Nakusalimu katika jina kuu la mwokozi wetu Yesu Kristo. Karibu tujifunze maneno ya uzima..
Kwanini mara nyingine tunakuwa ni wepesi kufanya dhambi, ni wepesi kuwasengenya majirani zetu, ni wepesi kwenda kuzini, licha ya kwamba tunasema tumeokoka, au tupo karibu na Mungu, lakini bado ni wepesi kutazama picha chafu mitandaoni na kufanya masturbation….
Ni kwasababu tunamdhania Mungu yeye ni kama sisi, kwamba anaelewa tu! Ni madhaifu ya kawaida ya mwili..Na kibaya Zaidi pale tunapoona Mungu hachukui hatua yoyote ya adhabu katika ouvu tulioufanya, pengine pale tulipoenda kutazama picha chafu mitandaoni halafu Mungu akakaa kimya, halafu kesho yake tena tukarudia jambo hilo hilo na bado akawa yupo vilevile, hakuna lolote baya amelifanya katika Maisha yetu, kesho kutwa tena tukaenda kuzini, jambo likawa vilevile, kanisani tunahudhuria, kwaya tunaimba, maombi tunafanya, wala hakuna shida yoyote, wiki ijayo tukaanza kuwazungumizia vibaya majirani zetu, tulikuwa hatuli rushwa wala hututoi rushwa lakini tulipoanza kula rushwa na tukaona hakuna jambo lolote baya lililotukuta basi ndio ikawa desturi yetu kufanya hivyo, licha ya kuwa unasema ni mkristo.
Imekuwa hivyo hivyo miaka nenda miaka rudi, unawaza moyoni na kusema “hata Mungu anaelewa mambo haya”, ndio maana haniadhibu kwa lolote, Unadhani yeye ni kama wewe, Unadhani anavyowaza juu ya maovu ni kama wewe unavyowaza, unamchukulia kama mtu mwenzako asiyeweza kujali mambo madogo madogo kama hayo, unadhani kuwa hawezi kukuacha, wala kukuadhibu kwa vitu kama hivyo..
Lakini leo sikiliza Neno la Mungu linavyosema..
Zaburi 50:16 “Bali mtu asiye haki, Mungu amwambia, Una nini wewe kuitangaza sheria yangu, Na kuliweka agano langu kinywani mwako?
17 Maana wewe umechukia maonyo, Na kuyatupa maneno yangu nyuma yako.
18 Ulipomwona mwivi ulikuwa radhi naye, Ukashirikiana na wazinzi.
19 Umekiachia kinywa chako kinene mabaya, Na ulimi wako watunga hila.
20 Umekaa na kumsengenya ndugu yako, Na mwana wa mama yako umemsingizia.
21 NDIVYO ULIVYOFANYA, NAMI NIKANYAMAZA; UKADHANI YA KUWA MIMI NI KAMA WEWE. Walakini nitakukemea; Nitayapanga hayo mbele ya macho yako.
22 Yafahamuni hayo, Ninyi mnaomsahau Mungu, Nisije nikawararueni, Asipatikane mwenye kuwaponya”
Angalia tena ule mstari wa 21 anasema.. “Ndivyo ulivyofanya, nami nikanyamaza; ukadhani ya kuwa mimi ni kama wewe”…Unaona, Mungu anapokaa kimya kutokana na dhambi zako unazozifanya kwa siri, usidhani yeye anakufurahia tu!.. Unasema umeokoka na huku unayo mambo yako ya siri ambayo unajua kabisa ni machukizo kwa Mungu, lakini Mungu hakusemeshi kwa lolote na wewe umestarehe tu, unadhani Mungu ni kama wewe, ataendelea na wewe hivyo siku zote..La! Anasema atakurarua na asipatikane mtu wa kukuponya..
Hasemi atakupiga tu, halafu basi au atakuadhibu, hapana anasema atakurarua..Na unajua anayerarua ni mnyama mkali kama vile simba, maana yake ni kuwa atakuharibu vibaya sana, kiasi cha kwamba hutaweza kusimama tena baada ya hapo, hata uombeweje, au uhubiriweje, hutaweza tena kusimama…Ndio maana anasema hapo “asipatikane mtu wa kukuponya”
Na ujumbe huo Mungu anausema kwa wale wote wanaomsahau..Inamaanisha kuwa hapo mwanzo walishawahi kuwa wake, lakini wakamzoelea wakamwona kama yeye ni kama wao, wakawa hawaogopi tena kufanya dhambi mbele zake..
Ndugu ikiwa wewe ni mmojawapo, Basi wakati wako wa kutubu kwa kumaanisha ndio huu, pengine umebakisha kipindi kifupi sana kukumbana na makucha hayo ya Mungu (Usitafute kuujua upande wa pili wa ghadhabu ya Mungu, kwasababu inatisha sana).. Ikiwa unafanya dhambi kisirisiri za kujirudia rudia ambazo hazimpendezi Mungu, na umekuwa ukizifanya kwa muda mrefu sasa na Mungu amekaa kimya tu, ni heri usiendelee kuzifanya, kwasababu kwa kukaa kwake kimya hivyo usidhani yeye ni kama wewe..
Hivyo chukua hatua sasa ya kuuimarisha wokovu wako, na Mungu atakusamehe na kuiahirisha ghadhabu yake kwako.
Kumbuka hizi ni nyakati za mwisho, hakuna haja ya kuthibitishiwa tena kuwa tunaishi katika majira ya kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo, hali halisi yenyewe inaonekana kwa mambo yanayoendelea sasa hivi duniani, hivyo huu si wakati wa kuweka mguu mmoja kwa Kristo na mwingine nje, huu ni wakati wa kuzama moja kwa moja kwa Bwana, kwasababu UNYAKUO sasa ni wakati wowote.
2Petro 1:10 “Kwa hiyo ndugu, jitahidini zaidi kufanya imara kuitwa kwenu na uteule wenu; maana mkitenda hayo hamtajikwaa kamwe”.
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
JINSI NEEMA YA MUNGU ILIVYOKUWA KUBWA KWA MKE WA LUTU.
MUNGU WETU, JINSI LILIVYO TUKUFU JINA LAKO DUNIANI MWOTE!
KWANINI UNAPASWA UJIWEKE TAYARI SASA, KABLA YA ULE WAKATI KUFIKA?.
KWA VILE ALIVYOKUWA MTU WA HAKI.
KRISIMASI (CHRISTMAS) NI NINI? JE IPO KATIKA BIBLIA?
Mitume wote waliopita walikuwa ni watu weupe hata manabii wote waliopita hadi Ma-papa ni ngozi nyeupe. ni kweli ngozi nyeusi ililaaniwa ?
Kipindi kifupi kabla ya ghadhabu ya Mungu kumwagwa juu ya dunia, biblia imetabiri kuzuka kwa mambo ya ajabu sana na ya kutisha ulimwengu…na mambo hayo yapo mengi ikiwemo kuzuka kwa manabii wa uongo na makristo wa uongo, lakini pamoja na hayo yapo mengine matatu ya muhimu, ambayo ni …1) VITA 2) TAUNI na 3) NJAA.
Luka 21:10 “Kisha aliwaambia, Taifa litaondoka kupigana na taifa, na ufalme kupigana na ufalme; 11 kutakuwa na MATETEMEKO MAKUBWA YA NCHI; NA NJAA NA TAUNI mahali mahali; na mambo ya kutisha na ishara kuu kutoka mbinguni”.
Kama tujuavyo mgonjwa kabla hajaanza kuumwa anakuwa anaanza kuonyesha dalili kwanza, labda ataanza kusikia kichefuchefu na baadaye akawa sawa, muda kidogo atasikia kichwa kinamuuma lakini si sana..na baadaye tena homa lakini si sana..kiasi kwamba anaweza akazivumilia dalili zile na kuendelea na shughuli zake kipindi cha mwanzoni..na wakati mwingine hata akajisikia nafuu kabisa kana kwamba haumwi tena….
Lakini siku ikifika yenyewe ambapo ugonjwa ule utanyanyuka..huo ndio wakati ambao kila siku kwake itakuwa ni afadhali na jana kuliko leo…zile dalili alizokuwa anazisikia mwanzo, kama kichwa kuumwa kidogo, homa kidogo, sasa vinazidi na kujizidisha na kuwa vikali mara nyingi zaidi..hapo atasikia kichwa kikiumwa hata mara kumi ya kile alichokuwa anakisikia hapo mwanzo..Homa inajizidisha mara nyingi kuliko mwanzo na mara nyingine anajikuta anaishia tu kalala kitandani. Mtu anapofikia hali ya kuumwa kiwango hiki huwa anatamani hata afe atokane na mateso hayo.
Sasa mambo hayo yanafananishwa na siku za maangamizi ya dunia zitakavyokuwa …Wengi wetu hatujui nini maana ya dalili ya siku za mwisho…Dalili maana yake ni mwanzo wa kitu…Hivyo biblia inavyosema kuwa dalili za siku za mwisho ni hizi au zile, inamaanisha kuwa mwisho wa siku mambo yatakuwa ni mabaya kuliko hata mwanzo.
Sasa Bwana Yesu alisema dalili mojawapo ya siku za mwisho ni kuwepo kwa matetemeko makubwa ya nchi(Luka 21:11)…maana yake ni kwamba siku yenyewe ya mwisho wa dunia ikifika kutakuwepo na tetemeko kubwa lisiloelezeka mara nyingi zaidi ya yale ya dalili..
Kadhalika Bwana Yesu alivyosema kwamba vita ni dalili mojawapo ya siku za mwisho, maana yake ni kwamba Siku yenyewe ya mwisho wa dunia ikifika kutakuwa na vita kubwa na kali na ya ajabu ambayo haijawahi kutokea, ambayo madhara yake hayajawahi kufananishwa na vita yoyote huko nyuma..na vita hiyo itakuwa si nyingine zaidi ya vita vya Har -magedoni.Kama hizi vita zilizopo sasa tumezoea kusikia watu elfu kadhaa wamekufa..vita hiyo ya mwisho ya Harmagedoni itamaliza mamilioni ya watu.
Pia alisema dalili nyingine ni NJAA, na njaa hiyo inasababishwa na kukosekana kwa mvua na kunyanyuka kwa wadudu wanaoharibu mazao kama nzige waliotokea wakati wa Farao, na waliopo sasa..Siku ya kuharibiwa dunia Itatokea Njaa ambayo haijawahi kuwa mfano wake…Baada ya watu kuifurahia chapa ya mnyama kwa kitambo..Mungu ataipiga dunia nzima kwa njaa..ambapo maji yote yatageuka kuwa damu na mifereji na mito..na mvua itaacha kunyesha(Ufunuo 16:4-6).
Kadhalika Bwana Yesu alisema dalili nyingine ya siku za mwisho ni KUZUKA KWA MAGONJWA MABAYA ambayo yanafanishwa na Tauni kibiblia(Luka 21:11)...magonjwa hayo yatakuwa hayana tiba na yanayoambukiza kwa kasi…Dalili za magonjwa hayo zimeanza kuonekana tangu mwanzo mwa karne ya 21, na mpaka kufikia sasa yameshaongezeka idadi..Kama ijulikanavyo kuna ugonjwa sasa unaoitwa Corona ulimwenguni.. Ugonjwa huu ni dalili tu (mwanzo wa utungu)..ambapo siku yenyewe ya mwisho ikifika ambayo inaweza kuwa hata leo..utazuka ugonjwa mpya ambao utakuwa ni mbaya kuliko huu uliopo sasa…utakuwa ni ugonjwa wa virusi mfano wa huu wa sasa…
Ugonjwa huu utashambulia ngozi na kusababisha majipu ya vidonda ambavyo vinaoza(Biblia inasema majipu yake yatakuwa ni mabovu, maana yake ni ya kuoza) na utakuwa unateseka kwa muda mrefu..Utakuwa ni tofauti na huu uliopo sasa ambao baada ya siku kadhaa mtu anaweza kupona…ugonjwa huo wa majipu utakuwa hauna tiba na wala hautakuwa unapona wenyewe, utampata kila mtu ambaye atakuwepo ulimwenguni wakati huo…
Ufunuo 16: 2 “Akaenda huyo wa kwanza, akakimimina kitasa chake juu ya nchi; pakawa na jipu baya, bovu, juu ya wale watu wenye chapa ya huyo mnyama, na wale wenye kuisujudia sanamu yake”.
Mambo haya sio hadithi bali ni mambo ambayo yatakuja kutokea dhahiri kabisa. Siku za ugonjwa huo jua litashushwa pia na kuwaunguza wanadamu wote wenye ugonjwa huo, duniani kutakuwa sio sehemu ya kuishi tena..kila mtu atakuwa kivyake akiugulia na kuteseka kivyake vyake kutakuwa hakuna hospitali itakayopokea wagonjwa kwasababu hata wauguzi wenyewe watakuwa na ugonjwa huo..(Hiyo itakuwa sio siku za dalili tena bali ya ugonjwa wenyewe, dalili ni wakati huu wa sasa).. Unyakuo upo karibu sana kutokea!..Kwasababu kabla ya siku hizo..watakatifu watanyakuliwa kwanza.
Ishara za magonjwa haya ni kutuonyesha kuwa Hukumu tayari imeshatamkwa juu ya ulimwengu..kama vile ambavyo ugonjwa unavyomwingia mtu..na hatua za kwanza ni dalili..na sasa tupo katika dalili ya ghadhabu ya Mungu. Hii hofu iliyopo sasa si hofu, hofu hasaa itakuja wakati huo wa mapigo hayo ya Mungu.
Ni nini kifanyike sasa? Katika hatua hii ya dalili?
Kinachopaswa kufanyika sasa ni kujiweka tayari tu…Tunajiwekaje tayari?..ni kwa kutubu, kujiosha mioyo yetu, kuacha dhambi na kuzidi kujitenga na ulimwengu kila siku… Kuacha kuziabudu sanamu na kuzisujudia , Kuacha ulevi, kuacha rushwa, kuacha wizi, kuacha matusi, kuacha kutazama picha za ngono, uasherati, kuacha kwenda ma disko, kuacha kuvaa nguo za kuonyesha maungo, na vimini na suruali kwa wanawake….mambo haya ndiyo yanayoisukuma ghadhabu ya Mungu imwagike haraka ulimwenguni na juu yako wewe..ni kama mgonjwa ambaye tayari kashaanza kuonyesha dalili, halafu bado hazingatii tiba..pasipo kujua kuwa ndio anazidi kujiharibu na kuuvuta ugonjwa zaidi..
Wakolosai 3: 5 “Basi, vifisheni viungo vyenu vilivyo katika nchi, uasherati, uchafu, tamaa mbaya, mawazo mabaya, na kutamani, ndiyo ibada ya sanamu; 6 kwa ajili ya mambo hayo huja ghadhabu ya Mungu”.
Umeona mstari wa 6, usemavyo?… “kwa ajili ya mambo hayo huja ghadhabu ya Mungu”..Soma tena..
Waefeso 5:5 “Maana neno hili mnalijua hakika, ya kwamba hakuna mwasherati wala mchafu wala mwenye tamaa, ndiye mwabudu sanamu, aliye na urithi katika ufalme wa Kristo na Mungu.
6 Mtu asiwadanganye kwa maneno yasiyo na maana; kwa kuwa kwa sababu ya hayo hasira ya Mungu huwajia wana wa uasi”.
Unaona tena? mstari wa mwisho huo wa 6.. “kwa kuwa kwa sababu ya hayo hasira ya Mungu huwajia wana wa uasi”
Hiyo pekee ndiyo njia ya kujikinga na kujiepusha na ghadhabu ya Mungu…
Utauliza kutokana na tatizo hili lililopo sasa…je ! ni sahihi kunawa mikono na kutosalimiana na mtu kwa kushikana mikono njiani?
Kama tunavyoambiwa ni wajibu wa kila mtu kusimama pindi wimbo wa Taifa unapoimbwa…na wakristo pia wanatii agizo hilo..Hivyo na agizo la kunawa mikono popote tufikapo, tuingiapo na tutokapo wakristo tunatii bila shuruti kwasababu hakutupunguzii chochote katika Imani yetu…Tukijua ya kwamba mioyo yetu tayari imeoshwa kwa sabuni ya kimbinguni (Damu ya Yesu)..Na tumaini letu halipo katika maji na sabuni za mwilini bali katika maji na damu ya Yesu Kristo. Hiyo ndiyo inayotutakasa na kutulinda na kutuepusha na ghadhabu ya Mungu. Hivyo hatuna hofu, na hatuogopi kwasababu tunamtegemea Bwana, wakati ulimwengu unaogopa magonjwa, na njaa na vita sasa…sisi tunaigopa dhambi tu!..
Zaburi 125:1 “Wamtumainio Bwana ni kama mlima Sayuni, Ambao hautatikisika, wakaa milele.
2 Kama milima inavyouzunguka Yerusalemu, Ndivyo Bwana anavyowazunguka watu wake, Tangu sasa na hata milele”.
Lakini kama tukinawa mikono na mwili mzima mahali popote tuingiapo na tutokapo na huku mioyoni mwetu bado kuna uasherati, bado kuna wivu, hasira, wizi, ufisadi, ibada za sanamu, rushwa, na ulevi hakuna chochote tunachoweza kuepuka…Maji na sabuni na mlo kamili kamwe haviwezi kutuepusha na ghadhabu ya Mungu…Havijawahi katika agano la kale na hata katika agano jipya.
Hivyo kwa hitimisho kama hujampa Yesu Kristo maisha yako, Hizi ni siku za mwisho..huhitaji kuhadithiwa na mtu tena..leo hii ile mipira uliyokuwa unajitumainisha nayo kuwa itakupatia faraja iko wapi? Kule kubet ulikokuwa unajitumainisha nako kuko wapi?…Zile visa na zile biashara zako ambazo ulikuwa unajitumainisha nazo unazifanya ulimwenguni kote ziko wapo leo?, elimu unayojitumainia iko wapi?, disko unayojitumainishia nayo iko wapi? Katika mataifa makubwa zimeshafungwa labda na kwako inaweza kuwa hivyo siku sio nyingi, wale waliokuwa wanakuambia kwamba dunia haitafikia mwisho wako wapi leo?..Uliwahi kufikiri kwamba ingetokea siku moja miji mikubwa mikubwa ingekosa watu barabarani?, mashule mengi ulimwenguni yangefungwa?,
umewahi kutafakari kwamba siku moja ingefika mamilioni ya watu hawataruhusiwa kwenda kazini wala makanisani?..Naam Hali inaweza kurudi kama kawaida na maisha yakarudi kama mwanzo na hata zaidi ya pale..lakini je! Umejifunza nini?…bado upo tu nje ya safina?
Huu ni mwanzo tu kwamba tutubu kwasababu siku yenyewe… ikifika hata hii Neema ya kutubu na ya kusikia mahubiri haitakuwepo?….Siku yenyewe ikifika itakuwa haiwezekani kabisa hata kwenda kanisani, licha ya kutafuta mtu wa kukuhubiria, hata kwa njia ya mitandao halitapatikana…wanaohusika na mitandao watakuwa matatizoni, vituo vya satellite vyote vitafungwa…Chapa ya mnyama itakuwa inafanya kazi na kipindi kifupi baada ya kuipokea chapa hiyo magonjwa hayo yataanza..
Yeremia 28:7 “Lakini lisikilize sasa neno hili nilisemalo, masikioni mwako, na masikioni mwa watu wote, 8 Manabii waliokuwako kabla ya zamani zangu, na zamani zako, walitabiri juu ya nchi nyingi, na juu ya falme kubwa, habari ya vita, na ya mabaya, na ya tauni”.
Kabla ya dunia kufikia maharibifu hayo..waliokuwa ndani ya Kristo watakuwa wamenyakuliwa je utakuwa miongoni mwao?..
Kama hujatubu..Na upo tayari kufanya hivyo leo hii, Basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie maisha yako yote kama ilivyokuwa hata kwetu sisi. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.
EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, . NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.
ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.
AMEN.
Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji Mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.
UFUNUO: Mlango wa 16.
NENO NI LILE LILE, LAKINI UJUMBE NI TOFAUTI.
MWISHO WA DUNIA UTAKUJAJE?
KWANINI UNAPASWA UJIWEKE TAYARI SASA, KABLA YA ULE WAKATI KUFIKA?.
Jambo mojawapo ambalo lilikuwa linamfanya Daudi asichoke kumsifu Mungu, ni vile alivyokuwa anajijengea mazoea ya kuutafakari ukuu wake kila mahali alipokuwepo.. Daudi alikuwa akizitazama mbingu sana, akiangalia jinsi nyota na mwezi vilivyowekwa angani na Mungu kwa namna ya ajabu na ya kushangaza..
Nakuambia kuna raha na changamko fulani la kipekee linaingia ndani yako, pale unapotenga muda wako mrefu kutafakari kazi za Mungu hususani vitu vya asili kama vile mbingu, na milima, na mabonde na mito na bahari….
Zaburi 8:1 “Wewe, MUNGU, Bwana wetu Jinsi lilivyo tukufu jina lako duniani mwote! Wewe umeuweka utukufu wako mbinguni; ….
3 Nikiziangalia mbingu zako, kazi ya vidole vyako, Mwezi na nyota ulizoziratibisha;”
Wakati mwingine tunajiuliza watu kama hao ambao hawakuwa na Darubini (Telescope) ya kuangalia magimba yaliyo mbali sana na dunia, lakini walimsifu Mungu kwa namna ile na kumfurahia, Je! Wangekuwepo katika wakati wetu huu, wangemsifu Mungu kwa jinsi gani?..Kwasababu ule wakati wao macho yao yaliishia kuona nyota tu za hapo angali, lakini sisi tunaishi katika kipindi cha teknolojia ya hali ya juu ndio tunaojua kuwa hata hizi nyota na hili jua, na huu mwezi, ni vitu vidogo sana ukilinganisha na matrilioni na magimba mengine Mungu aliyoyaumba huko angani.. kwa ufupi ni kwamba kila kitu unachokiona angani, ikiwemo na hizo nyota zote, ni sawa na chembe moja ya mchanga katika michanga yote iliyopo baharini..Sasa embu jiulize huyu ni Mungu wa namna gani, kaumba vitu vingapi tusivyovijua sisi kwa akili zetu?
Na sisi pia, ila sifa zetu ziwe na nguvu, tutoke nje tuutazame ukuu wa Mungu, tuutafakari sana, tutenge hata muda tuziangalie mbingu sana. Sio kila siku usiku na mchana tu tunakuwa bize tu na shughuli zetu, halafu jumapili ndio tunakwenda kumsifu Mungu kanisani..Ni lipi litakalotufanya tumsifu yeye kwa kumaanisha kabisa?..Wakati mwingine si tutakuwa tunafanya hivyo kinafki?…
Vile vile tutafakari jinsi alivyoviumba viumbe vyake mbali mbali, ili tujue kuwa haja bahatisha kutuumba na sisi jinsi tulivyo, Tutafakari kwanini amuumbe mnyama mmoja na shingo ndefu, lakini mwingine amnyime lakini wote wakawa wanaishi bila shida yoyote, kwanini mwingine ampe miguu mingi (kama jongoo) lakini mwingine asimpe kabisa miguu (mfano nyoka), lakini Yule asiye na miguu akawa na mbio, tena sana kuliko Yule mwenye miguu mingi…Kwanini mwingine amempa mbawa akawa anaruka na kupaa juu sana (Tai), na mwingine akampa mbawa kama hizo hizo lakini hawezi kuruka(kuku) akionyesha kuwa kupewa mbawa sio kigezo cha wewe kuruka,
Tujiulize kwanini mwingine amepewa meno lakini hawezi kula mifupa (ng’ombe) lakini mwingine hana meno na mwororo lakini chakula chake ni mifupa (konokono) kwanini mwingine hana mdomo unaofanana na binadama kama vile nyani, lakini mwingine mwenye mdomo wa ndege lakini hata haukaribiani na mtu, lakini anao uwezo wa kuiga lugha ya mwanadamu ukadhani ni mtu anazungumza kumbe ni ndege (kasuku)..Kuonyesha kuwa sio wepesi wa ulimi ndio unamfanya mtu azungumze, bali ni kujaliwa tu, bubu hana matatizo yoyote katika ulimi wake, lakini ni Mungu ndiye alimfanya awe vile. N.k n.k
Tukiyatafakari hayo na mengine mengi tutaona mambo ya Mungu jinsi yalivyo mengi..Na tutakuwa na amani na kumshukuru Mungu kwa jinsi alivyotuumba.. Vile vile hapo ndipo tutakapojua kuwa kumbe Mungu hategemei bidii zetu kutunyanyua au kutushusha, hategemei mpaka tupate elimu ndio atufikishe mahali Fulani, hatagemei mpaka tuwe na miguu miwili, au mikono miwili ndio atupigishe hatua nyingine…Bali ni kwa neema zake tu..
Hivyo ni jukumu letu sote kumsifu Mungu wetu, daima, kwa mambo yake ya ajabu, na uumbaji wake. Na huko ndipo tutakapomwona katika maisha yetu.
ZABURI 150
1 Haleluya. Msifuni Mungu katika patakatifu pake; Msifuni katika anga la uweza wake.
2 Msifuni kwa matendo yake makuu; Msifuni kwa kadiri ya wingi wa ukuu wake.
3 Msifuni kwa mvumo wa baragumu; Msifuni kwa kinanda na kinubi;
4 Msifuni kwa matari na kucheza; Msifuni kwa zeze na filimbi;
5 Msifuni kwa matoazi yaliayo; Msifuni kwa matoazi yavumayo sana.
6 Kila mwenye pumzi na amsifu Bwana. Haleluya.
Bwana akubariki.
Tafadhali “Share” na kwa wengine.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
Je! Ni halali kuoa/kuolewa na mtu ambaye tayari anao watoto?
1Wathesalonike 5:18 “Shukuruni kwa kila jambo; maana hayo ni mapenzi ya Mungu kwenu katika Kristo Yesu. 19 MSIMZIMISHE ROHO;”
Roho Mtakatifu anafananishwa na moto…Wakati ule wa Pentekoste Roho aliposhuka juu ya wale watu..alishuka mfano wa ndimi za moto…Hakushuka kama ndimi tu, bali kama ndimi za moto.. Maana yake ni kwamba Roho Mtakatifu anafananishwa na moto kwa tabia zake.
Sasa maana ya ndimi za moto ni nini?…Maana yake ni katika vinywa vyao zilitoka lugha zenye kuchoma kazi zote za Adui…Ndio maana muda mfupi tu baada ya tukio lile, wale mitume waliposimama na kuwashuhudia watu, walichomwa mioyo yao kwa namna isiyokuwa ya kawaida, na siku hiyo hiyo wakatubu watu elfu tatu na kubatizwa.
Matendo 2:1 “Hata ilipotimia siku ya Pentekoste walikuwako wote mahali pamoja.
2 Kukaja ghafula toka mbinguni uvumi kama uvumi wa upepo wa nguvu ukienda kasi, ukaijaza nyumba yote waliyokuwa wameketi.
3 Kukawatokea ndimi zilizogawanyikana, kama ndimi za moto uliowakalia kila mmoja wao.
4 Wote wakajazwa Roho Mtakatifu, wakaanza kusema kwa lugha nyingine, kama Roho alivyowajalia kutamka.
Na walikuwako Yerusalemu Wayahudi wakikaa, watu watauwa, watu wa kila taifa chini ya mbingu.
6 Basi sauti hii iliposikiwa makutano walikutanika, wakashikwa na fadhaa, kwa kuwa kila mmoja aliwasikia wakisema kwa lugha yake mwenyewe.
7 Wakashangaa wote, wakastaajabu wakiambiana, Tazama, hawa wote wasemao si Wagalilaya?
8 Imekuwaje basi sisi kusikia kila mtu lugha yetu tuliyozaliwa nayo?”
Tukienda mpaka mstari wa 37 unasema..
“37 Walipoyasikia haya WAKACHOMWA MIOYO YAO, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu?
38 Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.
39 Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu wamjie.
40 Akawashuhudia kwa maneno mengine mengi sana na kuwaonya, akisema, Jiokoeni na kizazi hiki chenye ukaidi.
41 Nao waliolipokea neno lake wakabatizwa; na siku ile wakaongezeka WATU WAPATA ELFU TATU.”.
Unaona? Hapo walichomwa mioyo yao?..sasa kilichowachoma ni nini…ni maneno ya moto yaliyokuwa yanatoka katika vinywa vya wale mitume walipokuwa wanawahubiria, siku zote walikuwa wanaishi na wakina Petro lakini maneno yao yalikuwa hayawachomi, lakini siku hii ya Pentekoste baada ya kupokea ndimi za moto..Maneno yao yakawa na uwezo wa kuchoma nia za Adui shetani ndani ya mioyo ya watu na kuwafanya waitii Injili. Hiyo yote ni kutokana na Roho waliyempokea na si kingine.
Hali kadhalika ndimi hizi hizi za moto walizozipokea Mitume ambazo kwa maneno yale machache tu siku ile waliweza kuwavuta watu wengi kwa Kristo takribani elfu 3…Ndio moto huo huo ambao wakiomba kitu kwa Mungu wa mbingu na nchi Mungu anawasikia na kuwajibu haraka zaidi kuliko wangekuwa hawana roho..Kwasababu ndimi hizo hizo zinaingia mpaka kwenye moyo wa Mungu na kwenda kumshawishi Mungu kwa kuugua kusikoweza kutamkwa na hivyo kupokea majibu kwa haraka sana..(Kumbuka neno ndimi ni wingi wa neno ULIMI, na ulimi ni neno linalowakilisha Lugha/usemi)..
Hivyo Usemi uliovuviwa Roho Mtakatifu unakuwa ni usemi wa moto. Kwahiyo mtu yeyote mwenye Roho Mtakatifu anapoomba iwe kwa kunena kwa lugha au isiwe kwa kunena kwa lugha, ule usemi wake mbele za Mungu unakuwa kama ni moto..unapenya mpaka kwenye vilindi vya moyo wa Mungu na kumshawishi kwa namna isiyoelezeka..hiyo ndiyo maana ya lile neno linalosema “Roho hutuombea kwa kuugua kusikoweza kutamkwa (Warumi 8:26)”.
Maana yake ni kwamba tunapoomba tukiwa na Roho Mtakatifu lugha zetu hizi mbele za Mungu haziendi kama za watu wengine wa kawaida bali zinakwenda zikiwa zimejazwa nguvu mara nyingi zaidi za kuushawishi moyo wa Mungu kuliko tunavyoweza kuelezea..Kama tu vile mtu mwenye Roho Mtakatifu anavyohubiri, hatatumia nguvu nyingi kumshawishi Yule mtu aokoke..bali yale maneno yake yatakwenda kama moto wa Roho kuugua ndani ya Yule mtu kwa namna isiyoweza kutamka, na hatimaye Yule mtu kukata shauri kuokoka.
Lakini sasa huyu Roho Mtakatifu anaweza kuzimishwa..na ndio biblia inatuambia hapo.. “Msimzimishe Roho”..Maana yake ule moto wa Roho ndani ya mtu unazima. Maneno yake yanakuwa hayana nguvu tena ya kumbadilisha mtu, wala yanakuwa hayana nguvu tena kuushawishi moyo wa Mungu kwa kuugua kusikoweza kutamkwa.
Mtu anapofikia hali kama hii ambapo “Roho kashazima ndani yake”…atalazimisha kutumia nguvu zake za kimwili na hekima yake ya kibinadamu na kila mbinu kumshawishi mtu amgeukie Mungu na atashindwa..
1Wakorintho 2:4 “Na neno langu na kuhubiri kwangu hakukuwa kwa maneno ya hekima yenye kushawishi akili za watu, bali kwa dalili za Roho na za nguvu,
5 ili imani yenu isiwe katika hekima ya wanadamu, bali katika nguvu za Mungu”.
Hali kadhalika maombi yake siku zote yatakuwa sio ya kuushawishi moyo wa Mungu..
Sasa ni mambo gani yanayomzimisha Roho ndani ya Mtu?
Jambo la kwanza ni kuudharau msalaba na kumfanyia Jeuri Roho Mtakatifu kwa kulidharau Neno lake…Neno lake linaposema hivi, na ndani ya moyo wako Roho Mtakatifu anakushuhudia kabisa kwamba jambo hili kulifanya sio sawa,..lakini wewe unalipuuzia, unadharau au unaonyesha jeuri mbele yake unafanya yale yasiyompendeza..hapo ule moto ambao pengine ulikuwa umeshaanza kuwaka ndani yako unazima ghafla.
Waebrania 10:29 “Mwaonaje? Haikumpasa adhabu iliyo kubwa zaidi mtu yule aliyemkanyaga Mwana wa Mungu, na kuihesabu damu ya agano aliyotakaswa kwayo kuwa ni kitu ovyo, NA KUMFANYIA JEURI ROHO WA NEEMA?”
2.Pili unapompinga Roho Mtakatifu kwa matendo yako..Kumpinga maana yake hukubaliani na kile anachokisema..Kwamfano biblia inasema.. “Waefeso 5.18 Tena msilewe kwa mvinyo, ambamo mna ufisadi; bali mjazwe Roho;”..Na wewe unasema maana yake sio hiyo bali ni nyingine, na huku unaendelea kujihalalishia ulevi..hapo unampinga Roho Mtakatifu..Au biblia inaposema..
“1Timotheo 2:9 Vivyo hivyo wanawake na wajipambe kwa mavazi ya kujisitiri, pamoja na adabu nzuri, na moyo wa kiasi; si kwa kusuka nywele, wala kwa dhahabu na lulu, wala kwa nguo za thamani;
10 bali kwa matendo mema, kama iwapasavyo wanawake wanaoukiri uchaji wa Mungu.”…
Na wewe unasema maana yake sio hiyo bali ni nyingine..hapo unapingana na Roho Mtakatifu na hivyo upo hatarini kumzimisha Roho.
Matendo 7:51 “Enyi wenye shingo gumu, msiotahiriwa mioyo wala masikio, siku zote mnampinga Roho Mtakatifu; kama baba zenu walivyofanya, na ninyi ni vivyo hivyo”.
Ili tufanikiwe katika kila kitu hapa duniani, tunamhitaji Roho Mtakatifu..Huyo ni kama moto, akizimika ndani yetu hakuna chochote tutakachoweza kufanya..hata maombi yetu yatakuwa ni bure mbele za Mungu..Na kama tayari kashazima ndani yetu suluhisho la kuurudisha ule moto wake ni kutubu na kuanza kumtii Roho Mtakatifu, na kutompinga wala kulidharau Neno lake.
Kama hujampa Yesu Kristo maisha yako basi mpe leo, ulitii Neno lake wala usiudharau msalaba kwani ni kwa faida yako, tubu leo kwa kumaanisha kuziacha dhambi zote ulizokuwa unazifanya, na nenda kabatizwe katika ubatizo sahihi wa kuzamishwa na kwa jina la YESU, na Roho Mtakatifu atashuka juu yako kama moto.
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
Je! hizi roho saba za Mungu ni zipi? na je zinatofautiana na Roho Mtakatifu?
MAFUNDISHO YA MASHETANI
KWANINI AWE PUNDA NA SI MNYAMA MWINGINE?
SIKUJA KULETA AMANI DUNIANI, BALI MAFARAKANO.
JINSI ROHO MTAKATIFU ANAVYOWAFUNULIA WATU MAANDIKO.
Urithi tulioahidiwa sisi wanadamu ni UZIMA WA MILELE. Na tumeahidiwa huo na Mungu wetu pale tu tunapomwamini Yesu Kristo. Mtu aliyemwamini YESU KRISTO, anakuwa ni mrithi wa Ahadi za Mungu zote pamoja na Maisha ya daima.…lakini wakati wa kupokea urithi bado unakuwa haujafika, ila katika roho ameshachaguliwa kuwa mrithi..kama tu vile mtoto anapoweza kuchaguliwa kuwa mrithi kabla hata ya wakati wa kurithishwa kufika..Ndivyo mtu aliyezaliwa mara ya pili anavyokuwa…Wakati utakapofika baada ya maisha haya kupita ndipo tutakapokabidhiwa vyote mikononi mwetu kama vile Bwana Yesu baada ya kumaliza kazi alivyokabidhiwa vyote na Baba…Mamlaka yote ya mbinguni na duniani alikabidhiwa.
Lakini habari ni kwamba urithi huu mtu anaweza kununua na kadhalika unaweza kuuuza..
Biblia inasema..
Marko 10:17 “Hata alipokuwa akitoka kwenda njiani, mtu mmoja akaja mbio, akampigia magoti, akamwuliza, Mwalimu mwema, nifanye nini nipate kuurithi uzima wa milele?
18 Yesu akamwambia, Kwa nini kuniita mwema? Hakuna aliye mwema ila mmoja, ndiye Mungu.
19 Wazijua amri, Usiue, Usizini, Usiibe, Usishuhudie uongo, Usidanganye, Waheshimu baba yako na mama yako.
20 Akamwambia, Mwalimu, haya yote nimeyashika tangu utoto wangu.
21 Yesu akamkazia macho, akampenda, akamwambia, Umepungukiwa na neno moja. Enenda, ukauze ulivyo navyo vyote, uwape maskini, nawe utakuwa na hazina mbinguni; kisha njoo unifuate”.
Unaona hapo, ili uupate uzima wa milele hauna budi uuze baadhi ya mambo/vitu ulivyonavyo, na maana ya kuuza ni KUUTOA MOYO WAKO katika vitu ambavyo ulikuwa unaona vina maana katika maisha yako..Unatoa moyo wako kwenye fedha, unatoa moyo wako kwenye umaarufu, kwa kumaanisha kabisa sio kwa unafki, unatoa matumaini yako na moyo wako kwenye elimu yako, unatoa moyo wako kwenye anasa unazozifanya na dhambi na mambo yote ya kidunia, unakuwa kama ndio leo umeanza kuishi. Kiasi kwamba hakuna chochote cha nje tena kinachoweza kukusisimua au kilicho na nafasi kubwa katika moyo wako zaidi ya Yesu.
Kama Mtume Paulo alivyofanya…
Wafilipi 3:7 “Lakini mambo yale yaliyokuwa faida kwangu, naliyahesabu kuwa hasara kwa ajili ya Kristo.
8 Naam, zaidi ya hayo, nayahesabu mambo yote kuwa hasara kwa ajili ya uzuri usio na kiasi wa kumjua Kristo Yesu, Bwana wangu; ambaye kwa ajili yake nimepata hasara ya mambo yote nikiyahesabu kuwa kama mavi ili nipate Kristo”
Ukiingia gharama za namna hiyo za kuacha kila kitu kwaajili ya Kristo, hapo ni sawa umeuza kila kitu na kwenda kununua kitu cha thamani..Hivyo ufalme wa mbinguni una gharama, tena sio ndogo..kubwa sana..
Vivyo hivyo ufalme wa mbinguni UNAWEZA KUUZWA…Pamoja na kuwa unanunulika kwa gharama kubwa lakini pia unaweza kuuzwa..na unaweza kuuzwa hata kwa gharama ndogo sana….Hapa ni pale mtu aliyekuwa amepewa neema ya kumjua Kristo anapogeuka na kuidharau Neema ile na kuamua kuiacha na kurudia ulimwengu. Huyo nafasi yake inachukuliwa na mwingine, kama Yuda alivyouza nafasi yake kwa tabia yake ya WIZI, na kusababisha nafasi yake kupewa mwingine alyeitwa Mathiya.
Kadhalika Esau naye alivyouza nafasi yake ya urithi kwa chakula cha siku moja na kupewa Yakobo ndugu yake.
Waebrania 12:16 “Asiwepo mwasherati wala asiyemcha Mungu, kama Esau, aliyeuuza urithi wake wa mzaliwa wa kwanza kwa ajili ya chakula kimoja.
17 Maana mwajua ya kuwa hata alipotaka baadaye kuirithi baraka, alikataliwa (maana hakuona nafasi ya kutubu), IJAPOKUWA ALIITAFUTA SANA KWA MACHOZI”
Kama tunavyosoma hapo juu..Kuna wakati utafika kwa wale walioidharau Neema waliyopewa , wakati huo utakuwa ni wa majuto, na kilio na uchungu mwingi, watu watatamani kwa machozi warudishwe angalau dakika tano nyuma warekebishe makosa yao, lakini watakosa hiyo nafasi…watakapoona uasherati waliokuwa wanaufanya umewaponza wameikosa mbingu, ulevi waliokuwa wanajifurahisha nao kwa kitambo umewaponza, rushwa walizokuwa wanakula ziliwapofusha macho n.k..Wakati huo utakuwa ni wakati wa majonzi makubwa na majuto kama ya Yuda na Esau….Yuda baadaye alipokuja kujua makosa yake alilia mpaka kufikia kujinyonga kuona Maisha hayana maana tena…na Esau naye aliitafuta ile nafasi yake kwa machozi lakini hakuipata tena.
Bwana atusaidie tusiuze urithi wetu kwa vitu vichache vya dunia vinavyopita…badala yake tuutafute na kuununua kwa gharama zote. Ili siku ile tutakapoyaona yale ambayo jicho halijawahi kuona wala sikio kusikia furaha yetu iwe timilifu.
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
LIVUNJENI HEKALU HILI, NAMI KATIKA SIKU TATU NITALISIMAMISHA.
Sabato halisi ni lini, Je! ni Jumapili au Jumamosi?, Ni siku gani itupasayo kuabudu?
Kuota unaanguka chini maana yake ni nini?
Ndoto hii huwa inachukua maumbile tofautitofauti, wengine wanaota wanaanguka kutoka kwenye ghorofa refu sana, wengine kutoka kwenye mti mrefu, wengine kwenye shimo lisilokuwa na mwisho, wengine wanaota wanaanguka kutoka angani. Wengine wanaangukia kwenye maji n.k.
Maadamu kiini cha ndoto ni Kuanguka kutoka sehemu fulani, basi ujue ndoto hiyo ni tahadhari kubwa kwako kutoka kwa Mungu, kwani Biblia inasema..
Ayubu 33:14 “Kwa kuwa Mungu hunena mara moja, Naam, hata mara ya pili, ajapokuwa mtu hajali.
15 Katika ndoto, katika maono ya usiku, Usingizi mzito uwajiliapo watu, Katika usingizi kitandani;
16 Ndipo huyafunua masikio ya watu, Na kuyatia muhuri mafundisho yao,
17 Ili amwondoe mtu katika makusudio yake, Na kumfichia mtu kiburi;
18 YEYE HUIZUIA NAFSI YAKE ISIENDE SHIMONI, Na uhai wake usiangamie kwa upanga.
19 Yeye hutiwa adabu kwa maumivu kitandani mwake, Na kwa mashindano yaendeleayo daima mifupani mwake”;
Unaona huo mstari wa 15 unasema Mungu kumbe anaweza kuzungumza na mtu mara moja, katika ndoto na asipojali atazungumza naye hata mara mbili..ili tu amzuie nafsi yake isiende shimoni. Hivyo fahamu kuwa ndoto hiyo ni Mungu anazungumza na wewe kukuonya.
Ni vizuri kujua katika biblia inapozungumza kuanguka inamlenga ibilisi mwenyewe kwasababu yeye peke yake ndio anayetajwa akianguka kutoka mbinguni..Bwana Yesu alisema..
“…Nilimwona Shetani, akianguka kutoka mbinguni kama umeme(Luka 10:18)..
Sasa inaposema alimwona shetani akianguka inamaanisha kuwa hapo mwanzo alikuwa sehemu sahihi lakini kuna wakati ulifika alifanya mambo fulani yasiyofaa ndio yakamfanya atoke katika ile sehemu yake na aanguke chini kwa kasi sana kama umeme.. na hicho si kingine Zaidi ya dhambi ya uasi..
Hivyo tendo la kuanguka ni tendo linalofunua uasi.. Shetani alipoasi ndipo alipoanguka chini, Vivyo hivyo na mtu yeyote leo hii anapomuasi Mungu, ni ishara kuwa anaanguka kutoka katika uwepo wa Mungu na mwisho wake unaenda kuwa mbaya kama ulivyokuwa kwa shetani.
Kwahiyo ikiwa unaota unaanguka chini, tena mahali ambapo hufiki, basi ujue hiyo ni tahadhari kwako, kuwa unaanguka kutoka katika neema ya Mungu, mrudie Mungu wako kabla mlango wa neema haujafungwa.. Yaangalie Maisha yako, na matendo yako, unaona kabisa hayaendani na njia ya wokovu..unaona kabisa hata Kristo akirudi leo hii utaachwa kutokana na njia zako na mienendo yako.
Kwa kuwa Mungu anakupenda na anaona mwisho wako utakavyokuwa kama wa shetani, ndio maana anakuonyesha ndoto kama hiyo, anachotaka kwako ni utubu dhambi zako, umgeukie yeye. Ukitubu leo kwa kumaanisha atakuokoa, na kukusafisha kabisa..Anachohitaji kwako ni moyo wa kumaanisha, kabisa, Hivyo kama kweli umemaanisha kufanya hivyo leo basi ujue uamuzi unaoufanya ni mzuri..Usijiangalie wewe ni muislamu, au mkristo ikiwa Kristo hajaumbika ndani ya Maisha yako, haijalishi wewe ni nani, umepotea tu na hata ukifa leo huwezi kwenda mbinguni..
Hivyo kama unapenda Yesu leo awe mwokozi wako, na kiongozi wa Maisha yako basi
Basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie maisha yako yote kama ilivyokuwa hata kwetu sisi. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Biblia inasema saa ya wokovu ni sasa, hivyo usingojee Kesho, haitakuwa yako..
Sasa ukishajitenga sehemu yako mwenye, piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.
EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.
ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.
AMEN.
Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo,
Sasa Mungu akishaona umegeuka kabisa kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.
Ubarikiwe sana
Unaweza pia kujiunga na kundi letu la mafundisho Whatsapp, au kuwasiliana nasi kwa link hii
Kwa mgawanyo bora wa masomo download App hapa>> App wingu la mashahidi
Mada Nyinginezo:
NIFANYE NINI ILI NILITIMIZE KUSUDI LA MUNGU.
NINI TUNAJIFUNZA KWA MWANA MPOTEVU NA NDUGUYE?
CHAGUA NI JIWE LIPI LITAKALO KUFAA KWA UJENZI.
DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.
MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.
Jini Mahaba yupo kibiblia?, Mtu mwenye jini mahaba anakuwaje?
Moja ya elimu inayowachanganya wengi na inayopotoshwa ni Elimu juu ya mapepo..
Mapepo kwa lugha nyingine wanaiwa majini…Ni kitu kimoja kinachojulikana kwa majina mawili tofauti, ni kama MWANADAMU na MTU. Hayo ni majina mawili tofauti lakini yanaelezea kitu kimoja.
Sasa mapepo ni roho za malaika walioasi mbinguni, ambao walitupwa chini pamoja na kiongozi wao mkuu shetani. Baada ya kutupwa chini ndio yakaitwa mapepo.
Mapepo hayo yanaweza kumwingia mtu na kumfanya awe na tabia yoyote ile wanayotaka wao. Mapepo haya yanaweza kumwingia mtu na kumfanya awe mwizi, mengine yanaweza kumfanya mtu awe mlevi, mengine yanaweza kumfanya mtu awe mzinifu au mwenye tabia ya zinaa.
Sasa mapepo ambayo yanawafanya watu wabadilike tabia na kuwa wazinifu au kuhisi wanafanya mapenzi na watu wakati wa kulala ndio hayo WATU wanayoyaita MAJINI MAHABA. Lakini kiuhalisia mapepo hayo hayana jinsia yoyote kwasababu ni roho. Na haya yanapomwingia mtu yoyote ambaye hajaokoka.(yaani ambaye hajampokea Yesu Kristo kama Bwana na mwokozi wa maisha yake) yanamfanya anakuwa mtumwa wa dhambi hiyo ya zinaa katika ndoto au katika maisha yake ya kawaida..Kwa mtu wa kawaida huwa hayamtokei kwa wazi lakini kwa wale ambao wamekufa kabisa kiroho na wamejiuza kwa shetani huwa yanaweza kujidhihirisha kwa macho kabisa..
Lakini kumbuka shetani siku zote ni mwongo pamoja na mapepo yake yote, biblia inasema shetani anao uwezo wa kujigeuza na kuwa hata malaika wa Nuru (Kasome 2Wakoritho 11:14), hivyo sio ajabu kuweza kujigeuza na kuwa hata mwanamke mzuri au mwanamume mzuri wa kuvutia, lakini ndani yake ni pepo mbaya na mchafu. Watu wengi wanadanganyia na kufikiri kuna mapepo ya kike..Ndugu usidanganyike hakuna kitu kama hicho…hayo ni maroho tu hayana jinsi, shetani ni baba wa uongo siku zote.
Kwa asili roho hizi za mapepo huwa hazimtokei mtu kwa wazi kama tulivyotangulia kujifunza hapo juu, isipokuwa kwa mtu ambaye tayari amejiuza kwa shetani moja kwa moja, hususani kama mtu ni mshirikina, au mganga au mchawi kabisa, huyu anaweza kuziona kwa macho..Lakini kwa wengine ambao wapo nusunusu, vuguvugu..roho hizi zinawaendesha katika ndoto tu na katika tabia zao. Katika ndoto wanakuwa wanaota wanafanya zinaa na katika tabia wanakuwa wanatabia zilizokithiri za uasherati mpaka wengine kuwafanya kuwa mashoga au wasagaji, au walawiti au wafiraji.
Na zifuatazo ni njia mapepo haya yanayozitumia kuingia ndani ya watu.
Kujitazama kwenye kioo hakuna uhusiano wowote na kuingiwa na roho hizo..Isipokuwa mtu mwenye tabia ya kujipamba, na kujichubua, kusuka suka, kuchonga nyusi anakuwa na tabia ya kujiangalia kwenye kioo mara kwa mara..hivyo hiyo tabia ya kujipamba na kuchonga nyusi ndio mlango wa mapepo hayo kuingia lakini sio kujitazama kwenye kioo.
Biblia inasema katika..
Ufunuo 21:27 “Na ndani yake hakitaingia kamwe cho chote kilicho kinyonge, wala yeye afanyaye machukizo na uongo, bali wale walioandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo”.
Kilicho kinyonge kinachozungumziwa hapo ndio hicho chenye roho ya mapepo ndani yake..Kwasababu mtu mwenye roho ya mapepo atakuwa na tabia tu fulani chafu ambazo watu wenye tabia hizo biblia inasema hawataurithi uzima wa milele. Mtu mwenye pepo la zinaa/jini mahaba ni lazima atakuwa mzinifu na mbinguni hawataingia wazinifu..Mtu mwenye pepo la ulevi ni lazima atakuwa tu mlevi na mbinguni hawataingia walevi.
Ufunuo 21:8 “Bali waoga, na wasioamini, na wachukizao, na wauaji, na wazinzi, na wachawi, na hao waabuduo sanamu, na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili..”
Mbinguni wataingia tu watu wenye Roho Mtakatifu..ambao ni watakatifu.
Waebrania 12:14 “Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na huo utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao; “
Kwanza ni kwa kumpa Yesu Kristo maisha yako, unatubu kwa kudhamiria kabisa kuacha dhambi na kisha unajiepusha na milango kujitenga na milango hiyo sita hapo juu tuliyoiona ambayo ndio mlango ya kuingiwa na roho hizo chafu. Na roho hizo zitakuacha kabisa na utakuwa huru.
Bwana akubariki
Kwa mgawanyo bora wa masomo download App hapa>> App wingu la mashahidi
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Yakobo 5:7 “Kwa hiyo ndugu, vumilieni, hata kuja kwake Bwana. Tazama, mkulima hungoja mazao ya nchi yaliyo ya thamani, huvumilia kwa ajili yake hata yatakapopata mvua ya kwanza na ya mwisho.
8 Nanyi vumilieni, mthibitishe mioyo yenu, kwa maana kuja kwake Bwana kunakaribia”.
Kwanini mtume huyu alifananisha kumngojea Bwana na uvumilivu na wa mkulima anayengojea mazao ya nchi, mpaka atakapopata mvua ya kwanza na ya mwisho.?
Hii Mvua ya kwanza na mvua ya mwisho ni ipi?
Mvua ya kwanza kwa jina lingine ni mvua ya masika, na mvua ya mwisho ni mvua ya vuli..Israeli tangu zamani hadi sasa ni nchi ya jangwa, sio kama huku kwetu kwenye ukanda wa kitropiki, ardhi ina unyevunyevu wakati wowote, kiasi kwamba hata ukitaka kuchimba kisima popote unakutana maji chini..Jambo hilo huwezi kulikuta katika nchi za jangwa kama vile Israeli..
Hivyo wakulima walikuwa wanategemea sana misimu ya mvua ili kulima na kupanda, wakati mwingine wowote ilikuwa haiwezakani kutokana na kwamba ardhi kuwa kame na ngumu.
Hivyo wakulima ilikuwa inawapasa wangojee wakati wa mvua tu, ndipo wafanye kazi za ukulima, Kwasababu hata mito haikuwepo, na hata kama ipo basi haijitoshelezi yote kwa kilimo cha umwagiliaji..Na hiyo ilikuwa inawafanya wasubirie tu wakati wa mvua, na utakapofika huwa basi wanafanya kazi kama vichaa kwa uvumilivu wote na kwa subira yote kwasababu wanajua upo wakati ambao hawataweza kufanya kazi tena.. Sasa kulingana na Jeografia ya Israeli, mvua ya masika kwao ilikuwa inaanza mwezi wa 10-11, na vuli mwezi 3-4, tofauti na huku kwetu ambapo ni kinyume chake.
Sasa masika ilikuwa ikishaanza tu wakulima wote wanatoka wanaingia mashambani na kuanza kuandaa mashamba na kupanda mbegu zao, na kuzipalilia…Mpaka itakapoisha, Lakini baadaye tena mvua nyingine ndogo ndogo zilikuwa zinaendelea si kali kama zile za Masika ndio hizo za Vuli, ili kustawisha tu mazao, na kuifanya ardhi isipoteze unyevu wake, mpaka misimu yote ya mvua itakapoisha moja kwa moja
Sasa ndio hapa Mtume Yakobo anafanisha kumngojea kwetu Bwana kama mkulima aliye katika msimu wa kilimo chake anavyovumilia mpaka mazao yake yatakapopata mvua zote mbili yaani ya kwanza na ya mwisho… Na akishamaliza basi huvuna na kuyaweka ghalani, jasho lake, na taabu yake sasa inakuwa imekwisha..
HIVYO,MVUA YA KWANZA, NA YA MWISHO ROHONI INAFUNUA NINI?
Vivyo hivyo na sisi tunaomgonjea Bwana, Tulishanyeshewa mvua ya kwanza, siku ile ya Pentekoste takribani miaka 2000 iliyopita, Kazi ikaanza..sasa kuanzia huo wakati tumekuwa tukilima, na kupanda, na kupalilia shamba la Bwana..Lakini pia iliahidiwa mvua nyingine itakayokuja huko mbeleni ambayo itakayokamilisha taabu yetu ya ulimaji..
Ndugu kama hujui ni kuwa tayari tumeshaingia katika kipindi cha msimu wa mwisho wa mvua ambayo ndio ile mvua ya mwisho ya vuli (rohoni), Na mvua hii ilianza mwaka wa 1906, Huu ni wakati ambapo kwa mara nyingine tena Mungu aliijilia dunia kwa vipawa na karama za roho, na kazi zile zile zilikuwa zinatendeka wakati ule wa Pentekoste ya mitume miaka 2000 iliyopita, mambo ambayo hapo katikati yalikuwa hayafanyiki, wala hayaonekani.. Hivyo kuanzia wakati huo ndio, Karama zile zote za rohoni zilianza kurejeshwa katika kanisa tena upya, vilevile Mungu akanyanyua watumishi wake wengi waaminifu kulithibitisha hilo kuwa wakati huo umeanza watu hao ikiwemo (William Seymor, baadaye William marrion Branham, Billy Granham, Oral Roberts, TL Osborn na wengineo wengi)
Tangu huu wakati injili ilianza kuhubiriwa kwa nguvu na ujumbe ulikuwa ni huu…WAKATI WA MAVUNO UMEKARIBIA!! BWANA ANAKARIBIA KULICHUKUA KANISA LAKE..
Wote hawa walikuwa na ujumbe huo, wote walijua tupo katika wakati ule wa MVUA YA MWISHO, wa mvua ya vuli..Na mpaka sasa ndipo mvua hiyo inakaribia kufika ukingoni kabisa… kwenda kugota..Na ikishagota, basi hakutakuwa ni mvua nyingine tena milele..
Ndugu hii neema unayoiona, unapoona unahubiriwa injili kirahisi hivi, Neno la Mungu limezagaa kila mahali, lakini unalipuuzia usidhani ilikuwa hivyo kipindi cha karne ya 19 kushuka huko chini..Hii miujiza unayoina na karama za rohoni unazoziona usidhani zilikuwepo muda wowote wa kanisa… Wewe Mungu amekupa neema ya kuishi katika msimu huu wa mvua ya Vuli rohoni, ambayo ipo karibuni kuisha..Lakini unaichezea hii nafasi..Upo wakati utaitamani lakini mlango wa neema utakuwa umeshafungwa..
Kipindi si kirefu, kanisa litanyakuliwa, wala hakuna mtu atakayesema mimi sikuambiwa wala sikujua, wakati huo Bwana atakusanya mavuno yake na kuyaweka ghalani na magugu kuyatupa motoni..Wote tunafahamu, hali ilivyo sasa, magonjwa ya kutisha yanavyozidi kuzuka, tetesi za vita, matetemeko,manabii wa uongo, watu kupenda fedha, watu kupenda anasa kuliko kumpenda Mungu, ushoga kama ilivyokuwa katika siku za Lutu, n.k. yote hayo yaliandikwa na tukaambiwa hizo ndio zitakuwa dalili kuu zitakazotutambulisha kuwa Kristo yupo mlangoni kurudi..
Lakini sisi tuliompokea tumeambiwa, tuyaonapo hayo..Basi ndio tunyanyue vichwa vyetu juu, kwasababu ukombozi wetu umekaribia..
Mvua hii ya neema ipo ukingoni, mkaribishe Bwana moyoni mwako kabla haijakoma kabisa moyoni mwako..Sisi sio wa kuambiwa tena tuvumilie kwasababu sisi tupo tayari wakati wa mavuno, waliokuwa wanapaswa wavulie ni wale wa makanisa mengine lakini sio sisi wa kanisa la mwisho la LAODIKIA.
Shalom.
Tafadhali “Share” Ujumbe huu na kwa wengine. Pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email, au Whatsapp au inbox yako ya faceboook, basi utujuze inbox nasi tutafanya hivyo. Vilevile usiache kutembelea website yetu hii (www wingulamashahidi org) kwa mafunzo zaidi.
Bwana akubariki sana.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Sabato halisi ni lini, Je! ni Jumapili au Jumamosi?, Ni siku gani itupasayo kuabudu?
Karibu tujikumbushe machache juu ya ujio wa Bwana Yesu, jinsi utakavyokuwa.
Bwana Yesu alikuja mara ya kwanza miaka ile 2,000 iliyopita…Alizaliwa na Bikira Mariamu, akasulubiwa na wayahudi, akazikwa, akafufuka baada ya siku tatu, na akapaa juu mbinguni kwa Baba…Mpaka muda huu tunapozungumza yupo mbingu za mbingu, amepokea Enzi na mamlaka yote ya mbinguni na duniani(1Timotheo 6:16). Lakini huko amekwenda kutuandalia makao (yaani nafasi zetu).
Baada ya muda mfupi atarudi tena kutuchukua tuende naye kwake, ili alipo nasi pia tuwepo..(Yohana 14:3).
Sasa siku ya kuja kutuchukua itakapofika, siku hiyo ndiyo inayoitwa SIKU YA UNYAKUO, Hatashuka duniani, bali atabaki pale mawinguni na atatuita sisi juu tupae kumfuata kule aliko..Siku hiyo tutaisikia sauti ya parapanda na muda huo huo uweza wa ajabu utashuka juu yetu ambapo kufumba na kufumbua tutajikuta miili hii yetu ya udhaifu imebadilika na kuwa kama wa kwake Bwana wetu Yesu. Na tutapaa juu, tutaicha hii ardhi kwa mara ya kwanza na kwenda juu sana…
Watu wa ulimwengu waliomkataa hawatamwona atakapotuita juu…watakaomwona ni wale tu ambao watanyakuliwa…kama vile alivyofufuka mara ya kwanza ni mitume wake tu na wafuasi wake wachache ndio waliomwona na wengine wote Mafarisayo na masadukayo hawakumwona, wala Pilato aliyemsulubisha hakujua chochote..ndivyo siku hiyo itakavyokuwa, wale wakristo ambao wameishikilia Imani mpaka siku hiyo itakapofika ndio watakaomwona Bwana mawinguni, na ndio watakaoisikia parapanda siku hiyo..
Sasa wafu ambao walitangulia kufa katika Kristo hawatasahaulika nao pia, kwasababu wao ndio watakaokuwa wa kwanza kuona tukio zima jinsi litakavyoendelea kwasababu watufufuliwa kwanza, kisha baadaye wataungana na sisi tulio hai na wote kwa pamoja tutavikwa miili ya utukufu. (kasome 1Wathesalonike 4:15)..
Na hali kadhalika wafu hao ambao watafufuka sio watu wote watawaona..hapana, watu wengine wakidunia watahisi tu labda kumetokea tetemeko la ardhi kama ilivyotokea siku ile Bwana aliyofufuka, lakini hawatamwona mtu yoyote….Watakaowaona wafu waliofufuliwa ni wale tu ambao wataungana nao kwenda kumlaki Bwana mawinguni.
Sasa Mbinguni, kutakuwa na karamu inaendelea kwa muda wa miaka saba, kutakuwa na raha isiyo na kifani..ambapo wakati huo duniani itakuwa inapitia kipindi cha dhiki kuu, na udhihirisho wa Mpinga-Kristo kwa watu waliosalia bila kwenda kwenye unyakuo, wachache watagundua Kristo amesharudi na wameachwa, wengi hawataamini na kuhisi ni uzushi tu umezuka..na hivyo watadanganyika kwa uongo wa mpinga-kristo na kuipokea chapa, na hatimaye kufa katika siku ya hasira ya Bwana ambapo Mungu mwenyewe ataiadhibu dunia kwa maovu yake kwa kupitia mapigo yale ya vitasa saba (Ufunuo 16).
Baada ya mambo hayo kuisha, Bwana kujilipizia kisasi kwa watenda maovu… Kristo pamoja na wale watakatifu wake ambao walikuwa wapo mbinguni katika karamu, watakuja duniani kwaajili ya ile vita ya Harmagedoni na kwa ajili ya kuanza utawala wa miaka 1,000..Wakati huo atakapokuja..wale watu wachache sana ambao wamebaki duniani ndio watakaomwona akija mawinguni kwa nguvu na utukufu mwingi.… atashuka na kulimalizia kundi dogo lililosalia katika vita vile vya Harmagedoni.. Hapo ndipo lile neno litakapotimia kwamba “kila jicho litamwona”…wataomboleza na kulia na kushikwa na hofu kuu, watakapomwona Kristo sio yule waliokuwa wanamwona kwenye picha au waliokuwa wanamsoma kwenye kitabu akija kwa upole na unyonge, wakati huu watamwona akija kwa utukufu mwingi kama umeme na ghadhabu nyingi.
Mathayo 24:30 “ndipo itakapoonekana ishara yake Mwana wa Adamu mbinguni; ndipo mataifa yote ya ulimwengu watakapoomboleza, nao watamwona Mwana wa Adamu akija juu ya mawingu ya mbinguni pamoja na nguvu na utukufu mwingi”.
Baada ya hapo utawala wa miaka 1,000 utaanza…na baada ya utawala huo itakuja mbingu mpya na nchi mpya, ambapo huko kutakuwa hakuna kufa, wala kuzeeka, wala kujaribiwa, wala kuteswa…Mambo ya kwanza yamekwisha kupita, atayafanya yote kuwa mapya..watakatifu wataishi na Bwana milele, katika utukufu usio na mwisho..Muda utasimama kutakuwa hakuna kuhesabu miaka, kwasababu maisha yatakuwa ni ya umilele.
Ufunuo 21:4 “Naye atafuta kila chozi katika macho yao, wala mauti haitakuwapo tena; wala maombolezo, wala kilio, wala maumivu hayatakuwapo tena; kwa kuwa mambo ya kwanza yamekwisha kupita.”
Bwana atausaidie tuwe miongoni mwa wale watakaokuwa wamealikwa katika karamu ya mwanakondoo mbinguni..
Ufunuo 19:9 “Naye akaniambia, Andika, Heri walioalikwa karamu ya arusi ya Mwana-Kondoo…”.
Wafu wafao sasa katika dhambi, hawatafufuliwa siku ya unyakuo itakapofika..watabaki kuzimu sehemu ya mateso..na siku moja watakuja kufufuliwa na kuhukumiwa kila mmoja kulingana na matendo yake(Ufunuo 20:13)..na baada ya kuhukumiwa watahamishwa kutoka kuzimu walipokuwepo na watakwenda kutupwa katika ziwa la moto lenye mateso makali Zaidi kuliko kule kuzimu walipokuwepo. Na huo ndio utakuwa mwisho wao.
Sio hilo tu, kwa wale waliokutwa wakiwa hai na wameachwa kwenye unyakuo na kuipokea chapa ya mpinga-kristo, hatapona hata mmoja wote baada ya kipindi kifupi watapitia mapigo makali ambayo yataletwa na Mungu mwenyewe kupitia vile vitasa 7..wakati wenzao waliokufa katika dhambi wakiwa jehanamu wanateseka wao watakuwa wanapitia mateso ya ghadhabu ya Mungu huku duniani, maji yote ya duniani yatageuzwa kuwa damu watu watasikia kiu mpaka kufikia hatua ya kuyanywa maji ya damu na kufa,(ili Mungu kuwalipizia kisasi kwa kuwa walimwaga damu ya watakatifu wake hivyo Mungu amewarushia hiyo damu wainywe), siku hizo jua litashushwa na kuwa kama moto juu ya wanadamu, mvua zitasimama kunyesha, na badala yake vitu vya ajabu vitaanza kuanguka kutoka mbinguni, na Bwana atawafanya watu wawe hawaelewani wao kwa wao hivyo kutakuwa na mapambano na vita vikuu,
Na katikati ya mateso hayo ya jua hilo kali, na kukosekana kwa maji na chakula duniani, Bwana ataleta magonjwa ya ajabu ya majipu ya ajabu juu ya wanadamu wote waliopokea chapa ya mnyama..kwahiyo mtu atakayeukosa unyakuo atakuwa hatna tofauti sana na mtu aliyekufa na kwenda kuzimu kutokana na mateso atakayoyapata akiwa hapa duniani.
Ufunuo 16:1 “Nikasikia sauti kuu kutoka hekaluni, ikiwaambia wale malaika saba, Enendeni, mkavimimine vile vitasa saba vya ghadhabu ya Mungu juu ya nchi.
2 Akaenda huyo wa kwanza, akakimimina kitasa chake juu ya nchi; pakawa na jipu baya, bovu, JUU YA WALE WATU WENYE CHAPA YA HUYO MNYAMA, NA WALE WENYE KUISUJUDIA SANAMU YAKE.
3 Na huyo wa pili akakimimina kitasa chake juu ya bahari, ikawa damu kama damu ya mfu, na vitu vyote vyenye roho ya uhai katika bahari vikafa.
Na baada ya kupitia mapigo hayo yote pamoja na kuuawa na mwanakondoo watakufa wote na kuungana na wenzao walioko jehanamu..wote kwa pamoja wakisubiria hukumu ya kutupwa katika ziwa la moto.
Hivyo unyakuo sio wa kukosa hata kidogo, Ni heri tukose hayo mengine yote lakini si unyakuo…Bwana atusaidie atukute tukiwa tunakesha katika roho kama alivyosema…
Marko 13:32 “Walakini habari ya siku ile na saa ile hakuna aijuaye, hata malaika walio mbinguni, wala Mwana, ila Baba.
33 Angalieni, kesheni, [ombeni], kwa kuwa hamjui wakati ule utakapokuwapo.
34 Mfano wake ni kama mtu mwenye kusafiri, ameiacha nyumba yake, amewapa watumwa wake amri, na kila mtu kazi yake, naye amemwamuru bawabu akeshe.
35 Kesheni basi, kwa maana hamjui ajapo bwana wa nyumba, kwamba ni jioni, au kwamba ni usiku wa manane, au awikapo jimbi, au asubuhi;
36 asije akawasili ghafula akawakuta mmelala.
37 Na hilo niwaambialo ninyi, nawaambia wote, Kesheni”
Ulevi ni usingizi, uasherati ni usingizi, wizi ni usingizi, usengenyaji ni usingizi, kiburi, hasira, matukano,rushwa, utapeli,uongo, uuaji, moyo unaowaza mabaya, na mambo yanayofanana na hayo.
Bwana atubariki.
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Kwanini Mungu aliikubali sadaka ya Yeftha ya kumtoa binti yake kafara?
Mwisho wa dunia utakuwaje?
Mwisho wa dunia maana yake ni hatua ambayo ustaarabu wa dunia utaifkia mwisho…Na mwisho wa dunia utahitimishwa na tukio moja kuu la vita vya HARMAGEDONI. Vita hivyo vitamaliza ustaarabu wote wa wanadamu…zitakuwepo vita ndogo ndogo zitakazotangulia, lakini vita hii kubwa ya mwisho ujulikanayo kama Harmagedon ndiyo itakayomaliza ustaarabu wote wa wanadamu.
Vita hii Biblia inaitaja kuwa ni vita kati ya Mungu mwenyezi na Wafalme wa Dunia..
Ufunuo 16:14 “Hizo ndizo roho za mashetani, zifanyazo ishara, zitokazo na kuwaendea wafalme wa ulimwengu wote kuwakusanya kwa vita ya siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi.
15 (Tazama, naja kama mwivi. Heri akeshaye, na kuyatunza mavazi yake, asiende uchi hata watu wakaione aibu yake.)
16 Wakawakusanya hata mahali paitwapo kwa Kiebrania, Har-Magedoni”
Vita hiyo Mwanakondoo yaani Yesu Kristo ataimaliza ndani ya muda mfupi sana kwa ushindi mnono..kwasababu yeye ni Bwana wa mabwana na Mfalme wa wafalme.
Siku hiyo pia kutakuwa na tetemeko kubwa la nchi ambalo mfano wake haujawahi kutokea na visiwa vitahama na ustaarabu wa dunia ndio utakuwa umefikia mwisho.
Ufunuo 6:12 “Nami nikaona, alipoifungua muhuri ya sita, palikuwa na tetemeko kuu la nchi; jua likawa jeusi kama gunia la singa, mwezi wote ukawa kama damu,
13 na nyota zikaanguka juu ya nchi kama vile mtini upukutishavyo mapooza yake, utikiswapo na upepo mwingi.
14 Mbingu zikaondolewa kama ukurasa ulivyokunjwa, na kila mlima na kisiwa kikahamishwa kutoka mahali pake.
15 Na wafalme wa dunia, na wakuu, na majemadari, na matajiri, na wenye nguvu, na kila mtumwa, na mwungwana, wakajificha katika pango na chini ya miamba ya milima,
16 wakiiambia milima na miamba, Tuangukieni, tusitirini, mbele za uso wake yeye aketiye juu ya kiti cha enzi, na hasira ya Mwana-Kondoo.
17 Kwa maana siku iliyo kuu, ya hasira yao, imekuja; naye ni nani awezaye kusimama?
Biblia inasema wasemapo amani! amani! ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafla
1Wathesalonike 5:3 “Wakati wasemapo, Kuna amani na salama, ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafula, kama vile utungu umjiavyo mwenye mimba, wala hakika hawataokolewa”
Kwahivyo tunaonywa tusidanganyike na amani hii ya dunia inayodanganya…Amani ya kweli ipo kwa Yesu tu!..nchi inaweza kutangaza kuwa tupo katika kipindi cha amani lakini kumbe ndio tupo mwishoni kabisa mwa nyakati.
Mkabidhi Yesu maisha yako kama hujafanya hivyo, kwasababu yeye ndiye njia ya kufika mbinguni na kuepukana na ghadhabu ya Mungu inayokaribia kumwangwa duniani kote katika siku hizi za mwisho, zinazoonekana zenye amani tele.
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Nini maana ya “Siku moja nyuani mwa Bwana ni bora kuliko miaka elfu”?