Category Archive Home

NINI MAANA YA SISI KUWA WATOTO WA MUNGU?

SWALI: Je Mungu anazaa?..Kama hazai kwanini sisi tunaitwa Watoto wa Mungu?..Je! Mungu ana mke?..na kama hana huoni kama ni kukufuru kusema kuwa sisi ni Watoto wa Mungu?


JIBU: Swali hili linaulizwa sana na watu wa Imani nyingine Lakini ni vizuri kufahamu kuwa Tukisoma Biblia kwa haraka haraka tu! au tukiitafsiri kwa fahamu zetu za kibinadamu pasipo sisi wenyewe kutenga muda kutafuta msaada wa Roho Mtakatifu kwamba atujalie Neema ya kuyaelewa maandiko tutaishia kukwama tunapoisoma biblia.

Kwasababu biblia inasema…2Wakorintho 3:6 “Naye ndiye aliyetutosheleza kuwa wahudumu wa agano jipya; si wa andiko, bali wa roho; kwa maana andiko huua, bali roho huhuisha”.

Hapo inasema andiko huua, bali Roho huhuisha…maana yake ni kwamba tukiyatafsiri maandiko bila msaada wa Roho tutaishia kupotea tu au kuiona biblia ni kitabu cha uongo…. Hivyo maandiko pekee bila Roho yatatupoteza….

Sasa tukirudi kwenye swali letu linalouliza..ni kwa namna gani sisi ni watoto wa Mungu?…ili kuelewa sisi tuliomwamini Yesu Kristo ni wana wa Mungu kwa namna gani…hebu turudi kutafakari Maisha ya kawaida tunayoyaishi sisi wanadamu. Katika kuyatafakari hayo kwa makini tutaweza kuelewa ni kwanini sisi (Tuliomwamini Yesu Kristo tunaitwa wana wa Mungu).

Hebu tumtafakari mtu mmoja maarufu aliyeitwa Julius Nyerere…ambaye alifanya jambo fulani la kishujaa la kwenda kuliletea taifa letu uhuru wakati huo…na kulifanya Taifa la Tanganyika kuzaliwa rasmi mwaka 1961, Sasa Kwa hekima za kibinadamu tunaweza kusema yeye ndiye aliyelizaa Taifa hili,..kwasababu kama si yeye kwenda kutafuta uhuru, bado kusingekuwa na Taifa linaloitwa Tanganyika na baadaye likaja kuwa Tanzania, linalojitegemea lenyewe, lenye serikali yake, lenye katiba yake, na mipango yake… hivyo si vibaya kumwita yeye Baba wa Taifa hili.…maana yake ni Baba wa Nchi hii…

Na sisi Raia tuliozaliwa ndani ya nchi hii tunajulikana kama wana au watoto wa nchi hii, ndio maana tunaiwa WANA-NCHI..akiwa mmoja anaitwa Mwana wa nchi hii (kwa kifupi mwana-nchi)..wakiwa wengi wanaitwa wana-nchi.

Kwahiyo mpaka hapo tumeshaona kuna BABA WA NCHI ambaye ni Mmoja aliyeitwa Julius na pia tuna Wana wa nchi ambao ni wengi..Na tumeshajua ni kwanini sisi Raia tunaitwa wana-nchi na kwanini Julius Nyerere anaitwa Baba wa Nchi, au Baba wa Taifa.

Sasa katika ufahamu huo..Hebu tafakari mtu mmoja anakuja na kuhoji… “Nyerere si Baba wa Taifa hili/nchi hii… ni lini Nyerere alioa akaizaa hii nchi? Mke wa Nyerere ni nani ambaye alimuoa na kuzaa naye watoto mpaka kufikia yeye aitwe Baba wa Taifa?”….Na mtu huyo huyo anaendelea kuhoji..sisi sio watoto wa hili Taifa wala sio wana wa hili nchi?… Ni lini hii nchi ilioa likatuzaa sisi mpaka tujiite sisi ni watoto wa hii nchi?..Mke wa hii nchi ni nani?…Hivyo sisi sio wana-nchi!..Tukijiita sisi ni wana-nchi tunakufuru! Na ni dhambi,.. Kwasababu nchi haiwezi ikaoa wala kuolewa, wala haiwezi kuzaa..hivyo…nakataa nakataa..

Umeona ufahamu wa huyu mtu?..Yeye chochote tu kinachoitwa mwana au mtoto au Baba au chochote ambacho kimezaliwa kwake anakitafsiri kwamba ni lazima kiwe aidha kimeoa, au kimeolewa kimwili… Sasa kwa ufahamu kama huo mtu wa namna hiyo ni ngumu kuelewa chochote. Mpaka atakapokubali kutulia kwanza na kukubali kujifunza ndipo atakapoelewa..

Kadhalika sisi tuliomwamini Bwana Yesu Kristo tunapoitwa wana wa Mungu au watoto wa Mungu…haimaanishi kuwa Mungu anazaa au ameoa, au ana mke na akatuzaa sisi..tukitafakari kwa namna hiyo bado ufahamu wetu utakuwa umefumbwa na hatutaweza kumwelewa Mungu kamwe…ingawa pengine tunaweza tukajiona tuna hekima.

U-wana wetu sisi ni wa namna ya Roho…sio wa namna ya mwili…Biblia inasema katika..

Yohana 1:12 “Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake;

13 waliozaliwa, si kwa damu, wala si kwa mapenzi ya mwili, wala si kwa mapenzi ya mtu, bali kwa Mungu”.

Tunapomwita Mungu wetu Baba ni kwasababu yeye ndiye chanzo cha uzima wetu na yeye ndiye aliyeutengeneza ufalme wa mbinguni…na kwa neema akatupa huo…Hivyo sisi ni wana wa huo ufalme!…kama vile tulivyo wana wa hii nchi..

Je umeelewa sasa?…Je! unataka leo kufanyika mwana wa Mungu?….Njia pekee ya kufanyika mwana wa Mungu ni kumwamini Yesu Kristo…Huwezi kufanyika mwana wa Mungu kama hujamwamini Mwana pekee wa Mungu Yesu Kristo.. “Wagalatia 3:26 Kwa kuwa ninyi nyote mmekuwa wana wa Mungu kwa njia ya imani katika Kristo Yesu.

YESU ANAWAPENDA WATU WOTE:

Hivyo mwamini leo kwa kutubu na kumwambia kuanzia leo nakuhitaji Ee Yesu mwokozi wangu… nadhamiria kabisa kuacha dhambi na kwenda kubatizwa na kulishika Neno lako, karibu moyoni mwangu nifanye kiumbe kipya, nabeba msalaba wangu kuanzia leo na kukufuata wewe, nishike mkono na kuniongoza njia yangu yote mpaka nitakapoimaliza safari yangu hapa duniani. Naomba pia unifanye sababu ya kuwa wokovu kwa wengine.”….

1Petro 2:9 “Bali ninyi ni mzao mteule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu wa milki ya Mungu, mpate kuzitangaza fadhili zake yeye aliyewaita mtoke gizani mkaingie katika nuru yake ya ajabu”

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Ikiwa utapenda tuwe tunakutumia masomo kwa njia ya whatsapp ya kila siku basi, bofya hapa uweze kujiunga >>> WHATSAPP Au tuandikie kwa namba hizi +255789001312

Mada Nyinginezo:

TUMEFANYIKA KUWA WANA WA MUNGU!

MISTARI YA BIBLIA KUHUSU WATOTO.

MJUE SANA YESU KRISTO.

WANA WA MUNGU, NA BINTI ZA WANADAMU.

Tofauti ya deni na dhambi ni nini?

Furaha ni nini?

Rudi Nyumbani:

Print this post

MAONO YA NABII AMOSI.

Shalom mwana wa Mungu, karibu tujifunze tena maneno ya uzima.

Amosi 3:7 “Hakika Bwana MUNGU hatafanya neno lo lote, bila kuwafunulia watumishi wake manabii siri yake”.

Maneno haya aliyaandika nabii Amosi..Alisukumwa kuandika hivyo, mara baada ya Mungu kumwonyesha mambo ambayo yalikuwa yanakwenda kuipata nchi ya Israeli katika wakati wake aliokuwa anaishi, pamoja na yale ambayo yalikuwa yanakwenda kuipata dunia nzima katika siku za mwisho. Hivyo akamshukuru Mungu, kwasababu aliona laiti kama yangemkuta kwa ghafla bila kujua angekuwa katika hali gani.

Hivyo, mambo mengine aliyoonyeshwa nabii Amosi, ni juu ya adhabu zitakazowapata matafa yaliyokuwa kando kando ya Israeli, na nchi ya Israeli kuchukuliwa utumwani. Alionyeshwa pia TETEMEKO KUBWA la ardhi ambalo lilikuwa linakwenda kuikumba nchi ya Israeli siku za usoni..Na ndio maana utaona mwanzoni kabisa mwa kitabu cha nabii Amosi aliandika na kusema maono yale alionyeshwa miaka miwili kabla ya tetemeko la Ardhi kutokea..

Amosi 1:1 “Maneno ya Amosi, aliyekuwa mmoja wa wachungaji wa Tekoa; maono aliyoyaona katika habari za Israeli, siku za Uzia, mfalme wa Yuda, na siku za Yeroboamu, mwana wa Yoashi, mfalme wa Israeli, miaka miwili kabla ya tetemeko la nchi”.

Unaona? Kama ukisoma utaona nabii Amosi, alionyesha mambo mabaya waliyokuwa wanayafanya Israeli, jinsi dhuluma za watu matajiri zilivyozidi, watu kula rushwa, watu kutokuwa waaminifu katika kazi zao, watu wasiotenda haki, na ziadi ya yote watu waliomsahau Mungu kwa ujumla, Hivyo akaonywa awaambie watubu wamrudie Mungu wao pengine Mungu atawasamehe na kughairi kuwaletea mapigo hayo,.. kwamba wamtafute yeye anayeweza kuleta uharibifu wa ghafla (Amosi 5:6-9) lakini hawakusikia hadi jambo hilo lilipowapata..

Amosi 8:8 “Kwa ajili ya hayo, je! Haitatetemeka nchi, na kuomboleza kila mtu akaaye ndani yake? Naam, itainuka yote pia kama huo Mto; nayo itataabika na kupwa tena kama Mto wa Misri”.

Tetemeko hilo lilikuja kutokea na lilikuwa kubwa ambalo halikuwahi kutokea katika nchi ya Israeli tangu lianze kuwa taifa, Nabii Isaya alionyeshwa pia athari za tetemeko hilo kwa jinsi lilivyokuwa kubwa katika siku hizo za mfalme Uzia..

Isaya 5:25 “Kwa sababu hiyo hasira ya Bwana imewaka juu ya watu wake, naye amenyosha mkono wake juu yao; akawapiga, navyo vilima vilitetemeka, na mizoga yao ilikuwa kama takataka katika njia kuu. Pamoja na hayo yote hasira yake haikugeukia mbali, lakini mkono wake umenyoshwa hata sasa”.

Watu walikufa wengi sana, nyumba nyingi zilibomoka, watu walikuwa wanakimbia ovyo ovyo kama vile vichaa mabarabarani,(Amosi 2:13-16) na ndio maana ukisoma tena kile kitabu cha Zekaria utaona habari hiyo inagusiwa tena ikifananishwa na tetemeko kubwa ambalo litakuja kutokea huko mbeleni Kristo atakaposhuka hapa duniani..

Zekaria 14:4 “Na siku hiyo miguu yake [yaani YESU KRISTO] itasimama juu ya mlima wa Mizeituni, unaoelekea Yerusalemu upande wa mashariki, nao mlima wa Mizeituni utapasuka katikati yake, upande wa mashariki na upande wa magharibi; litakuwako huko bonde kubwa sana; na nusu ya mlima ule utaondoka kwenda upande wa kaskazini, na nusu yake itaondoka kwenda upande wa kusini.

5 Nanyi mtakimbia kwa njia ya bonde la milima yangu; kwa maana bonde lile la milima litaenea hata Aseli; naam, mtakimbia, KAMA VILE MLIVYOKIMBIA MBELE YA TETEMEKO LA NCHI, SIKU ZA UZIA, mfalme wa Yuda; na Bwana, Mungu wangu, atakuja, na watakatifu wote pamoja naye”.

Unaona, Hapo Zakaria anawakumbushia tukio ambalo lilikuwa limeshatendeka miaka mingi sana huko nyuma, lakini bado machungu yake yalikuwa yanakumbukwa hadi huo wakati wa Nabii Zekaria.

Sasa, turudi pale kwa nabii Amosi, ambaye alionyeshwa mambo hayo kabla hata tetemeko halijatokea. Pamoja na kuonyeshwa tetemeko hilo..Lakini pia alionyeshwa na matukio mengine ambayo yatakuja kutokea katika siku za mwisho..Na ndio maana akaandika na kusema..

Amosi 5:18 “Ole wenu! Ninyi mnaoitamani siku ya Bwana; kwani kuitamani siku ya Bwana? Ni giza, wala si nuru.

19 Ni kama mtu aliyemkimbia simba, akakutana na dubu; au aliingia katika nyumba akauegemeza mkono wake ukutani, nyoka akamwuma.

20 Je! Siku ya Bwana haitakuwa giza, wala si nuru? Naam, yenye giza sana, wala haina mwanga”.

Nabii Amosi alionyeshwa hii siku inayoitwa siku ya Bwana..hakuona kingine zaidi ya giza tu, yaani mauti, akalia na kusema sio siku ya kuitamani hata kidogo..

Amosi 8:9 “Tena itakuwa siku hiyo, asema Bwana MUNGU, nitalifanya jua litue wakati wa adhuhuri, nami nitaitia nchi giza wakati wa nuru ya mchana”.

Ndugu yangu, mimi na wewe tusitamani tuwepo huo wakati, Mungu wetu ni wa rehema lakini pia biblia inatuambia ni mwingi wa ghadhabu, embu jaribu kufirikia wakati kama huu mchana saa 7, unaona jua linaondoka, dunia nzima inakuwa ni giza NENE, utakuwa katika hali gani?..na ahishii tu hapo, kumbuka kabla ya hilo jua kuondolewa kutakuwa kumeshatungulia mapigo ya vile vitasa 6 vya mwanzo tunavyovisoma katika Ufunuo sura 16 (Kama hujapata uchambuzi wa mapigo ya vitasa 7 tutumie ujumbe inbox tukutumie maelezo yake)…

Na pigo la mwisho kabisa litaishi na hili la nchi kutiwa giza na tetemeko kubwa la Ardhi ambalo halijawahi kutokea tangu dunia iumbwe hadi sasa,,,tetemeko hilo litakuwa na nguvu sana hadi visiwa vitahama, pengine hichi kisiwa cha Zanzibar utaenda kukikuta nchi ya Peru kule kama kitakuwa hakijatoweka kabisa..(Soma kwa muda wako Mathayo 24:29-31 na Ufunuo 16:17-21)

Kumbuka Tetemeko hilo litatokea ndani ya giza nene. litamaliza wanadamu wale ambao hawakwenda kwenye unyakuo wakati huo, kiasi kwamba kumpata mwanadamu mmoja duniani ni sawa na vile unavyotafuta kipande cha dhahabu kimoja ardhini kwa jinsi wanadamu watakavyoadimika..

Isaya alionyeshwa hivyo..

Isaya 13:9 “Tazama, siku ya Bwana inakuja, siku kali, ya hasira na ghadhabu kuu, ili iifanye nchi kuwa ukiwa, na kuwaharibu watu wake, wenye dhambi, wasikae ndani yake.

10 Maana nyota za mbinguni na matangamano havitatoa nuru yake; jua litatiwa giza wakati wa kucha kwake, na mwezi utaacha nuru yake isiangaze.

11 Nami nitaadhibu ulimwengu kwa sababu ya ubaya wake, na wenye dhambi kwa sababu ya hatia yao; nami nitaikomesha fahari yao wenye kiburi; nami nitayaangusha chini majivuno yao walio wakali;

12 nitafanya wanadamu kuadimika kuliko dhahabu safi, na watu kuliko dhahabu ya Ofiri.

13 Kwa hiyo nitazitetemesha mbingu, na dunia itatikiswa itoke katika mahali pake, kwa sababu ya ghadhabu ya Bwana wa majeshi, na kwa sababu ya siku ya hasira yake kali”.

Mambo hayo sio hadithi yatakuja kutokea, kama walivyoonyeshwa manabii hawa wa Bwana, hakuna asiyejua kuwa hizi ni nyakati za mwisho, na mambo hayo yatatimia katika majira yetu haya..

Lakini kabla hayajatokea Bwana ameshatupasha habari na anatuonya na sisi..Tumgeukie yeye, tuache dhambi, tutubu dhambi zetu. Ili unyakuo ukipita tusibakie hapa duniani..na kuiingia katika ghadhabu ya Mungu…Wengi wanadokezwa katika ndoto na maono jinsi siku hiyo itakavyokuwa..ni siku ya kutisha sana.

Kama hujatubu basi katika nyakati hizi za kumalizia ni vema ukafanya hivyo kwasababu muda ubakio ni mchache sana. Pia kaa mbali na mafundisho ya manabii wa uongo, ambao hawajali roho yako kwa kuacha kukueleza habari ya mambo ya yajayo, ya ulimwengu ujao, na hukumu ya Mungu, bali mafundisho ya kufanikiwa mwilini tu…Bwana Yesu alisema “Itakufaidia nini kuupata ulimwengu mzima na kisha kupata hasara ya nafsi yako?”

Hivyo tusisikilize mahubiri ya kujirudia rudia pokea hichi pokea kile wakati hata hatujui baada ya kifo ni nini kitaendelea, hujui endapo ukifa katika hali uliyopo ya kuishi na mke/mume ambaye hamjaona ni nini kitatokea!..tusiwafuate hao manabii wasioumia kusikia mtu kafa katika dhambi!.…Sisi tuwafuate manabii hawa waliothibitishwa na Mungu mwenyewe wanaotuonya kuhusu siku za Mwisho, na madhara ya dhambi.. kama nabii Amosi, Isaya, Danieli, Yeremia, Zekaria n.k. Ndio tutakwenda salama katika safari yetu hapa duniani.

Ubarikiwe.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Ikiwa utapenda tuwe tunakutumia masomo kwa njia ya whatsapp ya kila siku basi, bofya hapa uweze kujiunga >>> WHATSAPP Au tuandikie kwa namba hizi +255789001312

Mada Nyinginezo:

VIFUNGO VYA GIZA VYA MILELE.

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

UFUNUO: Mlango wa 16.

SAA YA KIAMA.

SIKU ILE NA SAA ILE.

UNYAKUO WA KANISA UMEPITA LEO!!

Rudi Nyumbani:

Print this post

Kwanini wanawake wengi huwa wanalipuka mapepo?

SWALI: Naomba kufahamu ni kwa nini katika mikutano mingi ya injili na sehemu za makusanyiko kama mashuleni na sehemu zingine Wanawake ndio hupatwa sana na kusumbuliwa na mapepo?


JIBU: Sababu kubwa ya tatizo hilo ni kitu kinachoitwa “maumbile”. Jinsi Adamu alivyoumbwa ni tofauti na Hawa alivyoumbwa biblia inasema hivyo…Hawa aliumbwa kama msaidizi..alitoka ubavuni mwa mwingine..Kwahiyo ni Dhahiri kuwa kwa namna moja au nyingine yule aliyetoka kwa mwenzake atakuwa dhaifu kidogo kuliko yule muhusika mwenyewe (yaani Adamu) 1Petro 3:7.

Ndio maana unaona mtu wa kwanza kuingiliwa na mapepo pale Edeni alikuwa ni Hawa, na huyo ndiye aliyeharibu mambo yote na kusababisha tuwe hivi tulivyo leo. Na biblia inasema Adamu hakudanganywa bali Hawa. Na ndio sababu biblia imesema wanawake wawe watulivu makanisani na pia hawana ruhusa ya kufundisha. Kwasababu kama wakiachiliwa kuongoza kundi makanisani ni rahisi kwa adui kutumia milango hiyo kama vile Hawa alivyotumika pale Edeni.

Kanisa la kwanza lilianzia pale Edeni, utukufu wa Mungu ulikuwa unashuka wakawa mpaka wanamwona Mungu uso kwa uso..lakini pepo likamwingia Hawa na kumdanganya kuharibu mambo yote….si Zaidi sasahivi?,… kumbuka Hawa aliumbwa pasipo dhambi ya asili hata kidogo lakini aliyaharibu mambo…. si Zaidi uliyezaliwa leo mwenye dhambi ya asili?.

1Timotheo 2:11 “Mwanamke na ajifunze katika utulivu, akitii kwa kila namna.

12 Simpi mwanamke ruhusa ya kufundisha, wala kumtawala mwanamume, bali awe katika utulivu. 13 Kwa maana Adamu ndiye aliyeumbwa kwanza, na Hawa baadaye.

14 WALA ADAMU HAKUDANGANYWA, ILA MWANAMKE ALIDANGANYWA KABISA akaingia katika hali ya kukosa”.

Lakini leo utaona wanawake wachungaji?..Jambo ambalo ni kinyume na maagizo ya Mungu…utasema mbona anajua tu kuhubiri na watu wanaokoka, mbona anaombea watu wanapona, mbona anatoa unabii na unatokea?..hicho sio kigezo!…hata mtu aliyemwasherati anaweza kuhubiri na watu wakaokoka?. Bwana Yesu alisema wengi watakuja siku ile na kusema Bwana hatukutoa pepo kwa jina lako? Hatukutoa unabii kwa jina lako? Lakini atawaambia siwajui mtokako!..Maana yake ni kwamba kutoa pepo, au kujua kuhubiri kwa kupangilia maneno sio kigezo cha mtu kukubaliwa na Mungu…bali kutenda mapenzi ya Mungu ndio kigezo cha kukubaliwa. Kutii Neno lake, Kasome (Mathayo 7:21-23).

Ni rahisi kutafuta maandiko machache machache kuchomeka ili kutetea hoja hiyo ya wanawake kuwa wachungaji…lakini maandiko yamesema wazi… “wanawake wawe watulivu”. Ila kama wewe au mimi tunajiona tunajua Zaidi au watu wa rohoni Zaidi na kuhisi kwamba pengine Mungu ana upendeleo fulani, au pengine alikuwa hamaanishi vile alikuwa anamaanisha vingine kusema vile..Hivyo sisi ni watu wa rohoni sana…Basi mstari huu unaweza ukatufaa Zaidi.

1Wakorintho 14: 34 “Wanawake na wanyamaze katika kanisa, maana hawana ruhusa kunena bali watii, kama vile inenavyo torati nayo.

35 Nao wakitaka kujifunza neno lo lote, na wawaulize waume zao wenyewe nyumbani mwao; maana ni aibu wanawake kunena katika kanisa.

36 Au je! Neno la Mungu lilitoka kwenu? Au kuwafikia ninyi peke yenu?

37 MTU AKIJIONA KUWA NI NABII AU MTU WA ROHONI, na ayatambue hayo ninayowaandikia, ya kwamba ni maagizo ya Bwana.

38 Lakini mtu akiwa mjinga, na awe mjinga”.

Neno linatuambia kama TUKITAKA KUWA WAJINGA, na tuwe wajinga!..Kama tunataka kuendelea kuwa wajinga kulazimisha kwamba anachoweza kukifanya mwanamke na mwanamume naye anaweza kukifanya pia, au anachoweza kukifanya mwanamume na mwanamke anaweza…basi tumepewa ruhusa ya kuendelea kuwa wajinga hivyo hivyo…

Lakini wanawake na wanaume wanaolisoma Neno na kulielewa sio wajinga. Wanalitii Neno la Mungu na kulifuata.

Bwana atusaidie sana.

Ubarikiwe.

Ikiwa utapenda tuwe tunakutumia masomo kwa njia ya whatsapp ya kila siku basi, bofya hapa uweze kujiunga >>> WHATSAPP Au tuandikie kwa namba hizi +255789001312

Mada Nyinginezo:

NAFASI YA MWANAMKE KATIKA KANISA

TUJIFUNZE JAMBO KWA WANAWAKE HAWA WAWILI:

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA WARAKA WA PILI WA YOHANA.

RABONI!

MARIAMU

MARIAMU AKUTANA NA ELISABETI.

WALE WAZEE ISHIRINI NA WANNE (24), WANA KAZI GANI?

MUNGU AKIKUPITA LEO, HAIMAANISHI KUWA HAJAKUCHAGUA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

WANA WA MUNGU, NA BINTI ZA WANADAMU.

Wana wa mungu, na binti za wanadamu,ni wakina nani leo hii?


Biblia inaposema kama ilivyokuwa katika siku za Nuhu, Ndivyo itakavyokuwa katika siku za kuja kwake mwana wa Adamu (Luka 17:26)..Yapo mambo mengi sana tunapaswa tuyachunguze yaliyokuwa yanatokea katika siku za Nuhu, Na leo tutaangazia jambo moja ambalo ndilo lililopelekea wakati ule dunia yote kuangamizwa.

Na jambo lenyewe si lingine zaidi ya kuchanganyikana kwa mbegu kati ya wana wa Mungu na binti za wanadamu. Leo hii nataka ufahamu kuwa wana wa Mungu wanaozungumziwa pale sio malaika, kama wengi wetu tulivyofundishwa, biblia inasema malaika hawaoi wala hawaolewi (Mathayo 22:3), na sisi watakatifu tukishakwenda mbinguni tutafanana na wao..Pamoja na hayo malaika hawajapewa miili ya kiduniani, bali wao ni roho watumikao biblia inasema hivyo (Waebrania 1:14)

Hivyo kusema wale wanaozungumziwa katika Mwanzo..Ni malaika wa Mungu walizini na wanadamu, hilo linakinzana na maandiko. Bali wale wanaotajwa pale kama wana wa Mungu ni wanadamu watakatifu wa Mungu, na binti za wanadamu ni binti za wana wa ulimwengu huu. Ndio maana unaona baada ya tukio lile walioadhibiwa kwa gharika ni wanadamu na si malaika ikimaanisha kuwa ni dhambi walizokuwa wanazitenda wanadamu na si malaika.

Lakini kwanini kulitokea makundi hayo mawili wakati huo?

Biblia inatuonyesha tokea mwanzo, kulikuwa na tofauti kati ya zao mbili kuu..Yaani uzao wa Kaini, na ule uzao wa Sethi.. Ule uzao wa Kaini ulikuwa na tabia zake tofauti kabisa ambazo tabia ya kwanza ulikuwa haumchi Mungu wala hauna habari na Mungu kama Baba yako Kaini alivyokuwa, pili ulikuwa ni mzao wa uuaji, utaona mtoto wa Kaini anashuhudia kuwa alikuwa muuaji hata zaidi ya baba yake (Mwanzo 4:23), tatu ulikuwa ni uzao wa kuoa tu nje ya utaratibu wa Mungu, kuoa wake wengi (Mwanzo 4:19), nne ulikuwa ni uzao wenye ujuzi na maarifa mengi sana ya kidunia..Utaona mwanzoni tu walishagundua vyuma, chuma, vyombo vya miziki na kuvitumia isivyopasa (Mwanzo 4:20-22)..n.k.

Lakini uzao wa Sethi, ulikuwa ni uzao mtulivu, walikuwa ni wafugaji tu, na baada ya kuona dunia imeharibika sana na kajitenga mbali na Mungu wao walienda kinyume na kuanza kuliitia jina la Bwana..yaani ikiwa na maana walikuwa ni watu wanaomtafuta Mungu sana, watu wa ibada, watu waliojitenga na mambo maovu n.k.

Mwanzo 4:25 “Adamu akamjua mke wake tena; akazaa mwana mwanamume, akamwita jina lake Sethi; maana alisema, Mungu ameniwekea uzao mwingine mahali pa Habili; kwa sababu Kaini alimwua.

26 Sethi naye akazaa mwana; akamwita jina lake Enoshi. Hapo ndipo watu walipoanza kuliitia Jina la Bwana”.

Hivyo dunia ilikuwa inajulikana wazi, kuwa kuna uzao wa Sethi, uliokuwa unajulikana ni uzao wa watu wanaojishughulisha na kumtafuta Mungu kwa bidi na wenye msimamo (kwasasa tunaweza kusema ni walokole), na uzao wa Kaini ambao kwasasa tuseme watu wa ulimwengu huu wasioamini hata kama kuna Mungu, wenye elimu na sayansi na teknolojia ya hali ya juu na kwa ujuzi wao huo wote hawamtaki Mungu.

Sasa ilikuwa ni rahisi Mungu kuivumilia dunia maadamu anaona bado uzao wake unamtafuta yeye na kujitenga na uovu duniani , na unajishughulisha na mambo ya imani, (Kama alivyomwambia Ibrahimu wakati Fulani kwamba endapo wakipatika wenye haki 10 hatateketeza mji, Mwanzo 18:32)

Lakini ilifikia wakati huu uzao wa Mungu, ambao ndio wale wanaoitwa wana wa Mungu, wakakengeuka wakajisahau wakashindwa kuvumilia walipoona dunia inavutia, watu waovu wanasitawi ulimwenguni, wakaanza kuwaona hao binti wa wana wa kibinadamu jinsi wanavyoishi kidunia…Jinsi wanavyovaa kizinzi, wakikatiza mitaa yao wakiwa na vimini, na vi-top, migongo wazi, wakiwa wamevaa suruali za kubana, wakiwa wamejipamba kwa ma-makeup za kisasa, na wanja, na mahereni ya dhahabu na chuka za bandia, na mawigi wasio na aibu wala haya, wakiwa wamejichubua na kubadili maumbo yao na mienendo yao kwa ujuzi wote…wakitembea bichi wakiwa na bikini tu.

Wakaingiwa na tamaa, hapo ndipo na wao wakaenda kuwaoa watu ambao Mungu alishawalaani..Na unajua kwasababu gani Mungu aliwakataza hata wana wa Israeli wasioe binti za mataifa mengine? Ni kwasababu hii hii aliyoiona kwa wakati wa Nuhu, ambayo ni kugeuzwa mioyo. Sulemani hakulisikia hilo pamoja na kuwa alikuwa ni mtu mwenye hekima na aliyependwa na Mungu sana, lakini wanawake hawa walimgeuza moyo mpaka akaenda kufanya ibada za miungu..Na kufarakana na Mungu.

Nehemia 13:25 ‘Nikagombana nao, nikawalaani, nikawapiga baadhi yao, na kuwang’oa nywele zao; nikawaapisha kwa Mungu, nikasema, Msiwaoze wana wao binti zenu, wala msiwatwae binti zao ili waolewe na wana wenu, wala na ninyi wenyewe.

26 Je! Sulemani, mwana wa Daudi, hakufanya dhambi kwa kutenda hayo? Lakini katika mataifa mengi hapakuwa na mfalme mwingine mfano wake. Tena alipendwa na Mungu wake, naye Mungu akamfanya mfalme juu ya Israeli; walakini wanawake wageni walimkosesha hata yeye’.

Vivyo hivyo, na hawa wana wa Mungu (Uzao wa Sethi) walipooana na binti za wanadamu (uzao wa Kaini) kuwa ni warembo na wazuri….wakabadilika tabia moja kwa moja, na wao pia wakamsahau Mungu, hivyo dunia nzima ikafanana na kuwaa kitu kimoja..Wote ni waovu. Mungu akiangalia haoni wa kumuhurumia, Na hapo ndipo Mungu alipofikia hatua ya kughahiri na kuiteketeza dunia nzima kwa maji.

Mwanzo 6:1 “Ikawa wanadamu walipoanza kuzidi usoni pa nchi na wana wa kike walizaliwa kwao,

2 wana wa Mungu waliwaona hao binti za wanadamu ya kuwa ni wazuri; wakajitwalia wake wo wote waliowachagua.

3 Bwana akasema, Roho yangu haitashindana na mwanadamu milele, kwa kuwa yeye naye ni nyama; basi siku zake zitakuwa miaka mia na ishirini.

4 Nao Wanefili walikuwako duniani siku zile;tena ,baada ya hayo ,wana wa Mungu walipoingia kwa binti za binadamu,wakazaa nao wana;hao ndiyo waliokuwa watu hodari zamani ,watu wenye sifa.

5 Bwana akaona ya kuwa maovu ya mwanadamu ni makubwa duniani na kwamba kila kusudi analowaza moyoni mwake ni baya tu sikuzote.

6 Bwana akaghairi kwa kuwa amemfanya mwanadamu duniani, akahuzunika moyo.

7 Bwana akasema, Nitamfutilia mbali mwanadamu niliyemwumba usoni pa nchi; mwanadamu na mnyama, na kitambaacho na ndege wa angani; kwa maana naghairi ya kwamba nimewafanya.

8 Lakini Nuhu akapata neema machoni pa Bwana”.

Unaona mambo yale yale yanajirudia leo hii duniani, wewe kama mwanamke, mwonekano wako unakutambulisha wewe ni binti wa nani? Kwamba wewe ni binti wa Kaini..Na wewe ndio unaowakoseshwa wana wa Mungu wengi kuwapeleka kuzimu..Unategemea vipi adhabu yako siku ile isiwe kubwa zaidi ya wote?. Kuambiwa hivyo sio kuhukumiwa kasome Mathayo 18:6 na Marko 9:42..Hujali leo nani anakutamani nani hakutamani… siku ile utalia na kuomboleza na hakutakuwa na nafasi ya kurekebisha makosa.

Vilevile wewe unayejiita mwana wa Mungu, unajichanganya na mambo ya ulimwengu huu, kuzini kwako ni jambo la kawaida, disko unakwenda, kwenye starehe upo hujui kuwa unajichanga mbegu yako na mbegu za kaini, nawe pia utaangamizwa pamoja na wao, ukifa leo hii..

Ezra 9:2 “Maana wametwaa binti zao kuwa wake zao, na wake za watoto wao; basi mbegu takatifu wamejichanganya na watu wa nchi hizi; naam, mkono wa wakuu na mashehe umetangulia katika kosa hili”.

Kumbuka hili neno “kama zilivyokuwa katika siku za Nuhu”. Hizi ndio siku hizo…Urembo na udunia uliopo leo hii ndio uliokuwa katika siku za Nuhu, upo viwango vya juu, huwezi katika kona mbili tatu ukakosa kuona duka au kituo cha kuuza urembo wa wanawake…mambo haya hayakuwepo wakati wowote kipindi cha nyuma. Fashion, ni moja ya silaha kuu ya ibilisi katika wakati huu.

Ni dua yangu kuwa utabadilika na kumpa Kristo maisha yako, uanze upya, ili ndani ya muda huu mfupi tuliobakiwa nao Bwana ayatengeneze maisha yako na kukufanya kuwa mwana au binti wa Mungu kweli kweli, kama alivyosema katika Neno lake..

Yohana 1:12 “Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake”

Hivyo uwezo huo wa kubadilishwa na kuwa mtoto wa Mungu kutoka kuwa mtoto wa KAINI ule uzao wa nyoka, hauji hivi hivi kwa nguvu zako, bali kwa kuzaliwa mara ya pili..Na kuzaliwa mara ya pili ni pamoja na kutubu na kukubali kubatizwa sawasawa na (Yohana 3:5). Hivyo Kama upo tayari leo hii kusema Bwana Yesu nataka uyageuze maisha yangu nikuishie wewe milele..

Basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie maisha yako yote kama ilivyokuwa hata kwetu sisi. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE,SITAKI KUFANYA DHAMBI TENA. NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.

AMEN.

Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo, Hapo ndipo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu…usiende mahali panapoabudiwa sanamu..Neno Mahali Mungu anapoabudiwa katika Roho na kweli.. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

MTI WA UZIMA NA MTI WA MAARIFA.

UZAO WA NYOKA.

WANA WA MAJOKA.

JE! UMECHAGULIWA TANGU ASILI?

NGUVU YA UPOTEVU.

DALILI NYINGINE INAYOUTAMBULISHA UZAO WA NYOKA

JE! Kaini alimpatia mke wake wapi?

UZAO WAKO UTAMILIKI MALANGO YA KUZIMU;

Uzao wa Mwanamke ni upi? Unaozungumziwa katika Mwanzo 3:15?

Rudi Nyumbani:

Print this post

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

Shalom, karibu tujifunze Biblia Neno la Mungu…

Roho Mtakatifu atusaidie leo tena katika kuyatafakari maneno yake.Kama tunavyojua kuwa matukio mengi ambayo yaliwahi kutokea nyakati za kale na kurekodiwa katika biblia…mengi ya matukio hayo ni unabii wa mambo yatakayokuja kutokea baadaye…Kwamfano tunaweza kuona tukio la kugharikishwa dunia wakati wa Nuhu..Bwana Yesu alisema katika siku za mwisho maovu yatakuwa kama yalivyokuwa katika siku za Nuhu..Na kwa namna ile ile gharika ilivyowajia kwa ghafla wakafa wote ndivyo itakavyokuwa katika siku za mwisho wakati watu wanasema kuna amani na salama ndipo hapo hapo uharibifu unapokuja kwa ghafla.

Kadhalika tunaweza kujifunza tukio mojawapo ambalo pia litatupa picha kujua ni nini kitatokea kipindi kifupi kabla kanisa la Kristo kunyakuliwa.

Siku chache kabla ya kuja kwa Bwana Yesu duniani yaani kabla ya kuzaliwa kwake…Shetani alikuwa ameshauona ule ujauzito wa Mariamu hivyo akaanza kutengeneza njia ya kumwondosha Bwana Yesu. Kabla ya kuzaliwa au kipindi kifupi tu baada ya kuzaliwa.

Ghafla tu wazo likamwingia Kaisari ambaye ndiye aliyekuwa mfalme wa dunia nzima…wazo likamwingia aandike orodha ya majina ya watu wote ulimwenguni…Kwa ufupi maana yake ni kwamba kila mtu anapaswa kwenda mjini kwao kuchukua namba ya utambulisho.

Ni wazi kuwa kuna mambo fulani fulani yalitokea duniani wakati huo mpaka yakahimiza sensa hiyo ifanyike..pengine ukusanyaji wa kodi ulikuwa mgumu hivyo ikahitajika kila mtu asajiliwe, au pengine walitaka kutathimini na kudhibiti kiwango cha watu wanaozaliwa duniani.. Au pengine kulitokea watu waovu ambao walikuwa wanavuruga amani, hivyo ili kuwadhibiti ilihitaji sensa kufanyika na kwa kupitia sensa hiyo kila mtu apate kitambulisho chake.

Ni kama leo matapeli wa mitandao wanavyoongezeka inalazimu serikai itoe tamko la kila mtu kusajili laini ya simu yake kwa alama za vidole, ili kuwadhibiti…na kuongeza usalama.

Sasa harakati kama hizi zilianza kipindi kabla hata ya kuzaliwa kwa Bwana Yesu lakini zilifikia kilele kipindi kifupi kabla ya kuzaliwa Bwana Yesu…Watu wote wakapokea namba.

Luka 2:1 ‘Siku zile amri ilitoka kwa Kaisari Augusto ya kwamba iandikwe orodha ya majina ya watu wote wa ulimwengu.

2 Orodha hii ndiyo ya kwanza iliyoandikwa hapo Kirenio alipokuwa liwali wa Shamu.

3 Watu wote wakaenda kuandikwa, kila mtu mjini kwao.

4 Yusufu naye aliondoka Galilaya, toka mji wa Nazareti, akapanda kwenda Uyahudi mpaka mji wa Daudi, uitwao Bethlehemu, kwa kuwa yeye ni wa mbari na jamaa ya Daudi;

5 ili aandikwe pamoja na Mariamu mkewe, ambaye amemposa, naye ana mimba.

6 Ikawa, katika kukaa huko, siku zake za kuzaa zikatimia,

7 akamzaa mwanawe, kifungua mimba, akamvika nguo za kitoto, akamlaza katika hori ya kulia ng’ombe, kwa sababu hawakupata nafasi katika nyumba ya wageni”.

Lakini kama wengi wetu tujuavyo…Ndani ya sensa ile kulikuwa na mpango wa Mungu wa Bwana Yesu kwenda kuzaliwa Bethlehemu ili maandiko yatimie…lakini pia kulikuwa na mpango wa Ibilisi mkubwa sana wa kumwangamiza BWANA YESU katika uchanga wake pamoja na mama yake na Baba yake. Alikuwa anasuka mpango wa kwenda kummaliza Bwana Yesu kule mjini kwake Bethlehemu..Ndio maana Herode alitoa tamko la kwenda kutafutwa Bwana Yesu lakini walipomkosa aliagiza watoto wote waliopo Bethlehemu wauawe…Jiulize kwanini si miji mingine yote duniani bali Bethlehemu tu!..shetani naye ana target..hapigi huko na huko ovyo ovyo tu..

Mathayo 2:11 “Wakaingia nyumbani, wakamwona mtoto pamoja na Mariamu mamaye, wakaanguka wakamsujudia; nao walipokwisha kufungua hazina zao, wakamtolea tunu; dhahabu na uvumba na manemane.

12 Nao wakiisha kuonywa na Mungu katika ndoto wasimrudie Herode, wakaenda zao kwao kwa njia nyingine.

13 Na hao walipokwisha kwenda zao, tazama, malaika wa Bwana alimtokea Yusufu katika ndoto, akasema, Ondoka, umchukue mtoto na mama yake, ukimbilie Misri, ukae huko hata nikuambie; kwa maana Herode anataka kumtafuta mtoto amwangamize.

14 Akaondoka akamchukua mtoto na mama yake usiku, akaenda zake Misri;

15 akakaa huko hata alipokufa Herode; ili litimie neno lililonenwa na Bwana kwa ujumbe wa nabii, akisema, Kutoka Misri nalimwita mwanangu.

16 Ndipo Herode, alipoona ya kuwa amedhihakiwa na wale mamajusi, alighadhabika sana, akatuma watu akawaua watoto wote wanaume waliokuwako huko Bethlehemu na viungani mwake mwote, tangu wenye miaka miwili na waliopungua, kwa muda ule aliouhakikisha kwa wale mamajusi.

Utajiuliza pia kwanini Bwana Yesu alisema, ole wao wenye mimba na wanyonyeshao siku hizo ?(Mathayo 24:19), Alisema hivyo akifananisha jinsi wanawake wale walivyoshikwa na uchungu wakati wa kuja kwake mara ya kwanza, ndivyo itakavyokuwa katika siku za kuja kwake hata mara ya pili, embu fikiria jinsi watoto wale, walivyokuwa wakichinjwa kama kuku mbele yao, wapendwa wako wanauawa kikatili,..Ni uchungu kiasi gani Na ndivyo itakavyokuwa katika siku za mwisho..

Mathayo 2:17 “Ndipo lilipotimia neno lililonenwa na nabii Yeremia, akisema,

18 Sauti ilisikiwa Rama, Kilio, na maombolezo mengi, Raheli akiwalilia watoto wake, Asikubali kufarijiwa, kwa kuwa hawako”.

Sasa kile kipindi kikikaribia kufikia dalili za watu kuingizwa katika kumbukumbu za mpinga kristo zitaanza…Mpinga-Kristo ataagiza watu wote kwenda kusajiliwa katika mfumo mpya wa kipinga-Kristo ambao huo utahusisha chips, kadi, vitambulisho vipya n.k..Kama vile Kaisari alivyotoa tamko kuandikwa orodha ya majina ya watu wote duniani ..(Na ndani yake kutakuwa na alama ya 666) Kila mtu atakwenda katika mji wake au makazi yake ya kudumu aliyopo kuhakiki taarifa zake kama vile Kaisari alivyotoa agizo la watu wote kwenda kuhesabiwa mjini kwao.

Wakati zoezi hilo lipo mbioni kutendeka hapo katikati unyakuo utatokea… Bwana atakuja mawinguni na kuwachukua walio wake na kuwaepusha na hiyo chapa..kama tu vile Yesu alipotokea duniani, alivyoondoshwa yeye pamoja na Mariamu na Yusufu kutoka Bethlehemu kukimbilia Misri mbali na ghadhabu ya Herode na Kaisari. Na kusababisha wale waliosalia walichinjwa kama kuku..

Mathayo 2:12 “Nao wakiisha kuonywa na Mungu katika ndoto wasimrudie Herode, wakaenda zao kwao kwa njia nyingine.

Vivyo hivyo wakristo watakaokosa unyakuo, ambao watabaki na kuikataa ile chapa watateswa na mpinga-Kristo kwa dhiki ambayo haijawahi kuwepo tangu kuumbwa ulimwengu. Na Kama tu vile wakati dhiki inaendelea Bethlehemu, inaendelea Yesu pamoja na wazazi wake walikuwepo Misri, Vivyo hivyo wakati dhiki kuu inaendelea, Yesu pamoja na watakatifu wake watakuwa mbinguni.

Je wewe ni familia ya Bwana Yesu Kristo ambaye siku ile utaepushwa na dhiki siku ile na kwenda mbinguni? Kama Mariamu mamaye Yesu na Yusufu walivyoepushwa?…Utauliza nitakuwaje Baba au Mama wa Yesu mimi, na hapo hapo niwe mtoto wa Yesu?

Jibu la swali hilo lipo hapa.

Mathayo 12.46 “Alipokuwa katika kusema na makutano, tazama, mama yake na ndugu zake walikuwa wakisimama nje, wataka kusema naye.

47 Mtu mmoja akamwambia, Tazama, mama yako na ndugu zako wamesimama nje, wanataka kusema nawe.

48 Akajibu, akamwambia yule aliyempasha habari, Mama yangu ni nani? Na ndugu zangu ni akina nani?

49 Akawanyoshea mkono wanafunzi wake, akasema, Tazama, Mama yangu na ndugu zangu!

50 Kwa maana ye yote atakayeyafanya mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni, huyu ndiye ndugu yangu, na umbu langu, na mama yangu”.

Je unafanya mapenzi ya Bwana Yesu? Au mapenzi ya shetani…mfano wa mapenzi ya shetani ni haya ulevi, uasherati, uzinzi, ufiraji, ulawiti,utoaji mimba, kujichua, kutazama picha za ngono mitandaoni, uabuduji sanamu, wizi, ulaji rushwa, usengenyaji n.k Biblia imetabiri watu wa namna hii hawataikwepa dhiki kuu…labda wawe wamekufa kabla ya hiyo siku kufika..lakini pia hata huko walipo hawapo sehemu salama…Hivyo suluhisho ni kukubali kubadili mtindo wa maisha yetu.

Kama hujaokoka okoka leo usisubiri kesho..Huwa Adui shetani akishaona umeujua ukweli kama huu unaousoma leo na akishaona unashawishika kumgeukia Kristo, anaweza hata akakusababishia kifo cha ghafla ili tu ufe ukiwa hujaokoka…hivyo usipuuzie habari njema za Yesu zinapoletwa mbele yako ambazo hutozwi hata senti kuzisikiliza unapewa bure kabisa…Jiulize ukifa leo utakuwa wapi? Jibu unalo matumaini yangu ni utamgeukia Kristo leo.

Bwana akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii 0789001312

Mada Nyinginezo:

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

MTINI, WENYE MAJANI.

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

UNYAKUO.

MPINGA-KRISTO

Mungu anasema hatagharikisha dunia na maji tena,.Kwanini watu wanasema dunia itaangamizwa?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Kwanini yule mtu hakukutwa na vazi la arusi wakati alialikwa?

SWALI: Kwanini yule mtu hakukutwa na vazi la arusi wakati naye pia alialikwa?. Inamaana wale wengine walipewa mavazi siku ile ya kuingia karamuni?


Tusome:

Mathayo 22:1  “Yesu akajibu, akawaambia tena kwa mithali, akisema,

2  Ufalme wa mbinguni umefanana na mfalme mmoja aliyemfanyia mwanawe arusi.

3  Akawatuma watumwa wake wawaite walioalikwa kuja arusini; nao wakakataa kuja.

4  Akatuma tena watu kwa wengine, akisema, Waambieni wale walioalikwa, Tazameni, nimeandaa karamu yangu; ng’ombe zangu na vinono vimekwisha kuchinjwa, na vyote vimekuwa tayari, njoni arusini.

5  Lakini hawakujali, wakaenda zao, mmoja shambani kwake, mmoja kwenye biashara yake;

6  nao waliosalia wakawakamata watumwa wake, wakawatenda jeuri, na kuwaua.

7  Basi yule mfalme akaghadhibika; akapeleka majeshi yake, akawaangamiza wauaji wale, akauteketeza mji wao.

8  Kisha akawaambia watumwa wake, Arusi i tayari, lakini wale walioalikwa hawakustahili.

9  Basi enendeni hata njia panda za barabara, na wote mwaonao waiteni arusini.

10  Watumwa wale wakatoka wakaenda njia kuu, wakakusanya wote waliowaona, waovu kwa wema; arusi ikajaa wageni.

11  Lakini alipoingia yule mfalme ili kuwatazama wageni wake, akaona mle mtu mmoja asiyevaa vazi la arusi.

12  Akamwambia, Rafiki, uliingiaje humu nawe huna vazi la arusi? Naye akatekewa.

13  Mfalme akawaambia watumishi, Mfungeni mikono na miguu, mchukueni mkamtupe katika giza la nje; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.

14  Kwa maana waitwao ni wengi, bali wateule ni wachache”


SWALI; Je! Inamaana kuwa wale wengine walipewa mavazi siku ile ya kuingia karamuni?

JIBU; Ndio wote waliolikwa pale walipewa vazi la arusi, kulikuwa na utaratibu walioupitia kwanza kabla ya kuingia kule harusini, kila aliyefika pale alihakikiwa kwanza na alipoonekana amekidhi vigezo ndipo akapewa vazi lile la Harusi, lakini yule mwingine alidhani ni kuingia tu, na yeye akajichanganya katikati ya kundi kinyemelewa..Na mwisho wa siku atakambulikana kwa mavazi yake yaliyotofauti na wengine….

Ndio makundi mawili yaliyopo katika kanisa la Kristo leo hii…wote wanasema yanasema nimeokoka nitakwenda mbinguni!! Lakini lipo linalotii na kufuata maagizo yote Kristo aliyoliekezeka..lakini lipo lingine linadhani maadamu tayari limeshakuwa mshirika wa kanisa basi hiyo inatosha, maadamu linatoa zaka, basi inatosha, maadamu linaimba kwaya inatosha, hakuna haja ya kwenda kubatizwa katika ubatizo sahihi, hakuna haja ya kuishi maisha matakatifu, hakuna haja ya kuomba, hakuna haja ya kujikana nafsi na kumfuata Kristo, hakuna haja ya kuhakiki ni nini kimpendezacho Bwana, na ni kipi hakimpendezi, lenyewe halina mzigo wowote na dhambi, linachopenda ni kuhubiriwa mafanikio tu, na kubarikiwa, lakini likigusiwa habari za toba halipendi.

Kufanya uzinzi ni kitu cha kawaida kwao, kuvaa nguo za nusu uchi si jambo ajabu pia, kuvaa suruali (wanawake) linaona ni sawa, kunywa pombe ni sawa, kwenda disko ni sawa, kukaa kwenye kampani za kidunia hakuna shida yoyote..

Sasa hawa katika ulimwengu wa roho, ni kweli waliitwa na Bwana lakini hawakuteuliwa…kwasababu hawakuwa tayari kulitwaa vazi jeupe la harusi ambalo ndio kama tiketi ya kuingia mbinguni.

Na ndio maana maandiko yanasema

Ufunuo 19:7  “Na tufurahi, tukashangilie, tukampe utukufu wake; kwa kuwa arusi ya Mwana-Kondoo imekuja, na mkewe amejiweka tayari.

8  Naye amepewa kuvikwa kitani nzuri, ing’arayo, safi; kwa maana kitani nzuri hiyo ni matendo ya haki ya watakatifu.

9  Naye akaniambia, Andika, Heri walioalikwa karamu ya arusi ya Mwana-Kondoo. Akaniambia, Maneno haya ni maneno ya kweli ya Mungu”.

Unaona?, hiyo kitani nzuri, ing’arayo safi ya kuingia karamuni ni matendo ya haki ya watakatifu…Hivyo na sisi hatutaingia mbinguni kwenye karamu ya mwanakondoo kama matendo yetu hayatakuwa ya haki hata kama tutajiita tumeokoka vipi… Haijalishi Bwana Yesu alitutokea, au tuliona maono, au tulitubu mwanzoni na Mungu akasikia toba yetu, kama hatutajizoeza kuishi maisha matakatifu biblia inasema hatutaweza kumwona Mungu pasipo huo (Waebrania 12:14)

Ubarikiwe.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii 0789001312

Mada Nyinginezo:

Naomba kujua watakaoenda mbinguni je! ni wengi au wachache?

Kuna ufufuo wa aina ngapi?

Kuna hukumu za aina ngapi?

Ule mfano wa wanawali 10 (Mathayo 25), wale watano hawakuwa na mafuta ya ziada katika chupa zao je yale mafuta ya ziada yanawakilisha nini?

KILA MTU ATATOA HABARI ZAKE MWENYEWE.

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

JUMA LA 70 LA DANIELI

MPINGA-KRISTO

MKUU WA ANGA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

KWANINI MUNGU ALIMTUMIA MUSA KWA VIWANGO VILE?

Shalom, Karibu tujifunze Neno la Mungu. Lipo swali ambalo tunaweza tukajiuliza siku ya leo, ni kwanini miujiza yote ile mikubwa namna ile Mungu alimtumia musa kuifanya na si mtu mwingine?…Licha ya kuwa ulikuwa ni mpango wa Mungu kuwaokoa wana wa Israeli kwa mkono hodari lakini pamoja na hayo ipo siri nyingine ambayo tunaweza kujifunza kwa Musa ambayo tukiijua na sisi basi Mungu atafanya kazi na sisi katika viwango vingine vya juu zaidi…

Mwanzoni kabisa wa huduma ya Musa, tunaona Mungu hakujidhihirisha kwake kwa njia ya wazi, ikiwa na maana kuwa hakumwona malaika, wala nabii, wala hakusikia sauti yoyote ikimwambia Njoo! Musa nataka nikutume., alichoona tu ni muujiza, kama na sisi tunavyoona leo hii miujiza ya wazi.. na hiyo ndio inayotupa uthibitisho kuwa wito wa Musa hakuwa wa kipekee sana kama wengi wetu tunavyodhani..

Kama unadhani kuona kijiti kinaungua halafu hakiteketei ni muujiza mkubwa zaidi ya unayoona leo hii roho za wafu zinafufuliwa kwa jina la Yesu kutoka mautini, jifirie mara mbili tena…

Lakini biblia inatuonyesha tabia ambayo Musa alikuwa nayo, pindi alipouona muujiza ule tu, hakupita kando, badala yake, moyo wake uliguswa sana, akasema muujiza huu hautanipita mpaka nijue maana yake ni nini, na ni nani aliyeweza kufanya maajabu makubwa kama haya..Ndipo Musa akasogea karibu..Embu jaribu kutengeneza picha akiwa pale akikitazama ki-mti kile cha kijani, kwa butwaa, akikiangalia mara mbili mbili, pengine anajiuliza kichwani, huyu aliyeweza kufanya hivi bila shaka atakuwa ni mkuu sana kwa maajabu na uweza, laiti ningemjua ningemng’ang’ania nisingemwacha….

Sasa wakati akiwa anafikiria hivyo na anataka kukaribia karibu zaidi ili azidi kuchunguza anachokiona ni macho yake au la! saa hiyo hiyo Mungu akaanza kuzungumza naye na kumwambia Musa,usikaribie mahali hapa, maana unaposimama ni nchi takatifu…..Tusome..

Kutoka 3:1 “Basi huyo Musa alikuwa akilichunga kundi la Yethro mkwewe, kuhani wa Midiani; akaliongoza kundi nyuma ya jangwa, akafika mpaka mlima wa Mungu, hata Horebu.

2 Malaika wa Bwana akamtokea, katika mwali wa moto uliotoka katikati ya kijiti; akatazama, na kumbe! Kile kijiti kiliwaka moto, nacho kijiti hakikuteketea.

3 Musa akasema, Nitageuka sasa, niyaone maono haya makubwa, na sababu kijiti hiki hakiteketei.

4 Bwana alipoona ya kuwa amegeuka ili atazame, Mungu akamwita kutoka katikati ya kile kijiti, akasema, Musa! Musa! Akasema, Mimi hapa.

5 Naye akasema, Usikaribie hapa; vua viatu vyako miguuni mwako; maana mahali hapo unaposimama ni nchi takatifu.”.

Kama tunavyojua sote baada ya hapo, ni nini kilitokea katika huduma ya Musa..Mungu alimtumia kwa ishara na miujiza isiyokuwa ya kawaida kwa kipindi chote..

Lakini tujiulize, Ni kwanini Mungu hakuzungumza naye moja kwa moja tangu mwanzoni na kumpa huduma ile kubwa, mpaka akaruhusu kwanza ageuke?

Ni kwasababu Mungu alikuwa anapima kujali kwake kwanza..Na ndio maana akatanguliza kwanza ule muujiza mdogo wa kijiti kuteketea, ili aone kama Musa atauthamini kwa kutaka kujua maana yake au La! ..Na laiti kama Musa asingeuthamini, na kupita zake kuendelea na mambo yake ya uchungaji kamwe Mungu asingekuwa na habari na Musa..maisha yangeendelea kama kawaida tu, kama vile hakuna chochote kilichotokea.

Mungu huwa anawaza na kusema, ikiwa muujiza mdogo kama huu hauthamini, atauthamini vipi nikija kumpasulia habari huko mbeleni, atathamini vipi siku nikijifunua kwake kama nguzo ya moto huko mbeleni?, atathamini vipi wakati nawashushia mana kutoka mbinguni? Atathamini vipi siku nikiyowatolea maji mwambani?.

Lakini Musa alithamini madogo yale, na Ndio maana Mungu alimtumia Musa katika makubwa pia.

Hata sisi ni kwanini Mungu hasemi na sisi au hatembei na sisi katika viwango vingine? Ni kwasababu hatuithamini miujiza ile midogo anayoipitisha mbele yetu sasa.. Tunaona ni kawaida tu..Musa hakuona kawaida….Kama Musa leo hii angeona wafu wanafufuliwa, tujiulize angemshangaa Mungu kwa viwango gani?..Je! yale Mungu anayotutendea ambayo tunaona kabisa ni miujiza mikubwa, Je yanatutafakarisha usiku na mchana, na kutufanya tumshangae Mungu na kumshukuru daima mpaka kumpa Mungu aone sababu ya kutufanyia na makubwa zaidi ya hayo? Je! yale tunayoona wengine wanatendewa na Mungu, na tunaona kabisa ule ni muujiza, Yule kaponywa, Yule kafunguliwa, Yule kaokolewa, Je hayo yanatuingia mioyoni mwetu kiasi cha kwamba yanatugeuza na kutufanya tumshangae Mungu kwa kipindi kirefu au tunayapuuzia tu?

Nataka nikuambie tukiyathamini hayo tunayoona leo hii kama madogo, na kuyatafakari sana, na kumsifu Mungu kwa ajili ya hayo, tuwe na uhakika kuwa tutafungua milango ya kuoiona miujiza mikubwa isiyokuwa ya kawaida katika Maisha yetu, au katika huduma zetu. Kama Mungu alimtumia Musa anaweza kututumia na sisi pia kudhihirisha utukufu wake kwa wasio mjua.

Lakini leo tukiyapuuzia, tujue kuwa hatutafika popote,..Tuthamini haya madogo tunayoyaona kwanza, na ndipo hayo makubwa mengine Mungu atuzidishie..tujifunze kwa mababa hawa waliotutangulia tufanikiwe..

Ubarikiwe.

Pia unaweza ukapata mafundisho haya Kwa njia ya Whatsapp yako, jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii 0789001312


Mada Nyinginezo:

KWANINI DAUDI ALIKUWA NI MTU ALIYEUPENDEZA MOYO WA MUNGU?

Nifanye nini ili niwe na uhakika nikifa naenda mbinguni?

MIILI YA UTUKUFU ITAKUWAJE?

FAHAMU ZA WATU HUWA ZINAONDOLEWA NA NINI?

Kwanini Mungu hakumuua Nyoka, akamwacha Hawa ajaribiwe katika bustani ya Edeni?

“Ninyi ni chumvi ya dunia” Andiko hilo lina maana gani?

Rudi Nyumbani:

Print this post

ITAFAKARI SIKU YA HUKUMU.

Shalom, Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe…Sio vibaya tukajikumbusha mambo ambayo tulishawahi kujifunza huko nyuma au kufundishwa..Bwana katika agano la kale aliwazuia wana wa Israeli kula wanyama ambao hawacheui…kucheua kama ilivyotafsiriwa kwenye biblia maana yake sio kutoa hewa mdomoni inayotoka tumboni..au kutapika…Hapana..kucheua ni tabia Wanyama wanayokuwa nayo ambapo baada ya kula nyasi huwa wanahifadhi chakula kile katika matumbo yao na kisha baadaye wanauwezo wa kukirudisha chakula kile na kukitafuna tena na kisha kukimeza kikiwa kimesagika vyema zaidi…Sasa mnyama kama nguruwe alikuwa hacheui, hivyo ni najisi…Ikifunua tabia ya aina ya watu fulani..ambao Hawana tabia ya kukumbuka mambo waliyojifunza nyuma, wala hawana tabia ya kurudia kutafakari tena na tena..wakila wamekula, hawana muda wa kukirudia tena kukitafakari, kukitafuna tena kile chakula…Na hiyo inawafanya wanakuwa warahisi kusahau mema yote na mazuri yote ambayo Mungu alishawhi kuwafanyia huko nyuma.

Lakini tukijifunza kujikumbusha mambo tuliyojifunza huko nyuma, na kurudia kuyatafakari tena na tena tunajiweka katika nafasi nzuri ya kumshinda yule mwovu, na hivyo katika roho sisi tunaonekana ni viumbe ambavyo si najisi mbele za Mungu.

Hivyo tujikumbushe kidogo kuhusu hukumu. Tuitafakari kidogo hukumu ya Bwana Yesu itusaidie kujua hukumu yetu itakuwaje huko mbeleni baada ya Maisha haya.

Kama tunavyojua Bwana alishtakiwa na Wayahudi (yaani wa-Israeli) lakini alisulubiwa na warumi (Yaani watu wa Mataifa). Kwahiyo jamii zote mbili: Wayahudi na sisi watu wa Mataifa) tuna hatia juu ya Damu ya Yesu. Ndio maana ukombozi na msamaha unatuhusu sote. Kwasababu wote tumetenda dhambi..

Warumi 3:23 “ kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu”..

Na kama Bwana Yesu alisimamishwa mbele ya kiti cha hukumu alivyokuwa hapa duniani…Na akahukumiwa mbele ya watu wote (wayahudi na watu wa mataifa), na akatoa hesabu ya mambo yote.

Yohana 19:13 “Basi Pilato, aliposikia maneno hayo, akamleta Yesu nje, akaketi juu ya kiti cha hukumu, mahali paitwapo Sakafu ya Mawe, au kwa Kiebrania, Gabatha”.

Vivyo hivyo siku ile ya hukumu watu wa mataifa yote duniani nao pia watasimama mbele zake yeye katika kiti cheupe cha hukumu. Na kila mmoja atatoa hesabu ya mambo yake aliyoyafanya alipokuwa hapa duniani.

Kwahiyo ufanyalo leo kumbuka kwamba siku moja litaletwa hukumuni..

Mhubiri 12:13 “Hii ndiyo jumla ya maneno; yote yamekwisha sikiwa; Mche Mungu, nawe uzishike amri zake, Maana kwa jumla ndiyo impasayo mtu.

14 Kwa maana Mungu ataleta hukumuni kila kazi, pamoja na kila neno la siri, likiwa jema au likiwa baya”.

Na zaidi tena Biblia  inasema..

Ufunuo 20:11 “Kisha nikaona kiti cha enzi, kikubwa, cheupe, na yeye aketiye juu yake; ambaye nchi na mbingu zikakimbia uso wake, na mahali pao hapakuonekana.

12 Nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wamesimama mbele ya hicho kiti cha enzi; na vitabu vikafunguliwa; na kitabu kingine kikafunguliwa, ambacho ni cha uzima; na hao wafu wakahukumiwa katika mambo hayo yaliyoandikwa katika vile vitabu, sawasawa na matendo yao.

13 Bahari ikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake; na Mauti na Kuzimu zikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake. Wakahukumiwa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake.

14 Mauti na Kuzimu zikatupwa katika lile ziwa la moto. Hii ndiyo mauti ya pili, yaani, hilo ziwa la moto.

15 Na iwapo mtu ye yote hakuonekana ameandikwa katika kitabu cha uzima, alitupwa katika lile ziwa la moto.”

Kama Bwana Yesu na ukamilifu wake wote alisimama mbele ya kiti cha Hukumu cha Herode…Sisi ni nani tuikwepe hukumu inayokuja?..Tujitahidi siku ile tusiwepo katika kundi la watu watakaohukumiwa mauti ya milele katika ziwa la moto..bali watakaohukumiwa kwa kupewa thawabu katika kuushinda ulimwengu.

Mathayo 25:19 “Baada ya siku nyingi akaja bwana wa watumwa wale, akafanya hesabu nao.

20 Akaja yule aliyepokea talanta tano, akaleta talanta nyingine tano, akisema, Bwana, uliweka kwangu talanta tano; tazama, talanta nyingine tano nilizopata faida.

21 Bwana wake akamwambia, Vema, mtumwa mwema na mwaminifu; ulikuwa mwaminifu kwa machache, nitakuweka juu ya mengi; ingia katika furaha ya bwana wako.

22 Akaja na yule aliyepokea talanta mbili, akasema, Bwana, uliweka kwangu talanta mbili; tazama, talanta nyingine mbili nilizopata faida.

23 Bwana wake akamwambia, Vema, mtumwa mwema na mwaminifu; ulikuwa mwaminifu kwa machache, nitakuweka juu ya mengi; ingia katika furaha ya bwana wako.

24 Akaja na yule aliyepokea talanta moja, akasema, Bwana, nalitambua ya kuwa wewe u mtu mgumu, wavuna usipopanda, wakusanya usipotawanya;

25 basi nikaogopa, nikaenda nikaificha talanta yako katika ardhi; tazama, unayo iliyo yako.

26 Bwana wake akajibu, akamwambia, Wewe mtumwa mbaya na mlegevu, ulijua ya kuwa navuna nisipopanda, nakusanya nisipotawanya;

27 basi, ilikupasa kuiweka fedha yangu kwa watoao riba; nami nikija ningalipata iliyo yangu na faida yake.

28 Basi, mnyang’anyeni talanta hiyo, mpeni yule aliye nazo talanta kumi”.

Tukikumbuka pia hakuna nafasi ya pili baada ya kifo..Mtu kaandikiwa kufa mara moja tu, na baada ya kifo ni hukumu kasome (Waebrania 9:27). Hakuna maombi yoyote yanayoweza kumwamisha mtu kutoka katika moto wa kuzimu na kumwingiza katika paradiso…Ukifa katika dhambi ndio tayari umepotea milele..Biblia inasema mti uangukiapo huko huko utalala (Mhubiri 11:3)…maana yake ukifa na kwenda kuzimu ndio huko huko utakuwepo milele.

Je umesimama katika Imani?..Unauhakika Kristo akija leo utakwenda naye. Bwana akusaidie, na Bwana atusaidie sote katika Jina la Yesu Kristo.

Ubarikiwe sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii 0789001312


Mada Nyinginezo:

PENGINE MUNGU ALISHASEMA NAWE KWA NJIA HII.

HATARI YA KUHUBIRI INJILI TOFAUTI NA ILIYOANDIKWA KWENYE BIBLIA.

HISTORIA YA ISRAELI.

Kuna ufufuo wa aina ngapi?

HAKIKISHA UNALIELEWA NENO.

UWE MWAMINIFU HATA KUFA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

MAMBO 5 AMBAYO KILA MKRISTO ANAPASWA KUFAHAMU.

Mambo 5 ambayo kila mkristo anapaswa kufahamu.


NJIA IMESONGA.

Kuvuka ng’ambo si kurahisi kama inavyodhaniwa na wengi.

Mathayo 7:13  “Ingieni kwa kupitia mlango ulio mwembamba; maana mlango ni mpana, na njia ni pana iendayo upotevuni, nao ni wengi waingiao kwa mlango huo.

14  Bali mlango ni mwembamba, na njia imesonga iendayo uzimani, nao waionao ni wachache”..

Hivyo usivunjike moyo, unapojikuta upo peke yako katika safari ya wokovu, kikubwa tu ni kukazana na Bwana, na kuhakikisha hurudi nyuma, kwasababu Bwana ameahidi kuwa pamoja na wewe safarini hadi mwisho.

MAJARIBU NI LAZIMA YAJE:

Yohana 16:33 “Hayo nimewaambieni mpate kuwa na amani ndani yangu. Ulimwenguni mnayo dhiki; lakini jipeni moyo; mimi nimeushinda ulimwengu”.

Usirudi nyuma unapokutana na utelezi safarini, mambo kama magonjwa, misiba, kupungukiwa, kuuudhiwa kwa ajili ya wokovu, kutukanwa, kupoteza n.k…utakutana nayo.Lakini Jipe moyo kama Bwana alivyosema..Kwasababu pamoja na hayo ameahidi kutuwekea na mlango wa kutokea, hivyo hayatadumu milele.

MAISHA NI MAFUPI.

Yakobo 4:13  “Haya basi, ninyi msemao, Leo au kesho tutaingia katika mji fulani na kukaa humo mwaka mzima, na kufanya biashara na kupata faida;

14  walakini hamjui yatakayokuwako kesho. Uzima wenu ni nini? Maana ninyi ni mvuke uonekanao kwa kitambo, kisha hutoweka”.

Tukilijua hilo pia basi tutautumia muda wetu vizuri kwa Bwana, kwasababu hatujui ni muda gani tuliobakiwa nao hapa duniani. Hivyo hatutaishi kwa kujisahau mpaka kupitiwa na mambo mengine tukasahau kuwa tupo ukingoni mwa safari.

HUKUMU INAKUJA.

Warumi 14:12  “Basi ni hivyo, kila mtu miongoni mwetu atatoa habari zake mwenyewe mbele za Mungu.

Tukijua kuwa utafika wakati ambao kila mkristo atasimama mbele ya kiti cha enzi cha Kristo na kueleza ni jinsi gani alivyoitumia talanta yake…Hiyo inatuhimiza, kila siku tuishi maisha ya kujitathimini , na vilevile kuitenda kazi yake kwa uaminifu wote na kwa bidii, ili tusiwe miongoni mwa  lile kundi la watumwa walegevu”.

UMILELE UPO.

Danieli 12:2 “Tena, wengi wa hao walalao katika mavumbi ya nchi wataamka, wengine wapate uzima wa milele, wengine aibu na kudharauliwa milele”.

Kuna kuishi maisha yasiyo na mwisho huko mbeleni. Fikiria unakwenda kuwa nani?  Tukilijua hilo, basi itatufanya tuwekeze kwa bidii kule ili thawabu zetu ziwe nyingi, tuwe matajiri katika ufalme wa Mungu, kwasabaabu utajiri wa kule utakuwa ni wa kudumu milele, lakini tusipowekeza chochote, mambo yatakuwa ni kinyume chake, tutakwenda kuwa watu wa kawaida milele, au tusifike kabisa…

Mimi na wewe tupige mbio tuumalize mwendo salama…

Shalom.

Mada Nyinginezo:

KWA KUWA NGUVU ZA MBINGUNI ZITATIKISIKA.

Je! Ni sahihi kwa mkristo kuoa/kuolewa na mtu wa imani nyingine?

JE! WATOTO WACHANGA WANAWEZA KUHUKUMIWA NA KUTUPWA MOTONI.

URIMU NA THUMIMU NI NINI KATIKA BIBLIA?

NGUVU YA MSAMAHA

WALE WAZEE ISHIRINI NA WANNE (24), WANA KAZI GANI?

DHAMBI ILIYOMKOSESHA SHETANI:

Rudi Nyumbani:

Print this post

MAJINI WAZURI WAPO?

Majini ni nini? Je kuna majini wazuri?, je pete za majini ni zipi? na namba za majini ni zipi?..Je kuna njia yoyote ya kupata utajiri wa haraka?

JIBU: Kwanza ni vizuri kufahamu majini ni nini?…Majini ni jina lingine la roho zilizoasi mbinguni, ambazo zilitupwa chini duniani pamoja na lusifa ambaye ndiye alikuwa kiongozi wao.

Majini jina lingine yanaitwa mapepo..wakati wakiwa mbinguni lusifa ambaye ndiye shetani aliwadanganya wasimame kinyume cha Mungu na kutaka kuwa kama Mungu…Lakini walishindwa vita vile na Malaika walio upande wa Mungu na kuishiwa kutupwa chini duniani.

Ufunuo 12:7 “Kulikuwa na vita mbinguni; Mikaeli na malaika zake wakapigana na yule joka, yule joka naye akapigana nao pamoja na malaika zake;

8 nao hawakushinda, wala mahali pao hapakuonekana tena mbinguni.

9 Yule joka akatupwa, yule mkubwa, nyoka wa zamani, aitwaye Ibilisi na Shetani, audanganyaye ulimwengu wote; akatupwa hata nchi, na malaika zake wakatupwa pamoja naye”

Kazi ya majini haya baada ya kutupwa duniani ni kwenda kinyume na kusudi la Mungu juu ya mwanadamu. Hivyo yanapambana usiku na mchana kuhakikisha kusudi la Mungu juu ya mwanadamu halifanikiwi. Majini haya au kwa lugha nyingine mapepo hayataki mwanadamu hata mmoja afike mbinguni. Hivyo yanatumia ujuzi wao na akili zao zote kuhakikisha yanatimiza malengo yao.

Kumbuka walioposhindwa vita mbinguni (kama tunavyosoma katika kitabu cha Ufunuo 12) hawakunyang’anywa na Mungu nguvu walizokuwa nazo wala ujuzi..walifukuzwa wakiwa na nguvu walizopewa na Mungu kadhalika na fahamu zao…Hivyo wanazo mpaka sasa nguvu… Ingawa sisi tuliookoka tumepewa nguvu zilizo kuu zaidi zao kupitia damu ya Yesu Kristo.

JE KUNA MAJINI WAZURI?

Majini wote ni wabaya hakuna jini hata mmoja aliye mzuri. Shetani aliye mkuu wa majini hayo anatumia nguvu kubwa kuwadanganya watu kwamba kuna majini wazuri..lengo lake ni ili watu wajishughulishe kuzitafuta roho hizo na kujishikamanisha nazo. Na kwa pamoja wafanye kazi ya kuziangusha roho nyingine.

JE PETE ZA MAJINI NI ZIPI?

Majini yanaweza kumwingia mtu yoyote kwa kupitia njia yoyote ile ambayo ipo kinyume na mapenzi ya Mungu sio pete tu!..Majini/mapepo yanaweza kumwingia mtu kwa kupitia mawigi ya kichwani, kwa kupita vipodozi, wanja, kwa kujichora tattoo,kwa kufanya ibada za sanamu na pia njia kuu ni kwa kupita kufanya uasherati na mtu ambaye si mke wako au mume wako na pia kwa kuangalia picha za ngono. Pete inaweza kuwa ni njia ya mwisho kabisa ya kuingiza majini ndani ya mtu.

Mtu anapokwenda kwa mganga au anapojiunga na kikundi fulani cha kichawi kama freemason na vingine anaweza kukabidhiwa pete, mkufu, picha au chochote kile…vitu hivyo ni mlango pia wa kuingiza roho za majini ndani ya mtu.

JE NAMBA ZA MAJINI NI ZIPI?

Maelfu ya watu wasio na ufahamu wanazunguka mitandaoni kutafuta namba za majini..Majini ni roho! hayawezi kuwa na namba za simu za mkononi. Mawakala wao ambao ni waganga wa kienyeji na wachawi ndio wenye namba za simu lakini si mapepo. Hayo ni maroho yanafanya kazi katika ulimwengu wa roho…

JE KUNA NJIA YOYOTE YA KUPATA UTAJIRI WA HARAKA KUPITIA MAJINI?

Uongo mkubwa shetani anaowadanganya wengi ni kwamba kwake kuna fedha za bure na za haraka!..Nataka nikuambie ndugu hicho kitu hakipo..lengo la shetani ni kukupeleka tu kuzimu hakuna lingine.

Njia ifuatayo ndiyo anayoitumia shetani kuwapatia watu mali kwa njia ya majini.

1.Anatumia mtu jini/pepo..Lile pepo linaweza kuwa la aina yoyote ile, aidha zinaa, ulevi, wizi, uuaji n.k Sasa lile jini, tuchukue mfano la zinaa linapomwingia mtu..au mtu anapokwenda kwa waganga kutafuta mali anapewa pete..Na ile pete ndani yake imebeba mojawapo ya hilo jini..labda tuseme la zinaa..Mtu anapoivaa lile pepo la zinaa linamwingia..yule mtu akitoka pale anakuwa mwasherati kupita kawaida…kama ni mwanamke anakuwa ni kahaba kupita kawaida…na hivyo linamsukuma kwenda kufanya kazi ya ukahaba. Na kwa kupitia hiyo kazi ya ukahaba ndipo anapopata fedha.. Lakini si kwamba anakaa tu na kisha fedha zinaingia.

Kadhalika na wizi, ni hivyo hivyo..pepo la wizi linamwingia na linakwenda kumfanya kuwa mwizi hodari..na kwa wizi ule anapata mali zisizohalali.

Na hivyo hivyo mauaji..Pepo linamwingia mtu na kumfanya aone kuua sio shida tena na kwa kupitia mauaji yale anapata kazi nyingi za ujambazi na hivyo kupata fedha kwa kazi hiyo.

Kwahiyo hakuna fedha za bure kwa shetani..Anakupa jini/pepo na jini hilo linakwenda kukutumikisha kupata hizo mali. Na hautakaa tu baada ya kuipokea hiyo pete..kwamba fedha zidondoke.

Hata wale wanaofanya uchawi ujulikanao kama chuma ulete..Nao pia wanavalishwa pepo hilo ambalo linawafanya wateseke kwa hali na mali kufanya uchawi huo..gharama wanazotumia kufanya uchawi huo ni mkubwa kuliko hata faida wanazozipata huko.

Hivyo kuyatafuta majini au kujishughulisha nao ni kujitesa na ni kwenda kinyume na mpango wa Mungu…Kufanya kazi na majini/mapepo ni kuwa Adui wa Mungu rasmi asilimia 100. Na kujitengenezea daraja zuri la kuwa miongoni mwa watakaoteswa sana katika ziwa la moto baada ya hukumu.

Na madhara ya kuwa na majini ni mauti..Majambazi wote kama Neema ya Kristo haitawapitia wanaishia kupigwa risasi, makahaba wote kama Neema ya Kristo haitawafikia wanaishia kufa kwa magonjwa…vivyo hivyo wezi wanaishia kuchomwa moto..Mafisadi wanaishia kufungwa..wachawi wanaishia kufa kifo cha ghafla n.k

Sasa kwanini kudanganyika na uwongo wa shetani kwamba kwake kuna fedha za bure?..Kwamba ni kuvaa pete tu, ni kuchinja mbuzi tu!..shetani anakuambia ni kuvaa pete tu lakini hakuambii ukahaba atakaokwenda kukutumikisha nao.

Hivyo kama Kama hujampa Kristo maisha yako. Mgeukie Leo..usitafute mali wala msaada kwa shetani na wala hakuna majini wazuri watakaokusaidia kupunguza ugumu wa maisha..shetani yeye kashaasi, anachokisubiria tu ni kutupwa katika ziwa la moto..na anataka kwenda na wengi..hivyo anatumia uongo wa kila namna kujaribu kuvuta watu kwake..tumwache aende yeye peke yake sisi tumgeukie Kristo tumaini la utukufu.

Bwana akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii 0789001312

Group la whatsapp Kwa mgawanyo bora wa masomo download App hapa>> App wingu la mashahidi


Mada Nyinginezo:

Rudi Nyumbani:

Print this post