Title Devis

Nini maana ya “katika wingi wa hekima mna wingi wa huzuni”.


SWALI: Biblia ina maana gani kusema “Katika wingi wa hekima mna wingi wa huzuni” Je! si sahihi kutafuta hekima?

Mhubiri1:17 “Nikatia moyo wangu ili kuijua hekima, na kujua wazimu na upumbavu; nikatambua ya kwamba hayo yote nayo ni kujilisha upepo.

18 Yaani, Katika wingi wa hekima mna wingi wa huzuni, Naye aongezaye maarifa huongeza masikitiko”.

JIBU: Ukisoma Sura hiyo ya kwanza yote, na zinazofuata utaona Sulemani alikuwa anaeleza jinsi alivyojibidiisha katika kutafuta mambo ya ulimwenguni, na hekima yake na kazi zote “zinazofanywa chini ya mbingu (Mhubiri 1:13)”.

Lakini hasemi alikuwa anayatafuta  mambo ya ki-mbinguni, hapana, na ndio maana utaona kila mahali anaishia kusema ni ubatili mtupu, sehemu zote, yaani maudhui ya kitabu cha mhubiri kinaeleza hatma ya kazi zote na shughuli zote zinazofanywa na wanadamu chini ya jua, na ndio maana mwishoni kabisa  mwa kitabu hicho utaona sasa Sulemani anatoa jibu la jambo la muhimu ambalo mwanadamu anapaswa alitafute siku zote za maisha yake..Anasema na hilo si lingine zaidi ya kumcha Mungu basi. (Soma Mhubiri 12:13).

Sasa tukirudi kwenye mstari huo anaposema “Katika wingi wa hekima mna wingi wa huzuni,Naye aongezaye maarifa huongeza masikitiko” Hamaanishi Hekima ya kimbinguni au maarifa ya kimbinguni,..Hapana!, kinyume chake hekima ya kimbinguni na maarifa ya kimbinguni ndio yanayomfanya mtu awe na amani na furaha na utulivu wa nafsi..Kumjua Yesu ambaye ndio hekima ya Mungu (sawasawa na 1Wakorintho 1:24), ni mwisho wa masumbuko yote, unakuwa umefunguliwa milele, hakuna huzuni yoyote wala masikitiko.. Unapolisoma gombo( ambalo ni Neno la Mungu), ndipo unapopata maarifa sahihi ya kuishi hapa duniani, na unafungua milango yote iliyofungwa.

Hivyo maarifa yanayozungumziwa hapo ni haya maarifa ya kiduniani tuliyonayo, kwasababu, pale mtu anapokuwa na elimu kubwa sana, inadhaniwa kuwa ndio itampa furaha ya kweli katika moyo wake, lakini matokeo yanaonyesha kuwa hilo sio kweli, Sulemani alilipata hilo akadhani ndio lingempa furaha aliyokuwa anaitazamia, lakini akagundua kuwa ni ubatili.

Ni jambo la kawaida, wanasayansi wanaokesha maabara usiku kucha, kutafiti na kugundua, asilimia kubwa huwa maisha yao sio ya furaha, kwasababu wanakuwa na hofu ya vitu vingi, hilo likitokea, au lile likizuka itakuwaje, maadui zetu wakitengeneza bomu la atomiki kama hili tunalotengeneza sisi itakuwaje? Dawa au kemikali hii madhara yake yatakuwaje miaka 10 mbele? N.k.n.k.. Maarifa yao na hekima zao zinapozidi kuongezeka huzuni nazo zinazidi kuongezeka…

Hivyo mwisho wa siku inakuwa ni huzuni juu ya huzuni tu na masikitiko juu ya masikitiko na ndio maana biblia inatuasa, tupende kuongeza maarifa kwa Mungu wetu zaidi kuliko sehemu nyingine yoyote kwasababu huko ndiko tutapata furaha ya kweli idumuyo na utulivu na amani isiyoisha.

Bwana Yesu (ambaye ndio hekima ya Mungu) anasema;

Mathayo 11:28 “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.

29 Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu;

30 kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi”.

Kwa Bwana Yesu ndipo penye pumziko la kweli.

Shalom.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618.


Mada Nyinginezo:

Hanithi ni nini katika biblia? (kumbukumbu 23:17)

WOSIA WA BWANA YESU KWA WANAFUNZI WAKE.

Bwana Yesu alimaanisha nini aliposema; Mafarisayo Hupanua HIRIZI zao, na kuongeza MATAMVUA yao?

SIKUKUU YA VIBANDA.

BWANA alimaanisha nini kwenye mstari huu Marko 2:21″ Hakuna mtu ashonaye kiraka cha nguo mpya katika vazi kukuu;?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Hanithi ni nini katika biblia? (kumbukumbu 23:17)

Hanithi ni nini?


Hanithi kibiblia ni mwanaume anayeingiliwa kinyume na maumbile, (Kwa lugha ya sasa wanajulikana kama mashoga), watu wote waliokuwa wanafanya hivi vitendo, waliitwa mahanithi,  na adhabu yake ilikuwa ni mpaka kifo.

Kumbukumbu 23:17 “Pasiwe na kahaba katika binti za Israeli, wala pasiwe na hanithi katika wana wa Israeli wanaume”.

Zamani katika Israeli watu wote waliokuwa wanahudumu kwenye madhabahu za miungu kama vile maashera n.k., walikuwa na desturi ya kufanya hivi vitendo kwa heshima ya miungu yao.

1Wafalme 14:23 “Maana hao pia wakajijengea mahali pa juu, na nguzo, na maashera, juu ya kila kilima kirefu, na chini ya kila mti wenye majani mabichi.

24 Na mahanithi walikuwako katika nchi, wakafanya sawasawa na machukizo yote ya mataifa Bwana aliowafukuza mbele ya wana wa Israeli”.

1Wafalme 15:11 “Basi, Asa akafanya yaliyo mema machoni pa Mungu, kama alivyofanya babaye Daudi.

12 Akawafukuza mahanithi katika nchi, akaziondoa sanamu zote walizozifanya baba zake”.

2Wafalme 23:7 “Akaziangusha nyumba za mahanithi, waliokuwamo nyumbani mwa Bwana, wanawake walipofuma mapazia ya Ashera”.

Hii ni roho ambayo mpaka sasa inatenda kazi, na katika hizi siku za mwisho, ilitabiriwa itajirudia kwa nguvu kama ilivyokuwa katika siku za Sodoma na Gomora, Unaweza kuona leo hii wimbi hili la watu linavyozidi kuongezeka kwa kasi duniani kiasi kwamba hata sheria za nchi zinaruhusu, na baadhi ya dini za uongo, na mpaka wanayo bendera yao duniani, kama unavyoweza kuiona katika picha juu, bendera hiyo yenye rangi ya upinde wa mvua, ndio kauli mbiu yao kuwa Mungu hataiangamiza dunia tena kama alivyoahidi, hivyo ndivyo wanavyojidanganya.. Lakini hawajui kuwa Mungu alisema  kweli hataigharikisha dunia kwa maji, lakini alisema ataiangamiza kwa moto.

2Petro 3:6 “kwa hayo dunia ile ya wakati ule iligharikishwa na maji, ikaangamia.

7 Lakini mbingu za sasa na nchi zimewekwa akiba kwa moto, kwa neno lilo hilo, zikilindwa hata siku ya hukumu, na ya kuangamia kwao wanadamu wasiomcha Mungu”.

Unaona? Hiyo ni dalili ya wazi kuwa hii dunia inakwenda kuangamizwa wakati sio mwingi.

Lakini sisi tuyoanapo hayo, ni wajibu wetu kujiimarisha na kusimama imara katika hichi kipindi kifupi tulichobakiwa nacho, kwasababu Unyakuo upo karibu.

Swali ni Je! Tumejiwekaje tayari kwa Kurudi kwa Bwana mara ya pili?

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618.

Mada Nyinginezo:

JINSI SODOMA NA GOMORA ILIVYOKUWA INAVUTIA SANA..

MAONO YA NABII AMOSI.

HIZI NI NYAKATI ZA KUJIINGIZA KWA NGUVU.

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Uzima wa milele ni nini?

Uzima wa milele ni nini kama unavyotajwa sehemu mbalimbali?


Jibu fupi, uzima wa milele ni maisha yasiyokuwa na mwisho. Yaani unaishi tu, na utaendelea kuishi, hivyo hivyo kwa siku zisizokuwa na ukomo, miaka milioni moja itapita, bado utaendelea kuishi, miaka trilioni moja itapita bado utaendelea kuishi, na hapo hata bado hujaanza kuishi, utaendelea na kuendelea, kamwe hakuna siku itakayofika na ukasema leo ni ukomo wa mimi kuwa hai, kamwe hutakaa ufe, utakuwa hai hivyo hivyo daima..huo ndio uzima wa milele.

Jambo kama hilo ukilifikiria sana, kuna mahali hata akili yako itafika na kugota, jaribu uone,, kwasababu ni jambo ambalo tangu umezaliwa halijawahi  kuwa sehemu ya maisha yako, tangu ulipokuwa mdogo mpaka unakua umekuwa ukijua kuwa siku moja maisha yako yatakwisha kwa kifo, lakini pale unaposikia kuwa hutakaa ufe tena, akili yako inaweza kushindwa  kulipokea jambo hilo kwa wakati huo.Lakini ukweli ni kwamba hilo litawezekana, lakini sio kwa kila mtu anayeishi leo hii duniani, bali kwa kundi Fulani tu la watu, si watu wote wataishi milele.

Na ndio maana biblia inasema, Karama ya Mungu ni uzima wa milele.

Warumi 6:23 “Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti; bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu”.

Karama ni zawadi, hivyo zawadi kubwa kuliko zote ambayo Mungu anaweza kumpa mwanadamu, si nyingine zaidi ya uzima wa milele. Yaani maisha yasiyokuwa na ukomo..Huoni kama hiyo ni zawadi iliyopitiliza?

Lakini kama hiyo mistari inavyojieleza, Mungu haitoi karama hiyo hivi hivi tu, bali  inasema anaitoa “katika Yesu Kristo Bwana wetu”. Yaani kwa kupitia Yesu Kristo, maana yake ni kuwa usipookolewa na Yesu huwezi kupokea uzima wa milele kwa namna yoyote ile, haijalishi una matendo mema kiasi gani.

Huwezi kuupata uzima huo kwa mwanadamu mwingine yoyote duniani au mbinguni, anayejiita, mtume, au nabii, au kuhani n.k. hakuna mwanadamu yoyote zaidi ya Yesu Kristo peke yake ndiye anayeweza kuachilia karama hiyo ya uzima wa milele ndani ya Mtu.

Na ndio maana yeye mwenyewe alisema.

Yohana 3:36 “Amwaminiye Mwana yuna uzima wa milele; asiyemwamini Mwana hataona uzima, bali ghadhabu ya Mungu inamkalia”.

Hivyo kila mtu anayemwamini na kumpokea, anakuwa tayari na uhakika huo kuwa ndani yake uzima wa milele upo. Hata akifa leo, siku ile ya ufufuo atafufuliwa na kuungana na watakatifu wengine, na kwa pamoja wataishi milele na Mungu mbinguni milele.

Yohana 3:16 “Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele”.

Sasa, mtu anampokeaje Yesu?. Anampokea Yesu kwanza kwa kutubu dhambi zake kwa kumaanisha kuziacha, na baada ya hapo anakua tayari kubatizwa katika ubatizo sahihi, Na kupokea Roho Mtakatifu. Hivyo kama wewe ni mmojawapo wa ambao hawana uzima wa milele ndani yao, na upo tayari leo kumruhusu Yesu ayabadilishe maisha yako.

Basi fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba na maagizo mengine >>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Na ikiwa umefuatisha maagizo hayo kwa dhati na kwa moyo wako wote, basi uwe na uhakika kuwa umeshapokea karama hiyo ya uzima wa milele ndani yako

Kwahiyo endelea kujifunza Neno la Mungu, na tafuta kanisa la kiroho litakalokusaidia kukua kiroho na Bwana atakuwa na wewe sikuzote. Mpaka siku ile ya paraparanda ya mwisho.

Shalom.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618.

Mada Nyinginezo:

USIUZE URITHI WAKO.

Nini maana ya maneno haya ya Bwana? “Nami nikiinuliwa juu ya nchi,NITAWAVUTA WOTE KWANGU”(Yohana12:32).

NAO WALIOKUWA WAMEKUSUDIWA UZIMA WA MILELE WAKAAMINI.

JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?

MADHARA YA KUPUUZIA MAAGIZO YA MSINGI MUNGU ANAYOKUPA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Mkomamanga ni nini? Na katika biblia unawakilisha nini?

Mkomamanga ni nini?


Komamanga ni tunda lenye mbegu ndogo ndogo nyingi ndani yake, ambalo linaliwa kwa kumumunywa mumunywa mbegu zake mpaka utamu wote uishe, au kwa kukamuliwa juisi, ni tunda lenye ladha nzuri sana, na kisayansi linavirutubisho vingi sana mwilini, kama hukuwahi kulifahamu tunda hili tazama picha juu.

Katika biblia tunda hili linawakilisha mfanikio, au uzuri wa aidha taifa, au kitu au mtu.

Kwamfano ukisoma mstari huu;

Kumbukumbu 8:6 “Nawe uzishike amri za Bwana, Mungu wako, upate kwenda katika njia zake, na kumcha.

7 Kwa kuwa Bwana, Mungu wako, yuakuingiza katika nchi nzuri, nchi yenye vijito vya maji, na chemchemi, na visima, vibubujikavyo katika mabonde na milima;

8 nchi ya ngano na shayiri, na mizabibu, na mitini, na mikomamanga; nchi ya mizeituni yenye mafuta, na asali”;

Utaona Mungu akilitaja tunda hili pamoja na mizabibu, na mitini, kuonyesha uzuri wa nchi ya ahadi ambayo Mungu aliwaambia wana wa Israeli wataiingia, kuonyesha ni jinsi gani nchi hiyo itakavyokuwa nzuri na yenye mafanikio makubwa..

Na ndio maana utaona hata sehemu nyingine, walipoasi, Mungu alitumia miti hii hii ya matunda kama mfano kuonyesha, alivyowafunguia milango ya Baraka na mafanikio katika mambo yao maovu, soma.

Hagai 1:18 “Tafakarini, nawaomba; tangu siku hii ya leo na siku zijazo; tangu siku ya ishirini na nne ya mwezi wa kenda, naam, tangu siku hiyo ulipowekwa msingi wa hekalu la Bwana tafakarini haya.

19 Je! Mbegu ingali ghalani? Naam, huo mzabibu, wala mtini, wala mkomamanga, wala mzeituni, haikuzaa kitu; tangu siku hii ya leo nitawabariki”.

Soma tena;

Yoeli 1:12 “Mzabibu umesinyaa, mtini nao umevia; Nao mkomamanga na mtende na mtofaa; Naam, miti yote ya mashamba imekauka; Maana furaha imekauka katika wanadamu”.

Pia tunda hili, linawakilisha mafanikio ya kazi za mtu.

Wimbo 6:11 “Nalishukia bustani ya milozi, Ili kuyatazama machipuko ya bondeni; Nione kama mzabibu umechanua, Kama mikomamanga imetoa maua”.

Wimbo 8:1 Laiti ungekuwa kama ndugu yangu, Aliyeyanyonya matiti ya mamangu! Kama ningekukuta huko nje, Ningekubusu, asinidharau mtu.

2 Ningekuongoza nyumbani mwa mamangu, Naye angenifundisha; Ningekunywesha divai iliyokolea,Divai mpya ya mkomamanga wangu.

Soma pia 1Samweli 14:2,

Hivyo kwa ujumla, tunda hili, limetumika kuwakilisha hali ya mafanikio ya taifa, mtu au kitu.

Lakini pamoja hayo ipo nchi ya mikomamanga halisi, kuliko ile ya Kaanani, ambayo wana wa Israeli waliingia lakini bado waliugua, walikufa, waliteseka n.k. , Nchi hiyo si nyingine  zaidi ya Yerusalemu mpya. Huko hakuna shida, wala njaa, wala magonjwa, wala vifo, wala ajali, wala dhiki, lakini  swali ni je! wewe na mimi tunayo nafasi humo?

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618.

Mada Nyinginezo:

MADHABAHU NI NINI?

JIHADHARI NA UONGO WA SHETANI UNAOKARIBIANA NA UKWELI.

MWEZI WA ABIBU/NISANI NI MWEZI GANI?

FANYIKA SIPORA WA KRISTO, UNYAKUO UPO KARIBU.

Wafilisti ni watu gani.

UNYAKUO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

YAFUATAYO NI MAWAZO YA ADUI HIVYO USIYASIKILIZE.

Adui yetu shetani, usiku na mchana anatafuta kutumeza, kama biblia inavyosema katika..1Petro 5:8 “ Mwe na kiasi na kukesha; kwa kuwa mshitaki wenu Ibilisi, kama simba angurumaye, huzungukazunguka, AKITAFUTA MTU AMMEZE”.

Hivyo anazo njia nyingi za kummeza mtu, na kila siku anabuni njia mpya…Lakini anayo moja maarufu anayoitumia ambayo ni ya MAWAZO.Anachofanya ni kupanda mbegu Fulani mbaya ndani ya mtu, ambayo hiyo mbegu inavyozidi kukuwa ndani yake inamletea kukata tamaa na mwisho kuanguka kabisa. Sasa yafuatayo ni baadhi ya Mawazo ambayo, ukiona yanakuja ndani yako, fahamu kuwa ni mawazo ambayo yamebuniwa na ibilisi, hivyo Yakatae na kuyapuuza.

  1. Mawazo ya kwamba Umemkufuru Roho Mtakatifu, au una dhambi isiyosameheka:

Hii ni silaha moja maarufu ya adui shetani kwa watu wa Mungu. Anayatengeneza mawazo haya ndani ya mtu, na kumfanya aishiwe nguvu ya kuendelea kumtafuta Mungu na kuwa na amani.

Hivyo wazo lolote linalokuja ndani yako kwamba tayari umemkufuru Roho Mtakatifu, kwasababu pengine ulishawahi kusema maneno Fulani wakati Fulani, kuikejeli injili. Au ulifanya dhambi Fulani kubwa sana, ambayo haielezeki, au ulirudi nyuma baada ya wokovu wako, na sasa unataka kutubu uanze upya, Ukiona hilo wazo linakuja ndani yako, kukuambia kuwa ulishamkufuru Roho Mtakatifu, Fahamu kuwa hilo ni wazo la ibilisi asilimia 100, hivyo lipuuzie usilipe nafasi hata kidogo. Hakuna mwanadamu aliyemkufuru Roho Mtakatifu na bado ana hofu ya Mungu..Lakini usipolipuuzia hili wazo na kuendelea kukaa nalo moyoni, litazidi kukua na mwishowe litakufanya usiendelee kumtafuta Mungu, na litakufanya uwe unakosa amani na furaha kila wakati.

  1. Mawazo ya kujiona kama Mungu anakuchukia:

Hii ni silaha nyingine ya shetani, kuharibu watu wa Mungu..Ukiona upo kwenye hili tatizo kwamba unaona kama Mungu anakuchukia, hakupendi anawapenda tu baadhi ya watu Fulani, au watumishi wake..Jua tayari upo katika shambulizi la adui yako shetani, tayari upo katika anga

zake anakuharibu kidogo kidogo. Fahamu kuwa Mungu hamchukii mtu yeyote yule hata yule mwovu kuliko wote, ingekuwa anakuchukia sidhani kama angekuumba uishi katika hii dunia, mpaka umejiona umetokea kwenye hii dunia, jua ni kwaajili ya upendo wake kwako. Hivyo hilo wazo la kujiona hupendwi ni kutoka kwa adui.

  1. Mawazo ya kujiona kwamba Mungu hasikii maombi yako:

Mungu anasikia maombi ya kila mwanadamu..kama kilio cha dhambi tu kinamfikia mbinguni, kwanini maombi yasimfikie?. Yanamfikia isipokuwa majibu ya maombi yanatofautiana mtu na mtu. Wapo ambao watapeleka maombi yao watajibiwa kama walivyoomba na wapo ambao hawatajibiwa, sasa wale ambao hawatajibiwa maombi yao, ipo sababu, na Mungu wa upendo atahakikisha wanaijua hiyo sababu kwa njia yeyote ile, ili warekebishe wapokee majibu ya maombi yao.. Kamwe hawezi kumwacha mtu yeyote hewani tu!, bila kumpa sababu ya kwanini hajapokea majibu ya maombi yake..Kinachowakwamisha wengi ni kukata tamaa

kirahisi…Unapokata tamaa tayari umekatisha safari yako ya kupokea baraka zako ukiwa katikati.

Kwa mfano, mtu anaweza kwenda kumwomba Mungu naomba unipe mume bora, au mke bora..lakini ukimwangalia ni kahaba, hivyo Mungu mwema hawezi kumpa kitu kizuri kabla hajamtengeneza kwanza…Kwahiyo wakati anasubiria majibu ya maombi yake, Mungu anamletea mhubiri, ambaye atamhubiria wokovu, na njia bora ya kuishi Maisha ya kumpendeza Mungu, anapotii na kukubali kubadilika na kuacha njia zake mbaya..Mungu ndipo anamletea jibu la

maombi yake aliyomwomba, analetewa mwenzi mwema wa Maisha, ambaye hatamsumbua na aliye mcha Mungu kama yeye. Lakini kama hatatii bado anataka kuendelea kukaa na ukahaba wake ndio atakaa hivyo hivyo kwa muda mrefu mpaka siku atakapofunguka akili, atarudia kuomba yale yale maneno lakini hataona majibu…

Hizo tu ndizo sababu za Mungu kuchelewesha majibu, lakini si kwamba Mungu hasikii maombi… Anayasikia, isipokuwa katika ujubuji wake ndio suala lingine.

Hivyo ukikosa kujiamini na kufikiri Mungu hajawahi kusikia maombi unayoomba chumbani kwako, au barabarani unapotembea, au kazini unapofanyia kazi…basi jua umeshambuliwa rohoni na adui shetani. Kazana kujua kwanini hujapata majibu lakini usifikiri kwamba hujasikiwa kabisa. Tayari umeshasikiwa, na uliloliomba limeshafanyiwa kazi, wewe fuatilia ombi lako lipo katika hatua gani sasa.

Marko 11:24 “Kwa sababu hiyo nawaambia, Yo yote myaombayo mkisali, aminini ya kwamba mnayapokea, nayo yatakuwa yenu”.

  1. Mawazo ya kufikiri kwamba Siwezi kumpendeza Mungu wala kuwa mtakatifu:

Ndugu ukifikiri kwamba unaweza kufikia kiwango cha utakatifu kiasi kwamba huna kosa kabisa..basi fahamu kuwa hutaweza kamwe kumtumikia Mungu, kumbuka bado tunaishi duniani,

na lazima tutakuwa na kasoro nyingi, ambazo nyingi hatuzijui kama tunakosea…Sasa kama Mungu angezihesabu hizo biblia inasema hakuna mtu angesimama. Baada ya kuokoka ukiamka asubuhi usianze kukaa kuhesabu makosa yako, ukifanya hivyo kamwe hutaweza kumtumikia Mungu, na shetani atakusumbua sana na kila dakika atakuletea mawazo wewe ni mbaya, wewe hustahili, wewe hufai, wewe umeshamkosea Mungu, hufai, hufai n.k

Ukiamka asubuhi anza kuhesabu ni mazuri mangapi umemfanyia Mungu wako, na kama hujafanya kabisa ndipo uhuzunike, na tafuta kufanya, na jioni ukirudi..Mwambie Bwana asante kwa hichi kizuri ulichoniwezesha kukufanyia siku ya leo, na pia naomba nisamehe makosa yangu

yote niliyokukosea wewe pasipo kujua siku ya leo. Na kama unayakumbuka baadhi uliyoyafanya hakikisha kesho unayarekebisha, na ukishatubu tu usianze kujilaumu laumu!..Ukifanya hivyo utaruhusu mashambulizi ya shetani kukuvamia na kukuletea mawazo yale yale kwamba Mungu

alichukizwa na wewe jana, hivyo hawezi kuendelea kutembea na wewe leo…Kwahiyo siku zote Vaa ngao ya Imani, ili uweze kuizima hiyo mishale ya adui. Mungu wetu wa upendo hakai huko mbinguni na karatasi na kalamu akitiki mabaya tunayoyafanya baada ya sisi kuokoka…hafanyi hivyo, yeye yupo kutazama mema yetu, maadamu tumeshaokoka na

kumwamini na tumeweka mbali Maisha ya dhambi. Basi tunakuwa tunahesabiwa haki kwa Neema na si kwa matendo. Na hivyo kidogo kidogo anatutakasa mpaka unafika wakati tunakuwa wakamilifu kabisa kwake.

Hivyo hizo ni silaha 4 za adui yetu shetani. Sasa kama hizi Habari ni mpya kwako, na kama zimekufungua macho, basi ni dalili ya kwamba ulikuwa huna Ngao mkononi mwako, hivyo

ulimfungulia shetani nafasi ya kukushambulia ndio maana husongi mbele kiimani, na hiyo ni kutokana na kwamba pengine nafasi ya kutafuta kumjua Mungu Zaidi katika Maisha yako ni ndogo, au ulikuwa umesongwa na hivyo kulifahamu Neno imekuwa ngumu kwako, kwahiyo nakushauri mtu wa Mungu usiruhusu tena kusongwa..Neno hili wakristo wote waliofanikiwa ambao umeona wamesimama na hawapelekwi ni kwasababu, wana ngao za Imani mikononi

mwao, ni kwasababu Hivyo vipengele 4 hapo juu wamevishinda tangu zamani. Hivyo ni wewe peke yako umebaki.

Anza kumtafuta Mungu kwa bidii, anza kusoma Neno kwa bidii, usipitishe siku bila kushika biblia, na usomapo usisome kwa kutimiza wajibu, Ukilisoma Neno la Mungu na kulielewa ndivyo linavyokaa ndani yako, na linakupa Imani na maarifa, na ndivyo linavyokuweka huru, Ukilikosa hilo kamwe usitegemee kumshinda shetani, na wala kamwe usitegemee kama utaweza kumtumikia Mungu. Kwasababu shetani hawezi kuruhusu umtafute Mungu kirahisi rahisi hivyo, ni lazima akuletee hivyo vita vya kimawazo, akishinda hivyo atakuletea na vya nje, sasa ni wajibu wetu kufahamu kuwa tupo vitani. Ni lazima upambane kumjua Mungu.

Mathayo 11:12 “Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatikana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka”

Bwana akubariki.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618

Mada Nyinginezo:

ESTA: Mlango wa 8, 9 & 10. (SIKU KUU YA PURIMU)

KWANINI LEO HII KUNA KUNDI KUBWA LA WAKRISTO WALIORUDI NYUMA?

NIMEOKOKA, ILA MUNGU NDIYE ANAYEJUA NITAKWENDA WAPI.

FAHAMU JINSI KRISTO ANAVYOPONYA WATU ROHO.

JE NI DHAMBI KUWA NA MAHUSIANO KABLA YA NDOA?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Moyo wake mwenye hekima upo upande wa kuume, maana yake nini?

SWALI: Nini maana ya huu mstari? Mhubiri 10:2 “Moyo wake mwenye hekima upo upande wa kuume; Bali moyo wake mpumbavu upo mkono wa kushoto”.


JIBU: Mstari huo unatuonyesha wazi kuwa kumbe moyo wa mwanadamu unao upande wa kukaa, haupo tu hewani bila una makao, ni aidha ukae upande wa mkono wa kuume, au upande wa mkono wa kushoto. Kumbuka moyo unaozungumziwa hapo sio huu wa nyama, bali ni ule wa rohoni ambao unaeleza tabia ya mtu.

Kama tunavyojua mkono wa kuume ni mkono wa heshima, mkono wa kuonyesha kujali, na usafi, tofauti na mkono wa kushoto, na ndio maana ukikutana na mtu yeyote mahali fulani huwezi kutoa salamu kwa mkono wa kushoto, bali utampa mkono wa kulia kuonyesha heshima, na kujali.

Vivyo hivyo na mioyo yetu, ikiwa haionyeshi Heshima, na usafi na kujali kwa Mungu na kwa wanadamu, rohoni inaonekana ipo upande wa kushoto. Na siku ile ya hukumu Mungu atatuweka upande wa mkono wake wa kushoto. Lakini tukiwa wasafi rohoni, na tunamjali Mungu na watu(hususani ndugu katika imani), siku ile Bwana atatuweka upande wa mkono wake wa kuume ambapo moyo upo.

Vifungu hivi vinaeleza wazi tabia zilizo upande wa mkono wa kuume na ule wa kushoto, Tusome;

Mathayo 25:31 “Hapo atakapokuja Mwana wa Adamu katika utukufu wake, na malaika watakatifu wote pamoja naye, ndipo atakapoketi katika kiti cha utukufu wake;

32 na mataifa yote watakusanyika mbele zake; naye atawabagua kama vile mchungaji abaguavyo kondoo na mbuzi;

33 atawaweka kondoo mkono wake wa kuume, na mbuzi mkono wake wa kushoto.

34 Kisha Mfalme atawaambia wale walioko mkono wake wa kuume, Njoni, mliobarikiwa na Baba yangu, urithini ufalme mliowekewa tayari tangu kuumbwa ulimwengu;

35 kwa maana nalikuwa na njaa, mkanipa chakula; nalikuwa na kiu, mkaninywesha; nalikuwa mgeni, mkanikaribisha;

36 nalikuwa uchi, mkanivika nalikuwa mgonjwa, mkaja kunitazama; nalikuwa kifungoni, mkanijia.

37 Ndipo wenye haki watakapomjibu, wakisema, Bwana, ni lini tulipokuona una njaa, tukakulisha, au una kiu tukakunywesha?

38 Tena ni lini tulipokuona u mgeni, tukakukaribisha, au u uchi, tukakuvika?

39 Ni lini tena tulipokuona u mgonjwa, au kifungoni, tukakujia?

40 Na Mfalme atajibu, akiwaambia, Amin, nawaambia, kadiri mlivyomtendea mmojawapo wa hao ndugu zangu walio wadogo, mlinitendea mimi.

41 Kisha atawaambia na wale walioko mkono wake wa kushoto, Ondokeni kwangu, mliolaaniwa, mwende katika moto wa milele, aliowekewa tayari Ibilisi na malaika zake;

42 kwa maana nalikuwa na njaa, msinipe chakula; nalikuwa na kiu, msininyweshe;

43 nalikuwa mgeni, msinikaribishe; nalikuwa uchi, msinivike; nalikuwa mgonjwa, na kifungoni, msije kunitazama.

44 Ndipo hao pia watajibu, wakisema, Bwana, ni lini tulipokuona wewe una njaa, au una kiu, au u mgeni, au u uchi, au u mgonjwa, au u kifungoni, tusikuhudumie?

45 Naye atawajibu, akisema, Amin, nawaambia, Kadiri msivyomtendea mmojawapo wa hao walio wadogo, hamkunitendea mimi.

46 Na hao watakwenda zao kuingia katika adhabu ya milele; bali wenye haki watakwenda katika uzima wa milele.

Umeona, hivyo Bwana atujalie tuwe na hekima, kuhakikisha kuwa mioyo yetu haipo upande wa kushoto, kwa tabia zilizoorodheshwa hapo juu.

Bwana akubariki.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618.


Mada Nyinginezo:

Shetani ni nani?

TABIA YAKO NI YA MNYAMA GANI?

JE UNAMTHAMINI BWANA?

UFUNUO: Mlango wa 1

YAKINI NA BOAZI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

PALE AHADI ZA MUNGU ZINAPOKUJARIBU.

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe daima, Ni siku nyingine tena Bwana ametupa neema ya kuiona, hivyo nakukaribisha tuzidi kuyatafakari maneno ya uzima maadamu siku ya ukombozi wetu inazidi kukaribia.

Mungu anapotupa Neno la ahadi, huwa haiishii hapo tu, bali kuna majira yanafika, hizo ahadi zinatujaribu, Utamwona Yusufu pindi alipopewa maono ya kuwa utafika wakati baba yake na mama zake na ndugu zake watamwinamia, (yaani kwa ufupi atakuwa mkuu), tendo lile alidhani lingetokea tu papo kwa papo, Lakini kama tunavyojua habari mambo ndio yalikuwa kinyume na matarajio yako, kwanza aliuzwa na ndugu zake, akaenda kuwa mtumwa Misri.

Na alipofika kwenye ile nyumba ya Potifa kama mtumwa walau akaanza kuona unafuu pale alipofanywa kuwa msimamizi wa mali na kazi za bosi wake, pengine akadhani Mungu kashaanza kumkumbuka, lakini mambo yakabadilika tena baada ya kukutana na mke wa Potifa na kumsababishia apelekwe gerezani, akafungwa  huko muda mrefu, tena lile gereza la wafungwa wa wafalme ambao hao hawana mdhamana, wanasubiria siku yoyote tu kuuawa.

Sasa mambo hayo yote Yusufu aliyoyapitia, hayakuletwa na shetani, bali ni Mungu aliyeruhusu ayapitie, zilikuwa ni ahadi za Bwana zikimjaribu kwa wakati ule. Aone kama Je! bado atashikamana na utimilifu wake kabla ya kuzipokea zile ahadi zenyewe?

Zaburi 105:17 “Alimpeleka mtu mbele yao, Yusufu aliuzwa utumwani.

18 Walimwumiza miguu yake kwa pingu, Akatiwa katika minyororo ya chuma.

19 Hata wakati wa kuwadia neno lake, AHADI YA BWANA ILIMJARIBU”.

Jambo kama hilo, tunaliona kwa Ibrahimu pia, Mungu alimuahidia kuwa atamfanya kuwa baba wa mataifa mengi, na uzao wake utakuwa mwingi kama nyota za mbinguni, lakini jambo hilo hakulipata siku hiyo hiyo, hakulipata mwezi huo huo, hakulipata mwaka huo huo..Bali ilipita miaka mingi, zaidi ya 25,akiwa mzee wa miaka karibu 100, ndipo dalili zinaanza kuonekana onekana kwa kumpata Isaka.

Lakini ghafla naye tena dalili hizo zinaenda kuzimwa, pale Mungu anapomwambia, amchukue Isaka akamtoe kafara mbele zake, kwa namna ya kawaida ni rahisi kusema huyu sio Mungu, lakini Ibrahimu alitii kwasababu alijua ni wakati wa Ahadi za Bwana kumjaribu. Akapanda na Isaka kule mlimani,  akijua kabisa tayari hana mtoto, wazo la kuwa Mungu ataghahiri halikupita katika akili yake hata kidogo.

Mwanzo 22:1 “Ikawa baada ya mambo hayo MUNGU ALIMJARIBU IBRAHIMU, akamwambia, Ee Ibrahimu! Naye akasema, Mimi hapa.

2 Akasema, Umchukue mwanao, mwana wako wa pekee, umpendaye, Isaka, ukaende zako mpaka nchi ya Moria, ukamtoe sadaka ya kuteketezwa huko juu ya mlima mmojawapo nitakaokuambia.

3 Ibrahimu akaondoka alfajiri, akatandika punda wake, akachukua vijana wawili pamoja naye, na Isaka mwanawe, akachanja kuni kwa ajili ya hiyo sadaka ya kuteketezwa, akaondoka, akaenda mpaka mahali alipoambiwa na Mungu.”

Umeona, agano la kale ni kivuli cha agano jipya.

Na sisi kama kanisa, Mungu ametupa ahadi zilizo kubwa zaidi ya akina Ibrahimu na Yusufu, tumepewa maono makubwa sana, na maono yenyewe ni kuurithi ufalme wa mbinguni, ahadi za kuketi pamoja na Yesu katika kiti chake cha enzi kule mbinguni, ahadi za kufanywa nguzo, ahadi za kuwa wafalme wa makuhani wa Bwana katika ile Yerusalemu mpya itakayoshuka kutoka mbinguni kwa Baba ambayo njia zake ni za dhahabu,

Unategemea vipi ahadi hizi zisitujaribu?

Zitatujaribu tu wakati mwingine, Mungu anafanya hivyo ili aone je! ni kweli tumemaanisha kwenda mbinguni au la? .Hivyo wewe na mimi tukipitia mazingira ya upingamizi, usifikiri kuwa ahadi ya Mungu ya kuwa mfalme na kuhani imebatilika kwetu…La! Haijabatilika hata kidogo..ipo pale pale.

Kupitia vikwazo vya namna mbalimbali kwa ajili ya imani yako, usitetereke hata kidogo, wala usikufuru, macho yako yasiache kuzitazama ahadi Mungu alizokuwekea mbele kama Ibrahimu na Yusufu. Hata kama hakuna dalili inayoonekana leo, fikiri juu ya uzuri wa mbinguni, Kwasababu moja ya hizi siku, parapanda italia, wafu watafufuliwa, kisha kwa pamoja tutaicha hii dunia kwa mara ya kwanza, tutakwenda mbinguni katika karamu tuliyoandaliwa na Bwana Yesu, tutaisheherekea hiyo kwa kipindi cha kirefu, tutazuru mitaa yote ya mbinguni, tutaona mambo ambayo jicho halijawahi kuona wala sikio kusikia, hapo tukiwa na miili ya utukufu, isiyoumwa, isiyozeeka, isiyougua, kisha tutarudi hapa duniani kutawala na Bwana Yesu kwa kipindi cha miaka 1000 kama wafalme, na baada ya hapo tutaingia katika ile Yerusalemu mpya, ambapo Makao ya Mungu yatakuwa pamoja na sisi wanadamu milele.

Mambo tuliyoandaliwa huko, hayajawahi kuingia katika moyo wa mwanadamu yoyote, biblia inatuambia hivyo. Kwahiyo tusichoke kumngojea Mungu, tusichoke kuzingojea ahadi za Bwana za milele. Utaona pamoja na kwamba Ibrahimu na Yusufu na Ayubu walipitia katika mapito yote yale, lakini mwisho wao ulikuwa ni mzuri, wa kufundisha na wa kuokoa na sio wa kukomoa, Yusufu kuuzwa utumwani ni kwasababu njaa ilikuwa mbele, hivyo alihitajika kwenda Misri kuwaandalia ndugu zake makao, na chakula, Ibrahimu kumtoa kafara mwanawe, ilikuwa ni ujumbe kwa kanisa juu ya dhabihu ya Yesu Kristo. N.k.

Vivyo hivyo na sisi tuliookoka, tusipozimia mioyo ahadi zetu zitatufikia.

Isaya 40:29 “Huwapa nguvu wazimiao, humwongezea nguvu yeye asiyekuwa na uwezo.

30 Hata vijana watazimia na kuchoka, na wanaume vijana wataanguka;

31 bali wao wamngojeao Bwana watapata nguvu mpya; watapanda juu kwa mbawa kama tai; watapiga mbio, wala hawatachoka; watakwenda kwa miguu, wala hawatazimia”.

Maran Atha.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618.


Mada Nyinginezo:

MADHABAHU NI NINI?

JE KUVAA PETE NI DHAMBI?

JISHUSHE ILI MUNGU AKUHUDUMIE.

Ibada ni nini,Na je ili ikamilike inapaswa iwe na nini na nini?

Je! Bwana Yesu alitumwa kwa Waisraeli tu peke yao?

Rudi Nyumbani:

Print this post

JIHADHARI NA UONGO WA SHETANI UNAOKARIBIANA NA UKWELI.

Biblia inasema shetani ni Baba wa uongo Yohana 8:44, Maana yake kazi yake ni kusema uongo, na uongo sio wa kudanganya watumishi wake, hao siku nyingi tayari ni wa kwake…anachokifanya ni kuwafundisha watumishi wake uongo, ili wakadanganye wengine…Ndio maana anaitwa Baba wa uongo.

Na uongo wake unakaribia sana kufanana na ukweli…ili hela bandia iweze kuwadanganya wengi ni lazima ikaribiane sana kufanana na hela halali…kwahiyo jinsi uongo unavyozidi kukaribiana na ukweli ndivyo unavyokuwa na nguvu zaidi..

Kwahiyo shetani anajua kabisa Neno la Mungu ndio KWELI…Kwahiyo ili atengeneze uongo wenye nguvu kubwa ni lazima autengeneze unaokaribiana sana kufanana na Kweli ya Neno la Mungu…maana yake ni kwamba atatumia maandiko/biblia kuupotosha ukweli katika utashi wa hali ya juu kiasi kwamba ni ngumu kugundua kama Neno hilo limepotoshwa…Huo ndio uongo wa shetani unaozungumziwa katika biblia…

Kama unakumbuka wakati anamjaribu Bwana kule jangwani, utaona alikuwa anatumia maandiko yaani neno la Mungu…hakuwa anatumia kitabu cha sayansi au mithali za wahenga…bali alikuwa anatumia Neno la Mungu kwamba imeandikwa hivi au vile…kiasi kwamba kama Bwana asingekuwa mtu wa Rohoni wa kulielewa Neno sana, na kufananisha maandiko vyema angenaswa na mtego wa Ibilisi na angeusikiliza uongo wake.

Na hadi leo mbinu ya shetani ni hiyo hiyo, ya kuligeuza Neno la Mungu la kweli kuwa uongo….

Kama wengi wetu tunavyojua Mungu alimwagiza Musa kutengeneza “Yule nyoka wa shaba” ambaye aliambiwa amnyanyue juu ili kila amtazamaye ambaye kaumwa na nyoka aweze kupona, andiko hilo linapatikana katika kitabu cha Hesabu 21:6-9.

Sasa kupitia andiko hili shetani kawadanganya watu kuwa Ni halali kutengeneza sanamu ya nyoka, au ya mtu Fulani katika biblia, au ya kitu na kuitazama, na kuisujudia au kuiheshimu na hata kuiabudu ili kupata faida Fulani kutoka katika hiyo, labda uponyaji au Baraka.

Sasa tukirudi katika habari hiyo ya nyoka wa shaba..utaona kuwa Mungu hakuwaambia wana wa Israeli waiabudu, wala waiangukie, wala waipe heshima yoyote, wala haikuwekwa pale kama kitu kitakatifu…bali Mungu aliiweka pale kwa lengo la kuwatafakarisha upumbavu wao walioufanya na wanaoufanya wa kumnung’unikia Mungu..na hivyo Mungu akawaonyesha kwamba amewachapa kwa kiboko cha nyoka (Ndio maana utaona ni fimbo iliyozungushiwa nyoka)..Ili watafakari, na kutubia uovu wao…na waliotazama na kutafakari ndio waliopona.

Kama wewe ni msomaji wa biblia utakuja pia kuona kuna wakati wafilisti walilichukua sanduku la Agano kutoka Israeli na Mungu akawapiga kwa majipu mabaya na tauni…ndipo wafilisti wakatengeneza sanamu za majibu na za panya kuzipeleka Israeli kuonyesha kwamba wametambua wamefanya kosa na wametambua kwamba Mungu kawaadhibu kwa majibu na Tauni ambayo inatokana na panya..na hivyo wanatubu..na walipofanya hivyo ndipo Mungu akaacha kuwapiga….kasome 1Samweli 6:1-11.

Sasa wafilisti hawakutengeneza hizo sanamu kwa lengo la kuziabudu, wala kuzipa heshima, wala kuzitumikia…bali kwa lengo la kutubu (kwamba wametafakari makosa yao na kujua mkono wa Mungu umekua juu yetu kama mfano wa hayo majibu)..

Kwahiyo hata wana wa Israeli Mungu aliwaambia waitengeneze sanamu ile ili iwatafakarishe, na ili wamwogope Mungu..kwamba wakimuudhi Mungu wao..anaweza kuwachapa kwa fimbo ya kitu chochote kile, inaweza kuwa fimbo ya nyoka, fimbo ya wanyama wengine wakali, fimbo ya magonjwa au chochote kile, na hivyo wamweshimu na kuzishika amri zake. Na wachache waliotii na kuelewa ujumbe walipona lakini wengine walikufa…na hata baada ya janga hilo kuisha kuna wachache ambao bado walikuwa hawajamwelewa Mungu wakaihifadhi sanamu ile na kuanza kuiabudu na kuifanya ni chombo cha ibada…pasipo kujua kuwa wanamchukiza Mungu kwa kuiabudu ile fimbo ya nyoka wa shaba…Mungu akawa anawaadhibu kwa kuiabudu lakini bado wakawa na shingo ngumu kutoivunja vunja ile fimbo ya nyoka wa shaba. Sanamu ile ilikuja kuendelea kupata umaarufu, hadi kufikia Israeli wengi kuiabudu.

Mpaka siku ilipofika alipotokea mtumishi wa Mungu, Mfalme Hezekia, alipoona Taifa linapotea kwa ibada za sanamu, kwa kuiabudu hiyo sanamu ya nyoka wa shaba…ndipo aliponyanyuka na kwenda kuivunja vunja na kuitowesha kabisa, na Mungu akambariki kwa kufanya hivyo.. Tusome..

2Wafalme 18:1 “Ikawa katika mwaka wa tatu wa Hoshea, mwana wa Ela, mfalme wa Israeli, Hezekia, mwana wa Ahazi, mfalme wa Yuda, alianza kutawala.

2 Alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala; akatawala miaka ishirini na kenda katika Yerusalemu; na jina la mama yake aliitwa Abiya, binti Zekaria.

3 Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana, mfano wa yote aliyoyafanya Daudi, baba yake.

4 Alipaondoa mahali pa juu, akazibomoa nguzo, akaikata hiyo Ashera; AKAIVUNJA VIPANDE VIPANDE ILE NYOKA YA SHABA ALIYOIFANYA MUSA; MAANA HATA SIKU ZILE WANA WA ISRAELI WALIKUWA WAKIIFUKIZIA UVUMBA; NAYE AKAIITA JINA LAKE NEHUSHTANI

5 Alimtumaini Bwana, Mungu wa Israeli; hata baada yake hapakuwa na mfano wake katika wafalme wote wa Yuda, wala katika hao waliomtangulia.

6 Maana alishikamana na Bwana, hakuacha kumfuata, bali alizishika amri zake Bwana alizomwamuru Musa”.

Umeona hapo mstari wa 4 ???…Aliivunja vunja maana yake ni kwamba, halikuwa agizo la Mungu kuiabudu, wala kuitolea uvumba, wala kuipa heshima yoyote ile…ni machukizo makubwa!.
Na sanduku la Agano ni hivyo hivyo, Mungu alitoa maagizo kwa Musa litengenezwe lakini hakuna mahali popote Mungu aliagiza liabudiwe…hata hivyo wana wa Israeli wakati Fulani walipojaribu kuligeuza kuwa ni chombo cha Ibada, liliwaletea laana badala ya Baraka kasome 1Samweli 4:1-11. Hakuna kitu chochote kile kwenye biblia nzima agano la kale wala agano jipya kinachoitwa sanamu ambacho Mungu alitoa maagizo kiabudiwe wala kitukuzwe. Ni uongo wa shetani ambao lengo lake ni kuugeuza ukweli wa Neno la Mungu.

Hivyo ndugu..usidanganywe na uongo wa shetani ambao unakaribia sana kufanana na ukweli..usidanganyike na kuabudu sanamu, usidanganyike na kuisujudia sanamu ya bikira Maria wala ya Petro, wala inayojulikana kama sanamu ya Bwana Yesu, wala usiisujudie misalaba, wala kitu chochote kile…Ni machukizo makubwa…biblia inasema..

Kutoka 20:4 “Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu cho chote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini duniani, wala kilicho majini chini ya dunia.

5 Usivisujudie wala kuvitumikia; kwa kuwa mimi, Bwana, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu; nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao,

6 nami nawarehemu maelfu elfu wanipendao, na kuzishika amri zangu”.

Na pia inasema..

Ufunuo 21:7 “Yeye ashindaye atayarithi haya, nami nitakuwa Mungu wake, naye atakuwa mwanangu.

8 Bali waoga, na wasioamini, na wachukizao, na wauaji, na wazinzi, na wachawi, na hao waabuduo sanamu, na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili”.

Bwana akubariki.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618.


Mada Nyinginezo:

Je! Bwana Yesu alitumwa kwa Waisraeli tu peke yao?

NA ROHO NA BIBI-ARUSI WASEMA, NJOO!

WAKATI WA BWANA KUKUVUSHA, NI LAZIMA ARUHUSU JESHI LA ADUI KUNYANYUKA.

MIJI YA MAKIMBILIO.

NA MTU MMOJA AKAVUTA UPINDE KWA KUBAHATISHA, AKAMPIGA MFALME

Rudi Nyumbani:

Print this post

“Bonde la vilio” ni nini katika biblia?(Zaburi 84:6)

“Bonde la vilio” ni nini katika biblia?(Zaburi 84:6)


Neno hili linaonekana mara moja tu katika biblia, tunalitosoma katika mistari hii;

ZABURI 84:4 “Heri wakaao nyumbani mwako, Wanakuhimidi daima.

5 Heri ambaye nguvu zake zatoka kwako, Na njia ziendazo Sayuni zimo moyoni mwake.

6 WAKIPITA KATI YA BONDE LA VILIO, Hulifanya kuwa chemchemi, Naam, mvua ya vuli hulivika baraka 7 Huendelea toka nguvu hata nguvu, Huonekana Sayuni kila mmoja mbele za Mungu”.

Ukianzia kusoma juu Zaburi yote hiyo ya 84 utaona inazungumzia uheri wa watu wale, wanaopenda kwenda nyumbani kwa Bwana kumtafakari yeye daima,kumuhimidi yeye, kumwabudu yeye, kusikiliza maneno yake, unazungumzia juu ya watu wale wanaopenda wakati kuwa uweponi mwa Mungu, nyumbani mwake kumtafakari yeye,..

Biblia inasema, watu wa namna hiyo hata ikifika wakati wakapita katika bonde la vilio, Mungu ataligeuza bonde hilo kuwa chemchemi ya maji, na  kulinyeshea mvua ya vuli.

Kibiblia yapo mabonde mengi, kama vile lilivyo bonde la uvuli wa mauti, ambalo tafsiri yake ni sehemu ambayo mtu atapita haoni tumaini la kuishi tena, inaweza ikawa ni maadui wanamwinda, au magonjwa yanamsumbua kama vile Kansa,Ukimwi n.k., au kesi za mauaji zinamkabili, au sehemu za hatari sana anazipitia sasa n.k..Hilo ndio bonde la Mauti ambalo Daudi alisema nijapopita hapo, sitaogopa mabaya kwa maana Bwana atakuwa pamoja nami (Zab 23:4).

Vivyo hivyo Bonde la vilio nalo lipo, bonde hili ni bonde la ukame, kiu na njaa, bonde la kutokuwa na kitu, na kupungukiwa kabisa, lakini kwa mtu Yule ambaye amekuwa akipenda kuwepo nyumbani mwa Bwana daima kumuhimidi, kumshukuru, kumsujudu, kumwabudu..Mungu anasema bonde hilo kwake litageuzwa na kuwa chemchemi ya vijito vya maji, na mvua ya vuli italinyeshea.

Wana wa Israeli walipita katika bonde hili walipokuwa jangwani , wakalia sana kwa kukosa maji, lakini Mungu aliwapasulia miamba maji yakatoka kama mto wakanywa wakafurahi.(Kutoka 17:1-7, Hesabu 20:1-8) Vivyo hivyo na mtu Yule ambaye Nyumbani kwa Mungu (Kanisani) na sehemu yeyote ile Mungu ambayo Mungu anakaa ndio mahali pake pa kustarehe. Mungu anasema hata ajapopitia wakati mgumu Mungu atakuwa mvua yake ya vuli.

Na ndio maana mtunzi wa Zaburi akamalizia na kusema..

Zaburi 84:10 “Hakika siku moja katika nyua zako Ni bora kuliko siku elfu. Ningependa kuwa bawabu nyumbani mwa Mungu wangu, Kuliko kukaa katika hema za uovu”.

Bwana atujalie na sisi tuone umuhimu wa kuwepo nyumbani mwake wakati mwingi.

Shalom.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618.

Mada Nyinginezo:

Nini maana ya “Siku moja nyuani mwa Bwana ni bora kuliko miaka elfu”?

FAIDA ZA KUFUNGA NA KUOMBA.

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

ROHO HUTUOMBEA KWA KUUGUA KUSIKOWEZA KUTAMKWA!

JINSI ROHO MTAKATIFU ANAVYOWAFUNULIA WATU MAANDIKO.

BONDE LA KUKATA MANENO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Je! Bwana Yesu alitumwa kwa Waisraeli tu peke yao?

SWALI: Je! Bwana Yesu alitumwa kwa Waisraeli tu peke yao au kwa watu wote wa mataifa..Maana yeye mwenyewe alisema katika Mathayo 10:5, kwamba wasihubiri kwa watu wa Mataifa.


JIBU: Tusome..

Mathayo 10:5 “Hao Thenashara Yesu aliwatuma, akawaagiza, akisema, Katika njia ya Mataifa msiende, wala katika mji wo wote wa Wasamaria msiingie.

6 Afadhali shikeni njia kuwaendea kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli”

Ni kweli Bwana aliwaagiza wanafunzi wake wasiende kuhubiri Injili kwa watu wa mataifa kipindi yupo nao, bali wawaendee kwanza wayahudi (yaani waisraeli). Sasa kwanini awazuie wasiende kuwahubiria watu wa Mataifa?

Jibu ni rahisi: Ni kwasababu wakati wa Mataifa kwenda kuhubiriwa injili ulikuwa bado hujafika. Tunaweza kujifunza katika mfano wa kawaida wa Maisha. Unapotengeneza bidhaa yako mpya na kuipeleka sokoni, huwa huanzi na soko kubwa, badala yake utawaambia wale wasambazaji wako, msiende mbali kwanza, hakikisheni kwanza hapa mtaani kwetu au mkoani kwetu bidhaa zetu zimefika.

Kwa sentensi hiyo, haimaanishi kwamba..bidhaa yako huna mpango wa kuivukisha mipaka siku za mbeleni…

Bali ni umefanya hivyo ni kwasababu unataka kazi imalizike hapa kwanza, ndipo iende pengine…Mahitaji ya hapa yakishajitosheleza kwamba watu wameikubali au wameikataa ndipo utanue na kwenda kuitangaza mahali pengine mbali Zaidi.. hiyo ndiyo hekima na akili.

Ndicho Bwana alichowaambia wanafunzi wake, kwamba kwa wakati ule waanze Injili kwa WaIsraeli kwanza, na ndipo wengine watafuata, wasirukie kwenda pengine, muda wa kwenda huko bado.. Ili tuelewe vizuri zaidi hebu tukisome tena kile kisa maarufu tunachokijua cha yule mwanamke mkananayo ambaye hakuwa Mwisraeli.

Mathayo 15: 22 “Na tazama, mwanamke Mkananayo wa mipaka ile akatokea, akampazia sauti akisema, Unirehemu, Bwana, Mwana wa Daudi; binti yangu amepagawa sana na pepo.

23 Wala yeye hakumjibu neno. Nao wanafunzi wake wakamwendea, wakamwomba, wakisema, Mwache aende zake; kwa maana anapiga kelele nyuma yetu.

24 Akajibu, akasema, SIKUTUMWA ILA KWA KONDOO WALIOPOTEA WA NYUMBA YA ISRAELI. 25 Naye akaja akamsujudia, akisema Bwana, unisaidie”.

Sasa tuishie hapo, na kisha twende tena tukakirudie kisa hiki hiki katika Injili ya Marko, ili tupate kuelewa Zaidi…

Marko 7:24 “Akaondoka huko, akaenda zake hata mipaka ya Tiro na Sidoni. Akaingia katika nyumba, akataka isijulikane na mtu; lakini hakuweza kusitirika.

25 Ila mara mwanamke, ambaye binti yake yuna pepo mchafu, alisikia habari zake, akaja akamwangukia miguuni pake.

26 Na yule mwanamke ni Myunani, kabila yake ni Msirofoinike. Akamwomba amtoe pepo katika binti yake.

27 Akamwambia, WAACHE WATOTO WASHIBE KWANZA; maana si vizuri kukitwaa chakula cha watoto, na kuwatupia mbwa.

28 Naye akajibu, akamwambia, Naam, Bwana, lakini hata mbwa walio chini ya meza hula makombo ya Watoto”.

Ukiusoma hapo kwa makini huo mstari wa 27?…utaona Bwana Yesu anamwambia huyo Mwanamke ambaye sio mwisraeli, anamwambia waache Watoto washibe KWANZA… Sasa kama wewe unaelewa Kiswahili vizuri, utakuwa pia unaelewa nini maana ya neno “KWANZA”… Neno kwanza maana yake, kinaanza hichi, halafu ndipo kifuate kingine.

Ndicho Bwana alichomaanisha hapo, kwamba waache Waisraeli wale KWANZA(yaani wapokee baraka hizi za rohoni kwanza), ndipo nyie watu wa mataifa mtafuata baadaye..Ndio maana mwishoni kabisa

mwa Injili yake, siku ile baada ya kufufuka kwake, aliwapa wanafunzi wake ruhusa sasa ya kwenda kote ulimwinguni kuhubiri injili, kwasababu wakati wa mataifa umeshafika…

Luka 24:46 “Akawaambia, Ndivyo ilivyoandikwa, kwamba Kristo atateswa na kufufuka siku ya tatu;

47 na kwamba MATAIFA YOTE watahubiriwa kwa jina lake habari ya toba na ondoleo la dhambi, KUANZA TANGU YERUSALEMU.

48 Nanyi ndinyi mashahidi wa mambo haya.

49 Na tazama, nawaletea juu yenu ahadi ya Baba yangu; lakini kaeni humu mjini, hata mvikwe uwezo utokao juu”

Mstari huo wa 47, umehitimisha jibu la swali letu.. Kwahiyo Injili ni kwa watu wote na mataifa yote, Ilianzia Yerusalemu (yaani kwa waisraeli)..na sasa inahubiriwa kwenye mataifa yote..na imeshafika kila Taifa duniani, mpaka mataifa ambayo ni ngumu kufikiwa, lakini imeshapenya…anasubiriwa tu yule kondoo wa Mwisho kuingia ndani ya Neema, ule mwisho ufike, kama alivyosema..Marko 13: 10 “Na sharti Injili ihubiriwe kwanza katika mataifa yote” na Mathayo 24:14 “Tena habari njema ya ufalme itahubiriwa katika ulimwengu wote, kuwa ushuhuda kwa mataifa yote; hapo ndipo ule mwisho utakapokuja”

Je umetubu dhambi zako na kumpokea Kristo?..Kama bado unasubiri nini..Ni wapi leo injili haihubiriwi?..unadhani tunaishi nyakati gani hizi?…Dunia inaisha na Zaidi ya yote ibilisi anafanya kazi kwa nguvu sana nyakati hizi za mwisho, kuwapotosha watu, na kuwaaminisha kwamba hakuna Mungu , wala mwisho wa dunia, Mkabidhi leo Kristo Maisha yako kama hujafanya hivyo bado, na ukabatizwe na kupokea Roho Mtakatifu, ili upate kuokoka.

Bwana akubariki.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312 / 0693036618.

Mada Nyinginezo:

JINA LAKE KWA KIEBRANIA NI ABADONI, NA KWA KIYUNANI NI APOLIONI.

Tofauti kati ya Myunani, Farisayo na Sadukayo ni ipi?

JIEPUSHE NA UNAJISI.

Rudi Nyumbani:

Print this post