Category Archive Uncategorized @sw-tz

UTUKUFU NA HESHIMA.

Utukufu na Heshima.


Mungu wetu ndiye anayestahili utukufu na heshima yote..biblia inatuambia hivyo katika..

Ufunuo 4:11  “Umestahili wewe, Bwana wetu na Mungu wetu, kuupokea UTUKUFU NA HESHIMA na uweza; kwa kuwa wewe ndiwe uliyeviumba vitu vyote, na kwa sababu ya mapenzi yako vilikuwako, navyo vikaumbwa”.

Lakini Pamoja na hayo Mungu wetu sio mchoyo, yupo tayari kumvika utukufu na heshima kila mtu  ambaye atakuwa tayari kumpokea, na kuishi Maisha matakatifu na kuyashinda Maisha ya ulimwengu biblia inatuambia..

Warumi 2:10  “bali utukufu na heshima na amani kwa kila mtu atendaye mema, Myahudi kwanza na Myunani pia; 11  kwa maana hakuna upendeleo kwa Mungu”.

Unaona?. Kuna mambo mazuri sana, Mungu aliyotuandalia mbinguni, mambo ambayo jicho halijawahi kuona wala sikio kusikia, wala hayajawahi kuingia katika moyo wa mwanadamu. Tutavikwa mataji ya utukufu na heshima, tutang’aa kama jua, tutaishi Maisha ya raha na furaha milele, tutasahau yote tuliyopitia nyuma. Tutapewa miili ya utukufu isiyougua milele, isiyozeeka, isiyo chakaa, isiyo minyonge, isiyo na ulemavu. Na Zaidi ya yote Tutatawala la Mungu, tuyafurahia Maisha kwa miaka isiyokuwa na mwisho,.. Ni raha iliyoje? Ni heri tukose kila kitu duniani lakini tusikose, heshima hiyo Mungu aliyotuandalia kule ng’ambo.

Lakini, ni kinyume chake ni kwamba wale ambao leo hii duniani hawataki kuutafuta huu utukufu na heshima idumuo, utokao kwa Mungu, siku ile ya hukumu watapata hasira na ghadhabu ya milele.

Warumi 2:7  wale ambao kwa saburi katika kutenda mema wanatafuta utukufu na heshima na kutokuharibika, watapewa uzima wa milele;

8  na wale wenye fitina, wasioitii kweli, bali wakubalio dhuluma, watapata hasira na ghadhabu;

9 Utukufu na Heshima ya mwanadamu atendaye uovu, Myahudi kwanza na Myunani pia.

Tunaishi katika siku ambazo unyakuo, unaweza kutokea siku yoyote. Na watakatifu kunyakuliwa mbinguni. Dalili zote zinathibitisha hilo, na dalili mojawapo kuu ni hilo la kuzuka kwa magonjwa yasiyokuwa na tiba ambayo biblia imeyafananisha na TAUNI..Leo hii duniani tunaona magonjwa kama CORONA, yanatimiliza unabii wazi wazi mbele ya macho yetu…Tuseme nini tena?

Je wewe nawe bado upo nje ya Kristo? Ingia ndugu yake ndugu yangu, Kristo ayabadilishe Maisha yako. Ukiamua leo kwa dhati kutubu dhambi zako Kristo atakupa utukufu na heshima isiyoharibika kwako. Haijalishi ulikuwa mlevi kiasi gani, umetoa mimba nyingi namna gani, umeua watu wengi kiasi gani, umeloga sana watu namna gani, umezini mara nyingi namna gani..Kristo yupo tayari kukusamehe leo hii ikiwa kwa moyo wako wa dhati utakubali..

Kama upo tayari kufanya hivyo..

Basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie maisha yako yote kama ilivyokuwa hata kwetu sisi. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU  MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.

AMEN.

Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako.

Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.

Ubarikiwe sana.

Utukufu na Heshima, zina Mungu wetu daima.

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

UNYAKUO.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!

MAONO YA NABII AMOSI.

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Mungu ni Mungu tu!

Mungu ni Mungu tu!.


Watu wengi tunadhani, tunaweza kumuudhi Mungu au kumkomoa Mungu kiasi cha kumgharimu kupoteza kitu fulani, pale tunapofanya jambo lisilompendeza..

Biblia inasema hivi..

Ayubu 35:6 Ikiwa umefanya dhambi, umefanya nini juu yake? Yakiwa makosa yako yameongezeka, wamfanyia nini yeye?

7 Ikiwa u mwenye haki, wampa kitu gani? Au yeye hupokea nini mkononi mwako?

8 Uovu wako waweza kumwumiza mtu kama wewe; Na haki yako yaweza kumfaa mwanadamu.

Unaona, Kumbe hata haki zetu, au matendo yetu mazuri, hayamwongezi Mungu kitu chochote, hayamwongezei umri wa kuishi, kwa yeye tayari ni wa milele, hayamwongezei afya, wala chochote kile kizuri kwasababu vitu vyote vinatoka kwake.

Warumi 11:36 “Kwa kuwa vitu vyote vyatoka kwake, viko kwa uweza wake, tena vinarejea kwake. Utukufu una yeye milele. Amina”.

Tukisema, tujiue, hakumbadilishi yeye kuwa Mungu, tukisema hatumpendi bado hakumfanyi yeye kutokuwa Mungu, hata tukisema hayupo, ndio kabisa hakuubadilishi uungu wake. Ndege wataendelea kumsifu, jua litaendelea kuangaza majira yake, anga litaendelea kuwa la blue.

Hivyo tunachopaswa kufanya ni kujinyenyekeza mbele zake tu, haijalishi leo hii tunapitia magumu mengi kiasi gani, au mazuri mengi kiasi gani, tukiwa wanyenyekevu mbele zake, wakati wake ukifika tutauna wema aliotuwekea sisi tunaomtumainia ..Kuzielewa njia zote za Mungu hiyo haiwezekani, hata tupambane vipi, lakini tunachojua tu ni kuwa anatuwazia mawazo mazuri siku zote,

Yeremia 29:11 Maana nayajua mawazo ninayowawazia ninyi, asema Bwana, ni mawazo ya amani wala si ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za mwisho.

Hivyo ndugu yangu unausoma ujumbe huu pengine, bado hujaokoka, wakati uliokubalika ndio sasa, usiache leo ipite bila kuyasalimisha maisha yako kwa Kristo. Ukimaanisha na kudhamiria kweli kutubu, hapo ulipo haijalishi upo sehemu gani, Kristo atayageuza maisha yako mara moja, na kukupa badiliko la ajabu ambalo litakufanya ulistaajabie maisha yako yote..

Kama upo tayari kufanya hivyo basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie maisha yako yote kama ilivyokuwa hata kwetu sisi. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU  MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, . NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.

AMEN.

Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, kuanzia huu wakati, Kwasababu Mungu ameshaipokea toba yako . Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako sawasawa na Matendo 2:38.

Mungu ni Mungu tu!

Ubarikiwe sana.

Mada Nyinginezo:

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

CHUKIZO LA UHARIBIFU

UTENDAJI KAZI WA MPINGA-KRISTO.

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!

JINSI SODOMA NA GOMORA ILIVYOKUWA INAVUTIA SANA..

Rudi Nyumbani:

Print this post

UTOE MWILI WAKO KWA BWANA KWASABABU SI MALI YAKO.

Jambo linalotupa wengi kiburi ni kufikiri kwamba miili hii tuliyonayo ni mali yetu wenyewe..Lakini kama mtu ukitenga muda na kutafakari kwa kina utakuja kugundua kuwa mwili ulionao hauna mamlaka nao asilimia mia, na hivyo huo ni uthibitisho kwamba si mali yako kabisa..

Kama mwili ungekuwa ni mali yako ungekuwa na uwezo wa kujichagulia kimo, au rangi au jinsia…ungekuwa pia na uwezo wa kuyazuia mapigo ya moyo yasidunde pindi unapotaka, au ungekuwa na uwezo wa kuzuia damu isizunguke mwilini au mwili usitoe jasho wakati wa joto linapozidi kuwa kali. Lakini kama mojawapo ya mambo hayo huwezi basi ni uthibitisho kwamba huo mwili ni mali ya mtu mwingine ambaye wewe humjui. Kwa ujumla sio milki yako binafsi…Kama biblia inavyosema..

1Wakorintho 6:19 “Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, mliyepewa na Mungu? WALA NINYI SI MALI YENU WENYEWE”

Kwasababu hiyo basi ndio maana ni lazima tuishi chini ya amri za mwenye miili hii…akisema miili hii haipaswi kufanywa kituo cha dhambi..basi tunatii kwasababu sio mali yetu..akisema hatupaswi kuitumia kwa zinaa, au ulevi, au uasherati basi ni lazima tutii kwasababu sio ya kwetu ni yake yeye. Sisi ni wageni waalikwa au wapangaji tu ndani ya hii miili yake..Hatuna uhuru asilimia 100 wa kuiweka tunavyotaka sisi. Akisema hatupaswi kuivisha mavazi yapasayo jinsia nyingine, hatupaswi kuhoji kwanini au kwasababu gani.

Sasa hebu tujifunze Zaidi juu Mmiliki wa hii miili tuliyonayo.

Kuna wakati Bwana wetu Yesu aliulizwa swali lifuatalo na Mafarisayo…

Mathayo 22:17 “Basi utuambie, Waonaje? Ni halali kumpa Kaisari kodi, ama sivyo?

18 Lakini Yesu akaufahamu uovu wao, akasema, Mbona mnanijaribu, enyi wanafiki?

19 Nionyesheni fedha ya kodi. Nao wakamletea dinari.

20 Akawaambia, NI YA NANI SANAMU HII, NA ANWANI HII?

21 Wakamwambia, Ni ya Kaisari. Akawaambia, Basi, mlipeni Kaisari yaliyo ya Kaisari, NA MUNGU YALIYO YA MUNGU”

Ukisoma mstari huo wa 20 utaona Bwana anawauliza maswali mawili..1).Ni ya nani sanamu hii? Maana yake ile sura juu ya ile sarafu ni sura ya nani?…2).Na ni ya nani anwani hii?. Na wote wakajibu ni ya Kaisari..na yeye Bwana akawaambia vya Kaisari mpeni Kaisari na vya Mungu mpeni Mungu..

Sasa swali linakuja, vya Mungu ni vipi hapo?…Ndio vinaweza kuwa navyo pia ni fedha, (kama sadaka, zaka au malimbuko)..lakini hebu leo tuingie ndani Zaidi kujifunza vilivyo vya Mungu ni vipi.

Turudi kusoma kitabu cha Mwanzo..

Mwanzo 1: 26 “Mungu akasema, Na tumfanye MTU KWA MFANO WETU, KWA SURA YETU; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi.

27 Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba”.

Mpaka hapo utakuwa umeona vya Mungu ni vipi?…Miili yetu ndio vya Mungu tunavyopaswa tumpe..kwasababu miili yetu ndio imebeba SURA na MFANO wa Mungu…Kwahiyo kama Bwana alivyowaambia watu wampe kodi Kaisari kwasababu tu sarafu ile imebeba sura yake na anwani yake..zaidi sana tunapaswa tumpe Kristo miili yetu kwasababu imebeba sura na mfano wa Mungu..

Kwahiyo tunapaswa tujipime kila siku je hii miili yetu tunaiweka jinsi Mungu anavyotaka?…Je tunaiweka katika utakatifu, je tunaishughulisha katika kufunga na kuomba na kuifikisha kwenye nyumba za Ibada?..Kama hufanyi hivyo, kila ukifika muda wa kuomba unasema umechoka!..ukifika muda wa kufunga unasema unaumwa, ikifika siku ya kwenda kwenye ibada unasema unapumzika…Kumbuka utatoa hesabu siku ile kwa mwenye huo mwili.

Kama unautumia mwili huo kuufanyia uzinzi, au uasherati…jitafakari sana, kama unafikiri ni mali yako hiyo anza kujitafakari tena upya, kama unafikiri una uhuru wa kuitembeza bila mavazi au kuichubua, au kuiweka kila aina ya matangazo anza kujitafakari tena upya, kama unafikiri ni ya kupokea mimba na kutoa tu jinsi utakavyo hilo nalo lifikirie…

Bwana atusaidie daima..

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Mungu alikuwa anaongea na nani aliposema na “Tumfanye mtu kwa mfano wetu”,(Mwanzo 1:26)?

JINSI DHAMBI INAVYOMGHARIMU MTU SANA.

CHAPA YA MNYAMA

Maana ya ‘Usimjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake’

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!

CHUKIZO LA UHARIBIFU

KAMA TUNATAKA KUWA ASKARI WA BWANA, NI LAZIMA TUJUE VIGEZO.

Kwanini kabila la Dani limeondolewa kwenye Ufunuo 7?

Rudi Nyumbani:

Print this post

NAMI NINAZO FUNGUO ZA MAUTI, NA ZA KUZIMU.

Ufunuo 1: 17 “…Usiogope, Mimi ni wa kwanza na wa mwisho,

18 na aliye hai; nami nalikuwa nimekufa, na tazama, ni hai hata milele na milele. Nami ninazo funguo za mauti, na za kuzimu”.

Hayo ni Maneno ya Bwana wetu Yesu Kristo, akiliambia kanisa.. Sasa ukiona mpaka Bwana Yesu anasema anazo funguo za mauti, na kuzimu, ni dhahiri kuwa hapo mwanzo hakuwa nazo, zilikuwa kwa mwingine..Na huyo si mwingine zaidi ya Ibilisi.

Kumbuka Tahadhari ya kwanza Mungu aliyowapa Adamu na Hawa pale Edeni, kuhusu kula Tunda, haikuwa kwamba matokeo yake watakuwa uchi, au watajua mema na mabaya au watakula kwa jasho, au watazaa kuwa uchungu . Hapana, bali tahadhari aliyowapa ya kwanza na ya mwisho ilikuwa ni kuwa WATAKUFA(‘KIFO’)..Siku watakapokula matunda ya mti ule watakufa..akimaanisha watakufa kweli kweli..sio kwamba watakufa halafu siku moja watafufuka hapana, bali watakufa moja kwa moja..

Kwasababu Mungu alimwona muhasisi wa kifo hicho pale Edeni, Lakini wazazi wetu hawakuzingatia hilo badala yake wakala, Na matokeo yake ndio yale tuliyoyaona yalifuata baada ya pale..watu wakawa na makao mengine, baada ya pale yaliyoitwa KUZIMU. Chini ya mungu wao mpya aliyeitwa Ibilisi.

Na ndio maana katika agano la kale, hakukuwa na mtu aliyekuwa na uhakika wa maisha baada ya kifo, ni waisraeli tu ndio walifahamu hilo, nao si wote, isipokuwa wale tu waliokuwa wanafuatailia masuala ya Mesiya, ambaye alitabiriwa kuwa huko mbele atakuja kuwafufua wafu, lakini wengine waliosalia hawakujua hilo…

Na ndio maana tena utaona kulikuwa na mapambano makali kati ya mafarisayo na masadukayo, wengine waliamini kuna ufufuo wa wafu, na wengine hawakuamini hicho kitu (Soma, Matendo 4;1-2,23:7-8, Marko 12:18)..Ni kwasababu gani? Ni kwasababu suala la wafu kufufuliwa lilikuwa si jambo lililoandikwa kwa uwazi sana katika maandiko kama wengi wanavyodhani.. isipokuwa tu waliotambua jambo hilo ni wale waliokuwa wanafuatilia habari za Mesiya kuwa atakuja kufanya jambo hilo.

Kwahiyo wakati wote huo watu walikuwa wametawaliwa na roho ya mauti ya ibilisi.

Warumi 5:14 “walakini mauti ilitawala tangu Adamu mpaka Musa, nayo iliwatawala hata wao wasiofanya dhambi ifananayo na kosa la Adamu, aliye mfano wake yeye atakayekuja”.

Unaona wakati huo wote shetani alikuwa na funguo hizo, alikuwa wakati mwingine anao uwezo hata wa kuwaendea wafu walio watakatifu na kuzungumza nao, soma habari za samweli(1Samweli 28)..

Lakini sasa Kristo alipokuja alipindua kila kitu,(majira yakageuka), kwanza aliiondoa hofu ya mauti ambayo ilikuwa imewatawala wanadamu kwa muda mrefu tangu zamani..

Waebrania 2:14 “Basi, kwa kuwa watoto wameshiriki damu na mwili, yeye naye vivyo hivyo alishiriki yayo hayo, ili kwa njia ya mauti amharibu yeye aliyekuwa na nguvu za mauti, yaani, Ibilisi,

15 awaache huru wale ambao kwamba maisha yao yote kwa hofu ya mauti walikuwa katika hali ya utumwa”.

Na pili akaiteka ile Kuzimu iliyokuwa chini ya shetani, ambayo ndio ilikuwa makao ya wafu wote…

Na ndio maana siku ile alipokufa tu, utasoma makaburi yalipasuka na watakatifu wengi wakatoka makaburini

Mathayo 27:51 “Na tazama, pazia la hekalu likapasuka vipande viwili toka juu hata chini; nchi ikatetemeka; miamba ikapasuka;

52 makaburi yakafunuka; ikainuka miili mingi ya watakatifu waliolala;

53 nao wakiisha kutoka makaburini mwao, baada ya kufufuka kwake, wakauingia mji mtakatifu, wakawatokea wengi”.

Tangu huo wakati hadi leo ibilisi hajui wafu wapo wapi na wanafanya nini saa hii, anachojua tu, ni kuwa wale watakatifu wapo upande wa PEPO(Paradiso) na wale waovu wapo sehemu ya mateso (Jehanum)..Hana uwezo wa kuleta mzimu wa mtu yeyote aliyekufa kwasababu sasahivi Kristo ndiye anayewamiliki walio hai na waliokufa soma Warumi 14:9. Kwahiyo hivyo vinavyoonekana na watu vyenye sura kama za wapendwa waliokufa..kiuhalisia sio wale watu wenyewe, bali ni roho tu za mapepo zilizovaa sura za watu waliokufa…

Kristo sasa ameshashikilia mamlaka yote, ya mbinguni, ya duniani na ya kuzimu..Haleluya.

Hivyo ikiwa wewe ni mtakatifu, kama utakufa leo basi ujue roho yako na nafsi yako itakwenda sehemu salama, yenye raha na pumziko la kweli, mahali pasipoelezeka panapoitwa Pepo, lakini wewe ambaye ni mwenye dhambi, ukifa leo, shetani hakuchukui bali utakayekuchuwa na Mungu mwenyewe na kwenda kukutupa katika jehanamu ya moto ukingoja hukumu ya siku ile ya mwisho..

Unatanga tanga nini kwa waganga wa kienyeji? Hao hawatakusaidia chochote, unawatafuta wanadamu, hao nao hawawezi kukuondolea hofu ya mauti na mashaka uliyonayo sasa, kwamba ukifa utakwenda wapi..Anayeweza kufanya hivyo ni Kristo tu peke yake, mwenye funguo za mauti na kuzimu.Yeye ndiye atakayeweza kukufanya uwe huru na hofu ya kifo, kiasi kwamba hata ikitokea unakufa leo, utakuwa na uhakika kuwa roho yako imekwenda sehemu salama. Ukingojea siku ile kuu ya kwenda mbinguni kwa Baba.

Hivyo leo mpe Kristo maisha yako kama bado hujampa, vivyo hivyo kama ni vuguvugu huu ni wakati wa kuwa moto!.. Tubu dhambi zao kwa kumaanisha kuziacha, hizi ni nyakati za mwisho, parapanda italia wakati wowote, na Yesu atawafufua kwanza wale waliokufa katika haki nao kwa pamoja na sisi tulio hai tutakwenda kumlaki mawinguni,..lakini jiulize wewe mwenye dhambi utakuwa wapi siku hiyo?..Au ukifa leo hii ni nani atayekusaidia huko uendako? Shetani anaivizia roho yako kwasababu anajua ukifa katika dhambi ni umepotea kwelikweli hata yeye mwenyewe hata kuona milele…Hivyo acha leo ulevi, wizi, rushwa, anasa, uasherati, vipodozi unavyopaka, vimini unavyovaa, matusi unayotukana na mambo yote yanayofanana na hayo..Na upokee Roho Mtakatifu ambaye ni ahadi kwetu tutakaomwamini Yesu.

Uamuzi ni wako, tafakari tena kisha chagua uzima. Wokovu ni bure kwa wote wanaouhitaji..Kristo anaokoa kweli.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

TOFAUTI KATI YA HEKALU, SINAGOGI NA KANISA NI IPI?

Nifanye nini ili niondokane na Hofu maishani mwangu?

SI KWA FAIDA YA MWENYEZI, BALI KWA FAIDA YETU.

MWAKA WA BWANA ULIOKUBALIWA.

NAO WAKADHANI YA KUWA YUMO KATIKA MSAFARA;

Nini maana ya maneno haya ya Bwana? “Nami nikiinuliwa juu ya nchi,NITAWAVUTA WOTE KWANGU”(Yohana12:32).

Rudi Nyumbani:

Print this post

Hamtaimaliza miji ya Israeli hata ajapo mwana wa Adamu?

Bwana alimaanisha nini kusema “Hamtaimaliza miji ya Israeli hata ajapo mwana wa Adamu”


Tusome;

Mathayo 10:23 “Lakini watakapowafukuza katika mji huu, kimbilieni mwingine; kwa maana ni kweli nawaambia HAMTAIMALIZA MIJI YA ISRAELI HATA AJAPO MWANA WA ADAMU”

JIBU: Ukiusoma mstari huo kuanzia juu kabisa, yaani kuanzia mstari wa kwanza…Utaona ni Habari inayohusu tendo la Bwana Yesu kuwatuma wanafunzi wake kwenda kuhubiri injili katika miji ya Israeli…Na utaona alipowaagiza wakahubiri aliwapa na baadhi ya maagizo au masharti, kwamba wasichukue chochote na pia wawe wavumilivu kwa watakayoyapitia huko..Lakini mwishoni kabisa mwa maagizo tunaona Bwana anawaambia…“hamtaimaliza miji ya Israeli hata ajapo mwana wa Adamu”..

Sasa swali linalojitengeneza kwenye vichwa vyetu hapo ni kwamba…mbona Bwana Mitume walikuwa wameshaimaliza hiyo miji na Yesu bado alikuwa hajarudi?..ina maana mpaka leo injili haijasambaa kwenye miji yote ya Israeli ndio maana Bwana hajarudi mpaka leo?.

Jibu rahisi la swali hili tunaweza kulipata kwenye Habari kama hii hii katika kitabu cha Luka…Tusome,

Luka 10:1 “Basi, baada ya hayo Bwana aliweka na wengine, sabini, akawatuma wawili wawili wamtangulie kwenda kila mji na kila mahali alipokusudia kwenda mwenyewe.

2 Akawaambia, Mavuno ni mengi, lakini watenda kazi ni wachache; basi mwombeni Bwana wa mavuno apeleke watenda kazi katika mavuno yake.

3 Enendeni, angalieni, nawatuma kama wana kondoo kati ya mbwa-mwitu.

4 Msichukue mfuko, wala mkoba, wala viatu; wala msimwamkie mtu njia”

Tuvichunguze baadhi ya vipengele katika mstari huo wa kwanza ambavyo ndivyo vitakavyotupa dira ya kuelewa Habari nzima….katika mstari wa kwanza biblia inasema… “Bwana aliweka na wengine, sabini, AKAWATUMA WAWILI WAWILI WAMTANGULIE kwenda kila mji na kila mahali alipokusudia kwenda mwenyewe”…Zingatia hilo neno “WAMTANGULIE”..Kama wewe ni mswahili mzuri utaelewa maana ya neno “kutangulia” ni nini…kutangulia maana yake ni mtu anakwenda mahali kisha wewe unafuata baadaye…yaani anawahi kufika kule kabla wewe kufika…hiyo ndiyo maana ya kutangulia…

Hivyo mstari huo una maana kuwa “hao wanafunzi sabini na wale 12 Bwana aliokuwa anawatuma kwenda huko katika miji ya Israeli hakuwatuma tu…huko wenyewe…bali Bwana aliwaahidi kwamba atawafuata, hivyo aliwatuma tu kama wamtangulie.”

Ili kuelewa vizuri tafakari tena kamfano haka… “Umemwagiza mfanyakazi wako atangulie asubuhi na mapema sehemu ya kazi kuendelea na kazi, na ukamwambia hatamaliza kazi zote kabla ya wewe kufika hapo ofisini, maana yake utafika kabla hata hajamaliza kazi zote”.. Ndicho Bwana alichowaambia wanafunzi wake, kwamba huko wanakwenda naye pia atakuja kabla hawajaimaliza miji yote ya Israeli (Hilo ni neno la Faraja)…Na kweli aliiungana nao baadaye hakuwaacha yatima…

Sasa kuna jambo moja la kujifunza hapo…Kwamba Desturi ya Bwana ilikuwa hafiki mahali kabla ya kutuma kwanza wajumbe wake wakamtengenezee njia…Maana yake kabla ya yeye kuja mahali anatuma kwanza watumishi wake wakahubiri injili..Ndivyo alivyofanya kwa Yohana Mbatizaji…yeye alitumwa kumtengenezea Bwana njia na kuiandaa mioyo ya watu kabla Bwana mwenyewe hajaanza kuhubiri..ili atakapoanza kuhubiri vile Bwana atakavyohubiri visiwe ni vitu vigeni sana kwa watu wake.(kasome Yohana 10:41-42, na Luka 1:17).

Utaona sehemu zote kabla Bwana hajaenda mahali huwa anatuma wanafunzi wake kwanza na baadaye anaungana nao.. (kasome Luka 9:52-54, Marko 14:12-18, Marko 11:1-4)..

Ndugu Mpendwa hata sasa, Bwana bado anatuma watu wake kuitengeneza njia yake…Umesikia injili mara ngapi?, kila mahali upitapo, mtaani, kwenye magari, mashuleni, unapofanyia kazi?..lakini unadharau kwasababu labda anayekuhubiria umemzidi kipato, au umemzidi elimu, au umri?..Lakini lisikie hili neno ambalo Bwana Yesu alilisema..

Marko 9:37 “Mtu akimpokea mtoto mmoja wa namna hii kwa jina langu, anipokea mimi; na mtu akinipokea mimi, humpokea, si mimi, bali yeye aliyenituma”

Hako katoto unakokadharau sasa, huyo uliyemzidi elimu, pengine na kipato…huyo ambaye hata maandiko hawezi kuyatamka vizuri na anakuhubiria utubu umgeukie Mungu lakini unamchukulia unavyojua wewe…Bwana Yesu ambaye sasa hivi yupo mbingu za mbingu anamheshimu, siku ile tutaonyeshwa tumemkataa yeye Dhahiri.

Bwana atusaidie.

Kama bado hujampa Yesu Kristo Maisha yako, tupo ukingoni sana mwa siku za mwisho, ambapo ghafla tu unyakuo utapita na watakatifu watatoweka….waliobaki hawatasikia tena usumbufu wa mahubiri wanayohubiriwa sasa..watakuwa wamefungua jalada lingine la maisha..na watakatifu vivyo hivyo..Kwahiyo sio wakati wa kukaa nje..Mlango wa Safina unakaribia kufungwa, waasherati,walevi, wezi, watukanaji, watazamaji picha chafu mitandaoni, wanaokula rushwa, na wanaofanya kila aina ya machafuko biblia inasema sehemu yao itakuwa ni katika lile ziwa la moto. Ingia leo ndani ya Safina ya Yesu, wokovu unapatikana bure.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

Wewe u nabii yule akajibu la!..swali huyu ‘nabii yule’ ni nani?

JE! WEWE NI MWAKILISHI MWEMA?

Kwanini Bwana alisema Hakuna aliye mwema ila mmoja?

Kwanini Bwana alisema Hakuna aliye mwema ila mmoja?

Habari ile ya Pilato kuchanganya zile damu za wayahudi na pamoja na dhabihu zao,(Luka 13) ilihusu nini?

Rudi Nyumbani:

Print this post

BIBLIA INATUASA TUFANYE NINI KATIKA ZAMA HIZI ZA UOVU?

Waefeso 5:15 “Basi angalieni sana jinsi mnavyoenenda; si kama watu wasio na hekima bali kama watu wenye hekima;

16 mkiukomboa wakati kwa maana zamani hizi ni za uovu.

17 Kwa sababu hiyo msiwe wajinga, bali mfahamu ni nini yaliyo mapenzi ya Bwana.

18 Tena msilewe kwa mvinyo, ambamo mna ufisadi; BALI MJAZWE ROHO”;

Mwishoni mwa mstari huo wa 18 biblia inatuambia ‘”bali mjazwe Roho”.. Hili Ni neno endelevu, Sasa kumbuka Mtume Paulo alipokuwa anazungumza na kanisa hili la Efeso Alijua kabisa walishapokea Roho Mtakatifu tangu zamani walipoamini, na ndio maana likawa kanisa kubwa lilolitwa Efeso, Lakini hiyo haikumfanya mtume Paulo aone wamefika, bali aliwaasa siku baada ya siku wajazwe Roho, kwasababu alijua kuwa Roho anaweza kuzimishwa ndani ya mtu, hali kadhalika pia anaweza kujaa na kupungua kwa jinsi mtu atakavyokuwa makini au mzembe katika wokovu wake.

Hata sisi wakristo wa zama hizi ambazo uovu wetu ni mkubwa kuliko ule wa kanisa la Efeso, kusema tu, tumeokoka, au tumepokea Roho Mtakatifu, na huku bado uhusiano wetu na Mungu haueleweki haitoshi kutufikisha mbinguni, bali tunapaswa tujazwe Roho Mtakatifu siku baada ya siku mpaka siku ile ya Unyakuo itakapotukuta..

Kwasababu tukipuuzia jambo hilo, tutafananishwa na wale wanawali wapumbavu tunaowasoma katika Mathayo 25 ambao walikuwa wanamngojea Bwana wao lakini hawakuwa na mafuta ya kutosha ya kuwafikisha hadi ule wakati wa kumlaki Bwana wao.. matokeo yake saa ile ilipofika ya Bwana wao kutokea, ndio wakajishtukia kuwa taa zao zinakwenda kuzima…Sasa wakati wanakwenda kununua huku nyuma tayari Bwana arusi ameshawasili na kuwachukua wale aliowakuta wapo tayari na kuingia nao karamuni..Na wale wengine waliokwenda kuchukua mafuta waliporudi wakajikuta wameshachelewa.. Hasara ikawa ni kwao na taabu yao yote ya kumngojea Bwana ikiwa ni bure.. Japokuwa nao pia walikuwa ni wanawali (mabikira) yaani wameokoka, ambao wanamngojea tu Bwana wao kwa saburi kama wale wengine.. Lakini kwasababu ya kupuuzia jambo la msingi la mafuta katika chupa zao ikawafanya wakose karamu..

Siku zote mafuta yanafananishwa na Roho Mtakatifu..Tunapompokea Roho Mtakatifu siku zile za kwanza tulipookoka, tulipokea mafuta ya kuwasha tu vyombo vyetu vya usafari..Lakini tukiridhika na yale tu, hatutafika mbali. Ndugu ili kukivuka hichi kipindi cha Uovu uliokirithiri duniani sasa..Tunapaswa tuendelee kujazwa Roho..

Pengine utauliza nifanye nini ili nijazwe Roho Mtakatifu?

Roho Mtakatifu anaweza kuendelea kujaa ndani yetu, kwa walau mambo makuu manne.

  1. Kwa kuomba;

Biblia inasema, Luka 13:13 “Basi, ikiwa ninyi mlio waovu mnajua kuwapa watoto wenu vipawa vyema, je! Baba aliye mbinguni hatazidi sana kuwapa Roho Mtakatifu hao wamwombao?”

Ukiwa mtu wa kuomba, na kukataa uvivu kwa kutokusali walau saa moja kwa siku, ndivyo utavyojiongezea mafuta yako ya rohoni na hivyo Roho Mtakatifu atapata wigo mpana wa kuyatawala maisha yako siku baada ya siku.

    2.  Kwa kujifunza kwa bidii Neno la Mungu..; Neno ndio chakula cha uzima wa mtu. Usipojibidiisha kujifunza Neno la Mungu, kutafuta habari za uzima, usidhani kuwa Roho Mtakatifu atapata nafasi ya kukufundisha kitu chochote ndani yako. Kwasababu Mungu yupo katika Neno lake(Sauti ya Mungu ni Neno lake). Ukiwa umeokoka, halafu unaona uvivu kujifunza Biblia basi ujue Roho wa Mungu ameshazimika ndani yako kitambo..Na hivyo hata wakati wa unyakuo utakapofika utafananishwa na wale wanawali wapumbavu.

     3.  Kaa mbali na uovu; Siku zote dhambi inavutia, lakini mwisho wake ni mbaya..Tunapoivumilia dhambi katika maisha yetu ndivyo Mungu anavyouficha uso wake. Na matokeo yake Roho Mtakatifu anazimika, au anaondoka kabisa ndani yetu.(Isaya 59:2)

    4.  Tangaza habari njema: Ukiwafundisha wengine, na wewe hapo hapo Roho wa Mungu anakufundisha, ukiwafungulia wengine hazina ya maneno ya uzima, Roho Mtakatifu anapata nafasi ya kukufunulia wewe Zaidi na kukutumia, ili kuwaokoa watu wake..Na hivyo ni sharti atakaujaza tu Roho wake, kwasababu siku zote unafanya kazi yake..Na hapo utakuwa na nafasi nyingine ya kuwa karibu na yeye.

Hivyo tusiridhike tu, na hali za kiroho tulizopo, tukajificha nyuma ya kivuli cha Neno nimeokoka..Tunapaswa tujiulize Je! Mafuta tuliyonayo yanatutosha mpaka wakati wa kuja kwa Bwana? Kama sivyo basi huu ndio wakati wa kuzitengeneza upya taa zetu..kwa kuhakikisha kuwa kila siku Roho Mtakatifu anapata nafasi maishani mwetu..Ili ile siku ambayo hatujui ni lini itakapotujilia kwa ghafla basi tuwe na uhakika kuwa UNYAKUO hautatupita.

Ubarikiwe.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

JINSI ROHO MTAKATIFU ANAVYOWAFUNULIA WATU MAANDIKO.

Je! hizi roho saba za Mungu ni zipi? na je zinatofautiana na Roho Mtakatifu?

RABI, UNAKAA WAPI?

NA MTU MMOJA AKAVUTA UPINDE KWA KUBAHATISHA, AKAMPIGA MFALME

KUTUBU SIO KUOMBA REHEMA.

MATUNDA 9 YA ROHO MTAKATIFU

Rudi Nyumbani:

Print this post

Pakanga ni nini?

Pakanga ni mmea fulani mchungu uliokuwa unajulikana enzi za kale za biblia, ulikuwa ni mmea unaoota sehemu kame na ulikuwa ni mchungu sana..Hivyo kutokana na sifa ya mmea huo, chochote kile ambacho kingeleta uchungu mkali zamani kiliitwa jina la pakanga Kwa mfano kwenye biblia tunaona neno hilo likitumika sehemu mbali mbali…

Yeremia 23:15 “Basi Bwana wa majeshi asema hivi, katika habari ya manabii, Tazama, nitawalisha pakanga, nitawanywesha maji ya uchungu; kwa kuwa kutoka kwa manabii hao wa Yerusalemu kukufuru kumeingia katika nchi yote”.

Soma tena..

Mithali 5:3 “Maana midomo ya malaya hudondoza asali, Na kinywa chake ni laini kuliko mafuta; 4 Lakini mwisho wake ni mchungu kuliko pakanga; Ni mkali kama upanga wa makali kuwili”.

Yeremia 9:14 “bali wameenenda katika ushupavu wa mioyo yao wenyewe, na kuandamana na Mabaali, kama walivyofundishwa na baba zao.

15 Basi, Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, Tazama, nitawalisha pakanga, naam, watu hawa, nami nitawapa maji ya uchungu wayanywe.

16 Nami nitawatawanya kati ya mataifa, ambao wao hawakuwajua; wala baba zao, nami nitatuma upanga nyuma yao, hata nitakapowaangamiza kabisa”

Ufunuo 8:10 “Malaika wa tatu akapiga baragumu, nyota kubwa ikaanguka kutoka mbinguni, iliyokuwa ikiwaka kama taa, ikaanguka juu ya theluthi ya mito, na juu ya chemchemi za maji. 11 Na jina lake ile nyota yaitwa Pakanga; theluthi ya maji ikawa pakanga, na wanadamu wengi wakafa kwa maji hayo, kwa kuwa yalitiwa uchungu”.

Soma pia (Maombolezo 3:15,19), (Amosi 6:12), utaliona Neno hilo..

Hivyo biblia inapotumia hili Neno pakanga, inamaanisha uchungu mkali usio wa kawaida utakaowapata watu wanaotenda dhambi.. kama vile uasherati, uabuduji sanamu, utoaji wa unabii wa uongo n.k..

Hata leo Maisha yetu Mungu anaweza kuyatia pakanga, ikiwa tutaendelea kuishi Maisha ya kutokujali..Tuombe Bwana atuepushe na hayo mambo, huku tukikaa mbali na dhambi..Magonjwa haya tuyaonayo leo hii ni sehemu tu ndogo ya Pakanga, Ukilishangaisha ni hiyo itakayokuja kuachiliwa siku za mwisho ambapo watu watasaga ndimi, wakitamani vifo viwafikie, lakini mauti itawakimbia.. mambo hayo yatakuja baada ya unyakuo kupita.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

NI WAPI MAHALI SAHIHI PA KULIPA ZAKA?

KUTUBU SIO KUOMBA REHEMA.

Neno I.N.R.I kwenye msalaba wa Yesu maana yake ni nini?

Utii ni nini? na ni nani tunayepaswa kumtii au kutokumtii?

NDUGU,TUOMBEENI.

Bwana aliposema kuwa yeye ni “Mungu wa miungu” alikuwa na maana gani?..je! yeye ni Mungu wa sanamu?

TIMAZI NI NINI

Rudi Nyumbani:

Print this post

SI KWA FAIDA YA MWENYEZI, BALI KWA FAIDA YETU.

Tunapotenda Mema ni kwa faida yetu na si ya Mungu..kadhalika tunapofanya maovu ni kwa hasara yetu sisi na si hasara ya Mungu. Kwa mfano mtu anayezini biblia inasema anatenda dhambi juu ya mwili wake mwenyewe anafanya jambo litakalomwangamiza yeye mwenyewe.. maana yake anakuwa hana tofauti na mtu anayejiua…

Mithali 6:32 “Mtu aziniye na mwanamke hana akili kabisa; Afanya jambo litakalomwangamiza nafsi yake.33 Atapata jeraha na kuvunjiwa heshima; Wala fedheha yake haitafutika”

Kadhalika mtu anayeiba au anayeua, HAMKOMOI MUNGU..bali anafanya jambo ambalo litawaumiza wanadamu wenzake na hali kadhalika litakalomwaribu yeye mwenyewe baadaye. Na dhambi nyingine zote ni hivyo hivyo…zina madhara kwetu na si kwa Mungu…Vivyo hivyo tunapotenda mema, mema hayo tunapoyafanya si kwa faida ya Mungu bali kwa faida yetu sisi wenyewe..Bwana anapotuasa na kututaka tutende mema si kwaajili yake yeye, bali kwaajili yetu sisi..ni sawa na mtu anayekizuia kisu katika shingo ya mtu anayetaka kujiua..Ndivyo anavyofanya kwetu pale anapotuzuia tusifanye dhambi..ni kwa faida yetu si yake…endapo akituacha tu basi tutajimaliza na hakuna kitakachosalia…

Kwamfano Biblia inasema wapeni watu vitu nanyi mtapewa…(Luka 6:38) kipimo cha kujaa, na kushindiliwa hata kusukwa sukwa ndivyo watu watakavyowapa vifuani mwenu…kwamaana kipimo kile tupimacho ndicho tutakachopimiwa…Maana yake ni kwamba sio kwamba Mungu anatupa sheria ngumu ili yeye ajifurahishe moyo wake anapotuona tunamtii..hapana anafanya vile ili sisi tupate faida..yeye hatumwongezei chochote kwa wema wetu tunaoufanya…

Hivyo ukitenda mema na kuwapa watu vitu na wewe utapewa vitu siku moja kwa kiwango kile kile ulichowapa wengine…Kwahiyo mema ni kwa faida yetu sisi na si ya Mungu.

Kwahiyo Biblia inapotuonya tusizini, au tusifanye uasherati, au tusiibe, au tusiue, au tuwaheshimu wazazi wetu n.k ni kwafaida yetu ili tupate mema katika ulimwengu huu na ule unayokuja..Na si kwa sababu Mungu anapenda kutuangalia kama kwenye Tv huku duniani tukitenda mema, kwamba ndio chakula chake yeye..Ukifikiri/tukifikiri hivyo..tutakuwa bado hatujamwelewa huyu Mungu tunayemwabudu…

Soma maandiko haya:

Ayubu 35: 5 “Ziangalie mbingu ukaone; Na mawingu yaangalie, yaliyo juu kuliko wewe.

6 Ikiwa umefanya dhambi, umefanya nini juu yake? Yakiwa makosa yako yameongezeka, wamfanyia nini yeye?

7 Ikiwa u mwenye haki, wampa kitu gani? Au yeye hupokea nini mkononi mwako?

8 Uovu wako waweza kumwumiza mtu kama wewe; Na haki yako yaweza kumfaa mwanadamu”.

Umeona? Unapovaa vimini na suruali na kuonywa usivae kikahaba ni kwa faida yako mwanamke….Unapoua kwa kutoa mimba ni kwa hasara yako wewe na yule uliyemuua, …Unapojiongezea maasi juu ya maasi na dhambi juu ya dhambi, humpunguzii kitu Mungu kwasababu yeye haishi kwa dhambi zetu wala kwa haki yetu…Hivyo dhambi zako unazojiongezea juu kila siku ni sawa unasikia njaa na kukata kiungo chako kimoja kimoja kila siku ili ukile upunguze njaa..(hapo unajimaliza mwenyewe).

Unasikia mahubiri kila kona, ni kwasababu Mungu anakupenda na anataka upate faida wewe na si yeye..anataka usipate hasara wewe na si yeye..

Hili neno “hizi ni siku za mwisho” pengine umeshalisikia sasa hii ni mara ya elfu, na limeshakuchosha…lakini kipindi si kirefu hutalisikia tena kwasababu siku zenyewe zitakuwa zimeshatimia…Kristo atachukua walio wake na kila mtu atavuna alichokipanda akiwa hapa duniani. Na watakatifu watanyakuliwa..na dhiki kuu itaanza na siku ya Bwana itashuka ulimwenguni, wakati huo disko unazohudhuria sasa hazitakuwepo tena, bar unazokwenda kulewea hazitakuwepo tena, madili haramu na rushwa unazokula sasa hazitakuwepo tena…viwanda vinavyotengeneza mavazi yako ya kikahaba havitakuwepo tena, hakutakuwa na kurudi nyumbani kulala kutandani, wala kuangalia tv, wala kuingia internet..siku hizo zitahitimisha mambo hayo yote..Na baada ya hayo ziwa la moto litafunguliwa shetani na malaika zake watatupwa kwanza kwa maana lilitengenezwa kwaajili yao.

Kisha wote walio nje ya Kristo watafuata. Walio nje ya Kristo sio wale unaowategemea kwamba ni watu wa dini fulani..bali hata wewe uliye vuguvugu umbaye mguu mmoja upo nje mwingine ndani…ambaye ni mlevi lakini bado una jina la kikristo, ni mwasherani na mtembeaji uchi barabarani lakini bado unasali..wewe ndio mfano wa watakaoachwa wakati huo, na hiyo ni kulingana na maandiko na si mapokeo au mafundisho ya mtu binafsi aliyejiamulia tu kuzungumza.

Siku ya kunyakuliwa leo imekaribia sana kuliko jana na juzi…mwaka huu tumeukaribia unyakuo sana kuliko miaka ya nyuma..Hivyo huu ndio wakati wa kuongeza umakini wetu kuliko vipindi vya nyuma.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

MKARIBIE BWANA ZAIDI ILI UFANYIKE NGUZO.

NIMEOKOKA, ILA MUNGU NDIYE ANAYEJUA NITAKWENDA WAPI.

Chapa zake Yesu ni zipi hizo?

MUNGU WETU, JINSI LILIVYO TUKUFU JINA LAKO DUNIANI MWOTE!

KUTAKUWA NA MATETEMEKO YA NCHI, NJAA NA TAUNI.

KWANINI YESU KRISTO NI WA MUHIMU KWETU SASA?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Je! Mtume Paulo alimwabudu malaika aliyetembea naye?

SWALI: Je! Mtume Paulo alikuwa anamwabudu malaika wake aliyekuwa anatembea naye kama tunavyosoma katika Matendo 27:23?

JIBU: Tuusome huo mstari..

Matendo 27:23 “Kwa maana usiku huu wa leo malaika wa Mungu yule ambaye mimi ni wake, naye ndiye nimwabuduye, alisimama karibu nami,”

Mstari huu ukisomwa kwa haraka haraka ni rahisi kutafsiri kwamba Mtume Paulo alimaanisha kusema kwamba anamwabudu Malaika wake..Lakini ukiurudia tena taratibu utaona kwamba hapo Mtume Paulo hakumaanisha kuwa anamwabudu Malaika bali ni Mungu..

Sasa tunaweza kuiweka vizuri sentensi hiyo kama ifuatavyo; “Kwa maana usiku wa leo Malaika wa Mungu alinijia”…..sasa swali ni Mungu yupi?…ndio anaendelea kusema…Mungu yule ambaye mimi ni wake, naye ndiye nimwabuduye…

Hivyo ukirudia kusoma kwa namna hiyo huo mstari utapata tafsiri kamili.

Hivyo Pamoja na hayo tunazidi kujifunza kwamba tunapaswa kuzidi kuyachunguza maandiko, ili tupate kulielewa Neno la Mungu kama yeye Mungu wetu anavyotaka tulielewe..kwasababu ipo mistari mingi na Habari nyingi katika maandiko matakatifu ambazo wakati mwingine ni ngumu kuzielewa lakini tunapokaa chini na kutaka kumwuliza Roho Mtakatifu yeye ni mwaminifu na atatufulia, kwasababu tusipopata tafsiri kamili kwa msaada wa Roho Mtakatifu shetani anaweza kuitumia mistari hiyo hiyo kutukosesha na kutuhalalisha uovu wake…kama alivyoitumia baadhi ya mistari kuwadanganya watu kuhalalisha ulevi, zinaa, ndoa za mitara na hata ameshautumia mstari huu kwa baadhi ya watu kuhalalisha ibada za kuabudu malaika na ibada za sanamu.

Bwana atusaidie na kutubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mada Nyinginezo:

Je! Bwana Yesu alibatiza akiwa hapa duniani?

Je! Shetani alitolea wapi uovu?

Je ni wakina nani ambao hawataonja mauti mpaka siku ya kuja Bwana?

Ulinzi wa daima (eternal security) Je! ni neno la kimaandiko?

Kwanini Musa alipewa mbao mbili za mawe na sio moja au zaidi

Rudi Nyumbani:

Print this post

TAHADHARI YA NEEMA YA MUNGU.

Chukua tahadhari juu ya neema ya Mungu.


Hakuna ulinzi mkubwa ambao mwanadamu anaweza kuupata kama ulinzi wa kuwa ndani ya Yesu..Kama wengi wetu tunavyojua au tulivyosikia kwamba watu wote waliompokea Yesu Kristo uhai wao unakuwa umefichwa pamoja na Kristo.(Wakolosai 3:3). Kiasi kwamba tunalindwa dhidi ya nguvu za giza na mipango yote ya Ibilisi.

Wengi wetu tunaifurahia neema hii na kutamani kuingia ndani yake lakini hatujui kuwa ikichukiliwa isivyopaswa ina madhara makubwa kuliko kitu kingine chochote tunachoweza kukijua.

Neema ya Mungu inafananishwa na nyumba ya karamu, yenye mlango…Mathayo 7:13. Sasa kama tujuavyo nyumba yoyote ile ya muhimu kama Ikulu au ukumbi wa sherehe ya muhimu sana ina mlango na vile vile ina uzio…na mara nyingi kuta zake zinakuwa zimezungushiwa uzio mwingine ambao ni wa umeme..Na kama ni nyumba yenye umuhimu mkubwa zaidi ya hayo inakuwa na walinzi wanaotembea tembea wenye silaha kuizunguka, lengo ni kuzuia watu wa wasiruke ukuta na kuingia ndani…Na ikitokea mtu akijaribu kukiuka na kuusogelea ukuta kutaka kuruka aingie ndani ndipo anaweza akajikuta kapigwa risasi au kapigwa shoti ya umeme, na hivyo hata kuweza kujisababishia kifo…Lakini ulinzi huo haujawekwa kwaajili ya kuangamiza watu, bali kulinda usalama.

Na Neema ya Mungu ni hivyo hivyo…Ipo nguvu ya ziada iwalindao wale watu walioingia ndani ya Neema ya Kristo..Nguvu hiyo ndiyo inayotulinda dhidi ya nguvu zote za giza, dhidi ya shetani na majeshi yake (mapepo na wachawi) na kila mpango mwovu wa Ibilisi..Hivyo yoyote anayejaribu kuingia kutaka kuwaharibu watu wa Mungu walio chini ya neema ya Mungu basi atakuwa anajitafutia matatizo yeye mwenyewe..

Lakini jambo lingine la kuogopesha ni kwamba ikitokea mtu aliyeko ndani ambaye tayari kashaingia ndani ya jengo hilo, akatoka na kwenda kupanda ukuta na kurukia zile nyaya za umeme zilizouzunguka ukuta, yeye naye atajeruhiwa vile vile kama sio kufa kabisa. Maumivu yale yale atakayoyasikia Yule anayetaka kuruka ukuta na kuingia ndani ndio hayo hayo atayapata Yule anayetaka kuruka na kutoka nje.

Madhara atakayoyapata mchawi anayetaka kuwadhuru watu wa Mungu, ndio hayo hayo atakayoyapata mkristo anayeuacha wokovu na kuurudia ulimwengu. Mkristo ambaye ameshaonja kipawa cha Mungu na kuburudika na neema ya Mungu, na ghafla anarudia uasherati wake, anarudia wizi wake, anarudia matusi yake, anarudia mauaji yake, usagaji wake, utoaji mimba wake, mambo ambayo alikuwa ameshayaacha machafu anayarudia tena…akidhani kwamba mkono wa Mungu ni kinyume cha wale waliopo nje pasipo kujua hata waliopo ndani ambao wanataka kutoka vile vile mkono wa Mungu upo kinyume chao.

Wengi wetu hatupendi kusikia mambo kama haya kwasababu hatupendi kuumizwa mioyo, hatupendi kusikia habari mbaya, lakini fahamu kuwa tahadhari siku zote sio habari njema, lakini zina umuhimu sana katika maisha hususani katika siku za baadaye…hata vidonge tupewacho na wataalamu wa afya ambavyo vinatumika kwa tiba, bado vina tahadhari zake…lengo la tahadhari zile sio kuwatisha watumiaji wala kuwakatisha tamaa bali kuwanufaisha zaidi.

Vivyo hivyo Neema ya Kristo inayo tahadhari…Na ni lazima kila mtu aijue tahadhari hiyo, wahubiri wengi hawaifundishi kwasababu watakosa waumini, na wao bado wanatafuta waumini…Lakini sikia leo hii mtu wa Mungu tahadhari, ili baadaye tusije kujuta, na tahadhari hii haikuhusu wewe unayesoma tu, hapana hata mimi ninayeandika inanihusu. Biblia inasema..

Waebrania 10:26 “Maana, kama tukifanya dhambi kusudi baada ya kuupokea ujuzi wa ile kweli, haibaki tena dhabihu kwa ajili ya dhambi;

27 bali kuna kuitazamia hukumu yenye kutisha, na ukali wa moto ulio tayari kuwala wao wapingao.

28 Mtu aliyeidharau sheria ya Musa hufa pasipo huruma, kwa neno la mashahidi wawili au watatu.

29 Mwaonaje? Haikumpasa adhabu iliyo kubwa zaidi mtu yule aliyemkanyaga Mwana wa Mungu, na kuihesabu damu ya agano aliyotakaswa kwayo kuwa ni kitu ovyo, na kumfanyia jeuri Roho wa neema?”

Kama umeamua kumfuata Yesu basi umfuate kweli kweli..usiusogelee kabisa ukuta wa Neema..uwe ndani au nje ni upanga ukatao kuwili..Neno la Mungu linasema usizini…hizo ni kuta!..neno linasema usiibe, usiue hizo ni kuta..ukipanda na kuzivuka nguvu ya Mungu utakumaliza..ambayo hiyo Mungu hakuiweka kwaajili ya kuua watu, bali kwaajili ya kuwalinda watu wake.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

JE KUPONYWA NI UTHIBITISHO WA MUNGU KUWA NA WEWE?

USITUPE LULU ZAKO MBELE YA NGURUWE.

MWISHO WA DUNIA UTAKUJAJE?

NAO WALIOKUWA WAMEKUSUDIWA UZIMA WA MILELE WAKAAMINI.

Je kupiga miayo ni ishara ya mapepo?

Rudi Nyumbani:

Print this post