Category Archive Home

Kwanini Mungu aliikubali sadaka ya Yeftha ya kumtoa binti yake kafara?

SWALI: Kwanini Mungu aliikubali sadaka ya Yefhta, ya kumtoa binti yake kafara? Je Mungu anakubali sadaka za kuteketeza watu?


JIBU: Kabla ya kwenda kwa Yeftha turudi kwanza kwa Ibrahimu…swali ni je! Kwanini Mungu amwambie Ibrahimu akamtoe mwanawe kama sadaka ya kuteketezwa?..Je Mungu anaziridhia sadaka za kuchinja watu na kutoa kafara?..Kwanini asingemwambia akamtoe mbuzi tu na si mwanae? Ni muhimu kufahamu nyakati na majira Mungu aliyokuwa anatembea na watu wake…Zamani sana kabla Taifa la Israeli halijazaliwa…Kulikuwa hakuna mfumo maalumu wa kumwabudu Mungu…wengi walikuwa hawajui mapenzi kamili ya Mungu..Sheria ilivyokuja ndipo angalau watu wakaanza kumwelewa Mungu anataka nini.. Hivyo kabla ya Torati watu walikuwa hawaelewi kwa mapana Mungu anataka nini na hataki nini, au anapendezwa na nini na hapendezwi na nini…

Hivyo watu pia walikuwa wanatoa sadaka za kuteketeza watu (Au kuwapitisha watu kwenye moto) wakidhani wanampendeza Mungu…hali kadhalika watu walikuwa wanajitoa hata wao wenyewe wachomwe moto kama sadaka ya kuteketezwa wakijua wanampendeza Mungu… Hivyo hata wakati wa Ibrahimu, sadaka za watu kujitoa kuteketezwa zilikuwa zinaendelea…Na hivyo hata Ibrahimu alikuwa anajua ni sawa chochote kile Mtu anaweza kukitoa kama sadaka ya kuteketezwa kwa Mungu wake…

Kwasababu sheria bado ilikuwa haijaja!..Kwasababu sheria/Torati ndio ilikuwa kuwafumbua watu macho kuelewa mambo gani Mungu hayapendi na yapi anayapenda.

Warumi 7:7 “Tusemeje, basi? Torati ni dhambi? Hasha! Walakini singalitambua dhambi ila kwa sheria; kwa kuwa singalijua kutamani, kama torati isingalisema, Usitamani”.

Na Mungu aliutumia huo huo mfumo wao wa kuteketeza watu kumjaribu Ibrahimu…Ili kupitia huo amwonyeshe kuwa yeye haridhii sadaka za kuteketezwa watu..Ndio maana unaona alimwambia Ibrahimu akamtoe mwanawe kama sadaka ya kuteketezwa…na alipokuwa anaenda hata kabla ya kumchinja mwanawe Mungu alimzuia akamwonyesha mwanakondoo pembeni…akimfundisha kuwa Sadaka za kuwachinja wanadamu kama wanyama na kuwateketeza kwenye moto hazikubali na wala hazimfurahishi….bali sadaka za wanyama ndizo anazozikubali..ndio maana hakumruhusu amchinje mwanawe badala yake alimtumia mwanakondoo ambaye alitokea pale pale alipokuwepo…

Angekuwa anapendezwa na sadaka za watu asingemzuia Ibrahimu kumchinja mwanawe. Hivyo hiyo ikawa somo kwa Ibrahimu na wanawe kutojaribu kutoa sadaka za kuteketezwa watu..kwani Mungu hazikubali hizo hata kidogo. Na ilipofika wakati wa Sheria Mungu alitoa amri kwamba watu wasiwatoe wana wao kama sadaka ni machukizo na ni dhambi..Kasome Walawi 20:1-5,

Yeremia 7:30 “Maana wana wa Yuda wametenda yaliyo maovu machoni pangu, asema Bwana; wameweka machukizo yao ndani ya nyumba hiyo, iitwayo kwa jina langu, hata kuitia unajisi.

31 Nao wamepajenga mahali palipoinuka pa Tofethi, palipo katika bonde la mwana wa Hinomu, ILI KUWATEKETEZA WANA WAO NA BINTI ZAO MOTONI; jambo ambalo mimi sikuliagiza, wala halikuingia moyoni mwangu”.

Soma tena..

Yeremia 19:4 “Kwa sababu wameniacha mimi, nao wamepafanya mahali hapa kuwa mahali pageni, nao hapa wamewafukizia uvumba miungu mingine wasiowajua, wala wao, wala baba zao, wala wafalme wa Yuda; nao wamepajaza mahali hapa damu ya wasio na hatia;

5 nao wamemjengea Baali mahali pake palipo juu, ili kuwachoma moto wana wao, wawe sadaka za kuteketezwa kwa Baali; tendo nisiloliamuru mimi, wala kulinena, wala halikuingia moyoni mwangu;”

Na mwisho..

Yeremia 32:33 “Tena wamenigeuzia visogo vyao, wala si nyuso zao; ingawa naliwafundisha, niliondoka mapema na kuwafundisha, lakini hawakusikiliza ili wapate mafundisho.

34 Bali waliweka machukizo yao ndani ya nyumba iliyoitwa kwa jina langu, ili kuinajisi.

35 Tena walijenga mahali palipoinuka kwa Baali, palipo katika bonde la mwana wa Hinomu, ILI KUWAPITISHA WANA WAO NA BINTI ZAO KATIKA MOTO KWA AJILI YA MOLEKI, JAMBO NISILOWAAGIZA; WALA HALIKUINGIA MOYONI MWANGU KWAMBA WALITENDE CHUKIZO HILO; wapate kumkosesha Yuda”.

Mistari yote hiyo Bwana anasema tendo la kuteketeza watu kwenye moto hata halikumwingia moyoni mwake kabisa..Ni machukizo kufanya vile….Ndio maana hata Mungu alimzuia Ibrahimu. Sasa pamoja na kuwepo kwa sheria hizo..Bado wana wa Israeli walikuwa wanaendelea kufanya hizo sadaka..kama Bwana anavyosema hapo juu…Sasa tukirudi kwenye Biblia ndio tunamkuta Mtu ambaye anaitwa Yeftha ambaye alizaliwa baada ya sheria hiyo kuwekwa..

Huyu Yeftha alikuwa ni Mwamuzi wa Israeli ambaye alichaguliwa na Mungu kabisa…habari zake unaweza ukazisoma kwenye kitabu cha Waamuzi, historia ya maisha yake…Lakini kuna kipindi alitaka kwenda vitani kupigana na maadui zake ambao walikuwa ni maadui pia wa Taifa zima la Israeli..mtu huyu akamwekea Mungu nadhiri…pasipo kufikiri, akamwahidi Mungu endapo akipata ushindi chochote kitakachokuja mbele yake kumlaki atakitoa kuwa sadaka ya kuteketezwa..Bila kufikiri kuwa anaweza kuja hata ndugu yake au mwanawe…na aliposhinda akaja binti yake aliyemzaa kumlaki. Na kwasababu ameshaweka nadhiri ni lazima aitimize…hivyo akampitisha mwanawe kwenye moto…

Waamuzi 11:30 “Naye Yeftha akamwekea Bwana nadhiri, akasema, Kwamba wewe utawatia wana wa Amoni mkononi mwangu kweli,

31 ndipo itakuwa ya kwamba, kile kitakachotoka katika milango ya nyumba yangu kunilaki, hapo nitakaporudi na amani kutoka kwa hao wana wa Amoni, kitu hicho kitakuwa ni cha Bwana, nami nitakisongeza kiwe sadaka ya kuteketezwa”.

Sasa utauliza Yeftha alifanya dhambi kumpitisha mwanawe motoni?..Jibu ni ndio kwasababu alikwenda kinyume na Torati ya Mungu…iliyosema “msiwatoe wana wenu kuwapitisha motoni”…

Na utauliza pia je! Asingemtoa mwanawe pia angekuwa amefanya dhambi?..Jibu ni ndio angekuwa amefanya dhambi kwasababu amemwekea Mungu nadhiri ya upumbavu ambayo ameshindwa kuitoa…

Hivyo aidha angeitoa au asingeitoa bado Yeftha alikuwa hatiani?……Ingawa Yeftha alikuwa anamambo mengi ya kujifunza kutoka kwake lakini kwa hilo lilimtia doa kama lile la mke Uria lilivyomtia doa Daudi. Na ndio maana Yeftha hakutawala muda mrefu Israeli..alitawala miaka 6 tu wakati wengine walikuwa waamuzi wa Israeli hata kwa miaka 40..yeye alikaa miaka sita tu akafa..na ndiye mwamuzi aliyetawala muda mfupi kuliko wote.. Lakini yote hayo Mungu aliyaruhusu ili sisi tujifunze kwamba tusiweke nadhiri za upumbavu..Tujihadhari na nadhiri tunazoziweka…Nadhiri tuiwekeayo tuahakikishe inakubalika na Neno la Mungu na tumeifikira kwanza kabla ya kuiweka ili tusije tukajikuta tumejiweka katika mtego…(hali kadhalika tukio lile la Yeftha pia limebeba siri nyingine juu ya Yesu Kristo). Bwana akubariki. 

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Jehanamu ni nini?

MUNGU KUSEMA NA WEWE PEKEE, HAITOSHI KUKUPA USHINDI.

SADAKA YA MALIMBUKO.

JE UNAMTHAMINI BWANA?

JE KUCHOMA MAITI NI DHAMBI?

KIFO CHA MTAKATIFU POLIKAPI (Policarp).

SAKRAMENTI NI NINI, NA JE! IPO KATIKA MAANDIKO?

Rudi Nyumbani:

Print this post

KUSUDI LA MIMI KUWEPO DUNIANI NI LIPI?

Hili ni swali ambalo lilikuwa sana katika kichwa changu kabla sijamfahamu Yesu Kristo, vilevile lipo katika vichwa vya watu wengi leo hii duniani, na nimeshaulizwa pia mara nyingi na baadhi ya watu?.. Hili swali linaibuka kutokana na jinsi watu tulivyojikuta tu ghafla tumetokea duniani bila hata ya kikao Fulani cha makubaliano, na jinsi tunavyoondoka ghafla bila hata ya taarifa zozote,.. Hapo ndipo tunajiuliza sasa maana ya Maisha ni nini? Na ni nani aliye nyuma yake?..Hivyo inatufanya kila mmoja kwa njia yake mwenyewe aanze kuchunguza na kutafiti na kujaribu kila njia na kila mbinu, ili mwisho wa siku apate jibu lake moja ambalo litampa sababu ya yeye kuwepo hapa duniani..

Hata kama ni wewe leo hii unajiuliza swali hilo, hujakosea hata kidogo kufiria hivyo, unawaza vyema kabisa.. Lakini nataka nikupe ushauri mmoja, kabla hujaanza kuchunguza kwa njia zako wewe mwenyewe embu jaribu kwanza kutafuta waliowahi kujiuliza swali kama hilo na hatua walizochukua na mwisho wao ukawaje?..Ili usije ukajikuta unarudia njia zilezile za kwao, na mwisho wa siku ukafikia pale pale walipo ukawa umepoteza muda mwingi wa utafiti ambao sio wa lazima.

Lakini leo hii nitakupa majibu ya kibiblia.. Na kitabu pekee ambacho kimetoa majibu ya maswali hayo ni kitabu cha Muhubiri..Hivyo kama unahitaji kupata jibu la swali hilo nakushauri ukisome kitabu chote kile kwa utaratibu na kwa umakini kisha utapata jibu lake mwishoni.

Aliyeandika kitabu kile ni Sulemani mwana wa Daudi, ambaye biblia inarekodi sio tu alikuwa ni mfalme mkuu sana bali pia alikuwa ni mtu mwenye Hekima kuliko watu wote waliokuwa wanaishi duniani wakati ule, na alikuwa pia ni mtu Tajiri ambaye hakukuwa na mfano wako, kabla yake na hata baada yake..

Sasa ilifikia kipindi akatamani kujua sana nini maana ya Maisha, na atafanya nini ili apate raha duniani, au apate jibu moja la uhakika kuhusu Maisha ya wanadamu,..Akasema nitajaribu kila kitu, na kila njia kwanza naanzana na Elimu, akaitafuta elimu kwa bidii, akaipata akawa na elimu kubwa ya kufahamu kila kila mnyama, na mmea, na viumbe vyote duniani (1Wafalme 4:33-34) na hekima iliyopo ndani yao, akaweza kutatua mafumbo magumu sana, akatunga mithali nyingi sana. Na akaandika vitabu vingi sana, hiyo yote ilikuwa ni kwa lengo la kupata labda jibu Fulani la Maisha pengine angegundua jambo Fulani ambalo lingemsaidia kupata kanuni rahisi ya watu kuishi duniani, au Maisha ya raha, na ya uhuru au ya furaha..lakini alipojaribu kufanya hivyo, ndivyo alivyozidi kuongezea huzuni na masikitiko anasema hivyo (Mhubiri 1:18) ..

Akasema nitajaribu wanawake..Akaenda kuoa wake 700 wazuri wanaotoka katika majumba ya kifalme tu, na Masuria 300, aangalie labda akiwa na hao atayafanya Maisha kuwa bora duniani, au ya furaha ..hilo nalo halikumletea majibu aliyokuwa anayatafuta..

Akajajiengea makasri makubwa, na kujiwekea posho ya chakula cha mwaka mzima, kila siku kwake ilikuwa ni sherehe..lakini bado hakukipata alichokuwa anakitafuta..

Akajaribu pombe, akawa anakunywa divai, lakini bado hakuna lolote aliloliona ndani yake lingeweza kufichua fumbo kubwa la maisha..akajaribu “upumbavu na wazimu” biblia inasema hivyo katika (Mhubiri 1:17), yaani mambo yote ambayo unaweza kuona ni ya kipumbavu, au wendawazimu kama vile kujitukuza, pengine kucheza dansi, n.k. lakini hakuna hata mmoja liliweza kumpa maana ya mambo yote, ..

Akajaribu kuwa na malengo makubwa akawa mfanya biashara mkubwa duniani, aione labda akishafanikiwa hapo atakipata kitu alichokuwa anakitafuta..lakini bado anasema hakukipata..

Ndipo katika dakika za mwisho, sasa katika uzee wake..Anagundua siri hii kuwa mambo yote ni ubatili, mito inapotoka ndipo huko huko inaporudi, jua linapochomozea ndipo huko huko litakuja kuchomozea tena, upepo unapovuma ndio kulekule utakaporudi kila kitu kipo katika mzunguko wake, Yule Mungu niliyeanzana naye, nitakapojitaabisha kwenda mbali naye, nitakaposema simtaki tena nataka nitafute mwenyewe akili zangu niijue ukweli wa Maisha, ndiye yule yule mwisho wa siku nitamrudia…

Unaweza Ukaona kumjua yeye kunakunyima uhuru wa kuishi..Utakwenda kutafuta unachokitaka katika moyo wako, lakini mwisho wa siku utamrudia yeye..Na hapo utakuwa umeshachelewa sana..

Ndio maana Mhubiri anamalizia kwa kusema…Jumla ya mambo yote ni UMCHE MUNGU…

Mhubiri 12:13 “Hii ndiyo jumla ya maneno; yote yamekwisha sikiwa; Mche Mungu, nawe uzishike amri zake, Maana kwa jumla ndiyo impasayo mtu.

14 Kwa maana Mungu ataleta hukumuni kila kazi, pamoja na kila neno la siri, likiwa jema au likiwa baya”.

Unaona,..Mhubiri ni mmojawapo wa waliotusaidia sisi kufanya utafiti, ili na sisi tusianze tena kupoteza muda mwingi kukimbizana na mambo ya Maisha tuanze kutafiti kwa akili zetu..tukidhani kuwa tutafika mahali Fulani paki pekee ambako wengine hawajafika kuhusu maisha,…kumbe tupo kwenye mzunguko ule ule wa zamani..

Leo hii tutamwacha Mungu tukatafute fedha, lakini tukishaiapata bado tutaona mbona hatujalipata lile kusudi lenyewe ndani yetu?..Tutamdharau Mungu tutasema tukatafute hekima yetu wenyewe…ni kweli tutafahamu vyote lakini mwisho wa siku swali litaendelea kubakia pale pale maana ya Maisha ni nini?

Jibu pekee la maana ya Maisha lipo kwa yeye aliyetuumba?

Mche yeye basi!… Na kumcha yeye ni kuingia katika kanuni yake.. Ambayo aliiweka tangu zamani kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwenguni.. Na kanuni yenyewe ndio hii..

Yohana 3:16 “Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele”.

Ukimpata Yesu Kristo, hapo pekee ndipo utakapojua maana ya Maisha ni nini.. Kwasababu yeye anakupa uzima wa milele..Ukiwa na uzima wa milele wasiwasi wako utakuwa ni nini tena?….hutakuwa na hofu yoyote, na Maisha yako yatakuwa ya amani na furaha hapa duniani sikuzote..yaliyo mbali na utumwa wa hofu za Maisha..Hofu za kuogopa kesho itakuwaje..kwasababu Sulemani ndivyo alivyosema katika ..

Mhubiri 8:6 “Kwa maana kwa kila shauri kuna wakati na hukumu; kwa sababu mashaka ya mwanadamu yaliyo juu yake ni makubwa;

7 kwa kuwa hajui yatakayokuwako; kwa maana ni nani awezaye kumweleza jinsi yatakavyokuwa?

Hivyo kama na wewe bado unatafuta maaana ya Maisha, basi leo hii fahamu kuwa jibu ndio hilo hapo juu..acha kutanga tanga, mfuate YESU, akuponye nafsi yako, akupe tumaini la uzima wa milele..Uishi kwa amani siku zako zote ulizopo hapa duniani..Kwasababu kwingine kote hutapata..na kama ukijaribu kutafuta peke yako, ukweli ni kwamba utarudi hapo hapo kwa Mungu..Na wakati huo utakuwa umeshachelewa tayari.

Ikiwa upo tayari kufanya hivyo leo..Na kwamba unataka Kristo aingie ndani ya Maisha yako, akupe tumaini hilo na amani hiyo ya wokovu..

Basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie maisha yako yote kama ilivyokuwa hata kwetu sisi. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.

AMEN.

Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.

Ukizingatia hayo Bwana atakuangazia Nuru zake za wokovu daima hadi siku ile ya mwisho.

Ubarikiwe sana

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312 Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > WHATSAPP-Group

Mada Nyinginezo:

IVUMBUE INJILI YA KRISTO KUTOKA KATIKA KILA JAMBO.

Nifanye nini ili niwe na uhakika nikifa naenda mbinguni?

KARAMA YA MUNGU NI UZIMA WA MILELE.

Ikiwa sisi tuliumbwa na Mungu,Je! Mungu aliumbwa na nani?

NITAPOKEAJE NGUVU YA KUSHINDA DHAMBI?

JE UNAMTHAMINI BWANA?

CHACHU YA MAFARISAYO NA CHACHU YA HERODE.

Rudi Nyumbani:

Print this post

NIFANYE NINI ILI NILITIMIZE KUSUDI LA MUNGU.

Kusudi la Mungu ni lipi?

Jina kuu la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe. Karibu tujifunze maneno ya uzima,

Baadhi yetu tunadhani mpaka Mungu atakapotuambia tufanye hivi au tufanye vile ndipo hapo tutakuwa na uhakika kuwa tunalolifanya ni kusudi la Mungu,… Lakini Jambo lingine ambalo pengine hatufahamu ni kuwa kila wazo au kusudi tunalolifanya liwe ni jema au ni baya..ndani yake limebeba kusudi la Mungu..Hata shetani alipoingiwa na wazo la tamaa la kuwa kama Mungu, mpaka akaleta migogoro kule mbinguni, na baadaye akatupwa huku chini duniani na kuendelea na uharibifu wake, alikuwa analitimiza kusudi la Mungu.. na ndio maana Mungu hakumuua tangu ule wakati hadi sasa..Ni kwasababu anayohuduma yake hapo, Siku atakapomaliza kusudi lote la Mungu ndipo atakapoharibiwa katika lile ziwa la Moto.

Yuda alipoingiwa na wazo la kumsaliti Bwana Yesu, Ni kweli lilikuwa ni wazo bovu lakini ndani yake, kulikuwa na kusudi la Mungu timilifu kabisa, ilikuwa ni lazima iwe vile ili Kristo asulibiwe tupate wokovu..Ipo mifano mingi ya namna hiyo katika biblia mfano Farao kuwa na moyo mgumu, Samsoni kwenda kuwapenda wanawake wa kifilisti, n.k.

Leo tutatazama tena katika maandiko, Taifa lingine ambalo Mungu alilichagua kufanya mapenzi yake ya kuyapiga mataifa, japo lilikuwa halijui kuwa linaifanya kazi ya Mungu…Na kupitia hilo ndio tutajifunza somo letu la leo.

Isaya 10:5 “Ole wake Ashuru! Fimbo ya hasira yangu, ambaye gongo lililo mkononi mwake ni ghadhabu yangu!

6 Nitamtuma juu ya taifa lenye kukufuru, nitampa maagizo juu ya watu wa ghadhabu yangu, ateke nyara, na kuchukua mateka, na kuwakanyaga kama matope ya njiani.

7 Lakini hivyo sivyo akusudiavyo mwenyewe, wala sivyo moyo wake uwazavyo; maana katika moyo wake akusudia kuharibu, na kukatilia mbali mataifa, wala si mataifa machache.

8 Maana asema, Je! Wakuu wangu si wote wafalme?”.

Kwa ufupi taifa hili la Ashuru enzi za wafalme lilikuwa ni moja katika ya mataifa matatu yenye nguvu duniani..mengineyo yakiwemo Misri, na Babeli..Ni sawa na leo Marekani, Urusi na China jinsi yalivyo na nguvu za kijenzi duniani.. Ndivyo ilivyokuwa wakati huo..

Sasa kama wewe ni msomaji wa biblia utagundua kuwa Hili taifa la Ashuru lilikuwa ni kubwa, na lenye nguvu sana kijeshi, hili ndio Mungu alilolitumia kulichukua taifa la Israeli utamwani(yale makabila yote 10), na lile moja lililosalia ndio lilikuja kuchukuliwa utumwani na babeli baadaye..

Na sio tu Israeli peke yake, hapana, bali ukisoma biblia utaona liliyapiga na mataifa mengine mengi sana..kama biblia inavyotuambia hapo sio machache. Na ni Mungu mwenyewe alilinyanyua liwe na nguvu kiasi hicho ili alitumie hilo kuyapiga hayo mataifa yote ambayo yalikuwa yanaabudu sanamu.

Lakini sasa..ukisoma kwa makini mstari wa 7 unasema.. Lakini hivyo sivyo akusudiavyo mwenyewe, wala sivyo moyo wake uwazavyo; maana katika moyo wake akusudia kuharibu…

Unaona?..moyoni mwake alikuwa hafikirii kuwa ndiye Mungu anayemtumia kulipiza kisasi, bali yeye alikuwa anafiriki kuwa anayakomesha yale mataifa yaliyokuwa hayamtii, au alikuwa anawaza kujiongezea tu himaya yake,..apate mali nyingi na mateka mengi..Hivyo akawa anafanya kwa bidii sana na kwa jinsi alivyokuwa anafanya bidii Zaidi kutaka awe ngome thabiti kwa kuyapiga mataifa ndivyo alivyokuwa analitimiza kusudi la Mungu kirahisi Zaidi pasipo yeye kujijua…

Na ndio maana Bwana Yesu alimwambia Yuda…uyatendayo uyatende upesi..(Yohana 13:27)..Yaani yale maazimio mabovu yaliyokuwa ndani yake ya kutaka apate pesa kwa kumsaliti Bwana ayafanikishe upesi kwasababu kwa kupitia hayo ataharikisha pia kusudi la Mungu lifanyike haraka..

Lakini hawa wote tunaona mwisho wao ulivyokuja kuwa mbaya..Mataifa hayo yalikuja kuangamziwa vibaya..vilevile na Yuda..

Sasa nachotaka uone ni kuwa kanuni hiyo hiyo, wakati mwingine ndiyo Mungu huwa anayoitumia hata kutimiza mapenzi yake makamilifu ndani ya watu wake.

Mungu akitaka kufanya jambo lolote jema, labda tuseme la kumwokoa mtu fulani mlevi aliyeshindakana.. kwanza ataanza atamnyanyua mtu fulani..Na mtu huyo hajui kuwa ametumwa kwa mlevi, yeye akilini mwake anaweza kufikiri labda ni mtu tu fulani pale stendi……Lakini kumbe ndani yake anakwenda kulitimiza kusudi la Mungu alilolipanga juu ya mlevi Fulani aliyeko mahali pale.

Kwamfano anaweza ukasema ngoja nitoke nikasambaze kipeperushi vya injili stendi ya mabasi..Akatoka na vitano, akawapa watu 5 kisha akaondoka zake, mmoja wa wale 5 akawa sio mkristo, akakichukua akakisoma kisha akakiacha pale pale stendi kwenye daladala..Na baada ya muda mfupi akaja mtu mwingine akakiona kwenye siti kikamvutia akakichukua akaenda nacho nyumbani..akakiweka kwenye kabati ikapitia hata miaka 2,siku moja mume wake ambaye ni mlevi ametoka bar, akiwa katika kuyatafakari Maisha yake ya dhambi, akajisema moyoni Eee Mungu, Kama wewe unanipenda mimi basi naomba unionyeshe ni nini cha kufanya..Na saa hiyo hiyo wakati anayafikiria hayo anafungua kabati lake atafute biblia anakutana na kile kipeperushi ulichokisambaza wewe miaka 2 iliyopita, na ndani yake anakutana na ujumbe ambao ulikuwa unaendana na jambo lile lile alilokuwa anamwomba Mungu…Na mlevi huyo usiku huo huo anampa Bwana Maisha yake.. Na mbingu inaandika wewe umelitimiza kikamilifu kusudi la Mungu alilokupa la kwenda kumuokoa mlevi..ingawa wewe hujui chochote kinachoendelea.

Lakini ilikuwa ni sharti kwanza wazo fulani jema liingie ndani yako, kisha kwa kupitia hilo ulitimize kusudi la Mungu ambalo ulikuwa hujui ni lipi..Huo ni mfano tu..

Kwahiyo hivyo ndivyo Mungu anavyotimiza mapenzi yake kwa kupitia watu..Hatuwezi kuijua kazi yote ya Mungu..na ndio maana biblia inatuambia..

Mhubiri 11:4 “Mwenye kuuangalia upepo hatapanda; Naye ayatazamaye mawingu hatavuna.

5 Kama vile wewe usipojua njia ya upepo ni ipi, wala jinsi mifupa ikuavyo tumboni mwake mja mzito; kadhalika HUIJUI KAZI YA MUNGU, AFANYAYE MAMBO YOTE.

6 Asubuhi panda mbegu zako, Wala jioni usiuzuie mkono wako. Kwa maana wewe hujui ni zipi zitakazofanikiwa,kama ni hii au hii,au kama zote zitafaa sawasawa”.

Hivyo sisi tukijitoa kufanya kila kitu chema kinachohusiana na kazi yake, basi huko huko ndipo atakapotimiza kusudi lake alilolipanga kwa watu wake..

Na tena tukifanya kwa bidii Zaidi ndivyo Mungu atakavyotutumia Zaidi kutimiza makusudi yake..Kwahiyo kama wewe unahubiri basi ongeza bidii Zaidi katika kuhubiri kwako, usiangalie ni matunda mangapi leo hii nimeyapata kwa Kristo au la, maadamu unachokifanya kinaleta manufaa katika ufalme wa mbinguni, endelea usianze kujiuliza uliza, je ni kweli ninafanya mapenzi ya Mungu au la..Wewe fanya tena kwa bidii sana..na huko huko Mungu atakafanya kazi zake mwenyewe..Hivyo anza sasa kutumika..kwa kile Mungu alichokukirimia.

Lakini kama wewe ni mwovu kama lilivyokuwa taifa la Babeli, na Misri na Ashuru, ambayo baadaye baada ya kumaliza kusudi la Mungu la kuyapiga mataifa mengine, nayo pia yaliharibiwa..pamoja na Yuda na ibilisi mwenyewe siku ya mwisho, ndivyo itakavyokuwa na kwako, wewe ambaye unawapiga wengine, unawadhulumu wengine, unawaibia, unawasambazia ukimwi kwa makusudi mwisho wako utafika, pengine Mungu anaweza kukutumia kuwaadhibu hao lakini na wewe hutasalimika.. Mungu atakupiga na utakwenda Jehanaumu, na kule kitengo chako kitakuwa ni kikubwa Zaidi…Ni heri ukatubu dhambi zako sasa, Ili uokolewe.

Anza kuwaza vema kuyatenda yale yampendezayo Mungu.

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

SAYUNI ni nini?

HUYU MELKIZEDEKI NI NANI?

JE UNAMTHAMINI BWANA?

VICHEKESHO NA UTANI MADHABAHUNI

Nifanye nini ili niondokane na Hofu maishani mwangu?

Utii ni nini? na ni nani tunayepaswa kumtii au kutokumtii?

NI NINI KINAKUPATA UNAPOIPUUZIA INJILI?

Rudi Nyumbani:

Print this post

MAMBO YA KWANZA YAMEKWISHA KUPITA!

Karibu tujifunze Biblia.

Hizi tabu tunazoziona na kuzipitia sasa upo wakati umewekwa zitakwisha…

Ufunuo 21:3 “Nikasikia sauti kubwa kutoka katika kile kiti cha enzi ikisema, Tazama, maskani ya Mungu ni pamoja na wanadamu, naye atafanya maskani yake pamoja nao, nao watakuwa watu wake. Naye Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao.

 4  Naye atafuta kila chozi katika macho yao, wala mauti haitakuwapo tena; wala maombolezo, wala kilio, wala maumivu hayatakuwapo tena; kwa kuwa mambo ya kwanza yamekwisha kupita.

5  Na yeye aketiye juu ya kile kiti cha enzi akasema, Tazama, nayafanya yote kuwa mapya. Akaniambia, Andika ya kwamba maneno hayo ni amini na kweli.

6  Akaniambia, Imekwisha kuwa. Mimi ni Alfa na Omega, Mwanzo na Mwisho. Mimi nitampa yeye mwenye kiu, ya chemchemi ya maji ya uzima, bure.

7  Yeye ashindaye atayarithi haya, nami nitakuwa Mungu wake, naye atakuwa mwanangu”

Magonjwa ni mambo ya kwanza..Yatapita yote!…HIV haitakuwepo kule ng’ambo, Kansa haitakuwepo, upofu hautakuwepo, kutokusikia hakutakuwepo, ulemavu wa Ngozi, akili, wala viungo hautakuwepo, vita havitakuwepo, chuki wala kuchukiwa hakutakuwepo, maadui hawatakuwepo, visasi havitakuwepo, kuteswa hakutakuwepo, kupapambana kutafuta Maisha hakutakuwepo, vifungo havitakuwepo, magereza na mahabusu hayatakuwepo kule, maumivu, huzuni, unyonge na uchungu havitakuwepo, kupanda na mwingine kuharibu hakutakuwepo,…

Ni paradiso ya furaha isiyo ya kifani…Kule hakuna vidonda tena…wala kulia, wala kupokea taarifa mbaya za misiba…wala hofu haitakuwepo tena…wala mashindano wala mateso….Hayo ni mambo ya kwanza…Furaha tutakayoipata tutakapoingia huko itaimeza uchungu wote tuliokuwa tunaupitia duniani…

Hutakuwa na muda wa kukumbuka kwamba ulishawahi kupitia tabu…Utahisi uliumbiwa tu raha tangu zamani…Furaha utakayoipata huko hutakumbuka kwamba kuna siku ulishawahi kuteseka sana ukiwa duniani kiasi cha kufa…Hutakumbuka hata kidogo..utasahau kabisa!…Utajiri utakaoupata huko hutakumbuka kwamba ulishawahi kuwa maskini duniani…Utaona kama hukuwahi kuishigi sehemu nyingine Zaidi ya hiyo hapo kabla….Ni furaha isiyoelezeka…

Tujitahidi sana tufike huko kwasababu siku za kwenda huko zimekaribia sana kulinga na unabii wa kibiblia…Siku yoyote isiyotegemewa na wengi..parapanda italia, wafu watafufuliwa kwanza wale waliokufa katika Imani na utakatifu..na sisi tuliomwamini Yesu na kuishi Maisha ya usafi tutawaona na kwa pamoja wakitoka makaburini mwao, kisha tutaungana nao..na kufumba na kufumbua miili yetu itabadilishwa na kung’aa kama ya malaika wa mbinguni..na tutanyakuliwa juu mawinguni kukutana na Bwana wetu Kristo akitungoja mawinguni ili kutupelekwa mbali sana kule juu zaidi ya nyota zote na sayari zote kwenye Mbingu za Baba yetu Mungu mwenyezi..huko tutakwenda kula mema yote Mungu aliyotuandalia…

Ni mbali sana, juu sana, yaani “mbingu, na mbingu-za-mbingu-za-mbingu” Mungu aketipo kama biblia inavyomzungumzia katika 2Nyakati 6:18 .. Huko ndiko kutakuwa makao yako wewe ambaye leo hii umedhamiria kung’ang’ana na Yesu, uliyedhamiria kusema iwe isiwe siuachi wokovu..

Lakini tusipojiandaa leo, kinyume chake tukaendelea kudumu katika mambo ya dunia hii,..tukaendelea kudumu katika uasherati, wizi, ulevi, utukanaji, ibada za sanamu, tukaendelea kuidharau Injili ya msalaba wa Yesu, halafu Unyakuo ukipita leo hatutakwenda popote na hata tukifa kabla ya unyakuo kutokea hatutafufuliwa kwenda mbinguni.

Sasa itatufaidia nini kupata majumba tele leo, kupata viwanja vyote leo, kupata wake/ waume wengi leo, kupata umaarufu wote na kisha kupata hasara ya nafsi zetu?..si ni heri niendelee tu kuwa maskini lakini nisiikose mbingu…Kwasababu kama umaskini wangu utanifanya nimsogelee Mungu Zaidi, kama utanifanya muda wangu mwingi niutumie kwa Bwana, kama utanifanya nisiwe mtu wa kula rushwa au kupokea rushwa ni heri niendelee kuwa maskini lakini niwepo miongoni mwa wale watakaokwenda na Bwana siku ile..Kwa maana najua utajiri nitakaokuwa nao kule hautalinganishwi ni utajiri wa kupita wa hapa duniani.

Kwa kumalizia mstari huo mstari hapo juu unasema..

Ufunuo 21:5  “Na yeye aketiye juu ya kile kiti cha enzi akasema, Tazama, nayafanya yote kuwa mapya. Akaniambia, Andika ya kwamba maneno hayo ni amini na kweli.

6  Akaniambia, Imekwisha kuwa. Mimi ni Alfa na Omega, Mwanzo na Mwisho. Mimi nitampa yeye mwenye kiu, ya chemchemi ya maji ya uzima, bure.

7  Yeye ashindaye atayarithi haya, nami nitakuwa Mungu wake, naye atakuwa mwanangu.

8  Bali waoga, na wasioamini, na wachukizao, na wauaji, na wazinzi, na wachawi, na hao waabuduo sanamu, na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili.”

Maji ya UZIMA YANAPATIKANA BURE…kama hujaokoka, mlango wa wokovu upo wazi sasahivi..kwasababu bado huijui baadaye yako pengine umebakisha masaa tu ya kuishi, hivyo okoka leo..pale ulipo jitenge dakika chache omba toba kwa Mungu wako kwa yote na Maisha yote ya dhambi uliyokuwa unayaishi huko nyuma..Tubu kwa kumaanisha kabisa na kwa vitendo..dhamiria kuacha kuanzia leo pombe, rushwa, sigara, zinaa, wizi, uvaaji vimini, na suruali na uwekaji wa makeup kwenye uso wako..dhamiria kuacha yote hayo na kisha katafute ubatizo sahihi ukabatizwe..kumbuka ubatizo sahihi sio wa kunyunyiziwa..kama ulinyunyiziwa basi ulifanyiwa hivyo kimakosa..hivyo unapaswa ukabatizwe tena katika ubatizo sahihi wa maji tele (Yohana 3:23) na kwa Jina la Yesu Kristo kwaajili ya ondoleo la dhambi zako (Marko 16:16, Matendo 2:38, Matendo 8:16, Matendo 19:5, na Matendo 10:48). Na Bwana mwenyewe kupitia Roho Mtakatifu atakayeingia ndani yako atakuongoza kufanya yaliyosalia yaliyo mapenzi yake.

Wote tufike mbinguni..AMEN.

Bwana akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

WALE WAZEE ISHIRINI NA WANNE (24), WANA KAZI GANI?

NGUVU YA HEKIMA NA AKILI

NINI MAANA YA UCHAWI?

Inaruhusiwa Kula nyama ya Nguruwe kwa Mkristo wa Kweli?

Petro aliambiwa na Bwana Yesu UKIONGOKA WAIMARISHE NA NDUGU ZAKO. Je! kuongoka maana yake nini?

KWANINI MAISHA MAGUMU?

LULU YA THAMANI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

Nini maana ya “Siku moja nyuani mwa Bwana ni bora kuliko siku elfu”?

SWALI: Naomba kufahamu maana ya Neno hili, maana huwa nalisoma silielewi.. (Zaburi 84:10 “Hakika siku moja katika nyua zako Ni bora kuliko siku elfu. Ningependa kuwa bawabu nyumbani mwa Mungu wangu, Kuliko kukaa katika hema za uovu”) .


JIBU: Maana yake ni kuwa ukitumia siku yako moja kikamilifu kudumu uweponi mwa Bwana, tangu jua linapochomoza mpaka pale linapozama, hujatoka katika uwepo wa Bwana, aidha upo ibadani, au kwenye maombi, au katika kuifanya kazi yake..Basi ujue mbinguni siku yako hiyo inahesabika kuwa ni bora Zaidi ya siku elfu moja kama ungekuwa penginepo..

Jaribu kufikiria siku elfu moja ni sawa na miaka karibia miwili na robo tatu…Hivyo kama ukitumia siku 7 kikamilifu uwepo mwa Bwana, basi ujue inathamani zaidi ya mtu anayehangaika huku na huko kwa miaka 19 kutafuta kitu Fulani..

Na ndio maana Daudi anamalizia kusema.. Ningependa kuwa bawabu nyumbani mwa Mungu wangu, Kuliko kukaa katika hema za uovu..Bawabu ni mfunga na mfungua milango kwenye majumba makubwa ,ni kama mlinzi wa mlangoni..zamani kazi za mabawabu ni kazi ambazo hazikuheshimika, hata sasa ni vivyo hivyo…Kwahiyo Daudi hapo anamaanisha kuwa akipata ka nafasi kidogo tu kama kale cha bawabu  katika kumtumikia Mungu..basi ataifurahia na kuishangalia kuliko angepata kazi ya maofisi  ya mashirika makubwa makubwa n.k ya watu waovu…kwasababu anajua akiitumia vizuri siku yake moja hapo, inamletea faida mara elfu katika ufalme wa mbinguni kuliko kule kwengine.

Vivyo hivyo na sisi wakristo, tukiupata ufunuo huo, hatutaona shida kudumu katika mikusanyiko yenye ibada ndefu, hatutaona shida kumtumikia Mungu kikamilifu hata kama kazi yake itatugharimu kuchomoza kwa jua hadi kuzama kwake, hata kama itaonekana ni ya kudharaulika, hatutaona uvivu kusoma mahubiri marefu kwasababu tunajua ni kwa faida yetu wenyewe ..hatutajali ni masaa mangapi yamekwenda katika kuomba..Kwasababu tunajua mwisho wake  utakuwa ni wenye thamani nyingi Zaidi ya  siku 1000.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengine:


Mada Nyinginezo:

Nini tofauti kati ya Amri, sheria na Hukumu?

JE VIBWENGO NI KWELI VIPO?

KWANINI YESU KRISTO NI MWANA WA DAUDI?

HAKIKISHA UNALIELEWA NENO.

JE UNATAMANI KUMJUA MUNGU, NA HUJUI PA KUANZIA?

 KUWAHUDUMIA MALAIKA PASIPO KUJUA.

JE ADAMU ALIKUWA NA KITOVU?

Rudi Nyumbani:

Print this post

KAMA ZILIVYOKUWA SIKU ZA NUHU NA ZA LUTU.

Luka 17:26 “Na kama ilivyokuwa siku za Nuhu, ndivyo itakavyokuwa katika siku zake Mwana wa Adamu.27 Walikuwa wakila na kunywa, walikuwa wakioa na kuolewa, hata siku ile Nuhu aliyoingia katika safina, gharika ikashuka ikawaangamiza wote.

28 Na kadhalika, kama ilivyokuwa katika siku za Lutu, walikuwa wakila na kunywa, walikuwa wakinunua na kuuza, wakipanda na kujenga;

29 lakini siku ile Lutu aliyotoka Sodoma kulinyesha moto na kibiriti kutoka mbinguni vikawaangamiza wote.

30 Hivyo ndivyo itakavyokuwa siku ile atakayofunuliwa Mwana wa Adamu”.

Kuna mambo makuu manne ya kuzingatia hapo ambayo yalikuwa yanaendelea vipindi vifupi kabla ya Mungu kumwaga ghadhabu yake juu ya wanadamu wa kipindi hicho……ambayo yatajirudia tena kipindi kifupi kabla ya kurudi kwa Bwana Yesu Kristo..

Mambo hayo ndio haya… 1) KULA na KUNYA…2) KUOA na KUOLEWA …3) KUNUNUA na KUUZA…3) KUPANDA na KUJENGA

Leo tutaangalia moja baada ya lingine na kisha tutathmini wenyewe je! Tupo siku za mwisho au la?

1.KULA na KUNYWA.

Kama tunavyojua kula sio kubaya…Lakini mlo unaozungumziwa hapa ni ule wa ulafi, haramu..kama unaondelea katika nyakati hizi..watu wanakula hata vitu visivyolika wanakula madawa ya kulevya, ni n.k..na kadhalika vinywaji vinavyozungumziwa hapo sio maji…kwasababu hakuna ubaya wowote katika kunywa maji…bali unywaji unaozungumziwa hapo ni unywaji wa pombe, Unywaji wa madawa ya kuongeza kiwango cha maasi kama vile madawa yakuongeza matiti, makalio, kuuongeza ukubwa wa sehemu za siri, madawa ya kuongeza homoni za jinsia tofauti, watu wanakunywa madawa ya kujichubua na madawa ya kuongeza hisia za kufanya uasherati n.k hayo ndiyo yaliyokuwa yanaendelea hasaa katika kipindi cha Nuhu…yaliyosababisha gharika. Na sasa teknolojia tuliyonayo imekwenda Zaidi ya hapo..

Hali ilivyokuwa kipindi cha Sodoma na Gomara ilitabiriwa kujirudia tena vile vile katika siku za mwisho, karibia sana na kuja kwa pili kwa Bwana Yesu.

2) KUOA na KUOLEWA…(walikuwa wakioa na kuolewa)

Sehemu ya pili ni kuoa na kuolewa…Kumbuka hakuna ubaya wowote wa kuwepo kwa ndoa ya mume mmoja na mke mmoja…hata hivyo watakatifu Bwana Yesu akirudi na kuwakuta wapo kanisani wanafunga ndoa iliyo halali..watanyakuliwa na kwenda na Bwana..Hivyo kuoa na kuolewa Bwana Yesu alikokuwa anakuzungumzia pale ambapo kulikuwa kunaendelea katika kipindi cha Nuhu ni ndoa za kishetani.

Na ndio hizo ni kama zifuatazo…Ndoa za jinsia moja..yaani mwanamume anamwoa mwanamume mwenzake na mwanamke anamwoa mwanamke mwenzako..hizo ndizo zilikuwa zinaendelea kipindi cha Nuhu na Sodoma na Gomora…ndio maana utaona hata wakati wa sodoma na gomora wale watu wa mji walitaka kulala na wale malaika hawakujali kuwa ni wanaume..vivyo hivyo ndoa nyingine ya kishetani ambayo Bwana Yesu alikuwa anaimaanisha pale kwamba ilikuwa inaendela kipindi cha Nuhu na Sodoma si nyingine Zaidi ya Ndoa za mitara…Yaani mwanamume mmoja anaoa wake wengi mambo hayo yalifanywa na uzao wa Kaini soma (Mwanzo 4:19)…au mwanamke mmoja anaolewa na wanaume wengi jambo ambalo sasahivi limeongezeka kwa kasi kubwa sana…huwezi kosa ukoo mmoja ukakosa mtu aliyeoa mke Zaidi ya mmoja…

Halikadhalika ndoa nyingine ya kishetani Bwana Yesu aliyoimaanisha ni ndoa ya mwanadamu na mnyama..Duniani sasa katika historia tayari kuna mataifa yameshahalalisha ndoa kati ya wanadamu na wanyama…jambo ambalo ni laajabu sana…Na Zaidi ya yote ndoa hiyo inahudhuriwa na watu wengi na kuheshimiwa… Kutimiza unabii unaosema ”watakuwa wakioa na kuolewa”…

Na ndoa nyingine ya kishetani iliyokuwa inaendelea kipindi cha Nuhu na kujirudia tena katika kipindi chetu ni ndoa ya Mwaminio kuoana na mtu asiyeamini..pamoja na mabinti wadogo kufunga ndoa na watu wa makamo makubwa kutokana na tamaa za mali, na vijana kuoa wanawake wenye umri mkubwa kwa tamaa ya mali… Yote hayo ndiyo yaliyokuwa yanaendelea kipindi cha Nuhu…na yamejirudia kwa kasi tena kipindi hichi cha siku za mwisho.

3) KUNUNUA na KUUZA…(walikuwa wakiuza na kununua)

Kununua na kuuza pia sio kubaya..Hata hivyo Bwana akija na kumkuta mtu wake anauza mkate ulio halali dukani mwake atanyakuliwa hata katika hali hiyo…Hivyo kuuza na kununu Bwana alikokuwa anakuzungumzia hapo ni kwingine..

Na huko si kwingine Zaidi ya kununua na kuuza vitu visivyompendeza Mungu, kwamfano kununua mavazi yasiyompendeza Mungu..kama nguo fupi, vimini, kununua suruali kwa wanawake…kadhalika kuuza vipodozi, kuuza lipsticks, wanja, rasta, kuuza hereni, kuuza sigara, pombe, na vitu vyote visivyofaa…Leo hii jaribu kwenda sokoni uone ni vitu vingapi vya kukosesha vinavyouzwa…utahuzunika sana…katiza kona mbili kama hutaona pombe au sigara zinauzwa, Tunaishi katika siku za mwisho..wengi hawalijui hilo kwasababu wanadhani kununua na kuuza kunakozungumziwa pale ni peremende na siagi tu..

Tumefikia hatua ambayo ukihitaji chochote kile katika hii dunia unaweza kukinunua kwa fedha. Hata watu siku hizi wanajiuza wenyewe ili kupata fedha, kama hujui fanya tathimini ya madanguro yanayokuzunguka hutaamini mambo yanayoendelea kwa siri….na wako pia wanaouza viungo vyao ili kupata fedha…wako wanaouza mpaka figo..na wengine wanauza mpaka uchawi..na wapo wanaoununua.n.k.. Na msingi huo wa kuuza na kununua ndio utakaokwenda mpaka kipindi cha dhiki kuu ambapo mpinga-kristo ataona idadi ya mauzo na manunuzi inaongezeka kwa kasi hivyo itahitajika chapa kiasi kwamba hakuna mtu atakayeweza kununua wala kuuza bila kuwa nayo.

3) KUPANDA na KUJENGA….(walikuwa wakipanda na kujenga)

Kupanda na kujenga sio vibaya…hata hivyo mkristo aliyesimama katika Imani kamilifu ya utakatifu..akiwa shambani kwake anapanda mbegu zake za mahindi atanyakuliwa tu..hata hivyo Bwana alisema siku ile wawili watakuwa shambani mmoja atatwaliwa mwingine ataachwa (Mathayo 24:40)…hivyo kupanda Kristo alikokuzungumzia kulikokuwa kunaendelea kipindi cha Nuhu ni pamoja na kupanda vitu visivyofaa (kama ilivyokuwa siku za Nuhu ndivyo itakavyokuwa siku za mwisho)…mashamba ya bangi katika mataifa mengine ni kama mboga, na hata katika mataifa kama haya yetu vilimo hivyo vinaendelea..kadhalika kujenga kunakozungumziwa sio kujenga nyumba…Ndio kupoteza muda mwingi kujenga na kumsahau Mungu kuna madhara makubwa sana lakini pia kupoteza muda kujenga Bar, kujenga kumbi za disko, kujenga casino, kujenga jengo la massage, kujenga danguro, kujenga nyumba za wazinzi na kuziita nyumba za kulala wageni, kujenga kiwanda cha pombe, na sigara n.k Ujenzi huo ndio uliokuwa unaendelea wakati wa kipindi cha Nuhu na Lutu.

Vivyo hivyo kujenga nyumba ya kuishi na kuizindika.., kujenga nyumba na kutoifanya kuwa nyumba ya sala bali kama pango la wasioamini huo pia ndio ujenzi uliokuwa unaendelea wakati wa Nuhu na Sodoma na Gomora uliosababisha ghadhabu ya Mungu kumwagwa..

Ndugu yangu yakumbuke tena maneno haya Bwana Yesu aliyoyasema… “Na kama ilivyokuwa siku za Nuhu, ndivyo itakavyokuwa katika siku zake Mwana wa Adamu”. Upewe uthibitisho gani tena kwamba tunaishi katika siku za Mwisho ndipo uamini?..

Uthibitisho ni kuwa hayo mambo miaka ya hapo kati yalikuwa hayafanyiki sana..lakini katika nyakati hizi tunaozishi, ni jambo la kawaida sana..

Bwana atusaidie sana.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengine:


Mada Nyinginezo:

MTINI, WENYE MAJANI.

MAONO YA NABII AMOSI.

Je! Ni sahihi kuoa/kuolewa na mtu uliyemzidi umri?

MIHURI SABA

Naomba kujua watakaoenda mbinguni je! ni wengi au wachache?

HATUTAACHA KUJIFUNZA NENO KILA INAPOITWA LEO.

USIMPE NGUVU SHETANI.

Rudi Nyumbani:

Print this post

NGUVU ZA MUNGU

Nguvu za Mungu ni nini?, Nguvu ya Imani ni nini? Na jinsi gani ya kupokea nguvu za Mungu..

Karibu tujifunze maswali haya machache..

NGUVU ZA MUNGU NI NINI?

Kabla ya kuelewa nguvu za Mungu ni nini, ni vizuri tukajua maana ya nguvu.. “Nguvu maana yake ni uwezo wa kufanya kitu au jambo”..Kwahiyo nguvu za Mungu ni uwezo wa Mungu kufanya mambo…Nguvu hizo zinapomwingia mtu, Mtu huyo anakuwa na uwezo wa kufanya jambo kama Mungu.

Sasa tukitazama ulimwengu tunaweza kuona vitu vilivyoumbwa..ikiwa na maana kuwa ilitumika nguvu fulani kuviumba vitu hivyo..Na hiyo ni dhahiri kuwa sio nguvu inayotokana na  chakula..kwasababu hakuna mtu mwenye misuli mikubwa anayetegemea misuli iliyotengenezwa na chakula anachokula mwenye  uwezo wa kulining’iniza jua kule juu kabisa, au kuujaza mlima kwa mawe na udongo kwa kiwango kile…Hiyo inamaanisha kuwa  ni lazima kuna nguvu nyingine imetumika kufanya hayo..isiyotokana na chakula. Sasa kuivumbua nguvu hiyo iliyoyafanya hayo yote ndio tunarudi kwenye kitabu kinachoitwa biblia kupata jibu lake.

Waebrania 11:3 “Kwa imani twafahamu ya kuwa ulimwengu uliumbwa kwa neno la Mungu, hata vitu vinavyoonekana havikufanywa kwa vitu vilivyo dhahiri”.

Kwa kupitia mstari huo tunaweza sasa kupata majibu yetu kwamba vitu vyote Mungu aliviumbwa kwa Imani. Hivyo Imani ndio Nguvu ya Mungu…Na imani ya KiMungu inaposhuka ndani yetu nasi pia tunakuwa na nguvu za kufanya makubwa kama aliyoyafanya Mungu wetu.

Na tafsiri ya Imani tunaipata katika biblia hiyo hiyo..

Waebrania 11:1 “Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana.”.

NGUVU YA IMANI

Imani ina uwezo wa kufanya mambo makubwa ambayo kwa namna ya kawaida yanaweza kuonekana kama hayawezekaniki…Biblia inasema kwa Imani mtu anaweza kuhamisha milima.(1Wakorintho 13:2)

Luka 17:6 “Bwana akasema, Kama mngekuwa na imani kiasi cha chembe ya haradali, mngeuambia mkuyu huu, Ng’oka, ukapandwe baharini, nao ungewatii”.

Mathayo 17:20 “amin, nawaambia, Mkiwa na imani kiasi cha punje ya haradali mtauambia mlima huu, Ondoka hapa uende kule; nao utaondoka; wala halitakuwako neno lisilowezekana kwenu.

NAMNA YA KUPOKEA NGUVU  ZA MUNGU.

Kama tulivyotangulia kusoma kwamba nguvu za Mungu ni IMANI, Hivyo kupokea nguvu hizo ni sawa na kusema kupokea Imani kama ile ya Mungu.

Sasa namna ya kuipata hiyo Imani ambayo ndiyo nguvu zenyewe za Mungu tunaisoma kwenye Biblia kama ifuatavyo.

Warumi 10:17 “Basi imani, chanzo chake ni kusikia; na kusikia huja kwa neno la Kristo”.

Unapolisikia  Neno la Kristo na kulitafakari na kulielewa..kiwango fulani cha Imani kinajengeka ndani yako..na ujasiri unaongezeka pia..na mtu anavyozidi kulielewa zaidi na zaidi ndivyo imani yake inavyozidi kukua zaidi na zaidi…mpaka anapofikia kiwango cha kufanya makubwa.

Hivyo Neno la Mungu ndio Biblia takatifu, na ndio Neno la Kristo…Popote panapozungumziwa Neno la Mungu ndio hilo hilo neno la Kristo, na ndio hiyo hiyo Biblia takatifu…maneno hayo matatu yasikuchanganye.

Ukiwa na nguvu hizi za Mungu za kutosha hakuna chochote kitakachoweza kukushinda kama vile kwa Mungu hakuna chochote kinachoweza kumshinda sasa…kwasababu ana nguvu nyingi.

Je unataka leo uanze kupokea Nguvu hizi za Mungu?..anza kwa kulisoma Neno hili la Kristo na kulitii…

Mathayo 11:28 “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.

29 Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu;

30 kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi”.

Ukilisoma Neno hili na kulielewa na kukata shauri la kutubu na kumfuata Yesu kwa moyo wako wote..utakuwa ndio mwanza wa kupokea Nguvu za Mungu.

Bwana akubariki sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312

jiunge na channel yetu Kwa kubofya hapa >> WHATSAPP

Mafundisho mengine:


Mada Nyinginezo:

NINI MAANA YA UCHAWI?

KWA KUWA NGUVU ZA MBINGUNI ZITATIKISIKA.

KUOTA UNAKULA CHAKULA.

NITAPOKEAJE NGUVU YA KUSHINDA DHAMBI?

HUDUMA YA (ELIFAZI, SOFARI, NA BILDADI).

NENO LA MUNGU NI TAA

TENZI ZA ROHONI

Rudi Nyumbani:

Print this post

KUOTA MAFURIKO,KUOTA MAJI MENGI,KUOTA MAWIMBI.

kuota mafuriko
Wingu la Mashahidi
KUOTA MAFURIKO,KUOTA MAJI MENGI,KUOTA MAWIMBI.
Loading
/

Naomba kufahamu Je! Kuota mafuriko ni kiashiria cha nini?

Mafuriko kazi yake si nyingine Zaidi ya kugharikisha, tofauti na mvua ambayo kazi yake ni kustawisha na kuleta mazao.. Hivyo ikiwa unaota ndoto ya namna hii mara kwa mara, au imekujia mara moja lakini kwa uzito sana, ambao sio wa kawaida basi ujue bila shaka kuwa kuna mafuriko makubwa (rohoni) yapo mbele yako, wengine utakuta wanaota mto umefurika na unataka kuwachukua, na kwa chini maji yake yanakwenda kwa kasi sana, au wengine wanaota wapo baharini na mawimbi makubwa yanakipiga chombo chao kidogo, kisha kinaanza kuyumba yumba na kuanza kuzama, wangine wanaogelewa lakini maji yanawazidia wanashindwa kuendelea mbele..n.k. Hivyo Ukikutana na ndoto yoyote inayohusiana na maji mengi(mafuriko) ujumbe wake ni mmoja, kwamba HATARI IPO MBELE YAKO..Na mafuriko hayo hayaletwi na mwingine zaidi ya shetani.

Sasa ndoto hii inalenga makundi yote mawili.

Kundi la Kwanza:Ni la watu ambao hawajamjua bado Kristo. 

Watu ambao wapo mbali na wokovu, ambao Yesu Kristo hajawabadilisha Maisha yao. Ikiwa wewe ni mmojawapo na umeota ndoto ya namna hiyo, basi ujue kuwa ni Mungu anakuonyesha, ni jinsi gani, mwisho wako utakavyokuwa,..Nataka nikuambie Sikuzote ukiwa nje ya Yesu Kristo hakuna wimbi ambalo halitakuchukua, liwe kubwa au dogo..kwasababu nyumba yako hujaijengwa juu ya mwamba ulio imara..

Sikia Yesu anachokisema…

Mathayo 7:24  “Basi kila asikiaye hayo maneno yangu, na kuyafanya, atafananishwa na mtu mwenye akili, aliyejenga nyumba yake juu ya mwamba;

25  mvua ikanyesha, MAFURIKO YAKAJA, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, isianguke; kwa maana misingi yake imewekwa juu ya mwamba.

26  Na kila asikiaye hayo maneno yangu asiyafanye, atafananishwa na mtu mpumbavu, aliyejenga nyumba yake juu ya mchanga;

27  mvua ikanyesha, MAFURIKO YAKAJA, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, ikaanguka; nalo anguko lake likawa kubwa”.

Hivyo inategemea na maisha yako yalivyo, kama wewe ni mlevi basi ujue lipo furiko la mauti ibilisi amekuandalia kukuletea katika huo huo ulevi wako.., kama wewe ni mzinzi basi jiandae na furiko lihusianalo na uzinzi wako ambalo litakuchukua na kukupeleka moja kwa moja mpaka kuzimu..Kama wewe ni mlaji rushwa, ni mwizi, ni tapeli, ni muuaji, ni mshirikina, ni mwabudu sanamu, basi jiandae na furiko la mauti mbele yako..ambalo halitakuachia kichwa wala mkia..Utakwenda moja kwa moja, na ghafla utajikuta kuzimu..kwasababu hiyo ndio nia ya shetani sikuzote..Soma Ufunuo 12:14-17

Kundi la Pili: Watu ambao wameokoka.

Ikiwa wewe upo ndani ya Kristo(Umeokoka).. na unaota ndoto zihusianazo  na mafuriko, basi ujue ni aidha Mungu anakuonyesha hatari iliyopo mbele yako, hila ulizopangiwa na ibilisi hivyo Bwana anataka akuepushe nazo..

Hivyo hapo unapaswa uongeze viwango vyako vya maombi, usiwe mvivu omba kwa bidii, na kudumu katika utakatifu..Kiasi kwamba hata wimbi lolote(mafuriko) la ibilisi likikuta katika mazingira yoyote yale basi huwezi kupepesuka kwasababu umejengwa juu ya mwamba imara Yesu Kristo..

Au namna nyingine ni Mungu anakutahadharisha, utazame vizuri hali yako ya kiroho sasa…Pengine umerudi nyuma na hiyo itakuwa kwako rahisi kuchukuliwa na mawimbi ya mafuriko hivyo unapaswa uimarishe wokovu wako usimame imara..

ZABURI 124

“1 Kama si Bwana aliyekuwa pamoja nasi, Israeli na aseme sasa, 

2 Kama si Bwana aliyekuwa pamoja nasi, Wanadamu walipotushambulia. 

3 Papo hapo wangalitumeza hai, Hasira yao ilipowaka juu yetu 

4 Papo hapo maji yangalitugharikisha, Mto ungalipita juu ya roho zetu; 

5 Papo hapo yangalipita juu ya nafsi zetu Maji yafurikayo. 

6 Na ahimidiwe Bwana; Asiyetutoa kuwa mawindo kwa meno yao. 

7 Nafsi yetu imeokoka kama ndege Katika mtego wa wawindaji, Mtego umevunjika, nasi tumeokoka. 

8 Msaada wetu u katika jina la Bwana, Aliyezifanya mbingu na nchi”.

Amen.

Je! Ungependa kuokoka leo?

Ni vizuri ukafanya maamuzi hayo haraka..Usijiangalie labda wewe ni muislamu, au ni mkristo..ikiwa Kristo yupo mbali na wewe, haijalishi ulizaliwa katika dini au la, maisha yako sikuzote yatakuwa hatarini..Leo hii sikuambii umpe YESU Maisha yako, ili kusudi kwamba hatari hizo zisikukute mbeleni..Hapana pamoja na hayo ndani ya Kristo zipo faida nyingi utazipata..Kwanza kabisa atakupa uzima wa milele, Na Pili anakupenda na anakuhitaji wewe mwana wake uliyepotea.. aliyekuumba ukae katika uwepo wake..Umfurahie yeye na yeye akufurahie wewe.

Hivyo Ikiwa upo tayari leo hii Yesu aingie ndani yako..Na umemaanisha kweli kutaka kubadilika na akuokoe Maisha yako na dhambi zako zote basi..

Basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie maisha yako yote kama ilivyokuwa hata kwetu sisi. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU  MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, . NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.

AMEN.

Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.

Ubarikiwe sana

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312

   Jiunge na magroup yetu ya whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Mada Nyinginezo:

KUOTA UPO UCHI.

BONDE LA KUKATA MANENO.

NINI KINAFUATA SIKU ILE ILE YA KUOKOKA!

UVUMILIVU WA MUNGU ULIPOKUWA UKINGOJA.

TUUTAZAME PIA MWISHO WA UJENZI WETU.

UNYAKUO.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

KWANINI WENGINE WANYAKULIWE,NA WENGINE WAACHWE?

TOA SADAKA ISIYO NA KASORO KWA BWANA.

Rudi Nyumbani:

Print this post

JINSI MUNGU ANAVYOIPIGA NA KUIPONYA AFRIKA.

Leo hii dunia nzima inaishangaa Afrika kwa mambo mawili makuu : La kwanza ni umaskini wake, na pili jinsi lilivyojikita katika mambo ya Imani . Bara pekee lenye idadi kubwa ya watu wanaoishi kwa kuamini  “mungu” kwasasa ni Afrika tu. Jambo ambalo huwezi kuliona katika bara lingine lolote duniani.

Leo hii tutaona sababu za kibiblia ni kwanini tupo hivi, ili na wewe ujue ni wapi unapopaswa usimame..katika nafasi yako Afrika.

Watu wasioamini Mungu, wala wasioisoma biblia wanatafsiri umaskini wa waafrika ni kutokana na uvivu wao, na ujinga wao, lakini ukweli ni kwamba zipo jamii zenye watu wavivu kuliko hata waafrika, lakini bado wanao maendeleo makubwa zaidi yetu,.

Vilevile licha ya biblia kutuonyesha kuwa maendeleo makubwa tangu zamani yalianzia katika bara la Afrika lakini historia pia inathibitisha hilo kwamfano yale mapiramidi yalio kule Misri, na Ethiopia hadi leo hii hakuna Uinjinia wowote umewahi kufikia ile teknolijia..Hiyo ni kuonyesha kuwa sio kwamba waafrika ni wajinga kama wanavyofikiriwa..

Lakini Biblia inatuambia kuwa ni yeye Mungu mwenyewe ndiye aliyeifanya Afrika kuwa duni kuliko mataifa yote ulimwenguni. Na hiyo yote ni kwasababu ya miungu yao na sanamu zao..Ukisoma Kitabu cha Isaya sura ya 19 chote na Ezekieli sura ya 29 vinaeleza unabii juu ya bara la Afrika. Hatuwezi kuandika aya zote hapa kwa nafasi yako unaweza ukazisoma..lakini tutaangalia baadhi ya aya..

  1. Awali ya yote biblia ilishatabiri kuwa waafrika watawaliwa.

Tusome

Isaya 19:4 “Nami nitawatoa hao Wamisri na kuwatia katika mikono ya bwana mgumu; na mfalme mkali atawatawala; asema Bwana, Bwana wa majeshi”.

Sasa kumbuka sehemu nyingine biblia inapoitaja Misri ujue inawakilisha bara zima la Afrika..

Ilishatabiri kuwa juu ya utawala wa wakoloni, wa kibepari..

  1. Vilevile ilishatabiri kuwa itachukuliwa utumwani, kama vile wana wa Israeli walivyochukuliwa utumwani:

Ezekieli 29:12 “Nami nitaifanya nchi ya Misri kuwa ukiwa, kati ya nchi zilizo ukiwa, na miji yake, kati ya miji iliyoharibika, itakuwa maganjo muda wa miaka arobaini; nami nitawatawanya Wamisri kati ya mataifa, nami nitawatapanya kati ya nchi mbalimbali.

13 Maana Bwana MUNGU asema hivi; Mwisho wa miaka arobaini nitawakusanya Wamisri, na kuwatoa katika hizo kabila za watu, ambazo walitawanyika kati yao;

14 nami nitawarejeza Wamisri walio katika hali ya kufungwa, nami nitawarudisha hata nchi ya Pathrosi, hata nchi ya kuzaliwa kwao; NA HUKO WATAKUWA UFALME DUNI.

15 UTAKUWA DUNI KULIKO FALME ZOTE; wala hautajiinua tena juu ya mataifa; nami nitawapunguza, ili wasitawale tena juu ya mataifa”.

Unabii, huo ulitimia, Afrika ilianza kuangia utumwani na kutawaliwa kuanzia karne ya 16 na mpaka kufikia karne ya 19, utumwa ulikoma, hiyo ni miaka 400 kama vile wana wa Israeli walivyokaa Misri. Na Mungu alishasema itakuwa duni kuliko mataifa yote.

Lakini Kwanini Mungu aliruhusu hivyo? Je analipiza kisasi au anawachukia waafrika?

Jibu ni hapana sura hizo mbili zinatuonyesha Mungu alimua kufanya hivyo kwa watu wa Afrika kwasababu ya miungu yao, na sanamu zao, na uchawi wao, na uganga wao, na upigaji ramli wao (Isaya 19:3), ambavyo vimefaraka naye.. aliwadhoofisha kwa makusudi ili wajue kuwa hivyo vitu haviwezi kuwasaidia na kwamba wakati umefika sasa Mungu anawahitaji waafrika wamtumike yeye.

Kama tu leo hii, Mungu ameliadhibu bara hili lakini bado unaona waganga na uchawi bado ni mwingi, angaliacha katika mafanikio yake liwe kama mabara mengine yaliyofanikiwa duniani unadhani lingekuwaje? ndio lingekuwa chanzo cha machukizo yote ya ulimwengu mzima kotekote..rohoni na mwilini…Uchawi uliokuwepo kuanzia Misri(ambayo ipo ndani ya Bara la Afrika) ulikuwa ni wa viwango vya juu sana..walikuwa na uwezo wa kubadilisha fimbo kuwa nyoka. Mungu asingeukomesha saa hii ungekuwa umefikia viwango gani?

Hivyo Mungu ametupiga ili tumgeukie yeye hiyo ndio sababu kuu..Na jambo hilo ni kweli limezaa matunda, kwasababu leo hii Neema ya Mungu kweli ipo Afrika, idadi kubwa ya watu waliomaanisha kumtafuta MUNGU ipo Afrika, Hapo ndipo Mungu alipotuponyea..

Kitendo cha sisi kuchukuliwa utumwani, na kutawaliwa na mabepari, kulitufanya sisi tumtafute Mungu wa kweli.

Soma hapa biblia inavyosema..

Isaya 19:20 “Nayo itakuwa ishara na ushuhuda kwa Bwana wa majeshi katika nchi ya Misri; kwa maana watamlilia Bwana kwa sababu ya watu wawaoneao, naye atawapelekea mwokozi mwenye kuwatetea, naye atawaokoa.

21 Na Bwana atajulikana na Misri, na Wamisri watamjua Bwana katika siku hiyo; naam watamtumikia kwa dhabihu na matoleo, nao watamwekea Bwana nadhiri, na kuzitekeleza.

22 NAYE BWANA ATAPIGA MISRI, AKIPIGA NA KUPONYA; NAO WAKIRUDI KWA BWANA, ATAKUBALI MAOMBI YAO NA KUWAPONYA.

23 Katika siku hiyo itakuwako njia kuu itokayo Misri na kufika hata Ashuru; Mwashuri atafika Misri, na Mmisri atafika Ashuru, na Wamisri wataabudu pamoja na Waashuri.

24 Katika siku hiyo Israeli atakuwa wa tatu pamoja na Misri na Ashuru, watakuwa baraka kati ya dunia;

25 kwa kuwa Bwana wa majeshi amewabariki, akisema, WABARIKIWE WATU WANGU MISRI; na wewe Ashuru, kazi ya mikono yangu; na wewe Israeli, urithi wangu”.

Unaona, Mstari wa 21 unatuambia waafrika watajulikana na Bwana, watamtumikia kwa dhabihu na matoleo.. Lakini vilevile anasema atapiga na kuponya… na mstari wa 25 Mungu anasema, WABARIKIWE WATU WANGU MISRI.

Hivyo suala la umaskini wa Afrika, limeruhusiwa kabisa kwasababu hii, ili tumrudie yeye kwasababu anatupenda..

Umaskini wetu umesababishia utajiri wa Imani kwa Mungu..na ndio maana biblia inasema..

Yakobo 2:5 “…..Je! Mungu hakuwachagua maskini wa dunia wawe matajiri wa imani na warithi wa ufalme aliowaahidia wampendao”?

Hivyo itakuwa ni jambo la kushangaza, Mungu amekuweka wewe na mimi katika nchi kama hizi, halafu bado huielewi sauti ya Mungu inataka nini kwako hutaki kuyasalimisha maisha yako kwa Bwana Yesu anayekupenda… Unaishi katika nchi ambazo utasikia injili kila kona ya barabara inahubiriwa,..lakini bado unapuuzia na kudhihaki, mataifa mengine wanaagiza wamishionari kutoka Afrika wawapelekee Neno la Mungu, lakini wewe unaichezea neema hii…Sasa hata hichi ukikikosa, ni nini basi utakuwa nacho ndugu?

Kumbuka hata hivyo neema hii nayo haitadumu huku milele, hivi karibuni Mungu atairejeza Israeli ilipoanzia, biblia inatabiri hivyo, na hapo ndipo mataifa yote ulimwenguni yataurudia upagani waliokuwa nayo mwanzoni na kwa pamoja sasa yatafanya kazi na mpinga-Kristo, ili baadaye yaje kuungana kuishambulia Israeli katika vita ile kuu ya mwisho ya Harmagedoni.. (Neema ni kama jua linachomoza upande huu na kuzama upande ule hivyo sio ya kudumu..ni kitu kinachohama..mataifa mengine Neema ya kuisikia injili haipo kabisa..yaani ile nguvu ya kuvutwa haipo…muda wao ni kama ulishapita..Na sisi muda wetu unakaribia kuisha, na neema hii itahamia Israeli..huku itakuwa kuamini injili ni ngumu kama ilivyo mataifa ya magharibi sasahivi)

Lakini sisi tulioipokea neema ya kumwamini YESU KRISTO na sio mtu mwingine yeyote, tutakuwa tumeshakwenda kwenye unyakuo kama haijahamia Israeli..Lakini wewe ambaye unaupenda ulimwengu huu, ambaye bado unaipenda miungu ya ukoo wenu, unakwenda kwa waganga, unapiga ramli, unadharau injili ya msalaba ambayo unapewa leo bure bila malipo yoyote..basi ujiandae tu na kupigwa na mkono wa Bwana kila siku, na baadaye kuishia katika ziwa la moto..

Hizi ni nyakati za hatari, na kila siku tunaona mabadiliko ya dunia..muda huu ni wa nyiongeza tu, Unyakuo ni wakati wowote, parapanda italia wafu watafufuka.. Je! Umejiweka tayari..Jibu lipo moyoni mwako.

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Mitume wote waliopita walikuwa ni watu weupe hata manabii wote waliopita hadi Ma-papa ni ngozi nyeupe. ni kweli ngozi nyeusi ililaaniwa ?

WAKAMTUKANA MUNGU, WALA HAWAKUTUBU.

MJUMBE WA AGANO.

KIFO CHA MTAKATIFU POLIKAPI (Policarp).

UVUMILIVU WA MUNGU ULIPOKUWA UKINGOJA.

JINSI ROHO MTAKATIFU ANAVYOWAFUNULIA WATU MAANDIKO.

MAONO YA NABII AMOSI.

UNYAKUO.

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

Rudi Nyumbani:

Print this post

MJUMBE WA AGANO.

Jina la Bwana wetu Yesu Kristo libarikiwe..karibu tujifunze Biblia…

Malaki 3: 1 “Angalieni, namtuma mjumbe wangu, naye ataitengeneza njia mbele yangu; naye Bwana mnayemtafuta atalijilia hekalu lake ghafula; naam, yule mjumbe wa agano mnayemfurahia, angalieni, anakuja, asema Bwana wa majeshi”

Mpango wa Mungu katika kumwokoa mwanadamu umegawanyika katika sehemu mbili..Agano la kale(au kwa lugha nyingine agano la kwanza)..pamoja na Agano jipya (au agano la pili).

Ndio ni kawaida lazima viwepo vipande viwili ili kukikamilisha kiumbe hai..Na upande mmoja lazima uwe na nguvu kuliko mwingine…Kwamfano umbile la Mtu limegawanyika katika sehemu mbili zinazofanana…Upande wa kushoto na upande wa kulia…Ndio maana utaona mtu ana miguu miwili, macho mawili, mikono miwili, n.k Na kama ukizidi kuchunguza utaona pia..katika sehemu hizo mbili kuna upande mmoja upo na uwezo mkubwa kuliko upande mwingine..ndio utaona mtu anauwezo wa kuandika vizuri kwa kutumia mkono mmoja tu, na akijaribu kutumia upande mwingine inakuwa ni shida kidogo.. kadhalika anauwezo hata wa kupiga teke kitu kwa utashi Zaidi kupitia huo huo upande anaoutumia mkono wake kuandikia n.k Lakini pande zote hizo mbili zikishirikiana kwa pamoja uwezo unakuwa mkubwa Zaidi..mtu akinyanyua kitu kwa mikono miwili anafanikiwa Zaidi kuliko anayetumia mkono mmoja. N.k

Na biblia ni hivyo hivyo imegawanyika katika sehemu kuu mbili..Agano jipya na Agano la Kale. Agano jipya lina nguvu na uwezo na utashi Zaidi kuliko agano la kale…Ingawa maagano yote mawili ni lazima yaungane ili kulitimiza kusudi la Mungu. Kama vile tusivyoweza kusema hatuhitaji mkono wa kushoto kwasababu ni dhaifu kuliko wa kulia, au hatuhitaji mguu wa kushoto kwasababu ni dhaifu kuliko wa kulia..hapana..vyote viwili vina umuhimu wake..

Sasa Agano la kale mjumbe wake alikuwa Nabii Musa..ambaye ndiye aliyepewa zile amri na sheria awahubirie wana wa Israeli. Na sheria zile zilikuwa zinaandikwa kwenye mawe, na mbao..

Musa alihubiri….Mtu hatakiwi kuzini kwasababu sheria inasema usizini!…mtu hatakiwi kuiba kwasababu sheria inasema usiibe!…Ikiwa na maana kuwa kuna maandishi fulani ya kurejea ili kuzijua amri za Mungu..Kuna mahali fulani pameandikwa kwamba USIZINI! Ndio maana watu hawapaswi kuzini.

Hilo ndio Agano la kwanza…Sheria zilikuwa zimandikwa mahali fulani.

Lakini Agano la pili ambalo mjumbe wake ni Yesu Kristo..kama maandiko yanavyosema katika..

“Waebrania 12:24 “na Yesu mjumbe wa agano jipya, na damu ya kunyunyizwa, inenayo mema kuliko ile ya Habili”.

Yeye(Yesu) sheria za Mungu haziandiki kwenye mawe na mbao na kutupa sisi kama alivyofanya Musa…bali katika vilindi vya mioyo ya watu ndiko anapoziandikia…Maana yake ni kwamba mtu akitaka kupata uhakika kwamba ulawiti ni dhambi bila hata ya kwenda kurejea kwenye maandishi yoyote…inakuwa ile sheria tayari imeshaandikwa ndani yake..Kunakuwa kuna kitu fulani kinamshuhudia ndani yake na kumfundisha kwamba ulawiti ni machukizo kwa Mungu bila hata kwenda kusoma mahali popote…yaani zile sheria za Mungu zinakuwa zinaandikwa moyoni mwake. Kunakuwa kuna masomo fulani yanatiririka ndani yake kupitia hata vitu vya asili kiasi kwamba yule mtu anauwezo wa kutenda mapenzi ya Mungu bila hata kusukumwa sukumwa wala kuwekewa sheria na taratibu, na amri fulani za kufuata kama mtoto mdogo. Anakuwa kila kitu anachokifanya anajua sababu yake.

Ni kama mtu ambaye kakomaa kiakili ambapo anajua akilowa jasho tu anahitaji kwenda kuoga na kubadilisha nguo…anakuwa hana kitabu cha baolojia mbele yake ambacho anatembea nacho na kukirejea kila siku na kutafuta mahali panaposema mtu ni lazima aoge ndipo awe msafri Yeye mwenyewe tu ndani ya akili yake kuna masomo tayari ya umuhimu wa kujiweka msafi bila hata kufundishwa na mtu. Hahitaji kitabu cha baolojia kumfundisha umuhimu wa kuoga, hahitaji kuhubiriwa hubiriwa kila kona umuhimu wa kuoga..haihitaji kukalishwa semina na kukumbushwa kumbushwa…Kwani anajua wajibu wake..kwanza yeye mwenyewe tu atajikuta anapenda kuwa msafi…Na kila siku utakuwa anazidi kutafuta kujiweka kuwa msafi.

Na ndivyo hivyo hivyo Agano jipya linavyofanya kazi… linamfanya mtu atafute kuwa msafi (yaani Mtakatifu) bila kuwekewa sheria wala kusukumwa sukumwa..linamfanya mtu aone ndani yake kwamba kuna kila sababu ya yeye kujiweka mbali na uchafu wa ulimwengu huu, kujiweka mbali na anasa, uasherati, utukanaji, usagaji, wizi…Linazidi kumfanya aone sababu ya yeye kuiogesha roho yake kila siku kwa kujifunza Neno na maombi…Agano hili halihitaji kila siku kumkumbusha mtu wajibu wake.. Wote walioingia katika agano hili wanatimiza sheria ya Kristo ndani ya mioyo yao bila shuruti. Na hiyo yote inachochewa na Roho Mtakatifu atakayeingia ndani ya mtu.

Utauliza ni wapi katika maandiko, Agano hili la sheria kuandikwa ndani ya mioyo yetu lilitabiriwa..?

Waebrania 8:8 “Maana, awalaumupo, asema Angalia, siku zinakuja, asema Bwana, Nami nitawatimizia nyumba ya Israeli na nyumba ya Yuda agano jipya;

9 Halitakuwa kama agano lile nililoagana na baba zao, Katika siku ile nilipowashika mikono yao niwatoe katika nchi ya Misri. Kwa sababu hawakudumu katika agano langu, Mimi nami sikuwajali asema Bwana.

10 Maana hili ndilo agano nitakaloagana na nyumba ya Israeli Baada ya siku zile, asema Bwana; NITAWAPA SHERIA ZANGU KATIKA NIA ZAO, NA KATIKA MIOYO YAO NITAZIANDIKA; NAMI NITAKUWA MUNGU KWAO, NAO WATAKUWA WATU WANGU.

11 Nao hawatafundishana kila mtu na jirani yake, Na kila mtu na ndugu yake, akisema, Mjue Bwana; Kwa maana wote watanijua, Tangu mdogo wao hata mkubwa wao.

12 Kwa sababu nitawasamehe maovu yao, Na dhambi zao sitazikumbuka tena.

13 Kwa kule kusema, Agano jipya, amelifanya lile la kwanza kuwa kuukuu. Lakini kitu kianzacho kuwa kikuukuu na kuchakaa ki karibu na kutoweka”

Unaona hilo ndio agano jipya!… Ukitaka kutafuta ni wapi kwenye biblia Mungu kakataza sigara ni Dhahiri kuwa agano hili bado halijakuingia ndani yako..ukitaka kutafuta ni wapi kwenye biblia nguo za kubana na suruali, na vimini, na vipodozi vimekatazwa…fahamu kuwa bado agano hili halijaingia ndani yako, ukitafuta kwenye biblia ni wamendikwa usitoe mimba ni dhambi, au usitumie madawa ya kulevya.. Ni sawa na kutafuta ndani ya kitabu cha baolojia ni wapi pamekataza watu kupiga mswaki?

Je! Unataka kuingia ndani ya hili agano leo?..Yupo Mjumbe wake…ni lazima umkubali huyo kwanza…ukimkubali huyo na akiingia ndani yako atayaondoa yote ya kale na kuyafanya yote kuwa mapya..Atazibua ufahamu wako kwa Yule ROHO MTAKATIFU atakayekupa kiasi kwamba utaona kuzishika sheria za Mungu sio ngumu..utaona kuwa mtakatifu sio kugumu…

Unaona Watoto wadogo wanavyosumbua kuoga wenyewe mpaka uwalazimishe sana..lakini mtu mzima anakuwa anaoga hata mara 3 kwa siku kwa miaka 20..na wala hachoki?..Ndivyo na wewe Yesu Kristo atakachokifanya ndani yako…Ataigeuza akili yako kwa Roho wake Mtakatifu na kuwa kama ya mtu mzima…hutatamani hata kusikia harufu ya uasherati, wala matusi, wala uchungu, wala vinyongo, wala kujichua, wala kutazama picha chafu mitandaoni, wala pombe. Na juu ya hayo atakupa uzima wa milele.

Waebrania 9:15 “Na kwa sababu hii ni MJUMBE WA AGANO JIPYA, ILI, mauti ikiisha kufanyika kwa kukomboa makosa yaliyokuwa chini ya agano la kwanza, hao walioitwa waipokee ahadi ya urithi wa milele”.

Kama unataka leo Mjumbe huyo aingia ndani yako na kukutengeneza…

Basi uamuzi unaoufanya ni wa busara sana ambao hautakaa uujutie maisha yako yote kama ilivyokuwa hata kwetu sisi. Unachopaswa kufanya, hapo ulipo, chukua muda mchache ujitenge peke yako. Kisha piga magoti, kisha fuatisha sala hii kwa Imani, ukijua kuwa Mungu yupo hapo karibu na wewe pembeni yako kukusikia..Kisha ukiwa sasa katika utulivu Sema sala hii kwa sauti.

EE MUNGU BABA, NAJA MBELE ZAKO, NIKIWA NINAJITAMBUA KUWA MIMI NI MKOSAJI NA NIMEKUTENDA DHAMBI NYINGI, NA KWAMBA NIMESTAHILI HUKUMU. LAKINI WEWE MUNGU WANGU ULISEMA KATIKA NENO LAKO KUWA WEWE NI MUNGU WA REHEMA UNAYEWAREHEMU MAELFU ELFU YA WATU WANAOKUPENDA WEWE. NA LEO HII NINAKUJA MBELE ZAKO NAHITAJI MSAMAHA WAKO NA MSAADA WAKO MUNGU WANGU, NINATUBU DHAMBI ZANGU ZOTE KWA KUMAANISHA NA KWA MOYO WANGU WOTE, .

NINAKIRI KUWA YESU KRISTO NI BWANA, NA YEYE NDIYE MWOKOZI WA HUU ULIMWENGUNI. HIVYO NAOMBA DAMU YA MWANAO TAKATIFU INISAFISHE UOVU WANGU WOTE SASA NIFANYIKE KUWA KIUMBE KIPYA KUANZIA LEO NA HATA MILELE.

ASANTE BWANA YESU KWA KUNIPOKEA NA KUNISAMEHE.

AMEN.

Sasa ikiwa umefuatisha sala hiyo kwa Imani ..Hatua iliyobakia kwako ni kuithitisha toba yako kwa Vitendo ikiwa ulikuwa unafanya mambo yote ambayo hayampendezi Mungu unayaacha na kujitenga nayo, Sasa Mungu akishaona umegeuka kwa vitendo basi toba yako anaipokea na atakuja ndani yako wakati huo huo na kufanya makao ya milele kwako. Vile vile unahitaji, kutafuta kanisa la kiroho ambalo utajumuika na wakristo wengine katika kumwambudu Mungu katika Roho na Kweli, na kujifunza biblia ili uukulie wokovu. Na vilevile ili upate ubatizo sahihi wa kuzamishwa katika maji mengi na kwa jina la YESU KRISTO kwa ajili ya ondoleo la dhambi zako.

Ubarikiwe sana.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

TOFAUTI KATI YA SHERIA YA ROHO WA UZIMA NA SHERIA YA DHAMBI NA MAUTI!

KWANINI WENGINE WANYAKULIWE,NA WENGINE WAACHWE?

WANA WA MUNGU, NA BINTI ZA WANADAMU.

Kwanini Bwana Yesu, aliruhusu yale mapepo yawaingie nguruwe?

Sanduku la Agano lilikuwa linawakilisha nini katika Agano jipya?

ANGALIA USIJE UKANG’OA NGANO KATIKATI YA MAGUGU.

MAJINI WAZURI WAPO?

JE KUPONYWA NI UTHIBITISHO WA MUNGU KUWA NA WEWE?

Rudi Nyumbani:

Print this post