Kuabudu ni nini?
Kuabudu maana yake ni “kufanya Ibada”.. Kitendo cha kufanya Ibada ndio “kuabudu”. .
Hivyo Ibada yoyote ile ni lazima ijumuishe vitu hivi vitano vifuatavyo.
Hii ndio sehemu ya kwanza na ya muhimu katika Ibada.. Na kumbuka kujifunza sio kukariri, bali ni kukaa chini na kuyachambua maandiko kwa uwezo wa Roho kama vile Mwalimu na mwanafunzi wanavyofundishana wakiwa darasani.
Hichi ni kipengele cha pili cha muhimu katika ibada, ambacho kinaweza kuwa katika mfumo wa kumshukuru Mungu na kumsifu kwa (Aidha tenzi za rohoni, au kwa nyimbo za sifa na kuabudu au vyote kwa pamoja)
Hichi ni kipengele cha Tatu, na cha muhimu pia katika ibada…1Wakorintho 11:25 “Na vivi hivi baada ya kula akakitwaa kikombe, akisema, Kikombe hiki ni agano jipya katika damu yangu; fanyeni hivi kila mnywapo, kwa ukumbusho wangu”.
Maombi yanajumuisha pia dua na sala..na ili ibada iwe ibada ni lazima kuwepo na kipindi cha maombi, wakati huu ndio wakati wa fursa ya kupeleka haja zetu kwa Mungu wetu.
5 . Matoleo
Hichi ni kipengele cha mwisho kabisa, ambacho kinakamilisha IBADA. Biblia inasema (katika Kumbukumbu 16:16), kwamba tusiende nyumbani kwake, mikono mitupu. Matoleo ndio yanayokamilisha ibada. Hivyo mtu hawezi kusema leo nimekwenda kumwabudu Mungu bila kumtolea.
Hivyo mtu akivifanya vipengele hivyo vitano, katika ROHO NA KWELI, Basi anakuwa amemwabudu wa kweli wa mbingu na nchi.
Sasa utauliza, je tunamwabudu vipi Mungu katika Roho na kweli?. Inamaana tuingie katika ulimwengu wa roho?
Ni muhimu kufahamu kuwa kuishi katika Roho sio kuishi kwa kuona mambo yasiyoonekana kama mapepo, au malaika, au kuona mbingu au kuona maono, hapana hiyo siyo tafisiri ya kuishi kwa Roho au kuabudu kwa Roho.. Tafsiri ya kuishi kwa Roho ni kuishi kwa kulifuata Neno la Kristo… Mtu yeyote anayeishi kwa kuyafuata maneno ya Kristo, huyo ni mtu wa rohoni asilimia mia, hata kama maisha yake yote hajawahi kuona ono hata moja, au hajawahi kuona malaika, wala mapepo. Kwasababu biblia inasema Maneno ya Kristo ndio Roho.
Yohana 6: 63 “Roho ndiyo itiayo uzima, mwili haufai kitu; MANENO HAYO NİLİYOWAAMBİA Nİ ROHO, tena ni uzima”.
Hivyo tunapomwambudu Mungu katika roho na kweli, maana yake ni kwamba tunafanya ibada kulingana na jinsi NENO LAKE linavyosema katika ukweli wote na usafi wa moyo.
Je umempokea Kristo?.. kama bado hujampokea na unakwenda kanisani tu kutimiza wajibu fulani, basi jua hapo huendi kumwabudu Mungu katika Roho na Kweli, hivyo hakuna baraka zozote za rohoni ambazo ulikuwa unazipata. Lakini leo ukiamua kutubu, na kuacha dhambi..Kristo ataingia moyoni mwako na kukuponya..na atakusafisha kwa damu yake, na kukufanya uweze kumwabudu Mungu katika Roho na Kweli.
Kama leo hii upo tayari kumpokea, basi fuatilisha sala hii fupi ya toba kwa kufungua hapa >> SALA YA TOBA.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Kwanini Kuhani wa Mungu Eli alikufa kwa kuvunjika shingo, Na sio kwa njia nyingine yoyote salama?
Habari ya Eli ni funzo tosha kwa kanisa la Kristo leo hii. Mungu aliruhusu afe kifo cha aina hiyo, ili kutimiza mstari huu wa biblia;
Mithali 29:1 “Aonywaye mara nyingi akishupaza shingo, Atavunjika ghafula, wala hapati dawa”.
Kama tunavyoijua habari ya Eli,alikuwa kuhani wa Mungu kwa muda wa miaka 40, na katika ukuhani wake, alifanya kazi hiyo pamoja na wanawe wawili, lakini watoto wake hawa walikuwa waovu kupindukia, kwani waliwakosesha Israeli kwa tabia zao sizizoakisi ukuhani, na habari yao ikavuma kila mahali kuwa hawafai, kwani walikuwa wanaila dhabihu isivyostahili na zaidi ya yote, walikuwa wanalala na wanawake waliokuwa wanatumika mbele ya hema ya kukutania, mfano tu baadhi ya wakristo katika kanisa la Mungu leo hii.
Sasa dhambi hii ilikuwa ni kubwa sana, na Mungu alikuwa amekusudia kuwauwa wale watoto wawili wa Eli, na sio Eli mwenyewe, lakini tabia ya Eli ya kupuuzia na kuwaheshimu watoto wake zaidi kuliko Mungu, hilo lilimfanya Mungu amuue na yeye kwa kifo hicho. Kwasababu alijua kabisa uovu unaofanywa na wanawe lakini hakulitilia mkazo.
Eli alionywa mara tatu, mara ya kwanza alionywa na waisraeli, kuwa watoto wake hawafai na kwamba anapaswa awaondoe katika kazi ya ukuhani lakini hakusikia..
Akaonywa tena mara pili na Mungu kupitia nabii wake, (1Samweli 2:29), lakini bado hakuwaondoa, akawaheshimu wanawe kuliko Mungu.
Akaja tena kuonywa mara ya tatu kupitia mtoto Samweli, akaelezwa mpaka na hukumu itakayowakuta watoto wake, lakini yeye bado akaendelea kuwaacha wafanye machafuko yote hemani pa Bwana.
1Samweli 3:13 “Kwa maana nimemwambia ya kwamba nitaihukumu nyumba yake milele, kwa ajili ya ule uovu alioujua; kwa kuwa wanawe walijiletea laana, wala yeye hakuwazuia”.
Ndipo siku ya siku ilipofika, Wafilisti waliwavamia Israeli, wakawapiga, wakaliiba na sanduku la Agano, Na yeye akiwa amebaki hemani mwake kusubiria taarifa ya vita, kama tunavyoijua Habari, kijana mmoja alitoka huko akamletea habari, na kumwambia Israeli imepigwa, wanawe wote wawili wamekufa na kibaya zaidi Sanduku la Mungu limechukuliwa na wafilisti. Aliposikia tu habari hiyo akadondoka kwa nyuma, shingo yake ikavunjika na pale pale akafa.
1Samweli 4:13 “Alipofika, tazama, Eli alikuwa ameketi kitini pake kando ya njia, akingojea; maana moyo wake ulitetemeka kwa ajili ya sanduku la Mungu. Na yule mtu alipoingia mjini, akatoa habari, mji wote ukalia.
14 Naye Eli aliposikia kelele za kile kilio, akasema, Maana yake nini kelele za kishindo hiki? Yule mtu akafanya haraka, akaenda, akamwambia Eli.
15 Basi Eli umri wake umepata miaka tisini na minane; na macho yake yamepofuka hata asiweze kuona.
16 Yule mtu akamwambia Eli, Mimi ndimi niliyetoka jeshini, nami leo hivi nimekimbia toka jeshini. Naye akasema, Yalikwendaje, mwanangu?
17 Yeye aliyeleta habari akajibu, akasema, Israeli wamekimbia mbele ya Wafilisti, tena watu wengi sana wameuawa, hata na wana wako wawili, Hofni na Finehasi, wamekufa pia, na sanduku la Mungu limetwaliwa.
18 Ikawa alipolitaja sanduku la Mungu, Eli akaanguka kitini pake kwa nyuma, kando ya mlango, shingo yake ikavunjika, akafa; maana alikuwa mzee, tena mzito. Naye alikuwa amewaamua Israeli miaka arobaini”.
Hivyo kitendo cha Eli kufa kifo cha kuvunja shingo ni Mungu alikuwa anafundisha jinsi madhara yatakavyowakuta watu wale wanaopuuzia na kudharau maagizo yake.
Tengeneza picha Eli alikuwa ni kuhani lakini alikufa kifo cha ghafla tu kwa kosa la kudharau maneno ya Mungu. Vipi kuhusu sisi ambao kila siku Mungu anatuonya tuache hichi au kile lakini hatutaki kusikia, Mtu anazini na bado anasema ameokoka. Kila siku tunasikia maneno ya Mungu lakini bado hatutaki kuyakabidhi maisha yetu kwake.. Je! Ni kitu gani tunakitazamia siku za usoni?
Hututakufa kifo cha kuvunjika shingo kimwili, lakini rohoni tutavunjika shingo zetu ghafla, na hutakuwa na nafasi tena ya kumrudia Mungu, kwasababu hukumu tayari itakuwa umeshatolewa juu yetu.
Mithali 29:1 “Aonywaye mara nyingi akishupaza shingo, Atavunjika ghafula, wala hapati dawa”.
Inawezekana na wewe umeshaonywa mara nyingi kwa kupitia mahubiri ya Neno la Mungu, lakini ulikuwa umeshupaza shingo…. Kwanini leo, usimrudie muumba wako? Kwanini usianze maisha mapya na Kristo, uondokane na laana ya dhambi? Maisha ya dhambi yamekupa faida gani mpaka sasa, Ukifa leo ghafla huko utakapokwenda utakuwa ni mgeni wa nani?. Au Kristo akirudi leo wewe utakuwa wapi?. Kwasababu tupo ukingoni kabisa mwa nyakati, Kristo anarudi.
Ulimwengu huu umeshatamkiwa meme, mene, Tekeli na Peresi kitambo sana, Umeshatamkiwa IKABODI, Hakuna cha ziada zaidi ya kuharibiwa tu. Tubu dhambi zako kama bado hujatubu. Na pia tafuta kubatizwa ikiwa bado hujabatizwa. Na Mungu atakupa Roho wake Mtakatifu. Katika wakati huu wa kumalizia.
Maran Atha.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Kwanini Samweli aliruhusuiwa kuhudumu hekaluni kama vile Walawi wakati yeye ni mu-Efraimu?
Kitabu cha YASHARI kinachozungumziwa katika 2Samweli 1:17-18, ni kitabu gani?
Nzio ni kipimo cha ujazo wa kimimika kilichotumiwa zamani na wagiriki, Nzio moja ina ujazo wa karibia lita 40,
Katika biblia utaona ile habari ya Yesu kualikwa katika arusi kule Kana mji wa Galilaya, Neno hili lilitumika tusome;
Yohana 2:6 Basi kulikuwako huko mabalasi sita ya mawe, nayo yamewekwa huko kwa desturi ya Wayahudi ya kutawadha, kila moja lapata KADIRI YA NZIO mbili tatu.
Hivyo hapo unaweza kupata picha hapo, hayo mabalasi yalikuwa na ujazo mwingi kiasi gani. Kama kila balasi moja linachukua nzio mbili au tatu, ukikadiria hapo, ni kuwa balasi moja lina ujazo wa lita 80 mpaka 120.
Na mabalasi yalikuwa ni 6, hivyo ujazo wa maji yaliyowekwa pale na kubadilika kuwa divai ni karibia lita 480-720. Hivyo ni kiwango kikubwa sana. Hivyo unaweza kuona jinsi divai hiyo ingewahudumia watu wengi kiasi gani. Kumbuka mtu mmoja tu hawezi kunywa lita nzima ya divai, akijitahidi sana atakunywa nusu au robo.
Lakini ni nini Mungu alikuwa analifundisha kanisa?
Ni kuwa pale tulipo na mapungufu, yeye anaweza kutujaza, jambo hilo utaona tena alipoigawa ile mikate mitano na samaki wawili na kulisha maelfu ya watu. Na alifanya hivyo mara mbili , Hiyo ni kutuonyesha kuwa palipo na vichache, au pale ambapo hamna kabisa Mungu anaweza kugeuza kitu kingine kisichokuwa na thamani kikawa na thamani kwetu. Ipo mifano mingi sana katika biblia, utaiona ile habari ya Elisha na yule mwanamke ambaye mume wake alikuwa anadaiwa, mpaka akafa hajalipa deni, yule anayemdai akaja akataka kwenda kuwachukua watoto wake awafanye kuwa watumwa, lakini yule mama alipokwenda kwa Elisha amsaidie, Elisha akamwomba Mungu, ndipo akamwambia akachukue vyombo vitupu kisha amimine mafuta kwenye vyombo hivyo, kwa kadiri awezavyo kwasababu mafuta yale hataisha, kisha aende kuuza, na fedha itakayopatikana, alipe deni lake, na itakayobaki atumie yeye na familia yake(2Wafalme 4:1-7) .
Hiyo yote ni kuonyesha kuwa Mungu anaweza kutoa pale pasipowezekana na ndio maana anaitwa YEHOVA- YIRE, (yaani Mungu mpaji wetu). Hivyo na wewe ukimtegemea yeye atakutendea miujiza kama hiyo.
Lakini ni sharti kwanza uwe mwana wake. Swali ni Je! Kristo yupo ndani yetu? Majibu yote tunayo, lakini tujue kuwa hakuna kimbilio la kweli nje ya Kristo. HUO NDIO UKWELI PEKEE ULIODUMU DUNIANI KWA MIAKA YOTE.
Shalom.
Kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Je! mabalasi Bwana Yesu aliyoyatumia kugeuzia maji kuwa divai, yalitumika tu kwa kazi hiyo?
Hozi ni nini?
Hozi ni neno linalomaanisha himaya, ikijumuisha eneo na vitu mtu anavyomiliki.
Kwa mfano unaweza kuona, Yabesi, alimwomba Mungu ambariki na kumzidishia Hozi yake (Himaya yake), Hiyo akiwa na maana kuwa azidishiwe mifugo, azidishiwe uzao, azidishiwe mali, azidishiwe watumwa na wajakazi, azidishiwe ardhi, azidishiwe ukuu n.k. Na kweli kama tunavyosoma Mungu aliridhia maombi yake kwasababu alikuwa ni mcha Mungu, japokuwa alitokea katika chumbuko la huzuni.
1Nyakati 4:10 “Huyo Yabesi akamlingana Mungu wa Israeli, akisema, Lau kwamba ungenibarikia kweli kweli, na kunizidishia HOZI YANGU, na mkono wako ungekuwa pamoja nami, nawe ungenilinda na uovu, ili usiwe kwa huzuni yangu! Naye Mungu akamjalia hayo aliyoyaomba”.
Neno hilo utalisoma pia katika vifungu hivi;
1Nyakati 7:27 “na mwanawe huyo ni Nuni, na mwanawe huyo ni Yoshua.
28 Na HIZI NDIZO HOZI zao na makao yao; Betheli na vijiji vyake, na upande wa mashariki Naara, na upande wa magharibi Gezeri na vijiji vyake; na Shekemu pia na vijiji vyake, hata Aza na vijiji vyake;
1Nyakati 9:1 “Hivyo Israeli wote walihesabiwa kwa nasaba; na tazama, hizo zimeandikwa katika kitabu cha wafalme wa Israeli; na Yuda wakachukuliwa mateka mpaka Babeli, kwa sababu ya makosa yao.
2 Basi wenyeji wa kwanza waliokaa katika HOZI ZAO katika miji yao walikuwa Israeli, na makuhani, na Walawi, na Wanethini”.
Vivyo hivyo na sisi, tukimcha Mungu, mfano wa Yabesi Mungu anaweza kuzizidisha himaya zetu mfano wa Yabesi pale tutakapomwomba. Lakini vilevile tusipomcha yeye, anao uwezo wa kummilikisha mtu mwingine hiyama zetu na tukabakiwa hatuna kitu kama vile alivyofanya kwa wana wa Israeli, walipomuasi akawapeleka utumwani Babeli, na himaya zao zikamilikiwa na watu wengine.
Na himaya sio lazima tu iwe ile ya mwilini, Rohoni pia tunazo himaya, pale tunapomkataa Mungu maisha mwetu, hapo hapo adui yetu shetani ibilisi anapata nguvu ya kuzitawala himaya zetu. Na ndio hapo anakuwa na uwezo asilimia mia wa kujiamulia jambo lolote baya katika maisha yetu, hata kutuua ataweza, kwasababu tumekusoma Baraka na ulinzi wa ki-Mungu.
Hivyo sisi nasi pia tunawajibu wa kuzilinda HOZI zetu. Kwa kuupokea wokovu na kuulinda katika utakatifu. Ndipo Bwana atakapotuzidisha na kutuongeza kupita kiasi.
Swali ni Je! Upo ndani ya wokovu? Je! Hozi zako zipo mikononi nani? Jibu unalo, jibu ninalo. Lakini Yesu Kristo ndio mwokozi.
Shalom.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Shalom, Karibu tujifunze biblia, ambayo ni Neno la Mungu.
Ni vizuri kumjua Mungu ili tuwe na Amani.. Biblia inasema hivyo katika..
Ayubu 22: 21 “Mjue sana Mungu, ili uwe na amani; Ndivyo mema yatakavyokujia”.
Maana yake ni kwamba tukiyajua mapenzi ya Mungu na tabia za Mungu basi tutakuwa na AMANI, Na ndivyo mema yatakavyotujia.
Leo kwa neema za Bwana hebu tujifunze kidogo, juu ya tabia ya Mungu.
Wengi wetu katika Maisha tunayoishi, tunakumbana na majaribu mengi yanayoletwa na wanadamu wenzetu. Yaani wapo watu wanatumika na Adui shetani, kutuumiza sisi kihisia na kimwili, na mbaya Zaidi wanafanya hayo huku wanajua kabisa. Kwa lugha iliyozoeleka sasa watu hao wanaitwa MAADUI.
Leo hii ukimwuliza mtu yeyote je! Unao maadui?.. Ni ngumu kusikia mtu akisema kwamba sina maadui kabisa!.. Ni lazima utakuta mtu anao maadui, kwa vyovyote vile.
Wengine maadui zao ni watu wanaowanyanyasa, wengine maadui zao ni watu wanaowadharau kupita kiasi, wengine maadui zao ni watu wanaojisifu juu yao, wengine maadui zao ni watu wanaowaonea wivu n.k. Na katika nyakati hizi tunazoishi, asilimia kubwa ya watu wanaomlilia Mungu, ni kutokana na vita walizonazo dhidi ya wanaowaita maadui zao.
Utakuta mtu atakwenda kanisani kuomba Mungu amnyanyue kwenye kazi yake ili azikomeshe dharau za watu Fulani wanaomdharau, mwingine utakuta yupo kwenye mfungo wa maombi apate fursa Fulani, iwafunge midomo watu Fulani (ambao kwake yeye ndio kama maadui zake). Ni wachache sana ambao utakuta wanafunga kumwomba Mungu awape kazi nzuri, au fursa Fulani ili wamtumikie yeye kupitia hiyo.
Sasa hiyo hali ya kuingia kwenye vita dhidi ya maadui, haikuanzia hapa, ilianzia tangu kwenye biblia..Leo tutajifunza mifano kadhaa ya watu waliopambana na maadui zao, na kwa kupitia mifano hiyo, na sisi pia tutapata kujua hisia za Mungu, juu ya tunaowaita maadui zetu, Pamoja na namna ya kushughulika nao.
HANA na PENINA.
Hawa walikuwa ni wanawake wawili wa mwanaume mmoja aliyejulikana kama Elkana. Penina alikuwa na watoto lakini Hana hakujaliwa kupata Watoto, na kama tunavyojua kitu gani kilifuata, Biblia inasema Penina alianza kumchokoza sana Hana kwasababu ni tasa (1Samweli 1:6). Kwa ufupi ni kwamba alikuwa anamdhihaki na kumdharau sana..kisa tu yeye ana Watoto na mwenzie hana.
Kama wewe unayesoma ujumbe huu ni mwanamke, hebu jiweke kwenye hiyo nafasi, huna mtoto, halafu mwingine aliye naye anakukebehi kebehi, anakupa kupa vijimaneno vya kukumiza na kukudhalilisha. Bila shaka tayari huyo kashakuwa adui yako.
Ndicho kilichomtokea Hana, baada ya kuzungumzwa sana na mke mwenza, uvumilivu ukamshinda ikabidi aanze kumlilia Mungu. Na baadaye kama tunavyoijua Habari, Mungu akasikia kilio chake na yeye akampa Watoto.
Lakini hebu turudi kwa upande wa Elkana, ambaye ndiye mume wa wanawake wote wawili (Hana na Penina). Wakati Hana na Penina ni maadui, Elkana alikuwa anawapenda wote. Wakati Hana anajifungua mtoto wa kwanza, haikumfanya Elkana awachukie Watoto wa Penina, wala haikumfanya amchukie Penina. Ijapokuwa Penina na Hana walikuwa ni maadui.
Ndivyo hivyo hivyo kwa Mungu wetu, Yule ambaye ni adui wako wewe, yule unayemchukia…haimaanishi kwamba Mungu naye anamchukia kama unavyomchukia wewe…yule anayekuudhi sana, haimaanishi kwamba anamuudhi Mungu kama anavyokuudhi wewe. Hivyo usichukue hasira zako ukazifanya za Mungu.
Hebu tujifunze tena mfano mwingine.. wa SARA na HAJIRI. Hawa nao walikuwa ni wanawake wawili, ambao ilifika wakati wakashiriki mume mmoja aliyeitwa IBRAHIMU. Na ikafika kipindi pia wakawa ni maadui kwasababu Hajiri alipata mtoto na Sara hakupata. Na Hajiri ambaye ni kijakazi alianza kumdharau bibi yake, kwasababu hakuwa na mtoto. Hivyo kukawa na ugomvi mkubwa wa chini kwa chini..(maadui hao wawili wamekutana). Na ulipofika wakati wa Mungu kumfungua tumbo Sara, alimfukuza Hajiri Pamoja na mwanawe Ishmaeli.
Lakini je! Jiulize chuki aliyokuwa nayo Sara dhidi ya mtoto wa kijakazi wake Hajiri (yaani Ishamaeli), je! ndiyo hiyo hiyo iliyokuwa juu ya Ibrahimu kwa Ishamaeli?.. Au chuki Hajiri aliyokuwa nayo kwa Isaka mwana wa Sara, ndiyo hiyo hiyo aliyokuwa nayo Ibrahimu kwa Isaka?.. La!..sio hiyo hiyo, Badala yake utaona Ibrahimu aliwapenda wanawe wote na wala hakuna aliyekuwa anamchukia, ijapokuwa mama zao walikuwa hawapatani.
Vivyo hivyo, huyo unayemwona ni Adui yako leo, ambaye ni mtesi wako leo, ambaye anakufanya ulie na kuhuzunika usifikiri Mungu anamchukia kama unavyomchukia wewe. Atakachofanya Mungu ni kumweka mbali na wewe, lakini usifikiri atakuwa na kinyongo naye kama ulichonacho wewe juu yake..wala usifikiri Mungu atamwua kwasababu yako wewe.. Futa hayo mawazo!…Kuanzia leo “anza kumjua Mungu ili uwe na amani”..Wala usipoteze muda wako kumwombea maombi ya kufa..kwasababu hatakufa!!..Ni sawa na Sara kumtuma Ibrahimu akamwue Ishamaeli..atakuwa anapoteza muda wake tu!.
Hali kadhalika usiogope!..Adui yako atakapokuombea shari kwa Mungu..atakuwa anapoteza muda wake tu!..Kwasababu chuki alizonazo yeye juu yako, sizo alizonazo Mungu juu yako. Ni sawa na Hajiri kumtuma Ibrahimu akamwue Isaka. Ni kitu kisichowezekana, atakuwa anapoteza muda wake tu!! Usipoteze muda wako, kufanya hivyo.
Utajifunza tena jambo kama hilo hilo kwa wake wa Yakobo.
Hivyo kwa hitimisho..Bwana wetu Yesu Kristo aliyasema maneno haya…
Mathayo 5:43 “Mmesikia kwamba imenenwa, Umpende jirani yako, na, UMCHUKIE ADUI YAKO;
44 lakini mimi nawaambia, WAPENDENI ADUI ZENU, WAOMBEENI WANAOWAUDHI,
45 ili mpate kuwa wana wa Baba yenu aliye mbinguni; maana yeye huwaangazia jua lake waovu na wema, huwanyeshea mvua wenye haki na wasio haki.
46 Maana mkiwapenda wanaowapenda ninyi mwapata thawabu gani? Hata watoza ushuru, je! Nao hawafanyi yayo hayo?”
Kama unanyanyaswa..usipoteze muda kumwombe shari ndugu yako..kwasababu hayo sio mapenzi ya Mungu, wala usifurahie kuanguka kwake…je! Unadhani Elkana alikuwa anafurahishwa na ugomvi uliokuwepo kati ya Hana na Penina?..vivyo hivyo Mungu hapendezwi na sisi tunapokuwa na ugomvi na watu wanaotuchukia..na wala maombi ya magomvi hayampendezi..
Mithali 24:17 “Usifurahi, adui yako aangukapo; Wala moyo wako usishangilie ajikwaapo;
18 Bwana asije akaliona hilo, likamkasirisha; Akageuzia mbali naye hasira yake”.
Na pia usiogope! Mtu anapokuchukia au anapokufanyia ubaya..au anapokushitaki mbele za Mungu…fahamu kuwa anapoteza muda tu!..kwasababu Mungu hakuchikii kama yeye anavyokuchukia.
Bwana atubariki
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
SWALI: Naomba kufahamu kuwatema farasi maana yake ni nini?. Kwanini Mungu aliwaagiza wana wa Israeli wakati mwingine wawateme farasi za maadui wao vitani?
Neno hilo tunalisoma katika kifungu hiki;
Yoshua 11:6 “Bwana akamwambia Yoshua, Usiche wewe kwa ajili ya hao; kwani kesho wakati kama huu nitawatoa hali wameuawa wote mbele ya Israeli; UTAWATEMA FARASI ZAO, na magari yao utayapiga moto.
7 Basi Yoshua akaenda, na watu wote wa vita pamoja naye, ili kupigana nao hapo penye maji ya Meromu ghafula; wakawaangukia.
8 Bwana akawatia mkononi mwa Israeli, nao wakawapiga, na kuwafukuza hata kufikilia Sidoni ulio mkuu, na hata kufikilia Misrefoth-maimu, tena hata kufikilia bonde la Mispa upande wa mashariki; wakawapiga hata wasiwasaze hata mtu mmoja aliyesalia.
9 Yoshua akawafanyia vile vile kama Bwana alivyomwamuru; AKAWATEMA FARASI ZAO, na magari yao akayapiga moto”.
Kama tunavyojua Yoshua na wana wa Israeli walipovuka Yordani walikutana na maadui zao wengi kule Kaanani, maadui ambao walikuwa na uzoefu mkubwa wa kivita, na wenye majeshi mengi. Na hapa tunaona wana wa Israeli walipofika sehemu moja walikutana na huyu adui yao mmoja “Yabini” mfalme wa Azori ambaye hakumwendea peke yake bali alikwenda kukusanya nguvu kutoka katika mataifa ya kando kando yake ili yamsaidie kummaliza Yoshua na wana wa Israeli wote kwa ujumla,na biblia inasema lilikuwa ni jeshi kubwa kama mchanga wa bahari, wenye magari mengi ya vita na wafasi wengi sana.
Lakini utaona hapa Mungu anampa maagizo Yoshua na kumwambia kuwa watakapowapiga wasichukue chochote bali wayachome magari yao ya vita na wawateme farasi zao.
Kutema farasi maana yake nini?
Kutema ni kujeruhi tishu za misuli ya miguu, ambazo zinasababisha mtu au mnyama kuweza kutembea, au kukimbia au kuruka au kupanda. Tishu hizo ngumu kwa mwanadamu au kwa mnyama zipo sehemu ya nyuma ya miguu kuanzia kwenye paja hadi kwenye goti, na kwa mnyama vivyo hivyo kwenye miguu yake ya nyuma.
Tishu hizo zikikatwa huwa haziponyeki, na mtu au mnyama unakuwa mlemavu wa kudumu. Hawezi kukimbia, au kuruka au kutembea.
Hivyo ilikuwa ni desturi za kivita zamani na hata sasa, farasi wa kivita, wasiohitajika, hawakuachwa hivi hivi bali walitemwa (walikatwa tishu hizo) ili kusudi kwamba wasije tumiwa kwa vita tena na maadui zao. Kwahiyo wanyama hao walibakia kuwa hawana kazi yoyote tena baada ya hapo.
Sasa ni kwanini Mungu hakuwaruhusu wana wa Israeli wawachukue farasi wale, wawasaidie pengine kwa ajili ya vita vilivyokuwa mbele yao, lakini badala yake akawaamuru wawateme?
Ni kwasababu Mungu alitaka tegemeo lao liwe kwake na sio kwenye silaha au majeshi..Na kwamba wajue kuwa yeye huwa haikoi kwa silaha au kwa majeshi bali kwa Roho wake.
Daudi alisema..
Zaburi 20:7 “Hawa wanataja magari na hawa farasi, Bali sisi tutalitaja jina la Bwana, Mungu wetu”.
Na kama tunavyoona, wana wa Israeli hawakutumia magari wala farasi mahali popote walipovuka Yordani, lakini waliogopwa na maadui zao wote waliowazunguka, hiyo ni kwasababu walimtumaini Mungu peke yake ambaye angeweza kuwaokoa.
Vivyo hivyo na sisi, tukitaka tumshinde shetani kabisa kabisa au maadui zetu, hatupaswi kuweka tumaini letu kwa wanadamu au kwenye mali au chochote kile, bali tuweke tumaini letu kwa Yesu Kristo Bwana wetu, awezaye kutuokoa. Huku tukiwa tumezavaa silaha zote za haki (Waefeso 6) ili kusudi kwamba shetani akitaka kututema, sisi ndio tuwe wa kwanza kumtema yeye, Kwa jina la Yesu.
Bwana akubariki.
Je! Yesu akirudi leo unao uhakika wa kwenda naye? Je! Unahafahamu kwa hizi ndio zile nyakati ambazo biblia ilitabiri kutakuwa na makundi mawili ya wakristo? (yaani wanawali werevu na wanawali wapumbavu Math. 25) ambao wote wanadai wanamngojea Bwana? Lakini wale wapumbavu waliikosa karamu kwasababu hawakuwa na mafuta ya kutosha katika taa zao. Hivyo nyakati hizi kigezo cha kusema wewe ni mkristo pekee haitoshi, kusema wewe umeokoka haitoshi, unapaswa ujiulize ni nini kinachonipa uhakika ndani yangu kuwa Kristo akirudi leo nitakwenda naye?
Je! Mafuta ya Roho Mtakatifu yaliyo ndani yangu yaninitosha au yalishakwisha siku nyingi?
Maran Atha.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Jibu: Kuna tofauti ya Neno “kutakabari” na “kutabaruku”. Kutakabari ni “kuwa ni majivuno yanayotokana na kiburi” unaweza kusoma kusoma kwa urefu hapa >> KUTAKABARI
Lakini “kutabaruku” ambako ndiko tunakokwenda kukuzungumzia leo, maana yake ni “KUWEKA WAKFU”.
Sasa sikuku ya kutabaruku maana yake ni “Sikukuu ya kuweka wakfu”. Sikukuu hii ilianza kusheherekewa na Wayahudi (yaani waisraeli), miaka kadhaa baada ya Nabii wa mwisho katika biblia kutokea (yaani Nabii Malaki).
Sikukuu hii haikuwa miongoni mwa zile sikukuu 7 ambazo Musa aliagizwa na Mungu awape wana wa Israeli. Hivyo sherehe hii ilikuja kutengenezwa na baadhi ya wayahudi wachache kama ukumbusho wa kilichotokea katika Hekalu lao.
Sikukuu hii iliidhinishwa na Myahudi mmoja aliyeitwa Yuda Makabayo, pamoja na wazee wengine wa Israeli wachache, kipindi ambacho Mtawala Antiokia IV Epifane, alipozuka na kushuka Yerusalemu na kulitia unajisi Hekalu la Mungu, kama unabii unavyosema katika Danieli 8:9 (Ile Pembe ndogo).
Mtawala huyu aliwalazimisha wayahudi wote wasiabudu katika Nyumba ya Mungu, na badala yake kuwalazimisha kufuata desturi za kipagani,
Sasa ndipo wakatokea wayahudi hao wachache (Yuda Makabayo pamoja na wenzake) wakaingia porini kupambana naye na kumwondosha, na hatimaye KULIWEKA TENA WAKFU HEKALU ambalo alilichafua, huyu Antiokia IV Epifane. Na tangu muda huo wakaifanya hiyo tarehe, kuwa ni tarehe ya kuadhimishwa kwa jinsi Mungu alivyowafungulia mlango wa kurejeshwa kwa Ibada takatifu za Nyumba ya Mungu. Kwa urefu kuhusu Mtawala huyu pamoja na Yuda Makabayo fungua hapa >> Danieli Mlango wa 8
Sikukuu hii haina tofauti na ile ya akina Mordekai (Sikukuu ya Purimu). Ambayo Mordekai na Esta waliitengeneza kama kumbukumbu ya mambo Mungu aliyowafanyia, baada ya kuwaokoa na mkono wa Hamani, adui yao.
Esta 9: 27 “Wayahudi wakaagiza na kutadariki juu yao wenyewe, na juu ya wazao wao, na juu ya wote watakaojiunga nao, isikome, ya kwamba watazishika siku hizo mbili sawasawa na andiko lile, na kwa majira yake kila mwaka;
28 siku hizo zikumbukwe na kushikwa kwa vizazi vyote na kila jamaa, katika kila jimbo na kila mji; wala siku hizo za Purimu zisikome katikati ya Wayahudi, wala kumbukumbu lake lisiishe kwa wazao wao”
Sikukuu hii ya kutabaruku na hiyo ya Akina Mordekai zote hazikuwepo miongoni mwa sikukuu Bwana alizowaagiza kwa mkono wa Musa..Ni sikukuu zilizotengenezwa baada ya Mungu kuwafanyia mema watu wake, hivyo na wao wakazingeneza kama kurudisha shukrani kwa Mungu wao.
Ni jambo gani tunajifunza katika sikukuu hii ya kutabaruku?
Chochote tunachomfanyia Mungu, anakiheshimu.. Daudi alifikiria kumjengea Mungu nyumba, ingawa alijua kabisa Mungu hakai kwenye nyumba zilizotengenezwa na mikono ya wanadamu, lakini Mungu alimheshimu kwa mawazo yake hayo, na wala hakuidharau ile nyumba, zaidi ya yote aliitukuza sana kwa mwanawe Sulemani.
Vivyo hivyo hawa wakina Yuda Makabayo na wenzake, ambao walipenda kuadhimisha siku ya Nyumba ya Mungu kuwekwa tena wakfu, huku wakimshukuru kwa kumfanyia Ibada, Mungu aliiheshimu sikukuu yao hiyo..Ndio maana ilidumu mpaka wakati wa Bwana Yesu.
Yohana 10:22 “Basi huko Yerusalemu ilikuwa SIKUKUU YA KUTABARUKU; ni wakati wa baridi.
23 Naye Yesu alikuwa akitembea hekaluni, katika ukumbi wa Sulemani”.
Je umeokoka?..Kama bado unangoja nini?..kipindi si kirefu parapanda ya mwisho italia, na watakatifu ambao unadhani hawapo leo duniani, wataondolewa duniani…Na utakuwa umepoteza nafsi yako milele.. Hujui dakika tano mbele nini kitatokea..ukifa leo au parapanda ikilia leo utakuwa wapi?..kumbuka kuzimu ipo, na biblia inasema haishibi watu.. Mpokee leo Kristo kama bado hujafanya hivyo…
Kama upo tayari kutubu leo na kuanza safari mpya ya wokovu basi fungua hapa >> SALA YA TOBA
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Jibu: Kutakabari maana yake ni “kuwa na kiburi”…Na hicho kinaweza kuja kutokana na kujiamini sana, au kuwa na kitu fulani ambacho wengine hawana, na kujiona huhitaji kitu kingine chochote…Kutakabari huko kunazaa kujisifu au kujiona bora kuliko wengine, na kujiinua sana hata kudharau wengine au kumdharau Muumba.
Katika biblia tunaweza kuona mifano kadhaa ya watu waliotakabari..
Huyu alikuwa mtoto wa Mfalme Daudi, wakati Daudi alipokuwa mzee, alijiona yeye ni bora kuliko watoto wengine wote wa Daudi, hata pasipo kumshirikisha baba yake, akaenda kujitangaza kwa watu kuwa yeye ndiye mfalme, angali bado baba yake akiwa hai.
1Wafalme 1: 5 “Ndipo Adonia mwana wa Hagithi AKATAKABARI, akasema, Mimi nitakuwa mfalme. Akajiwekea tayari magari na wapanda farasi, na watu hamsini wapige mbio mbele yake”.
Lakini tunaona badae hakupata hicho alichokuwa anakitafuta, na nafasi hiyo alipewa Sulemani.
Wana wa Israeli ilifika wakati walimwacha Mungu, na hata kufikia hatua ya kuwatukana na kuwadharau manabii wake, na kupelekea ghadhabu ya Mungu kumwagwa juu yao kwa kuuawa na baadhi yao kupelekwa Babeli utumwani.
2Nyakati 36:15 “Naye Bwana, Mungu wa baba zao, akatuma kwao kwa mikono ya wajumbe wake, akiondoka mapema, na kutuma; kwa sababu aliwahurumia watu wake, na makao yake;
16 lakini waliwadhihaki wajumbe wa Mungu, na KUYADHARAU MANENO YAKE, NA KUWACHEKA MANABİİ WAKE, hata ilipozidi ghadhabu ya Bwana juu ya watu wake, hata kusiwe na kuponya.
17 Kwa hiyo akaleta juu yao mfalme wa Wakaldayo, aliyewaua vijana wao kwa upanga nyumbani mwa patakatifu pao, asiwahurumie kijana wala mwanamwali, mzee wala mkongwe; akawatia wote mkononi mwake”
Kutakabari huko kwa wana wa Israeli ndiko kukapelekea kuchukuliwa utumwani.
Nehemia 9: 29 “ukawashuhudia ili uwarudishe tena katika sheria yako; LAKINI WALITAKABARI, wasizisikilize amri zako, bali wakazihalifu hukumu zako, (ambazo mtu akizitenda ataishi katika hizo), nao wakayaondoa mabega yao, wakafanya shingo zao kuwa ngumu, wasitake kusikiliza”.
Yeremia 48: 29 “Tumesikia habari za kiburi cha Moabu; Ya kuwa ana kiburi kingi; Jeuri yake, na kiburi chake, na majivuno yake, Na jinsi ALIVYOTAKABARI moyoni mwake.
30 Najua ghadhabu yake, asema Bwana, ya kuwa si kitu; majisifu yake hayakutenda neno lo lote.
31 Kwa sababu hiyo nitampigia yowe Moabu, naam, nitapiga kelele kwa ajili ya Moabu yote; nitawaombolezea watu wa Kir-heresi”.
Na mfano wa wengine waliotakabari kupita kiasi ni Farao (soma Nehemia 9:10), Nebukadneza (Danieli 4:37) n.k
Madhara ya kutakabari.
Tukiwa watu wa kutakabari Tutaanguka kama walivyoanguka wana wa Israeli na wengine wote waliokuwa wakitakabari katika biblia..
Mithali 16: 18 “Kiburi hutangulia uangamivu; Na roho yenye KUTAKABARI hutangulia MAANGUKO”.
Bwana atusaidie tusiwe na roho ya kutakabari..bali tuwe wanyenyekevu kama Bwana wetu Yesu Kristo alivyokuwa..
Kama hujaokoka na ungependa kufanya hivyo leo..basi utakuwa umefanya uamuzi bora ambao hutaujutia maisha yako yote.. Fungua hapa kwa msaada wa sala ya Toba >> SALA YA TOBA
Shalom.
Tafadhali washirikishe na wengine, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Kwanini Mungu alisema hakuna mtu awazaye kuuona uso wake akaishi?
Utauliza je! Shetani ana uwezo wa kuzuia majibu ya maombi?. Jibu ni ndio!.
Kwanza ni muhimu kufahamu kuwa shetani kamwe hana uwezo wa kuzuia maombi kumfikia Mungu..Maombi yeyote yale mtu anayoomba, yanapanda juu kwa Mungu moja kwa moja..Lakini kitu pekee ambacho shetani anachoweza kufanya ni kuzuia majibu ya Maombi..
Tunaona jambo hili kipindi cha Nabii Danieli..
Danieli 10:12 “Ndipo akaniambia, Usiogope, Danielii; kwa maana tangu siku ile ya kwanza ulipotia moyo wako ufahamu, na kujinyenyekeza mbele za Mungu wako, maneno yako yalisikiwa; nami nimekuja kwa ajili ya maneno yako.
13 Lakini mkuu wa ufalme wa Uajemi alinipinga siku ishirini na moja; bali, tazama, huyo Mikaeli, mmoja wa hao wakuu wa mbele, akaja kunisaidia; nami nikamwacha huko pamoja na wafalme wa Uajemi”
Mkuu wa Uajemi, biblia inayomzungumzia hapo, ni Pepo lililowekwa kuwa kuu juu ya ufalme wa Uajemi..Hivyo kazi zote za giza zilizokuwa zinaendelea katika Taifa hilo la uajemi zilikuwa zinaratibishwa na pepo hilo.
Lakini utasoma hapo, Tangu siku ile ya kwanza tu Danieli alipotia moyo wake ufahamu, (yaani maana yake alipoanza kufikiria mambo ya kuomba)..tayari mawazo hayo yalishamfikia Mungu kama maombi..Na tayari majibu yalishatolewa..lakini Malaika yule alipokuwa anarudisha majibu kwa Danieli alizuiliwa na pepo hilo la Uajemi.
Sasa hivyo ndio vita vinavyoendelea hata sasa.. Vita vya Malaika wanaotuhudumia dhidi ya majeshi ya mapepo..Na vita hivyo si vingine zaidi ya vile vya hoja!..
Maana yake ni kwamba..Bwana anapoachilia majibu ya wewe kupata jambo fulani..shetani anakimbilia kupeleka hoja za mashitaka dhidi yako.. Anamwambia Bwana huyu mtu hastahili kupokea hicho unachompa kwasababu ana tabia hii, hii na ile…jana tu katoka kuiba, juzi katoka kuzini na wala hajatubu…Na wewe neno lako linasema husikii maombi ya waovu!..iweje umsikie na kumpa huyo kitu hicho?..Na mashitaka mengine mengi, anayapeleka mbele za Mungu kuhusu wewe.. Sasa mashitaka hayo kama ni ya kweli, basi Mungu hana upendeleo, shetani anashinda dhidi yako…Hivyo malaika yule aliyepewa jukumu la kukuletea baraka zako, anakuwa hawezi kukufikishia kile ulichoomba kutokana na kwamba umeonekana hustahili kukipokea kile kitu, kutokana na mashitaka ya shetani..
Ndivyo biblia inavyosema..
1Petro 5: 8 “Mwe na kiasi na kukesha; kwa kuwa MSHITAKI WENU IBILISI, kama simba angurumaye, huzungukazunguka, akitafuta mtu ammeze”.
Hapo inasema “mshitaki wenu” na si “mshindani wenu”..Maana yake kazi yake kubwa ni kutushitaki.. Na pia biblia inazidi kutufundisha jambo hilo hilo katika…
Ufunuo 12:10 “Nikasikia sauti kuu mbinguni, ikisema, Sasa kumekuwa wokovu, na nguvu, na ufalme wa Mungu wetu, na mamlaka ya Kristo wake; kwa maana ametupwa chini mshitaki wa ndugu zetu, YEYE AWASHITAKIYE MBELE ZA MUNGU WETU, MCHANA NA USIKU ”
Hivyo ni muhimu kufahamu kila kitu KIOVU tunachokifanya ni POINT kubwa kwa shetani, kwa ajili ya kutuzuilia maombi yetu na baraka zetu siku za mbeleni.
Na sio tu mambo mabaya tunayofanya ni POINT kwa shetani, hata mazuri tunayofanya bado shetani hatachoka kutushitaki kupitia hayo hayo mazuri…ndicho kilichomtokea Danieli pamoja na Ayubu Mtumishi wa Mungu..
Ayubu 1:6 “Ilikuwa, siku moja ambayo hao wana wa Mungu walikwenda kujihudhurisha mbele za Bwana, Shetani naye akaenda kati yao.
7 Bwana akamwuliza Shetani, Umetoka wapi wewe? Ndipo Shetani akamjibu Bwana, na kusema, Natoka katika kuzunguka-zunguka duniani, na katika kutembea huku na huku humo.
8 Kisha Bwana akamwuliza Shetani, Je! Umemwangalia huyo mtumishi wangu Ayubu? Kwa kuwa hapana mmoja aliye kama yeye duniani, mtu mkamilifu na mwelekevu, mwenye kumcha Mungu na kuepukana na uovu.
9 Ndipo Shetani akamjibu Bwana, na kusema, Je! Huyo Ayubu yuamcha Bwana bure?
10 Wewe hukumzingira kwa ukigo pande zote, pamoja na nyumba yake, na vitu vyote alivyo navyo? Kazi za mikono yake umezibarikia, nayo mali yake imeongezeka katika nchi.
11 Lakini nyosha mkono wako sasa, uyaguse hayo yote aliyo nayo, naye atakukufuru mbele za uso wako.
12 Bwana akamwambia Shetani, Tazama, yote aliyo nayo yamo katika uwezo wako; lakini usinyoshe mkono wako juu yake yeye mwenyewe. Basi Shetani akatoka mbele za uso wa Bwana”.
Unaona na hapo?..Ayubu anatenda mema lakini bado shetani hakuacha kumchochoe Mungu amuangamize..
Ayubu 2: 3 “Bwana akamwuliza Shetani, Je! Umemwangalia huyo mtumishi wangu Ayubu? Kwa kuwa hapana mmoja aliye kama yeye duniani, mtu mkamilifu na mwelekevu, mwenye kumcha Mungu na kuepukana na uovu; naye hata sasa anashikamana na utimilifu wake, UJAPOKUWA ULINICHOCHEA JUU YAKE, ILI NIMWANGAMIZE PASIPOKUWA NA SABABU”.
Hapo Bwana alimletea Ayubu mabaya kwa uchochozi wa shetani ijapokuwa Ayubu alikuwa mkamilifu, hebu jiulize kwa mtu ambaye sio mkamilifu, mzinzi, mwasherati, msengenyaji, mtukanaji n.k ni Mashitaka mangapi mabaya yanapelekwa mbele za Mungu na shetani dhidi yake??..
Hivyo ni muhimu kufahamu hilo kwamba shetani anao uwezo wa kuzuia majibu ya maombi yetu kwa njia hiyo.
Hivyo suluhisho pekee ili maombi yetu yasizuiliwe ni KUWA WAKAMILIFU MBELE ZA MUNGU KAMA AYUBU… Ndio ni kweli, Bwana alisikiliza uchochezi wa shetani na kumletea Ayubu yale majaribu, lakini haimaanishi kwamba kila uchochozi shetani anaoupeleka sasa kwa Mungu dhidi yetu, basi Mungu atausikiliza kama alivyousikiliza wa Ayubu, kama tukiwa wakamilifu. La Mwingi anaukataa kwasababu ni wakamilifu mbele zake, na zaidi ya yote anatuletea baraka badala ya mabaya shetani anayotutakia.
Lakini tusipojitahidi kuwa wakamilifu, kwa kuzishika amri zake na kuliishi Neno lake, basi tufahamu kuwa majibu ya maombi yetu yatakuwa ni ndoto, na badala yake tunaweza kupata matatizo badala ya baraka, kwasababu shetani yupo kutushitaki…
NA NI UKAMILIFU UPI AMBAO UTATUSAIDIA KUPATA MAJIBU YA MAOMBI YETU.
2. Kwa kuwa waombaji (Yohana 14:13, 1 Wathesalonike 5:17, Luka 22:40).
Na mengine yanayohusiana na mambo hayo… Tukiyafanya hayo, basi tunao uhakika wa maombi ya majibu yetu kutufikia, bila kuzuiwa na mamlaka ya giza. Na pia kama tuna uhakika kwamba tunayafanya hayo, basi tuombe kwa ujasiri na Imani, pasipo mashaka…
Na pia kumbuka sio kila jibu la ombi linalokawia ni limezuiliwa na shetani.. Hapana!..Mengine hayajazuiliwa isipokuwa wakati wake wa majibu bado haujafika…Ukifika wakati jibu litakufikia tu!. Ni sawa na mwanafunzi anayemwomba Mungu awe daktari, hawezi kupata jibu la ombi hilo siku ile anayoomba, kashasikiwa maombi yake lakini hana budi kupitia madarasa fulani ambayo yatamjenga ili wakati utakapofika wa kupokea jibu la ombi lake, awe kashaandaliwa kielimu vya kutosha, ndio hapo inaweza kumchukia hata miaka 15 mbeleni, mpaka hicho alichomwomba Mungu kitimie (sasa huo ni mfano tu!).. Na maombi mengine ni hivyo hivyo, unaweza kumwomba Mungu leo, usikipate hicho kitu leo leo..kikaya kutokea baadaye sana, baada ya Mungu kukuaandaa vya kutosha. Hivyo ni muhimu kulijua pia hilo.
Bwana atubariki na kutusaidia.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
FAIDA ZA MAOMBI.
FAIDA ZA MAOMBI YA USIKU
Je! kuna maombi yoyote ya kumtoa mtu aliyekufa kwenye mateso ya kuzimu?
MUNGU HANA MBARAKA MMOJA TU!..MWAMINI.
TUMEPEWA, SI KUMWAMINI TU KRISTO, ILA NA KUTESWA KWA AJILI YAKE;
Sala ya Uponyaji/Maombi ya uponyaji
Nakusalimu katika jina la Bwana Yesu Kristo.
Kusudi lingine kuu tukiachilia mbali lile la wokovu wa roho zetu ambalo lilimfanya Bwana Yesu aache enzi na mamlaka na ukuu kule mbinguni ashuke duniani, lilikuwa ni kutuponya na miili yetu pia.
Luka 4:18 “Roho wa Bwana yu juu yangu, Kwa maana amenitia mafuta kuwahubiri maskini habari njema. Amenituma kuwatangazia wafungwa kufunguliwa kwao, Na vipofu kupata kuona tena, Kuwaacha huru waliosetwa”,
Mathayo 8: 17 “Mwenyewe aliutwaa udhaifu wetu, Na kuyachukua magonjwa yetu”.
Isaya 53:4 “Hakika ameyachukua masikitiko yetu, Amejitwika huzuni zetu;..”
Ni Yesu peke yake, ndiye mwenye uwezo wa kuyaondoa magonjwa yetu yote moja kwa moja, hakuna mwingine anayeweza kufanya hivyo, na ndio maana tunamtumaini yeye. Na ni mapenzi yake kuwa sisi tuponywe(Soma Mathayo 8:2-3). Inawezekana wewe unayeusoma ujumbe huu, upo katika hali mbaya wakati huu, inawezekana upo mahutihuti hospitalini,au umekuwa ukisumbuliwa na huo ugonjwa kwa muda mrefu, umejaribu kwenda huko na kule bila kupata mafanikio yoyote, umepoteza fedha nyingi kwa ajili ya matibabu lakini hakuna matumaini yoyote. Pengine hata ulishahudhuria katika nyumba za maombi lakini bado hali yako ipo palepale, nataka nikuambie usivunjike moyo, hilo bado halimfanyi Yesu asikuponye ugonjwa wako.
Inawezekana unao ugonjwa wa siri, na unaogopa hata kuwaeleza watu, inawezekana umepata ugonjwa usioponyeka, Umepata Ukimwi, au Kansa, au Kisukari, n.k. Nataka nikuambie hayo yote si kitu kwa Bwana Yesu.
Kama Yesu alifanya muujiza wa kuuponya mwili wa mtu ambaye alikuwa ameshakufa kwa ugonjwa mbaya sana(Lazaro) na mwili wake ulikuwa tayari umeshaanza kutoa mafunza kaburini, lakini akauridisha na ukiwa mzima bila shida yoyote.. Si zaidi wewe ambaye bado hata hujafa, bado hata mwili wako hujaanza kutoa mafunza? Atakuponya.
Anachotaka kwako ni kuamini tu! Basi.
Na imani inakuja kwa kusikia, hicho ndicho chanzo cha Imani, (Warumi 10:17) Unapolisoma Neno lake, imani inajengeka, unasoma shuhuda mbalimbali za jinsi Bwana alivyowaponya watu katika maandiko ndipo imani yako kwake inavyojengeka, na kuwa kubwa zaidi,
Unaweza kufungua masomo haya, na shuhuda hizi mbili tatu, zitakusaidia kuiimarisha imani yako;
Zaburi 107:19 “Wakamlilia Bwana katika dhiki zao, Akawaponya na shida zao”.
Sala ya Uponyaji/Maombi ya uponyaji
Lipo kusudi la Mungu kukufikisha katika ukurasa huu kwa wakati huu; Kwa baada ya maombi haya mafupi ambayo tutakwenda kuomba pamoja amini kuwa kuna tendo linakwenda kutendeka ndani yako kuanzia huu wakati;
Tunapokwenda kuomba pamoja nataka mahali ulipo, weka mkono wako katika eneo la ugonjwa lilipo. Kisha zungumza maneno haya:
Bwana Yesu, wewe ni mponyaji wangu. Ulisema unalituma Neno lako ili uniponye(Zab 107:20).. Na pia ulisema Neno lako li hai tena lina nguvu, tena lina ukali kuliko upanga wowote ukatao kuwili (Waebr 4:12). Hivyo Bwana Yesu mponyaji wangu, naomba sasa ulitume Neno lako ndani ya mwili wangu likafanye uponyaji. Likaondoe magonjwa yote haya yanayonisumbua (yataje). Likakate kate kazi zote za ibilisi zilizopangwa ndani ya mwili wangu. Nikawe mzima kabisa sawasawa na maneno yako uliyosema katika Yeremia 30:17 ..kwamba utanirejesha afya yangu na kuniponya jeraha zangu. Naiita afya yangu sasa sawasawa na ahadi zako kwa jina la Yesu Kristo, nauita uzima wangu kwa jina la Yesu Kristo.
Asante Mungu wangu kwa upendo wako, na kwa uponyaji wako. Amen.
Basi ikiwa umeomba sala hiyo fupi: Hapo hapo na mimi nitakwenda kukuombea.
Ee Mungu baba, nakushukuru kwa mwanao huyu ambaye ameona msaada pekee, unatoka kwako na si kwa mtu mwingine yeyote. Baba nakuomba ikiwa ametenda dhambi iliyomstahili ugonjwa huo nakuomba Mungu wangu umsamehe, ikiwa amepata ugonjwa huo kwa nguvu za giza basi leo natangaza mwisho wake, kwa Jina la Yesu Kristo. Naomba kama mtumishi wako, umpe afya yake, ili akajue kuwa hakuna mwingine awazaye kutuokoa sisi isipokuwa wewe YEHOVA, na kwa kupitia ushuhuda huo akapate kwenda kulitangaza jina lako kuu kwa mataifa. Asante kwa uponyaji huo ambao tayari umeshaanza kuingia katika mwili wake. Amen.
Sasa kama nilivyosema, zidi kuamini kuwa tayari Kristo amekuponya. Lakini pia ikiwa bado hujaokoka, (Yaani bado hujampa Yesu Kristo maisha yako) Ni vema ukafanya hivyo sasa. Kwasababu hali nyingine haziwezi kuondoka ndani ya mtu, kama mtu mwenyewe hajaamua kukubaliana na Yule anayekwenda kumponya.
Kumbuka wokovu wa roho yako ni bora zaidi kuliko huo wa mwili wako. Ukiponywa mwili, halafu roho ikaangamia faida yake ni nini? Lakini vikiponywa vyote ni faida jumla jumla. Tukizingatia kuwa hizi ni siku za mwisho na Yesu yupo mlangoni kurudi. Hatuna muda tena kwa kuvumiliana na shetani nyakati hizi za hatari, Hivyo bila kuchelewa, fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba ya kupewa maelekezo mengine >>>> SALA YA TOBA
Bwana akubariki sana.
Kama utahitaji maombezi zaidi, basi wasiliana nasi kwa namba hizi bure, +255 693036618/ +255 789001312
Mada Nyinginezo: