Title Devis

AKIJUA YA KUWA ANA WAKATI MCHACHE TU”.

Ufunuo 12:12 “Kwa hiyo shangilieni, enyi mbingu, nanyi mkaao humo. Ole wa nchi na bahari! Kwa maana yule Ibilisi ameshuka kwenu mwenye ghadhabu nyingi, akijua ya kuwa ana wakati mchache tu”.

Shalom, katika mistari hiyo biblia inatuonyesha kuwa shetani naye anayo kalenda ya muda kichwani pake. Aishi hoe hae tu, kuna kipindi alifanya kazi zake akijua bado kuna muda, lakini kuna wakati ulifikia kwa jinsi mambo yanavyokwenda, na mabadiliko aliyoyaona akajua kabisa kweli  hana  muda tena hapo wa kuchezea, muda aliobakiwa nao ni mchache.

Na sikuzote mtu mwenye majira ya muda kichwani, hata utendaji kazi wake unatofautiana kulingana na majira husika, Kwamfano, wanariadha, pale wanaposikia kengele imelia ya “mzunguko”  wa mwisho, utaona badala wapunguze mwendo kwasababu wamechoka,  kinyume chake utaona ndio wanaongeza kasi, kana kwamba ndio wameanza riadha, kwasababu wanajua hicho ndicho kipindi cha lala salama.

Mwanafunzi ambaye amebakisha wiki moja au mbili mpaka afanye mtihani wake wa kuhitimu, utaona hata usomaje wake katika kipindi hicho unabadilika, ataanza kuzingatia masomo, atakuwa tayari kukesha kila siku kwenye kusoma, mambo ambayo huko nyuma alikuwa hayafanyi kwa nguvu hizo.

Wachezaji mpira, utaona zinapokaribia dakika 5 mpira kuisha, utaona aina ya uchezaji wao nao unabadilika kwa pande zote mbili, ule upande uliofungwa utaona ndio unaongeza mashambulizi zaidi hata Yule kipa ambaye anakaa pale golini muda wote, ataondoka kwenda kuongeza mashambulizi kwa  upande wa pili, ili tu kuhakikisha wanarudisha magoli waliyofungwa.

Halikadhalika, ule upande uliofunga nao, utaacha kupeleka mashambulizi upande wa pili, utaona kwanza kikosi chote kinarudi nyuma, ili kulinda ushindi wao, adui zao wasirudishe magoli. (Sasa huo ni mfano tu, haimaanishi kila kinachofanyika kwenye hiyo michezo kipo sawa).

Ndivyo ilivyo kwa shetani wakati huu wa siku hizi chache alizobakiwa nazo, anaelewa hakuna muda tena wa kuchezea, hivyo kama ni mpira anaucheza kwa nguvu zote, ikiwa umemfunga (yaani umeokoka), atahakikisha mashambulizi atakayokuletea ni mazito, Na kama wewe ni mwenye dhambi,(hapo ni sawa na amekufunga) basi atahakikisha ulinzi atakaoweka ili usiufikie wokovu unakuwa ni mkubwa sana.

Ndugu, vizuizi shetani alivyonavyo leo, watu wasimfikie Mungu ili watubu dhambi zao, sio kama alivyokuwa navyo zamani, na hiyo yote ni kwasababu anajua muda wake ni mchache sana, anajua hivi karibuni mambo yote yanakwenda kuisha, atashikwa na kutupwa katika lile ziwa la moto..Na ndio maana anakusonga uwe busy ni mambo ya kidunia usipate muda wa kumtafakari Mungu,

Anakusonga na Ma-movie na Ma-series kutwa kuchwa uyawaze hayo,  ili muda wako wote uyawaze hayo usipate nafasi ya kuyatafakari maandiko, mwisho ukukute kwa ghafla, ufe uende kuzimu, au uukose unyakuo.

Anakusonga kwenye anasa na starehe, na pombe, na simu, na magroup ya kidunia, ili muda wako mwingi uumalizie huko, usahau kuwa muda uliobakiwa nao ni mchache, kwamba ni wajibu wako sasa kwa muda uliobakiwa nao hapa duniani ni kuhakikisha mbingu huikosi.

Shetani anajua huu ni  muda wa nyongeza tu, dakika 90 zenyewe zilishaisha, lakini sisi tunaishi kama vile ndio tupo dakika za 5 za kwanza, tunasubiria dalili zipi tena ndio tuamini kuwa Yesu yupo mlangoni? Mapigo kama haya ya Corona ndio zile tauni ambazo zilitabiriwa zitaipiga dunia  siku za mwishoni kabisa (Luka 21:11),  na cha kuogopesha zaidi biblia inasema, pale watakaposema mbona kama kuna Amani, ndipo hapo uharibifu utakapowajia kwa ghafla,

Siku moja utaamka asubuhi, utaiona dunia ni nzuri, jua linachomoza kama kawaida, jua linazama, uchumi wa nchi unaimarika, mikataba ya amani inasainiwa, sayansi inazidi kusitawi na kufanya maisha kuwa marahisi zaidi,  una afya njema, una amani, lakini usiku huo huo, kumbe ndio unyakuo unapita..

Hapo ndipo wengi wataanza kujutia muda wao wameutumiaje hapa dunia. Hivyo tunapoina neema ya Kristo inalia ndani yetu leo, tujitahidi tuipokee, kwasababu muda uliobakia kweli ni mchache, Bwana Yesu alisema hivyo, shetani naye anasema hivyo moyoni mwake, na anataka iwe ni siri yake peke yake, ili atushambulie chap chap atumalize aishinde yeye. Lakini sisi tunapaswa tumshinde kwa kuutafuta wokovu kwa bidii.

Hivyo kama wewe  ni mwenye dhambi, leo fanya uamuzi, Tubu dhambi zote kwa kumaanisha kuziacha, kisha, tafuta ubatizo sahihi wa kuzamishwa kwenye maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo, kisha baada ya hapo utapokea Roho Mtakatifu, ambaye ndio muhuri wa Mungu kwako (Waefeso 4:30), kukulinda, kukuongoza, kukufariji, na kukufundisha, hata siku ya unyakuo itakapofika.

Bwana akubariki sana.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618.


Mada Nyinginezo:

HERODE NA PILATO, MAADUI WAWILI WAPATANA.

Baradhuli/Mabaradhuli ni nini au ni nani kwenye biblia?

Juya ni nini kwenye biblia? (Mathayo 13:47)

MATUNDA 9 YA ROHO MTAKATIFU

KALAMU YA CHUMA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Kuota unachimba viazi, mihogo,madini n.k Kuna maanisha nini?

Kuota unachimba viazi, mihogo, vitunguu, karoti, madini n.k Kuna maanisha nini?


Inategemea na maisha unayopitia sasa, ikiwa shughuli zao za mara kwa mara ni za migodini au mashambani hususani katika kazi hizo za kulima viazi, au vyakula vya ardhini, basi ndoto kama hizo kujirudia rudia  ulalapo litakuwa ni jambo la kawaida sana kwasababu biblia inasema ndoto huja kutokana na shughuli nyingi Mhubiri 5:3,

Hivyo kama upo katika mazingira hayo, basi ndoto hiyo usiitilie maanani sana kwasababu haibebi ujumbe wowote wa rohoni, zaidi sana hizo ni ndoto za mwili.

lakini ikiwa sivyo na imekujia kwa namna ya kipekee, yaani kwa uzito Fulani, basi inaweza ikawa ishara ya kuwa Mungu anakufungulia milango ya rizki mbeleni.

Biblia inasema.

Ayubu 28:5 “Katika ardhi ndimo kitokeamo chakula; …”.

Unaona, hivyo ikiwa utakaa katika hali ya kuyatenda mapenzi ya Mungu, basi ipo milango mingi sana, Mungu kakuwekea mbele yako, kwa hicho unachokifanya, na hata zaidi ya hapo. Ni wewe tu kuishi maisha yampendezayo Mungu wako.

Kwa muda wako soma, Kumbukumbuku la Torati sura ya 28 yote uone Baraka Mungu alizowawekea wale wote watakaoyashika maagizo yake kwa bidii.

Hivyo ili na wewe ndoto hizo ziwe kweli, hakikisha kwanza Kristo yupo ndani yako, kama hujaokoka hakikisha una mkabidhi Kristo maisha yako leo, na pia kuanzia huu wakati unaishi maisha kulingana na yeye anachotaka kulingana na Neno lake, baada ya hapo kuwa tayari kwa wema wake kujidhihirisha maishani mwako, lakini nje ya hapo, hilo linaweza lisikufikie kabisa.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618

Au jiunge moja kwa moja whatsapp kwa kubofya chini.

Group la whatsapp  Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Mada Nyinginezo:

KUOTA UNAJIFUNGUA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Konde la Soani ni nini? (Zaburi 78:12,43)

Konde la Soani ni nini?


Soani/konde la Soani ni mji uliokuwa Misri, upande wa mashariki mwa bonde la mto Nile, tazama picha juu. Hili ndio eneo ambalo Musa alionyesha miujiza yote ya Mungu kwa Farao, pale alipomtaka awaaachie huru wana wa Israeli akakataa.

Hivi ni  baadhi ya vifungu vinavyoelezea Neno hilo.

Zaburi 78:11 “Wakayasahau matendo yake, Na mambo yake ya ajabu aliyowaonyesha.

12 Mbele ya baba zao alifanya mambo ya ajabu, Katika nchi ya Misri, konde la Soani.

13 Aliipasua bahari akawavusha; Aliyasimamisha maji mfano wa chungu”.

 

Zaburi 78:42 “Hawakuukumbuka mkono wake, Wala siku ile alipowakomboa na mtesi.

43 Alivyoziweka ishara zake katika Misri, Na miujiza yake katika konde la Soani.

44 Aligeuza damu mito yao, Na vijito wasipate kunywa”.

 

Hesabu 13:22 “Wakapanda katika Negebu, wakafika Hebroni; na Ahimani, na Sheshai, na Talmai, wana wa Anaki, walikuwako huko. Nao Hebroni ulijengwa miaka saba kabla ya Soani wa Misri”.

Vifungu vingine ni Isaya 19:11,13, Ezekieli 30:14.

Tazama chini maana ya maeneo mengine katika biblia.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Mto Frati upo nchi gani, Umuhimu wake katika biblia ni upi?

WAKATI WA BWANA KUKUVUSHA, NI LAZIMA ARUHUSU JESHI LA ADUI KUNYANYUKA.

PARAPANDA ITALIA.

NAO WALIOKUWA WAMEKUSUDIWA UZIMA WA MILELE WAKAAMINI.

RUDI KUMPA MUNGU UTUKUFU.

UFUNUO: Mlango wa 19

Rudi Nyumbani:

Print this post

Nasaba ni nini kibiblia?(1Nyakati 9:1, Tito 3:9)

Nasaba ni nini kibiblia?


Ni mfululizo wa majina ya watu au watawala  katika ukoo mmoja, Kwamfano kitabu cha Mathayo sura ile ya kwanza kinaonyesha nasaba ya Bwana wetu Yesu Kristo (yaani ukoo wake tangu Ibrahimu mpaka kuzaliwa kwake), Na kile cha Luka sura ya tatu kuanzia mstari wa 23-38, kinaeleza ukoo wake tangu kuumbwa kwa Adamu, yaani huyu alimzaa huyu, na huyu akamzaa huyu,  hivyo hivyo mpaka vizazi vyote vipite hapo katikati. Hiyo ndio maana ya Nasaba.

Wana wa Israeli nao pia walihesabiwa kwa nasaba,

Na hivi ni baadhi ya vifungu ambavyo utakutana na neno hilo;

1Nyakati 9:1 “Hivyo Israeli wote walihesabiwa kwa nasaba; na tazama, hizo zimeandikwa katika kitabu cha wafalme wa Israeli; na Yuda wakachukuliwa mateka mpaka Babeli, kwa sababu ya makosa yao”.

1Nyakati 5:1 “Na wana wa Reubeni, mzaliwa wa kwanza wa Israeli; (kwa maana ndiye aliyekuwa mzaliwa wa kwanza, lakini, kwa kuwa alikinajisi kitanda cha babaye, haki yake ya mzaliwa wa kwanza walipewa wana wa Yusufu, mwana wa Israeli; tena nasaba isihesabiwe kwa kuifuata hiyo haki ya mzaliwa wa kwanza”.

Tito 3:9 “Lakini maswali ya upuzi ujiepushe nayo, na nasaba, na magomvi, na mashindano ya sheria. Kwa kuwa hayana faida, tena hayana maana”.

1Timotheo 1:4 “wala wasiangalie hadithi na nasaba zisizo na ukomo, ziletazo maswali wala si madaraka ya Mungu yaliyo katika imani; basi ufanye hivyo”.

Soma pia,

1 Nyakati 5:7, 9:22 2Nyakati 12:15, 31:16,17,19, Ezra 2:62,8:2.

Hata sisi pia tunahesabiwa kwa nasaba rohoni, pale unapomletea mmoja kwa Kristo, mbinguni inarekodi kuwa huyo ni mwana wa wako uliyemzaa kwa Bwana, na Yule uliyemzaa akakomaa akaenda kumleta mwingine kwa Kristo, anaonekana kuwa yeye ndiye aliyemzaa, hivyo hivyo, lakini chanzo ni wewe.

Na hiyo inafanya jina lako liwe kubwa katika ufalme wa mbinguni, kulingana na Nasaba yako.

Je! Na sisi tunayo juhudu katika kumzalia Mungu matunda?. Kama hatuna tunapaswa tuanze ili tujijengee daraja zuri mbinguni.

Shalom.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tazama tafsiri ya maneno mengine chini.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618.

Mada Nyinginezo:

Marijani ni nini katika biblia(Ayubu 28:18,Mithali 8:11)?

Rangi ya kaharabu ni ipi kibiblia(Ezekieli 1:4,27,8:2)?

NINI MAANA YA SISI KUWA WATOTO WA MUNGU?

UCHAWI WA BALAAMU.

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

MAONO YA NABII AMOSI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Kabari ni nini kwenye biblia?(Yoshua 7:21,24)

Kabari ni nini?


Kabari ni ni kipande kikubwa cha kitu Fulani aidha mbao, chuma,  dhahabu, shaba n.k.. (donge)

Katika biblia tunaona wana wa Israeli walipoingia nchi ya ahadi na kuwepo maagizo kuwa vitu vyote vya thamani watakavyovikuta kule vitatolewa wakfu kwa Bwana(Yoshua 6:19), lakini tunaona walipofika kulikuwa na mtu mmoja aliyeitwa Akani, mwana wa Karmi, huyu alipofika tu aliyeingiwa na tamaa, pale alipoona vitu vya thamani, ikiwemo hizi kabari (vipande) vya dhahabu, hakuvithaminisha kwa Bwana, bali alikwenda kuvificha(Yoshua 7:11).

Akasababisha mpaka taifa zima la Israeli kupigwa na kufadhaishwa mbele ya maadui zao. Hiyo ikawafanya wapepeleze tatizo ni nini, ndipo walipogundua kuwa ni huyu Akani ameficha baadhi ya vitu vya thamani walivyovikuta kule, hivyo wakamkamata na kumuua.

Yoshua 7:21 “Nilipoona katika nyara joho nzuri ya Babeli, na shekeli mia mbili za fedha, na kabari YA DHAHABU, uzani wake shekeli hamsini, basi nalivitamani nikavitwaa; tazama, vimefichwa mchangani katikati ya hema yangu, na ile fedha chini yake…..

24 Kisha Yoshua, na Israeli wote pamoja naye, wakamtwaa Akani, mwana wa Zera, na ile fedha, na Lile joho, na ile KABARI YA DHAHABU, na wanawe, na binti zake, na ng’ombe zake, na punda zake, na kondoo zake, na hema yake, na vitu vyote alivyokuwa navyo, wakavileta juu hata bonde la Akori”.

Hiyo inatufundisha nini? Inatufundisha kuwa tusiwe na tamaa ya mali ikiwa sisi ni watoto wa Mungu, kwani haitatugharimu maisha yetu tu, bali itagharimu kama sio kuathiri na maisha ya wengine pia. Na ndio maana biblia inasema,

1Timotheo 6:10 “Maana shina moja la mabaya ya kila namna ni kupenda fedha; ambayo wengine hali wakiitamani hiyo wamefarakana na Imani, na kujichoma kwa maumivu mengi”.

Bwana atusaidie, tupende kujikusanyia  zaidi kabari za ufalme wa mbinguni kuliko hizi za hapa duniani..Kwani za hapa duniani ni za kitambo tu, lakini zile zinadumu milele.

Shalom.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tazama tafsiri ya maneno mengine chini.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618.

Mada Nyinginezo:

Mkatale ni nini katika biblia? (Matendo 16:24)

Daawa ni nini kama tunavyosoma katika biblia?

Kwanini Yesu Kristo ni mwana wa Adamu?

FANYIKA SIPORA WA KRISTO, UNYAKUO UPO KARIBU.

JIEPUSHE NA UNAJISI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

RUDI KUMPA MUNGU UTUKUFU.

Kuna tofauti ya kumpa Mungu utukufu na kumshukuru Mungu. Mungu anapokufanyia jambo zuri, lakukupa faraja na furaha, na moyoni ukafurahi, ni kawaida ya kila mwanadamu mwenye moyo wa shukrani, huwa anakwenda kupiga magoti na kumshukuru Mungu wake kwa alilomtendea aualiyomtendea, na zaidi sana huwa anaambatanisha hata na sadaka yake ya shukrani.

Sasa hilo ni jambo moja ambalo linampendeza sana Mungu wetu, pale tunapomshukuru, lakini lipo lingine linalompendeza pia ambalo litatufungulia milango ya baraka mara mbili. Na jambo hilo si lingine zaidi ya KURUDI KUMPA MUNGU UTUKUFU.

Kurudi kumpa Mungu utukufu, ni kitendo cha kurudi na kutangaza kwa wazi, yale yote Mungu aliyokufanyia.. Hivyo Mungu wako anakuwa anatukuzwa katikati ya watu.

Ni jambo linalodharaulika na wengi lakini ni la umuhimu sana. Kurudi kumpa Mungu utukufu…Je umeshawahi kurudi kumpa Mungu utukufu kwa jambo lolote jema alilokufanyia?

Hebu tusome hichi kisa maarufu kwenye biblia..

Luka 17:11 “Ikawa walipokuwa njiani kwenda Yerusalemu, alikuwa akipita katikati ya Samaria naGalilaya.

12 Na alipoingia katika kijiji kimoja, alikutana na watu kumi wenye ukoma; wakasimama mbali,

13 wakapaza sauti wakisema, Ee Yesu, Bwana mkubwa, uturehemu!

14 Alipowaona aliwaambia, Enendeni, mkajionyeshe kwa makuhani. Ikawa walipokuwa wakiendawalitakasika.

15 Na mmoja wao alipoona kwamba amepona, alirudi, HUKU AKİMTUKUZA MUNGU KWA SAUTİ KUU;

16 akaanguka kifudifudi miguuni pake, akamshukuru; naye alikuwa Msamaria.

17 Yesu akajibu, akanena, Hawakutakaswa wote kumi? Wale kenda wa wapi?

18 JE! HAWAKUONEKANA WALİORUDİ KUMPA MUNGU UTUKUFU İLA MGENİ HUYU?

19 Akamwambia, Inuka, enenda zako, imani yako imekuokoa”

Waliponywa wote kumi lakini ni huyu mmoja tu ndiye Aliyepaza sauti yake, kwa sauti kuu, akitangaza jinsi alivyoponywa njia nzima, mpaka alipofika kwa Bwana Yesu..Pengine wale 9 walikwenda kutoa sadaka zao za shukrani tu!..Lakini hawakumtukuza Mungu, walakutangaza waliyofanyiwa kwa wazi, kwasababu zao wenyewe, labda waliona aibu, au waliogopa kutengwa, au kuonekana wa kikale…Lakini huyu hakujali hayo, alitangaza kwa watu lililomtokea kuanzia mwanzo hadi mwisho..

Na hivyo likawa ni jambo jema mbele za Mungu..

Je na wewe ulishawahi kurudi kumpa Mungu utukufu?… Bwana alipokuponya ugonjwa ambao ilikuwa ni ngumu kupona, je! Ulishawahi kusimama na kutangazia watu wawili au watatu mambo makuu Mungu aliyokufanyia?..au uliishia kuwatukuza madaktari tu! Kwamba walikupambania lakini hukuwahi kumtaja Mungu maneno yasiyozidi mawili?..Kama ndivyo basi badilika leo.

Je ulishawahi kumpa Mungu utukufu kwa huyo mtoto uliyempata ambaye ulihangaika miaka mingi bila kupata mtoto?..Ni kweli pengine ulitoa sadaka ya shukrani, hiyo ni vizuri…lakini bado haitoshi…Mungu wako anapaswa atukuzwe mbele za watu kwa hicho alichokufanyia.. Inapaswa watu wamwonapo mwanao aliyekupa Mungu, wamfikirie Mungu wako na si daktari wako wala jitihada zako.

Nyumba Mungu aliyokupa, mali alizokupa, afya aliyokupa, uzima anaokupa, cheo alichokupa, elimu aliyokujalia, nguvu alizokupa n.k…Je Mungu wako anatukuzwa katika huo? Au jitihada zako?..Watu wanapaswa wakitazama cheo chako wanakumbuka ushuhuda uliowasimulia wa jinsi Mungu alivyokuweka pale kimiujiza, na sio wanakumbuka jinsi ulivyopambana…Watu wanapokuona leo umesimama ni mzima, wanapaswa wakumbuke ushuhuda uliowaambia jinsi ulivyokuwa hatiani kupona na ukamwomba Mungu na Mungu akakufungulia mlango wa uponyaji… ili Mungu wako atukuzwe kwao.

Watu wanapokuona una hiki au kile..wanapaswa wautafakari uzuri wa Mungu wako, na utukufu wake, kwa utukufu uliomrudishia wakati unavipata hivyo…kila kitu wajue ni Mungu kakusaidia na si nguvu zako.

Na hatumpi Mungu wetu utukufu kwa yale aliyotutendea kwa kuwawekea watesi wetu CD za  mipasho!.. Kwasababu siku hizi zipo nyimbo za dini ambazo hazina tofauti na nyimbo za kidunia (Taarabu)..zimejaa maneno ya kiburi na ushindani. Kwamba Mungu kanitendea hichi ili maadui

zangu waone waumie moyo…Hapana! mpango wa Mungu sio maadui zetu waumie moyo na waone Mungu alichotufanyia halafu basi!. Mungu hatupiganii ili awachome watu mioyo, bali ili awageuze nia zao wamgeukie yeye.

Hivyo ukimpa Mungu utukufu mbele za watu, jinsi inavyopaswa, kwa kutangaza kwa kina ulipotoka na ulipo sasa, na jinsi gani Mungu alivyokuokoa, kwa neema…Wale wanaokusikiliza akili zao zitahama kutoka kushindana na wewe, na kuhamia kumtafakari Mungu wako, na hivyo nao pia wamtamtamani Mungu wako aliyekutendea mambo makuu namna hiyo. Na watakuuliza “nami nifanyaje Mungu anitendee kama alivyokutendea wewe”

Lakini ukianza kuwawekea mipasho, watakuchukia na hawatavutiwa na unachokiamini, hivyo utakuwa nawe pia unaifanya kazi ya ibilisi ya kuwapeleka watu mbali na Mungu, na moyoni ukidhani umemtukuza Mungu kwa nyimbo zako hizo za kiburi na majivuno kumbe ndio unaenda kinyume na mapenzi ya Mungu.

Hivyo Usiache kamwe kurudi kumpa Mungu utukufu kwa jambo lolote lile analokutendea, hata liwe dogo kiasi gani…Nenda kalitangaze kanisani, kalitangaze kwa rafiki zako, kalisimulie kwa ndugu, kalisimulie kwa yoyote yule ambaye utapata nafasi ya kumsimulia..hakikisha tu lengo lako ni Mungu atukuzwe na si wewe utukuzwe, au kujisifu.

Bwana akubariki.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618.

Mada Nyinginezo:

JE KUNA UISLAMU KATIKA BIBLIA?

Mavu ni nini katika biblia?(Kutoka 23:28, Kumb 7:20)

UTAWALA WA MIAKA 1000.

CHAPA YA MNYAMA

WINGU KUBWA LA MASHAHIDI.

BABA YANGU ANATENDA KAZI HATA SASA!.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Hedaya ni nini katika biblia (Zaburi 68:29, Isaya 18:7)?

Hedaya ni nini?


Hedaya ni neno linalomaanisha zawadi. Ni zawadi inayotolewa kuonyesha shukrani,  au kuridhishwa kwa wema Fulani uliofanyiwa au  kwa uzuri wake.

Katika biblia Neno hilo tunaliona katika vifungu vifuatavyo;

Zaburi 68:28 “Ee Mungu, uziamuru nguvu zako; Ee Mungu, uwe hodari uliyetufanyia makuu.

29 Kwa ajili ya hekalu lako Yerusalemu Wafalme watakuletea hedaya”.

Zaburi 76:11 “Wekeni nadhiri, mkaziondoe Kwa Bwana, Mungu wenu. Wote wanaomzunguka wamletee hedaya, Yeye astahiliye kuogopwa”.

Isaya 18:7 “Wakati huo Bwana wa majeshi ataletewa hedaya na watu warefu, laini; Watu watishao tangu mwanzo wao hata sasa; Taifa la wenye nguvu, wakanyagao watu, Ambao mito inakata nchi yao; mpaka mahali pa jina la Bwana wa majeshi,mlima Sayuni”.

Hata sisi leo hii kila mmojawetu analojukumu la kumpelekea Mungu wetu hedaya,

Na tunampelekea kwa njia mbili:

Njia ya kwanza: ni kwa sifa za midomo yetu: Yaani kumsifu na kumwabudu, na kumpa shukrani kwa vinywa vyetu kwa wema wake wote anaotutuendea, na kwa ukuu wake wote alionao ulimwenguni kote.

Njia ya pili: Ni kwa Kumtolea sadaka: Unapotoa sadaka( yaani fedha, mali n.k.), ni unaonyesha shukrani kwa Mungu, kwa kile alichokufanyia, unaonyesha shukrani kwa neema aliyokupa ya uhai, na kila kitu.

Hivyo huo ni wajibu wa kila mmojawetu. Na hiyo ndio tafsiri ya Hedaya kibiblia.

Shalom.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tazama maana nyingine za maneno chini;

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618.

Mada Nyinginezo:

Mkatale ni nini katika biblia? (Matendo 16:24)

Daawa ni nini kama tunavyosoma katika biblia?

 

UHARIBIFU HAUNA KIFUNIKO.

TAFUTA KUIFANYA KAZI YA MUNGU KWA HUDUMA MUNGU ALIYOIWEKA NDANI YAKO.

NA MTU MMOJA AKAVUTA UPINDE KWA KUBAHATISHA, AKAMPIGA MFALME

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita..

CHUKIZO LA UHARIBIFU

Rudi Nyumbani:

Print this post

JE! MAWAZO YAKO UMEYAELEKEZA WAPI HAPA DUNIANI?

Yusufu alipochukuliwa Misri alikuja kuwa mtu mkuu, kama tunavyosoma katika biblia, lakini kilichomtofautisha yeye na ndugu zake mbele za Mungu, sio ule ukuu aliokuwa nao, wala sio kile cheo alichokipata, hapana, bali ni mahali ambapo moyo wake ulikuwepo pindi alipokuwa Misri, utaona japokuwa aliishi kule kwa miaka mingi sana, tangu akiwa kijana mdogo kabisa, lakini moyo wake wote ulikuwa katika nchi ya ahadi ya baba zake, na ndio maana utaona alipokaribia kufa aliwaambia wana wa Israeli, kuwa siku watakapopandishwa kutoka katika nchi ya Misri na Mungu, basi mifupa yake wasiiache kule, bali waibebe mpaka nchi ya kaanani.

Kutoka 13:19 “Musa akaichukua ile mifupa ya Yusufu pamoja naye; maana, alikuwa amewaapisha sana wana wa Israeli, akisema, Mungu hana budi atawajilia ninyi; nanyi mtaichukua mfupa yangu kutoka hapa pamoja nanyi’.

Tofauti na wale watoto wengine 11 wa Yakobo, japokuwa walikaribishwa tu Misri, hawakuwepo kule maisha yao yote, lakini walipofika, waliishi kama ndio nyumbani kwao, mawazo ya kurudi Kaanani hayakuwepo, na ndio maana hata waliposikia habari za Yusufu kuondolewa mifupa yake, hilo halikuwawazisha nao waseme hivyo, kwasababu uzuri wa Misri ulishawaridhisha mioyo yao.

Utaona hiyo tabia Yusufu aliyokuwa nayo aliirithi kutoka kwa baba yake Yakobo, kwani alipokuwa Misri kwa kipindi kifupi, aliwaambia, atakapokufa wahakiishe hawamziki katika nchi ile, bali katika nchi ya Baba zake walizozikiwa (yaani Kaanani).

Mwanzo 49:29 “Akawaamuru, akasema, Mimi ninakwenda kukusanywa pamoja na watu wangu; mnizike pamoja na baba zangu, katika pango iliyomo shambani mwa Efroni, Mhiti;

30 katika ile pango iliyomo shambani mwa Makpela, iliyo mbele ya Mamre katika nchi ya Kanaani, aliyoinunua Ibrahimu pamoja na shamba kwa Efroni Mhiti, pawe milki yake ya kuzikia.

31 Humo walimzika Ibrahimu, na Sara mkewe; humo wakamzika Isaka, na Rebeka mkewe; nami humo nikamzika Lea”;

Unaona, hicho pia ndicho kilichomtofautisha Yakobo kwa Esau.. sikuzote, wana wa urithi, hawatazami ya hapa, bali wanatazama ya mbele, wanaishi kama wapitaji, na mazingira huwa hayawakwamishi hata kidogo kutokuwaza makao yao ya milele, utajiri hauwakwamishi, vyeo vyao vya muda, haviwafanyi wasahau makao yao halisi, hata hali ngumu za kimaisha haziwakwamishi wasiwaze kurejea nchini mwao siku moja.

Na ndicho utakiona pia kwa Danieli, japokuwa alichukuliwa utumwani Babeli, hadi akawa mtu mkuu katika nchi ile ya kipagani, Lakini kila siku (mara tatu kwa siku) alikuwa haachi kuomba dua juu ya Yerusalemu, madirisha yake yalikuwa yamefunguliwa kuelekea Yerusalemu ilipo, mbali sana, maelfu kwa maelfu ya kilometa, lakini aliiwaza kila wakati na kuiombea kana kwamba alikuwa Israeli. Tofauti na wayahudi wote waliochukuliwa utumwani Babeli kwa wakati ule.(Danieli 6:10)

Utamwona Nehemia naye, japokuwa alikuwa ni mnyweshaji wa Mfalme wa Umedi na Uajemi, lakini akili yake yote, na mawazo yake yote, yalikuwa Yerusalemu, akawa anaulizia habari za mji na hekalu linaendeleaje kila wakati, hadi siku moja aliposikia hali ya mji sio nzuri, kuta zake zimeharibiwa, alilia na kufunga na kuomboleza kwa muda mrefu (Nehemia 1)

Watu kama hao wanaonyesha ni kama kwa bahati mbaya tu walikuwepo katika nchi ya ugenini, wengine walitumainia kabla hawajafa wataiona Yerusalemu, lakini mpaka wanakufa hawakuiona, lakini mioyo yao ilikuwa huko.

Waebrania 11:13 “Hawa wote wakafa katika imani, wasijazipokea zile ahadi, bali wakaziona tokea mbali na kuzishangilia, na kukiri kwamba walikuwa wageni, na wasafiri juu ya nchi.

14 Maana hao wasemao maneno kama hayo waonyesha wazi kwamba wanatafuta nchi yao wenyewe.

15 Na kama wangaliikumbuka nchi ile waliyotoka, wangalipata nafasi ya kurejea.”.

Swali Na sisi ambao tunasema ni wapitaji hapa duniani (Kizazi cha watakao nyakuliwa) Je siku zote tunaishi maisha ya kuutafakari urithi wetu wa kimbinguni tuliowekewa, Je tunaitafakari hiyo Yerusalemu mpya ya kimbinguni? Au tunaishi tu hapa duniani kama tumefika?

Shughuli za ulimwengu zinatuzidi mpaka hatuyawazi tena mambo ya mbinguni? hatuwezi kusema tupo busy, zaidi ya Yusufu ambaye dunia nzima alikuwa anaihudumia kwa chakula, na isitoshe alikuwa ni waziri mkuu wa taifa kubwa ulimwenguni, lakini aliiwaza Yerusalemu kiasi cha kukataa kuzikwa kwenye nchi isiyo yake..Sisi hatuwezi kuwa bize zaidi ya Danieli na Nehemia ambao wao walikuwa ni wakuu katika nchi ya Babeli na Umedi, lakini walilia usiku na mchana juu ya Yerusalemu mji wao..wengine mpaka wakaenda kuukarabati.

Lakini sisi tunao mji ulio mkuu kuliko yao. Tunapoishi hapa duniani tukumbuke kuwa, biblia inasema, kule hakitaingia kilicho kinyonge, maana yake ni kuwa hawataingia wasiokuwa na mpango nao, hawataingia ambao hawaulizii habari zake sasa, watakaoingia kule ni wale tu waliostahili kuingia humo, Si kila mtu atauingia huo mji wa kimbinguni, haijalishi utasema leo umeokoka,

Hivyo tuanze sasa kuishi maisha ya kama watu waonaomngojea Bwana wao (Luka 12:36), kwasababu muda tuliobakiwa nao ni mchache sana, Siku ya ukombozi wetu imekaribia, Parapanda wakati wowote italia, kisha tutakwenda mbinguni kwenye karamu ya mwana-kondoo, na baada ya hapo utafuata utawala wa miaka 1000, wakati huo wote tutakuwa tukijiandaa kwa ajili ya mbingu mpya na nchi mpya na hiyoYerusalemu mpya ishukayo kutoka mbinguni.

2Petro 3:13 “Lakini, kama ilivyo ahadi yake, mnatazamia mbingu mpya na nchi mpya, ambayo haki yakaa ndani yake”.

Ufunuo 21:1 Kisha nikaona mbingu mpya na nchi mpya; kwa maana mbingu za kwanza na nchi ya kwanza zimekwisha kupita, wala hapana bahari tena.

2 Nami nikauona mji ule mtakatifu, Yerusalemu mpya, ukishuka kutoka mbinguni kwa Mungu, umewekwa tayari, kama bibi-arusi aliyekwisha kupambwa kwa mumewe.

3 Nikasikia sauti kubwa kutoka katika kile kiti cha enzi ikisema, Tazama, maskani ya Mungu ni pamoja na wanadamu, naye atafanya maskani yake pamoja nao, nao watakuwa watu wake. Naye Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao.

Tukose vyote, tupitwe na vyote, lakini tusikose mambo hayo ambayo biblia inasema jicho halijawahi kuona wala sikio kusikia.

Bwana akubariki.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618.


Mada Nyinginezo:

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA KITABU CHA RUTHU:

WAKATI WA KRISTO KUSIMAMA,UMEKARIBIA SANA.

MAMBO 5 AMBAYO KILA MKRISTO ANAPASWA KUFAHAMU.

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 2

JE! KUNA UCHAWI KATIKA KUTENDA WEMA?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Nini tofauti kati ya Roho Mtakatifu na Roho Takatifu?

JIBU: Roho Mtakatifu na Roho Takatifu ni kitu kimoja, inategemea neno hilo limetumika wapi

Roho wa Mungu anapozungumza ndani yetu, au kutuongoza, au kutufundisha..anakuwa kama ni mtu yupo ndani yetu akifanya hizo kazi..anakuwa kama ni mtu mwingine mpole ndani yetu anazungumza nasi, anatufundisha, anatushauri, anatufariji, anatutia moyo, anatuongoza n.k..Hivyo hiyo tabia ya kuwa kama mtu wa pili ndani yetu, ndiyo inayofanya biblia sehemu zote iitaje Roho ya Mungu, kwa cheo cha uutu. (yaani Roho M-takatifu).

Hali kadhalika, linapokuja suala la tabia ya Roho ya Mungu, ni sahihi kabisa kusema Roho ya Mungu ni Roho Takatifu, ni Roho Nyenyekevu, ni Roho Tulivu, Ni roho Njema (Danieli 5:12) n.k Hapo hatujaivisha uutu lakini tumeielezea sifa yake.

Yapo madhehebu yanayofanya mambo haya yawe magumu kwa maneno hayo mawili, na hata mengine yamebadilisha biblia zao, kila mahali palipoandikwa kwenye biblia neno Roho Mtakatifu, yamebadilisha na kuweka Roho Takatifu..Hivyo kwao ni kosa kutumia neno Roho Mtakatifu mahali popote. Vile vile yapo mengine ni kosa kutumia neno Roho Takatifu. Pasipo kujua kwamba maneno yote mawili ni sahihi, inategemea ni wapi yametumika.

Kumbuka pia ni wajibu wa kila mmoja aliyeokoka kuwa na Roho Mtakatifu.

Mungu atubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

JE WAJUA?

MAKEDONIA.

Roho, Nafsi, na Mwili vina utofauti gani?

Yuko azuiaye sasa hata atakapoondolewa! ni nani huyo?

JE VIBWENGO NI KWELI VIPO?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Mungu anaposema yeye ndiye achunguzaye “viuno na mioyo” anamaanisha nini?

SWALI: Mungu anaposema yeye ndiye achunguzaye “viuno ya mioyo” anamaanisha nini, Je! hivyo viuno ni vipi? Kama tunavyovisoma katika vifungu vifuatavyo;

Yeremia 11:20 “Lakini, Ee Bwana wa majeshi, uhukumuye haki, ujaribuye viuno na moyo, nijalie kuona kisasi chako juu yao; kwa maana nimekufunulia wewe neno langu”.

Yeremia 17: 10 “Mimi, Bwana, nauchunguza moyo, navijaribu viuno, hata kumpa kila mtu kiasi cha njia zake, kiasi cha matunda ya matendo yake”.

Yeremia 20: 12 “Lakini, Ee Bwana wa majeshi, wewe wawajaribu wenye haki, waona viuno na mioyo, nijalie kuona kisasi chako juu yao; kwa maana nimekufunulia wewe neno langu”.

Zaburi 7: 9 “Ubaya wao wasio haki na ukome, Lakini umthibitishe mwenye haki. Kwa maana mjaribu mioyo na viuno Ndiye Mungu aliye mwenye haki”.

Ufunuo 2:22 “Tazama, nitamtupa juu ya kitanda, na hao wazinio pamoja naye, wapate dhiki kubwa wasipotubia matendo yake;

23 nami nitawaua watoto wake kwa mauti. Na makanisa yote watajua ya kuwa mimi ndiye achunguzaye viuno na mioyo.

Nami nitampa kila mmoja wenu kwa kadiri ya matendo yake”.

Ukisoma pia Mithali 23:16 , na Ayubu 31:19 inazungumzia maneno hayo hayo;


JIBU: Mara nyingine biblia inapolitaja Neno viuno haimaanishi tu hivi viuno vya miili yetu tunavyovivalia mikanda, hapana, bali viuno sehemu nyingine linatumika kumaanisha NIA au WAZO, la mtu. Mungu kabla hajambariki mtu au kumuhukumu au kumsamehe huwa anatazama vitu hivyo viwili, cha kwanza ni Moyo na cha pili ni Nia.

Kwamfano, Mungu anaweza kumsamehe mtu dhambi zake bila hata ya kuzungumza maneno yoyote kwenye kinywa chake kuonyesha anaomba msamaha, Yaani ule moyo tu wa kujutia dhambi zake, moyo wa kuugua, moyo wa kusema kosa hili sitakaa nilirudie tena, siku baada ya siku anajutia makosa yake, na hataki kuyatazama wala kuyarudia tena, hiyo tayari ni toba inayozungumza sana mbele za Mungu kuliko sala za toba elfu mtu anazoongozwa kila siku na huku hana majuto na dhambi zake.

Jambo kama hilo utaliona kwa Yule mwanamke kahaba, aliyekwenda kumlilia Yesu, utaona hakuzunguza Neno lolote lakini Bwana Yesu alimwambia umesamehewa dhambi zako. (Luka 7:37-48)

Vilevile Mungu huwa anachunguza Nia, kwa mfano wengi wetu tunamuhukumu Yuda kama ndiye aliyempeleka Yesu msalabani, lakini ukisoma pale utaona Yuda hakuwa na Nia ya Bwana Yesu kufikishwa katika mateso na kusulibiwa na ndio maana akawaomba watakapomchukua wasimtendee dhara lolote (Marko 14:44), kwani yeye lengo lake lilikuwa ni kupata pesa tu..Lakini alipoona wale watu wamevuka mipaka, mpaka kwenda kumsulibisha alijuta kwa kulia sana, hadi ikamfanya aende kujinyonga, kwa madhara aliyosababisha, Hivyo Mungu anayechunguza Nia hatamuhukumu kwasababu alimpeleka Yesu msalabani bali atamuhukumu kwa kosa lingine la kutokuwa na moyo mkamilifu kwake kama ilivyokuwa kwa mitume wenzake.

Huo ni mfano tu,

Hivyo nasi tunapaswa tuwe makini sana, usiende kuzini ukamwambia Mungu nilipitiwa, yeye hashawishiwi kwa maneno , anachunguza moyo na Nia ya mwanadamu zaidi ya fikra zetu. Hivyo tusijidanganye tuna la kujitetea mbele zake, hata Siku ile ya Hukumu (Anachunguza viuno vyetu). Halikadhalika hata ukitenda tendo la haki, huna haja ya kumwambia Mungu, kumbuka hiki kumbuka kile, yeye anajua yote (Mhubiri 5:8).

Bwana atusaidie,

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

Malaika wa maji ni yupi na Je kuna aina ngapi za malaika?

JINSI MUNGU ANAVYOIPIGA NA KUIPONYA AFRIKA.

BWANA WA MAJESHI.

JINSI YA KUSOMA BIBLIA.

Nini maana ya Usiwe mwovu kupita kiasi? (Mhubiri 7:17)

Rudi Nyumbani:

Print this post