Category Archive Home

KILA KIUNGO LAZIMA KISHUGHULIKE.

Kanisa la Kristo limefananishwa na mwili wa binadamu. Kama vile mwili ulivyo na viungo mbalimbali, mfano mikono, miguu, macho, masikio, mdomo n.k. vikiongozwa na kitu kimoja cha muhimu kiitwacho kichwa. Vivyo hivyo na kanisa la Kristo. Biblia inasema sisi tu viungo mbalimbali na kichwa chetu ni Kristo.

Sasa kama vile katika mwili tunajua hakuna kiungo hata kimoja kisichokuwa na shughuli yoyote vivyo hivyo sisi kama viungo hakuna hata mmoja anayesema ameokoka akawa hana shughuli yoyote ya  kufanya katika mwili wa Kristo. Tena sifa nyingine ya viungo ni  kwamba vyote huwa vina vinashirikiana kwa umoja usiokuwa wa kawaida.

Waefeso 4:16 “Katika yeye mwili wote ukiungamanishwa na kushikanishwa kwa msaada wa kila kiungo, kwa kadiri ya utendaji wa kila sehemu moja moja, huukuza mwili upate kujijenga wenyewe katika upendo”.

Umeona huwezi kusema umeokoka, miezi inapita, miaka inapita, hakionekani chochote unachokichangia katika mwili wa Kristo,..Ukiona hivyo basi ujue ulishakufa kutoka katika mwili wa Kristo, na hivyo ulishakatwa na kutupwa nje siku nyingi. Hutambuliki, ukijiona ni wa kuhubiriwa tu daima, lakini wewe hakionekani chochote unachomfanyia Kristo,ni lazima ujitathimini tena mara mbili wokovu wako.

Tabia ya viungo vilivyo hai vya Kristo ni hizi.

1.Kwanza kiungo kinakuwa kinalihudumia kanisa la Kristo kwa mali zake: Ni jukumu la kila mkristo kumtolea Mungu ili kazi ya injili izidi kuenda mbele, na hii sio tu kwamba inawahusu wanaopelekewa injili tu, bali pia kwa Yule anayeipeleka injili, yeye pia anao wajibu wa kumtolea Mungu, sehemu ya alivyo navyo kwa kadiri alivyokirimiwa neema.. Kwasababu jukumu hilo ni la kila kiungo.

2. Pili ni wajibu wa kila kiungo kuliombea kanisa: Maombi ni sehemu ya maisha ya mkristo yoyote, ni lazima aliombe kanisa lote la Mungu kwa ujumla duniani kote, Si rahisi kukutana viungo vyote kwa wakati mmoja, lakini maombi yanawakutanisha katika roho..Hata viungo katika mwili si vyote vinavyokutana, lakini vinajuana, na kusaidiana kwa kuchukuliana udhaifu, vivyo hivyo na sisi, kuliombea kanisa la Kristo ni wajibu wetu kila siku kama wakristo. Macho hayawezi kujiosha yenyewe ni lazima mikono iisaidie, na kadhalika hata mkono mmoja unauhitaji mkono mwingine..

3. Tatu; Kiungo ni lazima kifanye kazi ya kupeleka habari njema kwa wengine: Jukumu ambalo tulipewa wote na Bwana wetu ambaye ni Kichwa, ni kwamba tuenende ulimwenguni mwote, tukawafanye mataifa kuwa wanafunzi (Mathayo 28:19).. Hivyo kila mmoja wetu kwa jinsi alivyopewa karama, anayowajibu wa kuifanya kazi ya kuwahubiria wengine kwa jinsi awezavyo. Ikiwa ni muhubiri, unawajibu wa kuhubiri kwa bidii, ikiwa ni mwinjilisti, mwalimu, mtume, nabii, mwimbaji, mwandishi, n.k. Unafanya vyote kwa bidii, na katika Roho na kweli..Na hiyo inathibitisha kuwa wewe ni kiungo kilicho hai.

Hizo ni ndizo dalili zinazothibitisha uhai wa viungo vya Kristo.  Lakini ni kwanini watu wengi wanaosema ni wakristo wamekosa vigezo hivyo  vitatu kwa pamoja?

Ni kwasababu hawataki kukaa ndani ya Kristo kumtii yeye, ambaye ndiye anayewajalia watu uhai huo. Ndugu usipokitii kichwa, kamwe huwezi kufanya lolote mwilini. Bwana Yesu mwenyewe alisema.

Yohana 15:4 “Kaeni ndani yangu, nami ndani yenu. Kama vile tawi lisivyoweza kuzaa peke yake, lisipokaa ndani ya mzabibu; kadhalika nanyi, msipokaa ndani yangu.

15 Mimi ni mzabibu; ninyi ni matawi, akaaye ndani yangu nami ndani yake, huyo huzaa sana; maana pasipo mimi ninyi hamwezi kufanya neno lo lote.

6 Mtu asipokaa ndani yangu, hutupwa nje kama tawi na kunyauka; watu huyakusanya na kuyatupa motoni yakateketea”.

Umeona,..Ukiwa hutakubali kumaanisha kuyasalimisha maisha yako moja kwa moja kwa Kristo, yaani kukataa maisha ya mguu mmoja ndani mwingine nje, kamwe hutaweza kuwa kiungo hai, hata iweje. Wewe utakuwa ni sawa na tawi lililokatwa linangojea tu kutupwa motoni. Na pia kumbuka huwezi kuwa na karama zote, hata viungo vya mwili vinatufundisha, lakini utakuwa na karama yako ya kipekee ambayo itakuwa ya muhimu katika kanisa la Kristo.

Huu ni wakati wa wewe, kufanyika kiungo hai Kristo..Ikiwa upo tayari kufanya hivyo, basi tubu makosa yako, mrudie Kristo, nenda kabatizwe kama ulikuwa hujabatizwa ipasavyo hapo kabla, kwa ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji tele sawasawa na (Yohana 3:23 na Matendo 2;38). Kisha kuanzia huo wakati anza kuishi maisha yanayouhakisi wokovu.

Na kuanzia huo wakati  wewe mwenyewe utaona tu, Kristo anavyoanza kukutumia kwa ile karama atakayoishusha ndani yako..Na wewe pia utakuwa kiungo chenye kazi yake maalimu ndani ya mwili wa Kristo. Siku ile ya mwisho kikisubiriwa kupewa heshima yake ya kipekee.

Bwana akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

KIFO CHA MTAKATIFU POLIKAPI (Policarp).

JE KUHUDUMU KWA NYIMBO ZA INJILI KUKOJE?

MIILI YA UTUKUFU ITAKUWAJE?

Maana ya ‘Usimjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake’

NIMEOKOKA, ILA MUNGU NDIYE ANAYEJUA NITAKWENDA WAPI.

Uasherati wa Kiroho maana yake nini?

Rudi Nyumbani:

Print this post

NA YEYE ALIYEKETI JUU YA WINGU AKAUTUPA MUNDU WAKE JUU YA NCHI, NCHI IKAVUNWA.

Jina la Bwana Yesu libarikiwe. Karibu tujifunze maneno ya uzima.

Biblia inasema..

Ufunuo 14:14 “Kisha nikaona, na tazama, wingu jeupe, na juu ya wingu hilo ameketi mmoja, mfano wa Mwanadamu, mwenye taji ya dhahabu juu ya kichwa chake, na katika mkono wake mundu mkali.

15 Na malaika mwingine akatoka katika hekalu, akimlilia kwa sauti kuu yeye aliyekuwa ameketi juu ya lile wingu, Tia mundu wako, ukavune; kwa kuwa saa ya kuvuna imekuja; kwa kuwa mavuno ya nchi yamekomaa.

16 Na yeye aliyeketi juu ya wingu akautupa mundu wake juu ya nchi, nchi ikavunwa”.

Ndugu saa ya mavuno, ipo karibu sana..tena Sanaa.. Utauliza tunajuaje kuwa ipo karibu? Tunajua kutokana na jinsi tunavyoona magugu na ngano yanavyojitenga kwa kasi katika kanisa la Mungu, na katika dunia kwa ujumla. Baadhi ambao walikuwa wanasema huyo Yesu mbona hahukumu dunia, nataka niwaambie wapo kwenye uwezekano mkubwa sana wa kukumbana na hukumu hiyo wakiwa bado hai, kama hawatageuka..

Hawajui kuwa Siri ya Mungu ya kutowahukumu waovu tangu zamani, imejificha ndani ya ule mfano wa magugu na ngano ambao Bwana Yesu aliutoa kwa makutano, embu tusome kidogo..

Mathayo 13:24 “Akawatolea mfano mwingine, akisema, Ufalme wa mbinguni umefanana na mtu aliyepanda mbegu njema katika konde lake;

25 lakini watu walipolala, akaja adui yake akapanda magugu katikati ya ngano, akaenda zake.

26 Baadaye majani ya ngano yalipomea na kuzaa, yakaonekana na magugu.

27 Watumwa wa mwenye nyumba wakaenda wakamwambia, Bwana, hukupanda mbegu njema katika konde lako? Limepata wapi basi magugu?

28 Akawaambia, Adui ndiye aliyetenda hivi. Watumwa wakamwambia, Basi, wataka twende tukayakusanye?

29 Akasema, La; msije mkakusanya magugu, na kuzing’oa ngano pamoja nayo.

30 Viacheni vyote vikue hata wakati wa mavuno; na wakati wa mavuno nitawaambia wavunao, Yakusanyeni kwanza magugu, myafunge matita matita mkayachome; bali ngano ikusanyeni ghalani mwangu.

Na tafsiri yake ilikuwa ni hii..

37 Akajibu, akasema, Azipandaye zile mbegu njema ni Mwana wa Adamu;

38 lile konde ni ulimwengu; zile mbegu njema ni wana wa ufalme; na yale magugu ni wana wa yule mwovu;

39 yule adui aliyeyapanda ni Ibilisi; mavuno ni mwisho wa dunia; na wale wavunao ni malaika.

40 Basi, kama vile magugu yakusanywavyo na kuchomwa motoni; ndivyo itakavyokuwa katika mwisho wa dunia.

41 Mwana wa Adamu atawatuma malaika zake, nao watakusanya kutoka katika ufalme wake machukizo yote, na hao watendao maasi,

42 na kuwatupa katika tanuru ya moto, ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.

Hakuyang’oa magugu, kwasababu magugu yakiwa machanga ni ngumu kuyatambua, yanafanana sana na ngano.

Vivyo hivyo Zamani ilikuwa ni ngumu sana kuwatambua watu ambao ni mashoga katika kanisa la Kristo, Lakini leo hii tunawaona tena wana vyama vyao na viongozi wao katika hayo wanayoyaita makanisa yao. Zamani, ilikuwa ngumu kuona mtu anayejiita mkristo halafu ni mzinzi, lakini leo hii utawaona tena kwa mavazi yao ya kikahaba , utaona waasherati wazi wazi katika nyumba ya Mungu, na wengine wanajiita wachungaji na manabii…Wahuni ilikuwa ni ngumu kuwajua ndani ya kanisa, lakini leo utawaona wazi wazi..n.k

Mambo hayo kama ukifuatilia historia utaona Kuanzia karne ya 19 kushuka chini, hayakuwepo kabisa,..Vilevile dunia nzima ilikuwa inaamini walau kuna kitu kinachoitwa Mungu..Lakini leo hii, utaona wimbi kubwa la watu ulimwenguni lisiloamini Mungu kabisa..Hiyo ni ishara kuwa ngano na magugu tayari yameshajitenga, na kukomaa..Ulikuwa huwezi kuona mkristo anajihusisha na miziki ya kidunia, lakini leo hii utawaona kwa staili za uimbaji wao..

Utajiuliza ujasiri wote huo wameutolea wapi?.. Sio ujasiri, bali ni magugu yamekomaa sasa, yanajitofautisha na ngano halisi za Mungu. Haziwezi kuishi Maisha matakatifu kwasababu zenyewe hazikuwa ngano tangu awali, mwanzoni zilijifanya tu kama wakristo ili zipate hifadhi ya mvua ya neema, lakini sasa zimeshakua hazihitaji tena kujificha..

Na hiyo ndio inayokwenda kupelekea wavunaji (malaika) wa Bwana, waje kuuvuna ulimwengu huu wakati sio mwingi.

Wawafunge matita matita, kabla ya kwenda kuwateketeza kwenye lile ziwa la moto. Na hiyo inakuja pale mtu anapohubiriwa njia ya kweli lakini anashupaza shingo yake, wale malaika wanachofanya ni kumtia muhuri, ambayo ndio Kamba yenyewe. Sasa Hilo likishakutokea basi mtu huyo ni ngumu kumgeukia Mungu, ataendelea kuwa hivyo hivyo mkaidi, mpaka mwisho…

anachosubiria ni hukumu tu ya mwisho. (Na hiyo ni kulingana na maandiko na sio kumhukumu Mtu). Wokovu hauna uvuguvugu..

Hichi si kipindi tena cha kuishi Maisha ya kutokujali, si wakati wa kufurahia maovu kanisani, si wakati wa kuiga kila staili ya Maisha inayozuka ulimwenguni, si wakati wa kupokea kila aina ya elimu za uongo zinazohubiriwa na manabii wa uongo, Huu si wakati wa kushikilia dini, Bali Ni wakati wa kuujenga uhusiano wako wewe na Mungu. Kabla ya nyakati za hatari hazijafika..

Kumbuka..Yule malaika alimbiwa..

Tia mundu wako, ukavune; kwa kuwa saa ya kuvuna imekuja; kwa kuwa mavuno ya nchi yamekomaa.

Kipindi chenyewe ndio hichi.. Je! Unasubiria uwekwe kwenye kundi la magugu? Kama sivyo basi yasalimishe Maisha yako kwa Kristo na yeye atakuponya. Kimbilia msalabani upate wokovu wa kweli, ambao sasa unapatikana bure, utafika wakati hautapatikana kabisa.

Ubarikiwe.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

Je! ni sahihi kwa Mkristo kusherekea siku yake ya kuzaliwa.[Birth day]?

KWANINI UBATIZO NI WA MUHIMU.

KWARESMA IPO KIMAANDIKO?

KUTUBU SIO KUOMBA REHEMA.

Biblia inamaana gani kusema;aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi?

MUUNGANIKO WA MADHEHEBU NI MPANGO WA MPINGA-KRISTO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

 Je kualikwa kwenye sherehe za watu ambao si wakristo ni dhambi?

SWALI: Je ni sahihi kualikwa kwenye karamu za watu wasio wakristo (mfano waislamu kwenye sikukuu zao za eid au futari) na kula nao ni dhambi?


JIBU: Swali hili jibu lake lipo katika kitabu cha 1Wakorintho 8, Mtume Paulo kwa uweza wa Roho alifafanua jambo hili, akasema chakula hakituhudhurishi mbele za Mungu (Maana yake hakitusogezi mbele za Mungu)..tukila hatuonekani watakatifu mbele za Mungu na wala tusipokula hatujipunguzii kitu kutoka kwa Mungu…(1Wakorintho 8:8).

Tunajua Mungu ni mmoja na ndiye aliyeumba vitu vyote, Naye ni Yehova, sababu hiyo basi hakuna mchele wowote ulioumbwa na shetani, wala muhogo ulioumbwa na mungu fulani mwenye jina fulani aliyeko Asia, wala hakuna pilipili iliyoumbwa na mungu fulani aliyopo mashariki ya kati tofauti na Yehova, n.k. vyote hivyo vinatoka kwake.

Hiyo ikiwa na maana kwamba chakula chochote kilichopikwa kwa mimea au viungo vyovyote vinavyopatikana katika dunia tunayoiishi vimetengenezwa na Mungu mmoja na ni halali kuliwa. Ukipita njiani na kukuta mpera na una njaa usiogope kula! Hakuna chochote kitakachokupata, ukitumiwa zawadi ya chakula fulani na baada ya kumshukuru Mungu kile kwa Imani, utakuwa hujafanya kosa lolote mbele za Mungu.

Ukifika mahali umekaribishwa chakula usianze kuuliza uliza kimetoka wapi, au kimepitia wapi au kimetengenezwa na nini…wewe baada ya kumshukuru Mungu kula!, lakini wenyewe wakikwambia chakula hichi ni wakfu kwaajili ya miungu yetu hapo usile kwasababu ukila utawafanya na wao waamini kwamba miungu yao ipo sawa…na kama kuna mkristo aliyemchanga kiroho karibu yako akikuona umekula chakula hicho atashawishika kuamini kwamba ni sahihi kuabudu hiyo miungu na hivyo utamsababisha aanguke kitu ambacho hakimpendezi Mungu mtu yoyote apotee..Kwahiyo kwaajili ya dhamira za hao watu ili wasitie muhuri ibada hizo, hapo tu ndio biblia imetukataza tusile…

Na kuna tofauti ya “chakula cha sherehe” na “chakula cha sadaka”…Chakula kinachopikwa kwenye sherehe ya mtu asiyeamini sio chakula kinachotolewa sadaka, hata Bwana alialikwa mara nyingi na watu wenye dhambi na wasioamini na alikula …chakula kinachotolewa sadaka ni kwa mfano unakuta labda kuna msiba umetokea, na wahusika wananjinja kuku fulani maalumu wa kimatambiko na damu yake imemwagwa sehemu fulani na nyama ya yule kuku inapaswa iliwe na watu fulani maalumu..sasa nyama ya yule kuku aliyefanyiwa matambiko ndio mfano wa chakula kilichotolewa sadaka kwa sanamu, hicho ndio tunapaswa kuwa nacho makini…Lakini pilau iliyopikwa au chakula kingine chochote kilichopikwa kwenye huo msiba kisichohusisha matambiko sio chakula kilichotolewa sadaka kwa sanamu….Na sherehe ni hivyo hivyo.

1Wakorintho 10:25 “Kila kitu kiuzwacho sokoni kuleni, bila kuuliza-uliza, kwa ajili ya dhamiri; 26 maana, Dunia ni mali ya Bwana na vyote viijazavyo.

27 Na mtu asiyeamini akiwaalika, nanyi mnataka kwenda, kuleni kila kitu kiwekwacho mbele yenu bila kuuliza-uliza, kwa ajili ya dhamiri.

28 Lakini mtu akiwaambia, Kitu hiki kimetolewa kiwe sadaka, msile, kwa ajili yake yeye aliyeonyesha, na kwa ajili ya dhamiri.

29 Nasema, dhamiri, lakini si yako, bali ya yule mwingine. Maana kwa nini uhuru wangu uhukumiwe na dhamiri ya mtu mwingine?

30 Ikiwa mimi natumia sehemu yangu kwa shukrani, kwa nini nitukanwe, kwa ajili ya kitu nikishukuriacho?

31 Basi, mlapo, au mnywapo, au mtendapo neno lo lote, fanyeni yote kwa utukufu wa Mungu.

32 Msiwakoseshe Wayahudi wala Wayunani wala kanisa la Mungu,

33 vile vile kama mimi niwapendezavyo watu wote katika mambo yote, nisitake faida yangu mwenyewe, ila faida yao walio wengi, wapate kuokolewa.”

Kwahiyo ikiwa ni ndugu yako au jirani yako (labda ni muislamu au mhindu ), na amekualika kwake au kwenye sherehe yao na amekuandalia chakula kwajinsi anavyojua yeye…kula bila kuhojihoji hufanyi dhambi kwa Mungu….isipokuwa tu amekupa chakula kilichotolewa sadaka na amekueleza

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

Chapa zake Yesu ni zipi hizo?

 

SAKRAMENTI NI NINI, NA JE! IPO KATIKA MAANDIKO?

Kwanini Bwana aliongea na Abramu baada ya kutengeana na Lutu?

MUUNGANIKO WA MADHEHEBU NI MPANGO WA MPINGA-KRISTO.

https://wingulamashahidi.org/2018/06/27/maswali-na-majibu/

Je! Ni halali kuoa/kuolewa na mtu ambaye tayari anao watoto?

Zile mbao mbili za mawe Musa alizoambiwa achonge zilikuwaje?

Biblia inamaanisha nini inaposema “Tusitweze unabii”?

RABI, UNAKAA WAPI?

Rudi Nyumbani:

Print this post

UUMBAJI BORA WA MUNGU, UPO NDANI YA MWANADAMU.

Habari ya uumbaji ina mafunzo mengi sana. Biblia inatuambia Mungu alimuumba mwanamume na mwanamke kwa mfano wake(Mwanzo 1:27). Lakini katika siku sita za uumbaji, Tunaona kulikuwa na uumbaji mmoja muhimu ulikosekana., Embu tengeneza picha mpaka Mungu anastarehe siku ya saba, mwanamke hakuwepo,..Ni kama vile Mungu alijifanya amemsahau hivi..Lakini kulikuwa na sababu kubwa mno ya yeye kufanya hivyo.

Alimwacha Adamu awepo peke yake duniani kwa kipindi fulani kirefu, aone uumbaji wake wote, aushangae huo, aseme ama kweli Mungu ameumba..kila kitu kweli ni kizuri, tazama jua, tazama, nyota, tazama twiga, tazama nyangumi, tazama hiki tazama kile, vyote ni vikamilifu, vimejitosheleza kweli kweli, sihitaji kingine…

Lakini hakujua kuwa Mungu alikuwa hajaukamilisha uumbaji wake bado (hiyo siri alikuwa nayo mwenyewe), ameihifadhi mpaka wakati mtimilifu utakapofika.

Sasa baada ya Mungu kumuacha Adamu kwa kipindi chote hicho kirefu, pengine miezi, miaka inapita aendelee kufikiria hivyo hivyo kuwa kila kitu ndio tayari, mpango wote umekamilika, Mungu kamaliza uumbaji wake, , shughuli zinaendelea kama kawaida bustanini.. Lakini wakati ulipofika wa Mungu kuikamilisha kazi yake alishuka bustanini tena kama muumbaji yule yule wa zamani..

Tungeweza kudhani labda angeshuka ardhini amtoe mwanadamu mwingine kwenye udongo mwekundu, lakini mambo yalikuwa ni tofuati, alimkabili Adamu moja kwa moja..Na mara moja Akamletea usingizi mzito sana. Wakati Adamu akiwa ndotoni, mkono wa Mungu ulianza kupita sehemu ya ubavu wake, pengine mfano wa kisu kikali(hatujui), tunachojua ni kuwa aliundoa ubavu wake mmoja, jaribu kutengeneza picha operasheni iliyokuwa inafanyika pale ni ya namna gani..Si ajabu hata Mungu alimletea usingizi mzito..

Hatushangai hata madaktari wa leo wameiga mbinu hiyo ya Mungu ya kufanya operasheni, yaani kumpiga kwanza mtu nusu-kaputi ili apotelee usingizini kabla ya kumfanyia matibabu makubwa..Wanafanya hivyo Si kwamba hawapendi mtu aone operasheni ile hapana, kwanza ni ili kuepuka usumbufu, chukulia mfano ikiwa mtu yule ataona tumbo linakatwa na utumbo unatolewa nje au anaona kichwa chake kinapasuliwa, anaweza asikubali, au akaogopa kupitiliza na mwisho wa siku akasababisha operesheni isiende vizuri au hata kifo kabisa..Na ndivyo ilivyokuwa kwa Mungu..Alikuwa anamfanyia Adamu operasheni yenye umakini sana, ya kuumba kitu bora kuliko vyote alivyovifanya ndani ya siku zile 6.. Hivyo ikamgharimu atafute njia itakayomfanya awe na utulivu, na ndio akatumia njia ya usingizi mzito, kwasababu kinachokwenda kuumbwa ni bora sana.

Sasa Mungu alipomaliza kuutoa ubavu wake mmoja, akarudishia nyama eneo lile, ndipo akauchukua ule ubavu akamuumbia Hawa. Na kazi ilipomalizika, bwana Adamu akazinduka usingizini, kujitazama anajiona kama vile mwili umepungua, na kuangalia pembeni anamwona mgeni, ambaye si wa pale bustanini. Na kumtazama vizuri anaona hafanani na swala, hafanani ni mbuzi bali anafanana na yeye, anazungumza kama yeye, anaumbile linalokaribia kufanana na la kwake.. Hapo ndipo alipogundua kuwa ni ile sehemu ya mwili wake ameumbwa yule mtu.

Na Adamu alipomwangalia tena hakuona wa kulinganishwa naye katikati ya uumbaji wote ambao Mungu alishawahi kufanya.

Sasa Ni jambo gani Mungu alikuwa anamwonyesha Adamu?

Alikuwa anamwonyesha kuwa uumbaji wake bora unatoka ndani ya mtu, na si penginepo.. Hakuna mwanaume asiyejua katika uumbaji wote wa Mungu hakuna hata kimoja kinachoweza kufananishwa na mwanamke.

Vivyo hivyo somo hilo Mungu hakumfundisha Adamu tu peke yake,..Bali na Hawa pia, pale alipomwekea uwezo wa kubeba mimba, ambapo aliruhusu kiumbe kikae ndani ya tumbo lake kwa miezi 9, lakini baada ya ya hapo, ghafla anatokea tena mwanamume..

Na vivyo hivyo hakuna mwanamke asiyejua kuwa katika uumbaji wote wa Mungu, hakuna kilichoumbwa bora kama mwanamume…Lakini mwanamume huyo anatoka katika tumbo lake na sio mbinguni au ardhini tena. Na kwa kupitia mzunguko huo huo duni leo imejaa watu.

Mambo hayo hayo yanaendelea rohoni hata sasa, Uumbaji mkamilifu wa Mungu unatimia ndani ya Maisha ya wanadamu..ikiwa tu tutamruhusu aifanye kazi yake mwenyewe ndani yetu bila kusumbuliwa..Mungu anataka kufanya makubwa kupitia sisi, kuliko angefanya yeye mwenyewe. Lakini ni sisi hatuwi watulivu kufanyiwa operasheni.

Tunashindana na Mungu, kwa mambo mengi maovu,anapotuambia tuache Maisha ya dhambi, hatuwi tayari kufanya hivyo, tunapoambiwa tusivae nguo zisizompa Mungu utukufu hatuwi tayari, tunapoambiwa tuombe, hatutaki, tunapoambiwa tuikimbie zinaa sisi tunairidhia, biblia inapotuonya tuache hiki au kile hatutaki kutii, tunachosema ni Mungu haangalii mwili anaangalia mavazi, tunapoambiwa tujitenge na mambo ya ulimwengu, tunamwona kama anatunyima uhuru wetu, kila siku tunashindana na mkono wake.. na wakati huo huo tunataka Mungu aumbe mambo makubwa maishani mwetu..Ataumbaje katika hali hiyo ya masumbufu?

Mungu anahitaji utulivu wa roho, tukiukosa huo tusitazamie uumbaji wowote. Tusitazamie Mungu kufanya miujiza maishani mwetu. Ikiwa wewe ni mwenye dhambi, huu ni wakati wako sasa wa kumrudia Mungu, Anza kujenga uhusiano wako vizuri na Mungu, ndipo Mungu naye achukue nafasi ya kuumba mambo mazuri ndani yako.

Tubu dhambi kwa kumaanisha kuziacha, na pia nenda kabatizwe kulingana na matendo 2:38, na Bwana atakupa kipawa cha Roho wake mtakatifu atakayekuongoza na kukutia katika kweli yote na kukupa utulivu wa roho.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

JE! MTUMISHI KUTOKUWA NA FEDHA NI ISHARA KUWA KUNA TATIZO KATIKA IMANI YAKE?

JE KUPONYWA NI UTHIBITISHO WA MUNGU KUWA NA WEWE?

 

MJUMBE WA AGANO.

Je! Ule mwiba uliokuwa katika mwili wa Paulo ulikuwa ni nini?

MAHALI UNAPOPASWA USIMVUMILIE SHETANI HATA KIDOGO.

KUWA WEWE.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Je! Mwanamke anapaswa afunikwe kichwa anapokuwa ibadani?

Jibu la swali hili linahitaji unakini mkubwa kwasababu lisipoeleweka vizuri ni rahisi kusema biblia ina ubaguzi wa kijinsia au biblia haimaanishi hivyo inavyomaanisha.

Hebu tusome mistari michache ifuatayo..

1Wakorintho 11:3 “Lakini nataka mjue ya kuwa kichwa cha kila mwanamume ni Kristo, na kichwa cha mwanamke ni mwanamume, na kichwa cha Kristo ni Mungu.

4 Kila mwanamume, asalipo, au anapohutubu, naye amefunikwa kichwa, yuaaibisha kichwa chake.

5 Bali kila mwanamke asalipo, au anapohutubu, bila kufunika kichwa, yuaaibisha kichwa chake; kwa maana ni sawasawa na yule aliyenyolewa.

6 Maana mwanamke asipofunikwa na akatwe nywele. Au ikiwa ni aibu mwanamke kukatwa nywele zake au kunyolewa, na afunikwe.

7 Kwa maana kweli haimpasi mwanamume kufunikwa kichwa, kwa sababu yeye ni mfano na utukufu wa Mungu. Lakini mwanamke ni utukufu wa mwanamume.

8 Maana mwanamume hakutoka katika mwanamke, bali mwanamke katika mwanamume.

9 Wala mwanamume hakuumbwa kwa ajili ya mwanamke, bali mwanamke kwa ajili ya mwanamume.

10 Kwa hiyo imempasa mwanamke awe na DALILI YA KUMILIKIWA KICHWANI, kwa ajili ya malaika”.

Katika mistari hii Mtume Paulo aliindika kwa uongozo wa Roho Mtakatifu ili kufikisha ujumbe kwa kanisa lote la Mungu kwa wote watakaosoma waraka huo, na waraka huo haukuwahusu wakorintho tu kama wengi wanavyotafsiri..bali ililihusu kanisa la Kristo kwa ujumla, ikiwemo na sisi watu wa nyakati hizi za mwisho.

Sasa kama ukisoma mistari hiyo utaona, Imejikita sana katika Eneo la KICHWA…Na imezungumzia vichwa vitatu…1) kichwa cha Kristo, 2) Kichwa cha Mwanamume 3) Kichwa cha mwanamke…

Tukianza na kichwa cha Kwanza, ambacho ni cha Kristo, biblia imekitaja kuwa ni Mungu mwenyewe…maana yake aliyekuwa na mamlaka juu ya Kristo ni Mungu peke yake, ambaye ndiye Baba yake..

Na pili kichwa cha Mwanamume ni Kristo..maana yake ni kwamba..Kristo ndiye mwenye mamlaka juu ya kila mwanamume…

Na tatu kichwa cha kila mwanamke ni mwanamume…Maana yake ni kwamba mwenye mamlaka juu ya mwanamke ni mwanamume…Na mamlaka hayo mwanamume alipewa na Mungu pale Edeni (Mwanzo 3:16)

Sasa kwasababu mwanamume ndiye kichwa cha Mwanamke…basi mwanamke ni lazima aonyeshe dalili au ishara ya kumilikiwa katika kichwa chake…na ishara hiyo sio nyingine zaidi ya kufunika kichwa…Ni kama vile ulivyo utaratibu wa mwanamke kuvishwa shela linalofunika mpaka kichwa wakati wa harusi au anapovishwa pete, ni kuonyesha ishara ya kumilikiwa na mwingine…Ndivyo hivyo hivyo kila mwanamke anapaswa afunike kichwa anapokuwa kanisani kuonyesha ishara ya unyenyekevu, na ya kumilikiwa na wanaume ambao ndio vichwa vyao.

Sasa wengi wakisikia hili neno kutawaliwa/kumilikiwa wanachukia na linawakwaza!..wanadhani wameambiwa waabudu wanaume, (kumbuka anayestahili kuabudiwa ni Bwana wetu mmoja tu Yesu Kristo)!..Lakini katikati yetu wanadamu Mungu katuweka chini ya milki ya watu wengine,ili kufikisha ujumbe Fulani wa rohoni. Kwamfano Mtoto yoyote yule awe wa kiume au wakike anapokuwa mdogo anakuwa yupo chini ya milki ya wazazi wake, kwa faida yake huyo mtoto…Sasa mtoto akichukia kumilikiwa na wazazi wake atakuwa ni mgonjwa, kwasababu Mungu akitaka kumlisha au kumbariki ni lazima atumie wazazi wake/walezi wake kumbariki huyo mtoto. Na ndio hivyo hivyo, katika roho wanawake wote ni milki ya wanaume, ndivyo Mungu alivyopenda iwe hivyo, hakuna awezaye kubadilisha, na hiyo pia ni kwa faida ya wanawake..

Mwanamke yoyote anayekataa kutawaliwa au kumilikiwa na mwanamume akidhani atakuwa anamwabudu, anajimaliza mwenyewe!…ukitaka mambo yako yaende sawa kubali kumilikiwa, lakini ukitaka laana kataa kumilikiwa!…Vivyo hivyo unapokuwa kanisani mwanamke ukitaka ufaidike na ibada yako FUNIKA KICHWA CHAKO!, kama ishara ya kumilikiwa!…na tena biblia hapo kwenye mstari wa 10 inasema wazi kabisa kwamba “kwaajili ya malaika funika kichwa chako”….Maana yake ni kwamba malaika wa Bwana wanaopita kanisani kwaajili ya kuwahudumia watakatifu kulingana na Waebrania 1:14, wanapopita na kukuta kichwa chako kipo wazi, na tena umeweka wigi, au rasta hawawezi kukuhudumia…

Na ndio kazi ya shetani kuyafanya yale mambo madogo yaonekane sio maana sana, ili watu wasipate Baraka kutoka kwa Mungu..

Funika kichwa mwanamke wa kikristo uwapo ibadani, hilo ni Neno la Mungu na lipo katika agano jipya na si la kale, Usilidharau Neno la Mungu kwa kiburi cha kupandikiziwa na shetani, usikubali shetani akichezee kichwa chako..kumbuka ndio utukufu wako upo hapo, biblia inasema hivyo.

Kama maneno haya unafikiri ni ya uongo, hebu fanya utafiti siku moja, kisafishe kichwa chako, vaa vizuri, funika kichwa chako kwa kitambaa/kilemba, halafu nenda kanisani..utaona utofauti wa siku hiyo na siku nyingine, ndipo utakapojua kuwa Neno la Mungu sio uwongo…Utaona hata maneno yanayotoka katika kichwa chako yanakuwa na nguvu na uweza, hata uombaji wako utakuwa tofauti,,utatembea na jeshi la malaika wa mbinguni. Vilevile jambo hilo linaambatana na kujisitiri, ukiwa ni mwanamke wa kuvaa ovyo ovyo tu kila mahali, kamwe hutakaa uuone utukufu wa Mungu haijalishi utasema wewe umeokoka kiasi gani.

Hilo ni Neno la Mungu.

Bwana akubariki.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

NAFASI YA MWANAMKE KATIKA KANISA

NAO WALIOKUWA WAMEKUSUDIWA UZIMA WA MILELE WAKAAMINI.

NI NANI ALIYEWALOGA?

USIMZIMISHE ROHO.

NI NINI TUNAJIFUNZA JUU YA MT. DENIS WA UFARANSA?

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Kwanini Bwana alirejea Tiro na Sidoni kwa mfano wa Sodoma?

SWALI: Kwanini Bwana Yesu aliitaja Tiro na Sidoni, kwamba kama ingeliona miujiza ile aliyoifanya kule Bethsaida ingalitubu kwa kuvaa magunia na majivu. Kwani miji hii ilikuwa ni ya namna gani, na ilifanya kosa gani?


JIBU: Tusome..

Mathayo 11:21 “Ole wako, Korazini! Ole wako, Bethsaida! Kwa kuwa kama miujiza iliyofanyika kwenu ingalifanyika katika Tiro na Sidoni, wangalitubu zamani kwa kuvaa magunia na majivu.

22 Walakini nawaambieni, itakuwa rahisi Tiro na Sidoni kustahimili adhabu zao siku ya hukumu kuliko ninyi.

23 Nawe Kapernaumu, je! Utakuzwa mpaka mbinguni? Utashushwa mpaka kuzimu; kwa kuwa kama miujiza iliyofanyika kwako ingalifanyika katika Sodoma, ungalikuwapo mji huo hata leo”.

Ukitazama kwa karibu utaona Bwana Yesu aliiona miji hiyo miwili (yaani Tiro na Sidoni), ilifanana na Sodoma na Gomora kwa tabia zake.

Kumbuka Sodoma na Gomora iliangamizwa kwa maovu yaliyopindukia, Vivyo hivyo Tiro na Sidoni ziliangamizwa, lakini wengi wetu hatufahamu iliangamizwaje? Na Kwa kosa gani..Na hiyo ni kutokana na kwamba habari zao hazipo wazi sana katika biblia kama vile zilivyokuwa za Sodoma na Gomora.

Jaribu kufikiria mpaka biblia inamfananisha mfalme wa Tiro na Shetani mwenyewe..Ujue kuwa ilikuwa inamwangaza shetani mwenyewe duniani kwa tabia zake..Tutakuja kuona huko mbele..

Sasa ukisoma agano la kale, utagundua kuwa mji huu ulikuwa ni mkubwa sana kibiashara hususani ule wa TIRO, Ujenzi wa Hekalu la Mfalme Sulemani kwa sehemu kubwa ulitegemea njenzo na vifaa kutoka katika nchi hizi mbili (Soma 1Nyakati 22:4)..

Hivyo enzi zile za wafalme, mataifa haya mawili yalitajirika kwa haraka sana, japokuwa mataifa kama Babeli na Ashuru yalikuwa bado yapo juu yao, lakini mataifa haya mawili yalikuwa na nguvu kubwa sana kiuchumi, ni sawa leo tuyaite CHINA, huku Babeli na Ashuru yabakie kuwa , Marekani na Urusi. Jinsi leo hii China ilivyochangamka kibiashara ndivyo ilivyokuwa miji hiyo miwili.

Sasa ukipata muda unaweza kusoma kitabu cha Ezekieli kuanzia sura ya 26 mpaka ya 28, Ujione jinsi mataifa haya yalivyosifiwa na Mungu kuwa imara kibiashara na kiuchumi, Na jinsi Mungu alivyoyatamkia maangamizo yao, siku moja, ambayo yatatelekezwa na mfalme wa Babeli Nebukadreza..

Ukisoma pale utaona inasema..

nchi hiyo kwa jinsi ilivyokuwa nzuri mpaka ikajiita “Ukamilifu wa Uzuri” hakuna wa kufananishwa nayo. Jinsi Ilivyokuwa kiini cha biashara cha mataifa yote, mpaka Nchi ya Tarshishi ile Yona aliyoikimbilia, ilitegemea kufanya biashara na Tiro, watu wasomi na wenye akili walikuwa wanaishi humo (TIRO).. kila aina ya biashara ya madini na mawe, biashara ya wanyama, na vifaa vya kivita zilifanyika humo. Biashara za nguo na urembo wa kila namna, biashara ya vyakula na matunda. walikuwa na jeshi kubwa la kutosha, mpaka wakawa wanawauzia silaha mataifa mengine.

Hiyo ndio ikampa kiburi mkuu wao mpaka afikie hatua ya kujilinganisha na Mungu, kutokana na Hekima na utajiri aliokuwa nao na fedha nyingi..Na Yezebeli Yule tunayemsoma kwenye biblia alitokea huko(Ndiye aliyemwingiza mungu baali Israeli)..Hivyo Mungu akapanga siku ya maangamizo yao..(Ezekieli 28:1-10)

Biblia inasema Wafalme wa kila mahali watatetemeza kwa jinsi anguko lake litakavyokuwa(Tiro), wakisema wewe uliyekuwa mwenye nguvu imekuaje umeanguka ghafla hivi, kirahisi,

Ezekieli 27:32 “Na katika kulia kwao watakufanyia maombolezo, na kukuombolezea, wakisema, Ni nani aliye kama Tiro, kama yeye aliyenyamazishwa kati ya bahari?

33 Bidhaa zako zilipotoka katika bahari, uliwajaza watu wa kabila nyingi; uliwatajirisha wafalme wa dunia, kwa wingi wa mali zako, na kwa utajiri wako”.

Ezekieli 26: 1 “Ikawa katika mwaka wa kumi na mmoja, siku ya kwanza ya mwezi, neno la Bwana likanijia, kusema,

2 Mwanadamu, Kwa sababu Tiro amesema juu ya Yerusalemu, Aha! Yeye amevunjika aliyekuwa lango la kabila za watu; amenigeukia; nitajazwa kwa kuwa sasa ameharibika;

3 basi Bwana MUNGU asema hivi; Tazama, mimi ni juu yako, Ee Tiro, nami nitaleta mataifa mengi kupigana nawe, kama bahari iinuavyo mawimbi yake.

4 Nao wataziharibu kuta za Tiro, na kuibomoa minara yake; tena nitakwangua hata mavumbi yake yamtoke, na kumfanya kuwa jabali tupu”.

Ukiendelea sasa kusema Ezekieli 28:11-19 utaona Mungu akitoa unabii wa shetani, na jinsi anguko lake lilivyokuwa kule mbinguni kwa kivuli hichi hichi cha mfalme wa Tiro.

Vivyo hivyo na Sidoni naye alikuwa pacha wake, soma habari iliyosalia utaona hilo. Kama vile tu Gomora alivyokuwa pacha wa Sodoma.

Sasa watu wa miji hiyo walitiwa kiburi kwa mali na fedha, wakamsahau Mungu muumba wa mbingu na nchi, wakawa wanaishi maisha ya dhambi, wanawaza tu mambo ya kidunia hadi siku moja Mungu alipoleta uharibifu wao kwa mkono wa Nebukadneza.

Lakini tunaona pale Bwana Yesu anasema.. Laiti ingeliona miujiza iliyokuwa inafanywa na yeye, basi miji hiyo miwili ambayo imefananishwa na utawala wa shetani kwa kujiinua..Watu hao wangalitubu tena kwa kuvaa nguo za magunia na majivu. Mpaka na mfalme wao angetubu.

Tengeneza picha, ni sawa na leo hii, kila mahali tunasikia shuhuda nyingi, tunaona miujiza mingi Kristo akiifanya, mpaka wafu wanafufuliwa mbele ya macho yetu lakini bado tunaupuuzia wokovu, tunaona kama ni habari za kale.

Tujiulize Je siku ile tutastahimili vipi adhabu ya hukumu?.

Ni wazi kuwa kama ziwa la moto litakuwa kali sana, basi kwa vizazi vyetu litakuwa limechochewa mara 7 zaidi,.Bwana atusaidie tusiupuuzie wokovu, Kristo alilipa gharama kubwa sana kwa ajili yetu..kwahiyo tusiudharau wokovu hata kidogo.

Bwana akubariki.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

JINSI SODOMA NA GOMORA ILIVYOKUWA INAVUTIA SANA..

MAHALI UNAPOPASWA USIMVUMILIE SHETANI HATA KIDOGO.

MTANGO WA YONA.

FAHAMU JINSI KRISTO ANAVYOPONYA WATU ROHO.

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!

CHUKIZO LA UHARIBIFU

Rudi Nyumbani:

Print this post

USIABUDU SANAMU.

Sanamu ni kitu chochote kile kinachotengenezwa chenye umbile aidha la malaika wa mbinguni, mwanadamu, mnyama, au mimea…Mwanadamu yoyote anayetengeneza kitu chochote chenye mifano ya hivyo vitu tayari kashatengeneza sanamu.

Sasa sio dhambi kutengeneza sanamu…ikiwa ina lengo lisilo la kiibada…kwamfano sanamu zilizopo makumbusho, hizo lengo lake ni la kumbukumbu, pia sanamu za Wanyama kama tembo, samaki,swala,watu n.k zilizopo sehemu za makumbusho au sehemu za maonyesho, au ambazo zinawekwa mahali kama nembo ya nchi au urembo wa mji sio dhambi…

Tatizo kubwa ni pale zinapotengenezwa kwa lengo la Ibada!…kwamba inapofikia hatua ya mtu kuamini kwamba sanamu ile ya tembo ina UUNGU ndani yake na hivyo inahitajika kuogopwa au kusujudiwa, kwamba Sanamu ya mtu yule ambaye alikuwa shujaa wa Taifa letu ina Uungu ndani yake, sanamu ile ya Mtakatifu aliyewahi kuishi Ina Uungu ndani yake, na hivyo inastahili kusujudiwa, na kupewa heshima fulani na hata kutukuzwa..Hilo ndio tatizo.

Sasa kuzitumikia na kuzisujudia sanamu kwa namna hiyo ndiko kunakoitwa IBADA ZA SANAMU. Na hizi ibada za sanamu zilianzia kwa wapagani, na shetani ameziingiza mpaka kwenye kanisa..na amewapofusha watu macho na kuwafanya wasione kabisa ukweli kuwa wanaabudu sanamu..

Kwamfano utaona sanamu ya mtakatifu fulani wa kwenye biblia labda tuseme Petro, au Paulo au Hana…imewekwa pale na inapewa heshima kana kwamba ni Paulo mwenyewe yupo ndani ya ile sanamu, inapewa heshima kana kama ni Petro mwenyewe yupo ndani ya ile sanamu kiasi kwamba mtu anaogopa hata kuikanyaga kwa bahati mbaya..kwasababu anahisi kabisa yule pale ni Petro, au Paulo amesimama…

Unakuta imewekwa sanamu ya Bwana Yesu pale, mtu anaogopa hata kuitazama usoni akihisi ni Bwana Yesu Mwenyewe yupo pale anamtazama,…hivyo inamfanya aende kwa adabu na staha na moyo wa ibada mbele ya ile sanamu, hatimaye kujinyenyekeza chini yake na hata kutaka kubarikiwa chini ya ile sanamu…HAYO NDIYO MACHUKIZO MBELE ZA MUNGU…Hiyo ndiyo sababu Bwana amesema Kwamba tusizichonge kabisa kama zitatupeleka katika kuzisujudia na kuzitumikia kwasababu zinamtia Mungu WIVU…Maana yake ni kwamba badala moyo wako uwe mbinguni Mungu aliko, na akili yako uipeleke mbinguni, na mawazo yako uyapeleke mbinguni mahali alipo…wewe unayapeleka kwenye ile sanamu iliyopo mbele yako, unayapeleka katika picha iliyopo mbele yako, hicho ndicho kinachomtia Mungu wivu.

Na inafika mbali Zaidi hadi wengine wanaziundia sala maalumu za kuombea, yaani wanafanya sanamu hizo kama nyezo au daraja la kuwasiliana na Mungu.

Kutoka 20:4 “Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu cho chote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini duniani, wala kilicho majini chini ya dunia.

5 Usivisujudie wala kuvitumikia; kwa kuwa mimi, Bwana, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu; nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao,

6 nami nawarehemu maelfu elfu wanipendao, na kuzishika amri zangu”.

Mungu wetu anataka tumwabudu katika roho na kweli…na si katika sanamu…

Yohana 4:20 “Baba zetu waliabudu katika mlima huu, nanyi husema ya kwamba huko Yerusalemu ni mahali patupasapo kuabudia

21 Yesu akamwambia, Mama, unisadiki, saa inakuja ambayo hamtamwabudu Baba katika mlima huu, wala kule Yerusalemu.

22 Ninyi mnaabudu msichokijua; sisi tunaabudu tukijuacho; kwa kuwa wokovu watoka kwa Wayahudi.

23 Lakini saa inakuja, nayo sasa ipo, ambayo waabuduo halisi watamwabudu Baba katika ROHO NA KWELI. Kwa maana Baba awatafuta watu kama hao wamwabudu.

24 Mungu ni Roho, nao wamwabuduo yeye imewapasa kumwabudu katika roho na kweli”

Umeona Mungu aabudiwi kupitia sanamu fulani, wala kilima fulani wala mtu fulani wala malaika fulani..yeye anaabudiwa katika roho na kweli…Laiti kama angekuwa anapenda tumwabudu kwa kumuuona…asingekuwa kama alivyo leo…angejidhihirisha duniani kote na wote tungeijua sura yake, na picha yake ingezagaa kila mahali, tungeiabudu na kuisujudia na wote tungekuwa na nakala ya picha hiyo…tungeiweka mpaka kama nembo ya Hela yetu..lakini hajayaruhusu hayo kwasababu anataka sisi tusimwabudu kupitia picha yake..anataka tumwabudu katika ROHO NA KWELI.

Hatumwoni lakini tunaamini yupo…Na hiyo Imani ya kwamba hatumwoni lakini tunaamini yupo, ndiyo ya thamani kwake…na ndiyo anayotaka tumwabudu nayo…

Kama ni picha ya Bwana Yesu au mtakatifu yoyote iwepo tu kama “lugha ya picha” na si chombo cha ibada wala kichukuacho sehemu ya hisia za mtu kana kwamba ndio kitu chenyewe halisi….Bwana anataka tukiweka sanamu/picha ya mtakatifu fulani tuichukulie ile picha kama vile tunavyoichukulia picha/sanamu ya mnyama iliyopo makumbusho…Hakuna mtu anayeweza kwenda mbele ya sanamu tembo na kuiogopa na kuipa heshima kana kwamba ni tembo halisi yupo pale, hakuna mtu anayeweza kuona sanamu ya simba akatetemeka na kukimbia, hakuna mtu anaweza kuona sanamu ya ng’ombe akaenda kukamua maziwa chini yake…Na sisi hatupaswi kwenda kukamua baraka kutoka kwenye sanamu ya mtakatifu Mariamu tulioitengeneza sisi au ya Bwana mwenyewe.

Shetani ameshalijua hilo, Hivyo alichokifanya ni kwenda kujipachika nyuma ya sanamu hizo, ili mumwabudu kisirisiri. Hivyo unapojihusisha na mojawapo ya ibada hizo ujue kabisa unamwabudu shetani.

2Wakorintho 6:16 “Tena pana mapatano gani kati ya hekalu la Mungu na sanamu? Kwa maana sisi tu hekalu la Mungu aliye hai; kama Mungu alivyosema, ya kwamba, Nitakaa ndani yao, na kati yao nitatembea, nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.

17 Kwa hiyo, Tokeni kati yao, Mkatengwe nao, asema Bwana, Msiguse kitu kilicho kichafu, Nami nitawakaribisha.

18 Nitakuwa Baba kwenu, Nanyi mtakuwa kwangu wanangu wa kiume na wa kike,

Bwana atubariki na kutusaidia.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

MAFUNDISHO YA MASHETANI

DANIELI: Mlango wa 3

Sabato halisi ni lini, Je! ni Jumapili au Jumamosi?, Ni siku gani itupasayo kuabudu?

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!

CHUKIZO LA UHARIBIFU

UNYAKUO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Maneno haya yana maana gani?..” Avaaye asijisifu kama avuaye “

1.Naomba kuelezewa maana ya huu mstari tafadhali,  unaosema; Mfalme wa Israel akajibu, akasema, Mwambieni ” Avaaye asijisifu kama avuaye ”  huyu mfalme alikuwa anamaanisha nimi kusema hivyo? (1Wafalme 20:11)


JIBU: Hiyo ni mithali iliyokuwa inatumika wakati huo,  kama leo watu wanavyosema “usitukane mamba kabla hujavuka mto”..Na hapo ni hivyo hivyo…hapo huyu Benhadadi alikuwa ameshajitangazia ushindi dhidi ya Israeli kabla hata ya vita…(Ni kama vile anameshawadharau anaokwenda kupigana nao kabla hata hajapigana nao), Ndio Mfalme Ahabu akamwambia avaaye asijisifu kama avuaye…maana yake avaaye mavazi ya vita ambaye ndio kwanza anakwenda vitani asijisifu kama yule mtu ambaye tayari ameshavimaliza vita na kashinda! na hivyo sasa anavua mavazi yake na kusherehekea ushindi..Hiyo ndio maana yake huo mstari.

Na ukifuatilia Habari hiyo utaona jinsi Mungu alivyowapigania Israeli kutokana na kiburi hicho cha mfalme wa Shamu, kuwadharau Israeli Pamoja na Mungu wao.

1Wafalme 20: 10 “Ndipo Ben-hadadi akatuma kwake, akasema, Miungu wanifanyie hivi na kuzidi, yakiwa mavumbi ya Samaria yatatosha makonzi ya watu wote walio miguuni pangu.

11 Mfalme wa Israeli akajibu, akasema, Mwambieni, Avaaye asijisifu kama avuaye.

12 Ikawa, Ben-hadadi alipolisikia neno hilo, naye alikuwa akinywa, yeye na wafalme, mabandani, aliwaambia watumwa wake, Jipangeni. Wakajipanga juu ya mji.

13 Na tazama, nabii akamjia Ahabu mfalme wa Israeli, akasema, Bwana asema hivi, Je! Umeona makutano haya yote walio wengi? Angalia, nitawatia leo mkononi mwako; nawe utajua ya kuwa ndimi Bwana”.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

YEZEBELI ALIKUWA NANI

DANIELI: Mlango wa 11

NA MTU MMOJA AKAVUTA UPINDE KWA KUBAHATISHA, AKAMPIGA MFALME

Neno I.N.R.I kwenye msalaba wa Yesu maana yake ni nini?

Kwanini yule mtu afe kwa kuliwa na simba?

Rudi Nyumbani:

Print this post

MAHALI UNAPOPASWA USIMVUMILIE SHETANI HATA KIDOGO.

Katika injili utaona zipo sehemu kuu mbili ambazo Bwana alimfukuza shetani waziwazi.. sehemu ya kwanza ni pale shetani alipotaka amsujudie kwa mapatano kuwa atampa milki zote za ulimwengu.Na sehemu ya pili ni pale Shetani alipomfariji kuwa hatapitia mabaya yaliyo mbele yake..

Tusome..

Mathayo 4:8 “Kisha Ibilisi akamchukua mpaka mlima mrefu mno, akamwonyesha milki zote za ulimwengu, na fahari yake,

9 akamwambia, Haya yote nitakupa, ukianguka kunisujudia.

10 Ndipo Yesu alipomwambia, NENDA ZAKO, SHETANI; kwa maana imeandikwa, Msujudie Bwana Mungu wako, umwabudu yeye peke yake”.

Na mahali pengine ni..

Mathayo 16:21 “Tangu wakati huo Yesu alianza kuwaonya wanafunzi wake ya kwamba imempasa kwenda Yerusalemu, na kupata mateso mengi kwa wazee na wakuu wa makuhani, na waandishi, na kuuawa, na siku ya tatu kufufuka.

22 Petro akamchukua, akaanza kumkemea, akisema, Hasha, Bwana, hayo hayatakupata.

23 Akageuka, akamwambia Petro, NENDA NYUMA YANGU, SHETANI; u kikwazo kwangu; maana huyawazi yaliyo ya Mungu, bali ya wanadamu”.

Bwana aliona ipo mipaka ambayo mtu yeyote au kiumbe chochote hakipaswi kuvuka, Na kwamba yeyote atakayejaribu kufanya hivyo si tu kukemewa bali ni kufukuzwa kabisa.. Na shetani alifukuzwa na Bwana katika vitu hivi viwili..Kwanza ni pale alipotaka asujudiwe hilo tayari lilikuwa ni kosa kubwa machoni pa Bwana haijalishi ni ahadi ngapi nzuri zilifuata mbele yake..

Leo hii watu wengi wapo tayari, kumwabudu shetani kisa mali, wapo tayari kubadili imani kisa wanawake/wanaume, wapo tayari kula rushwa kisa wanaahidiwa pesa nzuri, wapo tayari kuua na kutoa kafara ili wawe matajiri, wapo tayari kujiuza ili wapate kipato, wapo tayari kupiga ramli wawaridhishe wazee wa ukoo, wapo tayari kufanya lolote lile haijalishi ni kinyume na mapenzi ya Mungu kiasi gani ili wapate faida Fulani au unafuu Fulani..

Ndugu hatua kama hiyo ukifikia ikiwa wewe ni mkristo Usimwangalie shetani mara mbili, usimvumilie shetani hata kidogo!, mfukuze kwa kishindo chote, haijalishi leo hii unapitia katika hali ngumu kiasi gani..Kumbuka hata wakati shetani anamletea Kristo majaribu kama haya ya kuahidiwa ulimwengu mzima na milki zote, alikuwa katika hali ya njaa, hajala siku 40, hana kibanda, wala biashara wala nini..Lakini alimwambia ondoka, hapa, kwa namna nyingine tunaweza kusema nisikuone eneo hili tena.

Sehemu nyingine ambayo unapaswa usimvumilie shetani ni pale, Mungu anapokuonyesha mafanikio Fulani makubwa mbeleni lakini sharti kwanza upitie mateso Fulani au dhiki Fulani kabla ya kuyapata, lakini shetani anatokea na kukwambia usihofu hutapitia..Hapo hupaswi kusikiliza, ni kumfukuza tu..

Embu jaribu kufiria mfano Bwana angeyasikiliza yale maneno ya shetani yaliyokuwa ndani ya kinywa cha Petro, mambo yangekuwaje leo hii? ni wazi kuwa hadi leo hii mimi na wewe tusingepata neema ya wokovu, kwasababu Kristo asingesulibiwa..Damu isingepatikana kwa ajili ya ondoleo la dhambi zetu… Lakini aliona wimbi kubwa la wanadamu linakwenda kuokolewa na ibilisi hataki hilo litendeke..akajaribu kumbunia njia za kulikwepa.

Hata Mtume Paulo, kuna wakati alijua kabisa kuwa vifungo na dhiki vinamngoja huko mbeleni, lakini hakukubali kukatishwa tamaa na watu, kwamba abaki asiende Yerusalemu. Watu wanadhani Roho Mtakatifu kumwambia Paulo vile, ilikuwa ni kumzuia asiende hapana, bali alikuwa anampa taarifa ya mambo yatakayomkuta huko mbeleni, kwasababu ni kawaida ya Mungu kuwapata watu wake taarifa kabla mabaya hayajawakuta.. Lakini Ni wale watu waliokuwa naye ndio waliomwambia asiende, lakini yeye hakukubali, akawaambia..

Matendo 21:12 “Basi tuliposikia haya, sisi na watu wa mahali pale, tukamsihi asipande kwenda Yerusalemu.

13 Ndipo Paulo alipojibu, Mnafanya nini, kulia na kunivunja moyo? Kwa maana mimi, licha ya kufungwa, ni tayari hata kuuawa katika Yerusalemu kwa ajili ya jina lake Bwana Yesu”.

Alifanya hivyo kwasababu aliona wingi wa matunda atakayoyaleta kwa Mungu ni mengi akifananishwa na dhiki fupi za kitambo, zitakazoletwa na shetani.

Hivyo na sisi wakristo, tusiruhusu mambo hayo mawili shetani ayalete mbele yetu..kwanza tusiruhusu tamaa za ulimwengu kutufarakanisa na Mungu wetu, Pia tusiruhusu dhiki za kitambo zikatukosesha Baraka Mungu alizotuchumia huko mbeleni…

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP


Mada Nyinginezo:

KUTAHIRIWA KIBIBLIA

VICHEKESHO NA UTANI MADHABAHUNI

JE KUHUDUMU KWA NYIMBO ZA INJILI KUKOJE?

Je kuweka mapambo kama mikufu, vikuku na kutoboa pua ni dhambi?

JINSI SODOMA NA GOMORA ILIVYOKUWA INAVUTIA SANA..

KWANINI UBATIZO NI WA MUHIMU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Je ni dhambi kuota unafanya kitu Fulani ambacho ni kinyume na mapenzi ya Mungu?

Ni dhambi kuota unafanya kitu kiovu kama uzinzi, uuaji, wizi, uasherati, au ulevi?


JIBU: Ndoto huja pasipo hiari ya mtu..hakuna mtu anayeweza kupanga aote nini leo au kesho…Zinakuja tu zenyewe pasipo mtu kupanga….Lakini ndoto nyingi ni MATOKEO ya kitu Fulani ambacho kinaendelea katika maisha ya mtu.

Kwamfano umelala na njaa..usiku utajikuta unaota unakula!,(Isaya 29:8) umeshinda ukifanya shughuli Fulani siku nzima ukilala utajiona unaendelea kufanya vile vitu katika ndoto…kabla ya kulala ulikuwa unatazama kitu Fulani kwenye luninga au mtandaoni ambacho kimegusa hisia zako…utakapolala ni rahisi sana kukiota kile kitu

Vivyo hivyo..umekuwa karibu na mtu Fulani kwa muda mrefu katika maisha yako ghafla akaondoka au akafariki..Ni lazima utakuwa unamwota ota mara kwa mara. Kwahiyo ndoto nyingi ni matokeo ya kitu Fulani ambacho kinaendelea katika maisha ya mtu..Ndio maana biblia imeweka wazi jambo hilo katika..

Mhubiri 5:3 “Kwa maana ndoto huja kwa sababu ya shughuli nyingi; na sauti ya mpumbavu kwa njia ya wingi wa maneno”.

Kwahiyo ukiota unaiba na ndoto inajirudia rudia ni matokeo ya kitu ambacho kinaendelea katika maisha yako… “Hiyo ndoto uliyoiota sio dhambi”…lakini ni ujumbe kwamba katika maisha yako kuna uwezekano bado kuna vimelea vya wizi…hivyo zidi kuyachunguza kwa undani maisha yako na kuyatakasa…Ukiona unafanya uasherati, ni hivyo hivyo…chunguza mtindo wa maisha yako unayoishi, labda bado unatabia ndogo ndogo pengine unaridhia picha chafu au video chafu ambazo unapishana nazo kwenye mitandao, au bado unayaendekeza mawazo machafu ya zinaa yanapokujia kichwani mwako..kwahiyo ndio maana zinaendelea mpaka kwenye kichwa chako unapolala..

Na jambo muhimu la kufahamu ni kwamba kama ulikuwa umetoka kwenye dunia moja kwa moja ukaokoka…Bwana anakuwa amekusamehe maisha yako na dhambi zako, lakini madhara ya dhambi katika maisha yako hayataondoka siku ile ile unapookoka..yataondoka kidogo kidogo mpaka mwisho wake kuisha kabisa…yaani kama ulikuwa ni mzinzi wa kupindukia kabla ya kuokoka…

Siku ile unapookoka Roho Mtakatifu anaiondoa ile tabia ndani yako…lakini utaendelea kuvuna matokeo ya uzinzi wako kwa kipindi Fulani, ndio hapo hayo mandoto ya mambo uliokuwa unayafanya nyuma yanaweza kuendelea kwenye kichwa chako kwa kipindi kadhaa (Hayo ndio madhara  ya dhambi)…

Lakini yajapo hayo baada ya kumwamini na kupokea Roho Mtakatifu usiogope!.. unapoota unafanya hayo mambo katika ndoto baada ya kumwamini Yesu, na ilihali hayo mambo katika maisha yako halisi umeshayaacha kitambo…unachotakiwa kufanya ni kuikataa hiyo hali…na kusema mimi sio huyo!!!..usiruhusu kuikubali hiyo hali kwamba ni wewe…Ikatae!, usikubali kukata tamaa wala kuwa mdhaifu…na itafika kipindi Fulani hayo mandoto yatakwisha kabisa….

Wengi wanapofikia hatua kama hii, wamemwamini Yesu, wamekwenda kubatizwa na wamepokea Roho Mtakatifu lakini wanapojikuta baada ya siku kadhaa wanaota wanafanya mambo ambayo wameshayatubia, wengi wanarudi nyuma na kuvunjika moyo na kuhisi hawakutubu vizuri…Na hapo shetani anachukua nafasi ya kuwarudisha tena katika mambo waliyokuwa wanayafanya, na mtu anasimama kurudia rudia kuokoka hata mara 100 katika maisha yako..

Na jambo lingine ambalo litakusaidia kuepukana kwa haraka na ndoto za namna hiyo, ni kuwa mwombaji na mtafakariji wa Neno, walau Sali kila siku lisaa limoja, kama Bwana Yesu alivyotuagiza, lakini kama utakuwa maisha yako ya kuomba, hali hizo zitaendelea kukurudia rudia bila kikomo..Maombi ni ngao ya majaribu ya shetani. Ukisema umeokoka halafu maombi yanakushinda, basi bado hujaokoka.

Hivyo kwa ujumla dhambi ni mbaya na ina madhara! Na inatesa hata baada ya kuiacha!…Ukiingia mkataba na shetani, hutatoka kirahisi. Ni sawa na gari lililokuwa kwenye mwendo likapiga breki ghafla..Matairi yatasimama, injini itasimama lakini gari litazidi kuendelea mbele kidogo…na dhambi ni hivyo hivyo..utaacha uasherati, ulevi, na kila kitu siku ile unaokoka lakini mambo hayo yataendelea katika ulimwengu wako wa ndoto, lakini ukizingatia hayo tuliyoyasema utaepukana na hizo hali kwa haraka sana.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Group la whatsapp


Mada Nyinginezo:

KUOTA UNAFANYA TENDO LA NDOA.

Kuota unafanya Mtihani.

KUOTA UNAOLEWA/UNAOA.

KUOTA UNAKULA CHAKULA.

KUOTA UNANG’OKA MENO.

Rudi Nyumbani:

Print this post