Category Archive Home

SAA YA KUHARIBIWA IIJIAYO ULIMWENGU WOTE.

Saa ya kuharibiwa iliyo tayari kuujilia ulimwengu wote Inakuja..

Ufunuo 3:10 “Kwa kuwa umelishika neno la subira yangu, mimi nami nitakulinda, utoke katika saa ya kuharibiwa iliyo tayari kuujilia ulimwengu wote, kuwajaribu wakaao juu ya nchi”.

Kuna saa ya kuharibiwa inakuja huko mbeleni, ni wakati ambapo kila mtu kwa macho yake atakuwa anaona jinsi dunia inavyokwenda kuisha ndani ya kipindi kifupi sana, kutokana na dhiki, na mapigo, pamoja na mambo ya kutisha yatakayokuwa yanaendelea duniani wakati huo.. Kipindi hicho kitakuwa ni kifupi sana, kisichozidi miaka 7 tu. Na kitaanza muda mfupi tu baada ya unyakuo kupita.

Unyakuo ndio utakaokuwa kalenda ya kututambulisha kuwa dunia imebakisha umri wa miaka 7 tu. Na ndio maana itamgharimu Mungu awaondoe kwanza wale wateule wake watakatifu ambao walikuwa wanalishika Neno la Subira yake.. Watu ambao maisha yao yote, mawazo yao yote yalikuwa yanaelekea mbinguni tu, waliojikana nafsi, waliotengwa na ulimwengu, hao tu ndio Mungu atakaowanyakua ..Ili kupisha uharibifu huo kuchukua nafasi yake.

Kama tu vile alivyomwondoa Henoko, kwa kumnyakua asikutwe na gharika, …ndivyo itakavyokuwa kwa watu hao wachache sana, watanyakuliwa wasionekane duniani, kama vile alivyomtenga Ibrahamu akawa mbali na Sodoma na Gomora ndivyo itakavyokuwa kwa wale ambao wanaishi Maisha ya uaminifu sasa, wataondoshwa katika ulimwengu huu kabla ya siku ile ya uharibifu, na watakwenda kumlaki Bwana Yesu mawinguni na moja kwa moja safari ya kwenda kumwona Baba itaanzia hapo.

Lakini wale wengine ambao ni wakristo-vuguvugu, hawatakwenda popote, watakuwa mfano wa Nuhu wataishuhudia dhiki, wataingia katika misukosuko ya dhiki kuu na mateso makali ambayo biblia inasema haijawahi kuwepo tangu kuwekwa kwa misingi ya ulimwengu, kama vile Nuhu alivyokuwa katika dhiki ndani ya Safina..Kama vile Lutu alivyokuwa anapitia dhiki ile ya misukosuko sodoma ya Gomora ilivyokuwa inachomwa, siku zake zote alikuwa ni mbioni tu,..ndivyo itakavyokuwa kundi hilo kubwa la wakristo wanaosema wameokoka lakini Maisha yao hayana ushuhuda wowote hawaishi kama watu wanaomngojea Bwana wao. Dhiki hiyo itakuwa ni sehemu ya Maisha yao. Mpinga-kristo atawawinda huku na huko kama kuku..

Ndugu biblia inavyosema DHIKI basi ujue ni dhiki kweli kweli ,licha tu ile ya mpinga-kristo yatakuwepo pia mapigo mengine ya Mungu kwa wale watakaoipokea chapa, kasome Ufunuo 16, hadi mwisho kabisa , wanadamu wataadimika kama Dhahabu biblia inasema hivyo katika (Isaya 13),kama leo hii usivyoweza kuikota dhahabu kama mawe barabarani ndivyo itakavyokuwa kwa watu wakati huo, Kama alivyotoka tu Nuhu na wenzake 7 katika ya mabilioni ya watu ndivyo itakavyokuwa siku hiyo, kama walivyotoka watatu tu yaani Lutu na Watoto wake wawili ndivyo itakavyokuwa kwa mabilioni ya watu waliopo leo hii duniani.. kikundi kidogo sana, na tena watakuwa ni wale watakaowahifadhi wayahudi katika ule wakati wa dhiki za mpinga-kristo, Lakini wewe uliyepo leo hii unaipinga injili sasa , siku hiyo utakuwa ni jivu limelala hapo chini au mzoga, na ndege watakuwa wanakula nyama yako.

Tukiachilia mbali ile vita ya Harmagedoni, siku yenyewe ambayo Bwana atashuka na mawingu ambapo kila jicho litamwona, na watu watamwombolezea, misingi ya dunia hii unayoiona itatikisika, na kutakuwepo na tetemeko kubwa la ardhi ambalo halijawahi kuwepo, kumbuka wakati huo hayo yanaendelea tayari dunia imeshakuwa giza, hakuna jua wala mwezi, wala nyota yoyote angani, tetemeko hilo litaitikisa milima, mpaka hivi visiwa vyote unavyoviona leo hii vitahama, wewe wakati huo utakuwepo wapi Siku ya kuharibiwa? Wafalme, watakuwa wakilia wakiomba milima iwaungukie wafe, lakini wasikumbane na hiyo hasira ya mwana-kondoo.

Ufunuo 6:12 “Nami nikaona, alipoifungua muhuri ya sita, palikuwa na tetemeko kuu la nchi; jua likawa jeusi kama gunia la singa, mwezi wote ukawa kama damu,

13 na nyota zikaanguka juu ya nchi kama vile mtini upukutishavyo mapooza yake, utikiswapo na upepo mwingi.

14 Mbingu zikaondolewa kama ukurasa ulivyokunjwa, na kila mlima na kisiwa kikahamishwa kutoka mahali pake.

15 Na wafalme wa dunia, na wakuu, na majemadari, na matajiri, na wenye nguvu, na kila mtumwa, na mwungwana, wakajificha katika pango na chini ya miamba ya milima,

16 wakiiambia milima na miamba, Tuangukieni, tusitirini, mbele za uso wake yeye aketiye juu ya kiti cha enzi, na hasira ya Mwana-Kondoo.

17 Kwa maana siku iliyo kuu, ya hasira yao, imekuja; naye ni nani awezaye kusimama”?

Unaona?

Mambo haya utayashuhudia wewe ambaye bado upo nje ya Kristo, na wewe ambaye unaishi Maisha ya uvuguvugu sasahivi. Dalili zote zinathibitisha kuwa sisi watu wa kizazi hichi, haya mambo yatatupata, na dalili kubwa ni kuwa huu ni wakati ambao watu wanamejisahau, na pale watu walipojisahau na wanaona kuna Amani biblia inasema Hapo ndipo uharibifu unapokuja kwa ghafla (1Thesalonike 5:2)….Swali ni Je! Tumejiwekaje tayari..

Je! Bado unaishi Maisha ya kubahatisha? Utasema tena ni kwanini mnahubiri hivyo kana kwamba mnao uhakika kuwa Yesu atarudi wakati wetu..Ndio tunahubiri hivyo kwa nguvu zote kwasababu anayejua siku na saa ya kiama, ametuambia tuhubiri hivyo kwa nguvu sana…

Luka 14:33 “ Angalieni, kesheni, [ombeni], kwa kuwa hamjui wakati ule utakapokuwapo.

34 Mfano wake ni kama mtu mwenye kusafiri, ameiacha nyumba yake, amewapa watumwa wake amri, na kila mtu kazi yake, naye amemwamuru bawabu akeshe.

35 Kesheni basi, kwa maana hamjui ajapo bwana wa nyumba, kwamba ni jioni, au kwamba ni usiku wa manane, au awikapo jimbi, au asubuhi;

36 asije akawasili ghafula akawakuta mmelala.

37 Na hilo niwaambialo ninyi, nawaambia wote, Kesheni.

Sasa ikiwa wewe, unasikiliza injili ya mapepo inayokuhubiria kuwa dunia haitaangamizwa, ujue kuwa upo hatarini sana,. Kama hujamaanisha kumfuata Bwana Yesu, basi ni heri ukafanya hivyo sasa kabla mlango wa neema haujafungwa..Chaguo ni lako, uamuzi ni wako..Lakini fahamu tu wale wanaolishika Neno la Subira yake leo hii, hao ndio watakaoepushwa na saa ile ya kuharibiwa..

Bwana, Mkuu wa uzima wetu akubariki.

Maran Atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

SAKRAMENTI NI NINI, NA JE! IPO KATIKA MAANDIKO?

TOFAUTI KATI YA HEKALU, SINAGOGI NA KANISA NI IPI?

Kwanini Bwana Yesu, aliruhusu yale mapepo yawaingie nguruwe?

Ikiwa sisi tuliumbwa na Mungu,Je! Mungu aliumbwa na nani?

Nini maana ya huu mstari ” Nimevipiga vita vilivyo vizuri, mwendo nimeumaliza, Imani nimeilinda;”?(2Timotheo 4:7)

SALA YA ASUBUHI

NINI MAANA YA SISI KUWA WATOTO WA MUNGU?

Rudi Nyumbani:

Print this post

Ni kura ya aina gani waliipiga wale watu waliosafiri na Yona?

Ni kura ya aina gani waliipiga wale watu waliosafiri na Yona..hata ikamwangukia Yona? Na je! Mungu anatumia kura kuchagua watu?


JIBU: Biblia haijasema ni kura gani ilipigwa pale, kama ni ya kurusha kete au kwamba kila mmoja aliandika maoni yake binafsi na walipoyaleta yote yakaonekana yanamlenga Yona…Hakuna ajuye, na wala biblia haijaandika..Lakini yote katika yote ni kwamba kura ilipigwa pale na ikamwangukia Yona.

Kikubwa tunachoweza kujifunza ni kwamba..Mungu anaweza kutumia njia yoyote kukamilisha kusudi lake..anaweza kutumia njia iliyo rasmi au isiyo rasmi…Kwamfano kama wewe ni mwanafunzi mzuri wa Biblia utagundua kuwa Mungu alimpa Daudi ufalme wote wa Israeli kwa njia ya fitina..Mungu Alimwahidia atakuwa Mfalme juu ya Israeli yote na akampaka mafuta kwa mikono ya Nabii Samweli…lakini siku ilipofika ya unabii huo wa kuwa Mfalme wa Israeli kutimia..hakupata ufalme kwa njia ya uchaguzi bali kwa njia ya fitina. Yaani mfalme aliyekuwa madarakani (mtoto wa Sauli )alifanyiwa fitina ndipo Daudi akaingia madarakani….

Kwani siku hiyo walitokea tu watu Fulani waliokuwa wanaishi kwenye nyumba ya Mfalme na hao watu wakamvizia mfalme aliyekuwa madarakani wakampiga na kumuua na kumkata kichwa,..na kumpelekea kile kichwa Daudi na kumwambia leo Mungu amewalipiza kisasi maadui zako. Ingawa Daudi hakukubaliana na uovu wao…lakini kukawa hakuna namna ni lazima kiti cha ufalme kikaliwe na mtu mwingine na huyo hakuwa mwingine zaidi ya Daudi (kasome 2Samweli 4:5-12).

Kwani Israeli walipoona mfalme wao kauawa kukawa hakuna namna zaidi ya kumweka Daudi Madarakani awe mfalme.. Na unabii wa yeye kuwa Mfalme juu ya Israeli yote ukatimia pale.

Hali kadhalika Mungu anaweza kumchagua mtu kwa njia yoyote ile iwe rasmi au isiyo rasmi..Na anaweza kumtumia mtu yoyote Yule kukamilisha kusudi lake, anaweza kumtumia mwovu au mwenye haki…kwa jinsi apendavyo yeye. Akitaka kumweka mtu mahali anaweza kutumia kura au asitumie kura. Mathiya alichaguliwa kwa kura kuwa miongoni mwa Mitume 12 wa Bwana Yesu kuchukua nafasi ya Yuda. Lakini Petro na Mitume wengine hawakuchaguliwa kwa kura…Na hiyo haikumfanya Mathiya asiwe miongoni mwa wale mitume 12.

Kadhalika Yona alichaguliwa kwa kura ili kuadhibiwa na Mungu. Mungu angeweza kuwaonyesha maono wale watu kuwa Yona ndio chanzo cha matatizo, lakini pale hakuitumia hiyo njia…angeweza kumtuma malaika akawatokea na kuwaambia Yona ndie chanzo cha lile tatizo lakini haikumpendeza..

Hata katika chaguzi za viongozi wa shule, kijiji, mtaa, au nchi…wote wanaochaguliwa na kushika nafasi hizo ni Mungu ndio kawaweka pale…Iwe wamewekwa kwa njia iliyo halali au isiyo halali kama ya uwizi wa kura au la!,..hiyo haijalishi..Ni Mungu ndio kawaweka pale..(Siku ya mwisho ndio watakwenda kujibu kwanini waliiba kura au kwanini hawakuwa waaminifu katika nafasi hizo)..Lakini maadamu tayari wapo katika hizo nafasi ni Mungu ndiye kawaweka…

Maraisi wote waliopo madarakani ni Mungu ndiye kawaweka katika nafasi hizo haijalishi waliiba kura au hawakuiba..haijalishi ni madiktekta au sio madiktekta, haijalishi wanamjua Mungu au hawamjui..Ni Mungu ndiye kawaweka kwa kusudi lake maalumu…wengine kwa kusudi kama la Farao, wengine kama la Yeroboamu, wengine kama la Nebukadneza, wengine kama la Mfalme wa Ashuru, wengine kama Manase, wengine kama Hezekia… Kila mmoja kawekwa pale na Mungu kwa kusudi maalumu…

Bwana akubariki.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

ROHO YA MPINGA KRISTO IKITENDA KAZI SIKU HIZI ZA MWISHO

KWANINI MUNGU ALIMTUMIA MUSA KWA VIWANGO VILE?

JE! MUNGU NI NANI?

Ni sahihi kumuita Mariamu mama wa Mungu?

ROHO YA MPINGA KRISTO IKITENDA KAZI SIKU HIZI ZA MWISHO

KWA VILE ALIVYOKUWA MTU WA HAKI.

KUOTA UMETUMBUKIA SHIMONI.

SI KILA KIPENDEZACHO KINATOKA KWA BWANA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

SALA YA ASUBUHI

Sala ya Asubuhi inapaswa iweje?..Na je kuna sala ya jioni pia?

Hakuna sala rasmi ya Asubuhi iliyotungwa kwamba watu wafuate mfumo wake lakini ni wajibu wa kila mtu anayeitwa mkristo kusali..Katika kusali au kuomba kuna vitu vikuu vitatu vya kuzingatia katika sala yoyote ile.. Cha kwanza ni Shukrani, cha pili ni kupeleka mahitaji na cha tatu ni kutangaza

Katika sala ya Asubuni pia ni muhimu kuzingatia hivyo vipengele vitatu. Mwishoni somo hili kuna somo lingine lenye kichwa kinachosema “FAIDA ZA MAOMBI”. Nakushauri ulisome ili uweze kuelewa uchambuzi wa vipengele hivyo vitatu vya maombi.

Lakini kama ndio kwanza umempa Kristo maisha, basi sala hii hapa chini kwa Asubuhi inaweza kukufaa. 

Unapoamka kabla ya kufanya kitu chochote kile, hata kabla ya kwenda kupiga mswaki.. Sali sala hii kwa kumaanisha na kwa muda mrefu kwa jinsi uwezavyo ukitaja hata  mambo ambao hayajaandikwa katika sala hii.

Sema…

Ee Baba yangu, Mungu muumba wa mbingu na nchi, nakushukuru kwa kuniamsha nikiwa mzima wa afya,(hata kama umeamka na udhaifu fulani mdogo huna buni kumshukuru Mungu pia)

Nasema ahsante sana ni kwa Neema zako tu, wapo ambao hawajaweza kuamka leo lakini mimi nimeamka.

Nakuomba unipe Neema yako katika siku ya leo inayoanza nikatembee katika mapenzi yako, nisikutende dhambi wala nisikuhuzunishe kwa jambo lolote, naomba ukaniepushe na majaribu yote, na mipango yote mibaya ya yule Adui aliyoipanga juu yangu na juu ya watu wangu na vitu vyangu na afya yangu na shughuli zangu katika hii siku ya leo.

Nijalie pia siku hii ya leo angalau niongeze kitu kimoja katika ufalme wako, hata itakapofika tena jioni nikapate kushuhudia matendo yako makuu na kukushukuru. Naomba haya machache katika Jina la Yesu Kristo.

Amen’.

Kumbuka pia tuna wajibu wa kusali muda wote na mahali popote sio tu asubuhi, au jioni…hapana bali hata tukiwa tunatembea, tunafanya kazi..tuna wajibu wa kuomba…sala ya jioni pia ni ya muhimu sana kama tu ilivyo sala ya Asubuhi.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

FAIDA ZA MAOMBI.

FAIDA ZA MAOMBI YA USIKU

UNATAKA KUBARIKIWA? BASI USIKWEPE GHARAMA ZAKE.

KIFO CHA MTAKATIFU POLIKAPI (Policarp).

HERI NINYI MLIAO SASA, KWA SABABU MTACHEKA.

JE NI KWELI MTU ANAWEZA KUTOKA NJE YA MWILI WAKE?.

MTAIFAHAMU KWELI NAYO HIYO KWELI ITAWAWEKA HURU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Bali wajane walio vijana ukatae kuwaandika hao.

SWALI: Biblia inamaana gani kusema   “Bali wajane walio vijana ukatae kuwaandika hao, maana, wakizidiwa na tamaa kinyume cha Kristo, wataka kuolewa;nao wana hukumu kwa kuwa wameiacha imani yao ya kwanza”.(1Timotheo 5:11-12).

Ni kwanini wahukumiwe kwa kuolewa kwao tena, wakati biblia inaruhusu wajane kuolewa?


JIBU: Kama ukisoma kuanzia mistari ya juu utaona zamani za mitume kulikuwa na utaratibu wa kuwakumbuka wajane katika posho la kanisa..Na kulikuwa na masharti yake ili uweze kuandikwa,

  • Sharti la kwanza ni lazima awe ameshuhudiwa kuwa huko nyuma aliishi na mume mmoja tu,

1Timotheo 5:1 “Mjane asiandikwe isipokuwa umri wake amepata miaka sitini; naye amekuwa mke wa mume mmoja”;

  • Pili ni lazima awe ameshudiwa kuwa na matendo mema, na awe ameshawahi kutoa  mchango wowote( wa huduma) katika kanisa la Mungu..

1Timotheo 5.10  “naye ameshuhudiwa kwa matendo mema; ikiwa amelea watoto, ikiwa amekaribisha wageni, ikiwa amewaosha watakatifu miguu, ikiwa amewasaidia wateswao, ikiwa amefuata kwa bidii kila tendo jema”.

  • Na tatu, awe hana amefikisha umri wa miaka 60 na Zaidi. Kama tulivyoona hapo kwenye mstari 1
  • Nne, Awe hana ndugu, wala wana, wala jamii ya kumsaidia.

5.4 Lakini mjane akiwa ana watoto au wajukuu, na wajifunze kwanza kuyatenda yaliyo wajibu wao kwa jamaa zao wenyewe, na kuwalipa wazazi wao. Kwa kuwa hili lakubalika mbele za Mungu.

  • Tano, awe ameweka tumaini lake lote kwa Bwana. Yaani ameamua  kudumu  katika kumtumikia Bwana na katika kufanya dua mchana na usiku.

5.5  Basi yeye aliye mjane kweli kweli, ameachwa peke yake, huyo amemwekea Mungu tumaini lake, naye hudumu katika maombi na sala mchana na usiku.

Hivyo mjane yeyote ambaye alikuwa amekidhi hivyo vigezo basi alikuwa anaruhusiwa kuandikwa katika kanisa, na kanisa lilikuwa linawatambua watu kama hao, na walikuwa wanatengewa fungu lao maalumu.

Lakini sasa kama tayari alishajitoa kikamilifu kwa Bwana namna hiyo, ameshaingia katika nadhiri kama hizo kwamba tumaini lao lote sasa ni kwa Bwana tu, mpaka anafikia hatua ya kuchukua uamuzi wa kwenda kuandikwa katika kitabu cha kanisa kwamba ni yeye ni mjane kweli kweli aliyemwekea Mungu tumaini lake lote, halafu inatokea ghafla tu anageuka na kutaka  kuja kuolewa tena….Sasa katika mazingira kama hayo watu wa namna hiyo maandiko haya ndio yanayowahusu.

5.12 wana hukumu kwa kuwa wameiacha imani yao ya kwanza..

Na ndio maana mtume Paulo akatoa angalizo kabisa, wajane wazee ni heri wasiandikwe waolewe, kwa namna nyingine ni kwamba  kama wanajijua siku moja  watakuja kuolewa basi wasijiingize katikati  ya wajane kweli kweli waliodhamiria kumuishia Mungu maisha yao yote vinginevyo watakuwa wanajitafutia hukumu ya bure..wakizidiwa na tamaa.

Ubarikiwe.

Mada Nyinginezo:

Je! Ni halali kuoa/kuolewa na mtu ambaye tayari anao watoto?

Je! Ni sahihi kwa mkristo kuoa/kuolewa na mtu wa imani nyingine?

NDOA NA TALAKA:

KUSUDI LA MIMI KUWEPO DUNIANI NI LIPI?

JE! UNAYATUNZA MAVAZI YAKO?

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

Kwanini kila nikitaka kusali naingiwa na uvivu?

USILALE USINGIZI WAKATI WA KUMNGOJEA BWANA.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

Rudi Nyumbani:

Print this post

JINSI SODOMA NA GOMORA ILIVYOKUWA INAVUTIA SANA..

Jinsi sodoma na gomora ilivyokuwa inavutia sana.

Mwanzo 13:10 “Lutu akainua macho yake, akaliona Bonde lote la Yordani, ya kwamba lote pia lina maji, kabla Bwana hajaharibu Sodoma na Gomora, lilikuwa kama bustani ya Bwana, kama nchi ya Misri hapo unapokwenda Soari.

11 Basi Lutu akajichagulia Bonde lote la Yordani; Lutu akasafiri kwenda upande wa mashariki; wakatengana wao kwa wao”.

Ndugu kama ulikuwa hujui, basi leo ujue, kuwa dhambi ni kitu kinachovutia sana! Kama dhambi ingekuwa haivutii hakuna mtu leo hii angenaswa na mtego wowote wa dhambi..Wengi wetu tunajua habari ya Lutu na mjomba wake Ibrahimu jinsi walivyopishana kauli kutokana na wingi wa mali walizokuwa nazo, mpaka ikafikia hatua sasa wajitenge kila mmoja achague upande wake wa kukaa.

Lutu akapewa kipaumbele cha kwanza cha kuchagua, akafanya utafiti wake wa mji bora wa kukaa, ndipo akaitazama miji yote iliyokuwa kando kando na pale walipokuwepo yeye na Ibrahimu, mwishowe akafanikiwa kuona miji mizuri sana, ambayo hakukuwa na mfano wake katika kaanani yote na miji yenyewe ni Sodoma na Gomora. Biblia inasema miji hiyo ilikuwa mfano wa BUSTANI YA MUNGU (Edeni). Ilikuwa nzuri karibia ifanane na Edeni..Hivyo sio kila mahali panapoonekana pazuri Mungu yupo…Uzuri wa sodoma na Gomora ulifananishwa na Edeni, lakini ilikuwa ni bustani ya shetani…Shetani naye anayo Edeni yake ambayo kwa uzuri inakaribi Ilikuwa ni miji yenye kijani kibichi, yenye chemchemi za maji, na mwonekano wa kuvutia.

Vivyo hivyo ilikuwa ni miji yenye ustaarabu uliomakini, yenye uchumi mkubwa, yenye fursa nyingi za biashara, isiyo na njaa wala kiu, miji ambayo mtu ukiishi unajua nini maana ya maisha,.mbali sana na hiyo Kaanani ambayo alikuwa anaishi yeye na Ibrahimu, ambayo ni jangwa tupu, hakuna hata chakula cha kutosha maji yenyewe ni ya shida, kama nusu-kijiji tu..

Na hiyo ndiyo sababu mojawapo iliyowafanya watu wa miji ile wasimwongope Mungu, wamuone kuwa si kitu cha maana sana kwao, wakaanza kujiamulia kuishi tu kama wapendavyo kama wanyama, wanazini wao kwa wao jinsia moja, wanazini na wanyama. N.k.

Sasa Lutu yeye hakuangalia nyuma ya pazia kuna nini..Yeye maadamu anaona fursa, na maisha mazuri akaamua kuingia moja kwa moja, kumbe kama sio neema ya Mungu ndio ulikuwa mwisho wake..

Biblia inatuambia wazi kabisa kama ilivyokuwa katika siku za Lutu ndivyo itakavyokuja kuwa katika siku za kuja kwake mwana wa Adamu.. Wote tunajua jinsi dunia ya leo ilivyo tofauti sana ile ya zamani, ustaarabu uliopo leo hii ni mkubwa sana, utajiri uliopo duniani leo hauwezi kulinganishwa na ule uliokuwepo wakati ule, teknolojia, elimu, uchumi, miundombinu ni ya ajabu sana, kiasi kwamba ukimleta mtu wa karne ya 18 ukamuonyesha miji ya kisasa iliyopo duniani pamoja na teknolojia tulizonazo anaweza kusema huu sio ulimwengu wa wanadamu, bali ni kitu kingine…

Lakini mambo hayo mawili yanakwenda sambamba, “mafanikio pamoja na uovu vinashadiiana”.. Leo hii huoni jinsi ndoa za jinsia moja zinavyohalalishwa kila mahali mambo ambayo huko zamani hayakuwepo?, ndoa za wanyama na wanadamu, uzinzi sasahivi kila mahali mtu akiwa na simu ya mkononi tu, tayari anaufahamu uzinzi wote wa ulimwenguni..jambo ambalo hata sodoma halikuwepo, Mungu leo hii anatukanwa hadharani, ukipeleka habari za Mungu tu unaonekana kama mpinga-uhuru wa haki za kibinadamu, unaonekana kama mtu wa kale mwenye itikadi za kizamani.

Na wana wa Mungu wanapoona, mbona Mungu hachukui hatua yoyote dhidi yao, nao pia wanakwenda kujichanganya na maovu yao, ..Hawajui kuwa wanajiangamiza wao wenyewe bila kujua.

Kule Sodoma..Siku ya maangamizo ilipofika haikumaliza hata siku moja, mji ile ilikuwa imeshakuwa jivu yote..Vivyo hivyo na siku ya maangamizi ya huu ulimwengu ambayo ipo mbioni kutokea ambayo biblia ilishasema itakuja kwa ghafla sana, tena na cha kuogopesha zaidi itakuja katika kipindi cha amani,..soma.

1Wathesalonike 5:2 “Maana ninyi wenyewe mnajua yakini ya kuwa siku ya Bwana yaja kama vile mwivi ajavyo usiku.

3 Wakati wasemapo, Kuna amani na salama, ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafula, kama vile utungu umjiavyo mwenye mimba, wala hakika hawataokolewa”.

Sasa kama na wewe upo katikati ya sodoma, usidhani itakuwa ni rahisi, kupona wakati huo ..

Mungu alishatuasa watoto wake tutoke huko, tujitenge nao mambo ya ulimwengu.. (Ufunuo 18:4)..Tusiyakaribia hata kidogo…Tutoke Sodoma wala tusiikaribie hata kidogo…Tukae nayo mbali sana maelfu ya Maili…Kumbuka sio tu Sodoma na Gomora pekee yake ndio ziliteketezwa wakati wa Nuhu..Biblia inasema hata ile miji iliyokuwa kando kando ya Sodoma na Gomora iliteketezwa pia (kasome Yuda 1:7)..Haikuwa na maasi kama Sodoma na Gomora..lakini kitendo tu cha kuwa karibu na miji hiyo tayari ilikuwa imeshanajisika nayo pia..Kadhalika leo..tunaaswa tukae mbali na uchafu wa dunia hii, wala tusifungwe nira na wasio amini kwa jinsi isivyo sawasawa. (2Wakorintho 6:14) ili nasi tusije tukachanganywa huko huko katika hasira ya Mungu.

1Yohana 2:15 “Msiipende dunia, wala mambo yaliyomo katika dunia. Mtu akiipenda dunia, kumpenda Baba hakumo ndani yake.

16 Maana kila kilichomo duniani, yaani, tamaa ya mwili, na tamaa ya macho, na kiburi cha uzima, havitokani na Baba, bali vyatokana na dunia.

17 Na dunia inapita, pamoja na tamaa zake, bali yeye afanyaye mapenzi ya Mungu adumu hata milele”.

Unaona? Ikiwa umeokoka halafu bado unapenda kwenda disko basi ujue upo Sodoma, umeokoka na bado unasikiliza miziki ya kidunia, unavaa nguo za kikahaba, vimini na masuruali, ujue unaishi sodoma bado..Na siku ile ya Unyakuo hutakwenda popote.. utabaki hapa chini ukingojea hukumu ya Mungu kulingana na Biblia.

Ni maombi yangu, hutachukuliwa na tamaa kama za Lutu, kwa kupenda mambo haya ya kitambo ya ulimwenguni, bali sote tutajitahidi tumtazame Kristo na mambo ya ufalme wa mbinguni, hadi siku ile ya ukombozi wetu utakapofika.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

MTU ASIYE PAMOJA NAMI YU KINYUME CHANGU.

Kwanini wanawake wengi huwa wanalipuka mapepo?

JE ADAMU ALIKUWA NA KITOVU?

MAJINI WAZURI WAPO?

NI NINI KINAKUPATA UNAPOIPUUZIA INJILI?

INJILI YA MILELE NI IPI KATIKA BIBLIA?

MIILI YA UTUKUFU ITAKUWAJE?

SADAKA YA MALIMBUKO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Ufisadi una maanisha nini katika biblia?

Ufisadi una maanisha nini katika biblia? (Ufisadi ni nini? Ni uwizi wa fedha nyingi au?)


JIBU: Neno ufisadi tofauti na linavyotafsiriwa siku hizi kwamba ni mtu anahujumu uchumi wa Taifa Fulani au shirika Fulani. Lakini katika biblia tafsiri yake ni tofauti.

Katika biblia neno fisadi limetumika kumtambulisha mtu mwenye tabia ya uzinzi na uasherati uliopindukia ambao hata haujali jinsia, umri wala maadili (unahusisha chochote kile ilimradi tu ni zinaa inafanyika)..Kwa lugha nyingine (ni ukahaba/umalaya mchafu). Hivyo popote pale katika biblia linapoonekana neno hili fahamu kuwa linamaanisha “ukahaba/ umalaya wa namna hiyo”.. Kwamfano tunaweza kusoma baadhi ya mistari michache inayozungumzia tendo hilo…

Waefeso 4:19 “ambao wakiisha kufa ganzi wanajitia katika mambo ya ufisadi wapate kufanyiza kila namna ya uchafu kwa kutamani”…..

Waefeso 5:18 “Tena msilewe kwa mvinyo, ambamo mna ufisadi; bali mjazwe Roho;”…

Maana yake ni kuwa ulevi na ukahaba/Umalaya ni pacha, vinakwenda sambamba…

Mstari mwingine ni kama huu..

Tito 1:6“ ikiwa mtu hakushitakiwa neno, naye ni mume wa mke mmoja, ana watoto waaminio, wasioshitakiwa kuwa ni WAFISADI wala wasiotii.

7 Maana imempasa askofu awe mtu asiyeshitakiwa neno ,kwa kuwa ni wakili wa MUNGU;asiwe mtu wa kujipendeza nafsi yake,asiwe mwepesi wa hasira,asiwe mlevi wala mgomvi,asiwe mpenda mapato ya aibu”.

Maana yake ni kwamba Watoto wa Maaskofu pia hawapaswi kuwa Malaya wala makahaba wala kujihusisha na vitendo vyovyote vya zinaa. Wanapaswa wawe watakatifu katika mwenendo wao ili wawe kielelezo kwa kanisa la Mungu. Mtu yoyote anayetaka kazi ya uaskofu kama Watoto wake ni wachafu kwa viwango hivyo biblia inasema hastahili kuwa Askofu..anapaswa awageuze kwanza Watoto wake ndipo aweze kulichunga kundi la Mungu.

Pia Wagalatia 5:19 inasema… “Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, UFISADI.”.. Na 2Wakorintho 12:21 pia inasema…“Nami nitakapokuja tena, Mungu wangu asije akanidhili kwenu, nami nikawasikitikia wengi waliokosa tangu hapo, wasiutubie uchafu, na uasherati, na ufisadi walioufanya”…

1Petro 4:3 “ Maana wakati wa maisha yetu uliopita watosha kwa kutenda mapenzi ya Mataifa; kuenenda katika ufisadi, na tamaa, na ulevi, na karamu za ulafi, na vileo, na ibada ya sanamu isiyo halali;

4 mambo ambayo wao huona kuwa ni ajabu ya ninyi kutokwenda mbio pamoja nao katika UFISADI ule ule usio na kiasi, wakiwatukana”

Mistari mingine pia ni katika kitabu cha Petro…

2 Petro 2:6 “ tena akaihukumu miji ya Sodoma na Gomora, akiipindua na kuifanya majivu, akaifanya iwe ishara kwa watu watakaokuwa hawamchi Mungu baada ya haya;

7 akamwokoa Lutu, yule mwenye haki aliyehuzunishwa sana na mwenendo wa UFISADI WA HAO wahalifu”. Kama tunavyojua miji ya Sodoma na Gomora kiwango cha uasherati walichofikia..hata kuwatamani Malaika.

Na mistari mingine mingi inazungumzia tendo hilo…Unaweza kupitia binafsi mistari ifuatayo..(Marko 7:22, Warumi 13:13, 2Petro 2:18, na Yuda 1:4).

Je! Swali linakuja….Mafisadi watakwenda mbinguni?..Jibu ni la! Kama biblia ilivyosema hapo juu…

Wagalatia 5:19 “Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, UFISADI,

20 ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi,

21 husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, KATIKA HAYO NAWAAMBIA MAPEMA, KAMA NILIVYOKWISHA KUWAAMBIA, YA KWAMBA WATU WATENDAO MAMBO YA JINSI HIYO HAWATAURITHI UFALME WA MUNGU”.

Unaona biblia imetuonya mapema kabisa kwamba watu wafanyayo hayo hawataurithi uzima wa milele?..Je ulevi ni suluhisho la kupunguza uzinzi na uasherati?..Jibu ni la! Kinyume chake Ndio kichochoe kikubwa cha ukahaba na umalaya huo(Ufisadi). Lakini Roho Mtakatifu ndiye jawabu la kuondoa tamaa ya uasherati na uzinzi.. kama Waefeso 5:18 inavyosema.. “Tena msilewe kwa mvinyo, ambamo mna ufisadi; bali mjazwe Roho;”…

Je umempokea Roho Mtakatifu?..ambaye ndiye msaada wetu wa kushinda dhambi? Kama bado unangoja nini?

Matendo 2:37 “Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu?

38 Petro akawaambia, TUBUNI MKABATIZWE KILA MMOJA KWA JINA LAKE YESU KRISTO, MPATE ONDOLEO LA DHAMBI ZENU, NANYI MTAPOKEA KIPAWA CHA ROHO MTAKATIFU.

39 Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu wamjie.

40 Akawashuhudia kwa maneno mengine mengi sana na kuwaonya, akisema, Jiokoeni na kizazi hiki chenye ukaidi.

41 Nao waliolipokea neno lake wakabatizwa; na siku ile wakaongezeka watu wapata elfu tatu”.

Njia ya kumpokea huyo Roho Mtakatifu ndiyo hiyo hapo juu..Kutubu kwa kudhamiria kuacha dhambi na kwenda kubatizwa….Na wewe Tubu leo, ukabatizwe katika Jina la YESU na utapokea kipawa hicho cha Roho Mtakatifu, kwasababu Mungu sio mwongo, Naye atakupwa uwezo huo wa kuzishinda hizo tamaa mbaya.

Bwana akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

KWA VILE ALIVYOKUWA MTU WA HAKI.

JUMA LA 70 LA DANIELI

JE WAKRISTO TUNARUHUSIWA KUSHEHEREKEA VALENTINE’S DAY?

WINGU KUBWA LA MASHAHIDI.

NJIA SAHIHI YA KUFUNGA.

NJIA YA ‘UTAJIRI MKUU’ KWA KIJANA.

TUMAINI NI NINI?

TENZI ZA ROHONI

Rudi Nyumbani:

Print this post

KIFO NI NINI?

Kifo ni nini?, Je ni kweli kila nafsi itaonja mauti?.

Kifo sio mtu, wala si kitu bali ni “hali”…Kitu kinapopitia hali ya kukosa “UHAI”. Tayari kitu hicho kinakuwa kimekufa.

Kwamfano tuchukue kifaa kinachoitwa SIMU. Simu ikikosa chaji simu ile inazima hivyo tunaweza kusema “imekufa chaji”..Sasa kitendo cha umeme kukosekana kwenye ile simu…Ni sawa na simu ile imekufa..kwasababu haiwezi kuwaka, spika zake haziwezi kufanya kazi, kadhalika haiwezi kutoa mlio wowote wala kufanya chochote mpaka ichajiwe tena.

Vivyo hivyo Uhai wa Mungu ni kama “UMEME” ndani mwetu…Huo unapokosekana au unapotoka ndani ya mwili wa mtu…Mtu yule anakuwa amekufa. Hawezi kunyanyuka, hawezi kuona kupitia macho..hawezi kuhisi, hawezi kujibu, hawezi kufanya chochote kile..Mwili wake unakuwa umekufa.(Hivyo kifo ni nini?..Ni hali ya uhai wa Mungu kutoka ndani ya kiumbe hai)

Lakini kitu cha kipekee na cha muhimu kufahamu ni kwamba..Mtu kaumbwa na sehemu mbili kuu, nazo ni UTU WA NDANI, na UTU WA NJE. Utu wa nje ndio mwili ambao ndio huu wenye vidole, macho ni mikono…Huu uhai wa kiMungu unapoondoka unazima!.

Kadhalika kuna utu wa ndani..Huu wa nje unapozima wa ndani bado upo..unakuwa bado una uhai wa Mungu. Hivyo unaendelea kuishi..Unaendelea kuona, kusikia, kufahamu ingawa hautumii macho ya damu na nyama wala viungo vya damu na nyama…Unatumia viungo vya rohoni kuona, kusikia, kuelewa n.k

Kama mtu alikufa akiwa ndani ya Imani ya Mwana wa Mungu Yesu Kristo, analo tumaini la kufufuliwa na kuvalishwa mwili mpya wa utukufu na kwenda mbinguni kwa Bwana…ambao huo haufi wala hauzeeki. Lakini kama mtu alikufa katika ndambi anakuwa hana tumaini hilo zaidi ya kungojea kwenda kutupwa katika Ziwa la Moto.

Je ni kweli kila nafsi itaonja mauti?

Jibu ni hapana! sio kila nafsi itaonja mauti…kwani mpaka sasa kuna ambao hawajaonja mauti na wameshavuka kutoka mautini kuingia uzimani…Mfano wa watu hao ni HENOKO na ELIYA. Hawa walinyakuliwa juu bila kuonja mauti..Hivyo ni uongo kusema kwamba kila nafsi itaonja mauti.

Vivyo hivyo biblia inasema siku ya Unyakuo wa kanisa itakapofika, wapo watakatifu ambao siku hiyo itawakuta wakiwa hai. Hao Biblia imesema watanyakuliwa wakiwa hai ambapo kufumba na kufumbua miili yao itabadilishwa na kuwa kama ya Malaika, na wataungana na watakatifu waliofufuliwa na kwa pamoja watakwenda kumlaki Bwana mawinguni.

1Wakorintho 15:51 “Angalieni, nawaambia ninyi siri; hatutalala sote, lakini sote tutabadilika,

52 kwa dakika moja, kufumba na kufumbua, wakati wa parapanda ya mwisho; maana parapanda italia, na wafu watafufuliwa, wasiwe na uharibifu, nasi tutabadilika”.

Na pia jambo hilo biblia imeliweka vizuri katika mstari ufuatao..

1Wathesalonike 4:13 “Lakini, ndugu, hatutaki msijue habari zao waliolala mauti, msije mkahuzunika kama na wengine wasio na matumaini.

14 Maana, ikiwa twaamini ya kwamba Yesu alikufa akafufuka, vivyo hivyo na hao waliolala katika Yesu, Mungu atawaleta pamoja naye.

15 Kwa kuwa twawaambieni haya kwa neno la Bwana, kwamba sisi tulio hai, tutakaosalia hata wakati wa kuja kwake Bwana, hakika hatutawatangulia wao waliokwisha kulala mauti.

16 Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko, na sauti ya malaika mkuu, na parapanda ya Mungu; nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza.

17 Kisha sisi tulio hai, tuliosalia, tutanyakuliwa pamoja nao katika mawingu, ili tumlaki Bwana hewani; na hivyo tutakuwa pamoja na Bwana milele”.

Hivyo wapo ambao hawataonja mauti kabisa…Na dalili zote zinaonyesha kwamba unyakuo unaweza kutokea katika kizazi chetu hichi kwasababu kila dalili zimeshaonekana na hata zimezidi na kuonekana vitu vingine ambavyo ni zaidi ya zile dalili…maana yake ni kwamba kuna uwezekano wa kulishuhudia tukio la unyakuo kwa macho yetu..

Je umejiandaa?..Utakuwa miongoni mwa watakaonyakuliwa?..kumbuka biblia inasema waasherati, wazinzi, waabudu sanamu, walevi, na wanaoupenda ulimwengu kuliko kumpenda Mungu hawataurithi uzima wa milele.

Bwana atusaidie sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

Roho, Nafsi, na Mwili vina utofauti gani?

NINI KINAFUATA SIKU ILE ILE YA KUOKOKA!

ANGALIA USIJE UKANG’OA NGANO KATIKATI YA MAGUGU.

Je! Ni kweli ubatizo wa maji hatuuhitaji tena?

KIFO CHA MTAKATIFU POLIKAPI (Policarp).

JIHADHARI NA KUOSHWA MIGUU ISIVYOPASWA.

CHUKUA MZIGO WA MWINGINE.

Rudi Nyumbani:

Print this post

KUOTA UMETUMBUKIA SHIMONI.

Ogopa wadanganyifu, ambao wanakuambia suluhisho la ndoto Fulani uliyoota labda tuseme kuota umetumbukia shimoni, au umekimbizwa na nyoka,au umezama kwenye maji au unafanya uasherati na mtu usiyemjua kwamba ukanunue dawa yao Fulani itakusaidia kutatua hilo tatizo.. Wengi wanaokuambia hivyo kama si washirikina basi uwe na uhakika ni matapeli.. Ndoto, au maono, ni mambo yanayotoka ndani ya mtu, yaani katika utu wake wa ndani, Hivyo hayawezi kutibiwa kwa tiba za nje, kama vile dawa na vidonge, Ni sawa na mtu aliyefiwa, huwezi kumwambia nenda kameze PAIN KILLER, tatizo lako la huzuni litakwishwa, badala yake utatumia njia ya kumfariji, ndipo hapo atakapogangika kwasababu ugonjwa wake ni wa moyoni na si nje..

Hivyo ni vizuri kufahamu, ndoto asili yake ni rohoni, Kwahiyo tiba yake ni lazima iwe ya rohoni na si ya  nje.

Kwa utangulizi:

Zipo ndoto za aina tatu.

  1. Ni zile zinazotokana na Mungu: Ambazo hizi zinachukua sehemu ya wastani ya ndoto anaziziota mtu kila siku.
  2. Ndoto zinazotokana na shetani: Hizi nazo zinachukua sehemu ya wastani wa ndoto mtu anazoziona kila siku.
  3. Ni zile zinazotokana na mtu mwenyewe: Hizi ndizo zinazochukua sehemu kubwa sana ya ndoto mtu anazoziota kila siku.

Sasa kama kuota umetumbukia shimoni: Mara nyingi wengine wanaota wapo ukingoni mwa shimo wanakaribia kuanguka, wengine wapo tayari chini  kabisa kwenye  shimo refu lenye giza, wengine wananing’inia ikingoni mwa shimo na kila wanapojaribu kujivuta juu watoke wanajiona ni wazito sana, wanahitaji msaada..n.k. zote hizo ujumbe wake ni mmoja. Kuwa maisha yako yapo hatarini kama hutachukua uamuzi ulisohihi Mungu anaokuagiza uufanye.

Ikiwa wewe umeokoka (yaani maisha yako yamefichwa ndani ya YESU KRISTO):  Na ndoto kama hii kuota umetumbukia shimoni imekujia kwa uzito sana, au imejirudia rudia mara nyingi, basi ongeza umakini wako kwa MUNGU,kwasababu mahali unaweza kwenda kukwamba usisonge mbele katika imani yako, pili omba sana, hususani katika mazingira uliyopo, na mambo unayoyafanya yote hakikisha unamtanguliza Mungu kwanza..Na Bwana atakuvukisha au kukukwepesha kabisa na majaribu hayo.

Soma  (Yeremia 38:6, Maombolezo 3:52-57).

Lakini kama wewe hujaokoka na unafanya mojawapo ya hivi vitu:

  • Wewe Ni mzinzi: basi ujue Mungu anakupa ujumbe huu..

Mithali 22:14 Kinywa cha malaya ni shimo refu; Anayechukiwa na Bwana atatumbukia ndani yake.

Mithali 23: 27 Kwa maana kahaba ni shimo refu; Na malaya ni rima jembamba.

Ukiendelea kuwa na tabia hiyo, mwisho wako utakuwa ni mbaya..Utaingia mahali ambapo utashindwa kutoka milele.

  • Ikiwa hutendi haki: Au unamuundia mwenzako visa, ili asisonge mbele, basi andiko lako ni hili.

Mithali 26: Achimbaye shimo atatumbukia mwenyewe; Naye abingirishaye jiwe litamrudia.

Zaburi 7: 14 Tazama, huyu ana utungu wa uovu, Amechukua mimba ya madhara, amezaa uongo.

15 Amechimba shimo, amelichimba chini sana, Akatumbukia katika handaki aliyoifanya!

16 Madhara yake yatamrejea kichwani pake, Na dhuluma yake itamshukia utosini.

Hayo yote yanajumuisha watu wote waovu..Kuwa hatma ya maisha yao ni shimo refu la mauti kama hawatatubu.

Hivyo yatengeneza mambo yako kwa Mungu haraka iwezekanavyo..Kumbuka Yesu ndio njia, na kweli na Uzima (Yohana 14:6), anakuonyesha hivyo kwasababu anakupenda ili utubu umgeukie yeye, uache dhambi ayasafishe maisha yako. Ni nani ajuaye kuwa leo kukukutanisha na ujumbe huu ni kwa makusudi yake maalumu UOKOKE LEO?..Hivyo usipuuzie wito huo, mruhusu leo ayaokoe maisha yako akutoe katika shimo hilo refu la mauti ambalo upo sasa, au kama haupo basi siku si nyingi utakuwepo,ukiendelea na tabia yako.

Lakini  Ikiwa unatii na upo tayari kufanya hivyo sasa.

Basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie maisha yako yote kama ilivyokuwa hata kwetu sisi. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU  MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.

AMEN.

Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.

Fanya Hivyo na Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

CHAGUA NI JIWE LIPI LITAKALO KUFAA KWA UJENZI.

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

MAONO YA NABII AMOSI.

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!

NINI KINAFUATA SIKU ILE ILE YA KUOKOKA!

Rudi Nyumbani:

Print this post

JILINDE NA UNAJISI, UNA MADHARA MAKUBWA.

Najisi ni kitu gani?


“Najisi” ni kitu chochote kinachokwamisha na kuundoa usafi wako wote, heshima yako yote au hadhi yako yote uliyokuwa nayo ..Kwamfano unaweza ukawa na nguo yako nyeupe, lakini kawino kadogo tu cheusi kakapita kwenye mfuko wa shati hilo, kakakufanya usilavae tena shati hilo kwa doa lile ..Sasa kale kadoa cha wino ndio najisi hivyo kameitia unajisi nguo nzima isifae tena..

Vivyo hivyo kwa watakatifu, yapo mambo mengi unaweza kweli ukayadhibiti na ukawa safi lakini mambo madogo madogo yakakuharibia ukaonekana sio safi tena mbele za Mungu haijalishi umejitahidi kuyazuia hayo mengine kiasi gani..

Ukisoma katika agano la Kale Mungu aliwaorodheshea wana wa Israeli mambo ambayo yatawafanya kuwa najisi..Na mojawapo ni kuigusa maiti, ya mtu aliyekufa au mnyama..Hata kama wewe ni kuhani ilikuwa ukigusa tu maiti basi hutaruhusiwa kufanya chochote hadi siku ya tatu ambapo utajiosha na kujitakasa kwa maji safi..Ukishamaliza kujisafisha hiyo peke yake haitoshi kuundoa unajisi kabisa, itakupasa usubiri hadi siku ya saba bila kwenda popote ndipo utakaporuhusiwa kuingia katika kusanyiko la Mungu.(Soma Hesabu 19:12).

 Kadhalika na baadhi ya wanyama kama vile nguruwe, na wengine wasioweza kucheua walikuwa ni najisi, ukiwala tu tayari umeshajitia unajisi.

Halikadhalika ilikuwa ukitokwa na uchafu sehemu zako za siri iwe ni mwanaume au mwanamke tayari umeshajitia unajisi, hivyo kama wewe ni mwanaume ulikuwa unaoga kwa maji safi, kisha unausubiri mpaka jioni hufanyi chochote ndipo ikishafika jioni utaruhusiwa kuingia kwenye kusanyiko la Mungu (Walawi 15:16), Lakini kama wewe ni mwanamke labda upo katika siku zako basi utasubiri siku 7, ndipo uruhusiwe kuingia katika kusanyiko(Walawi 12:4).

Vilevile kwa mwanamke aliyezaa, tayari ametiwa unajisi kwa tendo lile, hivyo kama amezaa mtoto mwanaume basi atasubiri siku 33 pamoja na siku 14 za uchafu wa siku zake, lakini kama amezaa mtoto wa kike atasubiria siku 66 pamoja na siku nyingine 14 pia..

Hivyo siku zote hizo za unajisi mtu haruhusiwi kuingia katika kusanyiko lolote la Mungu wala kutoa kafara yoyote kwa Mungu, japokuwa tayari ulishajisafisha na unaonekana upo safi lakini inakugharimu usibirie, kinyume chake ukifanya hivyo adhabu yake ilikuwa ni kifo..

Sasa tukirudi katika agano jipya..Unajisi wetu sio wa mwilini tena bali wa rohoni, yote hayo yalikuwa yanafunua unajisi wa Rohoni ambao ndio mkuu, Bwana Yesu alisema..

Mathayo 15:18 ‘Bali vitokavyo kinywani vyatoka moyoni; navyo ndivyo vimtiavyo mtu unajisi.

19 Kwa maana moyoni hutoka mawazo mabaya, uuaji, uzinzi, uasherati; wivi, ushuhuda wa uongo, na matukano;

20 hayo ndiyo yamtiayo mtu unajisi; lakini kula kabla hajanawa mikono hakumtii mtu unajisi’.

Kama vile tulivyoona unajisi wa mwilini, unaweza ukawa kweli umeshaoga na kusafishika lakini ulikuwa bado huruhusiwi kuingia uweponi mwa Bwana kwa kitambo Fulani, aidha kwa siku moja, au kwa wiki, au kwa mwezi, au kwa miezi miwili inategemea na aina ya unajisi uliokuwa nao..Vivyo hivyo na unajisi wa rohoni, mtu unaweza kweli ukasemehewa kwa alilolifanya lakini hilo bado lisimfanye arudi uweponi mwa Bwana muda huo huo..bali kinaweza kupita kitambo kirefu sana..

Kama Bwana Yesu alivyosema, mawazo mabaya ni moja ya mambo yanayomtia mtu unajisi, unaweza ukawa wewe sio mzinzi lakini ndani yako muda wote unawaza uzinzi, sasa hapo tayari jambo hilo limeshautia doa utakatifu wako, umejitia unajisi.. Utakwenda kutubu kweli na pengine Mungu atakusamehe, lakini kurudi kule uweponi mwa Bwana, ambapo ulikuwa nako mwanzoni kunaweza kukuchukua muda sana..ndio maana tunapaswa tuwe makini sana..

Mawazo kama haya yanapokujia ndani yako hupaswi kuyapa nafasi hata kidogo, unayakataa na kuyakemea, na hapo hapo kupeleka mawazo yako katika Neno la Mungu na ahadi zake. Hiyo ndiyo njia pekee ya kutokujitia unajisi na mawazo ya namna hiyo..Vilevile unaacha kutazama au kuangalia vitu ambavyo vinachochea unajisi huo..Kama utakuwa mtazamaji wa movie za kidunia muda wote ambazo hizo ndani yake huwezi kosa maudhui ya uasherati unategemea mawazo hayo yasikutawale? Yatakutawala tu, unasikiliza miziki ya kidunia yatakutawala tu, unachati kwenye magroup yao, unasikiliza mazungumzo yao, unasoma visa vya hadithi za kiasherati, unafuatilia magazeti ya kiasherati…mawazo kama hayo yatakuteka, na itakuwa nguvu kujitawala..matokeo yake unajitia unajisi, na kuifanya bidii yako kuwa sio kitu mbele za Mungu..

Kama wewe ni mtukanaji au unazungumza maneno yasiyofaa, au msengenyaji…tayari unajitia mwenyewe unajisi, haijalishi unafunga, saumu yako ni bure tu..kwasababu doa tayari limeshaingia,..unapaswa ujifunze kukizuia kinywa chako.

Na ndio maana ukitoka tu kuwaza mambo kama hayo maovu, au ukitoka tu kuzungumza maneno hayo, unaona ndani yako ukame mkubwa, ile nguvu labda ya kusali imepungua ghafla, au ule uwepo wa Mungu ghafla umepotea ndani yako..Sasa ukishaona hivyo basi ujue tayari ulishajitia unajisi..Unapaswa ukatubu na uache kivitendo..na hiyo inaweza kuchukua muda kidogo mpaka kuurudisha tena uwepo wa Mungu karibu na wewe…Hayo ndiyo madhara ya kujitia unajisi…inasababisha uwepo wa Mungu kukaa mbali na wewe kwa muda.

Hivyo biblia ilishatuonya tuilinde mioyo yetu, kuliko kitu kingine chochote,(Mithali 4:23) kwasababu humo ndimo zitokazo chemchemi za maji ya uzima. Hivyo Bwana atusaidie sote tukae mbali na unajisi wa aina yoyote, ili safari yetu isiwe na vikwanzo visivyokuwa na lazima.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Akawaambia Enendeni ulimwenguni mwote,MKAIHUBIRI INJILI KWA KILA KIUMBE.(Marko16:15.) Yesu Anamaanisha nini kusema MKAIHUBIRI INJILI KWA KILA KIUMBE?

Sabato halisi ni lini, Je! ni Jumapili au Jumamosi?, Ni siku gani itupasayo kuabudu?

Inaruhusiwa Kula nyama ya Nguruwe kwa Mkristo wa Kweli?

ZIKUMBUKE FADHILI ZA MUNGU

UNYAKUO.

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!

MJUMBE WA AGANO.

Rudi Nyumbani:

Print this post

JE WAKRISTO TUNARUHUSIWA KUSHEHEREKEA VALENTINE’S DAY?

Je wakristo tunaruhusiwa kusheherekea valentine’s day(siku ya valentine)? siku ya wapendanao?

Valentine kulingana na Historia alikuwa ni kuhani wa kikatoliki aliyekuwa anaishi Rumi katika karne ya 3..Aliishi Wakati wa Utawala wa Mfalme wa Rumi, aliyeitwa Claudius wa pili…Huyu Claudia alikuwa mpagani na akatengeneza sheria za kuwazuia wakristo kufanya baadhi ya mambo…Historia inasema huyu Claudia ilifika wakati akatamka kuwa Wanajeshi wote wa Rumi wanapaswa wawe wamejitoa kikamilifu kwa nchi yao..hivyo hawapaswi kuoa..Kwahiyo akapitisha sheria kwamba hakuna mwanajeshi yoyote anayepaswa kuoa. Akiamini kuwa jeshi bora linajengwa na watu ambao hawajaoa.

Lakini huyu Valentine (au valentino)..hakukubaliana na hilo shauri…Hivyo akawa anawafungisha ndoa kwa siri baadhi ya wanajeshi hao..Lakini alikuja kujulikana na taarifa zikamfikia mfalme..na akahukumiwa kifo.

Wakati akiwa huko gerezani historia inasema alimpenda binti wa mkuu wa gereza aliyekuwa kipofu, na alimhudumia mpaka akapata kuona tena…Na siku yake ya kuuawa ilipofika alimtumia mwanamke aliyempenda kadi yenye sahihi hii…“kutoka kwa Valentino wako”. Na akenda kuuawa..siku hiyo ya February 14, mwaka 270.

Miaka mingi ilipopita ndio baadhi ya watu wakaichagua iwe ni siku ya kupelekeana kadi zenye ujumbe wa mapenzi kama Valentino alivyofanya kwa yule mwanamke kabla ya kuawa kwake.

Sasa hadithi hiyo inahusiana nini na ukristo?..Valentino kumtumia kadi mwanamke huyo sisi inatuhusu nini?..Je! nini kiliendelea baada ya pale?…hakuna anayejua wala historia haijaeleza…Hivyo ni hadithi tu ambazo hazina faida yoyote kwetu sisi kuzienzi wala kuzishika…zaidi zinatutoa kwenye mstari wa imani yetu..

Ni hadithi tu ambazo maudhui yake ni kuongeza maasi na maovu duniani..na karamu za ulafi ambazo biblia imetuonya katika..1Petro 4:3…na kuchochea uzinzi..

Siku ya wapendanao ni ipi?..Bila shaka ni kila siku, hakuna siku moja maalumu ambayo upendo unazidi Zaidi au unaenziwa!…Upendo upo kila siku… kama ni upendo halisi!..lakini kama sio upendo halisi..labda unaweza kuwa na siku yake moja maalumu ya kuongezwa nguvu inayoitwa valentine’s day..Lakini kwa wakristo wa kweli upendo ni kila siku, unabubujika kila siku, kila saa..

Kwahiyo “Valentine’s day” ni sikukuu za kipagani, ambayo lengo lake ni kuwafanya watu wazame katika ulimwengu zaidi..na kuwafanya waupenda ulimwengu Zaidi ya kumpenda Kristo. Siku hii ndio siku disko zinajaa watu, siku hii ndio siku ambayo idadi kubwa ya watu wanafanya uasherati, siku hii ndio siku ambayo idadi kubwa ya watu ndio wanakwenda kulewa pombe…Wala hata sio siku ya watu kwenda kanisani, sio siku ya watu kwenda ibadani kumwabudu Mungu au kusali…Ni siku maalumu shetani aliyoiandaa ya watu kuzama ulimwenguni kusambazo upendo bandia ambao hata watu ambao hawajaona wanapelekea kadi hizo..Sasa itakuwaje sikukuu ya kiMungu hiyo?. Ni ushujaa gani kauonyesha kwa ajili ya kanisa la Kristo mpaka siku yake ihadhimishwe?

Upendo tunaopaswa tuusambaze ni upendo wa Kristo, Na sio upendo wa Valentino.

Bwana atusaidie kwa hilo.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

Je! mtu anapofunga kwa muda wa SAA 24,anapaswa kunywa maji au kitu chochote?

MAONO YA NABII AMOSI.

KIFO CHA REINHARD BONKEY KINAACHA UJUMBE GANI KWETU?

NI NINI TUNAJIFUNZA JUU YA MT. DENIS WA UFARANSA?

JINSI MUNGU ANAVYOIPIGA NA KUIPONYA AFRIKA.

ITAFAKARI SIKU YA HUKUMU.

Mtakatifu ni Nani?

Rudi Nyumbani:

Print this post