Daudi anapomwambia Mungu, kuwa GONGO LAKE na FIMBO YAKE vinamfariji, alikuwa anamaanisha nini?..
Jibu: Tusome,
Zaburi 23:1 “Bwana ndiye mchungaji wangu, Sitapungukiwa na kitu. 2 Katika malisho ya majani mabichi hunilaza, Kando ya maji ya utulivu huniongoza. 3 Hunihuisha nafsi yangu; na kuniongoza Katika njia za haki kwa ajili ya jina lake. 4 Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti, Sitaogopa mabaya; Kwa maana Wewe upo pamoja nami, GONGO LAKO NA FIMBO YAKO VYANIFARIJI”.
Zaburi 23:1 “Bwana ndiye mchungaji wangu, Sitapungukiwa na kitu.
2 Katika malisho ya majani mabichi hunilaza, Kando ya maji ya utulivu huniongoza.
3 Hunihuisha nafsi yangu; na kuniongoza Katika njia za haki kwa ajili ya jina lake.
4 Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti, Sitaogopa mabaya; Kwa maana Wewe upo pamoja nami, GONGO LAKO NA FIMBO YAKO VYANIFARIJI”.
Zamani wachungaji wa kondoo na Mbuzi, walikuwa wanatembea na Zana hizo mbili (Gongo na Fimbo), zilizokuwa zinazowasaidia katika shughuli zao uchungaji. Na kila zana likuwa na kazi yake.
GONGO: Hii ilikuwa ni kipande cha kifupi cha fimbo maalum, iliyonyooka, ambayo ilikuwa Nene kidogo na fupi, Na kazi ya Gongo, ilikuwa si nyingine Zaidi ya kupiga maadui wa mifugo kama Mbwa mwitu, dubu, Mbweha, fisi n.k Kwahiyo wachugaji walitembea nayo wakiwa katika uchungaji, ili kundi liwe salama..Fisi walipotokea kutaka kukamata kondoo, wachungaji waliwapiga kwa gongo hilo.
FIMBO: Hii ni Zana ya pili, ambayo haikuwa kwa lengo la kudhuru maadui, bali kwa lengo la kuwaongoza kondoo. Fimbo ya Mchungaji ilikuwa ni ndefu na yenye mkunjo mwishoni, na lengo la mkunjo huo ni kumvuta kondoo anapokuwa kwenye hatari au anapoelekea kwenye hatari, mkunjo ule unasaidia kuishika shingo ya kondoo au mguu wa kondoo na kumvuta kutoka kwenye hatari.. vile vile, kazi nyingine ya fimbo hiyo ni kuwaongoza kondoo wakae kwenye mstari, wasitoke.
Sasa swali ni kwanini Daudi aseme Fimbo ya Bwana na Gongo lake vinamfariji?
Ni kwasababu yeye (Daudi) anajifananisha na kondoo na Mungu anamfananisha na Mchungaji aliyeshika Fimbo na Gongo, kwamba kondoo anapoona kuwa mchungaji wake kashika Gongo, basi anakuwa hana wasiwasi kwasababu anajua gongo lile kazi yake ni kuwapiga maadui zake.. Hivyo Daudi hakuogopa maadui kwasababu Bwana ndiye mchungaji wake, hivyo gongo lile lilikuwa Faraja kwake.
Vile vile, Fimbo ya Bwana, ambayo ina mkunjo mwishoni, ilimfariji kwasababu yeye kama kondoo alijua hawezi kupotea, kwasababu ile Fimbo itamwongoza katika njia iliyonyooka, Zaidi sana hata atakapopita kando ya bonde la Mauti, Fimbo ile itamwongoza katika njia iliyonyooka, na hatapotea kamwe.
Na sisi katika roho ni kondoo na Yesu ni Mchungaji, Mkuu.. Ambaye naye pia ameshika Gongo na Fimbo, kutulinda na kutuchunga.
Waebrania 13:20 “Basi, Mungu wa amani aliyemleta tena kutoka kwa wafu MCHUNGAJI MKUU WA KONDOO, kwa damu ya agano la milele, yeye BWANA WETU YESU”
Umeona?..Bwana Yesu ni Mchungaji Mkuu wa Kondoo.. wengine ni wachungaji, lakini si wachungaji wakuu.., hali kadhalika wengine ni wachungaji, lakini si wachungaji wema… Lakini Bwana Yesu ni mchungaji Mkuu, na Mchungaji mwema.., anawachunga kondoo katika njia iliyo nyooka kwa fimbo yake, wala hakuna hata mmoja atapotea akiwa kwake, vile vile anaweza kutoa uhai wake kwaajili ya kuwaokoa kondoo..
Yohana 10:11 “Mimi ndimi mchungaji mwema. Mchungaji mwema huutoa uhai wake kwa ajili ya kondoo. 12 Mtu wa mshahara, wala si mchungaji, ambaye kondoo si mali yake, humwona mbwa-mwitu anakuja, akawaacha kondoo na kukimbia; na mbwa-mwitu huwakamata na kuwatawanya. 13 Yule hukimbia kwa kuwa ni mtu wa mshahara; wala mambo ya kondoo si kitu kwake”.
Yohana 10:11 “Mimi ndimi mchungaji mwema. Mchungaji mwema huutoa uhai wake kwa ajili ya kondoo.
12 Mtu wa mshahara, wala si mchungaji, ambaye kondoo si mali yake, humwona mbwa-mwitu anakuja, akawaacha kondoo na kukimbia; na mbwa-mwitu huwakamata na kuwatawanya.
13 Yule hukimbia kwa kuwa ni mtu wa mshahara; wala mambo ya kondoo si kitu kwake”.
Je! Umempokea Yesu leo?.. Je Bwana Yesu ni mchungaji wako?.. kama hujampokea Yesu, bado wewe ni kondoo uliyepotea, ambaye Bwana Yesu, mchungaji mwema ANAKUTAFUTA!!!, kwasababu hapo ulipo haupo salama, mbwa-mwitu wanasikia harufu yako toka mbali na wanakusogelea kwa kasi, fisi na dubu, wanasikia harufu yako na wanakukaribia ili wakudhuru, wakufanye kitoweo… Leo hii umemwona Mchungaji mwema Yesu Kristo, mkimbilie huyo uwe salama, ili hatimaye useme kama Daudi.. “Bwana ndiye Mchungaji wangu, sitapungukiwa na chochote, gongo lake na fimbo yake vyanifariji”.
Huko kwenye ulevi ulipo, umepotea, huko kwenye uzinzi, na uasherati ulipo umepotea, huko kwenye dansi ulipo na kwenye miziki, fasheni, na anasa za kidunia umepotea!.. haupo salama!.. Maisha yako yapo hatarini, wewe ni windo bora la mapepo yote, ni windo bora la wachawi, ni windo bora la mauti. Na vyote hivyo vinakutafuta.. Haupo salama kabisa!..kimbilia kwa Yesu…
Kama bado hujaokoka na unahitaji kuokoka ili uwe salama ndani ya Mchungaji mwema Yesu, basi wasiliana nasi inbox tuweze kuomba nawe, sala fupi ya kumkaribisha Bwana Yesu, maishani mwako.
Maran atha!
Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp: Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Mada Nyinginezo:
Naye atawachunga kwa fimbo ya chuma.
Kwanini Bwana Yesu aliwaambia wanafunzi wake wasichukue chochote isipokuwa fimbo tu?
Ni kwa namna gani Yesu ni Simba wa Yuda?
Kwa namna gani mauti hufanya kazi ndani yetu na uzima kwa wengine? (2Wakorintho 4:12).
JAWABU LA MAISHA YA MTU.
Rudi nyumbani
Print this post
Nakusalimu katika jina kuu la Yesu Kristo Bwana, nakukaribisha tena, katika kuyatafakari maneno ya uzima, maadamu siku ile inakaribia.
Bwana wetu Yesu Kristo alipokuja hapa duniani, dira yake ya kwanza haikuwa kwa kila mtu duniani, bali ilikuwa kwanza kwa Wayahudi, kisha watu wengine baadaye, ndio maana hata watu wa mataifa walipomfuata awaponye aliweka ugumu mkubwa kidogo kwao, na aliwaeleza waziwazi kabisa kuwa sikutumwa kwa ajili yenu bali kwa wayahudi.( Soma Mathayo 15:22-28),
Hata kipindi kingine, alipowatuma wanafunzi kuhubiri, aliwakataza kabisa wasiwafuate mataifa ikiwemo wasamaria, waliokuwa Israeli wakati huo, bali wayahudi tu.
Mathayo 10:5 “Hao Thenashara Yesu aliwatuma, akawaagiza, akisema, Katika njia ya Mataifa msiende, wala katika mji wo wote wa Wasamaria msiingie. 6 Afadhali shikeni njia kuwaendea kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli”.
Mathayo 10:5 “Hao Thenashara Yesu aliwatuma, akawaagiza, akisema, Katika njia ya Mataifa msiende, wala katika mji wo wote wa Wasamaria msiingie.
6 Afadhali shikeni njia kuwaendea kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli”.
Umeona, kwahiyo kusudi la awali la Kristo lilikuwa ni kumalizana kwanza na wayahudi.. Lakini kuna wakati, ratiba zake zilivurugwa, Hivyo akalazimika tu kutumiza kusudi lake la kuokoa kwa muda kwa watu wa mataifa aliokutana nao..
Embu tusome..
Yohana 4:3 “aliacha Uyahudi, akaenda zake tena mpaka Galilaya. 4 NAYE ALIKUWA HANA BUDI KUPITA KATIKATI YA SAMARIA. 5 Basi akafika kunako mji wa Samaria, uitwao Sikari, karibu na lile shamba ambalo Yakobo alimpa Yusufu mwanawe. 6 Na hapo palikuwa na kisima cha Yakobo. Basi Yesu, kwa sababu amechoka kwa safari yake, akaketi vivi hivi kisimani. Nayo ilikuwa yapata saa sita. 7 Akaja mwanamke Msamaria kuteka maji. Yesu akamwambia, Nipe maji ninywe”.
Yohana 4:3 “aliacha Uyahudi, akaenda zake tena mpaka Galilaya.
4 NAYE ALIKUWA HANA BUDI KUPITA KATIKATI YA SAMARIA.
5 Basi akafika kunako mji wa Samaria, uitwao Sikari, karibu na lile shamba ambalo Yakobo alimpa Yusufu mwanawe.
6 Na hapo palikuwa na kisima cha Yakobo. Basi Yesu, kwa sababu amechoka kwa safari yake, akaketi vivi hivi kisimani. Nayo ilikuwa yapata saa sita.
7 Akaja mwanamke Msamaria kuteka maji. Yesu akamwambia, Nipe maji ninywe”.
Umeona hapo, tafakari vizuri, Bwana hakuwa na lengo la kuzungumza chochote pale Samaria, bali, mawazo yake yalikuwa ni kwenda Galilaya kwa wayahudi..Lakini sasa ili kufika Galilaya ilimlazimu apitie Samaria., Hakuna namna.. Samaria ilikuwa ni njia panda ya kufika Galilaya..
Na alipofika pale biblia inatuambia, alikuwa amechoka sana, lakini je! Alale tu? Kisa hakutumwa kwao? Au akae tu apumzikie, huku akitazama roho za makafiri zikipotea?.. Ni wazi kuwa hata kama ni mimi, ningekuwa sijatumwa mahali Fulani, halafu nimechoka, ya nini kujisumbua kufanya nisiyoagizwa? Ningelala zangu..
Lakini kinyume chake, ilimpasa aghahiri hata kula chakula, aghahiri hata uchovu wake, aanzane na yule mwanamke mwenye dhambi pale kisimani, jambo lililomfanya sio tu yule mwanamke mwenyewe kumshangaa, bali pia mitume wake paliporudi, kumwona anawahubiria mataifa tena mwanamke jambo ambalo yeye mwenyewe alilikataza, huko nyuma.
Yohana 4:9 “Basi yule mwanamke Msamaria akamwambia, Imekuwaje wewe Myahudi kutaka maji kwangu, nami ni mwanamke Msamaria? (Maana Wayahudi hawachangamani na Wasamaria.) 10 Yesu akajibu, akamwambia, Kama ungaliijua karama ya Mungu, naye ni nani akuambiaye, Nipe maji ninywe, ungalimwomba yeye, naye angalikupa maji yaliyo hai”.
Yohana 4:9 “Basi yule mwanamke Msamaria akamwambia, Imekuwaje wewe Myahudi kutaka maji kwangu, nami ni mwanamke Msamaria? (Maana Wayahudi hawachangamani na Wasamaria.)
10 Yesu akajibu, akamwambia, Kama ungaliijua karama ya Mungu, naye ni nani akuambiaye, Nipe maji ninywe, ungalimwomba yeye, naye angalikupa maji yaliyo hai”.
Ili ufikie Galilaya yako, huna budi kupitia Samaria, Ni Mungu mwenyewe ndio anayeruhusu hiyo hali, unasema nina mipango ya kwenda kuhubiri injili kwa watu Fulani mijini au vijijini, malengo ambayo ni mazuri, lakini leo hii unajikuta upo katika mazingira ya shule, ambayo hayatimizi malengo yako, Hapo hapo shuleni, kuwa muhubiri wa Injili, wahubirie wanafunzi wenzako, kwasababu imekupasa kwanza upitie hapo ndipo ufikie kule Mungu alikokuonyesha, au unakokutazamia.
Leo umejikuta katika mazingira ya kazini, usisubirie tu wakati Fulani kufika, ukasema bado bado. Kristo hakuwa na mawazo hayo. Alijua kabisa Samaria ni anapita tu, hana kusudi lolote pale, lakini aliwashuhudia Habari za wokovu, na hadi mwisho watu wengi wakamwamini hadi wakataka kumfanya awe mfalme wao, akakataa.
Kwahiyo wakristo wengi, sasa tumekuwa ni wa kusubiri suburi, tukisema ngoja kwanza nitoke hapa, au ngoja kwanza nimalize hiki au kile, ndio nitaanza kuifanya kazi ya Mungu.. Hujui ni kwanini Mungu kakupitisha hapo, tumia nafasi hiyo kumuhubiri Kristo,
Tumeambiwa, tuwe tayari wakati wote..ufaao na usiofaa.
2Timotheo 4:2 “lihubiri neno, uwe tayari, wakati ukufaao na wakati usiokufaa, karipia, kemea, na kuonya kwa uvumilivu wote na mafundisho”.
Halikadhalika Bwana Yesu mwenyewe alituambia tujifunze kwake,(Mathayo 11:29)..Na hili ni somo mojawapo tunapaswa tulitafakari kutoka kwake, ili mahali popote tulipo tuwe watu wa kumzalia matunda, bila kungojea tufike Galilaya yetu.
Shalom.
BADO UPO YERUSALEMU TU..GALILAYA HUTAKI KWENDA?
OLE WAKO KORAZINI NA BETHSAIDA.
TAFUTA UZIMA WA MILELE NA SI UZIMA TU!
JE MGOGORO WA URUSI NA UKRAINE,UMETABIRIWA KIBIBLIA?
Ni mlima gani Yule Mwanamke Msamaria aliokuwa anaumaanisha? (Yohana 4:19)
Ayari ni nini kama tunavyosoma katika biblia?
Kiburi cha Uzima ni nini? (1Yohana 2:16)
Hema ya kukutania ni nini, na ilikuwaje?
NDIPO HUENDA AKACHUKUA PEPO WENGINE SABA.
SWALI: Isaya 59:5 ina maana gani?
Isaya 59:5 Huangua mayai ya fira, na kusuka wavu wa buibui; yeye alaye mayai yao hufa, na hilo livunjwalo hutoka nyoka.
JIBU: Ni mstari unaoeleza asili ya watu waovu.
Anasema huangua mayai ya fira. Fira ni aina ya nyoka wenye sumu kali sana, ambao kwa kawaida mtu akikutana nao, ni lazima awaue, au akikuta mayai yao ni lazima ayakanyage, kwasababu, asipofanya hivyo yakitotolewa wataleta madhara, Lakini mtu mwovu biblia inasema ni kinyume chake huyatotoa. Ikiwa na maana ni mtu ambaye anaona madhara Fulani yanakuja mbele kwa wengine badala ayaangamize, yeye ndio anayekuwa wa kwanza kuyakumbatia.
Mfano mmojawapo wa hawa ni manabii wa uongo, wanaojua kabisa, dhambi ina madhara, na mtu asipoishi katika utakatifu hawezi kumwona Mungu (Waebrania 12:14), lakini kwasababu hawataki kupoteza watu, kwa tamaa za pesa, hawawaonyi juu ya mambo kama hayo, kinyume chake ndio wanawasogeza kabisa kwenye mambo ya mwilini, biashara na mali, wanamsahau Mungu. Halafu wanakufa katika dhambi zao na kwenda kuzimu.
Vilevile anasema husuka wavu wa buibui. Kama vile tunavyojua buibui anaposuka wavu wake, ni kwa lengo la kunasa wadudu awale. Halikadhalika asili ya watu wa waovu ndivyo ilivyo, huandaa mazingira yote, ya wenzao kunaswa katika mambo maovu na kuangamia.
Kwamfano unapomwombea adui yako afe, ni sawa na mtu anayeunda wavu wa uangamivu. Bwana alisema tuwaombee, lakini sisi tunawatakia mauti, tena katika maombi.
Kwa ufupi, hii ni tabia ya kutengeneza kama sio kufurahia anguko la wengine.
Hivyo biblia inatuonyesha pia tukiwa na tabia kama hizo, zinatufanya na sisi Mungu asitutee na kutupa haki zetu kwa vile tumwombavyo, nasi majibu yanakuja kinyume chake.. Pale tunapotazamia jema linakuja ovu,na tunapotazamia nuru linakuja giza, tunalithitibitisha hilo katika vifungu vinavyofuata..
Isaya 59:6-9
6 Nyavu zao hazitakuwa mavazi, wala hawatajifunika kwa kazi zao; kazi zao ni kazi za uovu, na vitendo vya udhalimu vimo mikononi mwao. 7 Miguu yao hukimbilia mabaya, nao hufanya haraka kumwaga damu isiyo na hatia; mawazo yao ni mawazo ya uovu; ukiwa na uharibifu zaonekana katika njia kuu zao. 8 Njia ya amani hawaijui; wala hapana hukumu ya haki katika miendo yao; wamejifanyizia njia zilizopotoka; kila apitaye katika njia hizo hajui amani. 9 KWA SABABU HIYO HUKUMU YA HAKI I MBALI NASI, WALA HAKI HAITUFIKILII; TWATAZAMIA NURU, NA KUMBE! LATOKEA GIZA; TWATAZAMIA MWANGA, LAKINI TWAENDA KATIKA GIZA KUU.
6 Nyavu zao hazitakuwa mavazi, wala hawatajifunika kwa kazi zao; kazi zao ni kazi za uovu, na vitendo vya udhalimu vimo mikononi mwao.
7 Miguu yao hukimbilia mabaya, nao hufanya haraka kumwaga damu isiyo na hatia; mawazo yao ni mawazo ya uovu; ukiwa na uharibifu zaonekana katika njia kuu zao.
8 Njia ya amani hawaijui; wala hapana hukumu ya haki katika miendo yao; wamejifanyizia njia zilizopotoka; kila apitaye katika njia hizo hajui amani.
9 KWA SABABU HIYO HUKUMU YA HAKI I MBALI NASI, WALA HAKI HAITUFIKILII; TWATAZAMIA NURU, NA KUMBE! LATOKEA GIZA; TWATAZAMIA MWANGA, LAKINI TWAENDA KATIKA GIZA KUU.
Hivyo tupambane, kwa bidii zote tusiwe vyombo vya shetani vya kuunda mabaya kwa wengine.
Bwana atusaidie.
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini auPiga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Injili iliyopo kwa Samaki aina ya Eeli.
Lumbwi ni nini katika biblia?
Wibari ni nani?(Mithali 30:26)
Santuri ni nini? (Danieli 3:5,10)
Biblia inaposema “Wote tumetenda dhambi” si inamaanisha hakuna mtakatifu duniani?
MFANO WA MAMBO HAYO NI UBATIZO.
Donda-Ndugu ni nini?
Ipo tofauti ya “Uzima” na “Uzima wa milele”.
Uzima, kila mwanadamu anao, na si wanadamu tu peke yao wenye uzima, bali hata Wanyama wanao uzima, na hata ndege na mimea. Lakini Pamoja na kwamba Uzima upo kwa viumbe vingi, lakini Uzima wa milele haupo kwa wote.
Uzima wa Milele ni kitu kingine kabisa…ambacho Mtu hana budi kukitafuta.. Na asipokitafuta na kukipata ataishia kuwa na uzima tu wa kitambo, ambao hautadumu sana, kwasababu wote wasio na uzima wa milele ndani yao, wakishakufa hawatafufuliwa na kuendelea kuishi, badala yake wataangamizwa katika ziwa la moto.
Na Uzima wa milele (ambao kwa lugha nyingine unaitwa “UZIMA TELE”), Unapatikana kwa mmoja tu ambaye ni Yesu.
Yohana 10:10 “…mimi nalikuja ili WAWE NA UZIMA, KISHA WAWE NAO TELE”.
Umeona?..Bwana Yesu amekuja ili tuwe na UZIMA, yaani tuwe na Afya, tuishi Maisha ya heri katika mwili, lakini hajaishia hapo, bali pia tuwe na UZIMA TELE, (Yaani tuwe Uzima wa Milele).
SASA SWALI NI JE TUTAUPATAJE UZIMA WA MILELE?
Jambo moja linalowachanganya wengi, ni kudhani kuwa kuwa na maadili mazuri au kuwa na dini nzuri, au KUSHIKA AMRI 10, ndio kupata Uzima wa milele, pasipo kujua kuwa kuzishika amri 10, au kuwa na dini nzuri, au dhehebu zuri, kama mtu “hajaamua kujikana nafsi ya kumfuata Bwana Yesu” ni kazi bure.. Dini yake nzuri huyo mtu, au maadili yake mazuri, au sifa yake nzuri bado, hakutampa uzima wa milele.
Hebu tusome kisa kifuatacho.. (Zingatia vipengele vilivyoanishwa kwa herufi kubwa).
Mathayo 19:16 “Na tazama, mtu mmoja akamwendea akamwambia, Mwalimu, nitende jambo gani jema, ili nipate UZIMA WA MILELE? 17 Akamwambia Kwani kuniuliza habari ya wema? Aliye mwema ni mmoja. LAKINI UKITAKA KUINGIA KATIKA UZIMA, zishike amri. 18 Akamwambia, Zipi? Yesu akasema, Ni hizi, Usiue, Usizini, Usiibe, Usishuhudie uongo, 19 Waheshimu baba yako na mama yako, na, Mpende jirani yako kama nafsi yako. 20 Yule kijana akamwambia, Haya yote nimeyashika; nimepungukiwa na nini tena? 21 Yesu akamwambia, UKITAKA KUWA MKAMILIFU, ENENDA UKAUZE ULIVYO NAVYO, UWAPE MASKINI, NAWE UTAKUWA NA HAZINA MBINGUNI; KISHA NJOO UNIFUATE”.
Mathayo 19:16 “Na tazama, mtu mmoja akamwendea akamwambia, Mwalimu, nitende jambo gani jema, ili nipate UZIMA WA MILELE?
17 Akamwambia Kwani kuniuliza habari ya wema? Aliye mwema ni mmoja. LAKINI UKITAKA KUINGIA KATIKA UZIMA, zishike amri.
18 Akamwambia, Zipi? Yesu akasema, Ni hizi, Usiue, Usizini, Usiibe, Usishuhudie uongo,
19 Waheshimu baba yako na mama yako, na, Mpende jirani yako kama nafsi yako.
20 Yule kijana akamwambia, Haya yote nimeyashika; nimepungukiwa na nini tena?
21 Yesu akamwambia, UKITAKA KUWA MKAMILIFU, ENENDA UKAUZE ULIVYO NAVYO, UWAPE MASKINI, NAWE UTAKUWA NA HAZINA MBINGUNI; KISHA NJOO UNIFUATE”.
Hapo nataka uone maswali, huyu mtu aliyomwuliza Bwana na Majibu Bwana aliyompa.. Swali la kwanza huyu mtu alitaka kujua jinsi ya kuupata UZIMA WA MILELE. Lakini utaona Bwana Yesu alimwambia akitaka KUUPATA UZIMA, (Zingatia; sio uzima wa milele, bali Uzima tu), azishike amri.
Ikiwa na maana kuwa Kuzishika amri 10 peke yake hazimpi mtu UZIMA WA MILELE, bali zinampa tu UZIMA. (aishi Maisha marefu hapa duniani na ya heri) Sawasawa na Walawi 18:5.
Walawi 18:5 “Kwa ajili ya hayo mtazishika amri zangu na hukumu zangu; ambazo MTU AKIZITUMIA ATAISHI KWA HIZO; mimi ndimi Bwana”.
Lakini swali la pili, huyu mtu alilomwuliza Bwana Yesu ni kwamba, tayari ameshazishika hizo amri, ni kitu gani alichopungukiwa Zaidi?.
Na Bwana Yesu alipoona kuwa anauhitaji UZIMA WA MILELE na si UZIMA TU!. Ndipo akamwambia “akauze kila kitu alichonacho kisha amfuate” kwa ufupi, ajikane nafsi yake ajitwike msalaba wake na kumfuata.
Lakini kwasababu yule mtu alikuwa anautaka Uzima na si Uzima wa milele, hakutaka kufanya vile, akaondoka!.. Na akaondoka akiwa na Uzima, na heri katika Maisha, lakini hana Uzima wa milele, jambo la kuhuzunisha sana.
Ndugu unayesoma ujumbe huu, maandiko yanasema kuwa Yesu Kristo ni yeye yule, jana na leo na hata milele, habadiliki (kasome Waebrania 13:8), Maana yake ni kuwa vigezo vyake ni vile vile, kwa jinsi alivyomwambia huyu bwana, kwamba akauze vyote amfuate ndipo apate uzima wa milele, ndivyo anavyotuambia hata watu wa leo.
Sio kwamba huyu ndugu, alikuwa na bahati mbaya mpaka aambiwe vile na Bwana Yesu. Hapana!. Maneno hayo hayo aliwaambia pia wanafunzi wake kabla ya kumfuata..
Luka 14:33 “Basi, kadhalika kila mmoja wenu asiyeacha vyote alivyo navyo, hawezi kuwa mwanafunzi wangu”.
Sasa kuacha vyote kunakozungumziwa hapo ni kukitoa kitu katika moyo wako moja kwa moja, kama ni mali, Rafiki, ndugu, au chochote kile, unakitoa moyoni mwako na kuwa tayari kuyafanya mapenzi ya Mungu..Kama kimeondoka kweli moyoni mwako, basi hata ukiwa nacho kimwili hakina madhara yoyote, kwasababu kiwepo au kisiwepo, hakikusumbui kwasababu huna muunganiko nacho kiroho.. Lakini kama umekiondoa kimwili lakini moyoni mwako bado kipo, bado utakuwa hujafanya chochote..
Hivyo hiyo ni kanuni KUU sana, ambayo sote tunapaswa tujifunze. Gharama za kuupata uzima wa milele si ndogo. Zinahitaji kujikana nafsi kweli kweli, na kubeba msalaba na kumfuata Yesu.
Hebu kwa kumalizia tuisome faida hiyo ya kujikana nafsi na kumfuata Yesu kwa kumalizia mistari ya chini..
Mathayo 19:22 “Yule kijana alipolisikia neno lile, akaenda zake kwa huzuni; kwa sababu alikuwa na mali nyingi. 23 Yesu akawaambia wanafunzi wake, Amin, nawaambieni, ya kwamba itakuwa shida tajiri kuingia katika ufalme wa mbinguni. 24 Nawaambia tena, Ni rahisi zaidi ngamia kupenya tundu ya sindano, kuliko tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu. 25 Wanafunzi waliposikia, walishangaa mno, wakisema, Ni nani basi awezaye kuokoka? 26 Yesu akawakazia macho, akawaambia, Kwa wanadamu hilo haliwezekani; bali kwa Mungu yote yawezekana. 27 Ndipo Petro akajibu, akamwambia, Tazama, sisi tumeacha vyote tukakufuata; tutapata nini basi? 28 Yesu akawaambia, Amin, nawaambia ya kwamba ninyi mlionifuata mimi, katika ulimwengu mpya, atakapoketi Mwana wa Adamu katika kiti cha utukufu wake, ninyi nanyi mtaketi katika viti kumi na viwili, mkiwahukumu kabila kumi na mbili za Israeli. 29 Na kila mtu aliyeacha nyumba, au ndugu wa kiume au wa kike, au baba, au mama, au watoto, au mashamba, kwa ajili ya jina langu, atapokea mara mia, na kuurithi uzima wa milele”.
Mathayo 19:22 “Yule kijana alipolisikia neno lile, akaenda zake kwa huzuni; kwa sababu alikuwa na mali nyingi.
23 Yesu akawaambia wanafunzi wake, Amin, nawaambieni, ya kwamba itakuwa shida tajiri kuingia katika ufalme wa mbinguni.
24 Nawaambia tena, Ni rahisi zaidi ngamia kupenya tundu ya sindano, kuliko tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu.
25 Wanafunzi waliposikia, walishangaa mno, wakisema, Ni nani basi awezaye kuokoka?
26 Yesu akawakazia macho, akawaambia, Kwa wanadamu hilo haliwezekani; bali kwa Mungu yote yawezekana.
27 Ndipo Petro akajibu, akamwambia, Tazama, sisi tumeacha vyote tukakufuata; tutapata nini basi?
28 Yesu akawaambia, Amin, nawaambia ya kwamba ninyi mlionifuata mimi, katika ulimwengu mpya, atakapoketi Mwana wa Adamu katika kiti cha utukufu wake, ninyi nanyi mtaketi katika viti kumi na viwili, mkiwahukumu kabila kumi na mbili za Israeli.
29 Na kila mtu aliyeacha nyumba, au ndugu wa kiume au wa kike, au baba, au mama, au watoto, au mashamba, kwa ajili ya jina langu, atapokea mara mia, na kuurithi uzima wa milele”.
Je! Umejikana nafsi na kumfuata Yesu? Au unajitumainia dini yako?, huyu kijana alikuwa na dini na ameshika amri zote lakini hakuwa na uzima wa milele ndani yake?, unadhani wewe na dhehebu lako utautolea wapi?..
Maadili yako yatakupa Uzima tu!, ni kweli utabarikiwa kwa kuishi vizuri duniani, kwa kuwa na moyo mzuri, lakini kama Yesu hajaingia ndani yako, huna uzima wa milele.
Ukitaka uzima wa milele weka dhehebu lako pembeni, weka dini yako pembeni, weka mali zako pembeni, weka uzuri wako pembeni, weka umaarufu wako pembeni, weka sifa zako pembeni, na kila kitu chako, weka kando nenda kama mshamba mbele zake Bwana Yesu, kama asiyejua chochote, kama mtu aliyezaliwa leo, kama vile kondoo aliyetayari kuchungwa…Bwana Yesu anataka moyo uliojiachia kwake, moyo wa unyenyekevu..hapo ndipo atakapokuonyesha njia na kukupa uzima wa milele?.
Kama hujaokoka basi hakikisha siku ya leo haipiti bila kuokoka, kwasababu hujui ni nini kitatokea kesho, tafuta mtu aliye mkristo, aombe Pamoja na wewe katika sala fupi ya kumkaribisha Bwana Yesu maishani mwako, au wasaliana nasi kwa namba zilizopo chini ya somo, tutakusaidia kwa hilo.
Bwana akubariki.
Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp: Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312 Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp
NUNUA MAJI YA UZIMA.
MFALME ANAKUJA.
OLE WAO WANAOJITAHIDI KUMFICHA BWANA MASHAURI YAO.
FANYIKA SIPORA WA KRISTO, UNYAKUO UPO KARIBU.
SWALI: Kwanini watu watakaohukumiwa siku ile ya mwisho, wanaonekana kutofautishwa katika sehemu mbili, wengine watatokea “baharini”, na wengine katika “mauti na kuzimu”. Kwanini iwe hivyo na tofauti ya maeneo hayo ni ipi?
Ufunuo 20:11 “Kisha nikaona kiti cha enzi, kikubwa, cheupe, na yeye aketiye juu yake; ambaye nchi na mbingu zikakimbia uso wake, na mahali pao hapakuonekana. 12 Nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wamesimama mbele ya hicho kiti cha enzi; na vitabu vikafunguliwa; na kitabu kingine kikafunguliwa, ambacho ni cha uzima; na hao wafu wakahukumiwa katika mambo hayo yaliyoandikwa katika vile vitabu, sawasawa na matendo yao. 13 BAHARI IKAWATOA WAFU WALIOKUWAMO NDANI YAKE; NA MAUTI NA KUZIMU ZIKAWATOA WAFU WALIOKUWAMO NDANI YAKE. Wakahukumiwa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake. 14 Mauti na Kuzimu zikatupwa katika lile ziwa la moto. Hii ndiyo mauti ya pili, yaani, hilo ziwa la moto. 15 Na iwapo mtu ye yote hakuonekana ameandikwa katika kitabu cha uzima, alitupwa katika lile ziwa la moto”.
Ufunuo 20:11 “Kisha nikaona kiti cha enzi, kikubwa, cheupe, na yeye aketiye juu yake; ambaye nchi na mbingu zikakimbia uso wake, na mahali pao hapakuonekana.
12 Nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wamesimama mbele ya hicho kiti cha enzi; na vitabu vikafunguliwa; na kitabu kingine kikafunguliwa, ambacho ni cha uzima; na hao wafu wakahukumiwa katika mambo hayo yaliyoandikwa katika vile vitabu, sawasawa na matendo yao.
13 BAHARI IKAWATOA WAFU WALIOKUWAMO NDANI YAKE; NA MAUTI NA KUZIMU ZIKAWATOA WAFU WALIOKUWAMO NDANI YAKE. Wakahukumiwa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake.
14 Mauti na Kuzimu zikatupwa katika lile ziwa la moto. Hii ndiyo mauti ya pili, yaani, hilo ziwa la moto.
15 Na iwapo mtu ye yote hakuonekana ameandikwa katika kitabu cha uzima, alitupwa katika lile ziwa la moto”.
JIBU: Hukumu ya mwisho kabisa ni hukumu ijulikanayo kama “hukumu ya kiti cheupe cha enzi cha mwanakondoo”. Ni hukumu inayokamilisha wafu wote walioko makaburini, mbali na watakatifu.
Haitachagua wakubwa, wala wadogo, vijana au wazee. Waovu wote watafufuliwa wakati huu na kila mmoja atahukumiwa sawasawa na matendo yake, kisha atatupwa katika lile ziwa la moto, aangamie huko milele.
Lakini biblia inatuonyesha siku hiyo waovu hao watatoka sehemu kuu mbili,
Kumbuka, lugha iliyotumika hapo ni lugha ya kinabii, na sio halisi kabisa kwamba bahari inayo wafu wake. Hapana.
Je Bahari ikawatoa wafu waliokuwa ndani yake, kunamaanisha nini?.
Tukianzana na wafu waliokuwa baharini. Tabia ya bahari sikuzote ni kubwa, haina mwisho, ukipotea humo, umepotea moja kwa moja. Na kibiblia maji mengi(bahari) inamaanisha ulimwengu.
Ufunuo 17:15 “Kisha akaniambia, Yale maji uliyoyaona, hapo aketipo yule kahaba, ni jamaa na makutano na mataifa na lugha”.
Hii ikiwa na maana sikuile ya mwisho, wafu wote, yaani waovu wa mataifa yote, wa lugha zote, waliokufa tangu Adamu, hadi wakati wa kurudi kwa Bwana Yesu kulinyakuwa kanisa lake (siku ya unyakuo). Wote hao watakuwa katika kundi la wafu watokao baharini. Watafufuliwa na kuhukumiwa.
Mauti na kuzimu kulifunua nini?
Lakini mara baada ya unyakuo kupita. Kuna tukio lingine litafuata, ambalo linajulikana kama dhiki kuu.
Kipindi hichi kinajulikana kama kipindi cha utawala wa shetani(mpinga-kristo), watu wengi sana watauliwa, kutokana na dhiki ambayo Mungu ataruhusu shetani aisababishe, kwa waovu wote, watakaobakia duniani. (Tukiachia mbali wale ambao watakataa chapa ya mnyama). watauawa.
Ukisoma Ufunuo 6:8 inasema.
“Nikaona, na tazama, farasi wa rangi ya kijivujivu, na yeye aliyempanda JINA LAKE NI MAUTI, NA KUZIMU AKAFUATANA NAYE. Nao wakapewa mamlaka juu ya robo ya nchi, waue kwa upanga na kwa njaa na kwa tauni na kwa hayawani wa nchi”.
Umeona huyu farasi wa kijivujivu anaitwa mauti, akiambatana na kuzimu. Ambaye ni ibilisi akifanya kazi yake wakati huo. Naye atasababisha vifo vya robo ya watu waliopo duniani wakati huo. Kwamfano kwa dunia ya sasa ni Zaidi ya watu BILIONI 2, watauawa, na hiyo itakuwa ni katika mapigo ya ghadhabu ya Mungu, na vita vya Harmagedoni, na magonjwa, na wote hawa watakaokufa moja kwa moja watakuwa chini ya “Mauti na kuzimu”.
Sasa biblia inaposema Mauti na Kuzimu ikatoa wafu wake, umeshaelewa kuwa ni wafu waliokufa katika hichi kipindi cha Dhiki kuu, ambao kimsingi walikuwa chini ya mpanda farasi wanne, aliyeitwa mauti na kuzimu.
Sasa kwanini sehemu zote mbili zitajwe?
Ni kuonyesha kuwa hukumu hiyo haitambakisha mfu hata mmoja. Itakuwa ni hukumu ya ulimwengu mzima kwa wale ambao hawakunyakuliwa, Au kuikataa cha ya mnyama.
Ikiwa leo hii umekufa kama mlevi, au fisadi, au kihaba, utakapokufa utakwenda katika Habari la kiroho. Lakini ikiwa utakufa katika dhiki kuu, vilevile utakwenda katika katika mauti na kuzimu. Na wote siku ya mwisho mtafufuliwa. Na kuhukumiwa, kila mmoja kwa kipimo chake. Kisha mtatupwa katika ziwa la moto.
Ndugu, hukumu ya Mungu ni ya kuiogopa sana, kwasababu hakuna nafasi ya pili baada ya kifo. Ukifa leo ghafla, ni moja kwa moja jehanamu ukisubiria siku hiyo ya ufufuo ifike, Kwanini hayo yote yatukute? Watu walio kuzimu leo hii Ni kilio na majuto ndivyo vinavyoendelea, wanatamani wangepata hata dakika 2 za kutubu lakini hawana. Wewe muda unao. Lakini unafurahia ulimwengu.
Mgeukie Kristo, leo akusamehe dhambi zako. Tubu kwa kumaanisha kabisa kuuacha ulimwengu na tamaa zake zote. Dhamiria kumfuata Yesu, naye atakuokoa, katika dakika hizi za majeruhi. Kumbuka Unyakuo ni wakati wowote, hilo linafahamika. Muda umeisha, dalili zote zimeshatimia. Mlango wa neema kwa mataifa hivi karibuni utafungwa.
Maran Atha.
DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.
MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.
MAOMBOLEZO YA HADADRIMONI.
Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita.
MPINGA-KRISTO
UTAWALA WA MIAKA 1000.
DOWNLOAD PDF
WhatsApp
Injili ya Yesu Kristo imejificha katika viumbe vya asili. Bwana mahali biblia inamfananisha Bwana Yesu na Mwanakondoo, sehemu nyingine kama Simba, sehemu nyingine Bwana Yesu anafanishwa na “Jiwe” , mahali pengine Roho Mtakatifu anafanishwa na Huwa (njiwa).
Lakini pia kuna mahali Bwana Yesu alituwaambia tuwatazame kunguru pamoja na Maua ya kondeni (Luka 12:24), na sehemu nyingine aliufananisha mbinguni na Wafanya biashara, na sehemu nyingine wakulima, na sehemu nyingine aliufananisha na wavuvi wanaokwenda kuvua..Na sehemu nyingine aliwafananisha watu kama samaki wanapaswa kuvuliwa.
Kwahiyo kwa ufupi ni kwamba Injili ya Bwana Yesu Kristo imejificha pia katika viumbe vya asili. i.
Hivyo wakati mwingine hatuna budi kujifunza juu ya baadhi ya viumbe, na kupata hekima..
Leo tutamtazama Samaki mmoja aitwaye Eeli.
Je unamjua Samaki aina ya Eeli? Je unayajua maajabu yake?, na Injili gani imejificha nyuma ya Maisha yake?
Eeli ni Samaki ambao ni familia moja na Kambale. Samaki hawa wanaishi katika maji mafupi, . Lakini Samaki hawa maajabu yake ni kwamba wanatengeneza umeme mkubwa sana katika miili yao, ambao umeme huo wanautumia kujilinda dhidi ya maadui na kujitafutia vitoweo.
Eeli anapokumbana na hatari mbele yake, labda Samaki mwingine aliye mkubwa kuliko yeye, au kiumbe kingine chenye kutishia usalama wake, basi huitoa shoti hiyo na kumpiga adui yake.
Na kiwango cha umeme Samaki Eeli mmoja anachoweza kuzalisha kwa pigo moja ni mpaka Volti 650, na wakati Volti za 150 tu zinatosha kumuua Mwanadamu, lakini yeye hutoa hadi volti hizo 650, ambazo kama zikimfikia mwanadamu, sio tu kumuua papo kwa hapo, bali pia zinaweza kumuunguza viungo vyake vya ndani.
Lakini Pamoja na kwamba Samaki huyu, anayo silaha hatari namna hiyo kuliko samaki wote, ambayo inaweza kumuua mtu au kiumbe hai chochote ndani ya dakika moja, lakini bado ni Samaki mpole sana, bado hayupo katika orodha ya viumbe au viumbe hatari duniani. Hayupo hata 100 bora ya viumbe hatari, hata samaki sangara kamzidi kwa ukali!.
Ni samaki ambaye ni hatari sana lakini anayejihadhari sana na maadui zake, na asiyetumia uwezo wake wote kiasi kwamba hata ikitokea kakanyagwa na mtu ndani ya maji kwa bahati mbaya, yeye hutoa kiwango kidogo tu cha shoti, ambacho kitamshtua adui yake, amwache au akae mbali naye lakini si kumuua kabisa.
Tofauti na Samaki wengine kama samaki jiwe, au jelly au papa ambao hawana silaha kali kama hiyo, lakini ni wakorofi mno, kiasi kwamba akipita adui mbele yao, au akihisi hatari basi ana uwezo wa kutumia uwezo wake wote, kudhuru.
Laiti Eeli angekuwa mwenye hasira kama za Papa, au samaki mwingine yeyote, leo hii engeshika nafasi ya kwanza kwa viumbe hatari ulimwenguni. Kwasababu hakuna kiumbe chochote chenye silaha kali kama hiyo, hata nyoka ijapokuwa sumu yake ni kali na inayoua kwa haraka, kama mtu hajapatiwa matibabu..
Eeli yeye silaha yake ya shoti, inaua papo kwa hapo endapo akitumia uwezo wake wote. Na kutokana na maisha yake hayo imemfanya kuwa moja ya samaki wanaoishi muda mrefu sana, mpaka kufikia miaka 85.
Ni nini tunajifunza kwa Eeli?
Na sisi kama watu wa Mungu, tunazungukwa na nguvu za Mungu, kwa kiwango kikubwa sana… Lakini Nguvu hizi hatupaswi kuzitumia kuharibu wengine, nguvu hizi zimo ndani yetu, kutulinda tu na mishale ya yule adui, lakini si kutufanya tuonekane watofauti duniani.
Hebu tumtazame mmoja aliyekuwa kama huyu Samaki Eeli, ambaye alikuwa na nguvu nyingi kuliko wote, lakini hakuutumia uwezo wake wote..
Tusome,
Luka 9:51 “Ikawa, siku za kupaa kwake zilipokuwa karibu kutimia, yeye aliukaza uso wake kwenda Yerusalemu; 52 akatuma wajumbe kutangulia mbele ya uso wake; wakaenda wakaingia katika kijiji cha Wasamaria, ili kumtengenezea mahali. 53 Lakini wenyeji hawakumkaribisha kwa vile alivyouelekeza uso wake kwenda Yerusalemu. 54 Wanafunzi wake Yakobo na Yohana walipoona hayo, walisema, Bwana, wataka tuagize moto ushuke kutoka mbinguni, uwaangamize; [kama Eliya naye alivyofanya]? 55 Akawageukia, akawakanya. [Akasema, Hamjui ni roho ya namna gani mliyo nayo.] 56 Kwa maana Mwana wa Adamu hakuja kuziangamiza roho za watu, bali kuziokoa. Wakaondoka wakaenda mpaka kijiji kingine”.
Luka 9:51 “Ikawa, siku za kupaa kwake zilipokuwa karibu kutimia, yeye aliukaza uso wake kwenda Yerusalemu;
52 akatuma wajumbe kutangulia mbele ya uso wake; wakaenda wakaingia katika kijiji cha Wasamaria, ili kumtengenezea mahali.
53 Lakini wenyeji hawakumkaribisha kwa vile alivyouelekeza uso wake kwenda Yerusalemu.
54 Wanafunzi wake Yakobo na Yohana walipoona hayo, walisema, Bwana, wataka tuagize moto ushuke kutoka mbinguni, uwaangamize; [kama Eliya naye alivyofanya]?
55 Akawageukia, akawakanya. [Akasema, Hamjui ni roho ya namna gani mliyo nayo.]
56 Kwa maana Mwana wa Adamu hakuja kuziangamiza roho za watu, bali kuziokoa. Wakaondoka wakaenda mpaka kijiji kingine”.
Hapo Bwana Yesu alikuwa ana uwezo wa kushusha moto, na ndani ya dakika moja wale wale wasamaria wangekufa wote, bila kubakia hata mmoja lakini, hakuutumia uwezo wake huo, bali aliwarehemu kwasababu alikuwa anajua hawajui watendalo. Soma tena kisa kama hicho hicho katika Mathayo 26:51-53.
Na sisi pia hatuna budi kuwa kama Bwana Yesu..Bwana Yesu alipigwa lakini hakurudishwa, ingawa alikuwa na uwezo wa kurudisha mapigo makali, alitukanwa lakini hakurudisha matusi, aliambishwa lakini hakuabisha, ingawa alikuwa na uwezo wa kuabisha..n.k.
Alikuwa mfano wa Eeli ambaye anao uwezo mwingi lakini ni pole..
Wafilipi 4:5 “Upole wenu na ujulikane na watu wote. Bwana yu karibu”.
Hatupaswi kuwalaani watu kwa jina la Bwana, hata kama wanatumia nguvu za giza, tunachopaswa kukilaani na kukiharibu ni zile kazi wanazozifanya, na tunazilaani kwa kuomba, kuhubiri, kusoma Neno na kuishi maisha matakatifu..
Tuwe kama Eeli.
UNAMCHUKULIA YESU KWAKO KAMA NANI?
NI KWA NAMNA GANI SHETANI ANAIZUIA INJILI?
Je! Ni kweli kuna samaki mtu (Nguva) Baharini.
UVUVI BORA HAUCHAGUI, CHA KUVUA.
Nini tofauti ya Uwezo na Uweza kibiblia?
SWALI: Mwandishi, alimaanisha nini, kusema Mimi ni mweusi-mweusi, lakini ninao uzuri, msinichunguze kwa kuwa ni mweusi-mweusi? (Wimbo 1:5-6)
JIBU: Tusome,
Wimbo 1:5 “Mimi ni mweusi-mweusi, lakini ninao uzuri, Enyi binti za Yerusalemu, Mfano wa hema za Kedari, Kama mapazia yake Sulemani. 6 Msinichunguze kwa kuwa ni mweusi-mweusi, Kwa sababu jua limeniunguza. Wana wa mamangu walinikasirikia, Waliniweka niwe mlinzi wa mashamba ya mizabibu; Bali shamba langu mwenyewe sikulilinda”.
Wimbo 1:5 “Mimi ni mweusi-mweusi, lakini ninao uzuri, Enyi binti za Yerusalemu, Mfano wa hema za Kedari, Kama mapazia yake Sulemani.
6 Msinichunguze kwa kuwa ni mweusi-mweusi, Kwa sababu jua limeniunguza. Wana wa mamangu walinikasirikia, Waliniweka niwe mlinzi wa mashamba ya mizabibu; Bali shamba langu mwenyewe sikulilinda”.
Huyu ni mwanamke , anayejaribu kueleza hali yake ya nje jinsi inavyoonekana, ilivyo tofauti na uhalisia wake wa ndani. Anaanza kwa kusema mimi ni mweusi-mweusi, lakini ninao uzuri, Yaani japokuwa naonekana ni mweusi, nisiyevutia, lakini ninao uzuri wa kupendwa hata na mfalme,
Mstari wa 6 anaendelea kueleza Weusi wake, ulitokana na nini,.. Anasema, ulitokana na kazi za mashambani, ambazo aliwekwa kama mlinzi azisimamie, ikiwa na maana muda wote a jua linapochomoza jua linapozama, ni lazima awepo pale alitunze,
Wakati ndugu zake, wakiwa wamestarehe nyumbani kwenye uvuli wa makasri, wakila na kufurahi, yeye yupo mashambani anatanga na jua.
Na kwa kawaida, mtu anayekaa kwenye jua muda mrefu Ngozi yake itakuwa nyeusi tu, na vilevile itapunguza mvuto. Ndicho kilichomkuta huyu binti, aliyekuwa tofauti na mabinti wengine, kama ilivyozoeleka kuwa mabinti huwa hawakai mashambani, wala hawafanyi shughuli za ulinzi, . Lakini yeye alikuwa hivyo, na katika hayo yote anasema bado anaoozuri unaotoka ndani.
Huyu binti anafananishwa na watumishi wa Mungu, wanaotumika katika shamba la Mungu, ambao pengine kutwa kucha wanajitaabisha kuwapelekea wengine Habari njema,(Vijinini na mijini, na kwa njia mbalimbali), sasa kwa taabu hizo, kwa kawaida ni lazima watakosa vitu vingi vyema, kwasababu muda wote wapo mashambani, pengine watakuwa wadhaifu kimwili/au kimwonekano, watakuwa hawana mali, watakuwa hawana mvuto wowote. Lakini Bwana anawaona ni wazuri sana,
Mtume Paulo aliliona hilo akasema,
2Wakorintho 4:16 Kwa hiyo hatulegei; bali ijapokuwa utu wetu wa nje unachakaa, lakini utu wetu wa ndani unafanywa upya siku kwa siku. 17 Maana dhiki yetu nyepesi, iliyo ya muda wa kitambo tu, yatufanyia utukufu wa milele uzidio kuwa mwingi sana; 18 tusiviangalie vinavyoonekana, bali visivyoonekana. Kwa maana vinavyoonekana ni vya muda tu; bali visivyoonekana ni vya milele.
2Wakorintho 4:16 Kwa hiyo hatulegei; bali ijapokuwa utu wetu wa nje unachakaa, lakini utu wetu wa ndani unafanywa upya siku kwa siku. 17 Maana dhiki yetu nyepesi, iliyo ya muda wa kitambo tu, yatufanyia utukufu wa milele uzidio kuwa mwingi sana;
18 tusiviangalie vinavyoonekana, bali visivyoonekana. Kwa maana vinavyoonekana ni vya muda tu; bali visivyoonekana ni vya milele.
Kuonyesha kuwa utu wetu wa nje, waweza kuchakaa kwasababu ya utumishi, lakini ule wa ndani wafanywa upya kila siku, Sehemu nyingine aliandika Maisha ya utumishi ni ya kufa kila siku, kujitoa kwa wengine na sio kwa ajili yako, kama huyu binti (1Wakorintho 15:31).
Hivyo na wewe ambaye, unamtumikia Bwana kwa uaminifu, pengine wajiuliza, mbona mwonekano wangu haupo, kama nilivyokuwa hapo nyuma simtumikii? Fahamu kuwa upo shambani, jua litakuwa ni lako, lakini uzuri wako unatoka ndani na Mungu anauona, na anapendezwa na wewe.
Siku zitakuja, utapewa mwili wa utukufu, mwili usioonja uharibifu, mwili wa milele, ndipo utakapojua kuwa wewe ulipendwa na Bwana, na hiyo haikuwa kwa mwonekano wako, lakini kwa uaminifu wako.
UBATILI.
KUJIPAMBA NI DHAMBI?
Biblia ina maana gani inaposema akonyezaye kwa jicho huleta masikitiko?
Biblia inamaana gani kusema “vipo sita, naam saba”?
Kuvyaza ni nini katika biblia? (Ayubu 21:10).
KWANINI MIMI?
ANGALIA UZURI WAKO, USIGEUKE KUWA KITANZI CHAKO.
NJIA NYINGINE YA KUPATA REHEMA NA KIBALI KUTOKA KWA MUNGU.
Je unajua ubatizo unaua na vile vile unaokoa?.
Ipo siri kubwa sana katika ubatizo ambayo laiti watu wengi wangeijua wangeutafuta kwa bidii zote.
Hebu tusome mistari ifuatayo,
1 Petro 3:20 “watu wasiotii hapo zamani, uvumilivu wa Mungu ulipokuwa ukingoja, siku za Nuhu, safina ilipokuwa ikitengenezwa; ambamo ndani yake wachache, yaani, watu wanane, WALIOKOKA KWA MAJI. 21 MFANO WA MAMBO HAYO NI UBATIZO, UNAOWAOKOA NINYI PIA SIKU HIZI; (siyo kuwekea mbali uchafu wa mwili, bali jibu la dhamiri safi mbele za Mungu), kwa kufufuka kwake Yesu Kristo”.
1 Petro 3:20 “watu wasiotii hapo zamani, uvumilivu wa Mungu ulipokuwa ukingoja, siku za Nuhu, safina ilipokuwa ikitengenezwa; ambamo ndani yake wachache, yaani, watu wanane, WALIOKOKA KWA MAJI.
21 MFANO WA MAMBO HAYO NI UBATIZO, UNAOWAOKOA NINYI PIA SIKU HIZI; (siyo kuwekea mbali uchafu wa mwili, bali jibu la dhamiri safi mbele za Mungu), kwa kufufuka kwake Yesu Kristo”.
Hapo kuna vitu 3 vya kuzingatia katika mistari hiyo..na tutatazama kipengele kimoja baada ya kingine.
1. WATU WANANE WALIOKOKA KWA MAJI.
Hapa tunachoweza kuona ni kwamba..“kumbe maji ni njia ya wokovu?”. Nuhu pamoja na mkewe na wanawe watatu na wake zao, jumla nafsi 8, waliokoka kwa maji!!!!!
Wakati wengine wasioamini wanaangamia kwa maji, Nuhu aliyeamini, maji hayo hayo yanamwokoa na ghadhabu ya Mungu. Hili ni jambo la kwanza la kuzingatia…hebu tulitazame jambo la pili.
2. MFANO WA MAMBO HAYO NI UBATIZO, UNAOWAOKOA NINYI PIA SIKU HIZI.
Kumbe kama Nuhu alivyookoka kwa Maji zamani hizo, na sisi siku hizi hatuna budi kuokoka kwa kupitia maji hayo hayo? Yaani kwa Kubatizwa. Si ajabu Bwana Yesu alisema katika Marko 16:16 kuwa..“Aaminiye na kubatizwa ataokoka”..na si “atakayeamini tu peke yake”
Huu ni ufunuo mkubwa sana ambao Mtume Petro alifunuliwa na Roho Mtakatifu..
Kumbe wakati sisi tunasoma habari za gharika ya Nuhu kama gazeti, kumbe nyuma yake kuna ufunuo wa ubatizo..
Si ajabu na Yohana Mbatizaji pengine naye alitolea ufunuo wa ubatizo humu humu. Unapomwamini Yesu (Ni sawa na umeingia ndani ya safina kama Nuhu)..unapobatizwa kwa kuzamishwa katika maji mengi na kuibuka juu (Ni sawa na umeingia kwenye gharika ukiwa ndani ya safina na umetoka salama).
Na kama vile baada ya gharika Mambo yote yakawa mapya kwa Nuhu, akaingia katika ulimwengu mpya na kuanza maisha mapya, yale ya kwanza yenye shida na dhuluma na maasi yamepita. (Kwa ufupi uchafu wote wa kwanza ukaondoka).
Vivyo hiyo na sisi tunapobatizwa katika roho tunaondoa uchafu wote unaozunguka maisha yetu ya kiroho… Yale maisha ya kale yanazikwa, zile dhambi za kale zinaisha nguvu, kile kiburi cha kale kinafifia n.k Faida hii kuu inatupeleka katika kipengele cha tatu na cha mwisho.
3. SIYO KUWEKEA MBALI UCHAFU WA MWILI, BALI JIBU LA DHAMIRI SAFI MBELE ZA MUNGU.
Kumbe lengo la ubatizo sio kuondoa uchafu wa mwilini kama JASHO au VUMBI..bali ni kuondoa uchafu wa rohoni ambao huo ndio jibu la Dhamiri zetu safi mbele za Mungu.
Swali ni Je! umebatizwa ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Bwana Yesu kulingana na Matendo 2:38?.
Kama bado unasubiri nini na tayari umeshajua faida zote hizi?..Haraka sana katafute ubatizo sahihi, kwa gharama zozote baada ya wewe kumwamini Bwana Yesu na kutubu dhambi zako.
Kama unapata ugumu kupata sehemu ya ubatizo, basi unaweza kuwasiliana nasi kwa namba zilizopo chini ya somo, tutakusaidia, kukuelekeza mahali karibu na ulipo.
UBATIZO NI NINI NA ULIO SAHIHI NI UPI?
KWANINI UBATIZO NI WA MUHIMU.
Je! Ni kweli ubatizo wa maji hatuuhitaji tena?
Je! Unaweza kubatizwa na usipokee Roho Mtakatifu?. Na Je! Unaweza kupokea Roho Mtakatifu kwa kuwekewa mikono?
JE! UMEBATIZWA UBATIZO SAHIHI?
Sulemani kwa uvuvio wa Roho alipewa kujua kati ya mambo sita yanayomchukiza Mungu, mojawapo ni mikono imwagayo damu za watu.(Mithali 6:17).
Na sehemu nyingi sana katika maandiko utaona Bwana akiwakemea watu wake kwa dhambi hii ya umwagaji damu, kwamfano ukisoma hapa utaona anasema,
Isaya 1:15 “Nanyi mkunjuapo mikono yenu, nitaficha macho yangu nisiwaone; naam, mwombapo maombi mengi, sitasikia; mikono yenu imejaa damu. 16 Jiosheni, jitakaseni; ondoeni uovu wa matendo yenu usiwe mbele za macho yangu; acheni kutenda mabaya; 17 jifunzeni kutenda mema; takeni hukumu na haki; wasaidieni walioonewa; mpatieni yatima haki yake; mteteeni mjane”.
Isaya 1:15 “Nanyi mkunjuapo mikono yenu, nitaficha macho yangu nisiwaone; naam, mwombapo maombi mengi, sitasikia; mikono yenu imejaa damu.
16 Jiosheni, jitakaseni; ondoeni uovu wa matendo yenu usiwe mbele za macho yangu; acheni kutenda mabaya;
17 jifunzeni kutenda mema; takeni hukumu na haki; wasaidieni walioonewa; mpatieni yatima haki yake; mteteeni mjane”.
Soma na hapa pia;
Ezekieli 9:9 “Ndipo akaniambia, Uovu wa nyumba ya Israeli na Yuda ni mwingi sana, nayo nchi imejaa damu, nao mji umejaa kupotosha hukumu; maana husema, Bwana ameiacha nchi hii, naye Bwana haoni”.
Sehemu kadha wa kadha, Mungu alipowaona watu wake aliona damu nyingi mikononi mwao.. (Isaya 59:3, Yer 22:3, Eze 23:37, 45).
Sasa ni rahisi kudhani kuwa, katika mwili ni kweli walikuwa ni wauaji, wanawaua watu kwa siri au wanauana wao kwa wao ovyo . Hapana si kweli, Waisraeli hawakuwa hivyo. Kama tu vile walimwengu wengi wasasa walivyo leo.
Hivyo wenyewe hawakuelewa Mungu alikuwa anawaonaje matendo yao kwa jinsi ya Roho,
Hadi Bwana Yesu alipokuja kutufunulia jambo hilo katika agano jipya Mungu alikuwa anamaanisha nini;
Tusome.
1Yohana 3:15 “Kila amchukiaye ndugu yake ni mwuaji: nanyi mnajua ya kuwa kila mwuaji hana uzima wa milele ukikaa ndani yake”.
Akaeleza, kwa undani Zaidi, jinsi mtu wa namna hii ambaye, anamchukia ndugu yake, anavyostahili adhabu sawa tu na yule Mhalifu aliyemwaga damu ya mtu.
Mathayo 5:22 “Bali mimi nawaambieni, Kila amwoneaye ndugu yake hasira itampasa hukumu; na mtu akimfyolea ndugu yake, itampasa baraza; na mtu akimwapiza, itampasa jehanum ya moto”.
Ndugu unayesoma haya maneno, tufahamu kuwa, tunaweza tukawa ni waombaji wazuri, ni waalimu wazuri, ni wasaidizi wazuri, ni wachungaji wazuri, lakini mbele za Mungu tukawa watu hatari sana, tukaonekana kama wahalifu sugu kabisa, ambao tumeuwa roho za watu wengi sana, mikono yetu inabubujika damu, tumeshika visu, na mapanga, na mashoka, tunaua, na bado tunaendelea kuua watu kila siku. Sababu ni nini? Sababu ni chuki zilizopo mioyoni mwetu kwa watu wengine.
Tunapokuwa na visasi na watu, au hasira, Mungu anatuona tunastahili jehanamu ya moto. Hata sadaka yetu tunayompelekea yeye bado anaiona ni chukizo kubwa sana, ndio maana asema tusiitoe mpaka tutakapopatana kwanza na majirani zetu.
Mathayo 5:23 “Basi ukileta sadaka yako madhabahuni, na huku ukikumbuka ya kuwa ndugu yako ana neno juu yako, 24 iache sadaka yako mbele ya madhabahu, uende zako, upatane kwanza na ndugu yako, kisha urudi uitoe sadaka yako”.
Mathayo 5:23 “Basi ukileta sadaka yako madhabahuni, na huku ukikumbuka ya kuwa ndugu yako ana neno juu yako,
24 iache sadaka yako mbele ya madhabahu, uende zako, upatane kwanza na ndugu yako, kisha urudi uitoe sadaka yako”.
Hivyo, tujifunze kuachilia, ili tusiwe wauaji, na njia pekee ya kuweza kuishinda hiyo hali, ni kuwa mtu wa kutafakari sana Neno la Mungu. Kwani Neno ni tiba, inayotupa maonyo,na Faraja na ushauri, ukiona hiyo hali inakushinda, fahamu kuwa kiwango chako cha utafakariji wa maandiko ni kidogo..
Lakini tunaposoma lile Neno mfano lile andiko linalosema, ndugu yako akikusoma, mara ngapi umsamehe.. Na Bwana akajibu na kusema, hata SABA MARA SABINI.. Yaani mara 490, kwa siku moja,(Mathayo 18:22) tutagundua ni nini maana ya msamaha.. Ni Zaidi ya vile tunavyofikiria, ni Zaidi ya kuachilia mambo yote, na kukubali kuonekana mjinga, ni Zaidi ya kukubaliana na kila hali. Hapo ndipo tutakapojua hakuna sababu ya kushikamana na kila jambo ndugu zetu au marafiki, au majirani zetu wanayotufanyia, au kutuudhi kwayo.
Kwasababu katika hayo yote hawajawahi kuyarudia mara 490, kwa siku, pengine ni mara mbili tu au kumi. Hivyo tunapaswa tusamehe.
Bwana atusaidie sana, mkono yetu iwe safi kama ya mwanakondoo wake Yesu Kristo.
Ndipo tutakapomkaribia Bwana wetu na kutubariki.
Ayubu 17:19 “Lakini mwenye haki ataishika njia yake, Naye mwenye mikono safi atazidi kupata nguvu”.
RACA
KIFAHAMU KIGEZO CHA KUSAMEHEWA NA MUNGU.
MISTARI YA BIBLIA KUHUSU UPENDO.
Unyenyekevu ni nini?
JIFUNZE NAMNA YA KULITUMIA NENO LA MUNGU.
JE! DAMU INA UMUHIMU WOWOTE KATIKA MAISHA?
USIWE ADUI WA BWANA
MIAMBA YENYE HATARI.
Jina la Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo, libarikiwe.
Zipo njia nyingi za kuvuta rehema za Mungu, juu yako.. baadhi ya hizo ni kuwa Mwombaji, mtoaji, na mtu wa kusamehe.
Lakini ipo njia nyingine ambayo tukiijua basi, siku zote tutakuwa watu wa kupata rehema kutoka kwa Bwana na hata kama kuna mabaya tuliyofanya mbele za Mungu, basi anatusamehe na kughairi kutuadhibu.
Na njia hiyo si nyingine Zaidi ya “kutojilipiza kisasa” au kutofurahia “anguko la wanaofanya vita nawe”.
Watu wengi leo hususani Wakristo, wanakosa maarifa kwa kudhani kuwa Mungu anapendezwa sana na anguko la maadui zao. Hivyo kila siku, na kila saa wanawaombea shari maadui zao, na kila siku wanakaa wakisubiria anguko lao ili wafurahi.. (Kama vile Nabii Yona alivyokaa chini ya mtango, akingoja kuona Ninawi inaangamizwa).
Na hiyo yote ni kutokana na jinsi tulivyofundishwa au kujifunza. Pasipo kujua kuwa hayo sio mapenzi ya Mungu kabisa.. Ingekuwa Mungu ana hasira sana na adui yako, nadhani asingemuumba kabisa.. Lakini mpaka unamwona anaishi, jua ni mapenzi ya Mungu yeye awepo pale..
Sasa hebu tujifunze mstari ufuatao ili tuweze kuelewa vizuri..
Mithali 24:17 “Usifurahi adui yako aangukapo; Wala moyo wako usishangilie ajikwaapo; 18 Bwana asije akaliona hilo, likamkasirisha; Akageuzia mbali naye hasira yake”.
Mithali 24:17 “Usifurahi adui yako aangukapo; Wala moyo wako usishangilie ajikwaapo;
18 Bwana asije akaliona hilo, likamkasirisha; Akageuzia mbali naye hasira yake”.
Umeona hapo?..Anasema usifurahi, ukimwona adui yako anaanguka!.. kwasababu Bwana kamwangusha kwa lengo la kumnyenyekeza na si kwa lengo la kumwangamiza kabisa!, kama wewe unavyofikiri..
Hivyo unaposhangilia anapoadhibiwa na Mungu, jambo hilo halimpendezi kabisa Mungu… na Bwana akiona unashangilia kuanguka kwake, basi anaghairi ule ubaya na kukugeukia wewe. (Kwasababu na wewe sio kwamba ni mkamilifu mbele zake, kwamba haustahili adhabu yoyote, unazo kasoro nyingi sana, isipokuwa Mungu ni mvumilivu kwako).
Vile vile, watu wanaofanya vita na wewe na kukushutumu, kukusengenya, kukulaumu, kukuudhi, kukuumiza, au hata kukutesa pasipo hatia yoyote, usijaribu kamwe kuwarudishia mabaya, wala kuwashitaki mbele za Mungu, wewe waombee rehema…na kubali mashutumu yao..Kwasababu kwa kufanya hivyo, Mungu, sio kwamba utakuona wewe ni mjinga mbele zake, kinyume chake utaonekana mwenye busara na hivyo utapata rehema Zaidi na kibali mbele zake.
Usichukizwe na laana watu wanazokulaani, kwasababu laana hizo kwako, ndio baraka kwako, mashutumu hayo unayoshutumiwa, Mungu anayasikiliza na yanamhuzisha, hivyo Bwana atakupa wewe rehema kwa mashutumu hayo, atakuhurumiwa kwa masengenyo hayo…N.k
Daudi aliijua hii siri, ndio maana kamwe hakuwahi kutoa Neno la laana kwa waliokuwa wanamlaani, wala hakuwahi kufurahia kuanguka kwa waliokuwa wanaitafuta roho yake, ndio maana utaona alilia sana, siku Sauli alipokufa, vile vile alilia sana Absalomu, mwanae alipokufa!..ambao hawa wote walifanyika maadui zake.
Sasa ni kwanini hakuwalaani waliokuwa wanamlaani?, ni kwasababu alijua KUWA KULAANIWA KWAKE NA WATU NDIO KUBARIKIWA KWAKE NA BWANA.
Utakumbuka wakati Fulani alipokuwa anamkimbia Mwanae Absalomu, alikutana na mtu mmoja aliyeitwa Shimei, mtu huyo alianza kumlaani, lakini Daudi hakurudisha laana hata moja, wala hakumwua ingawa alikuwa anao huo uwezo.
2 Samweli 16:5 “Basi mfalme Daudi alipofika Bahurimu, tazama, kulitoka huko mtu wa jamaa ya nyumba ya Sauli, jina lake akiitwa Shimei, mwana wa Gera; ALITOKA, AKALAANI ALIPOKUWA AKIENDA. 6 Tena akamtupia Daudi mawe, na watumishi wote wa mfalme Daudi; na watu wote na mashujaa wote walikuwako mkono wake wa kuume na mkono wake wa kushoto. 7 Na Shimei alipolaani, alisema hivi, NENDA ZAKO! NENDA ZAKO! EWE MTU WA DAMU! EWE MTU USIYEFAA! 8 Bwana amerudisha juu yako damu yote ya nyumba ya sauli ambaye umetawala badala yake; naye bwana ametia ufalme katika mkono wa absalomu mwanao; kisha, angalia, wewe umetwaliwa katika uovu wako mwenyewe, kwa sababu umekuwa mtu wa damu. 9 Ndipo Abishai mwana wa Seruya, akamwambia mfalme, Mbona mbwa mfu huyu amlaani mfalme bwana wangu? Na nivuke, nakusihi, nikaondoe kichwa chake. 10 Mfalme akasema, Nina nini na ninyi, enyi wana wa Seruya? Kwa sababu yeye analaani, na kwa sababu Bwana amemwambia, Mlaani Daudi, basi, ni nani atakayesema, Mbona umetenda haya? 11 Daudi akamwambia Abishai, na watumishi wake wote, Angalieni, huyu mwanangu, aliyetoka viunoni mwangu, anautafuta uhai wangu; si zaidi Mbenyamini huyu sasa? MWACHENI ALAANI, KWA SABABU BWANA NDIYE ALIYEMWAGIZA. 12 LABDA BWANA ATAYAANGALIA MABAYA YALIYONIPATA, NAYE BWANA ATANILIPA MEMA KWA SABABU YA KUNILAANI KWAKE LEO. 13 Basi wakaendelea njiani Daudi na watu wake; SHIMEI NAYE AKAAENDELEA JUU YA UBAVU WA KILE KILIMA, KWA KUMKABILI, HUKU AKIENDELEA, AKILAANI, AKIMTUPIA MAWE, NA KURUSHA MAVUMBI”.
2 Samweli 16:5 “Basi mfalme Daudi alipofika Bahurimu, tazama, kulitoka huko mtu wa jamaa ya nyumba ya Sauli, jina lake akiitwa Shimei, mwana wa Gera; ALITOKA, AKALAANI ALIPOKUWA AKIENDA.
6 Tena akamtupia Daudi mawe, na watumishi wote wa mfalme Daudi; na watu wote na mashujaa wote walikuwako mkono wake wa kuume na mkono wake wa kushoto.
7 Na Shimei alipolaani, alisema hivi, NENDA ZAKO! NENDA ZAKO! EWE MTU WA DAMU! EWE MTU USIYEFAA!
8 Bwana amerudisha juu yako damu yote ya nyumba ya sauli ambaye umetawala badala yake; naye bwana ametia ufalme katika mkono wa absalomu mwanao; kisha, angalia, wewe umetwaliwa katika uovu wako mwenyewe, kwa sababu umekuwa mtu wa damu.
9 Ndipo Abishai mwana wa Seruya, akamwambia mfalme, Mbona mbwa mfu huyu amlaani mfalme bwana wangu? Na nivuke, nakusihi, nikaondoe kichwa chake.
10 Mfalme akasema, Nina nini na ninyi, enyi wana wa Seruya? Kwa sababu yeye analaani, na kwa sababu Bwana amemwambia, Mlaani Daudi, basi, ni nani atakayesema, Mbona umetenda haya?
11 Daudi akamwambia Abishai, na watumishi wake wote, Angalieni, huyu mwanangu, aliyetoka viunoni mwangu, anautafuta uhai wangu; si zaidi Mbenyamini huyu sasa? MWACHENI ALAANI, KWA SABABU BWANA NDIYE ALIYEMWAGIZA.
12 LABDA BWANA ATAYAANGALIA MABAYA YALIYONIPATA, NAYE BWANA ATANILIPA MEMA KWA SABABU YA KUNILAANI KWAKE LEO.
13 Basi wakaendelea njiani Daudi na watu wake; SHIMEI NAYE AKAAENDELEA JUU YA UBAVU WA KILE KILIMA, KWA KUMKABILI, HUKU AKIENDELEA, AKILAANI, AKIMTUPIA MAWE, NA KURUSHA MAVUMBI”.
Je na sisi leo hii tunaweza kukubali mashutumu namna hii?.. kiasi kwamba wanaotusengenya na sisi hatuwarudishii masengenyo, wala kuwalaumu?.. kiasi kwamba tunahuzunika kuanguka kwa wanaoshindana nasi?
Tukifikia hatua hii tutapata kibali sana Mbele za Mungu. Unaona Daudi hapo baada ya kukubali mashutumu na laana anasema.. “MWACHENI ALAANI, KWA SABABU BWANA NDIYE ALIYEMWAGIZA. LABDA BWANA ATAYAANGALIA MABAYA YALIYONIPATA, NAYE BWANA ATANILIPA MEMA KWA SABABU YA KUNILAANI KWAKE LEO. ”
Daudi alijua ili kupata Mema, hana budi kukubali laana, ili kupata kibali hana budi kukubali mashutumu. Na si Daudi peke yake, utaona pia na Ayubu, katika Maisha yake yote anasema hajawahi kufurahia anguko la wanaomchukia au wanaoshindana naye.. jambo lililomfanya apate kibali kikubwa sana mbele za Mungu, na kuonekana kuwa mkamilifu kuliko watu wote waliokuwepo chini ya jua katika kipindi chake..
Ayubu 31:29 “Kama nilifurahi kwa kuangamia kwake huyo aliyenichukia, Au kujitukuza alipopatikana na maovu; 30 (Naam, sikukiacha kinywa changu kufanya dhambi Kwa kuutaka uhai wake kwa kuapiza);”
Ayubu 31:29 “Kama nilifurahi kwa kuangamia kwake huyo aliyenichukia, Au kujitukuza alipopatikana na maovu;
30 (Naam, sikukiacha kinywa changu kufanya dhambi Kwa kuutaka uhai wake kwa kuapiza);”
Na sisi ili tupate rehema na kibali na baraka, na Mema kutoka kwa Mungu, hatuna budi kuwa kama Daudi na Ayubu..Ni kanuni inayoonekana kama ni ngumu, lakini ndio iliyokubalika mbele za Mungu. Injili za kupiga maadui, na kutwa kuchwa kushindana na maadui zako na kusubiria kuona shari yao ili ufurahie nataka nikuambie ni injili za kuzimu, ingawa kwa nje zinaonekana kama zina hekima.. Bwana Yesu Mkuu wa uzima alisema maneno haya..
Mathayo 5:43 “Mmesikia kwamba imenenwa, Umpende jirani yako, na, Umchukie adui yako; 44 lakini mimi nawaambia, WAPENDENI ADUI ZENU, WAOMBEENI WANAOWAUDHI, 45 ili mpate kuwa wana wa Baba yenu aliye mbinguni; maana yeye huwaangazia jua lake waovu na wema, huwanyeshea mvua wenye haki na wasio haki. 46 Maana mkiwapenda wanaowapenda ninyi mwapata thawabu gani? Hata watoza ushuru, je! Nao hawafanyi yayo hayo?”
Mathayo 5:43 “Mmesikia kwamba imenenwa, Umpende jirani yako, na, Umchukie adui yako;
44 lakini mimi nawaambia, WAPENDENI ADUI ZENU, WAOMBEENI WANAOWAUDHI,
45 ili mpate kuwa wana wa Baba yenu aliye mbinguni; maana yeye huwaangazia jua lake waovu na wema, huwanyeshea mvua wenye haki na wasio haki.
46 Maana mkiwapenda wanaowapenda ninyi mwapata thawabu gani? Hata watoza ushuru, je! Nao hawafanyi yayo hayo?”
Unataka Rehema?, unataka kibali?, unataka Mema kutoka kwa Mungu??.. huna budi kukubali mashutumu, kwasababu Kristo naye alikubali mashutumu na kejeli na kudharauliwa lakini sasa ana utukufu kuliko vitu vyote.
Bwana YESU ANARUDI!!
VITA DHIDI YA MAADUI
KUTUBU SIO KUOMBA REHEMA.
NJIA MUNGU ALIYOIWEKA KWA KILA JAMBO.
BASI, IWENI NA HURUMA, KAMA BABA YENU ALIVYO NA HURUMA
MLANGO MWINGINE WA ADUI KUTULETEA MAJARIBU.