Category Archive Home

TAFUTA KUWA NA AMANI NA WATU WOTE.

Waebrania 12:14 “Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na huo utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao”.

Ni agizo la Mungu kwamba tuwe na amani na watu wote..Ukijiona una shari na mtu au watu basi kuna tatizo mahali…Sio kila jambo ni la kupambana nalo, na njia ya kupambana na moto ni kuuzima na si kujitosa ndani ya moto. Hivyo tunapoudhiwa si wakati wa sisi kulipiza kisasi, ni wakati wa kuyazima hayo maudhi, kwa hekima na upole.Na mara nyingi kitu kinachowasha moto katika miasha yetu ni ULIMI.

Yakobo 3:5 “Vivyo hivyo ulimi nao ni kiungo kidogo, nao hujivuna majivuno makuu. Angalieni jinsi moto mdogo uwashavyo msitu mkubwa sana.

6 Nao ULIMI NI MOTO; ule ulimwengu wa uovu, ule ulimi, umewekwa katika viungo vyetu, nao ndio uutiao mwili wote unajisi, huuwasha moto mfulizo wa maumbile, nao huwashwa moto na jehanum”

Unaona hapo? Biblia inasema pia ukiweza kuuzuia ulimi wako hata SIKU YAKO ITAKUWA NJEMA…na ndivyo utakavyopata amani..

1Petro 3:10 “Kwa maana, Atakaye kupenda maisha, Na kuona siku njema, Auzuie ulimi wake usinene mabaya, Na midomo yake isiseme hila.

11 Na aache mabaya, atende mema; ATAFUTE AMANI, aifuate sana”

Hivyo mara zote tukijifunza kukaa kimya na kuwa wapole na wenye busara…basi ni lazima tu tutakuwa na amani na watu wote….Sisemi kwamba hautakuwa na watu wanaokuchukia kabisa,…hapana watu wanaokuchukia watakuwepo tu! lakini hawatakuwa na la kufanya kwako kwasababu muda wote watakuona ni mtu wa amani. Watatafuta maneno kwako lakini hawatayapata…hivyo mwisho wa siku wataachana na wewe, na kuendelea kufikiri mambo yao mengine.

Lakini ukiwa ni mtu wa kujibiza, kamwe vita kwako havitaisha..na hakuna siku utapata amani…kama mtu akikuudhi wewe nawe unajibu mashambulizi kwa kumrudishia maneno…nataka nikuambia hakuna siku utakuwa na amani, utakuwa ni mtu wa kugombana tu kila siku, na wa kukosa raha, na muda mwingine kuweka vinyongo tu…na pasipo kujua kuwa tatizo kubwa lipo upande wako.

Mithali 15:1 “Jawabu la upole hugeuza hasira; Bali neno liumizalo huchochea ghadhabu”.

Kila mahali jaribu kuwa mpole…hiyo ndiyo njia ya kupata Amani na watu wote…Na kuwa mpole sio “udhaifu”….Bwana wetu Yesu alikuwa ni mpole(Mathayo 11:28) na mtu mpole mara nyingi sio mtu wa kuzungumza sana, na sio mtu wa kuzungumza mambo ya wengine (msengenyaji).

Wafilipi 4:5 “Upole wenu na ujulikane na watu wote. Bwana yu karibu”.

Sisi kama wakristo tukiudhiwa kwa maneno sio lazima tujibu neno,.. ukiumizwa hupaswi na wewe kumuumiza..kila wakati tafuta namna ya kulitatua tatizo badala ya kulichochea…na kwa jinsi utakavyoonesha bidii ndivyo Mungu atakavyozidi kukupatanisha na wale ambao wanaonekana ni maadui zako wa kudumu..Na hivyo utazidi kuwa na amani.

Mithali 16:7 “Njia za mtu zikimpendeza Bwana, Hata adui zake huwapatanisha naye”.

Hivyo Bwana anavyotuambia tutafute kwa bidii (maana yake tufanye kila tuwezalo) tuwe na amani na kila mtu, kama vile tunavyofanya bidii kuutafuta utakatifu ambao hakuna atakayemwona Mungu asipokuwa nao.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

KAMA UNAPENDA MAISHA, NA KUTAKA SIKU YAKO IWE NJEMA.

NI NINI TUNAJIFUNZA JUU YA MT. DENIS WA UFARANSA?

Mtu astahiliye hofu ni yupi?

FAHAMU ZA WATU HUWA ZINAONDOLEWA NA NINI?

DANIELI: Mlango wa 9

UPENDO NI NINI NA JE! KUNA AINA NGAPI ZA UPENDO?

Kwanini biblia inasema mtu wa rohoni huyatambua yote?

Rudi Nyumbani:

Print this post

MATENDO YETU YANAPIMWA KATIKA MIZANI.

Ukisoma katika biblia utakuta kuna mahali Bwana alikuwa anasema maneno haya…

1Wafalme 16: 25 “Omri akafanya yaliyo mabaya machoni pa Bwana, akatenda maovu kuliko wote waliomtangulia”

1Wafalme 16: 30 “Ahabu mwana wa Omri akafanya yaliyo mabaya machoni pa Bwana kuliko wote waliomtangulia”.

Utaona hapo huyo Mfalme aliyeitwa Omri alifanya machukizo makubwa kuliko baba zake waliomtangulia…na anakuja kupata mtoto anayeitwa Ahabu na huyo mtoto anafanya naye mabaya kuliko yeye na wote waliomtangulia…Maana yake ni kwamba hali ya mtoto inakuwa ni mbaya kuliko ya mzazi, na ya mjukuu ni mbaya kuliko ya Baba na babu.

Sasa unaweza kujiuliza ni kwanini Bwana aweke hilo neno “ naye akafanya mabaya kuliko wote waliomtangulia”?..Jibu ni kwasababu matendo yetu yanapimwa yakilinganishwa na ya waliotutangulia..

Kama baba kaua mtu mmoja, na mtoto wake akaua wawili…basi maasi ya mtoto yamezidi yale ya Baba mara mbili…yaani kama yangewekwa katika mizani basi mzigo wa mtoto ni mkubwa kuliko wa Baba.

Kadhalika kama mtoto kafanya mema kuliko baba yake basi matendo yake kama yakiwekwa katika mizani yataonekana yamezidi ya Baba yake…na kama Baba yake amefanya mema kuliko yeye basi matendo ya Baba yake katika mizani ya kimbinguni ni mazito kuliko ya mtoto, na hivyo ya mtoto yataonekana yamepunguka…

Ndicho kilichomtokea Mfalme Belshaza wa Babeli…Mfalme huyu ijapokuwa alikuwa anayajua matendo ambayo Mungu wa Israeli alimfanyia Baba yake…lakini bado matendo yake yalikuwa maovu kuliko baba yake…Na mema yake yalionekana ni pungufu kuliko mema ya Baba yake katika mizani ya kimbinguni. Kwani Baba yake alimheshimu Mungu lakini yeye hakumweshimu na kwenda kuvichukua vyombo vitakatifu na kuvitumia kwa karamu zake za kiasherati.

Na Bwana akamwambia maneno haya..

Danieli 5:27 “TEKELI, umepimwa katika mizani nawe umeonekana kuwa umepunguka”.

Maana yake ni kwamba matendo mema aliyoyafanya baba yake yamezidi ya kwake…Bwana Mungu alitegemea matendo ambayo angeyafanya yazidi ya baba yake lakini kinyume chake yamepungua, na hivyo akamhukumu.

Biblia inasema….

2 Samweli 2:3 “Msizidi kunena kwa kutakabari hivyo; Majivuno yasitoke vinywani mwenu; Kwa kuwa Bwana ni Mungu wa maarifa, NA MATENDO HUPIMWA NA YEYE KWA MIZANI”.

Ndugu matendo yetu yanapimwa katika mizani kila siku yakilinganishwa na ya wengine kama sisi…kizazi chetu kinapimwa katika mizani kikilinganishwa na vizaza vilivyotangulia..

Mathayo 12:41 “Watu wa Ninawi watasimama siku ya hukumu pamoja na watu wa kizazi hiki, nao watawahukumu kuwa wamekosa; kwa sababu wao walitubu kwa mahubiri ya Yona; na hapa yupo aliye mkuu kuliko Yona”.

Mahali tunapoishi, tunapofanyia kazi tunapimwa…kila tunalolifanya linapimwa linalinganishwa na la wengine. Hata maisha tunayoishi sisi kama wakristo yanapimwa ndio maana Bwana Yesu alisema..

Mathayo 5:20 “Maana nawaambia ya kwamba, Haki yenu isipozidi hiyo haki ya waandishi na Mafarisayo, hamtaingia kamwe katika ufalme wa mbinguni”.

Unapovaa suruali binti wa Mungu ambaye umezaliwa katika mazingira ya kikristo, pengine hata baba yako ni mchungaji…na unasema unakwenda mbinguni…ukumbuke kuna mwingine kama wewe mwenye umri kama wa kwako mahali fulani ambaye ni mzuri kuliko wewe na mwenye umbo zuri kuliko lako lakini havai hizo suruali wala vimini, ingawa mazingira yote yanamruhusu kufanya hivyo…yeye ameshinda katika mazingira magumu ya vishawishi vingi lakini wewe umeshindwa katika mazingira marahisi..Jua upendo wako kwa Mungu unapimwa!.

Unaposhindwa kumtafuta Mungu kwa kazi yako unayofanya masaa 8 tu kwa siku, na kusema upo bize sana…kumbuka kuna mwingine aliye bize kuliko wewe mwenye kufanya kazi masaa 10 mahali pengine lakini hakosi ibada, wala hakosi muda wa kusali na kuomba na kusoma Neno…ingawa anachoka kulko wewe…Fahamu kuwa upendo wako unapimwa!

Hivyo ndugu huu ni wakati wa kujipima kabla ya kupimwa!…na kujitathimini upya…

Kumbuka siku zote, usilisahau hili Neno utembeapo, uishipo…matendo yako yanapimwa katika mizani.

Ayubu 31: 5 “Kwamba nimetembea katika ubatili, Na mguu wangu umeukimbilia udanganyifu;

6 (Na nipimwe katika mizani iliyo sawasawa, Ili Mungu aujue uelekevu wangu);

Bwana atubariki

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

Je! Mwanamke anapaswa afunikwe kichwa anapokuwa ibadani?

KISIMA CHA MAJI YA UZIMA NI KILE KILE CHA ZAMANI.

NINI TUNAJIFUNZA KWA MWANA MPOTEVU NA NDUGUYE?

ZIKIMBIE TAMAA ZA UJANANI! NA MTU YEYOTE ASIUDHARAU UJANA WAKO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

WALA SIJIHUKUMU HATA NAFSI YANGU.

Kuna hatua unafika Mungu anahitaji umuangilie sana yeye kuliko kujiangalia nafsi yako ili uweze kusonga mbele katika kumtumikia. Lipo tatizo kubwa ambalo lilishawahi kunikumba mimi, siku za mwanzoni nilipookoka, na naamini linawakumbuka watu wengi hata sasa waliookoka, Jambo hilo mtume Paulo alishaliona na kulitolea ufumbuzi wake kwa ufunuo wa Roho..

Kuna wakati unafika, unaona kila jambo unaloweza kujaribu kulifanya unaona pengine linaweza likawa linamkosea Mungu, au kama umefanya dhambi fulani ukatubu, unaona kama vile Mungu hajakusamehe vizuri, au amekukakasirikia, na hiyo inakufanya ujilaumu muda mwingi, Unajihukumu na kuhitimisha kuwa Mungu hawezi kuwa na mimi tena, Mungu hawezi kunitumia, Mungu ananiona mimi ni mchafu sana, Nimeuhuzunisha moyo wake sana hivyo ameshakata tamaa na mimi..

Paulo alisema hivi..

1 Wakorintho 4:1 “ Mtu na atuhesabu hivi, kuwa tu watumishi wa Kristo, na mawakili wa siri za Mungu.

2 Hapo tena inayohitajiwa katika mawakili, ndiyo mtu aonekane kuwa mwaminifu.

3 LAKINI, KWANGU MIMI, SI KITU KABISA NIHUKUMIWE NA NINYI, WALA KWA HUKUMU YA KIBINADAMU, WALA SIJIHUKUMU HATA NAFSI YANGU.

4 MAANA SIJUI SABABU YA KUJISHITAKI NAFSI YANGU, lakini sihesabiwi haki kwa ajili hiyo; ila anihukumuye mimi ni Bwana.

5 Basi ninyi msihukumu neno kabla ya wakati wake, hata ajapo Bwana; ambaye atayamulikisha yaliyositirika ya giza, na kuyadhihirisha mashauri ya mioyo; ndipo kila mtu atakapoipata sifa yake kwa Mungu”.

Kama tunavyojua Paulo ni mtu ambaye mawazo yake yote yalielekea kwa Mungu sana, alikuwa anajitahidi kwa kadiri awezavyo kumpendeza Mungu lakini pengine katika Nyanja fulani za Maisha yake ya huduma alishawahi kufanya makosa kadha wa kadha, au alishawahi kushindwa kufanikisha hiki au kile kwa ajili ya Mungu, kiasi kwamba hata yeye mwenyewe au watu wengine wangemwona kama ameshindwa kabisa, lakini hapa anasema..

“Lakini, kwangu mimi, si kitu kabisa nihukumiwe na ninyi, wala kwa hukumu ya kibinadamu, wala sijihukumu hata nafsi yangu.

4 Maana sijui sababu ya kujishitaki nafsi yangu”

Unaona madhaifu yake hayakuwa sababu ya yeye kujihukumu kuwa anafaa au hafai mbele za Mungu, japokuwa hilo halimthibitishii kuwa anafaa, lakini hakuruhusu ajihukumu kwasababu haoni sababu kwanini afanya vile, Pengine aliwaza Mungu hakuwahi kumwambia kuwa hampendi, Au Mungu hakuwahi kumuonyesha katika maono kuwa hamtaki tena? Kama sivyo, ni kwanini ajihukumu mwenyewe?

Hivyo Paulo aliamua kuendelea kuishi Maisha ya kumtegemea Kristo kuliko kuutegemea ukamilifu wake wote umsaidie katika huduma yake, na hiyo ilimfanya afike mbali, japokuwa alikutana na milima na mabonde,

Lakini kumbuka jambo kama hili halimuhusu mtu anayefanya dhambi za makusudi. Wewe kama mzinzi, Maisha yako yapo mbali na wokovu unafanya dhambi kwa makusudi, ndani yako hakuna hofu yoyote ya Mungu, ujue kuwa hata kama hutajihukumu, basi dhamira yako itakushuhudia ndani yako kuwa kuwa wewe ni mnafki na mwovu. Na utahukumiwa siku za mwisho…Na kumbuka mojawapo ya dhambi za makusudi kabisa, zisizo za madhaifu, ni dhambi ya uzinzi na uasherati. Mtu anayefanya uasherati baada ya kuokoka anafanya dhambi ya makusudi inayostahili hukumu. Hivyo kama unaifanya ndugu iache mara moja.

Lakini ikiwa upo ndani ya Kristo, na una kiu kweli ya kuzidi kumpendeza Mungu na unajitahidi kujizuia kwa kila kitu kiovu, basi kataa hukumu yoyote inayokuja ndani ya moyo wako inayokuambia wewe hufai, kataa mawazo yote yanayokuambia unachofanya kwa Mungu hakimpendezi hata kidogo, kataa hayo mawazo yanayokuambia Mungu hana mpango wa wewe, yakija yaulize mbona Mungu hajawahi kuniambia hilo jambo?. Endelea kumtumikia Mungu kwa karama aliyoiweka ndani yako..

Ikiwa ulifanya makosa Fulani madogo, basi rekekebisha makosa yako, kisha endelea kusonga mbele, mtazame Kristo, na yeye atakuwa na wewe siku baada ya siku, Vilevile usikubali hukumu kutoka kwa mtu yeyote ikutaabishe moyo,..yupo mtu anaweza kukuambia wewe bado hujaitwa na Mungu kwa kutazama maisha uliyokuwa unaishi huko nyuma?…na akakwambia Mungu hawezi kukutumia mtu kama wewe, muulize mbona Mungu hajawahi kunisemesha mambo kama hayo? Wengine wanaweza kukutamkia maneno ya laana hata kama yataonekana yana ukweli ndani yake lakini wewe yakatae matazame Kristo, endelea na safari…

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

JE! NI LAZIMA WATU WOTE WANENE KWA LUGHA?

Je! Ni kweli ubatizo wa maji hatuuhitaji tena?

JE KUNA UISLAMU KATIKA BIBLIA?

Ni uthibitisho upi unaoonyesha kuwa kuna MBINGUNI na KUZIMU?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Je mtu akifa anakuwa hana dhambi tena?

 Je ni kweli mtu akifa anakuwa hana dhambi tena kufuatia hili andiko Warumi 6:7 “kwa kuwa yeye aliyekufa amehesabiwa haki mbali na dhambi.”


JIBU: Bwana Yesu alisema haya maneno mahali Fulani…

Yohana 8:21 “Basi akawaambia tena, Mimi naondoka, nanyi mtanitafuta; nanyi MTAKUFA KATIKA DHAMBI yenu; mimi niendako ninyi hamwezi kuja………

24 Kwa hiyo naliwaambieni ya kwamba MTAKUFA KATIKA DHAMBI ZENU; kwa sababu msiposadiki ya kuwa mimi ndiye, MTAKUFA KATIKA DHAMBI ZENU”.

Bwana Yesu aliwaambia Waandishi na Mafarisayo maneno hayo..kuonyesha kuwa Kama mtu akikataa kutubu dhambi angali hai na kumwamini basi atakufa na hizo dhambi zake (maana yake hizo dhambi zake zitamfuata hata huko anakokwenda, na atahukumiwa kulingana na hizo).

Hilo utalithibitisha katika andiko hili..

1Timotheo 5:24 “Dhambi za watu wengine zi dhahiri, zatangulia kwenda hukumuni; wengine dhambi zao zawafuata”.

Kwasababu hiyo basi mstari huo wa Warumi 6:7, haumaanishi kuwa mtu mwenye dhambi anapokufa basi anakuwa hana dhambi tena…bali unamaanisha kuwa mtu “yeye aliyekufa Pamoja na Kristo, amehesabiwa haki mbali na dhambi”…Maana yake mtu aliye ndani ya Kristo hakuna hukumu ya adhabu juu yake kwasababu anakuwa amevuka kutoka mautini kuingia uzimani, ingawa bado anaishi ulimwenguni.

Ndio maana ukianzia mstari wa 6 na kuendelea kidogo mpaka wa 8 utaelewa vizuri..anasema..

Warumi 6: 6 “mkijua neno hili, ya kuwa utu wetu wa kale ulisulibishwa pamoja naye, ili mwili wa dhambi ubatilike, tusitumikie dhambi tena;

7 kwa kuwa yeye aliyekufa amehesabiwa haki mbali na dhambi.

8 Lakini tukiwa tulikufa pamoja na Kristo, twaamini ya kuwa tutaishi pamoja naye”

Hivyo andiko hilo linatuhusu sisi sote…Hatuna budi kufa Pamoja na Kristo, kila mmoja wetu kwa kumwamini yeye na kutubu dhambi na kufufuka Pamoja naye kwa njia ya ubatizo wa maji na wa Roho Mtakatifu.

Warumi 6:3 “Hamfahamu ya kuwa sisi sote tuliobatizwa katika Kristo Yesu tulibatizwa katika mauti yake?

4 Basi tulizikwa pamoja naye kwa njia ya ubatizo katika mauti yake, kusudi kama Kristo alivyofufuka katika wafu kwa njia ya utukufu wa Baba, vivyo hivyo na sisi tuenende katika upya wa uzima”

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

ROHO YA MPINGA KRISTO IKITENDA KAZI SIKU HIZI ZA MWISHO

USIFE NA DHAMBI ZAKO!

TUMAINI NI NINI?

NAMI NINAZO FUNGUO ZA MAUTI, NA ZA KUZIMU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

USO WAKE ULIKUWA UMEHARIBIWA SANA ZAIDI YA MTU YE YOTE.

Wokovu huu ambao tumeupata bure, tusidhani yule aliyetugawia hakuingia gharama yoyote kuupata,..Halikuwa ni jambo la kukaa mbinguni tu na kusema niamnini mimi mtaokoka!..Hilo lisingewezekana kamwe, ili kuunda kitu kinachoitwa “wokovu” ilimpasa afuate kanuni Fulani..ilimpasa kwanza aache enzi na mamlaka yote mbinguni, awe hana kitu, kisha ashuke hapa duniani, aishi kama mwanadamu mwingine yoyote yule aliyezaliwa na mwanamke, aumwe wakati mwingine, audhiwe, apitie umaskini, kisha na yeye pia ajaribiwe na shetani, aonekane kama atashinda au la, ..Lakini kama tunavyosoma aliyashida yote kwa muda wa miaka 33 bila kutenda dhambi yoyote licha ya kupitia vipingamizi vyote vya kibinadamu..

Lakini sio hilo tu, ilimgharimu uhai pia, ili aweze sasa kukikamilisha hicho kitu kinachoitwa WOKOVU KWA MWANADAMU.. Ndio hapo akalazimika aende msalaba akapigwe afe, damu imwagike ili kusudi kwamba mimi na wewe tupokee huo wokovu kwa gharama alizoingia..

Lakini wengi wetu tunadhani mateso aliyoyapita yalikuwa ni ya kawaida tu, biblia inatuambia Bwana aliharibiwa uso wake, na mwili wake, Zaidi ya mwanadamu mwingine aliyewahi kuishi hapa duniani..

Soma..

Isaya 52:13 “Tazama, mtumishi wangu atatenda kwa busara, atatukuzwa, na kuinuliwa juu, naye atakuwa juu sana.

14 Kama vile wengi walivyokustaajabia, (USO WAKE ULIKUWA UMEHARIBIWA SANA ZAIDI YA MTU YE YOTE, NA UMBO LAKE ZAIDI YA WANADAMU),

15 ndivyo atakavyowasitusha mataifa mengi; wafalme watamfumbia vinywa vyao; maana mambo wasiyoambiwa watayaona; na mambo wasiyoyasikia watayafahamu”.

Jaribu kuchua muda utafakari!, chukua muda utafakari hata dakika 15 au 20, fikiria huo uso uliwezekanikaje kuharibiwa Zaidi ya mtu yoyote hapa duniani, na mwili wake vivyo hivyo, ndipo utakapofahamu kuwa mapigo aliyopigwa Bwana hayakuwa ya mwanadamu wa kawaida, alikuwa kama nyama buchani, kile unachokifahamu kwenye filamu ni mfano mdogo wa jinsi Bwana alivyokuwa anaonekana, na hiyo yote ilimpasa apitie vinginevyo mimi na wewe tusingeupata wokovu..

biblia inasema..

“Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, NA KWA KUPIGWA KWAKE SISI TUMEPONA”.(Isaya 53:5)

Uso wake na mwili wake usingeharibiwa kwa mapigo mabaya kama yale ambayo mengine hata hayajaandikwa kwenye biblia, mimi na wewe leo hii tusingeufikia uponyaji wa roho zetu. Lakini jiulize wewe ndugu ambaye bado hujamwamini yeye licha ya kwamba umekusogezea wokovu huo bure mbele yako bila malipo yoyote..Jiulize, siku ya leo ukifa katika hali yako ya dhambi utawezaje kuokoka?

Kumbuka wokovu unapatikana bure, sasa bila gharama yoyote, usisubiri mpaka mlango wa neema ufungwe ndipo uje uutafute, hilo halitawezekana tena, wakati huo ukifika wewe utakuwa ni wa kusubiria tu kwenda jehanamu ya moto, lakini leo hii ukiyasalimisha Maisha yako kwake, licha tu ya kwamba unayo tiketi ya kwenda mbinguni, lakini pia ile damu yake ya thamani iliyomwagika pale msalabani wakati huo huo itaanza kukunenea mema juu ya Maisha yako angali ukiwa bado hapa duniani.

Hivyo tubu ndugu kama bado hujafanya hivyo..maadamu Bwana Yesu ni Rafiki yetu wa kweli, anayetupenda upeo.

Jina lake libarikiwe daima.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

YATAFUTE YALIYO JUU SIKU ZOTE.

Kwanini Mungu alisema hakuna mtu awazaye kuuona uso wake akaishi?

KIFO CHA REINHARD BONKEY KINAACHA UJUMBE GANI KWETU?

NI KITU GANI PETRO NA YOHANA WALIKIGUNDUA KABURINI?

KANUNI RAHISI YA KUFANIKIWA.

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!

NGUVU YA MSAMAHA

Rudi Nyumbani:

Print this post

Kwanini Yesu Kristo ni mwana wa Adamu?

JIBU: Vipo vyeo vitatu maalumu ambavyo vilimtambulisha Bwana Yesu Kristo…1) Mwana wa Mungu 2) Mwana wa Adamu 3) Mwana wa Daudi. Vyeo hivi kila kimoja kina maana yake..

Sasa kabla ya kuendelea mbele zaidi…ni muhimu kufahamu kuwa cheo cha “Mwana” ni cheo cha “urithi”…Maana yake ni kwamba mfano ukiwa na mtoto wako mmoja wa pekee huyo atarithi kila ulicho nacho…ikiwemo enzi yako yote, mali zako pamoja na hata jina lako…

Sasa katika biblia..mahali popote ambapo Neno Mwana linaanza kwa herufi kubwa…hilo linamzungumzia mtu mmoja tu maalumu ambaye ni Yesu Kristo…lakini ukiona neno “mwana” limeanza kwa herufi ndogo kama hivyo, basi fahamu ni mtu mwingine tofauti na Yesu anayezungumziwa hapo.. Kwa mantiki hiyo basi “wana wa Mungu” wapo wengi lakini “Mwana wa Mungu ni mmoja tu”…mimi na wewe tuliompokea Yesu ni wana wa Mungu….kadhalika wana wa Daudi wapo wengi..lakini “Mwana wa Daudi” ni mmoja tu ambaye ni Yesu…Sulemani alikuwa pia ni ‘mwana wa Daudi’, Hezekia, Yosia, Manase wote hao walikuwa ni wana wa Daudi….Hali kadhalika pia “wana wa Adamu wapo wengi”…mimi ni mwana wa Adamu(au kwa kifupi Mwanadamu)..wewe ni mwana wa Adamu lakini “Mwana wa Adamu” yupo mmoja tu ambaye ni Yesu…ni kama vile miungu wapo wengi lakini Mungu ni mmoja tu!.

Sasa tukirudi kwenye shabaha yetu ya msingi, ambapo tumeona kuwa Neno ‘mwana’ linazungumzia ‘urithi’

Hivyo basi vyeo hivyo vitatu tunaweza kuviweka katika mnyumbuliko ufuatao…1)Mrithi wa Mungu 2) Mrithi wa Adamu na 3) Mrithi wa Daudi.

Sasa unaweza kujiuliza Kristo alirithi nini kutoka kwa hawa watatu?

  1. Mrithi wa Mungu.

Kama mtu ataitwa Mwana wa Mungu maana yake ni kwamba ni Mrithi wa enzi yote ya Mungu na Ukuu …na huyo si mwingine zaidi ya Yesu Kristo, ambaye alirithishwa vyote.

Waebrania 1:1 “Mungu, ambaye alisema zamani na baba zetu katika manabii kwa sehemu nyingi na kwa njia nyingi,

2 mwisho wa siku hizi amesema na sisi katika MWANA, ALIYEMWEKA KUWA MRITHI WA YOTE, TENA KWA YEYE ALIUFANYA ULIMWENGU.

3 Yeye kwa kuwa ni mng’ao wa utukufu wake na chapa ya nafsi yake, akivichukua vyote kwa amri ya uweza wake, akiisha kufanya utakaso wa dhambi, aliketi mkono wa kuume wa Ukuu huko juu”

Kwahiyo hiyo ndio sababu ya Kristo kujulikana kama MWANA WA MUNGU..Ni kwasababu amerithi milki zote za Mungu..

Mathayo 28:18 “Yesu akaja kwao, akasema nao, akawaambia, Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani”.

  1. Mrithi wa Daudi.

Cheo cha pili ni cheo cha MWANA WA DAUDI/Mrithi wa Daudi..Sasa ili kujua ni kwanini Kristo aliitwa mwana wa Daudi ni vizuri kumjua kwanza Daudi alikuwa ni nani…(kwa maelezo marefu unaweza kututumia ujumbe inbox tutakutumia somo lake)…lakini kwa ufupi ni kwamba Daudi alikuwa ni mfalme pekee aliyepata Hekima ya kufikiria kumjengea Mungu nyumba ya kifalme katika wa Yerusalemu…na hivyo kumfanya Mungu kuuchagua ule mji kuwa makao makuu yake ya kifalme Duniani (yaani Yerusalemu).

Kama sio Daudi basi mpaka leo pengine Mungu asingekuwa na mji wake maalumu duniani kati ya miji ya Israeli…(Tusingelisikia hili neno Yerusalemu au Sayuni likirudiwa rudiwa katika maandiko, kwani ungekuwa mji kama miji mingine tu, wala ile Yerusalemu mpya kwenye ufunuo pengine ingeitwa kwa jina lingine)…

Lakini Daudi ndiye aliyefanya Yerusalemu ikawa mji wa kifalme wa mwokozi..na Mungu alimwahidi hatakosa mtu wa kukaa katika kiti cha kifalme kutoka katika uzao wake…na katika uzao wake huo yupo mmoja ambaye ni mkuu sana alitabiriwa kutokea huko na huyo si mwingine zaidi ya YESU KRISTO mwenyewe(kasome Mathayo 1:1-17) ambaye atakuwa mfalme juu ya Dunia nzima! Na ndiye atakayeijenga Yerusalemu mpya ile itakayoshuka kutoka mbinguni…na kukaa na watu wake. Na ndio maana Kristo ilimpasa aitwe mwana wa Daudi kufuatana na yale Daudi aliyoyafanya na kukabidhiwa.

  1. Urithi wa Adamu.

Na cheo cha Mwisho cha Yesu Kristo ni cheo cha MWANA WA ADAMU au Mwana wa mtu,…sasa kama tunavyomjua Adamu alikuwa ni mtu wa kwanza kuumbwa na kupewa Urithi wote na mamlaka yote duniani, kwamba atawale kila kitu, na kwamba viumbe vyote vitamwogopa!….lakini kama tunavyojua aliuuza na kuupoteza ule urithi wake aliopewa na Mungu kwa adui shetani…Hivyo ili urithi huo umrudie tena mwanadamu..basi hakuna budi aje kutokea Adamu mwingine wa pili, ambaye atakaribiana sana kufanana na Yule Adamu wa kwanza,…ambaye ataurithi ule urithi na enzi yote aliyopewa Adamu ya kwanza…

1Wakorintho 15:45 “Ndivyo ilivyoandikwa, Mtu wa kwanza, Adamu, akawa nafsi iliyo hai; Adamu wa mwisho ni roho yenye kuhuisha”.

Adamu wa pili atakuwa ni mwanamume kama Yule wa kwanza, naye atapewa mamlaka kama Yule wa Kwanza wa pale Edeni, na yeye ni lazima awe wa kwanza kuumbwa …na huyo si mwingine zaidi ya Yesu Kristo..ambaye ndiye limbuko letu rohoni na ndiye aliyekabidhiwa mamlaka yote ya duniani. Hiyo ndiyo sababu Yesu anaitwa Mwana wa Adamu…ni kwasababu amerithi mamlaka yote na enzi yote Yule Adamu wa kwanza aliyokuwa nayo (aliyopewa na Mungu)..

Mathayo 11:27 “Akasema, Nimekabidhiwa vyote na baba yangu; wala hakuna amjuaye Mwana, ila Baba; wala hakuna amjuaye Baba, ila Mwana, na ye yote ambaye Mwana apenda kumfunulia”.

Hivyo Yesu Kristo ndiye Mwanzo na Mwisho, Alfa na Omega…Ndiye mwanadamu kamili, ndiye aliye na mamlaka yote sasa, ndiye mwenye enzi ya kifalme, ndiye Mungu mwenyewe katika mwili. Na ndiye njia ya kufika mbinguni…Kama hujamwamini wala kumpokea…ni vyema ukafanya hivyo kwasababu hakuna njia nyingine yoyote unaweza kumfikia Mungu kama isipokuwa kwa kupitia yeye..

Ufunuo 22:12 “Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo.

13 MIMI NI ALFA NA OMEGA, MWANZO NA MWISHO, WA KWANZA NA WA MWISHO.

14 Heri wazifuao nguo zao, wawe na amri kuuendea huo mti wa uzima, na kuingia mjini kwa milango yake”.

Bwana atubariki. Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

KWANINI YESU KRISTO NI WA MUHIMU KWETU SASA?

USIPOKUWA MWAMINIFU, NAFASI YAKO ITACHUKULIWA.

TAZAMA, MWISRAELI KWELI KWELI, HAMNA HILA NDANI YAKE!

Kuna ufufuo wa aina ngapi?

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

MAJESHI YA PEPO WABAYA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

VUKA UJE MAKEDONIA UTUSAIDIE.

Shalom,

Nakukaribisha tutafakari pamoja vifungu vifuatavyo vya maandiko, naamini lipo jambo utajifunza mwishoni mwa somo..

Matendo 16:6 “Wakapita katika nchi ya Frigia na Galatia, wakikatazwa na Roho Mtakatifu, wasilihubiri lile neno katika Asia.

7 Walipofika kukabili Misia wakajaribu kuenda Bithinia, lakini Roho wa Yesu hakuwapa ruhusa,

8 wakapita Misia wakatelemkia Troa.

9 Paulo akatokewa na maono usiku; alimwona mtu wa Makedonia amesimama, akimsihi, na kumwambia, Vuka, uje Makedonia utusaidie”.

Wengi wetu tunafahamu vipingamizi pekee mtume Paulo alivyokuwa anapitia vya kuhubiri injili vilitoka kwa shetani, lakini hatujui kuwa kuna wakati mwingine Mungu mwenyewe alikuwa anamzuia Paulo asihubiri injili japokuwa alitamani kufanya hivyo,.

Mungu anafanya hivyo sio kwamba hataki watu wahubiriwe injili kama ilivyo kwa shetani, hapana, bali ni kawaida yake kuwapa vipaumbele vya kwanza wale ambao wanaonyesha kiu ya kutaka kumjua yeye.

Ili kutimiza haya maandiko.

Mathayo 5:6 “Heri wenye njaa na kiu ya haki; Maana hao watashibishwa”.

Na haya..

Mathayo 5:3 “Heri walio maskini wa roho; Maana ufalme wa mbinguni ni wao”.

Kama ukichunguza hiyo mistari utaona, Mungu hakumkataza Paulo kufika kabisa katika hiyo miji iliyotajwa hapo juu, lakini aliifikia na kuipita, kuonyesha kuwa kama kungekuwa na utayari wa wenyeji wa pale kutamani kumjua Mungu basi wangeanzwa kwanza wao, kisha ndio wafuate wale wengine..

Jaribu kufikiria anafika pale Frigia, anataka tu kuanza kuhubiri Mungu anamzuia, anaondoka anaenda mji unaofuata Galatia huko nako Mungu anamzuia anaondoka tena anafikiria labda ashuke kwenye miji mingine ya Asia (ambayo ndio kama Efeso, Smirna, Pergamo, Laodikia n.k. ) lakini huko nako Mungu anamwambia asihubiri chochote aondoke…

Haishii hapo anaondoka tena Asia anafika mji ulioitwa Misia ili aanze kuhubiri bado Mungu anamkataza, anafika Troa bado Mungu hampi kibali, wakati sasa akiwa hapo Troa ukingoni kabisa mwa mji ndipo Mungu anamwonyesha maono ambayo yalikuwa yanaonyesha jinsi watu wa kule Ng’ambo ya bahari Makedonia walivyokuwa wanahitaji msaada mkubwa sana wa kiroho..

Ndipo hapo utaona inamgharimu Paulo kuvuka bahari sasa asafiri, mpaka kwenye hiyo miji ya Makedonia ambayo, ilikuwa ni Filipi, Thesalonike, na Beroya.. Ili kuihubiri injili.. Si jambo rahisi

Ili kuelewa vizuri jaribu kutengeneza picha labda mtumishi wa Mungu anatoka nchi ya mbali Afrika Magharibi labda tuseme Ghana, anafika nchi za Afrika ya kati kama vile Congo n.k., Mungu anamwambia pita usihubiri, anafika mpaka nchi zetu za Afrika mashariki, Anaanzia Uganda anaambiwa pita, anafika Kenya anaambiwa pita, anafika hapa Tanzania, bado Mungu anamwambia usihubiri hapo, sasa akiwa ameshavuka kote toka kigoma, akiwa pale Daresalaam, Mungu anamwambia panda Meli nenda taifa la India wapo watu wangu kule wanahitaji msaada wa kunijua mimi..

Ndivyo ilivyokuwa kwa Mtume Paulo na wenzake, walienda Makedonia na kweli kule walikutana na watu ambao kwanza walikuwa ni maskini, lakini walikuwa tayari kumtolea Mungu kwa moyo wao wote..na zaidi ya yote walikuwa tayari kulipokea Neno la Mungu, mfano watu wa Beroya ndio wale ambao walikuwa wapo tayari kuchunguza maandiko ya kujua ufasaha wa yote,

2Wakorintho 8:1 “Tena ndugu zetu, twawaarifu habari ya neema ya Mungu, waliyopewa makanisa ya Makedonia;

2 maana walipokuwa wakijaribiwa kwa dhiki nyingi, wingi wa furaha yao na UMASKINI WAO uliokuwa mwingi uliwaongezea utajiri wa ukarimu wao.

3 Maana nawashuhudia kwamba, kwa uwezo wao, na zaidi ya uwezo wao, kwa hiari yao wenyewe walitoa vitu vyao;

Hivyo mimi na wewe tunajifunza nini?

Mungu ni yeye ule jana na leo na hata milele, kama mengi ya makanisa ya Asia hayakustahili kupewa neema ya wokovu kwanza, atafanya na kwetu vivyo hivyo kama hatutakuwa tayari kuipokea.

Tupaswa tujiulize je! mioyo yetu ni kweli ina kiu ya kumjua Mungu, kiasi kwamba mpaka rohoni Mungu anatufananisha na watu wa Makedonia?.. Vuka, uje Makedonia utusaidie?. Je! ni kweli tunaonyesha tunahitaji msaada kutoka kwa Mungu? Je tunastahili msaada?.. Kama ni kweli tunaonyesha tunahitaji msaada, basi hapo ndipo Mungu atakapofungua njia ya kutusaidia, kwa namna ya ajabu.

Na tunaonyesha tunahitaji msaada kwa namna gani?.. Tunaonyesha kwa bidii yetu sisi ya kutafuta yeye kwa nguvu zetu zote, kwa akili zetu zote, kwa mioyo yetu yote na kwa Roho zetu zote.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

SAYUNI ni nini?

Mitume wote waliopita walikuwa ni watu weupe hata manabii wote waliopita hadi Ma-papa ni ngozi nyeupe. ni kweli ngozi nyeusi ililaaniwa ?

USIPOKUWA MWAMINIFU, NAFASI YAKO ITACHUKULIWA.

TABIA YA KIPEKEE USIYOIJUA KUHUSU NENO LA MUNGU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

USIISHI BILA KUIFANYA KAZI YA MUNGU KABISA..

Shalom mtu wa Mungu, karibu tuyatafakari maandiko…leo ni siku nzuri Bwana aliyotupa..hivyo ni vyema tukachukua nafasi hii kulitafakari Neno lake kwa ufupi..

Kumbuka siku zote kuwa baada ya kumpokea Kristo, kila mmoja wetu anawajibu wa kuifanya kazi ya Mungu kupitia karama Mungu aliyoiweka ndani yake. Kuna hatari kubwa sana ya kutoitumia karama Mungu aliyoiweka ndani yako kabisa….Na madhara makubwa yapo baada ya maisha haya…wakati ule ambapo watakatifu watapewa thawabu zao wewe hutakuwa na chochote…

Katika siku ile waliokuwa waaminifu kwa karama zao watapewa thawabu kubwa zaidi..na wale waliokuwa walegevu na kuleta faida ndogo katika ufalme wa mbinguni watalipwa kidogo, na wale ambao hawajafanya kitu kabisa hawatapewa chochote…

Lakini ni heri kufanya hata kama ni KIDOGO sana ukapata kitu kule kuliko kutofanya kabisa…

Hebu naomba usome mfano huu Bwana alioutoa…inawezekana ulishawahi kuusoma hapo kabla mara nyingi, na kuurudia rudia…. lakini hebu chukua muda tena sasa hivi kuusoma hadi mwisho taratibu, pasipo kuruka kipengele hata kimoja, kuna kitu cha kipekee sana nataka tujifunze leo.

Luka 19:11 “Waliposikia hayo, aliongeza kusema mfano, kwa sababu alikuwa karibu na Yerusalemu, na wao walidhani ya kuwa ufalme wa Mungu utaonekana mara.

12 Basi akasema, Mtu mmoja, kabaila, alisafiri kwenda nchi ya mbali, ili ajipatie ufalme na kurudi.

13 Akaita watu kumi katika watumwa wake, akawapa mafungu kumi ya fedha, akawaambia, FANYENI BIASHARA HATA NITAKAPOKUJA.

14 Lakini watu wa mji wake walimchukia, wakatuma wajumbe kumfuata na kusema, Hatumtaki huyu atutawale.

15 Ikawa aliporudi, ameupata ufalme wake, aliamuru waitwe wale watumwa aliowapa fedha, ili ajue faida aliyopata kila mtu kwa biashara yake.

16 Akaja wa kwanza, akasema, Bwana, fungu lako limeleta faida ya mafungu kumi zaidi.

17 Akamwambia, Vema, mtumwa mwema; kwa vile ulivyokuwa mwaminifu katika neno lililo dogo, uwe na mamlaka juu ya miji kumi.

18 Akaja wa pili, akasema, Bwana, fungu lako limeleta mafungu matano faida.

19 Akamwambia huyu naye, Wewe uwe juu ya miji mitano.

20 Akaja mwingine akasema, Bwana, hili ndilo fungu lako, ambalo nililiweka akiba katika leso.

21 Kwa maana nilikuogopa kwa kuwa u mtu mgumu; waondoa usichoweka, wavuna usichopanda.

22 Akamwambia, Nitakuhukumu kwa kinywa chako, mtumwa mwovu wewe. Ulinijua kuwa ni mtu mgumu, niondoaye nisichoweka, na kuvuna nisichopanda;

23 BASI, MBONA HUKUIWEKA FEDHA YANGU KWA WATOAO RIBA, ili nijapo niipate pamoja na faida yake?

24 Akawaambia waliosimama karibu, Mnyang’anyeni hilo fungu, mkampe yule mwenye mafungu kumi.

25 Wakamwambia, Bwana, anayo mafungu kumi.

26 Nawaambia, Kila aliye na kitu atapewa, bali yule asiye na kitu atanyang’anywa hata alicho nacho”.

Mfano huo unamhusu Bwana Yesu mwenyewe, yeye ndio mfano wa huyo mtu kabaila..ambaye aliondoka na kwenda nchi ya mbali(mbinguni) kutuandalia ufalme…na alipoondoka alitupatia vipawa (karama) akatuambia tukawafanye watu wote kuwa wanafunzi (maana yake kuwahubiria na kuwageuza wamwamini yeye kila mmoja kwa kipawa alichopewa)…Na siku moja atarudi kutoka huko nchi ya mbali(mbinguni)…alipokwenda kututengenezea ufalme…atarudi duniani kwaajili ya utawala wa miaka 1,000 (Ufunuo 20).. Na siku atakaporudi atawaangamiza wale wote ambao hawakumkubali (yaani watu waovu)..Na baada ya kuwaangamiza waovu wote ndipo atakapowakusanya watumishi wake waliompokea…na hapo kila mmoja ataketi na kutoa hesabu ya faida aliyoileta katika ufalme wa mbinguni..

Watasimama wachungaji, watasimama waimbaji, watasimama mitume, watasimama mashemasi, waalimu, manabii, maaskofu, wazee wa kanisa, waumini wote na kila mmoja atatoa hesabu jinsi alivyoitumia karama yake…waliofanya vizuri watapewa mamlaka makubwa na waliokuwa wavivu watakosa vyote…

Sasa katika kisa hicho tunasoma kuna mmoja alifukia talanta yake chini…kwa uvivu akijitumainisha kwamba Bwana huwa hasaidiwagi kazi…yeye anang’oa pando asilolipanda, kazi ambayo hajaifanya yeye anaiharibu!…kwahiyo akajifariji kwamba Mungu huwa hasaidiwi kazi…hatutegemei hata tusipokwenda kuhubiri walio wake watakuja tu!.. kwanza unaweza kwenda kuhubiri ukakosea kosea maneno ndio ukawa umemuudhi badala ya kumfurahisha……pia sio lazima sana kumtolea kwani hata tusipochangia chochote kwenye kazi yake yeye ni tajiri na sisi ni mavumbi hivyo atafanya njia tu kwa vyovyote vile(hasaidiwi kazi)……pia yeye hahitaji sana sifa zetu, tayari anao malaika wengi wanaomwimbia….. n.k

Kwahiyo kwa kujitumainisha huko na visingizio hivyo… mtu wa namna hii akawa hafanyi kazi ya Mungu akafananishwa na mtu aliyefukia fedha yak echini ya shimo…siku ile ikafika na Bwana akamhukumu kwa kinywa chake…

Ndugu mpendwa baada ya kuokoka…usikae ufikiri kwasababu Mungu ni mkuu basi hatutegemei sisi….Ni kweli hatutegemei anaweza kufanya asilimia mia pasipo sisi…lakini hataki tuwe wajinga!…Sio kwasababu kasema maneno haya…

Matendo 7:49 “Mbingu ni kiti changu cha enzi, Na nchi ni pa kuwekea miguu yangu; Ni nyumba gani mtakayonijengea? Asema Bwana,

50 Au ni mahali gani nitakapostarehe? Si mkono wangu uliofanya haya yote?”

Basi na sisi ndio tubweteke tusimjengee nyumba…kwasababu amesema yeye hakai kwenye nyumba zilizofanywa na mikono yetu…Ndugu Usikae ufikiri hivyo kamwe!.. Daudi aliujua vizuri huo mstari pamoja na Sulemani mwanawe lakini walimjengewa Bwana nyumba hivyo hivyo…na Mungu akapendezwa nao..Sikia maneno Sulemani aliyoyasema..

1Wafalme 8: 26 “Sasa, Ee Mungu wa Israeli, nakusihi, ulithibitishe neno lako, ulilomwambia mtumishi wako, Daudi, baba yangu.

27 LAKINI MUNGU JE? ATAKAA KWELI KWELI JUU YA NCHI? TAZAMA, MBINGU HAZIKUTOSHI, WALA MBINGU ZA MBINGU; SEMBUSE NYUMBA HII NILIYOIJENGA!

28 Walakini uyaelekee maombi ya mtumwa wako, na dua yake, Ee Bwana, Mungu wangu, uisikilize sauti na maombi ya mtumwa wako, aombayo mbele zako leo.

29 Macho yako yafumbuke na kuielekea NYUMBA HII usiku na mchana, mahali hapa ulipopataja, ukasema, Hapa ndipo litakapokuwapo jina langu; ili uyasikie maombi ya mtumwa wako aombapo akikabili mahali hapa”.

Walijua Mungu mbingu hazimtoshi na huku duniani ni mahali pa kuwekea miguu yake..lakini walilazimisha kumjengea Mungu duniani japokuwa waliyajua hayo maandiko…na mpaka leo Hekalu la Sulemani linajulikana.

Vivyo hivyo na wewe..usiseme Bwana ana malaika wengi…usiseme Bwana hahitaji fedha yangu kwani dhahabu zote na fedha zote ni za kwake… Usiseme sio lazima kujisumbua kuhubiri kwani Bwana anao watumishi wengi…usiseme sio lazima kujisumbua kuimarisha kazi ya Mungu kwasababu Mungu hahitaji msaada kutoka kwetu..ukifanya hivyo utakuwa umefukia talanta yako chini uliyopewa…

Na Mwisho kabisa Bwana alimwambia Yule mtu aliyefukia ile fedha chini maneno haya…” BASI, MBONA HUKUIWEKA FEDHA YANGU KWA WATOAO RIBA”… Mtu anayeweka fedha kwa watoa riba…maana yake haendi kuifanyia shughuli yoyote ile hela..ni kuiweka tu baada ya wakati Fulani inajizalisha…ni kama vile umemkopesha mtu hela…Sasa kazi ya kukopesha haitumii jasho lolote…ni kuwekeza tu hela na kusubiria faida basi!….Hata hiyo kazi nyepesi ambayo haihitaji jasho! Bwana angetegemea aione kwa huyu mtu lakini hakuiona..

Kadhalika na wewe…inawezekana huwezi kabisa kusimama mimbarani, au kwenda mitaani kuhubiri… basi angalau wekeza kwenye kazi ya Mungu kwa fedha zako au mali zako kwa uaminifu, nunua kinanda, nunua mifuko kadhaa ya cement, au nunua chochote kile uwezacho kipeleke nyumbani kwa Mungu…kwasababu unapomtolea Mungu, fedha au mali zile zinakwenda kutumika katika kuifanya kazi ya Mungu na hivyo unaleta faida katika ufalme wa Mbinguni… ukifanya hivyo angalau Bwana atakuheshimu siku ile utakuwa umeiweka talanta yako kwa watoa riba…

Bwana atusaidie sana katika hayo..

Kama bado hujampa Yesu maisha yako…tunaishi katika siku za mwisho, Kristo yupo mlangoni kurudi…hivyo tubu leo kwa kumaanisha kuacha dhambi zote unazozifanya kama ulevi, rushwa, anasa, uasherati, uuaji, ufiraji, ulawiti,ushoga, usagaji, utazamaji wa picha za ngono, kujichua na nyingine zinazofanana na hizo…Tubu leo kwa dhati na amua kuziacha…na baada ya kuomba rehema Bwana atukusamehe kama alivyoahidi…Na amini kashakusamehe kama umetubu kwa dhati!..Na baada ya hapo tafuta ubatizo sahihi ambao ni wa maji tele na kwa jina la Yesu ambalo ndio jina la Baba, Mwana na Roho Mtakatifu…na baada ya hapo Roho Mtakatifu ambaye tayari atakuwa ameshafika karibu yako atakupa uwezo wa kuzishinda hizo dhambi ulizoziacha..ili usizirudie tena…na mengine yaliyosalia atakuongoza kuyafanya.

Maran atha

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

USITUPE LULU ZAKO MBELE YA NGURUWE.

Ni rahisi zaidi ngamia kupenya tundu ya sindano.

MAOMBI YA VITA

FAIDA ZA MAOMBI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

NI KITU GANI PETRO NA YOHANA WALIKIGUNDUA KABURINI?

Shalom..

Asubuhi ile Mariamu Magdalene alipokwenda kaburini na kukuta jiwe limeondolewa na mwili wa Yesu haupo, aliondoka ghafla na kwenda kuwapa taarifa wanafunzi wa Yesu, na kuwaambia Bwana hayupo kaburini wamemwiba na hatujui ni wapi walipompeleka..

Taarifa hiyo ya kushtusha iliwafanya watu wawili waondoke mahali pale kwa kasi sana, mmoja alikuwa ni Yohana na mwingine alikuwa ni Petro ili kwenda kuthibitisha kama waliyoelezwa ni kweli au La..

Yohana 20:2 “Basi akaenda mbio, akafika kwa Simoni Petro na kwa yule mwanafunzi mwingine ambaye Yesu alimpenda, akawaambia, Wamemwondoa Bwana kaburini, wala hatujui walikomweka.

3 Basi Petro akatoka, na yule mwanafunzi mwingine, wakashika njia kwenda kaburini.

4 Wakaenda mbio wote wawili; na yule mwanafunzi mwingine akaenda mbio upesi kuliko Petro, akawa wa kwanza kufika kaburini.

5 Akainama na kuchungulia, akaona vitambaa vya sanda vimelala; lakini hakuingia.

6 Basi akaja na Simoni Petro, akaingia ndani ya kaburi; akavitazama vitambaa vilivyolala,

7 na ile leso iliyokuwako kichwani pake; haikulala pamoja na vitambaa, bali imezongwa-zongwa mbali mahali pa peke yake.

8 Basi ndipo alipoingia naye yule mwanafunzi mwingine aliyekuwa wa kwanza wa kufika kaburini, akaona na kuamini.

9 Kwa maana hawajalifahamu bado andiko, ya kwamba imempasa kufufuka”.

Sasa ukiangalia hapo, utagundua Yohana alipofika pale kaburini na kuchungulia kwa mbali, aliona kweli Bwana hayupo na vitambaa vya sanda vimelala pale chini, pengine hilo lilimpa uhakika kuwa kweli mwili wa Bwana uliibiwa usiku na kuhamishwa pale na kupelekwa mafichoni sawasawa na maneno ya Mariam Magdalene..

Lakini tunaona Petro alipokuja baadaye kidogo, yeye kuishia pale mlangoni tu, bali alipitiliza moja kwa moja mpaka ndani kabisa mwa kaburi pale Bwana alipokuwa amelazwa ili kuthibitisha jambo hilo, Lakini alipofika karibu aliona jambo lingine la kushangaza kidogo, ambalo ndio lililowapa uhakika kuwa Bwana hakuibiwa bali ni kweli alifufuka..

Jambo hilo pengine hata wewe hukuwahi kulifahamu, ukisoma huo mstari wa 7 utaona vitambaa vya sanda vilikuwepo kweli pale chini sawasawa na Yohana alivyoona kule nje, lakini ile LESO ya kichwani biblia inasema haikuwa Pamoja na vitambaa bali ilizongwa zongwa mbali kabisa mahali pake yenyewe.. Sasa hilo neno kuzongwa zongwa biblia inamaanisha KUKUNJWA VIZURI, yaani hiyo leso ya kichwani ilikunjwa vizuri kwa utashi na Bwana mwenyewe kisha akaenda kuiweka kwa mbali kidogo na vile vitambaa vilivyokuwa vimefungwa mwilini mwake, pengine kwenye mwamba wa juu kidogo, mbali na pale alipokuwa amelala..

Hilo ni jambo la kufikirisha sana… Kama kweli wezi walikuja kumuiba wasingekuwa na muda wa kuikunja leso na kuiweka sehemu yake yenyewe mfano wa mtu anayekunja shati lake na kuliweka kabatini.. mwizi hawezi kufanya kazi kama hiyo..

Hilo ni tendo linaloonyesha kuwa Bwana hakuibiwa, bali alifufuka, na alipofufuka alianza kujifungua yeye mwenye taratibu, alipoliza, akaichukua ile leso ya kichwa akaanza kuikunja bila haraka yoyote akaenda kuiweka ndipo akaondoka..

Hilo ndilo lililowafanya Petro na Yohana biblia iseme katika mstari wa nane, wakaamini..

Habari hiyo inatufundisha nini?

Hatuwezi tukaufahamu ukweli wa Kristo kwa kuambiwa ambiwa tu, vilevile bado hatuwezi kuelewa siri ya kufufuka kwake kwa kusimama mlangoni mwa kaburi lake, Tutaelewa siri za Kufufuka kwa Kristo kwa kuzama kabisa mule kaburini alipokuwepo kama Petro, yaani kuwa tayari kufa na Kristo na kufufuka Pamoja naye kwa Habari ya dhambi, ndipo tutakapoelewa siri za kufufuka kwake kwa mapana na marefu..

Tukubali tu tusipotaka kuzama ndani katika wokovu, kamwe hatutakaa tuelewe maana ya ufufuo maishani mwetu, tukiwa wakristo vuguvugu, au wakristo jina, au wakristo wa kusita sita, wakristo wa kuvutwa vutwa tujue kuwa wapo tuliowaacha nyuma mfano wa Petro watatutangulia siku moja kuzijua siri za Kristo kuliko sisi ambao tunajiona tumeshajua kila kitu, na huku bado tupo mguu mmoja nje mwingine ndani.

Naamini hatutakuwa wasikiaji tu wa hadithi, bali tutayatendea kazi, tutazama kaburini kuuthibitisha ufufuo,…hicho ndicho Bwana anachokitaka maishani mwetu.

Bwana atubariki sote.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

SHETANI ANAITHAMINI HATA MAITI YAKO.

JE! PAKA KULIA USIKU NI ISHARA YA UCHAWI?

ZIKIMBIE TAMAA ZA UJANANI! NA MTU YEYOTE ASIUDHARAU UJANA WAKO.

Nitaitofautishaje sauti ya Malaika na ya Roho Mtakatifu?

HAPO NDIPO WATU WALIPOANZA KULIITIA JINA LA BWANA.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

Rudi Nyumbani:

Print this post

TUNA JUKUMU LA KWENDA KUTEKA MATEKA.

Shalom, mtu wa Mungu..karibu tuyatafakari maandiko pamoja,

Biblia inasema…

2Wakorintho 10:3 “Maana ingawa tunaenenda katika mwili, hatufanyi vita kwa jinsi ya mwili;

4 (maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome;)”

Kazi ya kwenda kuvua watu inafananishwa na shughuli za wanajeshi vitani…Wanajeshi wanapotaka kushambulia mahali huwa hawampi adui taarifa…na wanafanya hivyo, wanashtukiza tu…na wakisha angamiza wote wanateka mateka na kuchukua nyara vitu vyao..

Na katika kazi ya uvuvi wa watu ni hivyo hivyo…Hatupaswi kuingia mkataba na adui, wala kushauriana naye…tunachopaswa kufanya ni kila mara kuvamia kambi ya adui na kuteka mateka..

Unaposikia msukumo wa kuhubiri, sio suala la kusema hapa panafaa au hapafai..unachopaswa kufanya ni unavamia!…kwasababu katikati ya kambi ya Adui kuna mateka…na mateka unawaweka huru kwa kuwavamia..Ingawa vita utakutana navyo hiyo ni kawaida hata kambi ya adui akivamiwa ghafla ni lazima ijibu mashambulizi kidogo hata kama inajua itakwenda kushindwa..

Ukiwa shuleni, hata mwanya mdogo unaoupata, usipoteze muda…hubiri Habari njema, ukiona mgonjwa mahali mwanya huo ulioupata mnyang’anye shetani hilo teka…Mwombee apone na mhubirie, Ukikutana na mtu mwenye mapepo..itumie hiyo fursa vizuri, ya kuyakemea hayo mapepo yamwondoke na kumweka huru huyo mtu, na kisha Mweleze Habari za Yesu…

Usitazame huyu ni mkubwa kuliko mimi hawezi kunisikiliza, huyu ana elimu kuliko mimi, huyu ana heshima kuliko mimi, anavaa vizuri kuliko mimi, ni mwalimu wangu, ni kiongozi wangu, au nimekutana naye tu siku ya kwanza usiyaangalie hayo hata kidogo.. Kwasababu silaha ulizo nazo zina NGUVU! Kuifanya kila Fikra imtii Kristo. Wapo maprofesa waliobadilishwa fikra zao wakamtii Kristo na watu ambao hawajasoma hata darasa moja..Wapo maraisi waliowekwa huru na injili ya watu ambao hawajasoma hata darasa moja. Wapo waliokuwepo sugu lakini leo hii ni watumishi wa Mungu. Kwahiyo vaa silaha na ingia kazini..

Nguvu ile ile iliyokubadilisha wewe ndiyo hiyo hiyo itakayowabadilisha na wengine..wewe mpaka umemtii Kristo ni kwasababu Kristo alimtumia Mtumishi wake kuja kumnyang’anya shetani wewe ambaye ulikuwa mtumwa wake…Na baada ya kumpokonya shetani ndipo akakufanya wewe kuwa TEKA lake. Na hakuishia hapo akakupa na wewe Kipawa (yaani karama)..ambayo ni silaha na kazi yake mojawapo ni kwenda na wewe kuteka mateka mengine na kuyaleta kwa Kristo.

Waefeso 4:7 “Lakini kila mmoja wetu alipewa neema kwa kadiri ya kipimo cha kipawa chake Kristo.

8 Hivyo husema, Alipopaa juu aliteka mateka, Akawapa wanadamu vipawa”.

Hivyo kama umempa Kristo Maisha yako…ni jukumu lako kwenda kuteka mateka…kwasababu tayari silaha unayo…kama ni mtaani ingia anza kuhubiri, na utaona matokeo, kama ni shuleni ni hivyo hivyo, kama ni kusafiri huko na huko fanya hivyo kwa nguvu zote kwa karama Mungu aliyoiweka ndani yako, kama ni katika mahospitali na magereza..usikawie kawie..Nenda kwasababu Mungu atakuwa Pamoja nawe siku zote kukuongoza… yakumbuke haya maneno ya Yesu mwenyewe Bwana wetu aliyoyasema..

Mathayo 28:18 “Yesu akaja kwao, akasema nao, akawaambia, Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani.

19 Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu;

20 na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; NA TAZAMA, MIMI NIPO PAMOJA NANYI SIKU ZOTE, HATA UKAMILIFU WA DAHARI”

Atakuwa Pamoja na wewe hata ukamilifu wa dahari!…dahari maana yake ni nyakati/wakati….Hivyo hapo maana yake ni kwamba ameahidi kuwa “Pamoja nasi mpaka mwisho wa nyakati”…Lakini hiyo ni kama tutaondoka na kwenda kuwafanya mataifa yote kuwa wanafunzi…na kuwafanya kuwa mateka wa Kristo.

Bwana atusaidie kumuamini..

Kumbuka pia katika kwenda kuhubiri kuwa mwaminifu na kuwa na nia ya Kristo, sio nia ya kuwa maarufu au kutafuta fedha, bali ya kutafuta roho za watu…huku ukijua kuwa una thawabu yako mbinguni na Kristo anakuja upesi..

Ufunuo 22:12 “Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo.

13 Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, wa kwanza na wa mwisho”.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

MKUU WA UZIMA AKUWEKE HURU.

Kuungama ni nini?

UTASIMAMA PEKE YAKO SIKU ILE.

Katika biblia Neno “Mshenzi” linatajwa.Kwanini liwekwe?

KUTAKUWA NA MATETEMEKO YA NCHI, NJAA NA TAUNI.

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!

USIPUNGUZE MAOMBI.

Rudi Nyumbani:

Print this post