DON’T BE AFRAID WHEN YOU GO DOWN.

JE YESU ATARUDI TENA?

Bwana Yesu alikuja, akaondoka naye atarudi tena?

Swali ni je! atarudi kufanya nini?

Jibu: Atarudi  kuitawala hii dunia pamoja na watakatifu wake, Biblia inasema dunia hii, enzi na Mamlaka amepewa Yesu na Mungu Baba…Mamlaka hayo, hapo mwanzo yalitoka kwa Mungu…akampa Adamu…Adamu akayapoteza, na shetani kuyachukua…Na alipokuja Yesu Kristo, shetani alinyanganywa mamlaka hayo na na kukabidhiwa Yesu Kristo. Hivyo ni lazima Kristo aje kutawala dunia..Kwasababu hakuna mamlaka yoyote isiyokuwa na Utawala.

Mathayo 28:18 “Yesu akaja kwao, akasema nao, akawaambia, Nimepewa mamlaka yote mbinguni na duniani”.

Na kama atakuja kutawala, wapo watu waovu wasioupenda utawala wake, hivyo hao atawaondoa..na wale wanaoupenda atawapa thawabu na nafasi za kutawala naye.

Ufunuo 2:20 “Tazama, nasimama mlangoni, nabisha; mtu akiisikia sauti yangu, na kuufungua mlango, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye pamoja nami.

21 Yeye ashindaye, nitampa kuketi pamoja nami katika kiti changu cha enzi, kama mimi nilivyoshinda nikaketi pamoja na Baba yangu katika kiti chake cha enzi”

Kwa urefu jinsi utawala huo utakavyokuwa fungua somo hapa chini lenye kichwa kinachosema UTAMBUE UTAWALA WA MIAKA 1000

Bwana akubariki.


Mada Nyinginezo:

UTAWALA WA MIAKA 1000.

KATI YA UNYAKUO WA KANISA, DHIKI KUU, VITA VYA HAR-MAGEDONI, UTAWALA WA MIAKA 1000, VITA YA GOGU NA MAGOGU, HUKUMU YA KITI CHA ENZI CHEUPE. JE, NI KIPI KINAANZA NA KINGINE KUFUATA?

BWANA ALIPOSEMA KUWA YEYE NI “MUNGU WA MIUNGU” ALIKUWA NA MAANA GANI?..JE! YEYE NI MUNGU WA SANAMU?

JE! WATAKAOENDA MBINGUNI NI WENGI?


Rudi Nyumbani:

Print this post

Mwanamke Mshunami

SWALI: Katika Biblia tunamsoma Mwanamke mmoja aliyeitwa Mshunami, ambaye alimsaidia Nabii Elisha sehemu ya malazi wakati wa huduma yake..Mwanamke huyu aliitwa Mshunami

2 Wafalme 4:12 “Akamwambia Gehazi mtumishi wake, Mwite yule Mshunami. Naye alipokwisha kuitwa, akasimama mbele yake. 13 Akamwambia, Sema naye sasa, Tazama, wewe umetutunza sana namna hii; utendewe nini basi? …”

Sasa Swali Mshunami maana yake nini?

JIBU: Ukisoma Mlango huo kuanzia juu kidogo, utaona kuwa Mshunami sio jina la mtu bali ni jina la sehemu..

2 Wafalme 4:8 “Hata ikawa siku moja, Elisha alikwenda Shunemu; na huko kulikuwa na mwanamke mmoja mwenye cheo; naye akamshurutisha aje ale chakula. Ikawa kila alipopita njia ile, huingia kula chakula”.

Kwahiyo Mshunami sio jina la Mtu, bali ni jina la mahali…Katika Israeli kulikuwa na mahali panapoitwa “SHENEMU” Kwahiyo mtu yeyote awe mwanamke au mwanamume kama ametokea sehemu hiyo basi aliitwa Mshunami…Ni sawa na nchi Tanzania, yeyote aliyetokea huko ataitwa Mtanzania.

Hivyo SHUNEMU ilikuwa ni Eneo la Israeli, lililokuwa urithi wa kabila la Isakari…Tunalithibitisha hilo katika kitabu cha…

Yoshua 19:17 “Kisha kura ya nne ilitokea kwa ajili ya Isakari, maana, ni kwa ajili ya wana wa Isakari kwa kuandama jamaa zao.

18 Na mpaka wao ulifikilia Yezreeli, na Kesulothi, na Shunemu

Na sio tu huyu mwanamke aliyemsaidia Nabii Elisha alitokea huko shunemu, kuna wanawake wengine pia biblia imerekodi walitokea huko huko shunemu…Mmoja wapo na Abishagi aliyeletwa kwa Mfalme Daudi

1 Wafalme 1:3 “Basi wakatafuta kijana mzuri mipakani mwote mwa Israeli, wakamwona Abishagi, Mshunami, wakamleta kwa mfalme.

4 Naye kijana huyo alikuwa mzuri sana; akamtunza mfalme, akamtumikia; walakini mfalme hakumjua”

Mungu akubariki


Mada Nyinginezo:

VIFUNGO VYA GIZA VYA MILELE.

TUSIFUNGWE NIRA PAMOJA NA WASIOAMINI.

KWANINI TUWE WENYE BUSARA KAMA NYOKA?

JE! NI KWELI DUNIA ILIUMBWA TAKRIBANI MIAKA 6000 ILIYOPITA? NA JE! SHETANI ALIKUWEPO DUNIANI WAKATI DUNIA INAUMBWA?

TUMEAMBIWA TUNAPOSALI TUSIPAYUKE-PAYUKE, JE! HUKO KUPAYUKA PAYAUKA NDIO KUPI?


Rudi Nyumbani:

Print this post

KUOTA UNAPAA.

Mpaka mtu au kitu kiweze kupaa ni wazi kuwa kimefanikiwa kushinda hali inayoweza kukivuta chini. Na ndio maana kinachopaa kama ndege huwa kina kasi zaidi na kinaona mbali sana tofauti na kitu kinachotembea. Hata mtu akijiona kwenye ndoto anapaa kutoka sehemu moja hadi nyingine huwa anajiona ni mwepesi sana, na anayokasi tofauti na anavyoota ndoto nyingine.

Sasa ndoto hizi zinaweza kutoka katika vyanzo viwili, chanzo cha kwanza ni kwa Yule mwovu. ili kujua ndoto uliyoota inatoka kwa Yule mwovu, utaona pengine unapaa na watu usiowajua na wanakupeleka usipojua, au unaenda sehemu za kutisha, na unapoamka unakuwa huna amani umejawa na hofu na wasiwasi mwingi, ukiona hivyo fahamu kuwa ndoto hiyo ni ya kutoka kwa Yule mwovu, hivyo kama wewe ni mkristo, unapaswa uikemee saa hiyo hiyo kwa jina la YESU na mambo kama hayo hayatakutokea tena..

Lakini ikiwa unaota unapaa tu katika mazingira ya kawaida labda tuseme nyumbani, au hata kama ni maeneo usiyoyajua lakini ni ya asili na unajiona unaowezo wa kuruka mbali sana kama vile upo mwezini, na ndoto hiyo inajirudia rudia na ukiamka huoni chochote,kawaida tu, basi unapaswa uzingatie kwasababu ni Mungu anakupitishia ujumbe wake hapo na hivyo umefanya vema kutafuta kujua tafsiri yake.

Sasa kama bado upo nje ya YESU KRISTO, Mungu anakuonya furaha yako, au mafanikio yako, ni ya muda tu, Kwasasa unaweza ukawa katika hali ambayo huwezi ukajifananisha na wengi, pengine umefanikiwa, au umesoma zaidi, au umepiga hatua Fulani, lakini mwisho wako utakuwa ni mbaya sana, kama hutamrudia muumba wako. Unapojiona unapaa ni ishara ya kufanikiwa Fulani.

Ayubu 20:4 “Je! Hujui neno hili tangu zamani za kale, Tangu wanadamu kuwekwa juu ya nchi,

5 Ya kuwa shangwe ya waovu ni kwa muda kidogo, Na furaha ya wapotovu ni ya dakika moja tu?

6 Ujapopanda ukuu wake mpaka mbinguni, Na kichwa chake kufikilia mawinguni;

7 Hata hivyo ataangamia milele kama mavi yake mwenyewe; Hao waliomwona watasema, Yuko wapi?

8 ATARUKA MFANO WA NDOTO, asionekane; Naam, atafukuzwa kama maono ya usiku,”

Hivyo tubu umgeukie Mungu, kama ulikuwa unafanya mambo maovu, Tubu, uishi kama mkristo, kama ulikuwa unafanikiwa kutoka katika biashara haramu kama uuzaji pombe, au madawa ya kulevya,  au rushwa au ushirikina acha mara moja mgeukie yeye…Bwana YESU anasema itakufaidia nini kuupata ulimwengu mzima halafu upate hasara ya nafsi yako.?..Unafanikiwa sasa lakini mafanikio yako yatakupoteza hivyo mgeukie Mungu..Bwana anakupenda na ndio maana anakuotesha ndoto za namna hiyo.

Lakini kama upo ndani ya Kristo, basi fahamu kuwa Mungu anakusisiza uzidi kumtazama yeye zaidi kwasababu anaompango wa kukushushia vipawa vya kimbinguni zaidi, kwasababu sikuzote mbinguni ndipo vipawa vilipo..

Zaburi 68:18 “Wewe umepaa juu, umeteka mateka, Umepewa vipawa katikati ya wanadamu; Naam, hata na wakaidi, Bwana Mungu akae nao”.

Hivyo songa mbele, kama ulikuwa unalegalega ungeza nguvu zaidi Bwana yupo karibu na wewe usiangalie mazingira yanayokuzunguka, zidi kumtafuta Mungu kwa bidii.ili kupaa kwako kusiishie tu hapa duniani bali mpaka mbinguni..Kama vile Kristo, alimpendeza Mungu akapaa hadi mbinguni kwa Baba, na sisi pia tumewekewa siku moja ya kupaa  moja kwa moja na siku hiyo ndio ile siku ya UNYAKUO ambayo tutwenda kumlaki Bwana Yesu mawinguni. Maran Atha!

Ubarikiwe!

Group la whatsapp Kwa mgawanyo bora wa masomo download App hapa>> App wingu la mashahidi

Mada Nyinginezo:

KUOTA UPO UCHI.

KUOTA UNAFANYA MTIHANI.

KUOTA NYOKA.

KUOTA MTU ALIYEKUFA.

FUATILIA NDOTO HII, UTAJIFUZA KITU.

MTETEZI WAKO NI NANI?

UNYAKUO.


Rudi Nyumbani:

Print this post

MATESO YA MWENYE HAKI

Zaburi 34:19 “Mateso ya mwenye haki ni mengi, Lakini Bwana humponya nayo yote”.

Wengi wanauliza inawezekana mwenye haki akapitia mateso?..Jibu ni ndio! Mwenye haki anapitia mateso..

Tunaweza kuchukua mifano kadhaa katika Maandiko, Yusufu alikuwa mwenye haki, alimheshimu Baba yake kuliko kaka zake 11, hakusema uongo kwa Baba yake, na zaidi ya yote alipendwa na Baba yake kutokana na haki yako..Lakini tunasoma alipitia mateso makali…Alinusurika kuuawa na ndugu zake, aliuzwa Utumwani, akawa mtumwa, zaidi akafungwa gerezani akakaa huko sehemu ya mateso kwa miaka mitatu. Lakini kama maandiko yanavyosema Mateso ya mwenye haki ni Mengi lakini Bwana atamponya nayo yote. Hataacha hata moja!!

Tangu akiwa na kijana wa miaka 16 mateso yake ndio yalianza, na yalikuja kupungua akiwa na miaka 30 na kuisha kabisa akiwa na miaka 37…Bwana alimponya nayo yote…

Kadhalika Ayubu, alipotelewa na mali zake zote ndani siku moja, kondoo, Mbuzi, punda, ngamia, Wafanyakazi na zaidi ya yote akafiwa na Wanawe wote na akakaa vile kwa muda mrefu mpaka mkewe akamshauri amkufuru huyo Mungu wake akafe…Lakini Biblia inasema Mateso ya mwenye haki ni mengi, lakini Bwana atamponya nayo yote..

Ulipofika wakati wa kuponywa alivipata vyote alivyovipoteza kwa wakati mmoja na mara mbili zaidi.

Ipo mifano Mingi, unaweza ukaenda kuisoma mwenyewe, mifano kama ya akina Hana, Yefta, Daudi, Ruthu, Bathsheba, n.k

Wa  mwisho mwenye haki kuliko wote na aliyepitia Mateso makuu kuliko wote ni BWANA WETU YESU KRISTO, Huyo alitemewa mate wazi wazi bila kosa lolote je wewe ambaye una dhambi ulishawahi kuchukiwa kiasi hicho cha kutemewa mate wazi wazi?!..yeye alisulibiwa akiwa tupu, je wewe ulishawahi kuchukiwa kiasi cha watu kufikiria kukuua kikatili kiasi hicho?

Kwahiyo kama unapitia mateso kwa ajili ya Imani yako nataka nikupe Moyo, Bwana atakuponya nayo yote, haijalishi ni siku ngapi, wiki, miezi au miaka mingapi itapita lakini siku moja utauona wokovu wa Bwana. Kama Bwana Yesu alivyouona wa Mungu kumfufua na kumweka juu sana zaidi hata ya Malaika.

Hivyo ukipitia mateso mtafakari Yesu,  yeye aliponywa nawe utaponywa!

Waebrania 12:2 “tukimtazama Yesu, mwenye kuanzisha na mwenye kutimiza imani yetu; ambaye kwa ajili ya furaha iliyowekwa mbele yake aliustahimili msalaba na kuidharau aibu, naye ameketi mkono wa kuume wa kiti cha enzi cha Mungu.

3 Maana mtafakarini sana yeye aliyeyastahimili mapingamizi makuu namna hii ya watendao dhambi juu ya nafsi zao, msije mkachoka, mkizimia mioyoni mwenu”.

Ubarikiwe sana, Kama Hujampa Yesu Maisha yako, Ni vyema ukafanya hivyo kabla siku ya Unyakuo haijafika.


Mada Nyinginezo:

IKO NJIA IONEKANAYO KUWA SAWA MACHONI PA MTU.

MNGOJEE BWANA

JE! MUNGU ANAUPENDELEO KWA WANAUME ZAIDI YA WANAWAKE?

JE! KUFANYA MASTURBATION (PUNYETO) NI DHAMBI?


Rudi Nyumbani:

Print this post

KUOTA UPO UCHI.

Ufunuo 16:15 “(Tazama, naja kama mwivi. Heri akeshaye, na kuyatunza mavazi yake, asiende uchi hata watu wakaione aibu yake.)”

Kipindi Fulani nyuma kabla sijampa Bwana maisha yangu, niliota ndoto moja ambayo hadi leo sitaisahau, niliota nimejikuta nipo uchi, halafu nakatiza barabarani mjini maeneo ya posta Dar es salaam, sasa nilipojiona nipo vile nikawa ninatafuta namna ya kujificha..

Nikawa ninajibanza banza kwenye vikona vya majengo, nikivizia watu wapungue kisha nikimbilie upande mwingine, hivyo hivyo hadi kigiza kingie nikimbilie nyumbani, na kweli nilifanikiwa kujificha ficha hivyo hivyo nisionekane na watu au marafiki zangu mpaka nilipofanikiwa kufika  nyumbani nikafurahi sana kwasababu nilijiona kama sijaoenekana  na watu wengi, hususani na wanaonijua, lakini muda kidogo nikashangaa marafiki zangu wa chuo, tena wa kike wananijia kwa mshangao, wakiniambia mbona tumeona picha zako na video zako zimezagaa mtandaoni ukiwa uchi unakatiza barabarani, kwa kweli wakati nikiwa huko huko kwenye ndoto niliishiwa nguvu, nilijiona nipo katika aibu na fedheha ya milele isiyoweza kufutika, nikawa nawaza ni heri nisingezaliwa, kwasababu jambo kama  lile halina tofauti na wale wanaoigiza mikanda ya video za zinaa, ambalo litaendelea kuwepo mitandaoni daima..

Sasa wakati nikiwa katika hali mbaya sana huko huko kwenye ndoto neno moja la kiingereza likaja mbele yangu, ambalo sikuwahi hata kulijua wala kulisoma mahali popote na hilo ndilo lililonifanya mpaka leo hii ninaikumbuka ndoto hiyo na neno lenyewe ni hili “NUDE”.. Muda huo huo nikashutuka,  nikafurahi kwa kuwa kwa kuwa ilikuwa ni ndoto lakini nikasema ngoja nilitazame kwenye kamusi ya kiingereza lile neno lina maana gani ndipo nikakuta lina maana ile ile ya UCHI kama nilivyokuwa katika ndoto.

Kwa kweli nilikaa muda mrefu sana bila kuelewa ndoto ile ilikuwa na maana gani. Lakini siku nilipokuja kumpa Kristo maisha yangu, ndipo Bwana aliponifundisha maana ya ile ndoto niliyoita.. Nataka nikuambie ukiota ndoto yoyote upo uchi, halafu upo katikati ya kadamnasi, au mahali popote pale iwe shuleni, au kazini, au stendi ya mabasi, au sokoni, basi fahamu kuwa ndivyo hali yako ya kiroho ilivyo kwa sasa.

Sikuzote UCHI unazaa ni Aibu, na Aibu inakupelekea mtu kwenda kujificha..Adamu na Hawa walipoasi pale Edeni, walijiona kuwa wapo uchi, ndipo aibu ikawaingia na hapo hakuna kingine zaidi ya kwenda kutafuta namna ya kujisitiri..

Mwanzo 3:8 “Kisha wakasikia sauti ya Bwana Mungu, akitembea bustanini wakati wa jua kupunga; Adamu na mkewe wakajificha kati ya miti ya bustani, Bwana Mungu asiwaone.

9 Bwana Mungu akamwita Adamu, akamwambia, Uko wapi?

10 Akasema, Nalisikia sauti yako bustanini, nikaogopa kwa kuwa mimi ni uchi; nikajificha”.

Hivyo unapoota ndoto hii moja kwa moja ujue  kuwa utukufu wa Mungu umeondoka juu yako, au upo mbioni kuondoka  kabisa juu yako kama hutataka kutubu dhambi zako, Na ndio maana Mungu anakuonyesha kwa jinsi hiyo hiyo unavyoweza kuona aibu ndivyo itakavyokuwa siku ile siri zako zote na dhambi zako zote unazofanya kwa siri zitakapowekwa wazi mbele ya malaika wake wote wa mbinguni

Warumi 2:16 katika siku ile Mungu atakapozihukumu siri za wanadamu, sawasawa na injili yangu, kwa Kristo Yesu.

Danieli 12:2 “Tena, wengi wa hao walalao katika mavumbi ya nchi wataamka, wengine wapate uzima wa milele, wengine aibu na kudharauliwa milele”.

Jiulize siku hiyo utakuwa katika aibu ya namna gani, utakuwa katika hali ya kudharauliwa kwa namna gani…ubaya zaidi aibu hiyo itakuwa ni ya milele..Mimi nilipokuwa katika dhambi Mungu aliniotesha hilo na haikuwa mara moja, ziliendelea kuja hivyo hivyo  mara kwa mara mpaka nilipompokea Bwana Yesu.

Vilevile ndoto hii haimuhusu aliye nje ya Kristo tu peke yake hapana hata Yule ambaye yupo ndani ya Kristo lakini bado ni vuguvugu, Kristo anamtaka na yeye ayatengeneze mambo yake sawa kabla ya siku za aibu ya milele hazijamfikia..

Ufunuo 3:14 “Na kwa malaika wa kanisa lililoko Laodikia andika; Haya ndiyo anenayo yeye aliye Amina, Shahidi aliye mwaminifu na wa kweli, mwanzo wa kuumba kwa Mungu.

15 Nayajua matendo yako, ya kuwa hu baridi wala hu moto; ingekuwa heri kama ungekuwa baridi au moto.

16 Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa changu.

17 Kwa kuwa wasema, Mimi ni tajiri, nimejitajirisha, wala sina haja ya kitu; nawe hujui ya kuwa wewe u mnyonge, na mwenye mashaka, na maskini, na kipofu, NA UCHI.

18 Nakupa shauri, ununue kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto, upate kuwa tajiri, NA MAVAZI MEUPE UPATE KUVAA, AIBU YA UCHI WAKO ISIONEKANE, na dawa ya macho ya kujipaka macho yako, upate kuona.

19 Wote niwapendao mimi nawakemea, na kuwarudi; basi uwe na bidii, ukatubu.

20 Tazama, nasimama mlangoni, nabisha; mtu akiisikia sauti yangu, na kuufungua mlango, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye pamoja nami.

21 Yeye ashindaye, nitampa kuketi pamoja nami katika kiti changu cha enzi, kama mimi nilivyoshinda nikaketi pamoja na Baba yangu katika kiti chake cha enzi.

22 Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa”.

Unaona? Mungu anakupenda na anahitaji siku ile uweze kuketi pamoja naye katika kiti chake cha enzi, lakini kama tu leo hii utakuwa tayari kununua kwake mavazi meupe ili aibu ya uchi wako isionekane ambayo hiyo inakuja kwa KUTUBU, yaani kuufungua tu mlango wa moyo wako aingie ndani yako..Fungua tu mlango naye ataingia, anakupenda ndio maana anakuonyesha ndoto kama hizo.

Ubarikiwe.

Group la whatsappJiunge na Group letu ya whatsapp, la masomo ya kila siku kwa kubofya hapa > Group-whatsapp


 

 

Mada Nyinginezo:

KUOTA UNAFANYA MTIHANI.

KUOTA NYOKA.

KUOTA UNASAFIRI.

MTETEZI WAKO NI NANI?

FUATILIA NDOTO HII, UTAJIFUZA KITU.

TOFAUTI KATI YA NDOTO NA MAONO NI IPI?


Rudi Nyumbani:

Print this post

KWANINI MAISHA MAGUMU?

Jibu jepesi la swali hili ni kwasababu hapo nyuma tulitoka nje ya kusudi la Mungu.

Tangu mwanzo Mungu hakumuumba mwanadamu ateseke wala asumbuke kwa namna ambayo tunaiona sasa hivi, Mungu alikuwa tayari ameshamwandalia mazingira marahisi sana ya kuishi kiasi kwamba siku zake zote tangu kuumbwa kwake hadi milele na milele asingewahi kujua kama kuna kitu kinachoitwa jasho, wala maumivu kwenye mwili wake…lakini kwasababu wazazi wetu wa kwanza waliasi, ndio ikawa chanzo cha kuvurugika mpango mzima au mfumo mzima wa maisha ambayo  Mungu alitupangia sisi tuuishi.

Mwanzo 3:17 “Akamwambia Adamu, Kwa kuwa umeisikiliza sauti ya mke wako, ukala matunda ya mti ambao nalikuagiza, nikisema, Usiyale; ardhi imelaaniwa kwa ajili yako; kwa uchungu utakula mazao yake siku zote za maisha yako;

18 michongoma na miiba itakuzalia, nawe utakula mboga za kondeni;

19 kwa jasho la uso wako utakula chakula, hata utakapoirudia ardhi, ambayo katika hiyo ulitwaliwa; kwa maana u mavumbi wewe, nawe mavumbini utarudi.”

Unaona hapo? Leo hii unahangaika huku na kule, chakula unakula cha shida, nguvu unayoitumia kutafuta pesa haiendani na unachokipata, kujenga tu nyumba 1 inakuchukua miaka 20 kumalizika kana kwamba unajenga mji wa New York, bado matibabu yanakuumiza kichwa, bado elimu, bado familia, bado ndugu, bado jamii inayokuzunguka, n.k. vyote hivyo vinakufanya uone kama haya maisha hayakupendi, mpaka unaliza swali kama hilo, unafika mpaka kwenye ukurasa huu..Fahamu kuwa ni Mungu ndiye kakuleta hapa anataka kusema na wewe.

Lakini pamoja na kuwa tulitoka nje ya mpango wake, hakutuacha yatima, aliahidi kutandalia makao mengine mapya ambayo raha yetu ile ya mwanzo tuliyokuwa nayo itarejea na hata pengine zaidi ya pale na hiyo inakuja mara  baada ya maisha haya kuisha, lakini pia aliahidi hata tukiwa hapa hapa duniani kwenye dhiki hizi nyingi, bado atakuwa na sisi kuhakikisha kuwa anatupa WEPESI wa maisha …Lakini neema hiyo ameahidi kuitoa tu kwa wale ambao watakuwa tayari kumpokea..

Bwana Yesu alisema maneno haya:

Mathayo 11:28 Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.

29 Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu;

30 kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi.

Unaona Ni YESU tu pekee ndiye anayekuahidia PUMZIKO LA MAISHA YAKO. Hakuna mwanadamu yoyote anaweza kukuahidi kitu kama hicho, ukiwa ndani ya Kristo atakupa AMANI ambayo hata kama mfukoni huna kitu, utajiona wewe ni zaidi ya tajiri yeyote duniani, utakupa tumaini ambalo, litakufanya usione haya maisha kuwa ni kitu cha kukisumbukia sana..atakutunza atakulinda atakuhifadhi..

Unachopaswa ni kumpa tu maisha yako, kuanzia leo aanze kuyaongoza nawe utaona wema wake

Anasema:

 Onjeni mwone ya kuwa Bwana yu mwema; Heri mtu yule anayemtumaini. (Zaburi 34:8).

Na hiyo inakuja kwa kutubu kabisa kwa kumaanisha kuacha dhambi zako zote…Na baada ya hapo atakuja ndani yako, lakini sharti ukabatizwe katika ubatizo wa kuzamishwa katika maji mengi, kwa Jina la YESU KRISTO upate ondoleo la dhambi zako, kama hukuwahi kufanya hivyo na yeye wenyewe atakupa kipawa cha Roho Mtakatifu atakaye kulinda, na kukupa wepesi wa maisha haya. Mpaka siku ile ya kwenda mbinguni.

Mathayo 6:25 “Kwa sababu hiyo nawaambieni, Msisumbukie maisha yenu, mle nini au mnywe nini; wala miili yenu, mvae nini. Maisha je! Si zaidi ya chakula, na mwili zaidi ya mavazi?

26 Waangalieni ndege wa angani, ya kwamba hawapandi, wala hawavuni, wala hawakusanyi ghalani; na Baba yenu wa mbinguni huwalisha hao. Ninyi je! Si bora kupita hao?

27 Ni yupi kwenu ambaye akijisumbua aweza kujiongeza kimo chake hata mkono mmoja?

28 Na mavazi, ya nini kuyasumbukia? Fikirini maua ya mashamba, jinsi yameavyo; hayafanyi kazi, wala hayasokoti

29 nami nawaambia, ya kwamba hata Sulemani katika fahari yake yote hakuvikwa vizuri kama mojawapo la hayo.

30 Basi, ikiwa Mungu huyavika hivi majani ya kondeni, yaliyopo leo, na kesho hutupwa kalibuni, je! Hatazidi sana kuwavika ninyi, enyi wa imani haba?

31 Msisumbuke, basi, mkisema, Tule nini? Au Tunywe nini? Au Tuvae nini?

32 Kwa maana hayo yote Mataifa huyatafuta; kwa sababu Baba yenu wa mbinguni anajua ya kuwa mnahitaji hayo yote.

33 Bali utafuteni kwanza ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa.

34 Basi msisumbukie ya kesho; kwa kuwa kesho itajisumbukia yenyewe. Yatosha kwa siku maovu yake.”

Ubarikiwe.


 

Mada Nyinginezo:

JAWABU LA MAISHA YA MTU.

JE! KUBET NI DHAMBI?

JEHANAMU NI NINI?

MAMBO (2) YATAKAYOKUTENGA NA IMANI SIKU HIZI ZA MWISHO.

AMIN! NAWAAMBIA KIZAZI HIKI HAKITAPITA.

JINSI MWISHO ULIVYOKARIBIA.


Rudi Nyumbani:

Print this post

Nini maana ya Neno Haleluya.

Hili ni Neno lenye asili ya kiebrania, lenye muunganiko wa maneno mawili “Halelu”, na “Yah”..Halelu ikiwa na maana “msifu” na “Yah” ikiwa na maana “Bwana” ..”Yah” ni ufupisho wa Neno Yehova,..Hivyo Haleluya Ni neno lililomaanisha kumsifu Bwana kwa nyimbo za furaha..

Kama wewe ni msomaji wa biblia utaona likijitokeza sehemu nyingi katika maagano yote mawili, Kwenye agano la kale utaliona kwenye kitabu cha Zaburi, na katika agano jipya utaliona  kwenye kitabu cha Ufunuo.

Zaburi 106:1 “Haleluya. Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema, Kwa maana fadhili zake ni za milele.

2 Nani awezaye kuyanena matendo makuu ya Bwana, Kuzihubiri sifa zake zote?”

 

Zaburi 113:1 “Haleluya. Enyi watumishi wa Bwana, sifuni, Lisifuni jina la Bwana”.

 

Ufunuo 19:1 “Baada ya hayo nikasikia sauti kama sauti ya makutano mengi, sauti kubwa mbinguni, ikisema, Haleluya; wokovu na utukufu na nguvu zina BWANA MUNGU wetu”.

Hata sasa Neno hili tunalitumia wakristo pale tunapomsifu Mungu kwa furaha.. Au tunapoufurahia ukuu wake. Wewe nawe usione aibu kulitamka Neno hili kwa nguvu pale uufurahiapo utukufu wa Mungu.

Bwana akubariki.


 

Mada Nyinginezo:

BWANA ALIMAANISHA NINI KUSEMA JIKANE MWENYEWE?

BWANA ALIMAANISHA NINI KUSEMA “WAACHE WAFU WAZIKE WAFU WAO.(MATHAYO 8:21)?

JE! KITABU CHA YASHARI NI KITABU GANI? (2SAMWELI 1:17-18),

JE! KUBET NI DHAMBI?

JE! KUFANYA MASTURBATION (PUNYETO) NI DHAMBI?

UWEZA WA MUNGU UNAONEKANA WAPI?

UNYAKUO.


Rudi Nyumbani:

Print this post

SAA YA KIAMA.

Wingu la Mashahidi
Wingu la Mashahidi
SAA YA KIAMA.







/

Cha kushangaza ni kwamba wakristo tu peke yetu ndio hatujui saa tunayoishi na muda gani mchache tuliobakiwa nao, na hata kama tunajua basi wengi bado hatujachukulia kwa uzito jambo hili ukilinganisha na jinsi wanasayansi na shetani wanavyolichukulia kwa upande wao..Wanasayansi leo hii wameunda saa yao maalumu ijulikanyo kama “Doomsday clock” (saa ya kiama), ambayo hiyo inawakaumbusha ni wakati gani wanaoishi sasa, wameifananisha na saa  yetu hii ya kawaida, kwamba mshale ukifika tu saa 6 kamili usiku basi usiku wa manane umeanza, vilevile na siku mpya imeanza, Hivyo hiyo saa yao sasa ipo katika muundo huo huo kwamba zimebaki dakika chache sana kabla ya kuingia usiku wa manane wao(yaani kiama), wanakadiria kuwa  miaka yote ya nyuma saa hiyo ilikuwa haijafikia usiku wa manane lakini  kuanzia  mwaka 1947 ilifikia dakika 7 kabla ya kuingia usiku wa manane, na hiyo ni kwa jinsi walivyokuwa wanaona hali ya dunia inavyokwenda kwa matetesi ya vita vya mabomu ya Atomiki, kwamba muda wowote vita vinaweza kuanza na vikianza tu basi itachukua muda mfupi sana dunia kuwa sio sehemu tana ya kuishi mwanadamu.

Na kila siku mshale wao unapanda, mwaka 2015 walikadiria ni dakika 3 tu zimebaki , mwaka 2017 walikadiria dakika 2.5, mwaka jana walikadiria dakika 2 kabla ya kufikia saa 6 ya usiku wao…Yaani tafsiri yake ni kuwa hatari ya kukifikia kiama cha dunia ni kikubwa kuliko inavyodhaniwa katika miaka iliyopita…

Kama ulikuwa hujui sikuzote Mungu kabla hajaleta uharibifu wa hii dunia ni sharti kwanza wanadamu wajiharibu wenyewe, Ndivyo ilivyokuwa hata katika kipindi cha Nuhu, watu walijiharibu wenyewe kupindukia kukawa hakuna tena sababu ya maisha na ndipo Mungu akamaliza kila kitu (Mwanzo 6:12), ndugu  usione ukadhani kuwa duniani kuna amani, usidanganyike na siasa za dunia, ni jambo la kawaida kuficha ukweli ili watu wasiwe na wasiwasi lakini  nyuma yake ipo hofu kubwa ambayo wao wenyewe wanaitambua, pamoja na wanasayansi wao, kwa huu ugunduzi wa mabomu ya Atomiki ambayo hata leo kwenye vyombo vya habari unaona mataifa mengi yanagombana kila siku kuhusu hayo, kwasababu wanajua vita vikishaanza basi ndio mwisho wa kila kitu,..

muda mfupi chini nitakuonyesha video fupi, ya jaribio la kwanza la bomu la Atomiki lilidondoshwa huko Urusi tarehe 30 Octoba 1961, ukubwa wake ukiachilia mbali yale ya Nagasaki na Heroshima yaliyomaliza vita ya pili ya dunia kwa kuuwa  zaidi ya watu laki 2 kule Japan. Hili ni mara 1000 zaidi ya yale kwa uharibifu wake, tazama video fupi chini uone lilivyodondoshwa.

Lakini kabla hayo hayajatokea Unyakuo utakuwa umeshapita, katika ule mfufulizo wa maono 7 aliyoonyeshwa mtumishi wa Mungu maarufu William Branham  na kuambiwa hayo yatatokea kabla ya kuja kwa pili kwa Kristo, kama wengi tunafahamu na tunavyosoma katika historia, matano kati ya yale yalitimia kama yalivyo mawili bado, William Branham alionyeshwa kabla ya kutokea vita ya pili ya dunia jinsi hitler atakavyonyanyuka na kuiongoza dunia yote katika vita na jinsi  kifo chake kitakavyoishia na kuwa cha kiajabu ajabu, habari hiyo aliihubiri na ikajulikana na watu wote kabla hata ya kutokea kwa vita ya pili ya dunia, hilo lilikuwa ni ono la pili kati ya yale saba, sasa ono la saba ambalo lilikuwa ndio la  mwisho alionyeshwa kuangamizwa kwa taifa la Marekani, anasema alisikia mlipuko mkubwa usio wa kawaida nyuma yake na alipogeuka hakuona kitu chochote zaidi ya vipande vya mabaki na moshi tu,…Na hicho si kingine zaidi ya bomu la nyuklia.

Sasa hiyo alioneshwa kwa taifa lake, jambo hilo litakuja kuwa ulimwenguni kote, lakini mpaka hayo yote yatokee unyakuo utakuwa umeshapita, Mpaka sasa unaweza kuona ni saa gani hii tunaishi, Kama wanasayansi watu wa kidunia hawaishi kama vile wanayo wiki moja mbeleni, iweje mimi na wewe leo tuishi kama vile tuna maelfu ya miaka mbeleni,..Bwana anakuja, dalili zote zinaonesha, sijui tanataka tuoneshwe dalili zipi tena ndio tuamini na sisi kuwa tunaishi ukingoni mwa wakati..laiti kama na sisi tungekuwa na saa yetu basi saa yetu ingesoma tupo  visekunde vichache kabla ya kwenda katika unyakuo kwa Baba na kuanza kwa utawala mpya wa miaka 1000 wa Bwana wetu YESU KRISTO..

Tazama video fupi chini ya bomu lijulikanalo kama TSAR BOMBA, jinsi lilivyoachiwa ili ufahamu yatakayowakuta wale wote watakaokosa unyakuo.

Bwana Yesu akubariki sana Mtu wa Mungu, Tafadhali share na wengine


Mada Nyinginezo:

KATI YA UNYAKUO WA KANISA, DHIKI KUU, VITA VYA HAR-MAGEDONI, UTAWALA WA MIAKA 1000, VITA YA GOGU NA MAGOGU, HUKUMU YA KITI CHA ENZI CHEUPE. JE, NI KIPI KINAANZA NA KINGINE KUFUATA?

SIKU YA BWANA INAYOTISHA YAJA!

KITABU CHA UZIMA NI KIPI?

KUZIMU NI MAHALI PA NAMNA GANI ,JE! HUKO WANAISHI WATU WAKIFA NA KWENDA KUPATA MATESO AU NI VINGINEVYO?


Rudi Nyumbani:

Print this post

KUSAMBAA KWA ROHO YA MPINGA-KRISTO.

Cheo cha Mpinga-Kristo, kimeshafunuliwa Zaidi ya Karne moja iliyopita huko nyuma, nacho si kingine Zaidi ya cheo cha ki-PAPA, Wakati wa Mwisho utakapofika atanyanyuka mmoja atakayekikalia hicho kiti, ambaye atafanya mambo maovu na ya ajabu, yale yote yaliyotabiriwa katika maandiko matakatifu. Huyo bado hajafunuliwa kwasasa jina lake ni nani?… Lakini hatatoka pengine mbali na kiti hicho cha Kipapa..Lakini kwasababu tunajua majira na nyakati, kwamba hizi ni siku za mwisho, labda huyu aliyeko sasahivi ndiye!..au kama siye miongoni mwa wachache sana wanaokuja huko mbeleni atakuwa mmojawapo!…Huyo ndiye atakayeihimiza chapa! Huyo ndiye atakayeidanganya dunia kuwa ataleta amani! Lakini badala yake ataipeleka kwenye matatizo na kiama.. Na ndiye atakayetafuta kwenda Yerusalemu kwenye Hekalu litakalotengenezwa kule hivi karibuni kule Israeli aabudiwe pale kama Mungu (2Wathesalonike 2).

Vipo viishara vingi vinavyotuthibitishia utendaji kazi wake, katika kizazi chetu…lakini pia kipo kiashiria kimoja kikubwa sana! Cha kutufanya tuzidi kuwa macho na kufunguka fahamu zetu, kujua ni majira gani tunaishi.

Kiashiria hicho si kingine Zaidi ya Roho yake huyo Mpinga-Kristo kuwavaa watu(wanaojiita watumishi),

Leo hatutazungumzia, jinsi hii roho ilivyoyavaa makanisa pamoja na serikali..Bali tutaangalia ni jinsi gani imewavaa wanaojiita watumishi.

Zamani, kusikia Mtu anayejiita mtumishi wa Mungu, kuwa na walinzi wa pembeni (ma-bodyguards) ilikuwa ni jambo la kushangaza sana…Hata hivyo halikuwepo kabisa, kwasababu Bwana Yesu mwenyewe ambaye sisi tunamwita Bwana! Hakuwa na mabody-guards, wapo watu wanasema wale mitume walikuwa ma-bodyguards wake, huo sio ukweli, bodyguard huwa anatembea na silaha na kazi yake ni kumlinda Yule ili asidhuriwe anakuwa tayari hata kuua ili kwamba tu Yule anayelindwa akae salama, lakini Bwana hakuwaita mitume kwa kazi hiyo, ya kumlinda yeye, kinyume chake Petro alipojaribu kufanya hivyo kwa kumkata Yule mtu sikio alimkemea …Zaidi ya yote yeye mwenyewe alijitoa kwa hiyari yake kufa kwa ajili ya wengi, ingawa alikuwa na uwezo wa kuagiza malaika waje wampiganie lakini hakutumia uwezo huo, ili kwamba awe sadaka kwa wengine (soma Mathayo 26:51-54 )…

Na Neno lake linatuambia kama yeye alivyojitoa kwa ajili yetu na sisi pia tunapaswa tujitoe kwa ajili ya wengine. (1Yohana 3:16)

Lakini leo ni kinyume chake utaona Mhubiri anakwenda kuhubiri injili na Mabody-guards ambao wameandaliwa mahususi kumtetea yeye, na ndani ya kifuko yao wamebeba silaha..yote hiyo hataki kufa! au Anaogopa kufa!..Ukimgusia habari za kwenda kuhubiri bila bodygurds anapambana na wewe!..Leo malengo ya wahubiri wengi ni kununua Helikopta na ndege, ili hatimaye waziandike majina yao, na wajulikane dunia nzima, na hatimaye waonekane mbele ya vyombo vya habari ili wapate heshima duniani kote…

Sasa hiyo yote imetoka wapi? Na kwanini haikuwepo kipindi cha nyuma?

Jibu ni rahisi! Hiyo yote ni ile nguvu ya mpinga-Kristo mkuu imewavaa hawa watumishi!….Roho ya Mpinga kristo ndiye inayowafanya watafute fahari na ufalme katika dunia hii, sasa roho hiyo haijaanzia kwao, bali imeanzia kwenye kile cheo cha Mpinga Kristo mwenyewe, (yaani kiti cha upapa)…Papa ambaye anajulikana kama mhubiri maarufu, ndiye Mhubiri pekee aliye kinyume na Kristo, ambaye analindwa na JESHI! Linaloitwa “Swiss guards” linalomzunguka na kumlinda kila anakokwenda..Mabodyguard hao kabla ya kumlinda Papa, wanaapa kuwa tayari hata kuutoa uhai wao ili tu kumlinda Papa asife!…jambo ambalo Kristo aliye Bwana hakufanya, wala hakutamani kulindwa kwa namna hiyo…hivyo si ajabu leo kuwaona hawa wahubiri wengine wadogo wakifanya hayo hayo…wakiajiri mabodygurd kuwalinda hadi madhabahuni..ni roho ile ile ya mpinga-kristo ipo kazini.

Papa ana ndege yake maalumu inayoitwa “Alitalia Flight AZ4000” inayokaribiana sana kufanana na Ndege ya Raisi wa Marekani Airforce one… roho hiyohiyo imewavaa manabii wa uongo wanaozuka sasahivi, nao pia wanafanya juu chini kumiliki ndege kama ya Papa, lengo lao sio kutumia hizo kumuhubiri Kristo, bali kujihubiri wao wenyewe na ufahari wao.

Papa anaabudiwa na ana pete iliyopo mkononi mwake ambao maelfu ya waumini wa kikatoliki, wamkaribiapo ni lazima waibusu, mkononi mwake…roho hiyo hiyo imewavaa manabii wa uongo leo, wanatafuta kwa bidii kuangukiwa na kusujudiwa..na hata watu kuwapa heshima fulani kubwa ya kipekee…Na mambo mengine mengi Papa anayafanya yameshaanza kuonekana kwa wanaojiita wahubiri.

Ndugu tuonapo Mambo hayo yaliyo kinyume na Kristo, ambapo hapo kwanza yalikuwa yanafanyika na mtu mmoja tu Papa, lakini sasa yanafanyika na maelfu ya watu wanaojiita watumishi wa Mungu, ni wakati wa kunyanyua vichwa vyetu juu, kwasababu ule mwisho umekaribia sana..Ile roho ya mpingakristo imeshateka ulimwengu mzima…kinachosubiriwa ni unyakuo tu! Dhiki kuu ianze..Ni kama ugonjwa! Ulioanzia kichwani kama upele lakini sasa umeenea mwili mzima…hiyo ni dalili mbaya!

Tabia hii, ikishamalizika kusambaa, itamsaidia baadaye mpingakristo kufanya kazi yake kirahisi. Atakapoanzisha chapa, afanye kazi kirahisi kwasababu watakuwepo watu wengi watakaosapoti mambo anayoyafanya…Kwasasa yataonekana si ajabu tena.

Je umeokolewa? Na kama umeokoka una uhakika na wokovu wako? Biblia inasema

2 Petro 1:10 “Kwa hiyo ndugu, jitahidini zaidi kufanya imara kuitwa kwenu na uteule wenu; maana mkitenda hayo hamtajikwaa kamwe”

Ufunuo 3:20 “Tazama, nasimama mlangoni, nabisha; mtu akiisikia sauti yangu, na kuufungua mlango, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye pamoja nami.

21 Yeye ashindaye, nitampa kuketi pamoja nami katika kiti changu cha enzi, kama mimi nilivyoshinda nikaketi pamoja na Baba yangu katika kiti chake cha enzi”.

Bwana akubariki.

Tafadhali share na wengine


Mada Nyinginezo:

ROHO YA MPINGA KRISTO IKITENDA KAZI SIKU HIZI ZA MWISHO

NYAKATI SABA ZA KANISA NA WAJUMBE WAKE.

MPINGA-KRISTO NI NANI?

CHAPA YA MNYAMA NI NINI?


Rudi Nyumbani:

Print this post

KUOTA UMEBEBA MTOTO.

Sehemu kubwa ya ndoto tunazoziota mara kwa mara huwa hazitokani na Mungu wala shetani bali zinatokana na sisi wenyewe..

Na hizi huathiriwa aidha na shughuli tunazozifanya kila siku, au mazingira yanayotuzunguka, Kwamfano, ikiwa wewe ni kondakta wa magari, na kazi ndio hiyo unayofanya kila siku, basi tarajia kuwa ndoto utakazokuwa unaota mara kwa mara zitahusiana na ukondakta utajiona unapiga debe, au upo kwenye magari,, au kama wewe ni mkulima ambaye mara zote  unashida mashambani, tazamia pia ndogo zako nyingi usiku zitahusiana sana na mambo ya mashambani,..

Na vivyo hivyo, ndoto nyingine nyingi kama hizo zinakuja kutokana na shughuli mtu anazozifanya mara kwa mara..

Mhubiri 5:3 “Kwa maana ndoto huja kwa sababu ya shughuli nyingi; na sauti ya mpumbavu kwa njia ya wingi wa maneno.”

Vile vile ndoto nyingine huja kutokana na mabadiliko ya mwili yetu, kwamfano ikiwa jana usiku ulilala bila kula, tazamia kuwa usiku utaota ndoto zinazoendana na vyakula vyakula aidha unakula lakini hushibi, au unakunywa, au kama ulilala ukiwa umebanwa na mkojo, tarajia kuwa usiku utaona unakojoa mara kwa mara n.k.

Isaya 29:8 “Tena itakuwa kama mtu mwenye njaa aotapo, kumbe, anakula; lakini aamkapo, nafsi yake haina kitu; na kama mtu mwenye kiu aotapo, kumbe, anakunywa; lakini aamkapo, kumbe, anazimia, na nafsi yake inatamani; hivyo ndivyo utakavyokuwa huo wingi wa mataifa waletao vita juu ya mlima Sayuni.”

Hivyo ndoto za namna hii zinawapata watu wengi wakidhani kuwa wameoteshwa na Mungu au shetani kumbe ni ubongo wao ndio umewaotesha, nataka nikuambie sio kila ndoto ni ya kuitilia maanani, ndoto za namna hii zikikujia zipuuzie tu.. kwasababu huwa hazibebi tafsiri yoyote yamaana ya rohoni.

Kama hujafahamu bado kuzitofautisha ndoto unazoziota zinadondekea katika kundi lipi..basi Pitia kwanza hili somo kisha ndio tuendelee..>>> NITAJUAJE KAMA NDOTO NI YA MUNGU AU YA SHETANI?

Sasa Ikiwa ndoto uliyoota unaamini haitokani na mwili wako, inakupa utata mwingi na huwa inajirudia mara kwa mara, basi lipo jambo unapaswa ujue hapo.

Kumbuka Sikuzote kitu kinachobebwa  ni mzigo, lakini tatizo sio mzigo bali ni mzigo wa aina gani umebebwa, kwamfano kuna kuota umebeba maiti, au kuota umebeba mbao, au kuota umebeba jeneza unatembea  nalo,  hapo ndipo unapopaswa kuangalia sana hicho kilichobebwa ni nini…kwasababu vyote hivyo vinaeleza hali ya mtu ilivyo rohoni.

Sasa kama umeota ubeba mtoto,  na upo ndani ya Kristo fahamu kuwa mtoto ni jukumu, na jukumu lenyewe linahusiana na uleaji. hapo ni Mungu anakuonyesha kuwa kuna jukumu amekupa, au kama halipo sasahivi basi jiandae kukutana nalo hivi karibuni..Inaweza ikawa kwenye huduma yako ya utumishi, au familia yako, au kazini kwako, au popote pale ulipo..

Hivyo unachopaswa kufanya ni kutokulalamika, unapokutana na vizuizi, wala usikasirike mambo kama hayo yakujiapo, ongeza uhusiano wako kwa Mungu. Kwasababu jukumu ni ukomavu. Inawekana Mungu amekupa watu wa kukaa chini yako, hivyo usiwachukie na kuwaona ni mzigo, kaa nao, hujui pengine Mungu ameweka Baraka zako kwako kwa kupitia hao. Au wanakutegemea wewe uwape msaada ya kiroho usiwakatae wala usikwepe hilo jukumu, hujui mbeleni watakuja kuwa nani kwako na kwa wengine..Ndivyo ilivyokuwa kwa Mariamu, hakukataa kumbeba mtoto Yesu pepote alipoambiwa aende, lakini leo hii tunajua ni jinsi gani Bwana Yesu amempa Heshima kubwa.

Mathayo 2:12 “Nao wakiisha kuonywa na Mungu katika ndoto wasimrudie Herode, wakaenda zao kwao kwa njia nyingine.

13 Na hao walipokwisha kwenda zao, tazama, malaika wa Bwana alimtokea Yusufu katika ndoto, akasema, Ondoka, umchukue mtoto na mama yake, ukimbilie Misri, ukae huko hata nikuambie; kwa maana Herode anataka kumtafuta mtoto amwangamize.”

14 Akaondoka akamchukua mtoto na mama yake usiku, akaenda zake Misri;

15 akakaa huko hata alipokufa Herode; ili litimie neno lililonenwa na Bwana kwa ujumbe wa nabii, akisema, Kutoka Misri nalimwita mwanangu.”

Lakini kama unajijua upo nje ya Kristo fahamu pia, Mungu anakukumbusha, unabeba jukumu ambalo halitakuwa na faida kwako mbeleni.

Lakini Pia kama unaota umebeba kitoto kisichoeleweka, kibwengo si kibwengo, kama kinakuwekea mzigo mzito usioweza kuubeba, kinakukosesha raha, basi ujue hilo ni pepo, linasimama nyuma yako kukukawiisha katika safari yako ya wokovu hapa duniani, unachopaswa kufanya ni kudumu katika maombi, ombea kila eneo ulilopo, na kila jambo unalolifanya, ili kufunga milango yote shetani anayoweza kuitumia kukurudisha nyuma..

Vile vile kama unaota unabeba jeneza fahamu hiyo ni ishara kuwa unaenda kujiangamiza mwenyewe, hivyo angalia maisha yako, kama upo nje ya Kristo tubu haraka sana na anza kuishi au kufanya mambo yanayompendeza yeye katika eneo ulilopo.

Bwana akubariki.

Group la whatsappJiunge na Group letu ya whatsapp, la masomo ya kila siku kwa kubofya hapa > Group-whatsapp


Mada Nyinginezo:

TOFAUTI KATI YA NDOTO NA MAONO NI IPI?

MTETEZI WAKO NI NANI?

VITA BADO VINAENDELEA.

HUYU AZAZELI NI NANI TUNAYEMSOMA KATIKA(WALAWI 16:8)

UNAMFAHAMU MUNGU WA KWELI?

MAFUNUO YA ROHO.


Rudi Nyumbani:

Print this post