Hema ya kukutania kama jina lake lilivyo, ni hema iliyotengenezwa mahususi kwaajili ya “kukutania”.
Katika biblia, Musa aliongozwa na Bwana Mungu kutengeneza Hema ndogo maalumu, ambayo kupitia hiyo, Mungu ataweza kukutana na watu wake na kuzungumza nao.
Hema hiyo Musa aliambiwa aitengeneze nje ya kambi, Na haikuwa ya kudumu, bali ya kuhama hama, kwasababu wana wa Israeli walikuwa bado wapo katika safari ya kwenda Kaanani, hivyo ilikuwa ni ya kutengenezwa na kuvunjwa. (Tazama picha juu).
Na mtu yeyote alipokuwa na jambo ambalo anataka kuuliza kwa Bwana, basi alimfuata Musa, na kisha Musa huingia ndani ya hiyo hema kusikia kutoka kwa Bwana.
Hapo awali ni Musa tu, ndiye aliyekuwa na ruhusa ya kuingia ndani ya Hema, baadaye Haruni naye alikuja kupata nafasi ya kuingia, baada ya sheria za kikuhani kuongezwa.
Na Ishara itakayoonesha kuwa Bwana ameshuka juu ya Hema hiyo tayari kuzungumza na watu wake, ni ile Nguzo ya wingu ambayo iliyokuwa inawaongoza wana wa Israeli mchana.
Nguzo hiyo iliposhuka na kukaa juu ya hema basi wana wa Israeli wote walijua Bwana ameshuka na kuna jambo au ujumbe anataka kuutoa. Nguzo hiyo kwa jina lingine iliitwa “utukufu wa Bwana”.
Hivyo uliposhuka huo utukufu basi Musa aliingia ndani ya hiyo hema kusikia Bwana anasema nini.
Mfano utaona wakati Haruni na Miriamu walipomnung’unikia Musa juu ya mke wake wakiMisri , jambo ambalo halikumpendeza Mungu…utaona “Utukufu wa Mungu”, yaani ile nguzo ya wingu ilionekana juu ya hema.
Hesabu 12:1 “Kisha Miriamu na Haruni wakamnenea Musa kwa sababu ya mwanamke Mkushi aliyekuwa amemwoa; maana, alikuwa amemwoa mwanamke Mkushi. 2 Wakasema, Je! Ni kweli BWANA amenena na Musa tu? Hakunena na sisi pia? BWANA akasikia maneno yao. 3 Basi huyo mtu, huyo Musa, alikuwa mpole sana zaidi ya wanadamu wote waliokuwa juu ya uso wa nchi. 4 BWANA akanena ghafula na Musa, na Haruni na Miriamu, na kuwaambia, Tokeni nje ninyi watatu, mwende hemani mwa kukutania. Basi hao watatu wakatoka nje. 5 BWANA akashuka katika nguzo ya wingu akasimama pale mlangoni pa Hema, akawaita Haruni na Miriamu, nao wakatoka nje wote wawili. 6 Kisha akawaambia, Sikizeni basi maneno yangu; Akiwapo nabii kati yenu, Mimi, BWANA, nitajifunua kwake katika maono, Nitasema naye katika ndoto. 7 Sivyo ilivyo kwa mtumishi wangu, Musa; Yeye ni mwaminifu katika nyumba yangu yote; 8 Kwake nitanena mdomo kwa mdomo Maana, waziwazi wala si kwa mafumbo; Na umbo la BWANA yeye ataliona. Mbona basi ninyi hamkuogopa Kumnenea mtumishi wangu, huyo Musa?. 9 Hasira za BWANA zikawaka juu yao; naye akaenda zake. 10 Kisha hilo wingu likaondoka kutoka pale juu ya hema; na tazama, Miriamu akawa mwenye ukoma, mweupe kama theluji; Haruni akamwangalia Miriamu, na tazama, yu mwenye ukoma. 11 Kisha Haruni akamwambia Musa, Ee bwana wangu nakusihi sana usituwekee dhambi juu yetu, kwa kuwa tumefanya ya upumbavu, na kufanya dhambi”.
Hesabu 12:1 “Kisha Miriamu na Haruni wakamnenea Musa kwa sababu ya mwanamke Mkushi aliyekuwa amemwoa; maana, alikuwa amemwoa mwanamke Mkushi.
2 Wakasema, Je! Ni kweli BWANA amenena na Musa tu? Hakunena na sisi pia? BWANA akasikia maneno yao.
3 Basi huyo mtu, huyo Musa, alikuwa mpole sana zaidi ya wanadamu wote waliokuwa juu ya uso wa nchi.
4 BWANA akanena ghafula na Musa, na Haruni na Miriamu, na kuwaambia, Tokeni nje ninyi watatu, mwende hemani mwa kukutania. Basi hao watatu wakatoka nje.
5 BWANA akashuka katika nguzo ya wingu akasimama pale mlangoni pa Hema, akawaita Haruni na Miriamu, nao wakatoka nje wote wawili.
6 Kisha akawaambia, Sikizeni basi maneno yangu; Akiwapo nabii kati yenu, Mimi, BWANA, nitajifunua kwake katika maono, Nitasema naye katika ndoto.
7 Sivyo ilivyo kwa mtumishi wangu, Musa; Yeye ni mwaminifu katika nyumba yangu yote;
8 Kwake nitanena mdomo kwa mdomo Maana, waziwazi wala si kwa mafumbo; Na umbo la BWANA yeye ataliona. Mbona basi ninyi hamkuogopa Kumnenea mtumishi wangu, huyo Musa?.
9 Hasira za BWANA zikawaka juu yao; naye akaenda zake.
10 Kisha hilo wingu likaondoka kutoka pale juu ya hema; na tazama, Miriamu akawa mwenye ukoma, mweupe kama theluji; Haruni akamwangalia Miriamu, na tazama, yu mwenye ukoma.
11 Kisha Haruni akamwambia Musa, Ee bwana wangu nakusihi sana usituwekee dhambi juu yetu, kwa kuwa tumefanya ya upumbavu, na kufanya dhambi”.
Pia unaweza kusoma juu ya habari ya Dathani na Kora walipoinuka na kutaka wao ndio wawe viongozi wa mkutano badala ya Musa.
Hesabu 16:19 “ Kisha Kora akutanisha mkutano wote kinyume chao mlangoni pa hema ya kukutania; na utukufu wa BWANA ukatokea mbele ya mkutano wote. 20 Kisha BWANA akanena na Musa na Haruni, na kuwaambia, 21 Jitengeni ninyi mkaondoke kati ya mkutano huu, ili nipate kuwaangamiza mara moja. 22 Nao wakapomoka kifudifudi, wakasema, Ee Mungu, Mungu wa roho za wenye mwili wote, je! Mtu mmoja atafanya dhambi, nawe utaukasirikia mkutano wote? 23 BWANA akasema na Musa, na kumwambia, 24 Nena na mkutano, na kuwaambia, Ondokeni ninyi hapo karibu na maskani ya Kora, na Dathani, na Abiramu”.
Hesabu 16:19 “ Kisha Kora akutanisha mkutano wote kinyume chao mlangoni pa hema ya kukutania; na utukufu wa BWANA ukatokea mbele ya mkutano wote.
20 Kisha BWANA akanena na Musa na Haruni, na kuwaambia,
21 Jitengeni ninyi mkaondoke kati ya mkutano huu, ili nipate kuwaangamiza mara moja.
22 Nao wakapomoka kifudifudi, wakasema, Ee Mungu, Mungu wa roho za wenye mwili wote, je! Mtu mmoja atafanya dhambi, nawe utaukasirikia mkutano wote?
23 BWANA akasema na Musa, na kumwambia,
24 Nena na mkutano, na kuwaambia, Ondokeni ninyi hapo karibu na maskani ya Kora, na Dathani, na Abiramu”.
Mistari mingine inayozungumzia juu ya hema ya Bwana na utukufu wake huo ni pamoja na Kutoka 40:34, Walawi 1:1, na Hesabu 2:17.
Lakini je hiyo Hema ya kukutania sasa ni wapi?
Hema yetu ya kukutania sasa ni kwenye Neno la Mungu (Biblia), hapo ndipo tutakapoonana na Mungu, tutakaposikia kutoka kwa Mungu,tutakapopata maonyo na faraja. Hapo ndipo penye utukufu wa Mungu.
Hakuna mahali pengine tutakapopata kusikia Sauti ya Mungu, isipokuwa katika Neno lake.
Hivyo hatuna budi kujifunza biblia kila siku.
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali. Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312 pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
Mada Nyinginezo:
Tofauti ya kazi ya Damu ya Yesu na Jina la Yesu ni ipi?
MUNGU HATAZAMI MOTO WA KIGENI,KUWA MAKINI!
NATAKA REHEMA, WALA SI SADAKA!
JE NI HALALI KUOA WAKE WENGI, AU KUTOA TALAKA?
Rudi nyumbani:
Print this post
SWALI: Nini maana ya huu mstari,
Mithali 31:6 “Mpe kileo yeye aliye karibu na kupotea; Kampe divai yeye aliye na uchungu nafsini. 7 Anywe akausahau umaskini wake; Asiikumbuke tena taabu yake”.
Mithali 31:6 “Mpe kileo yeye aliye karibu na kupotea; Kampe divai yeye aliye na uchungu nafsini.
7 Anywe akausahau umaskini wake; Asiikumbuke tena taabu yake”.
Je tunaruhusiwa kunywa pombe, tunapokuwa katika shida?
JIBU: Kumbuka agano la kale lilikuwa ni agano la mwilini, hivyo walitafuta kila mbinu za mwilini ili kutatua matatizo ya mtu, kwamfano utaona ilikuwa ili kutatua tatizo la zinaa na migororo katika ndoa, waliruhusiwa kutoa talaka, au kuoa wake wengi. Lakini jambo kama hili haukuwa mpango wa Mungu tangu mwanzo.
Mathayo 19:7 “Wakamwambia, Jinsi gani basi Musa aliamuru kumpa hati ya talaka, na kumwacha? 8 Akawaambia, Musa, kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu, aliwapa ruhusa kuwaacha wake zenu; lakini tangu mwanzo haikuwa hivi”.
Mathayo 19:7 “Wakamwambia, Jinsi gani basi Musa aliamuru kumpa hati ya talaka, na kumwacha?
8 Akawaambia, Musa, kwa sababu ya ugumu wa mioyo yenu, aliwapa ruhusa kuwaacha wake zenu; lakini tangu mwanzo haikuwa hivi”.
Na ndio maana utaona, japokuwa waliruhusiwa kufanya hivyo, lakini bado tatizo la uzinzi halikutatuliwa lote, kwamfano Daudi alikuwa na wake wengi, pamoja na Masuria wengi, lakini bado hakuacha kwenda kutafuta wake za watu, na kuzini nao (Mke wa Uria). 2Samweli 11&12..Kwasababu kiu ya uzinzi haizimwi kwa kuoa wake wengi.
Vivyo hivyo, Na katika masuala ya kuondoa huzuni, au uchungu moyoni, walikuwa na desturi, kwamba mtu aliye katika hali hiyo, mfano kama kafiwa na watoto wake wote, au mke n.k. kama vile Ayubu Walikuwa wanawapa pombe, wanywe kwa kipindi hicho iwasahaulishe matatizo yao. Lakini hilo halikufanikiwa kwa wakati wote, kwasababu pombe ikiisha tu kichwani, huzuni yake inarudia tena pale pale..kwasababu kiu ya huzuni haiwezi kukatwa kwa pombe..Mungu aliruhusu tu iwe hivyo kwa muda, kwasababu ya mazingira waliyokuwa nayo kwa wakati ule, lakini halikuwa kusudi lake tangu mwanzo.
Na ndio maana sasa katika wakati wa agano jipya Mungu alileta suluhisho la moja kwa moja la mambo yote rohoni na suluhisho lenyewe ni ROHO MTAKATIFU.
Bwana Yesu alisema..
Yohana 7:37 “Hata siku ya mwisho, siku ile kubwa ya sikukuu, Yesu akasimama, akapaza sauti yake akisema, Mtu akiona kiu, na aje kwangu anywe. 38 Aniaminiye mimi, kama vile maandiko yalivyonena, mito ya maji yaliyo hai itatoka ndani yake. 39 Na neno hilo alilisema katika habari ya Roho, ambaye wale wamwaminio watampokea baadaye; kwa maana Roho alikuwa hajaja, kwa sababu Yesu alikuwa hajatukuzwa”
Yohana 7:37 “Hata siku ya mwisho, siku ile kubwa ya sikukuu, Yesu akasimama, akapaza sauti yake akisema, Mtu akiona kiu, na aje kwangu anywe.
38 Aniaminiye mimi, kama vile maandiko yalivyonena, mito ya maji yaliyo hai itatoka ndani yake.
39 Na neno hilo alilisema katika habari ya Roho, ambaye wale wamwaminio watampokea baadaye; kwa maana Roho alikuwa hajaja, kwa sababu Yesu alikuwa hajatukuzwa”
Roho Mtakatifu akishaingia ndani ya mtu, anafanya kazi ambayo pombe imeshindwa, madawa ya kulevya yameshindwa, anamwondolea mtu hofu yote, uchungu wote, tamaa yote, wasiwasi wote na mashaka yote, na kiu yote ya uovu milele. Na ndio maana mtu aliyejazwa na Roho Mtakatifu vizuri huwa anaonekana kama mlevi, mtu asiyejali ni nini anakipitia saa hiyo..Kama tunavyoona siku ile ya Pentekoste.
Matendo 2:15 “Sivyo mnavyodhani; watu hawa hawakulewa, kwa maana ni saa tatu ya mchana; 16 lakini jambo hili ni lile lililonenwa kwa kinywa cha nabii Yoeli, 17 Itakuwa siku za mwisho, asema Mungu, nitawamwagia watu wote Roho yangu, na wana wenu na binti zenu watatabiri; na vijana wenu wataona maono; na wazee wenu wataota ndoto”.
Matendo 2:15 “Sivyo mnavyodhani; watu hawa hawakulewa, kwa maana ni saa tatu ya mchana;
16 lakini jambo hili ni lile lililonenwa kwa kinywa cha nabii Yoeli,
17 Itakuwa siku za mwisho, asema Mungu, nitawamwagia watu wote Roho yangu, na wana wenu na binti zenu watatabiri; na vijana wenu wataona maono; na wazee wenu wataota ndoto”.
Hivyo, sisi hatuna ruhusu ya kunywa pombe, kwasababu ndani ya pombe, biblia inasema upo UZINZI, na matendo mabaya, lakini katika Roho Mtakatifu upo uhuru. Ukinywa pombe unatenda dhambi.
Waefeso 5:18 “Tena msilewe kwa mvinyo, ambamo mna ufisadi; bali mjazwe Roho;”
Kwahiyo mstari huo hauhalalishi ulevi, kama tu vile uoaji wa wake wengi usivyokuwa halali sasa, japokuwa uliruhusiwa katika agano la kale.
Tutambue ujumbe wa saa tunayoishi.
Bwana akubariki.
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.
JE! ULEVI NI DHAMBI?.
Nini maana ya msiwe waalimu wengi (Yakobo 1:3)?
Je Lutu alikwenda kuwahukumu watu wa Sodoma na Gomora? Kulingana na Mwanzo 19:9?
USIJITUMAINISHE JUU YA SIRA YAKO ANGALI UPO KATIKA DHAMBI.
Nini maana ya Usiwe mwovu kupita kiasi? (Mhubiri 7:17)
Rudi nyumbani
Jibu: Tusome,
Mathayo 11:19 “Mwana wa Adamu alikuja, akila na kunywa, wakasema, Mlafi huyu, na mlevi, rafiki yao watoza ushuru na wenye dhambi! Na hekima imejulikana kuwa ina haki kwa kazi zake”.
Kabla ya kujua kama Bwana Yesu alikuwa ni mlevi au la!..tujiulize kwanza kama alikuwa kweli Mlafi?.
Kama Bwana hakuwa mlafi basi ni wazi kuwa pia hakuwa mlevi.
Lakini swali la kujiuliza ni kwanini walimwona kama mlafi na Mlevi?
Jibu ni kwasababu muda mwingi alikuwa anashinda na wenye dhambi akiwafundisha.
Kikawaida ukionekana mara kwa mara unazungumza na walevi, au unashinda na walevi, ni rahisi na wewe kuzushiwa ni Mlevi hata kama si mlevi, vile vile unapoonekana mara kwa mara unaingia kwenye nyumba za watu, na wakati mwingine kula nao ni rahisi kuzushiwa ni mlafi.
Sasa Bwana Yesu naye alikuwa ni mtu wa kuzunguka mara nyingi kwenye nyumba za watu, hususani wenye dhambi pale walipomwalika, hivyo hiyo ikamfanya wale wasiomwelewa kufikiri ni mlafi, kufikiri kwamba anazunguka kwenye hizo nyumba kutafuta kula, kumbe Bwana hakuwa anaingia kwenye nyumba za watu kutafuta chakula bali kutafuta roho zao.
Utalithibitisha hilo siku alipokwenda kwa Zakayo mtoza ushuru katika Luka 19:2-8, na alipokwenda kwa Simoni mkoma katika Mathayo 26: 6-13, Na sehemu nyingine zote.
Hivyo kwa hitimisho ni kwamba Bwana hakuwa mlevi, kama vile jinsi ambavyo hakuwa mlafi.. Ila alionekana na baadhi ya watu kama mlevi kutokana na jinsi alivyokaa muda mwingi na wenye dhambi, ambao ndani yake wamo walevi…
Lakini hekima yake ilikuwa na nguvu kuliko yao, kwasababu aliwaambia maneno yafuatayo..
Marko 2:16 “Na waandishi na Mafarisayo walipomwona anakula pamoja na watoza ushuru na wenye dhambi, waliwaambia wanafunzi wake, Mbona anakula pamoja na watoza ushuru na wenye dhambi? 17 Yesu aliposikia aliwaambia, Wenye afya hawahitaji tabibu, bali walio hawawezi; sikuja kuwaita wenye haki, bali wenye dhambi”.
Marko 2:16 “Na waandishi na Mafarisayo walipomwona anakula pamoja na watoza ushuru na wenye dhambi, waliwaambia wanafunzi wake, Mbona anakula pamoja na watoza ushuru na wenye dhambi?
17 Yesu aliposikia aliwaambia, Wenye afya hawahitaji tabibu, bali walio hawawezi; sikuja kuwaita wenye haki, bali wenye dhambi”.
Na sisi hatuna budi, kuiiga hekima ya Bwana Yesu, ya kuwapelekea injili wale wasio na afya, watu walio katika vifungo vya giza walio katika manyumba, walio katika masoko yao ya kujiuza miili yao, walio mahospitalini, mitaani n.k na sio muda wote kudumu kanisani tu!..mahali ambapo tayati kuna nuru, tayari kuna watu wenye afya.
Bwana atusaidie.
Maran atha.
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali. Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 3
Je! Daudi hakuwa mtoto wa ndoa wa Yese? (Zab 51:5)
Biblia inamaanisha nini iliposema “wakidhania kuwa ulevi wakati wa mchana ni anasa;?
YANAYOENDELEA SASA KATIKA MADHABAHU YA MUNGU ROHONI.
DOWNLOAD PDF
WhatsApp
SWALI:Tunasema Yesu karejesha kila kitu Adamu alichopoteza pale Edeni, Lakini kiuhalisia mbona hajarejesha kila kila kitu, mbona tunaona kifo bado kipo, mbona waovu ndio wanaotawala dunia, mbona magonjwa na ajali vinakithiri duniani?
JIBU: Ni kweli kabisa Bwana wetu Yesu Kristo, amekabidhiwa umiliki wa vitu vyote, Kuanzia juu mbinguni, mpaka huku duniani, vyote vipo chini yake. Na kazi kuu aliyokuja kuifanya ni kuvirejesha vyote vilivyoharibiwa na adui, katika nafasi yake, na hata Zaidi yah apo.
Mathayo 11: 27a Akasema, Nimekabidhiwa vyote na baba yangu;..
Soma pia,
Waefeso 1:20 “…. akamweka mkono wake wa kuume katika ulimwengu wa roho; 21 juu sana kuliko ufalme wote, na mamlaka, na nguvu, na usultani, na kila jina litajwalo, wala si ulimwenguni humu tu, bali katika ule ujao pia; 22 akavitia vitu vyote chini ya miguu yake, akamweka awe kichwa juu ya vitu vyote kwa ajili ya kanisa; ambalo 23 ndilo mwili wake, ukamilifu wake anayekamilika kwa vyote katika vyote”.
Waefeso 1:20 “…. akamweka mkono wake wa kuume katika ulimwengu wa roho;
21 juu sana kuliko ufalme wote, na mamlaka, na nguvu, na usultani, na kila jina litajwalo, wala si ulimwenguni humu tu, bali katika ule ujao pia;
22 akavitia vitu vyote chini ya miguu yake, akamweka awe kichwa juu ya vitu vyote kwa ajili ya kanisa; ambalo
23 ndilo mwili wake, ukamilifu wake anayekamilika kwa vyote katika vyote”.
Basi kama ni hivyo, utauliza ni kwanini basi, hatuoni mamlaka yake yote yakitimia ulimwenguni?
Jambo ambalo watu wengi hawajui ni kuwa, Huduma ya Bwana wetu Yesu Kristo haijaishia pale tu alipopaa kwenda mbinguni..bali aliondoka kwa muda tu, akaahidi kurudi, Na ndio maana ujio wake,aliugawanya mara mbili, ambapo mara ya kwanza alikuja kwa lengo la kuokoa roho za watu na mauti, ndipo hapo akalazimika kufa msalabani, ili damu ipatikane kwa ajili ya ondoleo la dhambi. Hivyo kipindi chote hicho hakuhangaika, na mambo yoyote ya mwilini, au ya kiutawala, au ya kijeografia japokuwa alikuwa amekabidhishwa vyote.
Lakini ujio wake wa pili, hautakuwa tena kama ule wa kwanza, wenye lengo la wokovu wa roho za watu..Hapana, bali atakuja mahususi kwa lengo la kuukomboa huu ulimwengu na mifumo yake yote mibovu, Hapo ndipo atakapokuja kama mtawala, yaani MFALME WA WAFALME na BWANA WA MABWANA. Katika ule utawala wa miaka 1000 (Ufunuo 19:16)
Sasa atakapokuja katika awamu hii,
1) jambo la kwanza atakalofanya ataleta Amani duniani. Kutimiza lile andiko kwamba siku ile Mbwa-mwitu atalala Pamoja na mwana-kondoo, mtoto anyonyaje atacheka kwenye tundu la nyoka. (Isaya 11:5-9, 65:25)
2) Pili atadhibiti uchungu; Watu hawatazaa t tena kwa uchungu (Isaya 65:23)
3) Tatu atabidhibiti, magonjwa na maajali: Hilo ndilo litakalowafanya watu waweze kuishi miaka mingi hata karibia na 1000. (Isaya 65:20). Biblia inasema kipindi hicho, mtu atayekufa na miaka mia ataitwa mtoto mchanga.
4) Nne atadhibiti uharibifu: Yaani Hutajenga, akakaa mwingine, wala hutapanda akala mwingine..(Isaya 65:22)
5) Tano atadhibiti dhambi: Kumbuka wakati huo shetani atakuwa amefungiwa, na mtu yeyote atakayeonyesha dalili za uvunjifu wa amani, fimbo ya chuma, itamlalia.(Ufunuo 12:5)
6) Na mwisho kabisa atamalizana na MAUTI, huyu ndiye adui wa mwisho.
Kiasi kwamba hakutakuwa na kifo tena ulimwenguni, wala machozi, wala maombolezo.
Hapo ndipo atakamporejeshea Baba mamlaka yote. Na kazi yake itakuwa imekwisha ya ukombozi. Na ndio hapo tutaingia katika ile mbingu mpya na nchi mpya, ambayo Jicho halijawahi kuona wala sikio kusikia.
1Wakorintho 15:24 “Hapo ndipo mwisho, atakapompa Mungu Baba ufalme wake; atakapobatilisha utawala wote, na mamlaka yote, na nguvu. 25 Maana sharti amiliki yeye, hata awaweke maadui wake wote chini ya miguu yake. 26 ADUI WA MWISHO ATAKAYEBATILISHWA NI MAUTI”.
1Wakorintho 15:24 “Hapo ndipo mwisho, atakapompa Mungu Baba ufalme wake; atakapobatilisha utawala wote, na mamlaka yote, na nguvu.
25 Maana sharti amiliki yeye, hata awaweke maadui wake wote chini ya miguu yake.
26 ADUI WA MWISHO ATAKAYEBATILISHWA NI MAUTI”.
Hivyo, kwa kipindi hichi tulichopewa hapa katikati, tangu siku alipopaa hadi sasa, ni kuhakikisha kila mmoja, anaupokeo huo ukombozi wa roho yake, kwa gharama yoyote ile. Na hiyo inakuja tu kwa kumwamini Yesu Kristo, na kumpokea Roho wake.
Lakini kama mtu atakutwa katika hali ya dhambi hadi siku anayorudi mara ya pili, ajue kuwa hakuna neema tena ya ukombozi juu yake kwasababu Kristo ameshabadili ofisi. Wakati huo, atawaangamiza waovu wote kwa kuwaua kwa pumzi yake (Ufunuo 19:21). Kisha kwenda kuwatupa katika ziwa la moto.
Hivyo, uovu unaouna leo hii duniani ni wa kitambo tu, vita unavyoviona, uchungu, magonjwa na vifo, vyote vina muda mfupi. Hivi karibu Bwana anarudi, kuja kutawala na sisi kwa muda wa miaka 1000. Ndani ya hichi kipindi kila kitu kitarejeshwa katika hali yake.
Na ndio maana huna sababu ya kukimbizana na huu ulimwengu mbovu, ambao tumezungukwa na hatari ya kila namna, ndugu jiwekee hazina mbinguni, kwenye huo ulimwengu ujao wa amani unaokuja.
Lakini kwa bahati mbaya si wote watapokea neema hii ya kutawala na Kristo. Ikiwa utakufa leo katika hali yako ya dhambi. Utabakia huko huko makaburini hadi siku ile ya ufufuo, kisha uhukumiwe na kutupwa motoni.
Je! Bado unaendelea katika dhambi zako? Bado unaichezea tu hii neema? Kisa Kristo ni mpole sasa kwako unadhani atakuvumilia hivyo katika hali yako ya dhambi milele ? Ndugu yangu. Bwana Yesu Kristo ni mkuu kuliko unavyoweza kufikiri, utalithibitisha hilo, siku ile atakaporudi mara ya pili. Ambapo biblia inasema kila kinywa kitakiri, na kila goti litapigwa. Na mataifa watamwombolezea.
Heri ukampa Yesu Kristo Maisha yako angali bado una muda mchache, hivi karibuni Parapanda italia, Na Kristo atabadili ofisi yake.
Maran Atha.
KWANINI YESU NI ADAMU WA PILI?
Kwanini Mungu aliwaita Adamu na Hawa jina moja?
TAFAKARI SANA KABLA YA KUAMUA HATIMA YAKO.
Biblia inaposema “Wote tumetenda dhambi” si inamaanisha hakuna mtakatifu duniani?
HUTATAMBUA LOLOTE, SIKU YA UNYAKUO IKIFIKA.
SWALI; Naomba kuuliza katika ufunuo 21:27 kwamba hakitaingia kilicho kinyonge hili neno kinyonge linamaanisha nini? Je ni watu dhaifu mfano vilema?
Ufunuo wa Yohana 21:27 [27]Na ndani yake hakitaingia kamwe cho chote kilicho kinyonge, wala yeye afanyaye machukizo na uongo, bali wale walioandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo.
JIBU: “Kinyonge” kinachozungumziwa hapo si mtu mlemavu, kama ingekuwa hivyo Bwana Yesu asingesema..kiungo chako kimoja kikikukosea king’oe ni heri uingie mbinguni mlemavu kuliko kuwa viungo vyako vyote na kuishia kuzimu.(Mathayo 5:29-30)
Lakini kinyonge kinachozungumziwa hapo ni kipi?
Kitu kinyonge sikuzote ni kitu kisichokuwa na nguvu ya kustahimili mtikisiko fulani aidha mapigano,ugonjwa,Dhoruba, mateso n.k.
Vivyo hivyo katika roho mtu asiyekuwa na nguvu ya kuushinda ulimwengu huyo ni sawa na mnyonge. Na ndio maana Bwana Yesu alisema maneno haya..
Mathayo 11:12[12]Tangu siku za Yohana Mbatizaji hata sasa ufalme wa mbinguni hupatikana kwa nguvu, nao wenye nguvu wauteka.
Utajiuliza ni kwanini Bwana arejee siku za Yohana mbatizaji, na sio siku za labda, Isaya, au Musa, au Samweli? Bali Yohana Mbatizaji?
Alisema hivyo, ili kutupa picha na sisi tunapaswa tuishi Maisha ya kuukana ulimwengu, mfano wa Yohana mbatizaji..Ambaye biblia inasema Maisha yake yote, aliishi majangwani mbali na ulimwengu, na matokeo yake akawa akiongezeka nguvu rohoni kila siku (Luka 1:80).
Hivyo na sisi tunapaswa tuushinde ulimwengu, ili tuweza kuuteka ufalme wa Mungu, ikiwa uzinzi utatushinda, ikiwa anasa na tamaa za ujanani zitatushinda, basi sisi ni wanyonge, na hivyo, kamwe hatutakaa tuuingie ule mji mpya wa Yerusalemu, utakaoshuka kutoka mbinguni. Kwasababu watakaoingia kule ni watakatifu tu walioushinda ulimwengu, na si vinginevyo.
Huu si wakati wa kuikumbatia dhambi..na kusema kwamba mimi siwezi kuushinda ulimwengu, ni wajibu wako kushindana mpaka ushinde…hupaswi kuwa mnyonge. Kumbuka wewe ukishindwa haimaanishi kuwa mwingine kashindwa.
Lakini tutawezaje kufikia hapo?
Tutafika kwa njia moja tu nayo ni kwa kumaanisha kabisa kuacha dhambi, na kujitwika misalaba yetu na kumfuata Yesu kwa gharama zozote zile.
Shalom.
MAANA WEWE, BWANA HUKUWAACHA WAKUTAFUTAO”.
KWANINI MIMI?
Je aliyezungumza na Musa kule jangwani ni Mungu mwenyewe au malaika wake?
Kama tunaokolewa kwa neema kwanini wokovu tuupate kwa nguvu?
Warumi 8:29 “Maana wale aliowajua tangu asili, aliwachagua tangu asili wafananishwe na mfano wa Mwana wake, ili yeye awe mzaliwa wa kwanza miongoni mwa ndugu wengi. 30 Na wale aliowachagua tangu asili, hao akawaita; na wale aliowaita, hao akawahesabia haki; na wale aliowahesabia haki, hao akawatukuza”.
Warumi 8:29 “Maana wale aliowajua tangu asili, aliwachagua tangu asili wafananishwe na mfano wa Mwana wake, ili yeye awe mzaliwa wa kwanza miongoni mwa ndugu wengi.
30 Na wale aliowachagua tangu asili, hao akawaita; na wale aliowaita, hao akawahesabia haki; na wale aliowahesabia haki, hao akawatukuza”.
Ni kweli maandiko hapo yanasema Bwana anawajua walio wake tangu asili.
Ili Mungu awe Mungu ni lazima ajue mambo yote, ni lazima aujue mwisho katika mwanzo. Vinginevyo asipojua hivyo, huyo sio Mungu.
Lakini pamoja na kujua hatima zetu wote, bado hajatuambia ni nani ataokolewa na nani hataokolewa. Nafasi ya kuokolewa ipo kwa wote, kadhalika nafasi ya kupotea ipo kwa wote, ni jukumu letu sisi kupambana ili tusijikute tumeingia katika hilo kundi la ambao hawataokoka na kuingia katika ziwa la moto.
Bwana Yesu alijua tangu mwanzo ni Nani atakayemsaliti, na akawaambia mapema wanafunzi wake kwamba mmoja wenu atanisaliti, Lakini hakutaja jina kwamba ni Yuda!. Aliachia hapo katikati, kila mtu ajihisi kama ni yeye, ili lengo kila mtu ajitathmini mienendo yake na ajihadhari na roho ya usaliti.
Lakini Bwana kwa kusema hivyo, hakuacha kuendelea kuwahubiria wanafunzi wake, au hata Yuda na wanafunzi pia waliendelea kuhubiri, kwasababu siri ya atakayemsaliti alikuwa nayo Bwana na sio wao..Hivyo kazi waliyokuwa nayo ni kuendelea na kuhubiri injili, na kujitahidi wasitimize huo unabii…
Marko 14:18 “Nao walipokuwa wameketi chakulani, wakila, Yesu alisema, Amin, nawaambia, Mmoja wenu, naye anakula pamoja nami, atanisaliti. 19 Wakaanza kuhuzunika, wakamwambia mmoja mmoja, Je! Ni mimi? 20 Akawaambia, Ni mmoja wa hao Thenashara, ambaye achovya pamoja nami katika kombe”.
Marko 14:18 “Nao walipokuwa wameketi chakulani, wakila, Yesu alisema, Amin, nawaambia, Mmoja wenu, naye anakula pamoja nami, atanisaliti.
19 Wakaanza kuhuzunika, wakamwambia mmoja mmoja, Je! Ni mimi?
20 Akawaambia, Ni mmoja wa hao Thenashara, ambaye achovya pamoja nami katika kombe”.
Na hata sasa Mungu anatuambia lipo kundi litakalomsaliti, lipo litakaloingia katika ziwa la moto, lakini hajataja majina, hivyo ni wajibu wetu sisi kupambana tusiwe mojawapo ya hao.
Sasa swali tunalopaswa tujiulize kila mmoja wetu ni hili:
Utajuaje kama wewe utaangukia katika kundi la watu ambao wataingia jehanamu ya moto?..
Hautajua kwa tafsiri ya jina lako, wala kwa rangi ya uso wako, wala kwa kimo chako, wala kwa jinsia yako wala kwa kabila ulilotokea au familia uliyotokea.
Bali utajijua kwa tabia zako!. Kama maisha yako bado ni ya dhambi, ya anasa, ya kiulimwengu na uzinzi na uasherati, ya kuabudu sanamu, ya kutokujali mambo ya Ki-Mungu kama Yuda, ingawa unaonywa mara nyingi..basi fahamu kuwa upo miongoni mwa lile kundi lililotabiriwa kutourithi uzima wa milele.
Kadhalika kama upo ndani ya Kristo, na umepokea Roho Mtakatifu, na unayafanya mapenzi yake basi fahamu kuwa upo katika kundi la watu waliotabiriwa uzima wa milele.
Kwahiyo kwa hitimisho ni kwamba injili tunapaswa tuendelee kuihubiri kama mitume walivyoendelea na kazi hata baada ya kujua kuwa miongoni mwao yupo atakayemsaliti Bwana..zaidi sana tujihadhari na dhambi ili tusiwe miongoni mwa watakaotupwa katika ziwa la moto.
2 Timotheo 2:19 “Lakini msingi wa Mungu ulio imara umesimama, wenye muhuri hii, Bwana awajua walio wake. Na tena, Kila alitajaye jina la Bwana na auache uovu“
Biblia ina maana gani inaposema akonyezaye kwa jicho huleta masikitiko?
NI LIPI KATI YA MAKUNDI HAYA, WEWE UPO?
WAKATI AHADI INAPOKARIBIA, HUWA KUNA MAMBO YANATOKEA.
Neno Saumu lina maana gani katika biblia?
Tofauti na desturi za mataifa mengi ya sasa zilivyo, kwamba mtu akitaka kuapa, huwa anashika kitabu Fulani cha dini kama vile biblia, au anaweka mkono wako kifuani ndipo anatamka kiapo chake..Zamani kulingana na desturi wa wayahudi ilikuwa ni mtu anaweka mkono wake, chini ya paja la anayemwapisha.
Pajani kibiblia ni sehemu ambayo ipo karibu sana na viungo vya uzazi.. Sehemu nyeti, ambapo hapawezi kufikiwa kama jambo lililopangwa halihitaji umakini sana. Ni sawa na leo watu wanavyotumia biblia mahakamani kuapa, ni kitabu nyeti sana, kiasi kwamba mpaka kimetumiwa hiko ni kuonyesha umakini wa kile unachotakiwa kukifanya.
Na ndivyo ilivyokuwa kwa Ibrahimu, na Yakobo. Kwamfano Ibrahimu alipotaka mwanawe Isaka apatiwe mke kutoka katika nyumba ya Ndugu yake, aliyekuwa mbali sana, alimwita mtumwa wake, akamwapisha kwamba akamletee binti sawasawa na alivyomwagiza, Hivyo ili kuthibitisha kuwa mtumwa wake atayatekeleza yale aliyoagizwa, akachukua mkono wake, na kuulia katika paja lake, kuonyesha pia kwamba yupo tayari kutii kila agizo lililoamriwa juu yake.
Mwanzo 24:2 “Ibrahimu akamwambia mtumishi wake, mzee wa nyumba yake, aliyetawala vitu vyake vyote, Tafadhali uutie mkono wako chini ya paja langu, 3 nami nitakuapisha kwa Bwana, Mungu wa mbingu, na Mungu wa nchi, kwamba hutamtwalia mwanangu mke katika binti za Wakanaani ambao nakaa kati yao;”… 9 Yule mtumishi akaweka mkono wake chini ya paja la Ibrahimu bwana wake, akamwapia katika neno hilo. 10 Kisha huyo mtumishi akatwaa ngamia kumi katika ngamia za bwana wake akaenda zake, maana mali zote za bwana wake zilikuwa mkononi mwake, akaondoka, akaja mpaka Mesopotamia, mpaka mji wa Nahori.
Mwanzo 24:2 “Ibrahimu akamwambia mtumishi wake, mzee wa nyumba yake, aliyetawala vitu vyake vyote, Tafadhali uutie mkono wako chini ya paja langu, 3 nami nitakuapisha kwa Bwana, Mungu wa mbingu, na Mungu wa nchi, kwamba hutamtwalia mwanangu mke katika binti za Wakanaani ambao nakaa kati yao;”…
9 Yule mtumishi akaweka mkono wake chini ya paja la Ibrahimu bwana wake, akamwapia katika neno hilo. 10 Kisha huyo mtumishi akatwaa ngamia kumi katika ngamia za bwana wake akaenda zake, maana mali zote za bwana wake zilikuwa mkononi mwake, akaondoka, akaja mpaka Mesopotamia, mpaka mji wa Nahori.
Jambo kama hilo tunaliona pia kwa Yakobo, siku ile alipokaribia kufa, alimwita Yusufu na kumwambia, aweke mkono wake chini ya paja lake, ali amwapie, kwamba hatamzika kule Misri bali, katika nchi ya Baba yake.
Mwanzo 47:29 “Siku za kufa kwake Israeli zikakaribia; akamwita mwanawe Yusufu, akamwambia, Kama nimeona kibali machoni pako, weka mkono wako chini ya paja langu, ukanifanyie rehema na kweli; nakusihi usinizike katika Misri. 30 Lakini nitakapolala pamoja na baba zangu, unichukue toka Misri, unizike katika kaburi lao. Akasema, Nitafanya kama ulivyosema. 31 Akanena, Niapie. Naye akamwapia. Israeli akajiinamisha kwenye mchago wa kitanda”.
Mwanzo 47:29 “Siku za kufa kwake Israeli zikakaribia; akamwita mwanawe Yusufu, akamwambia, Kama nimeona kibali machoni pako, weka mkono wako chini ya paja langu, ukanifanyie rehema na kweli; nakusihi usinizike katika Misri.
30 Lakini nitakapolala pamoja na baba zangu, unichukue toka Misri, unizike katika kaburi lao. Akasema, Nitafanya kama ulivyosema.
31 Akanena, Niapie. Naye akamwapia. Israeli akajiinamisha kwenye mchago wa kitanda”.
Lakini sisi katika agano jipya, hatujapewa ruhusa ya kuapa bali Bwana Yesu alisema, maneno yetu yawe Ndio, ndio.. Au Sio,..sio..Na si zaidi. (Mathayo 5:33-37). Hakuna sababu ya kuapa, kwasababu hatuna mamlaka ya kutangua au kuthibitisha chochote katika maisha yetu kana kwamba vipo chini ya uwezo wetu.Sisi si Mungu.
Naomba kujua nini maana ya kuteguka uvungu wa paja?
Je Bwana Yesu alikuwa na mchoro (tattoo) katika paja lake? (Ufunuo 19:16).
JE! NI KWELI UMEMFUATA YESU?
Kwanini Yesu aliwakataza mitume wake kumdhihirisha?
Ipo tabia moja ya kipekee ya wageni waliostaarabika. Kikawaida wageni walio wastaarabu huwa wanaonyesha tabia fulani baadhi ambazo wenyeji wanapaswa wazijue ili waweze kuchukuliana nao na kuendana nao.
Kikawaida mgeni sio mtu wa kuonyesha moja kwa moja kwamba anajitaji jambo fulani kutoka kwa mwenyeji, mgeni akija kukutembelea bila shaka hawezi kukuomba chakula hata kama ana njaa sana, utaona atakaa na wewe kimya, na tena utakapofika wakati wa kuondoka, utaona anaondoka bila hata kukukumbusha suala la chakula, tena utaona anaondoka kwa furaha sana, na wakati mwingine hata kwa kukupa asante nyingi. Lakini moyoni, hajafurahishwa sana!.
Hivyo ni wajibu wako wewe kupambanua ni nini mgeni anahitaji kwa wakati huo. Kama ni chakula, au makazi au malazi.. Ili ajisikie yupo nyumbani kadhalika awe huru kuzungumza nawe zaidi..
Ukiona mgeni kakutembelea asubuhi jua kuna kitu anakihitaji kwako kwa asubuhi hiyo usimfanye akae mpaka jioni, wala usijifanye huelewi, ukiona mgeni kafika kwako mchana wakati wa kupata riziki, ujue ana nafasi pia katika hicho chakula, ukiona anashinda kwako mpaka jioni, ujue pengine anahitaji kulala kwako, mwekee mazingira ya kulala kwasababu pengine kuna jambo na atakapoona umemwelewa hali yake na umemruhusu ale chakula chako, au alale kwako, basi ni rahisi zaidi kusikia mengi kutoka kwake, au kukufunulia mengi.
Lakini ukimnyima riziki, au makazi, au malazi.. utafikiri kweli umemkomoa lakini hutasikia mengi, ambayo angetaka kukuambia..
Kadhalika Kristo naye kuna wakati anakuja kwetu kama Mgeni, au anatukaribia kama mgeni, na anakuwa anaonyesha tabia zote kama za mgeni. Atakuwa ana njaa, lakini atajifanya kama hana njaa, atakuwa anatamani kuja kulala na sisi lakini atajifanya kama anapita tu!. Ndicho kilichowatokea wale watu wawili waliokuwa wanakwenda Emau.
Hebu tuisome habari hiyo vizuri katika kitabu cha Luka.
Luka 24:13 “Na tazama, siku ile ile watu wawili miongoni mwao walikuwa wakienda kijiji kimoja, jina lake Emau, kilichokuwa mbali na Yerusalemu kama mwendo wa saa mbili. 14 Nao walikuwa wakizungumza wao kwa wao habari za mambo hayo yote yaliyotukia. 15 Ikawa katika kuzungumza na kuulizana kwao, Yesu mwenyewe alikaribia, akaandamana nao. 16 Macho yao yakafumbwa wasimtambue. 17 Akawaambia, Ni maneno gani haya mnayosemezana hivi mnapotembea? Wakasimama wamekunja nyuso zao. 18 Akajibu mmoja wao, jina lake Kleopa, akamwambia, Je! Wewe peke yako u mgeni katika Yerusalemu, hata huyajui yaliyotukia humo siku hizi? 19 Akawauliza, Mambo gani? Wakamwambia, Mambo ya Yesu wa Nazareti, aliyekuwa mtu nabii, mwenye uwezo katika kutenda na kunena mbele za Mungu na watu wote; 20 tena jinsi wakuu wa makuhani na wakubwa wetu walivyomtia katika hukumu ya kufa, wakamsulibisha. 21 Nasi tulikuwa tukitumaini ya kuwa yeye ndiye atakayewakomboa Israeli. Zaidi ya hayo yote, leo ni siku ya tatu tangu yalipotendeka mambo hayo;…………….. 25 Akawaambia, Enyi msiofahamu, wenye mioyo mizito ya kuamini yote waliyoyasema manabii! 26 Je! Haikumpasa Kristo kupata mateso haya na kuingia katika utukufu wake? 27 Akaanza kutoka Musa na manabii wote, akawaeleza katika maandiko yote mambo yaliyomhusu yeye mwenyewe. 28 Wakakikaribia kile kijiji walichokuwa wakienda, NAYE ALIFANYA KAMA ANATAKA KUENDELEA MBELE. 29 Wakamshawishi wakisema, Kaa pamoja nasi, kwa kuwa kumekuchwa, na mchana unakwisha. Akaingia ndani kukaa nao”.
Luka 24:13 “Na tazama, siku ile ile watu wawili miongoni mwao walikuwa wakienda kijiji kimoja, jina lake Emau, kilichokuwa mbali na Yerusalemu kama mwendo wa saa mbili.
14 Nao walikuwa wakizungumza wao kwa wao habari za mambo hayo yote yaliyotukia.
15 Ikawa katika kuzungumza na kuulizana kwao, Yesu mwenyewe alikaribia, akaandamana nao.
16 Macho yao yakafumbwa wasimtambue.
17 Akawaambia, Ni maneno gani haya mnayosemezana hivi mnapotembea? Wakasimama wamekunja nyuso zao.
18 Akajibu mmoja wao, jina lake Kleopa, akamwambia, Je! Wewe peke yako u mgeni katika Yerusalemu, hata huyajui yaliyotukia humo siku hizi?
19 Akawauliza, Mambo gani? Wakamwambia, Mambo ya Yesu wa Nazareti, aliyekuwa mtu nabii, mwenye uwezo katika kutenda na kunena mbele za Mungu na watu wote;
20 tena jinsi wakuu wa makuhani na wakubwa wetu walivyomtia katika hukumu ya kufa, wakamsulibisha.
21 Nasi tulikuwa tukitumaini ya kuwa yeye ndiye atakayewakomboa Israeli. Zaidi ya hayo yote, leo ni siku ya tatu tangu yalipotendeka mambo hayo;……………..
25 Akawaambia, Enyi msiofahamu, wenye mioyo mizito ya kuamini yote waliyoyasema manabii!
26 Je! Haikumpasa Kristo kupata mateso haya na kuingia katika utukufu wake?
27 Akaanza kutoka Musa na manabii wote, akawaeleza katika maandiko yote mambo yaliyomhusu yeye mwenyewe.
28 Wakakikaribia kile kijiji walichokuwa wakienda, NAYE ALIFANYA KAMA ANATAKA KUENDELEA MBELE.
29 Wakamshawishi wakisema, Kaa pamoja nasi, kwa kuwa kumekuchwa, na mchana unakwisha. Akaingia ndani kukaa nao”.
Hapo katika mstari wa 29 maandiko yanasema.. “NAYE ALIFANYA KAMA ANATAKA KUENDELEA MBELE.” Yaani baada ya kuzungumza nao muda wote huo, umefika wakati wa kuingia ndani, yeye anajifanya kama anataka kuendelea na safari!.. Hebu jiulize endapo wale watu wangekuwa wachoyo, na kusema kile chakula chetu kule ndani kinatutosha tu sisi wawili, huyu mtu mwache aendelee zake, je wangekosa mangapi?..au wangesema kile kitanda chetu kule ndani kinatutosha tu sisi wawili na si mwingine watatu, wangekosa mangapi?..Lakini tunaona walielewa hali ya mgeni kwamba kamwe hawezi kusema naomba jambo fulani kama anaona wenyeji hawana huo moyo.. Sasa hebu tuone wangekosa nini endapo wangemruhusu Bwana aende zake.. Tuendelee mbele kidogo katika mistari hiyo…
Luka 24:29 “Wakamshawishi wakisema, Kaa pamoja nasi, kwa kuwa kumekuchwa, na mchana unakwisha. Akaingia ndani kukaa nao. 30 Ikawa alipokuwa ameketi nao chakulani, alitwaa mkate, akaubariki, akaumega, akawapa. 31 Yakafumbuliwa macho yao, wakamtambua; KISHA AKATOWEKA MBELE YAO. 32 Wakaambiana, Je! Mioyo yetu haikuwaka ndani yetu hapo alipokuwa akisema nasi njiani, na kutufunulia maandiko? 33 Wakaondoka saa ile ile, wakarejea Yerusalemu, wakawakuta wale kumi na mmoja wamekutanika, wao na wale waliokuwa pamoja nao”,
Luka 24:29 “Wakamshawishi wakisema, Kaa pamoja nasi, kwa kuwa kumekuchwa, na mchana unakwisha. Akaingia ndani kukaa nao.
30 Ikawa alipokuwa ameketi nao chakulani, alitwaa mkate, akaubariki, akaumega, akawapa.
31 Yakafumbuliwa macho yao, wakamtambua; KISHA AKATOWEKA MBELE YAO.
32 Wakaambiana, Je! Mioyo yetu haikuwaka ndani yetu hapo alipokuwa akisema nasi njiani, na kutufunulia maandiko?
33 Wakaondoka saa ile ile, wakarejea Yerusalemu, wakawakuta wale kumi na mmoja wamekutanika, wao na wale waliokuwa pamoja nao”,
Umeona, kumbe sio kila mgeni ni mgeni wa kawaida tu!, si kila anayekuomba ni kwasababu anashida, si kila anayetaka kuja kukaa na wewe ni kwasababu yake yeye, wengine wanataka kuja kwako kwa faida yako wewe, wengine wanataka kula chakula chako kwa faida yako wewe… Unyonge wa Kristo kwako ni kwasababu anataka wewe upate faida.
Hivyo hata leo hii, Kristo anakuja mioyoni mwetu kama mgeni, hivyo hatuna budi tumpe nafasi.
Jambo moja wengi wasilolijua ni kwamba Kristo sio dikteta, kwamba tunapompokea basi ataanza kututumikisha kama maroboti, siku zote anakuwa kama mgeni..maana yake unapompa nafasi zaidi ndivyo anavyojifunua kwako zaidi, unapomkataa anakuacha na kukupita..wala hakulazimishi, ingawa atakuonyesha kila dalili za kutamani kuendelea kukaa na wewe…
Na sio tu katika hatua ya kumpokea yeye, bali hata baada ya kumpokea Yeye, endapo tukijitenga naye..na kujikuta tumezama kwenye mateso au majaribu hatakuja kutulazimisha atusaidie, atasogea karibu na sisi, kuonyesha ishara ya kutaka kutusaidia, lakini kama hatutampa basi hatatupa msaada..
Utasema hilo tunalithibitisha vipi kimaandiko…Hebu tusome kile kisa cha Bwana kutembea juu ya maji ni nini kiliwatokea mitume, na kwa jinsi gani Bwana aliwasaidia.
Marko 6:48 “Akawaona WAKITAABIKA kwa kuvuta makasia, kwa maana upepo ulikuwa wa mbisho; hata ilipopata kama zamu ya nne ya usiku akawaendea, akitembea juu ya bahari; AKATAKA KUWAPITA. 49 Nao walipomwona anatembea juu ya bahari, walidhani ya kuwa ni kivuli, wakapiga yowe, 50 kwa kuwa wote walimwona, wakafadhaika. Mara akasema nao, akawaambia, Changamkeni; ni mimi, msiogope”.
Marko 6:48 “Akawaona WAKITAABIKA kwa kuvuta makasia, kwa maana upepo ulikuwa wa mbisho; hata ilipopata kama zamu ya nne ya usiku akawaendea, akitembea juu ya bahari; AKATAKA KUWAPITA.
49 Nao walipomwona anatembea juu ya bahari, walidhani ya kuwa ni kivuli, wakapiga yowe,
50 kwa kuwa wote walimwona, wakafadhaika. Mara akasema nao, akawaambia, Changamkeni; ni mimi, msiogope”.
Ukisoma habari hiyo sehemu nyingine utaona, Baada ya Bwana kuingia chomboni, ule upepo ulikoma!.
Lakini nataka tuone hapo kwenye mstari wa 48, maandiko yanasema “AKATAKA KUWAPITA”.. Umewahi kujiuliza kwanini alikuwa anataka kuwapita?.. Ni kwasababu bado alikuwa hajaona kibali cha yeye kutoa msaada…ndio maana akataka kuendelea mbele
Sasa kama Kristo aliweza kufanya hivyo kwa wanafunzi wake!, ambaye aliwachagua yeye mwenyewe, atashindwaje kufanya kwangu na kwako?.
Huu ni wakati wa kumpa Kristo nafasi na kumfanya mwenyeji ndani yetu…
Unajua kabisa huelewi maandiko unapoyasoma, lakini bado humpi Yesu nafasi katika maisha yako, bado kwako ni mgeni mnyonge!.. Kwenda kanisani kwako ni jambo la kusukumwa na kulazimishwa!, kujikana nafsi kwako ni jambo zito.. ukiambiwa uache kuvaa suruali tu! Ni shida, uache vimini na mavazi yasiyo na heshima ni shida.. Kristo atajifunuaje kwako!.. Hawezi kwasababu akiangalia huku na huko anaona milango kila mahali imefungwa!… Unapitia tabu lakini hata kumtolea Mungu huwezi, zaidi sana unapinga matoleo, pasipo kujua kuwa wakati mwingine ni kwa faida yako si ya Kristo.
Je! Kristo ni mgeni au mwenyeji kwako?
Bwana Yesu anasema..
Mathayo 25:41“Kisha atawaambia na wale walioko mkono wake wa kushoto, Ondokeni kwangu, mliolaaniwa, mwende katika moto wa milele, aliowekewa tayari Ibilisi na malaika zake; 42 kwa maana nalikuwa na njaa, msinipe chakula; nalikuwa na kiu, msininyweshe; 43 nalikuwa mgeni, msinikaribishe; nalikuwa uchi, msinivike; nalikuwa mgonjwa, na kifungoni, msije kunitazama”.
Mathayo 25:41“Kisha atawaambia na wale walioko mkono wake wa kushoto, Ondokeni kwangu, mliolaaniwa, mwende katika moto wa milele, aliowekewa tayari Ibilisi na malaika zake;
42 kwa maana nalikuwa na njaa, msinipe chakula; nalikuwa na kiu, msininyweshe;
43 nalikuwa mgeni, msinikaribishe; nalikuwa uchi, msinivike; nalikuwa mgonjwa, na kifungoni, msije kunitazama”.
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya ya kila siku kwa njia ya Whatsapp basi waweza kujiunga kwa kubofya hapa >>> WHATSAPP
YESU NI MFALME WA AINA GANI KWAKO?
Je! mwanadamu wa kwanza kuumbwa ni yupi?
“Si watu wa kutumia mvinyo sana”, je tunaruhusiwa kutumia mvingo kidogo?(1Timotheo 3:8).
Hapana hata mmoja aliyethubutu kuambatana nao;
Tarshishi ni mji gani kwasasa?
Kibiblia Kizazi ni kundi la watu linalozuka ghafla lenye tabia zinazofanana, linaweza kuzuka aidha kutokana na mabadiliko ya nyakati, au mabadiliko ya mazingira. Kwamfano, Wana wa Israeli walipokuwa Misri, chini ya Yusufu, waliishi kwa raha sana, Lakini Yusufu alipokufa pamoja na Yule Farao, kilinyanyuka kizazi kingine kisichokumbuka wema wa Yusufu, na hapo ndipo utumwa mgumu ulipoanza.
Vilevile, Wana wa Israeli walipofika katika nchi yao ya Ahadi, mwanzoni waliishi maisha ya kumcha Mungu sana, lakini wakati ulipopita mrefu kilinyanyuka kizazi kingine kisichomjali Yehova, hapo ndipo Israeli ilipoanza kuingia katika matatizo mengi sana.(Waamuzi 2:10)
Na katika hichi kipindi cha Siku za mwisho, tunapaswa tuwe makini sana, Zipo tabia ambazo utaziona kwa watu wengi sana, lakini kiuhalisia hazikuwepo huko nyuma. Hivyo ni vizuri ukafahamu aina ya vizazi vilivyopo duniani sasa hivi kulingana na biblia ili ujue wewe upo wapi na jinsi gani unapaswa ujiupeshe navyo.
Mathayo 12:39 “Akajibu, akawaambia, Kizazi kibaya na cha zinaa chatafuta ishara, wala hakitapewa ishara, ila ishara ya nabii Yona”.
Ni kizazi cha watu kinachozuka kinapenda tu usherati na uzinzi kuliko kitu kingine chochote ulimwenguni. Leo hii tazama mawazo ya vijana wengi yalivyo, sikiliza mazungumzo yao, mambo wanayoyafanya kwa siri,vitu wanavyotazama mitandaoni, video za ngono, ni jambo la kawaida kwao, na kibaya zaidi sio tu vijana, hadi wazee na watoto wamo katika kundi hili. Jambo ambalo hapo zamani halikuwepo. Hiyo ni kuthibitisha kuwa ni hiki ni kizazi kingine kimezuka, ambacho ni hatari sana.
Marko 8:38 “Maana kila mtu atakayenionea haya mimi, na maneno yangu, katika KIZAZI HIKI CHA UZINZI na dhambi, Mwana wa Adamu atamwonea haya mtu huyo, atakapokuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika watakatifu”.
Ndugu, jiupeshe, na mkondo huu, si lazima uishe kama ulimwengu unavyotaka, kizazi hiki kimeshahukumiwa na Mungu.
Kipo kizazi cha Nyoka.
Mathayo 3:7 “Hata alipoona wengi miongoni mwa Mafarisayo na Masadukayo wakiujia ubatizo wake, aliwaambia, Enyi wazao wa nyoka, ni nani aliyewaonya ninyi kuikimbia hasira itakayokuja? 8 Basi zaeni matunda yapasayo toba; 9 wala msiwaze mioyoni mwenu kwamba, Tunaye baba, ndiye Ibrahimu; kwa maana nawaambia ya kwamba Mungu aweza katika mawe haya kumwinulia Ibrahimu watoto”. 10 Na shoka limekwisha kuwekwa penye mashina ya miti; basi kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa motoni.
Mathayo 3:7 “Hata alipoona wengi miongoni mwa Mafarisayo na Masadukayo wakiujia ubatizo wake, aliwaambia, Enyi wazao wa nyoka, ni nani aliyewaonya ninyi kuikimbia hasira itakayokuja?
8 Basi zaeni matunda yapasayo toba;
9 wala msiwaze mioyoni mwenu kwamba, Tunaye baba, ndiye Ibrahimu; kwa maana nawaambia ya kwamba Mungu aweza katika mawe haya kumwinulia Ibrahimu watoto”.
10 Na shoka limekwisha kuwekwa penye mashina ya miti; basi kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa motoni.
Soma pia..Mathayo 12:34
Nyoka, alikuwa mwerevu sana kuliko wanyama wote mwituni, lakini alikubali kuwa chombo teule cha shetani. Uzao wake, ndio uliendelea mpaka kwa Kaini, na ndio maana watu wale walikuwa hodari sana , wagunduzi na wavumbuzi wakubwa, lakini waovu waliopindukia (Mwanzo 6:4). Ni watu ambao walikuwa hawana muda na Mungu, lakini kwa upande wa pili uzao wa Mungu, ulikuwa ni mnyenyekevu unaomtafuta Mungu usiku na mchana, vilevile na usio na masumbufu mengi ambao ulipitia kwa Sethi. (Mwanzo 4:26).
Inafunua hadi sasa, kwamba kizazi hiki kipo, Angalia dunia ya sasa, imestaarabika kuliko ile ya zamani, watu wanaelimu kubwa sana, wanagundua mambo makubwa sana, wamekwenda mpaka mwezini, lakini ukiwagusia habari za Mungu, wanakuambia hayo ni mawazo yako tu, hakuna Mungu,dini imetengenezwa na watu, wamejikita katika mambo ya mwilini, tu, elimu, utajiri, uvumbuzi basi, Mungu hayupo.
Ndugu, ikiwa na wewe upo katika jopo hili la watu, jiangue haraka sana, hichi ni kizazi, ambacho kipo ulimwenguni sasa.
Mithali 30:11 “Kuna kizazi cha watu wamlaanio baba yao; Wala hawambariki mama yao”.
Kuporomoka kwa maadili na nidhamu unakokuona leo, hakukuwepo huko nyuma. Leo utasikia mtoto anajibizana na mzazi wake, mwingine anampiga, mwingine anamzungumzia vibaya, wengine wametengeneza mpaka uadui na wazazi wao.. Kesi hizi ni nyingi sana sikuhizi..Wewe kama mtoto, wewe kama kijana, kuwa makini sana, kizazi hiki kimezuka ulimwenguni sasa. Unapoona, wenzako hawawaheshimu wazazi wao, na wewe usiwe mmojawapo.
Katika agano la kale mtu aliyejaribu kuonyesha utomvu wa nidhani kwa mzazi wake, sheria yake ilikuwa ni kifo. Jitathmini unawatii wazazi wako, Unawapenda?, unawabariki? Unawanenea mema? Unawaombea?.. Hata kama mzazi anakuudhi, huna ruhusu ya kurudisha baya kwa baya kwake. Vinginevyo upo chini ya laana ya kizazi hiki.
Mithali 30:12 “Kuna kizazi cha watu walio safi machoni pao wenyewe; Ambao hawakuoshwa uchafu wao”.
Hili kundi ni kubwa sana, Mtamuhubiria mtu na kumwambia pasipo kumwamini Kristo, huwezi kuokolewa, yeye atakuambia, mimi naamini matendo yangu ni safi, ninaamini Mungu hiyo inatosha, siwezi kuhukumiwa. Atakuwa radhi, kujihesabia haki, hata kama ni mzinzi, au mlevi..Haoni hatia yoyote kwa anayoyafanya. Yeye anachoamini ni kuwa Mungu hawezi kumchoma motoni milele,.Nimeshakutana na watu wa namna hii wengi sana. Wanaodhani kuwa kwa kile wanachokiamini, ndio tiketi ya Mungu kuwaokoa siku ile.
Ndugu kama upo katika hili kundi jiepushe nalo, Ikiwa bado hujaokoka, mkimbilie Yesu, yeye pekee ndiye mwenye uwezo wa kukusafisha dhambi zako, na sio kile unachokiamini.
Mithali 30:13 “Kuna kizazi cha watu ambao macho yao yameinuka kama nini! Na kope zao zimeinuka sana”.
Wapo watu ambao, kujishusha hakupo ndani yao. Wanajiona kuwa hakuna chochote kinachoweza kuwa msaada kwao, Mungu si kitu kwao, kwanini wakaombe, kwanini waende ibadani. Wapo radhi hata kuutukana wokovu, au kazi ya Mungu. Wanatumaini, mali zao, au ujuzi wao.
Kama tabia hizo zimeanza kuonekana ndani yako, geuka upesi.
Mithali 30:14 “Kuna kizazi cha watu ambao meno yao ni panga; Na vigego vyao ni kama visu. Ili kuwala maskini waondolewe katika nchi, Na wahitaji katika wanadamu”.
Utu umeondoka duniani, Yupo radhi kufanya biashara haramu, bila kujali kinaleta madhara mangapi kwa jamii, anauza madawa ya kulevya, anauza bidhaa zilizoisha ubora, wanadhulumu haki za wajane na mayatima kwa faida zao wenyewe. Anaua, ili apate mali, n.k.
Tunayoyaona, hayakuwepo zamani, tusiwe watu wenye tamaa ya mali.
Lakini pamoja na kuwepo kwa vizazi hivi vyote, vya watu waovu.. Biblia inasema pia, kitakuwepo kizazi cha watu wenye adili, wanaomcha Mungu, wanaotenda mapenzi yake.
Zaburi 112:1 “Haleluya. Heri mtu yule amchaye Bwana, Apendezwaye sana na maagizo yake. 2 Wazao wake watakuwa hodari duniani; Kizazi cha wenye adili kitabarikiwa”.
Zaburi 112:1 “Haleluya. Heri mtu yule amchaye Bwana, Apendezwaye sana na maagizo yake.
2 Wazao wake watakuwa hodari duniani; Kizazi cha wenye adili kitabarikiwa”.
Na ndio maana unaona pia wapo watakatifu wa Mungu leo duniani. Hawa ndio Bwana anaowatazama, na siku moja itafika Kristo atawahamisha kutoka katika huu ulimwengu kwa tukio la UNYAKUO na kuwapeleka mbinguni. Swali ni je wewe upo katika kizazi kipi?
Matendo 2:40 “Akawashuhudia kwa maneno mengine mengi sana na kuwaonya, akisema, Jiokoeni na kizazi hiki chenye ukaidi”.
Jibu unalo moyoni mwako.
Kumbuka Unyakuo upo karibu sana, dalili zote zimeshatimia, huna haja ya kuendelea kutangatanga na huu ulimwengu tena. Mgeukie Kristo akuokoe, ili uwe mmojawapo wa kizazi cha watu waadilifu.
pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp yanayotumwa kila siku basi bofya hapa >>> WHATSAPP
Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita..
BADO UPO YERUSALEMU TU..GALILAYA HUTAKI KWENDA?
FANYIKA SIPORA WA KRISTO, UNYAKUO UPO KARIBU.
Marago ni nini? ( Waamuzi 10:18)
Rushwa inapofushaje macho?
The word of God which shows that a woman must be abandoned when she is in her menstruation if from
Leviticus 15:19-33 19 And if a woman have an issue, and her issue in her flesh be blood, she shall be put apart seven days: and whosoever toucheth her shall be unclean until the even. 20 And every thing that she lieth upon in her separation shall be unclean: every thing also that she sitteth upon shall be unclean. 21 And whosoever toucheth her bed shall wash his clothes, and bathe himself in water, and be unclean until the even. 22 And whosoever toucheth any thing that she sat upon shall wash his clothes, and bathe himself in water, and be unclean until the even. 23 And if it be on her bed, or on any thing whereon she sitteth, when he toucheth it, he shall be unclean until the even. 24 And if any man lie with her at all, and her flowers be upon him, he shall be unclean seven days; and all the bed whereon he lieth shall be unclean. 25 And if a woman have an issue of her blood many days out of the time of her separation, or if it run beyond the time of her separation; all the days of the issue of her uncleanness shall be as the days of her separation: she shall be unclean. 26 Every bed whereon she lieth all the days of her issue shall be unto her as the bed of her separation: and whatsoever she sitteth upon shall be unclean, as the uncleanness of her separation. 27 And whosoever toucheth those things shall be unclean, and shall wash his clothes, and bathe himself in water, and be unclean until the even. 28 But if she be cleansed of her issue, then she shall number to herself seven days, and after that she shall be clean. 29 And on the eighth day she shall take unto her two turtles, or two young pigeons, and bring them unto the priest, to the door of the tabernacle of the congregation. 30 And the priest shall offer the one for a sin offering, and the other for a burnt offering; and the priest shall make an atonement for her before the LORD for the issue of her uncleanness. 31 Thus shall ye separate the children of Israel from their uncleanness; that they die not in their uncleanness, when they defile my tabernacle that is among them. 32 This is the law of him that hath an issue, and of him whose seed goeth from him, and is defiled therewith; 33 And of her that is sick of her flowers, and of him that hath an issue, of the man, and of the woman, and of him that lieth with her that is unclean.
Leviticus 15:19-33
19 And if a woman have an issue, and her issue in her flesh be blood, she shall be put apart seven days: and whosoever toucheth her shall be unclean until the even.
20 And every thing that she lieth upon in her separation shall be unclean: every thing also that she sitteth upon shall be unclean.
21 And whosoever toucheth her bed shall wash his clothes, and bathe himself in water, and be unclean until the even.
22 And whosoever toucheth any thing that she sat upon shall wash his clothes, and bathe himself in water, and be unclean until the even.
23 And if it be on her bed, or on any thing whereon she sitteth, when he toucheth it, he shall be unclean until the even.
24 And if any man lie with her at all, and her flowers be upon him, he shall be unclean seven days; and all the bed whereon he lieth shall be unclean.
25 And if a woman have an issue of her blood many days out of the time of her separation, or if it run beyond the time of her separation; all the days of the issue of her uncleanness shall be as the days of her separation: she shall be unclean.
26 Every bed whereon she lieth all the days of her issue shall be unto her as the bed of her separation: and whatsoever she sitteth upon shall be unclean, as the uncleanness of her separation.
27 And whosoever toucheth those things shall be unclean, and shall wash his clothes, and bathe himself in water, and be unclean until the even.
28 But if she be cleansed of her issue, then she shall number to herself seven days, and after that she shall be clean.
29 And on the eighth day she shall take unto her two turtles, or two young pigeons, and bring them unto the priest, to the door of the tabernacle of the congregation.
30 And the priest shall offer the one for a sin offering, and the other for a burnt offering; and the priest shall make an atonement for her before the LORD for the issue of her uncleanness.
31 Thus shall ye separate the children of Israel from their uncleanness; that they die not in their uncleanness, when they defile my tabernacle that is among them.
32 This is the law of him that hath an issue, and of him whose seed goeth from him, and is defiled therewith;
33 And of her that is sick of her flowers, and of him that hath an issue, of the man, and of the woman, and of him that lieth with her that is unclean.
Remember we have to know that not everything that took place on Old Testament is not the must to take place too in New Testament, Other things were just as a symbol in order to present the spiritual message to the New Testament.
For example for the issue of food Jesus came and correct by saying what enters a person doesn’t make a person unclean but from what’s comes out from a person because it comes from the heart, that’s why in anyways food doesn’t make a person to do mistakes before God if the food will be eaten by gratitude. But in the past animals who didn’t ruminate they were known as unclean,Which currently revealed in spiritual that people who chew spiritual food which they have been fed, they don’t have time to meditate on what they have been taught or what God has done for them or to work on the things which they have been taught.
Even in women issue when they are in menstruation normally the blood as blood doesn’t have a problem but ask yourself why that blood which comes out from reproductive organs seems to be unclean. This reveal that the dirt that produced due to adultery known as gross uncleanness to the person.
That’s why the bible tells us and the bed undefiled…(Hebrews 13:4)
That’s why we have to keep our body far from fornication.
But this doesn’t mean that bleeding make you unclean because that is automatically issue and it is not planned by a women. So it doesn’t come from the spirit to make one unclean. God use such example to show that things are much worse which comes from committing adultery . So when a women is bleeding that doesn’t make her to do not serve on altar or pray to God.
What she supposed to do is to make herself and her environment clean.
God bless you.
Related Topic:
What is the difference between flesh and spirit uncleanness?
JONAH’S VINE.
DO NOT BE CONCEITED.
Home: