Filipo na Nathanaeli, walikuwa ni marafiki wa karibu sana, wote wawili maisha yao yalikuwa ni maisha ya kuifuata dini, wakichunguza habari za Masihi na kuja kwake, Walikuwa ni watu wa kusoma torati na maandiko yote yanayomuhusu Masihi, maisha yao kwa muda mrefu yalikuwa ya namna hiyo, pengine walikuwa wanakutana kila siku au kila wiki, kuzungumza habari za masihi na kuja kwake, kutakuwa kwa namna gani, pengine wanasema, akija ataiokoa Israeli kutoka kwenye mikono ya maadui zao kwa kipindi kifupi sana, au akija ataifanya dunia kuwa na amani, au akija ufalme wake utakuwa ni mkuu sana n.k…
Waliishi maisha ya kutamani kumwona Masihi akija katika kipindi chao, mpaka siku moja ndoto ya Filipo inapokuja kuwa kweli akiwa katika kuzunguka zunguka kwake anakutana na mtu mmoja aliyeitwa YESU, halafu mtu huyo akamwambia Nifuate!..Filipo kumwona tu na kuona mambo aliyokuwa anayafanya moyo wake ulimwambia huyu ndiye..
Ndipo kwa furaha, hata bila kumwaga aliyemwita, pengine akasema moyoni mwake habari hii ni lazima imfikie rafiki yangu wa karibu ambaye maisha yake yote naye yalikuwa kama ya kwangu kutazamia tumaini la Israeli, ndipo akaenda kumtafuta Nathanieli kwa bidii mjini, akizunguka mtaa kwa mtaa, jaribu kufikiria pengine alikuwa na marafiki zake wengi na ndugu wengi lakini aliwapita wote na kwenda kumtafuta mmoja tu, ambaye ni Nathanaeli..Rafiki yake ambaye alijua tu akizisikia habari hizo moyo wake utaruka ruka kwa furaha, mtu ambaye, amekuwa na moyo wa kutaka kujifunza, asiyeshikiliwa na mapokeo ya kidini, asiye na hila, aliyetayari kugeuka anapoujua ukweli,.
Japokuwa Filipo alijua Masihi kulingana na maandiko hatokei Nazareti bali Bethlehemu ya Uyahudi, lakini hakusita kwenda kumpelekea habari hizo rafiki yake Nathanaeli kwasababu alimjua naye pia ni mtu msikiaji sikuzote ni mtu asiyekuwa hila moyoni mwake. Ni mtu ambaye yupo tayari kujifunza jambo jipya na kama ni kweli atalifuata kwa moyo wote bila kusita-sita,..
Sasa wakati Nathanaeli akiwa sehemu Fulani chini ya mtini, ghafla Filipo anatokea na habari ya kwanza anayomueleza inahusiana na ile ile habari ya siku zote ya Masihi.. Nathanaeli akiwa anamsikiliza kwa makini sana na kwa shauku, akamuuliza yuko wapi?
> Yupo Nazareti..Filipo akajibu.
Yohana 1:43 “Siku ya pili yake alitaka kuondoka kwenda Galilaya, naye akamwona Filipo. Yesu akamwambia, Nifuate.
44 Naye Filipo alikuwa mtu wa Bethsaida, mwenyeji wa mji wa Andrea na Petro.
45 Filipo akamwona Nathanaeli, akamwambia, Tumemwona yeye aliyeandikiwa na Musa katika torati, na manabii, Yesu, mwana wa Yusufu, mtu wa Nazareti”.
> Nathanieli akamuuliza..
Yohana 1:46 “…Laweza neno jema kutoka Nazareti? Filipo akamwambia, Njoo uone”.
Je! Inawezekana Masihi akatokea Nazareti kweli? Maandiko si yanatuambia atatokea Bethlehemu?…Filipo akasema hatuna haja ya kuongea mengi, wewe ni mtu ambaye ukiona ukweli upo tayari kubadilika twenda ukajionee..? Kwakuwa Nathanaeli alijijua kuwa yeye ni mtu ambaye si kasuku-wa-kidini asiye na hila ndani yake, akaondoka na Filipo kwa moyo mmoja, kwenda kuyahakiki hayo anayoyasema, kuangalia yamkini ndoto zake zinaweza kutimia kwa hayo aliyoyasikia….
Na alipofika tu na kukutana Na Bwana YESU mwenyewe tunaona habari ya kwanza ilikuwa ni hii:
Yohana 1:47 “Basi Yesu akamwona Nathanaeli anakuja kwake, akanena habari zake, Tazama, Mwisraeli kweli kweli, hamna hila ndani yake”.
Ndipo Nathanaeli akashtuka akajiuliza huyu mtu amewezaji kunijua kuwa Ndani yangu hakuna Hila?..Na mimi sijawahi kumwona hata siku moja, wala yeye kusikia habari zangu, kwanza anapokaa na mimi ninapokaa ni mbali, amewezaji kujua asili yangu ya rohoni..
> Ndipo Nathanaeli akamuuliza tena:
Yohana 1:48 “…. Umepataje kunitambua? Yesu akajibu, akamwambia, Kabla Filipo hajakuita, ulipokuwapo chini ya mtini nilikuona”.
Akashangaa tena, mahali ambapo Filipo alimpata kwa shida, Huyu Yesu ambaye alikuwa hanijui alikuwa ananiona pale, basi ataachaje kujua na mambo yangu mengine yote yaliyobakia.? Hakika huyu ndiye Masihi, Mwana wa Mungu, Mfalme wa Israeli..Sihitaji kujua zaidi ya hapo ndani yangu hamna hila,”
Moja kwa moja Nathanaeli, akaamini na kusema.
Yohana 1:49 “…Rabi, wewe u Mwana wa Mungu, ndiwe Mfalme wa Israeli”.
> Ndipo Yesu akamwambia…
Yohana 1:50 “…., Kwa sababu nilikuambia, Nilikuona chini ya mtini, waamini? Utaona mambo makubwa kuliko haya”.
Mwisho wa maneno yale Bwana Yesu akawaambia mitume wake…
Yohana 1:51 “Akamwambia, Amin, amin, nawaambia, Mtaziona mbingu zimefunguka na malaika wa Mungu wakikwea na kushuka juu ya Mwana wa Adamu”.
Unaona waliahidiwa kuyaona na makubwa zaidi ya yale waliyoyaona, lakini hiyo yote ni kwasababu waliamini katika vidogo, walikuwa tayari kumfuata Yesu kwa udhihirisho mdogo sana, hiyo ndio maana ya kutokuwa na HILA ndani yao..Na kwasababu hiyo waka ahidiwa kuonyeshwa na makubwa zaidi ya yale..kwamba siku zitakuja wataziona mbingu zimefunguka na maelfu kwa maelfu ya malaika wakishuka juu na kupanda juu yake ..Yaani kwa namna nyingine watafunuliwa utukufu wa Bwana Yesu kwa viwango vya juu sana..
Mtume Yohana, alifunuliwa sehemu ya utukufu huo, na ndio tunasoma katika kitabu chote cha ufunuo, Vivyo hivyo na mitume wengine walifunuliwa kwa sehemu zao ni kwa vile habari zao kila mmoja haziwezi kuandikwa kwenye biblia yote, lakini katika maisha yao yote ya huduma walikuwa wakiuna utukufu wa Yesu tofauti na hapo walipokuwa wanauona mwanzo.
Ukiachia mbali siku ile alipofufuka na siku ile walipomwona akichukuliwa na mawingu juu. Na siku ile alipokuwa akiomba mpaka malaika akatokea kumtia nguvu (Luka 22:43)
Ndugu YESU KRISTO, si kama wengi tunavyomfikiria leo hii, Mungu hajatufunuliwa makubwa yamuhusuyo kwasababu ya HILA iliyopo ndani yetu, tunaona ishara na miujiza na kazi zake nyingi anazozitenda lakini bado hatuwi tayari kumfuata kwa mioyo yetu yote kama vile mitume walivyofanya..tunategemea vipi ajifunue kwetu. Tukiambiwa tujikane nafsi tumfuate Bwana tunasema kufanya hivyo sio lazima…tukiambiwa twende tukabatizwe, ubatizo sahihi wa kimaandiko tunasema dhehebu letu halitufundishi hivyo? Hizo ndio hila zenyewe, tukiambiwa tusivae vimini na suruali na ma-hereni tunasema imeandikwa wapi kwenye biblia, hizo ndizo hila, ambazo zitatukwamisha tusimfuate YESU,..
Nathanaeli alifahamu kabisa kuwa Masihi ni lazima atokee Bethlehemu lakini aliposikia yupo Nazareti hakujifanya anajua, bali alikwenda kumsikiliza na baadaye ndipo alipojua kuwa ni kweli Bwana Yesu alizaliwa Bethelemu..Vivyo hivyo si kila jambo ulibishie tu kwa mara ya kwanza unapohubiriwa, Ondoa hila ndani yako na utii, mfuate kwanza Yesu na yeye mwenyewe kwa Roho wake mtakatifu atakafunulia kuwa hicho unachokifanya sasahivi ni sahihi au sio sahihi. Usiwe mtu mkaidi.
Yule ni Mfalme Mkuu sana, malaika wanamsujudia usiku na mchana huko mbinguni, ameketi sehemu ambayo kiumbe chochote hakiwezi kufikia, lakini pamoja na uweza wake, na nguvu zake nyingi namna hiyo, bado anatupenda na kujishughulisha na watu wanyonge kama sisi. Sasa kiburi cha nini mbele zake?
Kwanini leo hii usimkaribishe huyu Mfalme Mkuu ndani yako, ayageuze maisha yako?. Kama aliweza kufanya kwa Filipo na Nathanaeli, atafanya na kwako, kwasababu yeye ni Yule Yule jana na leo na hata milele..Unachopaswa kufanya ni kumfungulia mlango tu, na muujiza mkubwa utaanza kuona akiufanya katika maisha yako.
Kama upo tayari kufanya hivyo sasa. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.
EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI, NAYE NDIYE MFALME ATAKAYEKUJA. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.
ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.
AMEN.
Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo. Ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo kuanzia sasahivi, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.
Fanya kwanza hayo na YESU KRISTO ataanza kutembea na wewe katika maisha yako kwa namna ya ajabu sana.
Ubarikiwe.
Tafadhali share na wengine ujumbe huu.
Mada Nyinginezo:
MTUMAINIE YESU ASIYEISHA MATUKIO.
RABONI!
KWANINI YESU KRISTO NI MWANA WA DAUDI?
BASI MUNGU AKAMUADHIMISHA SANA..
YESU MPONYAJI.
KIWANGO CHA TATU CHA IMANI.
TULICHUNGUZE UMBO LA YESU NA MWENENDO WAKE.
LITANIA YA BIKIRA MARIA JE! NI SALA YA KIMAANDIKO?
Neno la Mungu linasema katika …
Warumi 14:10 “……. Kwa maana sisi sote tutasimama mbele ya kiti cha hukumu cha Mungu.
11 Kwa kuwa imeandikwa, Kama niishivyo, anena Bwana, kila goti litapigwa mbele zangu; Na kila ulimi utamkiri Mungu.
12 Basi ni hivyo, KILA MTU MIONGONI MWETU ATATOA HABARI ZAKE MWENYEWE MBELE ZA MUNGU”.
Siku ya hukumu inakuja..Ambapo kila mtu atatoa habari zake mwenyewe atasimama mbele ya kiti cha hukumu na kuhukumiwa iwe ni mtakatifu, iwe ni mwenye dhambi…Mhubiri 3:17 “Nikasema moyoni mwangu, Mungu atawahukumu wenye haki na wasio haki..”
Hukumu ya watakatifu itakuwa tofauti na hukumu ya wenye dhambi..Watakatifu hawatahukumiwa kwa lengo la kuadhibiwa, bali ajili ya thawabu. Aliyekuwa mwaminifu Zaidi atapewa thawabu nyingi Zaidi na aliyekuwa mwaminifu kidogo atalipwa kidogo. Lakini ambaye hakuwa mwaminifu kabisa huyo atahukumiwa adhabu ya kutupwa katika ziwa la moto pamoja na wenye dhambi.
Na wale walio waovu sana watahukumiwa Zaidi kuliko hao wengine.
Luka 12:47 “Na mtumwa yule aliyejua mapenzi ya bwana wake, asijiweke tayari, wala kuyatenda mapenzi yake, atapigwa sana.
48 Na yule asiyejua, naye amefanya yastahiliyo mapigo, atapigwa kidogo. Na kila aliyepewa vingi, kwake huyo vitatakwa vingi; naye waliyemwekea amana vitu vingi, kwake huyo watataka na zaidi”.
Na miongoni mwa watakaohukumiwa kutupwa katika ziwa la moto, kila mmoja atahukumiwa kulingana na matendo yake..Ufunuo 20:13 “Bahari ikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake; na Mauti na Kuzimu zikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake. Wakahukumiwa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake”
Ufunuo 2:23 “Na makanisa yote watajua ya kuwa mimi ndiye achunguzaye viuno na mioyo. Nami nitampa kila mmoja wenu kwa kadiri ya matendo yake.
Siku hiyo kama vile mwezi unavyoangaza watu wote wakiuona juu..ndivyo itakavyokuwa siku hiyo Maisha ya kila mtu yataangazwa tangu anazaliwa mpaka anakufa, siku moja baada ya nyingine, lisaa limoja baada ya lingine, dakika moja hadi dakika nyingine..mambo yote aliyoyafanya na kuyawaza kwa wazi na kwa siri yatawekwa hadharani. Na kila Neno na tendo litapimwa…Na kutakuwa na kuulizwa maswali kwanini ulifanya hivi au kwanini ulifanya vile, ulikuwa na lengo gani la kufanya vile. Na kila tendo na Neno litapimwa na kuangaliwa lilileta hasara kiasi gani katika ufalme wa Mbinguni..Na kila mtu atatoa habari zake mwenyewe, atatoa hesabu na sio maelezo..Kuna tofauti ya kutoa hesabu na kutoa maelezo..Biblia inasema hivyo..
Mathayo 12: 36 “Basi, nawaambia, Kila neno lisilo maana, watakalolinena wanadamu, watatoa hesabu ya neno hilo siku ya hukumu.
37 Kwa kuwa kwa maneno yako utahesabiwa haki, na kwa maneno yako utahukumiwa”.
Siku hiyo hakutakuwa na mtu mwingine pembeni kukusaidia kuzungumza…utazungumza wewe mwenyewe…sababu ya wewe kunena yale maneno ya matusi ni ipi, sababu ya wewe kuwa mwizi ni ipi, sababu ya wewe kuzungumza yale maneno ya makufuru ni ipi. Utatoa hesabu ya neno moja baada ya lingine, halitarukwa hata moja..Hata yale mambo ya siri ambayo unadhani hakuna mtu angeweza kuyajua..yatawekwa wazi siku ile.
Luka 12:2“ Lakini hakuna neno lililositirika ambalo halitafunuliwa, wala lililofichwa ambalo halitajulikana
3 Basi, yo yote mliyosema gizani yatasikiwa mwangani; na mliyonena sikioni mwa mtu katika vyumba vya ndani, yatahubiriwa juu ya dari”.
Ndugu Kama hujamkabidhi Yesu Kristo Maisha yako..Ni vyema ukafanya hivyo sasahivi..Mkabidhi yeye Maisha yako..si tu kwasababu hutaki kwenda hukumuni bali pia kwasababu unahitaji wokovu..Wokovu ni wa lazima kwa kila mtu, kama unapenda kweli Maisha basi utatamani kuishi milele..Na umilele huo haupo kwa mwingine zaidi ya Yesu kristo. Lakini usipomkubali Yesu Kristo leo, na kufuata mapenzi ya wazazi wako, au ndugu zako, au marafiki zako, au jamii yako..Nataka nikukumbushe tena na tena siku ile utasimama wewe peke yako.
Ukisoma Amri zote za Mungu, na kila mahali anapotoa maagizo yake, pote ni kama anazungumza na mtu mmoja mmoja…pote utaona anasema usiibe, usizini, usiabudu miungu mingine(Kutoka 20)…na hasemi msiibe, msizini au msiue..hutaona hicho kitu sehemu nyingi kwenye biblia..kasome kumbu 28 …..Hiyo yote ni kuonyesha kuwa maagizo ya Mungu anatoa kwa mtu mmoja..haijalishi hapo anapotoa hayo maagizo wapo watu wengi kiasi gani….anakupa maagizo wewe kama wewe na mimi kama mimi (anashughulika na mtu mmoja mmoja)…Sio mimi na mjomba wangu au na dada yangu…hapana mimi kama mimi..kwasababu siku ile nitakuwa peke yangu…Nitatoa habari zangu mwenyewe mbele ya kiti cha hukumu…
Biblia inazidi kusema katika..
Wagalatia 6:5 “Maana kila mtu atalichukua furushi lake mwenyewe”.
Hivyo leo hii kata shauri na kusema nimeamua kumfuata Yesu kwa gharama zozote zile mimi kama mimi peke yangu..Jitwike msalaba wako na jikane nafsi, kama ulikuwa unavaa vimini, na suruali kazichome moto sasahivi usitazame Rafiki zangu watanionaje, ndugu zangu waliozoea kuniona navaa hivyo vitu wananionaje usitazame kushoto wala kulia wala usitafute ushauri kwa mtu yoyote…
Kumbuka siku ile utakuwa peke yako..ulikuwa unaweka make-up katupe sasahivi vipodozi vyote, ulikuwa mlevi kamwage hizo pombe kwenye friji yako kama zipo, ulikuwa mvutaji wa sigara unaacha kwa vitendo, ulikuwa mwasherati unaacha, simu yako ilikuwa umeijaza nyimbo na video za kidunia zifute zote sasahivi na mambo mengine yote maovu unayavua leo. Na kisha piga magoti mwambie Bwana nimetubu! kwa vitendo kuanzia leo hayo mambo nimeacha..Na atakusamehe kwasababu yeye ni mwingi wa huruma na Rehema…na kuna amani ya ajabu itaingia ndani yako saa hiyo hiyo baada ya kuacha hayo mambo..Hiyo Amani itakayoingia ni uthibitisho wa msamaha wako.
Hivyo usimzimishe Roho, haraka sana tafuta kanisa la kweli la Kristo lililo karibu na wewe au mtu yoyote wa Mungu ambaye yupo karibu na wewe atakusaidia.. Na jifunze kusoma Neno la Mungu mwenyewe na kutafuta ubatizo sahihi, na Roho Mtakatifu atakusaidia kukuongoza na kukutia katika kweli yote ya kimaandiko..wala hatakuacha mguu wako upotee njia hata siku moja, atakuwa pamoja na wewe hata ukamilifu wa dahari kama alivyosema katika Neno lake.
Bwana akubariki.
Tafadhali share na wengine.
Mada Nyinginezo:
Kuna hukumu za aina ngapi?
Jehanamu ni nini?
MBINGUNI NI WAPI?
BONDE LA KUKATA MANENO.
USIPOKUWA MWAMINIFU, NAFASI YAKO ITACHUKULIWA.
MAUTI YA PILI NI NINI?
JIHADHARI NA KUOSHWA MIGUU ISIVYOPASWA.
Tukisoma kitabu cha Matendo ya mitume tunaona kikizungumza habari za matendo ya kishujaa yaliyofanywa na mitume wa Bwana, jinsi walivyofanya bidii kuieneza injili ya Kristo ulimwenguni kote, lakini pamoja na hayo biblia inatueleza pia yapo makosa yaliyofanywa nao wao katika huduma zao, Na lengo la Mungu kuruhusu yaandikwe ni ili kutufunza sisi nasi tusije tukayarudia makosa yale yale yaliyofanywa na wao katika utumishi wetu.
Sasa kama wewe ni msomaji mzuri wa biblia utakumbuka kuna wakati Mtume Petro alianza kutoka kidogo na msingi wa Imani Kristo aliompa kwa kuwaagiza watu wa mataifa mambo ambayo si sahihi wao kuyafanya, na huku akijua kabisa ukweli kwamba anachokifanya sio sawa, lakini alifanya vile kwa unafki ili tu kuwapendezesha wayahudi, Na mtume Paulo alipoligundua hilo alimkemea mbele ya wote..Tusome.
Wagalatia 2:11 ‘Lakini Kefa alipokuja Antiokia, nalishindana naye uso kwa uso, kwa sababu alistahili hukumu.
12 Kwa maana kabla hawajaja watu kadha wa kadha waliotoka kwa Yakobo, alikuwa akila pamoja na watu wa Mataifa; lakini walipokuja wao, akarudi nyuma akajitenga, huku akiwaogopa waliotahiriwa.
13 Na hao Wayahudi wengine wakajigeuza pamoja naye, hata na Barnaba pia akachukuliwa na unafiki wao.
14 Walakini, nilipoona ya kuwa njia yao haiendi sawasawa na ile kweli ya Injili, nalimwambia Kefa mbele ya wote, Ikiwa wewe uliye Myahudi wafuata desturi za Mataifa, wala si za Wayahudi, kwa nini unawashurutisha Mataifa kufuata desturi za Wayahudi?
15 Sisi tulio Wayahudi kwa asili, wala si wakosaji wa Mataifa,
16 hali tukijua ya kuwa mwanadamu hahesabiwi haki kwa matendo ya sheria, bali kwa imani ya Kristo Yesu; sisi tulimwamini Kristo Yesu ili tuhesabiwe haki kwa imani ya Kristo, wala si kwa matendo ya sheria; maana kwa matendo ya sheria hakuna mwenye mwili atakayehesabiwa haki.
17 Lakini ikiwa sisi wenyewe, kwa kutafuta kuhesabiwa haki katika Kristo, tulionekana kuwa wenye dhambi, je! Kristo amekuwa mtumishi wa dhambi? Hasha!’
Kumbuka Petro alijulikana kama nguzo katika kanisa, na hivyo ilikuwa ni rahisi kuaminiwa na kufuatwa kwa kila alichokuwa anakisema hata kama kwa namna Fulani kingeonekana kuwa sio sahihi, wengi bado wangemfuata tu, Na ndio maana tunasoma hapo biblia inasema, Wayahudi wengine wakajigeuza pamoja naye…Lakini tendo Hilo halikumshutua sana Paulo, pengine mamia ya wayahudi waliobadilishwa kuwa wakristo walifuatana na unafki wa Petro, wakawa nao wanakula pamoja na mataifa, na wakiwaona tu wayahudi wenzao wanakuja wanajigeuza na kuwashurutisha mataifa nao washike sheria za kiyahudi kama vile kutahiriwa, kutokula vyakula najisi, kutawadha baada ya kula n.k. mambo ambayo walikuwa hawayafanyi wakiwa na watu wa mataifa peke yao..Ni kinyume na agizo la Bwana.
Lakini hayo yote hayakumshutua sana Paulo, wala hakuwataja myahudi mmoja mmoja aliyechukuliwa na unafiki wa Petro, lakini alikwenda moja kwa moja kumtaja Barnaba ..na kusema
“Na hao Wayahudi wengine wakajigeuza pamoja naye, hata na Barnaba pia akachukuliwa na unafiki wao”.
Hata na Barnaba pia??
Kwanini Paulo alimstaajabia Barnaba.
Tunasoma tena katika biblia Barnaba alikuwa ni mtume mwenye karama ya kitofuati sana na wengine katika kanisa, aliitwa mwana wa faraja (Matendo 4:36), hakuwa tu faraja kwa ndugu wa kikristo peke yake bali alikuwa pia faraja kwa kanisa la Kristo kwa ujumla, tunaona mwanzoni kabisa alikuwa tayari kuuza shamba lake ili tu kuhakikisha fedha inapatikana miguuni pa mitume kulihudumia kanisa Matendo 4:36-37).
Utaona tena wakati ambao Paulo ndio kwanza kaguezwa kuwa mkristo, na kanisa linamwogopa kushirikiana naye kutokana na historia yake ya nyuma kuwa mbaya ya mauaji, Barnaba ndiye aliyekwenda kumchukua Paulo na kumtambulisha kwa mitume, ndipo akakubaliwa kukaa nao. Biblia inasema alikuwa ni mtu aliyejaa Roho Mtakatifu, na kila alipokwenda alikuwa analithibitisha kanisa kwa karama ya faraja iliyokuwa ndani yake, Huyu ndiye baadaye alikwenda kumchuka tena Paulo kutoka Tarso na kumleta Antiokia ili kuhudumu naye..(Matendo 11:25)..
Na baadaye wakiwa katika ziara za kuhubiri injili mataifa mengine, wakiwa wote pamoja, waliondoka na kijana mmoja kwenda kuhubiri nao aliyeitwa Marko, lakini huyu Marko hakumaliza nao safari, hiyo ni baada ya kuona kuna ugumu mbeleni, hivyo alirudia katikati na kuwaacha Paulo na Barnaba wakiwa katika nguvu chache, suala lile halikumpendeza sana Paulo, hivyo katika awamu ya pili ya kwenda kuhubiri tena wakati Paulo na Barnaba wanataka sasa kwenda kuyahakiki makanisa, huyu kijana Marko akataka kufuatana nao lakini Mtume Paulo kwasababu hakuwa na karama ya faraja na uvumilivu ndani yake hakumruhusu aongozane naye, akamchukua Sila badala yake..Lakini Barnaba hakutaka amuache akaondoka na Marko.
Huyu Marko akiwa chini ya matengenezo ya Barnaba baadaye alikuja kujirekebisha na kuwa thabiti kweli kweli katika Imani, hadi mtume Paulo utakuja kusoma huko mbeleni anasema anamfaa sana kwa utumishi. (2Timotheo 4:11). Na ndio huyu huyu aliyekuja kuandika kitabu cha Marko. Lakini kama Barnaba angemuacha, leo hii tungepata wapi injili nzuri ya Kristo kama ile ya Marko?, vilevile angemwacha Paulo, kule Tarso, au angemwacha kule mwanzoni alipokuwa anakataliwa na makanisa yote injili ya Paulo ingeeneaje katikati ya mataifa na kwetu sisi pia?.
Barnaba alikuwa amejitoa, hata suala la mke kwake halikuwa la muhimu sana, alizunguka kuyathibitisha tu kanisa kwa karama yake ya faraja iliyokuwa ndani yake, hususani kwa wakristo waliokuwa wanasumbuliwa na sheria za wayahudi, na wapagani..yeye alipokuwa akienda mafundisho yake tu na uwepo wake tu, basi kanisa lilisimama tena na kupata nguvu mpya.
Hivyo Paulo alimchukulia kama mlevi wa karibu wa Huduma yake na Kanisa la Kristo kwa ujumla, alijua atakapokuwepo Barnaba mambo yote yatakuwa sawa..Lakini sasa hapa anaona amekutana na Mtume Petro, na kibaya Zaidi anachokifanya yeye, ni kinyume na kitu Mungu alichokiweka ndani yake.
Mpaka Paulo anasema..Mpaka na wewe Barnaba?..Ni nini kimekutokea? Wewe huduma yako ni msingi wa kuwajenga mataifa imekuwaje umechukuliwa tena na unafki wa hawa wengine??..Wewe ndio ungepaswa uwakemee hawa wayahudi waache kuwataabisha mataifa waliomwamini Kristo wasijisumbue na torati, lakini leo hii na wewe umekuwa huzuni kwao badala ya faraja?
JE! NA SISI LEO TUNAAMBIWAJE?
Biblia inasema..
Ufunuo 3:11 “Naja upesi. Shika sana ulicho nacho, asije mtu akaitwaa taji yako”.
Bidii zetu katika kumtumikia Mungu tusiruhusu kuzimishwa na mtu yeyote,kisa yeye anacheo Fulani au ni kiongozi Fulani, kumbuka anayeweza kuchukua taji lako, sio tu shetani, bali hata askofu wako, mchungaji wako, kiongozi wako wa kiroho anaweza kuchukua na kukimbia nalo ukabakia huna kitu..Pale anapotaka kuizimisha karama yako ili tu matakwa yake binafsi yafanikiwe..Na wote mnajua kabisa mnachokifanya sio sahihi lakini bado mnaendelea kukifanya!! Pale Mungu anapokupa karama ya uponyaji, ulikuwa unawaombea watu wengi wanaponywa, lakini kanisani kwako wanakuambia hatuamini kama kuna uponyaji wa ki-ungu na wewe umeacha kutumia karama hiyo? ..Mungu anakuuliza Je! Hata na wewe umechukuliwa na unafki wao?
Pale Mungu anapokupa karama ya kunena kwa lugha, lakini kanisani kwako hawaamini mambo kama hayo, na wewe unawatii tu ili kuwapendezesha, Bwana anakuambia Je! Na wewe umechukuliwa na unafki wao?, Pale unaposikia ndani kuhimizwa kusali masafa marefu, lakini nyie mmefundisha tu kusoma liturjia za kimapokeo, Na huku unajua kabisa moyoni mwako unachokifanya sio sahihi na unaendelea kubaki hapo, Bwana anakuambia JE! Na wewe umechukuliwa na unafki wao?
Unajua kabisa moyoni mwako unahitaji wokovu, unamuhitaji Yesu ayabadilishe Maisha yako, lakini kwasababu Padri wako amekuambia ukipata kipaimara na komunio inatosha unamsikiliza na huku rohoni unazidi kutetereka..Roho Mtakatifu anakuambia Je! Na wewe unataka kuchukuliwa na unafki wao?
Toka huko!! Umgeukie Kristo, uanze kuishi kulingana na Neno la Mungu, Ili Mungu akutumie kwa jinsi apendavyo, na taji lako halitatwaliwa na mwingine. Kumbuka tena anayetwaa taji lako ni mtu si malaika wala shetani…Biblia inasema… Ufunuo 3:11 “Naja upesi. Shika sana ulicho nacho, asije MTU akaitwaa taji yako”.
Ubarikiwe sana
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii 0789001312Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group
Mada Nyinginezo:
Shalom, Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe. Karibu tujifunze tena maandiko siku ya leo. Kwasababu Neno la Mungu ndio mwanga wa njia zetu na taa iongozayo miguu yetu. Maana yake tukiwa na Neno la Mungu vya kutosha ndani yetu basi njia ya maisha yetu itakuwa wazi, tutakuwa tunajua tulikotoka, tulipo sasa na tunapokokwenda…kwasababu ile Nuru inamulika nyuma yetu, mahali tulipo na mahali tunapoelekea.
Kama wengi wetu tunavyojua kuwa muunganiko wa madhehebu na dini ni mpango wa Yule Adui. Lakini unaweza kujiuliza ni kwanini uwe ni mpango wa Adui na ilihali tunajua kuungana ni jambo jema na zaidi ya yote Biblia imehimiza tuwe na umoja.(Yohana 17:11, Yohana 17:21, Waefeso 4:3 na Waefeso 4:13)..Mistari yote hiyo inazungumzia suala la umoja. Lakini kwanini huu muunganiko wa madhehebu na dini usiwe ni mpango wa Mungu?. Kama kweli ni mtu wa kutafakari hili swali ni lazima utajiuliza..Na kama hutachunguza kwa makini unaweza ukajikuta unakubaliana nalo na kusema hakuna ubaya wowote kuwepo umoja huo au unaweza kujikuta unakuwa tu mshabiki wa kuupinga lakini usijue ni kwanini unaupinga..
Hivyo leo kwa neema za Bwana tutaangalia kasoro moja iliyopo katika muungano huo kwa kutumia Biblia na mifano dhahiri katika maisha …ambayo hiyo ndio itakayotufanya tuhukumu wenyewe kama kweli ni mpango wa Mungu au sio mpango wa Mungu..
Kabla ya kwenda kwenye biblia hebu tafakari mfano huu kisha tutakwenda kwenye maandiko..
Wanandoa wawili ambao wamefunga ndoa halali mbele ya madhabahu ya Mungu…wamegombana na kuachana na kila mmoja akaenda kuoa na kuolewa na mwingine…na huko walikokwenda kila mmoja akapata watoto..na wakawa wamekaa katika hali hiyo muda mrefu sana miaka mingi sana ikapita pasipo kuonana wala kuwasiliana kwa ufupi kila mmoja akawa ameanza maisha yake mengine na ana mipango yake…
Siku moja katika shughuli zao wakakutana mahali pamoja pa kazi kila mmoja akiwa na mpenzi wake mpya na watoto wake…
Sasa kwasababu tayari kila mmoja ana mpenzi wake mpya na familia mpya, na walishaachana kitambo na wameshakuwa watu wazima sana hata ule upendo haupo tena…. ikabidi watambulishane tu kwamba huyu alikuwa ni mpenzi wangu wa zamani lakini tulishaachana kitambo sana..kila mmoja akamtambulisha mwenziwe na sasa hatuna mahusiano yoyote…lakini kwasababu wote tumekutana na shughuli yetu ni moja basi hebu tushirikiane tufanye kazi pamoja tujiendeleze kiuchumi na kutunza familia zetu..
Hivyo familia hizo mbili zikaungana kufanya kazi pamoja…kwahiyo kukawa na kaumoja Fulani lakini si cha mahusiano bali cha maslahi fulani. Familia hizo zikawa zinakutana kuuziana bidhaa na kushirikishana fursa mpya za kazi, na kutekeleza mipango mengine ya kimaisha n.k..
Sasa hebu jiulize?..Huo muungano ni muungano wa ki-Mungu?…Ni kweli wameungana, wanasadiana kiuchumi, kimawazo na hata kifursa lakini mbele za Mungu wanaonekanaje?..Mbele za Mungu wanaonekana ni wazinzi na waliotengana…maandiko yanasema hivyo…
Luka 16:18 “Kila amwachaye mkewe na kumwoa mke mwingine azini; naye amwoaye yeye aliyeachwa na mumewe azini”.
Haijalishi watafanya vitu vingapi kwa umoja, mbele za Mungu wanaishi katika uzinzi, haijalishi wameachana kwa makubaliano mazuri kiasi gani, haijalishi watakwenda pamoja kusaidia mayatima na maskini kwenye makambi lakini mbele za Mungu bado ni wazinzi..Na hivyo huo umoja ni umoja wa shetani hata kama wanafanya mema elfu, wakifa wote wanakwenda motoni…Kwasababu Mungu hawezi kuunganisha wazinzi wawili wapatane..Badala yake Mungu angewarudisha kwanza warudiane ili wasiishi katika uzinzi..na ndipo hayo mambo mengine yafuate.
Ili uwe umoja wa KiMungu ilikuwa ni sharti kila mmoja amrudie mpenzi wake wa kwanza ambaye walifunga naye ndoa kanisani, na kuachana na huyu aliyenaye sasa….Endapo wangerudiana na kuungana kwa namna hiyo, hapo mbele za Mungu wangekuwa wameungana na hivyo ungekuwa tayari ni umoja upo katikati yao.
Ndicho kinachotokea kwenye madhehebu sasa…Shetani kawatenganisha wakristo na kuwaweka katika makundi makundi…dhehebu hili, na lile…kaondoa ule umoja wa Roho ambao ulianza pale Pentekoste ambapo hakukuwa na dhehebu lolote wote walikuwa wamoja…
Matendo 2: 44 “Na wote walioamini walikuwa mahali pamoja, na kuwa na vitu vyote shirika”.
Mitume hawakuanzisha madhehebu…waamini wote walikuwa ni kitu kimoja…Sasa shetani kashatutenganisha..halafu anataka kutuunganisha katika hali ya matengano tuliyopo…tupo tumetengana na bado anataka tuungane tusaidiane kifursa, TAG na EAGT tuungane tusaidiane kutatua matatizo Fulani Fulani ya kijamii, Lutheran na katoliki tuungane, Anglikana na Morovian tuungane ili tushirikiane kutatua kwa pamoja matatizo Fulani Fulani. Wakati kila mmoja msingi wa Imani zetu zimepishana.
Je! unadhani huo ni mwunganiko wa kiMungu?…La! hata kidogo sio muunganiko wa kiMungu kabisa… Ili uwe muunganiko wa kiMungu ni sharti wakristo wote tungepaswa tuungane na kuwa kitu kimoja katiba yetu ikiwa biblia na si kuunganisha madhehebu…pasipowepo kusema mimi ni wa dhehebu hili au lile..wote jina letu linapaswa liwe moja (wakristo), huo ndio umoja wa Roho unaozungumziwa katika maandiko kwamba tunapaswa tuwe nao..
Ni sawa na kijana kapewa gunia la mchele la kila 50, na akaambiwa akifika nyumbani auchanganye vizuri na kuutoa uchafu na kisha ahamishie ule mchele kwenye gunia lingine lililosafi zaidi…na kijana alipofika nyumbani akalifungua akaanza kutenga ule mchele kuuweka kwenye vifungashio tofauti tofauti .. akatenga kilo 5 akazifungia kwenye mfuko, kilo nyingine kumi kwenye gazeti, kilo nyingine 2 kwenye kichupa kidogo, nyingine 4 kwenye kopo nyingine 8 kwenye kijimfuko cha rambo nyingine 10 kwenye kiroba na hicho kiroba akakipiga lebo..mpaka zilipotimia zote 50. Na akavichukua hivyo vifungashio vyote na viroba vyote akavitumbukiza kwenye gunia hilo jipya la kila 50.Na kusema tayari kauleta pamoja ule mchele…hapo kauleta mchele pamoja au viroba pamoja?..Atakuwa hajatumia akili kwasababu alipaswa aumimine mchele wote uliosafi kwenye lile gunia moja haikuhitajika tena kufungwa matita matita. Na madhehebu yote ni vifungashio…ndani ya Gunia kuu la ukristo.
Na vifungashio hivyo Mungu kavikataa..Ndio maana anasema katika Ufunuo 18: 4 “Tokeni kwake enyi watu wangu..msishiriki dhambi zake”..Maana yake tutoke kwenye kamba za udini na madhehebu…tuunganike wakristo na si madhehebu..
Ndio Mungu kaweka tofuati ya utendaji kazi katika kanisa, Lakini kumbuka ni utofauti wa utendaji kazi, na sio utofauti wa Imani,..Leo hii katika ukristo zipo Imani tofauti tofauti haiwezekani mmoja anaamini mpatanishi kati ya Mungu na mwanadamu ni mmoja tu Yesu Kristo, mwingine anasema pembeni ya Yesu kuna mwingine anayeitwa Mariamu n.k. Halafu hao wote bado wawe kitu kimoja. Na kibaya Zaidi umoja huu unalenga kufikia hadi kuunganika na dini nyingine zisizomtambua hata Kristo.
Sasa tukirudi katika maandiko madhara ya muunganiko huo ni nini?
Madhara ya muunganiko wa madhehebu ni kuitengenezea njia roho ya Mpinga kristo kufanya kazi…Kumbuka Mpinga-kristo atakuwa ni mtu wa kidini na atakuwa mshirika wa muungano huo..Roho ya kumpinga kristo haianzii freemason, kama wengi wanavyofikiri, wala kwa waislamu, wala kwa mabudha…roho ya mpingakristo inaanzia kwenye huu umoja wa dini na madhehebu…Waliompinga Kristo wa kwanza wakati akiwa hapa duniani hawakuwa wachawi, wala watu wa mataifa bali walikuwa ni mafarisayo na masadukayo (watu waliokuwa wameshika sana dini).
Sasa mafarisayo na masadukayo yalikuwa ni madhehebu ya kiyahudi…Kila moja lilikuwa linadai linamjua Mungu zaidi ya lingine…hivyo yakatengana kama madhebu yalivyotengana leo..na baada ya kutengana wakati Bwana Yesu anakuja na kuhubiri…yakainuka yote kumpinga Bwana Yesu na kufanya shauri pamoja ya kumuua…Na muunganiko wa madhehebu leo hii utakuja kusimama kuwapinga wakristo wakweli katika siku za mwisho, na kuwaletea dhiki.
Yohana 16:2 “Watawatenga na masinagogi; naam, saa yaja atakapodhania kila mtu awauaye ya kuwa anamtolea Mungu ibada”.
Na yatamtengenezea njia pana Mpinga-Kristo ambaye atanyanyuka na kuutumia huo muungano kuiunda ile CHAPA YA MNYAMA. Ambapo itafikia kipindi watu hawataweza kununu wala kuuza bila kuwa mshirika wa umoja wa muungano huo.
Mathayo 22: 34 “Na Mafarisayo waliposikia ya kwamba amewafumba kinywa wale Masadukayo, walifanya shauri pamoja”.
Je upo chini ya kifungashio gani? Cha Neno la Mungu au cha dhehebu lako?..Je unajisifia dhehebu au Imani?..Hebu jifikirie tangu upo katika dhehebu lako umejifunza kuhusu kumjua Yesu kiasi gani?..unamjua Mungu kiasi gani,Neno unalifahamu na umelishika kiasi gani?..je umekuwa mtakatifu kiasi gani?..una uhakika kwa kiasi gani kwenda mbinguni?..Je umeshawahi kutenga muda mwenyewe pasipo kuambiwa kusoma maandiko?, au kusali au kwenda kuwahubiria wengine habari njema…
Kama hujawahi kufanya hayo na zaidi ya hayo na bado unajiisifia dhehebu…tenga muda ujitafakari tena ndugu yangu…Usijisifie dhehebu, wala usiufurahie kila muungano unaosimama mbele yako…Rudi katika Neno la Mungu ambalo ndio katiba yetu. Unyakuo umekaribia sana, Kristo anakaribia kuja na Mpinga-Kristo kashatengeneza mazingira yake yote ya kufanya kazi zake.
Bwana akubariki.
Tafadhali share na kwa wengine na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo ya kujifunza kwa njia ya inbox au whatsapp basi utatutumia ujumbe kwa namba hii 0789001312
Mada Nyinginezo:
MPINGA-KRISTO
MUUNGANO WA DINI NA MADHEHEBU YOTE, UMEKARIBIA.
Mitume wote waliopita walikuwa ni watu weupe hata manabii wote waliopita hadi Ma-papa ni ngozi nyeupe. ni kweli ngozi nyeusi ililaaniwa ?
ROHO HUTUOMBEA KWA KUUGUA KUSIKOWEZA KUTAMKWA!
Sabato halisi ni lini, Je! ni Jumapili au Jumamosi?, Ni siku gani itupasayo kuabudu?
NENO LA MUNGU NI DAWA ILIYO TOFAUTI NA DAWA NYINGINE.
Wakati mwingine Mungu anaweza kutumia rangi kutufikishia sisi ujumbe fulani, mfano mara baada ya Nuhu kutoka katika Safina Mungu alimpa agano la upinde wa mvua kama ishara kuwa hatateketeza tena kwa maji, ambalo lilikuwa na mkusanyiko wa rangi saba..Jiulize ni kwanini auvike upinde ule rangi nyingi, na si kitu kingine? Angeweza tu kuweka kitu fulani chenye mfano wa picha au wingu, lakini hakufanya hivyo ilimpendeza Mungu kutumia upinde wa rangi kusimamisha agano lake. Ni wazi kuwa mkusanyiko wa rangi zote zile saba, ziliwakilisha Neema, kuwa Mungu hataangamiza tena dunia kwa maji.
Hivyo tutaangazia tafsiri ya rangi katika biblia, na maana zake rohoni. Lakini awali ya yote ni vizuri kufahamu kuwa hakuna rangi yoyote iliyo bora Zaidi ya nyingine, wala yenye uwezo fulani wa ki-ungu Zaidi ya nyingine..Kwasababu wapo watu wameshafundishwa na manabii wa uongo na waganga wa kienyeji, elimu za mashetani zinazowaambia, ukivaa nguo ya rangi fulani au ukinunua kitu cha rangi fulani kinawakilisha laana au baraka fulani, kwamfano ukivaa nguo nyeusi roho ya misiba inakuandama, mimi mwenyewe binafsi nimeshakutana na watu wa namna hiyo, Na wengine wanasema ukivaa nguo nyeupe roho ya Mungu inakaa juu yako n.k…
Lakini hawajui kuwa biblia inasema shetani naye hujigeuza na kuwa mfano wa malaika wa Nuru.(ukisoma 2Wakorintho 11:14 utaona), Vivyo hivyo na watumishi wake wote. Hivyo hata yeye kutumuia rangi zinazoonekana zina utukufu kama nyeupe si jambo la kushangaza, anafanya sana tu, Ili kuthibitisha hilo ukisoma kitabu cha Ufunuo sura ya 6:2-3, utaona yule mpanda-farasi wa kwanza akiwa amepanda farasi mweupe..Lakini yule hakuwa anamwakilisha Mungu, bali mpinga-Kristo mwenyewe.
Hivyo hali hiyo ya kuangalia rangi ki-mwili ili kuamua hatma ya Maisha yao, imewafanya watu wengi wawe na hofu hata wanapokutana na mnyama wa rangi fulani tu labda tuseme, nyeusi wanawaogopa au wanakataa kuwafuga kwa kisingizio kuwa wanatumiwa na wachawi.
Ndugu jiepushe na mafundisho hayo, Na katika siku hizi za mwisho yamekuwa ni mengi sana. Unaweza kuona yana hekima na yamejaa mafunuo lakini kumbe ndivyo yanavyokupeleka mbali na Mungu.
Lengo letu ni kukusaidia wewe kuelewa tafsiri za rangi pale unaposoma biblia na kukutana na rangi fulani basi ujue zilimaanisha nini..Vilevile wakati Mwingine Mungu anaweza kusema na mtu kwa njia ya ndoto au maono, akamwonyesha rangi fulani na asijue maana yake.Lakini mfano akiwa na ufahamu wa kutosha wa kujua rangi zilisimama badala ya nini katika biblia itamsaidia kupata upambanuzi wa alichoonyeshwa au alichokisoma kirahisi.
Rangi zipo nyingi sana, lakini tatazigusia zile ambazo zinaonekana na kuzimetumika mara kwa mara katika biblia.
Rangi Nyeupe:
Hii ni rangi ya usafi, utakatifu, nuru, palipo na weupe hakuna chochote kinachoweza kusitirika, hata uchafu unaonekana kirahisi katika kitu cheupe, sehemu nyingi utaona Mungu anajitambulisha yeye kama mwenye mavazi meupe, kichwa cheupe na nywele nyeupe (Danieli 7:9, Ufunuo 1:14 ), na kiti chake cha enzi ni cheupe(Ufunuo 20:11), vilevile watakatifu watapewa mavazi meupe. (Ufunuo 3:5)
Mbingu pia ni nyeupe, Hivyo Mungu ukikutana na rangi hii, kwenye maandiko au kwenye maono sehemu kubwa ya ujumbe wake ni Utakatifu, au usafi war oho, au Uwepo wa Bwana.
Nyekundu:
Hii ni rangi ya mwadamu, Adamu alitolewa katika udongo mwekundu, hivyo Mungu akamwita Adamu, Rangi hii pia ni rangi ya uhai, na maangamizo, hatari. Hivyo jambo kama hili ukiliona. Ujue upo umwagaji damu mbeleni au hatari fulani, au maangamizo mbeleni..Ukisoma Ufunuo 17, utaona yule mwanamke kahaba, Babeli mkuu akiwa ameketi juu ya mnyama mwekundu sana, ikiashiria kuwa ni muuaji.
Ufunuo wa Yohana 17:1 “Akaja mmoja wa wale malaika saba, wenye vile vitasa saba, akanena nami, akisema, Njoo huku, nitakuonyesha hukumu ya yule kahaba mkuu aketiye juu ya maji mengi;
2 ambaye wafalme wa nchi wamezini naye, nao wakaao katika nchi wamelevywa kwa mvinyo ya uasherati wake.
3 Akanichukua katika Roho hata jangwani, nikaona mwanamke, ameketi juu ya mnyama mwekundu sana, mwenye kujaa majina ya makufuru, mwenye vichwa saba na pembe kumi.
4 Na mwanamke yule alikuwa amevikwa nguo ya rangi ya zambarau, na nyekundu, amepambwa kwa dhahabu, na kito cha thamani, na lulu, naye alikuwa na kikombe cha dhahabu mkononi mwake, kilichojawa na machukizo, na machafu ya uasherati wake.
5 Na katika kipaji cha uso wake alikuwa na jina limeandikwa, la siri, BABELI MKUU, MAMA WA MAKAHABA NA MACHUKIZO YA NCHI.
6 Nikamwona yule mwanamke amelewa kwa damu ya watakatifu, na kwa damu ya mashahidi wa Yesu. Nami nilipomwona nikastaajabu ajabu kuu”.
Unaona, ukisoma pia Ufunuo sura ya 6 utaona yule mpanda wa pili, akiwa amepanda farasi mwekundu sana, ikiashiria kuwa ataeleta mauaji vita n.k.
Ufunuo 6:3 “Na alipoifungua muhuri ya pili, nikamsikia yule mwenye uhai wa pili akisema, Njoo! 4 Akatoka farasi mwingine, mwekundu sana, na yeye aliyempanda alipewa kuiondoa amani katika nchi, ili watu wauane, naye akapewa upanga mkubwa.”
Hivyo ukiona rangi hii ukiona rangi hii nyekundu kwa sehemu kubwa imetumika kama hatari, umwagikaji damu, au dhiki, au machafuko yapo mbeleni.
Njano/Dhahabu:
Hii ni rangi inayowakilisha thamani ya kitu kilichotakaswa, ukisoma kitabu cha ufunuo utaona Mji ule Yerusalemu mpya njia zake zikiwa ni za dhahabu tupu (Ufunuo 21:18,21). Vilevile katika agano la kale vyombo vya madhabahuni vilivyokuwa ni vya dhahabu. Rangi hii pia inawakilisha moto, Moto hutakasa, na kusafisha, moto unamwakilisha Roho Mtakatifu.
Hivyo Rangi hii inasimama kama utakaso..Kitu kilichotakaswa, kimewekwa wakfu kwa ajili ya kazi fulani maalumu ya Mungu. Ni ishara kwamba kuna utakaso utapita ambapo utakufanya au kumfanya mtu awe thabiti kiimani kama dhahabu.
Zambarau: Rangi kifalme, rangi za kikuhani, mavazi ya Haruni yalikuwa yamenakshiwa na rangi za zambarau. Kutoka 26:1. Hata wale askari waliomsulibisha Bwana Yesu, waliyatwaa mavazi ya kifalme ya zambarau na kumvika ili wamdhihaki.(Marko 15:17). Hivyo rangi hii inawakilisha ukuu, utawala, au mamlaka fulani.. Hata tuliposoma hapo juu habari za yule Babeli mkuu mama wa makahaba tumeona alikuwa amevaa nguo za rangi ya zambarau, kuonyesha ameketi katika kiti cha kitawala, kama malkia,..
Hivyo ukikutana na rangi hii ujue inazungumzia Ufalme, au utawala fulani.
Nyeusi: Hii ni Rangi ya giza, uovu, upotevu, uchafu, . Sikuzote giza ni jeusi..Na ndio maovu yote yanapofanyikia.(Yuda 1:13). Hivyo utakapokutana na rangi hii basi ujue inasimama kuonyesha ufalme wa giza na mamlaka ya shetani. Hivyo kama ni katika mazingira ya maono basi unapaswa umuulize Mungu ushindane vipi na hali hiyo, kwasababu zipo nguvu za shetani mbeleni.
Kijani: Rangi ya uhai,ustawi, ubichi, palipo na uhai pana ukijani, mvua ikinyesha juu ya nchi, majani yanayochipuka huonekana katika rangi ya kijani..na hivyo ni rangi inayoashiria neema na baraka kutoka kwa Mungu.
Mwanzo 1:11 “Mungu akasema, Nchi na itoe majani, mche utoao mbegu, na mti wa matunda uzaao matunda kwa jinsi yake, ambao mbegu zake zimo ndani yake, juu ya nchi; ikawa hivyo.
12 Nchi ikatoa majani, mche utoao mbegu kwa jinsi yake, na mti uzaao matunda, ambao mbegu zake zimo ndani yake, kwa jinsi yake; Mungu akaona ya kuwa ni vyema.
Hivyo ukikutana na rangi hiyo katika maandiko au katika maono basi ujue neema ipo mbeleni.
Bluu: Hii ni rangi ya utukufu wa Mungu..nikiziangalia mbingu ni kazi ya vidole vyako (Zaburi 8:3)…Milima japo kwa karibu utaiona na rangi tofauti tofauti lakini ukiitazama kwa mbali utaona yote inabadilika na kuwa rangi moja ya bluu, vivyo hivyo hata na vyanzo vikubwa vya maji kama vile maziwa na bahari, ukiyatazama kwa mbali muonekana wao unabadilika na kuwa wa bluu..
Hivyo hii ni rangi ya utukufu wa Mungu.. Mungu kukuonyesha rangi hii basi ujue, Mungu anataka uuone utukufu wake. Usipoipenda rangi hii basi hii dunia itakuwa ya-kuboa sana kwako kwasababu popote utakapoutazama ukuu wa Mungu rangi hii utaiona.
Rangi nyingine ni kijivu jivu:
Hii inafunua mauti na kuzimu.
Ufunuo 6:7 “Na alipoifungua muhuri ya nne, nikasikia sauti ya yule mwenye uhai wa nne akisema, Njoo!
8 Nikaona, na tazama, farasi wa rangi ya kijivujivu, na yeye aliyempanda jina lake ni Mauti, na Kuzimu akafuatana naye. Nao wakapewa mamlaka juu ya robo ya nchi, waue kwa upanga na kwa njaa na kwa tauni na kwa hayawani wa nchi”.
Hivyo ikiwa utakutana na rangi kama hizi basi ujue hizo ndio maana zake kibiblia, Na kama tulivyosema, hakuna rangi iliyobora Zaidi ya nyingine tukizungumza kwa namna ya kawaida, usiache kuvaa nguo yako ya rangi nyeusi kwa hofu kuwa mapepo yatakuvamia, au rangi ya kijivujivu, hilo jambo halipo. Mungu akikuonyesha rangi fulani katika ndoto au maono au katika Neno lake basi ujue kuwa analengo la kukufundisha jambo fulani rohoni na sio mwilini.
Ubarikiwe.
Je! Umeokoka? Je unafahamu kuwa tunaishi katika siku za mwisho za kurudi kwa Bwana wetu Yesu Kristo, na kwamba UNYAKUO siku yeyote unaweza kupita? Unajua kuwa hili ndilo kanisa la mwisho lijulinalo kama Laodikia na kwamba hakutakuwa na kanisa lingine Zaidi ya hili? Je unafahamu kuwa Neema hii ya injili hatutakuwa nayo milele, hivi karibuni itaondoka na kurudi Israeli?. Na ikishaondoka huku kwetu ni basi tena, hakutakuwa na neema?..Dalili zote zimeshatimia, tazama manabii wa uongo wengi walivyo duniani, tazama maovu yalivyokithiri, ni uthibitisho tosha kuwa dunia hii imeshafikia ukomo wake.
Ikiwa utasema siku ya leo sitaki inipite bado nipo katika vifungo vya shetani Basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie maisha yako yote kama ilivyokuwa hata kwetu sisi. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.
EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.
ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.
AMEN.
Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.
Bwana akubariki.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kupofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Mada Nyinginezo:
HADITHI ZA KIZEE.
ZIFAHAMU NAMBA KATIKA BIBLIA NA MAANA ZAKE.
UMUHIMU WA YESU KWETU.
UWEPO WA BWANA HATA KATIKATI YA MATESO.
ALIKUWAKO NAYE HAYUKO, NAYE YU TAYARI KUPANDA KUTOKA KUZIMU.
LOLOTE ATAKALOWAAMBIA FANYENI.
MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.
CHUKIZO LA UHARIBIFU
Je kuna mbingu ngapi? Mbingu saba ni nini?..na kama zipo 7 je mbingu ya kwanza ni ipi, mbingu ya pili ni ipi, mbingu tatu pia ni ipi? na hatimaye zote saba?..
JIBU: Katika biblia tunasoma kumetajwa uwepo wa mbingu tatu tu.
2Wakorintho 12:2 ‘Namjua mtu mmoja katika Kristo, yapata sasa miaka kumi na minne, (kwamba alikuwa katika mwili sijui; kwamba alikuwa nje ya mwili sijui; Mungu ajua). Mtu huyo alinyakuliwa juu mpaka mbingu ya tatu’.
Huyu ni Paulo aliyenyakuliwa mpaka mbingu ya tatu. Sasa biblia haijataja uwepo wa mbingu nyingine zaidi ya hizi tatu. Na pia haijazitaja mbingu hizo tatu ni zipi..Lakini kwa Neema za Bwana na kwa kuyachunguza maandiko tunaweza kuzijua ni zipi.
Ipo mitazamo kadhaa juu ya hizi mbingu tatu zilizotajwa hapo juu…Lakini inayojulikana na wengi ni kwamba Mbingu ya kwanza ni hili anga tulionalo ambalo lina hewa yetu ya oksijeni tunayoivuta, kadhalika lenye mawingu na ambalo linanyunyiza mvua..
Na mbingu ya pili ni ile ya juu zaidi yenye magimba ya vimondo, nyota na sayari
Na mbingu ya tatu ni ile ambayo Malaika watakatifu wapo.
Huu ndio mtazamo unaojulikana na wengi. Lakini upo pia mwingine ambao ndio tunaamini ni wa ukweli na huo ni kama ufuatao.
1. Mbingu ya Kwanza: inahusisha anga lote tunaloliona kwa macho…yaani sayari, nyota, jua, mwezi, mawingu, vimondo n.k
2.Mbingu ya Pili: Ni mbingu isiyoonekana kwa macho ijulikanayo kama PARADISO au PEPONI. Ni mahali ambapo roho za watakatifu waliokufa katika Imani ya Yesu Kristo zinahifadhiwa. Mtakatifu anapokufa mwili wake unakwenda kuzikwa kaburini, unaoza lakini roho yake inachukuliwa na malaika watakatifu na kupelekwa paradiso au peponi mahali ambapo pana raha na pumziko, ambapo atakutana na roho nyingine za watakatifu waliokufa katika Imani.
Kwa pamoja watakaa huko paradiso wakingojea siku ya unyakuo ifike ambapo, siku hiyo itakapofika watarudi kuichukua miili yao ya asili na kisha kufumba na kufumbua watabadilishwa pamoja na wale watakatifu walio hai na kwa pamoja watapaa kwenda kumlaki Bwana Yesu mawinguni kwenda kuingia katika mbingu ya Tatu.
Yule mhalifu aliyesulubiwa na Bwana Yesu pale msalabani alipelekwa mahali huko ambako Bwana Yesu alimwambia atakuwa naye. (peponi).
3.Mbingu ya Tatu: Ni mahali ambapo Bwana Yesu Kristo yupo pamoja na malaika watakatifu, huko ndiko Bwana alikosema amekwenda kutuandalia makao. Huko hawaingii watu wasio kuwa na miili ya utukufu. Ni sehemu ya raha isiyo na kifani…Mambo yaliyomo humo biblia inasema jicho halijawahi kuona wala sikio kusikia, mambo ambayo Mungu kawaandalia wale wamchao.(1Wakorintho 2:9).
Hivyo jibu jepesi ya kwamba kuna mbingu ngapi kibiblia? Jibu ni tatu tu kama tulivyoziona hapo juu. Na wala hakuna mbingu saba.
Hivyo tujitahidi tuingie katika mbingu hiyo ya tatu kwa kuuvua utu wa kale wa dhambi na kuvaa utu mpya.
Waefeso 4:22 “mvue kwa habari ya mwenendo wa kwanza utu wa zamani, unaoharibika kwa kuzifuata tamaa zenye kudanganya;
23 na mfanywe wapya katika roho ya nia zenu;
24 mkavae utu mpya, ulioumbwa kwa namna ya Mungu katika haki na utakatifu wa kweli.
25 Basi uvueni uongo, mkaseme kweli kila mtu na jirani yake; kwa maana tu viungo, kila mmoja kiungo cha wenzake”
Na pia biblia inasema katika..
Waebrania 12:14 “Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na huo utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao;”
Bwana akubariki.
Tafadhali share na wengine. Maran atha
Mada Nyinginezo:
Je! mbinguni kuna malaika wa kike?. Na je! tukifika mbinguni tutafanana wote?
Shalom. Jina la kuu la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe.
Karibu katika mwendelezo wetu unaoangazia matendo ya baadhi ya watu walioishindania imani hadi kufa bila kuiacha..Tulishawaona baadhi nyuma na Leo tutamwangazia mwingine anayeitwa Mtakatifu Denis wa Ufaransa.
Mtu huyu, alitokea karne ya tatu, Ni maarufu sana katika historia ya nchi Ufaransa, na hata katika vitabu vinavyoelezea historia ya mauaji ya wakristo, Huyu alikuwa kama mmishionari aliyezaliwa Italy, na kusafiri yeye pamoja na wenzake wawili nchini Ufaransa kwa lengo la kupeleka habari njema za Yesu Kristo,..Alipofika kule, Mungu alikuwa pamoja naye kwani alikuwa na bidii kubwa sana ya kuwageuza watu kwa Kristo, na hata wale makuhani wa dini za kipagani walipoona wanapotezewa waumini wao wengi, wanageuzwa na kuwa wakristo, wakaamua kuwaaundia visa watu hawa. Kama tu vile wakati mtume Paulo alipofika Efeso na kuwageuza watu wengi, na wale wenyeji wa mji walipoona wanapata hasara ya watu kutonunua bidhaa za miungu yao wakawaletea visa, ili Paulo na wenzake waletewe dhiki. Na ndivyo ilivyotokea kwa hawa.
Na sasa serikali ya Rumi iliposikia habari yao, ikawakamata na kuwafunga, ikumbukwe kuwa Rumi wakati huo ilikuwa katika vita vikali dhidi ya watu wote waliokuwa wanaonekana kueneza imani ya kikristo duniani. Lilikuwa ni taifa la kipagani asilimia 100. Hivyo Waliwafunga wakawaacha magerezani kwa muda mrefu, na mwisho wa siku wakawatoa magerezani na kuwachukua mpaka katika kilele cha mlima mmoja ili kuwaua kwa kuwakata vichwa, waliwakata wote lakini walipofika kwa mtakatifu Denis, na kukiondoa kichwa chake, walishaangaa kuona anakiokota tena kichwa chake, na kuanza kutembea maili kadhaa, akihubiri injili kila alipopita.
Tendo hili liliwaogopesha watu wengi sana waliokuwa wanashuhudia maajabu yale, na mahali alipoacha kuhubiri na kuanguka chini Mahali palepale ndipo ulipogeuzwa mji ule na kuitwa kwa jina lake ambao hadi sasa upo huko ufaransa,. Na juu ya kaburi lake wakatoliki baadaye walijenga kanisa lijulikanalo kama Basilica of Saint-Denis. (lakini kumbuka huyu Mt. Denis mwenyewe hakuwa mkatoliki wala mafundisho yake hayakuwa ya kikatoliki bali ya kanisa la kwanza la mitume wa Yesu Kristo, yaani Neno la Mungu lisiloghoshiwa).
Hadi leo sanamu lake limewekwa huko katika makumbusho za kitaifa huko Paris. Hizi ni historia ambazo zimethibitishwa. Hatuna mengi ya kuzungumza Lakini Tukiwatazama watu kama hawa tunapata ujumbe gani?
Biblia inasema..
Waebrania 12:1 “Basi na sisi pia, kwa kuwa tunazungukwa na wingu kubwa la mashahidi namna hii, na tuweke kando kila mzigo mzito, na dhambi ile ituzingayo kwa upesi; na tupige mbio kwa saburi katika yale mashindano yaliyowekwa mbele yetu,
2 tukimtazama Yesu, mwenye kuanzisha na mwenye kutimiza imani yetu; ambaye kwa ajili ya furaha iliyowekwa mbele yake aliustahimili msalaba na kuidharau aibu, naye ameketi mkono wa kuume wa kiti cha enzi cha Mungu”.
Ikiwa tunazungukwa na watu waolikuwa tayari kufungwa, hadi kuuawa kwa kukatwa vichwa kama hawa na bado walikuwa hawana hata mpango wa kumwacha Mungu, hadi Mungu anawapa nafasi ya kuendelea kuhubiri angali vichwa vyao havipo, sisi je tunapaswa tuweje?..Ikiwa hatujafikia hatua ya kumwaga damu kwa ajili ya ushuhuda kwa Kristo, lakini ni rahisi kurudishwa nyuma na mambo madogo, madogo tu yasiyokuwa na maana, tujiulize siku ile tutawezaje kusimama pamoja na watu kama hawa mbele ya Kristo? Tutawezaje kupata thawabu moja na wao watu ambao wamepiga mbio bila kuishiwa pumzi, wameishindania imani ipasavyo, kama biblia inavyotuambia katika sura iliyotangulia waebrania sura ya 11
“36 wengine walijaribiwa kwa dhihaka na mapigo, naam, kwa mafungo, na kwa kutiwa gerezani;
37 walipigwa kwa mawe, walikatwa kwa misumeno, walijaribiwa, waliuawa kwa upanga; walizunguka-zunguka wakivaa ngozi za kondoo na ngozi za mbuzi; walikuwa wahitaji, wakiteswa, wakitendwa mabaya;
38 (watu ambao ulimwengu haukustahili kuwa nao), walikuwa wakizunguka-zunguka katika nyika na katika milima na katika mapango na katika mashimo ya nchi.
39 Na watu hao wote wakiisha kushuhudiwa kwa sababu ya imani yao, hawakuipokea ahadi;
40 kwa kuwa Mungu alikuwa ametangulia kutuwekea sisi kitu kilicho bora, ili wao wasikamilishwe pasipo sisi”.
Umeona mstari wa 40 unavyosema, hawakukamilishwa, hawakuipokea ahadi au thawabu yao, kwa ajili yetu sisi, mpaka sisi nasi tutakapomaliza mbio, ili kwa pamoja tupokee tuzo bora..Lakini kama sisi tutaendelea kuwa vuguvugu, na walegevu, tutaendelea kuuchezea wokovu, tutaendelea kuishi kama vile sio watu waliomaanisha kweli kuenda mbinguni, Siku ile biblia inatuambia tutatupwa katika giza la nje,.
Hakuna tukio lingine lolote tunalolisubiria mbele yetu isipokuwa tukio la unyakuo tu, dalili zote zimeshatimia, siku yoyote parapanda inalia na wafu waliolala katika Kristo, watafufuka, kisha wataungana na watakatifu walioko duniani, na kwa pamoja tutakwenda mbinguni kwenye karamu ya mwana kondoo.
Utajisikiaje siku hiyo kujiona umebaki hapa chini, na kibaya zaidi ukikumbuka umehubiriwa injili mara nyingi lakini ulishupaza shingo yako. Utakuwa katika hali gani..Hao ambao unawafurahisha siku ile wote kwa pamoja mtakuwa katika majonzi na majuto ya milele.
Huu ni wakati wa kumaanisha kumfuata Kristo kwa moyo wote, bila kujali, ndugu watakuonaje, marafiki watakuonaje, kazini watakuonaje, shuleni watakuonaje..ni wakati wa kupiga mbio kwa kutua mizigo yote ya dhambi, kisha kumtazama yeye aliyetuita,..Kumbuka toba ya kweli inatoka moyoni na sio kinywani, unaweza ukaongozwa sala ya toba hata mara 100 kama toba yako haikutoka moyoni ni sawa na kazi bure..yule mwanamke kahaba aliyemfauta Yesu akamlilia, akammwagia machozi yake mengi, miguu pake hakuwa anafanya jambo la kuigiza tu, kama linavyofanywa na wengi leo hii, bali alikuwa anaonyesha ni jinsi gani amemaanisha kutubu dhambi zake, na ukahaba wake, hadi akashindwa kuzungumza mbele zake,.na Yesu kuona vile tu bila hata ya kuisikia sauti yake au maneno yake, alisema amesamehewa dhambi zake..Unaona hakuongozwa sala yoyote pale, lakini alipoona moyo wake umetubu na kugeuka, japokuwa dhambi zake zilikuwa nyingi, alisamehewa zote..
Vivyo hivyo na wewe ukidhamiria kuacha dhambi zako kwa moyo wako wote, na kwa nguvu zako zote, ukageuka na kusema kuanzia leo mimi na ulimwengu basi nimeamua kumfuata Yesu bila kugeuka tena nyuma..Ujue kuwa hapo ndipo Mungu atakapokusamehe dhambi zako, kinachobakia kwako ni kuukamalisha wokovu wako kwa kwenda kubatizwa na kumwishia Kristo maisha yako yote yaliyobakia hapa duniani..
Hivyo kwa kumalizia unapokutana na hili Neno WINGU LA MASHAHIDI, kichwani kwako usiusahau ujumbe huo, kuwa lipo wingu kubwa la mashahidi wa Kristo linalotuzunguka, ndilo linalotuhimiza na sisi tupige mbio kama wao, katika mashindano tuliyowekewa mbele yetu kushinda tulivyokuwa tunapiga hapo mwanzo, na mbio hizo tunapiga kwa kutua kila mizigo ya dhambi inayotusonga kwa kadiri tuwezavyo ili tuwe wepesi Zaidi na zaidi..Ili na sisi tukapokee tuzo iliyobora kama wao, hata zaidi ya wao siku ile.
Ubarikiwe sana.
Mada Nyinginezo:
ANTIPA SHAHIDI WANGU, MWAMINIFU WANGU.
WINGU KUBWA LA MASHAHIDI.
JIFANYIE RAFIKI KWA MALI YA UDHALIMU.
KIFO CHA REINHARD BONKEY KINAACHA UJUMBE GANI KWETU?
HERI NINYI MLIAO SASA, KWA SABABU MTACHEKA.
TABIA YAKO NI YA MNYAMA GANI?
DANIELI: Mlango wa 9
UFUNUO: Mlango wa 11
Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe…Ni kwa Neema zake tumeiona tena siku ya leo..hivyo hatuna budi kumshukuru sana kwa Fadhili zake nyingi kwetu, na kuchukua nafasi hii angalau kujifunza Neno lake.
Masomo yaliyotangulia tuliona ni jinsi gani..Maagizo ya kushiriki meza ya Bwana na kuoshana miguu yalivyo ya muhimu sana kwa kila mkristo kuyazingatia. Kuoshana miguu ni tendo jepesi kulifanya lakini Adui kalifanya kuwa gumu na hata kuliharibu au kulifanya lifanyike isivyopaswa.
Ukiona unasema umeokoka lakini kuna ugumu katika kuosha miguu ya mtakatifu mwenzako basi kuna kasoro katika wokovu wako…Bwana Yesu alisema katika;
Mathayo 18:3.. “ Amin, nawaambia, Msipoongoka na kuwa kama vitoto, hamtaingia kamwe katika ufalme wa mbinguni.
4 Basi, ye yote ajinyenyekeshaye mwenyewe kama mtoto huyu, huyo ndiye aliye mkuu katika ufalme wa mbinguni.”
Ikiwa na maana kuwa kuna mambo madogo sana ambayo yanaweza kumkosesha mtu mbingu, na moja ya jambo hilo ni kukosa unyenyekevu.
Na kipimo cha kwanza cha unyenyekevu kwa kila mkristo ni kujishusha na kushika miguu ya mwenzake?..Je! unaweza kujishusha chini na kuosha miguu ya dada mwenzako? Na kuifuta kwa kitambaa??…Je! unaweza kujishusha chini na kuosha miguu ya jirani yako yenye mavumbi?…Kama huwezi basi Bwana Yesu anasema ni ngumu kuuingia ufalme wa mbinguni.
Yohana 13:12 “Basi alipokwisha kuwatawadha miguu, na kuyatwaa mavazi yake, na kuketi tena, akawaambia, Je! Mmeelewa na hayo niliyowatendea?
13 Ninyi mwaniita, Mwalimu, na, Bwana; nanyi mwanena vema, maana ndivyo nilivyo.
14 Basi ikiwa mimi, niliye Bwana na Mwalimu, nimewatawadha miguu, imewapasa vivyo kutawadhana miguu ninyi kwa ninyi.
15 Kwa kuwa nimewapa kielelezo; ili kama mimi nilivyowatendea, nanyi mtende vivyo.
16 Amin, amin, nawaambia ninyi, Mtumwa si mkuu kuliko bwana wake; wala mtume si mkuu kuliko yeye aliyempeleka.
17 Mkiyajua hayo, heri ninyi mkiyatenda”.
Lakini pamoja na hayo yote shetani naye anafanya kazi kwa nguvu kuhakikisha kwamba watu wanakwenda kuzimu kihalali…Anachokifanya ni kumfanya mtu afanye dhambi ya makusudi ili siku ile asiwe na la kujitetea mbele ya kiti cha hukumu. Kwamfano atamzuia mtu asiende kubatizwa katika ubatizo sahihi wa maji mengi, ambapo ni kitendo cha dakika moja tu kuzama mwili wote na kunyanyuka juu na anakifanya mara moja tu katika Maisha yake…atamzuia kufanya hivyo lakini atamshawishi kwa nguvu nyingi kwenda kila siku kuogelea kwenye fukwe za bahari au katika mabwawa ya starehe hata kwa masaa kadhaa bila kuchoka …Hiyo yote ni ili akose la kujitetea katika siku ile ya hukumu.
Kadhalika atamzuia mtu na kumfanya apinge vikali kukaa katika sala au ibada masaa 6 lakini atamweka katika kumbi za starehe au katika televisheni au mitandao kwa masaa hata 10 kwa siku..ili kwamba siku ile atakaposimamishwa mbele ya kiti cha hukumu asiwe na cha kujitetea.
Vivyo hivyo atamzuia leo hii asishiriki kuosha miguu ya watakatifu lakini huyo huyo kijana atakuwa tayari kwenda kuosha wanawake miguu katika vibaraza na masaluni. Na mwanamke hivyo hivyo hatataka kushiriki kufanya ibada ya kuosha au kuoshwa miguu kanisani na wanawake wenzake lakini kila baada ya siku 3 ataketi vibarazani kuoshwa miguu tena na jinsia tofauti na yake. Hiyo ndiyo kazi ya shetani kukoroga mambo…
Ndugu kama unafanya hivyo fahamu kuwa hutakuwa na la kujitetea siku ile ya hukumu.
Mwanamke au binti kama unakwenda kuoshwa miguu na kusuguliwa kucha na wanaume saluni au vibarazani..basi fahamu kuwa bado neema ya Mungu haijakaa juu yako (bado kuna nguvu za giza zimekushika)! Tena zimekushika kweli kweli..Unahitaji kumpokea Yesu Kristo kwasababu Mtu aliyeokoka kwa kudhamiria kabisa kumfuata Yesu Kristo, mambo hayo hawezi kuyafanya wala hata hayamwingii akilini…..
Vitu vya kwanza kabisa Roho Mtakatifu kumshuhudia mtu aviache ni uasherati na vichocheo vyake vyote. Na kichocheo kimojawapo cha uasherati ni kuoshwa miguu na wanaume vibarazani, hakuna namna yoyote kitendo hicho kisiwe kichocheo cha uasherati..hakuna!!..Kila anayefanya hivyo au anayefanyiwa kuna roho ya uasherati ipo ndani yake. (Na waasherati wote hawataurithi ufalme wa mbinguni biblia inasema hivyo katika 1wakorintho 6:9)…Na licha tu ya Roho ya uasherati kuna roho nyingine zinakuwa zinamwingia kila anayefanyiwa hivyo…
Wengi wanaooshwa miguu wakitoka pale shetani anaingiza roho ya muunganiko kati ya hao wawili, unakuta mtu alikuwa ameolewa lakini hampendi tena mume wake wala Watoto wake..anakuwa anapenda jamii ya watu au rika la watu kama wale waliomwosha miguu…na hata ile hamu na kiu ya kumtafuta Mungu inakufa!..Ile Nuru ndogo ambayo pengine ilikuwa imeshaanza kuangaza ndani yake inazima..hata kama alikuwa ametoka kwenye mahubiri na yamemchoma na hivyo ameamua kugeuka..kitendo tu cha kushuka pale na kuosha miguu..shetani anaiiba ile mbegu..Na Maisha ya huyo mtu yanaharibika mara mbili Zaidi. Na kama binti hajaolewa, kitendo cha kwenda kuoshwa miguu tayari ameikusanya hatima yake mikononi mwa shetani..kuolewa kwake inakuwa ni ngumu, au hata akiolewa ataolewa na mtu ambaye si sahihi..
Wanawake wengi imekuwa ni rahisi kushambuliwa na nguvu za giza kwa namna hiyo, kwasababu kila mlango wanaouona mbele yao bila kuhakiki kwanza wanaiga, na mwisho wa siku wanaangukia katika mitego ya shetani bila wao kujijua.
Madhara hayo pia yanawapata wanaume wanaooshwa miguu na wanawake au wanaooshwa vichwa masaluni na kufanyiwa massage. Madhara ni hayo hayo..
Hivyo kama unajiona unaweza kukesha kwenye mitandao usiku kucha huo ni uthibitisho kwamba unauwezo wa kukesha ukisali usiku mzima, kama ulikuwa unauwezo wa kuogelea masaa kadhaa bila kuchoka pwani basi unaweza kwenda kubatizwa kitendo cha dakika moja tu..kama ulikuwa unaweza kuosha au kuoshwa miguu masaluni..unaweza kufanya hayo hayo kwa watakatifu wenzako wa jinsia moja na wewe kanisani au manyumbani na ukapata baraka nyingi zaidi badala ya laana.
Ukiwaosha watakatifu wenzako miguu wa jinsia moja na wewe..utaonyesha ishara ya unyenyekevu na hivyo Bwana atakukweza badala ya kukushusha…Na pia utaongeza uhusiano wako na wakristo wenzako jambo ambalo halitampa nafasi shetani kuwajaribu.Na utafanikiwa katika mambo yote, na Zaidi sana kujiwekea nafasi nzuri ya kuingia mbinguni.
Ubarikiwe sana.
Kama ulikuwa hujaokoka na leo umekusudia kabisa kuokoka na kuacha vitu vyote viovu ulivyokuwa unavifanya ikiwemo kuhudhuria kuoshwa au kuosha miguu kwenye masaluni ya kike…
Basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie maisha yako yote kama ilivyokuwa hata kwetu sisi. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.
EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, .
NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.
ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.
AMEN.
Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, ikiwemo kuhuhudhuria kwenye vibaraza vya kuoshwa miguu na kuacha mambo yote ya kiulimwengu..Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.
Ubarikiwe sana
Mada Nyinginezo:
MEZA YA BWANA, NA KUTAWADHANA MIGUU.
LOLOTE ATAKALOWAAMBIA FANYENI.
Nini tofauti ya haya maneno. 1) KUOKOKA, 2) WOKOVU, 3) KUONGOKA.?
JE! UMEPOKEA KWELI ROHO MTAKATIFU?
JE! UNAYO NAFASI MBINGUNI?
KUOTA UNAFANYA TENDO LA NDOA.
KUOTA UMEPOTEA.
KUOTA UPO UCHI.
Neno la Mungu au kwa jina lingine linaitwa Gombo, ni dawa inayoponya maisha ya mtu kwa ujumla.Tofauti na Dawa nyingine, ambazo zinaweza kuishia kuponya mwili tu, na baada ya hapo hakuna kitu kingine zinaweza kufanya, na licha tu ya kutibu kifo bali hata nafsi iliyopondeka hakuna dawa yoyote inayoweza kuiponya isipokuwa Neno la Mungu peke yake, (Mithali 4:20-22), Na hiyo ndio inayolifanya Neno la Mungu liwe ni dawa bora kuliko dawa yoyote ambayo ilishawahi kuwepo duniani.
Lakini pia kabla ya kuzifurahia dawa tunapaswa tujifunze asili ya dawa jinsi zilivyo, kama mtu hajui dawa huwa zinaasili gani basi ni rahisi kukata tamaa na asikae arudie tena kuzijaribu ..Kwasababu sikuzote dawa huwa hazina ladha nzuri mdomoni, dawa nyingi ni chungu, tena chungu kweli kweli kiasi kwamba zinakufanya uzimeze nzima nzima, vinginevyo unaweza kutapika endapo ukizitafuna..Lakini tunajua pamoja na uchungu wake wote huo zikishafikia tumboni basi uchungu wote unakuwa umeisha hatuusikii tena, baada ya hapo tunasubiria tu matokeo mazuri ya kuponywa miili yetu, na mwisho wa siku tunazifurahi zile dawa, tunazisifia japokuwa hapo mwanzoni tulikuwa tunakunja nyuso zetu kama vile tunamezeshwa sumu.
VIvyo hivyo tunapaswa pia tujue asili ya dawa KUU (Neno la Mungu) pale tunapokusudia kulila, kwa lengo la kupata uzima, linatabia gani rohoni mwetu..Tofauti na dawa za asili kwamba tunapozila zinakuwa chungu mdomoni mwetu lakini zikifika tumboni zinakuwa ni raha..Neno la Mungu (Gombo) ni kinyume chake.. biblia inasema Mdomo ni tamu kama asali lakini likifika tumboni libadilika na kuwa chungu sana…
Yohana alipopewa kitabu kile (yaani Ufunuo ule) aule alipewa angalizo hilo mapema kabisa..tusome.
Ufunuo 10:8 “Na sauti ile niliyoisikia kutoka mbinguni ilinena nami tena, ikisema, Enenda, ukakitwae kile kitabu kilichofunguliwa katika mkono wa yule malaika, aliyesimama juu ya bahari na juu ya nchi.
9 Nikamwendea malaika yule nikamwambia kwamba anipe kile kitabu kidogo. Akaniambia, Kitwae, ukile, nacho kitakutia uchungu tumboni mwako, bali katika kinywa chako kitakuwa kitamu kama asali.
10 Nikakitwaa kile kitabu kidogo katika mkono wa malaika yule, nikakila; nacho kikawa kitamu kama asali kinywani mwangu, na nilipokwisha kukila tumbo langu likatiwa uchungu.
11 Wakaniambia, Imekupasa kutoa unabii tena juu ya watu na taifa na lugha na wafalme wengi”.
Ezekieli naye aliambiwa hivyo hivyo…
Ezekieli 2:9 ‘Nami nilipotazama, mkono ulinyoshwa kunielekea; na tazama, gombo la chuo lilikuwa ndani yake.
10 Akalikunjua mbele yangu; nalo lilikuwa limeandikwa ndani na nje; ndani yake yalikuwa yameandikwa maombolezo, na vilio, na ole!
3:1 “Akaniambia, Mwanadamu, kula uonacho; kula gombo hili, kisha enenda ukaseme na wana wa Israeli.
2 Basi nikafunua kinywa changu, naye akanilisha lile gombo.
3 Akaniambia, Mwanadamu, lisha tumbo lako, ulijaze tumbo lako kwa hili gombo nikupalo. Ndipo nikalila, nalo kinywani mwangu lilikuwa tamu, kama utamu wa asali”.
Unaona asili ya dawa KUU (Neno la Mungu), ni tamu kama asali, wengi tunaposikia habari za kwenda mbinguni kwa kumwamini tu YESU tunafurahia, tunaposikia Yesu anakupenda mwenye dhambi tunafurahia, tunaposikia mafunuo mapya kila siku Kristo anayotufundisha kila kona juu ya habari za ufalme wa mbinguni tunafurahia sana, ni asali nzuri, tunaposikiwa tunahesabiwa haki kwa neema, tunafurahia Zaidi, tunaposikia alifanyika maskini ili sisi tuwe matajari ni maneno mazuri yenye faraja..Hiyo inatufanya wengi tuvutiwe na wokovu, si ndio?..Lakini ili Neno la Mungu lifanye kazi yote ya kumwokoa mtu ni lazima lishuke tumboni limengenywe Uponyaji wa Roho yake uanze kufanya kazi na ndio hapo uchungu unapoanzia..
Wengi wanaishia kulitapika na kurudi nyuma, wanafananishwa na zile mbegu zilizoangukia kwenye miamba, ambao ni watu waliopitia dhiki kidogo tu kwa ajili ya lile Neno wakajikwaa wakarudi nyuma.., Pale Bwana Yesu anaposema jitwike msalaba wako unifuate, wengi hawataki kusikia hivyo, wanataka waendelee kukaa katika dhambi zao na huku wanasema wameokoka, wanataka waendelee kwenda disko na huku wanasema tumeokoka na tumebatizwa, wanataka waendelee kuvaa vimini na suruali na kuweka make-up na huku waseme tumeokoka tunampenda Yesu.
Wakidhani kuwa wameokolewa kweli,?.. Sio tu kufurahia unahubiriwa kila siku Neno la Mungu unasema sasa ninajua mafunuo mengi, ukadhani ndio tayari Umekamilishwa Maisha yako, Hapo ndugu bado hujaanza ikiwa hutataka kuyatiii maneno Bwana Yesu aliyoyasema, basi ujue kuwa wokovu wako ni batili.
Mathayo 16:24 “Wakati huo Yesu aliwaambia wanafunzi wake, Mtu ye yote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake, anifuate.
25 Kwa kuwa mtu atakaye kuiokoa nafsi yake, ataipoteza; na mtu atakayepoteza nafsi yake kwa ajili yangu, ataiona.
26 Kwani atafaidiwa nini mtu akiupata ulimwengu wote, na kupata hasara ya nafsi yake? Au mtu atatoa nini badala ya nafsi yake?
Injili imekuvuta kwa maneno mazuri na ya faraja kwa muda mrefu, umeshauona uzuri uliopo ndani ya Kristo kwa muda mrefu, umeshajua faida zote mtu anazozipata akimfuata Kristo, unaendelea kulifurahia tu Neno la Mungu mdomoni mwako lakini hutaki kulimeza, kisa tu unaogopa Baba atanitenga, mama atanichukia, marafiki watanionaje..kazini watanifikiriaje, wakisikia mimi nimeokoka,..Ndugu kama unapenda Kristo ayaokoe Maisha yako kikweli kweli unapaswa ufanye maamuzi hayo pia..
Mathayo 10:34 “Msidhani ya kuwa nimekuja kuleta amani duniani; la! Sikuja kuleta amani, bali upanga.
35 Kwa maana nalikuja kumfitini mtu na babaye, na binti na mamaye, na mkwe na mkwe mtu;
36 na adui za mtu ni wale wa nyumbani mwake.
37 Apendaye baba au mama kuliko mimi, hanistahili; wala apendaye mwana au binti kuliko mimi, hanistahili.
38 Wala mtu asiyechukua msalaba wake akanifuata, hanistahili.
39 Mwenye kuiona nafsi yake ataipoteza; naye mwenye kuipoteza nafsi yake kwa ajili yangu ataiona”.
Huu ni wakati wa kuyapokea maneno ya Mungu kwa moyo wote na kuyafanyia kazi, hizi ni siku za mwisho za kanisa la watu walio vuguvugu lijulikanalo kama Laodikia (Ufunuo 3:14)ambao watu wake ni watu walio vuguvugu wa hali ya juu sana..Na hao Kristo amesema atawatapika. Je na wewe unasubiri utapikwe baada ya kukaa katika uvuguvugu huo kwa muda mrefu?. Fanya uamuzi wa kulimeza Neno lote zima zima bila kujali ni nini kitakutokea mbele kwasababu kwa kufanya hivyo ndivyo utakavyoinusuru roho yako katika nyakati hizi za uvuguvugu ambao kila mtu hata mlevi, mzinzi, fisadi, hata msanii wa nyimbo za kidunia anasema ameokoka..
Bwana akubariki.
Mada Nyinginezo:
WAZAZI WA YOHANA NA YAKOBO.
NAMNA YA KUITAMBUA SAUTI YA MUNGU INAPOZUNGUMZA NA WEWE
KUOTA UNAKULA CHAKULA.
URIMU NA THUMIMU NI NINI KATIKA BIBLIA?
UNAMALIZAJE MWAKA WAKO, JE NA MUNGU AU SHETANI?
USILALE USINGIZI WAKATI WA KUMNGOJEA BWANA.
ANTIPA SHAHIDI WANGU, MWAMINIFU WANGU.
Jina kuu la Mwokozi wetu Yesu Kristo libarikiwe…Karibu tena tujifunze maandiko…kwa kuwa jukumu kuu tulilonalo kila siku ni kumjua sana Yesu Kristo mwana wa Mungu na kuhakiki kila siku ni nini kimpendezacho sawasawa na Waefeso 4:13 na 5:10.
Leo tutayatafakari maneno ya Bwana Yesu Kristo aliyoyasema katika kitabu cha Mathayo.
Mathayo 12:30 “Mtu asiye pamoja nami yu kinyume changu; na mtu asiyekusanya pamoja nami hutapanya”.
Ukianzia mstari wa juu kidogo utaona kuna tukio Fulani lilifanyika ambapo likamsababisha aseme hayo maneno..Lakini tukiyatafakari maneno hayo kwa undani tunaweza tabia mojawapo ya Mungu na hivyo kuchukua tahadhari kwa kila tunachokifanya..
Sasa mstari huo Bwana Yesu anasema… “Mtu asiye pamoja nami yu kinyume changu”…na… “Mtu asiyekusanya pamoja nami hutapanya”..Hizo ni sentensi mbili zinazozungumzia kitu kimoja.
Nimewahi kukutana na mtu anasema mimi simwamini Bwana Yesu lakini natenda haki, nasaidia maskini, sinywi pombe, siibi, situkani n.k..Je Mungu atanihukumu kwa sababu tu simwamini Yesu Kristo?..Mwingine atakuambia mimi simwamini Yesu lakini nampenda na namuheshimu na simpingi…..Nataka nikuambie ndugu yangu..kitendo tu cha wewe kutokuwa upande wa Yesu Kristo hata kama unatenda mema kiasi gani..mbele zake tayari upo kinyume chake..haijalishi unafanya mema mengi kiasi gani..kitendo tu cha wewe kujiepusha na yeye tayari upo kinyume chake..roho ya mpinga-kristo ipo ndani yako. Tayari unahesabika kama mtu unayempinga Kristo ..kwasababu anasema.. “Mtu asiye pamoja nami yu kinyume changu”
Kadhalika kama huifanyi kazi ya Mungu na umepewa hiyo neema…na unasema “aa mimi sifanyi kazi ya Mungu lakini siipingi kazi ya Mungu”…Nataka nikuambie kitendo tu cha wewe kutoifanya kazi ya Mungu na huku umepewa hiyo Neema…mbele zake unaonekana unaitapanya kazi yake…kwasababu anasema “Mtu asiyekusanya pamoja nami hutapanya”..Na wewe hukusanyi pamoja na Mungu, hivyo ni wazi kuwa unakusanya sehemu nyingine ambayo inakinzana na Mungu..Kitendo cha wewe kukataa kuifanya kazi ya Mungu na kuendelea kufanya mambo yako mengine, tayari unaiharibu kazi ya Mungu…Kwahiyo kuna madhara makubwa ya kukaa kutokuifanya kazi ya Mungu..kwasababu mbele zake tunaonekana kama tunaitapanya.
Ndio maana kuna mfano mmoja Bwana aliutoa na kusema..
Luka 13:6 “Akanena mfano huu; Mtu mmoja alikuwa na mtini umepandwa katika shamba lake la mizabibu; akaenda akitafuta matunda juu yake, asipate.
7 Akamwambia mtunzaji wa shamba la mizabibu, Tazama, miaka mitatu hii naja nikitafuta matunda juu ya mtini huu, nisipate kitu; uukate, MBONA HATA NCHI UNAIHARIBU?
8 Akajibu akamwambia, Bwana, uuache mwaka huu nao, hata niupalilie, niutilie samadi;
9 nao ukizaa matunda baadaye, vema! La, usipozaa, ndipo uukate”.
Nataka uuone huo mstari unaosema ..“Mbona hata nchi unaiharibu”..Maana yake ule mti ambao hauzai matunda kitendo tu cha kuendelea kuwepo pale tayari unaiharibu nchi/ardhi. Unaweza kusema si ubaki tu kwani usipozaa unaathari gani? …Biblia inasema “kwa kuendelea kuwepo pale unaiharibu nchi”.
Vivyo hivyo kuwepo kwako kama hufanyi kazi ya Mungu basi fahamu kuwa Unaiharibu kazi ya Mungu bila kujua…Kuwepo kwako kama hufanyi mapenzi ya Mungu basi unaiharibu kazi ya Mungu…kadhalika unaishi maisha ya kuvaa nusu uchi,kuvaa suruali na nguo zinazobana na fupi, na kupaka lipstick, wanja, kuvaa mawigi na hereni ni kweli una moyo mzuri unasaidia watu, una huruma na wakati mwingine unakwenda kanisani, na wala hutukani, wala huibi, …ni kweli unafanya mambo mazuri mengi lakini kwa mavazi yako unaiharibu kazi ya Mungu..kwasababu wakati Roho wa Mungu anafanya kazi kwa nguvu kuwahubiria watu waepukane na mavazi hayo ya kikahaba na mambo ya kidunia..wewe unafanya kazi ya kuwahubiria waendelee kuvaa kwa jinsi wanavyokuona wewe unavyoyavaa,…
Wakati Roho Mtakatifu anafanya kazi kwa nguvu kuwaonya watu waache kupaka hivyo vitu usoni na kichwani na wajiepushe na hukumu inayokuja…wewe unawahubiria mambo hayo ni sahihi kufanya kwa jinsi unavyoendelea kuyafanya….Hivyo unakwenda kinyume na kazi ya Mungu (unaiharibu kazi ya Mungu…) “Unakuwa hukusanyi pamoja na Kristo bali unatapanya”.. na hivyo unahesabika kwamba upo kinyume na Kristo (yaani mpinga-kristo)…haijalishi unafanya mema mengi kiasi gani.
Bwana akubariki.
Kama hujaokoka, mlango wa Neema upo wazi fanya hivyo leo..Tunaishi katika siku za mwisho, na Siku yoyote parapanda inalia, na watakatifu watanyakuliwa kwenda mbinguni..Na biblia inasema “ufalme wa Mungu unapatikana kwa nguvu”..Nao wenye nguvu ndio watakaouteka…Hivyo si wakati wa kujivuta vuta tena, Si wakati wa kuhubiriwa injili ya kubembelezwa..ni wakati wa kujitwika msalaba wako na kumfuata Kristo pasipo kuangalia nyuma au kuangalia ndugu au Rafiki anasemaje.
Hivyo unachopaswa kufanya sasa ni kutubu kwa kumaanisha kabisa…maana yake unaacha maisha yote ya dhambi uliyokuwa unaishi ambayo yalikuwa yanaifanya kazi ya Mungu iharibike..Unaacha ulevi, usengenyaji, wizi, rushwa, utukanaji, unaacha kujichua, unaacha visasi, wivu, uvaaji mbaya, unakwenda kuchoma vimini vyote na suruali na vipodozi vyote ulivyokuwa unatumia na mambo mengine yote yasiyofaa.
Na baada ya kufanya tendo hilo la Imani, utakuwa umemtii Kristo, na hivyo Neema ya kipekee itaachiliwa juu yako ambayo hiyo itakusaidia kushinda dhambi bila kutumia nguvu nyingi..utajikuta tu ile hamu na nia ya kufanya dhambi inakufa yenyewe…lakini sharti kwanza uamua kuacha wewe mwenyewe kwa vitendo ili Bwana aione Imani yako.
Na mwisho, tafuta kanisa la kiroho ambalo linamhubiri Yesu Kristo wa kwenye biblia jiunge hapo na pia ulizia ubatizo, ili ukabatizwe kama hujabatizwa,..kumbuka ubatizo sahihi ni ule wa kuzamishwa mwili wote kwenye maji mengi..na kwa Jina la Yesu Kristo sawasawa na (Matendo 2:38)..zingatia hilo sana..Na Bwana atakuongoza kufanya mengine yaliyosalia ikiwemo kukuuongoza na kukutia katika kweli yote ya maandiko.
Bwana akubariki sana.
Mada Nyinginezo:
Mbona Mungu anaruhusu watu wapate shida, ilhali ana uwezo wa kutuepusha?
Ulinzi wa daima (eternal security) Je! ni neno la kimaandiko?
Je! mtu aliyeokoka anaruhusiwa kumiliki Lodge ambayo ina Bar ndani yake?
Je kuzalishwa na mkunga wa kiume ni dhambi?
HAJANENA KAMWE MTU YE YOTE KAMA HUYU ANAVYONENA.
UFUNUO: Mlango wa 1
NENO NI LILE LILE, LAKINI UJUMBE NI TOFAUTI.