Category Archive Home

Utii ni nini? na ni nani tunayepaswa kumtii au kutokumtii?

Utii ni nini kibiblia?


Utii ni kitendo cha kukubali kufanya maelekezo au maagizo unayopewa na aliye na mamlaka ya juu Zaidi yako wewe bila kujali  linakubaliana na maamuzi yako au la!.

Lakini pamoja na hayo watu wengi hawajui kuwa utii unaweza pia kutanguliwa na isihesabiwe kuwa ni dhambi ya kutokutii mbele za Mungu, Lakini hiyo ni katika mazingira maalumu ambayo tutajifunza mbele kidogo katika somo letu hili.

Ili kujua ni wakati gani tunapaswa tusitii Ni vizuri kwanza tukawajua watu ambao biblia imetuagiza tuwatii wakati wote:

1 Utii kwa wazazi wetu:

Wakolosai 3:20  “Ninyi watoto, watiini wazazi wenu katika mambo yote; maana jambo hili lapendeza katika Bwana”

Hili ni agizo la Mungu kwa kila mwenye baba, au mama au mlezi, Mungu ametuagiza tuwatii wazazi wetu, kwa kila wanachotuelekeza kufanya. Na zipo baraka nyingi  katika kufanya hivyo  ikiwemo kupewa upendeleo wa kuishi umri mrefu hapa duniani

Kutoka 20:12 Waheshimu baba yako na mama yako; siku zako zipate kuwa nyingi katika nchi upewayo na Bwana, Mungu wako.

https://www.high-endrolex.com/12

Hata Bwana wetu Yesu Kristo alikuwa na utii huu ukisoma Luka 2:51 inasema .. “Akashuka pamoja nao mpaka Nazareti, naye alikuwa akiwatii; na mamaye aliyaweka hayo yote moyoni mwake.

Vivyo hivyo na sisi tunapaswa tuwe na huu utii kwa faida zetu wenyewe. Na pia kuyatimiza maagizo ya Mungu.

2 Utii kwa Mume:

Wake wamepewa maagizo ya kuwatii waume zao kwa kila namna.

1Petro 3:1 ” Kadhalika ninyi wake, watiini waume zenu; ……5  Maana hivyo ndivyo walivyojipamba wanawake watakatifu wa zamani, waliomtumaini Mungu, na kuwatii waume zao. 6  Kama vile Sara alivyomtii Ibrahimu, akamwita Bwana; nanyi ni watoto wake, mfanyapo mema, wala hamkutishwa kwa hofu yo yote”

Soma pia Wakolosai 3:18 utaliona jambo hilo hilo.. Ikiwa wewe ni mke, halafu huisikii sauti ya mume wako labda kwasababu anakipato cha chini au anamapungufu fulani, au ni mwenye dhambi usidhani kuwa Mungu yupo upande wako. Unapaswa umtii na ujishushe kwasababu hayo ndiyo maagizo ya Mungu.

#3 Utii kwa wazee:

1Petro 5:5  “Vivyo hivyo ninyi vijana, watiini wazee. Naam, ninyi nyote jifungeni unyenyekevu,..”

Mungu ametupa maagizo kama vijana, kuwathamini wazee, katika kanisa na vilevile katika jamii. Wanapotoa Mashauri hatupaswi kuwapinga au kujibishana nao,..Tukifanya hivyo tusidhani kuwa Mungu yupo upande wetu. Tunapaswa tuwape heshima kama vile wazazi wetu wenyewe ndivyo Mungu atakavyotufanikisha.

1Timotheo 5:17  Wazee watawalao vema na wahesabiwe kustahili heshima maradufu; hasa wao wajitaabishao kwa kuhutubu na kufundisha

1Timotheo 5.1  Mzee usimkemee, bali umwonye kama baba; na vijana kama ndugu;

#4 Utii kwa viongozi wetu wa Imani:

Bwana anatuagiza, tuwatii wale wanaotungoza katika njia ya wokovu. Na ndio maana Paulo alimwandikia Filemoni maneno haya:

Filemoni 1:21  “Kwa kuwa nakuamini kutii kwako ndiyo maana nimekuandikia, nikijua ya kuwa utafanya zaidi ya hayo nisemayo”

Lakini tukipashana nao kauli au kuwavunjia heshima, au kutowasikiliza, basi tujue kuwa tunampinga Mungu, na Hivyo Mungu hawezi kuwa upande wetu hata katika huduma zetu.

#5 Utii kwa mabwana zetu (ma-boss):

Waefeso 6:5  “Enyi watumwa, watiini wao walio bwana zenu kwa jinsi ya mwili, kwa hofu na kutetemeka, kwa unyofu wa moyo, kana kwamba ni kumtii Kristo;

6  wala si kwa utumwa wa macho tu kama wajipendekazao kwa wanadamu bali kama watumwa wa Kristo, mkitenda yampendezayo Mungu kwa moyo;

7  kwa nia njema kama kumtumikia Bwana wala si mwanadamu;

8  mkijua ya kuwa kila neno jema alitendalo mtu atapewa lilo hilo na Bwana kwamba ni mtumwa au kwamba ni huru.”

Ikiwa utamvunjia heshima boss wako, ukafukuzwa kazi, usidhani kuwa Mungu atakuwa na wewe hata katika hiyo kazi nyingine mpya utakayokwenda kuitafuta. Haijalishi wewe ni mkristo au la..Maadamu umewekwa chini ya boss wako, basi huna budi kutii yale yote anayokuagiza kufanya bila unafiki..

#6 Utii kwa wenye mamlaka (Serikali):

Tito 3:1  “Uwakumbushe watu kunyenyekea kwa wenye uwezo na mamlaka, na kutii, na kuwa tayari kwa kila kazi njema; 2  wasimtukane mtu ye yote, wasiwe wagomvi, wawe wema, wakionyesha upole wote kwa watu wote.

Serikali na mamlaka zote zinafanya kazi ya Mungu, hivyo pale inapotuagiza tulipe kodi tunapaswa kufanya hivyo, inavyotuagiza tusifanye hiki au kile tunapaswa tutii..Lakini kama tutakwenda kinyume na serikali, kwa kiburi chetu wenyewe basi tujue kuwa Mungu hapo nasi hawezi kuwa na sisi.

#7 Utii kwa Mungu:

Huu ndio utii ulio wa juu Zaidi kuliko wote.. Biblia inatuambia katika Yakobo 4:7  “Basi mtiini Mungu…”.. Utii huu tunaweza kuuona  ukijidhihirishwa katika ukamilifu wote kwa Bwana wetu Yesu Kristo.

Wafilipi 2:7  “bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu; 8  tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa MTII hata mauti, naam, mauti ya msalaba. 9  Kwa hiyo tena Mungu alimwadhimisha mno, akamkirimia Jina lile lipitalo kila jina; 10  ili kwa jina la Yesu kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi; 11  na kila ulimi ukiri ya kuwa YESU KRISTO NI Bwana, kwa utukufu wa Mungu Baba.

Inatuambia tena…

Waebrania 5:7  Yeye, siku hizo za mwili wake, alimtolea yule, awezaye kumwokoa na kumtoa katika mauti, maombi na dua pamoja na kulia sana na machozi, akasikilizwa kwa jinsi alivyokuwa mcha Mungu;

8  na, INGAWA NI MWANA, ALIJIFUNZA KUTII kwa mateso hayo yaliyompata;

9  naye alipokwisha kukamilishwa, akawa sababu ya wokovu wa milele kwa watu wote wanaomtii;

Vivyo hivyo na sisi kila mmoja Maisha yetu yanapaswa yawe ya utii, tukilitii Neno la Mungu, kila tunapoagizwa tulifanye.

Lakini sasa Je! ninapaswa kuwatii wote hawa hata kama mmojawao anachoniambia kinakinzana na maagizo ya Mungu?

Biblia imeweka wazi kabisa katika hali kama hiyo tunapaswa tusitii maagizo ya mtu yeyote bali ya Mungu kwanza..Ukisoma katika biblia utaona kuna wakati mitume walizuiliwa kuhubiri injili na wenye mamlaka na viongozi wa Dini lakini mitume walewale waliosema watiini wenye mamlaka ndio wakawa wa kwanza kusema..Imetupasa kumtii Mungu kuliko mwanadamu,

Matendo 5:27  “Walipowaleta, wakawaweka katika baraza. Kuhani Mkuu akawauliza,

28  akisema, Je! Hatukuwaamuru ninyi kwa nguvu, msifundishe kwa jina hili? Nanyi, tazameni, mmeijaza Yerusalemu mafundisho yenu, na mnataka kuileta damu ya mtu yule juu yetu.

29  Petro na mitume wakajibu, wakisema, Imetupasa kumtii Mungu kuliko wanadamu”

Leo hii mama au baba yako anaweza kukwambia ufanye mila za matambiko, Na huku wewe unajua kabisa jambo hilo linakinzana na maandiko, hapo hupaswi kumtii mzazi wako hata kama itaonekana amewavunjia heshima kiasi gani…

Wazazi

Au wazazi wanakushurutisha unywe pombe, au ufanye dhambi, hapo unaruhusiwa kutowatii kwasababu utii huo hautokani na Mungu na hivyo mbele za Mungu hutahesabika kuwa hajawatii wazazi wako.. Maandiko yanathibitisha hilo (Mathayo 10:37)

Serikali

Vilevile, Serikali imekupiga marufuku usiabudu. Au usihubiri injili, Hapo unapaswa usiitii serikali hata kama ni Mungu ndiye aliyeruhusu tutii mamlaka hizo. Ilimtokea Danieli, lakini yeye alihesabu mamlaka na Mungu ni kubwa kuliko mamlaka zote, hivyo alichofanya ni kufungua madirisha kabisa watu wote wamwone akiabudu, bila woga wowote, Na sisi vivyo hivyo hatupaswai kuogopa kuyashika maagizo ya Mungu Zaidi ya wanadamu.

Mume.

Au Mume, anakushurutisha mfanye tendo la ndoa kinyume cha maumbile, hapo hupaswi kumtii, mume wako, kwasababu maagizo hayo yanakinzana na Neno la Mungu..Hata kama akikutisha kukuacha, mwache aende, utiifu wa Mungu ni Zaidi ya utiifu mwingine wowote.

Au boss wako anakulazimisha uingie katika mikataba ya rushwa, Na huku unajijua kabisa kuwa unachofanya kinakinzana na Imani yako, hapo hupaswa kumkubalia, au anakulazimisha ufanya naye uzinzi, hapo pia hupaswa kumkubalia haijalishi ni boss wako anayeheshimika kiasi gani. Au maandiko yamekuagiza uwatii hao kiasi gani.

Hivyo UTIIFU wowote ni lazima upatane na maagizo ya Mungu, kama haukinzani na Neno la Mungu hapo unapaswa utii yote unayoelekezwa kwa moyo wote bila kiburi..Na ndivyo Mungu atakavyokufanikisha..

Kwasababu kinyume na hapo, ukosefu wa utiifu wowote, ni kazi ya shetani ambayo siku hizi za mwisho ndio umekita mizizi..

2 Timotheo 3:1  Lakini ufahamu neno hili, ya kuwa siku za mwisho kutakuwako nyakati za hatari.2  Maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, wenye kutukana, WASIOTII WAZAZI WAO, wasio na shukrani, wasio safi.

Je! Umeokoka?

Je ndani yako kiburi kimekaa? Je unajua kuwa watu wa namna hiyo hawataurithi uzima wa milele? Je Unafahamu kuwa tunaishi katika kanisa la mwisho lijulikanalo kama Laodikia, na hatutakuwa na kanisa lingine Zaidi ya hili, Na unyakuo ni wakati wowote kwasababu dalili zote zimeshatimia?.. Kwanini usimpe leo Kristo Maisha yako.? Kwanini usiwe na uhakika wa kwenda mbinguni hata ukifa leo?

Kama upo tayari kufanya hivyo sasahivi.. basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie maisha yako yote kama ilivyokuwa hata kwetu sisi. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, .
NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.

AMEN.

Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu, unatii sasa kwa kunayaacha na kujitenga nayo, Na Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.

Ubarikiwe sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako piga namba hii 0789001312

Group la whatsapp Kwa mgawanyo bora wa masomo download App hapa>> App wingu la mashahidi

Mada Nyinginezo:

MAAGIZO AMBAYO HAYAJAAGIZWA!

LISHIKILIE SANA LILE AGIZO LA KWANZA.

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA KITABU CHA TITO.

KWANINI YESU NI ADAMU WA PILI?

KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 3

Rudi Nyumbani:

Print this post

NGUVU YA MSAMAHA

Karibu tujifunze mambo yafuatayo; Nguvu ya msamaha ipo wapi? Biblia inaposema achilieni nanyi mtaachiliwa ina maana gani?Je kumpeleka mtu polisi au mahakamani ni kutokusamehe?

Neno Msamaha, halina tofauti sana na Neno ‘kuachilia’ au ‘kufungulia’. Unapomsamehe mtu aliyekukosea ni sawa na umemwachilia huru katika moyo wako. Huna naye deni tena, anakuwa anatoka katika kifungo cha moyo wako. Na kila mwanadamu anapaswa awe na huo uwezo wa kusamehe..Kwasababu msamaha ni ufunguo wa kitu kikubwa sana katika maisha.

Ingawa kwa akili za kawaida za kibinadamu ni ngumu kusamehe. Lakini ukiwa Mkristo(uliyeoshwa kwa damu ya Yesu Kristo na kufanyika kiumbe kipya) ni rahisi kusamehe. Na msamaha ule unaohusisha vitu ambavyo ni vigumu kusamehe huwa ndio unamaana kubwa sana na unafaida kubwa zaidi kuliko ule wa vitu vidogo.

Nguvu ya Msamaha upo katika Mistari ifuatayo.

Luka 6:36 ‘Basi, iweni na huruma, kama Baba yenu alivyo na huruma.

37 Msihukumu, nanyi hamtahukumiwa; msilaumu, nanyi hamtalaumiwa; achilieni, nanyi mtaachiliwa.

38 Wapeni watu vitu, nanyi mtapewa; kipimo cha kujaa na kushindiliwa, na kusukwa-sukwa hata kumwagika, ndicho watu watakachowapa vifuani mwenu. Kwa kuwa kipimo kile kile mpimacho ndicho mtakachopimiwa’

Hapo anasema ‘achilieni’….Faida za kuachilia ni nini?..mbele kidogo anasema ‘nanyi mtaachiliwa’. Ikiwa na maana kuwa unapomsamehe mtu na wewe umeweka deni mahali fulani la kusamehewa…kwa kipimo kile kile na uzito ule ule uliomsaheme mtu…Na wewe unalo deni la kusamehewa kwa kiwango hicho hicho mahali fulani..wakati fulani.

Wengi wetu hatujui au hatuna taarifa kuwa kuna Mungu juu anayeyatazama maisha..Ukishaikosa au kupungukiwa na hiyo Imani basi ni ngumu sana kuyaishi maneno ya Mungu. Siku zote kumbuka Mungu yupo juu anatutazama, kila tendo, kila neno na kila tukio tulifanyalo..na yeye hasahau, wala hasinzii, wala hapumziki..Kwahiyo kila kitu tukifanyacho kiwe kibaya kiwe kizuri anakirekodi na kila kitu kina mshahara wake..Vingine mishahara yao ni hapa hapa duniani na vingine ni kule katika ulimwengu ujao.

Ufunuo 22:12 ‘Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo’.

Kwahiyo kama ulitukanwa na hujasamehe…Na wewe pia hujasamehewa matusi ya siri uliyoyatoa moyoni mwako dhidi ya mwingine. Haijalishi unayakumbuka au huyakumbuki…mbele za Mungu hayajasahaulika hata moja.

Tusome tena mfano ufuatao wa mwisho.

Mathayo 18:21 ‘Kisha Petro akamwendea akamwambia, Bwana, ndugu yangu anikose mara ngapi nami nimsamehe? Hata mara saba?

22 Yesu akamwambia, Sikuambii hata mara saba, bali hata saba mara sabini.

23 Kwa sababu hii ufalme wa mbinguni umefanana na mfalme mmoja aliyetaka kufanya hesabu na watumwa wake.

24 Alipoanza kuifanya, aliletewa mtu mmoja awiwaye talanta elfu kumi.

25 Naye alipokosa cha kulipa, bwana wake akaamuru auzwe, yeye na mkewe na watoto wake, na vitu vyote alivyo navyo, ikalipwe ile deni.

26 Basi yule mtumwa akaanguka, akamsujudia akisema, Bwana, nivumilie, nami nitakulipa yote pia.

27 Bwana wa mtumwa yule akamhurumia, akamfungua, akamsamehe ile deni.

28 Mtumwa yule akatoka, akamwona mmoja wa wajoli wake, aliyemwia dinari mia akamkamata,akamshika koo,akisema Nilipe uwiwacho

29 Basi mjoli wake akaanguka miguuni pake, akamsihi, akisema, Nivumilie, nami nitakulipa yote pia.

30 Lakini hakutaka, akaenda, akamtupa kifungoni, hata atakapoilipa ile deni.

31 Basi wajoli wake walipoyaona yaliyotendeka, walisikitika sana, wakaenda wakamweleza bwana wao yote yaliyotendeka.

32 Ndipo bwana wake akamwita, akamwambia, Ewe mtumwa mwovu, nalikusamehe wewe deni ile yote, uliponisihi;

33 nawe, je! Haikukupasa kumrehemu mjoli wako, kama mimi nilivyokurehemu wewe?

34 Bwana wake akaghadhibika, akampeleka kwa watesaji, hata atakapoilipa deni ile yote.

35 Ndivyo na Baba yangu wa mbinguni atakavyowatenda ninyi, msiposamehe kwa mioyo yenu kila mtu ndugu yake’.

Umeona…Nguvu ya msamaha ipo kwenye vile unavyovisamehe…Unapomsamehe mtu 100 basi na wewe unastahili kusamehewa 100..Kadhalika unaposamehewa vitu 100 na wewe una deni la kusamehe vitu 100.

Hakunaga short-cut ya kupokea msamaha…bila kusamehe, hakikisha unasamehe kwanza ili na wewe pia usamehewe…Bwana Yesu alisema hivyo katika…

Mathayo 6:14 “Kwa maana mkiwasamehe watu makosa yao, na Baba yenu wa mbinguni atawasamehe ninyi.

15 Bali msipowasamehe watu makosa yao, wala Baba yenu hatawasamehe ninyi makosa yenu”.

Sasa utauliza hata mtu akinidhulumu vitu vyangu vyote nimsamehe?…Ndio msamehe..hiyo ni kwa faida yako binafsi…Utakuwa umemwachia Mungu wako deni kubwa la yeye kukurehemu wewe sawasawa na jinsi ulivyomsamehe mwingine…Ukumbuke huo mfano hapo juu.

Sasa swali lingine linakuja…Je kumpeleka mtu polisi au mahakamani ni kutomsamehe?

Yapo mazingira ya mtu kupelekwa polisi au mahakamani…ambapo sio dhambi.

Kwamfano imetokea mwizi kakuibia na umemfahamu, na ulipojaribu kumwendea ukakuta kakificha kile kitu au kashakitumia na hataki kukiri kwamba yeye ni mwizi wala kutubu…Mtu kama huyo moyoni unamsamehe kabisa kwa moyo wote…lakni pia anapaswa akashtakiwe kwa watu wa karibu au polisi ili asiendeleze wizi huo kwako na kwa wengine. (Kwa kufanya hivyo Sio dhambi) na hautahesabika kama hujamsamehe mbele za Mungu.

Kadhalika kama umedhulumiwa mali yako isivyo halali na kuna nafasi ya kuirudisha, pambana kuirudisha kwa hekima…Mfuate aliyeichukua mwambie akurudishie akikataa na kuna nafasi ya kumshtaki..mshataki ili aogope akurudishie na ili siku nyingine asirudie kufanya hivyo kwako au kwa wengine…Lakini akija kwako na kutubu na kukiri kwamba ni kweli kakudhulumu lakini mali ile kashaitumia na hana tena..na anatubu mbele zako…hapo huna budi kumsamehe asilimia zote na kumkumbatia. Hupaswi kwenda kumshtaki, kwasababu kashakiri kosa lake. Unapaswa umsamehe kabisa. (Ukikumbuka siku zote kwamba nguvu ya msamaha ipo katika kusamehe).

Ukiwasamehe waliokuudhi, Bwana atakusamehe uliyomuudhi…Ukiwasamehe waliokudhulumu…Bwana atakusamehe dhuluma ulizozifanya ndogo ndogo hata kama huzikumbuki…Ukimsamehe mtu aliyekuudhi siku moja na wewe utamuudhi mwingine na Bwana atampa moyo wa kukusamehe wewe.

Ukimsaheme mtu anayetamani kusamehewa na wewe, siku moja na wewe utasamehewa na mtu ambaye ungetamani akusamehe.

Mithali 16:7 “Njia za mtu zikimpendeza Bwana, Hata adui zake huwapatanisha naye”.

Bwana akubariki.

Usisahau tena “nguvu ya msamaha ipo katika kusamehe”

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii 0789001312


Mada Nyinginezo:

SAMEHE KUTOKA NDANI YA MOYO WAKO.

UMUHIMU WA KUOMBA MSAMAHA.

DHAMBI ISIYO NA MSAMAHA.

Kwanini pale Bwana Yesu alichukua hatua ya kumsamehe dhambi kwanza kabla ya kumponya yule mtu mwenye kupooza?(Marko 2).

UWEPO WA BWANA HATA KATIKATI YA MATESO.

DUNIANI MNAYO DHIKI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

IFANYE KAZI YA MUNGU PASIPO HOFU!

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe, karibu tujifunze Biblia..

Jambo mojawapo ambalo shetani anapenda kulitumia ili kuikatisha kazi ya Mungu ni kutumia vitisho?..Kwamfano utaona katika agano la kale wakati fulani ambapo Mungu aliwarudisha tena wana wa Israeli katika nchi yao baada ya kukaa utumwani Babeli kwa muda wa miaka 70 aliwaagiza watakaporudi wamjengee nyumba….Na kweli waliporudi walianza harakati za kuijenga nyumba ya Bwana huo Yerusalemu.Lakini kilichotokea ni kwamba..kazi ile haikudumu kwa muda mrefu..kwani maadui zao baada ya kuona wanaijenga nyumba ile waliwainulia visa…ikiwemo kwenda kupeleka taarifa kwa Mfalme kwamba watu baadhi fulani wanaijenga nyumba ambayo ilibomolewa kwa makusudi fulani…Hujuma zile zilipomfikia Mfalme akatoa amri kazi ile isimamishwe mara moja…Na wale watu wakamwogopa mfalme wakaacha kuifanya ile kazi..

Ezra 4:11 “Hii ndiyo nakili ya waraka waliyompelekea mfalme Artashasta; watumishi wako,watu walio ng`ambo ya mto wakadhalika.

12 Ijulikane kwa mfalme ya kuwa Wayahudi, waliokwea kutoka kwako, wamefika kwetu Yerusalemu; nao wanaujenga ule mji mwasi, mbaya; wamemaliza kuta zake, na kuitengeneza misingi yake.

13 Basi, ijulikane kwa mfalme, ya kuwa mji huu ukijengwa, na kuta zake zikimalizika, hawatatoa kodi, wala ada, wala ushuru, na mwisho wake wafalme watapata hasara.

14 Na sisi, kwa kuwa tunakula chumvi ya nyumba ya mfalme, wala si wajibu wetu kumwona mfalme akivunjiwa heshima, basi tumetuma watu na kumwarifu mfalme.

15 Ili habari zitafutwe katika kitabu cha tarehe za baba zako; ndivyo utakavyopata kujua kwa kitabu cha tarehe ya kuwa mji huo ni mji mwasi, wenye kuwadhuru wafalme, na maliwali, na ya kuwa wenyeji wake wamefanya fitina katika mji huo zamani; ndiyo sababu mji huo ukaangamizwa.

16 Twamwarifu mfalme ya kuwa mji huo ukijengwa, na kuta zake zikimalizika, hutakuwa na sehemu ya nchi ng’ambo ya Mto.

17 Ndipo mfalme akapeleka majibu;Kwa Rehumu,Bwana shauri, na Shimshai,mwandishi na wenzao wengine waliokaa katika Samaria,na penginepo ng`ambo ya mto, Salamu; wakadharika.

18 Ule waraka mlionipelekea umesomwa mbele yangu, nami nikaelewa na maana yake.

19 Nikatoa amri, na watu wametafuta habari; ikaonekana ya kuwa mji huu zamani umefanya fitina juu ya wafalme, na ya kuwa uasi na fitina zimefanyika ndani yake.

20 Tena walikuwako wafalme wakuu juu ya Yerusalemu, waliotawala nchi yote iliyo ng’ambo ya Mto; wakapewa kodi, na ada, na ushuru.

21 Sasa toeni amri kuwakomesha watu hawa kazi yao, mji huu usijengwe, hata mimi nitakapotoa amri. 22 Tena jihadharini, msilegee katika jambo hili; kwa nini madhara yazidi, na wafalme wapate hasara?

23 Hata nakala ya waraka huo wa mfalme Artashasta uliposomwa mbele ya Rehumu, Bwana shauri, na Shimshai, mwandishi, na wenzao, wakaenda Yerusalemu upesi, kwa Wayahudi, wakawakomesha kwa nguvu na kwa kuwashurutisha.

24 Hivyo kazi ya nyumba ya Mungu iliyoko Yerusalemu ikakoma; nayo ikakoma hata mwaka wa pili wa kutawala kwake Dario, mfalme wa Uajemi”.

Kama tunavyoona tendo hilo likawafanya wayahudi waiogope amri ya mfalme Zaidi ya maagizo ya Mungu ambayo waliambiwa waijenge nyumba ile bila woga!..Wakaendelea kukaa katika hali hiyo kwa muda mrefu mpaka Mungu alipozifunga mbingu mvua ziwe chache na chakula cha shida, Mpaka Mungu alipowatuma tena manabii wake Zekaria na Hagai kuwaambia watu watoke wakaijenge nyumba ya Mungu pasipo kuogopa chochote na Bwana atakuwa nao. Na walipowatii manabii wale walitoka na kwenda kukusanya vifaa vyote na vitu vyote vya ujenzi tayari kuanza kazi bila kujali tamko la mfalme..wakati wanaanza wale maadui zao tena wakapata taarifa na kumpelekea mfalme…

Lakini Mungu aliugeuza moyo wa mfalme kwa namna isiyoelezeka badala ya kuwapinga wayahudi kinyume chake alikubaliana nao..na zaidi ya yote akawafadhili kwa mali katika ujenzi wao..hivyo nyumba ya Mungu ikajengwa na kusitawi pasipo shida yoyote..Na Mungu akawabariki Israeli.

Ezra 5:1 “Basi manabii, Hagai nabii, na Zekaria mwana wa Ido, wakawafanyia unabii Wayahudi waliokuwako Yerusalemu na Yuda; waliwafanyia unabii kwa jina la Mungu wa Israeli.

2 Ndipo akaondoka Zerubabeli, mwana wa Shealtieli, na Yoshua, mwana wa Yosadaki, wakaanza kuijenga nyumba ya Mungu iliyoko Yerusalemu; na pamoja nao walikuwa manabii wa Mungu, wakiwasaidia.

3 Wakati ule ule Tatenai, liwali wa ng’ambo ya Mto, na Shethar-Bozenai, na wenzi wao, wakawajia, wakawaambia, Ni nani aliyewapa amri kuijenga nyumba hii, na kuumaliza ukuta huu?

4 Ndipo wakawauliza hivi, Majina ya watu wanaofanya ujenzi huu ni nani na nani?

5 Lakini jicho la Mungu lilikuwa likiwaelekea wazee wa Wayahudi, hao wasiwazuie, hata habari ile imfikilie Dario, ndipo jawabu litakapopatikana kwa waraka.

6 Hii ndiyo nakala ya waraka waliyompelekea mfalme Dario; na Tatenai, liwali wa ng’ambo ya Mto, na Shethar-Bozenai, na wenzake wa Kiajemi, waliokuwako huko ng’ambo ya Mto,

7 walimpelekea waraka nao; na maneno haya yakaandikwa ndani yake; Kwa Dario, mfalme; Salamu sana.

8 Na ajue mfalme ya kuwa sisi tuliingia nchi ya Yuda, tukafika kunako nyumba ya Mungu mkuu, iliyojengwa kwa mawe makubwa, na miti imetiwa katika kuta zake, na kazi hii inaendelea kwa bidii, na kusitawi katika mikono yao.

9 Ndipo tukawauliza wale wazee, tukawaambia hivi, Ni nani aliyewapa amri kuijenga nyumba hii, na kuumaliza ukuta huu?

10 Tukawauliza pia majina yao, ili kukuarifu wewe, tupate kuandika majina ya watu waliokuwa wakubwa wao.

11 Wakatujibu hivi, wakasema, Sisi tu watumishi wa Mungu wa mbingu na nchi, nasi tunaijenga nyumba iliyojengwa zamani sana, yapata miaka mingi, ambayo mfalme mkuu wa Israeli aliijenga na kuimaliza.

12 Lakini hapo baba zetu walipomkasirisha Mungu wa mbingu na nchi, hata akaghadhibika, akawatia katika mkono wa Nebukadreza, mfalme wa Babeli, Mkaldayo, naye ndiye aliyeiharibu nyumba hii, akawachukua watu mateka mpaka Babeli.

13 Lakini katika mwaka wa kwanza wa Koreshi, mfalme wa Babeli, Koreshi, mfalme, alitoa amri ijengwe tena nyumba ya Mungu.

14 Na vyombo vya dhahabu na fedha, vya nyumba ya Mungu, alivyovitoa Nebukadreza katika hekalu lililokuwako Yerusalemu, na kuviingiza katika hekalu la Babeli, vyombo hivyo mfalme Koreshi alivitoa katika hekalu la Babeli, akakabidhiwa mtu, jina lake Sheshbaza, ambaye alikuwa amemfanya liwali;

15 naye akamwambia, Chukua vyombo hivi, uende, ukavitie katika hekalu lililoko Yerusalemu, na nyumba ya Mungu na ijengwe mahali pake.

16 Ndipo ye yule Sheshbaza alipokuja, akaupiga msingi wa nyumba ya Mungu iliyoko Yerusalemu; na tangu wakati ule hata leo imekuwa ikijengwa, wala bado haijamalizika.

17 Basi, sasa, mfalme akiona vema, watu na watafute katika nyumba ya hazina ya mfalme, iliyoko huko Babeli, kama ni kweli ya kuwa mfalme Koreshi alitoa amri kuijenga nyumba hiyo ya Mungu katika Yerusalemu, na mfalme akatuletee habari ya mapenzi yake katika jambo hili”.

EZRA 6:1 Ndipo mfalme Dario akatoa amri, na watu wakatafuta katika nyumba ya vyuo vya tarehe, hapo akiba zilipowekwa katika Babeli.

2 Na chuo kimoja kilipatikana huko Akmetha, katika nyumba ya mfalme iliyo katika wilaya ya Umedi, na ndani yake maneno haya yameandikwa ili yakumbukwe.

3 Katika mwaka wa kwanza wa mfalme Koreshi, mfalme Koreshi alitoa amri, Kwa habari ya nyumba ya Mungu huko Yerusalemu, nyumba hiyo na ijengwe, mahali watoapo dhabihu, na misingi yake ipigwe na kufanywa imara sana; kuinuka kwake kuwe mikono sitini, na upana wake mikono sitini;

4 ziwepo safu tatu za mawe makubwa, na safu moja ya miti mipya; gharama zake zitolewe katika nyumba ya mfalme.

5 Na vyombo vya dhahabu na fedha, vya nyumba ya Mungu, ambavyo mfalme Nebukadreza alivitoa katika nyumba ya Mungu, iliyoko Yerusalemu, akavileta mpaka Babeli, na virudishwe, vikaingizwe tena katika hekalu lililoko Yerusalemu, kila kimoja mahali pake, na wewe uvitie katika nyumba ya Mungu.

6 Basi sasa ninyi, Tatenai, liwali wa ng’ambo ya Mto, na Shethar-Bozenai, na hao wenzi wenu wa Kiajemi, mlio ng’ambo ya Mto, jitengeni na mahali pale;

7 iacheni kazi hii ya nyumba ya Mungu, msiizuie; waacheni liwali wa Wayahudi, na wazee wa Wayahudi, waijenge nyumba hii ya Mungu mahali pake.

8 Tena, natoa amri kuwaagiza ninyi mtakayowatendea wazee hao wa Wayahudi, kwa kazi hii ya kuijenga nyumba ya Mungu; katika mali ya mfalme, yaani, katika kodi za nchi iliyo ng’ambo ya Mto, watu hao wapewe gharama zote kwa bidii, ili wasizuiliwe.

9 Na kila kitu wanachokihitaji, katika ng’ombe wachanga, na kondoo waume, na wana-kondoo, kwa sadaka za kuteketezwa watakazomtolea Mungu wa mbinguni, na ngano, na chumvi, na divai, na mafuta, kama makuhani walioko Yerusalemu watakavyosema, na wapewe vitu hivyo vyote siku kwa siku, msikose kuwapa;

10 wapate kumtolea Mungu wa mbinguni sadaka zenye harufu nzuri, na kumwombea mfalme, na wanawe, wapate uzima.

11 Pia nimetoa amri kwamba, mtu awaye yote atakayelibadili neno hili, boriti na itolewe katika nyumba yake, akainuliwe na kutungikwa juu yake; tena nyumba yake ikafanywe jaa kwa ajili ya neno hili.

12 Na Mungu huyu, aliyelifanya jina lake likae pale, na aangamize wafalme wote, na watu wote, watakaonyosha mikono yao kulibadili neno hili, na kuiharibu nyumba hii ya Mungu, iliyoko Yerusalemu. Mimi, Dario, nimetoa amri; na ifanyike kwa bidii nyingi.

13 Ndipo Tatenai, liwali wa ng’ambo ya Mto, na Shethar-Bozenai, na wenzi wao, wakafanya hayo kwa bidii, kwa sababu mfalme Dario alikuwa ametuma watu kwao.

14 Nao wazee wa Wayahudi wakajenga, wakafanikiwa, kwa msaada wa kuhubiri kwao Hagai nabii, na Zekaria mwana wa Ido. Wakajenga, wakaimaliza kazi yao, kwa maagizo ya Mungu wa Israeli, na kwa amri ya Koreshi, na Dario, na Artashasta mfalme wa Uajemi.

15 Nyumba hiyo ikamalizika siku ya tatu ya mwezi Adari, katika mwaka wa sita wa kutawala kwake mfalme Dario”

Unaona, Lakini endapo wangekaa na kuendelea kusubiri..huku wanaiogopa amri ya mfalme..wangeendelea kukaa katika hali ile ile na hakuna chochote kingetokea…

Hivyo inatufundisha kuwa…tusiogope Kuifanya kazi ya Mungu maadamu ni yeye ndiye aliyetuagiza…Bwana Yesu alisema…

Mathayo 28:19 “ Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu;

20 na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; na tazama, MIMI NIPO PAMOJA NANYI SIKU ZOTE, HATA UKAMILIFU WA DAHARI”.

Yupo pamoja nasi…haijalishi sheria ya nchi imesema tusihubiri…Hilo haliwezi kutuzuia sisi kuhubiri, haijalishi watu wanasema tusihubiri hiyo haipaswi kutufanya sisi tusihubiri..Haijalishi tayari kuna mswada ulipitishwa wa injili isihubiriwe…Injili itahubiriwa tu..Katika kuhubiri huko Bwana amesema atakuwa pamoja na sisi..Kama alivyokuwa na wayahudi hao hhapo juu.

Tujifunze tena katika habari hii ya mwisho..katika tutapata moyo zaidi katika kwenda kuhubiri habari njema…

Tusome…

Matendo 5:17 “Akaondoka Kuhani Mkuu na wote waliokuwa pamoja naye, (hao ndio walio wa madhehebu ya Masadukayo), wamejaa wivu,

18 wakawakamata mitume wakawaweka ndani ya gereza;

19 lakini malaika wa Bwana akafungua milango ya gereza usiku, akawatoa, akasema,

20 Enendeni mkasimame hekaluni mkawaambie watu maneno yote ya Uzima huu.

21 Nao waliposikia wakaenda alfajiri hekaluni, wakaanza kufundisha. Akaja Kuhani Mkuu nao waliokuwa pamoja naye, wakawakutanisha watu wa baraza, na wazee wote wa wana wa Israeli, wakatuma watu gerezani ili wawalete.

22 Hata watumishi walipofika hawakuwaona gerezani, wakarudi wakatoa habari,

23 wakisema, Gereza tumeikuta imefungwa salama, nao walinzi wamesimama mbele ya mlango; lakini tulipoufungua hatukukuta mtu ndani.

24 Basi jemadari wa hekalu na wakuu wa makuhani waliposikia haya, wakaingiwa na shaka kwa ajili yao, litakuwaje jambo hilo.

25 Mtu mmoja akaja akawapasha habari ya kwamba, Watu wale mliowaweka gerezani wako ndani ya hekalu, wamesimama wakiwafundisha watu.

26 Ndipo yule jemadari akaenda pamoja na watumishi, wakawaleta, lakini si kwa nguvu, kwa maana waliogopa watu wasije wakawapiga kwa mawe.

27 Walipowaleta, wakawaweka katika baraza. Kuhani Mkuu akawauliza,

28 akisema, Je! Hatukuwaamuru ninyi kwa nguvu, msifundishe kwa jina hili? Nanyi, tazameni, mmeijaza Yerusalemu mafundisho yenu, na mnataka kuileta damu ya mtu yule juu yetu.

29 Petro na mitume wakajibu, wakisema, Imetupasa kumtii Mungu kuliko wanadamu.

30 Mungu wa baba zetu alimfufua Yesu, ambaye ninyi mlimwua mkimtundika katika mti.

31 Mtu huyo Mungu amemtukuza kwa mkono wake wa kuume, awe Mkuu na Mwokozi, awape Waisraeli toba na msamaha wa dhambi.

32 Na sisi tu mashahidi wa mambo haya, pamoja na Roho Mtakatifu ambaye Mungu amewapa wote wamtiio”.

Katika habari hiyo unaweza kuuliza… “kwanini malaika wamevunja sheria ya nchi?”…Kwasababu wamewatoa watu gerezani kinyume na utaratibu na bado wanawarudisha wahalifu wakafanye yale yale waliyozuiliwa kuyafanya tena kule kule hekaluni wanapopingwa.

Hebu jiulize umekamatwa na jeshi la polisi kwa kosa fulani…na usiku malaika anakuja kukutoa mahabusu pasipo ripoti yoyote na kukuambia ukaendelee kufanya kile kile kitu ambacho umezuiliwa kukifanya…Unaona hilo linaingia akilini?..kwasababu biblia inasema pia “tutii mamlaka iliyokuu”..Sasa kwanini hapa mamlaka hiyo inavunjwa?.

Jibu ni kwasababu ipo mamlaka nyingine iliyo kuu Zaidi ya hiyo ambayo ilishasema “Tukahubiri Injili kwa kila kiumbe, na yeye atakuwa na sisi hata ukamilifu wa Dahari”. Hakuna mamlaka nyingine duniani, wala kuzimu ambayo inaweza kuzidi hiyo Amri. Hakuna kikundi chochote, wala chama cha siasa, wala dini,wala wenye mamlaka, wala serikali yoyote ambayo ipo juu ya hiyo AMRI.. Na wala hakuna chochote kinachoweza kuizuia isitekelezeke.. Injili itahubiriwa tu mamlaka ya nchi ipende au isipende..Amri iwe imetolewa au haijatolewa…iwe imehalalishwa au haijahalalishwa…Yesu Kristo yupo upande wa wanaoihubiri injili haijalishi ni vikwazo vingapi vinaonekana mbele..haijalishi kuna hatari kiasi gani endapo itahubiriwa…lakini Injili(yaani Neno la Mungu)…Litahubiriwa tu..Bwana Yesu Kristo atahakikisha inafika kwa kila kiumbe…na hiyo ni AMRI sio OMBI. Kwasababu mamlaka yote ya mbinguni na duniani kapewa yeye..na hakuna aliye juu yake.

Hivyo simama hubiri injili leo..usiangalie mazingira yanayokuzunguka..usiangalie hatari zinazokuzunguka..yeye amesema “atakuwa pamoja nasi hata ukamilifu wa dahari”…

Warumi 8:31 “Basi, tuseme nini juu ya hayo? Mungu akiwapo upande wetu, ni nani aliye juu yetu?”.

Ubarikiwe sana.

Kama hujaokoka..simama leo uokoke…Tubu kwa dhati na kusudia kuacha yote uliyokuwa unayafanya yaliyo kinyume na Neno la Mungu. Na Bwana atakupa kipawa cha Roho wake mtakatifu.

Maran atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii 0789001312

Mada Nyinginezo:

KUTOKUIHUBIRI INJILI,KUNA MADHARA GANI?

 

 

TAZAMA, MWISRAELI KWELI KWELI, HAMNA HILA NDANI YAKE!

MUUNGANIKO WA MADHEHEBU NI MPANGO WA MPINGA-KRISTO.

AINA YA MAADUI UTAKAOKUTANA NAO KATIKA SAFARI YAKO YA WOKOVU.

HERI YULE ATAKAYEKULA MKATE KATIKA UFALME WA MUNGU.

 

MADHARA YA KUPUUZIA MAAGIZO YA MSINGI MUNGU ANAYOKUPA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

AINA YA MAADUI UTAKAOKUTANA NAO KATIKA SAFARI YAKO YA WOKOVU.

Pale unapookoka au unapoamua kumtumikia Mungu ni vizuri kufahamu, aina za maadui ambao utakutana nao kuiharibu imani yako kwa namna moja au nyingine. Hiyo itakusaidia ili siku utakapokutana nao usiyumbishwe kiasi cha kukata tamaa ya kuendelea mbele.

#1 Adui wa kwanza ni Shetani na mapepo yake:

Luka 22:31 “Akasema, Simoni, Simoni, tazama, Shetani amewataka ninyi apate kuwapepeta kama vile ngano;

32 lakini nimekuombea wewe ili imani yako isitindike; nawe utakapoongoka waimarishe ndugu zako”.

Shetani akishaona umeokoka kweli kweli, hawezi kutulia tu kukuangalia unafanikiwa rohoni kiwepesi wepesi tu ni lazima atanyanyuka ili kukuandalia baadhi ya visa, hapo ndipo wengine atawaletea misiba, wengine atawasababishia kufukuzwa kazi, wengine magonjwa Fulani ya ajabu ajabu tu, wengine atawaletea majanga n.k. hiyo yote ni kwa lengo tu la kumfanya utetereke na ukate tamaa uiche imani yako, umkufuru Mungu..Kama alivyojaribu kufanya kwa Ayubu, kumletea majanga yote yale.

#2 Watu ya nyumbani kwako mwenyewe:

Mathayo 10:36 “na adui za mtu ni wale wa nyumbani mwake.

37 Apendaye baba au mama kuliko mimi, hanistahili; wala apendaye mwana au binti kuliko mimi, hanistahili.

38 Wala mtu asiyechukua msalaba wake akanifuata, hanistahili”.

Hapa ndipo shetani anapopenda kupatumia hasaa kwa mtu ambaye ndio kwanza mchanga kiroho, aliyekusudia kujitwika misalaba wake na kumfuata Yesu. Dada/Kaka unapoamua kumfuata Yesu kwa kujikana..jiweke tayari kupishana na baba yako au mama yako, au ndugu zako, au watoto wako, au jamii yako na marafiki zako, jiandae kuonekana umerukwa na akili, au umelogwa. Na Wakati mwingine kutengwa, kudharauliwa, na wengine wanafikia hatua hata ya kufukuzwa nyumbani, au kuzuiwa kula chakula au kunyimwa ada ya shule n.k. Ikiwa Yesu ni Bwana wetu ambaye hakuwa na dhambi hata moja hakuaminiwa na ndugu zake, (soma Yohana 7:5), Zaidi walipomwona anaanza kuhubiri walitaka kwenda kumkamata na kusema amerukwa na akili (Soma Marko 3:21). Si zaidi mimi na wewe ambao tunakasoro nyingi?.

Hata wewe ukimfuata yeye, utakutana na hayo hayo. Huwezi ukaelewana na ndugu zako wote moja kwa moja kwa uamuzi uliouchukua. Ipo sehemu utapishana nao tu. Lakini hilo lisikuvunje moyo. Songa mbele katika Imani…Ni shetani anawatumia tu lakini hao ni ndugu zako …Na hatawatumia hivyo milele kwa hivyo wapende tu.

#3 Ndugu yako wa karibu sana katika Imani:

Tofauti na ndugu wa mwilini. Adui mwingine ambaye unapaswa uweke akili kuwa unaweza kukutana naye mahali Fulani katika safari yako ya wokovu au huduma, ni ndugu mwenzako wa karibu sana katika imani.

Huyu ni Mtu ambaye huwezi kumtegemea, ni miongoni mwa wale ambao pengine unasali nao kila siku, unashirikishana nao kila siku habari njema za wokovu, unaokwenda kushuhudia nao, mnafanya kazi ya Mungu pamoja. Ghfla tu akakugeuka bila sababu yoyote yenye mashiko…anaweza kuingiliwa na kitu tu Fulani kidogo sana pengine tamaa Fulani, Na hiyo ikamfanya awe tayari kukusaliti au kuwa adui yako bila kujali mmekuwa katika safari pamoja kwa muda gani , bila kujali kwa kukusaliti huko kunakuachia madhara makubwa nyuma kiasi gani…

Hichi Ni chanzo ambacho huwezi kukitegemea, Hivyo jiweke tayari kiakili ili kusudi kwamba ikikutokea usivunje moyo kiasi cha kushindwa kuendelea mbele..

Mfano wa mtu wa namna hii ni Yuda. Alikuwa tayari kumuuza Bwana wake kwa tamaa ndogo tu ya fedha.

Zaburi 41: 9 “Msiri wangu tena niliyemtumaini, Aliyekula chakula changu, Ameniinulia kisigino chake”.

#4 Manabii wa uongo:

Mathayo 7:15 “Jihadharini na manabii wa uongo, watu wanaowajia wamevaa mavazi ya kondoo, walakini kwa ndani ni mbwa-mwitu wakali.

16 Mtawatambua kwa matunda yao. Je! Watu huchuma zabibu katika miiba, au tini katika mibaruti”?

Hawa licha tu ya kuwa na lengo la kukupotosha kwa mafundisho yao ya uongo., lakini pia kama wewe ni mtu wa Mungu uliyesimama wapo tayari hata kutoa ushuhuda wa uongo kinyume na wewe kwa lengo la aidha kujisafisha wao au kukuangusha wewe kwa makusudi ili wapate faida Fulani kutoka kwako.(3Yohana 1:10).

Hawa nao jiandae kukutana nao katika utumishi wako, au ukristo wako.

#5 Watumishi wenzako:

Hawa sio lazima wawe wa uongo, wanaweza wakawa wa ukweli, lakini kama hawajasimama vizuri, na kukosa ufahamu wa kuyapambanua maandiko vizuri, wanaweza kwa sehemu Fulani shetani akawatumia kuwafanya kuwa maadui wa Imani yako kwa muda.. Lakini bado wataendelea kubakia kuwa watumishi wa Mungu.

Mfano wa hawa ni Elfazi, Sofari, na Bildadi, Marafiki wa Ayubu. Ni wazee waliokuwa na hekima, washauri wa karibu sana wa Ayubu. Lakini walipoona Ayubu amekumbwa na matatizo kama yale, wao pasipo kukaa chini na kumwuliza Mungu ni nini maana yake..Wao wakakimbilia moja kwa moja kumlaumu Ayubu kuwa ametenda dhambi ndio maana yale yote yakampata..Na wakatumia vipengele kabisa vya maandiko ili kuthibitisha wanachokisema.. Na hiyo ndiyo iliyomfanya Ayubu akafadhaike zaidi hata ya kufiwa na watoto wake.

Kwasababu wale aliowategemea kuwa watakuwa na hekima ya kupambanua kilicho sahihi na kisicho sahihi, ndio wamekuwa wa kwanza kuwa mwiba kwake.

Vivyo hivyo, wapo watumishi ambao ni kweli wameitwa na Mungu, lakini watakapokuona unapitia katika hali Fulani kwenye imani tofauti na matazamio yao pengine ulitegemea na wao wawe wa kwanza kukuelewa..Ndio wanakuwa wa kwanza kukupinga tena wanatumia maandiko ..pengine ili tu kumridhisha mtu Fulani.

Hivyo hawa nao utakutana nao sehemu Fulani katika safari yako ya wokovu. Usiwachukie bali waombee kama Ayubua alivyowaombea marafiki zake, na baada ya muda mambo yote yatakuwa sawa.

#6 Viongozi wa dini za Uongo:

Nikisema viongozi wa dini za uongo simaanishi tu wale wa dini za mbali hapana, namaanisha wale ambao wanaonekana wapo katika Imani yako. Hawa ndio maadui wa ngazi ya juu sana, akitoka shetani na mapepo yake, hawa ndio wanaofuata .. wanaitumia serikali na wakati mwingine hata dola kupingana na kushindana na watu wa Mungu wa kweli.

Na hii itakupata ikiwa unaihubiri kweli kinyume na mafundisho yao. Wapo tayari kukupeleka mabarazani kukuhoji, na kukupiga na wakati mwingine hata kukuua..Vifo vingi vya mashahidi wa Yesu na mitume vilisababishwa na hawa.

Hawa ndio mfano wa Mafarisayo na Masadukayo. Walimpinga Bwana Yesu wakati wote, na kumpeleka kwa Herode na Pilato ili auawe.

Hata sasa, wapo wameshikamana na dola sana, na katikati ya hawa ndipo Yule mpinga-Kristo atakapotokea. Ibada za sanamu na mafundisho ya kipagani yasiyoambatana na maandiko ndiyo wanayoyahubiri.

Mathayo 10:17 “Jihadharini na wanadamu; kwa maana watawapeleka mabarazani, na katika masinagogi yao watawapiga;

18 nanyi mtachukuliwa mbele ya maliwali na wafalme kwa ajili yangu, kuwa ushuhuda kwao na kwa mataifa”.

Bwana anasema tazama nimekwisha kuwaonya mbele..(Mathayo 24:25).

Lakini pamoja na majaribu yote hayo, Mungu aliahidi kuwa hatamwacha mtu yeyote atakayemwendea,.Anamwachilia nguvu ya ziada ya kuweza kukabiliana na hivyo vizuizi,..Hapo ndipo mtu aliyeokoka anapojua kweli Mungu yupo pamoja na yeye. Lakini pia kwa kupitia hayo yote mwisho wake hauwi bure..

Ukiyastahimili hayo yote basi ufahamu kuwa thawabu yako ni kubwa sana mbinguni. Na Mungu atakufanya chombo chake kiteule kwa kazi yake.

Hivyo zidi kusonga mbele katika Imani ikiwa wewe upo tayari safarini katika wokovu. Ukifahamu kuwa taji lako limeshawekwa tayari mbinguni…

Luka 6:22 “Heri ninyi watu watakapowachukia, na kuwatenga, na kuwashutumu, na kulitupa nje jina lenu kama neno ovu, kwa ajili ya Mwana wa Adamu.

23 Furahiwani siku ile na kuruka-ruka, kwa kuwa, tazama, thawabu yenu ni kubwa mbinguni, maana, baba zao waliwatenda manabii vivyo hivyo”.

Hivyo furahi, kwasababu mbinguni unaheshimika. Kadhalika kumbuka pia kuwaombea wote wanaokuudhi, wote wanaotumika na shetani pasipo wao kujijua..waombee heri wala usiwaombee shari kama Bwana wetu Yesu Kristo alivyotufundisha..(katika Mathayo 5:43-46 na warumi 14:12).

Bwana akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii 0789001312

Mada Nyinginezo:

ZIFAHAMU HUDUMA KUU (10) ZA SHETANI DUNIANI.

ZIFAHAMU HOJA SABA ZENYE NGUVU MBELE ZA MUNGU.

NILIMWONA SHETANI, AKIANGUKA KUTOKA MBINGUNI.

NENO LA MUNGU NI DAWA ILIYO TOFAUTI NA DAWA NYINGINE.

NENO LA MUNGU NI DAWA ILIYO TOFAUTI NA DAWA NYINGINE.

JE! WATOTO WACHANGA WANAWEZA KUHUKUMIWA NA KUTUPWA MOTONI.

JE WAJUA?

NI NINI KINAKUPATA UNAPOIPUUZIA INJILI?

URIMU NA THUMIMU NI NINI KATIKA BIBLIA?

BONDE LA KUKATA MANENO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

WAKAMWACHA BWANA, NA KUITUMIKIA MIUNGU YAO WENYEWE.

Shalom. Karibu tujifunze Biblia…

Wana wa Israeli walipomwacha Mungu kwa muda mrefu na kuitumikia miungu mingine migeni.. Mungu aliwatoa katika nchi yao na kuwapeleka katika mataifa ya mbali..Israeli akaipeleka Babeli na baadaye Yuda nayo akaipeleka Ashuru nchi ikabakia tupu…Lakini mfalme wa Ashuru kuona nchi imebaki haina watu, akaamua kukusanya baadhi ya watu kutoka katika baadhi ya nchi za jirani na za mbali na kuwapa nchi hiyo ya Israeli waishi ndani yake..ili pasibaki patupu…Lakini hao watu wakaishi mule bila kujua kuwa ile ni nchi takatifu, na haipaswi kutiwa unajisi..Mungu akawaletea Wanyama wakali kama simba..mpaka walipojifunza kuishi kulingana na kawaida ya hiyo nchi…

Tusome..

2Wafalme 17:23 “hata Bwana akawaondoa Waisraeli wasiwe mbele zake, kama vile alivyosema kwa kinywa cha watumishi wake wote, manabii. Basi Waisraeli walichukuliwa mateka kutoka nchi yao wenyewe, waende nchi ya Ashuru, hata leo.

24 Naye mfalme wa Ashuru akaleta watu kutoka Babeli, na Kutha, na Ava, na Hamathi, na Sefarvaimu, akawaweka katika miji ya Samaria badala ya wana wa Israeli; wakaumiliki Samaria, wakakaa katika miji yake.

25 Basi ikawa, wakati ule walipoanza kukaa huko, hawakumcha Bwana; kwa hiyo Bwana akapeleka simba kati yao, nao wakawaua baadhi yao.

26 Kwa hiyo wakamwambia mfalme wa Ashuru, wakasema, Wale wa mataifa uliowahamisha, na kuwaweka katika miji ya Samaria, hawaijui kawaida ya Mungu wa nchi; kwa hiyo amepeleka simba kati yao, na tazama, wanawaua, kwa sababu hawaijui kawaida ya Mungu wa nchi.

27 Ndipo mfalme wa Ashuru akatoa amri, akasema, Mpelekeni mmojawapo wa makuhani, mliowachukua kutoka huko; aende akakae huko, akawafundishe kawaida ya Mungu wa nchi.

28 Basi mmoja wa makuhani waliochukuliwa kutoka Samaria akaenda akakaa katika Betheli, akawafundisha jinsi ilivyowapasa kumcha Bwana.

29 Lakini pamoja na hayo watu wa kila taifa wakajifanyia miungu yao wenyewe, wakaiweka katika nyumba za mahali pa juu, walipopafanya Wasamaria, kila taifa katika miji yao walimokaa.

30 Watu wa Babeli wakafanya Sukoth-benothi kuwa mungu wao, watu wa Kutha wakafanya Nergali, watu wa Hamathi wakafanya Ashima,

31 Waavi wakafanya Nibhazi na Tartaki; nao Wasefarvi wakawaunguza wana wao katika moto kwa Adrameleki na Anameleki, miungu ya Sefarvaimu.

32 Basi hivyo wakamcha Bwana, nao wakijifanyia wengine wao kuwa makuhani wa mahali pa juu, ambao waliwafanyia dhabihu katika nyumba za mahali pa juu.

33 WAKAMCHA BWANA, NA KUITUMIKIA MIUNGU YAO WENYEWE, sawasawa na kawaida za mataifa ambao wao walihamishwa kutoka kwao”.

Nataka tuone huo mstari wa 33 wa mwisho unaosema “WAKAMCHA BWANA, NA KUITUMIKIA MIUNGU YAO WENYEWE”…Sentensi hiyo maana yake walifanya vitu viwili kwa wakati mmoja…yaani walimcha Mungu na hapo hapo waliitumikia miungu yao.

Kwanini walimcha Bwana?..Ni ili tu wasiendelee kuuawa na simba…na kwanini waliendelea pia kuitumikia miungu yao waliyotoka nayo huko?…Ni kwasababu wanaipenda na hawawezi kuacha asili yao.

Kwahiyo ili kuendelea kuishi vizuri katika hiyo nchi, wasiendelee kuliwa na simba.. wakaona njia pekee ni kuchanganya mambo…Nusu Mungu,nusu sanamu…Nusu kutoa zaka nusu kufanya anasa, na kwenda kwa waganga…Nusu kufanya mema nusu kutenda mambo maovu…Nusu kutumikia Mungu wa kweli wa Israeli nusu kuitumikia miungu ya makabila yao waliyotoka nayo huko kwenye mataifa. Jambo hilo likawasababishia wakae chini ya laana muda mrefu badala ya baraka.

Huoni ni jambo linaloendelea hata leo..UVUGUVUGU. Nusu moto nusu baridi… Utakuta mtu ni mkristo anamtumikia Mungu wa kweli kanisani anakwenda na kuhudumu vizuri tu, analipa na zaka lakini akirudi kijijini kwao anaitumikia miungu ya mababu zake?.. atatoa kafara kidogo..atatambika kidogo, atatoa n.k…Mungu kwake ni kama kinga tu!..anamcha Mungu ili tu wachawi wasimpate, ili tu mambo yake yaende vizuri ili tu apate mke au mume wa kikristo, ili tu aeleweke kwenye jamii yake n.k lakini ndani kabisa wa moyo wake anaipenda na kuithamini miungu ya kwao. Tena ataisifia sana na kuiheshimu na kuiogopa kuliko hata Mungu wa kweli. Hatakosa matambiko yote ya kila msimu yanayofanyika kule. Ataendelea kuishikilia Imani yake na dhehebu lake ili tu asionekane kama ni mpagani wala mwabudu miungu… lakini ndani ya moyo wake anaiheshimu Zaidi miungu ya kwao…ndani ya moyo wake anazithamini Zaidi zile chale alizochanjwa na wale wazee waliomtambikia kuliko Mungu wa mbingu na nchi anayemfuata kila siku kanisani…Ataogopa Zaidi vitisho vya wazee wa mila lakini amri za Mungu hazitamwogopesha hata kidogo.n.k

Hivyo ndugu mpendwa…Bwana wetu Yesu Kristo alituonya sana kuhusu kuwa vuguvugu alisema…

Ufunuo 3:15 “Nayajua matendo yako, ya kuwa hu baridi wala hu moto; ingekuwa heri kama ungekuwa baridi au moto.

16 Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa changu.

17 Kwa kuwa wasema, Mimi ni tajiri, nimejitajirisha, wala sina haja ya kitu; nawe hujui ya kuwa wewe u mnyonge, na mwenye mashaka, na maskini, na kipofu, na uchi”

Na tena inasema katika ..

2Wakorintho 6:14 “Msifungiwe nira pamoja na wasioamini, kwa jinsi isivyo sawasawa; kwa maana pana urafiki gani kati ya haki na uasi? Tena pana shirika gani kati ya nuru na giza?

15 Tena pana ulinganifu gani kati ya Kristo na Beliari? Au yeye aaminiye ana sehemu gani pamoja na yeye asiyeamini?

16 Tena pana mapatano gani kati ya hekalu la Mungu na sanamu? Kwa maana sisi tu hekalu la Mungu aliye hai; kama Mungu alivyosema, ya kwamba, Nitakaa ndani yao, na kati yao nitatembea, nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.

17 Kwa hiyo, Tokeni kati yao, Mkatengwe nao, asema Bwana, Msiguse kitu kilicho kichafu, Nami nitawakaribisha.

18 Nitakuwa Baba kwenu, Nanyi mtakuwa kwangu wanangu wa kiume na wa kike”.

Mkristo Kufanya matambiko ya kimila ni dhambi, Mkristo kufanya matambiko ya marehemu ni dhambi, kuchanja chale ni machukizo mbele za Mungu…mtu wa Mungu hupaswi kufanya hivyo..kwenda kijijini kwenu kutafuta suluhisho la matatizo kwa mizimu ni machukizo makubwa mbele za Mungu…kwenda kusafisha nyota kwenu kwa mila za ulikotokea ni machukizo makubwa mbele za Mungu…Mkristo kwenda kufanya kafara yoyote na kujihusisha na kafara za kimila ni machukizo mbele za Bwana.

Sasa swali ni je! Tusiishi na ndugu wa ukoo wanaofanya hayo?..Jibu ni la! Tutaishi nao..lakini si kuchangamana nao kiimani..Unapookoka jambo la kwanza unalotakiwa kufanya ni kuhakikisha Imani yako na msimamo wako unatambulika na watu wote..hususani na familia yako na ukoo wako…Wote wanapaswa wajue kuwa wewe umegeuka na kuwa Mkristo, na siku ya kwanza wakikuambia ufanye hayo na kuwaeleza msimamo wako utawaudhi na dhiki lazima ije kidogo!..hivyo hilo weka akilini? Utapitia dhiki kwa kipindi Fulani na hata ikiwezekana kutengwa…lakini utafika wakati watakubaliana tu na wewe ulivyo!..Na mtaendelea kuishi kwa namna hiyo…

Usiogope laana watakazokulaani wala usiogope kwamba watakuloga…hakuna Uchawi juu ya Yakobo wala uganga juu ya Israeli likumbuke hilo siku zote (Hesabu 23:23). Wala huhitaji kuingia kwenye maombi ya vita kushindana wasikuloge..kitendo tu cha wewe kukana vile tayari kuna nguvu ya Mungu inakulinda kwa namna isiyokuwa ya kawaida..kwahiyo hakuna lolote litakalokupata.

Kadhalika kama nyumba yako umezindikwa kayaondoe hayo mazindiko yote sasahivi…kadhalika na vitu vingine vyote visivyo vya kikristo, usivichangaye na Ukristo wako….Unafahamu kabisa kwenye biblia hakuna sehemu yoyote Mungu alihusianishwa na sanamu, la mtakatifu yeyote, hakuna mahali popote sanamu la bikira Maria linaabudiwa, lakini wewe kwa kulijua hilo unasema nimeokoka, na bado unakwenda kuisujudia sanamu hiyo ili tu kuwaridhisha wazazi wako, nataka nikuambie hayo ni machukizo makubwa sana mbele za Mungu “Usimche Mungu na kuitumikia miungu yako”..Usijaribu kufanya hayo mambo mawili kwa wakati mmoja. Ni machukizo makubwa na yenye madhara mara mbili, kwasababu biblia ndio inayataja hayo kama uasherati wa kiroho.

Bwana akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii 0789001312

Mada Nyinginezo:

AGENDA KUBWA YA SHETANI KWA KANISA HILI LA LAODIKIA.

HISIA YA MUNGU ILIYO MBAYA KULIKO ZOTE.

Bwana aliposema kuwa yeye ni “Mungu wa miungu” alikuwa na maana gani?..je! yeye ni Mungu wa sanamu?

 

NI NINI KINAKUPATA UNAPOIPUUZIA INJILI?

MAANA YA RANGI KIBIBLIA.

MIILI YA UTUKUFU ITAKUWAJE?

TAZAMA, MWISRAELI KWELI KWELI, HAMNA HILA NDANI YAKE!

JE! MUNGU NI NANI?

Rudi Nyumbani:

Print this post

WALE WAZEE ISHIRINI NA WANNE (24), WANA KAZI GANI?

Wale wazee ishirini na wanne na akina nani na kazi yao ni ipi?


Kama wengi wetu tunavyofahamu Malaika watakatifu wamesifika kwa kazi moja kuu nayo ni kumsifu Mungu na kumwimbia, lakini mbali na sifa hiyo wamepewa pia kazi nyingine maalumu ya kufanya nayo ni ile ya kuwahudumia watakatifu..

Waebrania 1:14 “Je! Hao wote si roho watumikao, wakitumwa kuwahudumu wale watakaourithi wokovu?’’

Sasa hapa kwenye kuwahudumia watakatifu wengi tunadhani ni kuwalinda watakatifu dhidi ya adui tu basi..Lakini nataka nikuambie sio tu kuwalinda peke yake, vipo na vipengele vingine sana ambavyo Mungu akitufunulia tutashangaa sana, tutasema hata na hiki?.

Tukisoma Ufunuo sura ile ya 4 na ya 5 tutaona Yohana, akipewa neema ya kipekee ya kufunguliwa malango ya Mbinguni na kuonyeshwa kwa wazi mambo yaliyomo kule, na mfumo wake mzima jinsi ulivyo na ngazi zake zote zilivyo jipanga kabla ya kumfikia Mungu mwenyewe. Jambo ambalo hata Ezekiel hakuonyeshwa kwa uwazi kama alivyoonyeshwa Yohana, Kama ukisoma pale utaona picha nzima iliyopo ni kwamba kabla hujakifikia kile kiti cha enzi, utakutana kwanza na jeshi la malaika watakatifu maelfu kwa maelfu wamepazunguka pale kwenye enzi ya Mungu.

Kisha utaona tena katikati ya wale malaika, wapo wazee ishirini na wanne (24), wamekizunguka tena kile kiti cha enzi, na katikati ya wale wazee ishirini na wanne (24), wapo wale wenye uhai 4 waliojaa macho mbele ya nyuma (Ufunuo 4:6), na katikati ya wale wenye uhai wanne kipo kiti cha enzi cha Mungu mwenyewe.

Ufunuo 5:11 “Nikaona nikasikia sauti ya malaika wengi pande zote za kile kiti cha enzi, na za wale wenye uhai, na za wale wazee, na hesabu yao ilikuwa elfu kumi mara elfu kumi na elfu mara elfu,

12 wakisema kwa sauti kuu, Astahili Mwana-Kondoo aliyechinjwa, kuupokea uweza na utajiri na hekima na nguvu na heshima na utukufu na Baraka”.

Sasa tofauti na wengi tunavyodhani kuwa wale wazee ishirini na nne 24 (ni) wale watoto 12 ya Yakobo, na wale mitume 12 wa Bwana Yesu, ambao jumla yao ni 24. Lakini Mtazamo huo sio sahihi, Yohana akiwa mmoja wa mitume wa Bwana akiwa duniani hawezi kujiona tena mbinguni, ameketi na tena ameshikilia maombi ya watakatifu..Uona hilo haliwezekani.. kitendo cha wale kuitwa wazee haiwafanyi wao kuwa wanadamu..Tutaliona hilo muda mfupi mbeleni kidogo.

Kumbuka Mungu kawaumba malaika na maumbile mengi tofauti tofauti kulingana na kazi zao walizowekewa kuzifanya kwa ajili yetu sisi..Na Hawa wazee ishirini na nne (24) ni aina nyingine ya malaika watakatifu. Ambao wamechukua mfano wa wazee kwa maumbile yao, kama tu wale wenye uhai wanne, walivyokuwa na mfano wa viumbe vinne tofauti, ambapo wa kwanza alikuwa mfano wa simba, hiyo inamaanisha kuwa zipo tabia za simba waliziwakilisha, mwingine mfano wa ndama, wakiwakilisha tabia ya ndama achinjwaye, mwingine mfano wa sura ya mwanadamu, na mwingine mfano wa tai arukaye..wote hao waliwakilisha tabia Fulani zinazofanana na hao wanyama katika kuwahudumia watu..

Ukisoma juu ya ufunuo wa ile mihuri saba ndipo utafahamu vizuri ni jinsi gani maumbile yao yalifunua kazi za katika kanisa kwa kipindi husika..Na kama ulikuwa hujafahamu bado wakati huu tuliopo wa kanisa tupo chini ya mafuta ya mwenye uhai wa nne ambaye anafananishwa na tai arukaye..Tai ni mnyama anayeona mbali, na manabii wa Bwana wanafananishwa na Tai,..Katika wakati huu tunaoishi sasa, kama hutapewa jicho la TAI la kuona mbali, utachukuliwa na maji na udanganyifu wa shetani unaoendelea sasa hivi kwa kasi..

Kama hujapata kujua ufunuo wa kitabu kile cha mihuri saba, basi utanitumia ujumbe inbox nikutumie somo lake.

Sasa tukirudi kwa wale wazee ishirini na wanne (24), hawa wanaoonekana kama wazee, Ni kundi lingine la malaika wa Mungu wenye mfano wa tabia za wazee, siku zote wazee wanasifika kwa kuwa na hekima, na ndio wanaopewa kipaumbele katika mashauri, na viti vya mbele hata leo hii washauri wa Raisi asilimia kubwa ni wazee, hiyo yote ni kwasababu ya uzoefu wao katika mambo mengi na hekima..

Vivyo hivyo na kundi hili la malaika hawa, ni malaika Mungu aliowachagua, kuizunguka enzi yake, na kwa kupitia hao Mungu alichagua maombi ya watakatifu yapitie kwanza kwao, kisha kwa mwana-kondoo na moja kwa moja kwake. Si kila jukumu wamepewa malaika wote, wapo malaika wanaohusika na kupigana na sisi vitani kama Mikaeli na malaika zake, wapo wajumbe kama Gabrieli, wapo wanasimama kwa kila huduma, kama ilivyokuwa kwa Petro, na Paulo, biblia inasema walikuwa na malaika zao.

Vilevile na wazee ishirini na wanne (24), ni malaika waliokaribu sana na Mungu, kupeleka mashauri yao na hoja zao zenye hekima.

Ufunuo 5:8 “Hata alipokitwaa kile kitabu, hao wenye uhai wanne na wale wazee ishirini na wanne wakaanguka mbele za Mwana-Kondoo, kila mmoja wao ana kinubi, na vitasa vya dhahabu vilivyojaa manukato, ambayo ni maombi ya watakatifu.

9 Nao waimba wimbo mpya wakisema, Wastahili wewe kukitwaa hicho kitabu na kuzifungua muhuri zake; kwa kuwa ulichinjwa, ukamnunulia Mungu kwa damu yako watu wa kila kabila na lugha na jamaa na taifa”,

Moja ya jambo ambalo Mungu analiheshimu ni pale anapoona malaika zake watakatifu wanashiriki katika kuyawasilisha maombi yetu kwa Mungu..Na ndio maana Bwana Yesu alisema..

Mathayo 18:10 “Angalieni msidharau mmojawapo wa wadogo hawa; kwa maana nawaambia ya kwamba malaika wao mbinguni siku zote huutazama uso wa Baba yangu aliye mbinguni”

Hivyo ndivyo malaika wanavyofanya kazi usiku na mchana kuwahudumia wale watakaoukiri wokovu. Leo hii ukimkosesha, au ukimdharua mtakatifu ambaye ni mchanga kiroho ukamzuia asiendelee katika njia yake ya utakatifu..Jiangalie sana, Mungu anawasikiliza malaika zake kushinda hata wewe unavyoweza kufikiri.. wakipeleka mashtaka mabaya kwako mbele zake, sijui ni nini kitakupata, Na ndio maana wanajizuia wakati mwingine kufanya hivyo..soma

2Petro 2:11 “Wenye ushupavu, wenye kujikinai, hawatetemeki wakiyatukana matukufu; ijapokuwa malaika ambao ni wakuu zaidi kwa uwezo na nguvu, hawaleti mashitaka mabaya juu yao mbele za Bwana.

12 Lakini hao kama wanyama wasio na akili, ambao walizaliwa kama wanyama tu wa kukamatwa na kupotezwa, wakikufuru katika mambo wasiyoyajua, wataangamizwa katika maangamizo yao;

Hivyo kama wewe ni mtakatifu basi furahi kwasababu mbinguni unatazamwa sana. Lakini ikiwa wewe upo nje ya Kristo, unatazamia vipi maombi yako yatamfikia Mungu ukiwa katika hali hiyo, ni nani yupo upande wako kukusaidia?, Unategemea vipi Mungu akutumie malaika zake wakulinde?, Unategemea vipi Mungu akusikie wewe. Huoni kuwa maisha yako yapo hatarini. Leo hii shetani akisema ninaitaka roho ya huyu mtu, ni nani atakutetea, Kristo hayupo upande wako, vilevile na malaika zake hawapo upande wako.

Usisubiri Mungu awatumie malaika hawa kukuletea mapigo, Kwasababu upo wakati utafika huduma yao itakuwa imeisha kwa watakatifu. Watapewa kazi nyingine mpya ya kuleta mapigo juu ya hii dunia kama tunavyosoma katika Ufunuo 16, usitamani uwepo huo wakati, kwasababu watu watatamani kifo na kifo kitawakimbia jaribu kufikiri dunia nzima maji yanakuwa damu, jua linashushwa kuwaunguza watu, majipu mabaya ambayo hayajawahi kutokea yanawakuta watu, visiwa vinahama, mwezi unakuwa mwekundu kama damu..Jiulize siku hiyo utakuwa katika hofu kiasi gani…Ukijua kuwa baada ya kufa kwako utakwenda kuzimu moja kwa moja.

Leo dunia ipo katika amani hii ni kwasababu ya neema zake tu utubu. Kwasababu hapendi mtu yeyote apotee..Huu si wakati wa kuitazama dunia tena, bali Mungu hatuna muda mrefu hapa,..parapanda saa yoyote inalia….Ikiwa upo nje ya Kristo na leo hii unasema sitaki tena kuendelea kuishi maisha haya ya kuwa hatarini, basi uamuzi unaoufanya ni sahihi..

Kama upo tayari kufanya hivyo sasa kwa kumaanisha kabisa na wala si kwa kujaribu… Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha sasa ukiwa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI, NAYE NDIYE MFALME ATAKAYEKUJA. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.

AMEN.

Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithibitisha toba yako kwa Vitendo. Ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo kuanzia sasa hivi, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.

Fanya kwanza hayo na YESU KRISTO ataanza kutembea na wewe katika maisha yako kwa namna ya ajabu sana, Nawe pia utaingizwa katika jumuiya hii ya watoto wa Mungu, ambayo Mungu na dunia zinafanya kazi na wewe.

Ubarikiwe.

Tafadhali “Share” Ujumbe huu na kwa wengine. Vilevile kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email au whatsapp, tutumie ujumbe au piga namba hii 0789001312 Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Mada Nyinginezo:

UFUNUO: Mlango wa 4

UFUNUO: Mlango wa 5

UFUNUO:Mlango wa 6-( Maelezo ya Muhuri saba)

Nifanye nini ili niwe na uhakika nikifa naenda mbinguni?

JIHADHARI NA KUOSHWA MIGUU ISIVYOPASWA.

Kwanini kila nikitaka kusali naingiwa na uvivu?

JE! WATOTO WACHANGA WANAWEZA KUHUKUMIWA NA KUTUPWA MOTONI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

HAKIKISHA UNALIELEWA NENO.

 Jina la Mwokozi wetu Yesu Kristo libarikiwe..Karibu tujifunze Biblia..Taa iongozayo miguu yetu na mwanga wa njia yetu…Tabia mojawapo ya Mwovu ni kuiba angali vikiwa vidogo..Kuna uhusiano mkubwa sana wa KUSIKIA NENO LA MUNGU NA KULIELEWA.Hivyo HAKIKISHA UNALIELEWA NENO.

Biblia inasema.

Mathayo 13:18  “Basi ninyi sikilizeni mfano wa mpanzi.

19  Kila mtu alisikiapo neno la ufalme asielewe nalo, huja yule mwovu, akalinyakua lililopandwa moyoni mwake. Huyo ndiye aliyepandwa karibu na njia”.

Tabia mojawapo ya Mwovu ni kuiba angali vikiwa vidogo..Biblia imemfananisha mwovu na ndege..Ndege akipita juu na kuona mbegu zimekaa hadharani huzipitia na kuzila haraka san ana kuondoka…Kadhalika mwovu naye ni hivyo hivyo…anazunguka duniani kote kuiba mbegu za uzima zinazopandwa ndani ya mioyo ya watu kila siku. Anaziiba hizo kwasababu anajua zitakapomea na kuwa miti mkubwa zitamletea madhara makubwa sana katika ufalme wake.

Na mtu ambaye hajalielewa vizuri Neno ndiyo shabaha kubwa ya shetani.

Mwovu hawezi kulinyakua Neno ambalo mtu kalielewa…Huwa analinyakua lile ambalo Mtu hajalielewa…(yaani mtu kasikia tu lakini halijamwingia mpaka kwenye vilindi vya moyo wake).

Soma tena mstari huu..

Mathayo 13:23  “Naye aliyepandwa penye udongo mzuri, huyo ndiye alisikiaye lile neno, na kuelewa nalo; yeye ndiye azaaye matunda, huyu mia, na huyu sitini, na huyu thelathini”.

Umeona?..Kuna uhusiano mkubwa sana wa KUSIKIA NENO LA MUNGU NA KULIELEWA. Sio kusikia tu bali pia na kulielewa kunajalisha sana.

Kikawaida hata wewe ukisikia kitu na usipokielewa ni rahisi kukipuuzia na kile kitu hata kama kikiwa ni kizuri na chenye maana kiasi gani kama hujakielewa ni rahisi kukipita tu…Na Neno la Mungu ndio hivyo hivyo hatupaswi kulisoma tu ili tuwe tunajua mistari mingi au ili tuonekana mashupavu, au tutimize wajibu fulani tu..bali tunapaswa tulisome na kulisikiliza kwa masikio ya ndani kabisa ambayo yatatufanya tulielewe. Shetani kamwe hawezi kumwibia mtu kitu ambacho kakielewa.

Shetani kamwe hawezi kumtisha mtu, wala kumwangusha mtu ambaye kalielewa Neno. Zaidi anamwogopa sana mtu ambaye kausoma mstari mmoja na kauelewa kwa undani kuliko  watu mia ambao wamesoma biblia yote na kuikariri mistari yote kiufasaha na huku hawajaielewa hata kidogo…Hao hawaogopi watu ambao wamesikia maelfu kwa maelfu ya mahubirini yanayohubiriwa kila siku makanisani, mitaani, na mitandaoni lakini hawayatendei kazi hao hawawaogopi…Zaidi anawatafuta sana watu kama hao..

Unaposikia leo Injili ambayo inamtangaza Yesu Kristo, na inayokufafanulia madhara ya dhambi..Neno lile linapozungumzwa au libapohubiriwa ni sawa na mbegu zinarushwa ndani yako…na moyoni mwako unapokuwa mlegevu kuisikiliza sauti ya Mungu kwa bidii, na kuishia kuchukulia kawaida…mahubiri yale yanapoisha na ukaondoka bila hata kuuliza wala kufuatilia kulitendea kazi au kuuliza mahali ambapo hujaelewa…Basi upo hatarini kutokufikia kumjua Mungu…siku zote utabaki katika hali hiyo hiyo…Hutakaa upate uwezo wa kuishinda dhambi.

Neno la Mungu linahitaji umakini sana(hakikisha unalielewa neno)..usilisome tu au usilisikilize tu ili kusogeza muda..Lisome na kulichunguza kwa bidii kwasababu ni uweza wa Mungu uuletao wokovu. Wokovu huo ni lazima uonekane kwa kila Neno unalojifunza ndani yako…hata kama kuna mahali hatujaelewa tunapaswa tukatafute huku  na huko..tukaulize huku na kule mpaka Neno lile limekuwa Dhahiri kwetu, tumelielewa kweli kweli.

Kuuliza sio ujinga..tenga muda mfuate mchungaji wako, au mwalimu wako, au ndugu yako ambaye unaona anajishughulisha kwa sehemu fulani na mambo ya Mungu Muulize mstari huu unamaana gani?..mbona umenichanganya kidogo!..Muulize mchungaji wako mbona hapa maandiko yanasema hivi na hapa hatufanyi hivi?..Muulize ni kwanini Yesu Kristo alikuja duniani, mwulize unyakuo ni nini?,  mwulize kwanini sehemu moja kwenye biblia ubatizo unasema ni kwa jina la Baba,Mwana na Roho Mtakatifu na sehemu nyingine unasema ni  kwa jina la Yesu?..

Muulize  Israeli ni nini?, siku za mwisho zitakuwaje, mwulize kwanini leo kuna madhehebu mengi?..na maswali mengine mengi, pia uliza kwa watu wengi tofauti tofauti usikie nao wanasemaje kisha piga magoti mwombe Mungu akuonyeshe ukweli na yeye ni mwaminifu (amesema tukimtafuta kwa bidii tutamwona)…usikubali kubaki na maswali ambayo huyaelewi kwa muda mrefu…Hayo maswali ambayo huyaelewi ndio mbegu zenyewe hizo ambazo shetani anazitafuta kwasababu anajua mwishoni zikipata ufumbuzi zitaleta madhara makubwa sana kwake na wewe zitakuletea matunda makubwa sana…Na usipotilia maanani Kulijua Neno la Mungu kwa mapana…Shetani ataliiba na utabaki tu kuwa vile vile muda wote.

Tatizo kubwa tulilonalo wengi ni hofu!..Mtu anaogopa kwenda kumwuliza Mchungaji wake maswali…Bwana Yesu aliulizwa maswali na akayajibu yote…sasa mchungaji au mwalimu au Nabii yeye ni nani asiulizwe maswali?…Tunachopaswa kufanya ni kuwaendea tu kwa hekima na kwa heshima, na kwa unyenyekevu. Na vilevile Mchungaji unapoulizwa maswali, haimaanishi kuwa unajua kila kitu, au utajibu kila kitu kwa ufasaha wote .Lakini kile unachokiona ni kidogo ndani yako, ni kikubwa kwa mtu mwingine aliye mchanga kiroho. Kitamfaa sana kwa wakati huo, Na pia ukikosa majibu kabisa usone vibaya kumwambia sifahamu nitakwenda kutafuta, kuliko kumpotosha ili tu kukisimamia kile unachokiamini.

Bwana atusaidie sana

(hakikisha unalielewa Neno)

Maran atha.


Mada Nyinginezo:

NENO LA MUNGU NI DAWA ILIYO TOFAUTI NA DAWA NYINGINE.

WAZAZI WA YOHANA NA YAKOBO.

Kwanini kila nikitaka kusali naingiwa na uvivu?

JE! MTUMISHI KUTOKUWA NA FEDHA NI ISHARA KUWA KUNA TATIZO KATIKA IMANI YAKE?

KUOTA UNAKULA CHAKULA.

Roho, Nafsi, na Mwili vina utofauti gani?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Nifanye nini ili niwe na uhakika nikifa naenda mbinguni?

SWALI: Nifanye nini ili niwe nina uhakika kuwa hata nikifa ghafla leo hii, nina uhakika wa kwenda mbinguni kwa asilimia zote?


JIBU: Moja ya swali ambalo ukiwauliza wakristo wengi watakujibu kirahisi ni kuhusu kuokoka..Ukimuuliza Je! Umeokoka atakuambia ndio nimeokoka, lakini ukimuuliza, Ikitokea mfano umekufa ghafla leo Je! unao uhakika wa kwenda mbinguni?..Hapo ndipo utakapopata majibu tofauti tofauti, wengine watasema, siwezi kusema hilo Mungu ndio anayejua, wengine watasema kwa kweli hapo sijui, wengine watasema mimi sio Mungu na wengine watesema “natumaini” nitakwenda mbinguni, wengine watasema “ninaamini” itakuwa hivyo..Na wachache sana watasema ninao uhakika nitakwenda mbinguni..

Na katikati ya hao wachache wanaosema ninaohakika, ukiwauliza swali ni kipi kinakupa uhakika huo wa kwenda mbinguni, wengine wanatasema kwasababu ninaishi katika Maisha ya toba kila siku.

Lakini biblia inatuambia kila aliyemwamini mwana wa Mungu ni lazima awe na uhakika ya kuwa anao uzima wa milele ndani yake, na kwamba hata akifa leo atakuwa anaishi..

1Yohana 5:13 “Nimewaandikia ninyi mambo hayo, ili mjue ya kuwa mna uzima wa milele, ninyi mnaoliamini Jina la Mwana wa Mungu”.

Sasa wengi wanakosa Uhakika huu kwasababu hawajakamilishwa katika IMANI ya YESU KRISTO. Na ndio hapo utaona mtu anasema nimeokoka lakini bado anayo hofu akifa leo hajui atakwenda wapi, motoni au mbinguni? Maisha ya kubahatisha. Wengi hawafahamu kuwa Kuokoka ni Neno lenye maana pana sana, na hivyo sio suala la kuongozwa sala ya toba tu na kubaki kama ulivyo. Kuokoka ni jambo linaloleta badiliko ndani ya Maisha ya mtu. Bwana Yesu anafanya kazi ya kuyageuza Maisha ya mtu mpaka mtu huyo anafikia kiwango cha kupata uhakika wa uzima wa milele mwenyewe ndani yake bila hata ya kujilazimisha, au kihisihisi kama anao au hana..Ndani yake kunabubujika uzima wa milele.(Yohana 4:14)

Ni hatua (process)..sio tu kuongozwa sala Fulani ya toba halafu unaendelea kuishi Maisha ambayo ni kinyume na Kristo, halafu ukadhani uhakika huo utakuja wenyewe ndani yako.

Na hiyo inakuja kwa kuyatii maagizo yote Bwana anayompa mtu baada ya kutubu kwake. Akikuambua unapaswa ukabatizwe katika ubatizo sahihi mara baada ya kuokoka kwako, unatii kwa kufanya hivyo, akisema tena..

Yohana 2:15 “Msiipende dunia, wala mambo yaliyomo katika dunia. Mtu akiipenda dunia, kumpenda Baba hakumo ndani yake.

16 Maana kila kilichomo duniani, yaani, tamaa ya mwili, na tamaa ya macho, na kiburi cha uzima, havitokani na Baba, bali vyatokana na dunia.

17 Na dunia inapita, pamoja na tamaa zake, bali yeye afanyaye mapenzi ya Mungu adumu hata milele”.

Unafanya hivyo kwa kujitenga na mambo yote mabaya ya kidunia hii, kama vile ulevi, sigara,disko, anasa, matusi, miziki ya kidunia, rushwa, visasi, chuki, uasherati, utoaji mimba, vimini, mahereni, mawigi, suruali, lipsticks, wanja, n.k. unajitwika msalaba wako na kumfuata Yesu.

Na ukishafanya hivyo kwa kutii maagizo yote aliyokupa sasa hapo ndipo kuna amani Fulani inayotoka kwake na kuingia ndani yako, na hiyo ndiyo inajenga uhakika huo na kukushuhudia kuwa wewe ni mwana wa Mungu. Na hata ikitokea umekufa kwa ghafla haijalishi ni katika hali gani, huna wasiwasi kwasababu mbinguni utakwenda, kwasababu unashuhudiwa moyoni.

Lakini tukisema sisi tunaishi katika Maisha ya toba huwa tunatubu kila siku, na kila dakika na huku nyuma bado Yesu hajaleta badiliko lolote ndani yetu, hapo bado

tunajidanganya..Na mbinguni hatutakwenda. Hatubaatishi kwenda mbinguni, kwamba tunaotea saa atakayokuja atukute tumetubu.. Hivyo kumwamini Yesu na kuwa na uhakika wa uzima wa milele ni Zaidi ya kuongozwa sala ya toba, au kutubu mara kwa mara.. ni pamoja na kuyatii na kuyaishi yale yote anayokuagiza tangu siku ile uliposema nimeamua kumfuata Yesu.

Yohana 5:24 ‘Amin, amin, nawaambia, Yeye alisikiaye neno langu na kumwamini yeye aliyenipeleka yuna uzima wa milele; wala haingii hukumuni, bali amepita kutoka mautini kuingia uzimani’.

Natumai kuanzia leo wewe uliyeokoka ambaye umekuwa huna uhakika kuwa utakwenda mbinguni au la, naamini utaanza kuchukua uamuzi huo mpya wa kumfuata Yesu kwa moyo wako wote na kuyatii yote anayokuambia.., ili na wewe akupe uhakika huo wa kwenda mbinguni, lakini ukibakia katika hali hiyo hiyo ni uthibitisho kuwa huwezi kwenda mbinguni,..

Na kama Bado utakuwa bado hujamwamini Bwana Yesu na wewe unataka leo hii kuokoka, Yesu aanze kuyatengeneza Maisha yako upya, Basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie kama ilivyokuwa hata kwetu sisi. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGU. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.

AMEN.

Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithibitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.

Fanya hivyo na Bwana atakusaidia

Kwa mawasiliano/mafundisho zaidi kwa njia ya whatsapp, tutumie ujumbe kwenye namba hizi: +255789001312/ +255693036618

  Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Ubarikiwe sana.

Tafadhali share ujumbe huu na kwa wengine. Vilevile ikiwa utapenda tuwe tunakutumia masomo haya katika inbox yako ya facebook au whatsapp utatumia ujumbe,

Mada Nyinginezo:

BIBLIA INAITAJA NJIA KUU YA MFALME, NJIA HII NI IPI?

TUMAINI NI NINI?

Waoga ambao hawataurithi uzima wa milele ni watu wa namna gani?(Ufunuo 21:8).

NIFANYE NINI ILI MUNGU AYAJIBU MAOMBI YANGU?

TAFUTA UZIMA WA MILELE NA SI UZIMA TU!.

Biblia inasema tusiwe kwazo kwa yeyote, je! inawezekanikaje kwa dunia hii ya sasa?(2Wakorintho 6:3).

Zeri ya Gileadi ni nini?

Rudi Nyumbani:

Print this post

SI KILA KIPENDEZACHO KINATOKA KWA BWANA.

Na mkia wake wakokota theluthi ya nyota za mbinguni, na kuziangusha katika nchi.


Shalom. Ni siku nyingine tena tumepewa na Bwana. Karibu tujifunze Biblia. Leo tutajifunza njia mojawapo shetani anayotumia kuwaangusha watu.

Kama wengi wetu tunavyojua..historia ya shetani ni ndefu kidogo, ilianzia mbinguni…Huko biblia inasema alikuwa ni malaika wa sifa, Alikuwa ni kerubi wa sifa. Lakini alifanya aliyoyafanya akaiacha enzi yake na nafasi yake akatamani kuwa kama Mungu…baadhi walishawishika kumfuata, kama leo hii tu watu wanavyoshawishika kuwaabudu wanadamu wenzao…Lakini kundi lingine la malaika lililoongozwa na Mikaeli malaika mkuu walimpinga (ambalo hao walikuwa ni wengi kuliko wale walioungana naye) na ikasababisha vita mbinguni..theluthi moja (1/3) ikawa upande wa lusifa na ndio iliyoshindwa vita na theluthi (2/3) iliyokuwa upande wa Mikaeli.

Kumbuka Mungu hakuhusika kwenye hiyo vita, bali Malaika watakatifu, Mungu kamwe hapigani na viumbe vyake..yeye anakuwa tu upande wa wenye haki kuwafanikisha na waovu kuwafadhaisha..Kama alivyokuwa na Daudi vitani dhidi ya majeshi ya maadui zake wafilisti. Hivyo Mungu hata mbingni alikuwa upande wa Mikaeli na malaika zake (kasome Ufunuo 12:7-12).

Sasa leo hatutaingia kuzungumzia kwa undani hiyo vita..Lakini tutaangalia njia moja wapo lusifa aliyoitumia kuwaangusha Malaika walioasi mbinguni.

Tunasoma katika ufunuo..

Ufunuo 12:3 “Ikaonekana ishara nyingine mbinguni; na tazama, joka kubwa jekundu, alikuwa na vichwa saba na pembe kumi, na juu ya vichwa vyake vilemba saba.

4 NA MKIA WAKE WAKOKOTA THELUTHI YA NYOTA ZA MBINGUNI, NA KUZIANGUSHA KATIKA NCHI”.

Nataka tuuzingatie huo mstari wa 4 unaosema …Na mkia wake wakokota theluthi ya nyota za mbinguni, na kuziangusha katika nchi.”

Tunaweza kujiuliza kwanini hajasema mkono wake, au uso wake, au pembe zake..bali anasema mkia wake..Ikiwa na maana kuwa Ushawishi wa shetani haupo katika uso wake, wala pembe zake bali katika mkia wake…

Adui shetani anapotaka kumwangusha mtu, atakuja na uso mzuri, atamletea vitu vizuri usoni, vinavyovutia vyenye ahadi nyingi nzuri, na vyenye matumaini na kutia moyo, lakini nyuma yake anauzungusha mkia wake kumwangusha huyo mtu. Atakuonyesha fursa zote za kuiba, na kufanya ufisadi lakini mbeleni ameshakuandalia watu wa kukuchoma moto na kukufunga.

Atakuhubiria leo hii mafundisho mazuri ya kukufariji na dhambi, na atatumia maandiko kukushawishi kwamba ulevi sio dhambi, kwamba Mungu hawezi kuwahukumu watenda dhambi, Mungu siku zote ni Mungu wa rehema..Kwa uso atakuwa na mwonekano mzuri mbele yako na wa faraja lakini nyuma yake kwa mkia wake anakukokotea kuzimu. Atakuhubiria kuvaa vimini, na nguo zinazochora maungo yako hakuna shida, biblia inaruhusu, lakini yeye anajua ni wangapi unawapeleka kuzima kwa uzinzi wako, na kwamba Mungu naye hataweza kukuacha kwa kosa la kuwakosha wengine.. Ndivyo alivyowadanganya na malaika zake na kumwamini Hakuwafuata kwa ukali, bali kwa uzuri aliokuwa nao, na kwa ahadi nyingi, ingekuwa ni hivyo ni nani angemfuata..

..na hatimaye wakajikuta wote wametupwa chini..

Ndivyo shetani alivyo, pale ambapo anataka kumwangusha mtu hatakuja na mapembe, wala kwato…atajigeuza na kuwa malaika wa Nuru.

Hivyo kwa ufupi tu..Biblia inatuonya tujihadhari…Vitu vya ulimwengu huu vinavyoonekana ni vizuri kwa mwonekano, starehe, anasa, michezo, n.k. lakini vingi ni miradi ya shetani…Hivyo tuwe macho kila siku, sio kila kinachoonekana kwa macho au kinachoonekana kizuri kinatoka kwa Mungu, vingi vinatoka kwa Yule adui..Fashion zinatoka kwa Yule Adui, mitindo mitindo inatoka kwa Yule Adui, burudani nyingi na michezo mingi inayovutia na yenye ushawishi inatoka kwa yule adui. Hivyo Bwana atupe macho ya kuona. Maana hatukosi kuzijua fikra za shetani.

Ubarikiwe sana.

Tafadhali share na wengine ujumbe huu.

Mada Nyinginezo:

ANGUKO LA UFALME WA SHETANI:

UKWELI UNAOPOTOSHA.

VIFUNGO VYA GIZA VYA MILELE.

UFUNUO: Mlango wa 12

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

MPINGA-KRISTO

HERI YULE ATAKAYEKULA MKATE KATIKA UFALME WA MUNGU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

MIILI YA UTUKUFU ITAKUWAJE?

MIILI YA UTUKUFU ITAKUWAJE?: Bwana Yesu alipofufuka, alifufuka na mwili wa Asili..Na kisha baada ya kufufuka tu, mwili wake ule ukabadilishwa na kuwa wa utukufu. Sasa fahari ya miili ya utukufu ni mbali na miili ya asili, kama biblia inavyosema katika…

1Wakorintho 15:40  “Tena kuna miili ya mbinguni, na miili ya duniani; lakini fahari yake ile ya mbinguni ni mbali, na fahari yake ile ya duniani ni mbali.

41  Kuna fahari moja ya jua, na fahari nyingine ya mwezi, na fahari nyingine ya nyota; maana iko tofauti ya fahari hata kati ya nyota na nyota.

42  Kadhalika na kiyama ya watu. Hupandwa katika uharibifu; hufufuliwa katika kutokuharibika;

43  hupandwa katika aibu; hufufuliwa katika fahari; hupandwa katika udhaifu; hufufuliwa katika nguvu;

44  hupandwa mwili wa asili; hufufuliwa mwili wa roho. Ikiwa uko mwili wa asili, na wa roho pia uko.

45  Ndivyo ilivyoandikwa, Mtu wa kwanza, Adamu, akawa nafsi iliyo hai; Adamu wa mwisho ni roho yenye kuhuisha.

46  Lakini hautangulii ule wa roho, bali ule wa asili; baadaye huja ule wa roho”

Jambo moja lisilofahamika na wengi ni kwamba “hakuna mwili wa utukufu pasipo ufufuo”..Ufufuo unatangulia kwanza ndipo miili ya utukufu inafuata. Watakatifu waliokufa sasa hawana miili ya utukufu huko walipo.

Kwahiyo Hata sisi siku ya unyakuo ikifika kama tutakuwa tumekufa…Siku hiyo roho zetu zitatolewa paradiso kwanza mahali ambapo zilikuwa zimehifadhiwa(yaani Paradiso), tutarudishwa duniani kuvaa miili yetu ya asili ambayo ilikuwa imeoza kwenye udongo..siku hiyo Bwana atairudisha tena (ili litimie lile neno linalosema hautapotea  unywele wenu hata mmoja). Kama mtu alikufa na kansa na nywele zake zote zilinyonyoka siku hiyo atarudishwa na kuwa mzima bila kansa na akiwa na nywele zake zote. Hiyo yote ni Mungu kuonyesha kwamba Mauti haina nguvu juu ya watakatifu..funza hawana nguvu juu ya watakatifu, magonjwa hayana nguvu juu ya watakatifu, ulipoteza mkono na jicho kabla ya kufa, siku hiyo utafufuka ukiwa na mkono wako na macho yako mawili, ulemavu utashindwa n.k

 Tukiisha fufuka na kuwa na miili yetu ya asili isiyo na kasoro hata moja…kufumba na kufumbua tutabadilishwa miili yetu hii na kuwa miili ya utukufu..pamoja na wale watakatifu ambao watakuwa hai watabadilishwa pia. Kumbuka hatutavuliwa hii ya asili ambayo imeshafufuliwa…hapana…bali ni hii hii itabadilishwa na kuwa ya kimbinguni (kwa lugha ya kigeni tungeweza kusema inakuwa upgraded, inavikwa uwezo wa ajabu kutoka mbinguni)..

Au vinginevyo ufufuo utakuwa hauna maana…Kwasababu huko huko tulipokuwepo tungepewa hilo miili ya utukufu…lakini unaona lazima tufufuke kwanza kama Bwana Yesu alivyofufuka..turudi kwenye miili yetu ya asili kisha miili hiyo ibadilishwe..

1Wakorintho 15.51  “Angalieni, nawaambia ninyi siri; hatutalala sote, lakini sote tutabadilika,

52  kwa dakika moja, kufumba na kufumbua, wakati wa parapanda ya mwisho; maana parapanda italia, na wafu watafufuliwa, wasiwe na uharibifu, nasi tutabadilika.

53  Maana sharti huu uharibikao uvae kutokuharibika, nao huu wa kufa uvae kutokufa.

54  Basi huu uharibikao utakapovaa kutokuharibika, na huu wa kufa utakapovaa kutokufa, hapo ndipo litakapokuwa lile neno lililoandikwa, Mauti imemezwa kwa kushinda”

Unaona?..Hii inayokufa itavaa kutokufa..sio kwamba itatoweshwa na kuletwa mingine..hapana ni hii hii..

Sasa miili hiyo itakuwa imevikwa uwezo wa ajabu wa kimbinguni… …Uwezo huo ndio kama ule wa Bwana Yesu aliokuwa nao baada ya kufufuka na ule malaika watakatifu walionao sasa.

Unakuwa unauwezo wa kula na kunywa lakini hauishi kwa kula wala kunywa, Bwana Yesu alipofufuka alikula samaki na wanafunzi wake akatoweka  na chakula kile tumboni mwake lakini hakuishi kwa hivyo na hata sasa haishi kwa hivyo…Na pia mwili huo unakuwa na uwezo wa kubadilika badilika kama Malaika. Bwana Yesu baada ya kufufuka sehemu nyingine alionekana na sura nyingine(Marko 16:12)..sehemu nyingine alionekana kama malaika..(Yohana alimwona kwenye maono akiwa na macho kama miale ya moto), mwenye mavazi yanayong’aa sana.. Hata leo hii Bwana anaweza kumtokea mtu kwa umbo la mwanadamu wa kawaida kabisa akakaa naye na kula naye..na anaweza pia kumtokea mtu kwa umbo kama la malaika mwenye utukufu mwingi na mwanga mkali hata mtu asiweze kumtokea..kama alivyomtokea Mtume Paulo. Hizo zote ni tabia za huo mwili mpya wa utukufu. Na sisi tutakapofufuliwa tutafanana na Bwana Yesu katika kila engo..miili yetu itakuwa na tabia hizo hizo.

Mwili huo pia una uwezo wa kupotea na kutokea  mahali pengine kama Bwana Yesu, na pia una uwezo wa kupaa bila mbawa kama Bwana Yesu alivyopaa mbinguni ndio maana siku ile ya unyakuo tutapaa mbinguni na wengine hawataweza, na una upeo mkubwa wa kujua mambo yote. Na tabia nyingine nyingi, za kimbinguni mwili huo unao…ambazo hatuwezi kuzijua zote mpaka tutakapovikwa miili hiyo.

Hivyo itakuwa na uchungu sana kukosa kuvikwa mwili huo..Itakuwa ni uchungu sana wakati wa unyakuo wakati watakatifu wengine wanafufuliwa sisi tuwe tumebaki mautini. Ni heri tuteseke sasa lakini siku ile hatutateseka…ni heri tuonekane tumepoteza kila kitu hapa lakini mbele za Mungu tuonekane hatujapoteza kitu.

2Wakorintho 5:1  “Kwa maana twajua ya kuwa nyumba ya maskani yetu iliyo ya dunia hii ikiharibiwa, tunalo jengo litokalo kwa Mungu, nyumba isiyofanywa kwa mikono, iliyo ya milele mbinguni.

2  Maana katika nyumba hii twaugua, tukitamani sana kuvikwa kao letu litokalo mbinguni;

3  ikiwa tukiisha kuvikwa hatutaonekana tu uchi.

4  Kwa sababu sisi tulio katika maskani hii twaugua, tukilemewa; si kwamba twataka kuvuliwa, bali kuvikwa, ili kitu kile kipatikanacho na mauti kimezwe na uzima”.

 Ni heri uonekane mjinga na mshamba leo kwa kutokuvaa vimini, na masuruali, na kutokuweka makeup, ni heri ukafukuzwa kazi leo kwa kukataa kufanya uasherati, ni heri ukapitia kila aina ya dhiki leo kwa ajili ya Kristo hata ikiwezekana kufa…Lakini Bwana wetu Yesu alisema maneno haya..

Luka 21:17  “Nanyi mtachukiwa na watu wote kwa ajili ya jina langu.

18  Walakini hautapotea hata unywele mmoja wa vichwa vyenu.

19  Nanyi kwa subira yenu mtaziponya nafsi zenu”.

Bwana akubariki. Kama hujaokoka..Ni vizuri ukafanya hivyo leo, usingoje Kesho kwasababu biblia inasema “hujui yatakayozaliwa ndani ya siku moja”..Kifo ni kama usingizi..hujui saa utakayopotelea usingizini. Hivyo tubu sasahivi hapo ulipo…Jitenge dakika chache jitenge peke yako.Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia.. ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.

“Ee mungu baba, naja mbele zako, nikiwa ninajitambua kuwa mimi ni mkosaji na nimekutenda dhambi nyingi, na kwamba nimestahili hukumu. lakini wewe mungu wangu ulisema katika neno lako kuwa wewe ni mungu wa rehema unayewarehemu  maelfu elfu ya watu wanaokupenda wewe. na leo hii ninakuja mbele zako nahitaji msamaha wako na msaada wako mungu wangu, ninatubu dhambi zangu zote kwa kumaanisha na kwa moyo wangu wote, .

Ninakiri kuwa yesu kristo ni bwana, na yeye ndiye mwokozi wa huu ulimwenguni. hivyo naomba damu ya mwanao takatifu inisafishe uovu wangu wote sasa nifanyike kuwa kiumbe kipya kuanzia leo na hata milele.

asante bwana yesu kwa kunipokea na kunisamehe.

Amen”.

Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Ulikuwa na miziki ya kidunia kwenye simu yako ifute yote sasahivi usiache hata mmoja, kulikuwa na watu unamahusiano nao ya kiasherati, futa namba zao sasahivi.

Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo namna hiyo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Na kuna Amani fulani itaingia ndani yako ambayo hiyo ndio itakuwa uthibitisho wa wawe kufanyika kiumbe kipya. Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.

Bwana akubariki sana.

Tafadhali share na wengine.


Mada Nyinginezo:

LOLOTE ATAKALOWAAMBIA FANYENI.

JE NI KWELI MTU ANAWEZA KUTOKA NJE YA MWILI WAKE?.

MWILI NA DAMU YA YESU KRISTO.

Je! kuna ubaya wowote kuwaombea ndugu zetu waliokufa katika dhambi, Mungu awakumbuke katika ufalme wa mbinguni?.

Kuna Mbingu ngapi?

Rudi Nyumbani:

Print this post