SWALI: Kwanini Bwana Yesu, aliruhusu yale mapepo yawaingie nguruwe, kwanini asingeyatoa tu na kuyaacha yaende sehemu nyingine mbali na wale nguruwe, kwani kufanya vile si ni kama aliharibu biashara au mali za wengine?
JIBU: Kulikuwa na sababu kuu mbili kwanini lile tukio litendeke vile:Sababu ya kwanza ni kwasababu yale mapepo yenyewe yalimwomba Bwana yawaingie wale nguruwe..Na sababu ya pili ambayo ndio kuu, ni ili Mungu atengeneze ushuhuda wenye nguvu zaidi utakaoweza kuwavuta wanadamu wengi watubu kirahisi.
Kumbuka kuwa pale awali, Yesu alipoliuliza lile pepo jina lako ni nani..lilijibu na kusema jina langu ni LEGIONI kwasababu tupo wengi..Na Legioni kwa zamani lilikuwa ni jeshi lenye askari si chini ya 82,000..Hivyo piga hesabu mapepo yaliyokuwa ndani ya Yule mtu hayakupungua idadi hiyo, jaribu kufiria jambo hiyo si rahisi kuamini na wengi kama lingewezekana mtu kuwa na idadi kubwa ya mapepo namna hiyo .
Hivyo Yesu kuona vile, kuwa wameomba jambo ambalo litaufanya ushuhuda uwe na nguvu zaidi, na kwamba kwa kupitia huo utawahakikishia kuwa mapepo kweli yapo, na kwamba yanaweza kumuingia mtu kwa wingi wa idadi ile, na kwamba yanaweza kumvaa mtu na kumfanya afanye vitu ambavyo yeye mwenyewe hajataka kuvifanya ikiwemo hata kujiua..Ndio akaruhusu yawaingie wale nguruwe ambao walikuwa 2,000,.Ambayo kwa hesabu za haraka haraka nguruwe mmoja aliingiwa na mapepo si chini ya 40,..aliruhusu hivyo ili watu waone kwa macho yao, kwamba mapepo yapo na jinsi mapepo yakimwingia mtu yanavyomfanya na yanapompelekea mwishoni..MAUTINI..Kwahiyo kwa tukio lile ndipo tulipofahamu kuwa mapepo sio nadharia bali ni vitu halisi kabisa…
Hivyo wale wachungaji walivyoshuhudia kitendo kile tu, waliondoka na kwenda kuhubiri mashambani na na vijijini matendo makuu waliyoyaona kwa macho yao, ndipo wale watu waliohubiriwa na wachungaji pia wakaja kushuhudia kwa macho yao..kuona wale nguruwe wakielea ziwani wote wamekufa, na mtu Yule ni mzima kabisa wataachaje kuamini?…Kwasababu hakuna mtu mwenye nguvu ya kwenda kukamata nguruwe 2000 na kuwazamisha baharini..ni lazima kuna nguvu nyingine ya zida imehusika hapo.
Vile vile na Yule mtu aliyekuwa kichaa alipokwenda kuhubiri na kutoa ushuhuda ule mzito sio ajabu biblia inatuambia alipoenda kuhubiri huko Dekapoli watu wote WALISTAAJABIA, walichokistaajabia ni nini kama sio huu ushuhuda wa nguruwe kuingiliwa na mapepo?. Na hapo pia bila shaka wengi walitubu kwa kupitia ule. (Soma Marko 5:12-20)..Kama vile ulivyokuwa ushuhuda wa Nabii Yona…watu waliposikia jinsi alivyokaa tumboni mwa samaki siku tatu bila kufa..wakaamini na kutubu kwa ishara ile.
Hivyo hata leo hii, Kristo anaweza kuruhusu mtu apate hasara Fulani ili uwe ushuhuda wa kuwaponya watu wengine. Shetani alimwomba Mungu ampige Ayubu, kama tu haya mapepo yalivyoomba ruhusa Bwana Yesu kuiharibu mifugo ya wengine..Lakini kwa kupitia maisha ya Ayubu sisi leo hii tunaponyeka. Hivyo si kila adhabu ambayo hukustahili inapokupata, ikufanya umchukie Mungu, mengine ni kwa utukufu wa Mungu, zaidi zidi tu kusonga mbele maadamu wewe bado ni mwana wa MUNGU.
Ubarikiwe.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mafundisho mengine:
Mada Nyinginezo:
Kurudi Nyuma kiimani maana yake nini?..Nitapokeaje nguvu ya kushinda dhambi?
Shalom, Jina la Bwana wetu Yesu Kristo lizidi kubarikiwa..Karibu tujifunze maandiko.
Swali la kujiuliza leo ni nini maana ya kurudi nyuma…Mtu mmoja ukikutana naye na ukapata bahati ya kumwuliza je umeokoka?..Atakuambia ndio niliokoka ila nimerudi nyuma…Ukizidi kumwuliza je umerudi nyuma kwa namna gani atakwambia…Tamaa za kimwili zilinizidia hivyo nikajikuta ninarudi nyuma na kuangikia katika uasherati
Kama jambo hili unalipitia na wewe ndugu yangu wa thamani nataka leo hii nikuambie kuwa hukurudi nyuma…bali ulikuwa hujaokoka kabisa!…hivyo unapaswa uokoke. Leo nitakuambia mtu aliyerudi nyuma anakuwaje..
Mtu ambaye amempokea Yesu Kristo kikamilifu kama Bwana na mwokozi wa maisha yake, na kudhamiria kabisa kuuacha ulimwengu kwa vitendo, na kubeba msalaba wake na kumfuata Yesu na kwenda kubatizwa katika ubatizo sahihi…Mtu wa namna hiyo anakuwa tayari ameshaokoka..Na katika ulimwengu wa roho..anakuwa amekufa kwa habari ya dhambi, na yu hai kwa habari ya haki na anakuwa amehama kutoka mautini kuingia uzimani, na kuyavua matendo yote ya giza. Huyo anakuwa yupo chini ya mikono salama ya Yesu mwenyewe…Bwana Yesu anampa nguvu ya ajabu ya kushinda dhambi na ulimwengu kwa kutiwa muhuri na Roho Mtakatifu…Mtu huyo shetani hawezi tena kwa namna yoyote kumnyakua kutoka mikononi mwa Mungu…Uhai wake unakuwa unafichwa pamoja na Kristo.
Wakolosai 3:3 “Kwa maana mlikufa, na uhai wenu umefichwa pamoja na Kristo katika Mungu”.
Mtu huyo anakirimiwa uwezo wa ajabu wa kushinda dhambi..kiasi kwamba kutenda dhambi kwake ni uchaguzi..sio kitu kinachomlazimu kama vile pumzi…Shetani anapomletea vishawishi vya kufanya uasherati ni kama mtu anayepitisha viatu barabarani …hivyo ni uamuzi wa Yule mnunuzi aidha anunue au asinunue…vilevile na Yule muuzaji anakuwa hana uwezo wa kumlazimisha anunue au akivae(ni jambo la uchaguzi), halihusishi kulazimisha…Ndivyo shetani anavyokuwa mbele ya mtu aliyeokoka kikamilifu.
Lakini kwa mtu ambaye hajaokoka dhambi kwake ni sheria, sio jambo la kuchagua, ni lazima afanye, atake asitake..anakuwa mtumwa wa ile dhambi, anakuwa na wakati mwingine na uwezo wa kujizuia kwa kipindi Fulani lakini baada ya muda mfupi anairudia ile dhambi kwa kishindo..… shetani anapomletea ushawishi wa kutenda dhambi kuna nguvu ya ajabu inamsukuma kuifanya ile dhambi hata kama hapendi, na kisha anakwenda kuifanya…
Ndio maana unasikia mtu anakwambia yaani nashindwa kuitawala tamaaa yangu najikuta nafanya hiki au kile, nashindwa kuacha kufanya uasherati, nashindwa kuacha kujichua, nashindwa kuacha kuangali picha chafu za ngono, nashindwa kuacha kunywa pombe, nashindwa kuacha kuvuta sigara, nashindwa kuacha kusikiliza miziki ya kidunia n.k…. Sasa huyo ni mtu ambaye hayupo ndani ya Kristo..
Na hali hiyo ya kushindwa kuishinda dhambi inatokana na mtu mwenyewe hajaamua kumfuata Kristo kwa kujikana nafsi, anatamani kuokoka na huku bado anatamani kuendelea kuishi na girlfriend wake/boyfriend wake, anatamani kuokoka lakini bado anazipenda movie zake na tamthilia zake na miziki yake, anakuwa hayupo tayari kuviacha kwa vitendo…hivyo ule uwezo wa kushinda haushuki ndani yake.
Sasa kwa mtu ambaye kashaokoka kikamilifu na uwezo huo wa kushinda dhambi umeshuka ndani yake…kuna uwezekano wa kupitia vipindi Fulani vidogo vidogo vya kurudi nyuma..Kurudi kwake nyuma hakutakuwa kuvuka kabisa mstari na kurudia ulimwengu hata kufikia viwango vya kurudi kufanya uasherati au kurudi kutoa mimba, au kurudi kunywa pombe au kuvuta sigara…hapana..bali kurudi kwake nyuma kunakuwa ni aidha kupunguza kiwango chake cha kusali kidogo..pengine alikuwa anasali masaa kadhaa lakini sasa kajikuta kapunguza anasali muda mfupi …alikuwa ana upendo sana, anajigundua upendo wake umepungua kidogo…alikuwa anasaidia watu lakini kajikuta kapunguza…alikuwa anajituma kuhubiria wengine lakini kajikuta kapunguza…na sio kaacha kabisa hapana! Bali kapunguza….Mtu wa namna hiyo ndio KARUDI NYUMA KIIMANI!..Na si mtu karudi kwenye uasherati, karudi kwenye ulevi, karudi kwenye anasa ndio karudi nyuma…Huyo hajarudi nyuma bali alikuwa hapo kwanza hajaokoka kabisa!..hivyo anapaswa aokoke.
Na kama imetokea mtu kashaokoka kabisa na nguvu ile ya kushinda dhambi ilishashuka juu yake…kiasi kwamba dhambi mbele yake ikija ni chaguo…na si kiamrisho…kiasi kwamba alishaacha uasherati na kulikuwa hakuna nguvu yoyote ya kumchukua katika dhambi hiyo, alikuwa ameushinda ulimwengu kiasi kwamba uuaji kwake ilikuwa ni kitu ambacho asingeweza kukifanya kwa namna yoyote ile…Mtu wa namna hiyo akaamua kwa idhini yake kuchagua kurudi kwenye dhambi…Basi biblia imesema wazi kuwa mtu wa Namna hiyo amemsulubisha Kristo mara ya pili hivyo ile neema ya kuvutwa tena kurudi kutubu..inaondolewa kabisa…kamwe hatasikia tena nguvu ya kutubu na hivyo ataendelea kuwa mbaya hivyo hivyo mpaka mauti…Kwasababu nguvu inayotuvuta kwa Mungu na kutushikilia ndiyo inayoitwa Neema, sasa mtu aliyeipokea hiyo neema na kwa idhini yake anayarudia matapishi huyo haiwezekani kutubu…Sio kwamba siku moja atataka kutubu asisamehewe!..Hapana…bali ile hali ya kutaka kutubu inaondolewa ndani yake kiasi kwamba hatatamani hata kutubu tena. Anakuwa kama watu ambao hawataki kusikia injili kabisa.
2 Petro 2:20 “Kwa maana wale waliokwisha kuyakimbia machafu ya dunia kwa kumjua Bwana na Mwokozi Yesu Kristo, kama wakinaswa tena na kushindwa, hali yao ya mwisho imekuwa mbaya kuliko ile ya kwanza.
21 Maana ingekuwa heri kwao kama wasingaliijua njia ya haki, kuliko kuijua, kisha kuiacha ile amri takatifu waliyopewa.
22 Lakini imetukia kwao sawasawa na ile mithali ya kweli, Mbwa ameyarudia matapiko yake mwenyewe, na nguruwe aliyeoshwa amerudi kugaa-gaa matopeni”.
Na tena inasema katika Waebrania..
Waebrania 6:4 “Kwa maana hao waliokwisha kupewa nuru, na kukionja kipawa cha mbinguni, na kufanywa washirika wa Roho Mtakatifu,
5 na kulionja neno zuri la Mungu, na nguvu za zamani zijazo,
6 wakaanguka baada ya hayo, haiwezekani kuwafanya upya tena hata wakatubu; kwa kuwa wamsulibisha Mwana wa Mungu mara ya pili kwa nafsi zao, na kumfedhehi kwa dhahiri”.
Hivyo kama umeokoka kikamilifu, na unaona kuna nguvu ya kushinda dhambi ndani yako..Usigeuke kurudi nyuma ndugu yangu…usirudie uasherati wala uzinzi wala ulevi, wala utoaji mimba usiichezee hiyo Neema uliyopewa (Nguvu ya kushinda dhambi ni ya kuithamini sana kuliko kitu kingine, maana ndiyo Neema yenyewe hiyo)…Usipoithamini kutakuwa hakuna nafasi ya pili wewe au mimi kurudia utakatifu tena…Ndicho kilichomkuta shetani. Aliichezea neema na hivyo akajiharibia mwenyewe…
Kadhalika kama ulikuwa unadhani kwamba kwa kufanya kwako uasherati ni kwamba ulirudi nyuma baada ya kuokoka!…Na leo unataka kutubu!..Basi Neema ya kukuvuta kwa Kristo bali inalia moyoni mwako… Hivyo Leo fahamu kuwa hukurudi nyuma bali ulikuwa hujaokoka kabisa!!..Na kama leo hii unataka kutubu na kusema unataka kuokoka kabisa na kuacha dhambi na ulimwengu..Ukidhamiria kutoka moyoni kwa vitendo kwamba kuanzia leo na si kesho unaacha kutazama yale matamthilia ya kihindi na ya kifilipino unayoyatazama yenye maudhui ya kipepo, unaacha kuvaa vimini na unakwenda kuvipiga moto vyote sasa hivi, unaacha kuvaa suruali haijalishi una gauni moja tu, unaacha kupaka wanja, hereni, kuvaa wigi, kujichubua, unaacha kusikiliza miziki ya kidunia na unaifuta yote hata kwenye simu yako..na kuanzia leo ukisema ninaamua kumfuata Yesu kwa gharama zozote na kwamba upo radhi hata kuchukiwa, kutengwa, kuonekana mjinga na kujikana nafsi kwa viwango vyote na kwenda kubatizwa ubatizo sahihi…hapo ndipo utaona uweza wa Mungu juu ya maisha yako wa kushinda dhambi, utakapopokea uwezo wa kushinda Uasherati, ulevi, anasa, na vitu vyote vya kidunia kirahisi havitakuendesha na kukufanya ufanye jambo usilotaka wewe kulifanya.
Idadi kubwa ya watu wanaojiita wakristo hawajapokea uweza huo ndio maana wao kushinda dhambi ni ngumu…Bado hawajamuonja Kristo..Kumuonja Kristo maana yake ni kuonja huo uwezo ndani yako..Na pasipo huo uwezo kushuka ndani yako..kamwe huwezi kuishinda dhambi..kila siku utasema umeokoka, na kila siku utaongozwa sala ya Toba..lakini baada ya siku mbili tatu utarudia mambo yote ya kale…Fomula pekee ya kuipokea huo uwezo ni hiyo hapo juu…Amua kujikana nafsi kwa kuacha vitu vyote kwa vitendo.
Bwana akubariki sana.
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mafundisho mengine:
Mada Nyinginezo:
Naomba watu wote tusome hii…
Hakuna mtu asiyejua kuwa shetani, naye hujigeuza na kuwa mfano wa malaika wa Nuru (2Wakorintho 11:14)? Lakini tunapaswa tujiulize lengo la yeye kujibadilisha vile ni nini? Utagundua kuwa Hana lengo lingine zaidi ya kuuchafua utakatifu wa malaika ili na wao pia waonekane kuwa ni waovu. Vivyo hivyo na watumishi wake nao wanafanya kazi hiyo hiyo .. Ili mwisho wa siku tuhitimishe kuwa wote ni wabaya, wote ndio wale wale wapotoshaji.
Embu jaribu kuufikia tena vizuri ule mfano Bwana Yesu aliousema..
Mathayo 13:24 “Akawatolea mfano mwingine, akisema, Ufalme wa mbinguni umefanana na mtu aliyepanda mbegu njema katika konde lake;
25 lakini watu walipolala, akaja adui yake akapanda magugu katikati ya ngano, akaenda zake.
26 Baadaye majani ya ngano yalipomea na kuzaa, yakaonekana na magugu.
27 Watumwa wa mwenye nyumba wakaenda wakamwambia, Bwana, hukupanda mbegu njema katika konde lako? Limepata wapi basi magugu?
28 Akawaambia, Adui ndiye aliyetenda hivi. Watumwa wakamwambia, Basi, wataka twende tukayakusanye?
29 Akasema, La; msije mkakusanya magugu, na kuzing’oa ngano pamoja nayo.
30 Viacheni vyote vikue hata wakati wa mavuno; na wakati wa mavuno nitawaambia wavunao, Yakusanyeni kwanza magugu, myafunge matita matita mkayachome; bali ngano ikusanyeni ghalani mwangu”.
Umeelewa hapo? Ni kwanini magugu yaliachwa yaendelee kuwepo shambani hadi wakati wa Mavuno? Unadhani mwenye shamba alikuwa anapenda kuyaona yakiendelea kustawi shambani muda wote huo?, jibu ni la! lakini ilimpasa atumie hekima kwasababu alijua kama akitaka tu kuyashughulika kuyafyeka atajikuta anazing’oa na ngano ndani yake na mwisho wa siku atapata hasara kubwa ya kazi yake aliyoitaabikia..
Kwasababu wanasema wakati magugu yakiwa machanga, huwa yanatabia ya kushikamana sana na ngano, vilevile yanafanana mno kiasi kwamba kutofautisha gugu katikati ya ngano ni kazi sana..Hivyo ukijaribu kung’oa tu gugu moja, pembeni yake unaweza kuta zilikuwa ngano 6 zimejishikamanisha nayo, na mwisho wa siku ni hasara…Hivyo si kazi rahisi kama unavyofikiria, mahali pekee ambao utaweza kuziona na kuzing’oa bila kuathiri ngani ni wakati wa mavuno tu, kwasababu maumbile yako yanajitofautisha kabisa na ngano..
Ndugu yangu, tusiwe wepesi wa kutoa hukumu ya moja kwa moja kuwa makanisa yote ya kiroho, yanapotosha, makanisa madogo madogo ambayo hajasajiliwa yote ni feki, wachungaji wote ambao wanawaombea watu shida zao ni bandia, watu wote wanaokesha makanisani na kumwomba Mungu usiku na mchana ni wajinga, hawana akili, wote wanaomlilia Mungu ni wapumbavu, masikini waliokosa uelekeo wa maisha, wenye stress za maisha, wavivu na wasiojituma, wamekata tamaa, hawapendi kufanya kazi, wanapenda vya bure..
Ikiwa ni wapumbavu, wewe unataka wafanye nini ili wawe na hekima? Unataka waache kumlilia Mungu wao wakaililie pesa? Hiyo ndiyo iliyowaleta duniani?…Unataka Watumishi waache kuhudumu madhabahuni wote waondoke na wewe waende ofisi kutafuta pesa, ni nani basi atakayekaa kukuletea wewe injili,? Hata elimu yako inakufundisha kitu kinachoitwa Opportunity cost, ili uweze kufanya jambo moja kikamilifu ni lazima uache kufanya lingine..Huwezi kushika mawili kwa wakati mmoja..Na wengi wanaosema mambo kama hayo asilimia kubwa ni wale ambao hata Kristo hajaumbika vizuri ndani yao, wala hawayajua maandiko yanaagiza nini kuhusu mambo ya ibada..Si wote wanaomlilia Mungu hawajasoma kama wewe unavyofikiri, si wote wanaomtafuta Mungu, ni maskini kama wewe unavyodhani, si wote wanaokesha kuomba hawajui kuwa kuna kufanya kazi..
Tusitumie vigezo vya watu wachache wanaotumiwa na shetani kuliharibu kanisa la Mungu na kuhitimisha na wengine wote hawafai.. Wanaotumia mafuta ya upako, chumvi,sabuni, balbu, maji, wanaohubiri habari za mafanikio wakati wote, wanasahau toba ya msamaha, hao wote ndio mapando ya shetani yaliyowekwa ili kuwafanya watumishi wengine wote waonekane kuwa ni wa uongo…
Embu fumba kinywa chako, ishia tu kukemea, kukaripia na kuhubiri lakini usishiriki katika kuchua hatua yoyote ya nguvu, ili kutokomeza hilo suala na kuyaita makanisa yote ya kiroho ni (vibanda-Imani), na kutaka yote yafungiwe, au yawekwe masharti katika kuabudu.. wewe mwachie Mungu, yeye ndio atakayeshughulika nao, na yeye ndiye atakayewapukutisha mmoja baada ya mwingine, hiyo sio kazi yako rafiki.
Lakini ukijiona wewe una hekima zaidi ya Mungu..Angalia kuna roho ya mpinga-kristo inakunyemelea nyuma yako. Na Siku utakapoimpa ibilisi nguvu ya kutosha basi ujue kuwa wakati utafika hutaweza kuuza wala kununua wala kufanya jambo lolote kama hutakuwa na ile chapa ya mnyama…ambayo chumbuko lake litakuwa katika mambo kama hayo hayo ya ibada za sharti..
Maran Atha.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mafundisho mengine:
Mada Nyinginezo:
JIEPUSHE NA MANENO YA MANABII WA UONGO.
UNAWAFAHAMU MANABII WA UONGO?
CHAPA YA MNYAMA
DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.
JE! WEWE NI MBEGU HALISI YA KRISTO?
TOFAUTI KATI YA HEKALU, SINAGOGI NA KANISA NI IPI?
DANIELI: Mlango wa 12.
MAMBO 5 AMBAYO KILA MKRISTO ANAPASWA KUFAHAMU.
Kulingana na historia ya Taifa la Israeli, tangu zamani wakiwa jangwani walikuwa wanamwabudu Mungu kwa kumtolea Dhabihu za aina mbalimbali mbele ya ile hema ya kukutania kama Musa alivyoagaizwa na Mungu kufanya, Na hema hii ilikuwa ni ya kuhama hama sio rasmi. Lakini mara baada ya kuingia katika nchi yao ya ahadi, Mfalme Daudi baada ya kuona kuwa Mungu hana eneo rasmi la kuliweka jina lake, eneo ambalo watu wa makabila yote ya Israeli yatakusanyika kumtolea Mungu kafara, akaazimia ndani ya moyo wake kumjengea Mungu nyumba.. Hivyo Mungu akasikia matamanio yake, na kuyaridhia lakini kwa masharti kuwa mwanawe ndiye atakayemjengea Nyumba hiyo.
Hivyo mwanawe Sulemani akaja kumjengea Mungu Nyumba kwa mafanikio yote, ambayo Mungu aliitukuza na kuliweka jina lake huko katika mji wa Yerusalemu..Na Nyumba hiyo ndiyo iliyoitwa HEKALU. Hivyo Hekalu hili lilikuwa ni moja tu, watu wote walipanda kwenda kumtolea Mungu kafara zao mbele ya hekalu hili lililokuwepo Yerusalemu.
2 Nyakati 7:1 “Basi Sulemani alipokwisha maombi hayo, moto ukashuka kutoka mbinguni, ukateketeza sadaka ya kuteketezwa na dhabihu; utukufu wa Bwana ukaijaza nyumba.
2 Wala makuhani hawakuweza kuingia nyumbani mwa Bwana, kwa kuwa utukufu wa Bwana umeijaza nyumba ya Bwana.
3 Wakatazama wana wa Israeli wote, uliposhuka ule moto, utukufu wa Bwana ulipokuwapo juu ya nyumba; wakasujudu kifulifuli hata nchi sakafuni, wakaabudu, wakamshukuru Bwana, wakisema, Kwa kuwa ni mwema; kwa maana fadhili zake ni za milele”
Lakini mara baada ya wana wa Israeli kuchukuliwa tena utumwani Babeli, na nyumba ya Mungu kubomolewa, kukawa hakuna tena sehemu ya kwenda kumfanyia Mungu ibada na kutoa sadaka za kuteketezwa, Hivyo waliporudi tena Yerusalemu kutoka Babeli, iliwalazimu kuwa na makusanyiko madogo madogo kwa ajili ya kujifunzia torati, na kusoma Zaburi pamoja na Kufanya dua. Hayo ndio yaliyoitwa masinagogi, Na Huko ndipo madhehebu ya mafarisayo na Masadukayo yalipozaliwa. Na yaliendelea kusambaa karibu sehemu kubwa ya dunia.
Muda rasmi haujulikana yalianza hasaa wakati gani..Lakini ni kipindi cha kati ya kuchukuliwa babeli hadi kipindi cha karibu na kuja kwa Bwana Yesu Kristo.
Na ndio maana Biblia inarekodi Bwana Yesu alikuwa pia akizunguka katika masinagogi yao akihubiri.
Marko 1:38 “ Akawaambia, Twendeni mahali pengine, mpaka vijiji vilivyo karibu, nipate kuhubiri huko nako; maana kwa hiyo nalitokea.
39 Akaenda akihubiri katika masinagogi yao, katika nchi yote ya Galilaya, na kutoa pepo”
Unaona soma pia (Luka 4:16-21)
Kulingana na tafsiri ya kibiblia kanisa maana yake ni “walioitwa”..Wale walio mwamini Yesu Kristo, wakiwa wamekusanyika wawili au watatu kwa jina lake, tayari hilo ni kanisa. Japokuwa Neno hilo limezoeleka na wengi kama jengo linalotumiwa na wakristo kuabudia..
Hivyo kwa kuhitimisha hekalu lilikuwa ni moja, ambalo lilijengwa na Mfalme Sulemani, lakaja kubomolewa na Mfalme Nebukadneza wa Babeli, likaja kujengwa tena na Zerubabeli na kubomolewa na Warumi mwaka 70 W.K, Na litakuja kujengwa tena pale Jerusalemu katika siku za mwisho.. Lakini masinagogi yalikuwa mengi, ambayo tunaweza kuyaita makanisa ya wayahudi yakifundisha dini za kiyahudi.. Na makanisa ambayo leo hii tunayaona ni Makanisa ya kikristo yakifundisha imani ya YESU KRISTO..Hiyo ndio tofauti yao.
Shalom.
[embedyt] https://www.youtube.com/watch?v=4AC-rH1ndvo[/embedyt]
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mafundisho mengine:
Mada Nyinginezo:
Sanduku la Agano lilikuwa linawakilisha nini katika Agano jipya?
VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 7 (Yeremia na Maombolezo)
Nifanye nini ili niondokane na Hofu maishani mwangu?
Tofuati kati ya Myahudi, Mwisraeli na Muebrania ni ipi?
Nini Tofauti kati ya uzinzi na uasherati ?
Tofauti kati ya ndoto na Maono ni ipi?
TOFAUTI KATI YA SHERIA YA ROHO WA UZIMA NA SHERIA YA DHAMBI NA MAUTI!
Tofauti katika ya zaka na sadaka ni ipi?
Je madhabahu ni sehemu ya kufanyia mizaha, utani, vichekesho au vituko?..
Zaburi Sura ya kwanza kabisa na mstari wa kwanza unasema…
” Heri mtu yule asiyekwenda katika shauri la wasio haki; Wala hakusimama katika njia ya wakosaji; Wala hakuketi barazani pa wenye mizaha”.
Mtu anayefanya mizaha madhababuni au utani ni wazi kuwa hamheshimu Mungu..na hofu ya Mungu imeshaondoka ndani yake..hamwogopi tena Mungu…Yeye pale madhabahuni haoni tofauti na kumbi za kidunia. Na mtu akishafikia hali kama hiyo ni ngumu kutubu. Kama ilivyokuwa kwa wana wa Eli, ofni na Fineasi…waliidharau Nyumba ya Mungu na kuigeuza kituo cha kufanyia ukahaba..kwani walikuwa wanalala na wanawake waliokuwa wanahudumu katika hema ya Mungu(1Samweli 2:22)…Na walipoonywa hata hawakutaka kusikia.
Mithali 15:12 “Mwenye mzaha hapendi kukaripiwa; Wala yeye hawaendei wenye hekima”.
Madhabahuni sio sehemu ya kufanyiana mizaha, sio sehemu ya kujipigia piga picha (selfie), sio sehemu ya kupigia stori, sio sehemu ya kulia chakula, sio sehemu ya kuchumbiana, wala si sehemu ya kusimama huku unatafuna vitu mdomoni…wala si sehemu ya kupanda pale na huku umevaa kihuni au kikahaba…
Kadhalika madhabahuni si sehemu ya kuchezea DANSI, Kwamba unapanda na kucheza kidunia…wala si sehemu ya kwenda kufanya vituko kama vile jukwaa la vichekesho…Ni sehemu ya Ibada kwa Mungu wetu..
Mungu wetu hashuki pale kuja kukutana na vichekesho vyetu au mizaha yetu, au utani wetu…. anashuka pale kuja kukutana na haja zetu na dua zetu na mahitaji yetu…Hivyo kuigeuza kuwa sehemu ya vichekesho na mizaha ni kumkufuru Mungu na hivyo kujitafutia laana badala ya baraka.
Hata madhabahu za mashetani huwa hazifanyiwi mizaha si zaidi madhabahu ya Mungu aliye hai?
Kumbuka pale ni sehemu iliyorasimishwa kwa Mungu muumba wa mbingu na nchi, aliye msafi na mtakatifu na wala asiyekuwa na mizaha..Hivyo kama yeye mwenyewe anapaheshimu na kushuka hapo inatupasaje sisi?..Ukisoma katika kitabu cha Ufunuo 4 utaona Mungu anaonekana ameketi katika kiti chake cha enzi huku akiwa amezungukwa na wazee 24..Wale ni wazee na sio vijana, ikimaanisha kuwa wamekomaa kiakili na wenye busara na si mizaha…Hao ndio wanaomsogelea Mungu mbinguni..
Na sisi tunapomsogelea Mungu katika nyumba yake hatuna budi kuivaa hekima kama ya wazee ili tuweze kumkaribia Mungu kwa baraka na si laana..kwasababu yeye hapendi mizaha na wanaofanya utani.. kwasababu anatuheshimu sana hivyo na sisi tunapaswa tumheshimu zaidi sana.
Kama ni mchungaji, mwalimu au Askofu…
>ACHA! kufanya mizaha madhabahuni mwa Mungu aliye hai.
>ACHA KUTUMIA MASAA KUCHEKESHA WATU BADALA YA KUTIMIZA WAJIBU WAKO WA KUHUBIRI INJILI KAMILI YA YESU KRISTO
>ACHA Kutaniana na watu madhabahuni..Siku ile utatoa hesabu kila Neno lisilo na maana linalotoka katika kinywa chako.
> Kama wewe ni muumini, Madhabahuni na hata kanisani kwa ujumla sio mahali pa kukatiza katiza bila kuwa na shughuli yoyote ya maana, wala si mahali pa kupiga piga makelele…Ufikapo nyumbani mwa Mungu paheshimu, zima simu yako.. Na ukae utulie..Hata kama ni mtoto wa mchungaji au mke wa Mchungaji…Huna Ruhusa ya kupageuza pale Nyumbani..Hiyo ni kwa faida yako binafsi.
BWANA WETU ANAKUJA.
Mada Nyinginezo:
Ni kwasababu ile ile kwanini Henoko alitwaliwa, na wengine wakabaki, Na Eliya alinyakuliwa na wengine wakabaki. Mungu aliruhusu kwa makusudi kabisa watu hawa wawe mfano wa mambo hayo ili kutupa sisi picha halisi kitakachotokea siku ile ya Unyakuo…Tukianzana na Henoko biblia imeshatupa majibu kabisa ni kwanini alinyakuliwa ..Inasema Ni kwasababu alitembea na Mungu (alimpendeza Mungu) kwa miaka mia tatu (Mwanzo 5:22).
Mwanzo 5:24 “Henoko akaenda pamoja na Mungu, naye akatoweka, maana Mungu alimtwaa”.
Waebrania 11:5 “Kwa imani Henoko alihamishwa, asije akaona mauti, wala hakuonekana, kwa sababu Mungu alimhamisha; maana kabla ya kuhamishwa alikuwa ameshuhudiwa kwamba amempendeza Mungu”
Unaona Hawa ni watu ambao walivuka viwango vya kawaida vya kuishi Maisha ya kumpendeza Mungu tofauti na watu wengine..Na hivyo Mungu akaona si vema waendelee kuwepo mpaka siku ya mwisho ya uhai wao, akawatwaa. Ndivyo itakavyokuwa siku ile ya Unyakuo. Wengi tunavyodhani watakaonyakuliwa watakuwa ni wengi sana, kwamba hata kama mtu anaishi Maisha ya kutouthamini wokovu wake hapa duniani, naye pia atakwenda..Jibu ni hapana, watakuwa ni wachache sana nao ni wale watu ambao watakidhi hivyo vigezo vya kumpendeza Mungu kama Henoko…Soma Mathayo 7:14,na Luka 13:23.
Na ndio maana siku ile muda mfupi kabla ya kuja kwa Bwana biblia inatuonyesha kuwa kutakuwa na makundi mawili wa wakristo. Kundi la kwanza litajulikana kama wanawali wapumbavu, na kundi la pili litakuwa la wanawali werevu (Mathayo 25). Hawa werevu ndio wale ambao watatambua majira ya kujiliwa kwao, kutokana na dalili za mwisho wa dunia zinavyojionyesha, hivyo wataanza kutengeneza mambo yao sawa mapema kabisa kabla ya wakati ule kufika kama Henoko alivyojuwa kuwa dunia inakaribia kuangamizwa akatengeneza mambo yake sawa …
Hivyo ule wakati utakapokaribia na Mungu kuiona Imani yao , na utayari wao kuwa macho yao siku zote yapo mbinguni..Hao ndio watakaonyakuliwa na kutoweka ghafla..hawataonekana…Mungu atawaepusha na ile hukumu inayokuja pamoja na dhiki kuu.
Lakini wengine ambao ndio wale wanawali wapumbavu, wanasema wanamngojea Bwana lakini Maisha yao sio kama watu wanaomngojea Bwana kama biblia inavyotuasa katika Luka 12:35-36..Nusu dunia, nusu Mungu, hawajibidiishi kwa Mungu, wao wakishaokoka na kubatizwa hiyo tu inatosha,hakuna haja ya kujua Zaidi chochote kinachohusiana na Maisha baada ya hapa, kusikia habari za kwenda mbinguni kwao ni kama habari za kale,..Sasa hawa ndio siku ile watajikuta wameachwa…
Sasa Tukirudi kwa Eliya naye Kama vile Elisha alivyomshuhudia akiondoka mbele zake, na akalia kilio kikubwa sana..Ndivyo itakavyokuwa kwa kundi hili la wakristo hawa
vuguvugu,watakavyolia siku ile.. kwasababu siku hiyo watakuwa karibu sana na wale watakaonyakuliwa au watawashuhudia wakitoweka ..
Mathayo 24:40 “Wakati ule watu wawili watakuwako kondeni; mmoja atwaliwa, mmoja aachwa;
41 wanawake wawili watakuwa wakisaga; mmoja atwaliwa, mmoja aachwa”.
Unaona, unabii huu utatimia siku hiyo kwao, kwasababu watakuwa karibu sana na wale watakaonyakuliwa kwasababu wote ni watu wa kanisani?. Je! Utajisikiaje siku ile yule jirani yako anayejulikana kama mlokole ambaye unajua alikuwa amejikana nafsi hayupo?..Huyo rafiki yako ambaye unaenda naye ibadani kila siku ghafla tu anatoweka mbele ya macho yako? Utajisikiaje..Kuona huyo mke wako/mume wako ambaye hakuruhusu Maisha ya dhambi yamkaribie usiku ule ukiwa naye nyumbani ghafla anatoweka..Utajisikiaje, tafakari ndugu kuona mchungaji wako aliyekuwa anakukemea kila siku habari za kuvaa vimini, na suruali, na uzinzi hayupo tena.. Itakuwa ni kilio na kusaga meno kwako wewe unayejiita mkristo lakini ni vuguvugu..Na cha kusikitisha ni kuwa kundi hili litakaloachwa litakuwa ni kubwa sana.
Wakati huo wenye dhambi hawataelewa chochote, watasikia tu uvumi, lakini kwao haitakuwa habari ya kushutua kama kwako..Wenyewe watasikia tu kwenye vyombo vya habari kuwa watu fulani wachache sana wamepotea lakini watapatikana,..kwasababu hawatakuwa wengi, kama tunavyodhani leo hii… kumbuka alinyakuliwa Henoko tu peke yake kati ya mamilioni ya watu waliokuwa duniani wakati ule, alinyakuliwa Eliya tu kati ya mamilioni ya watu waliokuwa duniani wakati ule..Vivyo hivyo watanyakuliwa wachache sana katika ya mabilioni ya watu waliopo duniani leo hii..
Huu sio wakati wa kumwangalia mjomba, au shangazi, au ndugu, ili kumfuata YESU, Huu ni wakati wa kujitwika msalaba wako wewe kama wewe. Sio wakati wa kusema mbona fulani yupo hivi, mbona mchungaji wangu anaishi vile.. kumbuka wewe sio yeye, na yeye sio Mungu kwamba unaouhakika siku ile atanyakuliwa..Fanya bidii wewe kama wewe kuutafuta uhusiano wako binafsi na Kristo ili siku ile isikupite. Vivyo hivyo na mimi ninafanya hivyo..Na mtu mwingine yeyote anayejiita mkristo anapaswa afanye hivyo. Kwasababu kwenda katika unyakuo sio lelemama..
Tusipumbazwe na kundi hili kubwa la wanawali wapumbavu tulionao katika ukristo. Sisi tusonge mbele na Bwana atakuwa pamoja na sisi hadi siku ile ya uyakuo itakapofika.
Ubarikiwe sana.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mafundisho mengine:
Mada Nyinginezo:
KWANINI MUNGU ALIMTUMIA MUSA KWA VIWANGO VILE?
MAMBO 5 AMBAYO KILA MKRISTO ANAPASWA KUFAHAMU.
DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.
Kwanini wanawake wengi huwa wanalipuka mapepo?
Je! Ni kweli ubatizo wa maji hatuuhitaji tena?
WANA WA MUNGU, NA BINTI ZA WANADAMU.
NDUGU,TUOMBEENI.
Ufunuo 16:15 “(Tazama, naja kama mwivi. Heri akeshaye, na kuyatunza mavazi yake, asiende uchi hata watu wakaione aibu yake.)”
Vazi ni kitu kinachositiri mwili…Mwili ukikosa mavazi unakuwa tupu/uchi. Na ni aibu kuwa uchi…Lakini pia upo utu wa ndani ambao nao pia unahitaji mavazi..ukikosa mavazi nao pia ni sawa na upo uchi na aibu yake huo ndio kubwa zaidi.
Katika hichi kipindi cha kumgoja Bwana..Biblia inatuasa tuhakikishe nafsi zetu zina mavazi yapasayo…na Mavazi yenyewe si mengine zaidi ya matendo mazuri ya utakatifu. Tunasoma hilo katika
Ufunuo 19:7 “Na tufurahi, tukashangilie, tukampe utukufu wake; kwa kuwa arusi ya Mwana-Kondoo imekuja, na mkewe amejiweka tayari.
8 Naye amepewa kuvikwa kitani nzuri, ing’arayo, safi; kwa maana kitani nzuri hiyo ni matendo ya haki ya watakatifu”.
Kitani inayozungumziwa hapo ni “vazi zuri refu la thamani na leupe”…Hivyo hilo ndio vazi la utu wetu wa ndani..Na ndio Vazi la harusi Bwana Yesu alilolizungumzia katika..
Mathayo 22:11 “Lakini alipoingia yule mfalme ili kuwatazama wageni wake, akaona mle mtu mmoja asiyevaa VAZI LA ARUSI.
12 Akamwambia, Rafiki, uliingiaje humu nawe huna vazi la arusi? Naye akatekewa.
13 Mfalme akawaambia watumishi, Mfungeni mikono na miguu, mchukueni mkamtupe katika giza la nje; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.
14 Kwa maana waitwao ni wengi, bali wateule ni wachache”.
Maana yake hakuna mtu atakayeingia katika karamu ya Mwana-kondoo mbinguni kama hana hilo vazi la harusi ambalo ni UTAKATIFU
Biblia inazidi kulisisitiza hilo katika kitabu cha Waebrania..
Waebrania 12:14 “Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, NA HUO UTAKATIFU, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao;”
Unaona? Anasema “huo utakatifu”..maana yake “Hilo vazi”..pasipo kuwa nalo hakuna mtu atakayemwona Mungu.
Tunaishi kizazi ambacho watu wanasema hakuna watakatifu duniani…Na hiyo ni kutokana na watu kutoelewa nini maana ya utakatifu…utakatifu maana yake sio kujizuia kukanyaga sisimizi barabarani, au kujizuia kutokuchinja kuku…Hiyo sio maana ya utakatifu…Maana kwa viwango hivyo basi kusingekuwa na mtakatifu duniani….(Ukipenda kufahamu kwa urefu maana ya utakatifu fuatilia somo tuliloliandika kipindi cha nyuma kidogo lenye kichwa kinachosema ‘mtakatifu ni nani’ au kama itakuwa ngumu kulifikia unaweza kututumia ujumbe inbox tutakutumia).
Hivyo Nyakati hizi za mwisho wako wasiojua maana ya utakatifu na kadhalika wapo shetani aliowafumba macho wakidhani wao ni watakatifu na kumbe sio…wakidhani kuwa wana VAZI HILO LA HARUSI…kumbe hawana…wapo uchi..kama Bwana Yesu alivyosema katika ufunuo 3.
Ufunuo 3:16 “Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa changu.
17 Kwa kuwa wasema, Mimi ni tajiri, nimejitajirisha, wala sina haja ya kitu; nawe hujui ya kuwa wewe u mnyonge, na mwenye mashaka, na maskini, na kipofu, NA UCHI.
18 Nakupa shauri, ununue kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto, upate kuwa tajiri, NA MAVAZI MEUPE UPATE KUVAA, AIBU YA UCHI WAKO ISIONEKANE, na dawa ya macho ya kujipaka macho yako, upate kuona”.
Je unataka unayataka mavazi hayo uyavae na uchi wako usionekane?…Hatua za awali za kufanya ni kutubu na kumkaribisha Bwana Yesu moyoni mwako…Unatubu kwa kudhamiria kabisa kuacha ulimwengu na mambo yake yote…Unakusudia kuacha ulevi, uasherati, wizi, rushwa, anasa, utoaji mimba, usagaji, ufiraji, ulawiti, utoaji mimba, utazamaji picha na video za ngono, na mambo mengine yote ya kidunia..Na kisha ndio unamwambia Bwana akusamehe kabisa na Bwana Yesu atakusamehe kwasababu anatamani wewe utubu kuliko wewe unavyotamani…Na kama leo hii umeamua kufanya hivyo kwa kumaanisha kabisa…
Basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie maisha yako yote kama ilivyokuwa hata kwetu sisi. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.
EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, .
NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.
ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.
AMEN.
Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani … Hatua inayofuata ni Ubatizo, na kudumu katika Kujifunza Neno la Mungu..… VAZI HILO UTAKUWA UMEVIKWA katika roho yako…..Hivyo unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu Hiyo itakusaidia kuliweka safi vazi lako kila siku…. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.
Kumbuka haya maneno ya Bwana Yesu kila siku.. “Tazama, naja kama mwivi. Heri akeshaye, na kuyatunza mavazi yake, asiende uchi hata watu wakaione aibu yake.)”
Huu ni wakati wa kumalizia, hatuna muda mwingi..
Bwana akubariki sana.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312.
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mafundisho mengine:
Mada Nyinginezo:
Kwanini yule mtu hakukutwa na vazi la arusi wakati alialikwa?
WANA WA MUNGU, NA BINTI ZA WANADAMU.
USIMPE NGUVU SHETANI.
Je! Ni kweli ubatizo wa maji hatuuhitaji tena?
NINI KINAFUATA SIKU ILE ILE YA KUOKOKA!
HAKIKISHA UNALIELEWA NENO.
Je! Ni halali kuoa/kuolewa na mtu ambaye tayari anao watoto?
SWALI: Naomba kufahamu Je! Ni kweli ubatizo wa maji hatuuhitaji tena, tunaopaswa tuwe nao ni ule wa Roho Mtakatifu tu peke yake kama vile Yohana Mbatizaji alivyosema katika Mathayo 3:11 “Kweli mimi nawabatiza kwa maji kwa ajili ya toba; bali yeye ajaye nyuma yangu ana nguvu kuliko mimi, wala sistahili hata kuvichukua viatu vyake; yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu na kwa moto”?
JIBU: Katika mistari hiyo hakuna mahali popote Yohana amesema sasa ndio watu waache ubatizo wa maji, wautazame ule wa Roho Mtakatifu peke yake..Hakuna na Hiyo yote ni kutokana na utafsiri mbaya wa maandiko ambao unasababishwa na baadhi ya waalimu ambao hawamtegemei Roho Mtakatifu katika kuyatafsiri maandiko.
Embu leo tuangalie mtu mmoja katika biblia ambaye alilielewa hilo andiko na akachukua hatua stahiki katika kuwaelekeza watu katika njia ya kweli.
Kama tukisoma kitabu cha Matendo sura ile ya 10 kwa ufupi pale tunaona habari ya mtu mmoja aliyeitwa Kornelio, ambaye alikuwa anamcha Mungu sana kwa sadaka zake, lakini siku moja akatokewa na malaika na kupewa maagizo ya kwenda kumuita Petro aje kuwaelekeza cha kufanya.. Ndipo Petro alipoeletewa taarifa akaenda na alipowakuta akaanza kuwaeleza habari za Yesu, pindi tu anaanza kuwaeleza habari zile Roho Mtakatifu alishuka palepale, na watu wote wakajazwa na Roho Mtakatifu wakaanza kunena kwa lugha mpya.
Matendo 10:44 “Petro alipokuwa akisema maneno hayo Roho Mtakatifu akawashukia wote waliolisikia lile neno.
45 Na wale waliotahiriwa, walioamini, wakashangaa, watu wote waliokuja pamoja na Petro, kwa sababu Mataifa nao wamemwagiwa kipawa cha Roho Mtakatifu.
46 Kwa maana waliwasikia wakisema kwa lugha, na kumwadhimisha Mungu. Ndipo Petro akajibu,
47 Ni nani awezaye kuzuia maji, hawa wasibatizwe, watu waliopokea Roho Mtakatifu vile vile kama sisi?
48 Akaamuru wabatizwe kwa Jina lake Yesu Kristo. Ndipo wakamsihi azidi kukaa siku kadha wa kadha.
Sasa utaona hapo mara baada ya Petro kuona watu wamejazwa Roho Mtakatifu hakusema yatosha sasa, hakuna haja ya kubatizwa tena, Roho Mtakatifu anatosha kwasababu Yohana alisema hivyo…
Ukitaka kujua kuwa Petro naye aliufahamu huo mstari vizuri hata Zaidi yetu sisi, aliukumbuka pia hata alipokuwa palepale anawahubiria, Tunalithibitisha hilo mbele kidogo wakati sasa amesharudi Yerusalemu anawasimulia wayahudi tendo hilo la watu wa mataifa kupokea Roho Mtakatifu kama wao aliwaeleza mstari huo embu tusome alichokisema..
Matendo 11:15 “Ikawa nilipoanza kunena Roho Mtakatifu akawashukia kama alivyotushukia sisi mwanzo.
16 Nikalikumbuka neno lile la Bwana, jinsi alivyosema, YOHANA ALIBATIZA KWA MAJI KWELI, BALI NINYI MTABATIZWA KWA ROHO MTAKATIFU.
17 Basi ikiwa Mwenyezi Mungu amewapa wao karama ile ile aliyotupa sisi tuliomwamini Bwana Yesu Kristo, mimi ni nani niweze kumpinga Mungu?.
Unaona hapo?, Petro alilielewa hilo andiko kuwa hatupaswi kuuacha ubatizo wa maji, na ndio maana hata baada ya kuona Roho Mtakatifu alishuka juu yao kabla ya ubatizo bado aliagiza wakabatizwe. Hivyo na sisi pia agizo la ubatizo ni moja ya maagizo muhimu sana Bwana Yesu aliyotupa yanayoukamilisha wokovu wetu. Kila mtu aliyeamini hana budi kwenda kubatizwa haraka sana iwezekanavyo..Kama Bwana Yesu alivyosema..katika Marko 16:16 “Aaminiye na kubatizwa ataokoka; asiyeamini, atahukumiwa”.
Na tena katika ubatizo ulio sahihi wa mitume ambao ni ule wa kuzamishwa katika maji mengi (Yohana 3:23). na kwa jina la YESU KRISTO (Matendo 2:38, 8:16, 10:48, 19:5)..Ubatizo mwingine tofauti na huo ni batili. Mtu anapaswa akabatizwe tena.
Ubarikiwe.
Maran atha
Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
MTUMAINIE YESU ASIYEISHA MATUKIO.
KWANINI AWE PUNDA NA SI MNYAMA MWINGINE?
WAKAMTUKANA MUNGU, WALA HAWAKUTUBU.
Ni nini kinafuata siku ile ya kuokoka!? Ni swali linaloulizwa na wengi…
Shalom.Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe…Karibu tujifunze Biblia, Neno la Mungu ambalo ni mwanga wa njia zetu na Taa ya miguu yetu.
Watu wengi wanajiuliza ni nini kitafuata baada kumpokea Yesu, Nimeshatubu ndio! Je ni nini kinafuata baada ya hapo ili niendelee kusonga mbele katika Imani?. In
Baada ya kumruhusu Bwana Yesu Kristo aingie moyoni mwako…siku hiyo hiyo uliyofungua mlango wa yeye kuingia ndani yako..Tayari Roho Mtakatifu aliingia ndani yako…aliingia kama Roho ambayo pengine usingeweza kuhisi chochote nje…pengine ungesikia tu amani Fulani lakini usione chochote…Na Siku zinavyozidi kwenda kama utaendelea kuushikilia wokovu wako na kuukulia ndipo atakavyozidi kujaa zaidi ndani yako…Na utafikia kipindi utapokea Ujazo kamili wa Roho Mtakatifu kwaajili ya kazi yake.
Sasa siku hiyo unapotubu…hatua inayofuata kabla hata ya kwenda kutafuta kanisa la kujiunga, au kabla hata ya kwenda kubatizwa…hatua inayofuata ni kuacha yale yote uliyokuwa unayafanya…Kama ulikuwa ni mlevi unadhamiria kuacha ulevi pamoja na vyanzo vyake vyote..unaacha kwenda Bar, unakwenda kuvunja chupa zote za Bia ulizonazo nyumbani, unaacha kazi ya Bar kama ulikuwa ni muhudumu wa bar, unaiacha kampani yote ya walevi uliyokuwa unakutana nayo..
Kadhalika kama ulikuwa unavuta sigara, unakwenda kutupa pakti zote za sigara ulizokuwa nazo, unafuta namba za watu waliokuwa wanakuletea sigara hizo au bangi hizo…na unaacha moja kwa moja! Huachi kidogo kidogo hapana..unaacha moja kwa moja…usidanganywe na uongo wa shetani kwamba ukiacha ghafla utakufa!..hutakufa! Bwana atakusaidia kuishinda hiyo hali..Lakini ukiogopa na kuhisi kwamba utakufa utakapoacha madawa ya kulevya ghafla nataka nikuambie usipoacha ndio utakufa…hivyo acha!…Bwana hawezi kukuambia uache halafu ashindwe kujua namna ya kukuzuia usipate madhara, yeye si mwanadamu. Anaposema acha kitu Fulani anajua ni namna gani ya kukusaidia kushinda hicho kitu.
Kadhalika kama ni Mwasherati na unayejichua unaacha uasherati wako na kujichua kwako! Na mustarbation zako,..unaacha na vyanzo vyake vyote na malighafi zake zote…Unatoka kwenye huo mtandao wa makahaba uliopo sasa, unajitenga na kuliacha lile kundi ambalo mlikuwa mkikutana na kuzungumzia tu habari za zinaa..kama ulikuwa ni mfiraji na msagaji na shoga unaacha hivyo vitu kwa kumaanisha kabisa…tangu siku hiyo unatupa vile vitu ulivyokuwa unavitumia katika kusagana na unavichoma moto saa ile ile uliyomkaribisha Yesu moyoni mwako. Unafuta pia na picha zote chafu za ngono kwenye simu yako au laptop yako na unavunja vunja cd zote za ngono ulizokuwa nazo, na muvi zote ambazo unajua kabisa hazikujengi kwa lolote,na nyimbo zote za kidunia, unazifuta kwenye simu yako,. Kumbuka mambo haya yote yanapaswa yafanyike siku ile ile uliyookoka! Na sio baada ya wiki au mwezi.
Vivyo hivyo ulikuwa umepaka wanja, unakwenda kuufuta saa hiyo hiyo, na unakusanya kalamu zote za wanja na lipstick unakwenda kuzichoma moto..usimpe mtu baki …wala usitafute ushauri kwa mtu… wewe kuwa kama kichaa usiangalia kushoto wala kulia…vivyo hivyo kusanya nguo zako zote fupi na za kubana na suruali..kwa pamoja kazichome moto..hata kama utabakiwa na nguo moja tu..sema moyoni mwako kwamba “Umebeba msalaba wako umeamua kumfuata Yesu”..
Una suruali model unachoma, ulikuwa umenyoa mtindo ujulikanao kama kiduku, nenda kinyozi siku hiyo hiyo kaondoe…ulikuwa unacheza kamari, na kuhudhuria disko unahitimisha siku hiyo hiyo.. na pia kama ulikuwa unafuatilia matamthilia ya kiulimwengu ambayo dhima yake ni kuchochoea tamaa za vitu visivyofaa unaacha kuziangalia zote. Unapiga Break..Ulikuwa umejiunga na magroup ya whatsapp na facebook ya kidunia unaleft kwenye hayo magroup na kubakia tu na yale ya kikristo..Ulikuwa ni muhudhuriaji kwa waganga wa kienyeji na mshirikina na mchawi..unautupa na kuuchoma ushirikina wako na hirizi zako, na dawa zote ulizopewa na waganga….
Na mambo mengine yote ambayo hayajatajwa hapa maovu unayaacha..siku ile ile unayotubu…usisubiri baada ya siku 2 au tatu…Roho Mtakatifu hataweza kuvumilia ndani yako siku hizo zote ukiwa unaendelea na hivyo vitu…atakuacha! Na utabaki bila badiliko lolote. Na toba yako itakuwa ni bure.
Kitu ambacho watu wengi hawajui na kusababisha kila siku kuongozwa sala ya kutubu na kuwafanya wabakie katika hali ile ile ya kutokuwa na badiliko lolote rohoni..ni kwasababu huwa hawaamui kuacha dhambi pindi wanapomgeukia Kristo. Usipoamua kuacha vyote vya kiulimwengu na kumfuata Kristo hapo bado hujaokoka!..haijalishi umeombewa mara ngapi au umeongozwa sala ya kutubu mara ngapi.
Tunaona jambo hilo hata katika kanisa la kwanza…Watu baada ya kutubu walichoma mambo yao yote yaliyokuwa yanawafanya watende dhambi..
Matendo 19:17 “Habari hii ikajulikana na Wayahudi wote na Wayunani waliokaa Efeso, hofu ikawaingia wote, na jina la Bwana Yesu likatukuzwa.
18 Na wengi wa wale walioamini wakaja wakaungama, wakidhihirisha matendo yao.
19 Na watu wengi katika wale waliotumia mambo ya uganga wakakusanya vitabu vyao, wakavichoma moto mbele ya watu wote; wakafanya hesabu ya thamani yake, wakaona ya kwamba yapata fedha hamsini elfu”.
Unaona hapo!…Biblia inasema wakachoma mbele ya watu wote!..Na wewe choma usimwangalie mtu.
Sasa baada ya kufanya hayo yote, baada ya kuchoma suruali zako, kuchoma hirizi zako, vipodozi vyako, baada ya kujitenga na vikao vya walevi uliokuwa unalewa nao, baada ya kuleft magroup ya kidunia ambayo walikuwa wamekuzoea kuchangia mada, baada ya kufuta namba za wale uliokuwa unafanya nao uasherati, baada ya kuacha uasherati…
Hapo utakuwa umejikana nafsi yako!..Hivyo jambo litakalofuata hapo ni shetani kutaharuki, hapo ndipo atakaponyanyuka kinyume chako wewe, Huna budi kujaribiwa….Umemkataa shetani kwa ghafla namna hiyo! Ni lazima atanyanyuka ili kukupinga kwa nguvu..wale uliokuwa unafanya nao uasherati watakutafuta kwa nguvu na kutamani kukurudisha na kukutishia hivi au vile endapo hutarudiana nao…Huo ni wakati wa kubeba msalaba wako na kuendelea mbele..usirudi nyuma.
Wale wachawi wako ambao mlikuwa mnashuka wote vilindini..watakutafuta na kukurudia na kukutishia hivi au vile..huo ni wakati wa kubeba msalaba. Ndugu zako ambao walikuwa wamezoea kukuona ni mshabiki wa tamthilia Fulani au kitu Fulani cha kidunia watakuja na kukuuliza kulikoni?…
Huo ni wakati wa kusonga mbele usiangalie nyuma..Utapitia matusi, dhihaka, wakati mwingine kutengwa na kudharauliwa kwa kipindi Fulani lakini Kristo atakuwa upande wako…Japokuwa utakuwa unapitia dhiki nje lakini ndani yako kutakuwa na furaha ya ajabu na amani ambayo watu wa nje watakuwa hawawezi kuiona. Furaha hiyo na Amani hiyo Kristo haishushi kwa kila mtu tu, anayedai ameokoka, bali anaishusha kwa watu maalumu waliojitwika msalaba wao na kumfuata yeye.
Sasa ukiona kwamba baada ya kuokoka ndio hayo mambo yameanza…huo ndio uthibitisho kwamba kweli umempokea Kristo..lakini kama huoni chochote..basi jitathmini mara mbili mbili..inawezekana hakuna badiliko lolote katika maisha yako…
Na ukiyashinda hayo ambayo yatapita kwa muda tu, basi ipo neema ya ziada itaachiliwa kwako, na wewe utahesabiwa kama mwana wa Mungu, na mwanafunzi wa Kristo halali kama vile wale mitume wake, hivyo licha tu ya kupata uhakika wa kwenda mbinguni lakini pia jiandae kukutana na Kristo maishani mwako kwa viwango vingine ambavyo hukuwahi kukutana navyo au kumjua Kristo katika hivyo, tofauti na wanadamu wengine wa kawaida.
Hivyo ndugu yangu kama hujaokoka na leo unasema unataka kuanza maisha mapya na Kristo..gharama ni hizo hapo juu…kama upo tayari kuzichukua hizo gharama ni vyema lakini kama hujawa tayari..haulazimishwi…
Hivyo kama upo tayari, basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie maisha yako yote kama ilivyokuwa hata kwetu sisi. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.
“EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE. NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.
ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE”.
AMEN.
Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.
Zingatia hayo na Bwana atakusaidia.
Ubarikiwe sana
Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Maran atha!
Mada Nyinginezo:
NI NINI TUNAJIFUNZA JUU YA MT. DENIS WA UFARANSA?
KWANINI MUNGU ALIMTUMIA MUSA KWA VIWANGO VILE?
“Si watu wa kutumia mvinyo sana”, je tunaruhusiwa kutumia mvingo kidogo?(1Timotheo 3:8).
Biblia inatuonyesha yapo majaribio matatu ambayo shetani atajaribu kuyafanya ili kuupandikiza ufalme wake.
Jaribio la kwanza ni lile alilolifanya mbinguni, lakini akashindwa, pale alipopigwa na akina Mikaeli pamoja na malaika zake..
Ufunuo 12:7 “Kulikuwa na vita mbinguni; Mikaeli na malaika zake wakapigana na yule joka, yule joka naye akapigana nao pamoja na malaika zake;
8 nao hawakushinda, wala mahali pao hapakuonekana tena mbinguni.
9 Yule joka akatupwa, yule mkubwa, nyoka wa zamani, aitwaye Ibilisi na Shetani, audanganyaye ulimwengu wote; akatupwa hata nchi, na malaika zake wakatupwa pamoja naye”
Jaribio la pili, atakuja kulifanya mara baadaya ya unyakuo kupita..Hapo ndipo Ibilisi atayakusanya mataifa yote ulimwenguni yaliyomwasi Mungu ili kupigana na Mungu mwenyezi, Hii ndio ile vita ya Harmagedoni.
Ufunuo 16:13 “Nikaona roho tatu za uchafu zilizofanana na vyura, zikitoka katika kinywa cha yule joka, na katika kinywa cha yule mnyama, na katika kinywa cha yule nabii wa uongo.
14 Hizo ndizo roho za mashetani, zifanyazo ishara, zitokazo na kuwaendea wafalme wa ulimwengu wote kuwakusanya kwa vita ya siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi.
15 (Tazama, naja kama mwivi. Heri akeshaye, na kuyatunza mavazi yake, asiende uchi hata watu wakaione aibu yake.)
16 Wakawakusanya hata mahali paitwapo kwa Kiebrania, Har-Magedoni”.
Na jaribio la tatu na la mwisho, litakuja mara baada ya ule utawala wa miaka 1000 kuisha,.Pale atakapofunguliwa kwa muda mchache tu kayadanganya mataifa tena., siku hiyo mataifa yatakusanyika pamoja, na kwenda kuizingira kambi ya watakatifu, hili nalo litashindwa vilevile kwani muda huo huo moto utashuka kutoka mbinguni na kuwaangamiza wote..Na shetani mwisho wake utakuwa umefika..Na majeshi yake yote..Kwani atakamatwa na kutupwa katika lile ziwa la moto na kuteswa huko milele na milele.
Ufunuo 20:7 “Na hiyo miaka elfu itakapokwisha, Shetani atafunguliwa, atoke kifungoni mwake;
8 naye atatoka kuwadanganya mataifa walio katika pembe nne za nchi, Gogu na Magogu, kuwakusanya kwa vita, ambao hesabu yao ni kama mchanga wa bahari.
9 Wakapanda juu ya upana wa nchi, wakaizingira kambi ya watakatifu, na mji huo uliopendwa. Moto ukashuka kutoka mbinguni, ukawala.
10 Na yule Ibilisi, mwenye kuwadanganya, akatupwa katika ziwa la moto na kiberiti, alimo yule mnyama na yule nabii wa uongo. Nao watateswa mchana na usiku hata milele na milele”.
Sasa ukichunguza hapo utaona shetani tayari alishashindwa tangu zamani katika jaribio la kwanza, na hukumu yake ilishapitishwa kabla hata ya wanadamu kuumbwa..Alikuwa ameshatupwa chini akingojea siku yake ifike ateketezwa kabisa, Lakini ghafla alipoona Mungu anaanza kuiumba tena dunia, na kuifanya kuwa sehemu ya kukaliwa na viumbe hai, na kumwona mwanadamu aliyeumbwa na Mungu kwa mfano wake na sura yake amewekwa katika bustani nzuri ya Edeni..
Alijaribu bahati yake, aone kama ataweza kuupata ufalme kwa kupitia hawa wanadamu walioumbwa kwa mfano wake na sura yake, Na alipoona jaribio lake la kwanza limefanikiwa, ndipo alipopata nguvu ya kuiendeleza kazi hiyo kwa kasi, ikawa kazi yake ni moja tu KUDANGANYA. Basi..akawaletea huduma na nyingine nyingi kama vile uchawi, uuaji, uongo, wizi n.k ili atimize tu azimio lake la kuwateka wanadamu wote..
Alipoona watu wengi wanazidi kuwa upande wake, ndipo akazidi kupata nguvu ulimwenguni, nafsi yake ikahuika upya, mawazo yake ya kuwa ameshindwa yakafa, akazidi kuidanganya dunia kwa bidii kubwa hadi karibu watu wote ulimwengu wakatekwa na yeye kipindi cha Nuhu, ndipo akawa mungu wa ulimwengu huu.
Lakini Mungu alipoona hivyo akaiangamiza dunia katika gharika,..Sasa kuanzia huo wakati akawa anawatumia wanadamu kujaribu kuuangusha ufalme wa Mungu, kwasababu yeye mwenyewe tayari alishashindwa zamani..Akaanza kutumia wafalme wengi sana kujaribu kuuangusha ufalme wa mbinguni ndani ya watu wa Mungu Israeli, huo ndio mpango wake hadi siku za mwisho kutumia mataifa kupambana na uzao wa Mungu.
Lakini kama kawaida atashindwa..
Ninachotaka leo tuone ni kuwa.. Shetani kama shetani hawezi kupata nguvu kama sisi, wenyewe hatutamruhusu apate nguvu.
Unapovaa vimini, na nguo fupi na kutembea uchi barabarani unampa shetani ufalme na nguvu, na sababu za yeye kuendelea mbele kuiharibu hii dunia na kuwapeleka maelfu ya watu kuzimu..Unapokunywa pombe, unapofanya uzinzi, unapokwenda disko, unapofanya mambo yote yasiyompendeza Mungu..Basi hapo ni unampa ibilisi nguvu za kuimiliki hii dunia..
Hata mpinga-kristo atakaponyanyuka,hatanyanyuka kwa nguvu zake mwenyewe bali atapewa nguvu na watu waovu wasiomcha Mungu. Shetani yeye mwenyewe alishashindwa, na wala hana nguvu yoyote ya kupigana, ni kiumbe dhaifu tu cha kushindwa siku zote, alikuwa kwenye giza nene bila tumaini lolote, lakini pale tunapomsifia kazi zake, tunapozifurahia kazi zake, basi anahuika na kupata nguvu ya kuwaharibu watu.
Hizi ni nyakati za mwisho. Angalia mataifa yote sasa yanaelekeza macho yao Israeli, idadi ya mataifa yanayolipinga taifa la Israeli yanazidi kuongezeka kwa kasi, na huo ni mpango wa shetani mwenyewe tangu zamani..na hiyo ni mojawapo ya dalili za siku za mwisho,…kwasababu anajua kuwa Masiya (YESU KRISTO) atashukia pale, na pale ndipo patakapokuwa makao makuu yake wakati wa kipindi cha utawala wa miaka 1000. Hivyo anachofanya kwa bidii sasa kuyaleta mataifa haya yote pamoja, ili kutimiza lile azimio la vita vya harmagedoni,..
Leo hii wala usitishwe kuona migogoro ya mataifa mengine, labda Korea, na Marekani, au Irani, au Urusi ukadhani kuwa hayo ndiyo yataleta vita ya Harmagedoni, hapana, iangalie Israeli kwasababu pale ndipo lile bonde la kukata maneno litakapokuwepo,..Pale ndipo patakapokuwa mwisho wa kila kitu..tageti yote ya shetani ipo pale..
Ndugu kama hujaokoka, ni heri ukafanya hivyo sasa, tubu dhambi zako, mkaribishe YESU maishani mwako, ili uache kumpa nguvu shetani kiumbe cha kushindwa, na uanze kuujenga ufalme wa BWANA YESU KRISTO, Mfalme wa wafalme, ambaye ufalme ni wake, na nguvu, na utukufu hata milele..
Shetani wakati wake ni mfupi sana, lakini Bwana wetu YESU KRISTO, ni mfalme wa milele, yeye hashindwi, wala hashindani, atakapokuja kutawala na sisi wakati huo hakika tutaufurahia ufalme wake, atatufuta haya machozi, wala hizi shida hazitakuwepo tena, wala madhaifu, wala magonjwa, wala mateso wala shida…hivyo tukaze mwendo ili tufikie huo.
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Ikiwa utapenda tuwe tunakutumia masomo kwa njia ya whatsapp ya kila siku basi, bofya hapa uweze kujiunga >>> WHATSAPP Au tuandikie kwa namba hizi +255789001312
Mada Nyinginezo:
NILIMWONA SHETANI, AKIANGUKA KUTOKA MBINGUNI.
DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.
Nifanyeje niwe mwombaji mzuri, wa masafa marefu?