Category Archive Home

NGAZI 7 AMBAZO MKRISTO NI LAZIMA AZIPANDE KUUFIKIA UKAMILIFU.

Kuokoka tu peke yake hakutoshi, zipo ngazi saba, za kupanda ili kuufikilia ukamilifu Mungu anaotaka kuuona kwako kabla hujaondoka hapa duniani. Tunapomwamini Bwana Yesu, kwa kumkiri na kubatizwa, hatupaswi kuishia hapo hapo tu, kwani biblia inatuonyesha tutakuwa watu wasiokuwa na ushuhuda wowote, kama sio kufa kabisa kiroho.

Sasa kulingana na ufunuo Mtume Petro aliopewa na Roho mtakatifu aliandika mambo saba, ambayo mara baada ya mtu kuwa mkristo anapaswa atie bidii yeye mwenyewe kufanya bila kukawia kawia

Na mambo hayo tunayasoma katika kitabu cha 2Petro 1-12. Tukianzana na jambo la kwanza;

  1. WEMA

2Petro 1:5 “Naam, na kwa sababu iyo hiyo mkijitahidi sana kwa upande wenu, katika imani yenu tieni na wema, …..,

Tukishaamini, ni wajibu wetu kuonyesha Imani yetu kwa matendo yetu mema katika jamii inayotuzunguka,  na kwa watu wote. Wema ni kitendo cha kuonyesha kujali, kuthamini, nidhamu na uaminifu.

Sio kwasababu watu wa kidunia, hawasalimii wengine, na sisi tusiwasalimie watu, au hawawasaidii watu na sisi tusiwasaidie, hawawaelekezi watu na sisi tuwe hivyo hivyo,  huo sio wema, Halikadhalika wewe kama boss kazini kwako, kwasababu umeona, watu wengine wote wanawalipa wafanyakazi wao mshahara fulani kidogo na wewe unawaiga, huwapandishii  mishahara wa kwako au huwapi bonus kwa kazi wanazokufanyia labda kwasababu hazina elimu kubwa au vinginevyo, huo sio wema, wape tu.. Kumbuka ule mfano Bwana Yesu alioutoa, juu ya  wale watu aliowapeleka shambani mwake saa 11 jioni wamfanyie kazi, lakini kulikuwa na wale wengine waliokuwepo tangu asubuhi, na ulipofika wakati wa malipo walitaka wale waliochelewa walipwe kidogo kuliko wao. Lakini Yesu akawaambia..

Mathayo 20:14 “Chukua iliyo yako, uende zako; napenda kumpa huyu wa mwisho sawa na wewe.

15 Si halali yangu kutumia vilivyo vyangu kama nipendavyo? Au jicho lako limekuwa ovu kwa sababu ya mimi kuwa MWEMA”?

Unaona? Wema wema kama huu pia ni wa kuigwa, housegirl wako au mlinzi wako nyumbani.

 Barnaba naye alitajwa kama mtu mwema aliyeshuhudiwa na watu wote, kwa vile alivyokuwa anawajali sana ndugu, (Matendo 11:-25), hususani wale waliokataliwa, mpaka akaitwa mwana wa faraja.

Na sisi tunapaswa pindi tunapookoka, tupige hatua moja zaidi, tuonyeshe wema wetu kwa watu, tulionyeshee bidii, Kumbuka hilo ni moja ya matunda 9 ya Roho Mtakatifu yanayozungumziwa  katika Wagalatia 5:22. (Utu wema)

Warumi 12:21 “Usishindwe na ubaya, bali uushinde ubaya kwa wema”.

  1. MAARIFA

Petro anaendelea kusema..

“ 1:5..na katika wema wenu maarifa,”

Tukishakuwa na uhakika sasa wema upo ndani yetu, tupige hatua nyingine mbele ya kuongeza maarifa juu yake. Maarifa yanayozungumziwa hapa ni maarifa ya kumjua Mungu, sio ya kibinadamu.

Wakristo wengi sana tunakosa maarifa haya, na hivyo tunaangamia, hatujui utendaji kazi wa Mungu kulingana na wakati na majira tuliyopo ni upi, na ni nini tunapaswa tufanye. Kwamfano, kutokujua kuwa ipo nguvu ya upotevu iliyoachiwa na Mungu mwenyewe, leo hii duniani ili iwadanganye watu wasiotaka kuitafuta kweli, na kwamba nguvu hiyo inafanyakazi katikati ya manabii wa uongo, kwa kupitia miujiza ya kweli ya Mungu. Sasa kwa kukosa kujua maarifa hayo Kunatufanya tuangamie,.

Vilevile kuhusiana na neema ya wokovu, kwamba haitadumu milele kwetu sisi watu wa mataifa, upo wakati itaondolewa na kurejeshwa kule Israeli, na huku kwetu tutabakia kuwa kama mafarisayo na masadukayo. Hilo nalo halijulikani na wakristo wengi, na ndio maana ukristo unachukuliwa juu juu tu, na watu wengi, kwasababu wanadhani muda utaendelea kuwepo wakati wote.

Na mambo mengine mengi kama hayo, yaliyo katika maandiko. Hivyo Mungu anatutaka tuwe watu wa kujifunza Neno lake kila siku, na kuyachunguza maandiko na kwa kuwa tunaye Roho wake mtakatifu ndani yetu atatusaidia kuyaelewa yote, na siri zote na mpango wote wa Mungu unaoendelea nao katika wakati wetu huu tunaoishi.

Hivyo hiyo ni hatua ya pili ya ukomavu, kuhakikisha maarifa ya ki-Mungu yanajaa ndani yetu.

  1. KIASI

“1:6 na katika maarifa yenu kiasi”,

Sasa tukishakuwa na maarifa, tunapaswa tuongezee juu yake kitu kingine kinachoitwa kiasi. Wapo wakristo ambao wamekamilika katika maarifa na utu wema, lakini kiasi hawana, hawawezi kujizuia kwenye baadhi ya mambo, mpaka mwisho wa siku mambo hayo yanageuka kuwa kama dhambi kwao. Utakuta mtakatifu anawaza muda wote kazi za mikono yake, mpaka anakosa muda wa kuwa faragha na Mungu, Na wakati anapopaswa afanya hivyo anasema amechoka, atasali siku nyingine, ataendea ibadani wiki nyingine?

Au mwingine, anashikilia sana kufanya mambo yasiyomjenga, kama vile kutazama Tv, Au kuchati, au kuperuzi internet kuangalia vya kidunia tu..na atatumia muda wake mwingi huko, kufanya hayo mambo, lakini kwenye kusali atatumia muda mchache.

Biblia inatuambia sisi tulio wa mchana tuwe na kiasi (1Wathesalonike 5:8). Ili tupate muda wa kuwa karibu na Mungu wetu.

  1. SABURI

“1:6…Na katika kiasi chenu saburi”,

Anasema, tukishajifunza kuwa na kiasi, basi tuongezee na saburi pia. Saburi, ni uvumilivu/ustahimilivu katika Imani. Tukikosa  utahimilivu hususani pale tunapopishana na majaribu, ni ngumu sana kusonga mbele. Ni rahisi mtu kuacha Imani kwasababu anapitia njaa, au kwasasa hana kazi, au  yupo katika mazingira  yasiyofaa ya kubanwa, au ananyanyaswa na watu.

Mtume walikuwa wanafungwa na kupigwa, lakini bado walikuwa wanaendelea kuhubiri injili, kule kule walipofukuzwa.

Kukosa saburi, kwa ajili ya shida za kiulimwengu ambazo huwa hazidumu, ni ngumu sana kufikia kiwango ambacho Mungu alikitarajia kwetu, Vilevile kutokuwa wavumilivu katika huduma, au Imani, ni jambo ambalo linawakwamisha wakristo wengi sana, pale wanapoona matarajio yao hayajatokea kwa wakati walioupanga basi wanakata tamaa. Tumeaswa tusifike huko, tujifunze kuwa na saburi, kwasababu saburi ni mpango wa Mungu kwetu.

Warumi 5:3 “Wala si hivyo tu, ila na mfurahi katika dhiki pia; mkijua ya kuwa dhiki, kazi yake ni kuleta saburi;

4 na kazi ya saburi ni uthabiti wa moyo; na kazi ya uthabiti wa moyo ni tumaini;

Hivyo hili jambo pia tulihifadhi ndani ya mioyo yetu. Tuliruhusu liwe na nafasi yake. Kwasababu hizo ndio ngazi za kufikia ukamilifu wa Kristo.

  1. UTAUWA

“1:6…na katika saburi yenu utauwa”.

Utauwa ni tabia ya uungu. Mungu ni Mtakatifu, hivyo ili na sisi tuwe na uungu ndani yetu tunapaswa tuwe watakatifu, Lazima tujizoeshe kuishi maisha ya utakatifu ya kuikataa dhambi, na mambo yasiyofaa.

1Petro 1:16 “kwa maana imeandikwa, Mtakuwa watakatifu kwa kuwa mimi ni mtakatifu”

Ili tuweze kuishi maisha hayo tunapaswa tuwe watu wa maombi, watu wa kufunga, watu wa kuwatangazia wengine habari njema. Huo ndio utauwa ambao hata Bwana wetu Yesu Kristo alikuwa nao. Lakini kama hatutakuwa waombaji, bado hatukifikia kiwango hichi cha utauwa Bwana anachokizungumzia hapa.

  1. UPENDANO WA NDUGU

“1:7 na katika utauwa wenu upendano wa ndugu,”

Sasa ikiwa utauwa umeshakamilika ndani yetu, jambo lingine ambalo tunapaswa kulionyeshea bidii ni upendano wa ndugu. Kumbuka hatua hizi huwezi kuzifikia kama yale ya chini hayajakamilika kwanza.

Upendano wa ndugu unaozungumziwa hapa sio ule wa ndugu wa kimwilini, hapana, bali ndugu katika Kristo. Tunapaswa tufikie hatua hii ya kupendana sisi kwa sisi kama wakristo. Jambo ambalo limekuwa gumu sana kufikiwa na wengi wetu wa leo, kusengenyana, kurushiana maneno, kuumizana, kana kwamba hatujaokolewa na Bwana mmoja.

Hivyo tujitathimini sana, tugeuke, kwasababu mambo haya hayahitaji maombi bali bidii.

1Petro 1:22 “Mkiisha kujitakasa roho zenu kwa kuitii kweli, hata kuufikilia upendano wa ndugu usio na unafiki, basi jitahidini kupendana kwa moyo”.

Unaona, unahitaji bidii ili kuupata.

7)  UPENDO

“1:7…na katika upendano wa ndugu, upendo”.

Upendano wa ndugu ni tofauti na huu upendo unaozungumziwa hapa. Upendo huu ni upendo wa Ki-Mungu, ambapo mtu akiufikia huo basi mtu anakuwa karibu sana na Mungu, au kwa namna nyingine anakuwa anamjua sana Mungu.

Upendo huu ni upendo usio na masharti, kwamba kisa fulani kanifanyia hivi ndio nimtendee hivi hapana. Mungu aliupenda ulimwengu kisha akamtoa mwanawe wa pekee, sio kwamba tulimfanyia jambo jema kwanza, ndio maana akamtoa hapana, bali alimtoa kwa Pendo lake tu kwetu.

Huu ni upendo usio wa asili ya kibidamu au wanyama, bali asili yake ni mbinguni..Ndio ule unaozungumziwa katika 1Wakorintho 13 unasema..

4 Upendo huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu; upendo hautakabari; haujivuni;

5 haukosi kuwa na adabu; hautafuti mambo yake; hauoni uchungu; hauhesabu mabaya;

6 haufurahii udhalimu, bali hufurahi pamoja na kweli;

7 huvumilia yote; huamini yote; hutumaini yote; hustahimili yote.

8 Upendo haupungui neno wakati wo wote; bali ukiwapo unabii utabatilika; zikiwapo lugha, zitakoma; yakiwapo maarifa, yatabatilika.

Hapa ndipo kilele cha kila kitu.

Sasa tukishaweza kuyafikia hayo yote.. basi Mtume Petro anasema  kwanza tutakuwa si watu wavivu wasio na matunda, pili hatutakuwa watu wa kujikwaa kwaa ovyo katika imani na zaidi ya yote tutakuwa na uwezo wa kuyaona mambo ya mambo yanayokuja.

2Petro 1:8 “Maana mambo hayo yakiwa kwenu na kujaa tele, yawafanya ninyi kuwa si wavivu wala si watu wasio na matunda, kwa kumjua Bwana wetu Yesu Kristo.

9 Maana yeye asiyekuwa na hayo ni kipofu, hawezi kuona vitu vilivyo mbali, amesahau kule kutakaswa dhambi zake za zamani.

10 Kwa hiyo ndugu, jitahidini zaidi kufanya imara kuitwa kwenu na uteule wenu; maana mkitenda hayo hamtajikwaa kamwe.

11 Maana hivi mtaruzukiwa kwa ukarimu kuingia katika ufalme wa milele wa Bwana wetu, Mwokozi wetu Yesu Kristo”

Sasa tukishayajua hayo ni wakati wetu sisi sote tujitathimini tupo, katika hatua ipi na kisha, pale tulipozembea au tulipokwama tuanze kupatendea kazi kwa bidii. Tusiwe tu wasomaji wa makala,.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

LIFAHAMU SANA JAMBO HILI, ILI MUNGU AKUTUMIE.

Kitabu kifupi katika biblia ni kipi, na ujumbe wake ni upi?

Nini maana ya “katika wingi wa hekima mna wingi wa huzuni”.

NITAUPATAJE UPENDO WA KI-MUNGU NDANI YANGU?

NA BAADA YA LILE TONGE, SHETANI AKAMWINGIA.

Rudi nyumbani

Print this post

LIFAHAMU SANA JAMBO HILI, ILI MUNGU AKUTUMIE.

Tunapaswa tujue daraja kubwa sana la Mungu kututumia sisi kwa ajili ya kazi zake maalumu, ni kuishi maisha ya uchaji wa Mungu ambao  utashuhudiwa na watu wa nje. Kiasi kwamba hata Mungu akipitisha neno lake kinywani mwako, watu wengi wataamini moja kwa moja kwasababu maisha yako tayari yalishawashuhudia hata hapo kabla.

Tukiweza kufikia hapo, basi tujue Mungu atatufunulia mambo mengi sana, kwa ajili ya ufalme wake. Kwamfano katika biblia tunamsoma mtu mmoja anayeitwa Anania, Mtu huyu alitumwa na Mungu ili amfuate Paulo, amwombee, na ambatize. Unaweza ukajiuliza kwani hapakuwa na wakristo wengine pale karibu na ile nyumba ambayo Paulo alikuwepo, mpaka Mungu amtoe Anania mbali kidogo, aje pale?. Jibu ni kuwa walikuwepo, lakini Mungu alijua ili ushuhuda wa mtume Paulo baadaye uwe na nguvu katikati ya watu atakaowasimulia ilimuhitaji mtu, aliyejulikana kweli na watu wengi ni mcha Mungu na  mwaminifu, na ndio maana akampelekea huyu Anania..

Tusome kidogo..

Matendo 9:10 “Basi palikuwapo Dameski mwanafunzi jina lake Anania. Bwana akamwambia katika maono, Anania. Akasema, Mimi hapa, Bwana.

11 Bwana akamwambia, Simama, enenda zako katika njia iitwayo Nyofu, ukaulize katika nyumba ya Yuda mtu aitwaye Sauli, wa Tarso; maana, angalia, anaomba;

12 naye amemwona mtu, jina lake Anania, akiingia, na kumwekea mikono juu yake, apate kuona tena.

13 Lakini Anania akajibu, Bwana, nimesikia habari za mtu huyu kwa watu wengi, mabaya mengi aliyowatenda watakatifu wako Yerusalemu;

14 hata hapa ana amri itokayo kwa wakuu wa makuhani awafunge wote wakuitiao Jina lako.

15 Lakini Bwana akamwambia, Nenda tu; kwa maana huyu ni chombo kiteule kwangu, alichukue Jina langu mbele ya Mataifa, na wafalme, na wana wa Israeli.

16 Maana nitamwonyesha yalivyo mengi yatakayompasa kuteswa kwa ajili ya Jina langu.

17 Anania akaenda zake, akaingia mle nyumbani; akamwekea mikono akisema, Ndugu Sauli, Bwana amenituma, Yesu, yeye aliyekutokea katika njia uliyoijia, upate kuona tena, ukajazwe Roho Mtakatifu.

Sasa utajiuliza uaminifu wake, umeandikwa wapi kwenye maandiko? Tukisoma matendo sura ile ya 22, utaona mtume Paulo alipowekwa mbele ya baraza la wayahudi ili kutoa ushuhuda wake, utaona akimtaja mtu huyu kama ni mtu  aliyejulikana na wayahudi wote kwa utauwa wake..Sasa pale mbele kidogo utaona alisema..

Matendo 22:12 “BASI MTU MMOJA, ANANIA, MTAUWA KWA KUIFUATA SHERIA, ALIYESHUHUDIWA WEMA NA WAYAHUDI WOTE WALIOKAA HUKO,

13 Akanijia, akasimama karibu nami, akaniambia, Ndugu yangu Sauli, uone. Nikamwinulia macho yangu saa ile ile.

14 Akasema, Mungu wa baba zetu amekuchagua wewe upate kujua mapenzi yake, na kumwona yule Mwenye haki, na kuisikia sauti itokayo katika kinywa chake.

15 Kwa maana utakuwa shahidi wake kwa watu wote, wa mambo hayo uliyoyaona na kuyasikia.

16 Basi sasa, unakawilia nini? Simama, ubatizwe, ukaoshe dhambi zako, ukiliitia jina lake”

Unaona? Kumbe Sifa zetu nzuri kwa Mungu miongoni mwa watu wanaotuzunguka, ni daraja zuri la Mungu kututumia kwa shuhuda zake nzito, lakini kama tutaitwa watumishi, halafu mitaani tuna shuhuda za matukio ya kizinzi, au tutajiita wakristo tuliookoka lakini mitaani tunajulikana kama wasengenyaji, au watukanaji, tunategemea vipi Mungu atutumie? Kama tutakuwa wakristo halafu kazini kwetu tunaiba, Mungu atatutumiaje kama alivyomtumia Danieli?

Kumbuka Danieli alikuwa mwaminifu sana katika kazi yake ya uwaziri mkuu kule Babeli, pamoja na kwamba alikuwa katika shughuli za kidunia lakini Mungu alimtumia, kutufikishia sisi maono makubwa ambayo mpaka sasa hivi yanatusaidia. Hiyo yote ni kwasababu alishuhudiwa na watu wote, ni mtu anayemcha Mungu. Nasi pia Kama tutaitwa wakristo halafu mitaani tunaonakena tumevaa nguo zisizo na heshima, watu watatuheshimuje?

Kumbuka sisi ni barua tunayosomwa na watu wote, biblia ndio inatuambia hivyo 2Wakorintho 3:2. Kama watu hawatatuheshimu, basi tujue kuwa Mungu ndio Zaidi.

Hivyo ni wajibu wetu, tubadilike, tuanze kujenga shuhuda zilizo hai, kwa watu wanaotuzunguka, tuweke kando mambo yote yanayotukwamisha. Vikao vya usengenyaji tujiepushe navyo, tabia za kidunia pia tujitenge nazo, Na kwa kufanya hivyo, kidogo kidogo, ndivyo tutakavyomvutia Mungu atutumie kama alivyofanya kwa Anania.

Bwana atusaidie sote.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

SIRI YA KUFANIKIWA KWA MTUME PAULO.

Tofauti kati ya lijamu na hatamu ni ipi kibiblia?

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA WARAKA WA PILI WA YOHANA.

YONA: Mlango 1

JE! NI WAPI UTAPOKEA HISIA ZA KWELI ZA KI-MUNGU?

Rudi nyumbani

Print this post

JINSI MTUME PAULO ALIVYOUTHAMINI WITO WAKE, JUU YA WENYE VYEO.

Kuna maneno haya ambayo mtume Paulo alisema..

Wagalatia 1:15 “Lakini Mungu, aliyenitenga tangu tumboni mwa mama yangu, akaniita kwa neema yake,

16 alipoona vema kumdhihirisha Mwanawe ndani yangu, ili niwahubiri Mataifa habari zake; mara sikufanya shauri na watu wenye mwili na damu;

17 WALA SIKUPANDA KWENDA YERUSALEMU KWA HAO WALIOKUWA MITUME KABLA YANGU; bali nalikwenda zangu Arabuni, kisha nikarudi tena Dameski”.

Tukisoma maneno hayo tunaweza kuona kuwa kipindi kile kulikuwa na utamaduni Fulani, kwamba ikitokea mtu ana wito wa kumtumikia Mungu, ni lazima kwanza, apande kwenda Yerusalemu (kanisa lilipoanzia), akaonane kwanza na wale mitume wa Bwana ambao ni nguzo, kama vile Petro, na Yohana, ili atambuliwe au awekwe kwanza chini ya mafundisho yao ndipo akatumike,Tukisoma maneno hayo tunaweza kuona kuwa kipindi kile kulikuwa na utamaduni Fulani, kwamba ikitokea mtu ana wito wa kumtumikia Mungu, ni lazima kwanza, apande kwenda Yerusalemu (kanisa lilipoanzia), akaonane kwanza na wale mitume wa Bwana ambao ni nguzo, kama vile Petro, na Yohana, ili atambuliwe au awekwe kwanza chini ya mafundisho yao ndipo akatumike,

Lakini tunamwona mtu kama Paulo alikuwa wa tofauti sana, yeye baada ya kuamini, hakujisumbua kwenda kutafuta kukaa chini ya watu hao wakubwa wenye vyeo, bali, aliondoka na kwenda zake mbali mahali panapoitwa Arabuni, kwa muda wa miaka mitatu huko akiutafuta uso wa Mungu.

Na hata aliporudi, biblia inatuambia hakusubiri kwanza akatambulike kwenye makanisa ya wakristo ndipo akahubiri injili, bali, alianza kuhubiri injili hivyo hivyo, wao walichosikia tu ni kwamba yule aliyeliharibu kanisa zamani sasa hivi anamuhubiri Kristo. Sio kwamba alikuwa anajionyesha yeye anajua Zaidi hapana, bali hakuona umuhimu wa kufanya hivyo, kana kwamba ni kitu cha lazima sana.

Wagaliatia 1:21 “Baadaye nalikwenda pande za Shamu na Kilikia.

22 Lakini sikujulikana uso wangu na makanisa ya Uyahudi yaliyokuwa katika Kristo;

23 ila wamesikia tu ya kwamba huyo aliyetuudhi hapo kwanza, sasa anaihubiri imani ile aliyoiharibu zamani.

24 Wakamtukuza Mungu kwa ajili yangu”.

Pengine walipomuona anafanya kazi kwa bidii wengine walianza kuulizana je, mnamtambua huyu kwenye makanisa yenu? Wengine wakasema hapana, hatumjui Je! Mitume kule Yerusalemu wanamtambua? Wanasema hapana hawamtambui? Sasa katokea wapi huyu na injili hii ya moto namna hii?

Lakini hilo halikumfanya Paulo asihubiri injili, kisa hatambuliwi na mitume ambao ndio nguzo, bali aliitenda kazi akimwangalia yeye aliyemwita yaani YESU KRISTO. Na baada ya miaka mingi sasa, kama 14 hivi ndipo tunamwona anapanda kwenda Yerusalemu kuonana na mitume, kusikiliza mausia kutoka kwao. Lakini anasema alipofika kule hawakumuongezea chochote badala yake alimkuta Mtume Petro amekwenda kinyume na Imani, na hivyo akamkemea mbele ya wote.

Wagalatia 2:6 Lakini wale wenye sifa ya kuwa wana cheo; (walivyokuwa vyo vyote ni mamoja kwangu; Mungu hapokei uso wa mwanadamu); nasema, hao wenye sifa hawakuniongezea kitu;…….

11 Lakini Kefa alipokuja Antiokia, nalishindana naye uso kwa uso, kwa sababu alistahili hukumu.

12 Kwa maana kabla hawajaja watu kadha wa kadha waliotoka kwa Yakobo, alikuwa akila pamoja na watu wa Mataifa; lakini walipokuja wao, akarudi nyuma akajitenga, huku akiwaogopa waliotahiriwa.

13 Na hao Wayahudi wengine wakajigeuza pamoja naye, hata na Barnaba pia akachukuliwa na unafiki wao.

14 Walakini, nilipoona ya kuwa njia yao haiendi sawasawa na ile kweli ya Injili, nalimwambia Kefa mbele ya wote, Ikiwa wewe uliye Myahudi wafuata desturi za Mataifa, wala si za Wayahudi, kwa nini unawashurutisha Mataifa kufuata desturi za Wayahudi?

Mpaka mwishoni kabisa mwa huduma yake, Paulo anashuhudia kwa uvuvio wa Roho kuwa yeye ndiye aliyefanya kazi kuliko hata mitume wengine wote waliomtangulia. Na sisi tunalithibitisha hilo.

Sasa habari hiyo inatufundisha nini sisi wa kanisa la leo.

Kumbuka wenye vyeo na wenye sifa waliojulikana zamani ni 12 tu, ndio wale mitume wa Bwana Yesu, lakini leo hii wenye vyeo na wenye sifa katikati ya kanisa la Mungu, idadi yake haihesabiki. Kiasi kwamba watu wengi wameshindwa kumtumikia Mungu, kisa tu, kuna ngazi zimewekwa hapo juu yao, ambazo ni lazima wazipitie kutoka kwa viongozi wao waliowatangulia au wapate kibali kwanza cha kufanya hivyo.

Ndugu sio lazima upokee kila agizo chini ya kasisi wako, ndio ni vizuri kufanya hivyo, ikiwa huwekewi vikwazo, au hutumii nguvu nyingi kutumika, lakini mara nyingi zinakwamisha huduma za watu wengi sana Mungu alizoweka ndani ya mioyo yao. Wakati mwingine utaambiwa pitia shule ya biblia miaka 4, ndipo uhitimu utumike.

Si kila kitu ni cha kutafuta kujiweka chini ya mtu Fulani kwanza, wakati mwingine Mungu anataka aanze kutembea  wewe peke yako, akufundishe wewe kama wewe. Maadamu nia yako ni njema kwake, na una lengo kweli la kuujenga ufalme wa Mungu hilo tu linatosha.  Kumbuka hiyo haimaanishi kuwa usijifunze kutoka kwa wengine hapana, lakini ujijengee akilini kuwa, Mungu amekuita umtumikie yeye, na si wanadamu.

Alilolichagua mtume Paulo, ndio hilo na likamsaidia sana,. Nasi pia tujitahidi kupunguza mizigo ya kuwategemea wanadamu, zama hizi ambazo watu wa namna hiyo wapo wengi, unaweza ukajikuta unadumaza huduma Mungu aliyoiweka ndani yako.. Wewe fanya utakuja kuwafuata baadaye.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

JINSI PAULO ALIVYOPAMBANA NA UJINGA WA ROHONI.

Makao ambayo Yesu alikwenda kutuandalia ni yapi?

Nini maana ya “Tumejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii”?

Kwanini Yesu aliwakataza mitume wake kumdhihirisha?

ANGALIENI MWITO WENU.

Rudi nyumbani

Print this post

Makao ambayo Yesu alikwenda kutuandalia ni yapi?

SWALI: Yesu alimaanisha nini kusema ninakwenda kuwaandalia makao? Ni makao yapi hayo alikwenda kutuandalia.


JIBU: Tusome,

Yohana 14 :1 “Msifadhaike mioyoni mwenu; mnamwamini Mungu, niaminini na mimi.

2 Nyumbani mwa Baba yangu mna makao mengi; kama sivyo, ningaliwaambia; maana naenda kuwaandalia mahali.

3 Basi mimi nikienda na kuwaandalia mahali, nitakuja tena niwakaribishe kwangu; ili nilipo mimi, nanyi mwepo”.

Makao ni mahali ambao mtu ataweza kutulia na kuendesha aidha maisha yake au kufanya shughuli zake kama alivyokusudia yeye mwenyewe kwa utulivu.. Mtu asiyekuwa na makao yoyote, (yaani haishi kwenye nyumba, au kibanda) utagundua kuwa maisha yake ni ya kutanga tanga leo utamwona huku kesho kule, leo utamsikia yupo mji huu, kesho ule..hiyo yote ni kwasababu hana mahali pa kutulia. Anakuwa kama mgeni duniani.

Sasa ndivyo ilivyo pia katika roho, Mungu alipomuumba mwanadamu, alikuwa ni roho kamili, lakini sasa alipokusudia mwanadamu huyu aishi hapa duniani, alimuundia na makao yake maalumu (yaani Nyumba ya roho yake) ambayo ndio mwili,. Sasa mwili huo unamsaidia, aweze kuishi, kutulia, na kuipumzisha roho yake akiwa hapa duniani.

Na ndio maana mwili unaitwa nyumba ya roho. Lakini pia kuna roho nyingine ambazo zipo hapa duniani, ambazo hazikuumbiwa makao,(yaani miili), na roho hizo ni mapepo, ambayo Mungu aliyatupa dunia baada ya kuasi zamani sana miaka mingi kabla ya mwanadamu kuumbwa.

Sasa hizi roho kwasababu hazina miili ya kutulia, huwa zinazurura zurura hapa duniani bila kazi yoyote, hivyo zinachofanya ni kufanya bidii zote, kutafuta makao, na ndio hapo zinawaingia wanadamu ambao wapo nje ya wokovu. Zikishawaingia mule ndio zinapata pumziko. Lakini zikiwa nje, hakuna raha yoyote, na ndio maana Bwana Yesu alisema..

Mathayo 12:43 “Pepo mchafu, amtokapo mtu, hupitia mahali pasipo maji, akitafuta mahali pa kupumzika, asipate.

44 Halafu husema, Nitarudi nyumbani kwangu nilikotoka; hata akija, aiona tupu, imefagiwa, na kupambwa.

45 Mara huenda, akachukua pamoja naye pepo wengine saba walio waovu kuliko yeye mwenyewe, nao huingia na kukaa humo; na mtu yule hali yake ya mwisho huwa mbaya kuliko ya kwanza. Ndivyo itakavyokuwa kwa kizazi hiki kilicho kibaya”.

Umeona hiyo ndio kazi yao..kwasababu hawana maskani (Nyumba /Miili), hivyo huwa wanafanya juu chini, wakimwingia mtu wasitoke na kwenda kuzurura zurura tu.

Kwahiyo, tunaweza kuona hapo, mwanadamu anazo maskani mbili Na zote hizo ni nguzo muhimu za kumsaidia kuishi hapa duniani.

Maskani ya kwanza ni mwili wake mwenyewe, ambao Mungu kamwekea roho yake ndani yake. Na maskani ya pili ni nyumba/kibanda, ambayo anaweza kutulia ndani yake na kuishi na kuendeleza maisha yake.

Vivyo hivyo na huko mbinguni.

Tutakapofika kule zipo maskani za aina mbili, maskani ya kwanza, itakuwa ni hiyo miili ya kimbinguni, na maskani ya pili, itakuwa ni makao, kama makao, miji na majumba ya sisi kuishi.

Sasa Bwana Yesu aliposema anakwenda kutuandalia makao, alimaanisha yote, makao ya roho zetu, na makao ya hiyo miiili tutakayoipokea huko mbinguni.

Kumbuka miili hiyo haitakuwa kama hii inayoona uharibifu, iliyotengenezwa kwa udongo, hapana bali miili hiyo imeundwa na Mungu mwenyewe, Isiyougua, isiyozeeka, isiyosikia njaa, isiyo sinzia, isiyochoka.. Bwana Yesu alirahisisha akasema tutafanana na malaika, Kama vile tunavyowaona malaika na sisi ndio tutakuwa hivyo.

2 Wakorintho 5 :1 “Kwa maana twajua ya kuwa nyumba ya maskani yetu iliyo ya dunia hii ikiharibiwa, tunalo jengo litokalo kwa Mungu, nyumba isiyofanywa kwa mikono, iliyo ya milele mbinguni.

2 Maana katika nyumba hii twaugua, tukitamani sana kuvikwa kao letu litokalo mbinguni;

3 ikiwa tukiisha kuvikwa hatutaonekana tu uchi.

4 Kwa sababu sisi tulio katika maskani hii twaugua, tukilemewa; si kwamba twataka kuvuliwa, bali kuvikwa, ili kitu kile kipatikanacho na mauti kimezwe na uzima:.

Umeona, hivyo, siku ile ya unyakuo, ndipo tutapokea miili hiyo mipya ya kimbinguni, lakini ni sharti kwanza turudishwe kwenye miili yetu hii ya udhaifu, kisha ivaliwe na ile mipya, ndio tuende mbinguni. unaweza kujiuliza ni kwanini Mungu afanye vile, anafanya hivyo ili kutimiza maandiko yake kuwa hata nywele za vichwa vyetu zimehesabiwa, hakuna hata kimoja kitakachopotea (Mathayo 10:30).

1Wakorintho 5:51 “Angalieni, nawaambia ninyi siri; hatutalala sote, lakini sote tutabadilika,

52 kwa dakika moja, kufumba na kufumbua, wakati wa parapanda ya mwisho; maana parapanda italia, na wafu watafufuliwa, wasiwe na uharibifu, nasi tutabadilika.

53 Maana sharti huu uharibikao uvae kutokuharibika, nao huu wa kufa uvae kutokufa.

54 Basi huu uharibikao utakapovaa kutokuharibika, na huu wa kufa utakapovaa kutokufa, hapo ndipo litakapokuwa lile neno lililoandikwa, Mauti imemezwa kwa kushinda”.

Pengine leo hii unaoudhaifu Fulani katika mwili wako, lakini ukifika kule, hutauona huo udhaifu.  Hivyo tukaze mwendo tuyafikilie hayo tuliyoandaliwa. Na hiyo Yerusalemu mpya wa kimbinguni, ambayo itakushuka kutoka kwa Mungu mwenyewe. Miji mizuri yenye kuvutia na kupendeza. Mambo ambayo jicho halijawahi kuona wala sikio kusikia.

Hayo ndiyo makao ambayo Bwana Yesu alikwenda kutuandalia sisi kwa miaka 2000 sasa.

Bwana atutie nguvu.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Ukoma wa nyumba ulifunua nini zamani?

JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?

JE UNAIFANYA KAZI YA MUNGU?

Mafundisho

Biblia ina maana gani inaposema akonyezaye kwa jicho huleta masikitiko?

Rudi nyumbani

Print this post

Biblia ilimaanisha nini watu wasitoe vizazi vyao kwa Moleki?

Moleki ni nani? Na Kwanini Mungu alikataza watu kutoa vizazi vyao na kuwapa Moleki?

Walawi 20: 1 Kisha Bwana akanena na Musa, na kumwambia,

2 Tena uwaambie wana wa Israeli, Mtu awaye yote miongoni mwa wana wa Israeli, au miongoni mwa wageni waketio katika Israeli, atakayetoa katika kizazi chake na kumpa Moleki, sharti atauawa; wenyeji wa nchi watampiga kwa mawe.


Moleki ni mungu aliyeabudiwa katika nchi ya kaanani na nchi za kando kando, kama vile Amoni, mungu  huyu alikuwa tofauti na miungu mingine ya kipagani, kama vile Baali, kwani huyu, alihitaji kafara za watu ili kuwapa watu mahitaji yao. Walichokuwa wanakifanya ni kuwapitisha watoto wao katika moto na kuwatoa kafara.

Jambo ambalo Mungu aliwaonya na kuwakataza sana, wana wa Israeli tangu wakiwa jangwani, kabla hawajaiingia hiyo nchi ya ahadi kwamba watakapofika wasijihusishe na miungu hiyo ya uongo kwa namna yoyote ile, kwani Mungu alijua watu wake watakutana nayo.

Utalisoma hilo tena katika..

Walawi 18:21 “Nawe usitoe kizazi chako cho chote na kuwapisha kwa Moleki, wala usilinajisi jina la Mungu wako; mimi ndimi Bwana”.

Lakini pamoja na hayo, wana wa Israeli waliyakaidi maagizo ya Mungu wakaanza kuiga taratibu hizo za kishirikina za kuwatoa watoto wao kafara. Jambo hilo tunaweza kuona lilianzana  kwanza na mfalme Sulemani, ambaye ndiye aliyekuwa wa kwanza kabisa kumjengea madhabahu  mungu huyo katika Israeli, na hivyo ikawa chukizo kubwa sana. Na hiyo ndio ilikuwa sababu ya Mungu, kumshusha viwango mfalme Sulemani.

1Wafalme 11:7 “Sulemani akamjengea Kemoshi, chukizo la Wamoabi, mahali pa juu, katika mlima uliokabili Yerusalemu, na Moleki, chukizo la wana wa Amoni”.

Mambo hayo waliendelea kufanyika Israeli kwa kipindi kirefu, wengine wakidhani kuwa ni Mungu kaagiza, au kwamba Mungu ndio anavutiwa na kafara hiyo kuliko ya mbuzi na kondoo. Lakini hawakujua kuwa ni mambo ambayo yalikuwa ni machukizo makubwa sana kwa Mungu.

Yeremia 32:35 “Tena walijenga mahali palipoinuka kwa Baali, palipo katika bonde la mwana wa Hinomu, ili kuwapitisha wana wao na binti zao katika moto kwa ajili ya Moleki, jambo nisilowaagiza; wala halikuingia moyoni mwangu kwamba walitende chukizo hilo; wapate kumkosesha Yuda”.

Ni nini Bwana anataka tujifunze kwa watu hawa?

Kuchanganya desturi za miungu ya kipagani na ibada za Mungu muumba wa mbingu na nchi, ni mambo ambayo yanaendelea hata sasa hivi katika agano jipya.

Kwamfano kitendo cha kuweka sanamu za watakatifu walitaongulia, na kuabudu kupitia hizo, kufuatana na desturi zao, ambazo hazipo katika maandiko, ni machukizo makubwa sana. Kusali Rozari, ni machukizo kwa Mungu, vilevile kudhani kuwa wapo wapatanishi wengi kati ya Mungu na wanadamu, na Yesu ni mmojawapo tu ya wapatanishi hao,hayo ni makufuru mbele za Mungu. Kwani biblia inasema mpatanishi kati ya Mungu na mwanadamu ni mmoja tu, naye ni Yesu Kristo hakuna mpatanishi mwingine.

Hivyo ni lazima tuwe makini sana na tunachokiabudu, kwasababu hapo ndipo wivu wa Mungu unapolala. Tukijifanya hatuoni, tujue kuwa Mungu hatauvumilia upumbavu wetu, kama alivyofanya kwa wana wa Israeli. Kwasababu yeye mwenyewe ametuita tumwabudu katika Roho na Kweli na si katika ujinga na upagani.

Jina la Bwana libarikiwe.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Maashera na Maashtorethi ni nini?

Je! Bikira Maria ni MALKIA WA MBINGUNI?

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 2

Vyombo vya uzuri ni vipi vinavyotajwa katika biblia?

Rudi nyumbani

Print this post

NA VIUNGO VYETU VISIVYO NA UZURI VINA UZURI ZAIDI SANA.

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe,  Nakukaribisha katika kujifunza elimu ya ufalme wa mbinguni. Kumbuka kila habari katika biblia inayo ujumbe fulani nyuma yake. Hakuna habari isiyo na maana.

Leo kwa ufupi tutatazama habari ya mwamuzi mmoja aliyeitwa, Ehudi. Sasa wakati tunakwenda kutafakari habari zake naomba ufahamu kuwa Lengo la somo hili, ni kuamsha ile karama iliyo ndani yako ili  itende kazi..

Kuna wakati wana wa Israeli walimkosea sana Mungu, hivyo Mungu akawaweka chini mkono wa adui yao aliyeitwa Elgoni mfalme wa Moabu kwa muda wa miaka 18. Lakini walipomlilia Mungu, Mungu akawasikia  na kuwatumia huyu mwamuzi aliyeitwa Ehudi.

Biblia inatuambia Ehudi alikuwa ni mtu anayetumia SHOTO. Sasa biblia mpaka iandike habari kama hizo za mkono mtu anaotumia, inamaana kuwa lipo jambo la kujifunza. Ukisoma habari yenyewe pale utaona walimchukua huyu na kumpeleka kwa huyo mfalme wa Moabu ili awasilishe tunu zao ambazo walikuwa wanazipeleka kwa huyo mfalme mara kwa mara.

Sasa siku alipoenda, aliundaa upanga mrefu, kisha akauficha kwenye paja lake la kulia. Na alipofika mbele ya askari wake akazitoa zawadi hizo mbele yao..Lakini alipomalizia, hakuondoka bali aliomba aongee na mfalme faragha, kana kwamba kuna ujumbe amepewa na wakuu wa Israeli utokao kwa Mungu, amwambie, hivyo haipasi kila mtu asikie.

Ndipo mfalme akamchukua peke yake katika ukumbi wake, akawaondoa askari wake, akafunga milango. Sasa biblia inatuambia huyu Elgoni alikuwa ni mtu mkubwa sana, mwenye mraba minne, kiasi kwamba ili kumdondosha mtu kama huyo ilihitaji watu wengi, na sio mmoja tena wenye nguvu.

Lakini Mungu alilijua hilo,  na ndio maana akawatumia mtu kama Ehudi anayetumia shoto na si kilia ili kumdondosha huyo.

Kama tunavyosoma habari, aliutoa ule upanga wake, na kwa nguvu aliuzamisha kwenye Tumbo lake, ambalo pengine lilikuwa limefunikwa kwa nguo nzito, lakini upanga  ule ulipita kwa jinsi zile nguvu zilivyokuwa nyingi, kisha ukaenda kushikamana na mafuta ya tumboni na kutokea upande wa pili.. Lakini ni heri tu ungeingia upanga peke yake, biblia inasema, mpaka ule upini wa upanga ulizama ndani kabisa, usionekane. Jambo ambalo si rahisi hata kidogo kwa mtu kuuzamisha upini kwenye tumbo. Inahitaji presha kubwa sana ya kusukuma, ambayo kwa nguvu za kawaida za kibinadamu haiwezekani.

Waamuzi 3:21 “Ehudi akaunyosha mkono wake wa kushoto, akaushika huo upanga kuutoa hapo katika paja lake la kuume, akamtia tumboni mwake;

22 hicho kipini nacho kikaingia ndani pamoja na huo upanga wenyewe; nayo mafuta yakashikamana tena juu ya upanga, kwani hakuutoa tena upanga tumboni; nao ukatokea kwa nyuma”.

Unaona, ukisoma tena, utaona tena hata katika vita zamani, wana wa Israeli waliwachagua mashujaa wanaotumia shoto, kwasababu aliweka uwezo mkubwa sana wa shabaha ndani yao.

Waamuzi 20:15 “Hao wana wa Benyamini walihesabiwa siku ile kutoka hiyo miji, watu waume ishirini na sita elfu waliotumia upanga, zaidi ya hao waliokaa Gibea, ambao walihesabiwa watu wateule mia saba.

16 Katika watu hao wote walikuwako watu waume mia saba waliochaguliwa, wenye shoto; kila mmoja alikuwa anaweza kuutupia unywele mawe kwa teo, wala asikose”.

Tukiyafahamu haya turudi sasa katika kiini cha ujumbe wetu wa leo, kwasababu lengo sio kueleza umahiri wa watu wanaotumia shoto au kulia, hapana. Bali ni kutufundisha sisi mambo ya rohoni yahusuyo wokovu wetu.

Kumbuka mkono huu wa kushoto huwa haupewi heshima, wala hauwezi kutumiwa sehemu zote, hauwezi kutumia kulia chakula, au kumpia mtu mkono, n.k. Lakini uwezo na nguvu Mungu alioupa unazidi hata ule wa kulia.

Hiyo ni kuonyesha pia, Mwili wa Kristo unao viungo vingi, vingine Mungu amevikusidia kabisa vipewe  heshima, lakini vingine Mungu amevikusudia pia visiwe na heshima yoyote, lakini vimepewa nguvu na ufasaha wa hali ya juu.

1Wakorintho 12:23 “Na vile viungo vya mwili vidhaniwavyo kuwa havina heshima, viungo vile twavipa heshima zaidi; na viungo vyetu visivyo na uzuri vina uzuri zaidi sana.

24 Kwa maana viungo vyetu vilivyo na uzuri havina uhitaji; bali Mungu ameuungamanisha mwili, na kukipa heshima zaidi kile kiungo kilichopungukiwa;

25 ili kusiwe na faraka katika mwili, bali viungo vitunzane kila kiungo na mwenziwe”

Umeona? Ni lazima tufahamu si kila mtu atakuwa mchungaji, si kila mtu atakuwa mtume, si kila mtu atakuwa nabii, si kila mtu atakuwa mwalimu, zipo karama nyingi nzito na zenye nguvu  ambazo watu wanazo lakini wamezizimisha ndani yao kwasababu  wanachofikiria tu ni kuwa pale watakapokuwa wakristo basi ni kwenda kuwa wachungaji, au mitume au watu fulani maarufu wanaojulikana.

Na ndio maana karama nyingi za kipekee kama za miujiza, uponyaji, karama za ufasiri wa lugha, karama za faraja, za kukirimu n.k. hazionekani au zimekufa kabisa katika kanisa, kwasababu hatuziangalii hizo sote tunataka tukawe mitume, wachungaji na manabii.

Ukiona lipo jambo linaamka ndani yako kwa ajili ya Mungu, ambalo pengine lipo tofauti na wengine na unaona kabisa  linakupa furaha kulifanya, usilizimishe, lifanye hilo kwa bidii kwasababu huo ndio mwanzo wa kuijua karama yako. Na Mungu ameiweka hiyo ndani yako ili ilisaidie kanisa kwa sehemu kubwa sana. Fanya kile kitu kinachougua ndani yako sana.. Kama ni kumtolea Mungu, basi mtolee sana, kama ni kufundisha basi fundisha sana, kama ni kufanya uinjilisti ufanye huo kwa bidii, kama Mungu anakuonyesha mambo ya rohoni, yachochee hayo ili yakawe faida kwa mwili wote wa Kristo.

Kumbuka hakuna kiungo kisichokuwa na kazi  kanisani, maadamu umeokoka na umejazwa Roho, umuhimu wake ni lazima utaonekana tu. Lakini kazi ya kiungo ni ngumu kuonekana kama kitakuwa chenyewe chenyewe, hivyo kaa na watakatifu wengine, ndipo hapo utajua kwa urahisi karama yako ni ipi. Karama nyingine haziwezi kufanya kazi kama zitakaa zenyewe nyumbani,

Jitahidi ujue nafasi yako ni ipi ili umtumikie Mungu katika hiyo. Kwasababu kila mmoja wetu anatarajiwa na Bwana amzalie matunda.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

NITAIFAHAMU VIPI KARAMA YANGU?.

NINI TOFAUTI KATI YA KARAMA, UTENDAJI KAZI NA HUDUMA.

Vyombo vya uzuri ni vipi vinavyotajwa katika biblia?

USINIE MAKUU.

Neno “Via” linamaanisha nini katika biblia?

Nini maana ya msiwe waalimu wengi (Yakobo 1:3)?

Mchokoo ni nini katika maandiko? (Matendo 26:14)

Rudi nyumbani

Print this post

Kama Musa aliandika vitabu vya torati, Je! kifo chake alikiandikaje mule?

SWALI: Ukisoma kitabu cha kumbukumbu la torati sura ya 34 unaona Musa anakufa na kitabu kinaendelea kuandika mpaka kifo chake, je huoni kuwa ni makosa kusema vitabu vitano vya kwanza vya Biblia vimeandikwa na Musa? maana mtu hawezi kuelezea kifo chake kuwa amekufa lini na kuzikwa lini?asante.


JIBU: Kuhusu uandishi wa Musa juu ya kifo chake, pia hilo linawezekana, kumbuka Musa alikuwa ni mtu ambaye alikuwa karibu sana na Mungu, hivyo Mungu kumfunulia mambo yajayo sio jambo la kushangaza sana, kama aliweza kumfunulia mambo yaliyopita, tangu Adamu, na mambo yote yaliyotendeka pale Edeni, mpaka Nuhu na Gharika yake, mpaka sodoma na Gomora, angeshindwaje kumfunulia kifo chake na kukiandika?

Lakini pia, inawezekana, waandishi wengine walimalizia kitabu hicho kwenye ile sura ya  34, kama vile Yoshua, ambaye alikuwa  karibu sana na Musa, au Eleazari, ambaye alikuwa mtoto wa Haruni,mkuu wa kabila la lawi, mwingine ni  Samweli, au Ezra.

Hivyo Kwa vyovyote vile, tunapaswa tujue biblia ni kitabu kilichovuviwa na Roho Mtakatifu, na hivyo yapo matukio ambayo waandishi wake tunaweza tusiwajue moja kwa moja kwasababu lengo la kitabu kile sio kuwaeleza wao, bali ni ule ujumbe uliopo ndani yake.

Hivyo cha muhimu ni Bwana azidi kutupa macho ya kuyaelewa yote yaliyoandikwa ndani yake.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Mada Nyinginezo:

Rudi nyumbani

Print this post

nini maana ya kujikana nafsi na kujitwika msalaba?

SWALI: Bwana Yesu asifiwe. Naomba ya nifafanulie juu ya “kujikana mwenyewe” na “kujitwika msalaba” wako inamaanisha nifanye nini hasaa?


JIBU: Tusome..

Marko 8:34 “Akawaita mkutano pamoja na wanafunzi wake, akawaambia, Mtu ye yote akitaka kunifuata na ajikane mwenyewe, ajitwike na msalaba wake, anifuate.

35 Kwa kuwa mtu atakaye kuiponya nafsi yake, ataiangamiza, na mtu atakayeiangamiza nafsi yake kwa ajili yangu na kwa ajili ya Injili, huyu ataisalimisha.

36 Kwa kuwa itamfaidia mtu nini kuupata ulimwengu wote, akipata hasara ya nafsi yake?

37 Ama mtu atoe nini badala ya nafsi yake”?

Kujikana ni kukataa mapenzi yako na kukubali kufuata yale ya Mungu, haijalishi yatakuwa hayakupendezi au hayakufai kwa wakati huo namna gani.

Pale ambapo, Mungu anataka ufanye hivi, na wewe unaona nafsi yako haitaki kukifanya, kwasababu moja au nyingine. sasa kule kutii cha Mungu na kukataa cha kwako huko ndiko kujikana nafsi.

Kwamfano Mungu anaposema wanawake wavae mavazi ya kujisitiri,(1Timotheo 2:9) na wewe ni mvaaji mzuri wa nguo zinazochora maungo na zile za kiume, sasa unapokubali kutii yale ya Mungu, ukaanza kuvaa magauni, bila kujali nafsi yako inakuambia utakuwa mshamba, au watu watakuambia hupendezi, huko ndiko kujikana nafsi.

Au pale Mungu anapokuambia, kiungo chako kimoja kikikukosea kikate, kuliko mwili mzima kutupwa jehanamu, na kama tunavyojua kiungo ni kitu kinachojishikamanisha na wewe. Na vitu vinavyojishikamanisha na maisha yetu ni vingi, vingine vizuri, vingine vibaya, sasa pale ambapo, pengine  marafiki ulionao wanakukosesha, na kuchukua uamuzi wa kukata nao mazoea, na kuanza kutafuta marafiki wenye malengo na kimbingu na wewe, hapo ndipo umejikana nafsi.

Unapoacha, miziki ya kidunia, au kukesha kwenye muvi na kuchati  kwenye mambo yasiyokuwa na maana, na kuutumia muda huo kumtafakari Mungu, au kumtafuta yeye, huko ndiko kujikana nafsi Bwana Yesu anakokuzungumzia.

Pia Kujitwika msalaba, ni ishara ya kukubali dhiki kwa ajili ya Kristo. Kumbuka msalaba ni kitu ambacho Yesu alikibeba na kwenda kusulubishwa kwa hicho. Sio kitu ambacho alikwenda kukilalia. Ni sawa na mtu leo hii akuambie jivike mabomu yako, uende sehemu ya kujilipua.

Hivyo na sisi ili tuwe wanafunzi wa Kristo kweli, hatuna budi pia kukubali mashutumu na wakati mwingine kupitia dhiki kwa ajili ya jina lake. Hapo ndipo tutakuwa tumeonyesha tumeibeba misalaba yetu kweli kweli. Alama ya misumari yetu.

Biblia inasema..

2Timotheo 3:12 “Naam, na wote wapendao kuishi maisha ya utauwa katika Kristo Yesu wataudhiwa”.

Wafilipi 1:29 “Maana mmepewa kwa ajili ya Kristo, si kumwamini tu, ila na kuteswa kwa ajili yake;”

Na pia Bwana Yesu alisema..

Yohana 15:20 “Likumbukeni lile neno nililowaambia, Mtumwa si mkubwa kuliko bwana wake. Ikiwa waliniudhi mimi, watawaudhi ninyi; ikiwa walilishika neno langu watalishika na lenu”.

Hiyo ndio maana ya kujikana nafasi na kujitwika msalaba wako.

Bwana atujalie tuwe na moyo huo.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

YESU ANAKWENDA KUIBADILISHA OFISI YAKE.

ESTA: Mlango wa 4

MWANZO WA INJILI YA YESU KRISTO.

UFUNUO NI NINI, NA NITAPOKEAJE UFUNUO KUTOKA KWA MUNGU?

PINDO LA VAZI LAKE SASA LIMEREFUSHWA.

Rudi nyumbani

Print this post

YESU ANAKWENDA KUIBADILISHA OFISI YAKE.

Mungu anayo agenda, na usipojua agenda ya Mungu katika siku hizi za mwisho ni ngumu sana kuiona ile ng’ambo, Leo hii tunaishi maisha ya juu juu tu kwasababu hatujamjua YESU ni nani na tabia zake ni zipi kulingana na majira ya wakati.

Tunapenda kumjua tu katika ule upande wake mmoja, wa upole na unyenyekevu (Mathayo 11:29)..Lakini hatujui ule upande mwingine ambao anasema yeye ni MKEMEAJI, na MKANAJI, na MFUKUZAJI na MUUAJI WA WAOVU. Ikiwa leo hii hatutamwamini, halafu tukafa, au siku ile ya mwisho ikatukuta tupo katika njia zetu wenyewe, tujue kuwa tabia tutakazoziona kwake kipindi hicho zitatustaajabisha sana, tena sana.

Kanisa hili la mwisho tunaloishi linaloitwa Laodikia, ndio kanisa pekee kati ya yale saba, ambalo Bwana amelikemea vikali, kwa tabia zake, za kuwa vuguvugu.. Hii ikiwa na maana kuwa mimi na wewe kama tupo katika uvuguvugu huu uliopo sasa hivi duniani tujue kuwa tupo katika Hasira ya Kristo, ya kwenda kutapikwa.

Uvuguvugu wa kusema mimi nimeokoka, lakini maisha yako hayauhakisi wokovu ule wa kimaandiko, ndio tabia ya kanisa hili la mwisho ilivyo, mamilioni ya wakristo ndio hivyo walivyo leo hii. Jambo ambalo halikuwepo miaka ya zamani, ambayo watu hawakumchanganya Mungu na uovu, waliookoka walijulikana, waliokuwa waovu walijulikana. Hakukuwa na mtu aliyeshiriki meza ya Bwana na wakati huo huo ni mzinzi au mlevi, mtu anakwenda ibadani, halafu kesho pia anakwenda disco, hayakuwepo hayo. Waovu walijitenga, na watakatifu waliookolewa walijitenga, Lakini leo hii ni kawaida sana, kusikia hata mmiliki bar anasema ameokoka.

Ufunuo 3:15 “Nayajua matendo yako, ya kuwa hu baridi wala hu moto; ingekuwa heri kama ungekuwa baridi au moto.

3.16 Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa changu.

17 Kwa kuwa wasema, Mimi ni tajiri, nimejitajirisha, wala sina haja ya kitu; nawe hujui ya kuwa wewe u mnyonge, na mwenye mashaka, na maskini, na kipofu, na uchi.

18 Nakupa shauri, ununue kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto, upate kuwa tajiri, na mavazi meupe upate kuvaa, aibu ya uchi wako isionekane, na dawa ya macho ya kujipaka macho yako, upate kuona.

19 Wote niwapendao mimi NAWAKEMEA, na kuwarudi; basi uwe na bidii, ukatubu.

20 Tazama, nasimama mlangoni, nabisha; mtu akiisikia sauti yangu, na kuufungua mlango, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye pamoja nami”.

Lakini pia hakemei tu peke yake, kuna siku atasimama KUWAKANA na kuwaonea aibu watu wengi sana, mbele ya Baba yake, na mbele ya  maelfu ya malaika zake huko mbinguni. Ikiwa leo hii unamwonea Kristo aibu unaogopa kuitwa mlokole, unaogopa kuvaa vizuri mavazi ya kujisitiri kisa utaitwa mshamba, unaona aibu kumtumikia Mungu wako, siku ile utakuonea aibu na wewe kweli kweli, hata hatapeleka jicho lake kukangalia.. wakati wengine akiwapongeza na kuwasifia.wewe utakuwa kama mtu baki tu.

Marko 8:38 “Maana kila mtu atakayenionea haya mimi, na maneno yangu, katika kizazi hiki cha uzinzi na dhambi, Mwana wa Adamu atamwonea haya mtu huyo, atakapokuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika watakatifu”.

Halikadhalika na kumkana vivyo hivyo, naye pia atakukana siku ile.

Kama hilo halitoshi Bwana Yesu pia anasema, atawafukuza watu wengi sana, siku ile, sio wachache, bali wengi sana. Na watakaofukuzwa sio watu wasiomjua Kristo bali, ni sisi sisi tuliopo kanisani, tunaolitumia jina lake kutenda miujiza lakini hatutaki kuishi maisha yampendezayo yeye. Tunapenda maisha ya uvuguvugu.

Mathayo 7:22 “Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi?

23 Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu”.

Biblia bado inatuonyesha siku ile atakapotokea mawinguni atawaua wanadamu wengi sana watakaokuwa wameipokea ile chapa ya mnyama na kufanya vita naye..

Ufunuo 19:13 “Naye amevikwa vazi lililochovywa katika damu, na jina lake aitwa, Neno la Mungu.

14 Na majeshi yaliyo mbinguni wakamfuata, wamepanda farasi weupe na kuvikwa kitani nzuri, nyeupe, safi.

15 Na upanga mkali hutoka kinywani mwake ili awapige mataifa kwa huo. Naye atawachunga kwa fimbo ya chuma, naye anakanyaga shinikizo la mvinyo ya ghadhabu ya hasira ya Mungu Mwenyezi.

16 Naye ana jina limeandikwa katika vazi lake na paja lake, MFALME WA WAFALME, NA Bwana WA MABwana”.

Unaweza kuona jinsi mwonekano wa Bwana utakavyokuwa wa tofauti sana wakati ule?. Ndio hapo utakapojua ni kwanini biblia inasema mataifa watamwombolezea, kwasababu hatakuja tena na sura ya upole kama wengi wetu tunavyodhani, bali atakuja na jina jipya la kifalme, la kuteka na kutawala, la kutiisha lenye nguvu nyingi. Sio tena la kuokoa mtu.

Lakini kwa upande wa pili, kwa wale waliomtii, waliokubali kutembea katika njia zake, anasema atawakiri, na kuona fahari kwa ajili yao mbele za Mungu na za malaika wake, vilevile atawapa mamlaka ya kutawala pamoja naye kama wafalme, Na atawafuta machozi watakatifu wake wote.

Hivyo ndugu, leo hii Kristo bado kaketi kama mwana-kondoo, aliyechinjwa, mpole, mnyenyekevu, aokoaye, anakuvuta kwa upole mwingi kwake, ili usiopote katika aungamivu wa ulimwengu. Angalia wakati huu umebakia mchache sana, kabla ya yeye kwenda kubadilisha ofisi yake. Kwanini usitubu umrudie muumba wako?

 Damu yake bado ipo kukuokoa, na kukusamehe kabisa, mkaribishe leo kwenye moyo wako, akupe uwezo mpya wa kuushindwa huu ulimwengu. Pengine ulishamwamini au kumpokea lakini umekuwa mkristo vuguvugu mkristo jin, jambo ambalo ndio halitaki kabisa, amelikemea, hivyo toka kwenye huo uvuguvugu wako, toka katika udhehebu, mfuate Yesu kweli kweli, ondoa vizuizi vyote vinavyokufanya usiwe safi mbele za Mungu.  Na yeye mwenyewe atakutengeneza na kukufanya uwe tayari kwa ajili ya kwenda kwenye unyakuo ambao upo karibuni kutokea.

Natumai sote tutaanzana kuuonyesha mabadiliko mapya. Kabla ya mabadiliko yake hayajajidhihirisha kwetu.

Bwana akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

KARAMU YA MWANA-KONDOO.

UFUNUO: Mlango wa 2 part 3

UFUNUO: Mlango wa 14

ESTA: Mlango wa 8, 9 & 10. (SIKU KUU YA PURIMU)

UFUNUO: Mlango wa 19

Rudi nyumbani

Print this post

Neno Maganjo linamaanisha nini katika biblia?

Maganjo ni kitu kilichoharibiwa, kwa mfano jengo likiharibiwa labda tuseme kwa  kombora, lile gofu linalobakia ndio maganjo. Au mji unapochomwa moto, yale masalia salia ya mji, ndio maganjo.

Mungu amekuwa akitumia Neno hili kuonyesha jinsi adhabu yake itakavyokuwa kwa wasiomcha yeye.

Hivi ni baadhi ya vifungu ambavyo utaweza kukutana na Neno hilo;

Walawi 26:30 “Nami nitapaharibu mahali penu palipoinuka, na kuziangusha sanamu zenu za jua, nami nitaitupa mizoga yenu juu ya mizoga ya sanamu zenu; na roho yangu itawachukia.

31 NAMI NITAIFANYA MIJI YENU IWE MAGANJO, na mahali penu patakatifu nitapatia ukiwa; wala sitasikia harufu ya manukato yenu yapendezayo.

32 Nami nitaitia hiyo nchi ukiwa; na adui zenu watakaokaa huko wataistaajabia”.

Ezekieli 6:14 “Nami nitanyosha mkono wangu juu yao, na kuifanya nchi kuwa MAGANJO, tena ukiwa mbaya kuliko jangwa upande wa Dibla, katika makao yao yote; nao watajua ya kuwa mimi ndimi Bwana”.

Yeremia 51:42 “Bahari imefika juu ya Babeli, Umefunikwa kwa wingi wa mawimbi yake.

43 Miji yake imekuwa MAGANJO; Nchi ya ukame, na jangwa; Nchi asimokaa mtu ye yote, Wala hapiti mwanadamu huko”.

Yeremia 4:7 “Simba ametoka katika kichaka chake, ndiye aangamizaye mataifa; ameanza kushika njia, ametoka katika mahali pake; ili aifanye nchi yako kuwa ukiwa, miji yako ifanywe MAGANJO, asibaki mwenyeji ndani yake. 8 Kwa sababu hiyo jifungeni nguo za magunia; ombolezeni na kulia kwa uchungu; kwa maana hasira kali ya Bwana haikugeuka na kutuacha”.

Som pia Ezekieli 12:20, 29:12, Amosi 9:14

Hata sasa, huu ulimwengu, utakwenda kufanywa maganjo kipindi si kirefu, haijalishi umejengwa vizuri kiasi gani, haijalishi umeshafikia hatua ya kuwa ustaarabu mzuri namna gani,..Bwana Yesu alisema kuwa hakuna jiwe litakalosalia juu ya jiwe. Kila kitu unachokiona leo hii kitateketezwa, siku ile ya Bwana itakapofika. Kila kitu kitafumuliwa, moto utaisafisha kweli kweli hii dunia, kama vile gharika ilivyoisafisha dunia ya kwanza wakati ule wa Nuhu.

Soma.

2Petro 3:10 “Lakini siku ya Bwana itakuja kama mwivi; katika siku hiyo mbingu zitatoweka kwa mshindo mkuu, na viumbe vya asili vitaunguzwa, na kufumuliwa, na nchi na kazi zilizomo ndani yake zitateketea.

11 Basi, kwa kuwa vitu hivi vyote vitafumuliwa hivyo, imewapasa ninyi kuwa watu wa tabia gani katika mwenendo mtakatifu na utauwa,

12 mkitazamia hata ije siku ile ya Mungu, na kuihimiza; ambayo katika hiyo mbingu zitafumuliwa zikiungua, na viumbe vya asili vitateketea na kuyeyuka”?

Swali ni je! Mimi na wewe tumeekeza wapi maisha yetu?  Je ni duniani au mbinguni?..Kumbuka duniani ni tunapita, yapo maisha ya milele huko mbeleni yanatungojea.. Ni wajibu wetu kutambua lililo la muhimu kwanza, ambalo ni wokovu wetu, Lengo la Mungu kuifanya hii dunia kuwa maganjo si kwamba ni mbaya hapana, bali sisi ndio tumeifanya kuwa mbaya kwa dhambi zetu, na hivyo ni lazima iteketezwe tu.

Hivyo sisi sote tusiwe washirika wa hiyo ghadhabu ya Mungu. Kumbuka Unyakuo upo mlangoni. Na haya mambo hatutashangaa kuyaona yakitimia hata kwenye kizazi chetu.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Pomboo ni nini katika biblia?(Kutoka 25:5, Ezekieli 16:10)

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 2

KWA WALE WALIO NJE “YOTE” HUFANYWA KWA MIFANO.

UFUNUO: Mlango wa 14

Sodoma ipo nchi gani?

Rudi nyumbani

Print this post