Category Archive Uncategorized @sw-tz

Kuota upo na mtu maarufu/kuota unaongea na mtu maarufu.

Kuota upo mtu na maarufu/kuota unaongea na mtu maarufu kuna maana gani?

Ndoto zipo katika makundi makuu matatu, zipo ndoto zinazotokana na Mungu, pia zipo ndoto zinazotokana na shetani, halikadhalika zipo ndoto zinazotokana na mtu mwenyewe.

Ili kufahamu vizuri juu ya makundi haya. Bofya hapa usome. >>> Nitajuaje kama ndoto ni ya Mungu au ya Shetani?

Wengi wetu tunakosa shabaha pale tunapotaka kila ndoto ipatiwe tayari yake ya rohoni, lakini ukweli ni kwamba si kila ndoto inayotafsiri ya maana, husususani hizo zinazotokana na sisi wenyewe.

Sasa tukirudi kwenye swali Kuota upo na mtu maarufu/kuota unaongea na mtu maarufu kuna maana gani?

Jibu ni kwamba, ndoto nyingi za namna hii zinatokana na shughuli zetu za kila siku

Mhubiri 5:3 “Kwa maana ndoto huja kwa sababu ya shughuli nyingi; na sauti ya mpumbavu kwa njia ya wingi wa maneno”

Unaona Shughuli za kila siku ni Pamoja na yale mambo ambayo tunayoana mara kwa mara kila siku, au tunayasikia, kwamfano mtu kama raisi wa nchi, huyu ni mtu ambaye karibu kila siku tunamwona katika vyombo vya Habari, au tunamsikia katika radio, au tunamsoma katika magazeti, au tunamsikia akizungumziwa na watu wengine..

Ni mtu ambaye kila mmoja wetu amemkaa kichwani, kama vile tu ndugu zetu wa nyumbani. Hivyo mtu kuota raisi wa nchi, au kuota unaongea na raisi,au kuota uko na raisi si jambo la kushangaza.

Naamini ni maelfu ya watu kila siku yanamuota raisi wa nchi yao.

Na sio raisi tu, unaweza kumwota mtu mwingine yoyote maarufu, ambaye tayari anajulikana sana katika jamii, inaweza ikawa ni msanii, au mbunge, au mchungaji, au mchezaji n.k.

Hivyo ndoto ya namna hii, ikikujia usiitilie maanani sana.

Lakini ikija katika uzito wa hali ya juu, na ndoto yenyewe umeiota imeonekana kama ilikuwa ni kweli. Na ukaona kama ni bahati umekutana na mtu huyo,

Basi ujue ni Mungu anataka kukupa hisia  Fulani ya kipekee uionje pale unapokutana na mtu Fulani maarufu. Anataka uone, jinsi inavyokuwa,  ikiwa watu maarufu wa dunia hii ukikutana nao unajihisi wewe ni mtu Fulani spesheli uliyepata bahati, vipi kuhusu kukutana na yeye ambaye ni Maarufu na Mkuu kuliko watu wote na vitu vyote duniani siku ile? Utakuwa katika hali gani?

Anataka uone siku ile maelfu kwa maelfu wa watu watakapo kusanyika mbele zake , kupokea heshima zao kutoka kwake wewe utakuwa wapi?

Je! atakuita, uwe karibu naye, au atakukataa na kukufukuza?

Bwana Yesu mwenyewe alisema..

Luka 9:26  “Kwa sababu kila atakayenionea haya mimi na maneno yangu, Mwana wa Adamu atamwonea haya mtu huyo, atakapokuja katika utukufu wake na wa Baba na wa malaika watakatifu”.

Hivyo usimwonee haya Kristo mpe leo Maisha yako. Ili siku ile, atakapopokea heshima kutoka kwa watu wote na malaika zake, basi na wewe pia akuite.

Hiyo ndio maana ya Kuota upo na mtu maarufu/kuota unaongea na mtu maarufu.

Hivyo Kama upo tayari kumpa Yesu Maisha yako leo, utataka kuongozwa sala ya toba basi fungua hapa >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Ubarikiwe sana..

Group la whatsapp Kwa mgawanyo bora wa masomo download App hapa>> App wingu la mashahidi

Mada Nyinginezo:

KARAMU YA MWANA-KONDOO.

BASI MUNGU ALIMWADHIMISHA MNO.

MFALME ANAKUJA.

KWANINI YESU KRISTO NI WA MUHIMU KWETU SASA?

MTINI, WENYE MAJANI.

Uasherati wa Kiroho maana yake nini?

Rudi Nyumbani:

Print this post

KUOTA UNAKOJOA KITANDANI.

Kuota unakojoa kitandani kuna maanisha nini?


Ndio ni kweli zipo ndoto zinazotokana na Mungu, na ni vizuri kuzifahamu hizo, na pia zipo ndoto zinazotokana na shetani pia hizo ni vizuri ukazifahamu.. Kama utahitaji kuzijua kwa undani bofya hapa >> Nitajuaje kama ndoto ni ya Mungu au ya Shetani?

Lakini kuna ndoto pia ambazo hazitokani na Mungu wala shetani bali zinatokana na sisi wenyewe.. Na hizo ndizo tunazoziota katika Maisha yetu kwa sehemu kubwa, naweza kusema hata Zaidi ya asilimia 90.

Tatizo linakuja ni pale watu  wanapotaka ndoto zinazotokana na sisi  wenyewe basi wapate tafsiri yake ya kiroho. Hilo ndio linalowafanya wengi waangukie katika tafsiri za uongo.

Lakini leo ni vizuri ukaujua ukweli juu ya ndoto za kuota unakojoa kitandani.

Biblia inasema.

Isaya 29:8 “Tena itakuwa kama mtu mwenye njaa aotapo, kumbe, anakula; lakini aamkapo, nafsi yake haina kitu; na kama mtu mwenye kiu aotapo, kumbe, anakunywa; lakini aamkapo, kumbe, anazimia, na nafsi yake inatamani; hivyo ndivyo utakavyokuwa huo wingi wa mataifa waletao vita juu ya mlima Sayuni”.

Umeuelewa mstari huo?

Ndoto kama hizi za ukota unakojoa kitandani ni ndoto zinazotokana na mwili wenyewe. Na hiyo inakuja pale kibofu chako kinapojaa sana mkojo, Na hapo ndipo ubongo wako unatengeneza matukio ambayo yatakufanya ujione kama unajiokojolea ili tu aumke, uende ukakoje.. Na kama mwili utakuwa umezidiwa sana, na ndio hapo unakuta mtu anajikojolea kweli, aidha sana au kidogo.

Mwingine utakuta anaota anakojoa mkojo ambao hauishi, au kila saa anakojoa kojoa, unaona yote hiyo mifumo tu ya mwili.

Kama vile unapolala na njaa, usiku utajiona unatafuta chakula, au unakula haushibi, huo ni mfumo wa ubongo, kukuarifu kuwa mwili unahitaji chakula.  Vivyo hivyo unapojikuta katika ndoto ya kuota unakojoa kitandani, hupaswi kuwa na hofu au wasiwasi.

Ipuuzie tu, na kama inakuja mara kwa mara, hakikisha ulalapo hunywi maji mengi, au vitu vyenye maji maji, na kwa kufanya hivyo hutakaa uone  tena ikikurudia.

Hivyo kuota unakojoa kitandani ni ndoto ya ubongo wetu wenyewe. Ipuuzie

Shalom.

Group la whatsapp  Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

HAPO NDIPO WATU WALIPOANZA KULIITIA JINA LA BWANA.

KIFO CHA REINHARD BONKEY KINAACHA UJUMBE GANI KWETU?

JISHUSHE ILI MUNGU AKUHUDUMIE.

WACHUNGAJI WA BWANA MAKONDENI.

KILA MMOJA WENU AJUE KUUWEZA MWILI WAKE.

Kwanini Mungu anasema “Afanyaye malaika zake kuwa pepo”?

ZIKIMBIE TAMAA ZA UJANANI! NA MTU YEYOTE ASIUDHARAU UJANA WAKO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

KUOTA UMEFUNGA NDOA.

Kuota umefunga ndoa  kuna maanisha nini?


Ndoto ya namna hii mara nyingi inaangukia katika kundi la ndoto zinazozotokana na shughuli nyingi..

Mhubiri 5:3 “Kwa maana ndoto huja kwa sababu ya shughuli nyingi; na sauti ya mpumbavu kwa njia ya wingi wa maneno”.

Na hii inatokana na kwamba pengine umekuwa ukiwaza kuoa au kuolewa hivi karibuni, au umekuwa ukitamani sana  kuoa au kuolewa kwa muda mrefu lakini bado malengo yako ya ndoa hujayafikia, au umehudhuria ndoa nyingi, au umezitazama, n.k. 

 Hivyo siku zote zile unachokifanya sana, au unachokiwaza sana, ni lazima kitajirudia tu katika ndoto zako, kama sio mara moja basi ni mara kwa mara, hilo ni jambo la kawaida.

Kwa mfano utakuta mwingine amekuwa akitafuta sana ajira kwa muda mrefu, au amekuwa akiwaza sana  ajira kwa muda mwingi, hivyo mtu kama huyu kuota yupo kwenye interview litakuwa ni jambo la kawaida kwake..

Na ndivyo vivyo hivyo katika kuota umefunga ndoa..mara nyingi ni ndoto itokanayo na shughuli za kila siku.


Lakini pia lipo jambo lingine la rohoni unapaswa ujue. Kumbuka kuwa Mungu huwa anazungumza pia na watu  katika ndoto kwa kupitia Maisha ya kawaida kabisa ya siku zote. Hivyo Ikiwa ndoto hii ya kuota umefunga ndoa imekujia kwa uzito wa kitofauti..

Na ukaifarahia hiyo ndoa na ukatamani ingekuwa hivyo kweli, Fahamu kuwa Mungu anakuonyesha kuwa ipo HARUSI ILIYO BORA NA KUU kuliko hiyo, inayokuja huko mbele. Na hiyo si nyingine Zaidi ya mwanakondoo (Yesu Kristo na kanisa lake)

Hilo usilisahau hata kidogo, katika Maisha yako. Kwasababu biblia inatuambia itakuwa ni Harusi ya pekee sana, ambayo karamu yake itafanyika mbinguni. Wakati huo wapo watu watatamani kuingia lakini waseweze, kitakachobakia kwao ni kilio na kusaga, kwa kuikosa tu.

Harusi hiyo ya Bwana Yesu na kanisa lake sio kama hii ya kimwilini, hapana, bali itakuwa ni ya rohoni, ambapo ndoa inaanzia hapa hapa duniani, na karamu itakuwa ni mbinguni.

Huko ndipo tutakapokutana na mambo ambayo jicho halijawahi kuona wala sikio kusikia..ili kufahamu vizuri jinsi karamu hiyo itakavyokuwa..Fungua hapa >>>>> KARAMU YA MWANAKONDOO

Fahmu kuwa Hizi ni nyakati za mwisho, Unyakuo upo karibu, Yesu yupo mlangoni kurudi, kulinyakua kanisa lake Je! Umeokoka? Umemkabidhi Maisha yako? Kama bado ni vizuri ukafanya uamuzi huo sasa, kukutana na ujumbe huu sio bure.Bali Mungu anayo malengo makubwa na wewe maishani mwako… Fanya hima nawe pia usionekane umeikosa siku ile ya Harusi kuu ya mwana-kondoo.

Ufunuo 19:7 “Na tufurahi, tukashangilie, tukampe utukufu wake; kwa kuwa arusi ya Mwana-Kondoo imekuja, na mkewe amejiweka tayari.

8 Naye amepewa kuvikwa kitani nzuri, ing’arayo, safi; kwa maana kitani nzuri hiyo ni matendo ya haki ya watakatifu.

9 Naye akaniambia, Andika, Heri walioalikwa karamu ya arusi ya Mwana-Kondoo. Akaniambia, Maneno haya ni maneno ya kweli ya Mungu”

Shalom.

Group la whatsapp Kwa mgawanyo bora wa masomo download App hapa>> App wingu la mashahidi

Mada Nyinginezo:

KUOTA UPO UCHI.

KUOTA UNAPAA.

KUOTA UNAOLEWA/UNAOA.

KUOTA UNATOKA DAMU YA HEDHI.

KUOTA UNAOLEWA/UNAOA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

MAOMBI NI NINI

Maombi ni nini?


Neno maombi limetokana na neno kuomba, Kwamfano mtu unapokuwa na hitaji ya kitu Fulani, labda tuseme kazi, basi huwa unatuma maombi yako kwanza kwenye ofisi husika au shirika, kisha wanapitia  wasifu wako na kule wakisharidhiwa na maombi yako ndio wanakurudishia  majibu ya kile ulichokiomba.

Kamwe huwezi ukapeleka maombi ya kazi,  halafu yakarudi majibu ya mkopo, ya ufadhili, au ya kupewa bima badala yake..Hilo jambo halipo, kwa namna ya kawaida chochote kile unachokiomba ndicho utakachopewa, ukiomba ajira utarudishiwa majibu ya ajira, ukiomba mkopo utarudishiwa majibu ya mkopo, ukomba zabuni utarudishwa majibu ya zabuni, kamwe haiwezi ikavuka hapo.

Maombi ni nini katika ukristo?

Lakini katika Ukristo Maombi, yanavuka hiyo mipaka, hayalengi tu kupeleka hitaji na kujibiwa, halafu basi.. Bali yanakwenda mbele Zaidi na kufanya kazi nyingine nyingi kuliko hizo, na ndio maana maombi ni nyenzo muhimu sana kwa mtu yeyote anayejiita mkristo. Bila maombi umekwisha.

Watu wengi wanadhani, Mungu anakitazama tu kile  tunachokwenda kumwomba kwa wakati huo halafu atujibu iwe imeisha..ni vizuri tukafahamu kuwa kabla hata hatujamwomba Mungu chochote, tayari alishajua ni nini tunachokwenda kumwomba..

Mathayo 6:7  “Nanyi mkiwa katika kusali, msipayuke-payuke, kama watu wa mataifa; maana wao hudhani ya kuwa watasikiwa kwa sababu ya maneno yao kuwa mengi. 8  Basi msifanane na hao; maana Baba yenu anajua mnayohitaji kabla ninyi hamjamwomba”.

Hivyo mbele za Mungu, maombi ni ziadi ya kile tunachokifikiria. Ikiwa anajua tayari tunachokwenda kumwomba, unaweza ukajiuliza ni kwanini sasa atusumbue tuende tukamwombe?..Hapo ndipo utakapojua kuwa maombi kwa Mungu ni Zaidi ya kupeleka mahitaji.

Maombi ni nini..

Pale unapopiga magoti na kumwambia Mungu hiki na kile, hafamfikii tu kama mahitaji peke yake, bali yanajitafsiri kama kitu kingine pia..yanafika kwake kama harusi nzuri ya manukato, kama sauti ya upole ya kumwita aje ndani yako, kuku rehema, kukupa  neema zake, kukuponya n.k. Na hiyo inamfanya Mungu ashuke, na kuanza kuifanya kazi yake ndani ya maisha yako, ambayo hata wewe usiyoyajua..zaidi ya yale aliyokuwa anayaomba.

Na kwa jinsi unavyodumu zaidi katika maombi, ndivyo Mungu anavyotenda kazi zaidi ndani yako.

Mtu ambaye ni mwombaji mzuri, kamwe hawezi kushindwa na majaribu ya shetani, Bwana Yesu alishasema hivyo. Mtu ambaye ni mwombaji mzuri, huwa  nyingi maishani mwake zza mambo ya ajabu ambayo Mungu amemtendea..Vilevile mtu ambaye ni mwombaji mzuri huwa unakutana na Mungu sana katika njia zake.

Tofauti na Yule ambaye haombi kabisa.. Huyo ni sawa na gari linalotembelewa miaka 20 halipelekwi gereji.

Biblia inasema..

1Wathesalonike 5:16  “Furahini siku zote; 17  ombeni bila kukoma;”

Maombi  ni nini? Maombi ni kama karakana ya Mungu ndani ya moyo wa mwanadamu, pale tunapokwenda kuomba, anashuka kuyakarabati Maisha yetu..Hivyo suala la maombi ni jambo linalotakiwa liwe sehemu ya Maisha yetu na sio pale tu tunapojisikia.

Bwana wetu Yesu japo alikuwa ni Mungu katika mwili mkamilifu lakini alikuwa ni mwombaji mkubwa sana..

Luka 6:12  “Ikawa siku zile aliondoka akaenda mlimani ili kuomba, akakesha usiku kucha katika kumwomba Mungu. 13  Hata kulipokuwa mchana aliwaita wanafunzi wake; akachagua kumi na wawili miongoni mwao, ambao aliwaita Mitume”;

Na ndio huyo huyo alituambia..

Marko 14:38  “Kesheni mwombe, msije mkaingia majaribuni, roho i radhi ila mwili ni dhaifu”

Hivyo kama wewe umeokoka na sio mwombaji ni vizuri ukaanza sasa. Na Bwana alitupa kiwango cha kuomba cha siku ambacho walau kila mwaminio anapaswa akifanye..Nacho ni SAA MOJA kwa siku. Luka 14:37..Unaweza ukaona ni kirefu lakini ukijua kuwa yapo mambo mengi ya kuombea hutaona ni kirefu.

Maombi ni nini

Lakini ikiwa bado upo nje ya Kristo, Mungu hawezi kuyaumba Maisha yako vile anavyotaka, Lakini kama leo upo tayari kumkaribisha katika Maisha yako, basi uamuzi unaoufanya ni sahihi..

Bofya hapa kwa ajili ya sala ya toba..>> SALA YA TOBA

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

FAIDA ZA MAOMBI YA USIKU

MAOMBI YA VITA

ZIFAHAMU HOJA SABA ZENYE NGUVU MBELE ZA MUNGU.

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

UTAWALA WA MIAKA 1000.

NYAKATI SABA ZA KANISA NA WAJUMBE WAKE.

UTOE MWILI WAKO KWA BWANA KWASABABU SI MALI YAKO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

KUONGOZWA SALA YA TOBA

Kuongozwa sala ya toba.


Ikiwa leo upo tayari kufanya uamuzi wa kumgeukia Yesu Kristo, na kutaka akuokoe na kukusamehe dhambi zako kabisa, Basi ni uamuzi wa busara sana ambao, utaufurahia maisha yako yote, kama ilivyokuwa hata kwetu sisi. Kumbuka..

  • Kwa Yesu lipo tumaini la uzima wa milele.
  • Kwa Yesu Unapata utulivu wa nafasi na faraja. Alisema.

Mathayo 11:28 “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.

29 Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu;

30 kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi”.

  • Kwa Yesu zipo Baraka.
  • Na kwa Yesu upo msahama wa kweli:

Isaya 1:18 “Haya, njoni, tusemezane, asema Bwana. Dhambi zenu zijapokuwa nyekundu sana, zitakuwa nyeupe kama theluji; zijapokuwa nyekundu kama bendera, zitakuwa kama sufu”.

Kwa hiyo unapokuja kwake leo hii kwa kumaanisha, ujue kuwa hiyo mizigo ya dhambi uliyonayo haijalishi ni mingi kiasi gani ataitua mara moja, haijalishi uliuwa watu wengi namna gani, haijalishi ulizini nje ya ndoa mara nyingi kiasi gani, haijalishi ulikwenda kwa waganga mara nyingi namna gani..Ikiwa tu upo tayari leo kumkaribisha Yesu moyoni mwako basi ataitua, na kukusamehe kabisa kana kwamba hakuna chochote ulichowahi kumkosea..Na atakupa amani.

Hivyo kama leo ni siku yako ya kuyasalimisha maisha yako kwake, jambo la kwanza unalopaswa kufahamu ni kwamba, unapaswa umaanishe kutoka katika moyo wako, kuwa kuanzia sasa, wewe na dhambi basi, wewe na ulimwengu basi kabisa..

Hivyo kama umeshakuwa tayari kufanya hivyo basi..

Basi, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU  MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.

AMEN.

Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuwa na uhalali kwa kuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako.

Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.

Hongera kwa kuokoka.

Hivyo ikiwa utahitaji msaada zaidi basi, wasiliana nasi kwa namna hizi hapa chini..+255 789001312

Pia unaweza ukatutumia ujumbe tukuunge kwenye magroup yetu ya Whatsapp ya kujifunza Neno la Mungu.

Vile vile tunakualika kutembelea website hii, yenye mafundisho ya Neno la Mungu zaidi ya 1000, na maswali na majibu mengi sana yaliyojibiwa. Tazama chini, usome baada ya hayo.

Na Bwana akubariki sana.

Group la whatsapp jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Mada Nyinginezo:

MWAKA WA BWANA ULIOKUBALIWA.

RABI, UNAKAA WAPI?

TAZAMA, MWISRAELI KWELI KWELI, HAMNA HILA NDANI YAKE!

TOBA IGUSAYO MOYO WA BWANA.

KWANINI AWE NI PUNDA NA MWANA-PUNDA?

UNYAKUO.

UPENDO NI NINI NA JE! KUNA AINA NGAPI ZA UPENDO?

Rudi Nyumbani:

Print this post

IJUE NGUVU YA IMANI.

ijue Nguvu ya Imani ipo wapi?


Imani ni ufunguo wa mambo yote.. Ukiwa na Imani timilifu Bwana Yesu alisema unaweza ukauambia hata Mlima Kilimanjaro uondoke pale, na ukajitupe Baharini, na ukakutii..

Watu wanadhani maneno hayo alimaanisha  milima ya rohoni, kwamba unaweza ukayaambia matatizo ondoka hapa uende kule, hapana, bali  maneno yale ni ya mwilini kabisa.. Jambo ambalo wengi hatukubali kukiri ni kuwa hatuna Imani timilifu ya kufanya hivyo (Nami pia sina).

Joshua aliweza kusimamisha Jua, ambalo ni kubwa Zaidi ya dunia, kwanini leo hii isiwezekane, kuamini kuwa mlima ambao ni sehemu ndogo sana ya dunia unaweza kuhamishwa.

Hivyo hakuna jambo lolote linaloshindikana ukiwa na Imani timilifu. Bwana Yesu alisema hivyo katika Marko 9:23.

Lakini kutoweza kuhamisha milima haimaanishi kuwa huna Imani kabisa, hapana, Imani zinatofautiana viwango..Ili kufahamu vizuri juu ya hilo fungua hapa >>> IMANI MAMA NI IPI?

Embu ngoja nikupe mfano wangu mdogo sana..naamini utakuongezea kitu..

Kuna wakati nilikuwa nimepanga jumba sehemu fulani, sasa ilikuwa kila mwisho wa mwezi, tunalipia bili ya maji sh. 7000, na  bili ya umeme sh.15,000. Na sehemu hiyo hao wanaokuja kuchukua bili hizo walikuwa ni wakali kweli, haziwezi pita siku mbili bila kuja kukugongea hodi..

ujue nguvu ya Imani..

Ilikuwa ni mwezi wa pili, wakati huo hali kwangu haikuwa nzuri sana, lakini nilimwambia Mungu nitakuamini wewe, na ni wewe ndiye utakayenipa hifadhi mimi na ndugu yangu..Hivyo ulipofika mwisho wa mwezi tulishangaa, wale hawakuja kutugongea wakati ilikuwa ni desturi yao, mpaka ukaanza mwezi mwingine wa tatu, lakini hatukuwaona..zikawa zinapita tu tarehe, bado tunashangaa hatuwaoni, wapangaji wengine walienda kulipia lakini sisi hatujafuatwa..Ikaendelea hivyo hivyo, hapo mfukoni hatuna kitu, mpaka ikafika tarehe 25,..kipindi hicho na gesi nayo ikaisha ndani, tukawa kama vile hatuna kitu na mwezi mwingine unakwenda kuishia bado tunayo madeni ya nyuma na hatuna pesa ya matumizi..

Lakini siku hiyo tulikuwa tumekaa, tukajikuta tunaangalia tu M-pesa, cha ajabu tukashangaa kule kulikuwa ni sh.50,000 na hiyo namba hatujawahi kuitumia kwa miamala yoyote ya kifedha, tukaenda kutoa ili tukanunue gesi sh. 20,000, lakini tulipomaliza tu kutoa , mara wale watu wa umeme, wanakuja kutugongea mlango, na kutuambia tuwalipe pesa ya umeme wa mwezi uliopita.. Ndipo tukatoa ile hela tukawapa saa ile ile, tukafiria kwamba kama  tusingewapa siku ile sijui hali ingekuwaje!.

Lakini tulimwamini Mungu, tukajua kweli nguvu ya Imani ni kubwa. Yapo na mambo mengine mengi Mungu aliyonitendea kwa kumwamini tu..

ijue Nguvu ya Imani.

Hiyo yote ni kutaka kukupa moyo na wewe, ukimwamini Mungu, basi anaweza kukufanyia mambo makubwa katika Maisha yako.

Mifano mingi sana ipo katika biblia, ambayo ukiisoma itaikuza Imani yako sana.. Na ndio maana tunaambiwa..

Warumi 10:17  “Basi imani, chanzo chake ni kusikia; na kusikia huja kwa neno la Kristo”.

Hivyo unapoitafakari mifano mingi ya Imani katika Biblia ndivyo unavyoikuza Imani yako. Na ndio mpaka huko huko unajikuta unafanya mambo makubwa ya ki-imani yasiyoelezeka kibinadamu.

Lakini yote hayo ni mpaka uwe katika wokovu?

Je! Umeokoka?

Je! Unajua kuwa tunaishi katika siku za mwisho, na Yesu yupo karibuni kurudi? Na kwamba kanisa hili ndio kanisa la mwisho lijulikanalo kama Laodikia na kwamba hakutakuwa na kanisa lingine Zaidi ya hili? Unasubiri nini usimkaribishe Yesu maishani mwako akuokoe?

Fanya maamuzi upesi, kabla ya mlango wa neema haujafungwa.

Bwana akubariki.

ijue Nguvu ya imani ni kuu.

Mada Nyinginezo:

KIWANGO CHA TATU CHA IMANI.

ZIKIMBIE TAMAA ZA UJANANI! NA MTU YEYOTE ASIUDHARAU UJANA WAKO.

IMANI NI KAMA MOTO.

NGUVU YA SADAKA.

UNYAKUO.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

NYAKATI SABA ZA KANISA NA WAJUMBE WAKE.

Rudi Nyumbani:

Print this post

JINSI YA KUSOMA BIBLIA.

Fahamu jinsi ya kusoma biblia.


Awali ya yote ninakupongeza kwa nia yako kutamani kujua jinsi ya kusoma biblia. Hapo mwanzoni kabla sijamjua vizuri Mungu, kati ya  vitabu ambavyo nilikuwa ninaona ni vigumu kuvielewa, basi kimojawapo kilikuwa ni BIBLIA.

Lakini siku, na miaka ilivyozidi kwenda niligundua kuwa sio, nataka nikuambie hakuna kitabu kilicho kirahisi kama Biblia. Kwanini ninakuambia hivyo?.. Kwasababu ni kitabu kinachoweza kusomwa na watu wa makundi yote.  Mzee anaweza kukisoma, kijana anaweza kukisoma, asiye na elimu anaweza kukisoma mwenye PH.D anaweza kukisoma..Na wote wakafaidika na kilichoandikwa mule. Vilevile hakina ngazi yoyote ya awali kukipitia ndio uelewe kama vilivyo vitabu vingine. Leo hii ukihitaji kusoma kitabu cha Fizikia, itakugharimu kwanza upitie elimu za chini uwe na msingi, vinginevyo hutaweza kukielewa..Lakini biblia haina misingi hiyo.

Tena na cha kushangaza Zaidi ni kwamba, biblia imetoa nafasi ya kueleweka na watu wasio na elimu kuliko wenye hekima na ujuzi..(Luka 10:21)

Jinsi ya kusoma biblia.

Mambo ya kuzingatia kabla hujaanza kusoma biblia.

  • Kwanza: Omba Kabla hujaanza kusoma Habari yoyote, hata kama unaifahamu, mshirikishe kwanza Roho Mtakatifu, na mwombe msaada akusaidie kuyaelewa maandiko. Siri moja ya maandiko ni kuwa Habari ile ile inaweza ikawa na mafunuo mengi sana..Hivyo usipokuwa mnyenyekevu na kujiona kwamba Habari Fulani unaijua, nakuambia utabakia kuwa hivyo hivyo. Lakini ukimwomba kwanza Roho Mtakatifu akufunulie, maandiko basi utashangaa mambo mengi sana ambayo hukuwahi hata kuyafikiria.
  • Pili: Hakikisha upo katika utulivu wa kutosha. Mahali palipo na machafuko siku zote hata akili haiwezi kukaa katika utulivu wa kuzingatia kile kinachosomwa, na hivyo Roho Mtakatifu anakosa wigo wa kukufunulia, yale anayotaka kukufunulia. Hivyo kama upo kwenye makelele basi, subiri uwe katika utulivu, tenga muda wako, hususani usiku ni muda mzuri Zaidi.
  • Tatu: Tafakari Neno, Kumbuka Neno la Mungu halisomwi kama gazeti tu, Chukua muda mrefu kuyatafari maandiko Zaidi ya kuyasoma, ikiwa na maana mtu yule anayeitafakari sura moja vizuri, ni Zaidi na mtu yule atakayesoma kitabu kizima bila kutafakari chochote kilichoandikwa. Roho Mtakatifu anazungumza kwa kasi sana, pale mtu anapojibiisha kuitafakari Habari husika.
  • Nne: Endelea kutumia muda mwingi, katika kutafakari hilo Neno, kwa jinsi unavyokaa sana katika uwepo huo ndivyo unavyompa Roho Mtakatifu wigo wa kukufunulia maandiko katika uelewa mzuri zaidi. Mpaka dakika ya mwisho unamaliza, unatoka kitu ambacho hapo kabla hukuwahi kukijua, tena moyo wako ukiwa na amani ya kutosha.
  • Tano: Kuwa na daftari na kalamu. Hiyo itakusaidia kuandika kile Mungu anachokufundisha, kwa kumbukumbu la baada usije ukasahau, Kumbuka mwanafunzi mzuri ni yule anaandika chini kile mwalimu wake anachomfundisha, kila anapomfundisha. Hivyo na wewe hakikisha unakuwa na daftari lako.

Hivyo ukizingatia hizo hatua, utakuwa umeshajua jinsi ya kusoma biblia. Pia kumbuka, kwenye suala la kitabu kipi uanzane nacho, au kipi usianzane nacho, hilo halina umuhimu sana, unaweza kuanza na kitabu chochote kile na  huko huko Roho Mtakatifu mwenyewe atakufunulia mambo ya ajabu, Na kukufikisha pale anapotaka ufike kwa siku hiyo, kwasababu hiyo ndio kazi yake aliikusudia juu yetu.

Yohana 16:13  “Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho wa kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayanena, na mambo yajayo atawapasha habari yake”.

Jinsi ya kusoma biblia.

Pia Kujifunza biblia ni Pamoja na kusikiliza na mafundisho mengine ya Neno la Mungu yanayohubiriwa.. Yale yanakuwa kama TUTION kwako. Hivyo hapa pia yapo mafundisho mengi ya kukusaidia kuielewa biblia, kwenye website hii yapo mafundisho Zaidi ya 1000 ya mada mbalimbali, na Maswali na Majibu mengi sana, ambayo ukiyasoma naamini utapiga hatua kubwa sana katika kuielewa biblia..Hivyo kama upo tayari bofya hapa uende moja kwa moja katika orodha hiyo….>> MAFUNDISHO

                                                                                >> MASWALI NA MAJIBU

Bwana akubariki sana.

Jinsi ya kusoma biblia.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au tutumie ujumbe kwa namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Mihimili mikuu (4) ya mkristo katika safari yake ya wokovu.

USIPOLITENDEA KAZI NENO LA MUNGU.

JINSI ROHO MTAKATIFU ANAVYOWAFUNULIA WATU MAANDIKO.

TABIA YA KIPEKEE USIYOIJUA KUHUSU NENO LA MUNGU.

NENO LA MUNGU NI DAWA ILIYO TOFAUTI NA DAWA NYINGINE.

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

KABLA YA MAANGAMIZI, KRISTO HUWA ANAONYESHA KWANZA NJIA YA KUTOROKEA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

MHUBIRI.

Kitabu cha mhubiri kiliandikwa na mfalme Sulemani.

Kitabu hichi kinaeleza, jumla ya mambo yote, na mwisho kinatoa ushauri ni nini mwanadamu anapaswa achague.

Ikiwa wewe ni mmojawapo wa  wanaojiuliza nini maana ya maisha, ni nini ufanye ili upate mwisho mwema mwenye mafanikio, basi nakushauri ukipitie kitabu hichi cha mhubiri kwa utulivu, Kwasababu Mungu alikiandika mahususi kwa ajili ya watu wenye maswali kama ya kwako.

Kwa ufupi (Mhubiri)Sulemani anajaribu kueleza jinsi alivyoanza safari yake yake ya kutafuta kitu kitakachompa raha maishani, kitu kitakachotatua matatizo yake moja kwa moja, Hivyo akaanza kujaribu kufanya kwa bidii jambo moja hadi  lingine ili aone kama linaweza kumletea jawabu la maisha yake.,

  • Alijaribu kufanya biashara nyingi sana kuliko watu wote waliomtangulia duniani lakini hakupata kile alichokuwa anakitafuta..
  • Alijaribu starehe na anasa zote unaozijua wewe, lakini katika hivyo vyote bado hakupata jumla ya maisha.(Mhubiri 2:1)
  • Akajaribu kwa kujijengea makasri ya kifahari lakini bado hakuipata hiyo jumla ya maisha (Mhubiri 2:4)
  • Alijiongezea elimu kuliko watu wote ulimwenguni, alikuwa na elimu juu ya miti yote, na karibu viumbe vyote duniani lakini katika elimu yake, na hekima yake bado hakupata jumla ya mambo yote.(Mhubiri 1:13)

Mpaka mwisho wa siku akakata tamaa, akaona kila kitu ni sawa na ubatili tu, na kujilisha (kufuata) Upepo. Japokuwa alijusumbua kupata kila kitu roho yake inapenda,  lakini bado kile alichokuwa anakitazamia hakukipata.

Na ndipo mwisho wa siku  akagundua jumla ya mambo yote ambayo  mwanadamu anapaswa kuyafanya chini ya jua nayo si nyingine zaidi ya KUMCHA BWANA, NA KUZISHIKA AMRI ZAKE.

Hivyo mimi na wewe hatupaswi, kuanza tena, kufanya utafiti, wa kitu kitakachotupa jawabu la maisha duniani,..Sulemani alishatusaidia, ukisema leo hii wewe mwenyewe ngoja uanze, kwa akili zako na nguvu zako, kutafuta maana ya maisha, nakawambia utazunguka kote na utarudi pale pale Sulemani alipoishia. Na wakati huo utakuwa umeshachelewa.

Unasema, ngoja nitafute elimu sana, hiyo ndio itanipa raha, Mungu hawezi kunipa raha,..Ni kweli utaisumbukia na kuipata, na kufanikiwa lakini mwisho wa siku utakuja kugundua mbona bado kuna shimo ndani yako? Ile raha ambayo uliitazamia mbona hujaipata?

Unasema, ngoja nitafute mali, nijiwekee miradi, mingi, kwasababu hiyo itanipa raha.. Nataka nikuambie yupo aliyefanya kazi kubwa zaidi yako aliyeitwa Mhubiri Sulemani, lakini hilo mwisho wa siku halikumpa jawabu alilokuwa analitarajia.

Vivyo hivyo na wewe kama unataraji utapata raha, sehemu yoyote, aidha kwa waganga, au kwa wanadamu, na huku umemwacha Mungu nyuma, ukweli ni kwamba mwisho wa siku utakuja kugundua uliacha kitu cha thamani sana nyuma yako.

Sasa mwishoni kabisa mwa kitabu hicho cha mhubiri, maneno hayo ya Mhubiri Sulemani ndio tunayapata,

Anasema..

Mhubiri 12:13 “Hii ndiyo jumla ya maneno; yote yamekwisha sikiwa; MCHE MUNGU, NAWE UZISHIKE AMRI ZAKE, Maana kwa jumla ndiyo impasayo mtu.

14 Kwa maana Mungu ataleta hukumuni kila kazi, pamoja na kila neno la siri, likiwa jema au likiwa baya”.

Unaona, anasema, mche Bwana, uzishike amri zake. Hivyo ikiwa bado angali unao muda ndugu yangu, mimi na wewe tumtafute Mungu, kwasababu huyo ndio atakayetupa furaha yote ya maisha yetu..

Na ndio maana mhubiri juu kidogo  alisema..

Mhubiri 12:1 “Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako, Kabla hazijaja siku zilizo mbaya, Wala haijakaribia miaka utakaposema, Mimi sina furaha katika hiyo 2 Kabla jua, na nuru, na mwezi, Na nyota, havijatiwa giza; Kabla ya kurudi mawingu baada ya mvua;

3 Siku ile walinzi wa nyumba watakapotetema; Hapo wenye nguvu watakapojiinamisha; Na wasagao kukoma kwa kuwa ni haba; Na hao wachunguliao madirishani kutiwa giza;

4 Na milango kufungwa katika njia kuu; Sauti ya kinu itakapokuwa ni ndogo; Na mtu kusituka kwa sauti ya ndege; Nao binti za kuimba watapunguzwa;

5 Naam, wataogopa kilichoinuka Na vitisho vitakuwapo njiani; Na mlozi utachanua maua; Na panzi atakuwa ni mzigo mzito; Na pilipili hoho itapasuka; Maana mtu aiendea nyumba yake ya milele, Nao waombolezao wazunguka njiani.

6 Kabla haijakatika kamba ya fedha; Au kuvunjwa bakuli la dhahabu; Au mtungi kuvunjika kisimani; Au gurudumu kuvunjika birikani;

7 Nayo mavumbi kuirudia nchi kama yalivyokuwa, Nayo roho kumrudia Mungu aliyeitoa.

8 Mhubiri asema, Ubatili mtupu; mambo yote ni ubatili!”.

Ubarikiwe.

Kwa ziada ya masomo kuhusu kitabu cha Mhubiri, Fungua masomo haya;

ZIKUMBUKE SIKU ZIJAZO ZA GIZA, KWA MAANA ZITAKUWA NYINGI.

FANYA MAAMUZI KABLA HAZIJAKARIBIA SIKU ZA HATARI.

HEKIMA NI NINI? NA UFAHAMU UNAPATIKANA WAPI?

UBATILI.

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

habari za ziada.

Rudi Nyumbani:

Print this post

MAPEPO NI NINI?

Mapepo ni nini?


Mapepo ni Malaika walioasi zamani ambao hawakuilinda enzi yao mbinguni. (Yuda 1:6)

Na shetani mwenyewe akiwa kama pepo mkuu.

Sasa walipoasi ndipo wakatupwa duniani, na hiyo ilikuwa  kabla hata ya mwanadamu kuumbwa. Wote walikuwa wameshatupwa huku duniani wakisubiria hukumu yao ya mwisho.

Lakini mwanadamu alipoumbwa, na shetani akafanikiwa kumdanganya pale Edeni ndipo yeye na mapepo yake yote wakapata uhali wa mambo mengi ulimwenguni,

Haya mapepo yakaanza kuwaingia watu jambo ambalo lilikuwa haliwezekani hata kidogo, yakashikilia mambo mengi, na kufanikiwa kuharibu, kwa ufupi yalikuwa na uwezo wa kujiamulia kufanya chochote,  yakiongozwa na kiongozi wao mkuu shetani

Mpaka ilipofikia kipindi cha Yesu Kristo kuja duniani, hapo ndipo yalinyang’anywa sehemu kubwa ya mamlaka waliyokuwa nayo, waliyoyaiba kwa Adamu, Yesu ndio akayachukua yakawa ya kwake.

Ufunuo 1:17 “…………Usiogope, Mimi ni wa kwanza na wa mwisho,

18 na aliye hai; nami nalikuwa nimekufa, na tazama, ni hai hata milele na milele. Nami ninazo funguo za mauti, na za kuzimu”.

Hivyo mapepo yaliyopo duniani leo hii hayana nguvu tena juu ya mtu ikiwa tu, atakuwa ndani ya Kristo basi..Kwasababu yeye ndio aliyepewa mamlaka yote ya mbinguni na duniani kwa sasa (Mathayo 28:28)..

Zamani shetani alikuwa na uwezo hata, wa kuwaendea hata wafu na kuzungumza nao, utaona hilo katika kipindi cha Samweli jinsi Yule mwanamke mchawi alivyompandisha Samweli juu kuzungumza na Mfalme Sauli. Lakini sasahivi wafu wote wanamilikiwa na Yesu Kristo, kiasi kwamba ukifa leo, shetani hawezi kukufikia huko ulipo kwa namna yoyote ile.

Mapepo ni nini

Hivyo fahamu tu, ikiwa upo nje ya Kristo, kwa namna moja au nyingine, mapepo yatakusumbua tu, na lengo lao si lingine zaidi ya kukuua na kukupeleka kuzimu.. Ili kufahamu ubaya wa mapepo, fungua hapa usome >> Kwanini Bwana Yesu, aliruhusu yale mapepo yawaingie nguruwe?

Hivyo usijidanganye na kusema mimi siwezi kuwa na mapepo kisa tu hayajawahi kulipuka ndani yangu..Ndugu fahamu kuwa si mapepo yote ni ya kulipuka kama unavyodhani..

  • Mengine ni ya magonjwa.(Luka 13:11)
  • Mengine ni ya mateso/mkandamizo wa nafsi, mpaka kupelekea kujiua. Mf. Ndio Yule alimwingia Yuda ikampelekea kwenda kutenda dhambi na kujinyonga.
  • Mengine ni ya utambuzi: (Matendo 16:16)
  • Mengine ni mapepo bubu na kiziwi;(Marko 9:25)
  • Mengine ni ya kukudanganya.(1Wafalme 22:22) N.k.

Hivyo ikiwa wewe upo nje, kwa namna moja au nyingine ipo roho ya ibilisi imejishikamanisha  na wewe hata pasipo wewe kujijua. Njia pekee ya kuyaondoa ndani yako ni kumpa tu YESU KRISTO maisha yako. Ukishamwamini na ukatubu na ukabatizwa, basi maroho hayo yanaondoka ndani yako..Na wakati huo huo ROHO MTAKATIFU anaingia ndani yako. Hapo ndipo utakapojua tofauti yako ya wewe ni jana.

Luka 10:19 “Tazama, nimewapa amri ya kukanyaga nyoka na nge, na nguvu zote za yule adui, wala hakuna kitu kitakachowadhuru”.

Naamini mpaka hapo umeshafahamu kwa ufupi mapepo ni nini.

Usisahau kuwa hizi ni siku za mwisho, Na Yesu yupo mlangoni kurudi, na shetani naye analijua hilo vizuri, hivyo utendaji wake kazi sasa sio kama ule wa zamani, mapepo/majini yanatenda kazi kwa nguvu kuliko pale mwanzo. Hivyo nawe pia unaposikia habari za wokovu usikawie kawie kwasababu, shetani naye yupo karibu yako kuindoa hii mbegu iliyopandwa ndani yako.

Ufunuo 12:12 “Kwa hiyo shangilieni, enyi mbingu, nanyi mkaao humo. Ole wa nchi na bahari! Kwa maana yule Ibilisi ameshuka kwenu mwenye ghadhabu nyingi, akijua ya kuwa ana wakati mchache tu’.

Shalom.

Mada Nyinginezo:

MAJESHI YA PEPO WABAYA.

Kuna Malaika wangapi?

Kwanini Mungu anasema “Afanyaye malaika zake kuwa pepo”?

JIHADHARI NA UPOTEVU ULIOACHIWA SASA.

VIFUNGO VYA GIZA VYA MILELE.

UHARIBIFU WA MTU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

KWA KUPIGWA KWAKE SISI TUMEPONA.

Ndio kwa kupigwa kwake sisi tumepona!!

Tunao ujasiri wote wa kusema hivyo, kwasababu kuacha kwake enzi na mamlaka mbinguni, kisha kuja kuishi maisha ya taabu na mateso hapa duniani, kuanzia kuzaliwa katika zizi la ng’ombe, Kisha kuishi maisha ya umaskini tangu utoto wake hadi utu uzima,(japokuwa alikuwa ni tajiri)

1Wakorintho 8:9 “Maana mmejua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo, jinsi alivyokuwa maskini kwa ajili yenu, ingawa alikuwa tajiri, ili kwamba ninyi mpate kuwa matajiri kwa umaskini wake”.

Hakuwa hata na mahali pa kulaza kichwa chake, hata mbweha na ndege walimshinda, hiyo yote ni kwa ajili yangu mimi.

alijaribiwa zaidi yetu sisi, bila kutenda dhambi yoyote, alifunga na kukesha kwa kuomba kwa ajili yangu, na kama hiyo haitoshi, ilimgharimu kuingia matesoni ateswe na ibilisi, atemewe mate, apigwe mijeledi, agongelewe misumari, adhihakiwe, achomwe mkuki, halafu mimi nisiponywe roho yangu hilo litakuwa ni jambo lisiloingia akilini.

Kwa kupigwa kwake sisi tumepona.

Ni haki yako wewe na mimi kuupokea uponyaji wa roho zetu kwanza, na hiyo inakuja kwanza kwa kutubu dhambi zetu , kwa kudhamiria kutubu kwa kumaanisha kabisa kuuacha ulimwengu na tama zake, kisha ndio anakuja ndani yetu na kutuokoa na  kufanya makao na sisi. Na baada ya hapo atatuponya na miili yetu pia, kwasababu Kwa kupigwa kwake sisi tumepona, roho zetu na miili yetu pia.

Hivyo kabla sijakwenda kukuombe tatizo lako, Ni vema kwanza ukamkaribisha Bwana Yesu katika maisha yako. Ikiwa upo tayari kufanya hivyo leo basi unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU  MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.

AMEN.

Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Na Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu wako. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako(sawasawa na Matendo 2:38).

Sasa ikiwa wewe Ni mgonjwa, Kumbuka Bwana Yesu haponyi tu roho, anaponya pia miili yetu..mimi ninayekuandikia huu ujumbe ni shahidi alishaniponya mara nyingi, kwa kufuatisha maombi kama haya ninayokuombea vilevile atakuponya na wewe leo. Kwasababu Yesu ni yeye Yule.

Unachopaswa kufanya hapo ulipo..Weka mkono mahali unapoumwa, kisha.

Sema maneno haya kwa sauti.

EWE UGONJWA (UTAJE UGONJWA UNAO KUSUMBUA), MIMI NI MILKI HALALI YA MKUU WA UZIMA YESU KRISTO. NAKUAMURU KWA JINA LA YESU ONDOKA NDANI YANGU KUANZIA HUU WAKATI NA MILELE, KWA KUPIGA KWAKE SISI TUMEPONA. HAKUPIGWA BURE, HAKUDHARAULIWA BURE, HAKUTESWA BURE..BALI HIYO YOTE ILIKUWA NI MIMI NIUPOKEE UPONYAJI KAMILI WA ROHO YANGU NA MWILI WANGU. HIVYO ONDOKA NDANI YANGU SASA KWA JINA LA YESU KRISTO.

EE BWANA YESU, MWOKOZI WANGU, INGIA SASA NDANI YA MWILI WANGU, UNIRUDISHIE AFYA ULIYONIAHIDIA.

ASANTE KWA UPENDO WAKO.

JINA LAKO LIBARIKIWE DAIMA.

AMEN.

Sasa ikiwa  umefuatisha maombi hayo mafupi, basi kuwa na uhakika kuwa Kristo ameshakuponya tayari, ikiwa ulikuwa huwezi kufanya jambo Fulani anza kulifanya, ikiwa ni ugonjwa wa kwenye damu, nenda kapime, ikiwa ni wa viungo vyovyote vile Kristo ameshakuponya.

Hivyo usiache kwenda kushuhudia na kumpa yeye utukufu.

Bwana akubariki sana.

“Ndio Kwa kupigwa kwake sisi tumepona”.

Mada Nyinginezo:

YESU MPONYAJI.

JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?

FAHAMU JINSI KRISTO ANAVYOPONYA WATU ROHO.

RABI, UNAKAA WAPI?

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

 

CHUKIZO LA UHARIBIFU

Rudi Nyumbani:

Print this post