Katika maisha kila mwanadamu ambaye ameumbwa na Mungu mkuu, ni lazima ameumbiwa kitu kinachoitwa huzuni ndani yake. Maana yake ni kwamba ni lazima atapitia vipindi vya huzuni na vile vile atapitia vipindi vya furaha. Kila mwanadamu hata kama ni mtumishi wa Mungu ni lazima atapitia hivyo vipindi..Bwana wetu Yesu Kristo ambaye alikuwa ni mkamilifu asilimia zote alivipitia si zaidi sisi tusiokuwa wakamilifu?..Ni lazima tuvipitie. Na huzuni ni kama ugonjwa ukiwekwa katika mazingira Fulani inazidi na pia ikiwekwa katika mazingira Fulani unapungua.
Na huzuni inaweza kuja aidha kutokana na kupata taarifa mbaya, au umepatwa na jambo baya..au unakwenda kupatwa na jambo baya…au wakati mwingine inakuja pale linapotokea jambo ambalo hukulitegemea au hukulipanga, au hukutamani liwe hivyo lilivyo.
Mtu anapofikia hali kama hiyo anajikuta anazama katika dimbwi kubwa la mawazo, na kukosa hamu ya kufanya jambo lolote lile..hata hamu ya kula inatoweka, wakati mwingine hata hamu ya kuishi.
Siku ile ambayo Bwana ndio alikuwa anakwenda kusulibiwa, Huzuni kubwa iliwaingia wanafunzi wake, baada ya kuwaambia kwamba muda si mrefu atakwenda kusulibiwa, na ataondoka atakwenda zake kwa Baba..
Yohana 16:5 “Lakini sasa mimi naenda zangu kwake yeye aliyenipeleka, wala hakuna mmoja wenu aniulizaye, Unakwendapi?
6 Ila kwa sababu nimewaambia HAYO HUZUNI IMEJAA MIOYONI MWENU.
7 Lakini mimi nawaambia iliyo kweli; yawafaa ninyi mimi niondoke, kwa maana mimi nisipoondoka, huyo Msaidizi hatakuja kwenu; bali mimi nikienda zangu, nitampeleka kwenu”.
Na zaidi ya yote walipoambiwa kwamba mmoja wao atamsaliti..Ndio kabisa moto wote ukakata ndani yao..Wakati wanadhani kwamba Kristo atazidi kuendelea kuwepo, yeye anawapa taarifa za msiba, kwamba anakwenda kusulibiwa..wakawa wanawaza kwanini hayo yote yampate Bwana wao, sasa maisha yatakuwaje baada ya yeye kuondoka.
Na hata Bwana alipowachukua usiku ule kwenda kusali naye hata nguvu zilikuwa zimewaisha kabisa, hawakusali sana wakalala kwasababu ya huzuni nyingi..Tusome..
Luka 22:45 “Alipoondoka katika kuomba kwake, akawajia wanafunzi wake, AKAWAKUTA WAMELALA USINGIZI KWA HUZUNI.
46 Akawaambia, Mbona mmelala usingizi? Ondokeni, mkaombe, msije mkaingia majaribuni”.
Lakini katika hali kama hiyo, Bwana aliuona udhaifu wa mioyo yao kwamba wamechoka na wanahuzuni nyingi. Lakini aliwaambia waamke waombe..kwasababu roho i radhi lakini mwili ni dhaifu…Hivyo wanapaswa waishinde hali hiyo ya huzuni..kwasababu wana huzuni, lakini siku chache baadaye watakuwa na furaha. Hivyo alijaribu kuwaasa kwamba wajaribu kuishinda huzuni ambayo ilipelekea udhaifu wa mwili wasimame waombe kwasababu majaribu hayo ni ya siku chache tu..siku mbili baadaye watakuwa na furaha isiyo na kifani. Kwasababu aliwaambia bado kitambo kifupi hawamwoni (yaani atakufa na kuzikwa)..na tena bado kitambo kidogo watamwona tena (yaani siku atakapofufuka)..wataendelea kumwona mpaka Pentekoste na watakuwa na furaha kuu.(Soma Yohana 20:20).
Katika wakati huu unaoitwa wa pasaka miongoni mwa mambo mengi tunayojifunza basi ni muhimu kulijua hili pia…USIHUZUNIKE..Pengine umepitia shida Fulani, au umepata usumbufu Fulani, au huzuni Fulani, au tabu Fulani, au taarifa Fulani, au jambo lolote lile ambalo limekuletea huzuni kubwa moyoni hata umekata tamaa ya kila kitu na ya kuendelea mbele katika imani…Huo sio wakati wa kuzidi kuipalilia huzuni kwa kukata tamaa na kuiacha Imani, sio wakati wa kulala usingizi kwa huzuni..Bali ni wakati wa kusimama na KUOMBA kwa nguvu…ni wakati wa kuzidi kuendelea mbele kwasababu huzuni hiyo ni ya kitambo tu!. Baada ya siku chache itaondoka na furaha itakurudia kama mwanzo na utajuta kwanini siku chache nyuma ulikuwa unahuzunika…utajuta kwanini ule muda ambao ulikuwa na huzuni usingeutumia hata kuomba au kumsifu Mungu.
Hivyo simama sasa mtu wa Mungu, huu sio wakati wa kupalilia huzuni bali ni wakati wa kuomba..Mitume wa Yesu huzuni yao iligeuka furaha pale walipomwona Bwana kafufuka…nawe pale utakapoona kile kilichokuwa kimekufa kimefufuka, siku sio nyingi furaha yako itarudi. Hivyo usihuzunike..simama uombe, simama uendelee mbele kwasababu hatua zilizobakia mbele yako ni chache kuliko ulizoziacha nyuma. Hivyo sio wakati wa kunyongonyea ni wakati wa kuomba.
Bwana akubariki
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312.
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
Bwana wetu Yesu Kristo asifiwe ndugu yangu..
Nyakati hizi za mwisho tunazoishi sasa, ni nyakati ambazo zinakithiri kuwa na mseto wa watu wengi wanaojiita wakristo, leo hii ni rahisi kuona hata msanii wa kidunia anaimba nyimbo za Injili, ni rahisi kuona, mashoga wanatoa michango ya kujenga makanisa makubwa ulaya, wazinzi wanahudhuria kila jumapili ibadani, wengine mpaka wapo tayari kushiriki meza ya Bwana bila hofu nao wanaona ni kawaida tu. Ni kundi kubwa lenye mchanganyiko wa kila aina ya watu, wengine hawana hata mpango wa kufikiria maisha yao baada ya hapa, kinachowapeleka kwa Mungu tu, ni pengine waponywe waondoke, wengine wapate tu wachumba, wengine biashara zao ziende vizuri..basi hakuna cha zaidi baada ya hapo
Na wachache sana ndio wanaoutafuta wokovu wa kweli, ambao wapo tayari kumtii na kumfuata Yesu pale alipo yeye..
Embu leo kwa ufupi tuone habari moja ambayo, pengine unaijua sana, lakini tuiangalie kwa jicho lingine la ndani zaidi na naamini tutajifunza kitu kipya..
Na habari yenyewe ni ile ya Yesu akiwa bado kijana mdogo, alipokwenda na wazazi wake Yerusalemu kuila pasaka ya kila mwaka.. Lakini kama tunavyoijua habari baada ya sikukuu kuisha, ulipofika wakati wa kila mtu kurudi nyumbani kwake na katika taifa lake, wale waliotokea katika mikoa ya karibu kule Israeli walianza safari ya kurudi makwao, na wale waliotokea mataifa mengine ya mbali nao pia walianza kurejea makwao..
Lakini mambo yalikuwa tofauti kwa Bwana Yesu, yeye alibaki nyuma, wala hakuambata na makutano kurudi makwao, kama watu wengine walivyofanya, na kibaya zaidi hata wazazi wake hawakulijua hilo, wao wakakisia tu labda atakuwa katikati ya makutano wakirejea naye nyumbani…(Hilo ndio kosa linalofanywa na watoto wengi wa Mungu)
Luka 2:44 “Nao wakadhani ya kuwa yumo katika msafara; wakaenenda mwendo wa kutwa, wakawa wakimtafuta katika jamaa zao na wenzao;
45 na walipomkosa, wakarejea Yerusalemu, huku wakimtafuta.
46 Ikawa baada ya siku tatu wakamwona hekaluni, ameketi katikati ya waalimu, akiwasikiliza na kuwauliza maswali.
47 Nao wote waliomsikia walistaajabia fahamu zake na majibu yake.
48 Na walipomwona walishangaa, na mama yake akamwambia, Mwanangu, mbona umetutenda hivi? Tazama, baba yako na mimi tulikuwa tukikutafuta kwa huzuni.
49 Akawaambia, Kwani kunitafuta? Hamkujua ya kuwa imenipasa kuwamo katika nyumba ya Baba yangu”?
Kama tunavyoona hapo, ni wazazi wake tu pake yao, ndio waliokuwa walau wanamfikiria Yesu katikati ya ndugu zao wengi walioambatana nao, na walipoona Kristo hayupo katikati ya makutano, katikati ya wingi wa watu, katikati ya ndugu, katikati ya marafiki, katikati ya majirani, katikati ya wageni wa mataifa mengine, ndipo ikiwapasa wageuke wajaribu kwenda kuanza kumtafutia kule walipompotezea Yerusalemu.. ndipo wakamkuta yupo hekaluni katikati ya WAALIMU..
Na ni kama bahati tu walipita hekaluni, lakini kama wasingeingia kule, kamwe wasingemwona daima, wangehangaika Yerusalemu nzima wasingempata kwa muda mrefu sana..
NI KIPI MUNGU ANATAKA TUJIFUNZE?
Wakristo wachache wa leo hawajui kuwa, wapo katikati ya kundi kubwa la wakristo vuguvugu, linaloondoka mbali na mafundisho ya kweli ya Neno la Mungu.. na ndio maana wanapojaribu kumtafuta Kristo katikati yao ni kama vile hawamuoni, lakini wao bado wanataka kuendelea kutembea nao tu, hawajui kuwa kwa jinsi wanavyozidi kukaa nao ndivyo wanavyozidi kumpoteza YESU wasimpate kabisa..
Ndugu geuka kama ni wewe,..angalia ulipotoka, kule mlipotoka ndipo Kristo yupo,..Na! ulipotoka ni wapi?? Ni katikati ya waalimu, kule Kristo alipo, na waalimu makao yao huwa ni wapi?..Makao yao ni darasani sikuzote, wakiwafundisha wanafunzi, na hapo ndipo makao ya Kristo yalipo siku zote..
Hutampata sehemu nyingine yoyote, hutampata, kwenye michezo, maombezi, hutampata kwenye matamasha, hutampata kwenye taasisi za kidini, wala hutampata kwenye dhehebu lolote, wala katikati ya ndugu zako, au rafiki zao, au majirani zako, huko kote utapotea, Kristo hatembei katikati ya misafara ya watu wanaosafiri mbali na yeye bali Kristo utamwona PALE NENO LAKE LINAPOFUNDISHWA BASI..
Ukiona hupendi tena kujifunza Neno la Mungu basi ujue, upo mbali sana na Kristo kwa mujibu wa biblia, ukiona huna muda wa kusoma biblia, usijidanganye utakaa umwone Kristo akijifunua kwako, ukiendelea kudhani Kristo yupo katika msafara unaouona leo hii, wimbi la watu wengi wanaosema tumeokoka, lakini Neno la Mungu hawalifuati, ni wavivu katika kutamani kumjua Mungu, ukiwauliza habari ya unyakuo kwao ni kama habari mpya za kuchosha, ukiwauliza, habari za kwenda mbinguni kwao ni kama hadithi za kizee, muda wote ni kujionyesha tu, na kujisifia wameokoka, lakini biblia ni kama kitabu cha ziada tu kwao basi ujue wamempoteza Kristo katikati yao..
Bwana atusaidie nyakati hizi za hatari tusimpoteze yeye aliye mwamba wa wokovu wetu..
Maran Atha.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
https://wingulamashahidi.org/mafundisho-ya-ndoa/
Biblia inamaana gani kusema;aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi?
Katika 1Wafalme 20:35-37, Kwanini yule mtu afe kwa kuliwa na simba baada ya kukataa kumpiga yule nabii?..je Mungu anaruhusu watu kupigana?
JIBU:Tusome
1Wafalme 20:35-37 “Basi, mtu mmoja wa wana wa manabii akamwambia mwenzake kwa neno la Bwana, Nipige, nakusihi. Akakataa yule kumpiga.
36 Akamwambia, Kwa sababu hukuisikiliza sauti ya Bwana, angalia, mara ukitoka kwangu simba atakuua. Na mara alipotoka kwake, simba alimwona, akamwua.
37 Ndipo akaona mtu mwingine, akasema, Nipige, nakusihi. Yule mtu akampiga, hata kumpiga na kumtia jeraha”
Kuna wakati Mungu anatumia ishara za mwilini kuzungumza na watu wake au kufikisha ujumbe mahali..Kwamfano utaona Nabii Hosea aliambiwa aoe mwanamke wa kizinzi,
Hosea 1:2 “Hapo kwanza Bwana aliponena kwa kinywa cha Hosea, Bwana alimwambia Hosea, Enenda ukatwae mke wa uzinzi, na watoto wa uzinzi; kwa maana nchi hii inafanya uzinzi mwingi, kwa kumwacha Bwana”.
Lengo la Mungu kumwambia Hosea akaoe mwanamke wa kizinzi sio kuhalalisha uzinzi kwa watu wake, hapana bali ni kuwaonyesha watu wake jinsi na wao wanavyofanya uzinzi mbele zake kinyume chake katika roho…Hosea hakuwa mzinzi lakini aliambiwa akamwoe mwanamke mzinifu, ambaye ni kahaba mwenye wanaume wengi, ambaye hatulii. Sasa nafasi ya Hosea ambaye hakuwa mzinifu ilimwakilisha Mungu na huyo mwanamke wa kizinzi ililiwakilisha taifa la Israeli, kwa jinsi yule mwanamke alivyokuwa ni kahaba baada hata ya kuolewa na Hosea ndivyo Taifa la Israeli lilivyofanya uzinzi katika roho na kumwacha Mungu wao ambaye ndiye mume wao kama Isaya 55:5 inavyosema “Kwa sababu Muumba wako ni MUME WAKO; Bwana wa majeshi ndilo jina lake; na Mtakatifu wa Israeli ndiye Mkombozi wako; Yeye ataitwa Mungu wa dunia yote”
Sasa endapo Nabii Hosea angekataa maagizo yale Mungu aliyompa ya kwenda kumwoa mwanamke kahaba…na kusema hapana Bwana mimi sitaki kumuoa mwanamke yule ambaye ni mzinzi na kahaba hata nikimuoa bado ataendelea kuwapenda hao mabwana wake…Ni Dhahiri kuwa Hosea angetenda dhambi kwasababu amekataa shauri la Bwana la yeye kufanyika ishara kwa Israeli. Na hivyo angewafanya Israeli wasitubu, lakini ishara ile iliwafanya Israeli wengi watubu..Kwasababu walipokwenda kumuuliza wewe Nabii wa Mungu mbona unaoa mwanamke ambaye anamabwana wengi na zaidi ya yote tunamwona mkeo huyo yupo na mabwana wengine, unajisikiaje kwa hilo?..Ndipo Hosea atawajibu ni mfano wa nyinyi mlivyomwacha Mungu wenu ambaye ni mume wenu na kuigeukia miungu mingine kuiabudu..Hivyo mrudieni Mungu wenu ambaye ni Mume wenu kwasababu amewakasirikia sana.
Halikadhalika kuna wakati Mungu alimwambia nabii mwingine amwambie mwenzake kwamba ampige mpaka apate majeraha…ili kwa kupitia yale majeraha aonekane kama alikuwa katika vita vikali na aende kwa mfalme wa Israeli akiwa na yale majeraha…Ili mfalme adanganyike na kuamini kuwa ni kweli alikuwa kwenye mapambano kwasababu ana majeraha..na ndipo ampe fumbo ambalo litamtega…Na kweli mfalme alipomwona mtu anakuja mwenye majeraha akasema bila shaka mtu huyu atakuwa ametoka vitani kwa majeraha yale..na alipopewa lile fumbo na yule nabii kumbe lilikuwa linamhusu mfalme mwenyewe..kwasababu alimwacha huru Benhadadi ambaye alipaswa kumuua kabisa..
Hivyo akaambiwa sehemu yake ataichukua yeye. Unaweza kuisoma vizuri habari hiyo katika 1Wafalme 20:35-43.
Lakini yule mtu alikataa maagizo yale ya Mungu..ingawa aliambiwa ni maagizo kutoka kwa Mungu lakini akakataa kumpiga..hakujua kuwa kwa kukataa kule kungemfanya mfalme wa Israeli asiyaamini maneno yale ya Mungu…Na ikasababisha dhambi kwake, na ndio mbeleni akaenda kuliwa na simba..lakini yule mwingine hakulichukulia lile jambo la kumpiga nabii wa Mungu kwamba ni jambo la kumuumiza..bali aliona mbele kwamba kwa ishara ile ya majeraha ya yule nabii, mfalme ataamini ujumbe kutoka kwa yule nabii sawasawa na Neno la Mungu na hivyo atakuwa ameyatenda mapenzi ya Mungu Zaidi.
Hivyo ni jambo la kawaida kabisa Mungu kuzungumza kwa ishara za mwili, alifanya hivyo kwa Hosea, Kwa Ezekieli, na kwa manabii wengine wengi.
Bwana atubariki
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
Shalom, Naomba kufahamu kitendo cha kupiga miayo mara kwa mara hususani wakati wa maombi, Je! Ishara ya kuwa na mapepo au nguvu za giza?.
JIBU: Kwa namna ya kawaida kupiga miayo ni ishara ya mambo mawili makuu katika mwili, 1) Ya kwanza ni njaa, 2) Ya pili ni usingizi.
Hivyo tukirudi katika masuala ya maombi mkristo hapaswi kufikiria kuwa kupiga miayo ni kitendo cha mapepo au nguvu za giza, hapana bali ni mwitikio wa mwili wake mwenyewe, ukimwambia kuwa huu sasa ni wakati wa kwenda kupumzika umechoka, sio wakati wa kusali..Na ndio maana utagundua ni wakati tu wa kusali, au wa kusikiliza Neno watu ndio wanasikia uchovu wa hali ya juu, lakini wakitoka hapo hiyo hali inapotea yenyewe, utajiuliza ni kwa nini?
Ni kwasababu Biblia inatufundisha kuwa mwili ni adui wa mambo ya rohoni sikuzote, wakati roho yako ipo tayari hata kuzama muda mrefu kwenye maombi mwili wako utaanza kutoa sababu nyingi, mara umechoka, unapaswa ukapumzike, utakuletea mpaka hivyo viashiria vya miayo mingi, ili tu kukuthibitishia, na tena kama utakuwa unafikiria chakula muda wa maombi ndio kabisa utakuletea mpaka miayo ya njaa, mpaka utatetemeka wakati ni muda mfupi tu nyuma hapo ulitoka kula.
Wagalatia 5:17 “Kwa sababu mwili hutamani ukishindana na Roho, na Roho kushindana na mwili; kwa maana hizi zimepingana, hata hamwezi kufanya mnayotaka’’.
Hivyo, hali kama hiyo ikikujia, hupaswi kukemea mapepo, bali ni wakati kushindana na mwili wako mpaka ukutii wenyewe, na habari njema ni kuwa kwa jinsi utakavyozidi kuzama katika maombi, ndivyo hiyo hali itakavyokuwa inatoweka yenyewe ndani yako kidogo kidogo, mpaka mwishoni utajikuta unaweza kwenda muda mrefu mpaka utajiuliza ule usingizi mwanzoni ulitokea wapi.
Kwahiyo njia rahisi ni kuhakikisha wakati unaposali, peleka mawazo yako yote na fikra zako zote kwenye maombi na sio katika mambo mengine, ndivyo utakavyoweza kuushinda mwili kirahisi, na kama ni usiku unasali toka katika mazingira ya kitanda.
Mwisho, fahamu kuwa kama mkristo huwezi kuishi bila maombi.
Kwahiyo shindana na mwili wako mpaka uushinde, vinginevyo hutadumu muda mrefu katika imani au kama utaendelea kuwepo basi ujue maisha yako yatakuwa ni ya majaribu kila kukicha ambayo yangeweza kuepukika tu kwa maombi..
Mathayo 26:41 “ Kesheni, mwombe, msije mkaingia majaribuni; roho i radhi, lakini mwili ni dhaifu”.
Ubarikiwe.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Je! Ni sahihi kwa mkristo kuoa/kuolewa na mtu wa imani nyingine?
Mathayo 7:6 “Msiwape mbwa kilicho kitakatifu, wala msitupe lulu zenu mbele ya nguruwe, wasije wakazikanyaga chini ya miguu yao, wakageuka na kuwararua”.
Maneno hayo yalizungumzwa na Bwana wetu Yesu. Akifunua kuwa sio kila neno/kitukinawafaa baadhi ya watu. Hivyo tuwe na hekima tunapotoa au tunaposema vitu vyetu vilivyo vya thamani mbele za watu, kwasababu unaweza ukasema kitu ukadhani kitakuwa na manufaa kwa yule unayemwambia badala yake kitu kile kikageuka kuwa matatizo kwako.
Tutajifunza mfano mmoja muhimu katika biblia kisha kupitia huo tutapata kuelewa Zaidi kiini cha somo letu.
Wakati Mungu anamtokea Musa na kuzungumza naye kwa mara ya kwanza katika kile kijiti kilichokuwa kinawaka moto lakini hakiteketei…Alimwambia maneno haya..
Kutoka 3:6 “Mimi ni Mungu wa baba yako Ibrahimu, Isaka na Yakobo….
7 Hakika nimeyaona mateso ya watu wangu walioko Misri, nami nimekisikia kilio chao kwa sababu ya wasimamizi wao; maana nayajua maumivu yao;
8 nami nimeshuka ili niwaokoe na mikono ya Wamisri, niwapandishe kutoka nchi ile, hata nchi njema, kisha pana; nchi ijaayo maziwa na asali; hata mahali pa Mkanaani, na Mhiti, na Mwamori, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi.
9 Basi, tazama, kilio cha wana wa Israeli kimenifikilia; tena nimeyaona hayo mateso ambayo Wamisri wanawatesa.
10 Haya, basi, nitakutuma sasa kwa Farao, ili upate kuwatoa watu wangu, hao wana wa Israeli, katika Misri.”
Baada ya Mungu kumwambia maneno haya ya ahadi na ya Faraja..alimwambia akawaambie habari hizo wana wa Israeli…Kwamba wamejiliwa na wanakwenda kutolewa katika nchi ya Misri ya utumwa na kupelekwa nchi ya Ahadi. Hivyo Musa akaenda kuwaambia wana wa Israeli habari hizo nao wakafurahi.
Lakini jambo la kipekee ni kwamba Mungu alipomwambia Musa aende kwa Farao…alimwambia amwambie Farao maneno mengine tofauti na hayo…Tusome..
Kutoka 3:16 “Enenda, ukawakusanye wazee wa Israeli pamoja, ukawaambie, Bwana, Mungu wa baba zenu, Mungu wa Ibrahimu, Mungu wa Isaka, Mungu wa Yakobo, amenitokea, akaniambia, Hakika nimewajilieni, tena nimeyaona mnayotendewa huko Misri;
17 Nami nimesema, Nitawapandisha kutoka katika mateso ya Misri na kuwaingiza katika nchi ya Mkanaani, na Mhiti, na Mwamori, na Mperizi, na Mhivi, na Myebusi, nchi ijaayo maziwa na asali.
18 Nao watakusikia sauti yako; nawe utakwenda, wewe na wazee wa Israeli kwa mfalme wa Misri, na kumwambia, BWANA MUNGU WA WAEBRANIA, AMEKUTANA NASI; BASI SASA TWAKUOMBA, TUPE RUHUSA TWENDE MWENDO SIKU TATU JANGWANI, ILI TUMTOLEE DHABIHU BWANA MUNGU WETU.
19 Nami najua ya kuwa huyo mfalme wa Misri hatawapa ruhusa mwende zenu, la, hata kwa mkono wa nguvu”.
Sasa unaweza kujiuliza kwanini Mungu hakumwambia Musa amwambie Farao kwamba “Mimi ni Mungu wa Ibrahimu, Isaka na Yakobo nimeona mateso ya watu wangu jinsi gani unavyowatumikisha hivyo wape ruhusa waondoke waende nchi ya ahadi niliyowaahidia?”…Badala yake Mungu hakumruhusu Musa kumwambia Farao habari zozote kuhusu Ibrahimu, wala kuhusu mahali wanapokwenda..badala yake ni kama Mungu alimdanganya Farao kwamba wanakwenda tu kumtolea Mungu dhabihu jangwani kisha watarudi…kumbe ndio walikuwa wanakweda kutokomea huko.
Hivyo Farao akadanganyika akajua kuwa wana wa Israeli wanataka tu kwenda kumtolea Mungu wao dhabihu jangwani siku tatu na kisha watarudi kumbe nyuma yake kulikuwa na mpango mwingine wa wana wa Israeli kutokomea huko huko na kutokurudi tena…
Sasa japokuwa Farao alikuwa anajua ni kitendo tu cha kwenda na kurudi lakini alikuwa mgumu vile hebu tafakari laiti angejua kuwa wale watu ndio wamepanga wanaondoka kabisa kabisa hali ingekuwaje?..bila shaka vingeamka tena vita vingine visivyokuwa na maana.
Sasa Kwanini Mungu alifanya vile?, Ni kwasababu aliwazuilia wana wa Israeli wasitupe lulu zao mbele za nguruwe wasije wakazikanyaga mbele ya miguu yao na kugeuka na kuwararua.
Hivyo wana wa Israeli mpaka wanaondoka Misri…Farao alikuwa anajua kuwa ni wanakwenda tu na kurudi.. Hebu tusome mistari kadhaa kulithibitisha hilo..
Kutoka 5:2 “Farao akasema, Bwana ni nani, hata niisikilize sauti yake, na kuwapa Israeli ruhusa waende zao? Mimi simjui Bwana, wala sitawapa Israeli ruhusa waende zao.
3 Wakasema, Mungu wa Waebrania amekutana nasi; twakuomba, tupe ruhusa twende safari ya siku tatu jangwani, tumtolee dhabihu Bwana, Mungu wetu; asije akatupiga kwa tauni, au kwa upanga”.
Soma tena..
Kutoka 8:25 “Farao akawaita Musa na Haruni akawaambia, Endeni mkamtolee Mungu wenu dhabihu ndani ya nchi hii.
26 Musa akasema, Haitupasi kufanya hivyo; kwa kuwa tutamchinjia sadaka Bwana, Mungu wetu, na hayo machukizo ya Wamisri; je! Tutachinja sadaka ya hayo machukizo ya Wamisri mbele ya macho yao, wasitupige kwa mawe?
27 La, tutakwenda safari ya siku tatu jangwani, tumchinjie dhabihu Bwana, Mungu wetu, kama atakavyotuagiza.
28 Farao akasema, Mimi nitawapa ruhusa mwende, ili mmchinjie dhabihu Bwana, Mungu wenu, jangwani; lakini hamtakwenda mbali sana; haya niombeeni”.
Umeona hapo Farao anawaambia “lakini hamtakwenda mbali sana”…maana yake alikuwa anafikiri kwamba watarudi baada ya kutoka kule…na sehemu nyingine utaona Farao anawaambia waende tu huko jangwani watu walio wazee lakini Watoto wabaki na mifugo (soma kutoka 10:24)…Hivyo ikabakia kuwa siri ya Musa na wana wa Israeli kwamba siku yao ya kutoka Misri kikabisa kabisa imefika…Farao na waMisri hawakuijua hiyo siri, walidhani wanakwenda tu jangwani watarudi baada ya siku chache watakapomaliza kutoa sadaka zao hizo, watarudi na kuendelea kuwatumikisha.
Farao alikuja kushtuka kuwa kalaghaiwa na wale watu, wamekimbia na hawana mpango wa kurudi tena siku alipokuja kupata taarifa kuwa wale watu hawaelekea ile njia ya jangwa bali waligeuka na kurudi kuikabili bahari…Ndipo alipoelewa kuwa wamefanya makosa makubwa kuwaachilia waondoke.. Tusome
Kutoka 14:5 “Mfalme wa Misri aliambiwa ya kuwa wale watu WAMEKWISHA KIMBIA; na moyo wa Farao, na mioyo ya watumishi wake, iligeuzwa iwe kinyume cha hao watu, nao wakasema, Ni nini jambo hili tulilotenda, kwa kuwaacha Waisraeli waende zao wasitutumikie tena?”
Ndugu katika safari ya wokovu… si kila kitu kizuri Bwana anachokuambia ni cha kwenda kuwaambia watu kama kilivyo…Bwana amekuahidia au amekupa ufunuo fulani wa jambo lako zuri linalokuja mbele usikurupuke na kwenda kusimulia simulia huku na huko…kwa kufanya hivyo utakuwa umempa adui nafasi na mlango mzuri wa kuyaharibu maono yako uliyopewa..
Hali kadhalika Bwana anapokutoa leo katika ulimwengu(yaani katika dhambi)…ambao inafananishwa na Misri yetu…sio kila kitu ambacho Mungu kakufunulia ni cha kukieleza mbele za watu wa kidunia…Unatakiwa uondoke katika dhambi kwa njama kama hizo za wana wa Israeli..
Kwamfano Ulikuwa unauza Bar…na majirani zako wanauza bar kama wewe, sasa umempokea Yesu na Roho Mtakatifu amekushuhudia ndani yako kwamba, biashara hiyo ni ya utumwa wa dhambi na itakupeleka kuzimu…sasa wewe anza kuifunga hiyo haraka sio lazima uwaambie wale wanaokuzunguka sababu ya kuifunga, wewe jiponye nafsi yako kwanza huo sio wakati wa kuanza kuwahubiria….baada ya kuifunga na kuhakikisha marago yako yote umeyatoa Misri, ndipo uwaambie mimi nimeokoka na hiyo kazi siirudii tena….lakini ukiwahi kuwaambia kwamba nimeokoka na Kesho au Kesho kutwa nitaifunga hiyo Bar, au nitaacha hii kazi ya kujiuza, au nitaacha haya madili haramu tunayoyafanya, au nitaacha uvaaji wa nguo hizi na vimini hivi, au nitaacha dansi..ukianza kumwambia huyo mpenzi wako unayefanya naye uasherati kwamba sasa umeokoka hivyo kuanzia Kesho nakuacha…nataka nikuambie kwamba utakuwa umejiweka kupitia vita visivyokuwa na lazima…mwache kwanza huyo unayefanya naye uzinzi, ikiwezekana mtoroke baadaye akikuuliza kwanini umeondoka bila kuniambia mwambie ni kwasababu nimeokoka na siwezi tena kuishi Maisha ya uasherati…lakini ukimwambia huku bado upo naye nyumba moja….nakwambia shetani atakupelekesha kweli kweli na unaweza kujikuta huwezi kumwacha wala kuuacha ulimwengu….Utapitia vita visivyokuwa na sababu..
Vita vinatakiwa vianze baada ya wewe kuondoka katika ulimwengu..Ulimwengu unatakiwa ujue kwamba wewe umeokoka baada ya kuondoa marago yako yote ulimwenguni na sio wakati ambao wewe bado upo katika ulimwengu…kama vile wana wa Israeli walivyoondoa majeshi yao ndipo Farao akabutuka na kujua kuwa wale watu hawakwenda safari ya kwenda na kurudi..bali walipanga kupotelea moja kwa moja..ndipo akapanga majeshi kumfuatilia.
Hivyo kama hujaokoka leo? Huu ndio wakati wako sasa..Tubu mpokee Yesu, kutubu maana yake ni kugeuka na kuacha yale uliyokuwa unafanya mwanzo…na njia ni hiyo hiyo, fungasha marago yako yote na kimbia kimya kimpya!…usitoe taarifa kamili kwanini utatoka mpaka utakapotoka Misri…Toka Misri leo kwa njama zozote zile uwezazo…Toka kwenye ulevi, toka kwenye ulimwengu wa starehe za kidunia,miziki, toka kwenye huo mtandao wa wala rushwa, wizi, , utapeli, usengenyaji, uasherati, ulawiti,ufisadi…
Kwa mwanzo igiza hata unaumwa ili wakupe ruhusa utoke katika kampuni yao hiyo ya bia..na baadaye wakikuuliza mbona hurudi waambie mimi nimeokoka na huko sirudi tena..Igiza hata unakwenda kusalimia nyumbani ili tu huyo mtu unayeishi naye ambaye mnafanya naye uasherati akupe ruhusa uondoke na huko akiona hurudi akikuuliza vipi mwambie nimeokoka huku huku na Maisha hayo siyaishi tena. Jiponye nafsi yako kwa gharama zozote…
Dunia inapita na mambo yake yote..Bwana Yesu alisema itakufaidia nini upate ulimwengu mzima na upate hasara ya nafsi yako?…Ikimaanisha kuwa nafsi ni kitu cha kulinda kuliko kitu kingine chochote…hivyo kwa gharama zozote na njama zozote jiokoe nafsi yako na huu ulimwengu.
Bwana akubariki.
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312.
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
Je! Ni sahihi kwa mkristo kufikiria hivi?..
Jaribu kufikiria mfano huu..
Mtu mmoja alitamani sana kujua afya ya mwili wake, hivyo akakusudia kweli kwenda hospitali kupima afya yake kama ameathirika na Ukimwi au La, Hivyo akafanikiwa kwenda kuonana na daktari akachukuliwa vipimo vyote, Lakini alipomaliza kuchukuliwa tu vipimo akaondoka zake akarudi nyumbani kwake, daktari alipomaliza uchunguzi wake wa vipimo akarudi sasa ili ampe majibu yake, na kumpa ushauri nasaha lakini alipofika hakumwona..
Sasa akiwa kule nyumbani, siku zikapita, miezi ikapita, miaka ukapita, akawa anaishi Maisha ya furaha na ya amani kabisa, siku moja watu wakamuuliza vipi kuhusu afya yako, tunatumai sasa ipo njema kwasababu siku ile tayari ulishakwenda kuonana na Daktari..
Ndipo yeye akajibu, ndio! Natumai itakuwa ni njema!..Watu waliposikia vile wakashangaa kwa jibu lile, unatamai vipi tena? Wakati ulishapata uhakika kwa Daktari,..Lakini yeye akawajibu, ndio nilishaonana na daktari akanichukua vipimo vyote, ila majibu anayo yeye mwenyewe, mimi sijui kingine Zaidi ya hapo, Hivyo yeye Mungu ndiye anayejua kuwa mimi ni muathirika au La!. Hilo ni jukumu lake kama daktari, mimi sihitaji kujua sana kwasababu mimi sio daktari..
Fikiria mtu kama huyo wale watu walimwonaje? Ni Dhahiri kuwa watasema huyu atakuwa amerukwa na akili, alikwenda hospitali kufanya nini sasa kama hakupata majibu ya afya yake, ambayo yangempa uhakika wa afya yake kuwa ni njema au la!.
Na ndivyo ilivyo hata leo kwa mtu ambaye hajapata bado uhakika wa wokovu wake..Watu wengi ukiwauliza Je! Umeokoka watasema ndio, nilishaokoka zamani sana, mpaka nikabatizwa,..Ukizidi tena kuwauliza, sawa Je unaouhakika hata ukifa leo au Yesu Kristo akirudi leo utakwenda naye mbinguni.. hapo ndipo watakapokuambia ninatumai hivyo, wengine watakuambia hilo ni Mungu ndio analolijua..mimi siwezi kujua hukumu zake, na mwingine atakwambia,nikisema hivyo nitakuwa ninajihesabia haki, na kujiona mimi ni kitu fulani mbele za Mungu..wakati bado sijafika lolote linaweza kutokea.
Ndugu Neno WOKOVU ni Neno lenye msingi wa UHAKIKA chini yake, mfano huwezi kusema umeokolewa kwenye moto, na huku bado unajihisi kama upo bado mule mule motoni, vinginevyo hiyo itakuwa ni ndoto tu au bumbuazi fulani limekushika, lakini mfano ukiokolewa kutoka motoni na mtu fulani, utajiona kabisa jinsi unavyohama kutoka ulipokuwepo kwenye mateso na kwenda sehemu nyingine salama..Hivyo ni jambo la uhakika..
Na ndio maana biblia inaweka wazi kabisa kwa kutuambia…
2Wakorintho 13:5 “Jijaribuni wenyewe kwamba mmekuwa katika imani; jithibitisheni wenyewe. Au hamjijui wenyewe, kwamba Yesu Kristo yu ndani yenu? Isipokuwa mmekataliwa”
Unaona, ukiwa mkristo huendi tu ilimradi, huwi tu kama mshabiki fulani, bali kila hatua inajipima je! Mpaka sasa Kristo yupo pamoja nami au La!, Na je ikitokea leo hii safari yangu ya Maisha imekwisha ghafla Je nitakuwa upande wa haki au hukumu?
Sasa, swali unaloweza kujiuliza ni Je utaupataje Uhakika huo wa wokovu ndani yako?
Unapaswa uangalie mambo mawili la kwanza Ni Je! Tangu uliposema umeokoka, kuna badiliko lolote lililotokea ndani yako?..Je yale matunda ya Roho yamezalika ndani yako?
Sawasawa na Wagalatia 5:22 inayosema..
“Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu,
23 upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria”.
Hivyo kama hayo yapo ndani yako, basi hiyo ni hatua ya kwanza ya kukupa uhakika ndani yako.
Na jambo la pili, Je! Tangu ulipoubeba msalaba wako na kumfuata Kristo, Je! Ulipitia vipingamizi vyovyote katika hilo?..Kupitia majaribu sio sifa kwamba ni jambo jema, lakini shetani hawezi kukuangalia umeacha rushwa, akakuvumilia, umeacha ulevi na kuuza pombe kwenye biashara yako akakuangalia tu, umeacha kampani za marafiki wabaya na disko asikuletee udhia, umeacha ulimwengu kwa ujumla wake na mambo yake yote asikuletee dhihaka, umekatisha ghafla yale madili haramu uliyokuwa umepanga wewe na wenzako kwenda kuyafanya shetani akabaki anakutazama tu!..Umekatisha hayo mahusiano ya kiasherati ghafla anakutazama tu…wakati mwingine utapitia kupigwa au kutengwa, n.k. Sasa kama haya hayakuonekana ndani yako basi uhakika huo kuupata ni ngumu, Kristo na mitume wake waliyapitia hayo, vilevile na wewe utakumbana nayo kwa sehemu fulani katika safari yako ya wokovu.
Sasa Ikiwa hayo mambo mawili makuu yameonekana ndani yako, basi uhakika wenyewe wa kama upo katika njia sahihi ya wokovu utatokea wenyewe ndani yako, wala hautahitaji kuulizia bali Roho Mtakatifu mwenyewe atakushuhudia kuwa wewe ni mwana wa Mungu na umeokoka..
Sawasawa na Warumi 8:16 “Roho mwenyewe hushuhudia pamoja na roho zetu, ya kuwa sisi tu watoto wa Mungu;
Hivyo ndugu, kama bado mpaka sasa hujapata uhakika huo, Ujue tu, mbinguni hutakwenda haijalishi utasema niliongozwa sala ya toba, au nilibatizwa, au nilikuwa ninahudhuria kwenye maombi..Hutakwenda kwasababu suala la wokovu sio suala la kubahatisha au kuhisi hisi tu bali ni uhakika Mungu anaompa mtu akiwa bado hapa hapa duniani..Na kuwa na uhakika wa kwenda mbinguni sio kujihesabia haki..
Biblia inasema…
2Petro 1:10 “Kwa hiyo ndugu, jitahidini zaidi kufanya imara kuitwa kwenu na uteule wenu; maana mkitenda hayo hamtajikwaa kamwe”.
Ukisoma kwenye tafsiri nyingine hususani zile za kiingereza(kjv) Hilo Neno “jitahidini zaidi kufanya imara” linasema hivi..
“brethren, give diligence to make your calling and election sure…”
Neno SURE, linaamisha uhakika, maana yake ujitahidi kuufanya kuitwa kwako na uteule wako uwe wa uhakika..
Hivyo na wewe pia hujachelewa, ndani ya kipindi hichi kifupi cha maisha yako uliyobakiwa nayo hapa duniani, na kabla Bwana hajarudi, anza kuuthibitisha tena wokovu wako, kusudia kweli kuanzia leo kumfuata Kristo, anza kuzaa hayo matunda ya Roho, na kuwa tayari kuubeba msalaba wako..Na Bwana mwenyewe atauweka uhakika huo ndani yako. Nawe utaishi Maisha ya amani kila siku, ambapo hata wimbi lolote likisimama mbele yako, hata bunduki ikiwekwa mbele yako, huna wasiwasi kwasababu unajua ukifa tayari moja kwa moja utakuwa mbinguni kwa Baba.
Bwana akubariki sana.
Maran Atha.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
Mkaribie Bwana.
Shalom, karibu tujifunze Neno la Mungu..
Miongoni mwa watu waliokuwa wanamfuata Bwana Yesu kulikuwa na makundi manne..1) Makutano 2)Wanafunzi 3)Mitume 12 na 4) Nguzo.
Kundi la kwanza ambalo ni makutano, hawa walikuwa tu wanakusanyika kusikiliza mahubiri ya Bwana Yesu ambao mara zote Bwana alikuwa anazungumza nao kwa mifano, na kuwaponya magonjwa yao..baada ya hapo walikuwa wanarejea katika shughuli zao na maisha yao ya kawaida.
Kundi la pili ambalo lilikuwa ni la wanafunzi wa Yesu, hawa walikuwa wapo kama 70 hivi au zaidi kidogo..Kundi hili ni lile ambalo lilikuwa linamfuata Bwana Yesu lakini si kila mahali…Ni baadhi ya watu ambao waliamua kujitoa kumtumikia Yesu sehemu zote alizokuwa anakwenda…na hawa pia Bwana alikuwa anawatuma kuhubiri injili kila mahali ambapo Bwana alipokuwa anataka kwenda. (Soma Luka 10:1).
Kundi la tatu lilikuwa ni Mitume…Mitume hawa walikuwa 12 tu, na waliteuliwa na Bwana Yesu kati ya lile kundi la wanafunzi 70 waliokuwa wanamfuata Yesu.
Luka 6: 13 “Hata kulipokuwa mchana aliwaita wanafunzi wake; akachagua kumi na wawili miongoni mwao, ambao aliwaita Mitume”
Kundi la mitume ndio lilikuwa linamkaribia sana Bwana kuliko wale wanafunzi 70 na makutano..Hawa kila mahali Bwana alipokuwa na wao walikuwepo, walikula nae na kunywa naye…na mbele za Bwana ni kama vile walipendelewa zaidi kuliko wanafunzi wengine kwasababu kila mfano ambao Bwana aliokuwa anawafundisha makutano usioeleweka wao ndio walikuwa wanapata fursa ya kwenda kumwuliza akiwa peke yake, maana ya mifano hiyo, nafasi ambayo makutano wala wale wanafunzi wengine hawakuipata.
Lakini lilikuwepo kundi la mwisho ambalo ni la kipekee sana..ambalo hilo lilikuwa karibu sana na Bwana zaidi ya makundi hayo matatu yaliyotangulia…na kundi hilo lilitwaliwa kutoka miongoni mwa wale wanafunzi 12…Na hao walikuwa watatu tu ambao ni (Petro, Yohana na Yakobo)..Hawa watatu walijulikana kama NGUZO.
Wagalatia 2:9 “tena walipokwisha kuijua ile neema niliyopewa; YAKOBO, na KEFA na YOHANA, WENYE SIFA KUWA NI NGUZO, walinipa mimi na Barnaba mkono wa kuume wa shirika; ili sisi tuende kwa Mataifa, na wao waende kwa watu wa tohara;”
Kefa ni jina lingine la Petro(soma Yohana 1:42). Hawa watatu walijulikana kama nguzo…Maana yake walikuwa wanauhusiano wa kipekee na Bwana zaidi ya mitume wote, zaidi ya wanafunzi wote na zaidi ya makutano yote.
Utaona hawa watatu kila mahali ambapo Bwana alitaka kwenda peke yake (labda mlimani kusali, au kuwafunulia siri za ndani sana) aliwachukua hawa watatu tu Yohana, Yakobo na Petro, na si mitume wengine waliosalia..Hebu tuangalie mifano michache kulithibitisha hili..
Luka 9:27 “Nami nawaambia kweli, Wapo katika hawa wanaosimama hapa, ambao hawataonja mauti kabisa, hata wauone kwanza ufalme wa Mungu.
28 Baada ya maneno hayo yapata siku nane, aliwatwaa PETRO NA YOHANA NA YAKOBO, AKAPANDA MLIMANI ILI KUOMBA.
29 Ikawa katika kusali kwake sura ya uso wake ikageuka, mavazi yake yakawa meupe, yakimeta-meta.
30 Na tazama, watu wawili walikuwa wakizungumza naye, nao ni Musa na Eliya”
Unaona hapo walikuwepo mitume wote lakini Yesu aliwachagua tu hao watatu kwenda nao mlimani..kusali na huko akawafunulia ufunuo mkubwa namna ile, na wakaisikia sauti ya Mungu ikisema huyu ni mwanangu mteule wangu, msikieni Yeye. Ufunuo huo waliouona tu hawa watatu, na Bwana aliwaambia wasimwambie mtu mwingine yoyote mpaka atakapofufuka katika wafu. Maana yake ni kwamba wanafunzi hawa walikuwa na siri nyingi ambazo Bwana aliwafunulia ambazo mitume wengine hawakuzijua.
Tutazame mfano mwingine tena..
Mathayo 26:36 “Kisha Yesu akaenda pamoja nao mpaka bustani iitwayo Gethsemane, akawaambia wanafunzi wake, Ketini hapa, hata niende kule nikaombe.
37 Akamchukua Petro na wale wana wawili wa Zebedayo, akaanza kuhuzunika na kusononeka.
38 Ndipo akawaambia, Roho yangu ina huzuni nyingi kiasi cha kufa; kaeni hapa, mkeshe pamoja nami.
39 Akaendelea mbele kidogo, akaanguka kifulifuli, akaomba, akisema, Baba yangu, ikiwezekana, kikombe hiki kiniepuke; walakini si kama nitakavyo mimi, bali kama utakavyo wewe.
40 Akawajia wale wanafunzi, akawakuta wamelala, akamwambia Petro, Je! Hamkuweza kukesha pamoja nami hata saa moja?”
Hapo utaona Bwana alitenga makundi mawili..kundi la kwanza ambalo ndilo lile la mitume 9 aliliacha kule kwenye bustani ya Gethsemane….hakuenda nalo kuomba usiku ule, badala yake akawachukua Petro, na wale wana wawili wa Zebedayo ambao ni (Yohana na Yakobo), hao ndio akaenda nao kusali..na hao ndio aliowaambia wakeshe waombe pamoja na yeye wasije wakaingia majaribuni..kwasababu shetani ndio aliokuwa anawawinda zaidi kwasababu walikuwa na Bwana zaidi..Na kama wewe ni msomaji wa biblia utagundua kuwa wakiwa kule waliona tena ishara nyingine wakati Yesu akiwa anaomba jasho lake lilikuwa kama matone ya damu, na pia waliona malaika wakija kumtia nguvu…
mambo hayo mitume wengine waliosalia hawakuyaona…
Na hawa watatu, hata wakati wa Pentekoste na kuendelea ndio mitume Bwana alitembea nao kwa viwango vikubwa sana..mpaka watu wote wakawaita kuwa ni NGUZO YA KANISA. Kitabu cha Ufunuo wa Yohana, ambacho kimebeba siri nyingi za ufunuo wa siku za mwisho, na ujio wa Bwana Yesu kimendikwa na Yohana huyu…ambaye ndiye mmoja wao wa wale watatu.
Sasa kwanini wanafunzi hawa watatu waliteuliwa na Bwana kuwa karibu zaidi na yeye kuliko wengine wote?
Jibu ni kwamba, kwasababu walimpenda Bwana zaidi..Mungu hana upendeleo hata kidogo..kila dakika, kila muda walikuwa wanamtafakari Bwana, wanamfikiria yeye, wanamtumikia yeye, na wamejikana nafsi na kusema lolote liwalo tutamfuata Yesu Bwana wetu popote aendapo, kwa moyo huo Bwana akawapenda zaidi na hivyo kuwakaribisha wamsogelee zaidi kuliko wengine…Kama ni mwanafunzi wa Biblia utamjua Petro alivyokuwa anampenda Bwana…ilifika wakati akamwambia Bwana wajapochukizwa wote kwaajili yako mimi sitachukizwa..ijapokuwa alikuwa ni dhaifu lakini angalau hata alikuwa anaujasiri wa kusema hivyo tofauti na wengine…
Hali kadhalika Yohana na Yakobo ni hivyo hivyo,..walimpenda Bwana mpaka ikafikia wakati wakamwendea Bwana wao na kumwomba katika ufalme wake waketi mmoja mkono wake wa kuume na mwingine wa kushoto…(walimpenda Bwana mno na hivyo Bwana akawapenda zaidi). Yohana ilifika wakati akawa anaegemea kifuani mwa Yesu kila mahali…na ilifika kipindi Bwana akawaambia wazi wazi kuwa mmoja wao atamsaliti..na kila mmoja akawa anawasiwasi ni nani amtajaye..na Bwana akamfunulia Yohana peke yake kwamba ni Yuda kwa sauti ya chini, wengine hawakusikia.. kwasababu alikuwa karibu sana na yeye kifuani mwake…
Yohana 13:23 “Na palikuwapo mmoja wa wanafunzi wake, ameegama kifuani pa Yesu, ambaye Yesu alimpenda.
24 Basi Simoni Petro akampungia mkono, akamwambia, Uliza, ni nani amtajaye?
25 Basi yeye, hali akimwelekea Yesu kifua chake, akamwambia, Bwana, ni nani?
26 Basi Yesu akajibu, Ndiye mtu yule nitakayemtowelea tonge na kumpa. Akatowelea tonge, akalitwaa akampa Yuda, mwana wa Simoni Iskariote”.
Tabia ya hawa watatu kuwa tayari chochote Bwana alichowaambia ndizo zilizowafanya kuwa karibu zaidi na Bwana kuliko wengine, Bwana alipotaka kwenda kuomba walikuwa tayari kutaka na wao kwenda kuomba..walikuwa hawaonyeshi dalili za uvuvi ingawa walikuwa na madhaifu, walijinyima kila kitu ili tu wampendeze Yesu.
Vivyo hivyo Neno la Mungu linasema..Yakobo 4:8 “Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi. Itakaseni mikono yenu, enyi wenye dhambi, na kuisafisha mioyo yenu, enyi wenye nia mbili”.
Unapojikana nafsi na kumpenda Mungu zaidi, na kumfanya yeye ndio wakwanza kila mahali, hapo ndipo unapojitengenezea daraja zuri la Mungu kukukaribia zaidi..ndipo unapoongeza daraja zuri la Mungu kukupenda zaidi ya wengine, kukufunulia siri nyingi zaidi ya wengine…kukutumia na kukubariki. Unapoutafa uso wa Mungu kwa kusali, kufunga, kutenda mema zaidi ya wengine..mema yako yanapimwa mbele za Mungu kila siku na yanapoonekana yamezidi ya wengine wengi ndipo na wewe thamani yako inapanda mbele za Mungu, lakini kama leo ukiambiwa tu usali..hata dakika mbili humalizi, kusoma tu neno ni mara moja kwa wiki, na hata ukisoma unasoma tu mistari na sio mada nzima..hapo utafanyikaje NGUZO mbele za Mungu.?
Hivyo tusiridhike na uhusiano wetu na Mungu..Tuzidi kumkaribia Bwana..kutoka kuwa wanafunzi wake, hata mitume wake hata Nguzo..
Ufunuo 3: 12 “Yeye ashindaye, nitamfanya kuwa NGUZO katika hekalu la Mungu wangu, wala hatatoka humo tena kabisa, nami nitaandika juu yake jina la Mungu wangu, na jina la mji wa Mungu wangu, huo Yerusalemu mpya, ushukao kutoka mbinguni kwa Mungu wangu, na jina langu mwenyewe, lile jipya”.
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
Maran atha!
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
SWALI: Hujambo mpendwa,naomba nieleweshwe hili tafadhali katika mwanzo 22:14 utaona Ibrahimu alipaita mahali pale YEHOVA-YIRE ambapo alimtoa yule kondoo kuwa sadaka, badala ya Isaka, lakini ukisoma tena katika Kutoka 6:2-3 Mungu anamwambia Musa kwamba hakuwai kujidhihirisha kama YEHOVA kwa Ibrahimu ,Isaka, na Yakobo, bali Mungu mwenyezi. Je! Biblia inajipinga? Asante sana.
JIBU: Kumbuka vitabu vitano vya mwanzo vimeandika na mtu mmoja ambaye ni MUSA (Ambavyo ni Mwanzo, kutoka, Mambo ya Walawi, Hesabu na kumbukumbu la Torati ).. Na kama tunavyojua Musa aliviandika vitabu hivi alipokuwa jangwani (yaani akiwa njiani kuelekea nchi ya Ahadi).. Na katika kitabu cha Mwanzo ambacho ndicho tunapata huko habari za Ibrahimu…wakati anaziandika habari hizo akiwa jangwani tayari alikuwa ameshafunuliwa jina hilo jipya la Mungu yaana YEHOVA. Hivyo mahali popote ambapo alisoma habari za Ibrahimu, akimtaja Mungu kwa jina lolote lile yeye Musa ni lazima angeliandika kwa jina YEHOVA, kadhalika mahali popote ambapo Nuhu angemtaja Mungu kwa jina lolote lile yeye Musa angesahihisha katika maandishi yake na kuandika jina YEHOVA badala yake..na hivyo hivyo kwa Lutu, Yakobo, Isaka, Yusufu na wengineo.
Sasa utauliza mbona kila mahali katika vitabu hivyo vitano vya kwanza vya Musa kila mahali Mungu katajwa kama BWANA, na si hilo YEHOVA ??
Kumbuka Katika biblia yetu ya Kiswahili na ya kiingereza na ya lugha nyingine zote…kila mahali ambapo leo hii tunapasoma pameandikwa neno BWANA, Kwa asili hapakupaswa paandikwe hivyo…Sehemu nyingi katika agano la lake unapopaona pameandikwa neno BWANA, kwa asili pangepaswa paandikwe neno YEHOVA. Musa nyingi alizitafsiri kama Yehova..kwa mfano katika
Mwanzo 2:7 biblia inasema
“ Bwana Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai”…Mstari huu Musa aliuandika hivi “Yehova Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai ”
Lakini sasa watafsiri wa kwanza biblia waliona ili kuliheshimu zaidi hilo jina la Mungu si vyema kuandika jina hilo Tukufu na kuu kama lilivyo…Hivyo kwa hekima ya Roho ndipo likawekwa jina BWANA badala ya YEHOVA..Kitu ambacho ni kizuri!..kama tu vile isivyo hekima wala heshima kumwita mzazi wako jina lake halisi na badala yake unamwita jina lake la cheo “BABA”..huwezi kusema shikamoo Joseph badala yake utasema shikamoo Baba. Hivyo si dhambi kumwita Mungu BWANA kama inavyochukuliwa leo na ndugu zetu mashahidi wa Yehova wakidhani kuwa kumuita Mungu BWANA ni kumvunjia heshima..
Biblia zote, pale kwenye utangulizi, zimechapishwa na angalizo hilo pale mwanzoni kabisa.. Kuwa BWANA lilimaanisha YEHOVA.
Kwahiyo kitabu cha Mwanzo kimetaja Yehova na kitabu cha Kutoka kwasababu mwandishi ni huyo huyo mmoja, na aliviandika vitabu hivyo akiwa tayari ameshalijua jina la Mungu kamilifu yaani Yehova.
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
Kwanini Bwana alisema Hakuna aliye mwema ila mmoja?
Kwanini wanawake wengi huwa wanalipuka mapepo?
Kwanini kila nikitaka kusali naingiwa na uvivu?
KWANINI BWANA YESU ALISULUBIWA NA WEZI WAWILI?
Kwanini Mungu aliikubali sadaka ya Yeftha ya kumtoa binti yake kafara?
Ufunuo 12:12 “Kwa hiyo shangilieni, enyi mbingu, nanyi mkaao humo. Ole wa nchi na bahari! Kwa maana yule Ibilisi ameshuka kwenu mwenye ghadhabu nyingi, akijua ya kuwa ana wakati mchache tu.
13 Na joka yule alipoona ya kuwa ametupwa katika nchi, alimwudhi mwanamke yule aliyemzaa mtoto mwanamume.
14 Mwanamke yule akapewa mabawa mawili ya tai yule mkubwa, ili aruke, aende zake nyikani hata mahali pake, hapo alishwapo kwa wakati na nyakati na nusu ya wakati, mbali na nyoka huyo.
15 Nyoka akatoa katika kinywa chake, nyuma ya huyo mwanamke, maji kama mto, amfanye kuchukuliwa na mto ule.
16 Nchi ikamsaidia mwanamke; nchi ikafunua kinywa chake, ikaumeza mto ule alioutoa yule joka katika kinywa chake.
17 Joka akamkasirikia yule mwanamke, akaenda zake afanye vita juu ya wazao wake waliosalia, wazishikao amri za Mungu, na kuwa na ushuhuda wa Yesu; naye akasimama JUU YA MCHANGA WA BAHARI”.
Shalom, Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe, kama ukisoma mistari iliyotangulia kabla ya hiyo, utaona kuwa shetani kuna majira alijaribu kufanya vita katika mbingu, lakini alishindwa kama biblia inavyotuambia akatupwa chini na mahali pake hapakuonekana tena mbinguni kuanzia huo wakati.
Lakini biblia inatuambia pia alipotupwa, hakukaa katika eneo la nchi peke yake, au hakwenda baharini moja kwa moja , hapana, bali alikwenda kusimama juu ya mchanga wa bahari….Kwa namna nyingine alikwenda kusimama ufukweni mahali ambapo nchi na bahari vinakutana.
Shetani alifahamu kuwa, hivyo ndivyo vitu viwili vinavyoikamilisha dunia, hakuegemea tu upande mmoja afanye makao yake huo hapana..badala yake alisimama pale ufukweni ili aweze kuyaona na kuyatawala yale yanayotoka katika nchi na yale yanayotoka katika bahari. Na ndio maana baada ya pale biblia inasema “Ole wa nchi na bahari”, Kwa maana yule Ibilisi ameshuka kwenu mwenye ghadhabu nyingi, akijua ya kuwa ana wakati mchache tu..
Unaona? haituambii nchi tu peke yake, au bahari peke yake, hapana bali vyote viwili, kwasababu ndipo alipopania kuwanasa wanadamu.
SASA NCHI NA BAHARI KIBIBLIA VINAWAKILISHA NINI?
BAHARI: au sehemu yenye maji mengi, biblia imeshatupa majibu yake,.Tusome.
Ufunuo 17:15 “Kisha akaniambia, Yale maji uliyoyaona, hapo aketipo yule kahaba, ni jamaa na makutano na mataifa na lugha”.
Kumbe maji yanawakilisha jamaa, na makutano na mataifa na lugha…Yaani kwa ufupi watu wengi.
Vilevile, tunaweza kuona jambo lingine, pale Bwana Yesu alipochagua mitume wake, wengi wao aliwachagua kutoka katikakati ya wavuvi, akifunua kuwa watakuja kufanya kazi ya uvuvi wa watu wengi, yaani jamaa, na mataifa la Lugha, kama alivyomwambia Petro na Andrea katika (Mathayo 4:19)..
Hivyo Bahari inawakalisha watu wengi, kwahiyo shetani tangu alipoona ameshindwa hawezi tena kupigana yeye kama yeye aliamua sasa kuelekeza macho yake katikati ya watu ili apate nguvu, na chombo kikubwa anachokitumia ili kupata ufuasi mkubwa wa watu ni kupitia kitu kinachoitwa DINI, penye dini ndipo palipo na watu wengi, sio katika siasa au makabila..
Hivyo mpaka sasa yupo katika kilele cha kuzikutanisha dini zote na madhehebu yake yote ambayo tangu zamani yalishautupilia mbali uongozo wa Roho Mtakatifu na kufuata mapokeo yao ya kibinadamu, ili zikubaliane katika kitu kimoja.
Na ndio maana ukisoma ile sura inayofuata ya 13, utaona Yule joka aliposimama tu pale kwenye mchanga wa bahari, wakati huo huo wanyama wawili walitokea, mmoja alitokea baharini, na mwingine akatokea nchi kavu (Soma ufunuo sura ya 13 yote utaona)..Sasa Yule aliyetokea habarini ndiyo huyu atakayepata nguvu ya kuwa na wafuasi wengi sana duniani kwa kupitia dini…
NCHI: NI Hifadhi ya kimwili, tangu mwanzo, Mungu alipomuumba Adamu alimpa ardhi ailime na kuitunza kwasababu huko ndipo alipomchipulia chakula chake kitakachomfanya aishi hapa duniani.
Ayubu 28:5 “Katika ardhi ndimo kitokeamo chakula;…”..
Hata sasa chakula na utajiri vipo katika ardhi..Hivyo kwa lugha ya sasa nchi tunaweza kusema inawakilisha Uchumi,..Fedha, biashara, hazina, vitu vinavyoweza kumpatia mwanadamu Rizki ili aishi hapa duniani n.k…
Kwahiyo shetani kuona hivyo, alisimama pia katika eneo hilo.. tangu huo wakati akajikita kudhibiti mihimili hiyo miwili mikuu, Watu, na uchumi.. nchi na bahari..
Kwanza Ili awapate Watu anatumia kivuli cha dini, ambapo hivi karibu anaenda kutimiza adhma yake ya kuzileta dini zote zilizopoteza uongozo wa Roho Mtakatifu pamoja, zikiongozwa na ile dini mama ya Rumi, na cha ajabu biblia inatuambia watu wote na mataifa yote ambao majina yao hayakuandikwa katika kitabu cha uzima cha mwanakondoo tangu kuwekwa misingi ya ulimwengu wataufurahia huo utawala na mfumo mzima wa ibilisi ..
Na sasa ili kuwalazimisha watu wote waufuate huo mfumo wa mpinga-Kristo, shetani atamnyanyua mnyama mwingine ambaye atakuwa na nguvu ya kiuchumi sana,(taifa kubwa) ambalo hilo litayahimiza mataifa mengine yote yapokee maagizo kutoka kwa huo umoja wa dini duniani, na mtu yoyote atakayekataa kuupokea hataruhusiwa kununua wala kuuza, wala kufanya biashara yoyote, wala kuajiriwa mahali popote.. Unaona Jinsi hali itakavyokuwa mbaya.. Ni nani atapona hapo.
Haya ni mambo ambayo tunaweza kuyashuhudia siku za hivi karibuni wala tusidhani bado miaka mingi, jaribu kufikiria jinsi ugonjwa huu wa Corona ulivyozuka tu ghafla, na athari yake ndogo tu inawafanya watu wasiweze kutembea hata nje katika baadhi ya nchi, na imetokea tu ndani ya kipindi kifupi cha miezi mitatu tu, hakuna ambaye angeamini kuwa dunia ingeweza kuwa namna hii, dunia ambayo inashamra shamra za kila namna..Lakini mambo yamekuwa hivyo barabara zipo wazi..Hata matajiri na wana wa wafalme, na watu mashuhuri na fedha zao haziwasaidii wakati huu. Ndivyo mambo yatakavyobadilika ghafla tu wakati huo ukifika.
Shetani ameshajidhatiti vya kutosha, na ghafla tu, dini zote zitafikia muafaka mmoja zikiongozwa na dini ile mama ya Rumi, watafikia muafaka mmoja, watapata sapoti kutoka katika kila pembe ya dunia, watakuwa na kiongozi wao mmoja ambaye ndio atakuwa mpinga-Kristo..Huyo ataishawishi dunia iwe na ustaarabu mpya, Lakini lengo lake ni kuihimiza ile chapa ya mnyama ili awanase wanadamu wote.. Sasa kwa kuwa yeye amejikita katika masuala ya kiimani sana, kama tulivyosema atapata msaada mwingine kutoka katika taifa lenye nguvu ya kiuchumi duniani, ili kuyalazimisha mataifa mengine yote yamtii yeye kwa shuruti.
Mpaka wakati huo umefika ujue unyakuo tayari umeshapita ndugu yangu, sijui utakula nini wewe unayemkataa Yesu leo, wewe ambaye utakuwepo ulimwenguni wakati huo, pona yako itakuwa ni kufia njaa ndani, kama utakuwa hujakamatwa na kuuliwa kwa mateso yasiyokuwa ya kawaida.. Hakuna mtu yoyote atayevumiliwa na mtu au chombo chochote cha dola ambaye ataonekana hajapokea chapa hiyo ya mnyama.. usifikiri utapona..Ni ngumu sana ndugu, usidhani akaunti yako ya benki itakusaidia wakati huo, hilo jambo halitakuwepo, usidhani utakimbilia mafichoni, ondoa hayo mawazo, usidhani elimu yako itakusaidia kupata ajira wakati huo, acha kufikiria hivyo..Chapa utaipokea tu.
Hizi ni nyakati za hatari tunazoishi, ole wa nchi na bahari!…Kimbilio pekee ni Kristo tu saa hii..Ikiwa upo bado nje ya Kristo, basi fanya uamuzi wa Busara leo hii, tubu dhambi zako kwa kumaanisha kuziacha, omba toba kwa Mungu, nenda kabatizwe ikiwa bado hujafanya hivyo. huu ni wakati sasa wa kuamka usingizini.
Warumi 13:11 “Naam, tukiujua wakati, kwamba saa ya kuamka katika usingizi imekwisha kuwadia; kwa maana sasa wokovu wetu u karibu nasi kuliko tulipoanza kuamini”.
Bwana akubariki sana.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
UFUNUO: Mlango wa 13
UCHAWI WA BALAAMU.
CHUKIZO LA UHARIBIFU
DANIELI: Mlango wa 7
MWISHO WA DUNIA UTAKUJAJE?
Nini maana ya “Siku moja nyuani mwa Bwana ni bora kuliko miaka elfu”?
Hesabu 23:23 “Hakika hapana uchawi juu ya Yakobo, Wala hapana uganga juu ya Israeli”
Wengi tunalifahamu hili andiko na tunalitumia, pale tunapohisi roho za kichawi zinatunyemelea…Na tunapolitumia kwa Imani linaleta majibu hakika kwasababu ni pumzi ya Mungu…Lakini hebu leo tuingie kwa undani kidogo kujifunza juu ya Neno hili ili tupate faida mara mbili Zaidi.
Siku zote tunashauriwa tujifunze biblia na sio tuisome tu…tukichukua tu kipengele cha mstari wa biblia na kukitumia hicho bila kutafuta maana ya mstari huo, kwanini mwandishi aliandika hivyo, na Mungu alikuwa anamaanisha nini juu ya mstari huo..hapo tutakuwa hatujajifunza bali tumesoma tu..ambapo matokeo yake ni madogo kuliko kama tungeketi chini na kujifunza kuanzia juu chanzo cha mstari huo na dhima, na maudhui ya huo mstari ukoje.
Sasa tukirudi katika mstari huo hapo juu, kama ukianza kusoma kitabu hicho cha Hesabu kuanzia sura zilizotangulia kabla ya hiyo ya 23, utaona inahusu safari ya wana wa Israeli (au wana wa Yakobo), walipokuwa wanatoka Misri kuelekea nchi yao ya Ahadi,
Wakiwa njiani jangwani walikutana na kikwazo, Ilikuwa kwamba ili waendelee na safari yao iliwapasa wakatize katika nchi ya watu fulani ambao walijulikana kama wamoabu.
Nchi hiyo ilikuwa na mfalme na huyo mfalme akawakatalia wasikatize katika nchi hiyo, na hakukuwa na njia nyingine ya karibu isipokuwa kukatiza katika nchi hiyo..Ijapokuwa waliwaomba sana na kuwaahidi kwamba watalipia gharama zote za uharibifu wowote kama ukijitokeza katika kukatiza kwao lakini wenyeji wa mji ule walikataa katakata wakiongozwa na mfalme wao..Na kwa hofu Mfalme wao hakuishia tu kuwazuia bali alipanga pia kwenda kupigana nao, hivyo akatafuta pia namna ya kuwalaani(au kwa lugha rahisi kuwaloga) ili atakapokwenda kupigana nao aweze kuwashinda kirahisi bila kutumia nguvu nyingi.
Katika harakati za kutafuta mtu mashuhuri wa kuloga, akampata mtu anayeitwa Balaamu mchawi (Hesabu 24:1), huyu alikuwa ni mchawi wa viwango vya juu sana na aliyejulikana kwa kuloga hata mataifa, ambaye alitumia nguvu za giza, na alikuwa anauwezo wa kuisikia pia sauti ya Mungu..na kabla ya kuloga alikuwa anauwezo wa kupima kiwango cha kiroho mtu alichopo kabla ya kumwangusha…na sio hilo tu, alikuwa anazo mpaka mbinu mbadala zisizo za kuweza kumwangusha mtu bila kutumia uchawi wowote…(na huo ndio mbaya Zaidi ambao ndio alioutumia kuwaangusha wana wa Israeli).
Sasa alipoitwa kama wengi wetu tunavyoijua habari…haraka sana aliwajua wana wa Israeli ni watu gani…alijua ni watu wa Mungu na wamezungukwa na ukingo wa Mungu pande zote…hakuna namna ya kuweza kuwaingia kwa njia ya uganga wala uchawi (hakuna namna yoyote vibuyu na dawa za miti shamba zinaweza kufanya kazi juu yao)..hata hivyo alinusurika kifo njiani wakati anajaribu kutaka kwenda kuwalaani…Ili litimie lile neno la kwanza (akulaaniye atalaaniwa, na akubarikiye atabarikiwa).
Hivyo Balaamu alilijua hilo na alipofika kwa mfalme wa MOABU akamwambia wazi kabisa kwamba “HAKIKA HAPANA UCHAWI JUU YA YAKOBO, WALA HAPANA UGANGA JUU YA ISRAELI”.
Hiyo ndiyo asili ya Neno hilo…Ni mchawi Balaamu ndiye aliyeyasema maneno hayo sio Mungu kama wengi wetu tunavyodhani. Balaamu alikiri kabisa..Hivyo akaacha kujaribu kuwaloga/kuwalaani Israeli ambaye ndiye Yakobo, kinyume chake akawabariki, kwasababu alijua endapo angetaka kuwaalaani ni kujitafutia laana na kifo..hivyo akaamua kuhamia kwenye Mbinu yake ya pili ambayo ndiyo KUBWA NA KUU.
Hesabu 24:1 “Basi Balaamu alipoona ya kuwa ilimpendeza Bwana kuwabariki Israeli, hakwenda, kama hapo kwanza, ili kutafuta uchawi, bali alielekeza uso wake jangwani”
Mbinu hiyo siyo ya kutumia vitunguli tena/wala vibuyu/ wala ya kuwatamkia maneno mabaya..Mbinu hii ya pili ambayo ndio UCHAWI HASAA ni ya kuwakosesha wana wa Israeli na Mungu wao..Ili Mungu awakasirikie na kuwaadhibu yeye mwenyewe…kwasababu kuwaangusha kwa njia ya uchawi imeshindikana sasa dawa ni kuwachonganisha na Mungu wao..Hivyo akamfundisha Mfalme wa Moabu namna ya kuwakosesha wana wa Israeli ili wapigwe na Mungu wao..
Akamfundisha na kumwambia wawaalike wana wa Israeli baadhi katika sadaka za miungu yao na kuwapa wanawake wao walio wazuri na warembo, hivyo Wana wa Israeli watakapoona hivyo wataingia tamaa na kuzini na wanawake hao katika karamu hizo za miungu na hasira ya Mungu itawaka juu ya wana wa Israeli..Tusome
Hesabu 25:1 “Basi Israeli akakaa Shitimu, kisha watu wakaanza kuzini pamoja na wanawake wa Moabu;
2 kwa kuwa waliwaalika hao watu waende sadakani, sadaka walizowachinjia miungu yao; watu wakala chakula, wakaisujudu hiyo miungu yao.
3 Ikawa Israeli kujiungamanisha na Baal-peori; hasira za Bwana zikawaka juu ya Israeli”.
Ukiendelea kusoma utaona Mungu aliwakasirikia na aliwaua kwa pigo watu elfu 24. Kama sio mtu mmoja kwenda kurekebisha Israeli wote wangeisha siku hiyo mbele ya ghadhabu ya Mungu..Hivyo japokuwa Yule mchawi balaamu hakuwaloga kwa uchawi wa uganga na vibuyu lakini aliwaloga kwa kuwakosesha na Mungu wao.
Jambo hilo hilo linaendelea hata sasa katika nyakati hizi za agano jipya. Ni kweli hakuna uganga wala uchawi juu yako, umelindwa na kuzungukwa na kingo za moto pande zote, katika afya yako, katika kazi zako, katika familia yako, mpaka una ujasiri wa kusema Bwana ndiye anisaidiaye sitaogopa mabaya, wala uchawi wala uganga..Ndio shetani analijua hilo na wala hawezi kukuloga kwa vitunguli, wanaokuendea kwa waganga ni kweli wanapoteza muda..nataka nikuambie shetani akishalijua hilo wala hapotezi muda wake kukutumia watu kutafuta kukuloga wewe…kwasababu hawezi kulaani kilichobarikiwa…hviyo acha kufikiri kwamba wachawi wanakuwinda wewe uliyeokoka kweli kweli, walishaacha siku nyingi wakati ule walipogundua tu unazungukwa na jeshi la mbinguni…
Shetani anachofanya sasa juu yako ni kutafuta njia ya kukukosesha wewe na Mungu wako, ili Mungu akuadhibu…na anatumia watu mfano wa Balaamu..wanaoonekana nje ni watu wa Mungu kumbe ndani ni mbwa-mwitu wa kali…Hao watakwambia kuoa mke wa pili si dhambi, watakwambia kuziangukia sanamu na kuzibusu na kuzipa heshima sio kuzisujudia.
Na biblia imeshatabiri nyakati hizi za mwisho watu wengi wataangukia katika kosa hili la Balaamu..
Yuda 1:11 “Ole wao! Kwa sababu walikwenda katika njia ya Kaini, na kulifuata kosa la Balaamu pasipo kujizuia, kwa ajili ya ujira, nao wameangamia katika maasi ya Kora”.
Watakwambia kufanya matambiko ya ukoo sio dhambi, watakuwambia kuishi na mwanamke/mwanamume ambaye hamjaoana hakuna tatizo, watakuwambia kuzini ni mapungufu ya kila mtu, watakuweka katika kila kishawishi cha wewe kufanya dhambi, , Zaidi sana watakufariji katika dhambi na watakukemea katika kuwa mtakatifu…lengo na madhumuni ni kukukosesha wewe na Mungu wako ili Mungu akukasirikie na kukuangamiza (Huo ndio uchawi mkubwa shetani anaowalogea watu wa Mungu kuliko hata ule wa vibuyu)..
Bwana Yesu alisema maneno hayo Dhahiri katika Ufunuo.
Ufunuo 2:14 “Lakini ninayo maneno machache juu yako, kwa kuwa unao huko watu washikao mafundisho ya Balaamu, yeye aliyemfundisha Balaki atie ukwazo mbele ya Waisraeli, kwamba wavile vitu vilivyotolewa sadaka kwa sanamu, na kuzini”.
Je! Na wewe umedanganyika na uchawi huo wa Balaamu? Nabii wa uongo?..Unadhani shetani anahangaika na bati lako usiku na kundi lake la wachawi?..usidanganyike!..anahangaika sasa kukukosesha na Mungu wako. Hataki ulifahamu neno na anafanya juu chini ufe katika dhambi zako ili siku ile uingia katika adhabu ya hasira ya Mungu katika ziwa la moto. Hivyo mwache aende peke yake huko yeye na mabalaamu wake, sisi tujitenge na yeye kwa kutubu leo na kushika amri za Mungu na Neno lake, kwa kujitenga na uasherati wote, wizi, rushwa, anasa, tamaa mbaya, wivu, matusi, na mambo yote machafu na kuzidi kujitakasa kila siku, na kuishi katika utakatifu ndipo tutakapojiepusha na ghadhabu ya Mungu na kupata baraka zote alizozikusudia katika Maisha yetu. Hatuna haja ya kuogopa wachawi wa vibuyu kwasababu huko waliko wanakiri kwamba hakuna uchawi wala uganga kwa waliokoka..
Sisi tupambane kujilinda na dhambi ndilo jukumu tulilolonalo sasa.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 1
KIFO CHA MTAKATIFU PERPETUA NA FELISTA.
WAKAMTUKANA MUNGU, WALA HAWAKUTUBU.
NENO NI LILE LILE, LAKINI UJUMBE NI TOFAUTI.
VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 2
JINA LA MUNGU NI LIPI?