Mwanzo 13:14 Bwana aliongea na Abramu Alipotengana na Lutu na kumpa nchi. Sasa ni kwanini aongee naye baada tu ya wao kutengana?. inamana uwepo wa Lutu ulimzuia Mungu kumpa nchi Abramu?.
JIBU: Tatizo halikuwa kwa Mungu, bali kwa Ibrahimu. Yale mazingira aliyokuwa nayo Ibrahimu ndiyo yaliyokuwa kikwazo cha Mungu kuzungumza naye kwa wakati.
Jambo hilo halikuanzia hapo, utaona tangu Mungu alipomwambia atoke kule Uru ya ulkaldayo, Badala atoke yeye peke yake alitoka na baba yake ambaye alikuwa ni mpagani-mwabudu miungu, na hiyo ikamfanya akae sehemu moja iliyoitwa Harani kwa muda mrefu bila Mungu kuzungumza naye.. Na siku tu baba yake alipokufa ndipo Mungu akazungumza naye tena na kumwambia aondoke pale aende katika nchi ya Kaanani..Jambo ambalo lingepaswa liwe ni la safari ya moja kwa moja, lakini lilimfanya awe mtu wa vituo vituo kwa muda mrefu. Ni wazi kuwa baba yake alimpinga vikali sana, kwa mambo mengi.
Matendo 7:3 “akamwambia, Toka katika nchi yako na katika jamaa zako, ukaende hata nchi nitakayokuonyesha.
4 Ndipo alipotoka katika nchi ya Wakaldayo, akakaa Harani, akatoka huko baada ya kufa babaye, Mungu akamhamisha mpaka nchi hii mnayokaa ninyi sasa”.
Lakini hakuondoka peke yake tena kule Harani bali aliondoka na mjomba wake Lutu..Na walipofika huku, Mungu hakujifunua kikamilifu kwake mpaka walipotengana tena, ndipo baadaye Mungu alipoona utulivu wake sasa kazungumza naye tena.
Hiyo ni desturi ya Mungu tangu zamani. Akikuita unapaswa uondoke wewe kama wewe na kumfuata, kwasababu ukienda na mtu mwingine ambaye hana Habari na Mungu, ni wazi kuwa atakuja kuwa kikwazo kikubwa kwako huko mbeleni, unaweza wewe kutamani hivi, yeye atatamani kile, wewe ukiwaza muda huu nikasali, au nikashuhudie yeye akafikiri vile mkafanye biashara, na hiyo inakuwa kikwanzo kikubwa sana cha Mungu kuyatimiliza yale maono aliyoyaweka ndani yako.
Na ndio maana Bwana Yesu alisema, nimekuja kuleta upanga duniani….
Mathayo 10:34 “Msidhani ya kuwa nimekuja kuleta amani duniani; la! Sikuja kuleta amani, bali upanga.
35 Kwa maana nalikuja kumfitini mtu na babaye, na binti na mamaye, na mkwe na mkwe mtu;
36 na adui za mtu ni wale wa nyumbani mwake.
37 Apendaye baba au mama kuliko mimi, hanistahili; wala apendaye mwana au binti kuliko mimi, hanistahili”.
Hivyo tukitaka tufike mbali, au tukitaka Mungu atutumie ipasavyo hatuna budikuweka mbali vitu au kujitenga na watu ambao tunaona kabisa wanaweza kuathiri mwito wetu kiuwepesi.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
Je! Ule mwiba uliokuwa katika mwili wa Paulo ulikuwa ni nini?
Je! Ule mwiba uliokuwa katika mwili wa Paulo ulikuwa ni nini?
NINI NI KILICHOMFANYA IBRAHIMU AKUBALI KUMTOA MWANAWE SADAKA?
Kwanini Mungu aliikubali sadaka ya Yeftha ya kumtoa binti yake kafara?
Mungu ni Mungu tu!.
Watu wengi tunadhani, tunaweza kumuudhi Mungu au kumkomoa Mungu kiasi cha kumgharimu kupoteza kitu fulani, pale tunapofanya jambo lisilompendeza..
Biblia inasema hivi..
Ayubu 35:6 Ikiwa umefanya dhambi, umefanya nini juu yake? Yakiwa makosa yako yameongezeka, wamfanyia nini yeye?
7 Ikiwa u mwenye haki, wampa kitu gani? Au yeye hupokea nini mkononi mwako?
8 Uovu wako waweza kumwumiza mtu kama wewe; Na haki yako yaweza kumfaa mwanadamu.
Unaona, Kumbe hata haki zetu, au matendo yetu mazuri, hayamwongezi Mungu kitu chochote, hayamwongezei umri wa kuishi, kwa yeye tayari ni wa milele, hayamwongezei afya, wala chochote kile kizuri kwasababu vitu vyote vinatoka kwake.
Warumi 11:36 “Kwa kuwa vitu vyote vyatoka kwake, viko kwa uweza wake, tena vinarejea kwake. Utukufu una yeye milele. Amina”.
Tukisema, tujiue, hakumbadilishi yeye kuwa Mungu, tukisema hatumpendi bado hakumfanyi yeye kutokuwa Mungu, hata tukisema hayupo, ndio kabisa hakuubadilishi uungu wake. Ndege wataendelea kumsifu, jua litaendelea kuangaza majira yake, anga litaendelea kuwa la blue.
Hivyo tunachopaswa kufanya ni kujinyenyekeza mbele zake tu, haijalishi leo hii tunapitia magumu mengi kiasi gani, au mazuri mengi kiasi gani, tukiwa wanyenyekevu mbele zake, wakati wake ukifika tutauna wema aliotuwekea sisi tunaomtumainia ..Kuzielewa njia zote za Mungu hiyo haiwezekani, hata tupambane vipi, lakini tunachojua tu ni kuwa anatuwazia mawazo mazuri siku zote,
Yeremia 29:11 Maana nayajua mawazo ninayowawazia ninyi, asema Bwana, ni mawazo ya amani wala si ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za mwisho.
Hivyo ndugu yangu unausoma ujumbe huu pengine, bado hujaokoka, wakati uliokubalika ndio sasa, usiache leo ipite bila kuyasalimisha maisha yako kwa Kristo. Ukimaanisha na kudhamiria kweli kutubu, hapo ulipo haijalishi upo sehemu gani, Kristo atayageuza maisha yako mara moja, na kukupa badiliko la ajabu ambalo litakufanya ulistaajabie maisha yako yote..
Kama upo tayari kufanya hivyo basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie maisha yako yote kama ilivyokuwa hata kwetu sisi. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.
EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, . NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.
ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.
AMEN.
Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, kuanzia huu wakati, Kwasababu Mungu ameshaipokea toba yako . Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako sawasawa na Matendo 2:38.
Mungu ni Mungu tu!
Ubarikiwe sana.
Mada Nyinginezo:
SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?
CHUKIZO LA UHARIBIFU
UTENDAJI KAZI WA MPINGA-KRISTO.
Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!
JINSI SODOMA NA GOMORA ILIVYOKUWA INAVUTIA SANA..
Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe.
Kama wengi wetu tujuavyo, Ndoa ya kwanza ilifungishwa pale Edeni na Mungu mwenyewe. Na ilikuwa ndoa takatifu, iliyobeba msingi na dira ya ndoa nyingine zote zitakazofuata jinsi zinavyopaswa ziwe.
Katika ndoa ile ilihusisha Mtu mume mmoja (Adamu) na mtu mke mmoja (Hawa)..Kwa kupitia wazazi wetu hawa wawili ndio sisi sote tumetokea…ikiwa na maana kuwa ndoa kamili na takatifu inahusisha mume mmoja na mke mmoja…na si Zaidi. Hicho ni kigezo cha kwanza na cha muhimu.
Pia kabla ya ndoa ile kufungishwa, Maisha yalianza na Adamu kwanza, Mungu alimpa Adamu mimea, mashamba ya kulima, makazi na kila kitu, hapo kabla Hawa hajatokea…na Adamu akaanza majukumu yake ya shughuli pale Edeni kabla ya Hawa kutokea…Na Hawa alipotokea alikuwa kama msaidizi tu wa kazi ambayo tayari ilikuwa imeshaanza. Ikiwa na maana kuwa Mwanamume yoyote kabla hajadhamiria kuoa ni lazima angalau awe na mahali pa kujishikiza ili aweze kumhudumia huyo mkewe anayekuja kumwoa…
Na kumbuka Mungu hakumleta Hawa kwaajili ya tamaa za mwili za Adamu, hapana bali alimleta ili awe msaidizi kwake, kwa namna zote, kifikra, na hata katika kazi zake za kimaendeleo Adamu alizokuwa anazifanya…Ikiwa na maana kuwa lengo la kwanza la ndoa sio kukutana kimwili kama inavyochukuliwa sasa na wachache wasio na maarifa ya kutosha.
Hivyo mwanamke jukumu lake kubwa katika ndoa ni kushirikiana na mume wake, na kuyafanya majukumu yote ambayo mume wake angepaswa ayafanye, ikiwemo ya kihuduma na ya kiuchumi, Hawa hakupelekwa kwa Adamu kumtoa Adamu pesa!..bali awe msaidizi….Maana yake kitu ambacho hakijakaa sawa au hakijakamilika mikononi mwa mwanaume, mwanamke anakiweka sawa na kukimalizia.
Na jukumu kubwa Zaidi mwanamume na mwanamke walilopewa ni kujiepusha na Uovu…Na shetani huwa anawatumia wanawake wengi kuharibu ndoa kuliko wanaume..Kama Hawa mzazi wetu wa kwanza angekaa katika nafasi yake na kujiepusha na uovu, leo hii duniani kungekuwa ni paradiso, lakini kwa kuacha majukumu yake ya USAIDIZI na kwenda kula matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya ambayo Mungu hakumwagiza matokeo yake ndio yakawa yale…Na hata sasa mwanamke akiacha majukumu yake na kujikita katika ulimwengu huu, katika usengenyaji, umbea, katika kutoa siri za mume wake nje, katika kutomheshimu mume wake, kumdharau, kumdhalilisha, kumwaibisha, kuvaa kikahaba, kuwa mhuni, mlevi,mtu mwenye mizaha na kila aina ya udunia, anajiharibia mwenyewe na anaibomoa nyumba yake kwa mikono yake mwenyewe..
Na Ndoa takatifu ni lazima ihusishe watu wawili wenye Imani moja..Ni kinyume na maandiko kuoa/kuolewa na mtu asiyeamini baada ya wewe kuamini, Kama umeshamwamini Yesu Kristo na uweza wake hupaswi hata kidogo kutafuta kuoa/kuolewa na mtu asiye mkristo. Na ndoa yoyote ya kikristo lazima iwasilishwe na kubarikiwa mbele ya kanisa la Kristo. Sio sahihi kabisa kufunga ndoa za kimila wala za kiserikali baada ya kumwamini Yesu Kristo.
Na ni lazima kulipa mahari kwa ndugu wa mwanamke kabla ya kumwoa, kama huo ndio utaratibu wa familia ya mwanamke, Adamu hakulipa mahari kwasababu mkewe Hawa ,chimbuko lake lilikuwa ubavuni mwake, hakuwa na wazazi wala ndugu…lakini sasa kila mwanamke anao wazazi/ndugu/walezi…Huko ndiko alikolelewa, hakulelewa ubavuni mwako,…kwahiyo ni wajibu kumtoa kwa wazazi wake kwa utaratibu huo maalumu wa kulipa mahari…
Hata Hawa alipotolewa ubavuni mwa Adamu, Bwana Mungu aliparudishia nyama pale palipotolewa ili Maisha ya Adamu yaweze kuendelea, hakuacha shimo pale wala kidonda!…Na hali kadhalika unapomtoa mwanamke kwa wazazi wake ni lazima uzibe pengo uliloliacha pale, na hilo unaliziba angalau kwa mahari, sio unamwiba na kuacha huzuni kule na malalamiko na laana na maumivu.
kama utashindwa kulipa mahari ya kiasi hicho kidogo cha fedha utawezaje kuitunza na kuihudumia familia yako inayokuja huko mbele, ambayo pengine itahitaji matunzo ya gharama nyingi kuliko hizo za mahari??…kama hutaki kutoa mahari, maana yake bado hujaelewa maana ya kuoa, hivyo unapaswa ungoje mpaka utakapoelewa vyema maana ya ndoa ndipo uoe.
Na mwisho biblia inatuambia kuwa wakati tuliobakiwa nao ni mchache sana…wale ambao wameoa na wawe kama hawajaoa…ili muda mwingi tuutumie katika kuutafuta Zaidi ufalme wake na haki yake kwasababu unyakuo upo karibuni, na mbinguni tuendako hakutakuwa na kuoa wala kuolewa, yatakuwa ni mambo mapya huko ambayo ni ya muhimu Zaidi kuliko haya.
1Wakorintho 7:28 “Lakini, kama ukioa, huna hatia; wala mwanamwali akiolewa, hana hatia; lakini watu kama hao watakuwa na dhiki katika mwili nami nataka kuwazuilia hayo.
29 Lakini, ndugu, nasema hivi, muda ubakio si mwingi; basi tokea sasa wale walio na wake na wawe kama hawana;
30 na wale waliao kama hawalii; na wale wafurahio kama hawafurahi; na wale wanunuao, kama hawana kitu.
31 Na wale wautumiao ulimwengu huu, kama hawautumii sana; kwa maana mambo ya ulimwengu huu yanapita.
32 Lakini nataka msiwe na masumbufu. Yeye asiyeoa hujishughulisha na mambo ya Bwana, ampendezeje Bwana;
33 bali yeye aliyeoa hujishughulisha na mambo ya dunia hii, jinsi atakavyompendeza mkewe”
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
Mada Nyinginezo:
Mti wa MLOZI alioonyeshwa nabii Yeremia 1:12 tafsiri yake ni nini?
Ilikuwa ni mwaka wa 320, wakati wa utawala wa mfalme Licinius wa Rumi, Kumbuka zamani hizo Rumi ndiyo iliyokuwa inatawala karibu dunia nzima wakati huo na ndio iliyokuwa kichwa cha mbele kuwatesa na kuwaua wakristo ulimwenguni kote, Sasa huyu alikuwa ni mpagani, ambaye hakutaka kusikia Imani yoyote ya Kikristo.
Lakini upande wa pili kulikuwa na askari wa kirumi katika mji mmoja ulioitwa Sebaste (Kwasasa ni maeneo ya Uturuki) ambao jumla yao 40, waliotoka katika nchi mbalimbali walimwamini Kristo, na kuikiri Imani bila uwoga wowote,.Sasa alipopata habari alitoa amri kali ya kuzuia mtu yeyote kuabudu miungu mingine tofauti na yake, hivyo mfalme alichokifanya ni kutoa agizo, kwa mtu yeyote atakayeonekana anafanya hivyo atateswa vikali na kuuawa.
Lakini hawa askari, historia inatuambia wote hawa mashahidi 40 walikataa kusalimu amri, hivyo wakachukuliwa na kupelekwa kando kando ya ziwa la maji ya baridi (wakati huo ulikuwa ni msimu wa kipindi cha baridi kali huko Asia), ili wapigwe na baridi mpaka kuganda na kufa.
Na wakati huo huo Mfalme alitoa amri pembeni pawekwe bwawa la maji ya moto, na chakula kizuri, kwa yeyote atayesalimu amri atolewe na kuingizwa kwenye hilo bwana la moto apate moto, kisha alishwe vizuri.
Lakini katikati ya mateso hayo makali ambayo yaliwafanya wakae siku tatu usiku na mchana, mmoja wa wale 40 kweli alisalimu amri na kutoka kwenye maji yale ya baridi, hivyo wakabakia 39, lakini mmoja tena kati ya wale askari waliokuwa wanawasimamia akachomwa moyo sana, na usiku mmoja alipokuwa amelala kando kando ya moto kwenye barafu aliota ndoto, malaika ameshuka mbinguni, pale kwenye ziwa kisha akawavika wale askari mataji, anasema, aliyahesabu yalikuwa 39..
Alipoamka asubuhi akakata shauri, akavua silaha zake, akamkiri Kristo na saa hiyo hiyo akavua nguo zake za ki-askari, akaingia majini kuungana na wale 39 ili kutimiza idadi ya watu 40..
Na ilipofika siku ya nne asubuhi, wengi wao walikuwa wamekufa, lakini wale waliosalia hoi, waliuliwa, na miili yao ikachomwa moto, kisha, majivu yao yakaenda kutupwa kwenye mto.
Hivyo ndivyo walivyoishindania Imani mpaka kufa mashujaa hawa..
Biblia inatuambia..
Mathayo 16:25 “Kwa kuwa mtu atakaye kuiokoa nafsi yake, ataipoteza; na mtu atakayepoteza nafsi yake kwa ajili yangu, ataiona”.
Sisi tunaweza tusifikie huko kwenye kuchagua kifo au uzima kwa ajili ya Kristo, lakini kama tutashindwa kuchagua jambo jepesi la “kufa kwa Habari ya ulimwengu” kwa ajili ya Kristo , tusitazamie kamwe tutauona ufalme wa mbinguni.. sehemu nyingi biblia imetuonya kwa kutumia neno hili “MSIDANGANYIKE”..Ikiwa na maana, tunaweza kudanganyika, tukadhani kuwa kwa kuendelea kuwa walezi, siku moja tunaweza kuingia mbinguni, kwa kuendelea kuzini mara moja moja, kwa kutoa mimba, kwa kusagana, kwa kuvaa vimini na nguo za kikahaba, kwa kula rushwa, kwa kutazama picha za ngono mitandaoni, bado tukawa na nafasi ya kuingia mbinguni siku ya mwisho.
1Wakorintho 6:9 “Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? Msidanganyike; waasherati hawataurithi ufalme wa Mungu, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wafiraji, wala walawiti,
10 wala wevi, wala watamanio, wala walevi, wala watukanaji, wala wanyang’anyi”.
Biblia inatuambia tusidanganyike, njia ile imesonga sana, na wanaoyoiona ni wachache. Kama hatutakubali kufa kwa Habari ya ulimwengu mpaka tukaonekana sisi si kama wao, tusahau kuiona mbingu..
Kama kuacha kuvaa vimini, kuvaa suruali(wanawake), kunyoa viduku na kusuka rasta(wanaume),kuacha kampani za watu waovu, kuacha kusikiliza nyimbo za kidunia, kuacha kwenda disko, kuacha kula rushwa, kuacha kutazama picha za ngono, ni Ngumu basi, ni uzima wa milele ni wa watu wengine si wako! ….ni sawa na huyo askari mmoja aliyejaribu kuingia kwenye hayo maji ya baridi lakini uzalendo ukamshinda na kutoka kurudi kwenye mambo ya kidunia.
Ikiwa Mambo ya kujikana nafsi tu, yatatushinda, utawezaje kuutoa uhai wako kwa ajili ya Kristo, siku ile Je! tutawezaje kufananishwa na hili wingu kubwa la mashahidi wa Imani ambao walikuwa tayari kuyatoa Maisha yao (tena kwa kifo cha mateso) kwa ajili ya Kristo? (Waebrania 12:1)
Utasema mimi mazingira yanayonizunguka yananifanya nishindwe kuwa mkristo..Wenzako walikuwa ni wanajeshi wanatumika katika kazi ngumu za kidunia kushinda wewe lakini walikuwa tayari kumtanguliza Kristo kwanza.
Huu ni wakati wa kuvuta soksi zetu juu, na kuanza kuyatengeneza Maisha upya, nyakati hizi za mwisho si nyakati tena za kuvutwa vutwa tena katika wokovu, zama hizo zilishakwisha, kwasababu injili kila mahali anasikika sasa, huu ndio ule wakati Bwana Yesu alisema..
Mwenye kudhulumu na azidi kudhulumu; na mwenye uchafu na azidi kuwa mchafu; na mwenye haki na azidi kufanya haki; na mtakatifu na azidi kutakaswa (Ufunuo 22:11).
Hivyo kama wewe ni mtakatifu, pambana binafsi kuzidi kujitakasa, zidi kuogopa kuwa hapo katikati (vuguvugu), kwasababu biblia inasema walio hapo watatapikwa (Ufunuo 3:16 ). Hivyo ikiwa unajitahidi kufanya hivyo, kumbuka Bwana anakutia moyo na kukwambia, “Safari aliyoianzisha yeye moyoni mwako ataitimiza mpaka siku ile ya mwisho”.
Umeamua kuukataa ulimwengu, zidi kupiga hatua nyingine katika UTAKATIFU, haijalishi utaonekana umepotea kiasi gani, haijalishi utaonekana ni mjinga, endelea mbeleni.. lakini mwisho wako utakapofika utajikuta umetokea kwenye mji wa furaha…
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
CHUKUA MZIGO WA MWINGINE.
Chapa zake Yesu ni zipi hizo?
KUMBUKUMBU LA DHAMBI.
OLE WAO WANAOJITAHIDI KUMFICHA BWANA MASHAURI YAO.
KABLA YA MAANGAMIZI, KRISTO HUWA ANAONYESHA KWANZA NJIA YA KUTOROKEA.
USIMWOGOPE YEZEBELI.
Mara nyingi Mungu wetu akitaka kutupa ujumbe, au kumpa mtu ujumbe huwa anazungumza na sisi kwa mifano, au kwa ishara, na mifano hiyo inatusaidia kuzielewa vizuri hisia zake kwetu au kwa kitu fulani..…Kwamfano utaona Daudi alipowaacha wanawake waliokuwa wengi katika nchi yake na kwenda kumchukua mke wa Uria, utaona kabla Bwana hajampa ile adhabu alimpa mfano kwanza ambao ulimsaidia kuelewa kwa undani hisia ya Mungu juu yake kwa kile alichokifanya.
Hebu tusome kidogo,
2 Samweli 12:1 “Ndipo Bwana akamtuma Nathani aende kwa Daudi. Naye akamwendea, akamwambia, Palikuwa na watu wawili katika mji mmoja; mmoja wao alikuwa tajiri, wa pili maskini.
2 Yule tajiri alikuwa na kondoo na ng’ombe wengi sana;
3 bali yule maskini hakuwa na kitu, ila mwana kondoo mmoja, mdogo, ambaye amemnunua na kumlea; naye akakua pamoja naye, na pamoja na wanawe; hula sehemu ya posho lake, na kukinywea kikombe chake, na kulala kifuani mwake, akawa kwake kama binti.
4 Hata msafiri mmoja akamfikilia yule tajiri, naye akaacha kutwaa mmoja wa kondoo zake mwenyewe au mmoja wa ng’ombe zake mwenyewe, ili kumwandalia yule msafiri aliyemfikilia, bali alimnyang’anya yule maskini mwana-kondoo wake, akamwandalia yule mtu aliyemfikilia.
5 Ndipo hasira ya Daudi ikawaka sana juu ya mtu yule; akamwambia Nathani, Aishivyo Bwana, mtu huyo aliyetenda jambo hili, hakika yake astahili kufa;
6 naye atamrudishia yule mwana-kondoo mara nne, kwa sababu ametenda neno hili, na kwa sababu hakuwa na huruma.
7 Basi Nathani akamwambia Daudi, Wewe ndiwe mtu huyo. Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi, Nalikutia mafuta, uwe mfalme juu ya Israeli, nikakuokoa na mkono wa Sauli;
8 nami nikakupa nyumba ya bwana wako, na wake za bwana wako kifuani mwako; nikakupa nyumba ya Israeli na ya Yuda; na kama hayo yangalikuwa machache, ningalikuongezea mambo kadha wa kadha.
9 Kwa nini umelidharau neno la Bwana, na kufanya yaliyo mabaya machoni pake? Umempiga Uria, Mhiti, kwa upanga, nawe umemtwaa mkewe awe mke wako, nawe umemwua huyo kwa upanga wa wana wa Amoni.
10 Basi, sasa upanga hautaondoka nyumbani mwako, kwa sababu umenidharau, ukamtwaa mkewe Uria, Mhiti, kuwa mke wako.
11 Bwana asema hivi, Angalia, nitakuondokeshea uovu katika nyumba yako, nami nitawatwaa wake zako mbele ya macho yako, na kumpa jirani yako, naye atalala na wake zako mbele ya jua hili.
12 Maana wewe ulifanya jambo lile kwa siri; bali mimi nitalifanya jambo hili mbele ya Israeli wote na mbele ya jua”.
Na sehemu nyingine nyingi katika biblia, agano la kale na agano jipya utaona Mungu anazungumza kwa mifano kufikisha ujumbe wake au hisia zake kwa watu wake.
Lakini pia Mungu wetu anatumia mifano kutuonyesha hisia zake pindi tunapotubu na kumgeukia yeye… Wengi wetu hatujui ni jinsi gani Mungu anavyohisi juu yetu, na anavyotuhurumia, hususani pale tunapoghairi maovu yetu na mabaya yetu na kugeukia haki, wengi tunadhani Mungu huwa hasamehi, na anakumbuka kumbuka makosa yetu mara kwa mara…Hebu chukua muda tafakari ule mfano wa mwana mpotevu, Bwana alioutoa katika Luka 15:11-32, utaona jinsi gani Huruma za Mungu jinsi zilivyo kuu kwetu pindi tunapotubu na kuacha maovu.
“Luka 15:20 Akaondoka, akaenda kwa babaye. Alipokuwa angali mbali, baba yake alimwona, akamwonea huruma, akaenda mbio akamwangukia shingoni, akambusu sana.
21 Yule mwana akamwambia, Baba, nimekosa juu ya mbingu na mbele yako; sistahili kuitwa mwana wako tena.
22 Lakini baba aliwaambia watumwa wake, Lileteni upesi vazi lililo bora, mkamvike; mtieni na pete kidoleni, na viatu miguuni;
23 mleteni ndama yule aliyenona mkamchinje; nasi tule na kufurahi;
24 kwa kuwa huyu mwanangu alikuwa amekufa, naye amefufuka; alikuwa amepotea, naye ameonekana. Wakaanza kushangilia.”
Vilevile Sio mifano tu, hata katika ishara Mungu anazungumza na watu wake, kasome kitabu cha Ezekieli mlango wa 4 na wa 5 na Isaya 20:3.
Sasa hebu tuitazame ishara ya mwisho ambao tutazidi kufahamu hisia ya Mungu juu yetu pindi tunapogeuka na kutubu.
Kama wewe ni msomi wa biblia utakuwa unaijua vizuri habari ile ya Nabii Yona, jinsi alivyoikimbia sauti ya Mungu na mwishowe kujikuta yupo katika tumbo la nyangumi siku tatu, na baadaye kulazimika kuitii sauti ya Mungu na kwenda kuwahubiria watu wa Ninawi..Na alipowahubiria biblia inasema walitubu na kuacha njia zao mbaya..Na kwa tendo lile Mungu aliwasamehe na kughairi kuwaangamiza…Lakini kitendo kile cha Mungu kuwasamehe hakikumpendeza Nabii Yona, kwani alitafakari mateso aliyoyapitia yote na shida zote zile mpaka za kukaa tumboni mwa samaki siku tatu, na mwishowe Mungu hafanyi chochote?..yeye alitamani watu wauawe…Lakini hisia za Mungu hazikuwa hizo..yeye aliwahurumia watu wake, lakini Yona hakujua ukubwa wa huruma na hisia za Mungu juu ya watu wa Ninawi mpaka Mungu alipozungumza naye tena kwa ishara nyingine ya Mtango.
Kwani alipokuwa amekaa kwa mbali autazame mji ukiangamizwa, Mungu aliuotesha mtango ambao uliota ndani ya siku moja, ukawa na matawi yenye uvuli, na kwasababu jua lilikuwa kali na Yona alikuwa na hasira na uchungu.. alipouona ule mtango akaenda kukaa chini yake, apate kivuli, na pengine pia ale matango mawili matatu asahahu shida zake, na alipozidiwa na burudani za mtango ule siku nzima, akasahau habari za Ninawi na kuangamizwa kwake.
Lakini biblia inasema siku ya pili yake alivyoamka mambo yalibadilika, ule mtango uliliwa na buu na jua ukaupiga ukakauka, Yona kuona vile akakasirika tena..Hasira yake ikarudi kama mwanzo..kwanini mtango umekauka ambao ndio uliokuwa unamfanya asahau shida zake na apunguze hasira zake.
Kwa tukio hilo Mungu akampa somo Yona…kama vile ule mtango ulivyomfanya asahau shida zake na hasira zake kwa uvuli tu wa matawi yake, pengine na kwa matunda yake yaliyouzaa ndani ya siku moja, na ukamfanya pia auhurumie ule mtango..(Yona 4)
Ni hivyo hivyo watu wa Ninawi kwa kutubu kwao ni kama mtango ulioota juu ya kichwa cha Mungu, ambapo hapo kwanza Mungu aliwakasirikia watu wa Ninawi kwa maovu yao, lakini walipotubu na kuacha njia zao mbaya ni kama mtango ulioota juu ya kichwa cha Mungu, ukampa utulivu ndani ya moyo wake, na kumfanya asahau na kughairi mabaya aliyopanga kuwaletea watu wa Ninawi.
Hivyo kila siku tunapoghairi mabaya yetu, ndipo matawi yetu mbele za Mungu wetu yanavyoongezeka, na tunapozidi na kuzidi kuwa wasafi na hata kufikia hatua ya kuzaa matunda ndipo tunapomfanya Mungu wetu aburudike na kusahau mabaya yetu yote…Lakini tunapozidisha uovu, ni tunayapunguza wenyewe matawi yetu na hivyo dhambi zetu zinafika kwake na kumghadhibisha…
Hivyo Mungu wetu anatupenda na kutuhurumia…kuna uhusiano mkubwa sana wa matendo yetu na hisia za Mungu wetu..hivyo tujitahidi kuupendeza moyo wake ndipo tutakapata mema…kila siku tujisafishe, kama tulikuwa tumeacha matusi lakini bado vitabia vidogo vidogo vya ugomvi, vinatutawala tuvisafishe na hivyo..ndivyo tunavyozidi kujiepusha na hasira ya Mungu.
Mungu wetu anatupenda, Mungu wetu anatuhurumia na bado tunayo nafasi kubwa kwake.
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
BASI TUENDELEE KUMJUA MUNGU,NAYE ATATUJILIA KAMA MVUA YA VULI.
Zile mbao mbili za mawe Musa alizoambiwa achonge zilikuwaje?
Shalom.
Waefeso 6:12 “Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho”.
Biblia inatuambia biblia inatumia Neno “majeshi” ikimaanisha ni mengi na pia yapo makundi makundi, na inatumia pia neno “wabaya”.Ikimaanisha wanafanya kazi mbaya..
Sasa kabla ya kufahamu ni kwa namna gani yanafanya kazi, ni vizuri kwanza kujua Malaika watakatifu huwa wanafanya kazi gani kwa wanadamu. Kwasababu mapepo hapo kabla ya kuasi walikuwa ni malaika,hivyo baada ya kulaaniwa ndipo yakawa mapepo, na baadhi yao yakatupwa duniani, mengine yakapelekwa kwenye vifungo vya giza (2Petro 2:4),..Sasa haya yaliyopo duniani, hayafanyi kazi nyingine, Zaidi ya kuzitazama zile kazi za malaika watakatifu na kwenda kinyume nazo basi..
Ni mara chache sana mapepo yakitaka kumshambulia mtu, yanakwenda moja moja, huwa yanakwenda kama jeshi, yakisaidiana, kwasababu mbinu hiyo yaliwaiga malaika watakatifu..
Soma Habari za Elisha jinsi yule mtumishi wake, alivyofunguliwa macho na kuona majeshi ya malaika watakatifu yamewazunguka..
Utagundua pia na mapepo nayo yanafanya hivyo hivyo, utaona yule mtu aliyekuwa kule mlimani, uchi, Bwana alipoyaulizwa jina lao, yakasema, Legioni, maana yake tupo wengi (jeshi).
Hivyo ni vizuri kujua kazi ya malaika watakatifu duniani..Nao kazi yao kuu ni hii..KUWAHUDUMIA WATAKATIFU.
Hivyo, mapepo sikuzote ni kunyume na malaika..
Sasa kazi kuu ya malaika watakatifu duniani kama tulivyosema, si nyingine Zaidi ya KUWAHUDUMIA WATAKATIFU..Soma..
Waebrania 1:13 “ Je! Yuko malaika aliyemwambia wakati wo wote, Uketi mkono wangu wa kuume Hata nitakapoweka adui zako chini ya nyayo zako?
14 Je! Hao wote si roho watumikao, wakitumwa kuwahudumu wale watakaourithi wokovu?”
Unaweza kuona hapo malaika watakatifu hawajaagizwa kuwahudumia kila mtu tu duniani, isipokuwa wale watakatifu..kumbuka huduma, ni utumishi, malaika hawawatumikii watu waovu, bali watakatifu tu..
Sasa mapepo haya, kwasababu lengo lao sikuzote ni kwenda kinyume na malaika wa Mungu, nao pia wanafanya kazi ya kihuduma ya kuwaharibu watakatifu..na si watu wengine waovu kwasababu hao tayari walishapotea zamani..Mtu mwovu hashambuliwi na mapepo bali anatumiwa na mapepo kufanya kazi zao.
Hivyo ukiokoka leo, majeshi ya mapepo wabaya yanaanza huduma ya kutafuta njia ya kukuangusha uache wokovu. Hiyo ndiyo agenda yao ya kwanza…Hivyo ni vizuri ukajua namna ya kuyadhibiti, ili wokovu wao uwe na matunda na udumu.
Mambo ya kufanya unapooka ni lazima uwe mtu wa.
1) KUSALI: Bwana anasema..
Mathayo 2:41 “Kesheni, mwombe, msije mkaingia majaribuni; roho i radhi, lakini mwili ni dhaifu”. Hakuna namna unaweza kuzidhibiti/kuyashinda hizo roho kama si mtu wa maombi…
2) KUJIEPUSHA NA UOVU: Maovu, yanauficha uso wa Mungu, Hivyo inapelekea pia na malaika wa Bwana kuondoka, matokeo yake ulinzi wa Mungu unaondoka juu yako, na mapepo yanachukua nafasi ya kukuangusha.(Isaya 59:1-2 )
3) KUJIFUNZA NENO: Neno la Mungu likikaa kwa wingi ndani yako unakuwa na maarifa ya kutosha ya kumshinda ibilisi (Wakolosai 3:16). Kumbuka Kristo alimshinda shetani kwasababu Neno la Mungu lilikuwa kwa wingi ndani yake.
4) KUFANYA USHIRIKA NA WENGINE: Kukutanika na wengine, kanisani, kwenye vikundi vya maombi, kwasababu ukiwa peke yako upo hatarini shetani kukupindua lakini mkiwa wengi, ni ngumu ibilisi kukupata..(Waebrania 10:25).
Mhubiri 4:11 “Tena, wawili wakilala pamoja, hapo watapata moto; lakini mmoja aliye peke yake tu awezaje kuona moto?
12 Hata ikiwa mtu aweza kumshinda yule aliye peke yake, wawili watampinga; wala kamba ya nyuzi tatu haikatiki upesi”.
Hayo ni mambo makuu yatakayokusaidia kujikinga na majeshi haya, na kuyakaribisha majeshi ya Malaika wa Mungu yatembee nawe.
Kumbuka shetani Pamoja na malaika zake( yaani mapepo), wanafahamu kuwa muda wao ni mchache sana. Hivyo wanaongeza bidii katika kufanya kazi ya kuwaangusha watakatifu.
Sasa endapo mtu asipojibidiisha, na kukaa kuendelea na Maisha ya kawaida ya siku zote, baada ya kuokoka , ni ngumu mtu huyo kushindana na hayo majeshi ya mapepo, Utarudi tu nyuma kama sio kuucha wokovu kabisa.
Hivyo tuongeze bidii, na kuzingatia hivyo vigezo.
Ubarikiwe.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
Kuna nguvu katika mzaliwa wa pili.
Shalom, jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe,
Biblia inasema Israeli ni Mzaliwa wa kwanza wa Mungu..
Kutoka 4: 22 “Nawe umwambie Farao, Bwana asema hivi, Israeli ni MWANANGU MIMI, MZALIWA WA KWANZA WANGU;
23 nami nimekuambia, Mpe mwanangu ruhusa aende, ili apate kunitumikia, nawe umekataa kumpa ruhusa aende; angalia basi, mimi nitamwua mwanao, mzaliwa wa kwanza wako”.
Kama kuna mzaliwa wa kwanza maana yake kuna mzaliwa wa pili..Na kama vile mzaliwa wa kwanza hapo biblia imelitaja ni Taifa la Israeli..maana yake mzaliwa wa pili ni mataifa mengine yaliyosalia…Na hiyo ni sababu Taifa la Israeli ndio limekuwa la kwanza kushiriki Baraka za Mungu kabla ya sisi watu wa mataifa…Sababu pekee ndio hiyo, kwamba lenyewe ndio mzaliwa wa kwanza, kumjua Mungu.
Itakuwa ni ajabu watoto wa mwisho katika familia wanakuja juu na kuanza kumlaumu mzazi wao kwanini kaka yao amekuwa wa kwanza kunyonya kabla yao?, na kwanini wamerithi nguo za kaka yao na viatu vyake, lakini kaka yao hakurithi vyao? N.k Ukiona mtoto ananung’unika kwa ajili ya hayo basi kuna uwezekano akili yake haijakomaa vizuri…kwasababu kama ingekuwa imekomaa vizuri ingekuwa ni rahisi sana kujua ni kwanini kaka yake kamtangulia kwa kila kitu….angejua ni kwasababu kaka yake ndio kazaliwa wa kwanza na kisha yeye ndio akafuata…hiyo ndio sababu ya kipekee na hakuna nyingine.
Halikadhalika leo hii tutauliza ni kwanini Mungu aliwachagua kwanza Israeli na kuwapa upendeleo ?..Jibu ndio hilo hapo juu la Kutoka 4:22 kwamba Israeli ni MZALIWA WA KWANZA. Hivyo hana budi kunyonya baraka za Mungu kabla yetu, hana budi kuvivaa viatu vipya, na sisi watu wa mataifa tutakapozaliwa baadaye tutavirithi vile vile viatu..Ndio maana tunatumia kitabu cha biblia agano la kale ambalo limejaa Maisha ya Wana wa Israeli tu ili kujifunzia njia za Mungu.
Lakini ipo siri nyingine kubwa juu yetu sisi watu wa mataifa, ambao hatukuchaguliwa kuwa wazao wa kwanza. Na siri hiyo ipo katika msalaba.
Kwa kupitia Yesu Kristo, sisi watu wa mataifa, wakati wetu ulipofika wa kuzaliwa tulipata baraka mara dufu Zaidi ya wana wa Israeli. Bwana Yesu alitufanya sisi ambao hapo kwanza tulionekana kuwa sio warithi,..akatufanya kuwa warithi..Kwasababu urithi siku zote ulimhusu mzaliwa wa kwanza tu.
Waefeso 2:12 “kwamba zamani zile mlikuwa hamna Kristo, mmefarakana na jamii ya Israeli, wageni wasio wa maagano ya ahadi ile. Mlikuwa hamna tumaini, hamna Mungu duniani.
13 Lakini sasa, katika Kristo Yesu, ninyi mliokuwa mbali hapo kwanza mmekuwa karibu kwa damu yake Kristo.
14 Kwa maana yeye ndiye amani yetu, aliyetufanya sisi sote tuliokuwa wawili kuwa mmoja; akakibomoa kiambaza cha kati kilichotutenga”.
Umeona ni Neema ya namna gani hiyo?..Mimi na wewe hatukustahili kuitwa warithi, waliostahili kuitwa warithi ni jamii ya Wana wa Israeli peke yao, kwasababu wao ndio wazaliwa wa kwanza, lakini sasa sisi watu wa mataifa ni warithi kupitia msalaba wa Yesu Kristo…
Yakobo ulipofika wakati wa kuwabariki wana wa Yusufu, ambapo alitakiwa mkono wa kuume auweke juu ya mzaliwa wa kwanza na ule wa kushoto juu ya mzaliwa wa pili, kinyume chake mikono yake aliipishanisha kama ishara ya msalaba na ule wa kushoto akauweka juu mzaliwa wa kwanza na wa kuume juu ya mzaliwa wa pili(Mwanzo 48:8-17). Siri hiyo ni kubwa sana.
Tendo hilo lilikuwa ni ufunuo wa msalaba, kupitia msalaba Baba yetu wa mbinguni alitubariki sisi tuliokuwa wa uzao wa pili, baraka ambazo zingestahili kupokewa kwa mzao wa kwanza yaani wana wa Israeli. Ni neema kubwa sana tuliyopewa, ambayo hatupaswi kuipuuza hata kidogo..
Je bado unaupuuza msalaba?..je bado upo bize kutafuta fursa za fedha kuliko kutafuta kujua siri zilizopo katika msalaba?..Kumbuka urithi ambao wana wa Mungu wameahidiwa ni mbingu mpya na nchi mpya…Katika mbingu hiyo na nchi hiyo, hakuna kuumwa, hakuna kuteseka, hakuna dhiki, hakuna njaa..hakuna mwanzo wa siku wala mwisho..Milele na milele Watoto wa Mungu watang’aa na kuishi bila tabu wala dhiki, wala majuto..kwa ufupi biblia inasema kuna mambo ambayo jicho halijawahi kuona wala sikio kusikia tuliyoandaliwa.
Ni maombi yangu kuwa injili ya msalaba haitakuwa upuuzi kwetu..Kabla Biblia inavyosema katika..1Wakorintho 1:18 “Kwa sababu neno la msalaba kwao wanaopotea ni upuzi, bali kwetu sisi tunaookolewa ni nguvu ya Mungu”.
Kama hujaokolewa leo ni siku yako..huu sio wakati wa kutanga tanga na kushabikia udhehebu au udini uliokuwa nao..Kumpa Yesu Maisha yako sio dini mpya wala dhehebu jipya..ni Neno la Mungu..Hii neema ya msalaba tuliyoipokea ya kufanyika warithi haitadumu milele, ipo siku itaisha, na Neema hii inatufundisha kuukataa ubaya…maana yake ni kwamba ukiwa mwasherati, mzinzi, mwizi, mlevi, mtukanaji, mtoaji mimba, msagaji na mambo mengine yote yanayofanana na hayo yasiyompendeza Mungu, bado hujaingia katika neema hii, hivyo unahitaji kuingia katika Neema hii..
Kama upo tayari kufanya hivyo leo..basi uamuzi unaoufanya ni wa busara, unachopaswa kufanya hapo ulipo ni kujitenga dakika kadhaa peke yako na kuomba rehema mbele za Mungu kwa yote uliyoyafanya yasiyompendeza yeye…na dhamiria kutoyafanya tena kwa vitendo, tubia kwa dhati kabisa uasherati wako na usiufanye tena, usagaji wako, utoaji mimba uliokuwa unatenda, ukahaba, uvaaji nusu uchi kikahaba, wizi, utukanaji na mambo mengine yote ya siri..Na Bwana atakusamehe kwasababu yeye ni mwenye huruma na mwingi wa rehema, endapo umedhamiria kweli kwa dhati kuacha hayo matendo maovu uliyokuwa unayafanya.
Baada ya hapo, usikawie haraka sana katafute ubatizo sahihi kama hujabatizwa…kipengele hichi ni cha muhimu sana..Ingekuwa ni mimi mwanadamu natoa maagizo ya kupokea wokovu ningekiruka labda pengine kisingekuwa na maana sana kwangu, lakini sivyo kwa Mungu, kitendo hichi cha ubatizo kina maana sana kwake..hivyo akaagiza kwamba kila aaminiye ni lazima akabatizwe, hata mimi linalihusu agizo hili, hata mchungaji yoyote yule, hata Paulo lilimhusu, zaidi sana Bwana wetu yeye mwenyewe alikuwa kielelezo alikwenda kubatizwa..Hivyo hatupaswi kupuuza hata kidogo, nenda kabatizwe katika ubatizo sahihi wa maji tele na kwa jina la Yesu Kristo, ambalo ndio jina la Baba, Mwana na Roho Mtakatifu, ikiwa kweli umemaanisha kutubu na kumwishia Kristo, ukiona jambo hilo ni mizigo kwako, ni wazi kuwa bado hujatubu kwa kumaanisha..Lakini ukizingatia hilo Bwana atakupokea kabisa na Roho Mtakatifu atakuongoza kufanya yaliyosalia.
Na hapo utakuwa umekamilisha wokovu wako na kuzaliwa mara ya pili kulingana na maandiko.Kumbuka tunaishi katika siku za mwisho na majuto makuu yanakaribia kuja ulimwenguni kote kwa wale wote watakaomkataa Kristo. Bwana atusaidie mimi na wewe tusiwe miongoni mwao. Hizi ni nyakati za mwisho kweli kweli, wala si mzaha..
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
Kuna watu wawili ambao tunaweza kujifunza leo katika ile safari ya Bwana Yesu kuelekea Yeriko, Biblia inatuambia kulikuwa na mkutano mkubwa wa watu waliokuwa wakimfuata, kumbuka wote hao kila mmoja alikuwa anatamani Yesu amuhudumie binafsi, walikuwa ni watu wenye matatizo mbalimbali, wengine matatizo ya familia zao, wengine biashara, wengine magonjwa, wengine walimfuata kwa lengo tu la kumwona Yesu n.k.
Sasa katikati ya umati mkubwa wote huo wa watu, waliokuwa wanataka kuhudumiwa, Bwana alikutana na watu wawili wa kipekee..
Mtu wa kwanza:
Alikuwa ni Yule maskini kipofu..tusome habari yake:
Luka 18:35 “Ikawa alipokaribia Yeriko, mtu mmoja kipofu alikuwa ameketi kando ya njia, akiomba sadaka;
36 na alipowasikia makutano wakipita, aliuliza, Kuna nini?
37 Wakamwambia, Yesu wa Nazareti anapita.
38 Akapiga kelele, akisema, Yesu, Mwana wa Daudi, unirehemu.
39 Basi wale waliotangulia wakamkemea ili anyamaze; lakini yeye alizidi sana kupaza sauti, Ee Mwana wa Daudi, unirehemu.
40 Yesu akasimama, akaamuru aletwe kwake; na alipomkaribia, alimwuliza,
41 Wataka nikufanyie nini? Akasema, Bwana, nipate kuona.
42 Yesu akamwambia, Upewe kuona; imani yako imekuponya.
43 Mara hiyo akapata kuona, akamfuata, huku akimtukuza Mungu. Na watu wote walipoona hayo walimsifu Mungu”.
TAFAKARI: Huyu alikuwa ni kipofu, haoni, wala hakuwa na namna yoyote ile ya kumfikia Kristo ili ahudumiwe, lakini alikuwa wa kwanza kuhudumiwa na kumwona Kristo kwa karibu kuliko watu wote waliokuwa wanamfuata YESU tangu mbali, watu wenye macho, na wenye miguu, na wenye masikio, hata mmoja hakumteka YESU.
Mtu wa PILI:
Alikuwa ni Zakayo; Huyu alikuwa ni tajiri, lakini alifahamu utajiri wake usingemsaidia kumwona Yesu, licha tu ya kumkaribia..Na alipojaribu kupitia kutumia nguvu, walau kupiga vikumbo ili amwone tu Yesu, bado ilishindwa kutokana na ufupi wake.. Hivyo kwa namna ya kawaida kama kukata tamaa angepaswa awe ameshakataa tamaa siku nyingi..lakini turudie kusoma tena..
Luka 19:1 “Naye alipoingia Yeriko alipita katikati yake.
2 Na tazama, palikuwa na mtu, jina lake Zakayo, mkubwa mmoja katika watoza ushuru, naye ni tajiri.
3 Huyu alikuwa akitafuta kumwona Yesu ni mtu wa namna gani, asiweze kwa sababu ya umati wa watu, maana ni mfupi wa kimo.
4 Akatangulia mbio, akapanda juu ya mkuyu apate kumwona, kwa kuwa atakuja kuipitia njia ile.
5 Na Yesu, alipofika mahali pale, alitazama juu, akamwambia, Zakayo, shuka upesi, kwa kuwa leo imenipasa kushinda nyumbani mwako.
6 Akafanya haraka, akashuka, akamkaribisha kwa furaha”.
Kama tunavyosoma, alikwenda mbele akapanda juu ya mkuyu. Na Yesu alipopita alikuwa wa kwanza kumwona, na kumwita, akawashinda hata watu wengi ambao walikuwa warefu, wenye mbavu, wepesi..
Jambo gani tunaweza kujifunza:
Watu wengi tunafikiri madhaifu yetu ndio kikwazo cha sisi kutomkaribia Mungu, au kutokuwa watumishi wa Mungu..Tunaishia kusema, Ahh! Yule si ni kwasababu amezaliwa katika familia ya kikristo, au Yule si ni kwasababu anayo pesa ya kutosha kuendesha huduma, au Yule si ni kwasababu anayo miguu miwili ya kuhubiri injili..Au Yule si ni kwasababu ni kijana, au mtu mzima n.k.
Tunavisingizio vingi lakini hatujui, watu wanaonekana haiwezekani kumfikia Yesu kwa madhaifu yao,ndio wanaokuwa wa kwanza kufaidika na yeye, kama hawatakata tamaa katika kumtafuta kwa bidii katika hali zao hizo hizo.
Utashangaa siku moja Bwana anamfanya kuwa mchungaji, au mwinjilisti, wa jamii kubwa ya watu ambao tangu zamani walikuwa wanajiita ni wakristo.. lakini yeye hakuwa hata na dalili za kuwa mkristo, katokea katika jamii wa waabudu miti, au wachawi.
Hivyo katika hali uliyonayo ambayo pengine inakufanya ujione ni kikwazo cha wewe kumfikia Mungu, hupaswi kuvunjika moyo endelea kupaza sauti kwa Bwana, panda kabisa juu ya mkuyu mtafute Bwana kwa bidii, usiwaangalie waliokutangulia katika imani, wewe fanya kwa nafasi yako. Utashangaa tu wakati utafika utakuwa wa kwanza kuhudumiwa na Kristo, zaidi ya hao unaodhani wanamjua Mungu tangu zamani.
Sasa mambo hayo hayawezekani kama hujaokoka. Hivyo kama upo nje ya Kristo, huu ndio wakati wako wa kumkaribisha mwokozi moyoni mwako, Hivyo tubu kwa kumaanisha dhambi zako, kisha ukabatizwe, kisha Bwana atakupa Roho Mtakatifu, na kuanzia huo wakati na kuendelea, Kristo ataelekeza macho yake kukutazama wewe kwanza.
Ubarikiwe.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
Bwana Yesu alimaanisha nini aliposema; Mafarisayo Hupanua HIRIZI zao, na kuongeza MATAMVUA yao?
Shalom, Jina kuu la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe, karibu tujifunze Neno la Mungu..Ni muhimu kila mmoja wetu kuzaliwa mara ya pili na kupokea kipawa cha Roho Mtakatifu, na kazi ya Roho Mtakatifu ni kutufanya sisi kuwa watakatifu kama Baba yetu wa mbinguni alivyo mtakatifu..(1Petro 1:16).
Na kazi nyingine ya Roho Mtakatifu juu yetu ni kututumia sisi kuwavuta wengine kwa Kristo, na anaposhuka juu ya mtu anampa kipawa au karama…Karama hiyo ndiyo inayomtofautisha yeye na watu wengine..Haiwezekani watu wawili wakawa wanafanana asilimia mia..wanaweza kukaribiana huduma au karama lakini wasifanane asilimia mia. Hivyo ni muhimu sana kutojilinganisha na mwingine, wala kutotamani kuwa kama mwingine..
Kwamfano hebu tuichunguze karama ya kinabii kwa kujifunza juu ya manabii wa Bwana waliowahi kupita katika agano la kale….Tujifunze juu ya hawa manabii watatu MUSA, DANIELI na ISAYA.
Hawa watatu walikuwa ni manabii wa Bwana…na biblia inawaita wote ni manabii lakini kama ukichunguza kwa makini utaona kila mmoja alikuwa ni nabii kwa namna yake.
Tukianza na Musa, huyu hakuwa anaona maono ya siku za Mwisho, hakuwa anaona mambo yatakayokuja kutokea katika siku za mwisho kama vile siku ya Bwana, au hukumu ya mwisho wa dunia, hukumu ya wanadamu n.k Lakini Roho wa Mungu ajimtia mafuta mahususi kumfunulia torati, sheria ya Mungu, sheria za makuhani, na kumfahamisha yale yaliyotokea zamani..na alimtia mafuta kuwa kiongozi wa Taifa teule la Mungu, kuwatoa utumwani Misri na kuwapeleka nchi ya ahadi kaanani.
Lakini tukimtazama Nabii Danieli, huyu hakuwa anatembea na Mungu kama Musa…Musa alikuwa anaonana na Mungu uso kwa uso lakini Danieli hakuwa hivyo… Mungu alikuwa anamwonyesha Danieli mambo yatakayokuja kutokea siku za mwisho, kama kunyanyuka kwa mpinga Kristo, kunyanyuka kwa falme zitakazokuja kutawala dunia, kusimamishwa kwa chukizo la uharibifu na kujengwa kwa hekalu..mambo ambayo Musa pamoja na uhusiano wake wote na Mungu hakuonyeshwa.
Hali kadhalika tukirudi kwa Nabii Isaya…Huyu naye hakuwa kama Musa wala Danieli…Huyu Bwana Mungu alimwonyesha zaidi mambo yajayo ambayo yatatokea baada ya mwisho wa dunia, alionyeshwa mambo yatakayotokea wakati wa utawala wa miaka 1000, alionyeshwa zaidi unabii kuhusu Ujio wa Bwana Yesu na kuzaliwa kwake kwa uwazi zaidi kuliko manabii wengine wowote..Kabla ya Nabii Isaya hakukuwa na nabii yoyote aliyejua kuwa Masihi atazaliwa na bikiri, au Bwana Yesu atasulubiwa na kuchinjwa kama mwana kondoo, wala hakuna aliyejua kwamba Masihi atapigwa kwaajili ya dhambi zetu hata Nabii Musa hakuwa analijua hilo..japokuwa alikuwa anauuona uso wa Mungu.
Hatuna muda wa kutosha wa kumwangalia Nabii Yohana Mbatizaji jinsi Roho Mtakatifu alivyomtumia tofauti na manabii wengine wote, hatujamtazama Nabii Ezekieli na Hosea jinsi Mungu alivyowatumia kama ishara..hawa walikuwa wanaambiwa waoe wake wa kizinzi, wengine wale kinyesi, wengine walala upande mmoja kwa siku nyingi..Hatujamtazama Eliya na Elisha jinsi Mungu alivyowatumia kitofauti na manabii wengine.
Eliya hakutoa unabii wowote kuhusu ujio wa Masihi, wala mwisho wa dunia lakini alitabiri mambo yaliyokuwa yanatokea papo kwa hapo..na zaidi ya yote kwa ishara na maajabu mengi..
Sasa manabii wote tuliowatazama hapo juu Biblia inawaita MANABII WA BWANA…Lakini wote hawakuwa wanafanana…Na ndio hivyo hivyo kwa Wachungaji, wainjilisti, waalimu, mitume, waimbaji, wenye karama ya Imani, wenye karama za masaidiano, wenye karama za neno la hekima na maarifa n.k… Wote hawafanani.
1Wakorintho 12:4 “Basi pana tofauti za karama; bali Roho ni yeye yule.
5 Tena pana tofauti za huduma, na Bwana ni yeye yule.
6 Kisha pana tofauti za kutenda kazi, bali Mungu ni yeye yule azitendaye kazi zote katika wote.
7 Lakini kila mmoja hupewa ufunuo wa Roho kwa kufaidiana”.
Hivyo tunajifunza ni muhimu kukaa kila mtu katika nafasi yake..kwasababu kamwe hatuwezi kufanana..Katika karama moja kuna utendaji kazi hata elfu moja tofauti tofauti…
Sasa tatizo linakuja ni mtu kutamani kuwa kama mwingine, …Unapotamani kuwa kama mwingine vilevile, ni uthibitisho tosha wa kuiua karama iliyopo ndani yako, Kwasababu kamwe hatuwezi kufanana..hata wale mapacha wanaofanana sana ukizidi kuwachunguza utaona wanao tofauti..na unavyozidi kukaa nao ndio kabisa utaona wanatofautiana sana…hiyo ikionyesha kwamba katika nafasi zetu sisi wanadamu Mungu hajawahi kutuumba tukafanana asilimia mia kama vile sisimizi wanavyofanana..
Hivyo karama Mungu aliyoiweka ndani yako ni ya kipekee tofauti na ya mwingine, na Roho ameiweka ndani yako kwa makusudi yake ya kuwavuta wengine kwake. Hivyo tembea katika kile Mungu alichokiweka ndani yako.
Bwana atusaidie sana kuzifahamu na kuzithibitisha karama zetu ili tusimzimishe Roho ndani yetu…
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Maran atha!
Mada Nyinginezo:
Je! Ule mwiba uliokuwa katika mwili wa Paulo ulikuwa ni nini?
Je ni kweli huwezi kuijua karama yako mpaka uwekewe mikono na wazee?
USIPOWATAMBUA YANE NA YAMBRE, KATIKA KANISA LA KRISTO, UJUE UMEPOTEA.
JIBU: Tusome
2Wakorintho 12:7 “Na makusudi nisipate kujivuna kupita kiasi, kwa wingi wa mafunuo hayo nalipewa mwiba katika mwili, mjumbe wa Shetani ili anipige, nisije nikajivuna kupita kiasi.
8 Kwa ajili ya kitu hicho nalimsihi Bwana mara tatu kwamba kinitoke.
9 Naye akaniambia, Neema yangu yakutosha; maana uweza wangu hutimilika katika udhaifu.”
Kumekuwa na mtazamo mingi juu ya mwiba uliokuwa katika mwili wa Paulo, wengine wanabaki kudhani ni mwiba halisi kabisa uliwekwa ubavuni mwake, kwamba kila anapojaribu kujivuna basi unamtoboa..wengine wanasema ni kumbukumbu ya yale mambo mabaya aliyoyafanya kule nyuma hivyo Mungu alikuwa anamletea yale mawazo yanamsononesha na hivyo yanageuka kuwa kama mwiba kwake na anaacha kujivuna.
Lakini, katika hayo yote, tukiutazama tena kwa ukaribu ule mstari wa 7, unasema Mungu alimwekea mwiba katika mwili wake “Mjumbe wa shetani”..Hilo Neno mjumbe, ni Neno linalomaanisha mtu na sio mawazo fulani au kitu fulani. Hata katika akili ya kawaida mwiba wa kijiti una uhusiano gani na kujisifu?..Hivyo hapo Paulo hakuzungumzia kijiti cha mwiba au ugonjwa fulani katika mwili wake bali alikuwa anamzungumzia mtu fulani, ambaye ndiy aliyekuwa kama mwiba kwake…
Sasa swali lingine utauliza mbona kasema ni katika mwili na sio katika roho?..Jibu ni kwamba Neno mwili linaweza kumaanisha maisha ya mtu au watu…Hebu soma mistari ifuatayo Bwana aliyokuwa anawaambia wana wa Israeli tutazidi kuelewa..
Hesabu 33: 55 “Lakini kama hamtaki kuwafukuza wenyeji wa nchi watoke mbele yenu; ndipo hao ambao mtakaowasaza watakuwa kama sindano machoni mwenu, na kama miiba ubavuni mwenu, nao watawasumbua katika hiyo nchi ambayo mwakaa.
56 Kisha itakuwa, kama nilivyoazimia kuwatenda wao, ndivyo nitakavyowatenda ninyi”.
Waamuzi 2: 3 “Basi kwa ajili ya hayo mimi nilisema zaidi, Mimi sitawafukuza watoke mbele zenu; lakini watakuwa kama miiba mbavuni mwenu, na miungu yao itakuwa ni tanzi kwenu”.
Umeona hapo?..maisha ya mtu yanaweza kufananishwa na mwili, na mtu anayekusumbua na kukutesa katika maisha yako anaweza kufananishwa na mwiba mwilini mwako…
Lakini tukirudi kwa Mtume Paulo, huyu mtu ambaye alikuwa ni mwiba kwake alikuwa ni nani?
Tukisoma.. 2Timotheo 4:14 inasema..
“Iskanda, mfua shaba, alionyesha ubaya mwingi kwangu; Bwana atamlipa sawasawa na matendo yake.
15 Nawe ujihadhari na huyo, kwa sababu aliyapinga sana maneno yetu.”.
Biblia haijatoa habari zake ndefu juu ya huyu Iskanda, mfua shaba. Lakini inatueleza alikuwa kikwazo kikubwa sana wa Paulo, katika maisha yake na katika huduma yake.. Hajiatumia neno “Ubaya ” tu bali imetumia neno “Ubaya mwingi”.Kuashiria ni matendo mengi mabaya huyu Iskanda alimwonyesha Paulo.
Pengine, alikuwa anamzungia Paulo kwa ubaya tu wakati wote, alikuwa anazungumzia mapungufu yake tu, jinsi alivyokuwa muuaji huko nyuma (akiwaua na kuwatesa wakristo), akimshuhudia na maneno mengine ya uongo mbele za watu waliokuwa wanamwamini Paulo..Na hiyo ikawa inamfanya Yule Paulo ambaye anasifika kwa mafunuo mengi, na miujiza mingi, na huduma kubwa, kuonekana kuwa sio kitu katikati ya baadhi ya watu waliokuwa wanamwamini.
Hilo si ajabu kuliona hata leo unaweza kuliona kwa viongozi wengi wa nchi, Mungu anawanyanyulia wapinzani kama mwiba kwao, ili wazungumze mabaya yao tu, au mapungufu yao, haijalishi kiongozi huyo atakuwa amefanya mambo mangapi mazuri ya kimaendeleo kiasi gani. Mungu anaruhusu hayo ili kiongozi huyo asijivune kupita kiasi.
Ndivyo ilivyokuwa kwa Paulo kwa huyu Iskanda mfua shaba alikuwa mwiba mkubwa kwake, mpaka akamwomba Mungu amwondolee (amwue),
Soma:
1Timotheo 1:20 “Katika hao wamo Himenayo na Iskanda, ambao nimempa Shetani watu hao, ili wafundishwe wasimtukane Mungu”.
lakini Mungu alimwambia Neema yake yamtosha..Hivyo aliendelea kubakia nao, mpaka wakati wake ulipokwisha.
Vivyo hivyo na sisi, tukiwa watu wa kujivuna, kujiona sisi ni kitu Fulani, kisa tumepiga hatua kuliko wengine, au tuna kitu kikubwa kuliko wengine. Tukumbuke kuwa Bwana anaweza kutunyanyulia miiba, kututweza..
Shalom.
jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP
Mada Nyinginezo:
MIILI YA UTUKUFU ITAKUWAJE?
IVUMBUE INJILI YA KRISTO KUTOKA KATIKA KILA JAMBO.
FAHAMU JINSI KRISTO ANAVYOPONYA WATU ROHO.
JE! TUNAPASWA KUUAMINI UNABII WA SYLVIA BROWNE?
Je kuweka mapambo kama mikufu, vikuku na kutoboa pua ni dhambi?
Je! habari ya Yusufu, inabeba ujumbe gani kwa agano jipya?
JE NI DHAMBI KUWA NA MAHUSIANO KABLA YA NDOA?
Je! kuna maombi yoyote ya kumtoa mtu aliyekufa kwenye mateso ya kuzimu?