Category Archive Uncategorized @sw-tz

MSAMARIA MWEMA.

Msamaria mwema ni mtu wa nanma gani?


Ni kauli ambayo tunaisikia katika jamii yetu mara kwa mara. Na hiyo inatokea pale mtu mfano amekumbana na matatizo au shida Fulani halafu akakutana na mtu asiyemfahamu kisha akamsaidia kutatua tatizo hilo. Sasa mtu kama huyo baadaye akija kuulizwa ilikuwaje ukafanikiwa au ukafanikisha kitu kile katika yale mazingira? ..Ndio hapo utamsikia anasema nilikutana na msamaria mwema akanisaidia…

Lakini baadhi ya watu hawajui chanzo cha msamaria mwema ni nini?..

Habari yake tunaipata kutoka katika biblia, tusome,

Luka 10:25  “Na tazama, mwana-sheria mmoja alisimama amjaribu; akisema, Mwalimu, nifanye nini ili niurithi uzima wa milele?

26  Akamwambia, Imeandikwa nini katika torati? Wasomaje?

27  Akajibu akasema, Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa nguvu zako zote, na kwa akili zako zote; na jirani yako kama nafsi yako.

28  Akamwambia, Umejibu vema; fanya hivi nawe utaishi.

29  Naye akitaka kujidai haki, alimwuliza Yesu, Na jirani yangu ni nani?

30 Yesu akajibu akasema, Mtu mmoja alishuka toka Yerusalemu kwenda Yeriko, akaangukia kati ya wanyang’anyi; wakamvua nguo, wakamtia jeraha, wakaenda zao, wakimwacha karibu ya kufa.

31  Kwa nasibu kuhani mmoja alishuka kwa njia ile; na alipomwona alipita kando.

32  Na Mlawi vivyo hivyo, alipofika pale akamwona, akapita kando.

33  Lakini, MSAMARIA MMOJA katika kusafiri kwake alifika hapo alipo; na alipomwona alimhurumia,

34  akakaribia, akamfunga jeraha zake, akizitia mafuta na divai; akampandisha juu ya mnyama wake, akampeleka mpaka nyumba ya wageni, akamtunza.

35  Hata siku ya pili akatoa dinari mbili, akampa mwenye nyumba ya wageni, akisema, Mtunze huyu, na cho chote utakachogharimiwa zaidi, mimi nitakaporudi nitakulipa.

36  Waonaje wewe, katika hao watatu, ni yupi aliyekuwa jirani yake yule aliyeangukia kati ya wanyang’anyi?

37  Akasema, Ni huyo aliyemwonea huruma. Yesu akamwambia, Enenda zako, nawe ukafanye vivyo hivyo”.

Ni yapi tunajifunza katika Habari ya msamaria mwema?

  • Ili na wewe ufanyike msamaria mema, ni sharti uwe moyo wa huruma.
  • Ni sharti, uwe mwepesi kumsaidia mtu, ambaye hata haonyeshi dalili ya kuomba msaada kwako, lakini unajua kabisa yupo katika hali ya kuhitaji msaada.
  • Upo tayari kutoa hata mali zako, au vitu vyako vya thamani kwa ajili ya kumsaidia tu mtu

Sasa ukizingatia hayo, Basi mbele za Mungu utakuwa umekidhi vigezo vya kumpenda jirani yako kama nafsi yako.. Hapo utakuwa umeshida amri ya pili iliyo kuu kuliko zote, kama yule msamaria mwema.

Kumbuka  tendo hilo lina thawabu kubwa sana mbele za Mungu.

Hivyo ni wajibu wetu sote, kulikumbuka hilo wakati wote tunapoishi humu duniani, ili na sisi Mungu atuhurumie siku ile tuurithi uzima wa milele..

Mada Nyinginezo:

JIRANI YANGU NI NANI?

KUSUDI LA MIMI KUWEPO DUNIANI NI LIPI?

WAKATI ULIOKUBALIKA NDIO SASA.

MKARIBIE BWANA ZAIDI ILI UFANYIKE NGUZO.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

UNYAKUO.

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

ADAM NA EVA.

Adam na eva akina nani?


Hawa ni wazazi wetu wa kwanza.

Biblia inasema

Mwanzo 1:27 “Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba. 

28 Mungu akawabarikia, Mungu akawaambia, Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi, na kuitiisha; mkatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na kila kiumbe chenye uhai kiendacho juu ya nchi”.

Lakini kama tunavyojua waliasi, na ndio hapo ikawa chanzo cha matatizo ambayo ndio mpaka leo mimi na wewe yanatuathiri.

Hawa alidanganywa na nyoka kula matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya, Kumbuka “alidanganywa” wala hakushawishiwa, hii ikiwa na maana kuwa hakujua kuwa kitendo anachokwenda kukifanya kingekwenda kuleta madhara yoyote kwa mtu kwa udanganyifu alioambiwa na nyoka, kwasababu alidanganywa kuwa hatakufa, bali kinyume chake atafumbuliwa macho, atakuwa kama Mungu, akijua mema na mabaya.

1Timotheo 2:13 “Kwa maana Adamu ndiye aliyeumbwa kwanza, na Hawa baadaye. 14 Wala Adamu hakudanganywa, ila mwanamke alidanganywa kabisa akaingia katika hali ya kukosa”.

Lakini siku ile alipojaribu kujitetea kwa kumrushia nyoka mpira, hilo halikusaidia yeye kutoshiriki adhabu.

Vivyo hivyo na sasa, Udanganyifu mwingi umetokea leo hii duniani.. Lakini ni wajibu wako wewe kuujua ukweli na kuushika, kwasababu siku ile hautakuwa na la kujitetea na kusema, mimi mbona sikujua hili, au mimi mbona niliambiwa vinginevyo na watu wanaojiita watumishi wa Mungu.

Kumbuka si watu wote wanaojiita watumishi wa Mungu ni watumishi kweli wa Mungu,, Mtumishi wa Mungu ni lazima akufundishe kweli ya biblia, na kukuongozwa kwa Kristo na sio kwenye mambo ya ulimwengu huu.

Tusidanganywe kama Adam na Eva.

Ndio maana wakati huu wa machafuko mengi ya rohoni, ni vizuri ukawa na Kristo moyoni mwako, na kujifunza Neno la Mungu kwa bidii, ili likae ndani yako ibilisi asikushinde. Kwasababu kama Neno la Mungu halipo ndani yako kwa wingi, kamwe huwezi kuzishinda njama za mwovu,

Utakumbuka kilichomtokea Bwana Yesu kule jangwani, shetani alipomjia na maandiko na yeye alimjibu kimaandiko. Sasa huyo ni mwokozi wa ulimwengu yamemkuta. Itakuwaje mimi na wewe?

Tung’ang’anie NENO LA MUNGU. Maana hilo ndio silaha yetu nyakati hizi za mwisho dhidi ya mwovu shetani, ili tusiwe kama Adam na Eva.

Mada Nyinginezo:

UUMBAJI BORA WA MUNGU, UPO NDANI YA MWANADAMU.

MWAKA WA BWANA ULIOKUBALIWA.

JINA LA MUNGU NI LIPI?

NA UPEPO WA KUSI ULIPOANZA KUVUMA KIDOGO,

VUKA UJE MAKEDONIA UTUSAIDIE.

UZAO WA NYOKA.

KWANINI TUNAPASWA TUJIZUIE?

Rudi Nyumbani:

Print this post

WAFIRAJI KWENYE BIBLIA.

Je! biblia inasema nini juu ya wafiraji?


Ufiraji ni Neno  linalojumisha kitecho chochote cha kumwingilia mwanadamu mwanzako  kimapenzi kinyuma na maumbile.

  • Uwe unamwingilia mwanaume mwenzako (Ulawiti na ushoga),
  •  Au uwe Unamwingilia  mwanamke, hajialishi  ni mkeo, hicho tayari ni kitendo cha ufiraji.

Na ni dhambi biblia imesema hivyo na kwamba watu wote wanaofanya vitendo kama hivyo hawawezi kuurithi uzima wa milele.

1Wakoritho 6:9 “Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? Msidanganyike; waasherati hawataurithi ufalme wa Mungu, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala WAFIRAJI, WALA WALAWITI,

10 wala wevi, wala watamanio, wala walevi, wala watukanaji, wala wanyang’anyi”.

Watu wengi wanajidanganya na kudhani kuwa wakiwaingilia wake zao, maadamu tayari wapo nao katika ndoa, sio dhambi..Ndugu usidanganyike, tendo lolote la kumwingilia mtu mwingine kinyume na maumbile haijalishi ni rafiki, au jirani, au kahaba, au mke, hiyo tayari ni ufiraji.

Vinjari yetu, na chaguzi mbalimbali ili kukidhi kila ladha na bajeti, http://swisswatch.is/ replica watches inapatikana kwa kununua mtandaoni.

Na wafiraji wote watahukumiwa.

Kilichosababisha Sodoma na Gomora viangamizwe, kilikuwa ni kitendo hichi cha ufiraji,

Yuda 1:7 “Kama vile Sodoma na Gomora na miji iliyokuwa kando-kando, waliofuata uasherati kwa jinsi moja na hawa, wakaenda kufuata mambo ya mwili yasiyo ya asili, imewekwa kuwa dalili, wakiadhibiwa katika moto wa milele.
8 Kadhalika na hawa, katika kuota kwao, huutia mwili uchafu, hukataa kutawaliwa, na kuyatukana matukufu”.

Hivyo kama wewe ni mmojawapo tubu haraka sana, kwa kuacha kitendo hicho. Mgeukie Yesu Kristo ayaokoe maisha yako. Ikimbie hukumu ya Mungu. Ziwa la moto lipo kweli.

Jiepushe na utazamaji wa picha na video chafu za ngono zinazozagaa mitandaoni, watu wengi wanaingiliwa na hizi roho kwa kuzitazama tu. Utakuta hapo mwanzo, hakuwa hivyo lakini siku alipooanza kuzitazama tu, anaona kama, shinikizo fulani la nguvu linatoka ndani kumuhimiza kufanya hivyo.

Kama na wewe ni mmoja wapo basi, nakushauri, kaa mbali sana na mambo hayo, shetani anafahamu kuwa wakati wake ni mfupi aliobakiwa nao. Hivyo itazame sana mienendo yako.

Mada Nyinginezo:

JINSI SODOMA NA GOMORA ILIVYOKUWA INAVUTIA SANA..

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

SI KILA KIPENDEZACHO KINATOKA KWA BWANA.

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Baraka za Mungu.

Baraka za Mungu zinakujaje?


Ni vizuri kufahamu kuwa mafanikio sio Baraka, lakini Baraka zinaweza kupelekea mafanikio.

Unaweza ukawa ni tajiri na ukafanikiwa na mali zako zikawa ni nyingi sana, lakini ukawa bado hujabarikiwa na Mungu. Kwasababu mafanikio hata shetani naye anayatoa.

Hilo utalithibitisha katika kitabu cha Mathayo, siku ile ambayo shetani alipotaka kumtajirisha  Yesu kwa mapatano ya kumsujudia..Soma

Mathayo 4:8 “Kisha Ibilisi akamchukua mpaka mlima mrefu mno, akamwonyesha milki zote za ulimwengu, na fahari yake,

9 akamwambia, Haya yote nitakupa, ukianguka kunisujudia”.

Unaona, utajiri, na mali hatoi tu Mungu peke yake kama wengi wanavyodhani, bali shetani pia anatoa  tena anatoa kweli kweli, Lakini Baraka huwa Baraka huwa zinatoka kwa Mungu tu peke yake.

Tukilijua hilo sasa turudi, ili kujifunza Baraka za Mungu ni zipi.

Wagalatia 3:13 “Kristo alitukomboa katika laana ya torati, kwa kuwa alifanywa laana kwa ajili yetu; maana imeandikwa, Amelaaniwa kila mtu aangikwaye juu ya mti;

14 ili kwamba BARAKA YA IBRAHIMU iwafikilie Mataifa katika Yesu Kristo, TUPATE KUPOKEA AHADI YA ROHO kwa njia ya imani”.

Unaona, hapo Baraka ambayo Mungu aliiachia kwanza kwa Ibrahimu tunamjua kuwa alibarikiwa na Mungu, iliachiliwa hata na kwetu sisi kwa njia Yesu Kristo, Na Baraka yenyewe tuliyoipokea ni Roho Mtakatifu.

Leo hii hakuna Baraka kubwa kutoka kwa Mungu zaidi ya Roho Mtakatifu kuwa ndani ya mtu. Ukimkosa Roho Mtakatifu, wewe ni mlaaniwa. Lakini ukimpata Roho Mtakatifu basi umepata vitu vyote. Na mafanikio juu.

Huwezi kumpendeza Mungu kama huna Roho Mtakatifu yeye mwenyewe alisema..

Warumi 8:9 “……..Lakini mtu awaye yote asipokuwa na Roho wa Kristo, huyo si wake”.

Sasa Roho Mtakatifu tunampataje?

Tunampata kwanza kwa kutubu dhambi zetu  kwa kumaanisha, kisha tunakwenda kubatizwa katika ubatizo sahihi wa kimaandiko wa kuzamwishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO, ili tupate ondoleo la dhambi zetu, na baada ya hapo sasa Mungu atakupa kipawa cha Roho wake Mtakatifu ndani yetu. Sawasawa na Matendo 2:38

Matendo 2:38 “Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.

39 Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu wamjie”.

Sasa ukishakuwa na uhakika kuwa umeyafuata hayo maagizo yote kwa bidii, na umemaanisha kweli kutubu dhambi zako, na sio nusu nusu, yaani mguu mmoja nje, mwingine ndani, basi wakati huo huo Roho wa Mungu atashushwa ndani yako..(Wengi wanadhani Roho Mtakatifu ni mpaka unene kwa Lugha, hapana yeye ni zaidi ya hapo, kunena kwa lugha ni moja ya njia zake, lakini unapotubu na kubatizwa wakati huo huo Roho Mtakatifu ataingia ndani yako.) .

Na baada ya hapo sasa ndipo na mafanikio mengine yote yataambatana nawe kwa wakati wake, kwa kuwa umeyashika maagizo yake kwa bidii. Sawasawa na Kumbukumbu la Torati 28

1 Itakuwa utakaposikia sauti ya Bwana, Mungu wako, kwa bidii, kutunza kuyafanya maagizo yake yote nikuagizayo leo, ndipo Bwana, Mungu wako, atakapokutukuza juu ya mataifa yote ya duniani;

2 na baraka hizi zote zitakujilia na kukupata usikiapo sauti ya Bwana, Mungu wako.

3 Utabarikiwa mjini, utabarikiwa na mashambani.

4 Utabarikiwa uzao wa tumbo lako, na uzao wa nchi yako, na uzao wa wanyama wako wa mifugo, maongeo ya ng’ombe wako, na wadogo wa kondoo zako.

5 Litabarikiwa kapu lako, na chombo chako cha kukandia unga.

6 Utabarikiwa uingiapo, utabarikiwa na utokapo. 7 Bwana atawafanya adui zako wainukao juu yako kupigwa mbele yako; watakutokea kwa njia moja, lakini watakimbia mbele yako kwa njia saba.

8 Bwana ataiamuru baraka ije juu yako katika ghala zako, na mambo yote utakayotia mkono wako; naye atakubarikia katika nchi akupayo Bwana, Mungu wako.

9 Bwana atakuweka uwe taifa takatifu kwake, kama alivyokuapia; utakaposhika maagizo ya Bwana, Mungu wako, na kutembea katika njia zake.

10 Na mataifa yote ya duniani watakuona umeitwa kwa jina la Bwana, nao watakuwa na hofu kwako.

11 Bwana atakufanya uwe na wingi wa uheri, katika uzao wa tumbo lako, na uzao wa wanyama wako wa mifugo, na uzao wa nchi yako, katika nchi Bwana aliyowaapia baba zako kwamba atakupa.

12 Atakufunulia Bwana hazina yake nzuri, nayo ni mbingu, kwa kutoa mvua ya nchi yako kwa wakati wake, na kwa kubarikia kazi yote ya mkono wako; nawe utakopesha mataifa mengi, wala hutakopa wewe.

13 Bwana atakufanya kuwa kichwa, wala si mkia; nawe utakuwa juu tu, wala huwi chini; utakapoyasikiza maagizo ya Bwana, Mungu wako, nikuagizayo hivi leo, kuyaangalia na kufanya;”

Hivyo Baraka ya Mungu ni Roho Mtakatifu.Ukimpata huyo basi umepata kila kitu.

Lakini usidanganyike na kumwona kila mtu mwenye mafanikio na huku yupo mbali na Mungu ukadhani amebarikiwa…Huyo ni mlaaniwa tu mbele za macho ya Mungu.

Bwana akubariki.

Mada Nyinginezo:

Yuko azuiaye sasa hata atakapoondolewa! ni nani huyo?

KANUNI RAHISI YA KUFANIKIWA.

MISTARI SHETANI ANAYOITUMIA KUWAANGUSHA WATU

MISTARI SHETANI ANAYOITUMIA KUWAANGUSHA WATU

USIFIKIRI FIKIRI.

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Yesu ni Mungu?, Na Kama ni Mungu kwanini alikufa?

SWALI: Je! Yesu ni Mungu? Na Kama ni Mungu kwanini alikufa?


JIBU: Yesu alikuwa ni Mungu katika mwili (1Timotheo 3:16)…lakini hakuja kutafuta kuabudiwa wala kusujudiwa!…Mpaka Mungu amevaa mwili na kuja ulimwenguni, maana yake hajaja kutafuta kuabudiwa, kama angekuwa amekuja kutafuta utukufu wake basi, kulikuwa hakuna haja ya kuuvaa mwili na kushuka duniani, naamini Mbingu ilikuwa inamtosha…. hivyo ni lazima atakuwa amekuja kwa kusudi lingine na si la kutafuta utukufu. Hapo ndipo wengi wa wasio wakristo wanaposhindwa kuelewa, na baadhi ya walio wakristo.

Unapoona askari wa kuongoza barabarani (Traffic man), kaondoka barabarani na kaenda nyumbani kubadilisha nguo zake hizo nyeupe…na akavaa nguo za kiraia na kuingia mtaani basi ni dhahiri kuwa huko mtaani alikokwenda hajakwenda kutafuta kuongoza magari bali kaenda kutafuta mambo yake mengine ya kawaida..labda anaenda hospitalini au sokoni au kusalimia ndugu na marafiki, au kufuatilia mambo yake mengine ambayo ni tofauti na ya kikazi….. (ni kweli bado atabaki kuwa askari, lakini yupo nje ya ofisi yake), hivyo hataweza kuyatumia yale mamlaka aliyonayo ya kuongoza magari,…na akiwa barabarani na nguo zake za kiraia, hata watu wanaweza wasimtambue kama ni askari, atakuwa kama raia wengine tu, na magari atakuwa anayakwepa tu kama raia wengine, na atazingatia sheria zote za barabarani kama raia wengine…

Na Bwana Yesu ni hivyo hivyo…alipokuwa mbinguni alikuwa ni Mungu, anayestahili kuabudiwa na kuheshimiwa…aliposhuka duniani alikivua kile cheo cha Kiungu…na kuwa kama mwanadamu (kwa lengo la kuja kumkomboa mwanadamu na si kuabudiwa kama Mungu)..na baada ya kumaliza akarudi mbinguni alikotoka katika cheo chake.

Hivyo akiwa kama mwanadamu alikuwa hana budi aishi kama wanadamu wengine, hana budi awe mtu wa ibada kama watu wengine, hana budi ale, anywe, alale, achoke, apitie yote mwanadamu wa kawaida anayopitia na hata ikiwezekana afe…ili tu kusudi lake lililomleta duniani litimie la kumkomboa mwanadamu…lakini alikuwa bado ni Mungu.

Wafilipi 2: 5 “Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu;

6 ambaye yeye mwanzo alikuwa YUNA NAMNA YA MUNGU, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho;

7 bali ALIJIFANYA kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu;

8 tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba”.

Umeona hapo mstari wa 7?..unasema “ALIJIFANYA”..kama unakielewa Kiswahili vizuri utakuwa unajua maana ya “KUJIFANYA”..Maana yake ni kama kujigeuza/kuigiza kuwa kitu Fulani na kumbe sio…kwa lengo la kutimiza kusudi Fulani tu!…Hivyo Bwana Yesu aliyejifanya kuwa hana utukufu…ili ashuke aje kutukomboa na kutuonyesha njia jinsi mwanadamu kamili anayemcha Mungu anapaswe awe.

Hivyo kufa kwa Bwana Yesu, hakumfanyi yeye asiwe Mungu..na pia muujiza mkubwa duniani na mbinguni sio kutokufa!!… Huo ni muujiza mdogo sana…..“miujiza mkubwa ni uwezo wa mtu kuutoa uhai wake na kisha kujirudishia ule uhai”..Huo ndio muujiza mkubwa kuliko yote!..na uwezo huo alikuwa nao Yesu pekee yake.

Yohana 10:17 “Ndiposa Baba anipenda, kwa sababu nautoa uhai wangu ili niutwae tena.

18 HAKUNA MTU ANIONDOLEAYE, BALI MIMI NAUTOA MWENYEWE. NAMI NINAO UWEZA WA KUUTOA, NINAO NA UWEZA WA KUUTWAA TENA. Agizo hilo nalilipokea kwa Baba yangu”.

Sasa utauliza ni wapi, Yesu aliutoa uhai wake mwenyewe?…kasome Luka 23:46-47. Bwana Yesu aliutoa uhai wake mwenyewe! Hakuna mtu aliyemsaidia kuutoa..hata Pilato alishangaa imekuwaje amewahi kufa kiasi kile (Marko 15:44). Na aliurudisha uhai wake mwenyewe baada ya siku tatu (kule kaburini hakuna mtu aliyeenda kumfufua au kumwombea afufuke).

Alijirudishia uhai wake mwenyewe!..Nadhani huo ni muujiza mkubwa sana.. Je wewe unaweza kufanya hivyo????

Hata mfano nikikuwekea watu wawili mbele yako mmoja hawezi kuukata mguu wake na mwingine anao uwezo wa kuukata na kuurudisha….nikakwambia kati ya hao wawili ni yupi hapo wa kuogopwa zaidi??..Bila shaka utaniambia “Yule mwenye uwezo wa kuukata mguu wake na kisha kujirudisha tena ndiye wa kuogopwa zaidi kuliko huyo mwingine”.

Kwahiyo kuupima uungu wa Bwana Yesu na kifo chake ni hoja dhaifu!!..miungu ya kipagani ndio isiyo na uwezo wa kufanya hayo..lakini Mungu wa mbingu na nchi (YESU KRISTO) anaweza kufanya mambo yote. Mpaka sasa katika historia hajatokea nabii yoyote wala mtume yeyote aliyofanya miujiza kama aliyofanya Bwana Yesu, sasa kwanini asiwe Mungu?. Na siku moja atarudi na kila jicho litamwona na kila goti litapigwa, na kila kinywa kitakiri…Wengi itakuwa ni jambo la kushtukiza sana kwao, kwasababu hawataamini kwamba kweli ndiye!..kwasababu walidanganyika wakiwa duniani kwamba hatarudi.

Lakini anatupenda na wala hataki mtu yoyote apotee bali wote tuifikie toba, ili tuokoke na tuje kutawala naye milele.

Bwana atubariki tuzidi kumjua yeye!

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

Mbona Mungu anaruhusu watu wapate shida, ilhali ana uwezo wa kutuepusha?

Katika biblia Neno “Mshenzi” linatajwa.Kwanini liwekwe?

Kile kinara cha Taa ndani ya Hekalu la Sulemani kilikuwa kinawakilisha nini?

Je! Ni kweli ubatizo wa maji hatuuhitaji tena?

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Agano jipya ni nini?

Agano jipya ni nini?


Tukitamka neno “agano jipya”  tunathibitisha kuwa lilishawahi kuwepo agano la zamani (La kale) hapo kabla.

Hivyo ili kufahamu agano jipya ni nini, ni vizuri kwanza ukapata msingi wa agano la Kale, lilikuwaje.

Kama tunavyojua Biblia imeundwa na maagano makuu wawili, yaani jipya na la kale.

  1. Agano la Kale:

Sasa msingi wa agano la kale ulitoka kwa mtu mmoja aliyeitwa Ibrahimu. Mungu alipomuita hakumuita ilimradi tu, bali aliingia agano naye akamwambia atambariki na kumfanya kuwa baba wa mataifa mengi, ikiwa tu atakuwa mkamilifu na atakwenda  katika njia zake..Tusome.

Mwanzo 17:1 “Abramu alipokuwa mtu wa miaka tisini na kenda, Bwana akamtokea Abramu, akamwambia, Mimi ni Mungu Mwenyezi, uende mbele yangu, ukawe mkamilifu. 

2 Nami nitafanya agano langu kati ya mimi na wewe, nami nitakuzidisha sana sana. 

3 Abramu akaanguka kifudifudi. Mungu akamwambia, akasema, 

4 Mimi, agano langu nimefanya nawe, nawe utakuwa baba wa mataifa mengi, 

5 wala jina lako hutaitwa tena Abramu, lakini jina lako litakuwa Ibrahimu, kwani nimekuweka uwe baba wa mataifa mengi. 

6 Nitakufanya uwe na uzao mwingi sana, nami nitakufanya kuwa mataifa, na wafalme watatoka kwako. 

7 Agano langu nitalifanya imara kati ya mimi na wewe, na uzao wako baada yako, na vizazi vyao, kuwa agano la milele, kwamba nitakuwa Mungu kwako na kwa uzao wako baada yako. 

8 Nami nitakupa wewe na uzao wako baada yako nchi hii unayoikaa ugeni, nchi yote ya Kanaani, kuwa milki ya milele; nami nitakuwa Mungu wao. 

9 Mungu akamwambia Ibrahimu, Nawe ulishike agano langu, wewe na uzao wako kwa vizazi vyao baada. yako. 

10 Hili ndilo agano langu utakalolishika, kati ya mimi na wewe, na uzao wako baada yako, Kila mwanamume wa kwenu atatahiriwa. 

11 Mtatahiriwa nyama ya magovi yenu, na jambo hilo litakuwa ishara ya agano kati ya mimi na ninyi”.

Unaona, Jinsi Mungu alivyokuwa mwaminifu, baadaye Mungu akaja kumtimizia kweli agano aliliomuahidia, kwa jinsi uzao wake ulivyokuwa unaongezeka duniani kwa kasi, Lakini wakati huo wote uzao wake ulikuwa haumjui Mungu vizuri, ulikuwa bado haujajua kanuni za agano hilo ambalo Mungu aliloingia na Ibrahimu baba yao linavyopaswa liwe..

Ndio hapo wakiwa kule jangwani sasa Mungu anamtumia Musa kusema nao na kuwapa sheria na amri za kuzishika ili wafanikiwe..

Sheria hizo ndizo zilizoandikwa katika vitabu vya Torati: yaani

  • Mwanzo
  • Kutoka
  • Hesabu
  • Mambo ya Walawi
  • Kumbukumbu la Torati.

Hivyo vitabu hivyo vitano vilikamilisha Sheria yote ya Agano hilo ambalo Mungu aliingia na Ibrahimu.

Lakini hiyo peke yake haikuwa inatosha wana wa Israeli kumfahamu Mungu katika ukamilifu wote, Hivyo ilipasa  Mungu azungumze nao mara kwa mara kupitia watu mbalimbali wakamilifu na manabii wake.. Mfano tunamwona mtu kama Ayubu, Esta, Ruthu, kwa kupitia maisha ya hawa Mungu aliwafundisha wana wa Israeli jinsi ya kuishi katika njia zake. Vilevile akawa anasema nao mara kwa mara kupitia manabii wake wengi na waamuzi na mfano Samweli, Isaya, Yeremia, Danieli, Yona,Malaki N.k.

Hivyo kwa kupitia hao pia, na vitabu vyao walivyoviandika, iliwasaidia wana wa Israeli walishike na kulikumbuka agano ambalo aliingia nao zamani.

Kwahiyo tunapovisoma vitabu 39 vya Agano la Kale,.. tunafahamu kuwa ni jumuisho la sheria zote na kanuni zote za Mungu kwa wale alioingia nao agano kupitia Ibrahimu.

Sasa mpaka hapo umeshapata msingi wa Agano la kale kwa ufupi lilipoanzia..


      2.  Tukirudi kwenye agano jipya..

Hilo ni agano lingine lili bora zaidi kuliko lile la Ibrahimu.,

Hili nalo  Mungu aliingia katika agano na mtu mmoja tu, kama vile alivyoingia na Ibrahimu.. Na mtu huyo si mwingine zaidi ya YESU KRISTO.

Ibrahimu alipewa tu uzao wake wa kimwili, lakini huyu alipewa uzao wa wote wenye mwili wakimwamini tu kwa kuzaliwa mara ya pili.

Na ndio maana kuna umuhimu wa kila mmoja wetu kuzaliwa mara ya pili ili tufanyike kuwa uzao wake. yeye mwenyewe alisema..

Yohana 3:3  “Yesu akajibu, akamwambia, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa mara ya pili, hawezi kuuona ufalme wa Mungu”.

Na kubatizwa kwetu ndio ishara ya tohara yenyewe ya rohoni kama ilivyokuwa kwa Ibrahimu na watoto wake wote walipotahiriwa kwa kutolewa magovi. Vivyo hivyo na sisi tunapaswa tukabatizwe kama ishara ya kutahiriwa mioyo yetu.

Lakini tukishazaliwa mara ya pili, hilo tu peke yake haitoshi, ni sharti pia tujue kanuni, na amri Mungu anazozitaka za agano hili ili tuweze kudumu ndani yake. Kama Uzao wa Ibrahimu ulivyopewa.

Hapo ndipo vitabu vya Injili ya Yesu Kristo, na vile  vya mitume, viliandikwa kwa ajili yetu ili sisi sote tutakapovisoma na kuvishika basi tuweze kudumu na kuimarika katika hilo agano jipya la Damu ya Yesu Kristo.

Ndipo hapo tunakutana na vitabu 27 vya agano jipya.

Hivyo kwa kwa hitimisho fupi.. Agano jipya ni agano Mungu aliloingia na Yesu pamoja na uzao wake wote. Ambao mimi na wewe tunahesabiwa katika uzao huo  kwa kumwamini Yesu na kubatizwa.

Tukifanikiwa kufanya hivyo basi na baraka zote, Mungu alizomuahidia Yesu Kristo, na sisi sote pia tunazishiriki na kuzirithi, ikiwemo uzima wa milele.

Bwana akubariki.

Je! Na wewe upo ndani ya agano jipya? Kama bado basi fanya hima ukaribishe Yesu leo ndani ya maisha yako akuokoe ufanyike uzao wa kifalme. Kumbuka hii ni neema ambayo sisi watu wa mataifa hatukustahili, hivyo uiichezee hata kidogo..

1Petro 2:9  “Bali ninyi ni mzao mteule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu wa milki ya Mungu, mpate kuzitangaza fadhili zake yeye aliyewaita mtoke gizani mkaingie katika nuru yake ya ajabu; 10  ninyi mliokuwa kwanza si taifa, bali sasa ni taifa la Mungu; mliokuwa hamkupata rehema, bali sasa mmepata rehema”.

Haleluya.

Mada Nyinginezo:

TOBA IGUSAYO MOYO WA BWANA.

Je! habari ya Yusufu, inabeba ujumbe gani kwa agano jipya?

Bwana aliposema “sikuja kutangua torati bali kuitimiliza” alikuwa anamaanisha nini?

UTIMILIFU WA TORATI.

TAZAMA, MWISRAELI KWELI KWELI, HAMNA HILA NDANI YAKE!

Sanduku la Agano lilikuwa linawakilisha nini katika Agano jipya?

KUTAHIRIWA KIBIBLIA

MWAKA WA BWANA ULIOKUBALIWA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

UPENDO WA MUNGU.

Upendo wa Mungu ni upi?


Kwanza kabla ya kufahamu upendo wa Mungu upoje, ni muhimu kufahamu aina za upendo. Zipo aina kuu tatu za upendo.

  1. Aina ya kwanza ni Upendo unaotokana na hisia, ujulikanao kama EROS. Huu ndio upendo wa mke na mume, katika biblia tunaweza kuona Sulemani akiueleza kwa mapana na marefu katika kitabu cha Wimbo ulio Bora.

Wimbo ulio bora 1:13 “Mpendwa wangu ni kama mfuko wa manemane Ukilazwa usiku maziwani mwangu. 

14 Mpendwa wangu ni kama kishada cha hina, Katika mizabibu huko Engedi. 

15 Tazama, u mzuri, mpenzi wangu, U mzuri, macho yako ni kama ya hua.  16 Tazama, u mzuri, mpendwa wangu, Wapendeza, na kitanda chetu ni majani; 

17 Nguzo za nyumba yetu ni mierezi, Na viguzo vyetu ni miberoshi.”

  1. Upendo wa pili ni ule unaozuka kutokana na mahusiano mtu mmoja alio nao kwa mwingine, almaarufu kama PHILEO,. Huu unaweza ukawa upendo wa mtu na ndugu yake, mchezaji mwenzake, mfanyakazi mwenzake, mwanafunzi mwenzake, mkristo mwenzako, n.k. ni upendo ambao kama hakuna kitu cha kuwaunganisha pamoja, au faida fulani kupatikana, hauwezi kuzaliwa.

Upendo wa namna hii sio upendo mkamilifu sana (ikiwa na maana haujafikia viwango vile vyenyewe),  mkristo, kwasababu hata wenye dhambi wanaweza kuwa nao, Na ndio maana Bwana Yesu alisema..

Mathayo 5.46  “Maana mkiwapenda wanaowapenda ninyi mwapata thawabu gani? Hata watoza ushuru, je! Nao hawafanyi yayo hayo?

47  Tena mkiwaamkia ndugu zenu tu, mnatenda tendo gani la ziada? Hata watu wa mataifa, je! Nao hawafanyi kama hayo?

48  Basi ninyi mtakuwa wakamilifu, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu”.

  1. Upendo wa tatu ndio mkuu kuliko yote unajuliana kama AGAPE (UPENDO WA KI-MUNGU).

Huu ndio Upendo ambao Yesu alikuwa anaulenga kila mahali, Ni upendo usiokuwa na masharti, Unampenda mtu bila ya kuwa na sababu yoyote ya kukufanya umpende, haijalishi awe nawe anakupenda au hakupendi, anakuchikia au hakuchukii,  anakusema vibaya au hakusemi vibaya..Unapenda bila masharti, aina hii ya upendo ndio aliokuwa nao Yesu.

Biblia imeziorodhesha tabia za Upendo huo wa ki-Mungu katika kitabu cha Wakoritho wa kwanza. Tusome.

 1Wakoritho 13:4  “Upendo huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu; upendo hautakabari; haujivuni; 5  haukosi kuwa na adabu; hautafuti mambo yake; hauoni uchungu; hauhesabu mabaya;

6  haufurahii udhalimu, bali hufurahi pamoja na kweli;

7  huvumilia yote; huamini yote; hutumaini yote; hustahimili yote.

8  Upendo haupungui neno wakati wo wote; bali ukiwapo unabii utabatilika; zikiwapo lugha, zitakoma; yakiwapo maarifa, yatabatilika”.

Hivyo mpaka hapo sasa umeshauelewa huu upendo wa Mungu ni upi? Ni upendo usiojali wewe ni nani na ndio maana biblia ilisema..

Yohana 3:16 “Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele”.

Hivyo kama wewe ni mwenye dhambi ujue kuwa Mungu anakupenda na ndio maana anataka kukuokoa usiende kuzimu na dhambi zako, haijalishi ulimkosea kiasi gani, leo hii yupo tayari kukusamehe na kukupa uzima wa milele, Hivyo usikiapo ujumbe huu, usiufanye moyo wako kuwa mgumu bali, mgeukie yeye na akusemehe dhambi zako.

Hizi ni siku za mwisho ukifa na dhambi zako hakika utakwenda kuzimu.

Shalom.

Upendo wa Mungu, ni wa kipekee sana.

Mada Nyinginezo:

JINSI NEEMA YA MUNGU ILIVYOKUWA KUBWA KWA MKE WA LUTU.

JINA LA MUNGU NI LIPI?

UUMBAJI BORA WA MUNGU, UPO NDANI YA MWANADAMU.

UNYAKUO.

HUYU MELKIZEDEKI NI NANI?

Kwanini Yesu Kristo ni mwana wa Adamu?

WINGU KUBWA LA MASHAHIDI.

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita..

Rudi Nyumbani:

Print this post

SIKU ZA MWISHO WA DUNIA.

Siku za mwisho wa dunia zitakuwaje?


Ukweli ni kwamba dalili zote zinaonyesha kuwa tunaishi katika siku hizo.

Shetani anawapufusha watu wengi macho wasilione hilo, ili waendelee kujiburudisha katika mambo maovu ya ulimwengu huu ili siku hiyo iwajilie kwa ghafla kama ilivyowajiliwa watu wa Sodoma na Gomora, na watu wa Nuhu.

Kabla ya hii dunia kuisha kuna mambo kadha wa kadha ambayo yatatangulia.

  • Kwa ufupi tukio la kwanza ambalo ni kuu tunalolingojea sasa hivi ni tukio la UNYAKUO.

Ikiwa bado hujafahamu Unyakuo ni nini, na litawahusu nani na nani bofya hapa ili ufahamu >> UNYAKUO.

Sasa ikitokea mfano Yesu amerudi leo, na ameshanyakua watakatifu wake, basi dunia hii itakuwa imebakiwa na muda mfupi sana usiozidi miaka 7 tu mpaka iishe, Hiyo ni kulingana na unabii wa Danieli (Soma Danieli 9:24-27). Ili kufahamu vema bofya hapa >> DANIELI: Mlango wa 9

  • Sasa ndani ya hicho kipindi cha miaka saba Mpinga-Kristo atanyanyuka ili kuleta dhiki kuu kwa wale ambao watakuwa wamebaki hapa duniani hawakwenda katika unyakuo. Yeye ndiye atakayelisimamisha chukizo la uharibifu..Kwa maelezo marefu fungua hapa kufahamu Zaidi >> CHUKIZO LA UHARIBIFU
  • Sasa mpinga-Kristo akishamaliza kazi yake, kutakuwa na mapigo mengine ya Mungu ya vitasa saba, mahususi kwa ajili ya kuwaadhibu wale wote watakaokuwa hai ulimwenguni kwa wakati huo bofya hapa ili kujua urefu wa mapigo hayo. >> SIKU YA BWANA INAYOTISHA YAJA!
  • Kisha baada ya hapo  itafuata Hukumu ya Mungu kwa mataifa. Na hapo ndipo Mungu atakapotenga mbuzi na kondoo.. Kondoo atawaweka mkono wake wa kuume, na mbuzi atawaweka mkono wake wa kushoto.

Siku za mwisho wa dunia.

  • Na baada ya hapo utaanza utawala wa Amani wa miaka 1000 duniani wa Yesu Kristo(Hiyo ni baada ya dunia na waovu wote kusafishwa). Bofya hapa >> UTAWALA WA MIAKA 1000.
  • Na mwisho wa ule utawala wa miaka 1000 shetani atafunguliwa kwa muda tena kuwajaribu watu watakaokuwepo ulimwengu wakati huo..Hapo ndipo atakapokamatwa na kutupwa katika lile ziwa la moto.
  • Kisha kitakachofuata ni hukumu ya kiti cheupe cha enzi cha mwana-kondoo. Hapo ndipo mataifa yote yatapokusanyika yahukumiwe.
  • Na kila kitu kikishakwisha, Ile Yerusalemu mpya itashuka kutoka mbinguni. Na ndipo maskani ya Mungu itakuwa Pamoja na wanadamu. Na watu wataishi na Mungu milele na milele na milele isiyokuwa na mwisho. >> UFUNUO: Mlango wa 21

Hakutakuwa na machozi tena wala vilio, wala misiba, wala huzuni,wala magonjwa wala majaribu. Bali tutaishi na Mungu wetu katika furaha isiyokuwa na kifani milele na milele, kipindi hicho ndicho tutakachojua nini maana ya Maisha..kwasasa umilele wote huo tutakaishi na Mungu tutayajua mengi sana.

Ni jukumu letu mimi na wewe, kukaza mwendo kipindi hichi, ili tuhakikishe kuwa Unyakuo hautupiti.

Kufahamu zaidi juu ya siku za mwisho wa dunia, angalia mada nyinginezo chini..

Mada Nyinginezo:

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

MAONO YA NABII AMOSI.

BONDE LA KUKATA MANENO.

MPINGA-KRISTO

MIHURI SABA

NYAKATI SABA ZA KANISA NA WAJUMBE WAKE.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Je! Lewiathani ni nani?

Lewiathani ni nani?


Zaburi 104: 25 “Bahari iko kule, kubwa na upana, Ndimo mlimo viendavyo visivyohesabika, Viumbe hai vidogo kwa vikubwa.

26 Ndimo zipitamo merikebu, Ndimo alimo LEWIATHANI ULIYEMWUMBA ACHEZE HUMO.

27 Hao wote wanakungoja Wewe, Uwape chakula chao kwa wakati wake”

Vipo viumbe vingi vilivyopo ambavyo havijagunduliwa bado, na pia vipo baadhi ambavyo vilipotea wakati wa gharaka…tafiti zinaonyesha kuna idadi kubwa sana ya viumbe vinavyopotea kila siku duniani, inakadiriwa kuwa kati ya aina 200-2,000 ya viumbe vinapotea kila mwaka ulimwenguni ambayo ni idadi kubwa sana, na vipo pia ambavyo vinagunduliwa, ambavyo vilikuwa havijawahi kufahamika.

Sasa kama biblia inavyosema hapo juu kuna nyoka baharini aitwaye “lewiathani”..Huyo nyoka ni kweli yupo…Ni aina ya nyoka tu ambao pengine wanaweza kuwa wakubwa zaidi kuliko nyoka wa kawaida kama chatu au anakonda na wenye uwezo mkubwa, lakini wamo humo baharini, na Wanasayansi bado hawajawaona, lakini labda watakuja kuwaona au walishatoweka zamani kutokana na mabadiliko ya tabia ya nchi…lakini watu walioishi zamani waliwajua nyoka hao kiundani.

Lakini hilo sio la muhimu sana, kufahamu kama wapo au la!…na wala si suala la kuweka hofu, kwamba kitakuwa ni kiumbe cha kutisha sana na cha kuogopeka…Kwasababu viumbe vyote vilivyoumbwa na Mwenyezi Mungu vimewekwa chini ya Mwanadamu, avitiishe na kuvitawala, hakuna kiumbe chochote kilichomzidi mwanadamu kwa uweza na nguvu…Hivyo hata vikiwa na umbo kubwa na la kutisha kiasi gani, bado havitakuwa na akili kama mwanadamu, na vitakuwa chini ya mwanadamu tu!…haijalishi vitakuwa vimesifiwa kiasi gani katika biblia, bado havitakuwa na utashi wala akili ya kumzidi mwanadamu..

Kwamfano utaona katika biblia wanyama wengine wakisifiwa sana (Ayubu 40:16-24, na Ayubu 41:12-34), lakini bado haviwezi kulinganishwa na mtu.

Na huyu Nyoka anayeitwa LEWIATHANI ni hivyo hivyo..ni mnyama tu kama wanyama wengine, haijalishi atasifiwa kiasi gani lakini bado atakuwa ni mnyama tu atakayekuwa chini ya mwanadamu.

Ayubu 3:7 “Tazama, usiku huo na uwe tasa; Wala isiwe ndani yake sauti ya shangwe.

8 Na waulaani hao waulaanio mchana, Hao walio tayari kumwamsha huyo lewiathani”.

Sasa kwanini biblia imtaje huyu Lewiathani?.

Biblia mara nyingi inatumia Wanyama kuwafananisha na watu…kwamfano utaona shetani anatambulika kama JOKA (Ufu.12), kutokana na mnyama wa kwanza kukaribisha dhambi ulimwenguni kuwa “nyoka”..hali kadhalika Bwana wetu Yesu anafahamika kama “mwanakondoo” kutokana na tabia ya upole wa kondoo n.k

Hivyo pia Lewiathani kama nyoka aishie baharini tabia zake zimefananishwa na tabia za mpinga-Kristo ambaye siku za Mwisho Bwana atamwua.

Isaya 27:1 “Katika siku hiyo Bwana, kwa upanga wake ulio mkali, ulio mkubwa, ulio na nguvu, atamwadhibu lewiathani, nyoka yule mwepesi, na lewiathani, nyoka yule mwenye kuzonga-zonga; naye atamwua yule joka aliye baharini”.

Tunasoma pia katika…

2Wathesalonike 2:7 “Maana ile siri ya kuasi hivi sasa inatenda kazi; lakini yuko azuiaye sasa, hata atakapoondolewa.

8 Hapo ndipo atakapofunuliwa yule asi, ambaye Bwana Yesu atamwua kwa pumzi ya kinywa chake, na kumwangamiza kwa ufunuo wa kuwapo kwake;

9 yule ambaye kuja kwake ni kwa mfano wa kutenda kwake Shetani, kwa uwezo wote, na ishara na ajabu za uongo;

10 na katika madanganyo yote ya udhalimu kwa hao wanaopotea; kwa sababu hawakukubali kuipenda ile kweli, wapate kuokolewa”.

Siku za mwisho Bwana atamharibu mpinga-kristo na wafuasi wake wote…Bwana atusaidie kutuepusha na roho ya MpingaKristo ambayo inatenda kazi sasa.

Maran atha!

Mada Nyinginezo:

Je! Ni kweli kuna samaki mtu (Nguva) Baharini.

Kwanini Bwana alirejea Tiro na Sidoni kwa mfano wa Sodoma?

Je! Mwanamke anapaswa afunikwe kichwa anapokuwa ibadani?

https://wingulamashahidi.org/2019/08/30/maswali-na-majibu-2/

Nini maana ya ‘Usimwekee mtu mikono kwa haraka’?

Rudi Nyumbani:

Print this post

KUOTA UNACHEZA MPIRA.

Kuota unacheza mpira kuna maanisha nini kiroho?


Ndoto za namna hii kuwa zinakuja kutoka katika makundi mawili,

Kundi la kwanza ni kutokana na shughuli za kila siku.

Mhubiri 5:3 “Kwa maana ndoto huja kwa sababu ya shughuli nyingi;..”.

Kwamfano kuota unacheza mpira, asilimia kubwa ya ndoto hii huotwa na wanaume. Na hiyo ni kutokana na kwamba aidha mtu huyo kwa sasa anajishughulisha na mchezo wa mipira, au huko yumba alishawahi kucheza mpira, aisha shuleni au mitaani n.k..

Sasa ukiota ndoto ya namna hii mara kwa mara, basi huna haja ya kuwa na wasiwasi kwani ni ndoto tu, ambayo imekuja kutoka na shughuli za kila siku, Na hiyo inakuwa haina maana yoyote rohoni.

Kundi la Pili, ni kutokana na Mungu.

Lakini pia, ndoto kama hiyo inaweza kuja kwa namna ya kipekee sana, yaani kwa uzito usiokuwa wa kawaida, pengine ulikuwa unashindana sana kucheza, timu yako imezidiwa sana, au mmewazidi wale wengine sana, au wewe unacheza vizuri au vibaya kuliko wengine.. Kiasi kwamba ulipoamka  imekukaa sana akilini tofauti na ndoto ambazo ndoto ambazo unaotaga kila siku.

Basi ukiona hivyo lipo jambo Mungu anakukumbusha.

Kumbuka hapa dunia tupo katika mashindano, Na kila mmoja ni kama mchezaji, Na Lengo la mchezaji sikuzote ni kushinda tu, na sio kushindwa, ili mwisho wa siku akapokee medali ya dhahabu au kombe.

Biblia inasema..

1Wakoritho 9.24 “Je! Hamjui, ya kuwa wale washindanao kwa kupiga mbio, hupiga mbio wote, lakini apokeaye tuzo ni mmoja? Pigeni mbio namna hiyo, ili mpate.

25 Na kila ashindanaye katika michezo hujizuia katika yote; basi hao hufanya hivyo kusudi wapokee taji iharibikayo; bali sisi tupokee taji isiyoharibika.

26 Hata mimi napiga mbio vivyo hivyo, si kama asitaye; napigana ngumi vivyo hivyo, si kama apigaye hewa;

27 bali nautesa mwili wangu na kuutumikisha; isiwe, nikiisha kuwahubiri wengine, mwenyewe niwe mtu wa kukataliwa”.

Unaona, wewe kwa upande wako ulijiona unashiriki katika mchezo aina ya mpira, wengine wanaota wakikimbia riadha, wengine wakiogelea n.k.

Hivyo kuota unacheza mpira ni Mungu anakukumbusha kuwa upo kwenye mashindano ndugu. Sijui kwa upande wako maisha yako yapoje, kwasababu watu wengine Mungu anazungumza nao hata mara mbili au mara tatu, ili tu waelewe sauti ya Mungu..Lakini hawasikii. Soma hapa..

Ayubu 33:14 “Kwa kuwa Mungu hunena mara moja, Naam, hata mara ya pili, ajapokuwa mtu hajali.

15 Katika ndoto, katika maono ya usiku, Usingizi mzito uwajiliapo watu, Katika usingizi kitandani;

16 Ndipo huyafunua masikio ya watu, Na kuyatia muhuri mafundisho yao”,

Hivyo kama wewe ni mmojawapo na bado upo nje ya Kristo, ni heri ukajitathamini vizuri tena. Kwasababu Yesu anao mpango mkubwa na wewe katika maisha yako haijalishi wewe ni muislamu na nani. Unachopaswa kufanya ni kumgeukia tu yeye uanze kushindana mashindano ambayo alikukusudia wewe ushindane ya kwenda mbinguni.. Kwasababu lipo taji bora alilokuandalia.

Si bahati mbaya ukutane na ujumbe huu. Hivyo usipuuzie, Mungu anakupenda, na anataka kukuokoa.

Ubarikiwe.

Fuatilia vichwa vingine vya masomo vilivyoainishwa chini ikiwa utahitaji kumjua Kristo zaidi.

Group la whatsapp Kwa mgawanyo bora wa masomo download App hapa>> App wingu la mashahidi

Mada Nyinginezo:

Je ushabiki wa mpira ni dhambi?

USIYADHARAU MARUDIA YA BWANA.

KUOTA UPO UCHI.

KUOTA NYOKA.

FAHAMU TAFSIRI ZA NDOTO MBALIMBALI.

Rudi Nyumbani:

Print this post