Category Archive Home

NINI TOFAUTI KATI YA KARAMA, UTENDAJI KAZI NA HUDUMA.

Nini tofauti kati ya karama ya rohoni, utendaji kazi na huduma?. Vitu hivi vitatu ni ni ni hasa?

Shalom.Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe…Karibu tuongeze maarifa katika kujifunza Neno la Mungu..

Leo kwa Neema za Bwana tutajifunza  kidogo juu ya karama za Rohoni…Zinaitwa karama za rohoni kwasababu sio za mwilini..zipo karama za mwilini na za rohoni pia…Kila mwanadamu kaumbiwa na karama fulani ya mwilini…iwe anaijua au haijui..Na vile vile kila mtu anayo karama ya rohoni…

Karama ya rohoni lengo lake kuu ni kutumika kwaajili ya faida ya ufalme wa Mbinguni…Lakini mtu akiwa nje ya Kristo karama ile inakuwa inatumika na ajili ya ufalme wa giza aidha awe anajua au hajui. Sasa leo hatutaingia huko sana…bali tutajifunza maana ya KARAMA, HUDUMA na UTENDAJI KAZI.

Kama Umempa Yesu Kristo Maisha yako…na hujajua karama yako ni ipi..nakushauri ukatafute kujua maarifa hayo kwa bidii zote kwasababu ni muhimu sana kuyajua. Na kama hujui sehemu ya kuyapata tunalo somo juu ya hilo..kama ukilihitaji unaweza ukatutumia ujumbe ufupi inbox tukutumie.

Lakini leo hii tutaangazia tofauti kati ya KARAMA, HUDUMA na UTENDAJI KAZI.

Biblia inasema katika…

1Wakorintho 12:1 “Basi, ndugu zangu, kwa habari ya karama za roho, sitaki mkose kufahamu.

2  Mwajua ya kuwa mlipokuwa watu wa Mataifa, mlichukuliwa kufuata sanamu zisizonena, kama mlivyoongozwa.

3  Kwa hiyo nawaarifu, ya kwamba hakuna mtu anenaye katika Roho wa Mungu, kusema, Yesu amelaaniwa; wala hawezi mtu kusema, Yesu ni Bwana, isipokuwa katika Roho Mtakatifu.

4  Basi pana tofauti za KARAMA; bali Roho ni yeye yule.

5  Tena pana tofauti za HUDUMA, na Bwana ni yeye yule.

6  Kisha pana tofauti za KUTENDA KAZI, bali Mungu ni yeye yule azitendaye kazi zote katika wote.

7  Lakini kila mmoja hupewa ufunuo wa Roho kwa kufaidiana”

Kama tunavyoona hapo pana vitu vitatu…Karama, huduma…na utendaji kazi…Wengi imewawia ngumu kutofautisha vitu hivi..lakini leo kwa Neema za Bwana tutajifunza tofauti zake tukijifunza kupitia mifano ya kimaisha.

Mungu anapompa mtu karama… anaweza kumpa karama moja, au wakati mwingine mbili au tatu kwa mpigo…Lakini wengi Bwana anawapa karama moja tu ya rohoni… Na karama moja inaweza kuwa na utendaji kazi tofauti…Karama moja inaweza kuwa na utendaji kazi hata mara 100 tofauti tofauti..

Tuchukue mfano…Hospitalini kunaweza kuwa na madaktari 100, lakini wote hawatendi kazi inayofanana…wengine utakuta wamebobea katika mifupa, wengine vinywa, wengine Ngozi, wengine macho n.k Lakini wote hawa karama yao ni moja “udaktari/utabibu”…Na huduma yao wote ni moja “UAGUZI” wanaagua watu.  Hivyo tunaweza kurahisisha na kusema katika hospitali hiyo kuna watu 100 wenye karama moja na huduma moja lakini utendaji kazi tofauti.

Vivyo hivyo tukirudi kwenye SHULE.. shule inaweza kuwa na waalimu 50, kati ya hao kuna waalimu wa fizikia, kiingereza, biolojia n.k lakini wote hao karama yao ni moja “kufundisha” na huduma yao ni moja nayo ni UALIMU. Na vitengo vingine vyote vya kimaaisha ni hivyo hivyo…kwa wahandisi ni hivyo hivyo, kwa wanajeshi ni hivyo hivyo, utendaji kazi unatofautia n.k.

Tukirudi katika kanisa la Kristo ambalo ndio kitengo kikuu na cha juu na Taasisi iliyo kuu kuliko zote mbele za Mungu..Nalo pia lina watu wenye karama tofauti tofauti, huduma tofauti tofauti na utendaji kazi tofauti.

Kwamfano..Katika karama ya uimbaji wanaweza kuwepo waimbaji 100, kila mmoja akawa na namna yake ya kuimba, wengine wamejaliwa kuimba vyema katika nyimbo za kuabudu, wengine katika nyimbo za sifa, wengine katika nyimbo za tenzi za rohoni n.k hawa wote wanatenda kazi tofauti tofauti lakini karama yao ni moja “kuimba”, na huduma yao ni moja UINJILISTI kwa njia ya NYIMBO.

Hali kadhalika kwenye huduma ya kiualimu,watakuwepo waalimu wa Watoto kanisani, watakuwepo waalimu wa vijana kanisani, watakuwepo waalimu wa kila namna kulingana na Neema kila mtu aliyopewa, wengine waalimu kwa njia ya vitabu, wengine waalimu kwa njia ya mitandao, nk. mwalimu mmoja hawezi kufanana na mwingine kwa kila kitu…sasa hawa wote karama yao ni moja “kufundisha” lakini huduma yao ni moja tu “WAALIMU”..Haijalishi watakuwa wamejigawanya gawanya katika vitengo vingapi..lakini huduma yao ni hiyo hiyo moja tu.

Warumi 12:6  “Basi kwa kuwa tuna karama zilizo mbalimbali, kwa kadiri ya neema mliyopewa; ikiwa unabii, tutoe unabii kwa kadiri ya imani;

7  ikiwa huduma, tuwemo katika huduma yetu; mwenye kufundisha, katika kufundisha kwake;

8  mwenye kuonya, katika kuonya kwake; mwenye kukirimu, kwa moyo mweupe; mwenye kusimamia kwa bidii mwenye kurehemu, kwa furaha”.

Hali kadhalika wapo katika kanisa ambao wamepewa karama ya ndoto kama Danieli, wengine maono, wengine unabii, n.k hawa huduma yao ni “UNABII”.

Na karama nyingine zote zilizosalia, kama miujiza, Imani, Neno la Hekima, unabii n.k.. zina utendaji kazi tofauti na huduma tofauti tofauti.

Hivyo kwa hitimisho ni kwamba…kila karama inayo huduma..Na karama moja inaweza kuwa na utendaji kazi tofauti tofauti kulingana na mtu. Hivyo usitafute kujilinganisha na mtu mwingine, wala usitafute kufanana na mwingine..wala usimdharau mwingine..

Kama wewe unaweza kuona maono ya nini kitatokea kesho..mwingine anaweza kupewa kuliona jambo hilo hilo kwa njia ya ndoto, mwingine si kwa ndoto wala maono bali kwa ufunuo…Hivyo usijisifu kwa kuona maono wala kwa ndoto, wala kwa ufunuo..wote karama yenu ni moja “unabii”  lakini zinatenda kazi tofauti tofauti..

Wewe una karama ya Matendo ya miujiza, ukimwekea mtu mkono anapokea uponyaji..usijisifu kwa mwingine, kwasababu mwingine anaweza kumtamkia tu mtu na akapokea uponyaji, ule ule ambao wewe ungeufanya kwa kumwekea mikono..Mna karama moja isipokuwa utendaji kazi tofauti.nk. nk NK

Hivyo ni muhimu kuwa wanyenyekevu na pia kukaa kila mtu katika nafasi yake pasipo kunia mkuu..

Warumi 12:3  “Kwa maana kwa neema niliyopewa namwambia kila mtu aliyeko kwenu asinie makuu kupita ilivyompasa kunia; bali awe na nia ya kiasi, kama Mungu alivyomgawia kila mtu kiasi cha imani.

4  Kwa kuwa kama vile katika mwili mmoja tuna viungo vingi, wala viungo vyote havitendi kazi moja;

5  Vivyo hivyo na sisi tulio wengi tu mwili mmoja katika Kristo, na viungo, kila mmoja kwa mwenzake”

SASA JAMBO KUU LA MWISHO LA KUKUMBUKA ni  kuwa  karama yoyote au huduma yoyote uliyopewa..lengo la kupewa karama hiyo ni kuujenga mwili wa Kristo, sio kujionyesha wewe ni mtaalamu..au mjuzi, au una uwezo Fulani wa kipekee Zaidi ya wengine.. Mtu mmoja aliniuliza mtumishi nifanye nini ili niwe  na upako, wa kufufua wafu, na kuwekea watu mikono wapone saa hiyo hiyo, nifanye miujiza mikubwa, nikamuuliza unataka hayo yote kwa lengo gani,..hana jibu..Ndugu karama za rohoni sio za kujitafutia umaarufu au kuwa nazo tu basi..

Hizo Mungu kaziweka ili kuokoa Roho za watu wake.. hivyo unapaswa uitumie katika kuwaleta watu katika ufalme, watubu wamgeukie Mungu na kuucha ulimwengu kama wewe ulivyouacha Hilo ndio lengo kuu…Usipoitumia inavyopaswa siku ile utatoa hesabu..Ikiitimia kujipatia pesa utatoa hesabu, ukiitumia kulaania watu utatoa hesabu, ukiitumia kupotosha watu utatoa hesabu, ukiitumia kujitengenezea umaarufu wako na watu badala ya kumwogopa Mungu na kumtumikia Mungu wanakuogopa wewe siku ile utatoa hesabu..ukiitumia karama uliyopewa kujichukulia utukufu wewe badala ya kumpa Mungu utukufu..siku ile utatoa hesabu ndugu yangu…Siku ile utapoangaliwa na kuonekana karama uliyopewa hajaleta watu wowote katika ufalme wa mbinguni, utawajibishwa katika hilo..

Leo tumejua tofauti kati ya karama, utendaji kazi na Huduma, Bwana azidi kutusaidia sana..tuwe waaminifu hata siku ile ya kuja kwake.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

NITAIFAHAMU VIPI KARAMA YANGU?.

ROHO YA MPINGA KRISTO IKITENDA KAZI SIKU HIZI ZA MWISHO

TOA SADAKA ISIYO NA KASORO KWA BWANA.

KWANINI MUNGU ALIMTUMIA MUSA KWA VIWANGO VILE?

FIMBO YA HARUNI!

KARAMA ILIYO KUU.

ITAMBUE KARAMA YA MUNGU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Je! Shetani alitolea wapi uovu?

SWALI: Ikiwa Mungu aliviumba viumbe vyake vikiwa vikamilifu Je! Shetani alitolea wapi uovu?. Na Je! ni nani aliyeiumba  dhambi?.

JIBU: Kitu chochote kizuri tunachokiona,  mpaka tumejuwa kuwa ni kizuri basi tujue kuwa ni lazima kilikuwepo  kingine kibaya  ambacho kimeuthibitisha uzuri wake..kwamfano unapolamba sukari mpaka umejuwa kuwa sukari ni tamu ni kwasababu ulishakutana na kitu kama chumvi huko nyuma chenye ladha tofauti n hiyo , au unapouona mwanga, mpaka umejua kuwa  hii ni nuru, ni kwasababu ulishawahi kuliona giza huko nyuma ndipo ukaweza kuielewa vizuri nuru ni nini, kamwe usingekaa ujue kuwa huu ni mchana kama usingekaa uuone usiku ulivyo, usingekaa ujijue kama wewe una afya kama usingewahi kuugua..Na vitu vingine vyote tunavyoviona ni vizuri vivyo hivyo..Utagundua kuwa kibaya kipo kwa lengo la kukithibitha kizuri,  mpaka kujua huyu mtu anayo hekima, ni kwasababu mpumbavu yupo, mpole-kwasababu mkali yupo, mpaka kujua kuwa kuna mrefu ni kwasababu mfupi yupo, mweupe-kwa-mweusi, mwanamke-kwa -mwanaume..n.k.

Sasa Mungu alipoanza kuviumba viumbe vyake, aliviumba vyote vikiwa vikamilifu, ndipo hapo akawauumbia WEMA ndani yao, lakini hakuishia hapo tu, alitaka pia wajitambue kuwa wao ni wema, na hivyo wazidi kuupenda wema ndipo hapo akauumba na UBAYA pia, ili uuweze kuuthibitisha wema..

Hivyo tangu mwanzo malaika zake walipewa Ujuzi huo wa kuweza kujua mema na mabaya..Ili kusudi kwamba wazidi kuupenda wema  waliokusudiwa kuwa nao, na kuuzidi kuuchukia ubaya usiowafaa.

Ndipo hapo sasa, Malaika wakawa wanajua sasa ili sisi tuwe watakatifu kama Mungu ni lazima tuchukie matendo  yasiyoendana na utakatifu, ili tuwe wema ni lazima tuukatae ubaya wa kumchukia malaika mwenzetu na Mungu wetu, ili tuwe wakweli ni lazima tusisemezane uongo sisi kwa sisi….

Isaya 45:7 “Mimi naiumba nuru, na kulihuluku giza; mimi nafanya suluhu, na kuhuluku ubaya; Mimi ni Bwana, niyatendaye hayo yote”.

Maombolezo 3:38 “Je! Katika kinywa chake Aliye juu Hayatoki maovu na mema”?

Lakini sasa mambo yakaja kubadilika baadaye..Baadhi ya malaika, wakiongozwa na baba yao shetani, wakaanza kukengeuka, wakawa wanataka kuijitawala wenyewe, hivyo wakaona ni bora wachague yale mabaya ili  kutimiza adhma yao, sasa badala ya kupenda wakaanza kuchukia, wakawachukia malaika wenzao waliomtii Mungu vilevile wakamchukia na muumba wao aliyewaumba wao,  wakaanza kusema uongo, wakaanza kuharibu n.k.

Hapo ndipo dhambi ilipopata nguvu ndani yao, wakapungukiwa na utukufu wa Mungu, wakaonekana ni waovu, wakafukuzwa watoke mbinguni katika makao ya Mungu matakatifu.

Hivyo ukiuliza  uovu ulitoka wapi, fahamu kuwa ouvu na wema viliumbwa vyote pamoja viliumbwa na Mungu kila kimoja kikae katika sehemu yake kutimiza kusudi lake..Lakini wale waliokengeuka walipoupenda ubaya zaidi ya wema ndipo wakaonekana wakosaji…Hivyo shetani alitolea wapi uovu?..jibu> aliumbiwa nao.

Hata sasa, iwe wewe ni mkristo au sio mkristo, ujuzi huo wa mema na mabaya upo ndani yako tangu Edeni. Ulikuwa ni Mpango wa Mungu kabisa ubaya uwepo ndani ya mtu kwa makusudi maalumu mema.. Sasa ni jambo la wewe kuchagua moja kati ya hilo, ukipenda wema basi utajitahidi ukae mbali na ubaya, vivyo hivyo ukiupenda ubaya basi utafanya juu chini uwe mbali na wema.

Yohana 3:19 “Na hii ndiyo hukumu; ya kuwa nuru imekuja ulimwenguni, na watu wakapenda giza kuliko nuru; kwa maana matendo yao yalikuwa maovu.

20 Maana kila mtu atendaye mabaya huichukia nuru, wala haji kwenye nuru, matendo yake yasije yakakemewa.

21 Bali yeye aitendaye kweli huja kwenye nuru, ili matendo yake yaonekane wazi ya kuwa yametendwa katika Mungu”.

Lakini sisi tuliokoka tumeipenda Nuru, a ndio maana hukumu ya Mungu haipo juu yetu…kama maandiko yanavyosema katika Warumi 8:1

 Ubarikiwe.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

NI KWASABABU YA YESU KRISTO.

JE WAJUA?

TOFAUTI KATI YA HEKALU, SINAGOGI NA KANISA NI IPI?

WANA WA MUNGU, NA BINTI ZA WANADAMU.

TUMAINI NI NINI?

MAMBO 5 AMBAYO KILA MKRISTO ANAPASWA KUFAHAMU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

KIFO CHA MTAKATIFU POLIKAPI (Policarp).

Tunaweza kujifunza nini juu ya Kifo cha Mtakatifu Polikapi?

Polikapi aliishi kati kipindi cha mwaka 69-159 WK. Alikuwa ni askofu wa kanisa la Smirna ambaye alikuwa pia ni mwanafunzi wa Mtume Yohana.

Wakati ule wa kanisa la kwanza kama wengi wetu tunavyojua, Utawala wa Roma ulikuwa na vita vikali sana dhidi ya wakristo wote ulimwenguni. Na sababu kuu ilikuwa ni wao kukataa kuabudu miungu yao ya kipagani na sanamu za kirumi, na pale wanapoona watu wengi wanavutwa kuiacha Imani yao na kumgeukia Kristo ndipo walipozidisha mapambano makubwa dhidi ya wakristo.. Ilikuwa ni unachagua moja aidha umkane Kristo uishi au umkiri Ufe..

Ndio maana kwa kanisa la Kwanza, lile Neno la Mtume Paulo, linalosema.

Warumi 10:9 ‘Kwa sababu, ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, utaokoka’.

Lilikuwa linamaana kubwa sana, tofauti na linavyotafsiriwa sasa hivi..Kwasababu ilifikia hatua ukimkiri Yesu tu kuwa ni mwokozi wa huu ulimwenguni adhabu yake ilikuwa ni kifo cha kukatwa kichwa au kutupwa katika tundu la simba. Sio leo hii watu tunasema tumemkiri Yesu, lakini tukiambiwa tu tujitwike misalaba yetu tumfuate licha ya kuuawa, utasikia watu wanasema  hiyo ni dini ya itikadi kali..huo ni ulokole ule wa zamani..

Bwana atusaidie..

Sasa baada ya wakristo wengi kuuliwa katika kanisa la kwanza wengine kwa kutupwa katika viwanja vya simba na wengine kutundikwa kwenye miti, na wengine kukatwa vichwa ikafika wakati sasa wakawahitaji na wale viongozi wao wakuu wa juu kabisa wawaue, na mmojawapo alikuwa ni huyu Polikapi wa kanisa la Smirna lililokuwa Asia ndogo (ambayo ni Uturuki kwa sasa)..

Hapo ndipo harakati za kumtafuta Polikapi zilipoanza, wakatumiwa maaskari wa jeshi wengi sana kwenda kumtafuta, Lakini Polikapi aliposhauriwa na baadhi ya wafuasi wake ahame miji akimbilie mwingine, yeye alikataa, kinyume chake zile habari hata hazikumwogopesha bali alikwenda katika mojawapo ya nyumba ya marafiki zake, akawa akikaa huko usiku na mchana akiomba na kuliombea kanisa la Kristo ulimwenguni kote..Na siku tatu kabla ya kukamatwa kwake anasema aliona maono, katika maono hayo anasema aliona mto wa kulalia wa moto ulikuwa chini ya kichwa chake..Ndipo akaenda kuwaambia wafuasi wake kuwa atakwenda kuchomwa moto akiwa mzima…

Sasa wale askari walipofika  na kumkuta walishtuka kidogo, kumuona mbona ni mtu mzee ambaye hakukuwa hata na haja ya kumwendea na majeshi na askari na marungu, na mapanga?…Kama tu ile picha ya Bwana Yesu alipokuwa pale Gethsemane, wale askari walipomwendea na marungu na mapanga wakidhani atakuwa bonsa mwenye ma-boardguards na misuli mikubwa, lakini walimkuta jinsi wasivyotegemea…hata wakaanza kuhisi huyo siye Yesu waliotumwa kumtafuta labda kuna Yesu mwingine…ndio maana walikuwa wanakazana kumwambia Tunamtafuta Yesu, japo Bwana Yesu alikuwa anawaambia mnayemtafuta ndiye mimi..lakini bado walikuwa hawaamini wanachokiona.

Na vivyo Polikapi alipowaona wale askari, aliwakaribisha kwake kama vile wageni wake, akawapa chakula wakala, kisha akawaomba haja moja kabla hawajamchukua, nayo ni ‘kuomba Lisaa’ limoja kisha ndio wamchukue wampeleke kwenye uwanja wa mauaji..Ndipo wale askari wakamkubalia haja yake, Polikapi akaanza kuomba lakini maombi yake yalipitiliza mpaka masaa mawili, ndipo wale askari wakiwa pale wakaanza Kujijutia mioyoni ni kwanini walitumwa kuja kumshika mtu kama huyu mkarimu asiye na hatia…Lakini hakukuwa na namna ilibidi wafanye vile kama walivyoagizwa.

Na walipomleta sasa katika uwanja wa mauaji ambapo watu wengi walikuwa wanamngoja auawe, Lakini wale pia walipomwona kuwa ni mzee wakaona haileti maana sana  kumuua mzee kama yule. Hivyo utawala ukamtaka neno moja tu kwake kwamba “Amlaani Kristo, nao watamwachia”

Ndipo Polikapi akafungua kinywa chake na kuwaambia “Kwa miaka nane na mi-sita (akimaanisha miaka 86), nimekuwa nikimtumikia na hajawahi kunifanyia ubaya wowote. Nitawezaje kumkufuru Mwokozi wangu na mfalme wangu”?.

Lakini wale wakuu wa kirumi wakafanya kama,wanampa nafasi nyingine tena..wakamwambia.. “Wewe mzee Apa leo kwa mkuu wa Ngome hii na hiyo tu itatosha” tukuachie..(mkuu wa ngome ni mkuu wa miungu wanayoitumikia)..

Lakini Polikapi akawaambia.. “Kama mnamatumaini ninaweza kufanya kitendo kama hicho, nadhani mtakuwa mnajifanya kuwa hamjui mimi ni nani….Mnisikilize wote mimi ni mkristo!!

Wale wakuu wakaanza kumtishia kwa wale Wanyama wakali waliokuwa nao..Kisha wakamwambia tutakuchoma kwa moto..

Polikapi akawaambia “Mnanitishia kwa moto wa kitambo ambao baada ya muda mfupi tu utazima. Lakini mnajitoa ufahamu juu ya moto wa mateso ya milele ambao umeandaliwa kwa ajili ya watu waovu”.

Basi wakamchoma  Polikapi kama vile nyama choma iliyowekwa juu ya mkaa, lakini walipoona haungui wakammalizia kwa mkuki na alipokuwa anakiribia kufa alisema,

“Ninakubariki Baba kwa kunipangia hukumu hii ninayostahili, ili kwamba katika kundi la wafia Imani nami pia nikinywee kikombe cha Kristo”.

Hivyo ndivyo alivyokufa Mtakatifu Polikapi kama mshindania Imani mwaminifu..(kifo cha mtakatifu polikapi na watakatifu wengine vimebeba ujumbe wa muhimu sana kwetu)

Vivyo hivyo na sisi biblia inatuambia..

Waebrania 12:1  “Basi na sisi pia, kwa kuwa tunazungukwa na wingu kubwa la mashahidi namna hii, na tuweke kando kila mzigo mzito, na dhambi ile ituzingayo kwa upesi; na tupige mbio kwa saburi katika yale mashindano yaliyowekwa mbele yetu,

 2  tukimtazama Yesu, mwenye kuanzisha na mwenye kutimiza imani yetu; ambaye kwa ajili ya furaha iliyowekwa mbele yake aliustahimili msalaba na kuidharau aibu, naye ameketi mkono wa kuume wa kiti cha enzi cha Mungu”.

Ikiwa sisi hatujafikia hatua ya kumwaga damu, lakini tunaona ni shida kuishi Maisha ya kikristo tungekuwa wakati huo tungesemaje?. Lakini mimi na wewe tumepewa neema ya kumpokea Kristo katika kipindi cha amani kama hichi..Sasa tukishindwa kuipokea siku ile tutajiteteaje mbele za Mungu aliye hai?. Au tutajilinganishaje na mashahidi waaminifu kama hawa, wakina Antipa, Polikapi na wengine..?

Hivyo biblia inatuasa, tuitupilie mbali dhambi ile ituzingayo kwa upesi,..tupige mwendo..Tukubali sasa kujitwika misalaba yetu na kumfuata Kristo kwa gharama zozote, tukubali kuchekwa, kudharauliwa, tukubali kusemwa tunapotupa vimini na kuacha kuvaa suruali na wigi na kuacha usengenyaji …Tunapaswa tukubali hata dhihaka tunapoacha kuongozana na kampani za watenda mabaya, na walevi, na wezi….tunapoanza kuongeza viwango vyetu vya maombi, na kumtafuta Mungu kwa bidii..tukubali kupitia vita vya kiimani n.k.Hatupaswi kukisoma tu kifo cha Mtakatifu Polikapi na vifo vya watakatifu wengine kama hadithi bali kama mfano wa kuigwa katika vipindi tunavyopitia sasa.

Bwana atusaidie sana..

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

UNYAKUO.

USIMPE NGUVU SHETANI.

SAYUNI ni nini?

IVUMBUE INJILI YA KRISTO KUTOKA KATIKA KILA JAMBO.

HISTORIA YA ISRAELI.

KUFUKIZA UVUMBA NDIO KUFANYAJE?

Rudi Nyumbani:

Print this post

JE UNAMTHAMINI BWANA?

(Je unamthamini Bwana?) Jina la Bwana libarikiwe…Karibu tujifunze maandiko…

Neno la Mungu ni Mwanga wa njia yetu ielekeayo mbinguni na Taa iongozayo miguu yetu katika safari yetu ya mbinguni. (Zab 119:105).

Jambo la muhimu la kufahamu ni kuwa Mungu wetu aliyetuumba kamwe hawezi kumtumia mtu ambaye hayupo tayari..au moyo wake haupo tayari kumpokea yeye. Wakati mwingine mioyo yetu ya kutokuwa watoaji  inatuzuilia sisi kupokea Baraka kutoka kwa Mungu.

Hebu tujifunze mifano michache ya kwenye biblia jinsi Bwana alivyoweza kuwatumia watu katika kulitimiza kusudi lake..ambapo kwa kupitia mifano hiyo..tunaweza kutoka sehemu moja hadi nyingine kiimani..

Marko 14:12 “Hata siku ya kwanza ya mikate isiyochachwa, walipoichinja pasaka, wanafunzi wake wakamwambia, Ni wapi utakapo tuende tukuandalie uile pasaka?

13 Akatuma wawili katika wanafunzi wake, akawaambia, Nendeni zenu mjini; atakutana nanyi mwanamume amechukua mtungi wa maji; mfuateni;

14 na po pote atakapoingia, mwambieni mwenye nyumba, Mwalimu asema, Ki wapi chumba changu cha wageni, niile pasaka humo, pamoja na wanafunzi wangu?

15 Naye mwenyewe atawaonyesha orofa kubwa, imeandikwa tayari; humo tuandalieni.

16 Wanafunzi wakatoka, wakaenda mjini, wakaona kama alivyowaambia, wakaiandaa pasaka”.

Katika Tukio hilo..Tunamwona kuna mtu mmoja ambaye ni mcha Mungu biblia haijamtaja jina lake…Lakini Mtu huyu anaonekana alikuwa ni mtu mwenye uwezo kidogo kutokana na habari hiyo…kwasababu utaona anatajwa kuwa na Mtumwa, na pia anayo nyumba yenye ghorofa…Sasa kwa enzi hizo kumiliki nyuma ya ghorofa tena katikati ya Mji kama ule (Yerusalemu) si rahisi kama wewe sio mtu mwenye uwezo ni sawa na leo umilika nyumba ya ghorofa pale Posta Daresalaam…

Lakini pia kama ukichunguza mtu huyo ni lazima alikuwa anamjua Bwana Yesu sana..na pia alikuwa anafuatilia mafundisho yake na alikuwa anampenda sana…Ingawa pengine hakupata nafasi ya kukutana naye..Lakini pamoja na hayo ndoto yake kubwa ilikuwa ni siku moja akutane naye, amkaribishe kwake…

Sasa pengine alifunga na kuomba kwamba angalia msimu huu wa sikukuu amtembelee kwake…na hivyo akapanga pengine namna ya kumtafuta akakosa…moyoni mwake akiwa na mawazo hayo..wazo likamwingia aandae chumba kabisa kilicho kizuri tena ghorofani ili atakapompata Yesu wakati huo huo aingie kwenye chumba hicho isiwe baada ya kumpata ndipo aanze maandalizi.

Siku chache kabla ya sikukuu…moyo wake pengine ukiwa na shauku ya kumkaribisha Bwana…..Yesu akauona moyo huo maili kadhaa mbali na alipokuwa…kama vile alivyomwona Nathanieli siku ile alipokuwa chini ya mtini alipokwenda kuitwa na Filipo.

Yohana 1: 48 “Nathanaeli akamwambia, Umepataje kunitambua? Yesu akajibu, akamwambia, Kabla Filipo hajakuita, ulipokuwapo chini ya mtini nilikuona”.

Na ndivyo hivyo hivyo Bwana alivyouona moyo wa huyu mtu akiwa nyumbani kwake..tayari amemwandalia yeye chumba…Na kwasababu Roho ya kinabii ilikuwa juu ya Yesu akawaambia wanafunzi wake waende mjini watamkuta mtu kabeba mtungi wamfuate mpaka atakapoingia wamwulize mwenye nyumba

“Ki wapi chumba changu cha wageni, niile pasaka humo, pamoja na wanafunzi wangu”

Hebu tafakari hiyo sentensi… “Ki wapi chumba changu”..na si “ki wapi chumba chako”…Kitendo cha Yule mtu kukiweka tayari kile chumba kwaajili ya Bwana..tayari Bwana ameshakiheshimu na kukiita chumba chake na si cha Yule mtu tena…Hebu tafakari huyo mtu alifurahi kiasi gani kusikia vile??..Chumba kile alichomwandalia Bwana, Bwana amekijia…Ni furaha ya ajabu sana.

Ndugu yangu..Bwana hawezi kuja mahali ambapo hatujamwandalia…na Bwana akija mahali tulipomwandalia anakuja na Baraka. Sio kwamba Bwana alikuwa hana mahali pa kwenda…alikuwa na sehemu nyingi za kwenda lakini aliutazama mji mzima ni nani aliyekuwa na moyo wa kumpenda kwa dhati kuliko wote aende kwake…

Ndio maana sehemu nyingine Bwana Yesu alisema maneno haya…

Luka 4:25 “Lakini, kwa hakika nawaambia, Palikuwa na wajane wengi katika nchi ya Israeli zamani za Eliya, wakati mbingu zilipofungwa miaka mitatu na miezi sita, njaa kuu ikaingia nchi nzima;

26 wala Eliya hakutumwa kwa mmojawapo, ila kwa mjane mmoja wa Sarepta katika nchi ya Sidoni”.

Wajane walikuwepo wengi lakini Eliya hakutumwa isipokuwa kwa mwanamke wa Taifa la mbali..akakaa kwake na nyumba yake ikabarikiwa..mkate haukuwaishia.. Kadhalika kulikuwepo na matajiri wengi pale Yerusalemu lakini Bwana hakwenda hata kwa mmojawao isipokuwa kwa mtu huyu ambaye moyoni mwake alimpenda Bwana kiasi kwamba alikuwa tayari kumwandalia chumba kabla hata ya kumwona wala kumkaribisha.

Bwana anaitazama mioyo yetu ndugu?..Je tunamjali kiasi gani? Tafakari mfano mwingine tena huu wa mwisho..

Marko 11:1 “Hata walipokaribia Yerusalemu karibu na Bethfage na Bethania, kukabili mlima wa Mizeituni, aliwatuma wawili katika wanafunzi wake,

2 akawaambia, Nendeni mpaka kile kijiji kinachowakabili; na katika kuingia ndani yake, mara mtaona mwana-punda amefungwa, asiyepandwa na mtu bado; mfungueni, kamleteni.

3 Na mtu akiwaambia, Mbona mnafanya hivi? Semeni, Bwana anamhitaji na mara atamrudisha tena hapa.

4 Wakaenda zao, wakamwona mwana-punda amefungwa penye mlango, nje katika njia kuu, wakamfungua.

5 Baadhi ya watu waliosimama huko wakawaambia, Mnafanya nini kumfungua mwana-punda?

6 Wakawaambia kama Yesu alivyowaagiza, nao wakawaruhusu.

7 Wakamletea Yesu yule mwana-punda, wakatandika mavazi yao juu yake; akaketi juu yake”.

Katika habari hii, jambo ni lile lile…Hawa watu walikuwa na punda wao amefungwa pale..lakini pengine walishawahi kusikia habari za Yesu na kumwamini..na kutamani wangempatia angalau kitu Fulani…Na Bwana alipoiona mioyo yao…pale pale kwa kuwa yeye ni Nabii akawatuma wanafunzi wake kuwaomba punda yule amtumie kuingia naye Yerusalemu..Na wale wenye punda walipowauliza kwanini mnamfungua? Waliposikia kwamba ni Bwana anamhitaji…wala hawajauliza mara mbili mbili wala kuhoji..Ni wazi kuwa walifurahi mno na kujiona wenye bahati..

Ni wazi kuwa walikuwepo wengi wenye punda pale mjini lakini Bwana Yesu hakwenda kuchukua hata wa mmoja wao…Ni kwanini? Ni kwasababu hakuna chochote ndani yao cha kuuvuta Moyo wa Bwana Yesu uwaelekee wao…Pengine Bwana angeenda kwa mmoja wao na kuomba punda Yule wangeanza kusema…oo kwanza wewe unawapinga wazee wetu wa dini…oo kwanza wewe unajiita Mwana wa Mungu..oo wewe umetoka wapi, huna shughuli maalumu unazunguka tu…wengine wangeanza kumwita hata mwizi…wengine wangeanza kusema huna kazi ya kufanya unataka kuharibu mali za watu…

Vivyo hivyo walikuwepo wenye magari sio punda tu…kwasababu kipindi hicho yalikuwepo magari ya farasi watu wenye uwezo walikuwa wanayatembelea….Lakini hakukuwa na hata mmoja mwenye moyo wa dhati wa kutamani siku moja Bwana angelipanda gari lake…Lakini Bwana anauona moyo wa mtu mmoja anayetamani siku moja Bwana angepanda punda wake…Na Bwana anakwenda kwa Yule mwenye moyo uliomwelekea.

Ndugu yangu..habari hizi ni mifano inayotufundisha dhahiri..Jicho la Bwana linatazama kote kote ulimwenguni kila siku anatazama ni yupi, ni nani, na yuko wapi aliye tayari angalau kutoa chochote kwaajili yake?..Kumbuka yeye hana shida..lakini anaipenda mioyo ya utoaji…anaangalia ni mtaa gani kijiji gani kuna mtu ambaye anatamani angalau kitu chake kile, kingetumiwa na yeye…Anaangalia huku na huko..Anatamani sana kututembelea lakini hawezi kumtembelea mtu ambaye hataki kutembelewa na yeye..

Tafakari tena maneno haya ya kumalizia aliyoyasema juu ya siku ile ya mwisho itakavyokuwa..

Mathayo 25:31 “Hapo atakapokuja Mwana wa Adamu katika utukufu wake, na malaika watakatifu wote pamoja naye, ndipo atakapoketi katika kiti cha utukufu wake;

32 na mataifa yote watakusanyika mbele zake; naye atawabagua kama vile mchungaji abaguavyo kondoo na mbuzi;

33 atawaweka kondoo mkono wake wa kuume, na mbuzi mkono wake wa kushoto.

34 Kisha Mfalme atawaambia wale walioko mkono wake wa kuume, Njoni, mliobarikiwa na Baba yangu, urithini ufalme mliowekewa tayari tangu kuumbwa ulimwengu;

35 kwa maana nalikuwa na njaa, mkanipa chakula; nalikuwa na kiu, mkaninywesha; nalikuwa mgeni, mkanikaribisha;

36 nalikuwa uchi, mkanivika nalikuwa mgonjwa, mkaja kunitazama; nalikuwa kifungoni, mkanijia.

37 Ndipo wenye haki watakapomjibu, wakisema, Bwana, ni lini tulipokuona una njaa, tukakulisha, au una kiu tukakunywesha?

38 Tena ni lini tulipokuona u mgeni, tukakukaribisha, au u uchi, tukakuvika?

39 Ni lini tena tulipokuona u mgonjwa, au kifungoni, tukakujia?

40 Na Mfalme atajibu, akiwaambia, Amin, nawaambia, kadiri mlivyomtendea mmojawapo wa hao ndugu zangu walio wadogo, mlinitendea mimi.

41 Kisha atawaambia na wale walioko mkono wake wa kushoto, Ondokeni kwangu, mliolaaniwa, mwende katika moto wa milele, aliowekewa tayari Ibilisi na malaika zake;

42 kwa maana nalikuwa na njaa, msinipe chakula; nalikuwa na kiu, msininyweshe;

43 nalikuwa mgeni, msinikaribishe; nalikuwa uchi, msinivike; nalikuwa mgonjwa, na kifungoni, msije kunitazama.

44 Ndipo hao pia watajibu, wakisema, Bwana, ni lini tulipokuona wewe una njaa, au una kiu, au u mgeni, au u uchi, au u mgonjwa, au u kifungoni, tusikuhudumie?”

45 Naye atawajibu, akisema, Amin, nawaambia, Kadiri msivyomtendea mmojawapo wa hao walio wadogo, hamkunitendea mimi.

46 Na hao watakwenda zao kuingia katika adhabu ya milele; bali wenye haki watakwenda katika uzima wa milele.

Usipokubali kujitoa kwa Bwana kamwe usitegemee Baraka wala kupokea kutoka kwake…Naamini maarifa haya yatakusaidia kuchukua hatua ya kumthamini Bwana. (Je unamthamini Bwana?)

Ubarikiwe sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

SAKRAMENTI NI NINI, NA JE! IPO KATIKA MAANDIKO?

INGIENI KWA KUPITIA MLANGO ULIO MWEMBAMBA.

USIZITEGEMEE NGUVU ZAKO KUKUSAIDIA!

Ni sahihi kumuita Mariamu mama wa Mungu?

TOFAUTI KATI YA HEKALU, SINAGOGI NA KANISA NI IPI?

USIMPE NGUVU SHETANI.

Je! Ni kweli ubatizo wa maji hatuuhitaji tena?

UKITAKA KUMFUATA YESU NI SHARTI UACHE VYOTE!

Rudi Nyumbani:

Print this post

Ikiwa sisi tuliumbwa na Mungu,Je! Mungu aliumbwa na nani?

JIBU: Tukiweza kulijibu na swali hili “Ikiwa sisi tunakula ili tuishi, Je! Mungu naye anakula nini ili aishi?”…Basi tutaweza pia kulijibu hilo linaloulizwa kirahisi.

Awali ya yote ni vizuri kufahamu kuwa wazo lolote ambalo linakuja katika vichwa vyetu fahamu kuwa lilishawahi kuumbwa hapo kabla, Hivyo  wakati ulipofika na kuwekwa katika kichwa chako au changu, ndipo tukaliwaza, vinginevyo tusingekaa tuwe na wazo kama hilo vichwani mwetu kama hili la “Mungu aliumbwa na nani” kama halikuwahi kubuniwa na aliyetuumba.. hakuna wazo linalozuka lenyewe tu hewani, labda wewe ndio uwe wa kwanza kuligundua, ni kama kumputa tulizonazo kila kitu kilichomo ndani yake, kiliwekwa na mtu kwanza (installed)

Hivyo mpaka hapo ulipofikia kuwaza tu Mungu aliumbwa na nani, fahamu kuwa ni yeye mwenyewe alilibuni hilo wazo kisha akaliweka kwa makusudi katika ufahamu wako,..Hivyo usifikiri kuwa umegundua wazo la kumnasa Mungu, kama hilo la Mungu aliumbwa na nani,..nataka kwanza uondoe hilo akilini. Na aliamua kufanya hivyo ili wakati wake wa kufikirika ukifika ujiulize weee!!, uumize kichwa weee! kisha ukose majibu! … Wazo hilo alipenda tu ukose majibu yake, kama vile yale mengine alivyopenda upate majibu yake.

Jibu rahisi ni kuwa Mungu hatuwezi kumpima katika “wazo la kuumba au kuumbwa”..kwasababu hayo mawazo ya kuumba au kuumba aliyabuni yeye, hivyo hayawezi kuwa sehemu ya maisha yake..yeye, ni zaidi ya upeo wa fikra zetu.

Jaribu kuwazia mfano huu, unaohusiana na vitu tulivyoviumba sisi wanadamu ambavyo ni vya  elektroniki…Sasa kisa tu tumeviundia mfumo wa kutegemea umeme katika kujiendesha pale vinapoishiwa nguvu tunavichaji betri zako katika umeme.. Na kwamba visipochajiwa ni lazima tu vizime au vife kabisa, Simu zetu zinasema hivyo hivyo,  saa zetu hivyo hivyo , komputa zetu, na tochi zetu zinasema hivyo hivyo n.k..Halafu siku moja sasa eti  na vyenyewe vinaungana na kutuuliza  sisi tulioviumba maswali, vinasema Je! betri zenu ziko wapi, na mnachajiwa wapi? kwasababu hakuna maisha nje ya umeme?

Unaona lakini sisi je tunaishi kwa betri au umeme?…jibu ni la, maisha yetu yanaendeshwa na kitu kingine tofauti na wanachokifikiria, bali mambo hayo ya umeme  tumeviumbia vifaa vyetu vya elektroniki ili viishi kwayo..zaidi ya hapo haviwezi kujua jambo lingine linalotuhusu sisi..

Vivyo hivyo na sisi kwa kuwa tumezungukwa na mazingira ya  “kuumba na kuumbwa”,kila kitu tunaona ni lazima kiwe na chanzo chake ….Basi na sisi tunahitimisha na kusema Je Mungu naye kaumbwa na nani?..

Jibu  linalojitosheleza ndio hilo..Mungu hayupo katika viwango vya kibinadamu ni zaidi ya upeo wa fahamu zetu..hatuwezi kumpima katika mambo ya uumbaji.. ni sawa na leo uulize mwanga una ladha gani, au rangi ina harufu gani..na ndio maana tunapotoa jibu la mkato kuwa Mungu hajaumbwa basi ujue ni kwasababu hizo tunazozisema hapo juu….Mungu ni Zaidi ya upeo wa fikra na kwamba hatuwezi kumweka katika hilo kundi la uumbaji.

Ubarikiwe.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengine:

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Kwanini Mungu hakumuua Nyoka, akamwacha Hawa ajaribiwe katika bustani ya Edeni?

Je! Mungu anasababisha ajali, kwamfano ajali ya kivuko cha MV Nyerere kuzama?

Kwanini Bwana Yesu, aliruhusu yale mapepo yawaingie nguruwe?

Nifanye nini ili niondokane na Hofu maishani mwangu?

Utii ni nini? na ni nani tunayepaswa kumtii au kutokumtii?

KIFO CHA REINHARD BONKEY KINAACHA UJUMBE GANI KWETU?

SI KILA KIPENDEZACHO KINATOKA KWA BWANA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

USIJARIBU KUMGEUZA MUNGU MGANGA WA KIENYEJI,UTAKUFA.

Ipo mifano mingi katika biblia ya watu ambao, walijaribu kumgeuza Mungu kama mganga wa kienyeji na mwisho wao ukawa mbaya sana. Siku zote watu wanaokwenda kwa waganga utagundua wengi wao hawafahamiani hata na hao waganga wanaowaendea, wala hawana uhusiano nao wowote.

Wakifika pale wanaeleza tu matatizo yao, kisha mganga anawatamizia haja zao, kisha wanakwenda zao..Sasa jambo kama hilo usijaribu kulifanya kwa Mungu ni hatari mno.

Wana wa Israeli kuna wakati Fulani walikuwa wanajaribu kufanya hivyo hivyo, unakuta mtu kamwacha Mungu zamani, ndani yake kuna vinyago, hashiki torati ya Mugu, lakini pale anapokumbwa tu na matatizo fulani labda anaumwa, au anataka kufanya jambo Fulani ndipo anataka kwenda kumuuliza Mungu kwa kupitia nabii wake..Sasa karibu wote waliokuwa wanafanya hivyo Mungu alikuwa anawaua bila huruma.

Utajiuliza anawauaje?

Kama huyo nabii ni nabii wa kweli wa Mungu aliyesimama. Mungu atamwambia moja kwa moja kuwa atakufa. Ndicho pia kilichomkuta Yeroboamu na mkewe walipokwenda kuuliza habari za uzima wa mtoto wao kwa nabii Ahiya, walitabiriwa mabaya na vifo soma (1Wafalme14).

Lakini kama nabii huyo ni nabii wa uongo au vuguvugu..Mungu anachofanya ni anamdanganya Yule nabii aliyemwendea, Na Mungu anajua kabisa kwasababu unamwamini nabii Yule kwamba chochote atakachokuambia utafanya, kumbe huo ndio unakuwa mtego wa kwenda kukuangamiza wewe, Mfano huo tunaouna kwa mfalme Ahabu, pale alipotaka kwenda kupigana vita na mfalme wa Shamu, na biblia inasema Mungu akawadanganya wale manabii 400 wote wakamtabiria ushindi kumbe ndio ulikuwa unakwenda kuwa mwisho wake.. Mungu atakuahikishia hata kwa nabii zaidi ya mmoja unachokifanya ni sahihi, kumbe ni uongo ujue kabisa amekusudia kukuua soma (1Wafalme 22:1-39)..Ndicho kilichomkuta Balaamu, ilikuwa ni nusu afe, punda ndiye aliyemuokoa japokuwa ni Mungu ndiye aliyemwambia aende (Hesabu 22:1-34)..Wote hawa ni mfano wa watu waliojaribu kumgeuza Mungu mganga wa kienyeji kwamba wao wapewe tu haja za mioyo yao, mengine zaidi ya hayo hawataki..

Angalia jambo aliloambiwa Ezekieli na Mungu..

Ezekieli 14:1 Ndipo baadhi ya wazee wa Israeli wakanijia, wakaketi mbele yangu.

2 Ndipo neno la Bwana likanijia, kusema,

3 Mwanadamu, watu hawa wametwaa vinyago vyao na kuvitia mioyoni mwao, nao wameweka kwazo la uovu wao mbele ya nyuso zao. Je! Ni laiki yangu niulizwe na wao katika neno lo lote?

4 Basi sema nao, uwaambie, Bwana MUNGU asema hivi; Kila mtu wa nyumba ya Israeli atwaaye vinyago vyake na kuvitia moyoni mwake, na kuliweka kwazo la uovu wake mbele ya uso wake, na kumwendea nabii; mimi, Bwana, nitamjibu neno lake sawasawa na wingi wa sanamu zake;

5 ili niwakamate nyumba ya Israeli kwa mioyo yao wenyewe, kwa sababu wamefarakana nami kwa vinyago vyao……

7 Kwa maana kila mtu wa nyumba ya Israeli, au wa wageni wakaao katika Israeli, ajitengaye nami, na kuvitwaa vinyago vyake na kuvitia moyoni mwake, na kuliweka kwazo la uovu wake mbele ya uso wake, kisha kumwendea nabii, na kuniuliza neno kwa ajili ya nafsi yake; mimi, Bwana, nitamjibu, mimi mwenyewe;

8 nami nitaukaza uso wangu juu ya mtu yule, na kumfanya kuwa ajabu, awe ishara na mithali, nami nitamkatilia mbali, asiwe kati ya watu wangu; nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi Bwana.

9 Na nabii akidanganyika, na kusema neno, mimi, Bwana, nimemdanganya nabii yule, nami nitaunyosha mkono wangu juu yake, na kumwangamiza, asiwe kati ya watu wangu Israeli.

10 Nao watauchukua uovu wao; uovu wa nabii utakuwa sawasawa na uovu wake yule amwendeaye aulize neno;

Unaona hapo mstari wa 9? Anasema mimi Bwana nimemdanganya nabii Yule.. Kama ulikuwa unahitaji kupona, pengine nabii Yule atakupa maagizo Fulani ambayo ni kweli ameyapokea kutoka kwa Mungu, labda tuseme atakuambia Mungu kaniambia, funga siku tatu, kisha kula chakula kisichokuwa na chumvi tu, baada ya hapo utakuwa mzima..Kumbe jambo hilo ndio linakwenda kukuangamiza kabisa.. Na Mungu anafanya hivyo kwasababu umemdharau yeye kwa kumgeuza kuwa kama mganga wa kienyeji, angali ulikuwa unajua kabisa ndani ya moyo wako kuna dhambi umekataa toba, na utakatifu halafu unamwendea yeye akupe haja ya moyo wako wa dhambi..

Hata leo hii, Mungu anawaangamiza watu wengi kwa namna hiyo pasipo wao kujijua.. Wakati Mungu anawapigia kelele kila siku watubu, waache dhambi, watoe vinyago ndani ya mioyo yao, hawataki kusikia wala kuzingatia maagizo hayo, wanadhani Mungu anafurahishwa nao, wanadhani Mungu ni wa neema siku zote badala yake wakiwa bado ni walevi, wala rushwa, wazinzi, waabudu sanamu, washirikina, watazamaji pornography, wasagaji wanamwendea Mungu, kwa kupitia mtu anayejiita nabii, au mtume, au mchungaji, amwombee au amtatulie matatizo yake pengine ya kiafya, au ya kiuchumi, au ya kifamilia…Wahudumiwe tu kisha waondoke wakaendelee na maisha yao ya kawaida ya kila siku..

Ndugu kama ni wewe mmojawapo usijaribu kufanya hivyo tena,..Kwasababu UTAKUFA.. nenda kawatafuta waganga wa kienyeji itakuwa ni salama kwako, lakini sio Mungu kama unamwendea Mungu halafu hutaki kuacha dhambi.. Nakuambia ukweli UTAKUFA NDUGU…

Utaishia kudanganywa tu,..tena na Mungu mwenyewe, unakimbilia mafuta ya upako, unausahau mafuta ya roho yako (Roho Mtakatifu) ambayo yanaokoa roho yako, unakimbilia maji, unasahau maji ya uzima ambayo yanaokoa roho yako.. Timiza kwanza agizo la msingi ambalo ni wokovu na utakatifu..Ndipo Mungu akupe neema ya kutatuliwa na hayo mengine.

Vinginevyo utakufa, hata kama sio kwa njia hiyo, itakuwa kwa nyingine.

Au wewe ni mlevi, mzinzi, mwendaji disko, mlaji rushwa, halafu unakwenda kanisa kila siku, kunakufaidia nini sasa? na kibaya zaidi unashiriki na meza ya Bwana kabisa..Huko ni kujitafutia kifo ndugu. Break! ya kwanza kwa Mungu ni utakatifu (Waebrania 14:12),Mungu hapambwi kwa sadaka, au kwenda kwako kanisani, anachohitaji kwako ni Utakatifu kama yeye alivyo mtakatifu. Nje ya hapo wewe ni adui wa Mungu.

Hiyo ni tahadhari kwako, wewe..Umekwisha sikia, Mungu hadhihakiwa, apandacho Mtu ndicho atakachokuna maandiko yanasema hivyo.

Maran Atha.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengine:

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312 

Mada Nyinginezo:

UNAWAFAHAMU MANABII WA UONGO?

CHUKIZO LA UHARIBIFU

MPINGA-KRISTO

JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?

TAZAMA KRISTO YUPO HAPA,AU YUKO KULE MSISADIKI.

 

JUMA LA 70 LA DANIELI

DANIELI: Mlango wa 1

Rudi Nyumbani:

Print this post

CHUKUA MZIGO WA MWINGINE.

Katika Biblia kuna mahali panasema… “Mchukuliane mizigo na kuitimiza hivyo sheria ya Kristo (Wagalatia 6:2)”.

Lakini Biblia hiyo hiyo mbele kidogo katika mstari wa 6 inasema “Maana kila mtu atalichukua furushi lake mwenyewe (Wagalatia 6: 5)”.

Ni rahisi kuona kama biblia inajichanganya lakini sio kweli, biblia sikuzote ipo sawa,.Isipokuwa tu Mungu anahitaji tupate msaada wake katika kuyatafakari maandiko yake.

Biblia iliposema kila mtu atalichukua furushi lake mwenyewe…Ilikuwa inalenga juu ya matendo ya mtu..Kwamba kila mtu matendo yake yatamfuata mpaka siku ile ya hukumu..Na hayo anakuwa ni kama ameyabeba…atayabeba yeye peke yake na atasimama nayo mbele ya kiti cha Hukumu siku ile akiwa peke yake. Hivyo matendo ya mtu yanafananishwa na FURUSHI!.

Kadhalika Biblia iliposema tuchukuliane mizigo ilimaanisha tusaidiane sisi kwa sisi..Maana yake tukiwa na nguvu tunapaswa tuwasaidie wale wasio na nguvu..Ili tuwe wenye haki mbele za Mungu..na kwa kufanya hivyo tutakuwa tumeitimiza sheria ya Kristo ambayo ni UPENDO.(Yohana 13:34, 1Yohana 3:17-18).

Katika siku hizi za mwisho Biblia imetabiri kwamba upendo wa wengi utapoa!…Upendo wa watu kumpenda Mungu utapoa, kadhalika na upendo wa watu kupendana wao kwa wao utapoa. Na hivyo kuifanya dunia kuikosa hii sheria ya Kristo ambayo ni UPENDO.

Na biblia imetuasa kuwa kuna upendo wa Ulimi na upendo wa tendo.

1Yohana 3: 17 “Lakini mtu akiwa na riziki ya dunia, kisha akamwona ndugu yake ni mhitaji, akamzuilia huruma zake, je! Upendo wa Mungu wakaaje ndani yake huyo?

18 Watoto wadogo, tusipende kwa neno, wala kwa ulimi, bali kwa tendo na kweli”

Kwahiyo kama tumeokoka ni lazima tuitimize hiyo sheria ya Kristo. Tupendane kama matendo kama yeye alivyotupenda sisi. Sio tu kumuombea au kumuhurumia bali pia kutenda.

Na pendo hilo pia ni pamoja na KUCHUKULIANA MIZIGO.

Unaposikia mpendwa mwenzako ana tatizo hili au lile na unajua kabisa yupo katika shida ambayo hawezi kuzungumza..Usisubiri yeye akuambie wewe chukua hatua ya kwenda kumsaidia tatizo lake. Ukiona ndugu yako ni mgonjwa pamoja na kumwombea chukua hatua ya kwenda kumtazama, kumfariji na hata kumhudumia. Usiangalia wewe ulipokuwa na matatizo alikuja kukutafuta au la!..kuwa kama kipofu kwa mabaya uliyofanyiwa na uwe mkumbukaji wa mazuri aliyowahi kukufanyia…

Wengi wetu hatujui kuwa Neema ya Mungu juu ya Maisha yetu inaongezeka juu yetu siku baada ya siku, na pia inaweza ikapungua juu yetu endapo tukiipuuzia…Unapomsaidia mtu hususani mkristo mwenzako..na ukamsaidia kwa moyo kabisa…

Kuna Neema fulani inakuwa inaongezeka juu yako kiasi kwamba utakavyokuja tena kumsaidia mwingine hutasikia uzito kama ulivyosikia kwa yule wa kwanza…na hivyo hivyo watatu utakuwa mwepesi Zaidi…na kwajinsi unavyoendelea hivyo hivyo ile Neema ya utakatifu inaongezeka juu yako mpaka unafikia hatua kusaidia mtu kwako si jambo kubwa wala kukuwazisha kichwa, linakuwa linatoka lenyewe kama vile pumzi…Na Neema hiyo ya utakatifu inavyoongezeka juu yako inaambatana na Milango mikubwa sana ya Baraka…Kwasababu unakuwa umeshaaminiwa na Mungu sana…

Kwasababu Bwana anajua hata akishusha kwako kiasi fulani cha mali, asilimia 90 ya ile itakwenda kuwasaidia watu wake walioko katika shida..walioko katika uhitaji, anajua kiasi kikubwa cha ile fedha au mali itaenda katika kuiendeleza kazi ya yake…hivyo yule mtu anakuwa kama Bomba la Mungu la kupitishia baraka kwa watu wake…Hivyo na lenyewe haliwezi likakauka maji. Lakini mtu anayejizuia kuchukua mizigo ya wengine mtu huyo anakuwa kama ni bomba lililofungwa…Bomba lililofungwa haliwezi kupokea maji kutoka kwenye chanzo kadhalika haliwezi kujaza ndoo za maji zilizopo chini yake kwenye foleni..lakini lililofunguliwa kwa jinsi linavyotoa ndivyo linavyopokea.

Tenga muda nenda kajaribu kuwatafuta watu waliojizoeza kusaidia watu sana kiasi kwamba hata kutoa chochote kwao si shida..tenga muda wahoji waulize kama walishawahi kupungukiwa..watakupa shuhuda za ajabu sana…

Hivyo hatuna budi leo kujikumbusha jambo hili..ili tuzidi kuielewa Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo inavyofanya kazi.

Warumi 15:1 “Basi imetupasa sisi tulio na nguvu kuuchukua udhaifu wao wasio na nguvu, wala haitupasi kujipendeza wenyewe.

2 Kila mtu miongoni mwetu na ampendeze jirani yake, apate wema, akajengwe.

3 Kwa maana Kristo naye hakujipendeza mwenyewe; bali kama ilivyoandikwa, Malaumu yao waliokulaumu wewe yalinipata mimi”.

Kuwahubiria pia wengine habari za Mungu ni kuwachukulia mizigo yao…Bwana akikupa kitu na kile kitu hutaki kuwashirikisha wengine ukidhani kwamba watajua Zaidi kuliko wewe, au hawatakutaja wewe uliyewashirikisha hapo unajifungia mwenyewe bomba lako la neema. Mungu hawezi kukupa jambo jipya kama lile la zamani hujalitoa..Toa lile la zamani katika hazina yako washirikishe wengine bure! Ili Uweze kupokea lingine lakini ukiwa na moyo wa uchoyo na wivu na hutaki kutoa hazina Mungu aliyoiweka ndani yako kwa muda mrefu, ukisema ufunuo huu ni wangu tu…kamwe usitegemee kubarikiwa kwa vyovyote vile..

Bwana Yesu alisema katika Mathayo 13:52 “Akawaambia, Kwa sababu hiyo, kila mwandishi mwenye elimu ya ufalme wa mbinguni amefanana na mtu mwenye nyumba atoaye katika hazina yake vitu vipya na vya kale”.

Hivyo jizoeze kuwashirikisha wengine habari za Uzima..Umepata kitu fulani ambacho kimekusaidia wewe na umeona kuna wengine kama wewe wengi kinaweza kuwasaidia…huo ndio wakati wa KUWACHUKULIA MIZIGO YAO!..Na watakutaja mbele za Mungu katika maombi yao kwamba uliwasaidia na Mungu atakukumbuka na wewe na kukubariki.

Unaona mpendwa mwenzako anafanya kitu fulani cha kujiendeleza na anahangaika mno na wewe una ujuzi wa kutosha wa namna ya kumsaidia, usingoje akutafute, wala usimwonee wivu..wewe huo ndio wakati wa kumchukulia MZIGO!..Kama umekutana na nafasi za kazi na unaona pengine zitamfaa mtakatifu mwenzako Msaidie hata kama hapo alipo tayari kaendelea kuliko wewe. Wewe timiza wajibu wako kwasababu yupo Mungu juu anayetazama..Na mambo mengine yote ya kimaisha na ya ki-roho…SHERIA YA KRISTO NI ILE ILE UPENDO!! Na KUCHULULIANA MIZIGO.

Bwana akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengine:

Mada Nyinginezo:

KWANINI WENGINE WANYAKULIWE,NA WENGINE WAACHWE?

USIMPE NGUVU SHETANI.

INJILI YA KRISTO HAITANGAZWI KWA HATI MILIKI.

IVUMBUE INJILI YA KRISTO KUTOKA KATIKA KILA JAMBO.

KWA KUWA NGUVU ZA MBINGUNI ZITATIKISIKA.

TUUTAZAME PIA MWISHO WA UJENZI WETU.

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 7 (Yeremia na Maombolezo)

Je! Ni kweli ubatizo wa maji hatuuhitaji tena?

Rudi Nyumbani:

Print this post

UVUMILIVU WA MUNGU ULIPOKUWA UKINGOJA.

Uvumilivu wa mungu ulipokuwa ukingoja, siku za nuhu


Jina la Bwana wetu Yesu libarikiwe. Nakukaribisha tulitafakari Neno la Mungu, ambalo ndio pekee lenye uwezo wa kuokoa roho za watu.

Ndugu yangu nataka ufahamu kuwa kuzimu inafananishwa na GEREZA kubwa sana lenye Malango na makomeo yake..Soma (Isaya 38:10 na Ayubu 17:6) utalithibitisha hilo..Haisemi mlango au komeo tu kana kwamba ni mmoja mmoja, hapana Bali ma-lango, ma-komeo, Hii ikiwa na maana kuna kifungo, na magereza mengi tofauti tofauti kulingana na aina ya dhambi za watu. Kama ukifa leo katika dhambi basi lipo lango lako uliloandaliwa na watu wa aina yako katika gereza lenu. Na huko sio kukaa tu, hapana kuna shida na mateso ya hali ya juu sana..Wote wanakaa huko wakisubiria siku ile ya hukumu wahukumiwe kisha ndio watupwe katika lile ziwa la moto.

Na gereza la juu kabisa ni lile la shetani na malaika zake, ambalo kwasasa wapo baadhi yao huko wamefungwa wakingojea kutupwa kwenye lile ziwa la moto siku ile ya mwisho itakapofika, japo wapo wengine baadhi yao duniani wakizunguka, ndio hawa wanaoiharibu dunia..

2Petro 2:4 “Kwa maana ikiwa Mungu hakuwaachilia malaika waliokosa, bali aliwatupa shimoni, akawatia katika vifungo vya giza, walindwe hata ije hukumu”;

Lakini leo nataka tujifunze jambo moja, ambalo pengine huwa tunalipitia kila siku lakini hatulielewi.. Na jambo lenyewe ni lile la Bwana Yesu kushuka kuzimu, na kuwaendea roho waliokaa kifungoni..Embu tusome..

1Petro 3:18 “Kwa maana Kristo naye aliteswa mara moja kwa ajili ya dhambi, mwenye haki kwa ajili yao wasio haki, ili atulete kwa Mungu; mwili wake akauawa, bali roho yake akahuishwa,

19 ambayo kwa hiyo aliwaendea roho waliokaa kifungoni, akawahubiri;

20 watu wasiotii hapo zamani, uvumilivu wa Mungu ulipokuwa ukingoja, siku za Nuhu, safina ilipokuwa ikitengenezwa; ambamo ndani yake wachache, yaani, watu wanane, waliokoka kwa maji”.

Utaona hapo, tukio lililofuata baada ya Kristo kufa msalabani lilikuwa ni kushuka kuzimu, na kwenda kuzitembelea hizi roho zilizokuwa vifungoni, lakini biblia haiwataji wafungwa wote, bali inatuonyesha watu Fulani tu, katika gereza Fulani mahususi, ambalo Bwana Yesu alikwenda kuwahubiria… Na hao si wengine Zaidi ya watu wa kipindi cha Nuhu..Sio kwamba hakuenda kwa wengine lakini kulikuwa na sababu kwa nini walilengwa watu wale…kwasababu na sisi ndio tunaofananishwa na kundi hilo..

Sasa huko kuhubiri kunakozungumizwa sio kwenda kuhubiriwa labda watubu au wageuke, hapana, kuhubiri kupo kwa aina nyingi, kutangaziwa hukumu nayo ni moja ya mahubiri, alikwenda kuwatangazia hukumu yao, ni kwanini wao wanastahili adhabu kubwa kuliko wote..

Na dhambi yao ilikuwa si nyingine Zaidi ya kupuuzia “Uvumilivu wa Mungu” uliokuwa ukilia juu yao siku baada ya siku..

Walipokuwa wanajua kabisa ni kweli dunia inakwenda kuangamizwa lakini wanafanya makusudi kushupaza shingo zao, wakiiona Safina ikijengwa, kwa muda wa miaka yote hiyo, walipokuwa wakihubiriwa na Nuhu kwa muda mrefu sana wa miaka 120 watubu waache dhambi zao lakini wanakataa..Wakimsikia Nuhu akiwaambia Mungu anawapenda, hataki hata mmoja aangamie, lakini wao wanaenda kinyume chake, wanaishi Maisha ya uovu, wanazini makusudi, walewa makusudi, wanafanya uchawi na ushirikina..wanasema huyo Mungu anayesema ataangamiza dunia mbona hatumwoni akiangamiza, kashakufa, wewe Nuhu acha ukichaa, wewe ni mvivu, hutaki kujishughulisha wewe unawaza tu mbinguni, na Maisha mwilini utaishije sasa, umaskini wa akili na ulimbukeni wa kifikra?..

Lakini siku ilipofika uvumilivu wa Mungu uliposema Basiii…Hakusalia hata mmoja..na wote moja kwa moja wakapelekwa katika gereza lao moja mahususi, lililokuwa limetengwa kwa ajili ya watu wa namna hiyo wanaostahili hukumu ya juu Zaidi..Na ndipo huko Kristo alipowafuata kuzimu..

Biblia inatuambia kama ilivyokuwa katika siku za Nuhu ndivyo itakavyokuwa siku za kuja kwake mwana wa Adamu, Siku za Nuhu watu walipuuzia wokovu, japokuwa walielezwa kuwa dunia inakwenda kuteketezwa lakini walitukana..Ndivyo ilivyo leo hii, dalili zote za kuja kwa Kristo zimeshatimia katika karne hii ya 20 na 21,..Na mojawapo ya dalili ya juu kabisa ni kutokea na kuongezeka kwa kasi kwa manabii wa Uongo na makristo wa uongo..mambo ambayo ukimuuliza hata mtu aliyekufa mwaka 90’, atakwambia jambo hilo hatujawahi kuliona wala kulisikia kama limeshawahi kutokea katika historia..Lakini sisi leo hii tunalishuhudia kwa macho yetu, lakini badala watu watubu wamgeukie Mungu, ndio kwanza wanatoa maneno ya kudhihaki…huyo Yesu mpaka leo miaka 2000 imepita hajaja amekufa..,mizaha, jina la Kristo linatajwa kiholela holela mpaka kwenye comedy …. wanaudharau uvumilivu wa Mungu…

Moja ya siku hizi, hii dunia itafika mwisho.. Na kibaya Zaidi tumeambiwa mwisho huo utakuja kwa ghafla sana. Hakuna mtu atayetazamia kama kweli huo ndio wakati wenyewe..kwasababu biblia inatuambia utakuja wakati wa amani..sio wakati wa vita..leo hii tunaishi katika hicho kipindi.. Na kama ikitokea umekufa katika hali ya dhambi, ukijua kuwa kila siku umekuwa ukikutana na mahubiri na injili zinazokuhubiria ugeuke lakini hutaki..basi ujue gereza lako litakuwa ni lile la hali ya juu Zaidi kuliko lile la watu wa Nuhu na lile la watu wa sodoma na Gomora.

Mathayo 11:20 “Ndipo akaanza kuikemea miji ile ambamo ndani yake ilifanyika miujiza yake iliyo mingi, kwa sababu haikutubu.

21 Ole wako, Korazini! Ole wako, Bethsaida! Kwa kuwa kama miujiza iliyofanyika kwenu ingalifanyika katika Tiro na Sidoni, wangalitubu zamani kwa kuvaa magunia na majivu.

22 Walakini nawaambieni, itakuwa rahisi Tiro na Sidoni kustahimili adhabu zao siku ya hukumu kuliko ninyi. 23 Nawe Kapernaumu, je! Utakuzwa mpaka mbinguni? Utashushwa mpaka kuzimu; kwa kuwa kama miujiza iliyofanyika kwako ingalifanyika katika Sodoma, ungalikuwapo mji huo hata leo.

24 Walakini nawaambieni, itakuwa rahisi nchi ya Sodoma kustahimili adhabu yake siku ya hukumu kuliko wewe”.

Ukiona kwanini dunia mpaka dakika hii haijateketezwa, ujue kuwa sio kwamba Mungu anafurahia ulawiti wako, au uzinzi wako, au ulevi wako, au uvaaji vimini vyako, ni kwasababu uvumilivu wake unakungoja utubu, ili usiingie katika adhabu kuu ya siku ile.

Kama bado unasua sua, au upo vuguvugu ni wakati sasa wa kuanza kuyatengeneza mambo yako sawa na Mungu wako..Usijivunie dini au dhehebu,..wakati tuliopo ni wakati wa kuutafuta uhusiano wako binafsi na Mungu wako. Jiulize je! Ikiwa unyakuo utapita leo nitakuwa na uhakika wa kwenda na Bwana..Je! nikifa leo nitakuwa na uhakika wa kwenda mbinguni, au kwenye haya magereza ya milele nikiteseka huko usiku na mchana..

Watu wa kizazi chetu hichi ni watu ambao tumewekewa thawabu kubwa Zaidi kama tukishinda(Ufunuo 3:21)..Lakini pia tuzimbea na kuichezea neema tumeahidiwa adhabu iliyo kubwa zaidi kuliko wote waliotutangulia.. Hivyo uamuzi ni wetu sisi, Uzima au Mauti. Lakini sisi tunaopenda Maisha tutachagua uzima ambao unaletwa na Yesu Kristo tu peke yake,kwa kumwamini yeye na kujitwika misalaba yetu kila siku na kumfuata.

uvumilivu wa Mungu ni upendo kwetu.

Ubarikiwe.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312

Maran Atha.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengine:

Mada Nyinginezo:

VIFUNGO VYA GIZA VYA MILELE.

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

Kwanini yule mtu hakukutwa na vazi la arusi wakati alialikwa?

Kuna ufufuo wa aina ngapi?

WANA WA MUNGU, NA BINTI ZA WANADAMU.

 

MWISHO WA HAO WAMSAHAUO MUNGU.

KWA VILE ALIVYOKUWA MTU WA HAKI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

IVUMBUE INJILI YA KRISTO KUTOKA KATIKA KILA JAMBO.

Shalom..Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe…

Karibu tujifunze biblia…

Katika biblia kama wengi wetu tujuavyo…Kuwa maisha yanahubiri Injili, kadhalika vitu vya asili vinahubiri Injili…maana yake Mtu akijaliwa hekima mno kwa kuvisoma tu vitu vya asili anaweza kupata ufunuo mkubwa sana wa vitu vya ufalme wa Mbinguni..

Tukimwangalia kama Bwana wetu Yesu Kristo, kila mahali alikuwa anasema ufalme wa mbinguni umefanana na hiki au kile…Utaona kuna sehemu anasema

“ufalme wa mbinguni umefanana na mtu aliyepanda mbegu njema katika konde lake;

lakini watu walipolala, akaja adui yake akapanda magugu katikati ya ngano, akaenda zake.

Baadaye majani ya ngano yalipomea na kuzaa, yakaonekana na magugu. Mathayo 13:24-26”..

Sehemu nyingine anasema Ufalme wa mbinguni umefanana na mpanzi aliyetoka kwenda kupanda mbegu zake, nyingine ziliangukia njiani ndege wakazila, nyingine kwenye miamba, nyingine kwenye miiba na nyingine kwenye udongo mzuri.. Maana yake ni kwamba kumbe hata katika ulimaji na upandaji kuna injili ya Kristo mule.. kwamba inahitajika hekima kiuvumbua.

Hata jinsi wezi wanavyovunja usiku na kuiba..kuna injili ndani yake…(Bwana Yesu alilifananisha tukio la kuja kwake na tukio la wizi usiku wa manane wakati tulalapo)…Hata katika mafisadi kuna injili ndani yake (kasome Luka 16:1-12)..Hivyo inahitajika hekima ya kiMungu kuivumbua bila kuiga mabaya hao.

Vivyo hivyo ukirudi katika miti kuna injili(Mathayo 13:31-32), katika ndege kuna injili (kasome Mathayo 6:26)..katika mapishi kuna injili (kasome Mathayo 13:33)..katika kufanya biashara kuna injili (Mathayo 13:45)…katika wavuvi kuna injili (kasome Mathayo 13:47)….katika kutafuta Ajira kuna injili pia (soma Mathayo 20:1-10).

Kadhalika katika kuoa na kuolewa na kualikwa katika harusi kuna injili (kasome Mathayo 22:1-13)..

Kwahiyo utaona karibia kila kitu kinahubiri Injili…Hakuna kitu hata kimoja kisichohubiri Injili…Inahitajika tu hekima kupata fundisho au funzo la kiMungu katika kila kitu.. Na ndio maaana mtu kama Sulemani Mungu alimpa hekima nyingi ya kufahamu kanuni za ki-Mungu duniani kwasababu alitazama karibu kila kitu kwa jicho la kumwona Mungu ndani yake, ndipo Hekima ikaingia ndani yake..

1Wafalme 4:32 “Naye akanena mifano elfu tatu, na nyimbo zake zilikuwa elfu moja na tano.

33 Akanena habari za miti tangu mwerezi ulioko Lebanoni hata hisopo umeao ukutani; pia akanena habari za wanyama, na za ndege, na vitambaavyo, na samaki.

34 Wakaja wa mataifa yote ili waisikie hekima ya Sulemani, toka wafalme wote wa ulimwengu, waliokuwa wamepata habari za hekima yake”.

Hivyo huu sio wakati wa kulala tena bali wakati wa kumwomba Roho Mtakatifu atufungue macho ya rohoni tuweze kuielewa injili inayojihubiri yenyewe katika kila kitu na kuifanyia kazi…Tukiwatazama ndege na wanyama hatuoni wanyama mashoga wala wasagaji hiyo ni injili ikitufundisha kuwa usagaji na ushoga si mpango wa Mungu..ni machukizo mbele za Bwana Yesu.

Tv tulizonazo, internet pamoja na simu zinatuhubiria Injili…Leo hii tukio dogo tu likitokea katika kijiji Fulani ndani sana kwa kupitia simu za mkononi..ndani ya dakika chache sana litaweza kuwa limeshamfikia hata Raisi wa nchi…ikifunua kuwa hata mtu chochote anachokifanya akiwa hapa duniani ndani ya muda mfupi sana kitakuwa kimeshamfikia Mungu wa mbingu na nchi..

Mahakama zinahubiri Injili..kama mtu akikutwa na kosa ambalo linamfanya asiendelee kukaa katika jamii yake tuchukue mfano labda kaua…cha kwanza atakamatwa na mapolisi, na kupelekwa mahabusu, kabla ya kuhukumiwa kisha atapandishwa kizimbani mahakamani kusomewa hukumu yake na baada ya hapo magereza..atakaa huko bila kurudia maisha yake ya asili kwa kipindi cha chote cha maisha yake..

Na hukumu ya Mungu mwenyezi ndio ipo hivyo hivyo…

Leo hii mtu akifanya dhambi hata zikamfikia Mungu, na alishaonywa na hataki kutubu anaendelea tu kufanya kwa makusudi…mtu Yule atakufa katika dhambi zake..hapo ni sawa na amekamatwa, na moja kwa moja atapelekwa jehanamu/kuzimu kafungwa huko…ambapo ni mfano wa mahabusu(magereza ya kitambo)…atakaa huko kwa kipindi Fulani akingoja siku atakayopandishwa mbele ya kiti cheupe cha Hukumu cha Mungu mwenyezi..ambapo atahukumiwa kulingana na matendo yake na kasha kutupwa katika lile ziwa la moto ambalo linafananishwa na magereza ya milele katika mazingira ya dunia yetu.

Mambo yote tukiyatafakari kwa jicho hilo..hatutaendelea kuuchukulia wokovu wetu kama ni jambo si la kuchezea bali tutauheshimu na kuushikilia sana kwa maana ni kitu cha thamani tulichopewa. Hizi ni nyakati za mwisho.

Bwana atusaidie sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengine:

Mada Nyinginezo:

INJILI KULINGANA NA TEKNOLOJIA

Mbona Mungu anaruhusu watu wapate shida, ilhali ana uwezo wa kutuepusha?

LOLOTE ATAKALOWAAMBIA FANYENI.

Kwanini Bwana Yesu, aliruhusu yale mapepo yawaingie nguruwe?

JIHADHARI NA KUOSHWA MIGUU ISIVYOPASWA.

UFALME WA MUNGU HAUPATIKANI KIRAHISI.

Je! Ni kweli ubatizo wa maji hatuuhitaji tena?

UBATILI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

SAKRAMENTI NI NINI, NA JE! IPO KATIKA MAANDIKO?

Kulingana na kanisa Katoliki Sakramenti Ni ishara ya wazi ionekanayo, ya neema isiyoonekana, iliyofanywa na Yesu Kristo mwenyewe, itumike kutuletea au kutuongezea neema mioyoni mwetu.

Yaani kwa lugha nyepesi ni ishara za nje zionekanazo zilizobeba neema ya wokovu,  zilizofanywa  kwanza na Bwana Yesu, ambazo tukizifanya na sisi zitatuongezea neema moyoni mwetu ya kumkaribia Mungu Zaidi.

“Kulingana na kanisa Katoliki SAKRAMENTI hizi zipo saba (7), Nazo ni:

Ubatizo:

Kwamba kila mtu anayekuja katika ukristo ni sharti aupokee ubatizo, haijalishi ni Watoto wachanga, au vijana,au watu wazima, hawana budu kuupokea ubatizo. Ni ishara ya nje ya kuingizwa katika imani ya kikristo. Hii ni sakramenti ya kwanza.

Kipaimara:

Kipaimara ni Neno lenye maana ya “uthibitisho”. Kulingana na imani ya kikatoliki, ubatizo peke yake hautoshi, unahitaji kukamilishwa na tendo lingine la kipaimara kwa kuwekewa mikono. Hivyo Siku ambayo mtu huyo anapokea kipaimara hicho huwa anapakwa mafuta ya kunukia kwenye paji la uso wake yajulikanayo kama KRISMA, kama ishara ya kutiwa muhuri kuwa mtu huyo ni milki halali ya Bwana, kufuatana na andiko hili (Yohana 6:27). Hii ndiyo sakramenti ya pili.

Ekaristi Takatifu:

Kushiriki meza ya Bwana. Kuula mwili wa Bwana na damu yake.. (1Wakorintho 11:23-25). Kama vile Bwana Yesu alivyowaagiza wanafunzi wake wafanye vile kwa ukumbusho wake.

Mpako Mtakatifu:

Hii ni ibada maalumu kwa ajili ya wagonjwa kama ilivyofanywa na mitume kwa agizo la Yakobo (Yakobo 5:14) ..Mathayo 10:1, Marko 6:3…Hii nayo ni moja ya sakramenti ya Bwana.

Kitubio:

Inahusisha kuungama dhambi, na hii ni lazima uende mbele za Padri na kuzikiri dhambi zako mbele zake, na yeye atakuombea na dhambi zako zitaondolewa kama agizo ambalo Kristo aliwapa mitume wake..(Yohana 20:23).

Daraja Takatifu:

Uteuzi wa Vyeo katika kanisa..kama vile ukasisi, ushemasi, na uaskofu.Kama vile jinsi Bwana Yesu alivyowachagua mitume wake,.Na vivyo hivyo uteuzi katika kanisa ufanyike katika kuliongoza kundi, hiyo inafuatana na kuteuliwa na kuwekewa mikono na askofu wa jimbo.

Ndoa;

Ndoa ya wakristo ni sakramenti ya Yesu na kanisa lake. Ufunuo 21;9..Kama vile Kristo alivyoona na kanisa lake, vivyo hivyo ndoa inafunua sakramenti hiyo.

  • Kulingana na imani ya katoliki Sakramenti tatu za kwanza ni za kumuingiza mtu katika Ukristo.
  • Sakramenti mbili zinazofuata ni za uponyaji wa roho na mwili.
  • Sakramenti mbili za mwisho ni za kuhudumia ushirika katika kanisa na katika familia iliyo kanisa dogo.

Lakini Je! Maagizo haya yote ni ya kibiblia na Je ni lazima kila mkristo ayafuate ili apokelewa na Mungu?..

Ukweli ni kwamba agizo la ubatizo ni agizo la msingi katika Imani, lakini ubatizo unakuja kwa mtu aliyetambua kwanza kuwa yeye ni mwenye dhambi na hivyo anahitaji KUOKOLEWA. Hapo ndipo anapotubu na kwenda kubatizwa kwa hiari yake mwenyewe. Lakini mtoto mchanga hajatambua bado  jema na baya, wala yeye mwenyewe hajitambui hivyo ubatizo kwake hauna maana.. wao wanawekewa tu mkono, kama wakfu kwa Bwana. Lakini sio kubatizwa.. Hivyo suala la ubatizo kwa vichanga ni batili.

Ubatizo sahihi ni upi?

Kwahiyo ubatizo sahihi ni ule wa kujimbua kwanza, wewe ni mwenye dhambi na kwamba unahitaji kuokolewa, vile vile ni sharti uwe wa maji tele sawasawa na Yohana 3:23, Na uwe kwa jina la Yesu Kristo sawasawa na maandiko haya (Matendo 2:38, 8:16, 10:48, 19:5), ubatizo mwingine nje ya hapo ni batili kulingana na biblia, hivyo kama ulibatizwa tofauti na hapo unahitaji kwenda kubatizwa tena.

Vilevile Watoto wachanga ni kweli wanapaswa wawekewe mikono kama mbaraka kutoka kwa Bwana. Sawasawa na Bwana Yesu alivyofanya (Mathayo 19:14-15)..Lakini sio kwenda kupitia mafundisho Fulani ya mapokeo kwanza mwaka mzima na ndipo baadaye aje kuwekewa mikono na askofu au Padre..Agizo hilo halipo kwenye maandiko.

Utumizi wa mafuta.

Halikadhalika, utumizi wa mafuta kwa ajili ya kuombea wagonjwa si jambo la kuliundia kanuni..kwasababu sio mafuta yanayomponya mtu bali kinachoweza kumponya mtu ni damu ya Yesu tu peke yake. Kwasababu biblia imetuambia..yoyote tufanyayo tufanye yote kwa jina la YESU Kristo. (Matendo 4:12)

Na mwisho kabisa, kuwekewa mikono kwa ajili ya utumishi na waliokutangulia kwenye Imani ni jambo jema lakini pasipo hilo haimaanishi kuwa huwezi kutumika katika kuifanya kazi ya Mungu sawasawa na wale wengine. Ikumbukwe kuwa mitume 12 walichanguliwa kweli na Bwana Yesu Kristo, wakaishi naye, wakala naye, wakapewa agizo naye.Lakini biblia inatuambia Mtume Paulo alitenda kazi Zaidi ya hao wote, na yeye hakuwa miongoni mwa wale 12, wala hakuwahi kutembea na Yesu duniani,.

Utume wetu unathibitishwa na Roho Mtakatifu ndani yetu. Ni vema kumtafuta Roho Mtakatifu, kuliko kutafuta vyeo. Kwasababu yeye ndiye anayewatia nguvu wateule wake katika kumtumikia. Hata wewe Bwana anaweza kukufanya kuwa mtumishi wake, endapo tu utatii na kuwa mwaminifu kwa kila anachokulekeza kukifanya.

Hivyo ndugu, toka katika kamba za udini, na kamba za mapokeo, ambazo nyingi ya hizi zinakufunga usiomwone Mungu katika utimilifu anaotaka. Rudi kwenye Neno. Penda kujifunza kusoma biblia peke yako huku ukimwomba Roho Mtakatifu akusaidie. Penda pia kujifunza sehemu mbalimbali, na Roho Mtakatifu atakusaidia kuchagua kilicho sahihi na kutupa kisichosahihi, kwasababu ndiyo kazi yake hiyo Yesu aliyosema amemtuma duniani kwayo..(Yohana 16:13)

Je umeokoka?

Je! Unajua kuwa tunaishi katika kanisa la mwisho la saba lijulikanalo kama LAODIKIA, na UNYAKUO upo karibu..Siku yoyote wateule watotoweka na kwenda mbinguni kwa BABA..? Kama hujafanya hivyo ni heri ukamgeukia Mungu wako sasa, kwasababu muda tuliobakiwa nao ni mchache kabla PARAPANDA haijalia. Kama upo tayari kutubu dhambi zako leo na kusema nataka leo hii Bwana Yesu aanze kutembea na mimi maishani mwangu..

Basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie maisha yako yote kama ilivyokuwa hata kwetu sisi. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU  MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.

AMEN.

Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.

Ubarikiwe sana

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengine:

Mada Nyinginezo:

Nini maana ya Kipaimara?..Na je! Ni jambo la kimaandiko?

Je! Ni kweli ubatizo wa maji hatuuhitaji tena?

UNYAKUO.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

KWANINI WENGINE WANYAKULIWE,NA WENGINE WAACHWE?

JINSI ITAKAVYOKUWA KATIKA SIKU ILE

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!

Rudi Nyumbani:

Print this post