Swali: Maandiko yanasema Mungu anaketi katika Nuru (1Timotheo 6:16 na Yohana 1:5) lakini yanasema tena Mungu anakaa kwenye giza (1Wafalme 8:12) Je yanajichanganya?.
Jibu: Tuisome mistari hiyo kwanza kabla ya kuingia katika ufafanuzi.
1Timetheo 6:16 “ambaye yeye peke yake hapatikani na mauti, AMEKAA KATIKA NURU ISIYOWEZA KUKARIBIWA; wala hakuna mwanadamu aliyemwona, wala awezaye kumwona. Heshima na uweza una yeye hata milele. Amina”
Tusome tena kitabu cha Wafalme..
1Wafalme 8:12 “Ndipo Sulemani akanena, Bwana alisema ya kwamba ATAKAA KATIKA GIZA NENE. 13 Hakika nimekujengea nyumba ya kukaa, iwe mahali pa makao yako milele”
1Wafalme 8:12 “Ndipo Sulemani akanena, Bwana alisema ya kwamba ATAKAA KATIKA GIZA NENE.
13 Hakika nimekujengea nyumba ya kukaa, iwe mahali pa makao yako milele”
Je biblia inajichanganya?..
Jibu ni La! Biblia haijichanganyi mahali popote kwasababu ni Neno la Mungu lililojaa nguvu na Uweza na kweli.
Tukirudi katika mistari hiyo, ukweli ni kwamba Mungu juu mbinguni aliko, hayupo katika giza wala hakai katika giza, bali yupo katika Nuru kuu isiyoweza kukaribiwa sawasawa na andiko hilo la 1Timotheo 6:16 “…ambaye yeye peke yake hapatikani na mauti, AMEKAA KATIKA NURU ISIYOWEZA KUKARIBIWA”.
Ni sawasawa na jinsi tunavyomtolea matoleo yetu… Si kwamba yeye ana uhitaji na kwamba sisi tunaweza kumwongezea kitu, au tunaweza kumwibia, kiuhalisia sisi hatuwezi kumpa kitu Mungu, kwasababu vyote tutakavyompa ni vya kwake yeye, ndiye kaviumba… vile vile hatuwezi kusema tunamwibia Mungu kwasababu vyote yeye ni vya kwake..
Lakini linapokuja suala la mahusiano yake na sisi, Mungu aliye Mkuu na mweza huwa anajishusha na wakati mwingine kujifananisha na sisi, ndio maana utaona anajiweka na yeye kama mwanadamu mwenye kuhitaji kuhudumiwa kuhudumiwa, mwenye kuhitaji kupendwa, mwenye kujengewa nyumba n.k
Sasa katika hali hiyo ya kujishusha ili kujenga mahusiano yetu sisi na yeye, huwa anahitaji kufanyiwa vitu vilivyo bora kama tu sisi tunavyoweza kuwafanyia wale tunaowaheshimu vitu vilivyo bora, ndio hapo anaagiza tumtolee vile vinavyotugharimu sadaka zisizo kilema, vile vile na tumjengee Nyumba zilizo bora kuliko zetu tunazoishi.
Sasa Mfalme Daudi pamoja na Sulemani mwanae, kwa kutambua hilo waliwaza kumjengea Mungu nyumba yenye utukufu kuliko zao walizoishi. Waliona kule Sanduku la Mungu lilipo ni kwenye “giza nene” ndani ya Mapazia (yaani mahema).. Na wakati wenyewe wanakaa kwenye nyumba za Mierezi zilizojaa marumaru na mwangaza pande zote.
Hivyo dhamiri zao zikawagusa na kusema Mungu hatakaa kwenye “mapazia kule” bali atakaa kwenye nyumba kubwa yenye utukufu na mwangaza mwingi kuliko walizokuwa wanaishi wao, Ingawa walijua kabisa kuwa Mungu kwa ukuu wake na uweza wake hawezi kujengewa nyumba na wanadamu.. lakini waliadhimia kumjengea hivyo hivyo kwasababu walimjua Mungu katika viwango vingine tofauti na wengine walivyomjua.
1Wafalme 8:26 “Sasa, Ee Mungu wa Israeli, nakusihi, ulithibitishe neno lako, ulilomwambia mtumishi wako, Daudi, baba yangu. 27 Lakini Mungu je? Atakaa kweli kweli juu ya nchi? Tazama, mbingu hazikutoshi, wala mbingu za mbingu; sembuse nyumba hii niliyoijenga! 28 Walakini uyaelekee maombi ya mtumwa wako, na dua yake, Ee Bwana, Mungu wangu, uisikilize sauti na maombi ya mtumwa wako, aombayo mbele zako leo”.
1Wafalme 8:26 “Sasa, Ee Mungu wa Israeli, nakusihi, ulithibitishe neno lako, ulilomwambia mtumishi wako, Daudi, baba yangu.
27 Lakini Mungu je? Atakaa kweli kweli juu ya nchi? Tazama, mbingu hazikutoshi, wala mbingu za mbingu; sembuse nyumba hii niliyoijenga!
28 Walakini uyaelekee maombi ya mtumwa wako, na dua yake, Ee Bwana, Mungu wangu, uisikilize sauti na maombi ya mtumwa wako, aombayo mbele zako leo”.
2Samweli 7:1 “Ikawa, mfalme alipokuwa akikaa katika nyumba yake, hapo Bwana alipomstarehesha, asiudhiwe na adui zake waliomzunguka pande zote,
2 mfalme akamwambia Nathani, nabii, Angalia sasa, mimi ninakaa katika nyumba ya mierezi, bali sanduku la Mungu linakaa ndani ya mapazia. 3 Nathani akamwambia mfalme, Haya, fanya yote yaliyomo moyoni mwako; maana Bwana yu pamoja nawe. 4 Ikawa usiku uo huo, neno la Bwana likamfikia Nathani kusema, 5 Enenda, ukamwambie mtumishi wangu, Daudi, Bwana asema hivi, Je! Wewe utanijengea nyumba, nikae ndani yake? 6 Kwa maana mimi sikukaa ndani ya nyumba, tangu siku ile niliyowatoa wana wa Israeli katika Misri, hata leo, lakini nimekaa katika hema na maskani. 7 Mahali mwote nilimokwenda na wana wa Israeli wote, je! Nimesema neno lo lote na mtu ye yote wa waamuzi wa Israeli, niliyemwagiza kuwalisha watu wangu Israeli, nikisema, Mbona hamkunijengea nyumba ya mierezi? 8 Basi, sasa, mwambie mtumishi wangu, Daudi, maneno haya, Bwana wa majeshi asema hivi, Nalikutwaa katika zizi la kondoo, katika kuwaandama kondoo, ili uwe mkuu juu ya watu wangu, juu ya Israeli; 9 nami nimekuwa pamoja nawe kila ulikokwenda, na kuwakatilia mbali adui zako wote mbele yako; nami nitakufanyia jina kuu, kama jina la wakuu walioko duniani. 10 Tena nitawaagizia mahali watu wangu Israeli, nami nitawapanda, wapate kukaa mahali pao wenyewe, wasiondolewe tena; wala wana wa uovu hawatawatesa tena, kama hapo kwanza; 11 naam, kama vilivyokuwa tangu siku ile nilipowaamuru waamuzi, wawe juu ya watu wangu Israeli; nami nitakustarehesha mbele ya adui zako wote. Tena Bwana anakuambia ya kwamba Bwana atakujengea nyumba. 12 Nawe siku zako zitakapotimia, ukalala na baba zako, nitainua mzao wako nyuma yako, atakayetoka viunoni mwako, nami nitaufanya imara ufalme wake”
2 mfalme akamwambia Nathani, nabii, Angalia sasa, mimi ninakaa katika nyumba ya mierezi, bali sanduku la Mungu linakaa ndani ya mapazia.
3 Nathani akamwambia mfalme, Haya, fanya yote yaliyomo moyoni mwako; maana Bwana yu pamoja nawe.
4 Ikawa usiku uo huo, neno la Bwana likamfikia Nathani kusema,
5 Enenda, ukamwambie mtumishi wangu, Daudi, Bwana asema hivi, Je! Wewe utanijengea nyumba, nikae ndani yake?
6 Kwa maana mimi sikukaa ndani ya nyumba, tangu siku ile niliyowatoa wana wa Israeli katika Misri, hata leo, lakini nimekaa katika hema na maskani.
7 Mahali mwote nilimokwenda na wana wa Israeli wote, je! Nimesema neno lo lote na mtu ye yote wa waamuzi wa Israeli, niliyemwagiza kuwalisha watu wangu Israeli, nikisema, Mbona hamkunijengea nyumba ya mierezi?
8 Basi, sasa, mwambie mtumishi wangu, Daudi, maneno haya, Bwana wa majeshi asema hivi, Nalikutwaa katika zizi la kondoo, katika kuwaandama kondoo, ili uwe mkuu juu ya watu wangu, juu ya Israeli;
9 nami nimekuwa pamoja nawe kila ulikokwenda, na kuwakatilia mbali adui zako wote mbele yako; nami nitakufanyia jina kuu, kama jina la wakuu walioko duniani.
10 Tena nitawaagizia mahali watu wangu Israeli, nami nitawapanda, wapate kukaa mahali pao wenyewe, wasiondolewe tena; wala wana wa uovu hawatawatesa tena, kama hapo kwanza;
11 naam, kama vilivyokuwa tangu siku ile nilipowaamuru waamuzi, wawe juu ya watu wangu Israeli; nami nitakustarehesha mbele ya adui zako wote. Tena Bwana anakuambia ya kwamba Bwana atakujengea nyumba.
12 Nawe siku zako zitakapotimia, ukalala na baba zako, nitainua mzao wako nyuma yako, atakayetoka viunoni mwako, nami nitaufanya imara ufalme wake”
Ni nini tunachoweza kujifunza katika habari hii?.
Mungu ni mkuu lakini linapokuja suala la mahusiano yetu na yake anajiweka katika nafasi kama ya Mtu, Ikiwa unaishi katika nyumba nzuri yenye marumaru na Nuru kila mahali, lakini nyumba ya Mungu kule unakoabudu ni giza jitafakari mara mbili, (hapo ni sawa na umemweka Mungu kwenye giza) usiseme Mungu ni mkuu hawezi kujengewa nyumba.. ni kweli ni mkuu lakini anawivu kama wa mwanadamu wa kawaida (Kumbukumbu 4:24).
Kama humtolei Mungu vile vinavyopendeza, ukiwaza kwamba yeye ni tajiri kaumba vyote, na hana haja na chochote, tafakari mara mbili, hata Daudi aliwaza hivyo lakini bado aliwaza kumjengea Bwana Nyumba na Mungu akambariki na kumpa jina.
Kama Kitabu chako cha kumbukumbu za kazi ni kizuri lakini biblia yako ni makaratasi yaliyo chanika chanika, tafakari mara mbili.
Kama vitabu vyako na nyaraka zako zipo sehemu safi na katika hali nzuri lakini kitabu chako cha uzima (biblia) kipo makabatini na kwenye mikoba michafu, hapo umemwekea Mungu kwenye giza nene!! Na ni dharau za hali ya juu, tafakari mara mbili. Haya ni mambo madogo tu! Lakini yanatupunguzia utukufu mwingi sana na heshima yetu nyingi sana kwa Mungu
Maran atha!
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp: Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Je Kauli ya Mungu katika Warumi 11:4 na 1Wafalme 19:18 inajichanganya?.
Je! Siku ilihesabiwaje kabla ya jua na mwezi kuumbwa?
HAMA KUTOKA GIZANI
MKUU WA ANGA.
Maneno ya mchongezi ni kama vitoweo; Nayo hushukia pande za ndani za tumbo
Rudi nyumbani
Print this post
SWALI: Katika ule mlima mrefu, aliopanda Yesu na wanafunzi wake kuomba, kwanini atokewe na Musa na Eliya na sio manabii wengine? Mfano wa Isaya au Samweli?
JIBU: Awali ya yote yeye kutokewa na wale watu halikuwa Kwa lengo lake. Bali Kwa lengo la wale wanafunzi aliokuwa nao, Ili kutimizi mambo yafuatayo.
a) Unabii wa kwanza ni ule alioutoa Musa kuwa atakuja Nabii mwingine kama yeye na kwamba watu wamsikilize..
Kumbukumbu la Torati 18:15
[15]BWANA, Mungu wako, atakuondokeshea nabii miongoni mwa ndugu zako kama nilivyo mimi; msikilizeni yeye.
Soma pia Matendo 3:22-25,. Hivyo wayahudi walikuwa na matarajio ya kuona mtu anayefanana na Musa atakayeleta Sheria mpya akija duniani, lakini akiwa na nguvu na uweza mwingi mfano wa Musa..
Ndio sababu ya Musa kutokea mbele ya wanafunzi wake, ili Mungu awathibitishie huyu ndio yule Musa aliyemnenea habari zake.
b) Lakini pia unabii uliohusu kutangulia Kwa Eliya kabla ya Kuja kwake duniani.
Wanafunzi walikuwa na dukuduku kama huyu, ndiye Kristo aliyetabiriwa au sio, na kama ndio mbona Eliya hajatangulia mbele yake tukamwona? Kwasababu waliambiwa hivyo na waandishi. Lakini sasa walipomwona Eliya mwenyewe amesimama mbele ya Yesu wakaamini lakini bado hawakuelewa..Sasa walipokuwa wanashuka ndio wakapata nguvu ya kumuulizia hilo swali.. Na hili ndio likawa jibu lake.
Mathayo 17:9-13
[9]Na walipokuwa wakishuka mlimani, Yesu aliwaagiza, akasema, Msimwambie mtu ye yote habari ya maono hayo, hata Mwana wa Adamu atakapofufuka katika wafu. [10]Wanafunzi wake wakamwuliza, wakisema, Basi kwa nini waandishi hunena ya kwamba imempasa Eliya kuja kwanza? [11]Naye akajibu, akawaambia, Kweli Eliya yuaja kwanza, naye atatengeneza yote, [12]ila nawaambia, ya kwamba Eliya amekwisha kuja, wasimtambue, lakini wakamtenda yote waliyotaka. Vivyo hivyo Mwana wa Adamu naye yuaenda kuteswa kwao. [13]Ndipo wale wanafunzi walipofahamu ya kuwa amesema nao habari za Yohana Mbatizaji.
[9]Na walipokuwa wakishuka mlimani, Yesu aliwaagiza, akasema, Msimwambie mtu ye yote habari ya maono hayo, hata Mwana wa Adamu atakapofufuka katika wafu.
[10]Wanafunzi wake wakamwuliza, wakisema, Basi kwa nini waandishi hunena ya kwamba imempasa Eliya kuja kwanza?
[11]Naye akajibu, akawaambia, Kweli Eliya yuaja kwanza, naye atatengeneza yote,
[12]ila nawaambia, ya kwamba Eliya amekwisha kuja, wasimtambue, lakini wakamtenda yote waliyotaka. Vivyo hivyo Mwana wa Adamu naye yuaenda kuteswa kwao.
[13]Ndipo wale wanafunzi walipofahamu ya kuwa amesema nao habari za Yohana Mbatizaji.
Utakumbuka kabla ya kupanda mlimani aliwaliza watu kuwa wanamzungumzia kuwa yeye ni nani? Wanafunzi wakamjibu kuwa wanasema yeye ni Eliya, wengine mmojawapo wa manabii wa Kale.n.k. Hivyo kulikuwa na utata mwingi. Lakini siku hiyo alitoa utata huo Soma.Mathayo 16:13-18.
Mitume walipoona sura za manabii wao wa kale wamesimama mbele ya Yesu, mwenye utukufu mwingi sana kupitia wao. Wakaamini yeye ni zaidi ya manabii wote wakubwa Kwa wadogo waliowahi kutokea katika historia.
Musa alikufa, lakini Eliya alipaa.
Yesu ndio mtu pekee miongoni mwa wanadamu, aliyekufa, Kisha akazikwa, kisha akafufuka.na mwisho akapaa. Kwa hiyo Ile ilikuwa ni lugha ya kinabii, kueleza hatma yake na ndio maana hata manabii Hao walikuwa wakizungumza mambo yahusuyo kufa kwake na kufufuka.(Luka 9:31).
Hizo ndio zilikuwa sababu kuu za Bwana kutokewa na manabii wale wawili na sio wengine. Na walipokuwa wanashuka Akawaambia wanafunzi wake wasimwambie mtu mpaka atakapofufuka katika wafu.
Kufunua nini?
SI wote watamwona Yesu katika kilele Cha utukufu wake, isipokuwa wale tu walio na kiu na yeye. Ambao watakuwa tayari kuwa karibu naye wakati wote mfano wa Hawa wanafunzi watatu yaani Yohana, Petro na Yakobo.
Ukimpenda Yesu tumia muda mwingi kuwepo uweponi mwake. Utamjua sana Kwa mapana na marefu yake.
Je! Umeokoka? Je unatambua kuwa hizi ni siku za mwisho na Kristo yupo mlangoni kurudi? Dalili zote zimeshatimia, unasubiri nini usimpe Bwana maisha yako, embu fanya uamuzi leo. Tubu dhambi zako, mgeukie Yesu, Unyakuo usikupite. Ikiwa utapenda upate mwongozo huo, wasiliana nasi kwa namba zetu hizi bure +255693036618 /+255789001312
Shalom
TABIA YA WAZI INAYOWATOFAUTISHA MANABII WA UONGO NA WALE WA UKWELI.
Je Eliya aliandika waraka baada ya kupaa mbinguni?
UNAWAFAHAMU MANABII WA UONGO?
Wana wa Manabii walikuwa ni watu gani?
Je! Umeona asali? Kula kadiri ya kukutosha;
KUWA MAKINI, HATUA ZA UNYAKUO ZINAENDELEA.
LAKINI MAKINDA WAWEZA KUYATWAA UWE NAYO.
Jina la Bwana Yesu litukuzwe Daima. Nakukaribisha katika kuyatafakari maneno ya Mungu.
Lipo andiko ambalo tunaweza kuona ni la kinyonge lakini linatiba kubwa sana kama tukilitumia. Embu tuone ni nini mwandishi huyu mwenye hekima aliomba Kwa Bwana
Mithali 30:7-9
[7]Mambo haya mawili nimekuomba; Usininyime [matatu] kabla sijafa. [8]Uniondolee ubatili na uongo; Usinipe umaskini wala utajiri; Unilishe chakula kilicho kadiri yangu. [9]Nisije nikashiba nikakukana, Nikasema, BWANA ni nani? Wala nisiwe maskini sana nikaiba, Na kulitaja bure jina la Mungu wangu.
Nataka uone hapo aliposema..
“Usinipe umaskini wala utajiri;”
Katika maombi yetu ni rahisi sana kumwomba Mungu asitupe Umaskini, lakini ni ngumu sana kumwomba Mungu asitupe “UTAJIRI”.. Nadhani huo ndio ukweli..
Utajiri ni Ile Hali ya kuwa na uwezo wa kumiliki au kuwa na vitu vingi.
Lakini huyu mtu hapa anamwekea Mungu mipaka katika maeneo hayo mawili, yaani Utajiri na Umaskini, Kwa lugha nyingine anamwambia Mungu sitaki UTAJIRI.. na sababu anaitoa pale “Nisije nikashiba nikakukana, Nikasema, BWANA ni nani?”
Alijua Kuna madhara ya kuwa na tamaa ya kutaka vitu vingi, mfano kuwa na mabilioni ya pesa kwenye akaunti, kuwa na mahekari ya mashamba mengi, kuwa na nyumba nyingi za kuishi na za kupanga, kuwa na magari mengi n.k. Alijua hayo ni matamanio ya Kila mwanadamu lakini alikataa kuyaomba kabisa.
Lakini Watu wengi tunaposoma huu mstari tunaelekeza mawazo yetu kwenye mambo ya Mali tu. Lakini Bwana anamaanisha pia utajiri wa kiroho.
Uchu huu wa kupata Kila kitu, kuwa na Kila kitu, umewavaa watu wengi hata watumishi wa Mungu. Labda utaona anakwenda mbele za Mungu, maombi yake na matazamio yake ni kuwa na upako kuliko watu wote, anachotaka ni Mungu ampe karama zote za Roho. Yeye naye awe Nabii, awe Mchungaji, awe mwinjilisti, awe mwalimu, awe mtume, awe na karama zote 9 za Roho. Yaani atakaposimama mimbarani watu wamwone yeye ni kama Yesu. Awe mhubiri wa Dunia nzima wa kimataifa, mwenye mafunuo mengi kuliko wote duniani, mwenye kanisa kubwa kuliko yote duniani.
Maombi ya namna hii ni maombi ya utajiri. Na mara nyingi tunapoomba hivi Bwana Huwa hatupi, kwasababu si mapenzi ya Mungu kuomba vitu vilivyo zaidi ya uwezo wetu alivyotukirimia. Kila mmoja kawekewa kipimo chake na Mungu. Na katika hicho ndio tunaomba Mungu akibariki. Lakini si kila huduma Kila karama itakuwa ni yako.
1 Wakorintho 12:28-30
[28]Na Mungu ameweka wengine katika Kanisa, wa kwanza mitume, wa pili manabii, wa tatu waalimu, kisha miujiza, kisha karama za kuponya wagonjwa, na masaidiano, na maongozi, na aina za lugha. [29]Je! Wote ni mitume? Wote ni manabii? Wote ni waalimu? Wote wanatenda miujiza? [30]Wote wana karama za kuponya wagonjwa? Wote wanena kwa lugha? Wote wafasiri?
[28]Na Mungu ameweka wengine katika Kanisa, wa kwanza mitume, wa pili manabii, wa tatu waalimu, kisha miujiza, kisha karama za kuponya wagonjwa, na masaidiano, na maongozi, na aina za lugha.
[29]Je! Wote ni mitume? Wote ni manabii? Wote ni waalimu? Wote wanatenda miujiza?
[30]Wote wana karama za kuponya wagonjwa? Wote wanena kwa lugha? Wote wafasiri?
Hivyo pale tunapokuwa na Nia ya kiasi, ndipo Mungu anapotuongezea neema, na ndio tutakapomtumikia Mungu vizuri. Hekima inatufundisha tubadilishe matamanio. Yetu kutoka katika UCHU, mpaka “kutosheka na mishahara yetu”. Na hivyo tutafanya vizuri zaidi katika huduma, karama, na utumishi wetu Kwa ujumla. Watu watasaidika na kile ulichonacho sasa, kuliko kile usichokuwa nacho unakingoja.
Nabii Eliya ambaye alikuwa ni mkuu Kwa nguvu za Mungu, lakini pamoja na hayo hata katika maombi yake alisema “Mimi SI mwema kuliko Baba zangu (1Wafalme 19:4)”akataka Bwana asitishe huduma yake. Kwasababu aliona kama kipimo kile hakustahili kupimiwa.. Hakuwa na uchu wa kiroho. Si ajabu Kwanini Mungu akamtumia Kwa viwango vikubwa namna Ile.
Bwana atusaidie tuonyeshe sasa bidii katika nafasi zetu alizotukirimia leo, zaidi vile ambavyo tunavitazamia kesho. Tutumike Kwa kadiri ya alivyotujalia.
Shalom.
Mithali 24:17 inamaana gani kusema Tengeneza kazi yako huko nje?
Aibusu midomo atoaye jawabu la haki (Mithali 24:26)
Bilauri ni nini kibiblia?(Ufunuo 21:11,22:1)
Nini maana ya Mhubiri 10:16, inaposema Ole wako, nchi, akiwa mfalme wako ni kijana?
Nini maana ya Mithali 19:21Mna hila nyingi moyoni mwa mtu; Lakini shauri la Bwana ndilo litakalosimama.
Biblia inasema askofu anapaswa awe mume wa mke mmoja! Je! Wale wasiooa kwa ajili ya injili hawawezi kuwa maaskofu?
Je unajua kuwa kama utii wako haujatimia mbele za Mungu, kuna mambo utashindwa kuyafanya?? Kama utiifu wako kwake ni mdogo basi upo hatarini sana, Kama ulikuwa hulijui hili, basi ni vizuri ukalijua leo.
Hebu tusome maandiko yafuatayo..
2Wakorintho 10:3 “Maana ingawa tunaenenda katika mwili, hatufanyi vita kwa jinsi ya mwili; 4 (maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome;) 5 tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu; na tukiteka nyara kila fikira ipate kumtii Kristo; 6 tena tukiwa tayari kupatiliza maasi yote, KUTII KWENU KUTAKAPOTIMIA”
2Wakorintho 10:3 “Maana ingawa tunaenenda katika mwili, hatufanyi vita kwa jinsi ya mwili;
4 (maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome;)
5 tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu; na tukiteka nyara kila fikira ipate kumtii Kristo;
6 tena tukiwa tayari kupatiliza maasi yote, KUTII KWENU KUTAKAPOTIMIA”
Hapo mwishoni anamalizia kwa kusema “KUTII KWENU KUTAKAPOTIMIA”. Ni wengi wanalisoma hili andiko lakini hawafiki hapo mwisho, au hata wakifika hapo mwisho basi hawatafakari vizuri maana ya maneno hayo “Kutii kwenu kutakapotimia”.
Maana yake ni kwamba kama kutii kwako mbele za Mungu hakujatimia basi HUTAWEZA KUANGUSHA NGOME, hutaweza KUANGUSHA MAWAZO YALIYOINUKA juu yako na juu ya maisha yako na familia yako na shughuli zako… kama kutii kwako hakujatimia mbele za Mungu vile vile HUTAWEZA KUTEKA NYARA, wala hutaweza KUPATILIZA MAASI yoyote yaliyoinuka kinyume chako… Kwaufupi hutaweza kabisa kushindana vita vya kiroho!!..utaishia kusumbuliwa tu na shetani na wanadamu.
Mungu anapenda UTII, Na Utii una nguvu nyingi.. Kwa jinsi tunavyoongeza viwango vyetu vya kumtii Mungu ndivyo NGUVU ZETU ZA KIROHO ZINAVYOONGEZEKA.. Na hivyo tunakuwa na uwezo mkubwa wa kumshinda Adui na hila zake na njama zake.
Lakini leo hii kama Mungu anakuambia uache dhambi hutaki kumtii unategemea vipi Uwe na Nguvu za kuangusha Ngome ndani yako?, kama Ukiambiwa ukabatizwe hutaki kutii unategemea vipi uweze kuangusha ngome za mizimu ya ukoo wenu na mababu?.
Kama unaambiwa tu uache kuvaa mavazi hayo yasiyokupasa hutaki kutii, unategemea vipi hayo maradhi ya muda mrefu na hizo shida zikuondoke????.. Kama tu kumtii Mungu ni shida utawezaje kutiisha fikra nyingine imtii Kristo? Sawasawa na hilo andiko??.
Mtii Mungu kwanza ndipo uwe na nguvu za kuwafanya wengine wamtii Kristo…Ukikosa utii kwa Mungu ndivyo unavyojimaliza mwenyewe…
Na si kumtii Mungu leo na kesho kuendelea na mambo mengine… Hapana! Bali biblia inatufundisha kuwa utii wetu unapaswa uwe endelevu ndipo tufikie kiwango cha “kutimia” kule biblia unakokusema, ndipo matokeo yatakapoonekana.
Yakobo 4:7 “Basi mtiini Mungu. Mpingeni Shetani, naye atawakimbia. 4.8 Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi. Itakaseni mikono yenu, enyi wenye dhambi, na kuisafisha mioyo yenu, enyi wenye nia mbili”.
Je umeitii Injili?, Je umeitii kazi ya Mungu na maagizo yake yote?
KUTII NI BORA KULIKO DHABIHU.
Ngome ni nini? Kwanini Mungu anafananishwa na ngome?
Utii ni nini? na ni nani tunayepaswa kumtii au kutokumtii?
Je idadi ya askari waliohesabiwa katika 1Nyakati 21:5 na 2Samweli 24:9 inajichanganya?.
SWALI: Mstari huu unamaana gani? Mithali 19:21 Mna hila nyingi moyoni mwa mtu; Lakini shauri la Bwana ndilo litakalosimama.
JIBU: Kila moyo wa mwanadamu, unamatamainio mengi, lakini uhalisia ni kwamba sio matamanio yote ni ya ukweli au yanania nzuri baadaye, kwamfano mtu atataka mali nyingi, lakini moyo wake unasema atakapopata nyumba kubwa na gari atawakomoa waliomdharau, atalipiza kisasi, atafanya anasa ,atatembea kwa majigambo, ataongeza Masuria.
Na ndio maana mengi ya malengo kama haya yawezi kusimama kwa watoto wa Mungu, kwasababu yana hila nyingi nyuma yake. Mtume Yakobo aliliweka wazi jambo hili, ni kwanini wakati mwingine hatupokei majibu ya maombi yetu alisema..
Yakobo 4:2 “Mwatamani, wala hamna kitu, mwaua na kuona wivu, wala hamwezi kupata. Mwafanya vita na kupigana, wala hamna kitu kwa kuwa hamwombi! 3 Hata mwaomba, wala hampati kwa sababu mwaomba vibaya, ili mvitumie kwa tamaa zenu”
Lakini kinyume chake anasema Shauri la Bwana ndilo litakalosimama. Maana yake ni kuwa Hekima ya Bwana inayopima haya yote imaamua cha kutoa na kutokutoa. Hivyo si matamainio yako yote unayoyaona ni mema, basi yatakuwa mema pia mbele za Mungu, mengine yana udaganyifu mwingi. Ndio maana Yeremia 17: 9 inasema “Moyo huwa mdanganyifu kuliko vitu vyote, una ugonjwa wa kufisha; nani awezaye kuujua”?
Hivyo tuombapo jambo ni busara kumalizia na kusema “Bwana mapenzi yako yatimizwe”.
Amen.
Utakapoketi kwa chakula pamoja na mtawala Mwangalie sana
JE UPANGA UMEINGIA MOYONI MWAKO?.
VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 11 (Mithali, Wimbo ulio bora, Mhubiri)
Mruba ni mdudu gani kwenye biblia?(Mithali 30:15)
JIFUNZE KUDUMU UWEPONI MWA MUNGU.
Je ni kweli Yuda hakuwa na dhambi kwa kumsaliti Bwana, kwasababu tayari ilikuwa imeshatabiriwa?
Swali: Maandiko yanatuonyesha Tera, baba yake Abramu aliishi jumla ya miaka 205 (Mwanzo 11:32) na tena yanaonyesha kuwa Tera alimzaa Abramu akiwa na miaka 70 (Mwanzo 11:26), na ukirudi kwenye Mwanzo 12:4 biblia inatuonyesha tena Abramu alitoka nchi ya Harani alipofikisha miaka 75.
Sasa ukipiga mahesabu vizuri utaona miaka aliyoishi Tera baba yake Abramu isingepaswa iwe 205, bali iwe miaka 145 yaani (70+75=145) kama Abramu aliondoka kwelii Harani baada ya kifo cha babaye! , Lakini tunaona biblia inatuambia umri wa Tera ulikuwa ni miaka 205. (Je biblia inajichanganya!)
Jibu: Jibu ni kwamba Biblia haijichanganyi na wala haijawahi kujichanganya, vinginevyo ingekuwa ni kitabu cha uongo!. Lakini tunaona maneno yaliyomo ndani ya biblia ni ya uzima tena yenye Nguvu.
Sasa tukirudi kwenye swali letu, je! Abramu alitoka Nchi ya Harani kabla au baada ya kufa baba yake? Jibu ni kwamba alitoka BAADA YA BABA YAKE KUFA!, Na si kabla!. Tunalithibitisho hilo Zaidi katika kitabu cha Matendo ya Mitume..
Matendo 7:2 “Naye akasema, Ndugu zangu na baba zangu, sikilizeni: Mungu wa utukufu alimtokea baba yetu Ibrahimu, alipokuwa katika Mesopotamia, kabla hajakaa Harani, 3 akamwambia, Toka katika nchi yako na katika jamaa zako, ukaende hata nchi nitakayokuonyesha. 4 Ndipo alipotoka katika nchi ya Wakaldayo, AKAKAA HARANI, AKATOKA HUKO BAADA YA KUFA BABAYE, Mungu akamhamisha mpaka nchi hii mnayokaa ninyi sasa.
Matendo 7:2 “Naye akasema, Ndugu zangu na baba zangu, sikilizeni: Mungu wa utukufu alimtokea baba yetu Ibrahimu, alipokuwa katika Mesopotamia, kabla hajakaa Harani,
3 akamwambia, Toka katika nchi yako na katika jamaa zako, ukaende hata nchi nitakayokuonyesha.
4 Ndipo alipotoka katika nchi ya Wakaldayo, AKAKAA HARANI, AKATOKA HUKO BAADA YA KUFA BABAYE, Mungu akamhamisha mpaka nchi hii mnayokaa ninyi sasa.
Sasa kama ni hivyo kwanini hesabu ya miaka haikai sawa..badala ya miaka 145 anaonekana kufa akiwa na miaka 205?.
Jibu ni kwamba Tera hakumzaa Abramu akiwa na miaka 70, bali maandiko yanasema alipofikisha umri wa miaka 70 akamzaa Abramu, Nahori na Harani. (watoto watatu).
Mwanzo 11:26 “Tera akaishi miaka sabini, akamzaa Abramu, na Nahori, na Harani”.
Maana yake ni kwamba watoto hawa watatu walianza kuzaliwa baada ya Tera kufikisha miaka 70, na si kwamba wote watatu walizaliwa ndani ya mwaka mmoja, bali walizaliwa katika vipindi tofauti tofauti pengine walipishana miaka mitano mitano au hata kumi kumi au hata Zaidi ya hapo, lakini Tera alipofikisha miaka 70 ndipo alipoanza kuzaa!
Sasa swali la msingi hapa ni mtoto yupi aliyekuwa wa kwanza kuzaliwa na yupi aliyekuwa wa mwisho kati ya hao watatu..
Katika hiyo Mwanzo 11:26 tunaona Abramu akitajwa wa kwanza, sasa hiyo haimaanishi kuwa yeye ndiye aliyekuwa wa kwanza kuzaliwa!!.. Orodha hiyo imetajwa kufuatia heshima ya watu hao na si ukubwa!.. Abramu ndiye aliyetukuka mbele za Mungu Zaidi ya hao ndugu zake wawili ndio maana kawekwa hapo wa kwanza..kwasababu habari inayoendelea itamhusu yeye yeye na uzao wake.. hiyo ndio sababu ya yeye kutajwa wa kwanza na si nyingine.. Lakini kuhalisia aliyekuwa mkubwa kuliko wote pale ni Harani.
Tunajuaje Harani ndiye aliyekuwa mkubwa kuliko Abramu na Nahori?…
Kwanza Abramu alisafiri na Lutu, ambaye alikuwa ni mtoto wa Harani kaka yake.. Na wakati huo tayari Lutu alikuwa mtu mzima kipindi anasafiri na Abramu (Mwanzo 12:5)… Pili Abramu na Nahori aliyetajwa wa pili kwenye orodha alimwoa mtoto wa Harani kaka yake.
Mwanzo 11:29 “Abramu na Nahori wakajitwalia wake. Jina la mkewe Abramu aliitwa Sarai, na jina la mkewe Nahori ALIITWA MILKA, BINTI HARANI, ambaye alikuwa baba wa Milka na wa Iska”.
Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba Abramu hakuwa mtoto wa kwanza wa Tera bali huenda alikuwa wa pili au wa tatu, Harani ndiye aliyekuwa wa kwanza ingawa kwenye orodha ameonekana wa mwisho…na Tera hakumzaa Abramu akiwa na miaka 70 bali akiwa na miaka 130. Na Abramu aliondoka Harani alipofikisha miaka 75 baada ya kifo cha baba yake, ambaye alikufa akiwa na miaka 205.
Je! biblia inajichanganya katika 1Petro 2:13 na Matendo 5:29.
Je Henoko aliyeenda na Mungu alikuwa ni mwana wa Kaini? (Mwanzo 4:16)
WEWE U MUNGU UONAYE.
NINI KINAFUATA SIKU ILE ILE YA KUOKOKA!
Je Ni kweli haturuhusiwi kula nyama kulingana na Isaya 66:3?
Swali: Napenda kujua je!, idadi ya Wana wa Israeli waliouawa kwa pigo kule Shitimu ilikuwa ni Elfu 23 au elfu 24?..maana sehemu moja tunaona biblia inataja watu elfu 23 (1Wakorintho 10:8) na sehemu nyingine Elfu 24, (Hesabu 25:9) je biblia inajichanganya?.
Jibu: Biblia haijichanganyi sehemu yoyote kwasababu sio kitabu cha Uongo, bali ni kitabu kilichojaa maneno ya uzima wa Mungu, na ya kweli.
Sasa ili tuielewe vizuri tuisome habari yenyewe kuanzia ule mstari wa kwanza wa kitabu hicho cha Hesabu 25
Hesabu 25:1 “Basi Israeli akakaa Shitimu, kisha watu wakaanza kuzini pamoja na wanawake wa Moabu; 2 kwa kuwa waliwaalika hao watu waende sadakani, sadaka walizowachinjia miungu yao; watu wakala chakula, wakaisujudu hiyo miungu yao. 3 Ikawa Israeli kujiungamanisha na Baal-peori; hasira za Bwana zikawaka juu ya Israeli. 4 Kisha Bwana akamwambia Musa, Watwae wakuu wote wa hao watu, ukamtungikie Bwana watu hao mbele ya jua, ili kwamba hizo hasira kali za Bwana ziwaondokee Israeli. 5 Basi Musa akawaambia waamuzi wa Israeli, Waueni kila mtu watu wake waliojiungamanisha na Baal peori. 6 Na tazama, mtu mmoja miongoni mwa wana wa Israeli akaja na kuwaletea nduguze mwanamke Mmidiani mbele ya macho ya Musa, na mbele ya macho ya mkutano wote wa wana wa Israeli, hapo walipokuwa walia mbele ya mlango wa hema ya kukutania. 7 Naye Finehasi mwana wa Eleazari, mwana wa Haruni kuhani, alipoona jambo hilo, akaondoka hapo katikati ya mkutano, akashika fumo mkononi mwake; 8 akamwandama huyo mtu wa Israeli na kuingia ndani ya hema nyuma yake, naye akawachoma wote wawili kwa fumo lake, yule mume wa Israeli na huyo mwanamke kati ya tumbo lake. Basi pigo likazuiwa kwao wana wa Israeli. 9 Nao waliokufa kwa hilo pigo walikuwa WATU ELFU ISHIRINI NA NNE HESABU YAO”
Hesabu 25:1 “Basi Israeli akakaa Shitimu, kisha watu wakaanza kuzini pamoja na wanawake wa Moabu; 2 kwa kuwa waliwaalika hao watu waende sadakani, sadaka walizowachinjia miungu yao; watu wakala chakula, wakaisujudu hiyo miungu yao.
3 Ikawa Israeli kujiungamanisha na Baal-peori; hasira za Bwana zikawaka juu ya Israeli.
4 Kisha Bwana akamwambia Musa, Watwae wakuu wote wa hao watu, ukamtungikie Bwana watu hao mbele ya jua, ili kwamba hizo hasira kali za Bwana ziwaondokee Israeli.
5 Basi Musa akawaambia waamuzi wa Israeli, Waueni kila mtu watu wake waliojiungamanisha na Baal peori.
6 Na tazama, mtu mmoja miongoni mwa wana wa Israeli akaja na kuwaletea nduguze mwanamke Mmidiani mbele ya macho ya Musa, na mbele ya macho ya mkutano wote wa wana wa Israeli, hapo walipokuwa walia mbele ya mlango wa hema ya kukutania.
7 Naye Finehasi mwana wa Eleazari, mwana wa Haruni kuhani, alipoona jambo hilo, akaondoka hapo katikati ya mkutano, akashika fumo mkononi mwake;
8 akamwandama huyo mtu wa Israeli na kuingia ndani ya hema nyuma yake, naye akawachoma wote wawili kwa fumo lake, yule mume wa Israeli na huyo mwanamke kati ya tumbo lake. Basi pigo likazuiwa kwao wana wa Israeli.
9 Nao waliokufa kwa hilo pigo walikuwa WATU ELFU ISHIRINI NA NNE HESABU YAO”
Hapa tunaona ni watu elfu 24 waliokufa kwa pigo hilo… lakini tunaona idadi nyingine tofauti ikitajwa katika kitabu cha Waraka kwa wakorintho.
1Wakorintho 10:8 “Wala msifanye uasherati, kama wengine wao walivyofanya, WAKAANGUKA SIKU MOJA WATU ISHIRINI NA TATU ELFU”.
Sasa je! Biblia inajichanganya? Jibu ni La!
Ukweli ni kwamba idadi ya waliokufa kwa pigo ni watu elfu 24 na si elfu 23 lakini kwanini Paulo katika hiyo 1Wakorintho 10:8 aseme ni elfu 23?
Ni lazima uangalie ni nini Paulo alichokuwa anajaribu kukupitisha kwa watu wa wakorintho, Lengo na Nia ya Paulo ilikuwa ni kuwaonyesha madhara ya Uasherati, jinsi unavyoweza kuleta madhara makubwa ndani ya kipindi kifupi!.
Sasa hapa Paulo anasema walianguka watu elfu 23 “KATIKA SIKU MOJA”. Ikiwa na maana kuwa huwenda lile pigo lilienda Zaidi ya “siku moja” . Huwenda lilidumu siku mbili au Zaidi ya hapo! Ndipo likakoma!.. lakini katika ile siku moja tu ya kwanza walianguka watu elfu 23 (hiyo ni idadi kubwa sana)…na idadi ya wote waliokufa mpaka siku ya mwisho pigo lilipokoma ilikuwa ni watu elfu 24.
Sasa Paulo anajaribu kuwaonya Wakorintho jinsi uasherati unavyoweza kuleta madhara makubwa ndani ya kipindi kifupi kuliko wanavyodhania, kama ilivyokuwa kwa hawa wana wa Israeli walivyozini na wanawake wa Moabu..
Ndio maana tukirudi nyuma kidogo kwenye kitabu hicho hicho, mlango ule wa 6 utaona jinsi Paulo anavyoelezea ubaya wa dhambi ya uasherati..kwamba ni mbaya Zaidi ya dhambi zote mtu anazoweza kuzifanya katika mwili…
1Wakorintho 6:15 “Je! Hamjui ya kuwa MIILI YENU NI VIUNGO VYA KRISTO? Basi nivitwae viungo vya Kristo na kuvifanya viungo vya kahaba? Hasha!
16 Au hamjui ya kuwa yeye aliyeungwa na kahaba ni mwili mmoja naye? Maana asema, Wale wawili watakuwa mwili mmoja. 17 Lakini yeye aliyeungwa na Bwana ni roho moja naye. 18 Ikimbieni zinaa. Kila dhambi aitendayo mwanadamu ni nje ya mwili wake; ILA YEYE AFANYAYE ZINAA HUTENDA DHAMBI JUU YA MWILI WAKE MWENYEWE. 19 Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, mliyepewa na Mungu? Wala ninyi si mali yenu wenyewe; 20 maana mlinunuliwa kwa thamani. Sasa basi, mtukuzeni Mungu katika miili yenu”.
16 Au hamjui ya kuwa yeye aliyeungwa na kahaba ni mwili mmoja naye? Maana asema, Wale wawili watakuwa mwili mmoja.
17 Lakini yeye aliyeungwa na Bwana ni roho moja naye.
18 Ikimbieni zinaa. Kila dhambi aitendayo mwanadamu ni nje ya mwili wake; ILA YEYE AFANYAYE ZINAA HUTENDA DHAMBI JUU YA MWILI WAKE MWENYEWE.
19 Au hamjui ya kuwa mwili wenu ni hekalu la Roho Mtakatifu aliye ndani yenu, mliyepewa na Mungu? Wala ninyi si mali yenu wenyewe;
20 maana mlinunuliwa kwa thamani. Sasa basi, mtukuzeni Mungu katika miili yenu”.
Ni nini tunajifunza?
Kikubwa tunachoweza kujifunza ni madhara ya Uasherati, wengi wanasema nikishafanya uasherati nitatubu tu!..pasipo kujua kuwa uasherati wa mara moja unaweza kuleta madhara makubwa ndani ya muda mfupi!ll…Wana wa Israeli walipomaliza kufanya dhambi hiyo ndani ya siku moja walikufa watu elfu23, nafasi ya kutubu hawakuiona..
Vile vile dhambi ya uasherati inaweza kukuharibia mambo yako mengi ndani ya siku moja. Inaweza kukuharibia maisha yako moja kwa moja ndani ya siku moja, inaweza kukupeleka kuzimu ndani ya siku moja, na inaweza kukuletea majuto makubwa ndani ya siku moja, Zaidi sana biblia inasema mtu aziniye na mwanamke hana akili kabisa.
Mithali 6:32 “Mtu aziniye na mwanamke hana akili kabisa; Afanya jambo litakalomwangamiza nafsi yake”.
Itaishindaje dhambi ya Uasherati?.. Je kwa kuomba tu? Jibu ni La!..bali kwa kuikimbia kama Yusufu alivyoikimbia..
1Wakorintho 6:18 “Ikimbieni zinaa..”
Je! Miaka Israeli waliokaa Utumwani ilikuwa mingapi? (miaka 400 au 430) kulingana na Mwanzo 15:13 na Kutoka 12:40-42?, Je biblia inajichanganya?
Uasherati wa Kiroho maana yake nini?
Nini Tofauti kati ya uzinzi na uasherati ?
Nini maana ya siku moja kwa Bwana ni kama miaka elfu, na miaka elfu ni kama siku moja? (2Petro 3:8)
Kipaku ni nini kama tunavyosoma katika biblia?
Mhubiri 10:16 “Ole wako, nchi, akiwa mfalme wako ni kijana, Na wakuu wako hula asubuhi!”
Mstari huu umegawanyika katika sehemu mbili;
Hapo mhubiri anajaribu kueleza uhusiano uliopo kati ya uongozi na ukomavu wa mtu. Akatumia mfano wa kijana, kwasababu mara nyingi ni ngumu sana kuipata busara kwa vijana, kutokana na kuwa hawana uzoefu mwingi wa maisha na pia hawajaandaliwa vya kutosha, kumudu nafasi za uongozi, kinyume chake kitakachowaongoza ni hisia tu za ujana na si vinginevyo. Na ndio maana mtu kama Sulemani alilitambua hilo alipotawadhwa tu mfalme akiwa bado kijana mdogo, alimwomba Mungu ampe hekima ya namna ya kuwaongoza watu wake. Na Bwana akamjalia.
1Wafalme 3:7 “Na sasa, Ee Bwana, Mungu wangu, umenitawaza niwe mfalme mimi mtumwa wako badala ya Daudi baba yangu; nami ni mtoto mdogo tu; sijui jinsi inipasavyo kutoka wala kuingia. 8 Na mtumwa wako yu katikati ya watu wako uliowachagua, watu wengi wasioweza kuhesabiwa, wala kufahamiwa idadi yao, kwa kuwa ni wengi. 9 Kwa hiyo nipe mimi mtumwa wako moyo wa adili niwahukumu watu wako, na kupambanua mema na mabaya; maana ni nani awezaye kuwahukumu hawa watu wako walio wengi? 10 Neno hili likawa jema machoni pa Bwana, ya kuwa Sulemani ameomba neno hili”
1Wafalme 3:7 “Na sasa, Ee Bwana, Mungu wangu, umenitawaza niwe mfalme mimi mtumwa wako badala ya Daudi baba yangu; nami ni mtoto mdogo tu; sijui jinsi inipasavyo kutoka wala kuingia.
8 Na mtumwa wako yu katikati ya watu wako uliowachagua, watu wengi wasioweza kuhesabiwa, wala kufahamiwa idadi yao, kwa kuwa ni wengi.
9 Kwa hiyo nipe mimi mtumwa wako moyo wa adili niwahukumu watu wako, na kupambanua mema na mabaya; maana ni nani awezaye kuwahukumu hawa watu wako walio wengi? 10 Neno hili likawa jema machoni pa Bwana, ya kuwa Sulemani ameomba neno hili”
Walikuwepo pia wafalme wengine waliotawadhwa wakiwa wadogo kama Yoashi, lakini akasaidiwa na kuhani Yehoyada katika ufalme wake, na ukawa bora (2Wafalme 11-12)
Lakini tunakuja kuona kwa mwanawe Sulemani aliyeitwa Rehoboamu. Yeye naye alikuwa ni kijana lakini hakutaka mashauri kwa wazee waliomtangulia, kinyume chake, akasikiliza mashauri ya vijana wenzake Hivyo ikapelekea ufalme wake kugawanyika, na kupoteza makabila kumi kati ya kumi na mbili ya Israeli.(Soma 1Wafalme 12:1-16)
Maana yake kwamba kuwa na viongozi ambao wanatanguliza maslahi yao kabla ya kazi, nchi hiyo sikuzote huishia pabaya. Sikuzote watu wanakwenda kufanya kazi asubuhi, wakitarajia kile walichokihangaikia kutwa nzima ndio wakifaidi jioni, lakini hapa tunaona ni kinyume chake. Na jambo hili ni kweli, Tunaona katika baadhi ya mataifa yanayoendelea, wananchi wao wanapitia katika taabu, na umaskini wa hali ya juu, kutokana na kuwa viongozi wao, wanatazama maslahi yao binafsi wanapoingia madarakani na sio maslahi ya taifa.. Uchu wa madaraka na ukuu, ndio wanachokitazama lakini sio kujenga mataifa yao.
Hii inafunua nini rohoni?
Neno hili linawahusu, watumishi wote wa Mungu wanaosimama katika ngazi za uongozi. Ikiwa wewe bado ni kijana au mchanga katika huduma(hata kama una-mvi) na umepewa kundi ulichunge, Omba sana hekima kwa Mungu, pia kuwa tayari kujifunza kwa waliokutangulia, Sikuzote viongozi-wachanga, katika hatua za awali wanajiamini kuwa wanajua kila kitu, lakini kwa jinsi siku zinavyozidi kwenda ndivyo wanavyotambua kasoro zao nyingi. Hivyo ili kuepuka, kufanya makosa ya kiutumishi, tafuta sana msaada kwa Mungu katika hekima na mashauri.
Lakini pia, ikiwa wewe ni mchungaji, askofu, mtume, mwalimu, au unatumika katika huduma yoyote, epuka tamaa hususani ya mali. Si kila shilingi unayoipata uipeleke tumboni, au kujijengea majumba na biashara. Ni heri ukatazama kwanza hali ya kanisa la Kristo. Kama mchungaji mwema yakupasa kuipendezesha kwanza nyumba ya Bwana, kisha Baadaye Bwana mwenyewe ndio akupendezeshe wewe. Unatembelea gari ya Tsh milioni 40, halafu kanisa ni la makuti, Hapo ni nini unategemea kama sio ufukara wa kiroho hadi kimwili baadaye.
Kwahiyo hekima hizi zinatuonya, ili uongozi wetu usianguke mbeleni, hivyo tuzingatie sana maneno haya ya hekima. Bwana akubariki.
NJIA YA ‘UTAJIRI MKUU’ KWA KIJANA.
Je ile nyota ya asubuhi inamwakilisha shetani au Bwana Yesu?
VIJANA NA MAHUSIANO.
Bwana Yesu alikufa akiwa na umri gani?
Vifungu vya biblia kuhusu Uongozi.
NITAJUAJE KAMA MAOMBI YANGU YAMEFIKA (YAMEJITOSHELEZA)?
Makerubi wenye sura nne, ni kweli wapo? na je! wanyama wataenda mbinguni?
Swali: Tukisoma Marko 6:8, tunaona Bwana Yesu anawaruhusu wanafunzi wake “wabebe fimbo”, lakini tukirejea katika Mathayo 10:10 tunasoma habari tofauti, Bwana Yesu anawakataza wasibebe chochote hata fimbo..sasa mwandishi yupi yupo sahihi na yupi hayupo sahihi? Je biblia inajichanganya yenyewe?.
Jibu: Biblia kamwe haijichanganya mahali popote, vinginevyo kitabu kizima kitakuwa ni cha uongo!. Lakini kama ni kitabu cha kweli kilichojaa maneno ya kweli ya uzima, na Roho Mtakatifu basi hakiwezi kuwa kitabu cha ushuhuda wa uongo!, au unaochanganya!..kinachochanganyikiwa ni fahamu zetu katika kukielewa kitabu hicho, lakini chenyewe kama chenyewe hakina kasoro yoyote.
Awali ya yote tuisome mistari hiyo…
Marko 6:7 “Akawaita wale Thenashara, akaanza kuwatuma wawili wawili, akawapa amri juu ya pepo wachafu; 8 akawakataza wasichukue kitu cha NJIANI ISIPOKUWA FIMBO TU; wala mkate, wala mkoba, wala pesa za bindoni; 9 lakini wajifungie viatu; akasema, Msivae kanzu mbili”.
Marko 6:7 “Akawaita wale Thenashara, akaanza kuwatuma wawili wawili, akawapa amri juu ya pepo wachafu;
8 akawakataza wasichukue kitu cha NJIANI ISIPOKUWA FIMBO TU; wala mkate, wala mkoba, wala pesa za bindoni;
9 lakini wajifungie viatu; akasema, Msivae kanzu mbili”.
Hapa ni kweli tunaona Bwana anawaambia wasibebe chochote ila Fimbo tu!… Tusome tena habari hiyo katika kitabu cha Mathayo..
Mathayo 10:7 “Na katika kuenenda kwenu, hubirini, mkisema, Ufalme wa mbinguni umekaribia. 8 Pozeni wagonjwa, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, toeni pepo; mmepata bure, toeni bure. 9 Msichukue dhahabu, wala fedha, wala mapesa mishipini mwenu; 10 wala mkoba wa safari, wala kanzu mbili, wala viatu, WALA FIMBO; maana mtenda kazi astahili posho lake”.
Mathayo 10:7 “Na katika kuenenda kwenu, hubirini, mkisema, Ufalme wa mbinguni umekaribia.
8 Pozeni wagonjwa, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, toeni pepo; mmepata bure, toeni bure.
9 Msichukue dhahabu, wala fedha, wala mapesa mishipini mwenu;
10 wala mkoba wa safari, wala kanzu mbili, wala viatu, WALA FIMBO; maana mtenda kazi astahili posho lake”.
Hapa tunaona Bwana anawakataza hata Fimbo wasibebe, na ilihali kule kwenye kitabu cha Marko tunaona anawaambia wasibebe kitu kingine chochote isipokuwa Fimbo tu!.. Sasa mwandishi yupi ni wa kweli na yupi ni wa uongo?.
Jibu ni kwamba waandishi wote ni wa kweli hakuna aliye mwongo!,
Katika Marko Bwana anawaambia wasibebe vitu vya njiani isipikuwa FIMBO TU!.. Sasa fimbo hakikuwa chakula bali ni kifaa kinachomwezesha mtu kutembea katika milima na mabonde! Ni kama tu kiatu kilivyo msaada kwa miguu katika safari ndefu za miiba na mavumbi.. Fimbo na yenyewe ilikuwa ni hivyo hivyo..
Kwahiyo fimbo ilikuwa ni sehemu ya kitu cha msingi mtu anachoweza kuwa nacho kwa safari kama tu vile mtu alivyo na kanzu au kiatu au nguo.
Lakini sasa Bwana alichowakataza ni wao kubeba fimbo ya pili au ya tatu, kana Kamba moja ikivunjika basi kutakuwepo na akiba. Hicho ndicho kitu Bwana alichowakataza akawaambia wabebe fimbo moja tu!. Wasihofie endapo hiyo waliyonayo itapata itilafu, kwani huko wanakokwenda Mungu wa mbinguni atawafungulia mlango watapata nyingine.
Lakini pia sio Fimbo tu!, bali hata kanzu!.. wasibebe na kujifungasha mizigo ya kanzu nyingi, waende na hiyo moja tu iliyopo mwilini kwasababu huko waendako Baba yao wa mbinguni anajua kuwa wana haja na nazo, hivyo wasitie wasiwasi kwasababu mtenda kazi amestahili posho yake (watapata huko waendako). Ndio maana akawakataza wasibebe kanzu mbili…
Marko 6:8 “akawakataza wasichukue kitu cha NJIANI ISIPOKUWA FIMBO TU; wala mkate, wala mkoba, wala pesa za bindoni; 9 lakini wajifungie viatu; akasema, MSIVAE KANZU MBILI”.
Marko 6:8 “akawakataza wasichukue kitu cha NJIANI ISIPOKUWA FIMBO TU; wala mkate, wala mkoba, wala pesa za bindoni;
9 lakini wajifungie viatu; akasema, MSIVAE KANZU MBILI”.
Hapo mwisho anasema “msivae kanzu mbili” maana yake ile moja waliyonayo mwilini inatosha.. vile vile wasibebe fimbo nyingine ya pili, hiyo moja watakayokuwa nayo inatosha!..sawasawa na hiyo Mathayo 10:10..
Kwahiyo biblia haijichanganyi, bali shetani ndiye anayetuchanganya….
Sasa kufahamu ni somo gani tunaloweza kujifunza nyuma ya hii habari fungua hapa>>> Bwana alimaanisha nini kusema“maana mtenda kazi astahili posho lake”
Je suruali ni vazi la kiume tu?
Ni kwa namna gani Yesu ni Simba wa Yuda?
Gongo na Fimbo ni nini? Na vinawezaje kumfariji mtu? (Zaburi 23:4).
Je! habari ya muda aliotawala Mfalme Yekonia inajichanganya? (2Wafalme 24:8 na 2Nyakati 36:9).
Jibu: Biblia haijichanganyi mahali popote na haijawahi kujichanganya isipokuwa viwango vyetu vya kutafakari ndivyo vinavyotufanya tuone kuna utata mwingi kwenye biblia (na kumbuka tunapozungumzia biblia tunamaanisha ile yenye vitabu 66) na si zaidi ya hivyo!.
Vitabu 66 vya biblia ndivyo vilivyohakikiwa na Roho Mtakatifu kwa vizazi vyote kama Neno la Mungu lililo hai.
Sasa kabla ya kwenda kuitafakari mistari hiyo hebu tuisome kwanza..
Mwanzo 15:13 “Bwana akamwambia Abramu, Ujue hakika ya kwamba uzao wako utakuwa mgeni katika nchi isiyo yake, watawatumikia watu wale, nao watateswa muda wa MIAKA MIA NNE. 14 Hata na taifa lile, watakaowatumikia, nitawahukumu; baadaye watatoka na mali mengi”
Mwanzo 15:13 “Bwana akamwambia Abramu, Ujue hakika ya kwamba uzao wako utakuwa mgeni katika nchi isiyo yake, watawatumikia watu wale, nao watateswa muda wa MIAKA MIA NNE.
14 Hata na taifa lile, watakaowatumikia, nitawahukumu; baadaye watatoka na mali mengi”
Tusome tena,..
Kutoka 12:40 “Basi wana wa Israeli kukaa kwao, maana, muda waliokaa ndani ya Misri, ulikuwa NI MIAKA MIA NNE NA THELATHINI. 41 Ilikuwa mwisho wa miaka hiyo MIA NNE NA THELATHINI, ilikuwa siku ile ile, ya kwamba majeshi yote ya Bwana yalitoka nchi ya Misri”. Sasa swali ni hili, Mungu alimdanganya Abramu kuwa uzao wake utakaa miaka 400 na kumbe ni miaka 430?, je Mungu ni mwongo?
Kutoka 12:40 “Basi wana wa Israeli kukaa kwao, maana, muda waliokaa ndani ya Misri, ulikuwa NI MIAKA MIA NNE NA THELATHINI.
41 Ilikuwa mwisho wa miaka hiyo MIA NNE NA THELATHINI, ilikuwa siku ile ile, ya kwamba majeshi yote ya Bwana yalitoka nchi ya Misri”.
Sasa swali ni hili, Mungu alimdanganya Abramu kuwa uzao wake utakaa miaka 400 na kumbe ni miaka 430?, je Mungu ni mwongo?
Jibu ni la! Hakudanganywa, kwasababu hiyo miaka 430 bado ipo katika namba mia nne, Mungu hakumwambia kuwa atakaa miaka mia nne kamili, bali alimwambia tu miaka mia nne, ikiwa na maana kuwa inaweza kuwa ni miaka mia nne kamili au miaka 410 au 430 au 470 au hata 490 lakini haitazidi hiyo miaka 400 na kuwa 500.
Ni sawa mtu na mtu akuulize wewe una miaka mingapi na umwambie una miaka 30 au 40, unaweza kumpa namba ya ujumla lakini kiuhalisia huenda unayo miaka 30 na miezi 6 au na miezi 7,au una miaka 40 na miezi 8 au 9.. Kwahiyo wewe kumwambia kuwa una miaka 30 au 40 unakuwa hujamdanganya.. Ni kweli ndio miaka yako, isipokuwa hujapenda kumwambia na miezi iliyo mbele ya hiyo miaka..Ungekuwa umemdaganya endapo kama ungemwambia unayo miaka 30 kamili au 40 kamili, hapo utakuwa umemdanganya!..
Vile vile Bwana Mungu hakumwambia Abramu kuwa Uzao wake utakaa utumwani miaka 400 kamili, bali alimwambia tu utakaa miaka 400.. Na ndivyo ilivyokuwa.
Kwahiyo biblia haijichanganyi.. Tazama pia miezi aliyotawala Yekonia je unajichanganya? >>> YEKONIA ALITAWALA MUDA GANI?
Je umeokoka?..kumbuka kuwa hizi ni siku za mwisho, na unyakuo wa kanisa ni muda wowote kuanzia sasa.
Bwana akubariki.
Je! kuna mambo ambayo Mungu hawezi kuyafanya kulingana na Waamuzi 1:19?
Je! habari ya muda aliyotawala Mfalme Yekonia inajichanganya? (2Wafalme 24:8 na 2Nyakati 36:9).
Je kauli ya Bwana Yesu inajichanganya? Katika Yohana 8:14 na Yohana 5:31?