Title July 2020

WEWE NI BWANA UNIPONYAYE.

SALA FUPI YA UPONYAJI!

Zaburi 107:17 “Wapumbavu, kwa sababu ya ukosaji wao, Na kwa sababu ya maovu yao, hujitesa.
18 Nafsi zao zachukia kila namna ya chakula, Wameyakaribia malango ya mauti.
19 Wakamlilia Bwana katika dhiki zao, Akawaponya na shida zao.
20 Hulituma neno lake, huwaponya, Huwatoa katika maangamizo yao”.

(Uimbe wimbo huu uliotungwa na Don Moen, kufuatia Zaburi hiyo)

Mimi ni Mungu nikuponyaye,
Mimi ni Bwana mponyaji wako,
Hulituma Neno langu,
Na kukuponya magonjwa yako,
Mimi ni Bwana mponyaji wako.

Wewe ni Mungu,
Uniponyaye,
Wewe ni Bwana Mponyaji wangu,
Hulituma Neno lako,
Na kuniponya magonjwa yangu,
Wewe ni Bwana mponyaji wangu.

Urudie kwa kadri uwezavyo pale Upitiapo misiba, magonjwa na shida..mwambie “Mungu” wewe ni Bwana uniponyaye,.. wewe ni Bwana uniponyaye..wewe ni Bwana mponyaji. Na nguvu uponyaji utashuka juu yako, na kukuponya na magonjwa uliyonayo  au misiba unayopitia.

“Amen”


Mada Nyinginezo:

UPONYAJI WA YESU.

KWA KUPIGWA KWAKE SISI TUMEPONA.

NJIA SAHIHI YA KUMPATA MWENZA WA MAISHA KIBIBLIA.

UFALME WAKO UJE.

JIFUNZE KUJITOA KWA MUNGU NA KUWA MKARIBISHAJI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

JE NI LAZIMA MKRISTO AOE/AOLEWE?

Shalom karibu tujifunze biblia.

Mojawapo wa uhuru Mungu aliompa mwanadamu ni kuoa/kuolewa…Mtu yeyote anayeoa/kuolewa sawasawa na maagizo ya Mungu (yaani ndoa ya mume mmoja na mke mmoja) basi anabarikiwa.

Mathayo 19:4 “Akajibu, akawaambia, Hamkusoma ya kwamba yeye aliyewaumba mwanzo, aliwaumba mtu mume na mtu mke,

5 akasema, Kwa sababu hiyo, mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe; na hao wawili watakuwa mwili mmoja?”.

Lakini Pamoja na hayo sio lazima pia kuoa au kuolewa kwa sababu maalumu.

Kwamfano biblia inasema katika..

1Wakorintho 7:32 “Lakini nataka msiwe na masumbufu. YEYE ASIYEOA hujishughulisha na mambo ya Bwana, ampendezeje Bwana;

33 bali yeye aliyeoa hujishughulisha na mambo ya dunia hii, jinsi atakavyompendeza mkewe.

34 Tena iko tofauti hii kati ya mke na mwanamwali. YEYE ASIYEOLEWA HUJISHUGHULISHA NA MAMBO YA BWANA, APATE KUWA MTAKATIFU MWILI NA ROHO. Lakini yeye aliyeolewa hujishughulisha na mambo ya dunia hii, jinsi atakavyompendeza mumewe”.

Hivyo sababu kuu ya mtu kujizuia kuoa au kuolewa ni ili apate nafasi kubwa ya kujishughulisha na kazi ya Mungu.. Ni kweli Mume au Mke ni msaidizi mzuri pia katika kazi ya Mungu lakini…kuwa kumtumikia Mungu binafsi pia ni vizuri Zaidi.. Kwasababu ukiwa na mke/mume kuna mambo ya kidunia ambayo hautayakwepa…kwamfano vitakuwepo vipindi vya kutunza Watoto, vitakuwepo vipindi vya kutafuta sana vya kidunia ili kuitunza familia na mke au mume. Vitakuwepo vipindi vya kukaa pamoja faragha!..

Huwezi kusema unasafiri miezi 5 mbali na mke/mume wako umeenda kufanya huduma…ni lazima kwa sehemu Fulani utamkwaza tu mwenzako! au utakuwa hujamtendea haki. Na biblia inasema ukishaoa/ukishaolewa..mwili wako ni mali ya mwenzako, huna amri juu ya mwili wako(kasome 1Wakorintho 7:3-5)..Sasa hayo ndio baadhi ya mapungufu katika kuoa/kuolewa.

Lakini usipooa au usipoolewa…utakuwa huru Zaidi..unaweza kufunga safari muda wowote unaotaka kuifanya kazi ya Mungu, unaweza kufunga siku nyingi bila usumbufu, unaweza kwenda kusali mlimani kipindi kirefu au kuhubiri bila kukumbuka una jukumu Fulani umeliacha nyumbani …kadhalika, hutapata usumbufu wa Watoto wanahitaji hiki, wanahitaji kile.. kadhalika hutaishi kwa matakwa ya mtu Fulani, bali kwa kile Mungu anachokuongoza kila mara. Jambo ambalo lina faida katika ufalme wa mbinguni mara dufu kuliko hilo lingine.

Wa kwanza kabisa ambaye tunaona hakuoa na huduma yake iliikuwa na matokeo makubwa sana ni Bwana wetu Yesu. Mwingine ni Paulo ambaye ndiye aliyeandika mistari hiyo hapo juu kwa uwezo wa roho..Paulo hakuwa miongoni mwa Mitume 12 wa Bwana Yesu, lakini alifanya kazi kubwa kuliko hata mitume wa Yesu (kasome1Wakorintho 15:10), na wengine ni Yohana Mbatizaji na Eliya Mtishbi.

Lakini hilo sio lazima na wala sio amri, kwamba kila mtu ni lazima asiolewe/asioe. Ni jinsi mtu aonavyo yeye kwamba anaweza kujizuia au la!…Wapo wanaoweza kujizuia na wapo wasioweza!…Biblia inasema kama huwezi kujizuia ni afadhali uoe/uolewe kuliko kuwakwa na tamaa.

1Wakorintho 7:8 “Lakini nawaambia wale WASIOOA BADO, na wajane, Ni heri wakae kama mimi nilivyo. LAKINI IKIWA HAWAWEZI KUJIZUIA, NA WAOE; maana ni afadhali kuoa kuliko kuwaka tamaa”……

 

1Wakorintho 7:1 “Basi kwa habari ya mambo yale mliyoandika, ni heri mwanamume asimguse mwanamke. 2 Lakini kwa sababu ya zinaa kila mwanamume na awe na mke wake mwenyewe, na kila mwanamke na awe na mume wake mwenyewe”.

Bwana akubariki.

Kumbuka kama unaishi na mwanamke/mwanaume ambaye hamjafunga ndoa..basi mnaishi katika uzinzi!..haijalishi mmeishi miaka mingapi Pamoja, au mmezaa Watoto wangapi..Mnapaswa mkatubu na kufunga ndoa takatifu, mbele ya kanisa la Kristo, ndipo mbarikiwe (na ndoa sio sherehe na matarumbeta)..mmeshaishi miaka yote hiyo, sherehe ya nini tena?..hatua mliyopo ni ya kutubu tu, na kwenda mbele ya kanisa kufungishwa ndoa mbele ya mashahidi na kurudi nyumbani kuendelea na maisha basi haihitaji maandalizi kana kwamba ndio mmketana kwa mara ya kwanza!. Lakini msipofanya hivyo mkifa leo mtahukumiwa, hiyo ni kulingana na maandiko.

Na mwisho kama hujaolewa na unatafuta wa kukuoa..Ni vizuri ukamtafuta kwanza Mwokozi. Kwasababu ukifa leo bila mwokozi utapotea milele, na Zaidi ya yote mbinguni hakuna kuoa wala kuolewa, hayo mambo yataishia humu humu duniani..miili tutakayopewa tukifika kule haina hisia za kimwili. Huko tutaishi na Kristo milele. Hivyo Wokovu ni muhimu na wa kwanza katika Maisha, hayo mengine ndio yafuate.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Bwana alimaanisha nini kusema JIKANE mwenyewe?(Mathayo 6:24)

 MAVUNO NI MENGI

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA WARAKA WA TATU WA YOHANA.

MJUMBE ASIYEKUWA NA UJUMBE.

KUOTA UNASAFIRI.

USIPOKUWA MWAMINIFU, NAFASI YAKO ITACHUKULIWA.

UNYAKUO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

KITABU CHA UCHAWI.

Kabla ya kutafuta kitabu cha uchawi ni vizuri kufahamu kwanza Uchawi asili yake ni wapi.

Wapo watu wengi mitandaoni, wengine ni wachawi kweli, na wengine ni matapeli, wameandika vitabu wanakuambia ununue, na katika vitabu hivyo, wanaorodhesha njia mbalimbali za kutatua matatizo yako, au njia za kuwapiga maadui zao.. Lakini kabla hujafikiria kuungana nao ndugu yangu, ni vizuri kwanza ukafahamu uchawi asili yake ni wapi?

Uchawi ni kitendo cha kwenda kutafuta msaada kutoka katika mamlaka mengine tofuati na yale ya Mungu  ili kutimiziwa malengo Fulani, ya mwilini au rohoni. Na kama tunavyofahamu hakuna mamlaka mengine yaliyo tofauti na Mungu zaidi ya yale ya shetani.

Kwamfano, unapokuwa na uhitaji labda wa mke, na unaona kwa akili zako huwezi kumpata mwanamke umtakaye, hapo inakugharimu kutafuta msaada kutoka katika mamlaka nyingine..

Ndio hapo yanazuka mambo mawili, aidha uende kwa Mungu, au uende kwa shetani, ukienda kwa shetani utapata maagizo Fulani, yanatoka katika kitabu cha kichawi walichonacho, Vivyo hivyo ukienda kwa Mungu utapokea maagizo kutokana na kitabu kitakatifu cha Mungu kiitwacho BIBLIA.

Lakini jambo ambalo watu wengi hawajui ni kuwa, shetani hana lengo lolote zuri  na mwanadamu zaidi ya kumwangamiza, atakupa kwa lengo la kukuangamiza mwisho wa siku, na ukishakufa ni moja kwa moja unakwenda katika moto wa milele..

Zipo shuhuda nyingi za watu waliokwenda kwa waganga, kutafuta msaada wa shetani, lakini mwisho wake wameishia pabaya sana.. Na kibaya zaidi ulimwengu huu wa sasa, watu wengi wanakimbilia humo hawajui kuwa lile ni shimo kubwa sana la mauti..Ambalo ukiingia kutoka huko ni kugumu sana.

Usihatarishe maisha yako, kwa mambo ambayo hayakupeleki popote, Usije ukasema haujaambiwa, kukutana na ujumbe huu ni makusudi kabisa Mungu anakuonya, ikiwa wewe ni mmojawapo unayetafuta kujui kitabu cha uchawi, hizi ni siku za mwisho, biblia inasema hivi..

1Timotheo 4:1 “Basi Roho anena waziwazi ya kwamba nyakati za mwisho wengine watajitenga na imani, wakisikiliza roho zidanganyazo, na mafundisho ya mashetani;”

Unaona, biblia inasema wengi watajitenga na Imani na kusikiliza mafundisho ya mashetani,..Kumbuka Uchawi wa kwanza kabisa ulifanywa na Shetani pale Edeni, Ukitaka kujua uchawi wenyewe ni upi na madhara gani yalitokea baada ya pale..fungua hapa usome..>>>> JINSI WATU WANAVYOZAMA KATIKA USHIRIKINA NA UCHAWI.

Na ndio maana hata katika Israeli Mungu alipiga kabisa marufu watu wanaofanya uchawi, kwasababu alijua madhara yake kwao.

Kumbukumbu 18:9 “Utakapokwisha kuingia katika nchi akupayo Bwana, Mungu wako usijifunze kutenda kwa mfano wa machukizo ya mataifa yale.
10 Asionekane kwako mtu ampitishaye mwanawe au binti yake kati ya moto, wala asionekane mtu atazamaye bao, wala mtu atazamaye nyakati mbaya, wala mwenye kubashiri, wala msihiri,
11 wala mtu alogaye kwa kupiga mafundo, wala mtu apandishaye pepo, wala mchawi, wala mtu awaombaye wafu.
12 Kwa maana mtu atendaye hayo ni chukizo kwa Bwana; kisha ni kwa sababu ya hayo Bwana, Mungu wako, anawafukuza mbele yako.
13 Uwe mkamilifu kwa Bwana, Mungu wako”.

Hivyo ndugu, usifirie kutafuta eti hicho kinachoitwa kitabu cha uchawi, Ni heri utubu dhambi zako leo umgeukie YESU KRISTO, haijalishi wewe utakuwa ni muislamu, au mhindu, vyovyote vile, ukimpa Yesu maisha yako leo atakuokoa na kukupa uzima wa milele. Na atakupa pia vile vitu ambavyo ulikuwa na haja navyo kwa wakati wake.

Hivyo kama upo tayari leo kufanya hivyo, na unahitaji kuyakabidhi maisha yako kwake, basi fungua hapa kwa ajili ya sala ya Toba na Mungu akubariki..>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Pia unaweza pia kufungua na masomo mengine hapa chini ujifunze, naamini yatakutoa sehemu moja hadi nyingine kiroho.

Mada Nyinginezo:

 

Rudi Nyumbani:

Print this post

KIAMA KINATISHA.

Ikiwa leo hii Unyakuo utapita, na wewe ukabaki, basi fahamu dunia itakuwa na miaka 7 tu mbele yako kabla haijaisha, yaani kama leo ni mwaka 2020, basi haitapita mwaka 2027, kabla ya kila kitu unachokiona leo hii kuwa jivu.. Miaka hiyo saba imepatikana kutoka katika ule Unabii wa Danieli wa yale majuma 70, (Danieli 9:24) ambapo mpaka sasa limebakia juma moja tu, lenye miaka 7 kuanza.

Sasa katika hicho kipindi cha miaka 7 dunia haitakuwa tu umestarehe ikisubiria mwisho ufike hapana.. Kutaanza kuwa na mabadiliko ya haraka na ya ghafla sana duniani, jambo ambalo litawashitusha wengi, hapo ndipo ule unabii wa Bwana Yesu unaosema siku hiyo itawajilia kwa ghafla utakapotimia (Luka 21:34-35), kama tu unavyoona huu ugonjwa wa Corona ulivyoijilia hii duniani kwa ghafla bila taarifa, ndivyo itakavyokuwa hicho kipindi.

Miaka hii 7 inajulikana kama miaka ya dhiki, na imegawanyika katika vipengele vikuu viwili, Kipengele cha kwanza, ni cha miaka 3 na nusu, ya kwanza, na cha pili ni miaka 3 na nusu ya mwisho.

Sasa katika hiyo miaka mitatu na nusu ya kwanza, kitakuwa ni kipindi cha mpinga-kristo, kujiimarisha, na kuingia agano na watu(mataifa mengi),Danieli 9:27, ikiwemo taifa la Israeli,.na wakati wa watu kupokea chapa. Lakini wakati huo huo Wale manabii wawili (Mashahidi 2), tunaowasoma katika ufunuo 11, watasimama kuihubiria Israeli, kwa muda huo wa miaka mitatu na nusu ya kwanza,.Injili yao haitakuwa ya maneno matupu tu, bali itafuatana na mapigo kadha wa kadha mwishoni mwishoni karibia na kumaliza ushuhuda wao, soma Ufunuo 11, mapigo hayo yatakuwa ni makali na ya kutesa kiasi kwamba siku mpinga-Kristo atakapowaua, dunia nzima itafurahia tukio hilo na kuepelekeana zawadi wao kwa wao.

Sasa hiyo miaka 3 na nusu ya mwanzo itakapokwisha, Mpinga-Kristo atakuwa ameshapata nguvu za kutosha, wakati huo, ndio atanyanyuka sasa, kuleta dhiki kuu juu ya wale wote ambao hawatakuwa na chapa/Utambulisho wake (666).. Hapa hatanusurika mwanadamu yeyote ulimwenguni aliyeikwepa chapa hiyo, kutakuwa na mawili aidha upokee chapa, au ufe.. Na kifo sio cha kupigwa risasi au kunyongwa…Ni heri ingekuwa hivyo!…lakini kifo watakachokufa wale walioikataa chapa kitakuwa ni cha kuteswa mda mrefu sana…Watu watateswa hata kwa mwaka mmoja au miwili bila kuruhusiwa wafe…Ni mateso ya kuwekwa kwenye kambi maalumu za mateso..yale ya kale ambayo unatolewa macho, unavuliwa nguo, wakati wa baridi..halafu unafanyishwa kazi ngumu, huku unapewa mlo mmoja kwa wiki,(na mlo wenyewe ni supu tu) na huku unachapwa na viboko, yatakuwa ni mateso madogo sana…Watu watatamani wafe huko lakini hawatakufa..watateseka katika hiyo hali hata kwa miaka miwili ndio uje wafe!…

Bwana Yesu alisema dhiki hiyo ambayo itakuja kutokea haijawahi kutokea tangu dunia iumbwe na wala haitakaa itokee tena baada ya hapo.. Kiasi kwamba watakaowezi kuyastahimili hayo watakuwa ni watu wachache sana, wengine wote wataipokea chapa ya mnyama. Na jambo hilo litaendelea kwa muda wote wa miaka mitatu na nusu ya mwisho.

Hapo katika kutakuwa ni mapigo mengine mengi sana, mapigo ya baragumu saba yataendelea..na mapigo ya vitasa saba vya Mungu nayo pia yatafuata, mwishoni mwa miaka mitatu na nusu, kwa urefu wa somo hili fungua hapa >> SIKU YA BWANA INAYOTISHA YAJA!..hatuwezi kueleza yote hapa sehemu moja.

Sasa mwisho kabisa ya dhiki hizo kupita, unaweza kudhani, mambo ndio yamekwisha?, Wale waliopokea chapa, basi wamepona,? Hapana, ndugu kinyume chake huo ndio mwanzo wa ukurusa mwingine ujulikanao kama SIKU YA BWANA.

Hii siku ya Bwana, itakuwa ni kipindi cha siku 30 nyingine juu ya ile miaka saba kupita…Watu watadhani kuipokea chapa ndio kupona, lakini ni sawa na mtu aliyemkimbia Simba akakutana na dubu biblia inasema hivyo..ni heri wangekufa kwenye dhiki kuu ya mpinga-Kristo.

Amosi 5:18 “Ole wenu! Ninyi mnaoitamani siku ya Bwana; kwani kuitamani siku ya Bwana? Ni giza, wala si nuru.

19 Ni kama mtu aliyemkimbia simba, akakutana na dubu; au aliingia katika nyumba akauegemeza mkono wake ukutani, nyoka akamwuma”.

Hichi kipindi watakaokuwepo duniani hawataamini macho yao, watashikwa na butwaa la ajabu, kwasababu, watashuhudia hii dunia ikigeuzwa na kuwa kama mojawapo ya sayari Fulani huko angani isiyokaliwa na watu, Kwasababu hili jua tunaloliona litazimwa lote, (kutakuwa na giza kubwa) mwezi utakuwa mwekundu kama damu, nyota zote zitaondoka huko mbinguni kutakuwa na giza tororo ambalo halijawahi kutokea duniani…

Amosi 5:20” Je! Siku ya Bwana haitakuwa giza, wala si nuru? Naam, yenye giza sana, wala haina mwanga”.

Lengo la siku hiyo ya Bwana, ni kuifanya dunia kuwa ukiwa kama tulivyoikuta siku ile ya uumbaji..Mwanzo 1:1 “Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi. NAYO NCHI ILIKUWA UKIWA, TENA UTUPU, NA GIZA lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji”

Hivyo dunia itafanywa ukiwa tena..

Isaya 13:9 “Tazama, siku ya Bwana inakuja, siku kali, ya hasira na ghadhabu kuu, ILI IIFANYE NCHI KUWA UKIWA, na kuwaharibu watu wake, wenye dhambi, wasikae ndani yake.

10 Maana nyota za mbinguni na matangamano havitatoa nuru yake; jua litatiwa giza wakati wa kucha kwake, na mwezi utaacha nuru yake isiangaze.

11 Nami nitaadhibu ulimwengu kwa sababu ya ubaya wake, na wenye dhambi kwa sababu ya hatia yao; nami nitaikomesha fahari yao wenye kiburi; nami nitayaangusha chini majivuno yao walio wakali;

12 nitafanya wanadamu kuadimika kuliko dhahabu safi, na watu kuliko dhahabu ya Ofiri”.

Siku hii itaambatana na tetemeko kubwa la Ardhi ambalo halijawahi kutokea tangu dunia iumbwe, visiwa vitahama,..

Ufunuo 16:18 “Pakawa na umeme na sauti na radi; na palikuwa na tetemeko la nchi kubwa, ambalo tangu wanadamu kuwako juu ya nchi hapakuwa namna ile, jinsi lilivyokuwa kubwa tetemeko hilo.

19 Na mji ule mkuu ukagawanyikana mafungu matatu, na miji ya mataifa ikaanguka; na Babeli ule mkuu ukakumbukwa mbele za Mungu, kupewa kikombe cha mvinyo ya ghadhabu ya hasira yake.

20 Kila kisiwa kikakimbia, wala milima haikuonekana tena.

21 Na mvua ya mawe kubwa sana, ya mawe mazito kama talanta, ikashuka kutoka mbinguni juu ya wanadamu. Wanadamu wakamtukana Mungu kwa sababu ya lile pigo la mvua ya mawe; kwa maana pigo lake ni kubwa mno”.

Unaona, tutakayokuwa yanaendelea kwenye hii dunia wakati huo?? Ndugu kuna vifungu vingi sana vya kuandika hapa,vinavyoilezea hii siku ya kuogofya ya Bwana, lakini hatuwezi kuviorodhesha vyote, kwa muda wako pitia vifungu hivi (Yoeli 1:15, Yoeli 2:1, 2:11, Yoeli 3:14),

Sasa baada ya hayo kupita, Ndipo Kristo atatokea mawinguni, Na kila jicho litamwona, naye atawaua waliosalia na majeshi yao, na kumaliza kila kitu, wale waovu waliosalia (Mathayo 24:29-30, Ufunuo 19:11-21)..

Na baada ya hapo kutakuwa ni siku nyingine 45, juu ya zile siku 30, ambapo ndani ya siku hizo, wafu watafufuliwa watawale pamoja na yeye, pamoja na ile hukumu ya mataifa ya kuwatenga kondoo na mbuzi, na katika kipindi hicho hicho Kristo ataitengeneza tena hii dunia upya, Nayo itakuwa nzuri zaidi ya Edeni, nasi tutawala naye kwa kipindi kingine cha amani cha miaka 1000, wakati huo hakuna mwovu yoyote, ayatakayenusuruka..

Sasa hapa tumefupisha tu, unaweza kudhani kama hizi ni hadithi tu, au mambo hayo bado sana, yatachukua mamia ya miaka huko mbeleni, Lakini fahamu kuwa hivyo ndivyo shetani anavyotaka ujue ili siku ile ikujie kwa ghafla..Lakini maandiko yanakuambia hivi..

Sefania 1:14 “Hiyo siku ya Bwana iliyo kuu i karibu; I karibu, nayo inafanya haraka sana; Naam, sauti ya siku ya Bwana; Shujaa hulia kwa uchungu mwingi huko!

15 Siku ile ni siku ya ghadhabu, Siku ya fadhaa na dhiki, Siku ya uharibifu na ukiwa, Siku ya giza na utusitusi, Siku ya mawingu na giza kuu,

16 Siku ya tarumbeta na ya kamsa, Juu ya miji yenye maboma, Juu ya buruji zilizo ndefu sana.

17 Nami nitawaletea wanadamu dhiki, hata watakwenda kama vipofu, kwa sababu wamemtenda Bwana dhambi; na damu yao itamwagwa kama mavumbi, na nyama yao kama mavi.

18 Fedha yao wala dhahabu yao havitaweza kuwaokoa katika siku ile ya ghadhabu ya Bwana; bali nchi yote pia itateketezwa kwa moto wa wivu wake; maana atawakomesha watu wote wakaao katika nchi hii, naam, ukomo wa kutisha”.

Tusiwe na mengi ya kusema, ila ombi langu ni kuwa kama hujampa Kristo maisha yako, basi fanya uamuzi huu haraka, Kumbuka anakupenda sana, anakujali sana, anakuthamini, na anatamani sana uyarithi aliyokwenda kukuandalia miaka 2000 iliyopita kule juu mbinguni..Kwa muda wote huo! Ni lazima ni mambo mengi na mazuri aliyotuandalia….Wokovu wake ni bure, tena unapatikana sehemu yoyote, bila malipo. Fanya hivyo naye atajifunua kwako. (kiama kinatisha!)

Bwana akubariki, Bwana atubariki sote.

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

Kwanini Mungu anasema “Afanyaye malaika zake kuwa pepo”?

NA NENO LA BWANA LILIKUWA ADIMU SIKU ZILE.

IKIMBIE DHAMBI KWA GHARAMA ZOZOTE ZILE!

NA NENO LA BWANA LILIKUWA ADIMU SIKU ZILE.

Rudi Nyumbani:

Print this post

UBATIZO NI NINI NA ULIO SAHIHI NI UPI?

Kabla ya kufahamu ubatizo ni nini…Hebu jiulize mtu katokea na akakuuliza “kuzamisha maana yake ni nini?”..utamjibuje?…Bila shaka utamwelezea kwa kina kwamba ni kitendo cha kukitosa kitu chote kwenye kimiminika Fulani au kitu Fulani, pasipo kubakisha sehemu ambayo ipo wazi. Meli iliyopata ajali na kushuka chini ya bahari, tunasema meli hiyo imezama baharini. Mtu anayechimba shimo la taka akachimba chini sana na kuzitupa humo na kuzifukia, hapo ni sawa na kusema kazizamisha/kazizika.

Sasa mpaka hapo tutakuwa tumeshajua maana ya neno “KUZAMA au KUZAMISHA”..Sasa ukilichukua neno hilo “kuzamamisha”  ukalitafsiriwa kwa lugha ya kigiriki linakuwa ni BAPTIZO…Ni sawa uchukue Neno la kiswahili “kanisa” na kulitafsiri kwa kiingereza na kuwa “CHURCH”…Vivyo hivyo Neno “kuzamishwa” likitafsiriwa kwa kigiriki linakuwa ni Baptizo..neno hilo hilo likipelekwa kwa lugha ya kiingereza linakuwa ni “IMMERSION”..na linaweza kutafsiriwa kwa lugha mbali mbali..

Kwahiyo mtu anayesema “leo naenda chachi”..ni sawasawa na mtu aliyesema “leo naenda kanisani”…neno “chachi” sio Kiswahili, na wala sio kiingereza fasaha lakini utakuwa umemwelewa amemaanisha nini kusema hivyo.

Vivyo hivyo mtu akikuambia “leo nime batizwa kwenye maji” utakuwa umemwelewa kwamba amemaanisha leo kazamishwa kwenye maji…kwa lengo Fulani.. (katumia tu msemo wa kigiriki lakini utakuwa umeshamwelewa).

Kwahiyo mpaka hapo utajua kuwa hakuna mtu atakayekuambia kwamba kabatizwa kwenye maji halafu awe “amenyunyuziwa”…Mtu aliyenyunyuziwa hajabatizwa!…kwasababu kubatizwa sio kunyunyuziwa bali kuzamishwa kabisa. (mpaka hapo tutakuwa tumeshaelewa ubatizo ni nini)

TUKIRUDI KATIKA IMANI YA KIKRISTO.

Katika imani ya kikristo, yapo mambo ambayo yanafanyika kama ishara lakini yanafunua kitu kikubwa sana katika roho. Kwamfano utaona Bwana Yesu alitoa maagizo ya kushiriki meza ya Bwana, ambapo wakristo wakutanikapo wanakula mkate pamoja na divai. Hivyo ni vyakula vya kimwili lakini vinapolika kwa maagizo hayo ya Bwana Yesu vinakuwa vinafunua vitu vingine katika roho. Kwamba ni sawa na tunainywa damu ya Yesu na Mwili wake katika ulimwengu wa roho. Na alisema mtu asiyefanya hivyo basi hana uzima ndani yake. (maana yake hana ushirika na Yesu).

Yohana 6:53 “Basi Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambieni, Msipoula mwili wake Mwana wa Adamu na kuinywa damu yake, hamna uzima ndani yenu”.

Umeona ni agizo dogo tu, la kula chakula cha kimwili, lakini lina maana kubwa sana katika roho, sio la kulipuuza wala la kulifanya isivyopaswa…Na hapo hajasema tuonje!..bali tuule..

Kadhalika Bwana Yesu alitoa maagizo mengine yanayofanana na hayo ya watu kuzamishwa katika maji kwa jina lake(au kirahisi kubatizwa), ambapo alisema kwa kufanya hivyo katika mwili..kunafunua jambo kubwa sana katika roho, ambalo jambo lenyewe ni “kufa na kufufuka pamoja naye”

Wakolosai 2:12 “Mkazikwa pamoja naye katika ubatizo; na katika huo mkafufuliwa pamoja naye, kwa kuziamini nguvu za Mungu aliyemfufua katika wafu”.

Umeona na hapo?..maana yake usipobatizwa (yaani kuzamishwa katika maji)..basi katika roho bado hujafa wala kufufuka pamoja naye…wewe bado si wake!. Vile vile kama hujazamishwa na badala yake umenyunyuziwa hapo bado hujabatizwa, unapaswa ukabatizwe tena katika maji mengi.. kwasababu ndio tafsiri ya neno ubatizo.

Sasa yapo maswali machache machache ya kujiuliza?

Je ina maana kama mtu hajabatizwa katika maji mengi na badala yake katika kunyunyiziwa hawezi kwenda mbinguni?..Na kama hawezi vipi Yule mwizi aliyesulibiwa na Bwana pale msalabani..mbona yeye aliokolewa na wala hakubatizwa?..mbona wakina Musa hawakubatizwa?…mbona wakina Eliya hawakubatizwa?…Majibu ya maswali haya yote utayapata hapa >> Mtu akifa bila kubatizwa atakwenda mbinguni?

Hivyo ndugu mpendwa kamwe usiudharau “ubatizo”..kama bado hujaelewa kwa undani ubatizo ni nini, na umuhimu wa ubatizo tafadhali rudia kusoma tena taratibu na nakuomba chukua muda mwingi…katafute kuuliza huko na huko na pia piga magoti peke yako mwulize Roho Mtakatifu, halafu kasome biblia yako atakupa majibu.

Na ubatizo sahihi ni wa Jina la Yesu kulingana na mistari hii; Matendo 2:38, 8:16,10:48 na 19:5. Jina la Yesu ndio jina la Baba, Mwana na Roho Mtakatifu. Kufahamu haya zaidi fungua masomo mwisho kabisa mwa somo hili (sehemu ya chini)..yanaelezea kwa kina masuala ya ubatizo.

Bwana akubariki.

Kama hujampokea Yesu saa ya wokovu ni sasa. Kristo yupo mlangoni kurudi kuwachukua wateule wake..hivyo ingia leo ndani ya neema hii, kabla mlango wa neema haujafungwa. Yesu anakupanda na anataka kukupa raha nafsini mwako leo kama utamkubali…sawasawa na neno lake hili..

Mathayo 11: 28 “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.

29 Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu;

30 kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi”.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?

KWANINI UBATIZO NI WA MUHIMU.

Je, kama hauna ubatizo sahihi hauwezi kuwa na Roho Mtakatifu?

MAAGIZO YA BWANA YESU NI BORA KULIKO MAAGIZO YA DAKTARI:

BIBLIA TAKATIFU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

YATAMBUE MAJIRA YA KUJILIWA KWAKO.

Hivi unajua kuwa Wayahudi walikuwa wanamtazamia Kristo?..

Kila siku walikuwa wanamwomba Mungu wa mbingu na nchi… amtume Kristo wake duniani, aje awakomboe kutoka katika utumwa wa kirumi na wa dhambi. Na walidhamiria kabisa pindi atakapokuja wamheshimu na wamfurahie. Na hiyo ilimfanya kila mtu alitengeneza picha yake kichwani jinsi atakavyokuwa.

Lakini kama tunavyosoma biblia kipindi alipokuja hawakumjua kama ndio yeye…Na kosa kubwa walilolifanya ni KUTOKUJUA MAJIRA, hilo tu!. Siku zote ukishapoteza kujua majira, basi vitu vitakuja kwa kushtukiza mbele yako.

Umewahi kumwona mtu aliyepata tatizo Fulani na akapoteza kumbukumbu kabisa!..anakuwa katika hali ngumu sana, kwasababu anaweza kuja hata ndugu yake aliyeishi naye miaka yote na asimkumbuke hata kidogo!..kwake kila kitu ni kipya, lakini kumbukumbu zinapomrejea ndipo anashtuka huyu si ni Fulani?.

Umewahi kukaa na saa iliyopoteza majira?..Unaweza kujikuta kunapambazuka ukiwa bado kitandani ukidhani bado ni usiku, kwa kuitazama saa iliyopoteza majira! Hivyo na wewe ukapoteza majira.

Ndicho kilichowatokea wayahudi. Hawakujua wakati wa BWANA KUWAJILIA, walidhani Masihi hawezi kuja wakati kama huo, walijua ni kweli anakaribia kuja, lakini si katika kile kipindi walichopo..walizipeleka tarehe mbele kidogo..na wakajua Masihi atakapokuja atakuwa katika jumbe la kifalme, na atatawala kwa fimbo ya chuma, na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake.

Luka 19:43 “Kwa kuwa siku zitakuja, adui zako watakapokujengea boma, likuzunguke; watakuzingira na kukuhusuru pande zote;

44  watakuangusha chini wewe na watoto wako ndani yako, wasikuachie jiwe juu ya jiwe, kwa sababu hukutambua MAJIRA YA KUJILIWA KWAKO”.

Ndugu upo WAKATI WA KUJILIWA KWA KILA MTU!. Sizungumzii wakati wa kujiliwa kupata Maisha mazuri au nyumba nzuri au fedha nyingi, au mali bali wakati wa kujiliwa na NEEMA YA MUNGU. Kama Wayahudi walivyojiliwa na Bwana lakini hawakuyatambua majira hayo, wakaikataa na mpaka sasa wameachwa katika hali ya ukiwa. Na siku sio nyingi watajua makosa yao na kutubu na kugeuka kumwamini Mwokozi wao waliyemkataa miaka Zaidi ya eflu 2 iliyopita.

Luka 12:54 “ Akawaambia makutano pia, Kila mwonapo wingu likizuka pande za magharibi mara husema, Mvua inakuja; ikawa hivyo.

55 Na kila ivumapo kaskazi, husema, Kutakuwa na joto; na ndivyo ilivyo.

56 Enyi wanafiki, mwajua kuutambua uso wa nchi na mbingu; imekuwaje, basi, kuwa hamjui kutambua majira haya?”

Nguvu unayoisikia inakuvuta kwake jua ni majira ya kujiliwa kwako hayo…usiipuuzie hata kidogo! Na wala usikawie kawie…Na sasa tunaishi katika majira ya kurudi kwa Yesu mara ya pili. Wakati dunia inasema hawezi kuja leo..bado sana aje!…lakini alisema atakuja kama Mwivi…hawatajua chochote!…

Ukimwambia mtu kwamba Yesu amekaribia kurudi…kitu cha kwanza atatengeneza picha ya kipindi kirefu sana mbele, siku ambayo atatokea mpinga-kristo mwenye mapembe..pasipo kujua kuwa tayari Ofisi ya Mpinga-kristo ipo sasa duniani. na cheo chake kinajulikana…na tayari maandalizi ya ile chapa yapo tayari..Ni parapanda tu inasubiriwa mambo yote yaanze.

Huu ni wakati wa kuyasoma  na kuyatambua haya Majira tuliyopo!..tupoteze kujua kila kitu lakini tusipoteze kujua majira yetu ili mambo yasije yakatutokea ghafla..

1Wathesalonike 5:1  “Lakini, ndugu, kwa habari ya nyakati na majira, hamna haja niwaandikie.

2  Maana ninyi wenyewe mnajua yakini ya kuwa siku ya Bwana yaja kama vile mwivi ajavyo usiku.

3  Wakati wasemapo, Kuna amani na salama, ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafula, kama vile utungu umjiavyo mwenye mimba, wala hakika hawataokolewa”.

Bwana atubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

MWAKA WA BWANA ULIOKUBALIWA.

MPAKA UTIMILIFU WA MATAIFA UTAKAPOWASILI.

Kile kinara cha Taa ndani ya Hekalu la Sulemani kilikuwa kinawakilisha nini?

JE! PAKA KULIA USIKU NI ISHARA YA UCHAWI?

MAJONZI YA MTUME PAULO KWA NDUGU ZAKE.

UFUFUO TUNAOUSUBIRIA UTAHITIMISHA YOTE.

Kati ya Unyakuo,dhiki kuu, utawala wa miaka 1000 kipi kinaanza

Rudi Nyumbani:

Print this post

KWANINI UKATE TAMAA?

Kwanini ukate tamaa ya  kumtafuta Mungu? Nataka nikuambie hata Mungu mwenyewe akikuambia sikutaki haunifai, bado hupaswi kukata tamaa…

Kuna mbegu Fulani ya uharibifu ambayo shetani ameipanda ndani ya mioyo ya wakristo wengi, ambayo kuna hatua wanafikia ya kujiona kuwa hawafai tena mbele za Mungu, ya kujiona kuwa Mungu hawezi kuwa nao tena, ya kujiona kama hawastahili kwenda mbele za Mungu tena,….Hivyo wanaishia kukata tamaa ya kuendelea mbele pale wanapoona hata majibu ya maombi yao yanachelewa, nimekutana na watu wa namna hiyo wengi.

Lakini nataka nikuambie hupaswi kukata tamaa, wapo ambao Mungu alikuwa hana mpango nao,wengine hawakuwa  hata wakristo, na wengine walikuwa wamesha muudhi Mungu kupindukia kwa kiwango cha juu sana mpaka Mungu kuwatamkia vifo, lakini katika uovu wao hawakukata tamaa ya kumkimbilia Mungu awarehemu, si Zaidi wewe ambaye ulishaokoka? Kwanini ukate tamaa?

Zaburi 107:10 “Waliokaa katika giza na uvuli wa mauti, Wamefungwa katika taabu na chuma,

11 Kwa sababu waliyaasi maneno ya Mungu, Wakalidharau shauri lake Aliye juu.

 12 Hata akawadhili moyo kwa taabu, Wakajikwaa wala hakuna msaidizi.

13 Wakamlilia Bwana katika dhiki zao, Akawaponya na shida zao.

14 Aliwatoa katika giza na uvuli wa mauti, Akayavunja mafungo yao.

15 Na wamshukuru Bwana kwa fadhili zake, Na maajabu yake kwa wanadamu”.

Kumbuka Biblia ni kitabu kilichoandikwa ili kutuonya sisi, na kwa sehemu nyingine ili kututia nguvu, na kutufariji..

Kwa mfano embu mwangalie huyu mama ambaye hata wakati wake neema ya wokovu ilikuwa haijamfikia, alikuwa na miungu yake huko Tiro, pengine alipata hilo tatizo kutokana na dhambi zake kwa Mungu, lakini ilipofika wakati wa kutaka msaada kutoka kwa Mungu, hakujali “kutokujali kwa Mungu“, hakujali majibu makali kutoka kwa Mungu, bali aling’ang’ania mpaka akapata alichokuwa anakitafuta, haijalishi kuwa angeendelea kwenda kuiabudu miungu yake.

Mathayo 15:22  “Na tazama, mwanamke Mkananayo wa mipaka ile akatokea, akampazia sauti akisema, Unirehemu, Bwana, Mwana wa Daudi; binti yangu amepagawa sana na pepo.

23  Wala yeye hakumjibu neno. Nao wanafunzi wake wakamwendea, wakamwomba, wakisema, Mwache aende zake; kwa maana anapiga kelele nyuma yetu.

24  Akajibu, akasema, Sikutumwa ila kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli.

25  Naye akaja akamsujudia, akisema Bwana, unisaidie.

26  Akajibu, akasema, Si vema kukitwaa chakula cha watoto na kuwatupia mbwa.

27  Akasema, Ndiyo, Bwana, lakini hata mbwa hula makombo yaangukayo mezani pa bwana zao.

28  Ndipo Yesu akajibu, akamwambia, Mama, imani yako ni kubwa; na iwe kwako kama utakavyo. Akapona binti yake tangu saa ile”.

Unaona tabia ya huyo mwanamke?, Mfano mwingine ni Mfalme Ahabu..Ambaye tunajua alikuwa ni mume wa yule mwanamke mchawi Yezebeli, biblia inasema huyu Ahabu alikuwa mfalme mwovu, kuliko wafalme wote waliomtangulia na alishiriki kuwakosesha sana Israeli mbele za Mungu (1Wafalme 21:25), mpaka ikafikia wakati Mungu akamwambia inatosha sasa..kufa utakufa, na nyumba yako itakuwa jaa..

Lakini Habari hizo mbaya kutoka kwa Mungu zilipomfikia, haikumfanya akate tamaa, na kusema sasa ndio basi!, Mungu hawezi tena kunitazama, badala yake alikwenda kujinyenyekeza..

1Wafalme 21: 27 “Ikawa, Ahabu alipoyasikia maneno hayo, akayararua mavazi yake, akavaa magunia mwilini mwake, akafunga, akajilaza juu ya magunia, akaenda kwa upole.

 28 Neno la Bwana likaja kwa Eliya Mtishbi, kusema,

29 Huoni jinsi Ahabu alivyojidhili mbele yangu? Basi kwa sababu amejidhili mbele yangu, sitayaleta yale mabaya katika siku zake; ila katika siku za mwanawe nitayaleta mabaya hayo juu ya nyumba yake”..

Yupo na mwingine aliyetokea baada ya Ahabu, aliyeitwa Manase, Huyu ndiye alifanya mabaya Zaidi kuliko hata Ahabu na ndio aliyesababisha hata Mungu asiwasemehe Israeli tena, huyu alikuwa anawatoa mpaka Watoto wake kafara kwa kuwapitisha kwenye moto, alikuwa anakwenda kufanya uganga na mambo maovu kweli kweli..Mungu akachukizwa naye sana Ikiafikia hatua ya kuchukuliwa mateka kwa minyororo na pingu, na waashuru mpaka Babeli.

Lakini akiwa huko akijijua kuwa yeye ni adui wa kwanza wa Mungu,  alijinyenyekeza kwa Mungu akamlilia sana mpaka akasikiwa..

2Nyakati 33:12 “Hata alipokuwa katika taabu, akamsihi Bwana, Mungu wake, akajinyenyekeza sana mbele za Mungu wa baba zake.

13 Akamwomba; naye akamtakabali, akayasikia maombi yake; akamrudisha tena Yerusalemu katika ufalme wake. Ndipo Manase akajua ya kwamba Bwana ndiye Mungu”.

Sasa hiyo ni mifano michache ya watu ambao walikuwa ni waovu na wenye dhambi, ambao tayari walikuwa wameshahukumiwa tayari na Mungu kutokana na makosa yao..Lakini hawakukata tamaa, kujinyenyekeza kwake (sasa wewe kwanini ukate tamaa?)..Lakini sikuambii hivi ili na wewe ukafanye dhambi umwombe Mungu halafu akusikie hapana, hilo ni kosa.

Naandika hivi kwa ajili yako, wewe ambaye umeokoka, halafu unaona kama Mungu hawezi kukusikia, au hakujali.. Jiulize! tu kama Mungu Yehova alivisikia vilio vya wenye dhambi kama wakina Ahahu na Manase ambao walimkasirisha kwa kiwango kile, ataachaje kukusikia wewe ambaye, tayari ulishampa Maisha yako?..Anakusikia sana. Na anakuhurumia kuliko wewe unavyodhani, na anakujali, na anayasikia maombi yako…Hivyo huna sababu ya kukata tamaa?..Endelea mbele kumwamini na kumwomba kwa bidii.

Hebu soma tena hapa..

Zaburi 107: 4 “Walitanga-tanga jangwani katika njia ya nyika; Hawakuona mji wa kukaa.

5 Waliona njaa, waliona na kiu, Nafsi yao ilikuwa ikizimia ndani yao.

6 Wakamlilia Bwana katika dhiki zao, Akawaponya na shida zao.

7 Akawaongoza kwa njia ya kunyoka, Wapate kwenda mpaka mji wa kukaa”.

Zaburi 105:8 “Bwana ana fadhili, ni mwingi wa huruma, Si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa rehema”

Nataka nikuambie ukiwa umeokoka, Bwana anakupenda na yupo karibu sana na wewe kuliko hata wenye dhambi, ukiwa umeokoka kilio chako mbele zake kinasikika Zaidi kuliko kilio cha akina Ahabu na Manase.., Hivyo endelea tu kumtafuata Mungu kwa bidii zote kwasababu wewe ni wa thamani nyingi kwake, wenye dhambi wasikushinde, ng’ang’ana na Bwana, popote pale, atakuwa na wewe wakati wote..

Wanaomtegemea Mungu, mwisho wao huwa unakuwa mzuri kama wa Ayubu.

Yakobo 5:11 “Angalieni, twawaita heri wao waliosubiri. Mmesikia habari ya subira yake Ayubu, mmeuona mwisho wa Bwana ya kwamba Bwana ni mwingi wa rehema, mwenye huruma”.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

Kuungama ni nini?

MJUMBE ASIYEKUWA NA UJUMBE.

KUTUBU SIO KUOMBA REHEMA.

 Je kualikwa kwenye sherehe za watu ambao si wakristo ni dhambi?

NGUVU YA SADAKA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

JIFUNZE KUJITOA KWA MUNGU NA KUWA MKARIBISHAJI.

Shalom, mtu wa Mungu.. karibu tujifunze biblia Neno la Mungu, ambalo ni mwanga wa njia yetu na taa iongozayo miguu yetu.

Leo tujikumbushe umuhimu wa kuwa wakaribishaji, na wa kujitoa kuifanya kazi ya Mungu.

Kipindi kirefu kidogo nimekuwa nikiwasiliana na binti mmoja humu facebook, ambaye anaishi kwao na wazazi wake, kiukweli ni binti anayempenda Mungu na kujitoa kwa Mungu ingawa ni mdogo kiumri. Amekuwa akitutumia maswali kadha wa kadha na kumjibu..kama ni mfuatiliaji wa masomo ya humu utakuwa umewahi kusoma swali tulilolijibu linalouliza… “Yuko azuiaye sasa hata atakapoondolewa! ni nani huyo?”…na lingine “Nitaitofautishaje sauti ya Malaika na ya Roho Mtakatifu?”.. Maswali haya mawili yaliulizwa na huyu binti..Na yapo mengine aliyouliza ambayo majibu yake tulimtumia pasipo kuyaweka wazi.

Huyu binti ni mtanzania lakini anaishi Zambia, karibu na mpaka wa Tanzania. Japokuwa ni binti mdogo lakini amekuwa akituuliza maswali kuhusu siku za mwisho na pia maswali ya namna ya kwenda kuwahubiria wengine Habari za Yesu mitaani. Katika udogo wake tulimtia moyo asiache kuwashuhudia wengine kwa bidii zote, haijalishi mazingira aliyopo, na mambo mengine mengi tulimshauri. Alienda kuyafanyia kazi hayo tuliyomshauri..na baada ya muda akatuletea mrejesho kwamba ametoka kuwashuhudia baadhi… “Anasema ijapokuwa huku nilipo makanisa yamefungwa kutokana na hofu ya corona, lakini mimi nilitoka hivyo hivyo sikujali.. na niliowashuhudia wengine wametaka namba zangu niwaombee na kuwaongoza sala ya toba” (kama kawaida hizo ni Habari za furaha kwetu sisi kama wakristo).. 

Ni binti pia ambaye anayepitia changamoto nyingi, na hata nyumbani alipo sio kwamba ni watu wa Imani sana, hata wale anaowashuhudia na kuokoka anaogopa kuwakaribisha nyumbani kwasababu ya vita vya nyumbani….yaani kwa ufupi ni binti aliyejitoa kweli, na mwenye upendo wa ki-Mungu, yupo tayari kwenda kuwasaidia watu roho pasipo kujali mazingira aliyopo.

Sasa siku kadhaa nyuma, alipata mgeni kama yule Ibrahimu aliyekutana naye wakati anatoka kumpiga Kedorlaoma (Mwanzo 14:8-18).. 

Hebu msikilize…

“Jana asubuhi sana niliamka nikawa naosha vyombo asa nikaenda kumwaga maji machafu ya vyombo nje nikachukua funguo nikapitia kufungua geti kubwa la nje , nikasikia sauti ikiita jina langu kwa sauti ya mbaali niliisikia lakini nikajua labda Ni mawazo tu, ikaita Tena ile nataka kuingia ndani nikainua macho getini nikamuona Mtu nisiyemjua anabisha hodi nikafungua nilivyofungua nikamsalimia kwa Adabu na heshima ya Hali ya juu kama kawaida yangu japo alikuwa m-baba mrefu mweusi amevaa nguo mbaya mbaya za (kimasikini) Mimi simjui asa nikajua labda Ni mgeni wa Baba labda alimpigia simu aje , kumbe sio, akaniambia unahitaji nini nikamwambia hamna Baba, huku naendelea kumsikiliza kwa makini kwa karibu , akaniambia chukua pesa hizi usiwe na shida, akanipa na vyakula Kisha akatoa pesa nyingine akanipa Sasa ile nimeshapokea pesa na vitu, nikamwambia YESU anakupenda akasema ndio nawewe (Mimi) anakupenda pia nikamwambia Asante! ,Sasa nikaweka vitu chini nikwambie umeokoka?, unaitwa Nani? Ile nainuka sikumuona Tena yule m-baba” .

Mwisho wa nukuu.

Sasa Baada ya kumuuliza alikupa nini kingine tofauti na hizo pesa?…akaniambia alimpa BIBLIA, TENZI ZA ROHONI, DIARY Pamoja na KALAMU.

Ndipo nikajua ni malaika kamtembelea…Na bahati nzuri huyu binti anayajua maandiko na analijua hili andiko pia…

Waebrania 13:2  “Msisahau kuwafadhili wageni; maana kwa njia hii wengine wamewakaribisha malaika pasipo kujua”.

Hivyo baada ya tukio hilo ajijua kabisa ni malaika wa Bwana, na amani ya ajabu iliingia ndani yake..

Ndugu, haya mambo sio hadithi, ni vitu vya kweli kabisa…Kwasababu hata Mimi binafsi vilishawahi kunitokea mara mbili katika mazingira yanayokaribiana kufanana na huyu binti. Malaika wa Mungu mamilioni kwa mamilioni wanazunguka ulimwenguni..na wala usitegemee watakuja wamevaa nguo nyeupe na mabawa…Hapana!. Wale waliomtembelea Lutu hawakuwa na mavazi meupe, waliomfuata Ibrahimu chini ya mialoni ya Mamre hawakuwa na mavazi meupe…wanakuja kama watu tu wa kawaida kabisa..Ndio maana Paulo anasema “wengine mnawakaribisha Malaika pasipo kujua”.

Huyu binti yeye kaletewa zawadi chache za kumtia moyo kwamba azidi kusoma Neno na kujifunza (Ndio maana kapewa biblia na diary) Pamoja na kuwashuhudia wengine, na Bwana amemfanyia vile kumwonesha kuwa anampenda na yupo Pamoja naye kumhudumia katika mahitaji yake hata ya chakula hivyo asiogope! Na zaidi alimpa pesa nyingi sana..ndio maana kamtuma Malaika wake kumfariji.  Na ule ni udhihirisho mdogo tu wa mambo yanayoendelea katika roho, katika roho anazungukwa na hilo jeshi la malaika wengi sana. Popote anapokwenda wapo naye, kumlinda na kumtunza.

Jiulize je angekuwa si mtu wa kujali  na kujitoa kwa ajili ya roho za wengine malaika wa Bwana angetumwaje kwake?..Biblia inasema malaika ni viumbe wa roho wanaofanya kazi ya kuwahudumia Watoto wa Mungu wale watakaoirithi ahadi..na si kila mtu tu!

Waebrania 1:14  “Je! Hao wote si roho watumikao, wakitumwa kuwahudumu wale watakaourithi wokovu?”

Sasa angetumwaje kumhudumia kama angekuwa si mtu wa kuifanya kazi ya Mungu?..Malaika wa Mungu angetumwa amletee zawadi gani ya kumfariji kama angekuwa ni binti wa kushinda tu kuzurula zurula mtaani au kuzungumza umbea au kutembea tembea na wavulana mitaani?..Unaona?..hakuna chochote angeambulia…

Na kitu kimoja ambacho hakifahamiki na wengi ni kwamba Malaika wana kazi ya kupeleka mambo yetu mema tunayoyafanya mbele za Mungu..Lolote zuri unalolifanya malaika wanalipeleka kama hoja mbele za Mungu..kama utapenda tukutumie somo juu ya hilo..utatutumia ujumbe mfupi inbox.

Naamini ushuhuda wa huyu dada ni darasa tosha kwetu!…Katika nafasi tulizopo, hebu tujitoe kwa Mungu…usijitoe ili utokewe na Malaika hapana!..jitoe kwasababu unaona umuhimu wa wengine kuujua ukweli na kupata wokovu maishani mwao. Nafasi ndogo unayopata kama ni shuleni, nyumbani, kazini, kwenye mitandano, usitengeneze visingizio vingi..kwamba siwezi kwasababu ya hichi au kile..kwasababu nipo bize..Ifanye kazi ya Mungu, wengi bado wanahitaji kuokolewa. Malaika wa mbinguni wanafurahi mtu mmoja tu anapotubu! 

Bwana atubariki na Bwana atusaidie.

Kama hujaokoka!..Wokovu unaanzia hapa hapa duniani!..usidanganywe na shetani kwamba hakuna kuokoka duniani, usidanyike mtu wa Mungu…Tubu leo kama bado..na kisha acha yote machafu uliyokuwa unayafanya kama ulevi, uasherati, wizi, utazamaji pornograph, utukanaji, uuaji, usengenyaji na mengine yote..Na baada ya hapo, tafuta kanisa lililo hai, lililopo karibu na mahali ulipo, hakikisha unabatizwa hapo katika ubatizo sahihi wa jina la Yesu na wa kuzamishwa mwili wote(Matendo 2:38). Na baada ya hapo Roho Mtakatifu atakuongoza kufanya yaliyosalia.

Unyakuo upo karibu na hizi ni siku za mwisho..siku yoyote! Mambo yatageuka ghafla, unyakuo utapita, watakatifu watatoweshwa..dhiki kuu ya mpinga-Kristo itaanza, na ghadhabu ya Mungu itamwagwa duniani.. hakuna mtu atategemea, itakuwa ni ghafla tu!..kama vile corona ilivyozuka ghafla tu! pasipo ulimwengu kutegemea.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

 KUWAHUDUMIA MALAIKA PASIPO KUJUA.

MTU ASIYE PAMOJA NAMI YU KINYUME CHANGU.

UFUFUO TUNAOUSUBIRIA UTAHITIMISHA YOTE.

HUDUMU YA MALAIKA WATAKATIFU.

MAJESHI YA PEPO WABAYA.

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

KWANINI HUNA HAJA YA KUANDIKIWA JUU YA NYAKATI NA MAJIRA?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Neno la Mungu ni upanga.

Ni kwa namna gani Neno la Mungu ni upanga?


Biblia haisemi Neno la Mungu ni upanga tu, hapana bali inasema  ni zaidi ya upanga wowote mkali ukatao kuwili..

Waebrania 4:12 “Maana Neno la Mungu li hai, tena lina nguvu, tena lina ukali kuliko upanga uwao wote ukatao kuwili, tena lachoma hata kuzigawanya nafsi na roho, na viungo na mafuta yaliyomo ndani yake; tena li jepesi kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo.

13 Wala hakuna kiumbe kisichokuwa wazi mbele zake, lakini vitu vyote vi utupu na kufunuliwa machoni pake yeye aliye na mambo yetu.”.

Unaona? Ni zaidi ya upanga. Na kama tunavyojua upanga unaokata kuwili ni upanga ambao unatumika sana sana katika vita, yaani ukiupeleka upande wa kulia unakata na vilevile ukiurudisha upande wa kushoto bado unakata(Ufunuo 1:16, 2:12, 19:12).. Ni mfano wa msimeno unakata mbele na nyuma.

Sasa Mungu anakuambia Neno lake ni zaidi ya huo upanga. Akiwa na maana kuwa linakata pande zote, kwa wale wote watakaokwenda kinyume nalo, linakata matajiri, linakata maskini, linakata wenye vyeo linakata wasio na vyeo, linakata weupe, linakata weusi, linakata wenye dhambi vilevile linakata na waliookoka ikiwa hawatadumu katika maagizo yake.

Na kukata kwake sio butu, bali kwa ukali sana, likipita linatenganisha kabisa kabisa, yaani mfano Mungu akipitisha upanga katika taifa basi ujue taifa hilo ndio mwisho wake umefika, akipitisha upanga katika familia basi ujue ni upanga kweli kweli unaotenganisha, haijalishi  ndugu hao watakuwa wanapendana au wameshikamana kiasi gani.Soma.

Mathayo 10:34 “Msidhani ya kuwa nimekuja kuleta amani duniani; la! Sikuja kuleta amani, bali upanga.

35 Kwa maana nalikuja kumfitini mtu na babaye, na binti na mamaye, na mkwe na mkwe mtu;

36 na adui za mtu ni wale wa nyumbani mwake”.

Vilevile alisema, katika wakati wa Mwisho atayaangamiza mataifa kwa Neno lake, ambao ndio huo upanga utokao katika kinywa chake..

Ufunuo 19:14 “Na majeshi yaliyo mbinguni wakamfuata, wamepanda farasi weupe na kuvikwa kitani nzuri, nyeupe, safi.

15 Na upanga mkali hutoka kinywani mwake ili awapige mataifa kwa huo. Naye atawachunga kwa fimbo ya chuma, naye anakanyaga shinikizo la mvinyo ya ghadhabu ya hasira ya Mungu Mwenyezi.

16 Naye ana jina limeandikwa katika vazi lake na paja lake, MFALME WA WAFALME, NA Bwana WA MABwana”.

Hivyo, Mungu anatuasa tutubu, tumgeukie yeye, ili kusudi kwamba Neno lake, liwe chakula na uzima kweli badala ya upanga, Kwasababu kwa kupitia hilo hilo Mungu alifanya mbingu na nchi, kwa kupitia hilo hilo, alituumba sisi, kwa kupitia hilo hilo alinatuponya na kutuokoa, na kutubariki. Lakini kwa kupita hilo hilo atatuhukumu kama tusipotaka kuitii injili. Na ndio anatuhimiza mpaka sasa tutubu kwa kurudi kwake kumekaribia.

Ufunuo 2.16 Basi tubu; na usipotubu, naja kwako upesi, nami nitafanya vita juu yao kwa huo upanga wa kinywa changu.

Neno la Mungu ni upanga.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

USIPOLITENDEA KAZI NENO LA MUNGU.

UTASIMAMA PEKE YAKO SIKU ILE.

MAPAMBANO DHIDI YA SHETANI.

KWANINI TUNAPASWA TUJIZUIE?

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

UTAWALA WA MIAKA 1000.

ROHO ZILIZO CHINI YA MADHABAHU:

Rudi Nyumbani:

Print this post

Neno la Mungu la leo.

Neno la Mungu la leo ni lipi?


Kwanza nakupongeza kwa kupenda kutafuta kujua Neno la Mungu la leo..

Bwana Yesu alisema kila atafutaye huona (Mathayo 7:8), Hivyo kwa kuwa na wewe umetafuta kujua Neno la Mungu la leo kwako, basi ni hakika kuwa lipo jambo jipya Mungu atakufundisha.

Sio kwa bahati mbaya umefika mahali hapa.,

Paulo alimwambia Timotheo.

1Timotheo 4:13 “Hata nitakapokuja, ufanye bidii katika kusoma…..”

Unaona ni jukumu la kila mmoja wetu kuonyesha bidii katika kusoma(kujifunza) Neno la Mungu.

Wewe unaonyesha bidii hiyo  hivyo, usiache kupitia somo hili mpaka mwisho, lipo ambalo Mungu amekuandalia leo..

Lakini kabla hatujaendelea unaweza kufungua hapa  uingie katika horodha ya masomo ya kujifunza yaliyotangulia zaidi ya 1000, pamoja na maswali na majibu ..

>>> MAFUNDISHO MAPYA.


Leo tutajifunza nini maana ya Upendo na je! kuna aina ngapi za upendo?

Upendo ni kitendo cha kuonyesha hisia za tofauti za ndani kwa mtu mwingine, Ni hisia zinazoonyesha matokeo chanya, aidha umeridhishwa na mtu huyo, au umemkubali, au umemuhurumia, au unataka kumkaribia uwe karibu naye.

Kuna aina kuu tatu za upendo.

  1. Upendo unaotokana na Hisia, (Eros), Mfano wa upendo huu ni mke na mume. Sulemani aliutaja upendo huu sana katika kitabu cha Wimbo ulio bora (Wimbo 1:13-17)
  2. Upendo unatokana na  mahusiano mtu mmoja aliyo nayo kwa mwingine.(Phileo). Kwamfano unaweza ukawa unampenda mtu kutokana na kwamba ni mchezaji mwezako, au mfanyakazi mwenzako, au mkristo mwenzako, au mwanafunzi mwenzako n.k. mazingira yakishawatawanyisha, au itikidi zikitofautiana basi Upendo huu unakufa.
  3. Upendo wa ki-Mungu (Agape). Upendo huu ndio Upendo mkuu kuliko yote, Ni upendo usiokuwa na Masharti, Ni upendo ambao mtu anakupenda sio kwasababu ulimfanyia hiki au kile, au kwasababu unaendana naye kitu Fulani, hapana..Ni upendo usiohesabu mazuri wala mabaya kama kigezo cha kukupenda, ..

Upendo huu ndio ule ambao Mungu aliupenda ulimwengu hata akamtoa mwanawe wa pekee ili kila mtu amwaminiye asipotee bali awe na uzima wa milele (Yohana 3:16).

 Na Upendo aliokuwa nao Yesu, ukamfanya mpaka auote uhai wake kwa ajili yetu sisi wenye dhambi. Upendo wa namna hii ukiwa nao basi ujue kuwa Upo karibu na Mungu sana kuliko mwanadamu mwingine yeyote duniani.

Na unamjua Mungu, zaidi mwanadamu mwingine yoyote duniani haijalishi atasema anaona maono, au ana mafunuo mengi kiasi gani..

1Yohana 4:7 “Wapenzi, na mpendane; kwa kuwa pendo latoka kwa Mungu, na kila apendaye amezaliwa na Mungu, naye anamjua Mungu.

8 Yeye asiyependa, hakumjua Mungu, kwa maana Mungu ni upendo”.

Tabia za upendo huu unaweza kuzisoma katika kitabu cha 1Wakorintho 13:4-8

Kwa urefu wa maelezo haya juu ya aina hizi za upendo fungua hapa usome..>> UPENDO

Hivyo hiyo yote ni kuonyesha jinsi gani Mungu anatupenda na kutujali, Hivyo kama wewe ni mwenye dhambi ujue kuwa Mungu anakupenda bado na hivyo hataki upotee, uende kuzimu, mgeukie leo akuoshe dhambi zako. Ili ukaurithi uzima wa milele aliotuandalia. Hilo ndilo Neno la Mungu la leo.

Shalom.

Tazama vichwa vingine vya masomo chini, kwa maarifa zaidi ya kiroho.

Mada Nyinginezo:

RABI, UNAKAA WAPI?

KWANINI YESU ALIMUITA BABA YAKE “ABA”?

MANENO ALIYOWEZA KUTAMKA YESU TU PEKE YAKE.

SAMEHE KUTOKA NDANI YA MOYO WAKO.

WAFALME WATOKAO MAWIO YA JUA.

UNYAKUO.

Rudi Nyumbani:

Print this post