NA ZA KUZIMU.

JE MOYO WAKO NI MNYOFU MBELE ZA MUNGU

Je ni sahihi kumtenga mtu anapofanya dhambi kanisani?

Mbona Mungu anaruhusu watu wapate shida, ilhali ana uwezo wa kutuepusha?

Kwanini Mungu alisema hakuna mtu awazaye kuuona uso wake akaishi?

Rudi Nyumbani:

Print this post

JINSI DHAMBI INAVYOMGHARIMU MTU SANA.

Mwanzo 47:9 “Yakobo akamjibu Farao, Siku za miaka ya kusafiri kwangu ni mia na thelathini; siku za miaka ya maisha yangu zimekuwa chache, TENA ZA TAABU, wala hazikufikilia siku za miaka ya maisha ya baba zangu katika siku za kusafiri kwao.”

Hakuna dhambi isiyokuwa na gharama. Unaweza ukajiuliza ni kwanini Yakobo alimwambia Farao siku zake za kusafiri duniani zimekuwa ni za taabu, zisizoweza kufananishwa na za baba zake..?..

Ni kwasababu ya ujanja alioufanya wa kumdanganya baba yake na kuchukua mbaraka wa ndugu yake, Japo ni kweli ndani yake kulikuwa na mpango wa Mungu uliobeba ujumbe uliomhusu Mesia, lakini kitendo alichokifanya bado kilikuwa ni uovu..Na hiyo haikuzuia kutumikia adhabu ya uovu wake.

Na ndio maana utaona Yakobo baada ya kufanya kitendo kile alikimbilia kwa mjomba wake, hata yule mama yake aliyependana naye na kupatana kutenda uovu, ndio ikawa mwisho wa kuonana kwao tena mpaka mwisho wa miaka 20 mbeleni, kuonyesha kuwa upendo wowote wenye makubaliano yasiyo makamilifu huwa haudumu..

Na alipofika kwa mjomba yake Labani, na kukaa huko, akimtumikia kwa ajili ya Raheli mke wake, kwa miaka saba, akidhani sasa ndio anakwenda kumpata Raheli, kumbe mjomba yake Labani akamfanyia hila kama ile ile aliyomfanyia ndugu yake Esau, matokeo yake akapewa dada yake Lea ndio awe mke wake badala ya Raheli, hivyo Labani akamwambia akimtaka na Raheli pia ni lazima amtumie miaka saba mingine..

Akaendelea kuwa mtumishi kwa muda mrefu mingine, mpaka wakati anaondoka, Na kwenda kule Kaanani nchi ya baba yake. Huko nako Watoto wake wawili Simeoni na Lawi, wakamfanyia hila kwa kudanganya, mpaka wakaenda kuwauwa watu wasiokuwa na hatia (Mwanzo 34),

Kama hiyo haitoshi, mwanawe wa kwanza Reubeni, akamzunguka baba yake, naye pia akamfanyia hila akaenda kulala na mke wake.

Tena Zaidi ya hayo, Watoto wake wakamfanyia hila kubwa Zaidi, kumdanganya kuwa mtoto wake Yusufu ampendaye ameliwa na mnyama mkali porini..Ikimfanya alie sana na kuomboleza kwa uchungu mwingi..

Kwahiyo unaweza kuona Maisha ya Yakobo, yalikuwa ni ya kudanganywa danganywa tu, na kufanyiwa hila kila kukicha, tofauti na ilivyokuwa kwa Ibrahimu na Isaka..

Kwasababu biblia inasema…

Mathayo 7:2 “Kwa kuwa hukumu ile mhukumuyo, ndiyo mtakayohukumiwa; na kipimo kile mpimiacho, ndicho mtakachopimiwa”.

Na ndio maana utaona anakiri kabisa Maisha yake yalikuwa ni ya taabu,..Lakini mwishoni kabisa Mungu alikuja kumpa faraja, kupitia mwanawe Yusufu.

Sasa huyo alikuwa ni Yakobo, mtu aliyebarikiwa na Mungu, lakini hakuachwa bila adhabu ya muda mrefu hapa duniani. Tujiulize sisi ambao tunaoendelea kuishi katika Maisha ya dhambi, Maisha yetu sikuzote ni ya dhuluma, tutawezaje kupona tusipouthamini wokovu mkuu namna hii?

Mithali 11:31 “Tazama, mwenye haki atalipwa duniani; Basi mwovu na mkosaji si mara nyingi Zaidi”

Adhabu hizi za mwilini zinafunua zile za rohoni..Wapo wanaodhani ukifa tu, ndio umekufa hakuna adhabu baada ya hapa…Adhabu ipo kwa wakosaji wote. Lakini Neema ya Mungu pia ipo kutukinga na adhabu hizo.

Na neema yenyewe ni kupitia YESU KRISTO. Tukimkabidhi Maisha yetu atatusamehe na kutugeuza na kutufanya kuwa wapya tena. Atafuta hata deni la dhambi na adhabu tulizostahili kuzipokea katika utoaji mimba wetu, katika uuaji wetu, katika rushwa zetu, katika uongo wetu, katika wizi wetu, katika uzinzi wetu, katika utapeli wetu n.k. Na hiyo ndio faida ya agano hili jipya la neema lililo katika damu ya YESU.

Hivyo kimbilia leo msalabani ikiwa bado hujaaokoka, tubu dhambi zako, ukabatizwe, usamehewe dhambi zako kisha upokee Roho Mtakatifu, atakaye kuwa na wewe hadi siku ile ya mwisho ya Unyakuo.

Bwana akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!

KWANINI UNAPASWA UJIWEKE TAYARI SASA, KABLA YA ULE WAKATI KUFIKA?.

USIJITAFUTIE KULAMBWA NA MBWA KWA DHAMBI YA KUTAMANI.

MAONO YA NABII AMOSI.

Je Mtu anaweza kusema uongo, Na Mungu akambariki?

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

MPINGA-KRISTO

Rudi Nyumbani:

Print this post

Je ni sahihi kumtenga mtu anapofanya dhambi kanisani?

JIBU: Yapo makundi mawili kanisani..kundi la kwanza ni lile ambalo linahusisha washirika, ambalo ndani yake kuna wachungaji, waalimu, wainjilisti, mashemasi na waumini na wengineo…Kundi lote hili linahusisha washirika ambao tayari wameshamwamini Yesu Kristo, na kubatizwa na kupokea Roho Mtakatifu…hali kadhalika wameshajifunza Neno vya kutosha na kukolea katika maarifa ya ki-Mungu…hata kufikia kiasi cha kuweza kuwaelekeza na kuwaelekeza wengine katika njia ya wokovu.

Na kundi la pili ni lile la watu waliookoka karibuni, au walioingia katika Imani kipindi cha hivi karibuni..Wengi wa hawa unakuta ni wachanga kiimani, na mara nyingi wanakuwa ni wageni…Hivyo wanakuwa bado wanahitaji msaada katika kujifunza Imani na uweza wa Mungu..Na kwasababu wametoka katika ulimwengu bado kuna tabia baadhi baadhi wanakuwa hawajaziacha kutokana na kwamba pengine hawajajua Neno la Mungu linasemaje kuhusu mambo hayo wanayoyafanya.

Sasa katika lile kundi la kwanza ambalo linahusisha washirika ambao tayari wameshaijua kweli ya Mungu kwa utimilifu mkubwa…wameshajua na kufundishwa uasherati ni dhambi, wizi ni dhambi, ulevi ni dhambi n.k…Wakakengeuka na kurudia matapishi na kufanya mojawapo ya dhambi hizo ambazo tayari walishajifunza kuwa ni machukizo kwa Mungu…Mtu wa Namna hiyo kimaandiko ANAPASWA ATENGWE!!…Na endapo asipotengwa wale ambao wanapaswa wamtenge watakuwa WANAFANYA DHAMBI MBELE ZA MUNGU!!…Hivyo ni agizo la Mungu kwamba ni lazima atengwe…

Na kutengwa huko kunahusisha, yeye kutoonekana maeneo au mazingira ya kanisa kwa kipindi kirefu…Na washirika wengine hawatakiwi hata kumsalimia wala kushirikiana naye kwa lolote lile, hata hata kama atatubu…atakaa mwenyewe kwa kipindi chote hicho…mpaka wakati ambao Kanisa litasikia amani ya Roho kumrudisha…na wakati huo wa kutengwa huku akiwa katika hali ya toba na maombolezo, Mungu atakuwa anamrudi kwa aliyoyafanya. Hivyo hakuna raha yoyote katika kutengwa, kama kweli ni mtoto wa Mungu. Kwasababu asipotolewa katika kanisa, watu wote wataiga na hawatamwogopa Mungu..Hivyo ili kuzuia hilo, biblia imeruhusu kumwondoa mtu huyo ili kanisa zima lisiharibike…

Utauliza ni wapi maandiko yanasema hivyo?

1Wakorintho 5:1 “Yakini habari imeenea ya kuwa kwenu kuna zinaa, na zinaa ya namna isiyokuwako hata katika Mataifa, kwamba mtu awe na mke wa babaye.

2 Nanyi mwajivuna, wala hamkusikitika, ili kwamba aondolewe miongoni mwenu huyo aliyetenda jambo hilo.

3 Kwa maana kweli, nisipokuwapo kwa mwili, lakini nikiwapo kwa roho, mimi mwenyewe nimekwisha kumhukumu yeye aliyetenda jambo hilo, kana kwamba nikiwapo.

4 Katika jina la Bwana wetu Yesu, ninyi mkiwa mmekusanyika pamoja na roho yangu, pamoja na uweza wa Bwana wetu Yesu;

5 kumtolea Shetani mtu huyo, ili mwili uadhibiwe, ili na roho iokolewe katika siku ya Bwana Yesu.

6 Kujisifu kwenu si kuzuri. Hamjui kwamba chachu kidogo hulichachusha donge zima

9 Naliwaandikia katika waraka wangu, kwamba msichangamane na wazinzi.

10 Sisemi msichangamane kabisa na wazinzi wa dunia hii, au na wenye kutamani, au na wanyang’anyi, au na wenye kuabudu sanamu; maana hapo ingewalazimu kutoka katika dunia.

11 Lakini, mambo yalivyo, naliwaandikia kwamba msichangamane na mtu aitwaye ndugu, akiwa ni mzinzi au mwenye kutamani au mwenye kuabudu sanamu au mtukanaji au mlevi au mnyang’anyi; mtu wa namna hii msikubali hata kula naye.

12 Maana yanihusu nini kuwahukumu wale walio nje? Ninyi hamwahukumu hao walio ndani?

13 Lakini hao walio nje Mungu atawahukumu. Ninyi mwondoeni yule mbaya miongoni mwenu.”

Soma pia..

2Wathesalonike 3:14 “Na ikiwa mtu awaye yote halishiki neno letu la waraka huu, jihadharini na mtu huyo, wala msizungumze naye, apate kutahayari; 15 lakini msimhesabu kuwa adui, bali mwonyeni kama ndugu”.

Hivyo kuna hatari sana ya kufanya dhambi za makusudi baada ya kuujua ukweli..Tunakuwa tunakabidhiwa shetani ashughulike na sisi, Hivyo tujihakiki na Bwana atuepushe na hayo yote.

Maran atha!

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

Je! mtu aliyeokoka anaruhusiwa kumiliki Lodge ambayo ina Bar ndani yake?

Mahuru ndio nini?

Kwanini Mungu alisema hakuna mtu awazaye kuuona uso wake akaishi?

Je Mtu anaweza kusema uongo, Na Mungu akambariki?

Nini maana ya mstari huu: (Mtu ambarikiye mwenzake kwa sauti kuu asubuhi na mapema; Itahesabiwa kuwa ni laana kwake.Mithali 27:14 )?

https://wingulamashahidi.org/2019/09/01/maana-ya-huu-mstari-ni-ipi-mithali-144-zizi-ni-safi-ambapo-hapana-ngombebali-nguvu-za-ngombe-zaleta-faida-nyingi/

Rudi Nyumbani:

Print this post

MAOMBI YA VITA

Maombi ya vita yakoje?..Je! ni lazima kuomba maombi ya vita?

Maombi yamegawanyika katika sehemu kuu 3

  1. Maombi ya shukrani
  2. Maombi ya kuwasilisha haja mbele za Mungu.
  3. Na Maombi ya KUTANGAZA.

Katika aina aina ya kwanza ya maombi ni ile ya KUSHUKURU, Ambapo mwamini atapiga magoti au atasimama na kumshukuru Mungu kwa mema yote anayomtendea yeye binafsi, na familia yake, na jamaa zake, na Taifa lake…hali kadhalika na kwa kila kitu ambacho anastahili kukishukuru mbele za Mungu. Na maombi haya ndio maombi ya muhimu kuliko yote, na yanayopaswa kuchukua muda mrefu kuliko maombi mengine yoyote.

Aina ya pili ya maombi ni ya kuwasilisha haja mbele za Mungu…Haya ni yale ambayo mtu atapiga magoti na kumwomba Mungu hitaji fulani amtimizie, hilo linaweza kuwa hitaji lake binafsi au la mtu mwingine au la kanisa au la Taifa.

Na Aina ya tatu na ya mwisho ya maombi ni maombi ya KUTANGAZA…Katika aina hii ya mwisho ya maombi ndipo panapopatikana maombi ya vita kama yanavyotajwa na wengi, yanaangukia katika kundi hili.

Katika maombi ya kutangaza..hapa ndipo mtu atatumia kinywa chake na mamlaka aliyopewa kuamuru na kuamrisha kila nguvu zote za giza, zilizo kinyume na nguvu za Mungu zipate kuanguka chini kwa jina la Yesu..

Mfano wa maombi ya kutangaza ni maombi ya kutoa pepo. Tunapoamuru pepo amtoke Mtu au kitu kwa jina la Yesu hapo tumetangaza kile kitu kifunguliwe kwa mamlaka ya kimbinguni, na hivyo ni lazima kitii.

Hali kadhalika kama kuna maneno maovu, au mitego ya adui, au kuna mipango na mikakati iliyopangwa na wanadamu au watumishi wa shetani dhidi yako au ndugu,au jamaa au kanisa au Taifa, kwa kutumia vinywa vyetu na kwa jina la YESU, tunaweza kuifuta mipango hiyo, na ratiba hizo na mikakati hiyo, na ikafutika sawasawa na tulivyotamka/kutangaza.

Sasa maombi haya ndio yanayojulikana na wengi kama MAOMBI YA VITA..Mwamini anaweza kutumia muda wa kutosha kutamka baraka juu yake na kwa ndugu zake na kwa kanisa la Kristo kwa jina la Yesu, hali kadhalika anaweza kutangaza kufuta kila mipango ya ibilisi iliyopangwa juu yake, juu ya familia yake, ndugu zake, kazi zake, afya yake, kanisa lake, nchi yake na kila kitu kinachohusiana na yeye. Maombi haya yanaweza kuchukua masaa kadhaa kwa kadiri mtu alivyojaliwa kuomba, na yanaweza kufanyika kila siku. Na pia ni maombi ya muhimu sana. Na maombi haya yanahusisha kutoa au kupaza sauti kwa nguvu…Huwezi kukemea pepo lililopo ndani ya mtu kimoyomoyo…Katika biblia Bwana wetu Yesu, pamoja na Mitume walitamka kwa nguvu na pepo wakawatoka watu…Bwana alipoulaani ule mtini, alitoa sauti kutoka katika kinywa chake..Hali kadhalika tunapozilaani kazi za Adui shetani, ni lazima sauti zitoke katika vinywa vyetu. Sio lazima itoke sauti kama kilio, lakini angalau sauti isikike..Na ndivyo shetani na mapepo yake tutakavyoyaangusha chini..

Maombi haya hayana muda maalumu wa kuomba…Ni vizuri zaidi kuomba kwa pamoja kama kikundi, au peke yako binafsi wakati wa utulivu.

Kwa kina kuhusu Aina tatu hizi za maombi Mwishoni kabisa mwa somo hili chini kuna somo lenye kichwa cha FAIDA ZA MAOMBI. Lifungue hilo ulisome kwa msaada wa Roho Mtakatifu naamini utapata kuongeza kitu juu ya vile unavyovijua.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

FAIDA ZA MAOMBI.

JE MOYO WAKO NI MNYOFU MBELE ZA MUNGU

Je kuzalishwa na mkunga wa kiume ni dhambi?

KIJITO CHA UTAKASO.

MKARIBIE BWANA ZAIDI ILI UFANYIKE NGUZO.

KUTUBU SIO KUOMBA REHEMA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Hamtaimaliza miji ya Israeli hata ajapo mwana wa Adamu?

Bwana alimaanisha nini kusema “Hamtaimaliza miji ya Israeli hata ajapo mwana wa Adamu”


Tusome;

Mathayo 10:23 “Lakini watakapowafukuza katika mji huu, kimbilieni mwingine; kwa maana ni kweli nawaambia HAMTAIMALIZA MIJI YA ISRAELI HATA AJAPO MWANA WA ADAMU”

JIBU: Ukiusoma mstari huo kuanzia juu kabisa, yaani kuanzia mstari wa kwanza…Utaona ni Habari inayohusu tendo la Bwana Yesu kuwatuma wanafunzi wake kwenda kuhubiri injili katika miji ya Israeli…Na utaona alipowaagiza wakahubiri aliwapa na baadhi ya maagizo au masharti, kwamba wasichukue chochote na pia wawe wavumilivu kwa watakayoyapitia huko..Lakini mwishoni kabisa mwa maagizo tunaona Bwana anawaambia…“hamtaimaliza miji ya Israeli hata ajapo mwana wa Adamu”..

Sasa swali linalojitengeneza kwenye vichwa vyetu hapo ni kwamba…mbona Bwana Mitume walikuwa wameshaimaliza hiyo miji na Yesu bado alikuwa hajarudi?..ina maana mpaka leo injili haijasambaa kwenye miji yote ya Israeli ndio maana Bwana hajarudi mpaka leo?.

Jibu rahisi la swali hili tunaweza kulipata kwenye Habari kama hii hii katika kitabu cha Luka…Tusome,

Luka 10:1 “Basi, baada ya hayo Bwana aliweka na wengine, sabini, akawatuma wawili wawili wamtangulie kwenda kila mji na kila mahali alipokusudia kwenda mwenyewe.

2 Akawaambia, Mavuno ni mengi, lakini watenda kazi ni wachache; basi mwombeni Bwana wa mavuno apeleke watenda kazi katika mavuno yake.

3 Enendeni, angalieni, nawatuma kama wana kondoo kati ya mbwa-mwitu.

4 Msichukue mfuko, wala mkoba, wala viatu; wala msimwamkie mtu njia”

Tuvichunguze baadhi ya vipengele katika mstari huo wa kwanza ambavyo ndivyo vitakavyotupa dira ya kuelewa Habari nzima….katika mstari wa kwanza biblia inasema… “Bwana aliweka na wengine, sabini, AKAWATUMA WAWILI WAWILI WAMTANGULIE kwenda kila mji na kila mahali alipokusudia kwenda mwenyewe”…Zingatia hilo neno “WAMTANGULIE”..Kama wewe ni mswahili mzuri utaelewa maana ya neno “kutangulia” ni nini…kutangulia maana yake ni mtu anakwenda mahali kisha wewe unafuata baadaye…yaani anawahi kufika kule kabla wewe kufika…hiyo ndiyo maana ya kutangulia…

Hivyo mstari huo una maana kuwa “hao wanafunzi sabini na wale 12 Bwana aliokuwa anawatuma kwenda huko katika miji ya Israeli hakuwatuma tu…huko wenyewe…bali Bwana aliwaahidi kwamba atawafuata, hivyo aliwatuma tu kama wamtangulie.”

Ili kuelewa vizuri tafakari tena kamfano haka… “Umemwagiza mfanyakazi wako atangulie asubuhi na mapema sehemu ya kazi kuendelea na kazi, na ukamwambia hatamaliza kazi zote kabla ya wewe kufika hapo ofisini, maana yake utafika kabla hata hajamaliza kazi zote”.. Ndicho Bwana alichowaambia wanafunzi wake, kwamba huko wanakwenda naye pia atakuja kabla hawajaimaliza miji yote ya Israeli (Hilo ni neno la Faraja)…Na kweli aliiungana nao baadaye hakuwaacha yatima…

Sasa kuna jambo moja la kujifunza hapo…Kwamba Desturi ya Bwana ilikuwa hafiki mahali kabla ya kutuma kwanza wajumbe wake wakamtengenezee njia…Maana yake kabla ya yeye kuja mahali anatuma kwanza watumishi wake wakahubiri injili..Ndivyo alivyofanya kwa Yohana Mbatizaji…yeye alitumwa kumtengenezea Bwana njia na kuiandaa mioyo ya watu kabla Bwana mwenyewe hajaanza kuhubiri..ili atakapoanza kuhubiri vile Bwana atakavyohubiri visiwe ni vitu vigeni sana kwa watu wake.(kasome Yohana 10:41-42, na Luka 1:17).

Utaona sehemu zote kabla Bwana hajaenda mahali huwa anatuma wanafunzi wake kwanza na baadaye anaungana nao.. (kasome Luka 9:52-54, Marko 14:12-18, Marko 11:1-4)..

Ndugu Mpendwa hata sasa, Bwana bado anatuma watu wake kuitengeneza njia yake…Umesikia injili mara ngapi?, kila mahali upitapo, mtaani, kwenye magari, mashuleni, unapofanyia kazi?..lakini unadharau kwasababu labda anayekuhubiria umemzidi kipato, au umemzidi elimu, au umri?..Lakini lisikie hili neno ambalo Bwana Yesu alilisema..

Marko 9:37 “Mtu akimpokea mtoto mmoja wa namna hii kwa jina langu, anipokea mimi; na mtu akinipokea mimi, humpokea, si mimi, bali yeye aliyenituma”

Hako katoto unakokadharau sasa, huyo uliyemzidi elimu, pengine na kipato…huyo ambaye hata maandiko hawezi kuyatamka vizuri na anakuhubiria utubu umgeukie Mungu lakini unamchukulia unavyojua wewe…Bwana Yesu ambaye sasa hivi yupo mbingu za mbingu anamheshimu, siku ile tutaonyeshwa tumemkataa yeye Dhahiri.

Bwana atusaidie.

Kama bado hujampa Yesu Kristo Maisha yako, tupo ukingoni sana mwa siku za mwisho, ambapo ghafla tu unyakuo utapita na watakatifu watatoweka….waliobaki hawatasikia tena usumbufu wa mahubiri wanayohubiriwa sasa..watakuwa wamefungua jalada lingine la maisha..na watakatifu vivyo hivyo..Kwahiyo sio wakati wa kukaa nje..Mlango wa Safina unakaribia kufungwa, waasherati,walevi, wezi, watukanaji, watazamaji picha chafu mitandaoni, wanaokula rushwa, na wanaofanya kila aina ya machafuko biblia inasema sehemu yao itakuwa ni katika lile ziwa la moto. Ingia leo ndani ya Safina ya Yesu, wokovu unapatikana bure.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

Wewe u nabii yule akajibu la!..swali huyu ‘nabii yule’ ni nani?

JE! WEWE NI MWAKILISHI MWEMA?

Kwanini Bwana alisema Hakuna aliye mwema ila mmoja?

Kwanini Bwana alisema Hakuna aliye mwema ila mmoja?

Habari ile ya Pilato kuchanganya zile damu za wayahudi na pamoja na dhabihu zao,(Luka 13) ilihusu nini?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Wewe u nabii yule akajibu la!..swali huyu ‘nabii yule’ ni nani?

SWALI: Ukisoma Yohana 1:19-26 inaelezea habari za Yohana mbatizaji akijitambulisha yeye ni nani! Napata shida katika mstari wa 21, alipoulizwa ” wewe u nabii yule” akajibu la!.

Huyu nabii yule, ambaye wayahudi walimtegemea kuja, ni nani?

Maana Yohana alishaulizwa kama yeye ni KRISTO, au ELIYA mwanzoni na akakanusha kuwa yeye si hao…Sasa huyu nabii yule ni nani?


JIBU: Tusome..

Yohana 1:19 “Na huu ndio ushuhuda wake Yohana, Wayahudi walipotuma kwake makuhani na Walawi kutoka Yerusalemu ili wamwulize, Wewe u nani?

20  Naye alikiri, wala hakukana; alikiri kwamba, Mimi siye Kristo.

21  Wakamwuliza, Ni nini basi? U Eliya wewe? Akasema, Mimi siye. Wewe u nabii yule? Akajibu, La.

22  Basi wakamwambia, U nani? Tuwape majibu wale waliotupeleka. Wanenaje juu ya nafsi yako”?

Mstari huu umetafsiriwa vibaya hususani kwa watu wasio wakristo wanaosema huo ni unabii unaomzungumzia mtume Mohamedi, kuwa atakuja baada ya Kristo kuwarejeza watu kwa Mungu

Lakini biblia haitabiri jambo lolote kuhusu kuja kwa mtu mwingine baada ya Kristo, yeye ndiye Alpha na Omega, hakuna nabii au mtume mwingine yoyote ambaye atatumwa baada ya Kristo, kuwaongoza watu katika njia ya kweli..Kama mtu atajiita mtume au Nabii basi ajue huduma yake italenga katika kuwaelekeza watu kwa  huyu nabii mkuu Yesu Kristo,..Lakini sio kupokea maagizo yake tofauti yanayodai kuwa yanawaongoza watu kwa Mungu.

Sasa swali ni nani aliyekuwa anazungumziwa pale?

Kabla ya kufahamu ni nani aliyekuwa anazungumziwa pale, ni vizuri kufahamu Unabii Musa aliutoa huko nyuma kuhusu nabii mwingine ambaye Mungu atamnyanyua kama yeye, (Kumbukumbu 18:15-22)..Sasa biblia inaweka wazi kabisa nabii huyo aliyezungumziwa ni Yesu Kristo na hilo tunalithibitisha katika (Matendo 3:22-23) ukipata nafasi unaweza kuvisoma kwa muda wako vifungu hivyo…

Sasa Je hawa wayahudi walimaanisha nabii gani tena huyu? Ambaye walimuulizia Yohana..?

Jibu ni kwamba enzi zile wayahudi walikuwa na mitazamo mingi ambayo mengine haikuwa sahihi, na hiyo ni kutokana na kuwa na ukimya wa miaka mingi bila kuzukiwa na nabii yoyote Israeli, tangu nabii wa mwisho ambaye aliyejulikana kama Malaki..Hiyo ikawafanya wengi wao waamini kuwa wapo manabii wa kale kama Yeremia watafufuka au watashushwa kwa ajili ya kuwatolea unabii na maneno ya Mungu..

Na ndio maana utaona pale Bwana Yesu alipowauliza mitume wake, kuwa yeye ni nani walimjibu hivi..

Mathayo 16:13 “ Basi Yesu akaenda pande za Kaisaria-Filipi, akawauliza wanafunzi wake akasema, Watu hunena Mwana wa Adamu kuwa ni nani? 14  Wakasema, Wengine hunena u Yohana Mbatizaji, wengine Eliya, wengine Yeremia au mmojawapo wa manabii.

Soma tena..

Luka 9:7 “Na Herode mfalme akasikia habari za yote yaliyotendeka, akafadhaika kwa sababu watu wengine walisema ya kwamba Yohana amefufuka katika wafu,

8  na wengine ya kwamba Eliya ametokea, na wengine ya kwamba mmojawapo wa manabii wa kale amefufuka”.

Soma pia Luka 9:19..utaona jambo hilo hilo…

Mistari hii yote inathibitisha kuwa, wayahudi walikuwa wanatazamia kuwa mmojawapo wa manabii wa kale atanyanyuka kabla ya kuwasili masihi (Kristo) duniani, ambaye labda ni Yeremia, au Danieli, au Isaya… mtazamo ambao haukuwa sahihi.

Na ndio maana hata pale utaona sasa kwanini Yohana aliulizwa je “wewe u nabii yule” wakirejea mmojawapo wa manabii wa kale amekuja kuwahubiria maneno ya Mungu…Lakini yeye akajibu  La!.

Hivyo kwa hitimisho hakuna Nabii mwingine aliyetokea wala tunayemngojea sasa, atakayekuwa mkuu Zaidi ya Masihi YESU KRISTO. Huyo ndiye chapa na nafsi ya Mungu, na mkuu wa wa wafalme wa Dunia, na Bwana wa Mabwana.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

JE! MUNGU NI NANI?

Shetani ni nani?

Yeshuruni ni nani katika biblia?

Nini tofauti kati ya Amri, sheria na Hukumu?

NIFANYE NINI ILI NILITIMIZE KUSUDI LA MUNGU.

Neno I.N.R.I kwenye msalaba wa Yesu maana yake ni nini?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Je ni kweli huwezi kuijua karama yako mpaka uwekewe mikono na wazee?

SWALI: 1Timotheo 4:14 “Usiache kuitumia karama ile iliyomo ndani yako, uliyopewa kwa unabii na kwa kuwekewa mikono ya wazee.”.. Je ni kweli huwezi kuijua au kuitumia karama yako mpaka uwekewe mikono na wazee?


JIBU: Kwanza ni muhimu kufahamu wazee wanaozungumziwa hapo ni wakina nani?..wazee wanaozungumziwa hapo sio wazee wa ukoo, wala wazee wa vijiji, bali wazee wa Imani ambao ni viongozi wakongwe kiimani katika Kanisa…Na hawa wanaweza kuwa Wachungaji, Maaskofu au Mashemasi..ambao wamekaa muda mrefu wakitumika katika kazi ya Mungu. Wengi wa hawa Bwana anakuwa amewafundisha kipekee na kuwapitisha katika mambo mengi, hivyo wanakuwa wamekirimiwa hekima zaidi ya wengi katika ufahamu wa Neno..Kama vile Sulemani, alivyoandika hekima zile na kuwaita wale aliowaandikia “wanangu”

Mithali 3: 11 “Mwanangu, usidharau kuadhibiwa na Bwana, Wala usione ni taabu kurudiwa naye.

12 Kwa kuwa Bwana ampendaye humrudi, Kama vile baba mwanawe ampendezaye”.

Ni kama vile Mtume Paulo alivyowaita wanawe, wale aliowageuza na kumgeukia Kristo.

2Timotheo 2:1 “Paulo, mtume wa Kristo Yesu, kwa mapenzi ya Mungu; kwa ajili ya ahadi ya uzima ulio katika Kristo Yesu; kwa Timotheo, mwanangu mpendwa. Neema na iwe kwako, na rehema, na amani, zitokazo kwa Mungu Baba na kwa Kristo Yesu Bwana wetu”.

Sasa hili kundi katika kanisa ndio linaloitwa wazee wa kanisa. Lakini pamoja na hayo, sio wote ni watumishi wa kweli wa Mungu, wapo pia wazee ambao ni mapando ya shetani..biblia imesema tutawatambua kwa matunda yao.

Sasa tukirudi kwenye swali, Je ni lazima kuwekewa mikono na wazee hawa ili karama au huduma ijidhihirishe?, na kwamba pasipo kuwekewa mikono na wazee hawa huwezi kuifahamu karama yako au huwezi kuifanya kazi ya Mungu?

Jibu rahisi la swali hili ni HAPANA!..Mikono ya wazee haiumbi karama ndani ya mtu, wala haidhihirishi karama ndani ya mtu…bali ina bariki karama ambayo tayari ipo ndani ya mtu.

Wengi wasiouelewa mstari huu, wanafikiri mpaka wazifahamu karama zao ni lazima kwanza wawekewe mikono na wazee…jambo ambalo sio sahihi kibiblia.

Katika biblia Agano jipya, tunamsoma mtu anayeitwa Paulo na Barnaba…hawa baada ya watu wote kuijua karama ambayo Mungu kaiweka ndani yao, yaani karama ya kitume…Ndipo wazee wa kanisa wakawawekewa mikono kwa uongozo wa Roho Mtakatifu, kama kuibariki huduma/ karama ambayo tayari ipo ndani yao..na hawakuwawekea kwanza mikono ndipo wakawa mitume..Hapana…Paulo alikuwa mtume tayari na alikuwa ameshapokea maagizo ya utume wake kutoka kwa Bwana Yesu mwenyewe, tangu alipokuwa anaeleke Dameski…hivyo kilichokuwa kimesalia ni watu tu kuibariki huduma hiyo, na hata kama watu wasingeibariki bado Mungu angeendelea kuibariki tu, isipokuwa kuombeana kule kunazidi kuongeza neema ya Mungu juu ya huduma ya mtu, hivyo kuna umuhimu pia mkubwa sana…Tusome,

Matendo 13:2 “Basi hawa walipokuwa wakimfanyia Bwana ibada na kufunga, Roho Mtakatifu akasema, Nitengeeni Barnaba na Sauli kwa kazi ile niliyowaitia.

3 Ndipo wakiisha kufunga na kuomba, wakaweka mikono yao juu yao, wakawaacha waende zao”.

Umeona hapo?..Neno linasema “Nitengeeni Paulo na Barnaba kwa kazi ile niliyowaitia” maana yake..tayari walikuwa wameshapewa huduma/kazi na Mungu..na sio kwamba walipokea huduma au karama ile siku ile ya kuwekewa mikono au baada ya kuwekewa mikono.

Hali kadhalika hata sasa, mtu aliyeokoka anapewa huduma na Mungu mwenyewe na si mwanadamu…hakuna mantiki yoyote kwenda kutafuta kupokea karama yako kutoka kwa mtumishi au mchungaji au mwanadamu yoyote Yule..Mungu aliyekuita atakufunulia wewe mwenyewe wito aliokuitia….na baada ya kukufunulia, wewe mwenyewe utaujua na watu wote wa kanisa watauona wito wako…na wakishaona kwamba Fulani anawito kweli katika eneo Fulani, labda anahubiri Neno kwa bidii na kwa moyo, anaombea watu kwa bidii, anaimba kimaandiko kwa bidii, anafariji watu kwa bidii, anahudumia watu hivi au vile kwa bidii n.k..Hapo sasa ndipo wazee wanakusanyika pamoja kwa uongozo wa Roho Mtakatifu na kuweka mikono juu ya mtu huyo…Na lengo la kufanya vile ni kuibariki ile kazi Mungu aliyoianzisha ndani yake, kumbariki kwamba Bwana azidi kuichochea karama ile iliyomo ndani yake kwa bidii sana hilo tu na si kumpa ile karama..Na tendo hilo lina nguvu sana katika Roho.

Lakini sio tu, mtu hajaokoka, au hajui lolote, wala hatumiki popote na anakwenda kutafuta kuwekewa mikono ili aipate karama..kama leo hii utaona manabii wa uongo wanawaita watu na kuwashika na kuwaambia nimekupa karama ya kinabii, kuanzia leo utaona maono, au nimekupa karama ya kiualimu kuanzia leo utafundisha, au nimekupa karama ya kiutume, au ya uimbaji…hapo hutaambulia chochote zaidi ya maroho ya Yule adui. Vipawa na karama anayetoa ni mmoja tu! naye ni BWANA YESU! MKUU WA UZIMA. Huyo pekee ndio biblia inasema alipopaa mbinguni aliteka mateka akawapa wanadamu vipawa (Waefeso 4:8)…hivyo hakuna mwadamu wala mwinjilisti, wala mwalimu wala Padre, wala nabii wala papa mwenye uwezo wa kumpa mtu karama au kipawa.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

KUMBUKA, VIVUKO VYA YORDANI VINAKUNGOJA MBELENI.

NI WAPI MAHALI SAHIHI PA KULIPA ZAKA?

NA MTU MMOJA AKAVUTA UPINDE KWA KUBAHATISHA, AKAMPIGA MFALME

BIBLIA INATUASA TUFANYE NINI KATIKA ZAMA HIZI ZA UOVU?

DANIELI:Mlango wa 5

HATUA ZA ROHO MTAKATIFU KATIKA KUTUONGOZA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

KAMA TUNATAKA KUWA ASKARI WA BWANA, NI LAZIMA TUJUE VIGEZO.

Shalom mpendwa, Karibu katika kuyatafakari maneno ya uzima..

Tunaijua Habari ya Gideoni na wanajeshi wake 300, lakini ni vizuri tukajikumbusha tena, naamini lipo jambo jipya tutajifunza leo ndani yake..Tusome..

Waamuzi 7:4 “Bwana akamwambia Gideoni; Hata sasa watu hawa ni wengi mno; uwalete chini majini, nami nitawajaribu huko kwa ajili yako; kisha itakuwa ya kwamba yule nitakayekuambia, Huyu atakwenda pamoja nawe, ndiye atakayekwenda pamoja nawe; na mtu yule nitakayekuambia, Huyu hatakwenda pamoja nawe, basi mtu huyo hatakwenda.

5 Basi akawaleta watu chini majini. Bwana akamwambia Gideoni, Kila mtu atakayeyaramba maji kwa ulimi wake, kama vile arambavyo mbwa, huyo utamweka kando; kadhalika kila mtu apigaye magoti kunywa.

6 Na hesabu ya hao waliokunywa kwa kuramba-ramba, wakipeleka mkono kinywani, ilikuwa watu mia tatu; bali watu wengine wote walipiga magoti kunywa maji.

7 Bwana akamwambia Gideoni, Kwa watu hawa mia tatu walioyaramba maji nitawaokoa, nami nitawatia Wamidiani katika mikono yako; lakini watu hawa wote wengine na waende zao, kila mtu mahali pake”.

Amen.

Ukitazama hapo, utaona lile kundi la kwanza walipofika tu majini jambo la kwanza walipiga magoti, jambo ambalo wale wengine hawakulifanya…

Pili walikutanisha midomo yao na yale maji ya mto moja kwa moja.Kwasababu walikuwa na kiu sana, hivyo njia pekee walioina kuwa itaondoa kiu yao kwa haraka ni kwa kupelekea midomo moja kwa moja majini, ili wanywe kwa haraka haraka bila bugdha yoyote.

Tofauti na wale wenzao, ambao walikuwa kwanza wanayakusanya maji kwenye mikono yao, kisha wanayalamba kidogo kidogo, kisha tena wanachota na kulamba hivyo hivyo, kidogo kidogo hadi walipokata kiu yao..

Walikuwa wanahakikisha kwanza kile wanachokinywa kabla ya kukinywa, bila kujali kuwa yatakuwa yanakaa kidogo tu kwenye mikono yao, na kuvuja vuja..Bila kujali kujitesa kuchota chota kila mara.

Pia walikataa kupiga magoti kuelekea maji, bali waliinama tu, au walichuchumaa, na hiyo ikawapa wigo mzuri wa kuona hatari iliyo mbele yao, kiasi kwamba hata adui angetokea mbele yao wangeweza kuacha wanachokifanya na kupigana nao, tofauti na wale wengine..

Vivyo hivyo, hata sisi, ni kweli tupo ulimwenguni, na wakati mwingine itatupasa tuchume vya ulimwenguni kidogo, lakini tukijisahau kuwa tupo mapambanoni na adui yetu shetani yupo mbele yetu, tukayapigia magoti mambo ya ulimwengu huu.. yaani kufanya mambo ya ulimwengu huu kuwa ndio kila kitu kwetu.Tujue kuwa hatufai kwa ufalme wa mbinguni.

Sio kila kinachokuja mbele yetu, ni cha kukipaparikia kwa moyo wote, sio kila fursa ni kutoka kwa Mungu vingine ni mitego ya adui,..Unapaswa uchague kazi, unapaswa uchague marafiki, unapaswa uchague mazingira ya kuishi..Sio kila kazi ilimradi tu inakupa pesa ni ya kuifanya..Unapaswa uipitishe kwanza kwenye mikono yako ya rohoni, uangalie je! Hii kazi ni salama, haitaniletea athari yoyote katika wokovu wangu huko mbeleni? Je hii kazi ni kulingana na Neno?..

Sasa ukishaiona haiikinzani na Neno la Mungu na haina madhara kiimani, ndipo unairamba tena kidogo kidogo, na sio kuikurupukia.. Kila tenda inayokuja inaipitisha kwenye maandiko kwanza, je ina sumu ya adui?..kama askari hawa walivyoipitisha maji mikononi kwanza kabla ya kuyanywa…Unaitazama je! Ina rushwa ndani yake?, je ina utapeli ndani yake n.k

Lakini kama hutajiuliza chochote wewe, kila fursa inayokuja mbele yetu, tunaipaparikia hutufai kuwa askari wa Mungu..haijalishi ni nzuri vipi, kwasababu huwezi jua baadaye itakufanya hata ule wakati wako uliokuwa unautumia kuomba unamezwa na shughuli hizo, au jumapili yako ulikuwa unakwenda ibadani sasa, inaingiliwa na kazi hizo, au mavazi yako uliyokuwa unavaa ya staha yanageuzwa na kuwa ya kikahaba.

Vile vile na marafiki pia, sio kila mtu unayekutana naye ni lazima awe Rafiki yako tu, unapaswa umpitishe kwanza kwenye mikono yako ya rohoni, kisha ukimwona anaendana na Imani yako, ndipo uanze kuunga naye urafiki, tena kidogo kidogo, mpaka utakapomthitisha kamili baada ya muda mrefu..Wengi leo wanawachunguza marafiki kama ni washirikina tu!..hicho ndicho wanachoweza kuchuguza..lakini hawawez kuchunguza huyu rafiki kama ni mlevi, au kama ni mtu wa rushwa, au mtu wa kutomjali Mungu..wengi hayo macho hawana, wana macho tu ya kuchunguza ushirikina.

Vilevile na mazingira, sio kila mazingira yanayokujia mbele yako ni ya kuishi au kukubaliana nayo..chunguza kwanza..Chunguza chochote kile kabla hujakifanya ukikilinganisha na wokovu wako, Je, ni salama?..kwasababu wokovu ni kitu cha kulinda na kukipigania kuliko kitu kingine chochote. Biblia inasema Imani tumekabidhiwa mara moja tu!

Kwasababu mitego ya adui ipo kila kona. Mungu aliona mbele ndio maana hakuwaruhusu wale wengine waende vitani, kwasababu alijua huko mbeleni, askari wataishiwa nguvu sana, watakuwa na kiu na njaa, lakini bado mapambano hayajaisha, Je watakuwa tayari kutotazama mambo ya mwilini wakaendelea na mapambano? (Soma Waamuzi 8:4). Ndio maana akawatenga wale 300 tu..waliovumilia kunywa maji kwa uangalifu na taratibu taratibu.

Na sisi pia tukitaka tuwe askari kamili wa Kristo, Bwana atusaidie tuyazingatie hayo….

Mungu akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

Je Mtu anaweza kusema uongo, Na Mungu akambariki?

KILA MTU ATATOA HABARI ZAKE MWENYEWE.

BIBLIA INATUASA TUFANYE NINI KATIKA ZAMA HIZI ZA UOVU?

Je! habari ya Yusufu, inabeba ujumbe gani kwa agano jipya?

NINI NI KILICHOMFANYA IBRAHIMU AKUBALI KUMTOA MWANAWE SADAKA?

JE! KUBET NI DHAMBI?

Rudi Nyumbani:

Print this post

USIMWOGOPE YEZEBELI.

Mungu anapompa mtu kazi ya kufanya, na mtu yule akawa na hofu na maadui wa Imani yake au akawa anakawia kawia basi nafasi yake anapewa mtu mwingine…Moja ya sababu kati ya nyingi inayompelekea mtu kupoteza nafasi yake ya utumishi ni HOFU.

Hofu ya kuwaogopa maadui wa Imani yako, hofu ya kuogopa endapo ukihubiri kinyume na mifumo ya adui shetani itakuwaje?..endapo ukiziharibu na kuzidhihirisha kazi za shetani itakuwaje?..Endapo nikizitukana kazi za adui, kama Daudi alivyozitukana itakuwaje?..Nikizidhalilisha kazi za kichawi itakuwaje?..hofu ya kwenda kuhubiri vijijini kuhofia wachawi wa kule, hofu ya kutamke jina la Yesu palipo na nguvu za giza n.k…Hofu ya namna hii ina madhara makubwa sana kiroho..

Katika biblia tunajifunza mtu mmoja aliyeitwa Eliya, ambaye alipewa jukumu la kuisafisha Israeli na kumwondoa mungu baali katikati ya Taifa la Mungu, lakini mwisho wa siku akaingiwa na hofu..na kulikimbia kusudi..

Kama ni mwanafunzi wa biblia, utakuwa unaielewa vyema Habari ya Nabii Eliya jinsi alivyowaua wale makuhani 450 wa Baali na 400 wa Ashera jumla yao 850 (1Wafalme 18:16-40)..Idadi hii ilikuwa ni kubwa sana Eliya aliyoiua ambayo ikasababisha upungufu mkubwa wa makuhani wa Baali katika nchi ya Israeli, hivyo kupelekea kiwango kikubwa cha Uovu kupunguzwa Israeli…Kwani makuhani hao waliajiriwa na mwanamke Yezebeli kutoka huko Lebanoni kuja kuingiza miungu migeni katika Taifa Takatifu la Mungu..

Kwani makuhani hao wa Baali walikuwa wanafanya uchawi na kuipotosha Israeli nzima…Hata wakati wanashindana na Nabii Eliya kushusha moto juu ya ile sadaka, sio kwamba hawakuwa na huo uwezo..huo uwezo wa kutengeneza moto wa kimiujiza ulikuwa ni uchawi mdogo sana kwao, ndio maana walikuwa na ujasiri wa kukubali changamoto ile na Eliya….lakini kwasababu hakuna uchawi wowote ambao unaweza kuwa na nguvu mbele ya Nguvu za Mungu aliye hai, ndio maana ghafla walijikuta wameshindwa kutengeneza moto wao wa kichawi juu ya ile sadaka siku ile…

jambo ambalo hapo kabla halikuwa jambo gumu kwao kulifanya.

Hivyo walikuwa ni wachawi ambao waliajiriwa na mwanamke Yezebeli ambaye ndiye aliyekuwa malkia wa Israeli wakati huo..(2Wafalme 9:22)… Lakini Eliya pamoja na kuipunguza idadi hiyo yote ya wachawi juu ya Israeli, bado hawakuisha wote…wapo wengine ambao walikuwa wapo mbali…na wengine walibaki Samaria …na Zaidi ya yote hata Yezebeli mwenyewe ambaye alikuwa amewaajiri, alikuwa bado yupo hai…

Hivyo Eliya japokuwa alipunguza machukizo juu ya Israeli kwa sehemu kubwa..lakini bado alikuwa hajautoa ule mzizi wote. Na Mungu alimkusudia yeye ndiye autoe mzizi wote na aisafishe Israeli yote lakini kwasababu ya vitisho vya Yezebeli kuutoa uhai wake alimwogopa na kumkimbia kunusuru uhai wake.…Eliya akakimbia mpaka Herobu kwa hofu ya Yezebeli na kumwomba Mungu autoe uhai wake….Hivyo kwa hofu alimwomba Mungu aikatishe hudama yake…Na Mungu aliitoa Huduma hiyo na kuwapa watu wengine watatu waimalizie ambao ni HAZAELI, ELISHA na YEHU.

1Wafalme 19:15 “Bwana akamwambia, Enenda, urudi njia ya jangwa la Dameski; ukifika, mtie mafuta Hazaeli awe mfalme wa Shamu.

16 Na Yehu mwana wa Nimshi mtie mafuta awe mfalme wa Israeli; na Elisha mwana wa Shafati wa AbelMehola mtie mafuta awe nabii mahali pako.

17 Na itakuwa atakayeokoka na upanga wa Hazaeli, Yehu atamwua; na atakayeokoka na upanga wa Yehu, Elisha atamwua”.

Sasa Neno la Mungu ni lazima litimie kwa mkono wa Hazaeli na Elisha na Yehu..kwamba uovu wa baali na makuhani wake na waanzilishi wake waondolewe Israeli kwa mikono ya hawa watatu…Sasa Habari za mambo aliyoyafanya Elisha na Hazaeli zipo katika maandiko…Lakini leo nataka tumtazame huyu mtu wa mwisho anayeitwa YEHU, jinsi gani alilimaliza kusudi la Mungu vizuri.

Yehu, alitiwa Mafuta na Eliya mwenyewe awe mfalme juu ya Israeli…ingawa hakuwa mkamilifu sana, lakini Mungu alimpa ujasiri mkuu kuliko wa Eliya…pale ambapo Eliya alimwogopa Yezebeli na kumkimbia huyu Yehu alimfuata Yezebeli kwenye jumba lake la kifalme na kumtoa kwenye umalkia ili auawe…na sio hilo tu!…bali aliwaua manabii wote wa Baali ambao walikuwa wamesalia kwa siku moja Zaidi hata ya ile idadi ya Eliya aliyoiua kule Karmeli. Na akamtoa mungu anayeitwa baali katika Taifa la Israeli, na baada ya hapo, wana wa Israeli hawakuabudu tena baali..

2Wafalme 10:18 “Yehu akawakusanya watu wote, akawaambia, Ahabu alimtumikia Baali kidogo; bali Yehu atamtumikia sana.

19 Basi niitieni manabii wote wa Baali, wote wamwabuduo, na makuhani wake wote; mtu asikose kuwapo hata mmoja. Maana ninayo dhabihu kubwa ya kumtolea Baali; ye yote atakayekosa kuwapo hataishi. Lakini Yehu alifanya hayo kwa hila, ili awaharibu waliomwabudu Baali.

20 Yehu akasema, Takaseni kusanyiko la dini kwa Baali. Wakalitangaza.

21 Yehu akatuma wajumbe katika Israeli yote, nao wote waliomwabudu Baali wakaja, wala hakusalia mtu ye yote asiyekuja. Wakaingia nyumbani mwa Baali; ikajaa nyumba ya Baali tangu mlango hata mlango.

22 Akamwambia yule aliyekuwa juu ya hazina ya mavazi, Uwatolee mavazi wote wanaomwabudu Baali. Akawatolea mavazi.

23 Akaingia Yehu na Yehonadabu mwana wa Rekabu nyumbani mwa Baali, akawaambia waliomwabudu Baali, Tafuteni mkaangalie, asiwepo hapa pamoja nanyi mtu amtumikiaye Bwana, ila wamwabuduo Baali peke yao.

24 Wakaingia ili watoe dhabihu na sadaka za kuteketezwa. Basi Yehu alikuwa amejiwekea nje watu themanini, akasema, Mtu mmoja akiokoka wa watu niliowatia mikononi mwenu, amwachaye huyo, roho yake itakuwa badala ya roho yake.

25 Ikawa mara alipokwisha kutoa sadaka ya kuteketezwa, Yehu akawaambia walinzi na maakida, Ingieni mwapige; mtu awaye yote asitoke. Basi wakawapiga kwa makali ya upanga; walinzi na maakida wakawatupa nje, wakaenda mpaka mji wa nyumba ya Baali.

26 Wakazitoa nguzo zilizokuwamo nyumbani mwa Baali, wakaziteketeza.

27 Wakaibomoa nguzo ya Baali, na kuiangusha nyumba ya Baali, wakaifanya choo hata leo.

28 NDIVYO YEHU ALIVYOMHARIBU BAALI KATIKA ISRAELI”

Sasa katika Habari hiyo tunajifunza ni kwamba..kama sio Nabii Eliya kumwogopa Yezebeli, Mungu angelimaliza kusudi lote mkononi mwake,…kwasababu huyo Yezebeli ambaye alikuwa anamwogopa Yehu alikuja kumuua kirahisi sana, wala hata hakutumia upanga wala silaha kumuua…aliwaambia tu watu wamkamate wamtupe dirishani..hivyo tu!..(2wafalme 9:30-35).

Na sisi hatupaswi kumwogopa Adui shetani na vitisho vyake, katika kulitimiza kusudi la Mungu..Maadui wa Imani yetu ni wengi, na wana vitisho vikali…lakini hatupaswi kusikiliza vitisho vyao…

Haihitaji mapanga na marungu kumwangusha Yezebeli…ni amri tu! Kama Yehu alivyofanya…Na sisi haihitaji majeshi wala michanganyiko mingi kumwondoa Adui shetani mbele yetu..bali inahitajika amri tu!..Unatamka na Yezebeli anakwenda chini..

Hivyo usiogope mganga mtaani kwako, usiogope wachawi vijijini kwako, usiogope mwanasiasa mbele yako, usiogope chochote kijiitacho kikuu mbele yako ambacho kinakutishia Imani yako au huduma yako..wewe litazame kusudi la Mungu tu kulitimiza na kulimaliza.

Zekaria 4:6 “Akajibu akaniambia, akisema, Hili ndilo neno la Bwana kwa Zerubabeli, kusema, Si kwa uwezo, wala si kwa nguvu, bali ni kwa roho yangu, asema Bwana wa majeshi”..

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

NENO LA MUNGU NI DAWA ILIYO TOFAUTI NA DAWA NYINGINE.

NENO LA MUNGU NI TAA

NITAFUNGUAJE MILANGO ILIYOFUNGWA MBELE YANGU?

MAPAMBANO DHIDI YA SHETANI.

NAO WAKADHANI YA KUWA YUMO KATIKA MSAFARA;

UCHAWI WA BALAAMU.

KIFO CHA MTAKATIFU PERPETUA NA FELISTA.

Rudi Nyumbani:

Print this post